Simon Msuva aendelea kukiwasha vyema Wydad Casablanca

Kichwa Kichafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2017
Posts
44,855
Reaction score
189,385
Habari.

Muda huu ni saa 02:15 usiku ila naona notification ya Simon Msuva kutupia goal lake dakika ya 39 ya mchezo kwa timu yake ya Wydad Casablanca.

Simon Msuva a.k.a 'kibaba' naona anaendelea kupeperusha bendera ya Tanzania nchini Morocco na pia anaonekana kuwa na safari nzuri huko mbele zaidi.

Kwa mtazamo wangu naweza sema tutarajie makubwa kwa Mtanzania huyu katika soka.

Je, wewe una mtazamo gani kwa huyu jamaa?

Nawasilisha Mzee Mkoloni

Cc: Kichwa Kichafu
 
Anaiwakilisha nchi na Yanga

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Sasa hivi tunazingumzia Azam na yanga Msuva tutamzungumzia wakati mwingine
Mtani hutaki watani tupumzike hata kidogo usiku hata kulala jana hatujarudi majumbani.

Na tunashukuru leo ni public holiday sijui ingekuwaje ingekuwa siku ya kazi.

Hebu tuzungumze kuhusu Simon Msuva kwanza mtani.
 
Kuwakilisha anawakilisha ila sema umri sasa mazee,,kwenda ulaya kwny ligi kubwa itakua ngumu sana,,all in all he's doing the best hata akijaga stars naonaga he has impact than captain wetu mbabaishaji
 
Huyu jamaa kwa mtazamo wangu ni bora kuliko samata.
 
Huyu jamaa kwa mtazamo wangu ni bora kuliko samata.
Samata haongezi chochote kwenye timu yetu ya taifa..anakuwa kama Nchimbi tu wa Yanga.

Note..najua kuwa yeye ni 2nd all time scorer wa Tz..but hakuna la ajabu.
 
Samata ana zali tu lakini hana lolote
Mchango wa Msuva akiwa timu ya Taifa, unaonekana kabisa,

Yaani unamuona jamaa akipigana kutafuta matokeo,

Jamaa yetu huwa anatembea tu uwanjani.
 
Mchango wa Msuva akiwa timu ya Taifa, unaonekana kabisa,

Yaani unamuona jamaa akipigana kutafuta matokeo,

Jamaa yetu huwa anatembea tu uwanjani.
Kuna wakati mechi za taifa star samata alikuwa hayupo wakawa wanafanya vizuri ,Mara aliporudi matokeo yakaanza kuwa mabaya tena ,kwanza akiwa uwanjani kila mchezaji anampa mpira wakati wapo washambuliaji kibao halafu anapoteza
 
Kuwakilisha anawakilisha ila sema umri sasa mazee,,kwenda ulaya kwny ligi kubwa itakua ngumu sana,,all in all he's doing the best hata akijaga stars naonaga he has impact than captain wetu mbabaishaji
Caption wetu kajisahau akaze tusimsahau jumla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…