Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,772
- 22,598
Hata hivyo, Simba ambayo imeweka kambi Zanzibar kujiandaa na mchezo huo, itawasili Dar es Salaam Jumamosi saa 2:00 asubuhi na kuelekea moja kwa moja Hoteli ya Golden Tulip kupumzika kabla ya kutinga Uwanja wa Uhuru tayari kwa mchezo wao.
Akizungumza na Nipashe jana, Mratibu wa klabu hiyo, Abbas Ally, aliliambia Nipashe kuwa kwa sasa wachezaji wa timu hiyo wanaendelea na program yao kujiandaa na mchezo huo wa Jumamosi.
“Wachezaji wana morali ya juu, kila mmoja anauwaza na kuu kiria mchezo wa Juma- mosi..., kocha ( Joseph Omog) amekuwa akiwa- sisitizia umuhimu wa kushinda mchezo huu,” alisema Abbas.
“Hata kocha msaidizi (Masoud Djuma) ame- kuwa akiwahamasisha na amekuwa ra ki wa wachezaji kwa muda mfupi tu..., kiukweli kila kitu kinaenda sawa,” alisema Abbas.
Alisema mpaka ku kia jana, kikosi hicho cha wachezaji 24 kilichopo Zanzibar hakina maje- ruhi yoyote. “Leo ( jana) tumefanya mazoezi asubuhi na hatutakuwa na mazoezi ya jioni, ke- sho (leo) tunaendelea na mazoezi kwa kufuata program ya mwalimu,” alisema Abbas.
Simba inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesakama ilivyo kwa watani zao Yanga, imewaacha jijini Dar es Salaam wachezaji wake majeruhi Shomari Kapombe, Salim Mbonde pamoja na Said Mohamed ‘Nduda’ ambao wanaendelea kujiuguza.
Mchezo huo wa Jumamosi utatoa picha ya kinara katika msimamo wa ligi, kwa sasa Simba wanaongoza ligi kwa tofauti ya mabao huku ikigongana na Yanga kwa pointi, zote zina poin- ti 15 sawa na Mtibwa Sugar inayoshika nafasi ya tatu.
Hata hivyo, ushindani mkubwa upo kwa washambuliaji wa timu hizo, Emmanuel Okwi wa Simba na Ibrahim Ajibu wa Yanga ambao wamekuwa gumzo kwenye vikosi vyao huku wakifukuzana kwa mabao ya kufunga. Okwi ana mabao nane huku Ajibu akiwa na mabao matano .
IPP Media