Ulichosema mwanzo ni sahihi.
Sudani hadi sasa ana goal difference -2 kafungwa 5 kafunga 3.
Mazembe akimfunga Simba 3-0, Simba atakuwa wa goal difference 0 maana ana goal 4 na kafungwa 4.
Hivyo Mazembe atakuwa Bingwa kwakuwa na goal difference 2 kafunga 4 kafungwa 2.
Mazembe akimfunga Simba 2-0 atakuwa na GD 3-2 =1 na Simba atakuwa na GD 4-3=1 hivyo Mazembe anaweza kuwa Bingwa kwakuwa kamfunga Simba ktk mechi yao.
Karibuni kuchangia.
Naomba kuchangia hiyo aya ya mwisho, matokeo ya Simba kufungwa 2 - 0 moja kwa moja yanampa Ubingwa Simba. Nitaeleza.
Nianzie kwenye kanuni za mashindano kwanza:
Orodha ya ''viondoa mfanano'' (tie breakers) kwa mashindano haya viko kama ifuatavyo na vimepangwa kwa umuhimu yaani kinaanza kipi, kinafuata kipi (in order of preferences).
1. Goal differences
2. Head to head
3. Disciplinary performance
Huwezi kutumia kigezo cha pili kabla cha kwanza hakijashindwa kazi, vivyo hivyo huwezi kutumia cha tatu kabla ya cha pili hakijamaliza kazi yake.
1. Goal difference:
Hii ina sehemu mbili:
a)
Utofauti wa magoli ya uliyofunga dhidi ya yale uliyofungwa.
Mkifanana hapa, mnaangalia sehemu b.
b)
Idadi kubwa ya magoli ya kufunga.
Mfano; Mwenye magoli 2 ya kufunga na kafungwa 2 ana GD ya 0 Sawa na yule mwenye magoli 6 ya kufunga akiwa kafungwa 6.
Kwenye mazingira haya kigezo (1.a) hakitatoa mshindi, ila kigezo (1.b) kitampa faida huyu mwenye magoli 6.
Hivyo ni bora ufunge na kufungwa magoli mengi kuliko kufunga na Kufungwa magoli machache.
2. Head to head:
Hii nayo ina sehemu mbili:
a)
Matokeo ya jumla.
Aliyeshinda mechi baina yenu ndio anapata faida. Ikiwa mlitoka sare, kinaangaliwa kigezo b.
b)
Aliyetangulia kufunga goli mlipokutana.
Kama sare yenu ilikua ni ya magoli, basi kigezo hiki kitaamua mshindi.
NB: Sare ya 0-0 haitaamuliwa kwa kigezo hiki, tunaenda mbele....
3.
Nidhamu au disciplinary performance:
Ina sehemu mbili:
a)
Documented offences:
Hapa huwa wanaangalia kadi za njano na nyekundu, mwenye kadi chache anapewa ushindi.
Mkifanana hapa, wanaenda sehemu b.
b)
Undocumented offences:
Hapa wanaangalia idadi ya jumla ya madhambi (fauls) bila kujali kama kadi zilitolewa ama la. Aliyefanya madhambi machache anapewa ushindi.
NB: Hatutegemei mfanane hadi hatua hii, ikitokea hivi daaah itabidi turushe shilingi (natania, ila nayo inaweza kusimama).
Sasa tuje kwenye matokeo ya Mazembe 2 Simba 0. (Simba Bingwa).
GD watakua wanafanana wote wana +1.
Simba kafunga 4 kafungwa 3 wakati Mazembe kafunga 3 kafungwa 2.
Simba atakuwa bingwa kwa sababu ya sehemu ya pili ya kigezo hiki cha GD, kwa maana ya kwamba yeye ana magoli mengi ya kufunga 4.
Kwahiyo ni bora ufunge na kufungwa magoli mengi kuliko .....
Mazembe akishinda 3 Simba 1 (Simba Bingwa). Kivipi, njoo nayo;-
GD watakua wanafanana wote wana +1.
Simba kafunga 5 kafungwa 4 wakati Mazembe kafunga 4 kafungwa 3. Simba ana magoli mengi ya kufunga, anapewa ubingwa.
Mazembe akishinda 4 Simba 2 (Simba Bingwa kwa sababu tajwa hapo juu).
Nirudie kusisitiza:
''Bora ufunge na kufungwa magoli mengi kuliko kufunga na Kufungwa magoli machache''
Karibuni...