Simulizi: Asante kwa Kunifuta Machozi (Hisia Zangu)

Simulizi: Asante kwa Kunifuta Machozi (Hisia Zangu)

Abdallahking

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2018
Posts
3,985
Reaction score
10,840
JOSEPH SHALUWA = ASANTE KWA KUNIFUTA MACHOZI (HISIA ZANGU).jpg

Simulizi: ASANTE KWA KUNIFUTA MACHOZI (HISIA ZANGU)
Mwandishi: JOSEPH SHALUWA
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES


*****

SEHEMU YA 1 KATI YA 50

Edo wewe! Acha utani wako bwana... unajua kitakachotokea. Utaniudhi sasa...” akasema Lilian kwa sauti ambayo haikueleweka ilikuwa ya ukali au kudeka.

...Sikujua mwisho wangu ungekuwa hivi

EDO aligeuka tena. Kwa mara ya tatu anafanya hivyo wakati akielekea bafuni. Safari hii alimwangalia Lilian kwa macho yaliyojaa ubembe wa huba.

Alihisi moyo wake ukienda mbio kama saa mbovu!

Lilian alikuwa mbichi kabisa. Mwanamke mrembo kuliko neno lenyewe. Kwa namna Lilian alivyokuwa akimwangalia Edo aliyekuwa akisitasita kuingia bafuni, alionekana dhahiri hakuwa na mpango wa kubadili maamuzi yake.

Moyoni alionekana wazi kusimamia alichopanga. Hakuwa tayari kuyumbishwa! Kweli alimpenda sana Edo, lakini isingekuwa rahisi kwake, kutokana na upendo huo avunje agano lake.

Hapo Edo naye alikuwa na mawazo yake, alijaribu kufikiria ni kwa namna gani angemlaghai Lilian akubali kubadili maamuzi yake.

Kwa hakika ilikuwa kazi ngumu. Kazi ngumu kwelikweli. Pengine ingekuwa rahisi zaidi tairi la gari kupita juu ya mguu wa binadamu bila kuuvunja kuliko jambo lililokuwa mbele yao kufanyika.

Msimamo thabiti!

Lilian alikuwa amekaa kitandani, amevaa gauni zuri, refu la rangi ya buluu ya kung'aa. Tangu ameingia katika chumba cha hoteli hiyo na Edo, saa mbili zilizopita, hakuonekana kuwa na wazo la kutoa nguo zake.

Ni kama alipanga kulala nazo. Ahadi ya wawili hawa ni kutokukutana kimwili hadi watakapofunga pingu za maisha. Ni msimamo ambao Lilian alijiwekea siku zote.

Si kwamba walikutana siku hiyo... la hasha! Hawa ni wapenzi wa siku nyingi; uhusiano wao sasa umefikisha miaka mitatu. Kwa muda wote huo, hakuna siku waliyowahi kukutana kwenye uwanja wa huba.

Lilian pamoja na kuwa na umri wa miaka 22, bado alikuwa hajawahi kumjua mwanaume. Bado alikuwa amefungwa kwenye makaratasi. Kichwani mwake alisema: "Mtu pekee ambaye anapaswa kuchukua zawadi hii ni mume wangu pekee. Siwezi kumwamini Edo, hata kama nampenda.

"Edo atakula vinono vyangu ikiwa atatimiza ahadi yetu ya ndoa. Najua tunasoma, acha tutengeneze maisha yetu kwanza, baada ya hapo atanifaidi tu. Mimi ni wake tu."

Au ataniacha? Lilian akawaza tena.

"Mwenzetu vipi? Mbona umeganda hapo mlangoni?" Lilian akamwuliza Edo ambaye bado hakuwa na dalili za kutaka kuingia bafuni.

"Naingia mama, kwani kuna ubaya gani mtu kumwangalia mpenzi wake?" akajibu Edo.

"Hakuna ubaya kwa kweli, si vibaya mtu kumwangalia mpenzi wake. Nakubaliana na wewe lakini muda baby. Bado hatujala mpaka sasa hivi."

"Najua...njoo basi tuoge wote ili tuokoe muda."

"Edo wewe! Acha utani wako bwana...unajua kitakachotokea. Utaniudhi sasa..." akasema Lilian kwa sauti ambayo haikueleweka ilikuwa ya ukali au kudeka.

Haraka Edo akashika kitasa cha mlango wa bafuni. Akakinyonga kwa nguvu, kisha akasukuma mlango. Akaingia. Muda mfupi baadaye kilichosikika ndani ya bafu lile ilikuwa ni maji yakitiririka kutoka kwenye bomba la mvua.

Bado Edo alikuwa anapanga mashambuzi.

***

Edward Mhagama au Edo kama alivyojulikana na wengi alikuwa kijana mtanashati hasa. Hakuwa mtu wa wasichana sana. Mpaka anamaliza kidato cha nne alikuwa hajawahi kukutana na msichana yeyote kimapenzi.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 2 KATI YA 50

Alipoingia kidato cha tano, Shule ya Sekondari Lutengano, Tukuyu, Mbeya ndipo alipoanza utundu. Alijikuta akikutana kimapenzi na wasichana tofauti tofauti kwa muda mfupi.

Alipoanza tu kujua mapenzi, akajikuta amechanganyikiwa ghafla. Akiwa anamaliza kidato cha sita, alijishangaa amebadilika ghafla.

Hakutaka tena kuendelea na tabia yake ile ya kupenda wanawake. Kwa bahati nzuri, alipata alama nzuri na hivyo ikawa rahisi kwake kupata nafasi ya kuendelea na masomo ya chuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) sehemu ya Mlimani.

Hapo ndipo alipokutana na Lilian, yeye akiwa mwaka wa mwisho wa masomo, wakati Lilian akiingia mwaka wa kwanza. Alipata shida sana kufanikiwa kumnasa Lilian kwenye himaya yake.

Lilian hakuwa mtu wa wanaume kabisa. Hakujua chochote kuhusu mapenzi. Bahati nzuri kwa Edo ni kwamba alikuwa mcheza mpira wa kikapu mzuri sana, mchezo ambao Lilian alipenda kuungalia.

Hapo ndipo mwanzo wa uhusiano ulivyokuwa lakini sharti lilikuwa moja tu. Wasingekutana faragha mpaka watakapoingia kwenye ndoa.

Lilikuwa sharti gumu sana kwa Edo, lakini aliamua kulipokea kwa sababu alimpenda sana Lilian na ndani ya moyo wake alikuwa na uhakika kuwa hakutaka kuwa naye kwa ajili ya kujifurahisha tu bali kuingia kwenye ndoa.

Pazia la uhusiano wao likafunguka.

***

Mlango ulifunguka. Edo akatoka bafuni akiwa bado ana maji mwilini mwake. Hakuwa na nguo yoyote zaidi ya taulo kiunoni. Akatembea taratibu hadi ilipokuwa kabati ya kujipambia.

Ilikuwa siku ngumu sana kwao, ni siku ambayo walikubaliana kulala pamoja kwa vile tu, siku inayofuata, Edo alikuwa na safari ya kwenda Malaysia kwa ajili ya masomo. Wazazi wake waliamua kumpeleka nchini humo kutafuta Shahada ya Uzamili.

Hiyo ilimaanisha kuwa, Lilian angebaki pekee nchini kwa muda wote huo wa masomo. Mipango ilikuwa mizuri, Edo asingerejea nchini mpaka atakapomaliza masomo yake, maana wazazi wake walikuwa wameshamtafutia kazi ya muda kwa kipindi chote atakachokuwa likizo na siku za mapumziko.

Ratiba yake ilikuwa imebana kabisa. Walikuwa pamoja kwa ajili ya kuagana. Ahadi ikiendelea kutunziana heshima kwa kipindi chote hicho. Ndivyo makubaliano yao yalivyokuwa.

Edo hakujali, kama vile hapakuwa na mtu. Alijitoa taulo na kuanza kujikausha maji mwilini. Baada ya hapo akachukua manukato ya ngozi, akajipulizia mwili, kisha akatoa nguo na kuvaa.

Lilian alifumba macho. Aliona haya kumwangalia Edo. Alijua wazi kama angeendelea kumwangalia ni jambo gani lingejitokeza. Hilo alilijua kwa hakika kabisa.

Edo alitumia dakika mbili tu kujikamilisha. Akamfuata Lilian na kumshika mikono...

"Wewe, yaani umefumba macho kweli?" akauliza.

"Ndiyo!"

"Kwa nini?"

"Wewe hujui? Sitaki matatizo bwana."

"Nenda basi na wewe ukaoge."

"Nitafanya hivyo kwa sharti moja tu."

"Sharti gani?"

"Kama utaondoka na kwenda mgahawani, uniache mimi nioge peke yangu na nijiandae kabisa, nikiwa tayari nakufuata."

Edo akatulia kwa muda, akamwangalia Lilian kwa macho yaliyokuwa yanafikisha ujumbe fulani, kisha akamjibu: "Sawa."

Hakusubiri zaidi, alisimama na kuufuata mlango kisha akafungua na kuubamiza kwa nguvu. Ni kama alikuwa amechukia. Lilian hakujali. Akasimama na kwenda kuufunga ule mlango kwa...
 
SEHEMU YA 3 KATI YA 50

ufunguo kisha akarudi ndani.

Akavua nguo na kuchukua taulo kisha akaelekea bafuni. Alioga kwa uhuru sana. Alipomaliza kila kitu, alitoka na kumfuata mpenzi wake mgahawani.

"Umeniagizia chakula?" Lilian akamwuliza.

"Sasa nitajuaje unapenda chakula gani?"

Jibu lile lilionyesha chuki dhahiri iliyokuwa moyoni mwa Edo. Lilian akatulia kwa muda. Akanyoosha mikono yake na kuivuta ya Edo.

"Niangalie machoni," Lilian akamwambia Edo.

Edo akafanya hivyo.

"Nakupenda sana na ninajua malengo yetu yalivyo. Amini usiamini, kama utalazimisha unachotaka kitokee, nakuhakikishia tutauvunja uhusiano wetu wenyewe."

"Kwa nini unasema?"

"Umevumilia kwa miaka mingapi mpenzi wangu? Si mitano? Eeeeh? Kuna tatizo gani kusubiri kwa hiyo miaka miwili tu iliyobaki? Kuna haraka gani?

"Hivi utaniamini vipi mimi kuwa sitakuwa na mwanaume mwingine? Sikia dear, mimi sijawahi kukutana na mwanaume yoyote tangu kuzaliwa kwangu. Hii ni zawadi yako mpenzi.

"Ona...ukiniacha na hii hali itakuwa ni usalama na ulinzi wa kweli kwako. Siwezi kumpa mtu. Nitakupa wewe tu muda ukifika. Maana yake ni kwamba, ikiwa leo utanitoa usichana wangu, ukiondoka kesho, hata kama nikikutana na mwanaume mwingine huwezi kujua mpenzi.

"Nipe uhuru, niamini. Mbona mimi nakuamini mpenzi? Au huwa unafanya na wengine? Ni heshima kunioa nikiwa msichana kamili. Mpenzi wangu, acha papara!" alisema Lilian kwa sauti lakini kwa harakaharaka.

"Nimekuelewa mpenzi."

"Kweli?"

"Ndiyo."

"Umeagiza nini?"

"Nafurahi kula ugali na makange."

"Makange ya nini?"

"Unapenda nini?"

"Wewe umeagiza ya nini?"

"Samaki, sato."

"Uko sahihi kabisa mpenzi."

Mazungumzo yao yakabadilika, sasa ikawa ni kuhusu maisha yao yajayo na namna ya kudumisha uhusiano wao. Bado kichwani mwa Edo kulikuwa na matumaini.

Ni kweli alimpenda sana mpenzi wake Lilian, lakini alitamani sana japo apate fursa ndogo tu ya kujifurahisha nafsi yake. Ni jambo baya, alikiri lakini japo kidogo tu.

"Nitazungumza naye zaidi. Haiwezekani niwe naye kwa muda wote huo, nimevumilia. Leo nataka kusafiri kwenda Malaysia nimuache hivihivi, hapana bwana. Nitafanya kila njia," akajisemea moyoni mwake.

KILIKUWA kipindi cha ukimya mfupi. Lilian alimwangalia Edo kwa muda. Macho yake yalishatoa taswira ya kilichokuwa moyoni mwake.

Lilian alishajua mwenzake alikuwa katika hasira. Alikasirishwa na jambo ambalo lilikuwa na faida kwao wote wawili. Kukubali jambo lile lifanyike, kulimaanisha kukubaliana na kusitishwa kwa uhusiano wao.

Msimamo wake ulikuwa wa hali ya juu sana. Kuliko akubali kuuachia mwili wake utumike na Edo, hata kama alikuwa na mzigo wa mapenzi moyoni mwake, ilikuwa bora waachane.

Moyoni alijaa Edo pekee. Kuachana halikuwa jambo zuri kwa hakika. Uundaji wa maneno ukaanza kichwani mwake. Alitakiwa kuwa na maneno mazuri ya kumwambia Edo ili akubaliane na msiamo wake ambao tayari Edo alishaonekana kuushindwa!

Aliendelea kuung'ang'ania mkono wa Edo. Macho yake bado yalikuwa usoni mwa Edo ambaye naye alimwangalia kwa makini akisubiri ujumbe kutoka kwa mpenzi wake. Alijua ujumbe wenyewe usingekuwa mzuri sana kwake, lakini alitaka kusikia chochote kutoka kwake!

Macho ya Lilian yalitingishika, kope zikacheza kidogo kuruhusu usafi wa macho yake. Taratibu alifungua kinywa chake.
 
SEHEMU YA 4 KATI YA 50

Meno yake meupe peee yakaonekana.

Akauuma ulimi wake, akaanza kuzungumza: "Edward."

Edo akashtuka! Hakumbuki mara ya mwisho Lilian kumwita jina lake lote kikamilifu bila kulikatisha na kumwita Edo.

"Nakusikia."

"Mbona umeshtuka?"

"Nimeshangaa ulivyoniita jina langu lote maana si kawaida yako."

"Ni kweli, nimefanya hivyo kutokana na umuhimu wa jambo ninalotaka kukuambia."

"Sawa nakusikiliza."

"Mpenzi wangu jamani, mbona una hasira hivyo? Kuwa na utulivu kidogo basi baba!"

"Lilian nakusikiza."

"Ok! Nikuulize swali moja?"

"Uliza."

"Unanipenda?"

"Hata moyo wako unajua hilo," akajibu Edo akilengwa na machozi.

Ni kweli alikuwa amezungumza hisia zake za ndani kabisa. Hakuwa kwenye maigizo wakati akimwambia Lilian kuwa anampenda na moyo wake unatambua hilo!

Ni kweli, moyo wa Lilian ulitambua hisia za Edo.

"Najua baba. Kama ndivyo, hebu naomba unisikilize kwa makini... umevumilia kwa miaka mingapi mpenzi wangu? Si mitano? Eeeeh? Kuna tatizo gani kusubiri kwa hiyo miaka miwili tu iliyobaki? Kunah araka gani?

"Hivi utaniamini vipi mimi kuwa sitakuwa na mwanaume mwingine? Sikia dear, sijawahi kukutana na mwanaume yoyote tangu kuzaliwa kwangu. Hii ni zawadi yako mpenzi.

"Ona...ukiniacha na hii hali itakuwa ni usalama na ulinzi wa kweli kwako. Siwezi kumpa mtu. Nitakupa wewe tu muda ukifika. Maana yake ni kwamba, ikiwa leo utanitoa usichana wangu, ukiondoka kesho, hata kama nikikutana na mwanaume mwingine huwezi kujua mpenzi.

"Nipe uhuru, niamini. Mbona nakuamini mpenzi? Au huwa unafanya na wengine? Ni heshima kunioa nikiwa msichana kamili. Mpenzi wangu, acha papara!" alisema Lilian kwa sauti laini lakini haraka haraka.

Edo akatulia kwa muda.

"Kubaliana na mimi baba. Kubaliana na hii heshima mpenzi wangu."

"Nimekuelewa mpenzi wangu," akajibu Edo kwa sauti ya utulivu sana.

"Kweli?"

"Ndiyo."

"Umeagiza nini?"

"Nafurahi kula ugali na makange."

"Makange ya nini?"

"Unapenda nini?"

"Wewe umeagiza ya nini?"

"Samaki, sato."

"Uko sahihi kabisa mpenzi."

"Nawe utapenda kula kama mimi?" Edo akauliza.

"Ni lini tumekuwa pamoja tukala vyakula vya aina tofauti?"

"Ok! Ngoja nimwite mhudumu."

Edo akamwita mhudumu na kumuagizia mpenzi wake chakula kama alichoagiza yeye.

"Vije kwa wakati mmoja!"

"Sawa," mhudumu akaitikia akiondoka zake.

Mazungumzo yao yakabadilika, sasa ikawa ni kuhusu maisha yao yajayo na namna ya kudumisha uhusiano wao. Bado kichwani mwa Edo kulikuwa na matumaini.

Ni kweli alimpenda sana mpenzi wake Lilian, lakini alitamani sana japo apate fursa ndogo tu ya kujifurahisha nafsi yake. Ni jambo baya, alikiri lakini japo kidogo tu.

"Nitazungumza naye zaidi. Haiwezekani niwe naye kwa muda wote huo, nimevumilia. Leo nataka kusafiri kwenda Malaysia nimuache hivihivi, hapana bwana. Nitafanya kila njia," akajisemea moyoni mwake.

"Mbona kama unaonekana una mawazo sana?" akauliza Lilian.

"Hapana usijali, nipo sawa mpenzi wangu."

"Vizuri kama ndivyo."

Muda mfupi baadaye chakula kilikuwa mezani. Walifurahia sana chakula hicho. Makange ya sato yakikutana na mtaalamu anayejua kutengeneza, walaji lazima wafurahie.

***

Kadi iligusishwa kwenye kitasa cha mlango. Ukasikika mlio mdogo, Edo akausukuma, ukafunguka. Aliingia mara moja, kisha nyuma yake Lilian akafuatia.
 
SEHEMU YA 5 KATI YA 50

Akasukuma mlango na kuchomeka kadi pembeni ya mlango kulipokuwa na sehemu maalumu ya kuhifadhi. Baada ya hapo Edo akaenda kujilaza kwenye sofa kubwa lililokuwa ndani ya chumba kile.

Bado kichwani mwake alikuwa akiwaza namna ya kumpata Lilian.

"Lakini mpenzi, kwa nini unaonekana una mawazo sana?" Lilian akauliza.

"Lilian, siyo jambo rahisi kutengana kwa muda mrefu kiasi hicho. Miaka miwili ni mingi sana mpenzi wangu. Nafikiria kuhusu usalama wa penzi langu.

"Sina hakika kama utaweza kuvumilia kwa muda wote huo. Nalazimisha kuamini lakini moyo wangu unakataa kabisa mpenzi."

"Kwani ni muda gani tumekuwa pamoja baba?"

"Miaka mitatu."

"Katika kipindi chote hicho, kuna wakati ulihisi nakusaliti?"

"Hapana."

"Kwa nini kipindi hiki?"

"Hata mimi nashangaa, ngoja nijaribu."

Edo alisimama na kuvua tisheti yake, akatoa na suruali kisha akabakiwa na bukta na fulana nyepesi ya ndani. Akajitupa kitandani.

Aliingia ndani ya blangeti na kujikunyata. Ujanja wa joto la Dar es Salaam, ulizimwa na kiyoyozi kilichokuwa kikisambaza hewa taratibu ndani ya chumba kile. Lilian akasimama kwa muda akijishauri.

Akachukua taulo na kujifunga kifuani, kisha akaanza kuvua nguo zake huku akiwa amejikinga na taulo. Akachukua gauni la kulalia, akavaa na kwenda kitandani.

Aliingia kwenye blangeti na kuungana na Edo. Kwa ushawishi wa baridi, Lilian akajikuta akihitaji joto zaidi ya blangeti lililokuwa juu ya mwili wake.

Akamsogelea Edo. Ilikuwa nafasi ya dhahabu. Edo alimvuta Lilian upande wake na kumkumbatia sawasawa. Alikuwa akitetemeka kwa hisia kali za huba.

Kwa namna hali ilivyokuwa, ilikuwa vigumu sana kukubaliana na ukweli kuwa, alitakiwa kulala na mpenzi wake katika hali ile lakini bila kuvunja sharti walilokubaliana. Sharti la kutokukutana kimwili hadi watakapofunga ndoa.

"Nikuambie kitu Lilian?" Edo akasema.

"Niambie mpenzi."

"Ikiwa usiku wa leo hutanipa penzi lako, kesho nitakwenda Malaysia nikiwa sina mchumba niliyemuacha Tanzania. Sitajali muda niliopoteza kwako, ninachotaka ni penzi lako tu!" akasema Edo, safari hii machozi yakianza kutiririka machoni mwake.

Lilian hakujibu kitu!

ALILIA kama mtoto mdogo. Machozi yalitiririka machoni mwa Edo. Pamoja na mwanga hafifu chumbani mle, Lilian aliweza kuyaona vizuri machozi ya mpenzi wake.

Alikuwa analilia mapenzi. Edo alionekana hakuwa tayari kuondoka Tanzania na kumwacha mpenzi wake wa muda mrefu bila kukutana naye kimwili.

Lilian alichanganyikiwa sana. Hakutaka kumuudhi mpenzi wake, lakini pia hakuwa tayari kuvunja ahadi yake. Bado moyo wake ulimwambia alitakiwa kufanya hivyo baada ya kuingia tu kwenye ndoa yao.

?Edo mpenzi wangu? Lilian akaita.

?Maneno yako hayatakuwa na maana yoyote kwa sasa?

?Nisikilize kwanza mpenzi?

?Lilian najua unaweza sana kuongea. Najua ulivyo na maneno ya ushawishi. Ninachokuomba kama kweli una nia na mimi, kama kweli unanipenda, ikiwa kweli mimi ndiye mwanaume wako wa dhati, nakuomba sana, usikatae ninachokitaka.

?Utaniacha na mateso makubwa sana ya moyo. Sijui kwa nini moyo wangu una mashaka kiasi hiki. Sina amani hata kidogo. Najua utanisaliti tu Lily, utanisaliti mama,? alisema Edo akionesha msisitizo wa hali ya juu katika kile alichokiongea.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 6 KATI YA 50

?Siwezi kufanya hivyo baba, mimi nakupenda wewe tu, sina mwingine na wala sifikirii kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako. Kubaliana na maneno yangu nakuomba,? alisema Lilian.

?Unasema kweli??

?Kweli Edo.?

?Kwa nini hutaki kukutana na mimi sasa??

?Si kwa nia mbaya kama nilivyokuambia, nafanya hivyo kwa sababu nzuri. Kwani huwezi kulala na mimi bila kunigusa?

?Hebu vuta picha, itakuwa furaha kiasi gani kama siku ambayo utakuwa unafunga ndoa na mimi unikute nikiwa na usichana wangu? Sitaki kumkasirisha mama yangu.

?Aliniambia nihakikishe jambo hili nalisimamia. Sipendi kumkosea. Tafadhali kubaliana na mimi mpenzi wangu. Nakupenda Edo, wewe ni wangu wa pekee,? alisema Lilian kwa sauti tamu, laini ikionyesha kumaanisha alichosema.

Edo alinyamaza kwa muda. Alitakiwa kutafakari kwanza. Ni kama Lilian alikuwa makini na maneno yake na alijipanga kwa kila neno moja lililotoka kinywani mwake.

Pamoja na yote hayo, Edo alijikuta akiguswa sana na maneno ya mpenzi wake. Ni kweli alivumilia muda mrefu. Kwa nini kipindi hicho kifupi tu?

Alilegeza masharti moyoni mwake, akakubali kumuacha mpenzi wake Tanzania bila kumgusa kabisa. Hilo alilipasisha moja kwa moja moyoni mwake.

?Lilian,? akaita Edo.

?Abee Edo, mpenzi wangu.?

?Sikiliza maneno yangu.?

?Nakusikiliza baba.?

?Tazama macho yangu...?

?Nayaona baba.?

?Unaona nini??

?Machozi.?

?Machozi yapo kweli, hakuna kingine unachokiona zaidi ya machozi??

?Kwa kweli sioni kitu zaidi ya machozi.?

?Angalia kwa makini Lilian,? akasisitiza Edo.

Lilian akatulia. Hapo sasa akaamua kumwangalia kwa makini zaidi. Alimwangalia tena na tena.

Hola!

Hakuna alichokiona!

Aliishia kuona kilekile...

Aliona machozi ya Edo.

?Bado hujaona tu baby??

?Tafadhali naomba uniambie.?

?Sikia, nakupenda sana. Nakupenda kuliko utakavyoweza kufikiria. Nakupenda kwa moyo wangu wote na ninaamini hizi hisia zangu. Sijui kama nawe unanipenda mpenzi.?

?Nakupenda sana Edo, sina cha kusema au cha kukuonyesha ni kwa kiasi gani nakupenda, lakini fahamu kuwa nakupenda. Kitu pekee kitakachothibitisha kuwa nakupenda ni kukutunzia heshima yako mpaka siku tutakayofunga ndoa.

?Naamini hapo utakubaliana nami kuwa kweli nakupenda. Kwa sasa huwezi kuelewa mpenzi. Usichana wangu ndiyo zawadi ya pekee yenye thamani kuliko zote mpenzi wangu. Niamini baba, nenda salama chuoni, utanikuta. Mimi ni wako,? akasema Lilian.

?Kweli??

?Niamini mpenzi.?

?Nakuamini mama.?

Edo alitulia tena, ni kama alikuwa katika lindi fupi la mawazo. Aliikunja mikono yake kidogo, akanyoosha mguu wake mmoja, akiwa ndani ya blangeti, alijivuta hadi alipokuwa amelala Lilian.

Walitenganishwa na mto uliokuwa katikati yao. Edo aliunyakua haraka na kuurusha mgongoni mwake. Sasa walikutanisha miili yao. Kwa kasi ya ajabu, alimvutia Lilian kwake.

Akaenda mzimamzima!

Lilian hakuwa na nguvu lakini bado alikuwa akitaka kuona kitakachofanywa na Edo. Mwanaume wa maisha yake. Midomo ya Edo ikaanza kucheza.

Alikuwa anazungumza: ?Mpenzi wangu Lilian, lazima nikueleze kuhusu hili. Siwezi kuacha kusema maana naona inaweza kusababisha matatizo siku za baadaye.?

Lilian akashtuka!

Alitaka kujitoa kifuani mwa Edo, akamdhibiti. Haikuwa rahisi kuponyoka mikononi mwa mwanaume yule aliyekuwa mshirika wa kudumu wa mazoezi ya viungo.

?Tulia...? akasema Edo.
 
SEHEMU YA 7 KATI YA 50

?Niambie ni nini baba??

?Naheshimu sana hisia zangu za ndani. Sijui kwa nini nafikiria hivyo, lakini nahisi kama nikikuacha huku Tanzania lazima utanisaliti. Kama hisia hizi si za kweli, tafadhali naomba uthibitishe kwa kuwa mwaminifu.?

Lilian alihisi moyo wake ukiingiwa na ubaridi kama wa maji ya barafu. Hakutegemea kusikia maneno hayo kutoka kwa mpenzi wake Edo. Yalikuwa maneno mazito sana yaliyomchanganya.

?Edo?! Kweli unaweza kunifikiria hivyo baba??

?Lazima nikuambie kilichopo moyoni mwangu.?

?Naomba uwe na amani mpenzi wangu, usinifikirie vibaya hata kidogo. Mimi ni wako na nitaendelea kuwa wako milele. Tafadhali, safiri ukiwa na amani moyoni mwako kuwa nitakuwa salama na nitahifadhi mali zako!? akasema Lilian.

?Ok! Acha nikuamini. Nakupenda mpenzi. Tulale sasa, umeshakuwa usiku, kesho tutazungumza zaidi.?

?Sawa mpenzi wangu.?

Ilikuwa kama kifaranga cha kuku kikiwa kimekumbatiwa na mama yake, Lilian alilala kifuani mwa Edo. Ahadi yao iliendelea kuwa ileile, kwamba hawatafanya chochote usiku huo.

Ni ahadi ambayo ilitekelezwa!

***

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) ulikuwa bize sana jioni hiyo. Watu walikuwa katika pilikapilika za kusafiri au kupokea wageni wao kutoka ndani na nje ya nchi.

Edo na Lilian walikuwa miongoni mwao; kwao ilikuwa siku yenye maumivu makali ya moyo. Edo alikuwa anaachana na mwanamke wake akiwa na uhakika wa kutoonana naye kwa miaka miwili! Kilikuwa kipindi kirefu sana.

Kilikuwa kipindi ambacho Edo aliamini kingetosha kabisa kubadilisha historia ya uhusiano wao. Aliuona usaliti waziwazi kabisa. Kweli Lilian amvumilie kwa muda wote huo?

Miaka miwili?

Ilikuwa mingi sana. Ni muda ambao ungeweza kubadilisha chochote na akampoteza mpenzi wake. Alikuwa na mizigo yake, tayari kuingia chumba cha ukaguzi na kuendelea na taratibu nyingine za safari.

Walisimama wakiwa wanaangaliana, kila mmoja alionekana kuwa na mawazo yake kichwani. Edo alivumilia yote. Alikubaliana na yote. Alimwacha Lilian aamua mwenyewe. Amsaliti au amtunzie heshima.

?Nakuambia kwa mara nyingine nakupenda sana mpenzi wangu. Naondoka nikiwa nimekuacha na usichana wako, tafadhali nikirudi nikukute nao,? akasema Edo akimwangalia Lilian kwa hisia kali za mapenzi.

?Nakuahidi mpenzi wangu. Nimeshasema mengi, sina ya kuzungumza zaidi. Nakupenda sana, nakutakia safari njema!? akasema Lilian.

Haikuwa rahisi, lakini ndivyo ilivyokuwa na ilipaswa kuwa hivyo. Edo aliachiana na Lilian, akasogea kwenye foleni ya kuingia chumba cha ukaguzi.

Edo akageuza kichwa na kumwangalia Lilian, alichokutana nacho, kilimtisha sana. Alipigwa na butwaa!



Safari iliingia doa. Kwa alichokiona, Edo hakuwa na amani tena katika safari yake. Alimwangalia tena Lilian kwa lengo la kujiridhisha juu ya kile alichokuwa akikiona. Akapata uhakika kuwa ni kweli, hapakuwa na mabadiliko.



Abiria wengine waliokuwa kwenye foleni kuelekea chumba cha ukaguzi waligundua utulivu finyu wa Edo. Wakajua lazima kulikuwa na kitu kilichomsumbua.



Simu iliita mpaka ikakatika bila kupokelewa na Lilian. Edo akachanganyikiwa. Akageuka kumwangalia Lilian. Alikuwa amesimama palepale akimwangalia. Edo akamwonyesha ishara apokee.





Lilian akapokea!



“VIPI darling, kwanini unalia?” Edo akatamka kwa sauti tulivu iliyosikika barabara sikioni mwa Lilian.
 
SEHEMU YA 8 KATI YA 50



“Edo...” Lilian akaita badala ya kujibu swali. “Yes dear...” “Unanipenda?” “Nakupenda sana Lilian. Kwanini unaniuliza swali hilo, tena leo? Kwanini?” Edo akamwuliza. “Nataka kujua tu.” “Nakupenda Lilian, hata moyo wako unajua hilo.”



“Nafurahi kusikia hivyo mpenzi. Moyo wangu sasa angalau una amani. Safiri



salama mpenzi wangu. Nakupenda sana Edo.” “Ahsante sana mpenzi wangu.” Mpaka Edo akiwa anakata simu, bado Lilian alikuwa hajaitoa simu yake sikioni. Edo akapotea machoni mwake alipoingia tu kwenye chumba cha ukaguzi.



“Nafurahi kusikia hivyo mpenzi. Moyo wangu sasa angalau una amani. Safiri salama mpenzi wangu. Nakupenda sana Edo.” “Ahsante sana mpenzi wangu.” Mpaka Edo akiwa anakata simu, bado Lilian alikuwa hajaitoa simu yake sikioni. Edo akapotea machoni mwake alipoingia tu kwenye chumba cha ukaguzi.



Bado Lilian hakutaka kuondoka. Aliendelea kusubiri pale uwanjani hadi nusu saa baadaye. Kila ndege iliyokuwa ikianza kuruka uwanjani pale na Lilian kuiona, aliishia kupunga mkono.



Vyovyote itakavyokuwa, yeye aliamini kati ya ndege hizo, mojawapo mpenzi wake Edo angekuwa ndani yake. Ndicho kitu kilichokuwa akilini mwake.



Bahati mbaya sana kwake ni kwamba, kati ya ndege hizo alizokuwa akizipungia mkono, hapakuwa na hata moja ambayo ndani yake alikuwepo Edo.



Lilian aliondoka uwanjani pale akiwa mwenye huzuni sana. Bado Edo alikuwa akilini mwake, ilikuwa vigumu sana kumtoa kichwani mwake. Edo alikuwa kila kitu katika maisha yake.



Miaka miwili iliendelea kujirudia kichwani mwake.



Haikuwa rahisi kusubiri kwa muda wote huo, lakini moyoni aliamini angeweza maana alijua kushikilia msimamo wake sawasawa!



Miaka miwili iliendelea kujirudia kichwani mwake. Haikuwa rahisi kusubiri kwa muda wote huo, lakini moyoni aliamini angeweza maana alijua kushikilia msimamo wake sawasawa!



“Mimi nitakuwa sawa, naweza kujitunza kwa muda wote. Hakuna tatizo mimi kuwa mwaminifu kwake, mbona siku zote nimemvumilia? Kwanini iwe leo? Najua nitaweza tu,” akawaza Lilian akiwa uwanjani hapo.



Nusu saa baadaye aliamua kurejea chuoni, Edo akiwa amegoma kabisa kuondoka kichwani mwake. Pendo lake kwake lilizidi kukolea. *** Ilikuwa ni mishale ya saa kumi alasiri, jua likianza kupungua nguvu, ushindani mkali kati yake na mwezi ukiwa umeanza kwa mbali. Ni kama giza lilikuwa likijiandaa kushika hatamu baada ya nuru kutawala kwa siku nzima.





Ni jua ambalo pamoja na kwamba lilikuwa hafifu, liliweza kabisa kuchoma! Kwa wanafunzi waliokuwa katika maeneo ya kujisomea ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, jua hilo halikufua dafu! Siyo jua wala joto! Mazingira ya kijani kibichi yalisaidia sana kuzima joto na jua lililokuwa likiishilia.



Lilian alishuka ngazi taratibu, akielekea sehemu ya kujisomea kwenye kundi lake. Siku zote alipenda kusoma na rafiki zake watatu; Leila, Latifa na Lucy! Ni kama walichaguana. Wenyewe mara kadhaa wamekuwa wakijiita Double Twince lakini rafiki zao walipenda kuwaita zaidi Mapacha Wanne. Majina yao wote yalianza na herufi L.



Haikuwa majina tu; walifanana vitu vingi. Wote walikuwa weupe usiong’aa, warefu kiasi na wembamba kiasi.



Mionekano yao ilifanana. Huwezi kuwaita wanene lakini baadhi ya sehemu za maumbile yao ndiyo yaliyosababisha mgongano wa sifa zao.
 
SEHEMU YA 9 KATI YA 50



Vifua vyao vilikuwa vizuri vikipambwa na matiti makubwa kiasi yaliyoinuka! Wote hakuna aliyevaa sidiria. Ya kazi gani sasa wakati matiti yaliweza kusimama yenyewe bila msaada?



Hipsi zilikuwa kivutio kingine, mwisho ni milima ya haja iliyokuwa nyuma ya viuno yao! Hakika walifungasha. Kufungashia huko hakukuwa na maana kuwa walifanana na majimama, la hasha!

Milima yao iliendana kabisa na maumbo yao. Kwa mifanano ya maumbo walikuwa sawa, tatizo likawa kwenye tabia. Hasa kwenye maisha yao ya kimapenzi.

Leila na Lilian walikuwa na misimamo inayofanana. Leila alikuwa na mpenzi wake mmoja anayejulikana aliyeitwa Michael, maarufu zaidi kama Mike, Lilian yeye alitoka na Edo ambaye awali alikuwa akisoma naye chuoni hapo.

Latifa na Lucy wao habari zao zilikuwa nyingi! Hawakutulia na wanaume kabisa. Mikesha na kwenda klabu ilikuwa ndiyo michezo yao. Pamoja na yote hayo, bado wote kwa pamoja walikuwa na juhudi sana darasani na walikimbiza wenzao katika masomo yote.

Lilian alikuwa akitembea kwa pozi kama vile alikuwa akizionea huruma ngazi alizokuwa akitembea. Bado alishindwa kuondoa Edo kichwani mwake.

SASA ENDELEA...



ILIKUWA ndiyo kwanza siku ya pili inakatika baada ya kuagana na Edo. Hadi muda huo hakuwa na mawasiliano yoyote na Edo ingawa alimtumia waraka pepe tatu na zote hakujibu. Kwa mbali akawaona rafiki zake akina L wakiwa wamekaa kivulini wanajisomea.

Ni palepale pa siku zote!

Kwa kawaida walizoea kusomea sehemu moja. Lilian alikazana na kuwafikia. Lilikuwa kundi zuri sana la majadiliano kutokana na namna wote walivyokuwa na mtazamo mkubwa na uwezo wa kuelewa.

?Mambo zenu warembo?? Lilian akasalimia.

?Poa Lilian, vipi mwenzetu?? Leila alikuwa wa kwanza kuitikia salamu.

?Safi tu.?

?Karibu mrembo, tunatengeneza maisha hapa, hatupo tayari kuendelea kunyanyaswa na wanaume, elimu ndiyo mkombozi wetu wa kweli,? Latifa naye akasema.

?Kweli kabisa,? akajibu Lilian kisha akaketi na kutoa vitabu vyake.

Jambo lililomshangaza ni kwamba, muda wote aliofika hapo, Lucy hakusema kitu chochote! Lilian hakumfikiria vibaya, aliamini ni masomo ndiyo yaliyokuwa yamembana. Akanyamaza kimya na kuanza kupiga kitabu.

Wote wakawa kimya!

Dakika tano baadaye, Lucy alionekana kuchukua bahasha kwenye begi lake la vitabu na kumkabidhi Lilian. Alipokea kwa mshangao. Ilikuwa bahasha ndogo kiasi lakini iliyonona. Ilionekana ndani yake kuwa na makabrasha muhimu ila yaliyojaa.

?Ni nini??

?Utafungua baadaye.?

?Kama ni bomu je??

?Mh! Wewe naye, nani wa kukuwekea bomu sasa mtoto wa kike??

?Niambie ni nini basi??

?Mtoto una haraka sana wewe. Haya fungua!? akasema Lucy.

Lilian akafungua. Alikutana na burungutu la noti za elfu kumikumi!

Bahasha ilikuwa imejaa kiasi kwamba haikuwa rahisi kufungika vizuri.

?Zimetoka wapi??

?Hapo sasa tutazungumza baadaye.?

?Hapana Lucy, chukua pesa zako.?

?Acha upuuzi wewe, lini utakuwa na akili? Huyo Edo unayemn?ang?ania, unajuaje kuwa naye hakusaliti? Kwanza sasa hivi hayupo nchini, una wasiwasi gani? Tumia urembo wako vizuri mtoto, la sivyo utabaki unang?aa macho tu mjini hapa,? akasema Lucy kwa msisitizo.
 
SEHEMU YA 10 KATI YA 50

Lilian hakuwa mtoto, alishajua kuwa zile fedha zilitoka kwa mwanaume. Kwa Lucy na Latifa, kubadilisha wanaume lilikuwa jambo la kawaida kabisa.

?Lucy tunaheshimiana sana mimi na wewe, kumbuka kinachotukutanisha hapa ni masomo tena ni kwa vile hili ni kundi letu la kujisomea na ni zuri. Tuishi kwa kuelewana na kuheshimiana.

?Ni vyema kila mmoja akaheshimu hisia za mwenzake. Kwanini unataka kunilazimisha nifanye kitu ambacho sikipendi? Chukua pesa zako,? Lilian akasema kwa ukali sana.

?Sitaki, kama unaweza kuzichoma labda ufanye hivyo. Huo ushamba utakutoka lini? Kwani kula pesa ya mtu ndiyo kumkubali? Acha ujinga, kula maisha hayo, mambo mengine baadaye,? akasema Lucy akijiandaa kuinuka.

Ni kweli aliinuka.

Alikusanya vitabu vyake na makabrasha mengine, akaondoka zake. Pale akawaacha Latifa, Leila na Lilian wakimshangaa.

Ama kweli alishangaza!

?Sikia shosti, kwani wewe umeomba hela?? akasema Leila.

?Ndiyo nashangaa!?

?Sasa huna haja ya kushangaa, chukua mzigo utumie. Ni nani anaweza kukufuata kukudai? Kwani umekopeshwa? Tumia lakini akikuambia mambo ya wanaume kataa,? akasema Leila na kuungwa mkono na Latifa:

?Kweli kabisa, sioni tatizo.?

?Wewe na yeye ni walewale tu!? akasema Leila.

?Jamani hebu tusomeni basi, kwani Lilian ni mtoto? Kwanini tunatofautina kwa mambo binafsi? Yeye ni mtu mzima na anaweza kuamua chochote kwa utashi wake,? akasema Latifa.

Lilian alikuwa kwenye mzigo mzito wa mawazo lakini alipotafakari sana, hakuona sababu ya kukataa hizo fedha. Akaziweka kwenye mkoba wake na kuendelea kujisomea.

?Kibaya ni kumsaliti Edo, kama ni pesa sioni tatizo lake,? akajisemea moyoni mwake akiendelea kujisomea.

***

Edo alifika jijini Kuala Lumpur, nchini Malaysia salama kabisa. Alikuwa na maelekezo yote, hivyo haikuwa vigumu kwake kufika chuoni. Alipokelewa vizuri na kuelekezwa chumbani kwake kisha taratibu nyingine zikafuata.

Alikuwa mchovu sana kutokana na safari ndefu ya kutoka Tanzania hadi Malaysia. Siku tatu baadaye ndipo alipopata utulivu wa akili kidogo. Akiwa chumbani kwake, akakumbuka kuwasiliana na mpenzi wake.

Bado hakuwa na mawasiliano ya simu ya mkononi, simu alikuwa nayo lakini alikuwa bado hajapata usajili wa namba kutoka moja ya kampuni za simu nchini humo.

Alifungua laptop yake na kuingia kwenye akaunti yake ya waraka pepe. Alikutana na ujumbe kutoka kwa watu wengi sana, akiwemo Lilian ambaye alimwandikia mara tatu. Akaanza kusoma mmoja baada ya mwingine.

Hello,

Edo. Najua umefika salama mpenzi wangu. Pole na safari baba. Napenda kukuhakikishia kuwa, moyoni mwangu umejaa wewe pekee na hakuna nafasi ya mwingine zaidi yako. Nakupenda sana.

Ukipata ujumbe wangu, tafadhali unijibu.

Lilian.



Edo akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu kabisa. Akatulia kwa muda. Baadaye kidogo akafungua ujumbe unaoufuata.

Ujumbe huo ndiyo uliomshtua sana moyo wake. Aliuma meno kwa nguvu, akarudi kuangalia jina na anwani ya mtu aliyemtumia ili ajiridhishe kuwa Lilian ndiye aliyemtumia.

Ni kweli alikuwa ni Lilian!

Akazidi kuchanganyikiwa!

ALITEMBEA kwa maringo yaliyoonekana wazi. Hayakuwa ya kutafuta. Lucy alijua alivyo mrembo, hivyo kuonyesha maringo ilikuwa kichagizo cha jinsi alivyo.
 
SEHEMU YA 11 KATI YA 50

Wanafunzi wengine walikuwa wakimkodolea macho wakati akitembea taratibu akionekana asivyo na haraka na alipokuwa akielekea. Ni kweli hakuwa na haraka maana safari yake ilikuwa inaishia hosteli.

Pamoja na uzuri wa umbo lake, pia mavazi yake yalimshawishi kila mwanaume aliyekamilika kumwangalia kwa uchu wa mahaba mazito.

Kwa mwanaume mkamilifu, ingekuwa vigumu sana kwa Lucy kupita mbele yake bila kukata shingo kumwangalia. Lucy alizawadiwa urembo wa kutosha!

Alitembea hadi alipofika kwenye barabara kubwa ya lami, akasimama kupisha magari yapite kisha akavuka na kupanda kijimlima kidogo kuelekea hosteli.

Alipofika chumbani kwake, alijitupa kitandani, kisha akajilaza kwa mgongo na kuyarusha mcho yake juu ya dari na kuanza kuwaza...

?Siwezi kushindwa kumshawishi Lilian. Ni mtoto mdogo sana. Mimi namuweza. Hanishindi kwa lolote,? akawaza.

?Lazima aingie kingi,? akajisemea kwa sauti.

?Huyu mtoto mdogo tu kwangu, anajifanya ana msimamo. Itakuwa yeye...hapa Bongo akili kichwani.?

Lucy alikuwa kwenye lindi zito la mawazo. Kikubwa kilichokuwa akilini mwake ni milioni tano alizoahidiwa na mzee mwenye fedha zake, mfanyabiashara mkubwa jijini Dar es Salaam, Pamseck Kinga.

Kinga hujulikana zaidi kwa jina la Pam. Kazi aliyopewa na Pam ni kuhakikisha anamuingiza Lilian kwenye himaya yake. Kwa kuanzia Pam alimpa shilingi milioni moja kwenye bahasha ili ampelekee Lilian.

Fedha kwake ilikuwa siyo shida, tatizo kubwa lilikuwa matumizi tu!

Lucy akiwa bado yupo mawazoni, akifikiria mbinu nyingine mpya ya kumnasa Lilian kiulaini, simu yake iliita. Alipoangalia kwenye kioo akakutana na jina la Pam. Haraka akapokea.

?Nategemea kusikia kitu kizuri kutoka kwako, haya niambie,? sauti ya Pam iliunguruma simuni.

?Mh! Pam mbona una haraka sana baba??

?Lazima niwe na haraka. Namtamani sana huyo mtoto. Niambie umefikia wapi??

?Hatua nzuri.?

?Hatua nzuri siyo??

?Kabisa.?

?Nataka kujua kitu kimoja kwanza; amechukua huo mzigo??

?Ndiyo lakini kwa kumlazimisha sana.?

?Anajua ulipotoka??

?Hapana, lakini lazima atakuwa anahisi, kwani yeye mtoto? Kuna pesa inaweza kujipeleka yenyewe??

?Kweli lakini, dalili unazionaje??

?Pam usiwe na wasiwasi, niachie mimi hii shoo nitaisimamia mpaka mwisho.?

?Nakuamini Lucy, ni mtihani wako mdogo sana. Ukiufaulu milioni moja itakuwa halali yako.?

?Sema.?

?Nataka wikiendi hii uje naye club, utaweza??

?Milioni ipo??

?Kumbuka mimi ndiyo nimekuahidi.?

?Sawa, niachie mimi.?

?Nakutumia laki tano baadaye kidogo, ukifanikiwa kuja naye, laki tano yako nitakumalizia. Kumbuka matumizi mengine yote ambayo utakayotumia wewe na rafiki zako kutokana na ujio wenu nitalipia mimi.

?Hapo namaanisha kuanzia mambo ya salon na mengineyo nitarudisha. Kazi yako ni moja tu; kuhakikisha Lilian unakuja naye disko. Mambo mengine niachie mimi.?

?Kazi ndogo, tuma pesa hiyo kwa namba zangu za simu.?

?Robo saa ijayo fedha itakuwa tayari imeshakufikia.?

?Poa Pam.?

?Usiniangushe Lucy.?

?Umenisahau mara hii?? akasema Lucy huku akisindikiza na kicheko cha nguvu.

?Sawa.?

Pam akakata simu.

Lucy aliendelea kuisikiliza simu yake. Alipogundua ilikuwa imekatwa, akaitoa sikioni.

?Nitajua cha kufanya,? akasema.

Palepale akamtumia meseji Latifa iliyosomeka: ?Shoga, Pam amenipa dili lingine, amesema kama nikifanikiwa kwenda na Lilian club wikiendi hii, atanipa milioni moja.
 
SEHEMU YA 12 KATI YA 50

?Sasa nakupa dili, na wewe hapa nakushirikisha, utakula laki mbili. Naomba uanze kulianzisha.?

?Poa shoga yangu, miye tena? Huku huku naanza mambo,? akajibu Latifa.

***

Wiki moja bila Edo nchini Tanzania ilikuwa ngumu kwa Lilian. Chuo kilianza kuwa na ugumu kidogo. Kwa namna alivyojizoesha matumizi makubwa, bila Edo ilikuwa ni wakati mgumu sana kwake.

Pamoja na fedha wanayopewa wanafunzi wote kwa ajili ya matumizi, bado haikuweza kukidhi mahitaji yake ipasavyo. Umuhimu wa milioni aliyopewa na Lucy akiwa hajui ilipotokea ulionekana dhahiri.

Kwa kutumia hila na maneno laghai, Latifa na Lucy walifanikiwa kuwateka mawazo Leila na Lilian na kukubali kwenda disko, kichwani wakiamini walikuwa wanakwenda kwenye berthday.

Walipofika Masaki, kibao kikageuka. Wakaambiwa wanakwenda Klabu Maisha. Lilian aligoma, kwa ushawishi wa Lucy na Latifa, Leila akajikuta akiunga mkono, Lilian akajikuta akikubali kuingia. Lucy aliwalipia wote.

Disko lilikuwa limechangamka sana. Lilian alionekana kuwa mpole, akiwa amekaa kwenye kiti muda wote akinywa juisi. Latifa na Lucy walikuwa wamekolea kilevi, wakicheza kwa madaha muziki uliokuwa ukirindima.

Leila alijikuta akifuata mkumbo na kwenda kucheza na wenzake. Muziki ulipokolea, Lucy alikwenda kumvuta Lilian na kuelekea naye kwenye sehemu maalumu ya kuchezea muziki.

Kwa shingo upande, Lilian alijikuta akienda. Hakujua kuwa alikuwa akienda kukutana na Pam!

***

Edo aliendelea kusoma ujumbe ule zaidi ya mara tatu; maneno yalikuwa yaleyale. Safari hii aliamua kusoma kwa sauti:

Edo

Nilijua lazima hili lingetokea. Ni wiki tu tangu umeondoka, lakini tayari hisia za usaliti zimeanza kunukia. Nakuomba baada ya kusoma ujumbe huu, tafadhali endelea na maisha yako, nami niache na maisha yangu.

Siwezi kuendelea kulazimisha mapenzi mahali nisipopendwa. Kwa taarifa yako kwa sasa natafuta mwanaume mwingine ambaye ataweza kunithamini na kujua umuhimu wangu.

Kutokea muda utakaosoma ujumbe huu, ondoa kichwani mwako kuwa una mwanamke Tanzania anayeitwa Lilian.

Lilian.

Edo akaamua kujiridhisha tena kujua kama aliyetuma alikuwa ni Lilian. Ni kweli ulikuwa ujumbe kutoka kwa Lilian. Hilo alijihakikishia kwa asimilia mia moja!



Edo alihisi kichwa kinataka kupasuka !!!!



KICHWA cha Edo kilivurugika! Alianza kuhisi maisha yake machungu nchini Malaysia. Hakuwa tayari kumpoteza mpenzi wake, mwanamke ambaye aliingia moyoni mwake jumla!

Bado alikuwa na maswali mengi. Edo hakuamini kuwa Lilian, mwanamke wa ndoto zake ambaye walikaa muda mrefu na kuvumiliana, tena wakiahidiana mambo mengi amwambie kuwa asimtafute tena.

?Inawezekana kweli ikawa Lilian akanikataa kabisa? Mbona nachanganywa na hili jambo? Lilian amechanganyikiwa? Kinachompa kiburi ni nini? Imekuwa mapema sana kwake kufikia uamuzi huu.

?Sasa nimejua ni kiasi gani nampenda Lilian. Amejaa moyoni mwangu. Lilian ndiye mwanamke wangu. Amepatwa na nini jamani?? akazidi kuwaza.

Alipata wakati mgumu sana. Hakuwa na kitu cha kufanya zaidi ya kumjibu. Bado alitaka kusikia jibu kutoka kwa Lilian kabla ya kuyaaminisha moja kwa moja maneno aliyosoma kwenye waraka pepe.

Edo akamjibu.

Kwako,

Lilian. Nimesoma email zako, nimeelewa uamuzi wako lakini bado nashindwa kuelewa sababu hasa za wewe kuchukua uamuzi huo.
 
SEHEMU YA 13 KATI YA 50

Nimejiuliza maswali mengi lakini bado sijapata majibu.

Kweli Lilian umesahau mapema kiasi hicho? Kweli umesahau wema wangu wote? Sasa naanza kuamini kuwa, kumbe hukuwa na mapenzi ya dhati kwangu.

Nimeelewa ni kwanini ulikuwa unaninyima penzi lako. Bila shaka utakuwa umeshatolewa bikra ndio maana hukutaka nijue. Umeniumiza sana. Nahisi harufu ya damu mbichi ndani ya moyo wangu.

Hata hivyo, bado una nafasi ya kutafakari upya. Una muda wa kufikiri na kuamua vinginevyo kama utaona inafaa. Nakupenda sana kutoka ndani ya moyo wangu. Ahsante kwa yote lakini kumbuka sikupaswa kuachwa kwenye maumivu makali kiasi hiki, tena wakati huu wa mwanzoni kabisa wa masomo yangu huku Malaysia.

Moyo wangu unateseka!

Edo.

Kwa hakika Edo hakuweza kuvumilia, muda wote aliokuwa akiandika ujumbe ule, machozi yalikuwa yakimtiririka mashavuni mwake. Haikuwa rahisi kukubaliana na hali ile.

Hakuweza kufanya chochote tena, baada ya kutuma ujumbe ule kwa Lilian, alijitupa kitandani na kuanza kuvuta kumbukumbu za mpenzi wake upya kabisa.

Zilikuwa kumbukumbu za mateso sana. Lilian alikuwa amemtenda katika kiwango kikubwa sana!

***

Lilian aliingia kati. Lucy alikuwa na kazi ya ziada akimshawishi acheze. Kwa aibu akajikuta akicheza. Kwa mbali Pam na rafiki yake Big walikuwa wamekaa wakiendelea kukata kinywaji.

Walikuwa watu wenye fedha zao. Pam alikuwa akisubiri kwa hamu kukutanishwa na Lilian. Hilo ndio lilikuwa lengo lake. Usiku ule alikuwa Klabu Maisha kwa lengo moja tu, kukutana na Lilian.

Hiyo ilikuwa kazi maalumu aliyopewa Lucy aikamilishe. Latifa alikuwa beneti na Leila. Tayari alishamshawishi na kuonja mvinyo kidogo iliyomchangamsha!

Ni Lilian pekee ambaye alikuwa hajaonja kilevi mpaka muda ule. Lilian alivyozoea kucheza pale kwenye sehemu maalumu ya kucheza, Lucy alichepuka kidogo.

Hapo akamwonyesha Pam ishara na kwenda kuketi naye sehemu nyingine ambayo Lilian hakuwaona.

?Vipi mama lao?? akasema Pam akicheka.

?Poa baba lao!?

?Nataka kujua ulipofikia. Mambo yanakwenda vizuri?? akauliza Pam akionyesha wasiwasi kidogo.

?Usiwe na shaka baba, mambo yanaendelea. Hatua ya kwanza imeshafanyika. Si unamuona mrembo ndani ya nyumba? Kilichobaki hapa ni kuwakutanisha tu!?

?Utafanyaje sasa??

?Hapa ndio nawaza, lakini nadhani nimpe pombe akilewa, wewe unamaliza!? akashauri Lucy.

?Hapana Lucy. Kumbuka mimi simhitaji huyo msichana kwa siku moja. Nahitaji aendelee kuwa wangu. Kumnywesha pombe halafu ndipo niondoke naye najua hatafurahia.

?Unaweza kuwa mwisho wa uhusiano wetu. Kwanini nisitumie njia za kistaarabu? Kitu pekee unachotakiwa kufanya ni kunikutanisha naye tu. Mambo mengine niachie mwenyewe.?

?Kweli Pam??

?Kabisa.?

Lucy akarudi kuungana na akina Lilian kuendelea kucheza. Muziki ulikolea kwelikweli. Baadaye wakaamua kupumzika kidogo kwenye viti vyao.

Hapo Lucy akatoa wazo la kwenda kukaa na marafiki zake. Hakuna aliyejua hao marafiki ni akina nani isipokuwa Latifa tu. Wote wakakubali. Wakasimama na kuwafuata Pam na Big.

?Pam kutana na marafiki zangu, Leila, Latifa na Lilian,? akasema Lucy haraka kisha akawageukia rafiki zake na kuwaambia:

?Huyu ni rafiki yangu, anaitwa Pam!?
 
SEHEMU YA 14 KATI YA 50

?Nashukuru kuwafahamu, warembo sana.?

Wakacheka!

?Huyu hapa ni rafiki yangu mkubwa hapa mjini, mfanyabiashara mwenzangu, anaitwa Big!?

?Tumefurahi sana kukutana nanyi,? Latifa akajibu akijifanya hawafahamu.

Ukweli ni kwamba Latifa aliwafahamu wote. Vinywaji viliendelea, Leila akiwa ameshazidi kuchangamka. Lilian alikuwa kimya akitumia juisi ya matunda muda wote.

?Kwanini unakunywa juisi muda wote? Nafikiri ungekunywa wine kidogo ili uchangamshe mwili. Siyo kali, ni laini kabisa,? Pam akamwambia Lilian.

?Mh! Naogopa mwaya,? akasema Lilian akionekana kujawa na haya.

?Huna sababu ya kuogopa, ni nzuri. Tafadhali jitahidi unywe hata glasi moja tu!? akazidi kushauri.

?Kweli kaka Pam? Unaniahidi siyo mbaya??

?Acha ushamba bwana, kama ingekuwa inalewesha mimi ningekuwaje? Mbona nimekunywa muda wote na bado nipo poa,? sasa Leila alidakia.

?Haya bwana, ngoja nijaribu!? akajibu Lilian baada ya kupata ujasiri kutoka kwa rafiki yake Leila.

Bila kupoteza muda, Pam akachukua glasi mezani na kummiminia Lilian kisha akamkabidhi.

?Karibu ufurahie matunda ya mzabibu!? akasema Pam akijilamba midomo, tabasamu aliliachia.

Lilian akapokea akizidi kuonyesha aibu waziwazi. Akapiga funda moja kubwa. Akakunja uso kidogo kutokana na uchungu kiasi aliohisi kutoka katika mvinyo ule.

Maskini, hakujua hatari iliyokuwa mbele yake!







Pam alitabasamu! Lilikuwa tabasamu pana ambalo halikujificha kabisa. Alikuwa na haki ya kutabasamu maana alikuwa na uhakika kuwa kazi yake sasa ilikuwa ikielekea kuwa nyepesi kuliko kawaida.

Uso wa Lilian ulikunjika sawasawa. Kwa tabu akameza funda moja kubwa la mvinyo. Ikaingia kooni taratibu kabisa! Akatikisa kichwa kwa nguvu!

?Mh! Nitaweza kweli?? akasema Lilian.

?No! No! No! Utaweza. Sikia... hutakiwi kunywa nusunusu, kwakuwa ni mara yako ya kwanza unatakiwa kumaliza hiyo glasi yote kwanza, halafu kutokea hapo ndiyo utaanza kuzoea.?

?Paaaam!? Lilian akasema akimwangalia Pam machoni.

?Yes! Ndiyo ukweli kama unahitaji kuzoea. Siyo chungu sana bwana!?

?Ngoja nijaribu.?

Lilian akanyoosha mkono wake kisha akachukua glasi na kuipeleka kinywani mwake. Aliigika ile mvinyo yote. Aliposhusha glasi ilikuwa tupu kabisa.

?Mnawezaje lakini?? Lilian akauliza.

?Acha hizo bwana, endelea kufurahi,? Leila akasema akionekana tayari ameshalemewa na mzigo mzito kichwani.

Haraka Pam akachukua chupa yenye mvinyo kisha akaijaza tena ile glasi ya Lilian. Akamwangalia kwa jicho la kumkaribisha kisha akarudisha macho yake kwa Lucy.

Wakatabasamu!

Kuna nini tena?

Kazi nyepesi kiasi gani?

?Karibu mama, endelea kufurahi,? akasema Pam.

Sasa Lilian akaichukua tena ile glasi, huku akionekana kuwa na uzoefu kidogo. Alikunywa kidogo, kisha akarudisha glasi mezani.

?Kweli sasa umekua mtoto wa mjini, na wewe inaonekana utazoea mapema sana!? akasema Lucy.

?Kweli wewe una akili sana. Umegundua hilo kama mimi??

?Yeah, ndicho ninachokiona kwa Lilian,? akasema Latifa.

Kweli Lilian alionekana kuchangamka sana, glasi moja na nusu aliyokunywa tayari ilionekana kumbadilisha kabisa. Uchangamfu wake ukaongezeka ghafla. Hakuna ambaye hakujua kilichotokea.

Ilikuwa tabasamu la pombe!

Palepale Lucy akamwonyesha ishara Pam wasogee pembeni kwa ajili ya mazungumzo. Alianza Lucy kuondoka kisha akafuata Pam, wote wakisema kuwa wanakwenda msalani.

?Nipe changu,? akasema Lucy akitabasamu.

?Usijali, haina shida. Pesa yako utapata.?
 
SEHEMU YA 15 KATI YA 50

?Lakini si umeniamini sasa??

?Sana. Kinachofuata??

?Kinachofuata nini tena? Chukua mzigo ondoka nao.?

?Hapana Lucy, kama nilivyokuambia, nahitaji kumchukua huyu mwanamke kwa ridhaa yake mwenyewe,? akasema Pam.

Lucy akabetua midomo yake. Akasema: ?Sawa. Najua vizuri sana. Kwa hiyo??

?Sitaki kumfanya mateka,? Pam akasema kwa sauti tulivu sana.

Ilikuwa sauti iliyoonyesha busara, hekima na uvumilivu. Ndani ya moyo wake hakuwa hivyo, Pam alikuwa mwanaume wa aina ya tofauti kabisa na mwonekano wake.

?Utafanyaje??

?Nashauri tuwarudishe chuo, nitachukua namba yake ya simu kutokea kwake mwenyewe, halafu sasa nitawasiliana naye mwenyewe. Sitaki ajisikie kuwa amekubali kwa kulazimishwa au kwa kisingizio cha pombe.

?Nahitaji ridhaa yake mwenyewe. Nataka yeye akubali bila shinikizo la mtu mwingine. Nimeshasema nina malengo naye!?

Lucy akacheka!

?Mbona unacheka?? Pam akauliza.

Lucy akacheka tena.

?Mbona sikuelewi? Kwa nini unanicheka??

?Wewe unaweza kuwa na malengo na mwanamke wewe? Haya...umeanza lini mwenzetu??

?Fahamu hivyo Lucy, naomba ukubaliane na mikakati yangu maana najua mwisho wake utakuwa mzuri.?

?Sawa, acha nikubaliane na wewe.?

Wakarudi kujumuika na wenzao!

***

Pombe ilikuwa imewakolea sawasawa. Saa 8:30 usiku, waliamua kuondoka klabu na kurudi hosteli. Lilian na Leila walikuwa hawajiwezi kabisa kwa ulevi.

Lucy na Lilian waliingia kwenye gari la Pam, Leila na Latifa, wakaingia kwenye gari la Big, safari ya kuelekea chuoni ikaanza. Mazungumzo njia nzima yalikuwa ya kilevi.

Lilian alikuwa amekaa siti ya mbele ya Pam. Muda wote huo, Pam hakuwa na haraka ya kumweleza hisia zake. Waliposhika Barabara ya Sam Nujoma kwenye mataa ya Mwenge, Pam akaanza kuchombeza...

?Lilian, wewe ni mwanamke mrembo sana. Mwanaume yeyote ambaye atapata nafasi ya kukumiliki atakuwa mwenye bahati sana!? akasema Pam.

?Mh! Kweli??

?Kabisa.?

?Ahsante.?

?Leila,? Pam akaita tena kisha akatulia.

?Abee...?

?Natamani sana uwe mtu wa karibu yangu, hata kama haitakuwa mambo ya mapenzi lakini nitajisikia fahari kukusaidia katika mambo yako. Wewe ni mwanamke mrembo, hutakiwi kuteseka hapa mjini wakati wanaume tunaojitambua wenye fedha zetu tupo,? akasema Pam.

?Ahsante, haina shida, kama si kwa ubaya ni sawa tu.?

Hapakuwa na magari usiku huo, dakika tano baadaye gari lilikuwa limeegesha jirani na jengo la hosteli ambalo wanaishi akina Lilian. Muda mfupi baadaye Big naye alisimamisha gari.

Kwanza alishuka Lucy, kisha akafuata Lilian lakini kabla hajafanya hivyo, Pam alichomoa burungutu na kumkabidhi!

Zilikuwa milioni mbili!

?Zitakusaidia hizi!? akasema Pam kwa sauti yenye ushawishi wa fedha.

?Ahsante,? Lilian akaitika akizichukua zile fedha.

Akashuka garini na kumbusu mashavuni Pam. Mwanaume wa watu alisisimka sana. Alihisi kama shoti ya umeme ikimtembelea. Wakaongozana hadi kwenye gari la Big.

Latifa alikuwa tayari ameshashuka, Leila aligoma. Alitaka kuondoka na Big. Wote wakashangaa. Ni muda mfupi tu wamekutana na kuzungumza.

Kutoka Masaki mpaka chuoni tayari walishakuwa wapenzi! Lilikuwa tukio jipya kwa Lilian. Bado aliendelea kuwaza kuhusu burungutu la pesa alizopewa na Pam! Big akaondoa gari Leila akiwa pembeni yake.

Range Rover ya Pam ikaunguruma, akaingiza gia namba moja, akakanyaga mafuta!

Ikapepea!
 
SEHEMU YA 16 KATI YA 50

GIZA nene lililokuwepo lilizimwa na mwanga wa taa zilizokuwa katika majengo mbalimbali chuoni hapo. Pembeni ya kituo cha daladala, kulikuwa na Hosteli za Hall 5 chuoni hapo, jengo hilo lilikuwa na taa nyingi zilizowaka kwa mwanga mkali.

Sinema ya Leila ni kama ilikuwa imekwisha. Leila aliondoka zake na Big, likiwa jambo jipya kabisa kwa Lilian aliyebaki anakodoa macho.

Sasa walibaki watatu; Lilian, Latifa na Lucy. Latifa ndiye aliyekuwa kwenye gari la Big pamoja na Leila. Yeye ndiye aliyekuwa na majibu ya maswali ya Lilian.

?Vipi tena mwenzetu?? Lilian akamwuliza Latifa.

?Mwenzangu hata mimi nashangaa.?

?Unashangaa nini??

?Mi? niliwaona wanazungumza muda wote, kuna wakati Leila alikuwa akimlalia sana Big, tulipofika hapa akakataa kushuka. Sasa huwezi kubishana na mtu mzima mwenye akili zake,? akasema.

Wote wakaungana naye.

?Kwa hiyo amekwenda kulala naye?? Lilian akauliza.

?Unauliza swali gani hilo la kitoto??

?Poa, tuondokeni,? akasema Lucy.

Lilian hakujua kuwa wenzake walikuwa wakimshangaa yeye kwa kuwa kila kilichofanyika, hapakuwa na jambo la ajabu. Yalikuwa mambo ya kawaida sana kwao.

Waliongozana hadi chumbani mwao, wakaingia na kufunga mlango. Hapo sasa ndipo Lucy alipomwuliza kuhusu bahasha aliyokuwa amebeba...

?Vipi?? Lucy akamwuliza huku akiangalia ile bahasha kwa uchu.

?Amenipa, amesema zitanisaidia lakini nina wasiwasi sana kwa kweli. Hawezi kuwa anatumia gia hiyo kunishawishi kimapenzi?? Lilian akamwuliza Lucy.

?Wasiwasi wako tu, hawa ndiyo watu wa mjini wenye fedha zao, jifunze kula na kipofu, acha ushamba bwana!?

?Mh! Haya bwana.?

Pamoja na kwamba mvinyo aliokunywa ulikuwa ukimpeleka puta, akili yake ilikuwa ikifanya kazi kama kawaida. Kuna taa nyekundu ziliwaka kichwani mwake juu ya Pam.

?Nitaona mwisho wake!? akawaza.

***

Mlio wa meseji ndiyo uliomshutua Lilian usingizini. Akaamka na kuichukua simu yake haraka. Akafungua ujumbe na kuusoma. Ulitoka kwa Pam.

?Nilifurahi sana kupata wakati mzuri na wewe jana. Vipi umeamka salama??

Ilikuwa saa 2:30 asubuhi!

?Mh! Mapema yote hii? Ina maana hana mke? Au labda ameshakwenda kazini. Lakini kwa nini anakuwa na spidi kiasi hiki?? akawaza kabla ya kumjibu:

?Nami pia. Ahsante kwa fedha kaka Pam.?

?Zile ni pesa ndogo sana kwa ajili ya kukusaidia, usiwe na wasiwasi kuwa huru kwangu. Nimekuambia nataka uishi kama malkia, sitaki uteseke!?

?Nashukuru kusikia hivyo Pam, ahsante sana.?

?Masomo mema.?

Lilian hakuwa na kipindi cha asubuhi ya siku hiyo, alitakiwa darasani saa 8:00 mchana, hivyo hakuwa na sababu ya kuamka haraka hasa ukizingatia kuwa alikuwa na uchovu wa pombe wa jana yake.

Akaendelea kulala!

Simu ilimwamsha tena Lilian. Ilikuwa imeshafika saa 5 za asubuhi. Akajinyoosha pale kitandani kisha akaamka. Chumba chote kilikuwa tupu.

Lucy na Latifa walishaondoka chumbani hapo tangu saa tatu. Walielekea Baa ya UDASA kupata supu
 
SEHEMU YA 17 KATI YA 50

kwa lengo la kupooza mning?inio. Hilo halikumshtua sana Lilian.

Alipochukua simu yake, alishangazwa na namba zilizoonekana kupitia kioo cha simu yake. Hazikuwa namba za kawaida. Zilionekana wazi kuwa za nje ya nchi.

Simu ilikatika akiwa bado anashangaa. Sekunde chache mbele, simu ikaanza tena kuita kwa mara nyingine. Mara moja Lilian akapokea...

?Haloo,? sauti ya Lilian ilitoka ikionyesha wazi mashaka aliyokuwa nayo.

?Haloo!? sauti ya upande wa pili ikasikika.

Hapakuhitaji akili nyingi kwa Lilian kugundua kuwa aliyekuwa akizungumza simuni alikuwa ni mpenzi wake Edo aliyepo Malaysia. Alishtuka sana lakini moyoni alifurahi.

?Waooo baby, vipi za huko? Mbona umenisusa mpenzi?? akasema Lilian akionekana kuwa na furaha sana.

?Tena uishie hapohapo. Nilikuambia nini? Nilisema nikiondoka utabadilika na kweli hata wiki mbili hazijaisha tayari. Nashukuru sana kwa ujumbe wako. Naomba nikuhakikishie kuwa nimepata ujumbe wako na nimekubaliana na wewe.

?Siwezi kulazimisha mapenzi mahali nisipopendwa. Najua umekutana na mwanaume mwenye fedha, lakini tambua kuwa, mapenzi ya kweli yapo moyoni na siyo mfukoni kama unavyofikiri. Nashukuru sana kwa kunipotezea muda wangu, lakini nakuahidi sitakutafuta tena.

?Endelea na maisha yako na huyo unayemuona ana maana kwako. Ni vile tu hujajua. Ni vile hujafahamu maumivu ya mapenzi, lakini nataka kukuambia kuwa, moyoni mwangu nina maumivu makali sana. Moyo wangu unavuja damu,? akasema Edo kwa sauti iliyoonyesha kujawa na maumivu makali moyoni.

?Mbona sikuelewi Edo mpenzi wangu? Ujumbe wangu upi ambao nimekutumia? Sijakutumia ujumbe wowote mbaya!?

?Acha ujinga wewe, email zako zote nimesoma.?

?Email? Nimekutumia email ya namna gani hadi unaniambia maneno makali ya namna hiyo mpenzi wangu??

?Nimemaliza na sitaki maswali wala mawasiliano na wewe tena. Acha nisome. Kwa heri,? akasema Edo kisha akakata simu.

Lilian akachanganyikiwa! Akajiuliza sana kuhusu email anayosema Edo lakini hakukumbuka kitu. Alihisi kuchanganyikiwa. Alipojaribu kumpigia tena Edo, hakupokea.

Alirudia mara nyingi, bado hakupokea. Alishinda akilia mpaka muda wa kwenda darasani ulipofika. Alikaa kwenye kiti chake, macho yake yakiangalia mbele alipokuwa mhadhiri akifundisha, lakini hakuelewa chochote!

Mhadhiri aliyekuwa mbele yake, alikuwa kama kopo. Hakuelewa chochote. Kichwa kilimuuma mno. Mawazo yake yalikuwa kwa Edo tu. Hakuwa tayari kumpoteza mwanaume wa maisha yake!

Alijaribu kufikiri labda huenda kuna mtu amevujisha kuwa ameanza kutoka usiku na alirudishwa na mwanaume, lakini jambo hilo halikumwingia akilini mwake maana ilikuwa ndiyo mara ya kwanza, tena siku ya kwanza tu!

Aliwaza zaidi kuhusu email. Hilo ndilo lililomkosesha raha!

?Kuna kitu kimejificha hapa, nitakijua tu!? akajipa moyo.





Wingu zito lilitanda kichwani mwa Lilian. Alishindwa kuelewa hiyo email anayolalamikia mpenzi wake Edo ni ipi. Kichwa kilivurugika! Alitakiwa kutumia akili mpaka zile za akiba ili kujua kilichokuwa kikiendelea.

Mhadhiri aliendelea kufundisha mbele ya darasa lakini kichwa kilikuwa kizito sana
 
SEHEMU YA 18 KATI YA 50

. Hakuna kitu alichokuwa akikiingiza kutoka kwake.

Hakuona sababu ya kuendelea kuchanganyikiwa. Alikusanya vitu vyake, akasimama akiwa ameukunja uso wake, akatembea moja kwa moja mpaka mbele ya darasa.

Akanyoosha moja kwa moja kuelekea mlangoni. Hakutaka kuzungumza na Mhadhiri aliyekuwa mbele. Darasa zima likamshangaa. Si kwa sababu alitoka nje ya darasa bali namna alivyoonekana mwenye mawazo na uso uliokunjamana!

Alishuka kwenye ngazi fupi zilizokuwa mlangoni, kisha akanyoosha moja kwa moja hadi kwenye Jengo la Utawala. Hapo aliangalia kidogo ubao wa matangazo na kuondoka zake.

Alianza kutembea akielekea chumbani kwao. Alikuwa amechoka sana. Si kwa sababu ya pombe aliyokunywa jana yake, bali majibu ya Edo.

Wakati anatembea akielekea chumbani kwake, alijaribu kumpigia tena Edo mara kwa mara lakini hakupokea simu yake. Alihisi dunia yote imemgeuka.

Moyoni alikuwa na maumivu makali sana. Alivyoamua kuachana na simu ya Edo, simu nyingine iliingia. Alipoangalia kwenye kioo cha simu yake akakutana na jina la Pam.

?Mh! Ananipigia tena sasa,? akasema kwa sauti Lilian.

Hakupokea!

?Anataka nini huyu mbaba?? akajiuliza tena.

Lakini alihisi labda alikuwa na jambo muhimu la kumwambia, akaamua kupokea...

?Haloo...? ilikuwa sauti ya Pam kutoka upande wa pili.

?Haloo kaka Pam.?

?Najua uko chuo, vipi mambo yako??

?Salama.?

?Nahitaji kukutoa kwa chakula cha jioni leo.?

?Mh! Wapi??

?Siyo mbali, ni karibu na chuoni. Hapo Mlimani City, Samaki Samaki.?

?Peke yangu??

?Peke yetu.?

?Unamaanisha??
 
Back
Top Bottom