Simba wataendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu

Simba wataendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu

DITOPILE WAPILI

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2015
Posts
384
Reaction score
261
Klabu ya Simba itaendelea kuwa kichwa cha Mwendawazimu, kufungwa na kutofanya vizuri katika michuano ya Afrika iwapo itaendelea kushikiria akili na tamaduzi hizi,

Taarifa zinasambaa Papy Kambamba Tshishimbi anaondoka Yanga kuelekea Simba, taarifa hii imesambaa kwenye vyombo vya habari, pia post iliyotumwa na mchezaji wa SIMBA Ibrahimu Ajibu inaashiria Tshishimbi atatua SIMBA.

Kama kweli Simba inataka kufanya vizuri inabidi kuachana na wachezaji wa viwango vya kati, watafute mchezaji mkubwa kwa ajili ya kwenda kushinda mataji makubwa ya Afrika.

Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana, naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake.

Timu inahitaji wachezaji kama watatu (3) wakubwa, wanao cheza ligi na mashindano makubwa sio wachezaji wa wakujaribu jaribu.

Timu inasajiri wachezaji kiushabiki halafu wanakuwa hawana msaada kwenye mashindano kwenye mashindano makubwa.

Kama hizi taarifa za Tshishimbi kusaini Simba ni kweli basi kwenye bodi ya Simba kuna tatizo kubwa sana. Ni muda mrefu sana Simba ilikuwa inaongoza ligi hivyo kuwa na uhakika wa kushiriki michezo ya kimataifa kwa sababu hiyo ilitakiwa mpaka sasa iwe tayari imeshamaliza usajili wake kitambo sana. Sasa tetesi hizi za usajili mara Morison mara Tshishimbi inaelekea tatizo la mwaka jana la usajili bado halijatafutiwa ufumbuzi. Tshishimbi namkubali sana kwenye ligi ya ndani lakini kutokana na umri wake, majeraha ya mara kwa mara na kiwango chake kupanda na kushuka mara kwa mara sidhani kama ni wakati sahihi sasa kwa Simba kumsajili. Iwapo Simba wangemsajili Tshishimbi miaka miwili mitatu iliyopita kweli ningewasifu kwani wakati ule jamaa alikuwa moto wa kuotea mbali.

Simba kwa sasa inahitajika kusajili wachezaji wakupambana kwenye ligi ya mabingwa Afrika.Kwa mtizamo wangu mimi sioni kama Tshishimbi atakwenda kuongeza kitu kipya Simba. Simba ni timu kubwa sana kusubiri mpaka Yanga wawafanyie "scouting" ya wachezaji ni aibu sana. Hivi siku zote huwa najiuliza wale viongozi wa zamani wa Simba waliowaleta akina Okwi, Mafisango, Joseph Owino, Pawasa, Emmanuel Gabriel, Mbwana Samata n.k. si bado wapo . Viongozi wa sasa wasione aibu waende tu wakawaulize walikuwa wanafanyaje kuwapata wachezaji stahiki wenye viwango vya kuchezea Simba kuliko kuanza kuokota mara Tshishimbi au kuanza kugombana na Yanga juu ya mchezaji wao mpya mwenye kiwango Morisson.

Hivi viongozi wa Simba wameshajiuliza kuwa kuna wakina Morisson na Luis wangapi ambao hawana namba za kudumu kwenye timu kubwa za Afrika Kusini tu achilia mbali timu nyingine kubwa za Afrika ambazo zinajua nini maana ya "scouting"?. Nendeni mkawakusanya hao vijana kama wanne au watano hivi nina hakika mtatengeneza timu tishio Afrika ndani ya miaka miwili/mitatu tu. Wachezaji waandamizi wenye umri mkubwa wapo wa kutosha Simba ni wakati sasa wa kusajili vijana wenye vipaji na kiu ya mafanikio na matokeo yataonekana ndani ya muda mfupi.
 
"Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake'"

Simba ni timu kubwa, Tshimbimbi kabamba ni mchezaji mkubwa hapa kila upande naona utanufaika kama ni kweli
 
"Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake'"

Simba ni timu kubwa, Tshimbimbi kabamba ni mchezaji mkubwa hapa kila upande naona utanufaika kama ni kweli
Simba ina rasilimali nyingi tu lakini wanashindwa kuzitumia mnazijaza stoo tu zipigwe na vumbi. Fraga mchezaji mzuri sana lakini wanamsugulisha benchi, Mlipili sijui kipi kawakosea Simba, Ajib na Gadier kwenye ubora wao Yanga, kwenda Simba wamekuwa wachezaji wa kawaida kabisa wanaozea benchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake'"

Simba ni timu kubwa, Tshimbimbi kabamba ni mchezaji mkubwa hapa kila upande naona utanufaika kama ni kweli
Kuna watu wanaona kama wengine hawatumii akili. Simba sio mtu ni taasisi tena vichwa. Wakidhani weo wanaweza kufikiria zaidi ya Board ya Simba wanajidanganya. Halafu hao wachezaji wakubwa unajua thamani zao? Wale sio kuku tu unaenda kuchukua sokoni. Kwa hiyo Simba inajua imchukue nani kwa ajili ya nini na kwa budget ipi.
 
Uchebe aliwahi kusema ili simba ifanikiwe inabidi iwaondoshe waongo na watu wasio kuwa na elimu kwenye nafasi za utendaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchebe yupo sahihi kabisa
Mo.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kutoa mapovu, Ukiona wanaenda kinyume na wewe nunua timu yako uendeshe unavyojua uwalete hao wachezaji wakubwa alafu acha maneno mbao inauzwa tena bei ya nyanya kabisa
 
Ya Simba waachie Simba mnatakiwa mujadili mkataba wenu na GSM. Kwanini mambo 8 waliyoyataja kwenye barua yao leo HAYAPO KWENYE MKATABA WENU.

Kwenye mkataba wenu mlikubaliana nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dawa ni kuwasusia tunawapa vichwa sana tunavyojaa uwanjani Tshishimbi au Yondani sio wa kiwango cha kucheza hii Simba kumbuka Uchebe alimkataa hata yule beki wao tegemeo Lamini Moro ingawa aliletewa magarasa mengine.
 
"Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake'"

Simba ni timu kubwa, Tshimbimbi kabamba ni mchezaji mkubwa hapa kila upande naona utanufaika kama ni kweli
Ni kweli tumchukue huyo Tshishimbi na pia Morrison.
 
simba ni bora kama ingemsajili fei toto mwenye umri mdogo na muda mrefu wa kukijenga kikosi cha simba kuliko kumsajili mzee shishimbi ambae anenda kuongeza matata kwenye kikosi
 
"Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake'"

Simba ni timu kubwa, Tshimbimbi kabamba ni mchezaji mkubwa hapa kila upande naona utanufaika kama ni kweli
kwa hatua ilipo Simba sasa hivi, Simba inaangalia zaidi mashindano ya Afrika ambayo Tshishimbi hana maajabu wala nafasi ya kuinufahisha Simba.

Tshimbimbi ni mchezaji mkubwa kwa ligi yetu na kombe la mapinduzi.
 
Kuna watu wanaona kama wengine hawatumii akili. Simba sio mtu ni taasisi tena vichwa. Wakidhani weo wanaweza kufikiria zaidi ya Board ya Simba wanajidanganya. Halafu hao wachezaji wakubwa unajua thamani zao?Wale sio kuku tu unaenda kuchukua sokoni. Kwa hiyo Simba inajua imchukue nani kwa ajili ya nini na kwa budget ipi
Unazungumzia ile bodi ambayo, inafanya kile anachotaka Mo?
 
dawa ni kuwasusia tunawapa vichwa sana tunavyojaa uwanjani Tshishimbi au Yondani sio wa kiwango cha kucheza hii Simba kumbuka Uchebe alimkataa hata yule beki wao tegemeo Lamini Moro ingawa aliletewa magarasa mengine
Kweli kabisa yaani pesa ya kununua wachezaji wa kawaida fungu zima, Bora kununua mchezaji mmoja au wawili lakini ni GOALS MACHINE halafu awe na umri mdogo.
 
Klabu ya Simba itaendelea kuwa kichwa cha Mwendawazimu, kufungwa na kutofanya vizuri katika michuano ya Afrika iwapo itaendelea kushikiria akili na tamaduzi hizi,

Taarifa zinasambaa Papy Kambamba Tshishimbi anaondoka Yanga kuelekea Simba, taarifa hii imesambaa kwenye vyombo vya habari, pia post iliyotumwa na mchezaji wa SIMBA Ibrahimu Ajibu inaashiria Tshishimbi atatua SIMBA.

Kama kweli Simba inataka kufanya vizuri inabidi kuachana na wachezaji wa viwango vya kati, watafute mchezaji mkubwa kwa ajili ya kwenda kushinda mataji makubwa ya Afrika.

Tshimbimbi sio mchezaji mbaya, hapana naheshimu uwezo wa mchezaji huyu lakini kwa sasa Simba haitaji mchezaji wa kiwango chake.

Timu inahitaji wachezaji kama watatu (3) wakubwa, wanao cheza ligi na mashindano makubwa sio wachezaji wa wakujaribu jaribu.

timu inasajiri wachezaji kiushabiki halafu wanakuwa hawana msaada kwenye mashindano kwenye mashindano makubwa.



naungana na wewe kwenye hili tatzo hatuna pakusemea sio muda tena wa kutafuta wacheyaji wa kati kama mnataka kufika mbali kimashindano za klab bingwa
 
Back
Top Bottom