demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
MKITAKA UBINGWA FANYENI HIVI.
Nimesikia mazungumzo kibao kuhusu Matarajio ya Simba SC kutwaa ndoo msimu huu. Cha kushangaza zaidi hakuna anaye fahamu nini kifanyike ili muwe tishio katika mbio za Ubingwa wa msimu 2021/22.
Ushauri wangu kwenu ni kumtawaza Selemani MATOLA awe Kocha mkuu wa klabu au Kumfukuza mapema iwezekanavyo kabla hamjachelewa.
WHY?
Selemani MATOLA ndiyo mwenye kuongoza hujuma, figisu na chokochoko dhidi ya Timu akiwa na lengo kuu la kuhakikisha matokeo mabaya yanapatikana ili yapelekee kufukuzwa kwa Pablo.
Njama zake ni za siri mno hata baadhi ya viongozi wenu hawana uwezo wa kuamini hilo.
Tamaa yake kubwa ni kuweka Ufalme wake katika nafasi ya ukocha katika Klabu yenu. Baada ya kuona nafasi hiyo ni ngumu kuipata kiurahisi, sasa anapanga kuuonyesha Uongozi wenu kuwa makocha wazungu (Aussems, Da rosa, na Pablo) hawana uwezo wa kuifikisha mbali klabu.
Bila kujua. Hizo figisu zake zinashusha morali ya utendaji wa wachezaji haswa wale wazawa.
Hakikisheni mnampa timu haraka sana, kama itashindikana mfukuzeni kabisa kwenye benchi ufundi.
Narudia tena.
"Matumaini yenu ya ubingwa wa msimu huu yako katika kilindi cha Moyo wake ulio jawa na tamaa za kutaka kuwa Kocha mkuu wa Simba"
FORM ALIYONAYO YANGA SC
Kwa Yanga SC hii iliyoko kwenye form, nina uhakika matokeo mabaya kwake ni sare tu. Hivyo itawapasa kutoa sare mechi 4 ili kufikiwa alama na SimbaSC. Na wakati huo huo Simba SC ina kibarua cha kushinda mechi zake zote.
Je kwa hali iliyo ndani ya bench la ufundi la SIMBA SC unadhani inawezekana? Si rahisi.
KUMBUKIZI
Nakumbuka niliwahi kuiandikia barua AZAM FC iliyotaka imuondoe Iddi CHECHE kwenye bench lao la ufundi. Jambo jema ni kwamba wakatii.
Tamaa ile ile aliyokuwa nayo Cheche, sasa imeamia kwa Matola.
Matola ataitafuna klabu yenu chini kwa chini mpaka mkija kushtua Mnakuta YANGA SC Katwaa ndoo za ligi mara 3 mfululizo.
-Asiye Sikia la Mkuu...
Nimesikia mazungumzo kibao kuhusu Matarajio ya Simba SC kutwaa ndoo msimu huu. Cha kushangaza zaidi hakuna anaye fahamu nini kifanyike ili muwe tishio katika mbio za Ubingwa wa msimu 2021/22.
Ushauri wangu kwenu ni kumtawaza Selemani MATOLA awe Kocha mkuu wa klabu au Kumfukuza mapema iwezekanavyo kabla hamjachelewa.
WHY?
Selemani MATOLA ndiyo mwenye kuongoza hujuma, figisu na chokochoko dhidi ya Timu akiwa na lengo kuu la kuhakikisha matokeo mabaya yanapatikana ili yapelekee kufukuzwa kwa Pablo.
Njama zake ni za siri mno hata baadhi ya viongozi wenu hawana uwezo wa kuamini hilo.
Tamaa yake kubwa ni kuweka Ufalme wake katika nafasi ya ukocha katika Klabu yenu. Baada ya kuona nafasi hiyo ni ngumu kuipata kiurahisi, sasa anapanga kuuonyesha Uongozi wenu kuwa makocha wazungu (Aussems, Da rosa, na Pablo) hawana uwezo wa kuifikisha mbali klabu.
Bila kujua. Hizo figisu zake zinashusha morali ya utendaji wa wachezaji haswa wale wazawa.
Hakikisheni mnampa timu haraka sana, kama itashindikana mfukuzeni kabisa kwenye benchi ufundi.
Narudia tena.
"Matumaini yenu ya ubingwa wa msimu huu yako katika kilindi cha Moyo wake ulio jawa na tamaa za kutaka kuwa Kocha mkuu wa Simba"
FORM ALIYONAYO YANGA SC
Kwa Yanga SC hii iliyoko kwenye form, nina uhakika matokeo mabaya kwake ni sare tu. Hivyo itawapasa kutoa sare mechi 4 ili kufikiwa alama na SimbaSC. Na wakati huo huo Simba SC ina kibarua cha kushinda mechi zake zote.
Je kwa hali iliyo ndani ya bench la ufundi la SIMBA SC unadhani inawezekana? Si rahisi.
KUMBUKIZI
Nakumbuka niliwahi kuiandikia barua AZAM FC iliyotaka imuondoe Iddi CHECHE kwenye bench lao la ufundi. Jambo jema ni kwamba wakatii.
Tamaa ile ile aliyokuwa nayo Cheche, sasa imeamia kwa Matola.
Matola ataitafuna klabu yenu chini kwa chini mpaka mkija kushtua Mnakuta YANGA SC Katwaa ndoo za ligi mara 3 mfululizo.
-Asiye Sikia la Mkuu...