Simba SC kufukuza wachezaji wake tano wa kigeni

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Wanamsimbazi na hata baadhi ya viongozi mpaka sasa hawaamini kama timu yao ndio imeukosa ubingwa wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara msimu huu, lakini moja ya wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa klabu hiyo, Hamis Kilomoni amefichua siri nzito kuwa kuna wachezaji watano wa kigeni watatemwa na klabu hiyo.

Mshambuliaji wa Simba Mrundi ‘Laudit Mavugo’

Kilomoni amesema kuna wachezaji watano wa kigeni watatemwa klabuni hapo ili kupisha wazawa kuipigania klabu hiyo kwani wanagharama ndogo na wanajitoa kuipigania timu kwa jasho na damu.

Kilomoni aliyewahi kuwa mchezaji na kiongozi wa Simba kabla ya kuwa Mwenyekiti wa Baraza la wadhamini, alisema Simba haikupata huduma sahihi kwa nyota wake saba wa kigeni iliowasajili msimu huu kwa uwezo mdogo walionao, hivyo anaona ni bora idadi yao ipunguzwe ibaki wawili tu.
Alisema mabosi wa Simba walifanya kosa kubwa kuwadharau wachezaji wazawa na kuwakimbilia wageni ambao wamekuwa hawana msaada wowote zaidi ya kuitia gharama kubwa ya kuwahudumia.

Tulikuwa na wachezaji wengi kutoka kikosi B, lakini sijui nini kilitokea wakatolewa, huko waliko wanafanya vyema na hata kuisumbua Simba, halafu sisi tukakimbilia wageni saba ambao ukiniuliza faida yake hata sijaiona, nafikiri tunapaswa kuangalia upya hili suala la wachezaji wa kigeni halisaidii soka letu, Simba kama kuna wachezaji wa kigeni wanaostahili kubaki na walioisaidia timu wako wawili tu hawa wengine sioni wanachokifanya.” Alisema Kilomoni.

Hata hivyo Kilomoni hajawataja nyota wanaostahili kusalia, japo Simba kwa sasa ina wachezaji wa kigeni ambao ni Method Mwanjali, Juuko Murshid, Fredrick Blagnon, Janvier Bokungu, Laudit Mavugo, James Kotei na kipa Daniel Agyei.

Chanzo: Mwanaspoti
 
Wachezaji wanaochezea timu za bongo wanaingia mikataba ya kijinga sana
 
Simba wachezaji wa kuondoa ni hawa. Juma Luizio, Hamad Juma, kazimoto. Blagnon, pastori atanas, lufunga,
 
Mnawaonea tu, Simba ilitakiwa iwafukuze viongozi wote, baadhi ya washabiki mbumbumbu na wachezaji wote kasoro Kichuya tu.
sembo na GENTAMYCINE hawa ni mfano wa baadhi ya mashabiki wanaojielewa, hivyo wasifukuzwe.

Ni mtazamo wangu tu.
 
Tatizo la simba ni viongozi tu..hawajuwi fitna za mpira..wasiwaonee wachezaji...mpira una fitna kuanzia nje ya uwanja..hadi ndani ya uwanja...na wasipokuwa makini... YANGA wataleta fitna ILI MNYAMA AFUNGWE na mbao...
 
Lile limavugo linastahili kutimiwa kabisaaa nafasi yake ichukuliwe na ngoma kwa gharama zozote
Ngoma huyuhuyu anayekipiga Yanga aende tope fc? Acha utani hamna hela ya kumpa Ngoma nyinyi, kwanza ashapata timu kwa madiba huko atakubali vip kuja kucheza ndondo
 
Mnawaonea tu, Simba ilitakiwa iwafukuze viongozi wote, baadhi ya washabiki mbumbumbu na wachezaji wote kasoro Kichuya tu.
sembo na GENTAMYCINE hawa ni mfano wa baadhi ya mashabiki wanaojielewa, hivyo wasifukuzwe.

Ni mtazamo wangu tu.

Mwandishi aliyeandika hiyo taarifa nadhani atakuwa ni ' Mpumbavu ' namba moja kama siyo namba mbili duniani kote. Na sidhani kama kweli huyo Mwandishi ni ' analyst ' mzuri wa michezo hasa ' Soka / Kandanda / Fabo ' kwani kama angekuwa ni ' Mweledi ' wa ukweli asingethibutu kuandika huo ' Upupu / Upuuzi ' wake.

Hivi ni Kiongozi au Mwanasimba au nani katika benchi zima la Ufundi la Simba SC leo hii atataka Golikipa Daniel Agyei, Beki / Kiungo James Kotei, Beki ' Kisiki ' kabisa Juuko Murshid, mshambuliaji ambaye naweza nikadiriki kumtabiria mapema kuwa season ijayo ya VPL atafanya vizuri mno kwani tayari ameshaijua ' Ligi ' yetu Laudit Mavugo na Beki namba mbili ' Fundi na Mtaalam ' Janvier Besala Bokungu a.k.a Bandeko Nangai waachwe? Kama ni mchezaji wa kuachwa kwa maoni yangu basi angatakiwa awe Fredrick Blagnon kwani uchezaji wake ni kama wa homa ya vipindi mara anacheza vizuri mara anaharibu ila hata hivyo kama na Yeye ataaminika na kupewa muda zaidi basi naamini anaweza kubadilika msimu ujao na kuwa msaada mkubwa kwa Klabu yetu ya Simba kwani ana ' uzuri ' wake hasa wa kuwasumbua ' Mabeki ' na ' kulazimisha ' mashambulizi.

Ingekuwa ni amri yangu au hata uwezo wangu sioni haja au mchezaji yoyote yule wa ' Kigeni ' kuachwa bali napendekeza wapewe muda na kwa jinsi nilivyowaona msimu huu nina uhakika tena wa 100% kwamba kama tukiwaamini, kuwatia moyo na kuonyesha tunawajali mwakani hawa Wachezaji wote wa Kigeni wanaweza hata kutufanya Simba SC tutangaze ' Ubingwa ' wa VPL huku tukiwa tumebakisha michezo 10 ya kumaliza ' Ligi ' yetu ya ' Madafu '.

Ni hayo tu Mkuu.
 
Simba wachezaji wa kuondoa ni hawa. Juma Luizio, Hamad Juma, kazimoto. Blagnon, pastori atanas, lufunga,
Baaas, con mchezaj wa kigen wa kuondoka zaid ya blagnon, utamtoa nan kwa mfano?
 
Tatizo la simba ni viongozi tu..hawajuwi fitna za mpira..wasiwaonee wachezaji...mpira una fitna kuanzia nje ya uwanja..hadi ndani ya uwanja...na wasipokuwa makini... YANGA wataleta fitna ILI MNYAMA AFUNGWE na mbao...
Waibie siri maan hawashtuki tu mkuu,,,,

Sent from my HUAWEI Y330-U01 using JamiiForums mobile app
 
Lazima tufike pahala tuweke kumbukumbu,,mlisemaga katu hamto sajili mchezaji kutoka yanga,,,,leo ngoma tena.....

Sent from my HUAWEI Y330-U01 using JamiiForums mobile app
nyepesi nyepesi za hapa 'mujini' zinathibibitisha pasipo shaka kuwa ngoma na mali halali ya samba sc
kinacho subiliwa ni mkataba wake na yanga uishe by end of next month mambo yawekwe hadharan
 
Umeongea vzr sana mkuu, hv kuna tim maproo walioibeba zaid ya simba msim huu? Upuuz tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…