Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
WanaJF,
Mada hii itakuwa na 'Updates' za Matukio kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Simiyu. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka.Mkoa wa Simiyu ni mojawapo ya mikoa ya Tanzania, ulioko kaskazini-magharibi mwa nchi. Mkoa huu ulianzishwa rasmi mwaka 2012 baada ya kugawanywa kwa Mkoa wa Shinyanga. Simiyu umepewa jina kutokana na mto Simiyu ambao hupita katika maeneo yake. Makao makuu ya mkoa huu yapo mjini Bariadi.
MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA SIMIYU
Katika muhtasari wa maeneo ya utawala, mkoa huu una halmashauri ambazo zimegawanyika katika mamlaka za miji na wilaya.
Idadi ya watu
Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu katika Mkoa wa Simiyu ni 2,140,497; wanaume 1,034,681 na wanawake 1,105,816, ikiwa na wilaya 5.
Idadi ya Majimbo ya Uchaguzi
Mkoa wa Simiyu una jumla ya majimbo ya uchaguzi Saba
- Jimbo la Bariadi
- Jimbo la Busega
- Jimbo la Itilima
- Jimbo la Meatu
- Jimbo la Maswa Magharibi
- Jimbo la Kisesa
- Jimbo la Maswa Mashariki
Katika uchaguzi mkuu wa 2020 mkoa wa Simiyu, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilipata ushindi mkubwa katika nafasi za urais, ubunge, na udiwani.
Kwa upande wa urais, mgombea wa CCM, Hayati John Pombe Magufuli, alipata kura nyingi dhidi ya mpinzani wake mkuu, Tundu Lissu wa CHADEMA.
Kwa nafasi za Ubunge, CCM ilifanikiwa kunyakua viti vyote katika majimbo 7
Uchaguzi wa Madiwani, (CCM) walipata ushindi mkubwa kwenye nafasi za madiwani ikifanikiwa kushinda kata nyingi. Hii ilitokana na upinzani kukumbwa na changamoto nyingi, zikiwemo wagombea wao kuenguliwa kutokana na matatizo ya kisheria au kutokidhi vigezo
Updates
January
February
- Pre GE2025 - Wassira: CCM tutaendelea kushika dola kwa kupigiwa kura sio kwa mtutu wa bunduki
- Pre GE2025 - Wasira: Hatuwezi shindana na nusu CHADEMA, Ikulu wataiona kwenye Runinga
- Pre GE2025 - Mapokezi ya makamu mwenyekiti wa CCM Ndg.Stephen Wasira mkoani wa Simiyu
- Pre GE2025 - Mzee Wasira amuonya Mwenyekiti wa Mkoa wa Simiyu kubeba wagombea ubunge wasiokubalika kwa wananchi
- Pre GE2025 - Naibu waziri maji: Ukituma mbunge anayekubalika kwa mawaziri miradi ya maendeleo itajazana jimboni kwako
- Pre GE2025 - Esta Midimu Mbunge wa viti maalumu: Waziri Mkuu nakutuma kwa Mh. Rais ikimpendeza Jina la Mbunge Njalu Silanga lipite bila kupingwa
- Pre GE2025 - Simiyu: Mbunge wa jimbo la Itilima Njalu Silanga achangiwa Milioni moja na laki tano kwa ajili ya fomu ya kugombea ubunge, fomu ishalipiwa
- Pre GE2025 - Mbunge wa Itilima asema alijiunga CCM baada ya Mzee Manyoni kugushi saini yake, CCM wanazidi kuuthibitishia umma huwa wanafanya umafia kwenye uchaguzi
- Pre GE2025 - Njalu Silanga, Mbunge Itilima: Serikali imepeleka bilioni 85 kwa ajili ya miradi ya maendeleo Itilima, Simiyu
- Pre GE2025 - Waziri mkuu: Mpango wetu CCM ni kuhakikisha wagombea wetu watakapopita kwenye maeneo yetu wasipate kazi kubwa kueleza miradi ya maendeleo
- Pre GE2025 - Mbunge Silanga: Nitatangaza kujiuzulu wakulima wakifikia uzalishaji wa kilo 1,500 kwa Hekari
- Pre GE2025 - Naibu waziri maji: Ukituma mbunge anayekubalika kwa mawaziri miradi ya maendeleo itajazana jimboni kwako
- Pre GE2025 - Esta Midimu Mbunge wa viti maalumu: Waziri Mkuu nakutuma kwa Mh. Rais ikimpendeza Jina la Mbunge Njalu Silanga lipite bila kupingwa
- Pre GE2025 - Simiyu: Mbunge wa jimbo la Itilima Njalu Silanga achangiwa Milioni moja na laki tano kwa ajili ya fomu ya kugombea ubunge, fomu ishalipiwa
- Pre GE2025 - Mbunge wa Itilima asema alijiunga CCM baada ya Mzee Manyoni kugushi saini yake, CCM wanazidi kuuthibitishia umma huwa wanafanya umafia kwenye uchaguzi
- Pre GE2025 - Njalu Silanga, Mbunge Itilima: Serikali imepeleka bilioni 85 kwa ajili ya miradi ya maendeleo Itilima, Simiyu
- Pre GE2025 - Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Ashiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Maswa Mashariki
ZINGATIA: Mikoa yote ina mada yake ya 'Update' ili kuweka wepesi katika ufuatiliaji.