Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,351
- 9,855
Nawasalimia wana Msimbazi wenzangu!
Nimesikitishwa na mpira unaochezwa na timu yetu pendwa ya Simba (Lunyasi), timu siku hizi inacheza mpira mbaya sana, mpira makande, magoli yetu yenyewe yanapatikana kipapatupapatu kama ya utopolo. Leo nimeona takwimu eti Simba katika mechi 2 za ligi ndo tunaongoza kwa kupiga cross (cross 34!) Tangu lini Simba ikaongoza kwa kupiga cross na sio kupiga pass?
Kuna watu watakuja na utetezi kuwa timu Ina wachezaji wapya wengi, hivyo hawajaingia kwenye mfumo wetu wa Lunyasi. Hii sio kweli, maana ukiangalia kwenye timu iliyoanza (first eleven) ni wachezaji wawili tu ndo wageni ambao ni Inonga na Kanoute, lakin wengine wote ni walewale wapo zaidi ya misimu miwili. Na hata wanaosema kuondoka kwa Luis na Chama ni sababu ya timu kucheza hovyo siku hizi, nayo sio kweli, kuondoka kwa wachezaji wawili hakuwazuii watu kupiga pass na kucheza mpira uliozoeleka, maana hata hao wachezaji wawili walikuja waliikuta timu inacheza mpira biriani.
Tatizo kubwa ninaloliona ni kocha. Gomez ni kocha anaejali zaidi matokeo (results oriented) kuliko kujali namna ya hayo matokeo yanapatikanaje. Wana msimbazi tumezoea mpira biriani, Gomez alikuja akaikuta timu imetengenezwa na Uchebe na Kishingoo, na yeye akatembelea humo. Na zaidi ni Uchebe ndo aliitengeneza timu iliyocheza mpira biriani tunavyotaka.
Ombi langu kwa uongozi wanatakiwa wamuambie kocha sisi tunataka timu icheze mpira unaoeleweka, na sio mradi kupata ushindi wa style ya utopolo. Magoli ya kona na cross, yanatokana na piga nikupige. Kama Gomez hawezi kutupa mpira tunaotaka atimuliwe!
Nimesikitishwa na mpira unaochezwa na timu yetu pendwa ya Simba (Lunyasi), timu siku hizi inacheza mpira mbaya sana, mpira makande, magoli yetu yenyewe yanapatikana kipapatupapatu kama ya utopolo. Leo nimeona takwimu eti Simba katika mechi 2 za ligi ndo tunaongoza kwa kupiga cross (cross 34!) Tangu lini Simba ikaongoza kwa kupiga cross na sio kupiga pass?
Kuna watu watakuja na utetezi kuwa timu Ina wachezaji wapya wengi, hivyo hawajaingia kwenye mfumo wetu wa Lunyasi. Hii sio kweli, maana ukiangalia kwenye timu iliyoanza (first eleven) ni wachezaji wawili tu ndo wageni ambao ni Inonga na Kanoute, lakin wengine wote ni walewale wapo zaidi ya misimu miwili. Na hata wanaosema kuondoka kwa Luis na Chama ni sababu ya timu kucheza hovyo siku hizi, nayo sio kweli, kuondoka kwa wachezaji wawili hakuwazuii watu kupiga pass na kucheza mpira uliozoeleka, maana hata hao wachezaji wawili walikuja waliikuta timu inacheza mpira biriani.
Tatizo kubwa ninaloliona ni kocha. Gomez ni kocha anaejali zaidi matokeo (results oriented) kuliko kujali namna ya hayo matokeo yanapatikanaje. Wana msimbazi tumezoea mpira biriani, Gomez alikuja akaikuta timu imetengenezwa na Uchebe na Kishingoo, na yeye akatembelea humo. Na zaidi ni Uchebe ndo aliitengeneza timu iliyocheza mpira biriani tunavyotaka.
Ombi langu kwa uongozi wanatakiwa wamuambie kocha sisi tunataka timu icheze mpira unaoeleweka, na sio mradi kupata ushindi wa style ya utopolo. Magoli ya kona na cross, yanatokana na piga nikupige. Kama Gomez hawezi kutupa mpira tunaotaka atimuliwe!