Simulizi: Akwelina

Simulizi: Akwelina

SEHEMU YA 31 YA 50


Maneno ya Babu yalimpatia faraja Akwelina kwa kiasi kikubwa. Usiku ulizidi kukomaa siku hiyo Kakinga alichelewa sana kurudi nyumbani, Babu alipoona usiku unazidi kukomaa alimwambia Akwelina aingie ndani akalale lakini Akwelina alikataa kwa sababu alikuwa hajamuona Baba yake, Babu alijaribu kumshawishi Akwelina ili aingie ndani kutokana na baridi kuwa kali bado haikusaidia kitu. Baada ya masaa mawili kupita Kakinga alifika nyumbani akiwa amechoka sana siku hiyo , Akwelina alipomuona Kakinga alimkimbilia akamkumbatia , Kakinga akamuuliza Akwelina : Umekula binti yangu ?



Akwelina alijibu : Mama yangu yupo wapi Baba niruhusu kidogo tu nikamuone tafadhali nakuomba .



Kakinga alichukia sana akamjibu Akwelina kwa jazba na kwa sauti ya juu : Mimi ndio MAMA na BABA yako hakuna mwingine sihitaji uniulize tena hilo swali umenielewa ? Nenda ndani haraka ukalale kila mda Mama , Mama sasa kama hayupo Mimi nifanyaje ? Nenda ndaniii ??



Akwelina alilia sana baada kuona Baba yake anamkaripia, Kakinga alimuonea huruma Akwelina akambembeleza na kusema : Usijali mtoto wangu Mama yako atakuja siku moja sawa , Nisamehe kwa kukuogopesha mtoto wangu acha kulia Mama angu futa machozi .



Akwelina alimsikiliza baba yake akaacha kulia wakaingia ndani pamoja na Babu. Asubuhi na mapema palipo pambazuka Monna alikuwa katika Chumba alichofungiwa , Chumba hicho kilikuwa na mateso makali sana , Monna akiwa amechoka walikuja wanajeshi watatu wakamfunga kitambaa Monna kwenye macho alafu wakaondoka nae, baada ya hatua kadhaa walimfungua kitambaa kile Monna alijikuta yupo katikati ya watu wengi sana mfano wa Gereza, Monna akiwa bado anashangaa mazingira hayo alishikwa mkono alipogeuka alimuona Mama wa Akwelina , Mama huyo alimvuta Monna pembeni kisha akasema : Samahani mdogo wangu mtoto wangu niliyekupatia yupo hai na kama yupo hai ni mzima ? Daah masikini mtoto wangu ??



Monna alijibu : Yupo hai mtoto wako na anaitwa AKWELINA .



Mama alitokwa na machozi ya furaha akasema : Daah ahsante Mungu kumbe mtoto wangu mzima jamani ??



MONNA : Acha kulia mwanao ni mzima kabisa naomba nikuulize kwani ilikuaje na kwanini nilikukuta msituni na ukaamua kunipatia mtoto wako na hapa ni wapi ?



Mama alifuta machozi kisha akasema : Daah ni stori ndefu sana nakumbuka miaka kumi iliyopita nilikuwa ......





MAMA ?? Daah ni stori ndefu sana nakumbuka miaka 10 ( kumi ) iliyopita nilikuwa naishi na mume wangu #Steven maisha yetu yalikuwa yenye furaha na amani mume wangu alikuwa anapesa sana japo sikutambua anafanya kazi gani inayompatia pesa nyingi kama alizokuwa nazo, sikuhitaji sikuhitaji kumfatilia sana kwakua nilimuamini sana mume wangu. Siku moja mume wangu alikuja na Julius huyu ambaye ndio mmiliki wa eneo hili kwa sasa, Julius alikuwa mdogo wa mume wangu siku hiyo nilikuwa chumbani nikasikia wanatupiana maneno makali , baada ya muda mfupi nilisikia mlango unafungwa kwa nguvu nikatoka nje nikamkuta mume wangu peke yake akiwa na mawazo sana nilipomuuliza alinijibu “” Amechoka kufanya unyama kwa watu wasio na hatia “” ukweli sikuelewa anamanisha nini ikabidi nimuulize akasimama akaniambia



“” Leo mke wangu nahitaji utambue ukweli kuhusu Mimi lakini naomba usinichukie kwa ukweli wangu “”



Mume wangu alisimama akavua shati lake akanionesha alama iliyokuwa kwenye bega lake alikuwa ameandikwa neno #AKWELINA sikutambua neno lile lilikuwa na maana gani na kwanini alinionesha ile alama , Baada ya kunionesha aliniambia nikae chini kisha akasema



“” Mke wangu hili neno ni jina la…



“””” Nani monna hapa “” Monna na mama wa akwelina Walistuka baada ya askari mmoja aliyekuja akauliza jina la monna .



“” Ni Mimi hapa “” Monna alimjibu yule askari , yule askari alimchukua monna akaondoka nae. Monna alikasirika sana kwa sababu alitamani kujua mengi toka kwa mama wa Akwelina. Monna aliondoka na yule askari hadi ndani ya Chumba kimoja katika eneo hilo, Monna alipofika aliwakuta watu wengi sana wakiwa busy na computer ( kompyuta ) wakati anatazama huku na huko alimuona Patrick mbele yake hakutambua amekujaje mbele yake , Patrick akasema :



PATRICK ?? Oooh mrembo kipenzi changu wa zamani najua hujui kwanini upo hapa sio ?



MONNA ?? Ndio sijui hilo alafu samahani Mimi sio mpenzi wako bora kifo kuliko kuniita hivyo nakuchukia sana wewe mshenzi .



PATRICK ?? Hahaha tuliza hasira binti nimekuita hapa kuna kitu nahitaji kukuonesha muda huu upo tayari hebu tazama hapa katika computer hii unaona nini ?



Moyo wa monna ulipatwa na mshituko wa ajabu sana baada ya kumuona Kakinga akiwa anacheza na binti mdogo bila shaka monna alitambua yule ni akwelina monna alianza kutetemeka na kujiuliza maswali mengi kakinga yupo wapi hapo na wamewezaje kumuona. Kipindi monna anajiuliza maswali
 
SEHEMU YA 32 YA 50

mengi ndani ya kichwa chake Patrick alimsogelea akamwambia :-



PATRICK ?? Ndani ya mwili wa mtoto huyo kuna kitu cha thamani sana na popote alipo tukiamua kumtafuta tunampata na muda huu nazungumza na wewe tumeshatuma askari katika eneo hilo muda sio mrefu Kakinga na Akwelina wataletwa hapa na utawaona haha askari mrudisheni sehemu yake.



Askari walimrudisha monna sehemu alipokuwepo. Baada ya siku mbili majira ya mchana katika nyumba ya mvuvi akwelina alikuwa anang’oa majani akiwa anafanya shughuli hiyo alihisi kitu kibaya mbele yake , Akwelina akasimama akatazama mbele yake kwa umakini sana aka…





Akwelina akasimama akatazama mbele yake kwa umakini sana akaona nyasi zinatikisika kisha zinatulia, akwelina alikuwa binti jasili sana aliingia ndani akachukua panga alafu akaenda sehemu ile ambayo nyasi zilikuwa zinatikisika na kutulia, Kwa umakini wa kutosha bila woga alifika eneo hilo kabla hajafika sehemu husika ghafla alitokea mbwa wao akiwa na sungura mdomo kwake akwelina alistuka akapuuzia akageuka akarudi , Wakati huo wanajeshi waliotumwa na Patrick walikuwa wameshafika eneo hilo walimuona mtoto kwa mbali akiwa na mbwa pembeni kiongozi wao alifungua laptop akatazama picha ya mtoto walioagizwa ikabidi atumie bunduki yake aka zoom ( kukuza ) sura ya akwelina alipohakikisha ndio yeye alipiga sindano ya kifua. Sindano ile ilikuwa na madawa ikamfanya akwelina apoteze fahamu walipomsogelea ili wamchukue mbwa alijaribu kuwaziwia wakampiga risasi kisha wakaondoka na akwelina.



Muda ulisonga mbele hadi majira ya saa moja usiku majira hayo hayo kakinga na babu walifika nyumbani walishangaa giza limetawala nyumba nzima na haijawahi kutokea hofu ilitanda zaidi baada ya kimya kikubwa kilichotawala eneo hilo kakinga alianza kupata wasiwasi mkubwa sana akaingia ndani akachukua tochi akaanza kutembea huku na kule katika eneo hilo akiwa anamwita akwelina , Kakinga aliita sana bila mafanikio yeyote hali hiyo iliongeza hofu kwa kakinga. Katika kuzunguka huku na huko Kakinga alimkuta mbwa wao kafariki alipomchunguza aligundua yule mbwa alipigwa risasi Kakinga alitupa tochi chini akashika kichwa aligundua Akwelina atakuwa amechukuliwa na watu wabaya mvua ya machozi alianza kumwagika katika macho ya Kakinga.



Akwelina akiwa ndani ya gari pamoja na wale wanajeshi walitembea kwa muda mrefu kwa mwendo mkali kipindi chote hicho Akwelina alikuwa amefungwa kitambaa usoni ili asitambue sehemu alipokuwa anaelekea. Usiku huo huo kakinga alianza kutembea mtaa kwa mtaa akimuuliza yeyote aliyekutana nae , Baadhi ya watu katika eneo hilo walijua kakinga amechanganyikiwa. Asubuhi palipokucha wale wanajeshi walifika sehemu wakasimama wakamfungua akwelina kile kitambaa Akwelina alishangaa yupo sehemu ambayo ni tofauti na nyumbani kwao ( Mjini ) Akwelina akiwa anashangaa alishikwa mkono na msichana ambaye hamtambui, Muda huo huo simu ya huyo msichana ilipigwa akapokea :-



“””” Hellow who are you ( Habari wewe ni nani ) ?



?? ___ ?? Acha bwebwe zako hizo unaongea na kaka yako hapa Patrick , sikia warda huyo ni akwelina mtunze kesho kutwa unatakiwa uje nae huku makao makuu tumalize mchezo , Kakinga yupo mbali hawezi kujua kama mtoto yupo kwako na anaweza juaje kama yupo kwako sio rahisi hakikisha hatoroki sawa ?



WARDA ?? Sawa kaka nimekuelewa.



?? __ ?? Asubuhi njema .



Warda alimchukua akwelina akaingia nae ndani wale wanajeshi wakaondoka. Muda huo wa asubuhi kakinga alikuwa bado yupo mtaani akimtafuta akwelina, Alizidi kumtafuta bila kuchoka ghafla akasikia mtu anasema :-



“”” Kijana weka mikono juu ya kichwa chako alafu piga magoti kisha lala chini “”



Siku zote Kakinga alikuwa mbishi na anaejimini sana pamoja na kuambiwa hivyo aligeuka akamkuta mwanajeshi mmoja amemnyoshea bunduki, Hasira alizokuwa nazo kakinga zilimuongezea ujasili Kakinga akamvamia yule mwanajeshi bila kujali silaha aliyokuwa nayo , Kakinga alimzidi nguvu yule mwanajeshi akampiga sana akiwa anamuuliza mtoto alipo, kipigo kilivyozidi yule mwanajeshi alizungumza ukweli bila kupoteza muda Kakinga alimchukua huyo mwanajeshi akampakiza kwenye gari moja kwa hadi mjini. Walipofika mjini yule mwanajeshi alimpeleka sehemu mtoto alipokuwepo , Yule mwanajeshi alimwita , Warda alipokuwa ndani alichungulia mlangoni akamuona mwanajeshi wao akafungua mlango akatoka nje alipotazama upande wa kulia akakutana macho kwa macho na kakinga warda al…….





Warda alistuka sana baada ya kumuona kakinga mbele yake , yule mwanajeshi alipopata nafsi alikimbia , warda alipotaka kukimbilia ndani Kakinga aliziwia mlango akamshika shati akamsukuma hadi ndani kutokana na hasira alizokuwa nazo Kakinga alikunja ngumi ili ampige warda lakini kabla ya kitendo hicho akwelina alishika mkono wa baba yake akiwa anatokwa na machozi .



??”” Baba usimpige utamuumiza baba ” yalikuwa maneno ya akwelina akimuomba baba yake .



??__ Acha nimfundishe adabu huyu sio mtu mzuri kwako binti yangu huoni kwamba alitaka kukuchukua bila ruhusa yangu nahitaji nimfunze adabu huyu mwanamke ili siku nyingine akuogope “” Kakinga
 
SEHEMU YA 33 YA 50

alimjibu akwelina akiwa ana hasira.



Akwelina alijitahidi sana kumziwia baba yake, Kwa muda mrefu kakinga akakubali ombi la akwelina akamuachia warda akamshika mkono akwelina wakaondoka baada ya hatua kadhaa wakiwa wanaelekea nje ilisikika sauti ya warda ikisema:



??__ Naomba nikusaidie Kakinga mume wangu ili ufanikiwe hicho unachohitaji tafadhali.



??__ Funga mdomo wako kamwe siwezi kuwa na mke kama wewe usinifanye nibadili uamuzi huu “” yalikuwa ni majibu ya Kakinga akimjibu warda.



??__ Sawa sikatai lakini bila Mimi huwezi kumpata mama wa mtoto huyo “” Warda alimjibu kakinga .



Majibu ya warda yalimvunja nguvu kakinga akamtazama akwelina akaona dalili ambazo sio nzuri ikabidi aondoke. Warda alitumia njia zote lakini kakinga hakumsikiliza.

Baada ya kutoka kwa warda Kakinga aliamua kwenda sehemu aliyokuwa anaishi mwanzo kipindi cha nyuma sana wakati akwelina alipokuwa mdogo sana japo palikuwa mbali sana lakini walijitahidi wakafanikiwa kufika eneo kwa bahati nzuri kakinga alimkuta yule mwenyeji wake, Yule mwenyeji aliwapokea bila matatizo yeyote.



Yalipofika majira ya usiku monna akiwa ndani eneo lile alijitahidi akafika kwa yule mama wa Akwelina , monna alipofika alimkuta mama yule, Yule mama alipomuona monna cha ajabu alifurahi akasema:-



MAMA ?? Afadhali umekuja mdogo wangu .



MONNA ?? Kwanini Dada yangu ?



MAMA ?? Kesho ninahamishwa hapa napelekwa wapi masikini lakini namuachia mungu nilikuwa namuomba mungu utokeze ili nikuone Mara ya mwisho naweza hata kufa huko daah , Pia nilihitaji kukumalizia historia ya maisha yangu hadi nilipokutana na wewe sasa naomba unisikilize mume wangu aliponionesha ile alama akaniambia hivi :-

“”” Mke wangu hili neno ni jina la kampuni ya baba yetu alituachia Mimi na mdogo wangu Julius kabla baba hajafariki alituchora alama hizi kama kiapo ili tushirikiane , Kampuni hii ilikuwa mbaya sana ilikuwa inafanya mauaji , inanyanganya Mali za watu pia tulikuwa tunauza watu nje ya nchi kifupi kampuni hiyo ilikuwa mbaya sana na ilianzishwa na babu kabla baba yetu hajazaliwa nilikuepo ndani ya kampuni hiyo lakini ukweli sikupenda matendo ya kampuni hiyo. Baba alipofariki mama aliendeleza kusimamia kampuni yetu. Siku ya masiba wa mama kama unakumbuka sikuepo huku tanzania, Nilipofika hapa Tanzania nilifanya uchunguzi wangu nimegundua Julius ndio kafanya mauaji kwa mama ??



Mume wangu aliishia hapo nikamuona anasimama akachukua ufunguo wa gari akaondoka , Nilisubiri sana hadi majira ya usiku uchungu ukanishika mfanya kazi wangu wa ndani alinisaidia kupiga simu kwa daktari wetu akaja akanizalisha mtoto wa kike ambaye ndio niliyokupatia. Baada ya masaa mawili mume wangu akaja akiwa amechoka sana akanikuta nina mtoto cha ajabu akachukua kisu na na sindano ya nguo akaweka Uzi ndani ya sindano akamchukua mtoto akamchana katika tako lake la kesho akaweka ufunguo mdogo sana akamshona bila huruma Mtoto wangu alilia sana nilishindwa kuvumilia ikabidi nimfuate mume wangu akaniambia nimuache kwanza, kwakua nilikuwa namuamini nikamuacha alipomaliza kumshona aliondoka na mtoto hadi chumbani akafunga mlango. Nikasikia mtoto wangu analia sana muda kidogo akatoka nje akiwa na begi lenye vitu ndani yake pamoja na mtoto mkononi kwake alikuwa ametapakaa damu nyingi sana akaniambia nikimbie haraka pamoja nilikuwa na maumivu lakini nilijitahidi kukimbia nikiwa mbali na nyumba yetu nilisikia sauti ya mume wangu ikilalamika nilitamani kurudi lakini nikajikaza nikaendele kukimbia ndio nikakutana na wewe nikakupatia mtoto wangu sijui ule ufunguo ulikuwa na nini daah ….





Mama wa akwelina alishimdwa kuziwia hisia zake alianza kulia kwa uchungu pindi alipokumbuka maumivu aliyoyapata siku za nyuma , Moyo wa monna ulipatwa na huruma baada ya kufahamu ukweli kuhusu maisha ya akwelina pamoja na familia yake, Kilio kutoka kwa mama wa akwelina kilizidi kuiteka nafsi ya monna hali iliyomfanya monna ashushe mvua ya machozi katika macho yake, wakiwa katika majonzi hayo alikuja askari mmoja akamchukua mama wa akwelina kisha akaondoka nae japo mama huyo hakutambua wapi anapelekwa.



Siku iliyofuata asubuhi na mapema kakinga alijiandaa akaenda katika shule iliyokuwa karibu na sehemu wanapoishi alipofika shuleni hapo alizungumza na mwalimu mkuu kwa muda mrefu sana mwisho mwalimu mkuu alisema :-



”’ Kijana mlete mtoto wako apate elimu bora katika shule hii kwakua umenieleza maisha yako yalivyo nakupa nafasi ya pekee utalipa ada ya mtoto chochote utachokuwa nacho hata usijali kijana wangu nimeamua kukusaidia ili binti yako apate elimu bora nitakusaidia kila utapokwama katika ada ya mtoto.



Majibu ya mwl / mkuu yalimpatia matumaini makubwa sana kakinga hali iliyomfanya aondoke hadi sokoni akanunua nguo za shule kwa maandalizi ya akwelina mtoto wa pekee anayempenda sana, Mapenzi aliyokuwanayo kakinga kwa akwelina yalikuwa ya juu sana hadi watu wote waliokaribu yao waliamini akwelina ni mtoto wa kakinga aliyemzaa mwenyewe kwa upendo aliokuwa nao kakinga .



Asubuhi ya siku ya pili kakinga alimpeka akwelina shule kwa bahati nzuri alifanikiwa kumwandikisha
 
SEHEMU YA 34 YA 50

katika shule ile, furaha haikuwa kwa kakinga pekee hata akwelina alifurahi kuanza shule. Maisha ya akwelina alipoanza kusoma yalikuwa mazuri sana, akwelina alikuwa mtoto mwenye uwezo mkubwa katika masomo kwa uwezo huo aliokuwa nao akwelina alipendwa na wengi sana ndani ya shule ile. Miaka ilizidi kwenda mbele nae akwelina alizidi kukuwa siku hadi siku hatimae akwelina akawa msichana mwenye miaka kumi na sita ( Miaka 16 ) Miaka yote hiyo Julius na Patrick waliendelea kumsubiri warda na walipozungumza nae warda aliwambia :-

“” Kaka yangu patrick ondoa shaka akwelina yupo mikononi mwangu acheni kumtafuta na nimeondoka kidogo muda sio mrefu nitarudi ondoeni wasiwasi “” Maneno hayo yaliwafanya waache suala la akwelina kwa muda wakaendelea na kazi yao ya unyanganyi.



Katika ukuaji wa akwelina alikumbana na vikwazo vingi vilivyomlenga mama, Vikwazo hivyo vilikuwa vinampatia maumivu makali lakini hakuhitaji kumwambia baba yake ( kakinga ) kwakua siku zote alipojaribu kuuliza suala kuhusu mama yake baba alikuwa mkali sana na siku zote akwelina hakuhitaji kumfanya baba yake akose furaha. Siku moja katika siku za uhai majira ya usiku akwelina alikuwa nje akitazama juu , kakinga alipomtazama akwelina aligundua hana furaha ikabidi amsogelee kabla hajamgusa alisikia akwelina anasema :-

“”__ MAMA upo wapi __ “”



Maneno hayo yalimuumiza sana kakinga akarudi ndani akatafakari sana kisha akachukua begi alilohifadhi vitu vyote alivyopewa monna kipindi anakabidhiwa mtoto, kakinga akarudi nje akampa akwelina lile begi akasema :-



“”_ Binti yangu ndani ya begi hilo ndio kuna ukweli wote kuhusu mama yako kwahiyo fungua begi hilo ndani yake utafahamu ukweli wote **



Kakinga akarudi ndani akamuacha akwelina njia panda , ilimchukua muda sana lakini akajitahidi akafungua lile begi akakuta vitu sio vingi akapekua pekua akaona kitabu kidogo akakifunua kile kitabu, Ndani ya kitabu kile kiliandikwa _??



??_Leo tarehe 16 mimi Steven nimeamua kuandika maneno hayo ndani ya kitabu hiki kidogo kwa sababu maisha yangu na mke wangu JAMILA pamoja na mtoto wangu yapo hatarini …..





JAMILA pamoja na mtoto wangu yapo hatarini, Ndani ya mwili wa binti yangu katika tako lake la upande wa kushoto nimeweka ufunguo wa dhahabu. Najua mdogo wangu Julius lazima atakuja kufuata ufunguo huu kwa sababu ndani ya kampuni ya marehemu baba ambao inaitwa #AKWELINA kuna chumba kimoja chenye hazina zote na hati miliki ya kampuni hiyo.



Akwelina alisimama akafunika kile kitabu akaingia chumbani kwake akavua nguo akagusa tako lake akagundua kuna alama nyeusi, Akwelina hakuridhika akafinyafinya eneo hilo akaona kuna uvimbe ndani ya ngozi yake akagundua bila shaka huo uvimbe ndio ufunguo aliowekwa na baba yake. Akwelina alivaa nguo zake akaendelea kusoma kitabu kile .



??__ Leo hii hii nazungumza ukweli kuhusu kampuni ya baba hii ya akwelina, Kampuni hii imeanza muda mrefu sana kabla sijazaliwa kwa maana hata nilipozaliwa niliikuta hiyo kampuni. Siku nilipogundua matendo yanayofanyika ndani ya kampuni hiyo niliumia sana nikajaribu kuiteketeza kampuni hii lakini nilishindwa kwa sababu kuna viongozi wakubwa wapo katika kampuni hii ndio nikaamua kuiba ufunguo huu wanaoutegemea ili siku kitabu hiki kikiwafikia askari watenda haki naomba mkawasaidie watu waliomo ndani ya kampuni hiyo na naomba kwa ambaye ataemuokota binti yangu huyu akiwa bado ni mzima Naomba amlinde na amtunze binti yangu nampenda sana, Mimi sio wa kupona lazima Julius ataniua jina la mtoto wangu naomba aitwe HASMA , kuna picha nimeziweka ndani ya bahasha ndogo hao ndio washiriki wakuu wa kampuni hii, Kwaheri binti yangu nakupenda zaidi mungu akulinde daima.



Akwelina alimaliza kusoma kitabu hicho mikono ikimtetemeka kwa maumivu aliyokuwa anayapata ndani ya moyo wake. Kilio kisichokuwa na mfano kiliutawala moyo wa akwelina hali iliyomstua sana Kakinga alipokuwa chumbani kwake alisikia sauti ya akwelina ikilalamika kwa kulia sana. Ilimbidi kakinga amfuate Akwelina chumbani kwake akajaribu kumtuliza cha ajabu kwa Mara ya kwanza akwelina alimsukuma kakinga akadondoka chini. Ilikuwa kama ndoto kwa Kakinga akwelina akasimama akiwa na jaziba sana akamwambia Kakinga

?? Wewe sio mtu mzuri kwangu haiwezekani siku zote unanificha ukweli huu ambao nimeufahamu leo , Kumbe wewe sio baba yangu mzazi daah naumia sana kumbe baba yangu ameuwawa pamoja na mama yangu alafu umeendelea kunificha kweli maana yako ilikuwa ipi eeeh nakuuliza maana yako ilikuwa ipi ?



?? Akwelina binti yangu wewe leo hii unaweza kunisukuma Mimi !! ni kweli pengine Mimi sio baba yako mzazi lakini kwa shida nilizopata toka kwako kwa ajili ya kusaidia maisha yako mungu ndio anaejua lakini usijali haya ndio maisha, Sababu iliyonifanya nikufiche ukweli huu ulikuwa bado mdogo sana na ningekuaribu akili laiti kama ungetambua ukweli huu lakini bado hujachelewa unaweza kuondoka muda huu ili ukafanye hicho kilichopo akilini kwako umekuwa binti sasa na mwenye nguvu unaweza kuondoka
 
SEHEMU YA 35 YA 50

Akwelina.



Majibu ya Kakinga yalimfanya akwelina ajione mkosaji sana mbele yake bila kupoteza muda akwelina alipiga magoti mbele ya Kakinga akaomba msamaha, Kakinga alimnyanyua akwelina akamwambia:



__ Anaestahili kupigiwa magoti ni mungu pekee sio binadamu kwa sasa sina nguvu siwezi kukulinda tena ondoka binti Julius nenda katafute nguvu ili kesho nguvu hizo zikusaidie Mimi muda huu nina umri mkubwa siwezi kukulinda tena lakini usijali lala kesho tutazungumza vizuri.



Kakinga aliondoka moja kwa moja hadi katika Chumba chake, Usiku ulikuwa mrefu sana kwa akwelina kwa kitendo alichofanya kwa kakinga. Asubuhi na mapema akwelina alitoka chumbani kwake akaondoka hadi katika Chumba cha Kakinga alistuka kuona mlango upo wazi bila kupiga hodi akwelina aliingia hadi chumbani akakuta chumbani hakuna mtu kitu kilichompatia wasiwasi zaidi hakuona nguo hata moja ya kakinga. Hofu na wasiwasi ulitanda katika moyo wa akwelina aka…….





Hofu na wasiwasi ulitanda katika moyo wa akwelina akaanza kumtafuta Kakinga huku na kule alitumia muda mrefu sana kumtafuta baba yake mlezi ( kakinga ) toka majira ya asubuhi hiyo hadi usiku ulipotanda, lakini hakufanikiwa kumuona baba yake ?? kwakua giza lilikuwa limeshakuwa nene ilibidi akwelina arudi nyumbani, Njiani akiwa anarudi nyumbani alikuwa analia kama mtoto hali iliyomshangaza yeyote aliyekutana nae, baadhi ya watu aliokuwa anakutana nao walijaribu kumuuliza akwelina kama anatatizo ili wamsaidie ila majibu yake yalikuwa ni kilio tu. Akwelina alifika nyumbani salama japokuwa alikuwa na mawazo sana alipohitaji kuingia chumbani kwake aliona karatasi chini ya mlango akaiokota akaingia ndani akaifunua ile karatasi akaisoma ilikuwa imeandikwa ??



??__ Akwelina binti yangu sijui unanichukia kiasi gani kwa kukuficha ukweli wa maisha yako naomba nisamehe sana kwa hilo , Pili naomba usinitafute nimeenda mbali sana sio rahisi kuniona nilipo kwa sasa lakini usivunjike moyo binti yangu kwa uamuzi huu niliofanya, kuanzia muda huu unatakiwa uwe na nguvu na tegemea ulichonacho , Tegemea unachokiona kwa macho, Tegemea ulichonacho ili kupata ambacho huna, Jitegemee akwelina tarajia msaada kwa watu lakini usiwategemee binadamu sio wazuri.

Akwelina binti yangu jifunze kupitia ndege ,Ndege siku zote anapotuwa kwenye tawi la mti huwa hana hofu kwa sababu matumaini yake hayapo kwenye tawi alilotuwa, bali yapo kwenye mbawa zake. Tegemea uwezo wako , Usitegemee kuwezeshwa kwa sababu yeyote anaekupandisha anauwezo wa kukushusha pambana binti yangu nakutakia maisha mema akwelina.



Karatasi aliyokuwa anasoma akwelina ilikuwa kama imemwagiwa maji kutokana na machozi yaliyokuwa yanamtoka _



??Nisamehe baba siwezi kuwa imara bila wewe rudi baba rudi bab yangu nakuhitaji binti yako wewe ndio udhaifu wangu baba ?? alisema akwelina akiwa analia mno.



Baada ya miezi mitano kupita maisha ya akwelina yalikuwa magumu sana, akwelina akawa hafanyi vizuri katika masomo yake, Mwili wake ulikuwa dhoofu kwa kutokula vizuri , hali iliyowapatia maswali mengi Majirani wengine walimuonea huruma na kutupa lawama kwa kakinga kwa kusema



” Kakinga kamterekeza mtoto wake “



Baadhi yao walisema



” Kakinga sio mtu ni zaidi ya mnyama hawezi kumfanyia hivi binti yake “”



Miezi ilizidi kukatika mwalimu mkuu alimfuata akwelina akamuuliza tatizo linalomsumbua, Akwelina hakumficha alimueleza ukweli wote, Mwalimu mkuu akaamua kumchukua akwelina akaenda kuishi nae nyumbani kwake. Siku hadi siku hali ilizidi kuwa mbaya kwa akwelina ilikuwa ngum kwa mwalimu mkuu kumuelewa akwelina anatatizo gani linalomsumbua ikabidi amulize vizuri, Akwelina alijibu kwa unyonge



?? Namtaka baba samahani mwalimu wangu unaweza kuniletea baba yangu mbele yangu siwezi kuishi bila yeye siwezi Mimi namtaka baba ??



Mwalimu mkuu alijisikia vibaya sana alijaribu kumliwaza na kumpatia faraja kwamba ipo siku baba ake atarudi kidogo akwelina alifarijika. Jioni ya siku hiyo Julius alishindwa kuvumilia akamfuata Patrick akamkuta Patrick yupo anawatesa baadhi ya wafungwa Julius akamwita pembeni akamwambia :-



JULIUS ?? Kesho unatakiwa uanze uchunguzi rasmi kuhusu Akwelina bila shaka warda atakuwa anatudanganya sio mkweli au unasemaje kwa sababu hadi leo miaka mingi imepita .



PATRICK ?? Ni kweli ndugu yangu huyu warda huyu anampenda sana yule kijana ( Kakinga ) ambaye yupo na akwelina lakini usijali kesho nitamtafuta kwa kupita mtandao alafu nitawatuma askari wetu tutafanikiwa tu usijali lakini hivi ni kweli akwelina ni mtoto wako ?



JULIUS ?? Hapana yule ni mtoto wa kaka yangu elewa hivyo tu na hii ni siri olewako umwambie mtu yeyote.



Asubuhi ilipofika Patrick aliingia katika Chumba cha computer akamtafuta akwelina muda mchache akampata, GPS ikamunesha hadi mtaa aliopo kwa sasa Patrick alifurahi sana kisha …
 
SEHEMU YA 36 YA 50





Patrick alifurahi sana kisha akaita askari wengi wakachukua magari , Patrick akapanda ndege aina ya helicopter kwa ajili ya msako huo. Safari hiyo haikuwa ndefu kwa sababu walitumia vyombo vyenye nguvu sana na vinavyotembea kwa kasi kubwa kutokana na vyombo hivyo kuwa imara walifika mapema sana katika nyumba ya mwalimu mkuu ambapo mitandao yao ya GPS kwa kupitia kifaa kilichopo ndani ya mwili wa akwelina ilionesha wanaomtafuta yupo ndani ya nyumba hiyo bila kupoteza muda wale wanajeshi walivunja mlango ( geti ) Mlio wa geti hilo uliwastua wote waliokuwepo ndani akiwemo akwelina na familia ya mwalimu mkuu. Wale wanajeshi waliingia ndani wakawateka watu wote waliokuwepo ndani wakatoka nao nje lakini hawakumtambua akwelina ni yupi katika watu waliowateka japo mtandao ulionesha yupo hapo hapo.



©_ Tumewakosea nini askari wetu ? Mwalimu mkuu aliwauliza .



®_ Shida yetu sisi ni msichana anaeitwa akwelina na yupo hapa hapa na kama hutaki matatizo mzee mtaje huyo msichana ni yupi lakini usipozungumza ukweli hakika utajuta mzee wangu… Patrick alimjibu mwalimu mkuu kwakua aliambiwa jina na mdogo wake ( warda ) .



Kimya kilitawala kwa muda mrefu akwelina alikuwa anatetemeka sana kwa hofu alitambua lazima mwalimu mkuu atamtaja japokuwa alikuwa anajiuliza kwanini wale wanajeshi wanamtaka. Baada ya kimya kirefu patrick aliwapa kazi askari wake, Wale askari walimvuta pembeni mwalimu mkuu wakaanza kumpiga. Kichapo kilikuwa kikubwa zaidi mwalimu hakusema kitu japo alikuwa anapata mateso na maumivu makali, sauti ya mwalimu mkuu akiwa analalamika ilimfanya akwelina asimama akasema :-



?? AKWELINA ni Mimi hapa kuna shida gani au nimekosa nini ? Naomba msimsumbue mzee wangu .



Patrick alicheka sana , akacheka zaidi alafu akamsogelea akwelina akamzunguka akiwa anamtazama,



“” Umekuwa binti mkubwa kiasi hiki ama kweli wanawake mnakuwa kwa kasi sana , Askari mchukueni huyu binti tuondoke “” yalikuwa maneno ya Patrick.



Askari walimchukua akwelina wakaondoka nae hadi kwenye gari, bado akwelina alikuwa hajaelewa kafanya nini , Patrick aliamua kumjibu akwelina Baada ya kumuona anahoji sana :-



PATRICK ?? Sikia binti usitusumbue lakini sababu ya kukufuata hapa leo hii ni kwamba unakitu chenye thamani ndani ya mwili wako ambacho kitaifanya kampuni yetu inayoitwa AKWELINA izidi kuwa bora.



Akwelina alistuka baada ya kusikia maneno hayo akatambua watu hao sio watu wazuri akakumbuka maelezo yaliyokuwepo katika kitabu alichosoma , Ghafla akakurupuka akaanza kukimbia patrick na askari wake alianza kumkimbiza kwa kutumia miguu walimkimbiza kwa muda mrefu sana akwelina akachoka mwendo ukapungua wale askari kwakua walikuwa na mazoezi walimkaribia akwelina, walipotaka kumshika alitokea mtu akiwa na baiskeli katika baiskeli hiyo alikuwa amefunga miti mirefu mingi mno. Cha ajabu akawaziwia kwa kukaa mbele ya wale askari wakiwa na Patrick, yule mwenye baiskeli akashuka akamfuata akwelina wakati huo akwelina aliamua kukaa chini kwa sababu aliishiwa pumzi akamshika mkono akwelina akaondoka nae, Patrick pamoja na askari wake walifanikiwa kuvuka eneo lile kwa muda mrefu hali iliyowafanya wampoteze akwelina pamoja na mtu aliyewaziwia njia .



Safari ilizidi kuwa ndefu ilifika hatua akwelina alishindwa kabisa kutembea yule mtu akambeba hadi walipofika sehemu salama muda wote huo akwelina alikuwa hajamtambua yule mtu ikabidi amvue kofia aliyokuwa amevaa , Akwelina hakuamini kumuona kakinga ( baba mlezi ) yupo mbele yake, moyo wa akwelina ulipatwa na furaha ya ajabu ambayo hakutambua imetokea wapi akamkumbatia baba yake. Kakinga akaendelea kumbeba akwelina hadi katika nyumba moja ambayo ilikuwa nje ya jiji hilo walipofika alimshusha Akwelina akasema :-



KAKINGA ?? Hapa tupo sehemu salama .



AKWELINA ?? Nisamehe baba yangu nakupenda naomba usiniche tena wewe ndio kila kitu kwangu.



KAKINGA ?? Hatuna muda wa kupoteza inabidi uvumilie nikutoa kifaa ulichonacho mwilini kwako vinginevyo bado wataendelea kukufuata popote ulipo najua Patrick hakutoa kifaa hicho wakati ukiwa mdogo haijalishi kipi kitatokea kwako lakini lazima tukitoe kifaa hicho .



Akwelina alikuwa hajui suala hilo Kakinga aliingia ndani akachukua wembe pamoja na mkasi kisha ….





Kakinga aliingia ndani akachukua wembe pamoja na mkasi kisha akamsogelea akwelina akamuuliza kama yupo tayari, akwelina alikuwa japo alikuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake. Macho ya kakinga yaliangaza huku na huko akasimama akaokota kipande cha mti ..



“” Akwelina ng’ata kipande cha mti huu kitakusaidia kupunguza maumivu najua utaumia sana lakini vumilia ili uwe salama sawa mama”” alisema kakinga akiwa anampatia kipande hicho cha mti.



Akwelina alifanya kama alivyoambiwa na baba yake, Upasuaji ulianza bila dawa yeyote ambayo ingeweza kusaidia kupunguza maumivu ( ganzi ) katika upasuaji huo ( operation ) Kakinga alishika mkono
 
SEHEMU YA 37 YA 50

wa akwelina akasogeza kisu hadi katikati ngozi ya kwanza, Kisu kilipofika kwenye ngozi akwelina alisisimka mwili mzima akafumba macho na kuruhusu kisu kichane ngozi yake, Kakinga alichana ngozi akaifikia nyama akaichana pia bado hakufika sehemu ambayo kifaa kile kilikuwepo ikabidi ashindilie kisu kikazidi kuingia ndani zaidi, Akwelina alipata maumivu makali mno akapiga kelele kali ghafla akapoteza fahamu, Kakinga alitumia nafasi hiyo akafanikiwa kutoa kifaa ambacho kilikuwa kinamuonesha popote alipokuwepo, Kakinga alipomaliza kufanya kazi hiyo alimchukua akwelina moja kwa moja hadi kituo cha afya akamuomba daktari amshone akwelina katika jeraha lile daktari alitaka barua toka kituo cha polisi cha ajabu Kakinga alitoa pesa nyingi sana akampatia daktari ili amsaidie, Pesa ni kila kitu katika dunia yule daktari alitoa huduma haraka, Baada ya matibabu Kakinga alimchukua akwelina akarudi nae nyumbani muda wote huo akwelina alikuwa bado hajarudisha fahamu .



Baada ya kumkosa akwelina Patrick alirudi ndani ya kampuni yao akiwa amechoka sana walipofika Julius alimpatia adhabu Patrick pamoja na wenzake kwa kushindwa kumleta akwelina. Patrick aliwekwa katika Chumba alichokuwepo monna ghafla akasikia sauti ikicheka ndani ya chumba hicho , patrick alistuka sana akaanza kutembeza macho huku na huko akamuona monna mbele yake ;



“””Unaogopa nini Patrick mpenzi wangu hahaha kweli watu wanaopendena watakuwa pamoja kila sehemu umekuja hadi huku kunifuata Mimi jamani mpenzi??



Monna alimwambia patrick akiwa anacheka sana kwa dharau. Patrick alichukia sana baada ya kuona monna anamdharau, patrick alimpiga kibao Monna kisha akakaba shingoni akamwambia :-



PATRICK ?? Nitakuua monna sipendi mtu anidharau sipendi monnaaaa na hujui mtu anamatatizo gani ohoo .



MONNA ?? Mbona unachelewa niue sasa hivi utakuwa umenisaidia sana sina thamani katika maisha haya.



Patrick alimsukuma monna mbali, monna alidondoka chini lakini bado alikuwa anamcheka sana. Siku ya pili majira ya jioni akwelina alirudisha fahamu zake kitu cha kwanza alisema “” BABA UPO WAPI ‘” bahati nzuri baba hakuwepo mbali alisogea akwelina alizidi kufurahi furaha yake ilimfanya alie baba akamfuta machozi akamwambia :



KAKINGA ?? Kwanini unalia binti yangu ?



AKWELINA ?? Nimekukumbuka baba yangu leo hii furaha yangu imerejea tena nakupenda sana baba yangu.



KAKINGA ?? Usijali binti yangu kwa uwezo wa mungu nimenunua nyumba kubwa sana kwahiyo kesho asubuhi tutaenda nyumbani kwetu sawa mama ?



AKWELINA ?? Kweli baba woooh ?? kumbe uliponikimbia ulikwenda kutafuta pesa Mimi nilijua uliniacha kwa sababu nikikusukuma baba .



KAKINGA ?? Kukukimbia ?? !!



AKWELINA ?? Ndio baba umesahau kama ulinikimbia ?



KAKINGA ?? Ooooh ndio lakini usijali binti yangu nimeshasahau yaliyopita jiandae kesho safari.



Usiku wa siku hiyo ulikuwa mfupi sana kwa akwelina kwa sababu alikuwa na furaha sana siku hiyo. Asubuhi majira ya saa mbili akwelina alikuwa bado kalala akaamshwa na mlio mkali wa gari, akwelina alikurupuka hadi nje akamkuta Kakinga ndani ya gari zuri sana ikabidi arudi ndani akajiandaa haraka haraka alafu wakaondoka. Walitumia masaa kadhaa wakafika katika jumba zuri la kifahari bado ilikuwa ndoto kwa akwelina hakuamini alichokuwa anakiona, Lakini alishangaa kuona milango inafungwa yote baada ya kuingia ndani alafu Kakinga akacheka sana , kicheko kilizidi hadi kikampatia wasiwasi akwelina. Akwelina alimuuliza kakinga :-



AKWELINA ?? Kuna nini baba mbona unacheka sana ?



KAKINGA ?? Nimefanikiwa leo hahaha nimefanikiwa wooh. Unahitaji kujua kwanini nafurahi ?



AKWELINA ?? Ndio baba yangu .



Kakinga aligeuka upande wa pili , ambapo akwelina alikuwa anamuona kwa nyumba ( mgongoni ) akavua ngozi ya juu aliyokuwa amevaa, Ilikuwa kama maigizo mbele ya macho ya akwelina, Kakinga baada ya kuvua ngozi aliyokuwa ameivaa akwelina aliona umbile la mwanamke na sio mwanaume tena, Yule mwanamke alipogeuka akwelina alistuka kumuona yule dada ambaye kipindi alipokuwa mdogo Kakinga ( baba yake mlezi ) alitaka kumuua ambaye ni WARDA ????



Warda alipiga makofi wakatokea wanaume wanne wenye nguvu za kutosha alafu akasema :-



WARDA ?? Monna binti wa Kakinga hahaha kweli wewe ni kipofu nimeishi na wewe muda wote huo hujanitambua kama Mimi sio baba yako pole sana lakini usijali upo sehemu salama japo inamaumivu kwako nimekuokoa toka katika mikono ya kaka yangu kwa sababu ninataka kufanya kazi na wewe ila kazi hiyo haitakiwi uwe bikra na ndio maana nimewaleta wanaume hawa watoa bikra yako kabla kazi yetu haijaanza . Vijana fanyeni kazi yenu .



Wale vijana walimsogelea akwelina waka………



Wale vijana walimsogelea akwelina wakamshika wakamfunga kamba katika mikono yake ili iwe rahisi kufanya walichokusudia, akwelina alijitahidi kujiziwia ili asifanyiwe unyama huo Lakini kwakua wanaume hao walikuwa na nguvu za kutosha walifanikiwa kumdhibiti akwelina wakamlaza chini akwelina akiwa chini alifunga miguu yake ( kubana muguu ) hali iliyowafanya wale watu washindwe kumuingilia kimwili ( kumbaka ) Mmoja kati ya wale wanaume wanne alichukia sana baada ya kuona akwelina anawasumbua
 
SEHEMU YA 38 YA 50

akampiga ngumi ya tumbo , ngumi hiyo ilimpatia maumivu makali akwelina akapiga kelele kali za kuomba msaada , kelele hizo zilimstua mtu mmoja aliyekuwa amefungwa kamba ndani ya chumba cha pili katika nyumba hiyo hiyo. Yule mtu alijitahidi akakata kamba alizokuwa amefungwa kisha akavunja mlango akawakuta wanaume wanne wanataka kumbaka binti mmoja aliyekuwa amelala chini katika mikono yake amefungwa kamba na nguo za binti huyo zilikuwa zimechanika chanika alipomtazama vizuri yule binti alistuka akasema :-



“”” Haaaah ?? !! Warda pamoja na kuniteka na kunifungia ndani bado unataka kumfanyia unyama binti yangu haiwezekani leo sikuachi salama umewaleta watu wambake binti yangu leo utajua mimi ni nani nani ? Ninyi washenzi mnataka kuniharibia binti yangu ??. “” Kakinga alisema maneno hayo akiwa na hasira sana.



Kakinga aliwamia wale wanaume akaanza kupambana nao, Warda alipoona balaa hilo akafungua mlango akakimbia, Pambano liliendelea kwa muda mrefu kakinga akafanikiwa kumuua mmoja kati ya wale wanne. Wengine walipoona mwenzao kapoteza maisha walikimbia wote, Kakinga alimnyanyua binti yake akamkumbatia akiwa analia kwa hasira, Kakinga alijilaumu sana kwa kuondoka nyumbani na kumuacha akwelina peke yake hadi kupelekea kupata matatizo hayo, Suala hilo lilimpatia maumivu makali sana. Kakinga aliokota ile ngozi bandia aliyokuwa amevaa warda pamoja na kifaa maalumu kinachotoa sauti ya kakinga akasema :-



KAKINGA ?? Huyu warda mshenzi sana aliniteka siku ya pili baada ya kutoka nyumbani, nilikutana nae mtaani akiwa na wenzake akaniambia niungane nae ili akachukue hiyo kampuni yao inaitwa AKWELINA sijui, Nikakaa ndio akanifungia ndani lakini Mara ya mwisho alikuja na daktari mmoja akanivisha kifaa hiki katika shingo langu sikufahamu wanataka nini kumbe lengo lao lilikuwa hili daah pole sana binti yangu .



AKWELINA ???? Huyu dada sio mtu mzuri mara ya mwisho alinisaidia nilipokaribia kushikwa na wanajeshi wengi nilipomuangalia usoni niligundua ni wewe alikuwa anafanana na wewe na sauti ni kama yako baba yangu kumbe haukuwa wewe mungu wangu mimi daah baba yangu niahidi kwamba hautanikimbia tena nisamehe baba yangu bila wewe nitakufa mimi na leo ningekuwa nimeshabakwa usiondoke tena baba.



KAKINGA ?? Ni kweli binti yangu na nahisi alitambua kama kaka yake ( Patrick ) amekuja kukufuata wewe kwa sababu anakifaa kinachompatia taarifa na siku ya mwisho alipokea ujumbe wa sauti ukimjukisha wewe upo eneo gani, Sasa kwakua wanataka vita nilikuwa mpole kwa muda mrefu sasa nataka wanitambue Mimi ni nani tuondoke binti yangu .



Kakinga alimchukua akwelina wakaondoka moja kwa moja hadi walipokuwa wanaishi mwanzo Kakinga akachukua vitu vyote vinavyomuhusu akwelina kisha wakaenda mbali sana nje ya mji ambapo palikuwa ufukweni mwa bahari katika nyumba ya mzee aliyewahi kuwasaidia kipindi cha nyuma. Nyumba hiyo ilikuwa imebomoka ,Kakinga akaitengeneza na kuiboresha akishirikiana na akwelina kazi ilikuwa ngumu sana mwisho wakafanikiwa kuifufua nyumba ile. Yalipofika majira ya usiku akwelina alimuona baba yake hana furaha akamuuliza :-



AKWELINA ?? Kwanini una mawazo baba yangu na huna furaha ? Mimi ni mzima umenisaidia baba yangu toka katika mikono ya wale watu wabaya.



KAKINGA ?? Nimekumbuka mbali binti yangu kuna mzee aliwahi kutusaidia ulipokuwa mdogo sana sisi ndio tulisababisha kifo chake kwa maana bila sisi pengine angekuwepo duniani hadi leo alafu kwenye mkono wako umefanya nini ?



AKWELINA ?? Yule dada alipokuwa amevaa ngozi ya bandia yenye sura yako aliniambia anataka kunitoa kifaa kilichopo katika mkono wangu nilimuamini nikajua ni wewe nilipata maumivu makali sana sijui alinidanganya au ni kweli alinitoa kifaa japo sijui ni kifaa gani .



KAKINGA ?? Usijali binti yangu yote anajua mungu kama alitoa au hakutoa nina hasira sana moyoni mwangu kwa mateso na manyanyaso haya hivi hawajui kama Mimi niliwahi kuwa mwanajeshi ? nilifukuzwa kazi kutokana na hasira nilikuwa mkorofi sana, nilipoacha kazi ndio niliamua kufunga ndoa sitaki kuzungumza mengi lakini nahitaji nikupatie mazoezi makali ya kijeshi najua moyoni mwako unatamani kulipa kisasi hiyo ndio sababu inayonifanya nikufundishe mazoezi makali ili upate nguvu za kutosha na nakuahidi katika kisasi chako nitakuwa nawe hadi mwisho.



AKWELINA ?? Daah ahsante baba yangu nakupenda sana nawachukia watu hao wamepoteza maisha ya wazazi wangu ipo siku nitalipa kisasi kwa ajili ya wazazi wangu nisamehe baba sitokukosea tena nakuahidi .



Akwelina alifurahi akamsogelea baba yake mlezi ( Kakinga ) akalala katika miguu yake, Baada ya nusu saa akwelina alipitiwa na usingizi katika miguu ya baba yake mlezi, Kakinga alimbeba hadi chumbani akamlaza taratibu ili asistuke na kupoteza usingizi wake. Majira ya alfajiri muda ambao usingizi unakuwa mtamu zaidi Kakinga alimwamsha akwelina , akwelina aliamka kiunyonge alipofika nje alimkuta Kakinga ame….





Akwelina aliamka kiunyonge alipofika nje alimkuta Kakinga ameshika karatasi za aina mbili , Karatasi ya
 
SEHEMU YA 39 YA 50

kwanza ilikuwa inarangi nyeupe na nyingine ilikuwa inarangi nyeusi, Muonekano wa karatasi hizo zilimchanga akwelina kwa sababu hakutambua maana ya karatasi hizo.



“” Baba hizo karatasi zinaamana gani ? akwelina alimuuliza baba .



“” Vizuri sana binti yangu inaonesha wewe ni mchunguzi sana na kutokana na kuwa mchunguzi basi nakuahidi utafanikiwa sana katika maisha yako. Karatasi hizi ni mfano wa nafsi ya mwanadamu chochote tunachofanya sisi wanadamu kina faida na hasara ndani yake pia haya mazoezi ninayotaka kukufundisha usipokuwa makini nafsi yako itakuwa mbaya kama karatasi hii nyeusi lakini ukiwa makini nafsi yako itakuwa msaada mkubwa kwa watu wanaokuzunguka, Je upo tayari kuanza mazoezi haya ? Yalikuwa maneno ya Kakinga kwa akwelina.



Akwelina alifikiri sana maneno ya aliyoambiwa na baba yake mlezi .



“” Nipo tayari baba nakuahidi nitakuwa bora na makini katika mazoezi hayo ili niwe mwanadamu bora na mwenye nafsi nyeupe kama karatasi hiyo . Akwelina alimjibu baba akiwa anajiamini sana .



Baba ( Kakinga ) alifurahi sana. Mazoezi yalikuwa matamu katika majira hayo ya asubuhi kwa sababu yalikuwa mazoezi laini. Siku zilizofuata mazoezi yalianza kuwa magumu na yenye mateso ndani yake hali iliyosababisha akwelina aanze kuyachukia na kuyaogopa mazoezi hayo aliyokuwa anapewa na kakinga ( baba yake mlezi ) Furaha na shauku ilianza kutoweka ndani ya moyo wa akwelina kutokana na mateso aliyokuwa anayapata katika mazoezi. Baada ya mwaka mmoja kupita akwelina aliyazoea mazoezi ikapelekea akawa bingwa katika mapamba ilikuwa ngumu sana kwa kakinga kuamini uwezo aliyoupata binti yake kwa muda mfupi akasema:



KAKINGA ?? Hahaha binti yangu hakika wewe ni binti wa ajabu sana kwa uwezo ulionao kwa sasa sio rahisi kwa sababu kwa kawaida ili mwanafunzi afikie uwezo ulionao anatakiwa afanye mazoezi kwa miaka mitano ( 5 ) lakini wewe ndani ya mwaka mmoja umekuwa na uwezo mkubwa kiasi hicho duuh ajabu sana kwa uwezo wako kwa sasa inatakiwa wewe ndio unifundishe mimi sikuwezi katika mapambano hongera sana.



Kakinga aliingia ndani baada ya kuzungumza maneno hayo akamuacha akwelina katika mshangao mkali sana. Baada ya wiki moja kupita ndani ya kampuni Julius aliwatuma walinzi wakamlete Patrick , walinzi walimleta patrick mbele ya kiongozi wao ( julius ) Julius akamwambia patrick :-



JULIUS ?? Nakupa nafasi nyingine Patrick nenda kamtafute akwelina na uniletee hapa akiwa hai au amekufa nenda kaungane na mdogo wako Warda Chukua wanajeshi unaowataka kwa sababu usiporudi na akwelina hapa utanijua mimi ni nani pia mchukue huyo mke wa Kakinga ( Monna ) mtumie kama chambo ili kumpata Kakinga sawa?



PATRICK ?? Sawa kiongozi wangu ahsante kwa nafasi hii nakuahidi sitokuangusha tena.



JULIUS ?? Good unaweza kuondoka.



Patrick aliondoka hadi katika chumba chake akaoga alafu akachukua simu akampigia mdogo wake ( warda ), walizungumza kwa muda mrefu wakati huo akiwa anavaa nguo. Patrick alipomaliza kuvaa nguo zake aliondoka moja kwa moja hadi katika Chumba alichokuwepo monna akamchukua kama mzigo hali iliyompatia mashaka sana monna na kumfanya ajiulize maswali mengi bila kupata majibu, Patrick alimpeleka monna ndani ya Chumba chake walipofika alimwambia :-



PATRICK?? Kesho tunaenda mjini kumtafuta Kakinga lakini lengo sio mume wako tunamtaka akwelina na nawashangaa sana mnapoteza muda angalia leo hii wewe na mume wako mmetengana na kujenga chuki kubwa Baina yako na mume wako kwa sasa mume wako hana mapenzi na wewe kwa sababu ya mtoto ambaye sio wako duuh poleni sana lakini usijali Monna Mimi nakueleza ukweli toka moyoni sijui utaniamini au hautaniamini NAKUPENDA , Nakupenda monna amini hivyo na ndio maana nimekutoa leo ili tushirikiane kumtafuta mume wako tukimpata nitamuuliza kuhusu wewe alafu utaamini haya ninayokwambia kwa sasa Mimi ndio nakupenda lakini sio mume wako tena, Chaguo lipo kwako mwenyewe. Nenda kajiandae chakula kipo tayari na hiki ndio Chumba chako kuanzia leo .



Patrick alitumia maneno mazuri kumpoteza monna ili atimize lengo lake kwakua monna alikuwa ameshakata tamaa kuhusu Kakinga aliamini maneno ya Patrick. Siku ya pili asubuhi na mapema waliondoka hadi kwa warda walipofika Warda alitia mashaka uwepo wa monna pale lakini Patrick alimtuliza. Kwakua walifika majira ya mchana Patrick alimchukua monna wakaenda ziwani kupunga upepo ( kupumzika ) walipofika ziwani walitembea huku na huko kwakua jua kali lilikuwa kali ilibidi watafute sehemu yenye kimvuli kwa mbali waliona kibanda wakakisogelea walipofika karibu Patrick alimuona Kakinga alistuka sana akampigia simu warda baada ya muda mchache wanajeshi wengi walikizunguka kile kibanda wakati huo kakinga alikuwa hajui chochote.
 
SEHEMU YA 40 YA 50



Monna akamwita Kakinga , sauti ya monna ilimstua Kakinga kwakua alikuwa anaitambua, Kakinga alipogeuka alimuona monna akiwa na Patrick kakinga alipotaka kuingia ndani alipigwa sindano ya madawa. Sindano hiyo ilimvunja nguvu ( kupoteza nguvu ) kakinga akadondoka chini wale wanajeshi wakamchukua Kakinga wakamfunga kamba walipotaka kuondoka mbele yao walimuona akwelina …….



Walipotaka kuondoka mbele yao walimuona akwelina wanajeshi wote walinyanyua silaha zao juu wakajiandaa kumshambulia akwelina kabla ya kufyatua risasi Patrick aliwaziwia wanajeshi wake akasema kwa dharau :-



PATRICK ?? Hatuwezi kupoteza risasi zetu kwa binti kama huyu sisi ni wanaume mfungeni kamba na yeye kwa sababu lengo letu lilikuwa ni huyu binti .. Oooh hahaha akwelina ama kweli wewe ni mali ya pekee katika kampuni yetu yenye jina kama lako nikikuangalia nakosa jibu hivi Steven baba yako alifikiria nini kuweka ufunguo wenye thamani ndani ya mwili wako, Sijui alifikiria nini na ndio maana alikufa mapema alikuwa mjinga sana.



AKWELINA ?? Weee baba yangu hakuwa mjinga wewe chunga kauli yako hiyo ??



PATRICK ?? Mjinga tu sasa leo hii upo katika mikono yangu sasa ndio nini, alifanya ujinga pia alisahau kwamba siku zote mwanamke atabaki kuwa mwanamke tu, askari wangu fanyeni kazi yenu.



Maneno ya kejeli kutoka kwa patrick yaliutesa moyo wa akwelina mapigo ya moyo yalibadirika ghafla kutokana na hasira zilizomvamia akwelina, Wanajeshi ( askari ) walimfikia akwelina walipomgusa akwelina aliwashambulia kwa muda mfupi na hakuna aliyekuwa mzima, kitendo hicho kiliwastua wanajeshi wote hakuna aliamini kama akwelina anauwezo mkubwa kiasi kile , Wanajeshi walipoona wenzao wamepoteza maisha walishikwa na hasira wakatupa silaha chini wote wakamvamia akwelina, Kwa uwezo aliokuwa nao akwelina alitumia dakika kadhaa akawamaliza wote akabaki Patrick na monna wanatazamana, Patrick alikuwa anameza mate kwa hofu na woga.



Akwelina aliwasogelea Patrick pamoja na monna kabla hajawafikia alisikia sauti ya kike ikisema :-



“” Tulia hapo hapo binti kakinga kwa usalama wa baba yako piga magoti alafu weka mikono juu haraka “” Yalikuwa maneno ya warda .



Akwelina aligeuka akamuona msichana aliyetaka kumfanyia unyama mwaka mmoja uliopita ameweka kisu katika shingo la baba yake kipenzi na tegemeo la maisha yake, ilibidi akwelina afanye kama alivyoambiwa na warda Patrick alitumia nafasi hiyo hiyo akamfuata akwelina akamfunga kamba, Baada ya kumfunga kamba walimchukua akwelina pamoja na kakinga wakaondoka nao hadi ndani ya msitu mnene na wenye kutisha. Kakinga akiwa na akwelina walipata mateso makali sana kutoka kwa watu waliojifunika nyuso zao.



Ulipita mwezi mmoja , mwezi huo ulikuwa wenye mateso ndani yake kwa mateso waliyokuwa wanayapata Kakinga na akwelina walitamani kufa, Siku hiyo majira ya usiku monna alijitokeza mbele yao ?? Ilikuwa vigumu kwa kakinga kumuona monna mbele yake :-



“” Habari kakinga mume wangu kipenzi daah muda mrefu sijakuona mume wangu “” yalikuwa maneno ya monna.



“” Samahani dada baba yangu hana mke .Baba huyu mwanamke ni nani ?

Akwelina alimjibu monna na kumuuliza baba yake ( kakinga )



“” Akwelina binti yangu jaribu kuwa mtulivu huyo alikuwa mke wangu kipindi cha nyuma kabla hajaniacha pia unatakiwa umuheshimu sana kwa sababu yeye ndio aliyeokoa maisha yako kipindi ukiwa mdogo mama yako mzazi kabla hajapoteza maisha alimkabizi mtoto ambaye ndio wewe “” Kakinga alimjibu akwelina.



Majibu ya kakinga yalimshangaza sana akwelina na kutokuamini kama mwanamke aliyembele yake ndio aliyesaidia maisha yake, Kakinga akaendelea kusema :-



“” Jina lake anaitwa monna ni msichana aliyekupenda kipindi cha nyuma wakati huo alikuwa yupo tayari kupoteza maisha yake kwa ajili yako hakika alikuwa zaidi ya mama kwako na sio kwako pekee msichana huyo alikuwa ananipenda kuliko msichana yeyote hapa dunia lakini alichonifanyia siwezi kumsahau hadi siku nitayokufa Mimi.



Kakinga alimaliza kuzungumza maneno hayo, Monna akiwa analia sana. Monna alilia kwa muda mrefu mwisho akasema :-



MONNA ?? Akwelina mama yako mzazi bado yupo hai ni mzima wa afya japo yupo sehemu mbaya .



AKWELINA ?? Unasemaje ? ?? Mama yangu yupo wapi …..





AKWELINA ?? Unasemaje ? ?? Mama yangu yupo wapi ?



MONNA ?? Mama yako akwelina yupo usijali nitakuelekeza sehemu anapopatikana lakini muda hautoshi nimekuja hapa kuwasaidia mtoke sehemu hii kwa sababu kesho daktari bingwa anafika hapa Tanzania kutoka nje ya nchi. Najua kakinga unanichukia na huniamini tena kutokana na vitu nilivyokutendea. Mimi nakubali endelea kunichukia lakini tambua nakupenda sana na ndio maana nafanya yote haya mipango yao yote naifahamu sina mengi ya kuzungumza eneo hili.



Monna aliwafungua kamba haraka haraka kisha wakaondoka eneo hilo. Usiku ulizidi kukomaa monna na wenzake waliendelea kukimbia ndani ya msitu huo japo msitu huo ulikuwa unatisha mno, kakinga akiwa anakimbia alisimama ghafla. Kitendo hicho kiliwashangaza monna na akwelina ikabidi wasimame pia.



“” Kuna nini baba mbona umesimama ? akwelina alimuuliza baba .
 
SEHEMU YA 41 YA 50



“” Nimechoka kukimbia kila siku narudi eneo lile nahitaji kuanza kazi yangu kwa sasa sina hofu tena binti yangu umeshakuwa mkubwa ninaamini Unaweza kuishi maisha yeyote hata kama nikiwa nimekufa sasa Kwanini niendelee kukimbia hovyo hapana narudi kupambana nao wamenitesa sana washenzi hawa “”… Kakinga alimjibu akwelina akiwa na hasira zilizopiliza hadi kupelekea mwili wake kutetemeka.



Monna na akwelina walijaribu kumshawishi kakinga ili waendelee na safari lakini ilikuwa ngumu sana kakinga kukubali kuendelea na safari. Kakinga hakuzungumza tena aligeuka alipotoka akarudi kwa kukimbia kwa kasi sana, ilibidi akwelina na monna wamfuate nyuma. Walipokaribia eneo lile kakinga alisimama akasogea katika kichaka akatulia, akwelina alimsogelea kakinga akamwambia:-



AKWELINA ?? Kuna nini baba sijakuelewa kabisa japo umesema hauhitaji kuendelea kukimbia ?



MONNA ?? Jamani narudia tena muda hautoshi Patrick atafika hapa muda wowote na hatokuwa peke yake atakuja na askari wa kutosha na lengo lao wanataka kuupata ufunguo uliopo ndani ya mwili wa binti huyu akwelina mshauri baba yako kwa sababu wewe ndiyo anakusikia sana tuondoke jamani .



KAKINGA ?? Nisikilize monna kwanza tunashukuru kwa msaada wako lakini leo nahitaji kuonesha kitu kwa hawa wajinga najua lazima watakuja eneo hili lengo langu namtaka Patrick ili anipeleke huko katika kampuni yao leo.



MONNA ?? Njia hiyo hata mimi naifahamu nitawapeleka kakinga hebu jaribu kuelewa hapa sio sehemu salama na…



Kabla monna hajamaliza kuzungumza ulisikika mlio wa risasi , mlio huo uliwastua wote ghafla monna akadondoka chini, Kakinga na akwelina wakiwa katika mshangao mkali walizungukwa na askari wengi. Patrick akajitokeza akiwa na kisu hakuzungumza kitu alimfuata Monna wakati huo monna alikuwa chini akitokwa na damu nyingi akashika shingo lake akasema :-



PATRICK ?? Sikiliza wewe binti unatupatia ufunguo ulionao au nichukue maisha ya huyu mshenzi aliyetusaliti kweli unampenda sana mume wako huyu wa zamani , Binti unatupatia ufunguo au hutupatii zungumza haraka.



Patrick alipoona kimya kimezidi alipitisha kisu katika shingo la monna, monna alipiga kelele kali sana kelele zilizojaa simanzi , akwelina alimuonea huruma monna akasema ;-



AKWELINA?? Muache , Muache tafadhali nipo tayari kuwapa ufunguo alisaidia maisha yangu siwezi kukubali apoteze maisha kwa ajili ya ufunguo .



KAKINGA ?? Hapana akwelina hapana usikubali kutoa ufunguo .



PATRICK ?? Nilikueleza monna Kakinga hakupendi tena umeona , Sikia binti ufunguo upo wapi ?



AKWELINA ?? Upo ndani katika tako langu .



Patrick na wenzake walicheka sana walihisi akwelina anawatania..



“” Kweli siwatanii ufunguo upo ndani ya tako langu “”.. akwelina alimjibu Patrick .



Patrick alimsogelea akwelina akamvua suruali aliyokuwa ameivaa, Kakinga aligeuka pembeni hakuhitaji kuona mwili wa binti yake. Akwelina hakuleta kipingamizi chochote kwa sababu alihitaji kusaidia maisha ya monna, Patrick alifanikiwa kutoa ufunguo ndani ya tako la akw Chakwelina cha ajabu kilichotokea mbele ya macho ya Kakinga alimuona monna anasimama akiwa mzima, monna alimsogelea Akwelina akacheka sana :-

“” Pole sana binti yangu huruma yako imekuponza huu ulikuwa ni mtego pia nilihitaji kujua kitu kweli Kakinga hunipendi lakini ahsante tumefanikiwa kupata ufunguo huu.. Yalikuwa maneno ya monna .



Monna akiwa anajisifia na kuzungumza maneno ya dharau kwa akwelina, Monna alistuka amewekewa bastola kichwani alipogeuka alimuona Patrick akasema :-



“””” Hahahha hata wewe nilikutumia tu huna thamani tena mbele yangu unahitajika kufa monna …. Patrick alimwambia monna.



Wakati Patrick anazungumza na monna Kakinga ali……



____Leo imekuwa fupi kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu kesho tutakuwa pamoja mungu akipenda.







Wakati Patrick anazungumza na monna Kakinga alisimama kwa kasi sana akamvamia patrick kwakua patrick alikuwa hajajipanga ilikuwa rahisi kakinga kumshinda patrick. Wanajeshi waliokuja na patrick walipotaka kumsaidia kiongozi wao walimuona Patrick amenyanyua mikono juu akiwa amewekewa bastola kichwani kakinga akasema :-



KAKINGA ?? Wekeni silaha zenu chini haraka kabla sijafumua ubongo wa kiongozi wenu .



Wale wanajeshi walitaka kupinga kauli ya kakinga , Patrick akasema kwa nguvu akiwa anatetemeka mwili mzima kwa hofu ya kupoteza maisha yake :-



PATRICK ?? Weka silaha chini harakaaaaaa pumbafu ninyi ??



Wanajeshi wote waliweka silaha chini kakinga hakupoteza muda alimnyanganya ufunguo Patrick alafu akampatia akwelina kisha akasema:-



“”” Binti yangu ondoka haraka eneo hili kimbia nenda mbali, Usiwe na wasiwasi kuhusu maisha yangu hata kama nikipoteza maisha leo hii usijali nenda kasaidie dunia binti, Kuna watu wengi wanahitaji msaada kutoka kwako usipoteza muda nenda kawasaidie ??.



Maneno ya kakinga yalimtoa machozi akwelina aliondoka japo nafsi yake ilikuwa inatamani imsaidie kakinga ( baba yake mlezi ) akwelina aliondoka kwa kukimbia hali ya kuwa alikuwa na maumivu makali sana katika tako lake. Kakinga alizidi kumtazama akwelina anavyo ondoka mwanajeshi mmoja aliyekuwa nyuma ya kakinga alisimama kimya kimya akamnyanganya bastola kakinga, baada ya kumnyanganya bastola wanajeshi wote walisimama wakaanza kumpiga kakinga.
 
SEHEMU YA 42 YA 50.



Akwelina alizidi kukimbia ndani ya msitu huo wenye kutisha bila kutambua kama kakinga yupo kwenye matatizo, safari ya akwelina ndani ya Msitu huo ilikuwa ndefu sana hatimae akatoka nje ya msitu huo, Akwelina alianza kupata faraja baada ya kuona makazi ya watu ( miji ).Patrick na wenzake waliendelea kumpiga kakinga bila huruma, kipigo kilipozidi kakinga alipoteza fahamu wakamchukua kisha wakaondoka nae.



Yalipofika majira ya asubuhi akwelina alikuwa amelala ndani ya mtaro mkubwa ulikuwa unapitisha maji machafu katika mtaa aliokuwepo, Milio ya magari mbalimbali katika eneo lile ilimstua akwelina alisimama baada ya kuamka akatazama eneo hilo eneo hilo lilikuwa geni kwake ikabidi amulize mwanaume mmoja mpita njia akatajiwa jina la eneo hilo :-



“” Duuh sipajua hapa kaka yangu “” akwelina alimjibu yule mpita njia.



“” Wewe umetoka wapi “” mpita njia alimuuliza akwelina …



Akwelina alimjibu yule mpita njia sehemu anapoishi .



“” Pole sana dada huko unapotoka na hapa ni mbali sana unaweza kutumia masaa sita kufika eneo hilo kama ukipanda gari nauli ni shilingi elfu arobaini ( 40,000/= ) .”” yalikuwa maneno ya mpita njia akimueleza akwelina. Baada ya maelezo hayo mpita njia aliondoka akwelina alikaa chini kichwa kikamuuma sana kwa sababu alikuwa hana pesa yeyote na lile jeraha lilizidi kumtesa kwa kumpatia maumivu makali sana. Baada ya masaa matatu kakinga alirudisha fahamu akajikuta yupo kwenye gari ilionesha kuna sehemu anapelekwa ingawa alikuwa hajui wapi anapelekwa. Ilichukua muda mrefu kufika sehemu walipokuwa wanakwenda, Walipofika kakinga aliona neno kubwa limeandikwa AKWELINA ilimshangaza sana kuona jina la binti yake katika sehemu hiyo .



Hali ilizidi kuwa mbaya kwa akwelina kutokana na kutokwa na damu nyingi ghafla alishikwa na kizunguzungu akaondoka chini, watu walimpita kama hawamuoni japo eneo hilo watu walikuwa wengi wanaopita, akwelina alijaribu kujivuta kwa kutumia mikono yake lakini alishindwa akachukua ufunguo ambao alikuwa ameushika akauweka akaumeza bila maji kwa hofu ya kuupoteza. Katika watu waliokuwa wanapita Kijana mmoja mdogo alimuona binti anaomba msaada yule kijana alimwita kaka yake, Kaka alipofika alimbeba akwelina wakampandisha kwenye gari wakaondoka kuelekea hospital kwa sababu hali yake haikuwa nzuri.



Patrick na wenzake walipofika ndani ya kampuni walimfuata Julius wakamweleza yote yaliyowakuta Julius alichukia sana akachukua kipande cha chuma akamfuata kakinga akampiga nacho, Julius alitumia chuma hicho kama fimbo katika mwili wa kakinga. Kakinga alipasuka sehemu mbalimbali katika mwili wake damu zilimtoka kama maji, Julius hakuridhika akachukua kisu kilichokuwa katika kiuno cha Patrick akamfuata kakinga akasema:



“””Leo ndio mwisho wako umenisumbua kijana wewe “”



Julius alishika kisu vizuri alipotaka kumchoma kakinga , Monna alijitokeza mbele ya kakinga kile kisu kika…….





Kile kisu kikamchoma monna katika kiganja cha mkono kwa kasi ya kisu kile kilitoboa kiganja cha monna na kumuachia maumivu makali yalimfanya monna apige kelele kali:



“” Wewe msichana umetumwa au ndio mapenzi ya kweli , unabahati sana kisu hiki kuchoma katika kiganja cha mkono wako laiti kama kingefika katika tumbo lako hakika usingepona leo mpumbafu kabisa, Patrick mtoe mbele yangu huyu mwanamke mjinga anapiga fujo , Kakinga leo umepona kesho hautapona ninyi wawili peleka chumba cha giza hii takataka..””



Yalikuwa maneno ya Julius baada ya kumchoma kisu Monna. Patrick alimchukua Monna kisha akaondoka nae kama alivyoambiwa na Julius , Wanajeshi wawili walimpeleka kakinga ndani ya chumba cha giza walipofika ndani ya chumba hicho walimfungua pingu alafu wakaondoka. Baada ya masaa kadhaa kupita akwelina aliamka toka katika usingizi mzito baada ya kufumbua macho yake alimuona kijana mmoja mzuri akimtazama akwelina alizidi kuzungusha macho huku na huko akagundua yupo hospital.



“”” Nesiiii tafadhali njoo Mgonjwa wangu kafumbua macho “”” Yule kijana alimwita nesi .



Nesi alikuja akamfanyia vipimo akwelina alipogundua hali yake ipo vizuri alichukua karatasi nyeupe akaandika kisha akampatia yule kijana akasemwambia :-



NESI ?? Hakikisha unanunua dawa hizo zilizoandikwa hapo.



Yule nesi alimgeukia akwelina akaendelea kusema :-



NESI ?? Pole sana binti kwa sasa upo sawa hali yako sio mbaya hakikisha unasafisha donda lako ili liwahi kupona pole sana mungu atakusaidia utapona .



Akwelina alimshukuru sana yule kijana kwa msaada aliompatia, yule kijana alimpatia nguo Mpya akwelina kwakua hali haikuwa mbaya sana kwake alisimama akaenda chooni akabadirisha nguo kwa sababu nguo zake zilikuwa chafu sana, alipotoka chooni akwelina alisimama mbele ya yule kijana akasema :



AKWELINA __ ahsante sana kaka kwa msaada wako naomba nirudi nyumbani kwa sababu ninamengi ya kufanya japo naishi mbali eneo hili .



KIJANA__ Pole sana dada yangu naomba chukua business card yangu hii kama hautajali ukifika unapokwenda utanitafuta siku moja tunaweza kuonana yamungu mengi pia chukua pesa hizi zinaweza kukusaidia huko uendapo usizikatae pesa hizi nimependa kukupa toa wasiwasi dada yangu pia subiri nikuletee dawa zako sawa.
 
SEHEMU YA 43 YA 50.



Pesa zilikuwa nyingi sana akwelina alizipokea zile pesa akiwa haamini kama angeweza kupata pesa kama zile , akwelina alimshukuru sana mungu akachukua zile pesa. Yule kijana hakuchelewa alirudi haraka akampatia dawa, Akwelina alimshukuru sana yule kijana akaondoka hadi stenti ya magari akapanda gari ili arudi nyumbani, akiwa ndani ya gari akwelina alikuwa na mawazo sana hadi machozi yalimtoka kwa uchungu na hasira alizokuwa nazo, Gari hilo lilichukua muda mrefu kufika jijini alipokuwa anaishi akwelina, Kwa bahati nzuri walifika salama njia ilikuwa moja kwa akwelina alienda nyumbani kwao. Mazingira ya nyumbani kwao yalikuwa machafu kutokana na kutokuwepo kwao kwa muda mrefu.



Akwelina aliweka mazingira sawa kisha akaingia ndani. Yalipofika majira ya usiku akwelina alitoka nje akiwa na mawazo sana, akwelina akiwa ndani ya timbwi hilo la mawazo alistuka kumuona kakinga mbele yake ilibidi asimame kwa furaha alimkumbatia lakini cha ajabu alikumbatia hewa, Akwelina alicheka sana peke yake kama kichaa akajipiga makofi kichwani kwake ili kuondoa mawazo. Majira ya asubuhi yalipofika akwelina aliingia ndani akavaa nguo zake za mazoezi akaanza kupiga mazoezi japo kidonda chake kilikuwa bado kibichi , Siku hadi siku akwelina aliendelea kufanya mazoezi kwa bidii. Akwelina alifanya mazoezi kwa miezi mitatu bila kupumzika usiku na mchana , Mazoezi hayo yaliujenga mwili wa akwelina na kuupatia nguvu za kutosha. Siku moja majira ya jioni akwelina alikuwa barabarani akifanya mazoezi ya kukimbia kwa mbali alimuona msichana anakuja mbele yake nae akiwa anakimbia kwa muonekano alikuwa anafanya mazoezi , alipomkaribia aligundua yule msichana ni warda Akwelina ali.





Akwelina alihamia upande wa pili wa barabara Warda akiwa hajui chochote alizidi kumsogelea akwelina alipofika karibu zaidi akwelina alimshika mkono, Warda alishangaa sana akautazama mkono uliomshika , Mkono huo ulizidi kumshangaza warda kwa sababu ulikuwa unatetemeka mno, warda alipoitazama sura ya aliyemshika hakuamini kama ni akwelina. Kutokana na hasira alizokuwa nazo akwelina alimpiga sana warda, kipigo hicho kilimfanya warda apoteza fahamu akwelina akambeba warda kisha akaondoka nae na kuwaacha wapita njia midomo wazi.



Baada ya masaa manne kupita warda alirudisha fahamu akajikuta yupo kwenye kiti amefungwa kamba sehemu aliyokuwepo kulikuwa na giza nene lenye kutisha , warda alianza kutetemeka mapigo ya moyo wake yalizidi kwenda mbio.. Ghaflaaaa akatokea akwelina mbele yake akiwa ameshika nyundo warda alipiga kelele Akwelina akasema:-



“” Shiiiiiiiiiiiiii ‘ kimya hakuna atayeweza kukusaidia eneo hili hata upige kelele kiasi gani. Bado Sijasahau unyama wako siku ile kama ungefanikiwa leo hii nisingekuwa akwelina huyu wa sasa hivi, Kwanza ungeniathiri kisaikologia, Pili nisingekuwa bikra tena sasa leo nalipa unyama wote ulionitendea Mimi na baba yangu kipenzi “””



Maneno ya akwelina yalizidi kumzidishia wasiwasi warda, akwelina alisimama akaanza kumzunguka warda akiwa na nyundo mkononi akwelina alitumia nyundo hiyo kama fimbo katika mwili wa warda, Warda alipata maumivu makali sana baadhi ya viungo vya Warda viliteguka na kuvunjika kutokana na hasira alizokuwa nazo akwelina hakuchagua sehemu ya kupiga na hakuwa na huruma tena.



“”” Usiniue akwelina nisamehe nipo tayari kukupeleka sehemu ambayo baba yako yupo aaaaah … Ooooh mama nakufa mimi leo oooh mungu nisaidie nakufa mimi nisamehe akwelina mama nisamehe ????



Yalikuwa maneno ya warda akilalamika kutokana na kipigo alichokuwa anakipata. Pamoja na kulalamika kiasi hicho bado haikusaidia kitu akwelina aliendelea kushusha kipigo bila huruma :-



“”” Nisamehe binti yangu sina kosa mimi yote amesababisha kaka yangu patrick alimchukua mtoto wangu akiwa bado mdogo sana mtoto niliyempata katika ndoa yangu Mimi na kakinga baba yako japokuwa kakinga hadi sasa anatambua siku ile hospital wakati wewe ulipokuwa mdogo nilitoa mimba sio kweli sikutoa mimba mdogo wako yupo akwelina “”



Baada ya maneno hayo akwelina aliacha kumpiga warda akamuuliza :-



AKWELINA __ Unasema mdogo wangu mtoto wa baba yangu ! nieleze yupo wapi muda huu na ukinidanganya hutoki salama leo.



Hapana siwezi kukudanganya akwelina nakumbuka miaka mingi imepita nilipewa kazi na kaka yangu ambaye ndio huyo patrick , Tulitengeneza ajali na tukafanikiwa lakini ndani ya kazi hiyo nilimpenda baba yako ( kakinga ) nilitokea kumpenda sana nikaamua kufunga nae ndoa, nilipofunga ndoa nae Patrick pamoja na Julius walichukia sana wakaniambia nivunje ndoa yangu kipindi hicho tayari nilikuwa mjamzito nilipinga walichotaka , wakaniambia nimdanganye kakinga kwamba ujauzito wake nimeutoa. Kwa bahati nzuri nikasikia kakinga ametoroka kipindi hicho wewe ulikuwa mdogo sana, nilitunza mimba ile hadi nilipojifungua mtoto wa kiume walimchukua Mtoto wangu siku hiyo hiyo daah ?? inaniuma sana baada ya kumchukua waliniambia siku nikikupeleka wewe ndio watanipatia Mtoto wangu na siku ile nilipovaa ngozi ya bandia nilifanya vile ili nikupate lengo nikupeleke ili nikamchukue Mtoto wangu ningefanyaje Mimi akwelin ? Ukweli sikupenda kukufanyia unyama wote huo lakini Mimi ni mzazi nilihitaji kumsaidia mtoto wangu lakini hadi leo siitambui sura ya mtoto wangu ??
 
SEHEMU YA 44 YA 50.



Warda alimaliza kumsimulia akwelina maisha yake kwa ufupi akiwa analia sana, Japokuwa akwelina alikuwa na hasira lakini alishikwa na hudhuni mno, roho ya huruma ilichukua nafasi yake ndani ya moyo wa akwelina akadondosha ile nyundo chini akalia kwa uchungu ghafla akaacha kulia akasimama akamfuta warda akamwambia :-



AKWELINA __ Nipeleke sehemu baba yangu yupo nahitaji kumsaidia kakinga baba yangu kipenzi ..



Akwelina akamfungua kamba warda akampeleka katika kitanda kwakua warda alikuwa ameumia sana akwelina alimpatia huduma ya kwanza Warda akamshukuru akwelina kwa kumsamehe. Usiku huo huo akwelina alienda duka la madawa ( pharmacy ) akanunua dawa nyingi kisha akamuuliza mtoa huduma :-



AKWELINA __ Samahani dada leo imepita miezi kadhaa niliwahi kumeza ufunguo kwa bahati mbaya na kila nikienda chooni kwenye kinyesi siiuoni tatizo ni nini au daah hata sielewi ?



MTOA HUDUMA __ Ni kweli inawezekana kutokana na mmeng’enyo wa chakula lakini usijali nitakupatia dawa itayolainisha kinyesi tumboni kwako nahisi ufunguo huo unaweza ukatoka.



Akwelina alinunua dawa hiyo, alipofika nyumbani alitumia dawa aliyopewa baada ya dakika tatu tumbo lilianza kuuma akaenda chooni na wavu wake ambao alikuwa anautumia kila siku . Siku hiyo aliharisha sana kwa bahati nzuri akauona ufunguo ule alifurahi mno.



Yalipofika majira ya asubuhi na mapema ndani ya kampuni kakinga alikuwa bado yupo katika mateso makali sana , siku hiyo Julius aliingia katika chumba alipokuwepo kakinga akiwa na kijana mwenye miaka kumi na tano, Yule kijana alipomuona kakinga ametapakaa damu mwili mzima na akiwa amefungwa kamba alimuuliza Julius :-



“”” Huyo ni nani ambaye ametapaa damu mwilini mwake ?



JULIUS ___ Huyo ni baba yako mzazi





JULIUS ___ Huyo ni baba yako mzazi ..



Julius alitambua kijana bado hajamuelewa akaendelea kusema :-



JULIUS ___Natambua hujanielewa #BILALI huyo unaemuona mbele yako ni baba yako mzazi, Kwanini nasema ni baba yako ? Kwa sababu mama yako asingeweza kukuzaa wewe bila kubakwa na baba yako ambaye ndio huyo hapo .



BILALI ___ Mimi nimepatikana kwa kubakwa!! ?? hapana sio kweli alafu kwanini miaka yote nipo eneo hili na siku zote nambua wewe ndio baba yangu inakuaje leo unaniambia mambo kama haya ?



JULIUS ___ Upo sahihi bilali niliamua kukuchukua wewe kutokana na hali ya mama yako , Mama yako alikuwa anamaisha magumu sana lakini baba yako huyo hakuwa na huruma alimbaka na kumpatia ujauzito alafu akamkimbia , Mama yako aliishi kwa tabu sana hadi alipojifungua katika hospital ambapo nilikuwa nafanya kazi miaka ya nyuma.



BILALI ___ Mama yangu yupo wapi ?



JULIUS___ Mama yako alifariki siku ambayo anakuzaa wewe ( kujifungua ) kwakua Mimi ndio nilimsaidia kujifungua niliumia sana nikaamua kukuchukua wewe ili nikutunze na niliweka ahadi kwamba nitamtafuta huyo mshenzi alimsababishia kifo mama yako kwa bahati nzuri mama yako alinisimulia na picha ya huyu mjinga alinipatia, Nilimtafuta na nikampata leo hii yupo mbele yako utajua wewe utamfanyaje kwa ajili ya kifo cha mama yako …



Bilali alihisi kizunguzungu kwa kusikia maisha ya mama yake kabla hajapoteza maisha kama Julius alivyomueleza, Alishikwa na hasira mno bilali akamsogelea kakinga , Akautazama mwili wa kakinga akaona vidonda vipo vingi sehemu kubwa ya mwili wa kakinga , Bilali alisimama akatazama huku na kule akaona kipande cha chuma ambacho kipo ndani ya chumba hicho kwa ajili ya kumpatia adhabu kakinga, Bilali aliokota kile kipande cha chuma akarudi akachukua kile chuma akachoma katika kidonda kikubwa katika mwili wa kakinga. Kakinga alilia sana na kupiga kelele zenye maumivu makali ndani yake , Bilali hakuridhika akatupa chuma akatumia mikono yake kuendelea kufinya vidonda vya kakinga bila huruma kwakua vidonda vilikuwa vibichi maumivu yalikuwa makali sana ????????

__ “”” Kufa mshenzi wewe umembaka mama yangu na kumsababishia kifo sikuachi salama kufa kufa kufaaaaaaaaaa “””

Bilali alisema maneno hayo kwa hasira akiendelea kufinya ( kubinya ) vidonda vya kakinga, Bilali bado hakuridhika alisimama akamfuata Julius akachomoa bastola iliyokuwa kiunoni akahitaji kumpiga risasi kakinga Julius akamziwia kisha akamwambia :-



JULIUS __Tulia kijana wangu mtu kama huyu unatakiwa umpige risasi mbele ya macho ya watu ili kila mwenye tabia kama yake ajifunze kupitia yeye.



Julius alimchukua bilali akaondoka nae, Kakinga akiwa bado anamaumivu alisema moyoni kwake akiwa analia :-

“”” Ewe mungu nimekukosea nini Mimi ni bora unichukue kuliko mateso ninayopata ????.



Baada ya mwezi mmoja kupita warda alipata nafuu viungo vilivyovunjika vilirudi katika hali yake kama mwanzo. Siku hiyo akwelina hakuwepo nyumbani alikuwa ameenda mbali na nyumbani kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kutuliza akili, Akwelina alitumia muda mrefu sana katika mazoezi hayo jioni ilipofika akwelina alirudi nyumbani alipoingia ndani cha ajabu hakumuona warda, akwelina alimtafuta warda sehemu zote lakini hakumuona, Wakati huo warda alikuwa njiani anarudi nyumbani kwake japo hali yake haikuwa nzuri lakini alijitahidi kutembea hivyo hivyo ilimchukua muda mrefu sana kufika nyumbani kwake. Alipofika nyumbani alichukua silaha pamoja na vitu vyenye thamani kwake kisha akaondoka ili kurudi kwa akwelina. Usiku ulipotanda akwelina alikuwa yupo nje akiwa na mawazo sana ghafla
 
SEHEMU YA 45 YA 50.

akamuona warda akiwa na begi kubwa akwelina alifurahi kwa sababu alitambua bila warda hawezi kutambua sehemu Kakinga alipopelekwa, Akwelina alimsaidia warda wakaingia ndani .



Siku ya pili majira ya asubuhi wanajeshi walimchukua kakinga wakamfunga katikati ya uwanja mkubwa ndani ya kampuni hiyo , wakamchapa fimbo nyingi mbele ya watu wote wanaoishi ndani ya kampuni hiyo baada ya kumchapa sana alikuja Julius akiwa na bilali walipofika Julius alisimama akachukua kipaza sauti akasema :-



JULIUS ___ Leo ni siku muhimu sana kijana mnaemuona hapo alifanya unyama kwa msichana mmoja na kusababisha kifo chake na huyu ndio mtoto wa msichana huyo ambaye ni marehemu, Leo kijana huyu anataka kulipa kisasi BILALI kijana wangu muda ndio huu unesha upendo kwa mama yako hata huko alipo afurahi.



BILALI alichukua panga akamfuata kakinga alipo akaweka panga katika shingo la kakinga, Kakinga alifumba macho akiwa anatabasamu :-

“” Ahsante mungu kwa kusikia kilio changu “”” yalikuwa maneno ya kakinga. Bilali alinyanyua panga juu kisha aka….





Bilali alinyanyua panga juu kisha akashindwa kushusha panga lile katika shingo la kakinga baada ya kumuona Kakinga anatokwa na machozi, Julius alishindwa kumuelewa bilali kwa kumuona anashindwa kukata kichwa cha Kakinga :-



“” Maliza kazi bilali unafikiri nini “”



Julius alizidi kumpatia ujasili bilali lakini pamoja na Julius kumlazimisha bado nafsi ya bilali iligoma kukata kichwa cha Kakinga ilimchukua muda mrefu sana kufanya maamuzi ghafla alikaza mikono yake akashusha panga kwa kutumia nguvu nyingi watu wengi waliokuwa eneo hilo walifumba macho kwa muda walitambua bilali amekata kichwa cha kakinga, Julius alifurahi mno Julius alicheka zaidi kwa furaha cha ajabu alimuona bilali anamshika mkono kakinga akasimama nae kakinga akiwa hai bilali akamsogelea Julius akiwa amemshika mkono Kakinga alipofika karibu yake akamwambia :-



BILALI ?? Huyu ndiye baba yangu haijalishi nimepatikana kwa njia gani lakini bado atabaki kuwa baba yangu , Mama yangu hayupo duniani nikimpoteza na baba nitakosa furaha ya milele nimeamua kumsamehe baba yangu kwa sababu katika upatikanaji wangu alipanga mungu baba yangu hanakosa katika hilo .



JULIUS ?? Mtoto mjinga sana wewe pumbafu sikutegemea kama utakuwa mjinga kiasi hiki .



KAKINGA ?? Jina lako unaitwa bilali ? Sikia kijana Mimi sina mtoto japo nina mtoto wa kumlea maisha yangu yote sikubahatika kupata Mtoto huyu Julius anakudanganya muulize baba na mama yako wapo wapi lakini sio mimi, Sikutaka kukuambia haya yote kwa sababu nilikuwa nahitaji kufa kwakua umeshindwa kuniua ndio maana nakueleza haya Mimi sio baba yako.



JULIUS ?? Baba mjinga kama mtoto wake bilali ni mtoto wako aliyemzaa warda. Warda alikudanganya kwamba mimba waliitoa lakini sio kweli warda alijifungua mtoto nikamchukua na nilimpatia adhabu kwamba ili nimpatie Mtoto wake lazima aniletee akwelina mbele yangu na una bahati sana nilitaka damu yako leo ichukue maisha yako.



Julius alijisahau akaendelea kutoa siri mbele ya bilali kutokana na hasira alizokuwa nazo baada ya Bilali kushindwa kumkata kichwa Kakinga. Bilali hakuamini kama alikuwa anadanganywa bilali alichukia sana akamuuliza Julius akiwa jaziba:



BILALI ?? Bado sijaamini kama ulikuwa unanidanganya kwanini umenifanyia hivi kwaniniiiii !!!??



JULIUS ?? Weee tuliza kichwa chako hicho unamkaripia nani hapa ? mwenye umri kama wako pumbafu , sikia wewe bilali nilitaka leo umalize maisha ya baba yako ili nitimize malengo yangu ya kukulea ni kweli mama yako yupo hai pia kakinga hakumbaka mama yako. Umetambua ukweli utanifanya nini sasa ??



Mwili wa bilali ulisisimka kwa hasira hali iliyomfanya bilali amvamie Julius na kumshushia kipigo , Julius alipoona anapigwa na jabar alimwita mwanajeshi wake mkuu kwa sauti ya juu “”””” MTAWALAAAAAA “”” sauti hiyo ilimfikia mtawala alipokuwepo na kumfanya afike eneo husika haraka sana, Mtawala alipofika alimshika mguu bilali akamtupa mbali, bilali alipogeuka kumtazama aliyemtupa Alimuona mwanajeshi mmoja mwenye mwili mkubwa mno , Bilali alisimama japo alikuwa mdogo lakini alikuwa anajiamini na jasili sana, bilali alikimbia kwa kasi akamvamia mtawala bado haikusaidia kitu kutokana na nguvu alizokuwa nazo mtawala. Bilali alipigwa sana, mtawala alishika shingo la bilali alipotaka kumnyonga kakinga alisimama akampiga mtawala ngumi moja ambayo iliwashangaza macho ya watu , Mtawala alishuka chini na kupoteza maisha papo hapo. Julius hakuamini kama kakinga anauwezo mkubwa kama ule wanajeshi walipoona balaa hilo walimpiga kakinga sindano ya sumu akadondoka chini akapoteza fahamu wakamchukua kakinga pamoja na bilali wakawapeleka katika chumba cha giza .



Usiku wa siku hiyo akwelina na warda waliendelea kufanya mazoezi kwa bidii , baada ya kufanya mazoezi walisafisha miili yao wakatulia warda akamwambia akwelina
 
Back
Top Bottom