Japo kuwa Simba sc leo imeambulia point moja lakini kuna uwezekano wa kuipoteza baada ya kuvunja sheria hii
MBUMBUMBU KATIKA UBORA WETU!
Kikosi cha simba wachezaji 6 wa kigeni wameanza first eleven Badala ya 5!!
1)Daniel Agyei
2)Javier Bukungu
3)Juuko Murshid
4)James Kotei
5)Laudit Mavugo
6)Fredrick Blagnon
Kanuni inasemaje hapa???
Mmezidi umbeya nyie mashabiki wa Yanga ndio maana waarabu wamewasuta kwa kuwafunga 4G.
Pitia kanuni za VPL hapa chini uachane na uzushi wenu wa Kimbeya.
Kanuni: 57 Wachezaji wa Kigeni
(1) Klabu ya Ligi Kuu inaruhusiwa kusajili wachezaji saba (7) wa kigeni kutoka sehemu
yoyote duniani na inaweza kuchezesha wachezaji wake wote wa kigeni katika
mchezo mmoja wa Ligi Kuu.
(2) Wachezaji wa kigeni watathibitishwa usajili wao baada ya TFF kuhakiki usahihi wa
taarifa zao na kukamilika kwa taratibu za uhamisho wa kimataifa.
(3) Mchezaji wa kigeni wa ridhaa anayesajiliwa kwenye Ligi Kuu anaweza kuhamishwa
kwa kufuata utaratibu wa uhamisho wa kimataifa kwa wachezaji wa ridhaa.
(4) Wachezaji wa kigeni wanaoruhusiwa kusajiliwa ni wale wanaocheza katika timu za
Taifa za nchi zao au Ligi Kuu ya nchi husika.
(5) Mchezaji yeyote wa kigeni anayesajiliwa katika Ligi Kuu atalipiwa ada maalum ya
usajili ya US $2,000 (dola elfu mbili za Marekani) kwa msimu ili usajili wake uweze
kuthibitishwa na kuruhusiwa kucheza.