mambo magumu sana haya mkuu,huyu kijana namwonea huruma kweli kweli.Nadhani c vibaya akimjua mtu aliyemleta duniani ila huyo c baba yake...
Nadhani c vibaya akimjua mtu aliyemleta duniani ila huyo c baba yake...
Mimi ni kijana niliyehitimu kidato cha sita na kuchaguliwa kuingia chuo fulani kikuu huko Dom mwaka jana. Nimelelewa kwa mapenzi makubwa ya baba na mama ambyo yamenifanya niwe na mafanikio sana ya kishule na maisha kwa ujumla. Baba yangu amkuwa na rafiki wangu wa karibu sana na mara kwa mara huwa tunashauriana mambo mengi .
Wiki iliyopita mama alikuja kunitembelea na akaomba jmosi twende Dar. Nilipomuuliza kulikoni kwenda dar akasema eti anataka kunionyesha baba yangu, huyu aliyenilea na kunitunza kwa mapenzi makubwa mpaka leo si baba yangu mzazi! Nimepigwa na butwaa mpaka muda huu.
Naomba ushauri nifanyaje ndugu zangu? Akili inanizunguka.
***** Hii ni email niliyopokea toka maeneo ya Dodoma Kijana akiomba ushauri wa haraka juu ya hayo aliyoeleza*****