Simiyu: Watoto watatu wafariki dunia Simiyu

Simiyu: Watoto watatu wafariki dunia Simiyu

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
IMG_20230427_164414.jpg
IMG_20230427_164403.jpg
IMG_20230427_164419.jpg
IMG_20230427_164406.jpg
Watoto watatu wa Shule ya Msingi Itubukilo B, Kijiji cha Pugu, Kata ya Itubukilo Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, wamefariki dunia Aprili 25, 2023 baada ya mkokoteni waliokuwa wakisafiria kusombwa maji ukiwa unavutwa na ng’ombe.

Waliofariki ni Maleki Legi (16), Isaka Njile (14) na Wille Njile ambao ni watoto wa familia moja huku watoto wawili wakinusurika.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Simon Simalenga, akiwa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo, amefika katika eneo hilo na kujumuika na wananchi ambapo pamoja na kuwapa pole wafiwa amewaasa wazazi juu ya umuhimu wa kuzingatia malezi ya watoto hasa kipindi hiki cha mvua kubwa.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Simiyu, Inspector Faustine Mtitu, amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari pindi wavukapo mito na madimbwi kwani kumekuwa na maji mengi ambayo yanaweza kuleta maafa.

Wananchi wa Kijiji cha Pugu wameiomba Serikali kujenga kivuka cha daraja ili kuwa suluhisho kwa wananchi wa maeneo hayo kwani mto huo umekuwa ni hatari kwa maisha ya watoto wao kutokana na wanafunzi kutumia mto huo katika kuvuka kwenda shuleni.
 

Attachments

  • IMG_20230427_164414.jpg
    IMG_20230427_164414.jpg
    44.3 KB · Views: 5
  • IMG_20230427_164403.jpg
    IMG_20230427_164403.jpg
    51.8 KB · Views: 5
  • IMG_20230427_164419.jpg
    IMG_20230427_164419.jpg
    62.4 KB · Views: 5
  • IMG_20230427_164406.jpg
    IMG_20230427_164406.jpg
    63.5 KB · Views: 4
Back
Top Bottom