Simba yavunja Mkataba na Kocha wake Zoran Maki

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Klabu ya Simba imeachana na kocha wake mkuu Zoran Maki, akiwa ameifundisha timu hiyo kwa siku 67 pekee. Awali Zoran aliingia mkataba wa mwaka mmoja na Simba ambapo leo wamefikia makubaliano ya pamoja kuvunja mkataba huo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Babra Gonzalez.

Vilevile Simba wamesitisha mikataba ya Kocha wa viungo Sbai Karim na Kocha wa makipa Mohammed Rachid.

Wakati mchakato wa kumpata kocha mpya ukiendelea, timu itaongozwa na kocha wake msaidizi, Suleiman Matola.

 
Taarifa kwa umma.
Klabu ya simba imefikia makubaliano ya kuvunja mkataba wa kocha Zoran Maki pamoja na kocha viungo Sbai Karim pamoja na kocha wa makipa na Mohammed Rashid
 
Ndio mpira wetu wa kibongo, tulisema hapa Simba mkatupigia makele, timu hiyo waliosajili ni viongozi na si makocha. Mtawapa lawama makocha wakati viongozi ndio wanastahili lawama.Kama ikiwezekana muachieni Matola.
 
Nashauri kwa dhati na moyo mkunjufu kama Matola vyeti vyake vinakidhi vigezo tumuachie timu.

Wachezaji wanampenda.

Wachambuzi watakosa la kusema.

Pia Simba tutakuwa mfano wa kuingwa kuwaamini makocha wazawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…