Simba ni timu tishio kwa sasa klabu bingwa, imekamilika kila idara

Simba ni timu tishio kwa sasa klabu bingwa, imekamilika kila idara

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Hii ni timu tishio kwenye kundi lao kwa sasa, inacheza direct football ikiwatumia wachezaji wao hatari wenye kasi na nguvu kusukuma mashambulizi mbele, ni timu yenye beki imara sana wakiongozwa na beki kijana bwana joash onyango, Na ilo limeonekana kwenye mechi zote mbili walizocheza na timu ngumu sana ya vipers kutoka Uganda.

Pongezi nyingi sana ziende kwa bilionea anayewezesha pesa za usajili bwana Mo kafanya kazi kubwa sana kusajili wachezaji wakubwa wakina Sawadogo, Baleke, Kapama na wengineo wanaoifanya simba iwe tishio Afrika, Kiufupi nawaona simba mbali sana kwenye hii micheZo ya klabu bingwa Afrika na nawaona Horoya wakiacha alama zote kwa mkapa kutokana na mpira mkubwa wanaocheza hawa vijana wa Robertinho.

Timu iko vizuri sana kuanzia beki, viungo na washambuliaji kwakweli wamekamilika kila idara, Mashabiki wake ndio maana awana wasi wasi kabisa na timu yao, wanakula kuku kwa mrija stress kwao ni mwiko, Nawashauri sana wasiivuruge timu hii waiache ivyo ivyo ili wasije wakaaribu mipango ya kocha kufika nusu fainali au fainali ya klabu bingwa ambayo ndiyo ndoto ya kila mwanasimba wakiongozwa na mwenyekiti wao Bwana mangungu, Mama alitakiwa awaongeze mil.5 nyingine kwa pira lile la jana dhidi ya vipers ambao walipelekewa moto wa gesi mwanzo mwisho kudadadeki, Mwisho kabisa pongexi ziende kwa viongozi wote waliofanikisha kuitengeneza simba tishio inayoweza kuifunga timu yoyote nje ndani kama walivyofanya kwa vipers!
 
Nikiwa kama mshabik wa Simba 🦁🦁🦁
Bado hatuna aggressive strikers pia Kwa mechi ya Jana kocha wa vipers angesema chama apewe beki mmoja wa kutembea nae hakuna ambacho kingefanyika.

Bado tunachezea sana nafasi hatuna mtu mwenye uchu wa mabao pale mbele...

Wachezaji Bado wana Tatizo la football ⚽ psychology hili nalo lifanyiwe kazi....

Zile nafasi za kufunga ambazo sisi tulizikosa timu kama Raja lazima akuadhibu....

Sijamwona mshambuliaji tishio pale Simba 🦁🦁

Yaan asikwambie mtu timu zetu Zima safar sana watz Tunaupenda mpira sana....

Nitumie nafasi hii kuwapongeza Timu yangu SIMBA 🦁🦁

Simba 🦁 guvu moya🤓
 
Nina hofu na mechi yao ya marudio Morocco. Labda tuombee hao Raja Casablanca wachezeshe kikosi chao cha U20! Maana hao jamaa wanampiga mtu nyumbani na ugenini.

Kinyume na hapo, wanaweza kujikuta wamebakia na hizi pointi zao 6. Uzuri nafasi bado wanayo, pamoja na wapinzani wao wa karibu; timu ya Horoya. Hivyo wanatakiwa wapambane mpaka mwisho.
 
Huyo ni utopolo anaandika akiwa amebanwa kwa maumivu ya tumbo la kuharisha[emoji1787][emoji1787] walijua Simba haitashika hata nafasi ya pili kwenye kundi🫣🫣

Wewe uto tafuta pampasi uvae kwa usalama wako[emoji1322][emoji1322]
Ngada fc mbona amjiamini mnaweweseka tu, kwanini amuiamini timu yenu
 
Kaka Malafyale.

Ubahili wa Mwamedi Ndio chanzo Cha yote haya.

Simba Ina wachezaji WATANO TU.
Inonga, Chama, Saido, Manula, kapombe na shabalala .

SIMBA INA WACHEZAJI MIZIGO WENGI MNO.
Kanute, Banda, Ottara, Okwa, Onyango Umri, Sawadogo, Baleke.

Imagine una kiungo MZAMIRU na kanute.
Yanga Ina kiungo
BANGALA NA AUCHO.

MO ANAIHUJUMU SANA SIMBA.
KOCHA ASIGUSWE KABISA
 
Back
Top Bottom