Simba S.C: Huu ni msimu wa Mabadiliko

Simba S.C: Huu ni msimu wa Mabadiliko

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
Takwimu hazidanganyi.. Hebu tulingaanishe msimu uliopita na sasa mambo yakoje..

Mechi sita za mwanzo za Simba S.C katika msimu wa 2014/15 ndani ya VPL.
1. Simba 2-2 Coastal
2. Simba 1-1 Polisi
3. Simba 1-1 Stand United
4. Yanga 0-0 Simba
5. Prisons 1-1 Simba
6. Mtibwa 1-1 Simba
Mchanganuo wa mechi hizo 6.. Ni kama ifuatavyo;
Magoli ya Kufunga: 6
Magoli ya Kufungwa: 6
Mechi Tulizoshinda: 0
Mechi Tulizoshindwa: 0
Mechi Tulizodroo: 6
Mechi Ambazo Hatukuruhusu Goli: 1

Mechi sita za mwanzo za Simba S.C katika msimu wa 2015/16 ndani ya VPL.
1. African Sport 0-1 Simba
2. Mgambo JKT 0-2 Simba
3. Simba 3-1 Kagera Sugar
4. Yanga 2-0 Simba
5. Simba 1-0 Stand United
6. Mbeya City 0-1 Simba
Mchanganuo wa mechi hizo 6.. Ni kama ifuatavyo;
Magoli ya Kufunga: 10
Magoli ya Kufungwa: 3
Mechi Tulizoshinda: 5
Mechi Tulizoshindwa: 1
Mechi Tulizodroo: 0
Mechi Ambazo Hatukuruhusu Goli: 4

Ukiangalia kwa umakini hizo takwimu hapo juu utagundua haya yafuatayo;
1. Defence [Great Wall of China]
Katika mechi 6.. Mechi 4 hatujaruhusu goli hata 1.. [Takwimu hazidanganyi]
Ukiacha uwezo mkubwa wa kukaba.. Pia kama ikitokea mabeki wamepoteza mipira [japo ni mara chache saana], wana uwezo mkubwa sana wa kurecover mipira waliyopoteza.
2. Midfield.
Kwa sasa Simba S.C ndiyo timu yenye kiungo bora kabisa kwa sasa katika VPL.. Midfield hii ni bora kwa sababu, ni mahiri katika,
a] Kumaintain possession.. jambo ambalo linawapa mtihani mkubwa sana wapinzani wao
b] Kila mchezaji ana hamu sana ya kupasiwa mpira.. na wanapopata mpira hua wanafanya maamuzi sahihi
c] Wanaunganisha vyema defence na washambuliaji.. Hii imeisaidia katika akutengeneza balance ya timu.
d] Kuwadhibiti ipasavyo viungo wa timu pinzani.. Na hili huwezekana kwa kuwazuia na kuwanyima nafasi wapinzani.
3. Striking Force.
Simba ya sasa inatupia magoli inavyojisikia.. Ina uwiano wa goli mbili kwa kila mechi.. Na katika hili, kila kiumbe aliye katika 1st eleven ni mfungaji.. Si Beki wala Mido.. wote ni wafungaji.

Aminini Aminini nachowaaambia.. Simba hii ya msimu wa 2015/2016 ni ya Ulaya Ulaya.

Mungu Ibariki Simba Sports Club
 
Duh umechambua vizuri mdau, lakini mda bado sana waongeze tu kifua
 
Mchanganuo wa mechi hizo 6.. Ni kama ifuatavyo;
Magoli ya Kufunga: 10
Magoli ya Kufungwa: 3
Mechi Tulizoshinda: 5
Mechi Tulizoshindwa: 1
Mechi Tulizodroo: 0
Mechi Ambazo Hatukuruhusu Goli: 4

...

Mwelekeo mzuri sana, ... ila inauma kwamba hiyo mechi moja tuliyofungwa ni ya Yanga.
 
Mwelekeo mzuri sana, ... ila inauma kwamba hiyo mechi moja tuliyofungwa ni ya Yanga.

Hata mimi Mkuu.. mechi ya Yanga inanisumbua sana kichwa mpaka sasa. Naamini next time tukikutana nao, tutafute machozi tuliyonayo.
 
Duh umechambua vizuri mdau, lakini mda bado sana waongeze tu kifua

Uliyonena ni u kweli mtupu Mkuu.. ila vijana wavyozidi kukaa pamoja ndo wanazoeana vizuri, pia hata uelewano utakua mkubwa zaidi uwanjani.. Hivyo wapinzani wetu wajiandae vizuri tuu.. mana naona kipimo cha dozi tunazogawa kitaongezeka maradufu.
 
Simba imekuwa tamu kwa kuwa na kiungo bora, wanamiliki mpira na wanacheza sexy football. Ndio maana hadi sasa hakuna timu iliyoizidi possession ktk mechi sita ilizocheza. Lakini kwa kweli sina furaha sana wala amani na fowadi line
 
Back
Top Bottom