SI KWELI Simba SC wavunja mkataba na kocha wao Msaidizi, Selemani Matola, leo Oktoba 28, 2022

SI KWELI Simba SC wavunja mkataba na kocha wao Msaidizi, Selemani Matola, leo Oktoba 28, 2022

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
78991134.jpg

Yameibuka madai kwamba Simba SC imefikia uamuzi wa kuvunja mkataba na kocha wake msaidizi Selemani Matola.

Madai hayo yamechochewa na barua inayodaiwa kuandaliwa na Simba kusambaa mitandaoni.
 
Tunachokijua
Madai ya kuvunjwa kwa mkataba wa Kocha msaidizi wa Simba Selemani Matola zimeanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, leo Oktoba 28, 2022.

Mathalani, mtumiaji mmoja wa mtandao wa X ameweka ujumbe ukiambatana na picha ya tangazo la kufutwa kazi kwa kocha Matola.

JamiiForums imefanya mawasiliano na Meneja wa Kitengo Cha habari cha Simba (Ahmed Ally) ambaye amesema kuwa barua hiyo ni feki na wameamua kuipuuza.

img_20221029_161836_841-jpg.2401216

Ahmed Ally ameongeza kuwa kama taarifa hiyo Ingekuwa na ukweli basi ingepandishwa na kuwekwa wazi katika kurasa rasmi za klabu.

Selemani Matola aliwahi kuwa mchezaji wa Simba aliyepata mafanikio makubwa. Baada ya kucheza Soka Afrika Kusini kisha kustaafu, alijiunga na timu yake za Zamani kama kocha wa timu za vijana na sasa anahudumu kama kocha wa timu za vijana za Simba.
Back
Top Bottom