Simba yaahirisha safari ya Marekani kwa sababu kuna joto yaenda SA kwenye baridi

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Hii ni kwa mujibu wa mtendaji mkuu wa Simba kwamba Simba haikwenda kuweka kambi Marekani kwa kuhofia joto na wameenda South Afrika kwenye baridi.

Amesisitiza kuwa tatizo siyo ukata bali tabia nchi.

Source ITV habari!
 
Hii ni kwa mujibu wa mtendaji mkuu wa Simba kwamba Simba haikwenda kuweka kambi Marekani kwa kuhofia joto na wameenda South Afrika kwenye baridi.

Amesisitiza kuwa tatizo siyo ukata bali tabia nchi.

Source ITV habari!
Sehemu nyingi tu zina baridi wakati huu huko Marekani. Watafute sababu nyingine ya kufunikia ile sababu halisi.
 
Sehemu nyingi tu zina baridi wakati huu huko Marekani. Watafute sababu nyingine ya kufunikia ile sababu halisi.
Yanga nasikia wapo bigwa morogoro wakati walituambia wataenda chinaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Mimi mwenyewe nimeghairi leo kwenda Mbagala kwa sababu kuna joto, nitaenda Njombe kwenye baridi.

Kuna mlevi akaniuliza "ina maana hilo joto umelijua leo?"
Labda baridi zinakujaga ghafra
 
Kwa hiyo Simba imeghairishakwa vile Yanga imeghairisha?
Nyie yanga mnafuatilia sababu za simba kughaili mbona nyie hamjataja sababu za kughaili kutoka safari ya kwenda china mpaka kwenda bigwa morogoro...pilipili msiyoila yawawashia nini
 
Reactions: Tui
Safi sana mnyama namwaminia sana. Maamuzi yake daima huwa yana busara ndani yake..πŸ˜…πŸ˜…
 
Nani awape visa ya Marekani..wakati Ulaya tu kuna kumbukumbu ya wachezaji wenu kutoroka....
 
HUJAJIBU maswali
Huko ulaya tumewapeleka simba queens so hatujataka waongozane na kaka zao....vipi umeridhika????....najua ukisikia simba queens wapo ulaya wakati yanga mpo bigwa morogoro mnaiba matikiti lazima povu liwatoke πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚....sasa zamu yako kujibu....vipi china mliyosema mtaenda ndo hii china ya bigwa morogoro?????
 
Kwa hiyo Marekani ni ulaya?
 
Duh wewe jamaa unahitajika sana uwe na Manara hapo Msimbazi siyo kwa juhudi hizo
Juhudi zipi mkuu..nyie ni mafundi sana wa kuuliza kwanini simba wameenda south africa na si marekani kama walivyotangaza mwanzo...ila mnashindwa kuwauliza viongozi wenu kwanini wamepeleka timu bigwa morogoro na si china kama walivyowatangazia mwanzo...yaani ni mnakomalia yasiyowahusu wakati ya kwenu yanawashinda
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…