Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,501
- 28,711
Simba mchakato wao mzuri ila wamekwama walipokuwa wanaupeleka haraka kuna hatua wameziruka
Na inaonesha Simba walipokuwa wanabadili mfumo wao na kuwa wa hisa, walikuwa wamemlenga moja kwa moja Mo na sio wawekezaji mwingine na ndio maana wakaweka mpaka vipengele vya muwekezaji lazima awe mwanachama wa simba na amewahi kuisaidia simba. Sasa najiuliza kwa mfano Dangote au tajiri yeyote kutoka nje ya nchi akavutiwa kuwekeza kwenye timu ya simba basi atakosa hiyo nafasi kwa sababu sio mwanachama wa Simba na hajawahi kuisaidia Simba.
Simba walianza vizuri lakini haraka haraka ndio iliowaponza, walimuhitaji zaidi Mo kuliko mfumo wenyewe.
Bila kutumia akili vizuri huwezi kuona ni wapi tatizo lipo, na mchawi ataendelea kutafutwa tu mara waziri mara kilomoni mara shaffih, kumbe tatizo lipo kwengine.
Hakuna asiyependa Simba isonge mbele lakini kwenye huu mfumo wamejikwamisha wenyewe. Inabidi wakae chini waangalie wapi wamekosea na kurekebisha. Ikiwezekana wakae na Kilomoni waeleweshane na kumaliza yote. La sivyo kila mtu watamuona mbaya.
NB: FIFA haitaingilia mgogoro wowote wa Timu au Shirikisho la soka ambalo limeenda kinyume na sheria za nchi - TUNAKUMBUSHANA TU!!
Na inaonesha Simba walipokuwa wanabadili mfumo wao na kuwa wa hisa, walikuwa wamemlenga moja kwa moja Mo na sio wawekezaji mwingine na ndio maana wakaweka mpaka vipengele vya muwekezaji lazima awe mwanachama wa simba na amewahi kuisaidia simba. Sasa najiuliza kwa mfano Dangote au tajiri yeyote kutoka nje ya nchi akavutiwa kuwekeza kwenye timu ya simba basi atakosa hiyo nafasi kwa sababu sio mwanachama wa Simba na hajawahi kuisaidia Simba.
Simba walianza vizuri lakini haraka haraka ndio iliowaponza, walimuhitaji zaidi Mo kuliko mfumo wenyewe.
Bila kutumia akili vizuri huwezi kuona ni wapi tatizo lipo, na mchawi ataendelea kutafutwa tu mara waziri mara kilomoni mara shaffih, kumbe tatizo lipo kwengine.
Hakuna asiyependa Simba isonge mbele lakini kwenye huu mfumo wamejikwamisha wenyewe. Inabidi wakae chini waangalie wapi wamekosea na kurekebisha. Ikiwezekana wakae na Kilomoni waeleweshane na kumaliza yote. La sivyo kila mtu watamuona mbaya.
NB: FIFA haitaingilia mgogoro wowote wa Timu au Shirikisho la soka ambalo limeenda kinyume na sheria za nchi - TUNAKUMBUSHANA TU!!