Simba SC Mmepigwa Parefu. Kifua Hakiuzwi Kwa Miaka 5

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Moyo wangu umejaa huzuni na sononeko la hali ya juu baaada ya kuona watani zangu wanakosa mtu sahihi wa kukamilisha madili kwa manufaa ya klabu.

Kwa nchi zinazoendelea huwa kuuza "chest rights" (haki za kifuani) kwa mdhamini tena kwa mda wa miaka 5.

Mnajinyima fursa ya kupata madili ya juu zaidi katika siku za usoni.

Yaani hata kama baada ya miaka 3 akitokea potential sponsor anayetaka kuweka mpunga mrefu kwenye jezi inabidi asubiri mpaka mkataba mrefu uishe.

Kwani mliona wenzenu wajinga wallipo mpa SportPesa miaka 3?

Yes. Wamefanya hivyo kwa lengo la kutoa mwanya wa investors wengine wenye dau la juu wataojitokeza wakati wowoote hivi kaaribuni.

Wenzenu wana akili sana. Hawajakodisha shamba kwa mda mrefu.

Dah. Mmeniangusha sana watani.
 
Mkataba wa Simba ni 12.5 b kwa miaka 5 kinachoendelea ni ileile michezo wa 20b kwenye makaratasi.
Hizo 12.5B kwa mwaka ulizisaini wapi wewe, na mlikuwa na nani?

Ikiwa zile 20B ni za makaratasi, unaonaje ukinionyesha zilipo zile 40B zenu za Azam na 12 zenu na Spesa? Ukishindwa kunionyesha basi hata zenu ni za makaratasi.
 
TOFAUTI YETU NA WAO:

"Hii ni mara ya kwanza mdhamini mkubwa anakuwa na senior team pekee, huko nyuma mdhamini mkuu alikuwa kwa timu zote lakini sasa timu zingine tunaweza kuzitafutia mdhamini wake"-CEO wa Simba SC, @bvrbvra

#SimbaWeek #SimbaDay
#SimbaDay2022
#NipasheMichezo
#NipasheMwangaWaJamii
 
Mkataba wako na Azam TV miaka mingap?
 
Nilidhani sheria za fifa zinakataza ,kumbe muuza genge mmoja anamshauri tajiri namba moja nchini
 

Mbona yanga hakumpa sportpesa mwaka mmoja ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…