Simba tuache Wivu, Mafanikio ya Yanga yawe chachu kwetu

mwarabu feki

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2023
Posts
811
Reaction score
1,811
Kila mtu anajua kuwa Mmii mwarabu feki ni shabiki wa kutupwa wa Mnyama Simba S.C na Hilo nimelithibitisha Kwa nyuzi zangu nyingi humu jamvini.

Kitendo cha Yanga kutinga nusu fainali ya michuano hii mikubwa barani Afrika ni jambo ambalo kila mtanzania anapaswa kujivunia.

Wanasimba wengi wamechukizwa na mafanikio haya ya Yanga bila sababu yoyote ya msingi zaidi tu ni wivu.

Niwasihi Wana lunyasi wenzangu wakiongozwa na popoma GENTAMYCINE tusiwaonee gere Hawa ndugu zetu utopolo na badala yake tujifunze kufanikiwa kimataifa kupitia wao.

 
Kila mtu anajua kuwa Mmii mwarabu feki ni shabiki wa kutupwa wa Mnyama Simba S.C na Hilo nimelithibitisha Kwa nyuzi zangu nyingi humu jamvin...
Huku siku hizi mpaka wapumbavu mnajiona great thinkers

Form two aliyefeli anataka form six ajifunze kwake.

Yanga klabu bingwa iliwashinda Simba akabaki Hadi robo fainali, leo Unataka Simba ajifunze kwa aliyefeli.

HATUJIFUNZI KWA WALIOFELI NA KIPAUMBELE CHETU SI KOMBE HILO LA WALIOFELI.

Simba Ni timu ya MALENGO makubwa.
 
Ni Wivu tu[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Chungu lakini ni dawa [emoji847]
 
Mwaka jana mlikua kwenye kikombe cha waliofeli. Je mlifika wapi mkuu?? Acheni wivu kwenye uhalisia muwe wawazi tu kama yanga wamepiga hatua moja mbele kutoka mlipoishia.
 
Siwezi kujifunza kwa aliyekwama, tusifundishane ujinga tafadhali.
 
Siwezi kujifunza kwa aliyekwama, tusifundishane ujinga tafadhali.
Kumbuka pamoja na kuroga timu yetu ya Simba ilishindwa kuvuka hii hatua Mwaka Jana, tukaondoshwa na Orlando pirates, tuache Wivu
 
Form two wa halali ni bora kuliko form six wa jina la kununua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…