Simba SC kucheza mechi 3 za kirafiki dhidi ya Bandari FC, Mashujaa United na Black Eagles FC

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Mabingwa wa Nchi Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, anatarajia kucheza michezo mitatu ya kirafiki dhidi ya Bandari FC, kutoka nchini Kenya, Mashujaa United ya Kigoma na Black Eagles FC kutoka Burundi, kabla ya kuendelea na ligi kuu ya Tanzania Vodacom Premier League VPL.

Simba SC, itaanza kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi Bandari FC, Oktoba 12, 2019 kwenye Uwanja wa Taifa, kisha klabu ya Simba SC itaondoka kuelekea Kigoma kuwafuata Mashujaa United na kucheza nao mchezo Oktoba 14, 2019 kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika.

Simba SC, itamaliza ziara yake ya mechi za kujipima nguvu kwa kuingia tena dimbani Oktoba 16, 2019 kupepetana na Black Eagles ya Burundi kwenye Uwanja huo huo Lake Tanganyika.

•••Usikose Ukaambiwa..Simba SC yenye kusakata kandanda safi lenye viwango wa Shirikisho la soka Afrika CAF[/b]
 
Wale jamaa wa bondeni wameshukuru sana TFF kupeleka mbali mechi yao na Simba SC, kuna jambo baya sana lingetokea..![emoji23]
 
Kwa nini Mashujaa? Ni agizo la mganga wa timu au ni kutaka tu kuondoa soo kwa kuikamia kuifunga magoli mengi, ikibidi hata kwa kuwapa rushwa! baada ya kutolewa kwa aibu kwenye Azam Sports Federation Cup msimu uliopita?
 
Kwa nini Mashujaa? Ni agizo la mganga wa timu au ni kutaka tu kuondoa soo kwa kuikamia kuifunga magoli mengi, ikibidi hata kwa kuwapa rushwa! baada ya kutolewa kwa aibu kwenye Azam Sports Federation Cup msimu uliopita?
Na Bandari FC, Black Eagles kwa agizo la mganga? Tucheze na nyie basi kama mnaweza..!
 
Kwa sasa habari za Simba SC kuzipata si rahisi kama walivyozoea, kwahivyo hawa waandishi uchwara lazima wateseke..!

Umeona mambo ya usajili walivyosumbuka hawa waandishi, na ndivyo ilivyo sasa..SimbaNguvuMoja
Hamna kitu kama hicho, chunguza wote walotoa taarifa hizo ni wale mapopoma ambao wao kwao kupost jambo nzuri ni sawa na kukatwa shingo kwa wembe
 
Yanga ni UnderChura, hivi anashindwaje kufikia level ya Simba SC ya robo fainali..!
Wenzako wote waliofika group stages msimu uliopita wamerudi tena group stages, wewe tu umeishia preliminary stages, hii inadhihisha na kuthibitisha u underdog wako, kumbe yaliyokuwa yanasemwa kwamba mechi za home ulikuwa unacheza faulu nje ya uwanja ni kweli, sasa ukakutana na kiboko yako Du-songo akakufanya huna hamu mkuu.
 
Alisikika mlevi mmoja akisema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…