Simba SC wamechea kikubwa na kimkakati

Simba SC wamechea kikubwa na kimkakati

chibuOG

Senior Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
169
Reaction score
337
Simba Sports Club pamoja nakuwa na kundi kubwa la wachezaji wapya pamoja na benchi la ufundi jipya kabisa lakini bado wameonyesha kuwa wao ni timu namba moja kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Namba 6 kwa ubora kwa vilabu Afrika nzima.Yaani ule mpira waliocheza jana ndio huwa unampa ubingwa Al Ahly ya Misri,Unacheza kwa malengo sio tu ilimradi na kiwango kile naiona Simba ikifika mbali sana tena ikiwezekana hata kombe watachukua.

Halafu mnaombeza Fadlu Davis kwa kumuacha nje Mukwala na kumuingiza Valentino Mashaka naomba niwaambie ukocha ni taaluma na watu wanasomea kwahiyo muacheni Mtaalamu Fadlu afanye majukumu yake kwa taaluma yake.
 
Mpira wa kushindwa kupiga hata pasi 7 kwa usahihi?
Mpira wa kushambuliwa mwanzo mwisho?
Mpira wa kushindwa hata kutengeneza nafasi?
Mpira wa kushindwa kupata hata on target moja?
Wachezaji hata unyumbulivu hawana?
 
Mpira wa kushindwa kupiga hata pasi 7 kwa usahihi?
Mpira wa kushambuliwa mwanzo mwisho?
Mpira wa kushindwa hata kutengeneza nafasi?
Mpira wa kushindwa kupata hata on target moja?
Wachezaji hata unyumbulivu hawana?
Mpira una namna nyingi zakuangalia au kutazama
kishabiki
kifurukutwa
kinazi
kinafiki
kipinzani
kiufundi
n.k
Sasa sijui wewe uliangalia mpira kwenye namna ipi hapo?
Michuano ni CAF CONFEDERATION CUP KNOCK OUT STAGE halafu mechi ya kwanza ugenini kat ya mechi mbili zitakazoamua timu ya kwenda GROUP STAGE wewe kwa utaalamu wako ulitaka Simba Wachezeje?
 
Simba Sports Club pamoja nakuwa na kundi kubwa la wachezaji wapya pamoja na benchi la ufundi jipya kabisa lakini bado wameonyesha kuwa wao ni timu namba moja kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Namba 6 kwa ubora kwa vilabu Afrika nzima.Yaani ule mpira waliocheza jana ndio huwa unampa ubingwa Al Ahly ya Misri,Unacheza kwa malengo sio tu ilimradi na kiwango kile naiona Simba ikifika mbali sana tena ikiwezekana hata kombe watachukua.

Halafu mnaombeza Fadlu Davis kwa kumuacha nje Mukwala na kumuingiza Valentino Mashaka naomba niwaambie ukocha ni taaluma na watu wanasomea kwahiyo muacheni Mtaalamu Fadlu afanye majukumu yake kwa taaluma yake.
We jamaa Mpira tuliokuwa tunaangalia ndio huo uliangalia ama ulikuwa na WA kwako tofauti? Wachezaji ata kukaa na Mpira dk 1 ilikuwa shida wananyang'anywa na bado unasifia utumbo!
 
We jamaa Mpira tuliokuwa tunaangalia ndio huo uliangalia ama ulikuwa na WA kwako tofauti? Wachezaji ata kukaa na Mpira dk 1 ilikuwa shida wananyang'anywa na bado unasifia utumbo!
Kama huo utumbo waliocheza ndio ulifanya tukatoka suluhu ugenini basi ninaomba waendelee kucheza utumbo huo huo kila wakiwa ugenini ili tuendelee kupata suluhu ugenini.
Endelea kuangalia mpira hivyo hivyo ila wengine tunaangalia tofauti kwahiyo na maoni lazima yawe tofauti cha msingi tu jifunze kuheshimu hoja na maoni ya wenzako ili nawe maoni na hoja zako ziheshimiwe.
 
Simba Sports Club pamoja nakuwa na kundi kubwa la wachezaji wapya pamoja na benchi la ufundi jipya kabisa lakini bado wameonyesha kuwa wao ni timu namba moja kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Namba 6 kwa ubora kwa vilabu Afrika nzima.Yaani ule mpira waliocheza jana ndio huwa unampa ubingwa Al Ahly ya Misri,Unacheza kwa malengo sio tu ilimradi na kiwango kile naiona Simba ikifika mbali sana tena ikiwezekana hata kombe watachukua.

Halafu mnaombeza Fadlu Davis kwa kumuacha nje Mukwala na kumuingiza Valentino Mashaka naomba niwaambie ukocha ni taaluma na watu wanasomea kwahiyo muacheni Mtaalamu Fadlu afanye majukumu yake kwa taaluma yake.
Sahihi kabisa, tujue kuheshimu taaluma za watu. Pamoja na kwamba mimi pia sikukubaliana na kutolewa nje kwa Atebe, lakini nimekaa kimya kwa kuwa kuna kitu alikiona. Kwa jinsi walivyokuwa wanacheza wale waarabu, angeweza kuumia tukamkosa mechi muhimu ya marudiano.

Hata kuachwa nyumbani kwa Chasambi inawezekana ni mkakati maalumu maana safari ni ndefu na wachezaji watakuwa na uchovu, utahitaji watu ambao wataipa uhai timu.

Ukitaka kujua matokeo ni mazuri au mabaya kwa Simba, jiulize Al Ahly walikuwa wanataka matokeo gani na je waliyapata?
 
Mpira una namna nyingi zakuangalia au
kishabiki
kifurukutwa
kinazi
kinafiki
kiufundi
n.k
Sasa sijui wewe uliangalia mpira kwenye namna ipi hapo?
Michuano ni CAF CONFEDERATION CUP KNOCK OUT STAGE halafu mechi ya kwanza ugenini kat ya mechi mbili zitakazoamua timu ya kwenda GROUP STAGE wewe kwa utaalamu wako ulitaka Simba Wachezeje?
Majibu yatapatikana Dar tuvute subira, mchezo wa kutegemea kushinda nyumbani umeshapitwa na wakati, nakukumbusha tu kuwa Simba ilitoa sare na power dynamos ya 1-1 kwa Mkapa na UD Songo ilimtoa Simba hapo hapo kwa Mkapa.
 
Sahihi kabisa, tujue kuheshimu taaluma za watu. Pamoja na kwamba mimi pia sikukubaliana na kutolewa nje kwa Atebe, lakini nimekaa kimya kwa kuwa kuna kitu alikiona. Kwa jinsi walivyokuwa wanacheza wale waarabu, angeweza kuumia tukamkosa mechi muhimu ya marudiano.

Hata kuachwa nyumbani kwa Chasambi inawezekana ni mkakati maalumu maana safari ni ndefu na wachezaji watakuwa na uchovu, utahitaji watu ambao wataipa uhai timu.

Ukitaka kujua matokeo ni mazuri au mabaya kwa Simba, jiulize Al Ahly walikuwa wanataka matokeo gani na je waliyapata?
Umeanza kuelewa mpira ndugu yangu,Kwani unadhani Fadlu hajui Mukwala ni bingwa wa kuifanya Pressing? lakini bado aka opt kumchezesha Valentino Mashaka? Mechi za mtoano zina hesabu za dakika 180 sio dakika 90 kwahiyo jana ilichezwa mechi huku kichwani kukiwa na mawazo ya mechi ya marudiano.
 
Simba Sports Club pamoja nakuwa na kundi kubwa la wachezaji wapya pamoja na benchi la ufundi jipya kabisa lakini bado wameonyesha kuwa wao ni timu namba moja kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Namba 6 kwa ubora kwa vilabu Afrika nzima.Yaani ule mpira waliocheza jana ndio huwa unampa ubingwa Al Ahly ya Misri,Unacheza kwa malengo sio tu ilimradi na kiwango kile naiona Simba ikifika mbali sana tena ikiwezekana hata kombe watachukua.

Halafu mnaombeza Fadlu Davis kwa kumuacha nje Mukwala na kumuingiza Valentino Mashaka naomba niwaambie ukocha ni taaluma na watu wanasomea kwahiyo muacheni Mtaalamu Fadlu afanye majukumu yake kwa taaluma yake.
Hata Robertinho na Benchika walisomea ukocha na ni taaluma zao.

Lakini mliwatimua.
 
Kwa mtizamo wangu naona Simba walicheza kimkakati zaidi na walifanikiwa sana kwani walikuwa ugenini. Lakini hili lisiwafanye wabweteke kwani hata hao walibya watakuja kimkakati kwa hiyo Simba wawe makini sana. Simba wajue kabisa jamaa wakipata goli moja hapa wao watatakiwa wapate mawili.

Pia benchi la ufundi liwe linafanya sub mapema. Kwa mfano Balua ile mechi ilimshinda mapema sana ilitakiwa abadilishwe mapema baada ya dakika 30 tu. Na sio ajabu kwani taratibu tu atazoea hizo mechi za kimataifa. Kwenye benchi walikuwepo Kibu na Mukwala ambao wana uzoefu na mechi za kimataifa wangeweza kuwa msaada kwa timu. Pia Mutale aelekezwe acheze kitimu zaidi aache anao anao mpaka anapoteza mpira hovyo.
 
20240802_131306.jpg
 
Majibu yatapatikana Dar tuvute subira, mchezo wa kutegemea kushinda nyumbani umeshapitwa na wakati, nakukumbusha tu kuwa Simba ilitoa sare na power dynamos ya 1-1 kwa Mkapa na UD Songo ilimtoa Simba hapo hapo kwa Mkapa.
Ni kweli kabisa hayo uliyoyasema lakini mbona umechagua hayo tu vipi kuhusu comeback ya Nkana Red Devils pale LUPASO au vipi alivyoshinda home and away dhidi ya premiro de Agosto tena kocha akiwa Juma MGUNDA?

Mechi za kimataifa za Afrika tena hasa hizi za Vilabu zinachezwa nje ya uwanja zaidi ya Uwanjani kwahiyo kile unachokiona uwanjani ni maokeo ya mipango na maandalizi makubwa ya kukwepa na kuzuia hujuma mbalimbali kutoka kwa timu mwenyeji.Al Ahly hajatawala soka la Afrika kwa kuwa na timu nzuri kiwanjani tu fuatilia namna navocheza mechi zake za home na away halafu pia angalia mipango na maandalizi yake anapokuwa anaenda away utajifunza kitu kuhusu soka la Afrika.
 
Kwa mtizamo wangu naona Simba walicheza kimkakati zaidi na walifanikiwa sana kwani walikuwa ugenini. Lakini hili lisiwafanye wabweteke kwani hata hao walibya watakuja kimkakati kwa hiyo Simba wawe makini sana. Simba wajue kabisa jamaa wakipata goli moja hapa wao watatakiwa wapate mawili.

Pia benchi la ufundi liwe linafanya sub mapema. Kwa mfano Balua ile mechi ilimshinda mapema sana ilitakiwa abadilishwe mapema baada ya dakika 30 tu. Na sio ajabu kwani taratibu tu atazoea hizo mechi za kimataifa. Kwenye benchi walikuwepo Kibu na Mukwala ambao wana uzoefu na mechi za kimataifa wangeweza kuwa msaada kwa timu. Pia Mutale aelekezwe acheze kitimu zaidi aache anao anao mpaka anapoteza mpira hovyo.
Kweli ndugu yangu umeongea jambo lenyewe kabisa lakini kama Kocha unakuwa na Game Plan yako kwahiyo hata mchezaji akikosea mara mbili mara tatu ndani ya muda mfupi huwezi tu kumfanyia mabadiliko lazima uwe na subra na umuelekeze ili arudi mchezoni na kukupa ile faida uliyoikusudia.Mie namuelewa Fadlu kwanini alichelewa kufanya sub japo kuna watu walikuwa wako ovyo kimchezo lakini bado timu ilikuwa kwenye shape nzuri kiufundi na bado haikuruhusu goli.
 
Hata Robertinho na Benchika walisomea ukocha na ni taaluma zao.

Lakini mliwatimua.
COACHES ARE HIRED TO BE FIRED
Hamna kocha atafundisha timu milele,hata Guardiola aliondoka Barcelona.Makocha wengi wanafukuzwa Tanzania kwasababu timu zetu zote haziamini katika kitu kinaitwa PROJECT.Yaani kiufupi ni kwamba wanataka wakisajili leo wachezaji wapya na wakaleta kocha mpya basi washinde kila kombe lililopo mbele yao bila kujali chochote.Bahati mbaya ni kuwa FOOTBALL haiko hivyo ila sema ndo soka letu kivyetu vyetu.
 
Umeanza kuelewa mpira ndugu yangu,Kwani unadhani Fadlu hajui Mukwala ni bingwa wa kuifanya Pressing? lakini bado aka opt kumchezesha Valentino Mashaka? Mechi za mtoano zina hesabu za dakika 180 sio dakika 90 kwahiyo jana ilichezwa mechi huku kichwani kukiwa na mawazo ya mechi ya marudiano.
Hahah. Nimeliona dongo lako eti "nimeanza kuelewa mpira" 🤣😂🤣

Wale mechi ya marudiano wanaenda kukutana na Simba tofauti kabisa na waliyocheza nayo jana. Tahadhari za ulinzi zitaendelea kuwepo ila tutafika saaana golini kwao. Hawajakutana na Awesu, Chasambi, Mukwala na hata silent killer Karabaka. Wanajua wana shughuli pevu ndiyo maana walipagawa.
 
Jana Al ahly kacheza na bingwa wa kenya Gor mahia.

Mechi imechezwa Kenya ila Al ahly kashinda goli 3 kwa 0.

Simba kacheza na timu ambayo sio bingwa wa Libya.. na simba hajapiga shot on target hata moja.

Unaanzaje kusema simba anacheza kama Al ahly. Huku Al Ahly huwa anafunga magoli ugenini
 
Back
Top Bottom