BEFORE I DIE
SEHEMU YA 61
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Latoya unafahamu kabisa kwamba wanaume siku hizi ni waongo na hawaaminiki na ndiyo maana siku zote nimekuwa makini sana kuhusu watu hawa kwani sitaki kukuona ukiingia katika orodha ya watu walioumizwa na wanaume .Latoya wewe ni kiumbe mwenye roho nzuri sana na hupaswi kwa namna yoyote ile kuumizwa na mtu yoyote ile” akasema Elizabeth .Latoya akatabasamu na kusema
“ Elizabeth ,tutaongea zaidi jioni .Kuna mambo meng sana ambayo nataka tuyaongee,lakini kwa sasa nawahi hospitali” akasema Latoya huku akiinuka .Elizabeth naye akainuka na kuongozana na Latoya kuelekea katika sehemu liliko gari la kifahari la Latoya.
“ Elizabeth ,jambo lingine ambalo nataka ulifanyie kazi ni kwamba kuanzia sasa sitaki kuongozana na msafara wa walinzi.Nitakuwa nikitembea na dereva na mlinzi mmoja tu kama ikihitajika.Nataka kuanza kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine” akasema Latoya
Gari lake la kifahari sana lilikuwa limezingirwa na walinzi sita waliokuwa katika suti nyeusi.Latoya akasalimiana nao .Elizabeth akawaambia kwamba hawatalazimika tena kuambatana na Latoya kila aendako labda kwa sababu maalum tu.Mlango wa gari ukafunguliwa na mlinzi na Latoya akangia,gari ikaondoka akaeleka hospitali
ENDELEA………………………….
Baada ya Latoya kuondoka kuelekea hospitali,Elizabeth akapanda ghorofani hadi chumbani kwa Innocent akagonga mlango na Innocent akaufungua
“ Hallo Innocent,umeamkaje? Habari za toka jana? Akauliza Elizabeth huku akitabasamu
“ Nimeamka salama Elizabeth.Vipi wewe unaendeleaje? Habari za toka jana?
“ habari ni nzuri Innocent.Unaionaje hali ya Miami?
“ Uuhm ! Nimeipenda ni nzuri sana.Unajua hii si mara yangu ya kwanza kuja Marekani.Nimehitimu shahada yangu ya kwanza ya uchumi na fedha katika chuo kikuu cha Columbia New York kwa hiyo ninafahamu Marekani japo si kwa ukubwa wake.” Akasema Innocent
“ Ouh ! Sikujua kama umewahi kuishi na kusoma hapa.Kwa nini uliamua kurudi nyumbani Tanzania badala ya kubaki hapa na kutafuta kazi yenye maslahi manono kulingana na taaluma yako?
‘ Nilirejea nyumbani kwa sababu familia yangu walikuwa wakinihitaji.Nilitakiwa kuisimamia miradi ya familia.Pamoja na hayo nadhani ni mipango wa Mungu nirejee nyumbani kwani nisingefanya hivyo nisingekutana na Latoya na wala mimi na wewe tusingefahamiana.” Akasema Innocent na wote wakacheka
“ Innocent ,Latoya amekwenda hospitali.Sio mbali sana na hapa.Ni hospital aliyoijenga yeye mwenyewe kwa ajli yakuwahudumia watu wenye matatizo ya saratani.Ni moja kati ya hopsitali kubwa na iliyosheheni madaktari bingwa wa saratani.Naweza kusema kwamba ni moja kati ya hospitali tegemeo hapa marekani kwa kutibu Saratani.Kwa kuwa anaweza akachukua muda mrefu kidogo kule hospitali,ni jukumu langu kuhakikisha kwamba hauboreki kwa hiyo nitakuchukua na tutazunguka sehemu mbalimbali .” akasema Elizabeth
“ Hakuna shaka Elizabeth,nitafurahi sana kama ukifanya hivyo” akajibu Innocent
“ Ok Innocent wakati unaendelea kujiandaa ,ninakwenda mara moja chumbani kwa Latoya kuna kazi aliniachia ya kufanya chumbani kwake” akasema Elizabeth
“ Chumbani kwa Latoya? Innocent akashangaa
“ Kuna mtu anaruhusiwa kuingia chumbani kwa Latoya? Akauliza
“Ndiyo.Chumba cha Latoya ni ruksa kwa kila mtumishi kuingia wakati hayupo lakini wakati akiwa hapa huwa hapendi mtu yeyote aingie chumbani kwake.Kwani vipi Innocent mbona umeshangaa sana?
“ Its nothing.Utanipitia ukitoka huko” akasema Innocent .Elizabeth akamtazama na kutaka kusema kitu lakini akaghairi na kuondoka kuelekea chumbani kwa Latoya.
Kule Dares salaam hakuna mtu aliyewahi kukona chumba cha Latoya lakini hapa mtumishi yeyote anaruhusiwa kuingia katika chumba chake.Mhh ! filamu ya maisha ya Latoya bado inaendelea” akawaza Innocent
“ Innocent ni kijana mcheshi sana na amemfanya Latoya awe na furaha ya aina yake.Ingawa bado Latoya hajaniweka wazi kuhusiana na urafiki wao lakini ninaziona kila dalili za penzi zito kati yao” akawaza Elizabeth huku akikinyoga kitasa cha mlango wa chumba cha Latoya na kuingia ndani.Kitu cha kwanza alichokutana nacho ni harufu nzuri sana ya uturi ambayo hakuwahi kuisikia
“ wow ! sijawahi kuisikia harufu nzuri kama hii.” Akawaza Elizabeth na kutembea kwa haraka kuelekea katika meza ya vipodozi iliyokuwa imesheheni vipodozi vya kila namna na kuanza kuangalia chupa moja baada ya nyingine akitafuta chupa yenye harufu ile nzuri.Alizingalia chupa zote zilizokuwapo pale mezani lakini hakuipata chupa ile aliyokuwa akiitafuta.Akasimama mbele ya meza ile akajishika kiuno.
“ Nitamuuliza Latoya hii ni perfume gani yenye harufu nzuri na ya kuvutia namna hii.” Akawaza Elizabeth na kugeuka kwa dhumuni la kuelekea katika ile meza aliyoambiwa aitoe.Mara tu apogeuka nusura roho imtoke kwa kitu alichokiona.Mwili ulimtetemeka na nguvu zikamuishia .Aliuona mwisho wake .Alikuwa akitazamana na joka kubwa ambalo hajawahi kuliona katika maisha yake hata katika filamu.Lilikuwa ni joka kubwa jeusi lenye kichwa kikubwa zaidi ya kile cha binadamu.Eneo lile lilipokuwapo lile joka hakukuwa tena na ile meza ya mawe ambayo Latoya alitaka iondolewe bali joka lile kubwa.Kutokana na mstuko ule mkubwa alioupata,haja ndogo ikamtoka bila kujifahamu.Hizi zilikuwa ni sekunde chache lakini ngumu sana kuwahi kumtokea katika maisha yake sekunde ambazo alikuwa anatazama na joka lile la ajabu na la kutisha.
“Ee mungu wangu niokoe” akaomba Elizabeth na ghafla akahisi kama miguu yake inapata nguvu tena .Akajaribu kuuinua mguu wa kulia ukainuka na kitu cha kwanza alichokiona ni mlango uliokuwa wazi.kwa nguvu zake zote akatoka mbio kama mshale.Breki ya kwanza ilikuwa ni katika mlango wa chumba cha Innocent.Akauvamia kwa nguvu ukafunguka,akajitupa ndani.Innocent aliyekuwa anavaa akastuka baada ya kumuona Elizabeth ameingia mle chumbani na kuanguka chini
“ Elizabeth !! Innocent akashangaa na kumkimbilia pale chini
“ Elizabeth !! Elizabeth !! akaita Innocent kwa wasi wasi lakini Elizabeth hakuweza kuongea lolote alikuwa anaweweseka.Macho yalikuwa yamemtoka pima.Innocent akaogopa
“ Elizabeth nini imetokea? Akauliza tena lakini bado Elizabeth aliendelea kuweweseka .Innocent akahisi kuchanganyikiwa ,hakujua ni kitu gani kilichompata .Haraka haraka akachukua chupa ya maji ya kunywa akamnywesha halafu akamketisha sofani
Elizabeth akavuta pumzi ndefu .
“ Pole sana Elizabeth.” akasema Innocent.Bado Eliza aliendelea kutiririkwa na jasho jingi.Baada ya kama dakika kumi hivi Elizabeth akaanza kujisikia vizuri ingawa machozi hayakumkauka
“ Elizabeth nieleze nini kmekutokea? Unaumwa? Akauliza Inno
“ Innocent lets get out of here now.Hii ni sehemu hatari sana” akasema Elizabeth huku akitetemeka
“ Sikuelewi Elizabeth unamaanisha nini?
“ Innocent twende tuondoke haraka sana.Hii si sehemu salama hata kidogo” akasisitiza Elizabeth huku akiung’ang’ania mkono wa Innocent
“Hebu nieleze Elizabeth kimetokea nini?
Elizabeth akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Nimeona joka kubwa sana chumbani kwa Latoya.Sijawahi kuliona joka la namna ile toka kuzaliwa kwangu na hata katika filamu.Ni kitu cha kutisha sana” akasema Elizabeth na kuanza kulia tena
“Usilie Elizabeth tafadhali nyamaza kulia” Inno akambembeleza
“ Innocent ninaogopa mno.Ilibaki kidogo nipoteze maisha yangu.Innocent naomba uniondoe hapa” akasema Elizabeth
“ Hukuumia sehemu yoyote?
“ Hapana Inno .Nilipata nguvu nikawahi kukimbia.Innocent tafadhali naomba uniondoe hapa.” Elizabeth akazidi kulia
“Huyo nyoka uliyemuona alielekea wapi?
“Sifahamu.Niliwahi kukimbia.Nadhani bado yuko ndani ya chumba cha Latoya” akasema Elizabeth.Innocent akachukua kitambaa na kumfuta machozi
“ Kaa humu humu chumbani usitoke.Nakwenda kumuangalia huyo nyoka ili kama yupo tuwasiliane na vyombo vinavyohusika wafanye utaratibu wa kumuondoa” akasema Innocent
“Hapana huwezi kwenda huko.Ni joka kubwa mno halafu siwezi kuniacha humu ndani peke yangu.naogopa sana” akasema Elizabeth huku akimvuta mkono Innocent
“ Usiogope Elizabeth,hii ni sehemu salama hakuna lolote litakalokutokea Narudi sasa hivi “ akasema Innocent lakini Elizabeth hakuwa tayari kubaki peke yake
“ Tunakwenda sote.Sikubali kubaki peke yangu humu ndani” akasema Elizabeth huku akiinuka.Innocent akaamuangalia usoni halafu akamshika mkono akaufungua mlango wakatoka mle chumbani na kuelekea chumbani kwa Latoya.Elizabeth alikuwa bado anatetemeka.Walikwenda hadi katika mlango wa chumba cha Latoya ambao bado ulikuwa wazi.Innocent naye alikuwa anaogopa japokuwa hakutaka kuonyesha mbele ya Elizabeth.Inno akamfanyia ishara Elizabeth abaki pale mlangoni na yeye akaingia ndani huku akinyata.Aliangaza pande zote lakini hakuona dalili zozote za kuwepo kwa nyoka.Alifungua makabati yote hadi bafuni na chooni lakini hakukuwa na dalili zozote za hilo joka alilolisema Elizabeth.Alipohakikisha kwamba hakukuwa na nyoka yoyote mle chumbani akamfuata Elizabeth pale mlangoni aliyekuwa amesimama kwa woga huku akitetemeka
“ Umemuona” akauliza Elizabeth
“ Elizabeth hakuna dalili zozote za kuwepo nyoka humu chumbani” akasema Innocent.Elizabeth akastuka sana
“ No ! Innocent that cant be.I saw that snake.a huge snake”
“ Usihofu Elizabeth yawezekana amekimbia”
‘ Hapana Innocent.Haweze kutoroka.Ni mkubwa sana.Amepita wapi? Lazima atakuwa amejificha mahala humu chumbani.Angalia vizuri Innocent.Nina wasi wsi sana na maisha ya Latoya yako hatarini” akasema Elizabeth
“ Elizabeth nimetazama kote chooni bafuni na katika vyumba vyote vya karibu hakuna dalili zozote za kuwepo kwa huyo nyoka.”
“ Innocent believe me I saw a snake.Dont you believe me? Akasema Elizabeth huku akilia
“ I believe you Elizabeth” akasema Inno
“ If you do believe me then lets search the whole house till we find that damn snake” akasema Elizabeth.Innocent akamtazama usoni na kusema
“ Elizabeth nyoka uliyemuona ameondoka.”
Elizabeth akamuangalia Innocent kwa mshangao lakini kabla hajasema chochote Innocent akasema
“ Twende tuondoke hapa ndani”
“No Innocent.We need to find that snake” akasema Elizabeth na kuingia mwenyewe chumbani kwa Latoya.Macho yake yakatua katika meza ile ya mawe ambayo Latoya alitaka iondolewe ambayo dakika chache mahala pale aliliona joka kubwa.Akashangaa sana kwa maajabu yale
“Alikuwa katika meza hii ya mawe.Latoya aliniambia kwamba meza hii ibomolewe leo kabla hajarudi toka hospitali na nilikuja ili kuiangalia kabla ya kumleta fundi wa kuibomoa.Kitu cha ajabu ni kwamba baada tu ya kuingia humu ndani sikuiona meza bali hilo joka kubwa la kutisha.” Akasema Elizabeth huku akiendelea kulia machozi
“ Usiogope Elizabeth nitaibomoa hii meza” akasema Innocent
“ Hapana Innovent.Usiiguse hiyo meza.Nitawasiliana na walinzi ili waje waivunje.” Akasema Elizabeth halafu akachukua simu yake na kupiga akawaomba walinzi wawili chumba ni kwa Latoya .Wakati wakiwasubiri walinzi wale wafike.Innocent akaendelea kukishangaa chumba cha Latoya namna kilivyo kizuri
“ Latoya anachumba kizuri sana.Sielewei ni kwani ni kule dare s salaam hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia chumbani kwake au hata anayefahamu jinsi chumba chake kilivyo.Ninahisi Latoya hakutaka watu waingie chumbani kwake kuogopa kutokewa na mambo ya ajabu ajabu kama haya yaliyomtokea Eliuzabeth.” Akawaza Innocent na mara vijana wawili wakaingia mle chumbani wakaelekezwa kazi ya kufanya wakaianza kazi ile mara moja.
Hawakutoka mle chumbani hadi walipohakikisha kwamba madhabahu ile imeondolewa kabisa kisha wakatoka ndani ya chumba kile na kuelekea chumbani kwa Innocent
“Innocent miguu yangu yote haina nguvu hata kidogo.Sina hakika kama nitaweza kufanya kazi yoyote leo.Pengine nahitaji mapumziko kwa siku ya leo.Nilichokiona kimenistua mno na kitabaki katika kumbu kumbu zangu kwa miaka mingi sana.Nahitaji kuituliza akili yangu lakini kabla ya yote lazima nimtaarifu Latoya kuhusiana na jambo hili.Lazima nimuonye ili afanye uchunguzi juu ya joka lile na wapi limetokea.Inawezekana likawa limetoka katika msitu wa karibu” “ akasema Elizabeth
“Hapana usifanye hivyo Elizabeth.Usimwambie Latoya kuhusiana na ulichokiona chumbani kwake” Elizabeth akaonyesha mshangao wa dhahiri kwa kauli ile ya Innocent
“Innocent Kwa nini nisimuonye Latoya kuhusiana na joka lile hatari nililoliona chumbani kwake? Maisha yake yako katika hatari kubwa kama nisipomuonya mapema kuhusiana na joka lile.Lazima litafutwe na lipatikane” akasema Elizabeth
“ Elizabeth ,Latoya anakabiliwa na mambo mengi hivi sasa kwa hiyo sidhani kama kumweleza kuhusiana na joka hilo ni jambo la busara kwa wakati huu.Zaidi ya yote Latoya huwa hapendi mambo yanayohusiana na maisha yake yajulikane na ndiyo maana hata kule katika nyumba yake ya Dare s salaam hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kuingia chumbani kwake na wala hakuna anayefahamu chumba cha Latoya kikoje.Kwa hiyo naonba kila ulichokiona mle chumbani kibaki kuwa ni siri yako na usimweleze mtu mwingine yeyote”
“Innocent mbona sikuelewi unamaanisha nini? Akauliza Elizabeth
“ Kama nilivyokwambia kwamba yote uliyoyaona chumbani kwa Latoya usimweleze mtu yeyote hata Latoya mwenyewe” akasema Inno
“ Innocent naomba maelezo ya kina ni kwa nini nisimweleze Latoya kuhusiana na joka lile kubwa ambalo linayafanya maisha yake yawe hatarini?
“Hapana Elizabeth hutakiwi kufanya hivyo”
“kwa nini Innocent? Kama hutaweza kuniambia sababu lazima nitamwambia Latoya.Siwezi kukubali kuyaona maisha ya mtu wangu wa karibu yako hatarini.” akasisitiza Elizabeth
“Latoya anafahamu kila kitu” akasema Innocent .Elizabeth akamtazama kwa mshangao mkubwa
“Unamaanisha nini….??!!!!..oh gosh …!!! Latoya anajua kama kuna joka kubwa chumbani kwake?” akauliza Elizabeth huku akimuangalia Innocent kwa macho makali.Innocent akatikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na kile alichokiuliza
“ Ouh my gosh ! Siamini.Latoya anafahamu kuhusiana na joka lile na asinieleze kitu chochote? Kwa nini basi alinituma chumbani kwake wakati akifahamu kuna vitu vya kutisha kama lile joka? Alitaka niuliwe?
“Hapana Elizabeth.Si hivyo unavyofikiria” akasema Innocent
“Kama si hivyo nini maana ya kunituma chumbani kwake wakati akifahamu kwamba kuna joka kubwa la kutisha na la hatari? Kwa nini hakunipa tahadhari bado mapema? Hapana lazima anieleze ukweli kuhusiana na suala hli” akasema Elizabeth huku akitembea kwa kasi akitaka kutoka mle chumbani Innocent akamuwahi na kumshika mkono.
“Sikiliza Elizabeth.Kuna jambo ambalo unatakiwa ulifahamu”
“ Jambo gani Innocent? Akauliza Elizabeth
“twende bustanini” akasema Innocent halafu wakaongozana hadi bustanini wakaketi juu ya kiti cha kupumzikia
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 62
ILI[POISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Latoya anafahamu kila kitu” akasema Innocent .Elizabeth akamtazama kwa mshangao mkubwa
“Unamaanisha nini….??!!!!..oh gosh …!!! Latoya anajua kama kuna joka kubwa chumbani kwake?” akauliza Elizabeth huku akimuangalia Innocent kwa macho makali.Innocent akatikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na kile alichokiuliza
“ Ouh my gosh ! Siamini.Latoya anafahamu kuhusiana na joka lile na asinieleze kitu chochote? Kwa nini basi alinituma chumbani kwake wakati akifahamu kuna vitu vya kutisha kama lile joka? Alitaka niuliwe?
“Hapana Elizabeth.Si hivyo unavyofikiria” akasema Innocent
“Kama si hivyo nini maana ya kunituma chumbani kwake wakati akifahamu kwamba kuna joka kubwa la kutisha na la hatari? Kwa nini hakunipa tahadhari bado mapema? Hapana lazima anieleze ukweli kuhusiana na suala hli” akasema Elizabeth huku akitembea kwa kasi akitaka kutoka mle chumbani Innocent akamuwahi na kumshika mkono.
“Sikiliza Elizabeth.Kuna jambo ambalo unatakiwa ulifahamu”
“ Jambo gani Innocent? Akauliza Elizabeth
“twende bustanini” akasema Innocent halafu wakaongozana hadi bustanini wakaketi juu ya kiti cha kupumzikia
ENDELEA……………………….
“Haya niambie Innocent ulichotaka kuniambia” akasema Elizabeth.Innocent akakohoa kidogo na kusema
“Elizabeth Latoya ni rafiki yako wa tangu utotoni lakini bado hujamfahamu vizuri na wala hajawahi kukueleza chochote kuhusiana na yeye.”
“Hapana Innocent si kweli.Ninamfahamu Latoya vizuri sana kuliko mtu yeyote yule.” akasema Eliza
“nakubaliana nawe Elizabeth ,lakini si kila kitu unachokifahamu kwake.Kuna mambo mengine yanayomuhusu yeye peke yake na ambayo ni watu wachache sana wanaoyafahamu.” Akasema Inno
“ Ni mambo gani hayo Innocent.Unayafahamu?
“Ndiyo.Ninamfahamu Latoya japo si kiundani sana kama unavyomfahamu wewe” akasema Inno halafu akaanza kumweleza Elizabeth namna anavyomfahamu Latoya.Hakumficha kitu alimweleza kila kitu hadi alivyofanikisha kumuokoa toka kifo.Mpaka anamaliza simulizi ile Elizabeth alikuwa anatetemeka mwili mzima.Aliogopa kupita kiasi.Machozi mengi yalikuwa yanamtoka
“Kwa hiyo hayo ndiyo maisha ya Latoya ambayo hakuna aliyekuwa anayafahamu na hakutaka mtu yeyote ayafahamu.Nimekwambia haya yote kwa sababu sisi ndio watu wa karibu sana naye na ndio wenye jukumu kubwa la kuhakikisha kwamba maisha ya Latoya yanabadilika na kuwa ya kawaida.Ameaniahidi baada ya kutoka hospitali leo tutakuwa na maongezi marefu pengine kuna jambo anataka kunieleza kuhusiana na kilichotokea.Tafadhali naomba usimwambie kitu chochote kuhusiana na haya niliyokueleza hadi atakapokueleza yeye mwenyewe”
“Innocent nimeogopa sana.Mwili wote unanitetemeka.Sikuwahi kuota kama simu moja Latoya anaweza kuwa namna hii.Japokuwa niliwahi kusikia tetesi kama hizo kuhusiana na utajiri wake lakini nilizipuuza.Ni vigumu sana kuamini.Innocent siku yangu imeharibika.Nahitaji mapumziko na kutuliza akili yangu” akasema Elizabeth halafu akaaga na kuondoka zake
* * * *
Takribani masaa matano yamekwisha katika toka Latoya aanze kufanyiwa uchunguzi wa afya yake na jopo la madaktari bingwa.Vipimo vilionyesha hakuwa anasumbuliwa na tatizo lolote mwilini.Mifumo yote ilikuwa inafanya kazi vizuri.Kilichowaumiza vichwa madaktari ni kidonda kikubwa kilichokuwa mgongoni mwake.Vipimo vilirudiwa zaidi ya mara tatu ili kujiridhisha kwamba haikuwa ni saratani .
Hatimaye baada ya kazi ngumu iliyowachukua zaidi ya saa nane wakakamilisha kazi yao na Latoya akapelekwa katika chumba maalum cha kupumzika.Uso wake ulionyesha wasi wasi mkubwa.Hakujua angepewa majibu gani kuhusiana na afya yake kwani aliwaona namna madaktari wale walivyokuwa wakihangaika na hivyo kumpa mashaka kwamba kuna kitu hakikuwa sawa
Baada ya saa moja na dakika kama ishirini hivi,mlango ukafunguliwa na daktari mmoja kijana akaingia
“ Madam Latoya unajisikiaje? Akauliza yule daktari huku uso wake ukiwa na tabasamu
“ Najisikia vizuri sana” akasema Latoya
“madam Latoya Madaktari wako tayari na wanahitaji kukuona” akasema Dr Edwin halafu akaongozana na Latoya hadi katika chumba walichokuwamo madaktari wale bingwa waliomfanyia uchunguzi ule wa afya yake.Mara tu Latoya alipoingia mle chumbani wakasimama wote ishara ya kumpa heshima msichana huyu ambaye alikuwa mdogo sana kiumri kwao
“Poleni sana kwa kazi ngumu ya kutwa nzima ya leo” akaanzisha mazungumzo Latoya
“ Tunashukuru sana Madam.Pole sana nawe” wakasema kwa pamoja
“Madam Latoya tumekuita hapa ili tukupe matokeo ya uchunguzi wetu” akasema Dr Bill mkuu wa jopo lile la madaktari
“Mifumo yote ya mwili inaonyesha kufanya kazi vizuri kabisa.Hakuna mahala tulikogundua tatizo lolote katika upande huu wa ufanyaji kazi wa mifumo ya mwili.” Akasema Dr Bill huku akiendela kulisoma faili lililokuwa mbele yake.
“Pamoja na mifumo yote kuwa sawa lakini tumegundua tatizo kubwa katika kidonda kilichopo mgongoni.Kwa kweli hali yake si nzuri na kimetushangaza hata sisi pia.Tulidhani labda yaweza kuwa ni saratani lakini tumefanya uchunguzi na kugundua kwamba si saratani.Uchunguzi unaonyesha kwamba kidonda hiki kimetokana na virusi waitwao Sethypothes ambao wamekuwa wakiharibu tabaka la juu la ngozi na hivyo kusababisha kidonda hiki kuzidi kukua siku hadi siku.Virusi hawa huzaliana kwa wingi sana na huzalisha sumu iitwayo Altroutraczema ambayo huingia katika mfumo wa damu na kuangamiza chembe nyekundu za damu na kukusababishia upungufu mkubwa wa damu.Madam Latoya naomba nikiri kwamba ugonjwa huu ni hatari sana kwa afya yako na tunaendelea kufanya utafiti ili tuone kama unaweza kuambukiza watu wengine.Si nia yangu kukuogopesha lakini hatua iliyofikia hivi sasa ni mbaya na tunafanya kila tuwezalo kuweza kuupatia ufumbuzi ugonjwa huu.Kitu kingine kikubwa ambacho kinatuumiza sana vichwa vyetu ni kwamba mpaka hivi sasa hatujaweza kupata dawa ya kuwaangamiza virusi hawa.Virusi wa aina hii wana gamba gumu ambalo huweza kuwakinga dhidi ya sumu ya aina yoyote ile na hivyo kuwafanya wawe ni miongoni mwa virusi wasiotibika.Tumepeleka sampuli katika chuo kikuu cha Havard kwa uchunguzi zaidi. Tutashirikiana nao katika uchunguzi huu ili tuweze kupata dawa itakayoweza kuwaangamiza virusi hawa.” Akasema Dr Bill
“ Ouh Gosh ! Hili sasa ni balaa jingine.Nitafanya nini mimi? Akawaza Latoya na kuinama chini.Wote mle chumbani wakakaa kimya.Walimuonea huruma sana binti yule mdogo mwenye ugonjwa ule wa ajabu na wa kushangaza.Latoya akainua kichwa na kufuta machozi kisha akasema
“ Dr Bill naomba unifafanulie zaidi kuhusiana na ugonjwa huu.Kutokana na maelezo yako umesema kwamba virusi hawa wanazaliana kwa wingi sana je kuna uwezekano wa kidonda hiki kukua na kusambaa sehemu nyingine za mwili? Na je kama haitapatikana dawa ina maana nitakufa? Akauliza Latoya huku macho yake yakiwa yamejaa machozi.Dr Bill akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Madam Latoya,kuna uwezekano mkubwa sana kidonda hiki kikasambaa katika sehemu kubwa ya mwili kutokana na kukua kwa kasi kwa virusi hawa na kuendelea kushambulia sehemu ya juu ya ngozi.Hata hivyo tunaendelea kuwafanyia uchunguzi ili tujue ni sehemu zipi hasa za mwili ambazo wanazipenda “
“ Dr Bill hujajibu swali langu la pili,kama hakutapatikana dawa yoyote ,ina maana ninakwenda kufa?
“Madam Latoya ,tunajitahidi kufanya kila tunaloweza ili tuweze kupata dawa ya kuwadhibiti virusi hawa hatari.Lakini endapo itashindikana kupata dawa mapema nasikitika madam hakutakuwa na njia nyingine zaidi ya kupoteza maisha kwani kadiri virusi hawa wanavyoendelea kuzaliwa kwa wingi na ndivyo wanavyozalisha sumu kwa wingi na damu kuendelea kukauka kwa haraka.Katika uchunguzi tunaoendelea kuufanya tunataka kubaini kama sumu hiyo pia inaweza kuleta madhara mengine mwilini.Usiogope madam Latoya mimi na jopo la madaktari tukishirikiana na vyuo vikuu vya sayansi hapa Marekani tunakuahidi kufanya kila linalowezekana ili kulipatia ufumbuzi wa haraka jambo hili.Wakati uchunguzi wetu ukiendelea tutaendelea kukupatia tiba ikiwa ni pamoja na kukuongezea damu mara kwa mara.” Akasema Dr Bill.Hii ilikuwa ni taarifa mbaya sana kwa Latoya.Aliumia sana.Akainama akazama katika mawazo halafu akainua kichwa na kusema
“ Dr Bill naomba uniambie ni lini nitakufa? Ni muda gani toka sasa? Akauliza Latoya kwa hali ya kukata tamaa.
“ Madam Latoya,nakuomba usifikirie suala la kufa kwa sasa.Hilo linaweza kuokea lakini ni baada ya jitihada zote za kuwadhibiti virusi hawa kushindikana.Sisi kwa upande wetu kama madaktari ,tukishirikiana na wanasayansi tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba unapona.Kwa hiyo nakuomba madam Latoya ufute kabisa kichwani kwako mawazo ya lini utakufa” akasema Dr Bill
“ Ninaweza kumuambukiza mtu mwingine? Akauliza Latoya
“Kama nilivyokwambia awali ni kwamba kwa sasa bado hatuna uhakika kama virusi hawa wanaweza kusambaa na kwenda kwa mtu mwingine.Tutalibaini hilo katika uchunguzi wetu tunaoendelea kuufanya na endapo tutagundua kwamba virusi hawa wanaweza kusambaa kwa njia yoyote ile basi tutakutaarifu mara moja.Kwa hiyo mpaka tutakapokuwa na uhakika kwamba virusi hawa wanaweza kusambaa,unaweza ukaendelea kuchangamana na watu wako kama kawaida lakini kwa ushauri tu unaweza ukapunguza idadi ya watu unaoonana nao kwa sasa” akasema Dr Bill
“ Ahsante sana Dr Bill kwa niaba ya wote.Pamoja na hayo kuna jambo nataka kuwaomba”
“ Omba lolote madam Latoya.Tuko hapa kwa ajili yako”
“ najua jambo hili linaweza kuwa kubwa na taarifa zikasambaa dunia nzima .Nawaombeni sana jambo hili libaki kuwa ni siri yetu mimi na ninyi mlio ndani ya chumba hiki.Sitaki jambo hili lijulikane kwa sasa .Mko tayari kunisaidia kwa hilo?
“ Madam Latoya kwa sasa jambo hili litabaki kuwa miongoni mwetu lakini siwezi kukuhakikishia kwamba itaendelea kuwa hivyo siku zote.Usiri wa jambo hili utategemea sana majibu ya uchunguzi tunaoendelea kuufanya tukishirikiana na vyuo vikuu vya sayansi ya tiba.Endapo itathibitika kwamba ugonjwa huu unaambukiza basi hatutakuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuliweka wazi suala hili ikiwa ni pamoja na kuwafanyia uchunguzi watu wako wote wa karibu ili kubaini kama wameambukizwa.”
Baada ya maongezi marefu na ushauri toka kwa jopo lile la madaktari bingwa Latoya akapewa dawa mbali mbali za kumsaidia wakati uchunguzi wa kubaini dawa itakayoweza kuwaangamiza virusi wale ukiendelea
“Haya tena ni mambo mapya kabisa.Nilidhani nimekwepa kifo lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Hawataniacha kamwe .Wataendelea kuniandama hadi wahakikishe nimekufa.Nimechanganyikiwa sijui nifanye nini” akawaza Latoya.Machozi yakamtoka akachukua kitambaa na kujifuta
“ madam are you ok? Akauliza dereva wake wakati wakirejea nyumbani
“ I’m fine “ akajibu Latoya na kuinama.Ile ndoto aliyoota usiku ikamjia tena kichwani ,akayakumbuka maneno ya yule mzee
“ haya yote umeyataka mwenyewe Latoya.Yasingekukukuta haya kama ungefuata maagizo uliyopewa.Ulikwenda nje ya makubalinao na ukaenenda katika njia uliyoitaka wewe .Usidhani umeshinda ,tutakuandama usiku na mchana.Wewe ni wetu na hautaweza kutukimbia kamwe” maneno yale yakajirudia tena kichwani kwake na kumfanya atokwe na machozi
“ tumekwisha kupiga muhuri wetu mgongoni kwako kwa hiyo kaa ukijua kwamba maumivu haya unayoyasikia sasa yataendelea daima na yatakuwa yakizidi kuwa makali lakini kuna jambo moja tu ambalo unaweza kulifanya .katka kitabu chetu kitukufu ambacho wewe umekisaliti,fungua sura ya nne na usome aya ya sita,saba na nane na maumivu yote yatakwisha na utarejea katika hali yako ya kawaida tena”
“ Ouh gosh ! wameamua kuniadhibu kwa njia hii.Kama walivyoahidi kwamba hawataniacha ni kweli wanachokisema.Kamwe hawatakubali niwe na maisha ya kawaida.Ndoto yangu ya kuwa na Innocent mwanaume nimpendaye kuliko wote inaweza isifanikiwe.Lakini hapana siwezi kukubali kumpoteza Innocent.I’ve sacrificed a lot for him.Niliweka ahadi ya kumpata kabla sijafa na tayari nimempata.Nimekaribia sana kuikamilisha ndoto yangu na kuwa mwanamke mwenye furaha hapa duniani.Nitapambana na kila jaribu ,nitavumilia mateso yote kwa lengo moja tu ….. to be with Innocent before I die. Nimenusurika kuuawa na Brandon but I know I’m going to die soon kukutokana na hali ya kidonda hiki nilichowekewa mgongoni lakini kabla sijafa lazima niwe nimeutumia muda wangu uliobaki nikiwa na mwanaume wa misha yangu” akawaza Latoya na mara sura ya Innocent ikamjia,akavuta pumzi ndefu
“ Nashindwa nimwambie kitu gani Innocent ili aweze kunielewa.Anyway I have no option than to tell him the truth.All the truth about me and my life” akawaza Latoya
Toka hospitali hadi nyumbani kwa Latoya ni mwendo wa dakika tano.Baada ya kufika nyumbani ,akashuka garini na kusalimiana na watumishi wake.Alijitahidi kutabasamu na hakutaka kuonyesha sura ya huzuni.Hakutaka kuwapa wasi wasi watumishi wake aliowapenda sana.Alihisi mwili wake umechoka ,akapanda moja kwa moja ghorofani chumbani kwake.Kitu cha kwanza kukitazama mara tu alipoingia chumbani kwake ni endapo ile madhabahu imeondolewa.Akashusha pumzi baada ya kukuta tayari imeondolewa.
“ Thank you God” akasema taratibu na kukaa akitandani.Akachukua simu na kumpigia Elizabeth lakini simu yake haikupatikana.Latoya akastuka .Hata siku moja haikuwahi kutokea Elizabeth kuzima simu zake zote
“ Elizabeth ana tatizo gani? Kwa ninavyomfahamu hajawahi kuzima simu zake zote hata ile ya nyumbani.Anyway inawezekana amepatwa na dharura” akawaza Latoya halafu akainua tena simu na kupiga chumbani kwa Innocebnt
“ Hallow “ ikajibu sauti ya Innocent
“ Hallo Innocent,unaendeleaje?
“ Ouh Latoya,bado uko hospitali?
“ Hapana Innoceht ,nimerudi si muda mrefu sana.Niko chumbani kwangu”
“Vipi unaendeleaje?
“ Naendelea vizuri Inno” akajibu Latoya
“ Nashukuru kusikia hvyo.Tayari nilikiwisha ingiwa na wasi wasi baada ya kuona muda unakwenda na hurejei”
“ Usihofu Innocent,tayari nimekwiwsha rudi.Umelala?
“ hapana sijalala niko dirishani nikistaajabu mandhari nzuri na yakupendeza kulizunguka jumba lako”
“ Innocent namtuma mtumishi mmoja aje akuchukue na akulete chumbani kwangu.I cant wait to see you”
“ Latoya huna haja ya kumtuma mtumishi,nitakuja mwenyewe hata mimi nina hamu sana ya kukuona”
“ Unafahamu kilipo chumba changu? Akauliza Latoya
“ Ndiyo ninafahamu.Nakuja sasa hivi” akasema Innocent na kukata simu.Latoya akavuta pumzi ndefu
“Ninahofu sana sijui nitaanzaje kumweleza Innocent hadi anielewe.Hata hivyo lazima nimweleze kila kitu.Nitamueleza ukweli na nina amini atanielewa.Alikwisha jitolea kuwa na mimi na tayari anafahamu maisha yangu na amekutana na mambo mengi makubwa ambayo hakuna binadamu wa kawaida anayeweza kuyavumilia lakini yeye amevumilia na bado yuko na mimi.Mpaka leo bado sijapata wasaa wa kuongea naye na kufahamu aliwezaje kupambana hadi akaniokoa.Najaribu kujiuliza bila kupata majibu,Inno aliupata wapi ujasiri na nguvu ya kuweza kupambana hadi akafanikiwa kuniokoa? Nadhani ni wakati muafaka wa kufahamu pia kwa upande wake nini kilitokea” akawaza Latoya na mara mlango ukagongwa
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 63
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Usihofu Innocent,tayari nimekwiwsha rudi.Umelala?
“ hapana sijalala niko dirishani nikistaajabu mandhari nzuri na yakupendeza kulizunguka jumba lako”
“ Innocent namtuma mtumishi mmoja aje akuchukue na akulete chumbani kwangu.I cant wait to see you”
“ Latoya huna haja ya kumtuma mtumishi,nitakuja mwenyewe hata mimi nina hamu sana ya kukuona”
“ Unafahamu kilipo chumba changu? Akauliza Latoya
“ Ndiyo ninafahamu.Nakuja sasa hivi” akasema Innocent na kukata simu.Latoya akavuta pumzi ndefu
“Ninahofu sana sijui nitaanzaje kumweleza Innocent hadi anielewe.Hata hivyo lazima nimweleze kila kitu.Nitamueleza ukweli na nina amini atanielewa.Alikwisha jitolea kuwa na mimi na tayari anafahamu maisha yangu na amekutana na mambo mengi makubwa ambayo hakuna binadamu wa kawaida anayeweza kuyavumilia lakini yeye amevumilia na bado yuko na mimi.Mpaka leo bado sijapata wasaa wa kuongea naye na kufahamu aliwezaje kupambana hadi akaniokoa.Najaribu kujiuliza bila kupata majibu,Inno aliupata wapi ujasiri na nguvu ya kuweza kupambana hadi akafanikiwa kuniokoa? Nadhani ni wakati muafaka wa kufahamu pia kwa upande wake nini kilitokea” akawaza Latoya na mara mlango ukagongwa
ENDELEA……………………….
“ karibu ndani Innocent” akasema Latoya baada ya kuufungua mlango na kukutana na Innocent
“ Karibu sana Inno” akasema tena Latoya huku akimuelekeza Innocent aketi katika sofa zuri jeusi.
“ Pole sana Latoya,unaendeleaje? akasema Innocent
“ Naendelea vizuri Innocent.Zoezi la kupima afya lilichukua muda mrefu tofauti na nilivyotegemea.Umeshindaje leo? I missed you so much”
“ I missed you too Latoya.Nimeshinda salama lakini mawazo yote yalikuwa kwako.Nilitamani nikufuate hosptali” akasema Inno na wote wakacheka
“ Innocent nilishangaa ulponiambia unakifahamu chumba changu”
“ Sikuwa nakifahamu hapo kabla hadi leo hii asubuhi nilikuja humu na Elizabeth”
“ Elizabeth? Akauliza Latoya
“ Ndiyo.Nilikuja kumsaidia kuifanya kazi uliyomuagiza aifanye ya kuondoa ile madhabahu ya mawe.”
“ Ouh Nashukuru sana kwa hilo.Nimekuwa nikimtafuta Elizabeth simuni lakini simu zake zote hazipatikani .Nashangaa kwa sababu hii si kawaida yake.”
“Alipoondoka hapa aliniambia kwamba anahitaji kupumzika”
“ Anaumwa?
“Hapana haumiwi”
“Kama haumwi ana tatizo gani? Namfahamu vizuri sana Elizabeth ni mtumwa katika kazi yake na ni mara chache sana kumkuta amelala nyumbani.Lazima atakuwa na tatizo” akasema Latoya halafu akaangaliana na Innocent
“ Latoya, Elizabeth ana tatizo” akasema Inno
“ tatizo gani?
“ Asubuhi ya leo alikuja huku chumbani kwako kwa dhumuni la kuangalia namna atakavyoweza kuiondoa madhabahu ile uliyomuagiza .Alipofika humu chumbani alikutana na kitu kilichomstua sana”
“ Ouh gosh ! alikutana na kitu gani?Aliona nini? Latoya akauliza kwa wasi wasi mkubwa
“ Alikutana na joka kubwa sana ambalo hajawahi kuliona katika maisha yake”
“ ouh gosh !! Latoya akastuka sana
“ nini kilitokea?
“ Alifanikiwa kukimbia na kuja kuniita lakini nilipokuja humu chumbani sikukuta joka hilo.Elizabeth alipatwa na mstuko mkubwa sana ,ameshindwa kufanya chochote leo na akaniambia kwamba anahitaji kupumzika”
Latoya akashusha pumzi.Jambo lile likamstua sana.Akainama chini akafikiri halafu akasema
“ Kwa miaka mingi nimekuwa nikijitahidi kwa kila niwezavyo kuzuia mambo kama haya kuwatokea watu kama Elizabeth na ndiyo maana chumbani kwangu huwa haruhusiwa mtu mwingine aingie zaidi yangu.Nasikitika sana kwa alichokiona Elizabeth.Hakupaswa kukiona au kujua chochote kuhusiana na mimi kwani si watu wote wenye kuwa na uvumilivu na ujasiri kama ulivyo wewe Innocent.Toka umenifahamu umekutana na mambo mengi mazito na ya kutisha zaidi ya joka aliloliona Elizabeth lakini umeweza kuvumilia yote na hadi sasa bado uko hapa pembeni yangu.Sina hakika kama kuna mtu ambaye anaweza kuvumilia mambo kama uliyokutana nayo wewe .Kuna nyakati nashindwa kuamini kama wewe ni binadamu wa kawaida.Who are you Innocent? Are you an angel sent by God to help me? Akasema Latoya.Innocent akacheka kidogo na kusema
“ Latoya mimi ni Innocent ,rafiki yako ambaye siko tayari kukuacha hata sekunde moja.Wewe ni msichana mrembo na ambaye ninaweza kusema kuliko wote dunaini.Uzuri wako si wa sura pekee bali hata moyo.Unastahili furaha.Uso wako una stahili tabasamu muda wote na hicho ndicho pekee kitu ninachotaka kukifanya na hata kama nitakumbana na vikwazo vingi au hata kama ikinilazimu kufa then I’ll die trying” akasema Inno.Maneno yale mazito yakamliza Latoya
“ Innocent sijui nikwambie nini lakini fahamu kwamba wewe ni malaika wangu.Wewe ni binadamu wa pekee kabisa ambae umeweza kuingia katika maisha yangu na kugundua kwamba hayana furaha na ukajitahidi kwa kila namna kuhakikisha kwamba ninakuwa na furaha.Hakuna mwanadamu ambaye angeweza kusimama mahala pako kuhatarisha maisha yake kwa sababu ya mtu kama mimi.Innocent umeniokoa toka katika mikono ya kifo.Haikuwa kazi rahisi.Najua ulikutana na mambo mengi sana mazito na ya kutisha na ambayo nina hakika yalikushangaza sana na kukufanya ujiulize maswali mengi kuhusiana na mimi.Huu ni wakati muafaka wa kuyajibu maswali yako ,ni wakati muafaka wa kuufahamu undani wangu mimi ni nani .Unastahili kujua kila kitu kuhusiana na mimi.Here is my story “ akasema Latoya akainuka na kuchukua chupa ya maji ya kunywa akamimina katika glasi akanywa halafu akaketi sofani,akarekebisha koo lake tayari kwa kuianza simulizi yake
“Nilikuwa na umri wa miaka sita wakati baba yangu alipochaguliwa kuwa balozi wa Tanzania nchini Marekani.Tulihamia jijini Washington DC na kuanza kuishi pale.Siku moja baba alitembelewa na wageni wawili ofisini kwake.Hawa walikuwa ni Bwana na bibi Martin McKelly,mabilionea wakubwa nchini Marekani.Walikuwa wanahitaji maelekezo kuhusiana na utalii nchini Tanzania kwani walitegemea kuanza ziara ya kuizunguka dunia na kutembelea sehemu mbali mbali za kitalii na kituo chao cha kwanza kilikuwa nchini Tanzania.Baba kama balozi wa Tanzania aliwasaida sana mabilionea wale na wakafika nchini Tanzania.Walifurahi mno na baada ya kumaliza ziara yao na kurejea Marekani urafiki kati ya familia yetu na yao ukaanza.Mabilionea wale hawakujaliwa kuwa na mtoto kwa hiyo wakatokea kunipenda sana na kunihesabu kama mmoja wa wanafamilia yao.Kutokana na upendo wao kwangu waliwaomba wazazi wangu ili niende nikaishi nao katika jumba lao la kifahari.Wazazi wakakubali na nikahamia katika jumba lao la kifahari.Ni katika kipindi hiki bwana na Bi Mckelly walinihamisha toka shule niliyokuwa nasoma na kunipeleka katika shule ya watoto wa mabilionea wa Marekani.Hii ni shule inayosemekana kuongoza kwa kuwa na gharama za juu kabisa nchini Marekani.Katika shule hiyo watoto wenye asili ya kiafrika tulikuwa wawili tu kati ya watoto mia mbili na hamsini .Ukiacha mimi alikuwepo pia mtoto wa mwanamuziki mmoja tajiri sana nchini Marekani.Suala la mtoto wa balozi wa Tanzania kusoma katika shule ya watoto wa mabilionea lilitengeneza vichwa vya habari hapa Marekani na Tanzania wakihoji namna balozi huyo alivyoweza kupata pesa za kunisomesha katika shule hiyo yenye gharama kubwa.Bwana na Bi McKelly walijitokeza hadharani na kukiri kwamba wao ndio wanaonisomesha katika shule hiyo kwa sababu wananipenda na familia zetu ni marafiki wakubwa.Ni katika kipndi hiki ndipo nilipokutana na Elizabeth na kujenga urafiki ambao umedumu hadi leo hii.” Latoya akanyamaza akanywa maji na kuendelea
“Maisha katika jumba lile la bwana na Bi McKelly yalikuwa mazuri sana.Sikuwa nimewahi kuishi maisha ya kifahari namna ile.Hapo ndipo niliyafahamu maisha ya mabilionea.Niliishi kama mtoto wa mfalme.Nilitembelea magari ya kifahari sana.Nilikuwa na walinzi wangu maalum na watu wangu wa kunihudumia Nilivaa mavazi ya gharama kubwa,nilifundishwa kuvaa vito vya dhahabu na mapambo ya kila aina.Niliwahi kutolewa katika jarida moja la hapa marekani nikielezwa kama mtoto ninayeongoza kwa kuvaa vito na mapambo ya thamani kubwa nchini Marekani.Ni kweli nilikuwa mrembo .Nilikuwa napendeza na kila mtu alinisifu” akatulia akanywa maji kidogo na kuendelea
“Niliyazoea maisha ya ubilionea,nikayapenda .Baba na mama ambao kwao nilikuwa mtoto wao wa pekee waliingiwa na wasi wasi kutokana na aina ya maisha niliyoyaishi .Japokuwa bwana na Bi Mckelly waliwahakikishia kwamba hawataniacha nipotee kutokana na kuishi katika maisha ya kitajiri lakini mimi mwenyewe sikuwa tayari kuachana na maisha yale ya kifahari.Tayari nilikwisha yazoea na kuyapenda.Nilipata kila kitu nilichokihitaji ,niliheshimiwa na kupendwa.Kwa hiyo maisha haya ya ubilionea niliyaanza toka nikiwa na umri mdogo.” Latoya akatabasamu halafu akaendelea
“Nakumbuka wakati fulani shule zikiwa zimefungwa ,niliondoka na Bi Mckelly tukitumia boti yao ya kifahari .Tulikuwa tunazunguka katika visiwa mbali mbali .Tulifika hadi katika kisiwa kimoja chenye majumba ya kifahari sana.Usiku wa siku hiyo Bi McKelly alinifanyia jambo moja ambalo nililiona la ajabu mno.Aliniuliza kama ningependa kuyaona maisha yangu ya mbele namna yatakavyokuwa.Nilipatwa na mshangao kidogo kwa sababu hakuna mtu anayejua maisha yake ya mbele yatakuwaje lakini nilikuwa na hamu ya kutaka kujua namna maisha yangu ya mbeleni yatakavyokuwa.Nilimjibu ndiyo ninahitaji kuyajua maisha yangu ya usoni na akanipelekea katika jumba moja kubwa akaniingiza katika chumba kimoja chenye giza akatoka na kuufunga mlango
Mara tu alipotoka chumba chote kikajaa mwanga na mara ukutani nikaanza kuitazama filamu ya maisha yangu ya mbele namna yatakavyokuwa.Nilijiona nikiwa mwanamke tajiri mwenye nguvu na sauti.Niliuona utajiri nitakaokuwa nao .Niliona namna nitakavyopendwa na watu wengi niliyaona pia maisha yangu mazuri na ya kifahari.Wakati huo nilikuwa na umri wa miaka kumi na mitatu tu.Niliyafurahia maisha yale kwani ndiyo nilikuwa nayahitaji.Tayari nilikwisha onja ladha ya maisha ya kitajiri kwa hiyo sikutaka kuishi maisha mengine tofauti na maisha ya kitajiri.Niliyastaajabia sana maajabu yale makubwa na nikamuuliza Bi Mckelly inawezekanaje mtu ukayaona maisha yako ya mbeleni akaniambai kwamba muda utakapofika atanifahamisha kila kitu.Nilikuwa na hamu sana ya kutaka kujua kuhusu namna ilivyotokea .
Nikiwa na umri wa mikaka kumi na mitano Bwana na Bi Mckelly walipoteza maisha katika ajali ya ndege.Lilikuwa ni pigo kubwa sana kwangu.Japokuwa waliacha mali nyingi lakini mali hizo zilianza kupotea moja baada ya nyingine kutokana na kutokuwa na usimamizi makini.Biashara mbali mbali zikafungwa na baadhi ya mali kutaifishwa na mabenki kutokana na madeni waliyokuwa wakidaiwa.Wakati misuko suko hiyo ikitokea baba alimaliza muda wake wa ubalozi nchini Marekani hivyo ikamlazimu kurejea nchini Tanzania.Kwa kuwa bado nilikuwa nikiendelea na masomo hapa nchini Marekani walikubali nibaki na nitakapomaliza nitarejea Tanzania.” Latoya akanyamaza akameza mate na kuendelea na simulizi ya maisha yake
“Baada ya wazazi wangu kurejea Tanzania bado sakata la kupotea kwa mali za Bwana na Bi McKelly liliendelea.Siku moja alikuja mama mmoja akajitambulisha kwangu kwamba anaitwa Virginia strawberry.Alinifahamihsa kwamba alikuwa ni rafiki mkubwa wa bwana na Bi McKelly.Viriginia alinikumbusha siku Bi McKelly aliponionyesha filamu ya maisha yangu ya usoni na akaniuliza kama nilikuwa tayari kuyaishi maisha yale niliyoyaona katika filamu.Nilikubali haraka haraka kwa sababu kwa wakati ule sikuwa na mtu niliyemtegemea na tayari nilikwisha yazoea maisha ya ubilionea Sikuwa tayari kurejea kuishi maisha ya kawaida waliyoishi wazazi wangu.Siku iliyofuata niliondoka na yule mama tukaelekea katika jiji la Sao Luis Brazil.Pale nilipelekwa kwa mtu mmoja ambaye aliitwa kwa jina moja tu la Visca.Nilikuja kugundua baadae kwamba Visca ni cheo.Visca alinipokea vizuri sana na katika maongezi yetu aliniuliza endapo nilitaka kuwa mtu mwenye nguvu na sauti duniani.Kwa mara nyingine tena nilikubali na siku iliyofuata tukaelekea katika kisiwa fulani kidogo kinachosemekana kuwepo kati kati ya Amerika kusini na Bara Afrika.Na hapo ndipo mambo yote yalipoanzia.” Latoya akanyamza tena akanywa maji na kuendelea.
“Usiku nilikutanishwa na wazee watatu wenye ndevu nyingi ambao walianza kunipa maelezo ya utangulizi.Waliniambia kwamba walikuwa ni viongozi wa mtandao wa imani ya watu wenye nguvu duniani na ili kuufahamu vyema mtandao na imani hiyo nitalazimika kupitia mafunzo ya mwaka mmoja.Kwa kuwa nilihitaji sana utajiri nilikuwa tayari kwa lolote lile kwa hiyo nikakubali kuanza mafunzo yale ya mwaka mmoja ili kuufahamu mtandao ule wa imani ya watu wenye nguvu aliousema yule mzee.Kitu cha kwanza kabisa ambacho walianza kunifundisha wale wazee ni kuhusiana na Mungu.Nilifundishwa kwamba hakuna Mungu.Ilikuwa ni vigumu kwa siku za mwanzo kukubaliana nao lakini kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele nikajikuta nikikubaliana na hoja zao na kuamini ni kweli hakuna Mungu.Nilifundishwa kwamba mtu yeyote ambaye ana nguvu na uwezo wa kutenda jambo lolote ambalo binadamu wa kawaida hawezi kulitenda basi mtu huyo ni Mungu kwa hiyo watanifanya na mimi niwe Mungu.Baada ya miezi sita nilijikuta nikiamini kabisa kwamba hakuna Mungu.I believed there is no God and I myself is a God.” Akasema Latoya halafu akainama machozi yakamtoka. Akayafuta na kuendelea.
“Niliendelea na mafunzo yake na baada ya mwaka nikamaliza na kujiunga rasmi na mtandao ule unaoongozwa na Mungu wa giza ,shetani muasi mwenye nguvu kubwa ya ushawishi na lengo kuu la mtandao huu ni kuwalaghai wanadamu na kupoteza dira na mwelekeo wao kwa mwenyezi Mungu.Kuwajaza wanadamu anasa na starehe na kuwafanya wamsahau kabisa Mungu.Kuendeleza ugunduzi wa teknolojia mpya na za kisasa ili kuzidi kumfanya mwanadamu azidishe matendo machafu.Kuwateka kifikra kwa mitindo ya mavazi na urembo , kutumia vitu kama muziki na mitandao ili kuchochea matendo ya ngono.Hayo ni baadhi tu ya malengo ya mtandao huu wa kishetani.Nilikubali kuyatekekeleza hayo yote na nikatawazwa kuwa malkia wa kwanza mweusi wa mtandao huu.Pamoja na nguvu niliyopewa nilipewa pia masharti kadhaa.Moja ya masharti hayo ni kutokujihusisha kwa namna yoyote ile na jambo lolote linalohusiana na imani.Yaani siruhusiwi kukanyaga katika sehemu yoyote ya ibada na wala kushika vitabu vitakatifu au hata kulitaja kwa namna yoyote ile jina la Mungu.Endapo nitavunja sharti hilo la kwanza adhabu yangu itakuwa ni kumtoa sadaka mmoja wa wazazi wangu na damu yake ndiyo itakuwa imenitakasa tena.Sharti la pili nililopewa ni kwamba katika maisha yangu siruhusiwi kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi na mwanaume yeyote yule.Endapo ningevunja sharti hilo basi adhabu yake ni kifo.Ningeuawa na nafasi yangu kuchukuliwa na mtu mwingine.Nilikubaliana na masharti hayo na nikapigwa muhuri wa moto mgongoni kama alama ya maagano kati yangu na shetani mkuu.Muhuri huo niliopigwa ulisababisha kidonda kidogo mgongoni ambacho hakikuwa kikisababisha maumivu yoyote yale lakini kila pale ambapo nitakuwa nikienda kinyume na taratibu basi ningesikia maumivu makali sana ikiwa ni pamoja na kupoteza fahamu .Baada ya muhuri ule wa maagano kugongwa , nilivishwa kidoleni pete yenye nguvu ambayo kwa kupitia kwake ningeweza kusema kitu chochote kile na kikatokea,ningeweza kusababisha majanga ,maafa na kitu chochote kile.I was powerfull,very powerfull.They named me “Female black God”
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 64
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Moja ya masharti hayo ni kutokujihusisha kwa namna yoyote ile na jambo lolote linalohusiana na imani.Yaani siruhusiwi kukanyaga katika sehemu yoyote ya ibada na wala kushika vitabu vitakatifu au hata kulitaja kwa namna yoyote ile jina la Mungu.Endapo nitavunja sharti hilo la kwanza adhabu yangu itakuwa ni kumtoa sadaka mmoja wa wazazi wangu na damu yake ndiyo itakuwa imenitakasa tena.Sharti la pili nililopewa ni kwamba katika maisha yangu siruhusiwi kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi na mwanaume yeyote yule.Endapo ningevunja sharti hilo basi adhabu yake ni kifo.Ningeuawa na nafasi yangu kuchukuliwa na mtu mwingine.Nilikubaliana na masharti hayo na nikapigwa muhuri wa moto mgongoni kama alama ya maagano kati yangu na shetani mkuu.Muhuri huo niliopigwa ulisababisha kidonda kidogo mgongoni ambacho hakikuwa kikisababisha maumivu yoyote yale lakini kila pale ambapo nitakuwa nikienda kinyume na taratibu basi ningesikia maumivu makali sana ikiwa ni pamoja na kupoteza fahamu .Baada ya muhuri ule wa maagano kugongwa , nilivishwa kidoleni pete yenye nguvu ambayo kwa kupitia kwake ningeweza kusema kitu chochote kile na kikatokea,ningeweza kusababisha majanga ,maafa na kitu chochote kile.I was powerfull,very powerfull.They named me “Female black God”
ENDELEA………………………..
Hapo ndipo nilipoufungua ukurasa mpya katika maisha yangu.Nilianza kujulikana duniani kote.Nilifungua miradi mingi na kila mradi niliouanzisha uliniingizia fedha nyingi sana.Nilikuwa na biashara katika kila pembe ya dunia.Miradi mingine ilifunguliwa na watu hata nisiowafahamu kwa jina langu.Akaunti zangu zilifurika pesa.Nilitekeleza maagizo niliyopewa kwa kuanzisha makampuni mbali mbali ya nguo na vifaa vya elektroniki.Nguo nyingi zilizotengenezwa katika viwanda vyangu ni zile zenye kuhamasisha matendo ya ngono.Niliwatumia watu wenye majina makubwa na ushawishi duniani ili waweze kuzitangaza bidhaa za kampuni yangu.Kwa hili nilifanikiwa kwa kiasi kikubwa.Nilipeleka pesa nyingi pia katika kusaidia uvumbuzi wa kisayansi na kukuza teknolojia.Tulianzisha mpango wa kusambaza kompyuta kwa kila mwanafunzi ulaya.Lengo likiwa kukiteka kizazi cha watoto angali bado wadogo wajifunze na wafahamu matendo mbali mbali yakiwemo ya ngono na kuwafanya wahamasike na kushiriki vitendo hivyo.Kwa kupitia watu wakubwa na maarufu duniani tulihamasisha na kuchochea matendo ya mapenzi ya jinsia moja na mpaka hivi sasa watu wameonekana kuyakubali na wanayaona ni matendo ya kawaida na kuyafurahia.Tulitaka kizazi hiki cha watoto wadogo wajifunze hayo yote na hivyo kutengeza dunia iliyojaa maasi makubwa kwa Mungu.Ilianzishwa pia mitandao ya kijamii na idadi kubwa ya watu tayari wameipenda na ina mamilioni ya wafuasi duniani kote.Kupitia mitandao hii watu wanakutana na kujenga mahusiano yanayopelekea matendo ya ngono kuongezeka.Mitandao hii vile vile hutumika kujenga chuki miongoni mwa jamii moja na nyingine na kujenga mafarakano miongoni mwa mtu mmoja mmoja.Kupitia makampuni yangu tulifadhili pia mitandao ya kigaidi duniani na hivyo kuongeza mauaji ya watu wasio na hatia.Tulijenga hospitali kubwa kubwa duniani ambazo ziliongoza kwa matendo ya utoaji mimba.Haya ni baadhi tu ya mambo machafu yanayofanywa na mtandao huu wa kishetani lengo likiwa ni kupoteza idadi kubwa ya wanadamu.Innocent naomba ufahamu kwamba hali ni mbaya na watu wengi wanapotea kila siku katika mikono ya huyu mwovu.Maelfu kwa maelfu ya watu wanaangamia na kupotea kila uchao.Shetani anawatumia wanadamu katika kufanikisha malengo yake na anafanikiwa sana.” Latoya akanyamaza akainama akayafuta machozi na kuendelea.
“Mtandao huu umewahusisha watu wengi sana na wengine ni wakubwa na wenye majina na ushawishi duniani.Wamo pia viongozi mbali mbali wa dini na serikali.Miongoni mwao alikuwepo pia kardinali Gadner Barkov wa Brazil.Huyu alikuwa ni mtu mwenye nguvu na sauti kubwa katika kanisa .Ushiriki wake katika mtandao huu ulikuwa wa siri kubwa na ni watu wachache ambao walifahamu kama alikuwa ni kiongozi wa juu wa mtandao huu wa kishetani.Gadner alitokea kuwa rafiki yangu mkubwa na alinipenda sana.Kila mara katika vikao vyetu kama kuna mahala nilikosea au sikufanya vizuri basi yeye ndiye aliyekuwa mtetezi wangu.Ilitokea siku moja Gadner alinipigia simu usiku wa manane na kuniambia kwamba kesho yake nifanye juu chini nionane naye .Siku iliyofuata nilikwenda Brazil kuonana naye.Gadner alinieleza kwamba alipata maono akiwa usingizini.Alionyeshwa namna watu wanavyoangamia ,dunia inavyoangamia na maelfu ya watu wanavyopotea kila siku kutokana na mambo tunayoyafanya.Alionyeshwa idadi kubwa ya watu ambao tumekuwa tukiwasukumia katika shimo la moto mkubwa.Alionyeshwa pia idadi kubwa ya watu walio katika mtandao wetu ambao walikuwa wakiungua katika moto wa mkubwa.” Latoya akanyamaza akavuta pumzi ndefu na kusema
“Bado nayakumbuka maneno ya Gadner akiniambia kwamba
“Latoya tunawapoteza watu wengi sana na adhabu yetu ni kubwa machoni pa Mungu.Tunatakiwa tuiokoe dunia .Tunatakiwa tuache kuyafanya haya tunayoyafanya sasa na kumrudia Mungu wetu.Mungu wa kweli ambaye hakuna zaidi yake”
“ Gadner alinifumbulia kwamba hata marafiki zangu wawili ambao nao pia walikuwa ni wafuasi wa mtandao huu Melisa na Anna wako katika moto huo wakiungua.Nilistuka na kuogopa sana.Sikujua nifanye nini lakini Gadner akaahdi kunisaida nini cha kufanya.Baada ya siku tatu nilipata taarifa kwamba Gadner yu mgonjwa mahututi..Nikaenda haraka Brazil kumjulia hali .Aliponiona aliwaomba watu wote watoke nje tukabaki wawili tu mimi na yeye .Alinishika mkono wangu na kuniambia neno moja tu “ Latoya save the world” halafu akakata roho mikononi mwangu.Sikujua nifanye nini baada ya hapo.” Latoya akanyamza akafuta machozi na kisha akanywa maji kidogo na kuendelea na simulizi yake
“Nilipata wakati mgumu sana bada ya kifo cha Gadner na sikujua ningewezaje kuuokoa ulimwengu huu wakati tayari nilikwisha weka maagano na shetani.Siku moja mmoja wa wafanyakazi wangu alifariki dunia.Alikuwa ni mfanyakazi ambaye nilimpenda sana na niliumizwa mno na kifo chake.Bila kujitambua siku hiyo nikajikuta nimeingia kanisani kwa ajili ya ibada ya kumuombea marehemu.Nikiwa kanisani nilisikia kuna kitu kinanigusa moyo wangu.Nilisikia kama kuna sauti inaniita na kusema kwa uchungu
“ Latoya kwa nini unanitesa? Kwa nini unawaangamiza watu wangu?
“Nilifahamu sauti ile haikuwa ya binadamu.Nililia machozi mengi sana siku hiyo baada ya kugundua namna nilivyomuacha Mungu wa kweli na kumuangukia Mungu wa giza. Kila aliyeniona mle kanisani alidhani kwamba ninalia kutokana na kuguswa na kifo cha mfanyakazi wangu kumbe nilikuwa nikililia mambo mengine kabisa.Baada ya hapo nikahudhuria katika harambee ya ujenzi wa kanisa na nikatoa mchango mkubwa sana na hapo ndipo matatizo katika mgongo wangu ile sehemu niliyopigwa muhuri wa moto wa maagano yalipoanza.Nilikuwa nikisikia maumivu makali kupita kiasi yaliyonipeleka mara nyingine kuanguka na kupoteza fahamu na nilipozinduka nilijikuta nikiwa nimepoteza damu nyingi sana.Nilianza kuwa na mateso na maumivu makali mno kila siku na maisha yangu yakakosa furaha. Kuna nyakati nilitamani hata kufa kuliko kuendelea na mateso na maumivu yale niliyokuwa nikiyapata kila siku.Kutoka na hali hii ilinilazimu kutafuta daktari wa kunitibu na ili kuendelea kuificha siri ya ugonjwa wangu ilinilazimu kumfanya awe bubu na aliweza kuongea na mimi tu. Pamoja na mateso na maumivu yale makali lakini sikuacha kujitolea katika kujenga nyumba za ibada na adhabu yangu ikaongezeka.Viongozi waligundua kwamba nilikuwa nimetetereka kwa hiyo wakamuandaa mrithi wangu ambaye ni Brandon. Walianza kuniogopa pengine siku moja ningekuja kuwasaliti kwa hiyo wakaanza kujiandaa mapema.Niliendelea na ujenzi wa nyumba za ibada na kuanza kuifunga baadhi ya miradi ambayo ilikuwa ikifadhili matendo ya ugaidi ,utoaji mimba na ushoga na hapo ndipo nilipohukumiwa kifo.Nilianza kuwa mtu hatari kwao na tayari nilikwisha kiuka maagano.” Latoya akasimama na kuvuta pumzi ndefu na kusema
“Niliambiwa kwamba nitakutana na mrithi wangu katika msiba lakini sikufahamu ni msiba wa nani kumbe alikuwa ni mama yangu.Baada ya kumuua mama yangu nilipatwa na hasira sana na sikushiriki katika kitendo cha kunywa damu ya mama yangu kwa ajili ya kunitakasa na kunifanya mpya tena.Nilichoshwa na maisha yale na nilitamani kuishi maisha mengine yenye furaha na amani..” Machozi mengi yakamtoka Latoya akayafuta na kuendelea
“Siku ninaapishwa kuwa malkia wa giza,moja ya masharti niliyopewa ni kutojihusisha na suala lolote la mapenzi na wala sikutakiwa kuwa na mpenzi.Hili ni jambolililoniumiza mno kwani nilijikuta nikitamani kuwa na mpenzi na mimi nifurahie maisha kama wanawake wengine na hapo ndipo nilipowekaahadi ya lazimanimpate mwanaumewa ndotozangukablasijafa.Nilijitoa mhanga lakini tatizo likawa nitampata wapi mwanaume huyo?Nafahamukatika dunia ya sasa kunaulaghai mwingina wengi wa wanadamu hawana mapenzi ya kweli.Nilijua nitakufa hivi karibuni na nilitaka niyafurahie mapenzi na si kuteswa nayo.Pamoja na mambo yote niliyomkosea Mungu lakini bado aliendelea kuwa mwema kwangu na akanipatia kile ambacho nilikuwa nakitaka na kumuomba kila siku yaani mwanaume wa maisha yangu.Innocent you are that man of my dreams.Ni wewe ambaye niliamini nitakupata kablasijafa.Ni wewe ambaye nilikupenda kabla hata ya kukuona.Ni wewe ndiye niliyekuwa nakuota usiku na mchana.Ni wewe ndiye uliyeufanya moyo wangu uteseke kila siku na kukiuka maagano na Mungu wa giza..Innocent nakupenda sana kwa moyo wangu wote.Nakupenda zaidi ya ninavyoweza kukueleza.Nakupenda zaidi ya ninavyojipenda mimi mwenyewe”
Latoya akanyamaza na machozi mengi yakaendelea yakamtoka.Innocent ambaye uso wake ulikuwa umeloa jasho kutokana na simulizi ile ya Latoya alishindwa aseme kitu gani.Kutoka moyoni mwake alimpenda sana Latoya na ndiyo maana alikuwa tayari kufanya kila jambo kwa ajili yake.Siku zote alitamani kumweleza ukweli lakini aliogopa kufanya hivyo kutokana na mazingira yaliyomzunguka.Latoya bado aliendelea kulia kwa kwikwi,Innocent akanyanyuka sofani na kumuendea akaketi karibu yake na kumshika bega
“Pole sana Latoya.Nyamaza usilie.I’m here now for you.I’m here to stay”
Maneno yale ya Innocent yakamfanya Latoya anyanyue kichwa chake na kumtazama usoni.
“ Mara ya kwanza Sabrina aliponitamkia jina lako nilihisi kustuka na kutamani kuonana nawe.Nilikupenda kabla hata sijakutia machoni na siku ile nilipokuona kwa mara ya kwanza nilihisi kama vile nimeonana na malaika.Mapigo yangu ya moyo yalibadilika na niliona kama dunia imesimama.Nilimshukuru Mungu kwa kunikutanisha nawe kwani niliamini wewe ndiye yule ambaye nilikuwa nakuota usiku na mchana.Nilifahamu matatizo ninayokwenda kukutana nayo kwa kukupenda lakini tayari nilikwisha jitoa mhanga kwa lolote lile.Nilitamani sana nikwambie ukweli kwamba wewe ndiye mwanaume wa maisha yangu lakini kila nilipojaribu kufanya hivyo kulitokea kizingiti na kunizuia nisikutamkie ukweli wa moyo wangu.Kabla ya kuanza kwa safari ile nilitokewa na watu wawili wakaniambia kwamba ile safari ni safari yangu ya mwisho na kwamba nisingerejea tena kwani nilikuwa naenda kufa.Walinionya kwamba katika safari ile nisithubutu kuambatana nawe lakini kwa kuwa ninakupenda na wewe ndiye mwanaume wa ndoto zangu sikuwa tayari kufuata matakwa yao kwa hiyo nikaambatana nawe .Nilitaka nitumie hata siku mbili nilizokuwa nimebaki nazo pamoja nawe.Tukiwa safarini nilijaribu kutaka kukueleza ukweli lakini ikapiga ile radi na wewe kupotea.Sikukuona tena hadi ulipojitokeza kule kisiwani na kuniokoa toka kifo.Innocent najua umekumbana na vikwazo vingi sana na umeshuhudia mambo mengi makubwa na mazito.Naomba unisamehe sana Innocent kwa kukufanya ukaingia katika dunia ya giza isiyoonekana kwa macho ya kawaida na yenye mambo ya kutisha mno. ” Latoya akashindwa kujizuia na kuangua kilio.
“ Nyamaza kulia Latoya.Ni kweli nimekutana na mambo ya ajabu sana yasiyosimulika lakini nimeweza kuyashinda yote .Nilifanya yale yote niliyoyafanya kwa sababu ya upendo wangu mkubwa kwako.Latoya naomba na mimi nikiri kwamba ninakupenda sana na siku zote nimekuwa nikisubiri wakati muafaka ili niweze kukueleza ukweli wa moyo wangu namna gani ninavyokupenda.Mimi na wewe hatujajuana muda mrefu lakini siku ile ya kwanza tu nilipokuona nilihisi kuna muunganiko mkubwa kati yangu nawe.Uliingia moyoni mwangu toka sekunde ya kwanza kukutia machoni.Moyo wangu haukunidanganya kwamba wewe ndiye mwanamke wa maisha yangu na kukutana kwetu haikuwa ni kwa bahati mbaya.Ulinikaribisha nyumbani kwako na baada ya msiba wa Marina nilishindwa kabisa kuondoka kwa sababu nilihitaji kuwa karibu nawe.Nilijisikia furaha na amani niwapo karibu yako na ndiyo maana nimeweza kuvumilia yote mateso na magumu na nimekuwa na nguvu ya kupambana na yeyote yule aliyetaka kukudhuru.Latoya naomba nikiri kwamba mwanzoni nilipoanza kuishi pale nyumbani kwako nilipatwa na wakati mgumu sana kutokana na mambo niliyoyaona.Kuna nyakati nilitaka niondoke lakini moyo wangu haukuwa tayari kuondoka na kukuacha peke yako.Macho yangu yalikutazama hadi ndani kabisa ya moyo wako na kugundua kwamba haukuwa na furaha katika maisha yako.Niliweka ahadi ya kufanya kila niwezalo ili kukufanya uwe na furaha tena.Nilikumbana na majaribu mengi makubwa na ya kukatisha tamaa lakini niliyavumilia yote kwa sababu ya upendo wangu mkubwa kwako.Nakumbuka siku moja nikiwa nimelala niliota ndoto yenye uhalisia mkubwa .Nilikuwa sehemu fulani nikiwa na wazee Fulani na wakaniambia kwamba nitakuwa mlinzi wako na nikulinde dhidi ya wale wote wanaotaka kukuangamiza na mwisho wa yote mimi nawe tuiokoe dunia.Sikufahamu ni nani aliyekuwa anataka kukuangamiza .Baada ya kunipa maagizo yale waliuunguza mkono wangu wa kulia kwa moto.Nilipostuka nilisikia maumivu makali katika mkono wangu wa kulia maumivu ya kuungua moto.Siku hiyo ndiyo mama yako alipopoteza maisha.Nakumbuka ulirudi nyumbani ukiwa na simanzi nikataka kupeleka mkono wangu mgongoni kwako kwa lengo la kukufariji lakini nilipigwa na kitu kama chaji za umeme na pale pale mkono wangu ukapona.Yalikuwa ni mambo ya kustaajabisha sana kwangu.Wakati tukielekea nyumbani kwa wazazi wako kuonana na mjomba wako ambaye alikuzuia usikanyage msibani,nilipitiwa na usingizi na nikamuona tena Yule mzee mwenye ndevu nyingi na kanzu nyeupe pamoja na mshipi mwekundu kiunoni akaniambia kwamba niyasome maandishi yaliyokuwa katika ubao alioushika.Niliyasoma maandishi yale na akaniambia kwamba muda wowote ninapohitaji msaada basi niyatamke yale maneno niliyoyasoma katika ule ubao.Sikuyaelewa maana yake.Maneno yale ndiyo niliyoyatumia nyumbani kwenu na watu wote akiwemo mjomba wako na wazee wa ukoo wakanisikiliza na kutii kila nilichowaambia.” Akasema Innocent halafu akanyamaza kidogo na kumtazama Latoya ambaye macho yake hayakukaukiwa machozi.Akamfuta machozi na kuendelea.
“Siku ile tulipokuwa melini ulitaka kunieleza jambo lakini kabla hujatamka jambo ikapiga radi kubwa na sikuona kitu chochote tena zaidi ya giza nene.” Innocent alipofika hapa akanyamaza na kisha akavuta pumzi ndefu halafu akamueleza Latoya kila kitu kilichotokea hadi alipofanikiwa kumuokoa.Latoya akashindwa kuvumilia akalia machozi mengi.
“ Nyamaza kulia Latoya.Mambo haya yamekwisha na kilichobaki ni sisi kuangalia mambo ya mbele.Hakuna cha kuhofia tena”
Latoya akafuta machozi na kumtazama Innocent kisha akasema
“ Innocent sipati neno la kuweza kukushukuru kwa kazi kubwa uliyoifanya.Najua haya yote yamewezekana kwa msaada mkubwa wa Gadner ambaye lengo lake kubwa ni kuusambaratisha mtandao huu wa kishetani na kuzuia watu wasiendelee kupotea.Nashukuru umeniokoa Innocent.Lakini pamoja na hayo bado kuna tatizo kubwa”
“ tatizo gani Latoya?
“ Nilifanya maagano na shetani na kuahidi kutekeleza kila atakachoniagiza na kama ishara ya kuyalinda maagano yetu nilipigwa muhuri wa moto mgongoni muhuri ambao ni kidonda kidogo ambacho hakikuwa na maumivu wala madhara yoyote hadi pale nilipokwenda kinyume na maagano yetu.Pamoja na kuniokoa lakini bado hawajakata tamaa na lengo lao ni kuhakikisha ninapata mateso makali sana na kisha kuwarudia.Baada ya kuniokoa kutoka kule kisiwani,kidonda kile kilichokuwa kidogo,kimekuwa kikiongezeka kwa kasi na kuwa kikubwa na cha kutisha.Kibaya zaidi imebainika leo katika uchunguzi kwamba kidonda kile kimesbabishwa na virusi waitwao Sethypothes ambao ni virusi hatari wanaozaana kwa wingi wa ajabu ndani ya kipindi kifupi.Virusi hawa huzalisha kemikali iitwayo Altroutraczema ambayo ni sumu na huingia katika mfumo wa damu na kuua chembe nyekundu za damu na hivyo kunisababishia upungufu mkubwa wa damu.Virusi hawa wana tabia ya kubadilika na mpaka hivi sasa bado madaktari hawajaweza kugundua dawa ya kuwaangamiza. Na kutokana na kuzaliana kwa wingi wa ajabu inamaanisha kwamba kama haitapatikana dawa ya kuwaangamiza then I’m going to die very soon.” Akasema Latoya na uso wa Innocent ukaonyesha mstuko mkubwa
“No That’s not possible.There must be a way.!! akasema Innocent
“Innocent hakuna dawa ya kuweza kuwaangamiza virusi hawa kwa sasa kwa hiyo naomba niwe wazi kwako kwamba nitakufa hivi karibuni.I’m so sorry Inn…….” Latoya akashindwa kujizuia kulia kwa sauti kubwa.Innocent akahisi kuchanganyikiwa hakuelewa afanye nini.
“Innocent nasikitika sana kufa katika umri huu mdogo.Nilitamani sana kuendelea kuishi maisha ya furaha nikiwa nawe mwanaume wa maisha yangu lakini haitawezekana tena.Simlaumu mtu yeyote kwani mambo haya yote nimeyataka mimi mwenyewe.Tamaa ya mali na utajiri vimeniponza na sasa nitaviacha vyote.Pamoja na kupata vitu vyote nilivyokuwa navitaka sikuwahi kuwa na furaha katika maisha yangu hadi pale ulipotokea lakini nimechelewa sana.Sintaweza kuipata nafasi ya kufurahi pamoja nawe.Inaniuma sana kwani siku zote nilitamani kuishi maisha marefu nikiwa nawe hadi tufike uzeeni.” Machozi mengi yaliendelea kumtoka Latoya.Innocent naye alishindwa kujizuia machozi yakamtoka
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………
[07:17, 9/27/2016] PATRIC PENIELA: BEFORE I DIE
SEHEMU YA 65
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Virusi hawa huzalisha kemikali iitwayo Altroutraczema ambayo ni sumu na huingia katika mfumo wa damu na kuua chembe nyekundu za damu na hivyo kunisababishia upungufu mkubwa wa damu.Virusi hawa wana tabia ya kubadilika na mpaka hivi sasa bado madaktari hawajaweza kugundua dawa ya kuwaangamiza. Na kutokana na kuzaliana kwa wingi wa ajabu inamaanisha kwamba kama haitapatikana dawa ya kuwaangamiza then I’m going to die very soon.” Akasema Latoya na uso wa Innocent ukaonyesha mstuko mkubwa
“No That’s not possible.There must be a way.!! akasema Innocent
“Innocent hakuna dawa ya kuweza kuwaangamiza virusi hawa kwa sasa kwa hiyo naomba niwe wazi kwako kwamba nitakufa hivi karibuni.I’m so sorry Inn…….” Latoya akashindwa kujizuia kulia kwa sauti kubwa.Innocent akahisi kuchanganyikiwa hakuelewa afanye nini.
“Innocent nasikitika sana kufa katika umri huu mdogo.Nilitamani sana kuendelea kuishi maisha ya furaha nikiwa nawe mwanaume wa maisha yangu lakini haitawezekana tena.Simlaumu mtu yeyote kwani mambo haya yote nimeyataka mimi mwenyewe.Tamaa ya mali na utajiri vimeniponza na sasa nitaviacha vyote.Pamoja na kupata vitu vyote nilivyokuwa navitaka sikuwahi kuwa na furaha katika maisha yangu hadi pale ulipotokea lakini nimechelewa sana.Sintaweza kuipata nafasi ya kufurahi pamoja nawe.Inaniuma sana kwani siku zote nilitamani kuishi maisha marefu nikiwa nawe hadi tufike uzeeni.” Machozi mengi yaliendelea kumtoka Latoya.Innocent naye alishindwa kujizuia machozi yakamtoka
ENDELEA……………………
“ Hapana Latoya,usiseme hivyo.You wont die.You wont die “
“ Innocent hakuna namna ya kuweza kufanya labda ipatikane tiba ya virusi hawa vinginevyo I must die.I’m going to die Innocent” akasema Latoya.Akasimama na kuvua koti lake jeusi pamoja na kuipandisha juu fulana aliyokuwa ameivaa akamuonyesha Innocent kidonda kilichopo mgongoni.Innocent akastuka na kuogopa kutokana na hali ya kidonda kile.
“ Ouh Mungu wangu ! akasema Innocent
“ Innocent hiyo ndiyo hali halisi niliyonayo.Hakuna namna nyingine ya kukizuia na kukitibu kidonda hiki.Madaktari wamenihakikishia hivyo.I must die “ akasema Latoya kwa huzuni
“ Hapana Latoya,huwezi kufa.Please don’t say that again.You wont die.We must find a way”
“ Innocent najua unanipenda kwa moyo wako wote na ninafahamu umeumizwa sana na jambo hili .Hata mimi pia nimeumia sana kiasi kwamba ninahisi kama moyo wangu unakatwa vipande vipande lakini hatuwezi kupingana na ukweli kwamba nitakufa muda si mrefu lakini kabla sijafa kuna mambo ambayo nataka kuyafanya”
“ hapana Latoya usiseme hivyo.Moyo wangu unaumia mno.Why you have to die Latoya? No ! you cant die.” Akasema Innocent.Macho yake yalifunikwa na machozi
“ Innnocent naomba unisikilize.Hapo kabla ndoto yangu ilikuwa ni kumpata mwanaume wa maisha yangu ,nitakayempenda kuliko kitu chochote kabla sijafa.Ndoto hiyo tayari imetimia na nimekwisha kupata.Pamoja na kukupata lakini sintaweza kuishi na kufurahi nawe kwa muda mrefu.I must die Innocent.There are things I must do before I die” akasema Latoya.Innocent akafuta machozi na kupiga magoti akamtazama Latoya
“ Latoya naomba unisikilize.I’m not Go,I don’t have any power but I wont let you die.Latoya ugonjwa huu umesababishwa na maagano uliyoyafanya na shetani kiumbe ambaye ameumbwa na Mungu.Ni Mungu pekee mwenye uwezo wa kuamua hatima ya maisha ya mtu na si mwanadamu au kiumbe mwingine yeyote yule.I believe in God.Ni yeye pekee anayeweza kusema kitu na kikawa Latoya umemkosea sana Mungu lakini siku zote yeye amekuwa anatupenda hata pale tunapomkosea kwa kiwango cha juu sana na anatupa tena nafasi nyingine ya kutubu dhambi zetu na kumrejea.Hii ni nafasi nyingine umepewa ya kutubu dhambi zako na kujiweka katika mikono mitakatifu na yenye nguvu ya Mungu. Ni wakati sasa wa kuamua kubadili maisha yako na kumrudia bwana Mungu wa majeshi.So answer me do you believe in God?.
Latoya akafuta machozi na kusema
“I do Innocent.I do believe ni God…”
“Good…Fahamu kwamba ni yeye tu ambaye ana uwezo wa kukuponya ugonjwa huu.Kuna kanisa lolote hapa karibu? Akauliza Innocent.Latoya hakujibu kitu akabaki anamtazama
“ Latoya kuna kanisa lolote hapa karibu tunakoweza kumpata mtumishi yeyote wa Mungu? Akauliza tena Innocent lakini kabla Latoya hajajibu chochote kikatokea kitu cha ajabu sana.Macho ya Latoya yakabadilika na kuwa meupe na ulimi ukamtoka.Akaanguka sofani.
“ Latoya ! Latoya ! Innocent akaita lakini Latoya alikuwa amekakamaa pale sofani na povu lilikuwa linamtoka mdomoni.Innocent akaogopa sana.
“ Ouh Mungu wangu tafadhali muokoe Latoya. Akasema Innocent .Akili yake ikafanya kazi haraka haraka akashuka chini na kuomba aelekezwe mahala lilipo kanisa.Watumishi wote wakashangaa kwa hali ile aliyokuwa nayo Innocent na kwa haraka akapanda garini pamoja na dereva wa Latoya wakaondoka kwa mwendo wa kasi kuelekea kanisani.Walitumia dakika kama kumi hivi kufika kanisani na moja kwa moja Innocent akaingia katika ofisi ya askofu.Huku akihema akamwambia askofu Pater Wirth waongozane ili akamfanyie Latoya maombi.Bila tatizo askofu Peter akakubali na wakaingia garini na kuondoka kwa kasi ya ajabu kurejea katika makazi ya Latoya.Walipofika moja kwa moja wakapanda ghorofani huku wakikimbia hadi chumbani kwa Latoya.Askofu peter alipoiona hali ya Latoya alistuka
‘ Tumkimbize hospitali” akasema Askofu Peter
“ Hapana baba askofu huu si ugonjwa wa hospitali.Tunahitaji maombi yako ndiyo maana nimekufuata” akasema Innocent na askofu Peter akaomba aletewe ndoo ya maji na chumvi kisha akayabariki akachanganya na chumvi ile kuanza kufanya maombi huku akimnyunyizia maji Latoya aliyekuwa amelala sofani.Wakati akiendelea kuomba huku akimnyunyizia maji ghafla kitu cha ajabu kikatokea.Mwili wa Latoya ukaanza kutoa kitu mfano wa moshi.Innocent akaogopa sana.Askofu Peter hakustuka akaendelea kuomba kwa nguvu na kumnyunyizia maji na mara Latoya akaanza kugala gala na kuanguka sakafuni.Innocent akataka kumshika lakini askofu Peter akamzuia akaendelea kuomba Latoya akaanza kutapika damu halafu akanyoosha mikono na kulala kifudi fudi.
Askofu Peter alikuwa anatokwa na jasho jingi akamuinamia Latoya na kumuita
“ Latoya ! Latoya ! ..” Latoya hakutikisika .Askofu akamgeukia Innocent ambaye alikuwa amesimama huku akiwa na wasi wasi mkubwa
“ nahisi kuna kitu kizito mno humu ndani ambacho bado kinamfunga Latoya” akasema askofu Peter .Mara moja Innocent akakumbuka kitu
“ Kitabu..” akasema na kutoka mbio hadi chumbani kwake na kurudi na kitabu mkononi akamkabidhi askofu
“ Hiki ni kitabu chenye ibada za kishetani.” Askofu peter akakishika kitabu kile akakitazama na kukiweka chini akaanza kuomba huku akikimwagia maji yaliyobarikiwa.Taratibu chumba chote kikaanza kujaa moshi .Sauti mbali mbali za mivumo zikasikika.Zilisikika pia sauti za viumbe wa ajabu ajabu zikipiga kelele.Ilikua ni hali ya kuogofya sana lakini askofu Peter hakuogopa akaendelea na maombi .Chumba kikajaa moshi na ghafla moshi ule ukatoweka na biblia ile haikuonekana tena.Ilikuwa imetoweka na badala yake pale chini palionekana ndege mkubwa mweusi akipiga mbawa zake mara tatu na kuruka akatokea dirishani na kutokomea porini.Wakati akiruka alisababisha upepo mkali mle chumbani uliowasukuma askofu Peter na Innocent wakaanguka chini
“ Mungu wangu !!!..akasema askofu Peter akishangazwa na maajabu yale.Hakuwahi kushuhudia mambo ya ajabu na yakutisha kama yale toka alipoanza kazi hii ya utumishi wa Mungu
Baada ya dege lile kutoweka,wakainuka na kumwendea Latoya.Kitu cha kushangaza ile damu aliyokuwa akitapita Latoya iliyokuwa imetapakaa sakafuni ilikuwa imetoweka Latoya alikuwa mkavu na hakuonekana na hata chembe moja ya damu.
“ Latoya ! Latoya ..! akaita Innocent .Latoya akaitika kwa saut ya mbali sana
“ Unajisikiaje Latoya?
“ Maumivu..naumwa sana.” Akasema Latoya kwa taabu.Alionekana yuko katika maumivu makali mno.Innocent akamvua lile koti jeusi alilokuwa amevaa na ndipo askofu Peter akastushwa na kidonda kikubwa mgongoni mwa Latoya
“ Jesus Christ !! akasema askofu na kushusha pumzi.Akachukua maji na kunyunyiza juu ya kile kidonda huku akifanya maombi.Kila tone la maji lilipoanguka juu ya kidonda lilionekana kutoa moshi na Latoya akasikia maumivu makali sana akapiga kelele kwa sauti kubwa na kupoteza fahamu.Baada ya kupoteza fahamu askofu Peter akaamuru Latoya apelekwe hospitali kwani kidonda kile kilikuwa katika hali mbaya.Gari la wagonjwa likaitwa likaja kwa haraka na kumkimbiza Latoya hospitali.Wakati akikimbizwa hospitali Innocent na askofu Peter waliendelea na maombi .Baadaye askofu Peter na Innocent wakaelekea katika chumba cha maongezi na Innocent akamsimulia askofu Peter kila kitu kuhusiana na Latoya bila kumficha.Alianza kwa kumuelezea historia nzima ya Latoya.Hakuficha kitu chochote alieleza kila kitu.Alieleza namna walivyokutana na maisha yake na hadi alipofanikiwa kumuokoa kule kisiwani.Ilikuwa ni simulizi iliyomuacha kinywa wazi askofu Peter.Alitetemeka sana kwa simulizi ile.Akainua mikono juu na kumshukuru Mungu kwa yote halafu akamuomba Innocent apige magoti.Akamuombea na kumbariki kisha wakaongozana hadi hospitalini ambako aliendelea na maombi mengine kwa Latoya.Bado Latoya hakuwa na fahamu
Saa mbili za usiku Elizabeth alifika pale hospitali akihema na kuonyesha sura ya kuchanganyikiwa.Alitaka kujua hali ya Latoya.Bado Latoya hakuwa na fahamu.Innocent akamtuliza .
“Innocent nimechanganyikiwa hapa nilipo na sijui wapi pa kuanzia.Tafadhali nipe hali halisi ya Latoya” akasema Elizabeth kwa wasi wasi
“ Usiwe na hofu Elizabeth..Latoya atapona tu.Mungu atamsaidia” akasema Innocent
‘Innocent kuna jambo kubwa limetokea jioni ya leo”
“ Jambo gani hilo? Akauliza Innocent kwa wasi wasi
‘makao makuu yetu New York City yameteketea kwa moto na hakuna hata kitu kimoja kilichookolewa.Kila kitu kimeteketea”
“ Mungu wangu ..!! Innocent akasema kwa mstuko akashika kichwa chake
“ Nini kimesababisha moto huo?
“ hakuna anayefahamamu chanzo cha moto huo lakini kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba moto huo uliibuka ghafla na ulikuwa mkubwa kiasi cha kushindwa kudhibitiwa.Idadi isiyojulikana ya watu waliokuwamo ndani ya jengo hilo inasemekana wamepoteza maisha.Nilikuwa nimezima simu lakini kuna mtu alinifuata nyumbani akanieleza na nilipompigia simu Latoya kumfahamisha ndipo nilipoambiwa kwamba amekimbizwa hospitali.Innocent whats going on? Kwa nini mambo haya yanatokea sasa? What are we going to do? Nimechanganyikiwa Innocent.Nyaraka zote muhimu zimeteketea na sielewi nini tutafanya kuzipata tena.” Akasema Elizabeth huku machozi yakimtoka.Innocent akamtuliza na kumsimulia kila kitu kilichotokea nyumbani kwa Latoya na ghafla Elizabeth naye akaanguka na kupoteza fahamu
* * * *
Kuendelea kupona kwa haraka kwa kidonda cha Latoya kuliwashangaza mno madaktari na wanasayansi ambao waliokuwa wakivifanyia utafiti virusi vya Sethypothes waliokuwa wamesababisha kidonda kile virusi ambao hakukuwa na dawa yenye kuweza kuwaangamiza.Ni siku ya nane sasa Latoya akiwa bado amelazwa hospitali akiendelea na matibabu
Kupona kwa haraka kwa kidonda hiki kulichangiwa na maombi yaliyofanywa kila siku na askofu Peter ambaye kila uchao alifika hospitali akafanya maombi
Kwa sasa Latoya alikuwa anaendelea vizuri na aliweza hata kuinuka na kukaa mwenyewe kitandani.Kwa muda wa wiki nzima habari kuu iliyotawala vyombo mbali mbali vya habari duniani ni kuhusiana na kuungua moto kwa makao makuu ya kampuni ya Latoya ijulikanayo kama Latoya the world Co Ltd na kuteketeza kila kitu kilichokuwamo ndani.Bado chanzo cha moto huo uliosababisha kuungua moto kwa kampuni hii kubwa duniani yenye mamia ya makampuni ndani yake hakikujulikana .Kuungua kwa jengo hili kulisababisha mabilioni ya dola kupotea kwani kumbu kumbu nyingi muhimu zilipotea.Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Elizabeth ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni hii kubwa
Mchana huu Latoya akiwa chumbani hospitali Innocent akawasili akiwa ameongozana na askofu Peter.Uso wa Latoya ulikuwa umepambwa kwa tabasamu pana
“ Wow ! at last the African queen is back” akasema Innocent kwa furaha.Alifurahi sana kumkuta Latoya akiwa katika hali ile ya tabasamu kubwa.
“ Ouh Innocent my king..” akasema Latoya halafu akaikunjua mikono yake na kukumbatiana kwa furaha.Askofu Peter alibaki anatabasamu
“Unaendeleaje Latoya ? akauliza askofu Peter
“Naendelea vizuri sana baba askofu.Mungu ameniokoa.Amenirejeshea tena maisha yangu” akasema Latoya huku akishindwa kuyazuia machozi kumtoka
“Mwanangu,Mungu ni mwema sana na siku zote anatupenda .Hata pale tunapomkosea lakini bado yuko tayari kutupokea pale tunapotubu na kujuta dhambi zetu”
“Baba askofu ninataka kurejea katika kundi la watoto wa Mungu.Ninataka nitubu dhambi zangu makosa yangu yote na ninataka kubadilisha maisha yangu.Nimemkosea sana Mungu na sijui nifanye nini ili aweze kunisamehe.Naomba unisaidie baba askofu nahitaji kumrudia Mungu tena” akasema Latoya Askofu Peter akamtazama kwa makini na kuiona nia ya dhati ya kutaka kutubu dhambi zake zote
“ Latoya,siku zote bwana Mungu yuko tayari kumsamehe mtu yeyote anayetubu dhambi zake na kumuweka katika kundi la watoto wake.Katika Isaya 1:18 anasema “ sasa njooni nasi tunyooshe mambo kati yetu asema Yehova.Hata dhambi zenu zikiwa nyekundu zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji,hata zikiwa nyekundu kama kitambaa ,zitakuwa nyeupe kama sufu”
Askofu peter akamuomba Innocent atoke nje akabaki mle chumbani na Latoya ambaye aliitumia nafasi ile kujuta na kutubu dhambi zake.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 66
“Unaendeleaje Latoya ? akauliza askofu Peter
“Naendelea vizuri sana baba askofu.Mungu ameniokoa.Amenirejeshea tena maisha yangu” akasema Latoya huku akishindwa kuyazuia machozi kumtoka
“Mwanangu,Mungu ni mwema sana na siku zote anatupenda .Hata pale tunapomkosea lakini bado yuko tayari kutupokea pale tunapotubu na kujuta dhambi zetu”
“Baba askofu ninataka kurejea katika kundi la watoto wa Mungu.Ninataka nitubu dhambi zangu makosa yangu yote na ninataka kubadilisha maisha yangu.Nimemkosea sana Mungu na sijui nifanye nini ili aweze kunisamehe.Naomba unisaidie baba askofu nahitaji kumrudia Mungu tena” akasema Latoya Askofu Peter akamtazama kwa makini na kuiona nia ya dhati ya kutaka kutubu dhambi zake zote
“ Latoya,siku zote bwana Mungu yuko tayari kumsamehe mtu yeyote anayetubu dhambi zake na kumuweka katika kundi la watoto wake.Katika Isaya 1:18 anasema “ sasa njooni nasi tunyooshe mambo kati yetu asema Yehova.Hata dhambi zenu zikiwa nyekundu zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji,hata zikiwa nyekundu kama kitambaa ,zitakuwa nyeupe kama sufu”
Askofu peter akamuomba Innocent atoke nje akabaki mle chumbani na Latoya ambaye aliitumia nafasi ile kujuta na kutubu dhambi zake.
ENDELEA……………………….
BAADA YA WIKI TATU
Ni wiki ya tatu sasa imepita toka Latoya alazwe hospitali na kidonda chake kimepona.Huu ulikuwa ni muujiza mkubwa kwani madaktari bado hawakufanikiwa kupata dawa ya kuwangamiza virusi wale hatari
Hali yake iliendelea vizuri na akaruhusiwa kutoka hospitali akarejea nyumbani.Usiku wa siku hiyo aliyoruhusiwa kurejea nyumbani kuliandaliwa chakula maalum kwa ajili ya kuwashukuru wale wote waliokuwa pamoja naye katika kipindi kigumu cha ugonjwa na matatizo.Ilikuwa ni siku ya furaha kubwa kwa Latoya
Baada ya chakula cha usiku alielekea katika bustani yake iliyo juu ya ghorofa akiambatana na Innocent
“Innocent sijui nianzie wapi lakini naomba nichukue nafasi hii toka ndani kabisa ya moyo wangu nikushukuru sana kwa yote uliyonifanyia.Kwangu mimi nakuona wewe kama malaika wangu uliyetumwa kuja kuniokoa.Bwana Mungu amekutumia kunitoa upotevuni na kunirejesha nuruni.Haikuwa kazi rahisi lakini umepambana bila kuchoka na hatimaye leo hii niko hai bado.Umetimiza maneno yako uliyonitamkia kwamba uko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kunifanya niwe ni mwenye furaha.Ninafuraha sasa.Moyo wangu umejawa na furaha.Maisha yangu yana nuru mpya.Innocent siwezi kupata neno zuri la kuielezea furaha niliyonayo” Latoya akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Katika kipindi hiki kifupi ,nimejifunza kitu kimoja kikubwa.Nimejifunza kwamba maisha ni zawadi ambayo tunapewa na Mungu na kwa hiyo ni hiari yake Mungu kutujalia kuiona kesho.Kwa hiyo basi hatuna budi kuishi kila siku kama siku yetu ya mwisho hapa duniani.Tuishi kadiri ya mapenzi yake Mungu.Tutende matendo mema ,tuwajali masikini na wenye mahitaji na tuenende katika njia iliyo njema.Nimenusurika kifo kwa hiyo ninayafahamu vyema haya niyasemayo.Nilichungulia kuzimu na sitaki tena kurudia maisha yale.Mungu amenipa nafasi nyingine ambayo sitaki kuipoteza hata kidogo.Sitaki tena kumkosea kwani wote wafao bila kutubu dhambi zao hupotea.Kwa maana hiyo basi kuna mambo mawili muhimu ambayo nataka kuyafanya katika maisha yangu mapya.” Latoya akanyamaza akamtazama Innocent usoni na kusema
“Jambo la kwanza ninalotaka kulifanya ni kuzifunga na kuuza biashara zangu zote na fedha nitakazozipata nitazitumia katika kuanzisha biashara ambazo hazitakuwa na machukizo mbele za Mungu.Nitaanzisha makampuni ya kusindika vyakula,dawa za binadamu na nguo.Faida itakayopatikana ,nitaipeleka katika watu watu wenye uhitaji mkubwa wa msaada kama vile nchi zenye vita za wenyewe kwa wenyewe.Katika kambi za wakimbizi,na hata katika nchi zinazokabiliwa na umasikini mkubwa.Mungu anapenda tuutumie utajiri tulionao kwa manufaa ya wengine.Tutajikita vile vile katika miradi ya kuondoa umasikini katika jamii masikini kwa kujenga mashule,mahospitali , na bila kusahau kumjengea bwana nyumba zake za ibada ili watu wengi waweze kumtukuza na kumuabudu yeye pekee.Hili si jukumu dogo lakini nina imani kwa msaada wa Mungu na kwa uwepo wako karibu yangu nitaweza kufanya hayo yote niliyokwambia.Tutazunguka na kutoa misaada sehemu mbali mbali duniani na hivi ndivyo Mungu anataka tuishi.Tuyatoe maisha yetu kwa wenzetu.Tuhubiri upendo kwa vitendo.” Akasema Latoya halafu akanyamaza na kumtazama Innocent
“ Latoya kuna jambo ambalo nadhani bado hujaelezwa.Tulisubiri muda muafaka uwadie ndipo ufahamishwe”
“ Jambo gani hilo Innocent? Kuteketea kwa ofisi yangu? Akauliza Latoya huku akitabasamu
“ Umejuaje kama ofisi yako iliteketea? Akauliza Innocent kwa mshangao
“ Nilionyeshwa ndotoni namna ofisi yangu ilivyoteketea kwa hiyo nafahamu kila kitu.Hizi zote ni hatua za shetani kutaka kuchukua mali na vitu vyake.Mapambano haya yataendelea kila siku na vitu vingi vitapotea lakini mkono wenye nguvu wa Mungu aliye hai utatukinga dhidi ya kila ovu na hila za huyu mwovu.”akasema Latoya halafu kikapita kimya klifupi
“ Innoceht utakumbuka kwamba niliweka ahadi ya kumpata mwanaume wa maisha yangu kabla sijafa ahadi hiyo ikatimia.Innocent wewe ni zawadi kubwa kwangu ambayo kwayo nitaendelea kumshukuru Mungu siku zote.Wewe ni furaha yangu,pumzi yangu,wewe ni maisha yangu wewe ni kila kitu kwangu.Siwezi kuishi bila ya wewe.Wewe ni lulu ya thamani kubwa na kamwe sintakuwa tayari Lulu hii iniponyoke mikononi mwangu.Kwa sababu hiyo basi jambo la pili ambalo nataka kulifanya mapema sana ni kufunga nawe ndoa”
Innocent akaruka kwa furaha
“ OuhLatoya I love you,I love you soo much.” Akasema Innocent wakakumbatiana huku wote wawili machozi yakiwatoka
MIEZI SITA BAADAE
Kila mtu aliyekuwamo ndani ya ufukwe huu alikuwa na furaha ya aina yake.Shangwe na ndremo vilitawala katika ufukwe huu mkubwa uliokuwa umefurika watu wa kila tabaka.Walikuwepo mabilionea wakubwa wa ndani na nje ya nchi,viongozi mbali mbali wa serikali wa ndani na nje ya nchi,wawakilishi wa mashirika mbali mbali ya kimataifa na yale ya binafsi.Ni sherehe iliyowakutanisha watu wa kila tabaka kuanzia mabilionea hadi masikini wa chini kabisa.Kwa muonekano wake ilionekana ni kama sherehe ya kitaifa kutokana na kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu.Hii ilikuwa ni harusi ya kihistoria ya bilionea Latoya na mchumba wake Innocent ambao walifunga ndoa katika kanisa la Mt Patrick na baadae kufuatiwa na sherehe kubwa na ya aina yake katika ufukwe mkubwa unaolizunguka jumba la Latoya ambalo lijengwa upya baada ya kuungua moto.
Ni miezi takribani sita sasa toka Latoya aliponusurika kifo na kuamua kuachana na mtandao wa kishetani na kumrudia Mungu.Baada ya kunusurika aliushangaza ulimwengu pale alipotangaza kufunga na kuuza biashara zake zote .Wengi walimlaumu kwa maamuzi haya lakini hakurudi nyuma.Aliendelea kuushikilia msimamo wake na kufanikiwa kuyauza makampuni yake yote .Kama ilivyokuwa katika mipango yake,fedha alizozipata alizitumia katika kuanzisha makampuni mapya ya kutengeneza vyakula ,madawa ya binadamu na nguo.Aliyasambaza makampuni yake sehemu mbali mbali duniani kwa lengo la kurahisisha utoaji wa misaada kwa watu masikini.Wengi wa watu masikini waliufurahia uamuzi huu wa Latoya na kumuombea maisha marefu.Huu ulikuwa ni mwanzo wa maisha mapya ya bilionea Latoya mwanamke ambaye aliwahi kutumika katika mtandao wa kishetani na kuitwa Black female God kutokana na nguvu na uwezo aliokuwa nao.
Wakati sherehe zikiendelea Innocent akapewa nafasi ya kusema machache
“Ndugu zangu ,wageni waalikwa mabibi na mabwana,nashukuru kwa nafasi hii niliyopewa ya kusema machache.Kwanza kabisa nawashukuru nyote kwa kufika kwenu.Wengi wenu mmetoka katika kila pembe ye dunia kuja kuungana nasi.Latoya na mimi tunasema ahsanteni sana na Mungu awabariki. ” akasema Innocent baada ya kupewa nafasi ya kuongea machache katika harusi yao iliyofurika watu.Makofi mengi yakapigwa halafu akaendelea
“ Jambo la pili ninalotaka kulisema leo ni kwamba ,sote tumeumbwa na Mungu ,anatupenda ,anatujali kwa hiyo hatuna budi kuishi kulingana na maagizo yake.Ametuagiza tupendane kwa hiyo tupendane kama anavyotupenda yeye.Unapompenda mwenzio ,mpende kwa moyo wako wote, na uwe tayari hata kuutoa uhai wako kwa ajili yake.Huo ndio upendo wa kweli ambao tunapaswa kuuishi.Kila moja aliyeko hapa leo hii ajiulize nafsini mwake Je yuko tayari kuyaweka rehani maisha yake kwa ajili ya yule ampendaye? Kama ndiyo basi hongera sana lakini kama bado hauwezi kufanya hivyo kwa ajili ya yule umpendaye badilika sasa na ujitoe kwa ajili ya wale uwapendao.Ahsanteni sana na Mungu awabariki”
Yalikuwa ni maneno machache sana lakini mazito toka kwa Innocent ambaye siku hii ya leo alikuwa amependeza mno.Watu walimshanghilia sana hadi aliporejea kitini kukaa.Ikafuata zamu ya Latoya naye akaombwa aseme machache
“ Ndugu wageni waalikwa ,mabibi na mabwana,kwanza kabisa napenda nimshukuru Mungu kwa kunijalia nafasi hii muhimu ya kusimama mbele yenu na kusema nanyi machace.Tayari mume wangu mpenzi amekwisha toa shukrani zetu kwa kufika kwenu.Ndugu zangu wapendwa tumekusanyika hapa leo kwa sababu Mungu amependa tuwepo hapa.Ametujalia uzima na afya tele.Wengi walitamani sana kuwa nasi siku ya leo mahala hapa lakini hawajaweza kufika siku ya leo.Kwa sisi kuendelea kuishi hadi dakika hii kwanza tunapaswa kumshukuru sana Mungu na pili tunapaswa kuishi kila siku kama siku yetu ya mwisho.Hakuna kati yetu anayejua kama ataiona kesho.Ni Mungu pekee ambaye anajua hatima ya maisha ya kila mtu kwa hiyo tusithubutu kuichezea zawadi hii ya maisha au kuitumia visivyo.Tuitumie vizuri .Umepewa zawadi hii kwa malengo maalum ambayo unatakiwa uyakamilishe kabla hujafa.Kwa hiyo basi jiulize leo What am I suppose to do before I die”What do I want to achieve before I die? Whats my dream before I die? As for me I had a dream.My dream was to find a man of my life,a man that I’ll will love deeply with all my heart.Here I am today,standing before you proudly thanking God for helping me achieve my dream before I die.I’ve married a man that I love with all my heart.A man of my dream,a man that is worth to die for.” Makofi mengi yakapigwa halafu akaendelea
“ Kwa hiyo ndugu zangu tujenge tabia ya kujikumbusha kwamba siku moja tutakufa lakini tuzoee kujikumbusha vile vile kwamba nini ni ndoto zetu za kuzitimiza kabla hatujafa.Kila siku asubuhi unapoamka na kabla ya kulala usiku hili ndilo liwe neno lako kuu la kufikiria “ BEFORE I DIE” Asanteni sana”
Makofi mengi sana yakapigwa.Shangwe kubwa ikasikika wakati Latoya akirejea kuketi.Sherehe zikaendelea hadi saa nne za usiku ambapo Innocent na Latoya wakaondoka wakaeleeka hotelini na kuwaacha bado watu wakiendelea kusherehekea
“ Latoya katika ile hotuba yako fupi,umenifundisha jambo kubwa sana.Ni hotuba iliyokuwa na msisimko mkubwa.Kwa sasa baada ya kwamba tumekwisha kuwa mwili mmoja tujiulize na sisi whats our dream before we die?
Latoya akatabasamu na kusema
“we have lots of dreams but the first one is to make love all night long.Ouh Innocent I’m dying to be in your arms..Please take me to the moon” akasema Latoya kwa sauti laini .Bila kutaka maongezi zaidi Innocent akamvuta Latoya karibu yake na kumpagawisha kwa mabusu mazito mfululizo na kumfanya aanze kuweweseka.Innocent akaendelea kumtomasa sehemu mbali mbali za mwili wake na kumfanya Latoya apandwe na uchizi kutokana na raha aliyokuwa akiisikia.Hatimaye walishindwa kuvumilia na mara wakajikuta wakiogelea katika bahari pana sana ya mapenzi yenye raha isiyoelezeka.Kilichosikika humo chumbani ni vilio na miguno ya kimahaba.Latoya akaingizwa rasmi katika ulimwengu wa mahaba.Mwanzo mpya wa maisha yake akiwa na mwanaume ambaye aliweka ahadi ya kumpata kabla ya kufa kwake na tayari amekwisha mpata.
TAMATI