Simbachawene: Serikali kuangalia upya utaratibu wa kuanzisha Makanisa, Wachungaji watapaswa kuwa na Shahada ili kupunguza "Vibanda Imani"

Shahada hapa bongo haitasaidia.kwa sababu vyuo vyetu vimegawa shahada kama njugu, tuna watu wengi mtaani wengine wazururaji tu na hata akili haziwatoshi lakini wana shahada wengine hadi masters! Tuna matapeli wenye shahada. Tunao hadi vibaka wenye shahada. Kwa kifupi shahada siyo suluhisho la tatizo hili.
 
Mbona kagame kaweza

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
Kaweza Nini nchi Ina watu wangapi? Kule Kagame hahojiwi hapa tutahojiana Hadi kieleweke .Huwezi amka tu ukaja na kitu Cha upande mmoja kaulize hata kagame kama kathubutu kugusa Waislamu kuwa Wawe na digrii .Ngoma nzito kaikimbia na ubabe na ujanja wake wote
 
Ni ya Theology? Ndicho anachomaanisha Simbachawene.
Kulazimisha watu wawe na shahada za teolojia ni kuingilia uhuru wa kuabudu kwa sababu vyuo vinavyotoa shahada hizo vinaweza kuwa na mrengo wa imani unaopingana na imani ya huyu mhusika unayetaka awe na shahada.
Kwa mfano ukitaka mchungaji awe na shahada ya teolojia, unamaanisha akaisomee wapi: Makumira? Kipalapala? Hivi vyuo ni vya waluteri na wakatoliki, wakati mhusika hakubaliani na mafundisho yao!
Waweke tu sheria ya nchi inayolinda raia wote, basi. Mengine waachie watu uhuru. Jinai ishughulikiwe kama jinai tu.
 
Kuna vyuo vinatoa degree za theologia viko huru. Hata Open University unasoma
 
Mbona misikiti haihusiki kwenye sheria hiyo? Huo ni ubaguzi wa wazi dhidi ya wakiristu.
 

Anakwepa kwenda deep kwenye msingi wa tatizo, pale zilizovuka ni yebo yebo manake inaonyesha wazi ugumu wa maisha ndio chanzo hasa cha vifo, kiasi kwamba watu wanatafuta nafuu ilipo hata kama kwa kughalimu maisha yao na ya watu wengine. Bwana John udereva wake unaleta maafa sasa.

Hakuna mbunge wala waziri aliyekanyagwa pale.
 
Shahada sio muhimu sana,kuwe tu na taratibu na vigezo,kama mtu hakidhi hakuna kutoa huduma NA hili lifanyike kwa kuwashirikisha wadau ambao ni hizo (ministries) ili kuwe na uniformity...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesema kweli sana. Kuna matabaka katika makanisa pia kama ilivyo kwamba wa Gongolamboto ni tofauti na wa Masaki, kila tabaka lina watu wake linaowaelewa. Hawa tabaka la chini ndio hao wanaohangaika kwa manabii wa vibanda-umiza. Wa Mikocheni wako na Mama Lwakatare, sio kidini, company tu wapate pa ku-socialize, mama mwenyewe msanii mwanasiasa janjajanja. Makanisa makongwe kama RC na Lutheran wamejitahidi kuondoa matabaka kwa kusisitiza Jumuiya Ndogondogo ambako ndani ya jumuiya wote wanakuwa familia moja, lakini kwa kuwa jumuiya zimepangika kijiografia bado kuna jumuiya duni ambazo hata pa kukutana ni mtihani kama wa kule Mbagala, Keko Magurumbasi nk, na jumuiya tajiri kama za Oysterbay kwa viongozi. Bado kuna parokia fukara ingawa zinajitutumua kujenga majengo makubwa makubwa kwenye squatter areas. Matabaka ndiyo tatizo kubwa.
 

Ameongea tu.
Tatizo halikutokana na kiwango cha elimu kuwa chini, bali haya ni mambo ya kiimani na mafunuo.

Hivi Babu wa Loliondo alikuwa na elimu gani? Mbona maprof, madr, na watu wakada mbali mbali walieenda na kunywa dawa aka KIKOMBE bila kuulizaimedhibitishwa na TBS au la?

Mimi naona kila upande (Serikali, Kanisa na waumini) uwajibike ipasavyo na si kurushiana mpira
 
Vyuo vinavyotambuliwa na serikali Ni vya milengo fulani ya kiimani ya kidinii zao ambayo Wengine sio imani zao .Unaposema mtu awe na digrii ya kutoka chuo kipi Mfano chuo gani kikuu kinatoa digrii za unabii au utume kinachotambuliwa na serikali?
 
Waislam marufuku kupiga adhanaa Kigali.

Mbona wamekua wapole tu.
dodge
 
Hii comment ilipaswa kuwa thread,napendekeza ufanye hivyo au utawanyima watu fursa kupata maarifa au kuchallange!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…