tony92
JF-Expert Member
- Jul 17, 2013
- 2,398
- 3,691
Mkuu acha uongo boxer amecheza mechi nyingi katika nafasi ya beki wa kulia na huyo Gyan akiwa singida hajawahi kucheza namba 2 .Ukiacha utaahira utakuwa wa maana zaidi..ruvu wameingia full mkoko ila beki yao ya kulia ambayo ni tegemezi tariq abey hajaonekana kuwa bora leo,pia mtu kama abal kasim anaonekana hana ubora leo..
Kwa kigezo hicho kocha mkwasa anawatoa hata kipindi cha kwanza hakijaisha,kwa akili yako unadhani kama ingekuwa match fixing wangewatoa wachezaji tegemezi!??.
Juzi alianza full beki kulia boxer ambaye huwa haanzi,beki wa singida tegemezi ni gyan alieingia kipindi cha pili.
Pia wawa alianzia benchi,ulijiuliza kwanini???
Timu ya ruvu huwa hawawaheshimu simba hata siku moja,hawajawahi kujilinda dhidi ya simba,ila wakicheza ba yanga mara zote huwa wanapaki basi kwa kuwa wanawaheshimu yanga.
N.b ukicheza na timu yenye uwezo wa kumiliki mpira,na wachezaji wake wana uwezo na spidi kama simba au yanga na azam ukitaka pishana nao lazima..narudia LAZIMA ufungwe tuu.
Unaposema Wawa hajaanza mbona ni mechi ya 4 ya singida Wawa haanzi .
Tunafwatilia mpira vizuri huwezi tudanganya kirahisi hivi.
Hakuna kitu kinaitwa match fixing Tz ni upumbavu tu wa mashabiki kulinganisha kua wakiona timu imetoa draw na Simba basi wanaamini Yanga nayo atatoa nayo draw.