mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,126
- 5,068
LICHA ya kutimiza idadi ya wachezaji 12 wa kigeni, Mwanaspoti limebaini Simba inaendelea na mikakati ya chinichini ya kumalizana na mido mpya kutoka Nigeria. Lakini wanafikiria pia kumalizana na Mudathir Yahya.
Awali mabosi wa Simba pamoja na benchi la ufundi walikubaliana kufunga zoezi la usajili baada ya kumpata straika Mserbia, Dejan Georgijevic kama Mwanaspoti lilivyokuwa likikueleza.
Lakini baada ya kufanya tathimini ya pamoja na benchi la ufundi katika mechi mbili za kimashindano na moja ya kirafiki wamebadili maamuzi na sasa kabla ya dirisha la usajili kufungwa Agosti 31 watashusha kitu kwa siri sana.
Mwanaspoti linajua wamekubaliana kusajili kiungo mpya wa mkabaji na mezani wana majina mawili chaguo la kwanza kiungo mkabaji wa Kwara United kutokea Ligi Kuu ya Nigeria, Afeez Nosiru.
Nosiru anapewa nafasi kubwa ya kusajili na anaendelea na mazungumzo na Simba inayofikiria kumtoa kwa mkopo Victor Akpan kumrejesha Coastal Union.
Mbali na Nosiru pia mezani Simba ina chaguo la pili, kiungo wa zamani wa Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, Mkenya Teddy Akumu ambaye kwa sasa ni mchezaji huru. Lakini nafasi yake ni finyu.
Simba kama itashindwa kumalizana na Nosiru itahamia kwa Akumu aliye huru lakini lengo ni kuhakikisha mtu anatua kabla dirisha halijafungwa
Nosiru usajili wake ukikamilika anakuwa mchezaji watano anayecheza eneo la kiungo wa ukabaji kwani atawakuta, Jonas Mkude, Sadio Kanoute, Mzamiru Yassin na Erasto Nyoni.
Katika soka la ushindani Nosiru kabla ya kujiunga na Kwara United amewahi kupitia Niger Tornad msimu 2020-21, zote kutokea Nigeria.
Inaelezwa kama mambo yatakwenda vizuri kama yalivyo wakati huu muda wowote kuanzia sasa Nosiru anaweza kuwasili nchini akatambulishwa katika kikosi hicho chenye kiu ya kufanya vizuri msimu huu.
Meneja habari wa Simba, Ahmed Ally alisema dirisha la usajili bado lipo wazi na kama kutatokea mapendekezo ambayo kocha, Zoran Maki atakuwa anahitaji hawatashindwa kumtimizia haraka iwezekanavyo.
ISHU YA MUDATHIR
Aidha mabosi wa Simba wamefanya mawasiliano na kiungo wa zamani wa Azam, Mudathir Yahya lakini inaelezwa kwamba ni kama anadengua kwani muitikio wake ni mdogo.
Ingawa Simba wamepanga kiungo huyo aliyewahi kukipiga Singida United awe sehemu ya wachezaji wa ndani ya kikosi hicho kinachoongoza msimamo wa Ligi Kuu Bara kwa tofauti ya mabao ya kufunga baada ya raundi ya kwanza
Awali mabosi wa Simba pamoja na benchi la ufundi walikubaliana kufunga zoezi la usajili baada ya kumpata straika Mserbia, Dejan Georgijevic kama Mwanaspoti lilivyokuwa likikueleza.
Lakini baada ya kufanya tathimini ya pamoja na benchi la ufundi katika mechi mbili za kimashindano na moja ya kirafiki wamebadili maamuzi na sasa kabla ya dirisha la usajili kufungwa Agosti 31 watashusha kitu kwa siri sana.
Mwanaspoti linajua wamekubaliana kusajili kiungo mpya wa mkabaji na mezani wana majina mawili chaguo la kwanza kiungo mkabaji wa Kwara United kutokea Ligi Kuu ya Nigeria, Afeez Nosiru.
Nosiru anapewa nafasi kubwa ya kusajili na anaendelea na mazungumzo na Simba inayofikiria kumtoa kwa mkopo Victor Akpan kumrejesha Coastal Union.
Mbali na Nosiru pia mezani Simba ina chaguo la pili, kiungo wa zamani wa Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, Mkenya Teddy Akumu ambaye kwa sasa ni mchezaji huru. Lakini nafasi yake ni finyu.
Simba kama itashindwa kumalizana na Nosiru itahamia kwa Akumu aliye huru lakini lengo ni kuhakikisha mtu anatua kabla dirisha halijafungwa
Nosiru usajili wake ukikamilika anakuwa mchezaji watano anayecheza eneo la kiungo wa ukabaji kwani atawakuta, Jonas Mkude, Sadio Kanoute, Mzamiru Yassin na Erasto Nyoni.
Katika soka la ushindani Nosiru kabla ya kujiunga na Kwara United amewahi kupitia Niger Tornad msimu 2020-21, zote kutokea Nigeria.
Inaelezwa kama mambo yatakwenda vizuri kama yalivyo wakati huu muda wowote kuanzia sasa Nosiru anaweza kuwasili nchini akatambulishwa katika kikosi hicho chenye kiu ya kufanya vizuri msimu huu.
Meneja habari wa Simba, Ahmed Ally alisema dirisha la usajili bado lipo wazi na kama kutatokea mapendekezo ambayo kocha, Zoran Maki atakuwa anahitaji hawatashindwa kumtimizia haraka iwezekanavyo.
ISHU YA MUDATHIR
Aidha mabosi wa Simba wamefanya mawasiliano na kiungo wa zamani wa Azam, Mudathir Yahya lakini inaelezwa kwamba ni kama anadengua kwani muitikio wake ni mdogo.
Ingawa Simba wamepanga kiungo huyo aliyewahi kukipiga Singida United awe sehemu ya wachezaji wa ndani ya kikosi hicho kinachoongoza msimamo wa Ligi Kuu Bara kwa tofauti ya mabao ya kufunga baada ya raundi ya kwanza