Amesema yeye ni mnyama lakini alikuwa anaiunga mkono team ya FC

mkuu crasshwie asante sana kwa updates na hapa kandambili tunamuombea njaa hadi mwisho, i mean hapa tunaloga hadi kipenga cha mwisho.
 

hahahhahaah!! Jamaa ni mnyama na hapa hakuna kumuonea mtu huruma kuanzia tp mazembe hadi mafisadi.
 
Wakuu salama?
Najua hivi sasa tupo kwenye maandalizi mazito ya kuwaua mamba wa maembe wikiendi hii na kwa uwezo wa mungu na ari na uwezo wa wachezaji wetu naamini tutapata matokeo mazuri wikiendi

SWALI langu NI kuwa ni takribani miezi sita sasa tangu uongozi wetu ulivyotuambia juu ya ujenzi wa sports complex kule bunju, je kuna yeyote mwenye updates? Labda yule mkandarasi mshauri amekuja, tathmini ya uwanja imefanyika au na.. ?

Simba oyee!!! nguvu moja daima
 
ili tuwe mabingwa ni ku win mechi 2 tu na Azam ili ashiriki mechi za kimataifa inabidi amfunge yanga halafu akomae ashinde mechi zilizosalia kwa idadi nzuri ya magoli. simba na azam ndio zenye washambuliaji hatari kuliko timu yoyote msimu huu
 
Hivi bado hawajacheza tu i mean simba na mazembe
 
hawajacheza bado, kesho ndio wanashuka dimbani. Tunaomba maombi yenu wakuu.
 
TP mazembe wanashuka dimbani kesho kuikabili simba huku wachezaji wake wakionyesha kusumbuliwa na uchovu baada ya kucheza mechi nyingi msimu huu.
Source:mwanaspot.co.tz
 
TP mazembe wanashuka dimbani kesho kuikabili simba huku wachezaji wake wakionyesha kusumbuliwa na uchovu baada ya kucheza mechi nyingi msimu huu.
Source:mwanaspot.co.tz

Acha watanzania wajipe matumaini. Huo uchovu ndio uliowapa Sofapaka burungutu la 9 - 0 kutoka kwa hao TP Mazembe.
Kila la heri Simba. Ila mfahamu kwamba mna kazi kubwa sana hasa ukizingatia hamjapata international friend match hata moja, na mechi ya mwisho ilikuwa dhidi ya AFC ya Arusha. So kuna dalili za wazi za kifungwa kuliko vinginevyo.
 

mkuu hapa hakuna wasiwasi wowote,hawa TP mazembe mpaka sasa hivi tushawapiga , wachezaji wetu wapo fit kisaikologically na fizikali...hawa TP nimeangalia website zao wanatuogopa sana kutokana na historia yetu,, wanajua tushawahi kuwapiga Zamaleki...wao wenyewe wanajua kuwa mziki wetu si wa kitoto kabisa.
 

Mkuu, kama kweli hayo unayoongea ndo yapo vichwani mwa wachezaji wa Simba na viongozi wao, basi mtafungwa vibaya sana maana inaonyesha wazi wameshawafunga kisaikolojia pia. Yaani kweli unathubutu kuamini kinachoandikwa ktk web yao? Eti muziki wetu sio wa kitoto, kwa kutoka sare na Yanga na kuifunga AFC mbili bila??? Hivi kweli na wewe unaamini Mazembe wanawaogopa??? Yaani kuitoa Zamalek miaka kibao iliyopita ndio cha kuwatisha TP? Pole sana mkuu najua wewe ni mmoja wa watanzania walioathirika vibaya na soka la mdomoni, ila maandalizi ZERO! Tusubili tuone "MZIKI " wenu kesho ila usipotee kesho, uje tena hapa
 

wewe ni mkongo nini? Sijui kitu gani unakishangilia hapa.. Wewe unafikiri TP mazembe hatuwezi kuwafunga?wewe kuna siku ulishawahi kufikiria kuwa kuna timu ya africa ambayo ingeweza kuifunga Internacional ya Brazili? But TP mazembe waliwafunga hawa jamaa.. Sasa sisi kwa nini tusiwafunge TP mazembe? Mpira unadunda na hawa kesho tunawapiga .. Timu yetu ipo fit sana and dont undermine it kwa kuqoute mechi na AFC Arusha.. Sisi international tupo juu sana na tuna historia ya kwenda mbali. Na bila shaka wewe ndugu yangu utakuwa ni kandambili ndio maana unaloga hapa na kesho utafunga mdomo wako.
 
www. mwanaspoti.co.tz/wcreadnews.php?id=6207

Simba wamesema sisi ni baruti ambayo itaivunja mwamba wa TP mazembe
 
Simba huenda wakatumia mtindo wa 4-5-1 kwa kuweka ukuta mzito wa kumzuia Dioko huku wakishambulia kwa kuwatumia watu wenye kasi kama OKWI na SAMATA ambao watapambana na mabeki Kritsho Kasusula na Joel Kimuaki
 
Kikosi kitakachoshuka kesho:
Juma kaseja, Haruna Shamte,Amir Mafta,Kelvin Yondani,Juma Nyosso,Jerry Santo,Rashid Gumbo/Niko Nyagawa,Patrick Ochan,Emanuel Okwi, Mbwana Samata,Amri Kiemba
 
Kikosi kitakachoshuka kesho:
Juma kaseja, Haruna Shamte,Amir Mafta,Kelvin Yondani,Juma Nyosso,Jerry Santo,Rashid Gumbo/Niko Nyagawa,Patrick Ochan,Emanuel Okwi, Mbwana Samata,Amri Kiemba

Hiki kikosi ni kwa mujibu wa mazoezi.
 
Zitto Kabwe na Idd Azan wapo kwenye msafara tuwaombee wote na kikosi chetu.
 
Kikosi kitakachoshuka kesho:
Juma kaseja, Haruna Shamte,Amir Mafta,Kelvin Yondani,Juma Nyosso,Jerry Santo,Rashid Gumbo/Niko Nyagawa,Patrick Ochan,Emanuel Okwi, Mbwana Samata,Amri Kiemba

Ktk lineup hiyo nadhani Kaseja kama vile kachuja .... bora golini akae Bathez
 
Ktk lineup hiyo nadhani Kaseja kama vile kachuja .... bora golini akae Bathez

offcourse nakubaliana na wewe lakini hii sio kikosi kamili ni cha mazoezini tu so kesho uwanjani anaweza kushuka bartez kama kawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…