Simba SC ilibugi maeneo haya kiufundi katika kukabiliana na Yanga SC

Simba SC ilibugi maeneo haya kiufundi katika kukabiliana na Yanga SC

Simba ni kama vile haina uongozi au viongozi hawana uchungu na timu. Hayo yote yaliyoelezwa hapo juu yamesemwa sana hapa jamvini lakini hakuna hatua zilizochukuliwa. Na jambo ambalo ni kubwa na baya kama halitafanyiwa kazi haraka ni hilo la staminia na kasi kwani Simba pamoja na kushinda baadhi ya mechi lakini timu ilikuwa inakata moto dakika kuanzia ya 60/65. Na hili nafikiri Gamondi na benchi lake walilifanyia kazi sana kwani dhahama ndio ilianzia mida hiyo hiyo.

Yanga alipoondoka kocha wa mzuri wa viungo wametulia wametafuta kocha wa maana wa viungo ukija Simba tangu ameondoka Zrane hakuna kocha aliyekuja kumzidi Zrane au walau tu anayemfikia kiwango chake. Badala yake viongozi kwa ushauri wa Robertino wameenda kuleta kocha wa viungo mwenye kitambi maana yake hata yeye mwenyewe hajimudu afya yake. Timu hata ikiwa na wachezaji wenye vipaji vya namna gani kama ilivyo sasa hivi Simba lakini kama hawana stamina basi timu itaonekana ya kawaida tu matokeo yake yatakuwa mabovu.
 
1/ Aishi Manula hakupaswa kuanza/kucheza kabisa kwa sababu hakuwa na match fitness, japo kuwa benchi la ufundi lilikua na maono ya kumrudisha Aish Manula rasmi katika ligi kutokea Majeruhi lakini hesabu zimekua tofauti na vile benchi la ufundi lilivyoamini/kutegemea Aishi Manula angefanya vizuri katika Derby ya Kariakoo.

2/Ukuta wa YERIKO (Inonga na Che Malone) Hawa mabeki wote ni wacheza na jukwaa Bora hata Chemalone Fondoh anakua serious kidogo lakini Enonga utoto mwingi na kicheza na jukwaa ndiyo kitu anachoweza.

Simba sc waliposawazisha nilimuona Inonga alianza sifa anapokua na mpira anataka achezee mpira/apige chenga Mara amtishie Max Nzengeli kiufupi huo ni utoto.

Robertinho hapa angevunja mmoja angeanzia benchi na mmoja wapo angecheza na KENNEDY JUMA.

3/Viungo wakabaji Kati ya Ngoma na Kanuti mmoja wapo angeanza nje haswaa na Kanuti MZAMIRU angeanza, hii NI Derby na katika dabi ya karikoo huwa tunashuhudia dabi mbili Kati ya MZAMIRU na AUCHO.

Mzamiru huwa anamuweza sana AUCHO mpaka aucho anapaniki tofauti na Kanuti/Ngoma hapa Robertinho alibugi pakubwa sana Mchezaji mwandamizi Kama Mzamiru kuanzia benchi kwenye mechi Kama hii.

4/Chama na Saidoo ntibazonkiza hapa mmoja wao alipaswa kukaa benchi maana uchezaji Wa Yanga sc ni mpira wa speed ili uweze kupora mpira kwao unapaswa kuwakaba mawili wawili na msitegemee Viungo wakabaji.

Chama na Saidoo ntibazonkiza Hawa wote wakipoteza mpira siyo wakabaji Kama Viungo washambuliaji wa Yanga sc.

5/Uchoyo wa Kibu Denis kila anapopata mpira anataka afunge yeye sijui Kama Robertinho hakuliona hili kila anapopata mpira anataka apige golini tu hata Kama wenzie wamefungua nafasi wapasiwe mpira lakini hakufanya Hilo na kocha Robertinho hakumuambia mpaka anapata majeruhi.

6/Physical coach ajitafakari maana timu inacheza Kama imefungwa mawe miguuni wazito sana hakuna morali ndani ya kikosi kila mchezaji anacheza Kama anavyojua yeye.

7/Rotation ya wachezaji ni muhimu sana Shomari kapombe na Muhammed Hussein wanapaswa kupumnzika na vijana wadogo waanze kupata namba Israel mwenda na Duchu wapewe nafasi.

NB: Yanga sc ilikua Bora molari ya wachezaji na kupambana kwa Kasi ile ile mpaka mwisho ndiyo sababu ya KULETA matokeo Chanya kwao.
hakuna hata siku siku moja mzamiru aliweza kumdhibiti aucho,chama na saidoo umri umeenda na stamina hawana hawawezi katu kushindana na vijana wenye kasi wa yanga,kule tanga mliona.Nahisi sio kocha aliyempanga manula
 
Upo sahihi lakini ufa huo umeweza kuubaini kutokana na ubora walioonyesha Yanga. Kamajana Simba ingecheza na JKT Ruvu usingeona hayo mapungufu.

Hivyo basi kila durby team hata iwe nzuri kiasi gani kuna makosa madogo madogo sana huifanya team moja kupoteza. Tuendelee tusubiri mechi ijayo
Sio mechi ya derby tu kwa sisi wenye jicho la kimpira tulishaona matatizo kitambo sana. Kuna madogo mtaani huwa nawaambia wananikatalia sana. Simba ina matatizo makubwa sana kwenye backline na kiungo mkabaji. Mechi nyingi wanakua exposed sana ndio maana Gamondi alianza na viungo washambuliaji wengi
 
Simba ni kama vile haina uongozi au viongozi hawana uchungu na timu. Hayo yote yaliyoelezwa hapo juu yamesemwa sana hapa jamvini lakini hakuna hatua zilizochukuliwa. Na jambo ambalo ni kubwa na baya kama halitafanyiwa kazi haraka ni hilo la staminia na kasi kwani Simba pamoja na kushinda baadhi ya mechi lakini timu ilikuwa inakata moto dakika kuanzia ya 60/65. Na hili nafikiri Gamondi na benchi lake walilifanyia kazi sana kwani dhahama ndio ilianzia mida hiyo hiyo.

Yanga alipoondoka kocha wa mzuri wa viungo wametulia wametafuta kocha wa maana wa viungo ukija Simba tangu ameondoka Zrane hakuna kocha aliyekuja kumzidi Zrane au walau tu anayemfikia kiwango chake. Badala yake viongozi kwa ushauri wa Robertino wameenda kuleta kocha wa viungo mwenye kitambi maana yake hata yeye mwenyewe hajimudu afya yake. Timu hata ikiwa na wachezaji wenye vipaji vya namna gani kama ilivyo sasa hivi Simba lakini kama hawana stamina basi timu itaonekana ya kawaida tu matokeo yake yatakuwa mabovu.
FACT
 
Sio mechi ya derby tu kwa sisi wenye jicho la kimpira tulishaona matatizo kitambo sana. Kuna madogo mtaani huwa nawaambia wananikatalia sana. Simba ina matatizo makubwa sana kwenye backline na kiungo mkabaji. Mechi nyingi wanakua exposed sana ndio maana Gamondi alianza na viungo washambuliaji wengi
KWELI KABISA WASIPOANGALIA MAKUNDI HAWATOBOI
 
hakika game ilikuwa ni ngumu mno kwa upande wa mnyama ni suala tu la kusema asante Mungu coz kuna nafasi zilikuwa zinakoswa nyingi mnooo lasivyo tungesema mengine leo


Political is just liKe a war always, BOOST YOUR CONFIDENCE
[emoji16] NILIHESABU NAFASI ZILIZOKOSWA NI KAMA TATU HIVI.
 
hakuna hata siku siku moja mzamiru aliweza kumdhibiti aucho,chama na saidoo umri umeenda na stamina hawana hawawezi katu kushindana na vijana wenye kasi wa yanga,kule tanga mliona.Nahisi sio kocha aliyempanga manula
RAFU ZAKE MZAMIRU HUWA ZINAMTOA KWENYE RELI AUCHO.
 
Wewe ni muongo sana umesahau siku ya jumatano kwenye thread ya mo dewj kuteua kamati ya fitna na wewe uliweka matokeo ya simba kushinda 5 kwa Yanga O mwaka 2012 halafu ukasema ogopa sana wenye simba yao wakiungana? Halafu hapa unataka kujifanya eti ulishaonya
Kweli kabisa alisema.
 
Wewe ni muongo sana umesahau siku ya jumatano kwenye thread ya mo dewj kuteua kamati ya fitna na wewe uliweka matokeo ya simba kushinda 5 kwa Yanga O mwaka 2012 halafu ukasema ogopa sana wenye simba yao wakiungana? Halafu hapa unataka kujifanya eti ulishaonya
UMEMPIGA NA KITU KIZITO SANA HAWEZI KURUDI TENA.
 
Back
Top Bottom