Simba ya 2023 inafanana sana na Cameroon ya 1990

Simba ya 2023 inafanana sana na Cameroon ya 1990

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Mimi kwa kuwa ni mpenzi wa dhati wa soka, nimewahi kukaa na kuangalia mechi na wachezaji wa zamani na kujua kwa kina historia mbalimbali za soka maana bila kujua ulipotoka hauwezi kujua unapokwenda.

Leo nimewaza timu ya Simba inayoonekana kuwa na wakongwe wengi ambao wanaelekea ukingoni mwa career zao kama top players. Wakati mwingine hii inaongelewa kama ni udhaifu lakini kuwa na balance nzuri ya wachezaji wakongwe na vijana ni muhimu sana kwa championship team yoyote.

Mwaka 1990, timu ya taifa ya Cameroon, maarufu kama Indomitable Lions, ilikuwa ni nchi ya kwanza kutoka Afrika kuingia robo fainali katika Kombe la Dunia. Timu hiyo ilikuwa na wachezaji wengi wakongwe waliokuwa wanaenda kumaliza career zao na ilienda kuweka historia.

Walikuwa wanacheza mpira wa kuvutia, wenye madoido mengi, walikuwa na confidence ya hali ya juu hata walipokuwa wanacheza na miamba ya soka duniani. Ni aina ya timu ambazo zinatokea mara moja baada ya vizazi vingi kupita.

images - 2023-03-19T221100.729.jpeg


Naiona Simba hii ya wakongwe hawa kina Manula, Chama, Kapombe, Mzamiru na Onyango wakiwa wamechanyanyika na vijana kama Kanoute, Sakho na Banda.

Simba unaweza kusema wana character fulani ya timu inayojiamini, watakupa kila kitu ambacho The Indomitable Lions ya kina Roger Miller, Francois Omam Biyik, Mackanacky na wengine walikuwa wanakupa.

20230320_133040.jpg


20230319_221150.jpg


Kuna hadi magoli wanayofunga Simba yanafanana na magoli niliyoona walikuwa wanafunga Cameroon ya kipindi kile.

Embu ngoja tuone itakuwaje.
 
Hii Simba inacheza Kwa madoido? Game moja timu inashinda game inayofuata utawasikia mashabiki hatumtaki kocha.. Mkuu hapo umechemka sana. Ukweli hii Simba ni miongoni mwa timu mbovu na ubovu wao utakuwa exposed pale robo fainali
 
Hii Simba inacheza Kwa madoido? Game moja timu inashinda game inayofuata utawasikia mashabiki hatumtaki kocha.. Mkuu hapo umechemka sana. Ukweli hii Simba ni miongoni mwa timu mbovu na ubovu wao utakuwa exposed pale robo fainali
Endelea kuota...si mlisema haitafika robo fainali??
 
Duniani Kuna Mambo, Yaani Cameroon ya 1990 Ilikua na wachezaji wafananao na Simba hii ya Robertinyo!!! Kweli Jamiiforum Kuna watu awana adabu.
 
Hii Simba inacheza Kwa madoido? Game moja timu inashinda game inayofuata utawasikia mashabiki hatumtaki kocha.. Mkuu hapo umechemka sana. Ukweli hii Simba ni miongoni mwa timu mbovu na ubovu wao utakuwa exposed pale robo fainali
Al Hila akawafurushaa CL, mnabaki kulia na Simba, kwan imewafanya nn jaman? Kila mtu apite njia zakee.

Khaaaaaah [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna watu wengine mnajitafutia tu wenyewe dhambi aisee. Yaani kabisaa kikosi cha Cameroun cha mwaka 1990, unakifananisha na hii simba tia maji tia maji ya akina Kibu D!!

Kweli?
 
Duniani Kuna Mambo, Yaani Cameroon ya 1990 Ilikua na wachezaji wafananao na Simba hii ya Robertinyo!!! Kweli Jamiiforum Kuna watu awana adabu.
Cameroon ya 1990 ilikuwa na wachezaji ambao leo mngeita ni WAZEE.
 
Back
Top Bottom