Simba wana kibarua kigumu mbele ya KMC

Hongereni wote kwa kupasha kiporo chenu kikapashika.

Sapta Sapta sweetlee brave one Mtoto halali na hela na wengineo wengi
Kwa niaba ya Wanamsimbazi napokea pongezi hizo na nachukua fursa hii kukualika Jumapili pale kwa Mchina wakati tutakua tunahitimisha safari ya Nkana Red Devils kwenye michuano ya msimu huu ya CAF Champions League

Kama itakupendeza unakaribishwa kuunga mkono juhudi za Lunyasi na utapokelewa kwa kupewa kadi yenye picha ya Simba anaehaha kutafua mawindo
 
Shadeeya hebu tupe pongezi na zawadi ya ushindi pia

Ila kama anavyosemaga naniliu kua msema kweli ni mpenzi wa Mungu....wale watoto KMC waliniweka roho juu hasa dakika za mwisho...walitaka kutuvunjia heshima wale
Baada ya kumtoa Salamba, Haruna na Rashid Juma wakapoteana kabisa. Nna wasiwasi na uwezo wa kocha kuusoma mchezo. Kingebaki kile kikosi kingepata bao la tatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…