Simba tengenezeni timu acheni porojo zisizokuwa na maana

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Naona kuna kamjadala apa jukwaani kanakochagizwa na wajinga wachache ama kwa kutokuelewa au wanajua lakini wanapima kina cha maji, hii michezo ya timu pinzani kupewa motisha ya pesa kuikazia timu nyingine wahasisi wa hii michezo michafu ni simba.

Tunajua mwamed alitumia pesa nyingi nje ya bajeti kufanya hii michezo misimu iliyopita, rejea matukio ya wakina Makonda, rejea baadhi ya matukio mwadui anafungwa wachezaji wanalia baada ya kucheza jihad.

Sasa mi nafikiri kwakuwa wanaoleta nyuzi apa kilalamika kipindi kile walikuwa wanakenua na kufurahia basi ata sasa hivi wafunge midomo yao, mkuki kwa nguruwe, dawa ya moto ni moto ukicheka na kima utavuna mabua.
 
Kwamba simba ajenge timu ilihali utopolo timu ipo organized na ubingwa upo njenje mnakaribia kuubebelea si ndio? Ngoja baada ya mechi 10 kama hamtaanza kusema nabi hatufai apishe, yetu macho!
 
Huwezi linganisha kinachofanyika mwaka huu na kilichofanyika mwaka wowote ule
Mwaka huu kuna maagizo kabisa kwamba wachezaji wa simba kila mechi atleast wawili WAJERUHIWE VIBAYA IKIBIDI KUWA VILEMA

YAANI HADI MSIMU UNAISHA SIMBA ITAKUWA IMEBAKI NA WACHEZAJI WATANO WENYE AFYA NJEMA, HUO NDIYO UANA MICHEZO?

 
Kwamba simba ajenge timu ilihali utopolo timu ipo organized na ubingwa upo njenje mnakaribia kuubebelea si ndio? Ngoja baada ya mechi 10 kama hamtaanza kusema nabi hatufai apishe, yetu macho!
mwaka jana mechi mbili za kwanza , simba alitoa droo na mtibwa kwa shida akaifunga ihefu kwa shida maneno yaliyosemwa hayana tofauti na haya ya sasa , tofauti kubwa mwaka huu ni kwamba hizo pesa zinazoenda mikoani kupitia kwa wakuu wa mikoa mashabiki wa utopolo zina maagizo ya kuvunjavunja wachezaji wa simba
 
Huwezi linganisha kinachofanyika mwaka huu na kilichofanyika mwaka wowote ule. Mwaka huu kuna maagizo kabisa kwamba wachezaji wa simba kila mechi atleast wawili WAJERUHIWE VIBAYA IKIBIDI KUWA VILEMA...
Tunaomba tuwekeebvideo clip ya hayo maagizo. Kwahiyo Kagera sugar nao walivyokuwa wanawachezea Yanga rafu za kipumbavu walipewa maagizo?
 
Tunaomba tuwekeebvideo clip ya hayo maagizo. Kwahiyo Kagera sugar nao walivyokuwa wanawachezea Yanga rafu za kipumbavu walipewa maagizo?
utaendelea sana kusubiri hiyo video clip kaaa hapohapo usiondoke yaani badala ya kufurahia kwamba kila mechi lazima wachezaji watatu au wawili wa simba wajeruhiwe kwa pesa zinazombazwa na kale ka kikundi wewe unauliza video?

Kuna rafu ya kagera inakaribia uhuni uliofanyika Musoma na Dodoma?

Hayo mapesa yenu mwageni ila huo ujinga wa kutoa maagizo watu wavunjwe miguu na pua mmepitiliza sasa
 
Simba na Yanga ndo kawaida yao kutumia pesa nyuma ya panzia kama mgeni hili pole sana,Makonda aliwaahidi KMC waikazie ya Yanga msimu ule umesahau au wewe wa juzi kwenye hii game?
 
utaendelea sana kusubiri hiyo video clip kaaa hapohapo usiondoke yaani badala ya kufurahia kwamba kila mechi lazima wachezaji watatu...
Vitu ambavyo havina ushahidi ni kupoteza muda ligi ngumu hii pambaneni malalamiko waachieni CHADEMA
 
Tunaomba tuwekeebvideo clip ya hayo maagizo. Kwahiyo Kagera sugar nao walivyokuwa wanawachezea Yanga rafu za kipumbavu walipewa maagizo?
Wawachezee rafu gani wakati mliwapa muamala, mpaka wakawazawadia goli.

Hakuna beki anaweza fanya ujinga alioufanya beki wa Kagera siku ile, lile goli ni la Chupli chupli.
 
Pamoja nakuwajeruhi vibaya wachezaji wetu muhimu kina onyango, sacko, lwanga na kenedy juma, ila kina bwalya, inonga na duncan nyoni walionyesha uhalisia wa kikosi kipana!

japo uwanja mbovu duncan nyoni alionesha ladha ya pira biriani! shabalala na bwalya pia walijaribu kufanya mpira uvutie!

Sasa tunawafata waswana kwenye majuqumu ya kitaifa! wahapahapa waangalie champions league inachezwaje!
 
Wawachezee rafu gani wakati mliwapa muamala, mpaka wakawazawadia goli.

Hakuna beki anaweza fanya ujinga alioufanya beki wa Kagera siku ile, lile goli ni la Chupli chupli.
Na yule beki wa biashara aliyefanya upumbavu wa kumchezea rafu Sakho wakati alikuwa anauwezo wa kucheza ule mpira, je mlimlipa kiasi gani? Usipende kutumia hisia kwa makosa binafsi ya wachezaji wa timu kwa kujumuisha kuwa wamepewa pesa. Tumia akili usiendeshwe na mihemko
 
Kuna hujuma nyingi zinafanyika kwa timu yetu ya Simba,muda utasema.
 
Yaani leo Simba ndio wamegeuka wa kulalamika lamika hujuma. Kweli maisha yanaenda kasi sana.
Team kupewa maelekezo ya kuvunja wachezaji wa simba siyo hujuma? ile jana ni rasharasha nasikia wamegombezwa baada ya kuonekana watu hawajavunjika vizuri, unatka tusilalamike? yaani plan ni kwamba hadi mwisho wa msimu simba isiwe na wachezaji fit zaidi ya watano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…