Simba SC tuendelee tu kushangilia Nabi na wengineo kuondoka Yanga SC huku sisi tukiendelea kusajili ovyo ovyo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kuna Wachezaji watatu (siwataji) nimethibitishiwa na mtu wa ndani kuwa watasajiliwa na nimetumia siku tatu kuwatizama mmoja mmoja kwa utaalam wangu wa mpira na jicho la kuujua mpira na mchezaji sijaona hata mmoja anayetufaa Simba SC na kwa huu mtindo wa 10% ulioko Simba SC, najua watasajiliwa tu.

Tuendeleeni tu kushangilia Kocha Nabi kuondoka, Kocha wa Viungo wa Yanga SC kuondoka, Wachezaji Mshambuliaji Mayele na Kipa Diara kutaka kuondoka, huku sisi tukisajili kiboya (kipumbavu) halafu Ligi ikianza Yanga SC wakiwa wanashinda na kuchukua Makombe kama kawaida yetu tukimbilie kusema Yanga SC wanabebwa, wananunua Mechi na Serikali inawapendelea.

Mimi ninawaangalieni tu mkipotea.
 
Wewe ni mwekezaji?

Vitu vingine msipende kupoteza muda kuvijadili , kama timu itafanya vibaya wewe utapata hasara ipi? Je,10% imeanza leo Simba?

Na katika maisha nani hataki kupata? Maisha ya sadaka yapo mbinguni tu
 
Maskhara ya ukwel si mazur
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…