Simba SC - Kagera Sugar FC, Uwanja wa Uhuru

Da Gladiator

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
1,641
Reaction score
2,646
Priiiiiiiiiii, Vurumai za ligi kuu Tanzania Bara VPL, kuendelea leo Jumatano 04, Novemba 2020. Leo zitapigwa mechi tatu(3) katika viwanja mbalimbali.Hii ni baada ya hapo jana anaejiita bingwa wa kihistoria Dar Young Africans kutoa suluhu dhidi ya Gwambina FC, lakini katika uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam kuna bonge la mtanange kati ya Simba SC na Kagera Sugar FC.

Mechi hii ni muhimu sana tena sana kwa Simba SC, 'wekundu wa msimbazi' kushinda ili kukuza, kuinua na kuboresha morali kuelekea katika 'derby' ya Dar/Kariakoo mwishoni mwa wiki hii.

Je, Simba SC ama Kagera Sugar FC kuibuka mwamba ? Kaa nami/nasi usikose ukahadithiwa, Pira biriani, pira kachori, pira kababu, magoli mengi ni Simba SC.

Kumbuka mtanange ni kuanzia saa 1600Hrs.

Sidhani kama wenzetu wasingelibebwa jana wangelipona.

FT

Simba SC
2 - 0
Kagera Sugar FC

Magoli
-J R BoccO. 43', Penalty.
-S H NdemlA. 45'+5'.


KUELEKEA KARIAKOO DERBY.
[emoji966]Viingilio vya Pambano la watani wa Jadi, Simba SC na Dar Young Africans SC Jumamosi 07, 2020. Uwanja wa Mkapa .
VIP A. < > 30,000/=
VIP B. < > 20,000/=
VIP C. < > 15,000/=
Orange. < > 10,000/=
Mzunguko < > 7,000/= .



"Kulitaka mwana, kulipewa mwana".

#SimbaNguvuMoja.

#AnotherLevel.
View attachment 1619464
 
Kagera wataweza kweli ?!
Kagera saizi yao ni vyura....,

Simba taifa kubwa, wakimataifa tunasubiri league ya mabingwa ianze,...ndo anga zetu hizo..

Huku tunasubiri kuchukua ubingwa...ngoja hawa madogo warukeruke lakini bingwa anajulikana ni MNYAMA
 
Kagera wanafunga goli 2 leo,Simba Kama atashinda zaidi ni sawa.I bet matokeo ni 1-2 au sare.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…