Simba yatakiwa kulipa gharama viti kung'olewa kwa Mkapa

Simba yatakiwa kulipa gharama viti kung'olewa kwa Mkapa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamaganda Kabudi amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuwaandikia barua klabu ya Simba kuhusu ung'olewaji wa viti uliofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jana.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini wa Wizara hiyo, imesema barua hiyo itakayoelekezwa kwa Simba iwanakiri na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili gharama za uharibifu huo zilipwe.

Pia, Soma: Jeshi la Polisi latoa tamko baada ya mashabiki wa Simba kuvunja viti Uwanja wa Taifa

Vurugu ziliibuka jana Desemba 15, 2024 katika mechi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baina ya Simba dhidi ya CS Sfaxien, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

"Vitendo vilivyofanyika jana katika Uwanja wa Benjamin Mkapa havikubaliki na sio vya kimichezo, nakuelekeza Katibu Mkuu kuchukua hatua mara moja. Pamoja na kuwaandikia Simba Sports Club na TFF, wapeni ushirikiano Polisi ili watu wote waliokuwa wanang'oa viti na kuvitupa wakamatwe na wachukuliwe hatua za kisheria, lazima tabia hii ikomeshwe," amesema Profesa Kabudi.

Waziri Kabudi amewataka mashabiki wanaoingia katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuacha vitendo vya uharibifu wa uwanja kwa kuwa wanasababisha hasara kwa Serikali na kuharibu ubora wa uwanja.
IMG_1666.jpeg
 
Simba wamesha lalamikiwa na vilabu vingi vinavyo kuja kucheza Benjamin Mkapa, Uwanja wa Taifa CAF wanauangalia kwa jicho la karibu kutokana na timu Nyingi kulalamika hasa zichezapo na Simba.
Kuanzia Ulozi, Marefa na Sasa vurugu za Mashabiki.

Ili ku uweka Uwanja sehemu salama kabla Rungu halijatufikia kama Taifa, Simba mechi zao zihamishiwe Karume pale Tff.

Mechi za shirikisho hazina Tija yoyote katika mpira wetu Sasa Taifa lisi ingie aibu na kuendelea kupata hasara kwa vitu vya kipuuzi.

Uko shirikisho refa ana hongwa Dola 200 na Carton Moja ya MO energy baada ya mechi tuna Rudi kukarabati uwanja kwa mamilioni ya shilingi.
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamaganda Kabudi amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuwaandikia barua klabu ya Simba kuhusu ung'olewaji wa viti uliofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jana.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini wa Wizara hiyo, imesema barua hiyo itakayoelekezwa kwa Simba iwanakiri na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili gharama za uharibifu huo zilipwe.
View attachment 3177856
Pia, Soma: Jeshi la Polisi latoa tamko baada ya mashabiki wa Simba kuvunja viti Uwanja wa Taifa

Vurugu ziliibuka jana Desemba 15, 2024 katika mechi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baina ya Simba dhidi ya CS Sfaxien, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

"Vitendo vilivyofanyika jana katika Uwanja wa Benjamin Mkapa havikubaliki na sio vya kimichezo, nakuelekeza Katibu Mkuu kuchukua hatua mara moja. Pamoja na kuwaandikia Simba Sports Club na TFF, wapeni ushirikiano Polisi ili watu wote waliokuwa wanang'oa viti na kuvitupa wakamatwe na wachukuliwe hatua za kisheria, lazima tabia hii ikomeshwe," amesema Profesa Kabudi.

Waziri Kabudi amewataka mashabiki wanaoingia katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuacha vitendo vya uharibifu wa uwanja kwa kuwa wanasababisha hasara kwa Serikali na kuharibu ubora wa uwanja.
View attachment 3177852

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamaganda Kabudi amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuwaandikia barua klabu ya Simba kuhusu ung'olewaji wa viti uliofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jana.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini wa Wizara hiyo, imesema barua hiyo itakayoelekezwa kwa Simba iwanakiri na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili gharama za uharibifu huo zilipwe.
View attachment 3177856
Pia, Soma: Jeshi la Polisi latoa tamko baada ya mashabiki wa Simba kuvunja viti Uwanja wa Taifa

Vurugu ziliibuka jana Desemba 15, 2024 katika mechi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baina ya Simba dhidi ya CS Sfaxien, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

"Vitendo vilivyofanyika jana katika Uwanja wa Benjamin Mkapa havikubaliki na sio vya kimichezo, nakuelekeza Katibu Mkuu kuchukua hatua mara moja. Pamoja na kuwaandikia Simba Sports Club na TFF, wapeni ushirikiano Polisi ili watu wote waliokuwa wanang'oa viti na kuvitupa wakamatwe na wachukuliwe hatua za kisheria, lazima tabia hii ikomeshwe," amesema Profesa Kabudi.

Waziri Kabudi amewataka mashabiki wanaoingia katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuacha vitendo vya uharibifu wa uwanja kwa kuwa wanasababisha hasara kwa Serikali na kuharibu ubora wa uwanja.
View attachment 3177852
Tatizo waziri kawahi sana. Hili suala lina sura ya kimataifa. Adui zetu watatumia hii nyaraka kama ushahidi wa kutuadhibu zaidi. Si ajabu Simba ikacheza mechi zijazo bila mashabiki. Angetulia kwanza au wangefanya haya mambo kimya kimya bila kutoa nyaraka kama hii hadharani.


Siungi mkono fujo na lazima mashabiki wa Simba wale adhabu kali. Lakini hili suala lilihitaji timing na akili ya juu kidogo. Hapa tumejichoma wenyewe na wese letu.
 
Back
Top Bottom