SimbaNET Hooks into SEACOM

Jamani hawa ni SimbaNet kuna kampuni zingine zaidi ya sita ambazo nazo itaungwa kwenye SEACOM..Tusubiri hao na tuone ushindani wa kweli...as consumers we will always go for the cheapest and fastest provider!!
I hope TCRA wako upande wa consumers on this one lasi ivyo tutaliwa kama tunavyoliwa kwenye GSM networks!!
 
Inasikitisha kuona jinsi baadhi yetu tunavyoendelea kulalamika wakati tumepewa fursa nzuri ya kufurahi na kupongezana kwa haya maendeleo ya msingi.

Tunapaswa kuwa tunafurahi pamoja na ndugu zetu walio wateja wa SimbaNET bila kuwa na wivu wala usongo, kwani katika siku za usoni wenzao wengine tutawafuata pia katika huduma hii ya Internet kupitia marine cable. Na bei zitashuka tu, lakini lazima tuanze hapa kwa kuunganishwa kwenye mtandao, ndipo tupate kuliangalia suala la bei.

Hongereni sana wanaSimbaNET kwa kufanikiwa kutufungulia sote kiingilio cha SEACOM!
 
Nani amemuelewa huyu kaka blaza?
 
Yo Yo Vp hapo r u in? Make we na Melo ndo wataaluma wetu hapa tunategemea ushauri mkubwa kutoka kwenu. Hiyo sijui 80/80 itaniwezesha kuona clips za Youtube kweli?
Utaweza kuona ila nilazima uisubirie kwa mda kidogo.
 
Nani amemuelewa huyu kaka blaza?

Huyo mzushi tu. Swala ni moja kwamba at the end of the day tunahitaji unafuu wa bei na speed ya kutosha. Habari za ''tuunganishe kwanza then bei itashuka baadae'' ni uzushi. Hao watu lazima wawe wameshafanya mahesabu watwambie exactly bei itashuka kwa kiwango gani kwani wanajua bei wanayonunulia na gharama za uendeshaji, kwa nini wasijue bei ya kuuzia???????????
 
Nawapenda sana wabongo wenzangu..Mkifika kwa Mama Ntilie utasikia nina 500 nataka "wakushiba"..ie ujaziwe..sasa ukitaja ujaziwe si lazima uongeze pesa...?Huku kutaka kingi kwa bei ndogo nako Mh...!!!

Kaka Mtsimbe tuweke breakdown yenu kama hao wenzako wa Kenya.

ila wadau naomba tusilinganishe bei za TZ na Huko "Unyamwezini"
 

Maxence asante sana kwa picha nzuri za tukio la launching. Nilifurahi sana kukuona wewe na Mike. Si vibaya siku za mbeleni kufikiria kuwa na majournalist wa Jamii ili kucover matukio mbalimbali. Nimevutiwa na "Speed na Standars" yenu ya ku-cover matukio.

Maxence. nitumie kweny barua pepe nitakupatia. Kwa sasa si rahisi kwangu kuanika Price List yote hapa kwa sababu za kibiashara na kiushindani. lakini tumepunguza bei zetu kwa zaidi ya asilimia 50%.

Naamini kuna namna tunaweza kuisaidia JF.

karibu sana Maxe.
 
Kumbe huu mkonga haujapunguza kitu wabongo bana kwa kupenda super profit dah.
Sasa sijui hawa walioleta mkonga ndo wanawakamua au hawa maagent ndo mnatukamua maana bongo bana.

Fidel80;

Mkonga umepunguza bei sana. Mfano, kabla ya Mkonga bei ya chini kabiasa ya 1024/1024 Kbps au 1/1 Mbps ilikuwa zaidi ya $ 5000 kwa ISP nyingi.

Sasa hivi same capacity bei yake ni pungufu ya $ 1850 ambayo ni pungufu ya zaidi ya 60%. bado nina matumaini with time bei zitashuka.

Kwa sasa investmeny ya BW ni kubwa. Na BW ni recurrent ambayo huwezi ukatumaini itakulipoa baada ya miaka kadhaa. Kwa maana nyingine inabidi kama unanunua 155 Mbps kwa mwezi, tunakonunua hawajali kama umeiuza yote au la. Wao wanauza capacity na kukuchangi kwa hilo.
 
Maxence. nitumie kweny barua pepe nitakupatia. Kwa sasa si rahisi kwangu kuanika Price List yote hapa kwa sababu za kibiashara na kiushindani. lakini tumepunguza bei zetu kwa zaidi ya asilimia 50%.
d=
Dah Muheshimiwa kuna ubaya gani sisi wateja wenu tukijua price yenu mpya?. Basi naomba unipe ufafanuzi kidogo,mimi ni mteja wenu na nimechukua speed ya 128 kbps, je mta niongezea Bandwidth au mta ni punguzia bei?
 
wee acha tu maana raisi alituambia ati gharama zitapungua saaaana more than 70% lakini naona kama ndio zimeongezeke..au Sactus anakula cha juu?joking

lol umemtafutia balaa.....PM yake imeshajaa shoriiiizi


Yo Yo; unajua zama za backbone ya VSAT; Satellite Owners wanauza Uplink na Downlink peke yake. Kila moja ina bei yake. Unanunua uplink na downlink kutokana na mahitaji yako.

Katika Mkonga wa baharini Uplink na Downlink zote ni sawa kabisa na hili linafanya bei zishuke kwa asilimia zaidi ya 60%. Hata hivyo, utafititi wetu umebaini kuwa mara baada ya kuunganishwa na SEACOM, wengi matumizi yao yameongezeka. So, suluhu si kupunguza bei tu, bali pia ni kuongeza Bandwidth.
 


Lazy Dog;

Bei za mfano nilizozitoa hapo ni kwa makampuni, mashirika, serikali nk.

Tunazo special products za CDMA kwa matumizi ya binafsi na nyumbani. Bei yake ni affordbale sana kwa kila mtu. Product hii tunauza kupitia partners wetu. Unaweza mfano, ukanielezea budget yako, nikakushauri ni nini unataka.

Pia tuna Universal Access Program ambayo ni kwa maeneo ambayo si ya kibiashara kama wilayani na vijijini au mashuleni Primary na Secondary. Kwa maeneo hayo, unalipa kwa kadiri unavyotumia na tume-subsidize sana bei zake.

Kuhusu kuongeza 155 Mbps: tambua kuwa SimbaNET ndiyo ISP kubwa kwa maana ya kuuza Bandwidth kubwa (siyo idadi ya wateja) na mahitaji ya wateja yetu ni makubwa sana. Mfano, tayari wateja wengi wanataka waongezewe BW kwa mara mbili au tatu.

Pia wait for a big surprise before end of 2009! We promise bei zitapungua sana. Why? I cant tell u now the plans and strategies.
 
Ndugu,speed bado ni ile ile ambayo nilikuwa naipata siku zote,sijaona mabadiliko yoyote kwenye speed.Labda tu subirie tuone kama watatuongezea bandwidth...mimi nilichukua speed ya 128 kbps sijui wataniongezea au la.

JOSM;

Kama wewe ni mteja wetu:
VSAT Latency kwenda UK ilikuwa zaidi ya 600 Milliseconds
Sasa hivi latency kupitia Mkongo wa bahari ni kati ya 250-300 Milliseconds

Kwa hiyo speed imeongezeka zaidi ya mara mbili.

Kuhusu kuongezewa capacity: Kama uko DSM nilitegemee hilo, bila ya shaka utaongezewa. Sasa hivi Ma-Engineers wetu wanalishughulikia hilo na in a short time you should be Ok.
 

Yo Yo, usikate tamaa ni mapema sana. I promise that muda si mrefu hata wewe unaweza ku-affaord kwa package ya nyumbani kupata capacity ya kukuwezesha hata kuplay movies online.

Kwa sasa huwezi kupata majibu ya maswali yote hapa. Wasiliana nasi na utapewa taarifa husika unazohitaji.
 
Ahsante kwa ufafanuzi wako.
 


kapinga;

Bila ya shaka ISP nyingi zitaunganishwa. SEACOM wali-confirm katika Launching kuwa wana wateja 8 tayari. Hta hivyo kuna taarifa kuwa Vyuo vya Elimu ya Juu wamepewa 1 pair ya 155 Mbps hii ni mbali ya ile ya UDSM ambao pia wamepewa 155 Mbps.

Hata hivyo ni jambo jema unaponunua huduma tusiangalie bei tu, bali pia ubora. katika hili Customer/Technical Support ni muhimu sana.

Unfortunately TCRA hawana control katika prices unless kama kungekuwa kuna-Interconnection.
 

Asante sana Kaka Blaza.

Milango iko wazi kwa wale manaotaka kujiunga nasi. karibuni sana.
 
Utaweza kuona ila nilazima uisubirie kwa mda kidogo.

Ieleweke kuwa Mahitaji ya BW katika ku-Download Movies, Images, Voice na Documents kubwa ni tofauti na Brwsing ya kawaida.

Wakati 80/80 Kbps itatosha kwa matumizi ya kawaida, utahitaji BW kubwa kwa ajili ya kuplay movies otherwise buffering time itakuwa kubwa.
 
Mkuu tuporomoshee bei zenu basi tuzijue ambao tulikuwa hatuzijui ili tusinunue mbuzi kwenye gunia.

Mutensa; kwa sababu za kibiashara sitozibandika hapa. SimbaNET hatuuzi tu BW bali tunazingatia matumizi halisi ya mteja - Total Solution of Connectivity.
 
Mkuu kwani ukiweka bei kwa matumizi ya kawaida kama nyumbani hivi kuna ubaya gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…