Simba tunahitaji uniform kutoka Puma, Adidas, Nike au umbro kwa hatua hii Dewji usituangushe

Simba tunahitaji uniform kutoka Puma, Adidas, Nike au umbro kwa hatua hii Dewji usituangushe

Tushaingia level ingine mo tafadhali na bodi yako kaeni. Hatupaswi kuvaa jezii brand ambazo hazina jina hapa duniani.
Hatutaki vijora[emoji196][emoji196][emoji196][emoji196]
IMG-20210223-WA0100.jpg
 
Badala ya kuihimiza Simba itengeneze jezi zake hapa nchini ili iongeze kipato na kutoa ajira kwa watanzania wewe unawaza mambo ya aibu!!!
===
TUJITEGEMEE.
Acha kuwa na akili za kisukuma sio kila kitu lazima ufanye mwenyewe.

Leo hii spotpesa akianzisha mashindano timu zinacheza mpaka na timu za England.

Sasa kama mdhamini akiwa Abood si utacheza na timu za Moro.
 
Badala ya kuihimiza Simba itengeneze jezi zake hapa nchini ili iongeze kipato na kutoa ajira kwa watanzania wewe unawaza mambo ya aibu!!...
Acha ushamba wewe, dunia hii tunategemeana wewe unafikiri real Madrid anapovaa brand ya Adidas toka Germany ameshindwa kutengeneza brand yake? Tuondolee akili za ccm hapa
 
Vizuri! Kampuni hizi mfano;- Adidas, Puma, Nike, Umbro, Kappa na Lotto hutoa mikataba yenye fedha kuvaa jezi yenye nembo/iliyotengenezwa na mhusika.

Arsenal kupitia Adidas wanapokea billioni 112 na millioni 68 kila mwaka, kwa miaka mitatu.

Klabu husika inaweza kuomba kupitia tovuti rasmi za kampuni hizi, timu na jopo la wahusika watafanya assessment ya chapa ya klabu husika na kuipa thamani (value) na kuingia mkataba.

Jukumu la ubunifu, mauzo na kulinda chapa linakiwa chini yao, timu husika ikipokea pesa zilizoanishwa katika mkataba.
 
Wanaweza kutengeneza tatizo, Watanzania wengi hatuwezi kununua hizo jezi (ni bei ghali) na wao kama wawekezaji watapata hasara badala ya faida jambo ambalo hawapendi na linawakwaza kutowekeza!
 
wanaweza kutengeneza tatizo Watanzania wengi hatuwezi kununua hizo jezi ( ni bei ghali) na wao kama wawekezaji wapata hasara badala ya faida jambo ambalo hawapendi na linawakwaza kutowekeza!
Wewe ndio umeongea la maana. Akina MO ni wafanyabiashara na wanatafuta faida. Kwahiyo wakipiga hesabu zao za ROI na hali halisi ya mtaani wanaona bora walete mafekelo na matambara ili tununue tufurahie na wao waingize faida. Hakuna mswahili wa kununua jezi ya laki tatu!
 
Wewe ndio umeongea la maana. Akina MO ni wafanyabiashara na wanatafuta faida. Kwahiyo wakipiga hesabu zao za ROI na hali halisi ya mtaani wanaona bora walete mafekelo na matambara ili tununue tufurahie na wao waingize faida. Hakuna mswahili wa kununua jezi ya laki tatu!
Ni kweli Mkuu, mfano Jezi ya Mamelodi Sundowns inauzwa Takribani Laki 180,000 hadi 200,000/= TZS ni Watanzania wachache watakaoweza kununua hiyo jezi hivyo Mwekekezaji atakosa faida. Hizi za Yanga ni elfu 35,000 hadi 50,000 lakini bado Mashabiki wanalalamika kwamba ni bei ghali!
 
Ni kweli Mkuu Mfano Jezi ya Mamelodi Sundowns inauzwa Takribani Laki 180,000 hadi 200,000/= TZS ni Watanzania wachache watakaoweza kununua hiyo jezi hivyo Mwekekezaji atakosa faida . Hizi za Yanga ni elfu 35,000 hadi 50,000 lakini bado Mashabiki wanalalamika kwamba ni bei ghali!
Sisi uwezo wetu ni kati ya 5000 mpaka 20000. Zaidi ya hapo utatafuta wateja kwa darubini.

Sasa kwa bei hiyo ili mwekezaji+mfanyabiashara wa jumla+mfanyabishara wa rejareja+machinga muuza jezi wooote wapate faida na bei iwe kati ya 5000-20000 inabidi walete jezi zenye ubora mdogo au feki kabisa ili apate faida. Nahisi hizi ndio hesabu za Mo. Ila ulete nike na adidas jezi moja laki tatu, yaani mteja hupati.
 
Hicho kitu kwa Sasa sioni kikitekelezeka kwa sababu zifuatazo.

1) Wakati wa magori akiwa ceo, hao umbro walikuja na dili la kwamba tuwe tunanunua jezi kwao kwa mkataba wa kwanzA..Kisha Simba waje waziuze wenyewe wakati wao wakimonitor uuzwaji wa jezi na soko, Ili mkataba wa pili waone wanaingia dili la aina Gani Kati ya kuwapa simba pesa Kisha wao wauze jezi ama waendelee na kuwauzia simba..dili hilo likafa kwa sababu Simba haikuwa tayari kutoa pesa ..( kumbuka huu ndio mfumo wa kampuni zote hapo ulizotaja zinapotaka kuingia mkataba na timu ndogo na timu za Kati katika soko la Dunia na kikanda)

2) Sababu ya pili ni kwamba mwenye tenda ya jezi za Simba kwa Sasa pia ni mkurugenzi wa bodi ya klabu, ndugu Kassim Dewji upande wa mwekezaji, so utaona ni kwa namna Gani ni ngumu yeye kuacha dili hilo, kwani kwa jinsi ilivyo yeye ni wakala wa kampuni ya uhlsports kwa Tanzania na pengine hatuwezi jua inawezekana kala dili kwa niaba ya simba Kisha akija huku anasema yeye ni msambazaji na wakala.

3) Kwa kuzingatia hoja ya kwanza, ambapo Simba haipo tayari kutoa pesa kununua jezi za hayo makampuni kwa kipindi hiki na wao wangetaka kulipwa (kwa mujibu wa magori kipindi Simba wanasign mkataba na uhlsports ) Romario LTD (Kassim Dewji) ambao ndio wasambazaji wa Uhlsports wanaipa simba pesa Kama sehemu ya udhamini , kwa mujibu wa watu wa ndani Kassim anawpaa Simba tsh 2500 - 3000 kwa kila jezi inayouzwa.

So kumalizia kwa mujibu wa hoja hizo tatu..haswa ukizingatia hoja ya pili ambapo ndani yake Kuna kaundugu ni kwamba usijeukatarajia Simba Sc itavaa jezi zingine nnje ya hizo ambazo wanavaa hivi Sasa. Ukiona wamebadilisha ujue Romarioa kaachana na Uhlsports kaamia kwa watengenezaji wengine wa jezi
 
Ni kweli Mkuu Mfano Jezi ya Mamelodi Sundowns inauzwa Takribani Laki 180,000 hadi 200,000/= TZS ni Watanzania wachache watakaoweza kununua hiyo jezi hivyo Mwekekezaji atakosa faida . Hizi za Yanga ni elfu 35,000 hadi 50,000 lakini bado Mashabiki wanalalamika kwamba ni bei ghali!
Bro unajua kuwa , hizo kampuni pia zinaweza kutengeneza jezi za qualty ya chini Ili kuendna na soko husika!?

gormahia pale kenya wanavaa umbro Kama sikosei, fc leopard ya kenya wanavaa Puma ama umbro na wao..ni kwamba wakenya na mashabiki zao wananunua jezi kwao dola 100? Ambayo ni sawa na zaidi ya laki Moja!?
 
Acha ushamba wewe .dunia hii tunategemeana wewe unafikiri real Madrid anapovaa brand ya Adidas toka Germany ameshindwa kutengeneza brand yake? Tuondolee akili za ccm hapa
Acha kuwa na akili za kisukuma sio kila kitu lazima ufanye mwenyewe
Leo hii spotpesa akianzisha mashindano timu zinacheza mpaka na timu za England
Sasa kama mzamini akiwa abood si utacheza na timu za moro
Copy and paste bila tafakuli!!!
Adidas anatafuta sehemu ya kuwekeza....! Ndiyo maana kulikuwa na mchuano mkali kupata tenda hiyo ya real madrid. Sasa mjipime ninyi ushamba wenu ni wa kiwango gani!
====
While the company did not release financial figures of the deal, they did dispute earlier reported figures that had the deal being worth as much as €1.8bn to the club.

The new deal will run through 2028, with their previous deal set to expire in 2020.

Adidas has found itself in a fight for the top clubs in Europe with both Nike and Puma in recent years.

 
Segere watachezewa Simba wakifika Misri si la dunia hii
 
Kwenye madili kama hayo nadhani inakuwa ngumu, maana Simba kama taasisi zipo kama nne na zina migogoro
 
Back
Top Bottom