simba ndiyo mpango mzima na nawashangaa sana " malofa " fulani tena kupitia kwa " mpashkuna " wao kuwa timu yao ni ya kimataifa zaidi wakati hata ktk ile rekodi iliyotolewa hivi majuzi tu ya vilabu bora duniani na afrika klabu yao haipo huku simba sports club na wazee wa lamba lamba wakichomoza lakini kama hiyo haitoshi hivi utajiitaje " mzee wa kimataifa " wakati huna na hujawahi kuuza mchezaji hata mmoja nje ya nchi achilia mbali huko " ukimataifani " unakokusema? najua kimbilio lao hapa watajitetea kuwa wamemuuza nonda shabani wakati ukweli ni kwamba nonda shabani papii alimaliza mkataba wake yanga na kurudi kwao kisha akaanza mchakato wake binafsi wa kwenda kucheza soka nchi za nje na ndipo akaanzia klabu ya vaal professionals ya afrika ya kusini na najua kuna wengine watasema kuwa yanga imemuuza ngasa klabu ya bidvest ya africa ya kusini lakini kwangu mimi africa kusini ni kama " tandale " tu ila simba tuna rekodi kadhaa ya kuwauza wachezaji ulaya kuanzaia " machupa " nchini denmark, haruna moshi " boban " sweden na sasa " super okwinyo " tena nchini denmark na kuna tetesi xavi hernandez kiungo mahiri kabisa na mstaafu wa fc barcelona amependekeza kwa kocha wao mkuu kuwa waje tanzania kufanya mazungumzo na simba ili wamchukue fundi na mtaalam " said khamis ndemla " huku fc bayern munich nayo ikimtaka kwa udi na uvumba beki ya kushoto " fundi " ya simba mohamed hussein tshabalala na real madrid nao wako ktk mazungumzo ya mwisho na simba ili wamchukue nahodha hassan isihaka ili akakipige ktk timu yao ya " b " na baada ya hapo aje pengine kuwa mbadala wa beki " sergio ramos ". sasa kwa maelezo haya tu mafupi kati ya " mnyama " simba sports club na hao " washamba wa kimataifa " nani anastahili kweli kuitwa wa " kimataifa "?. simba mwaka huu tutauza wachezaji balaa huko " ulaya ".