Simulizi - change (badiliko)

CHANGE

Story by Elton Tonny

Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha

R-rated 18+


MUHTASARI MFUPI.....

Ndani ya wakati uliopo baada ya kujua historia ya maisha yake Namouih kabla hajaolewa na Efraim Donald. Ikiwa ndiyo usiku wa siku ambayo Efraim Donald alikuwa amerudi nyumbani baada ya kutoka safarini, haikuwa imechukua muda mrefu vya kutosha kumkwaza mke wake baada ya yeye kutotaka wapeane mahaba kwa kusema amechoka. Namouih kiukweli hakuweza kumwelewa Efraim vizuri. Tabia hii ilikuwa imeendelea kwa muda mrefu sasa, na mwanzoni ni kweli mwanamke huyu alihitaji muda kutokana na mambo mengi magumu aliyopitia kihisia, lakini kwa wakati huu alikuwa anamwonyesha wazi kabisa kwamba anataka kumpatia mapenzi kwa kuwa vidonda vyake vimepona, ila Efraim Donald akawa anampiga chini. Sasa hili jambo lingeendelea kuwa hivi mpaka wakati gani?

Asubuhi ya siku iliyofuata, Namouih kama kawaida aliamka na kujiandaa kwa ajili ya kazi, na wakati huu hakuwa amesumbuliwa na ndoto mbaya kama ile ya siku iliyotangulia. Efraim Donald akatokea huko juu chumbani Namouih alipokuwa mbioni kumalizia chai. Mwanaume akakaa kwenye kiti chake mezani hapo, huku akiuliza ni mambo gani ambayo Namouih angeshughulikia leo. Yaani alifanya ionekane ni kama hakukuwa na tatizo kabisa, na kwa sababu Esma alikuwa amefika hapo kumwekea vyombo kwa ajili ya chai, Namouih akaona amjibu tu kwa ufupi, akisema anaenda kumtetea msichana kwenye kesi ya ubakaji akiwa na Blandina.

Efraim Donald akampongeza na kupendekeza kwamba wamwalike Blandina leo jioni, aje kupata chakula pamoja nao kwa kuwa alimkumbuka sana rafiki yake huyo. Angalau hii ilifanikiwa kumfanya Namouih atabasamu, naye akasema angemwambia. Namouih alifika eneo la mahakama muda mfupi baadaye na kukuta watu kadha wa kadha wakiwa wameshafika, na Blandina tayari alikuwa hapo pia, lakini mwanasheria aliyetakiwa kumsimamia kijana mwenye tuhuma za ubakaji hakuwa amefika mpaka wanaingia ndani. Namouih akamuuliza ikiwa alikuwa ana taarifa yoyote kuhusu mwanasheria mpya wa Japheth, lakini rafiki yake akakanusha. Hata hakimu alipomuuliza Japheth mwanasheria wake alikuwa wapi, kijana huyu akatoa jibu lisilokuwa la uhakika.

Namouih akawa amekerwa sana na usumbufu wote huo alioona tokea mwanzo kabisa kwamba ungewafikisha huku. Kujiandaa kote halafu mtu anashindwa kuonyesha msimamo ni jambo lililomfanya akerwe sana, ndipo...

"Samahani mheshimiwa... samahani kwa kuchelewa..."

Wote waliokuwa hapo wakageuka nyuma baada ya kusikia maneno hayo yakisemwa kwa sauti ya juu na mwanaume fulani aliyeingia ndani hapo. Blandina aligeuka vizuri zaidi na kubaki amemwangalia kwa umakini sana, naye Namouih alipogeuka na kumwona, akabaki kumtazama kwa umakini pia kadiri alivyoendelea kupiga hatua kuelekea mbele. Walimfahamu. Alikuwa ndiyo yule yule kijana ambaye asubuhi ya siku ya Jumapili wakati wawili hao walipotaka kwenda kumpa pole rafiki yao, yule Mwantum, Blandina alijigonga kwake na kupasua chupa, kisha mwanaume huyo akamnunulia nyingine na kuchukua namba zake; yaani Draxton!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA SABA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Mwanasheria? Mwanaume huyo kijana mwenye sura nzuri, mwili imara wa kuvutia mwanamke yeyote yule, na pigo za kibabe kama siyo usharobaro, Draxton alikuwa ni mwanasheria? Blandina akamtazama Namouih machoni kwa njia ya mshangao, naye Namouih akamwangalia rafiki yake kwa ufupi kisha akamkazia macho mwanaume huyo.

"Kulikuwa na jam kidogo mheshimiwa... samahani sana kwa kuchelewa..."

Mwanaume huyo akasema hayo, akionekana nadhifu zaidi tofauti na jinsi alivyoonekana mara ya kwanza alipokutana na marafiki hawa wawili siku ile.

"Wewe ndiyo mwanasheria wake Japheth Warioba?" hakimu akamuuliza.

"Ndiyo, mimi ni mwanasheria wak...."

Mwanaume huyu alikuwa amefikia mbele zaidi, kwenye kimlango kidogo kilichopatenganiaha kule mbele na sehemu za mabenchi huku nyuma, naye akaishia hapo na kusimama kwanza. Namouih alimwangalia na kuona anainamisha uso wake kidogo kama vile anavuta hisia fulani hivi, halafu akageukia upande aliokaa Namouih na kumtazama machoni moja kwa moja. Alimwangalia Namouih kwa macho fulani hivi kama ya udadisi, ukali, yaani kama vile mtu anayejiuliza "huyu anafanya nini hapa," naye Namouih akamshusha na kumpandisha kisha akatazama mbele kwa njia iliyoonyesha hakumjali.

"Ningependa kuona utambulisho wako tafadhali," hakimu akasema hivyo.

Mwanaume huyu akaacha kumwangalia Namouih na kusema, "Bila shaka," kisha akavuka kimlango cha hapo na kwenda kumpa msomaji utambulisho wake yeye kama mwanasheria, halafu akasimama pembeni yake Japheth. Namouih alikuwa anamwangalia sana, hata Blandina alipigwa na butwaa kwa kweli, yaani hakutegemea.

Hakimu alipoona uthibitisho wa utambulisho wa mwanasheria huyo, akatamka kwa sauti, "Maximilian Draxton."

Hilo ndiyo lilikuwa jina lake. Draxton akatikisa kichwa kukubali, kisha hakimu akamrudishia msomaji utambulisho huo naye akaupeleka kwa mwanasheria huyo wa Japheth. Akaulizwa kwa nini hakuwa amevaa joho la mwanasheria, naye Draxton akamwambia hakimu kwamba lilisahaulika tu kwa sababu ya haraka yake kuja huku. Hivyo akatendewa tu kwa fadhili na mahakama kwa kupewa vazi kama hilo la ziada, kwa sababu ndiyo jinsi utaratibu wa mahakama ulivyokuwa; lazima kuvaa joho.

Mwanasheria huyu akalivaa hapo hapo na kuketi pembeni yake Japheth, na kijana huyu alionekana kutulia zaidi baada ya ujio huu wa Draxton. Sasa kulikuwa na hali ya utulivu zaidi, naye hakimu akaruhusu majibizano ya kesi a.k.a trial, yaanze. Taratibu hii huanza rasmi kwa mwanasheria wa mtoa mashtaka kutakiwa kutoa utangulizi wa mwanzo kuhusu mambo hakika ya kesi hiyo. Namouih akasimama na kuanza kuelezea jinsi kisa cha Agnes kilivyokuwa.

Binti huyu aliitwa Agnes Mhina, umri miaka 19, na alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na kijana aliyekwenda kwa jina la Japheth Warioba mwenye miaka 26. Mapenzi yao yalidumu kwa miezi isiyopungua 16, yaani karibia mwaka mmoja na nusu, na baada ya hapo, kama Agnes anavyodai, kukatokea hali ya kutoelewana baina yao, na hivyo binti huyo akaamua kuachana naye. Lakini huyo kijana wa kiume hakulichukulia suala hilo kirahisi, na kwa sababu ya ubinafsi akamlazimisha binti huyo kufanya mapenzi kwa njia yenye jeuri kubwa sana iliyomuumiza msichana. Huu ulikuwa ni ubakaji haijalishi hali ya uhusiano waliokuwa nao kabla, kwa sababu Agnes aliingiwa kinguvu na mwanaume huyo kijana bila ya yeye kutaka. Ushahidi wao wenye nguvu zaidi ulikuwa ni karatasi za vipimo kutoka kwa daktari zilizoonyesha kwamba kweli Agnes alibakwa, lakini pia kulikuwa na video kutoka kwenye kamera iliyotegeshwa ambayo ilichukua tukio hilo; sauti za Agnes na Japheth zikisikika vyema ndani yake.

Baada ya kuelezea hayo, Namouih akaketi, kisha hakimu akamuuliza mwanasheria wa mtuhumiwa kama naye pia alitaka kutoa utangulizi kwa upande wake, lakini Draxton akakanusha. Hii ilimfanya Namouih acheke kimoyomoyo kwa sababu aliona ni kama jamaa alikuwa hajui anachokifanya, kwa hiyo hakimu sasa akasema ulikuwa muda wa kuita mashahidi. Upande wa mtoa mashtaka, yaani Agnes, kulikuwa na mashahidi wanne tu ambao walitosha kabisa; mama yake Agnes, askari aliyemkamata Japheth, rafiki wa karibu wa Agnes aliyeitwa Mamu, na daktari aliyefanya vipimo vya Agnes. Upande wa mtuhumiwa Japheth haukuwa na shahidi hata mmoja, kwa hiyo ingetakiwa baada ya Namouih kuwahoji mashahidi wake, Draxton awahoji pia.

Mmoja baada ya mwingine wakaitwa na Namouih, naye akawauliza maswali mengi vizuri na kwa njia ambazo zilitokeza majibu yaliyoonyesha kwamba kweli janga lile lilimkuta Agnes. Mama yake alidai kwamba siku hiyo Agnes hakurudi nyumbani kabisa. Askari aliyemkamata Japheth siku tatu baada ya tukio akasema alimshika Japheth akiwa nyumbani kwao. Mamu akasema siku ambayo Agnes alibakwa, rafiki yake huyo alikwenda "getoni" kwake na kulala, na alimsaidia kupunguza maumivu sehemu zake za siri kabla ya kwenda kwa daktari. Daktari akasema kwamba kweli kama majibu yalivyoonyesha, binti alichubuka sana sehemu za siri, na hiyo ingesababisha vidonda, akikazia kuwa bila shaka Japheth alitumia jeuri ya kinyama.

Blandina alikuwa anamwangalia Draxton. Jinsi mwanaume huyo alivyokuwa ameweka umakini wake wote kule mbele, yaani ilikuwa kwa njia kuu sana, iliyomwambia kwamba hapo alikuwa na jambo lake muhimu. Baada ya Namouih kumaliza kuwahoji mashahidi wake, akarudi kukaa akiwa amewaambia waamuzi kwamba kutokana na hayo yaliyosemwa ni wazi kabisa kwamba upande wake ndiyo uliokuwa "mwathirika."

Sasa ikawa zamu ya mwanasheria wa mtuhumiwa kuwahoji mashahidi wale wale wa upande wa mtoa mashtaka. Draxton akanyanyuka na kwenda hapo mbele, na kila mtu alitulia sana ili waweze kuona kama angeweza kuweka mambo kuendana na njia ya Namouih ya kuzungumza bila hofu yoyote. Namouih na Blandina walikuwa wanamtazama kwa umakini pia.

Akaanza kumhoji mama yake Agnes, kisha akafata Mamu. Alikuwa na njia fulani hivi ya taratibu ya kuzungumza, iliyofanya aonekane kuwa mtu makini lakini aliyejua sana kucheza na akili. Aliuliza maswali kwa njia ambazo mwanzoni yangeonekana kutokuwa muhimu kabisa, lakini mwishoni angeyarudia kwa njia tofauti iliyowakosoa mashahidi hao na kuwaacha wakiwa wamechanganyikiwa. Mama ya Agnes na Mamu, wote walifika hatua ambayo hawakuweza kuendelea kuongea kutokana na kushindwa wajibu nini, na Draxton akawaruhusu tu warudi kukaa. Askari aliyemkamata Japheth aliongea kwa njia nzuri na ya uwazi kabisa kwa kujibu maswali yote bila kuchanganya mambo, naye akarudi kukaa pia.

Kisha sasa akaingia daktari wa Agnes. Draxton akauliza majina yake, amesoma wapi, alifanyia kazi wapi, na ikiwa aliamini kwamba umri wa Agnes ulimruhusu kuwa na mahusiano. Akaanza kuulizia wakati ambao vipimo hivyo vilichukuliwa, na ikiwa ni kweli kwamba binti alikuwa na michubuko basi ingesababisha vidonda ambavyo mpaka kufikia wakati huu bado vingekuwepo, na kwa kuwa ripoti hiyo ya vipimo ilitoka kwenye maabara yake binafsi, Draxton akapendekeza wachukue vipimo kwa mara nyingine tena, na wakati huu iwe ni kwa misingi ya mahakama ndani ya hospitali kubwa kabisa na siyo kwa hiyo ripoti kutoka maabara ambayo ilikuwa imeshatengenezwa tu haraka.

Namouih alipinga vikali hoja zake, akisema huo wote ungekuwa ni usumbufu kwa kuwa mbali na majibu ya vipimo hayo kuja yakionyesha ni kweli Agnes alibakwa, kulikuwa na ushahidi wa ile video ambayo ndiyo ilikuwa inakata maneno yote hapo. Daktari alikuwa amebaki kimya tu, hivyo Draxton akamwambia akakae Ili ashughulikie suala la video hiyo kwa kumhoji mtoa mashtaka mwenyewe, yaani Agnes. Hali ndani hapo ilikuwa imeanza kuwa rusha roho, kwa kuwa ilianza kuonekana kwamba Draxton anataka kufichua jambo fulani zito sana, lakini kila mtu alitaka kuona haya yote yangeishia wapi.

Mwathiriwa akapanda kizimbani hatimaye, na alikuwa binti mmoja ambaye kwa kumtazama tu ungesema ana nyodo sana, ila kwa hapo alikuwa anaonyesha unyonge wa hali ya juu. Draxton akamkaribia na kumpa tabasamu hafifu, huku Agnes akimtazama kwa njia fulani hivi ya kujihami.

"Mambo?"

Draxton akatoa salamu hiyo kumwelekea Agnes, kwa njia ya kirafiki kabisa. Namouih alikuwa ameshakerwa naye sana kufikia hapo ila basi tu, hakuwa na jinsi. Baada ya Draxton kuanzisha maswali kuhusu utambulisho wake Agnes, shule, kama alifanya kazi, muda aliokuwa kwenye uhusiano na Japheth, hata mara ambazo alifanya naye mapenzi, sababu ya kutoelewana kwao, na mambo mengine, akafikia swali hili:

"Ulimwambia nani kwanza baada ya jambo unalosema lilikupata kukupata?"

"Mamu..."

"Oh, siyo mama, ni Mamu?"

"Ndiyo..."

"Baada ya hapo ndiyo mkaenda kwa askari?"

"Ndiyo..."

"Na mkaulizwa maswali mengi kuhusiana na yaliyotokea?"

"Ndiyo..."

"Majibu yako yote kwa wakati huo yanafanana kabisa na kisa chote kilivyotokea usiku unaosemwa uliingiwa vibaya kimwili?"

"Napinga kauli mheshimiwa. Anauliza vitu visivyokuwa na uendani wowote kwenye ushahidi uliotolewa," Namouih akamwambia hakimu.

"Pingamizi limekataliwa," hakimu akasema.

Namouih akakaa na kuangalia pembeni kwa kukerwa.

"Unafikiri kwamba ikiwa uchunguzi ungefanywa kwa wakati huu kwa mara nyingine tena, kila kitu kinachodaiwa kuwa kimeshatokea kitaonekana kuwa ni kweli au uwongo?" Draxton akauliza.

Agnes akabaki kimya.

"Unajua utofauti uliopo kati ya kile ambacho watu wataamini kwa kuwa ni ukweli, na kile ambacho wanaamini kwa sababu wanafikiri wanaujua ukweli?"

"Napinga kauli mheshimiwa, ni mambo yasiyopatana na ushahidi," Namouih akaingilia kati.

"Pingamizi limekubaliwa," hakimu akasema.

Draxton akaendelea kumchimba Agnes....

"Okay, kwa hiyo ulisema kwamba siku hiyo mlikuwa wapi... motel... au lodge?"

"Lodge..."

"Jina la hiyo lodge?"

Agnes akabaki kimya.

"Haujui jina la hiyo lodge? Unalijua? Hulikumnuki? Unalikumbuka?"

"Napinga kauli mheshimiwa, anauliza maswali na kujijibu mwenyewe," Namouih akasema.

"Pingamizi limekataliwa..." hakimu akasema.

Draxton akaendelea...

"Mlikuwa na kawaida ya kukutana kwenye lodge eh?"

"Hapana..."

"Ilikuwa kwa siku hiyo tu?"

"Ndiyo..."

"Unajua kuwa kuitana mpaka kufika lodge inamaanisha kwamba ulikwenda kwa kupenda, siyo kwa kulazimishwa, endapo kama tayari mlikuwa mmeshaachana kwa kutoelewana?"

"Napinga kauli mheshimiwa...."

"Pingamizi limekataliwa. Maximilian endelea," hakimu akamkatisha Namouih.

"Elezea ilivyokuwa mpaka ukakubali kukutana naye lodge siku hiyo..."

"Ali... alinipigia simu, akaniomba sana tukutane kwa sababu alisema anataka kuniomba msamaha, ndiyo nikaenda halafu akanifanyia hivyo," Agnes akasema.

"Mwongo! We' ni mwongo!" Japheth akapayuka kwa sauti ya juu, naye akaambiwa atulie na kuiheshimu mahakama.

"Okay, kwa hiyo ukaenda lodge. Bila shaka lodge huwa zina watu ndani... na mtu wa mapokezi. Kwenye maelezo yako kwa askari ulisema Japheth alikulala kinguvu kwa muda usiopungua dakika 20 kufikia 30. Lodge hapo. Hakuna yeyote aliyesikia labda unapiga kelele au..."

"Aliniziba mdomo," Agnes akaongea upesi.

Namouih akakaza macho kwa mshangao. Hii ilikuwa kwa sababu fulani ambayo aliitambua haraka, na Draxton angeifunua muda siyo mrefu.

"Alikuziba mdomo. Kwa hiyo hakuna sauti yoyote iliyosikika, si ndiyo? Hamna mtu ambaye angeweza kuja kukusaidia eeh?"

Agnes akatikisa kichwa kukubali, bila kuelewa kwamba alikuwa amejikanyaga.

"Okay, sasa ndiyo tutaingia kwenye suala la video. Kwa hiyo... video iliyochukuliwa ilitokana na kifaa gani?" Draxton akauliza.

"Simu..."

"Simu ya nani?"

"Yangu."

"Uliitegesha wakati gani?"

"Nilipofika hapo."

"Hapo Lodge? Aah... kumaanisha wa kwanza kufika ilikuwa wewe? Kwa hiyo aliyelipia chumba ni wewe?"

"Alilipia yeye... angelipa baadaye..."

"Lodge... okay. Kwa hiyo ukaitegesha camera, halafu ndiyo akaja, toka amefika camera tayari ilikuwa inarekodi kila kitu, si ndiyo? Ulikuwa umeitegesha tu ili lolote ambalo lingetokea ije kuthibitika baadaye kwamba kweli lilitokea?"

"Pingamizi mheshimiwa, anauliza na kujijibu," Namouih akasema.

"Pingamizi limekubaliwa..." hakimu akasema.

"Okay. Kwa hiyo maongezi ya kuombana msamaha yakageuka kuwa show ya ubakaji... kwa nini?" Draxton akauliza.

"Alikuwa ananilazimisha me nikakataa... nikamwambia nataka kwenda nyumbani, mimi na yeye basi... lakini akanilazimisha... akanivuta kitandani akani... akanivua..."

Japheth alikuwa anatikisa kichwa huku akimtazama Agnes kwa njia iliyoonyesha hasira sana.

"Ilikuwa ni siku ya shule au weekend?" Draxton akamuuliza Agnes.

"Ilikuwa... ilikuwa siku ya shule... juma ngapi sijui..."

"Ulimuaga mama unaenda wapi?"

"Kwa rafiki yangu."

"Ilikuwa saa ngapi?"

Agnes akabaki kimya.

"Saa tatu? Saa nne? Usiku wa manane?"

"Pingamizi mheshimiwa, anauliza na kujibu..."

"Pingamizi limekataliwa..." hakimu akamkatisha tena Namouih.

Draxton akauliza, "Kwa hiyo, alipoanza kukugusa na kukuvuta kitandani, hukupiga kelele?"

"Nimekwambia aliniziba mdomo," Agnes akajibu kwa kukerwa.

Namouih akainamisha uso wake na kutikisa kichwa kwa kusikitika.

"Okay, hapo hapo, kwa mara nyingine tena, unasema alikuziba mdomo, si ndiyo? Sauti zinazosikika kwenye video uliyorekodi zilitoka wapi?" Draxton akauliza.

Agnes akabaki kinywa wazi na kushindwa kutoa jibu.

"Ni wewe mwenyewe ndiye uliyefika kwenye lodge, ukategesha simu yako kwa camera, si ndiyo?"

Kimya.

"Ulipanga hii yote Agnes, siyo?"

Kimya.

"Kwa hiyo Japhet alipofika, mkayajenga, au mkayavuruga? Kwenye video inaonyesha ukiwa tupu kabisa huku chini, alifika mkagombana tena lakini akawa na muda wa kukuvua nguo huku amekuziba mdomo? Ulivaa gauni tu usiku huo? Hukuvaa nguo yoyote ya ndani?"

"Pingamizi mheshimiwa..."

"Limekataliwa..."

"Ulivaa nguo ya ndani? Hukuvaa?"

"Nilivaa!" Agnes akasema huku machozi yakianza kumtoka.

"Oh, kwa hiyo tukiiangalia video tena tutaona nguo yako ya ndani inaondolewa, si ndiyo?"

Kimya.

"Mara ya mwisho umeangalja hiyo video ilikuwa lini Agnes? Hautakiwi kusikika ukilia kama ilivyo kwenye video kwa kuwa alikuziba mdomo wako, si ndiyo? Hizo sauti kwenye video ni kutokea wapi sasa? Haupigani naye kabisa, miguu iko juu vizuri tu, si ndiyo? Ulimfungulia miguu yako we' mwenyewe si ndiyo? Ndiyo kilichotokea usiku huo, lakini sasa hivi tuna mambo mengine kabisa, siyo? Majibu ya vipimo yalikuwa yako au ya nani sasa? Ikiwa siyo yako daktari ameyatoa wapi...?"

Agnes akatazama upande wa mabenchi kule nyuma.

"Kwa nini umemwangalia daktari?" Draxton akamuuliza, bila yeye kuwa amegeuka nyuma.

Agnes akamwangalia huku pumzi zake zikiongezeka kasi.

"Unaweza kuwaambia waamuzi sababu inayokufanya ushindwe kutoa majibu? Ni kwamba hukumbuki vizuri kilichotokea au? Unakumbuka? Haukumbuki? Unakumbuka lakini ni kwamba haujui?"

Agnes akiwa kama shahidi mkuu hapa akashindwa kutoa majibu na kuendelea tu kulia.

Draxton akaendelea kuuliza, "Unakumbuka kwamba umetoa kiapo cha kusema ukweli tu, na ukweli mtupu? Unajua ni nini kitakupata ikigundulika umedanganya chini ya kiapo?"

"Pingamizi mheshimiwa... anamsukuma shahidi kupita kiasi," Namouih akaingilia kati.

Hakimu akatulia kidogo, kisha akasema, "Pingamizi limekubaliwa."

Draxton akaendelea kuuliza maswali kama hayo bila kumpumzisha Agnes afikirie hata mara moja. Watu wote walikuwa wanaangaliana na kusikika wakinong'ona, kwa kuwa itikio la Agnes lilionyesha wazi kwamba alikuwa njia panda. Namouih akamtazama sana Agnes, akishindwa kuamini kama kweli kuna mwanamke angeweza kudanganya kuhusiana na jambo kama hilo, kwa sababu ilikuwa wazi kwa yeyote hapo kwamba binti alikuwa amedanganya. Akaendelea kulia tu akiwa kizimbani hapo, hivyo Draxton akamwambia hakimu kwamba alikuwa amemaliza maswali yake, naye angependa kutoa maoni yake ambayo alikuwa ameamua kusubiri mpaka wakati huu ili aweze kuyasema.

Akawaambia waamuzi kuwa mambo mengi kuhusiana na tuhuma za tukio hilo yalitakiwa kufanyiwa uchunguzi kwa mara nyingine tena. Sawa ushahidi walikuwa nao, lakini alitaka wahakikishe kabisa kwamba ushahidi huo uliokuwa halali vinginevyo wangejikuta wanatoa uamuzi wa kumfunga kijana asiyekuwa na hatia. Alielewa kwamba hii ndiyo iliyokuwa mara ya mwisho ya usikilizaji wa kesi hii kabla ya hukumu, lakini katika siku hizo chache mpaka kuifikia tarehe yenyewe, wangekuwa wameshapata uthibitisho wa kuaminika zaidi. Kwanza, Agnes afanyiwe vipimo kwa mara nyingine tena, na pili, video ile ichunguzwe vizuri badala ya kufikia mikataa isiyo ya kweli kwa kuwa tu "sauti zao zilisikika."

Baada ya hapo, mwanasheria Draxton akaenda kukaa kwenye kiti pembeni yake Japheth. Ilikuwa ni wonyesho mzuri sana wa stadi ya kazi, na aliifanya ionekane kuwa rahisi sana ingawa ilikuwa jambo gumu kufichua mambo kwa njia aliyotumia. Namouih akabaki kimya tu baada ya Agnes kurudi kutoka kizimbani na kukaa pembeni yake, akijiona kama mpuuzi kwa kiasi fulani, ingawa bado moyo wake haukutaka kukubali kwamba Agnes alikuwa amedanganya. Akamwambia kwa uhakika kwamba asijali sana kuhusu maneno yenye kuchanganya ya mwanasheria yule, kwamba bado upande wao ulikuwa na nguvu zaidi.

Binti huyo alikuwa amejikanyaga kweli kwenye sehemu ile ya kuzibwa mdomo, na ikawa wazi kwamba kisa hiki chote kilikuwa ni uwongo mkubwa sana, ingawa bado hukumu haikuwa imetolewa. Hakimu akamuuliza mwanasheria wa mtoa mashtaka ikiwa alitaka kuhoji mashahidi kwa mara nyingine tena, lakini Namouih akakanusha. Hivyo akawaomba wanasheria watoe kauli zao za hitimisho baada ya hayo, naye Namouih akasimama tena na kutoa maoni yake, akifuatwa na Draxton ambaye alikazia tena mambo aliyokuwa amesema.

Baada ya hapo, kundi la waamuzi 6 (jurors) likaingia kwenye chumba kingine kutoka sehemu hiyo ili wajadiliane kwa ufupi kuhusu mambo yote hayo, wakiwaacha watu wanasubiri warudi ili kujua wamefikia mkataa gani. Wakati huu, Namouih alikuwa anaongea na Agnes, akitaka kujua kwa nini ilionekana kama binti amedanganya tokea mwanzo, lakini akawa anasema hakudanganya bali mwanasheria yule mwingine alikuwa amemchanganya tu. Namouih akamwambia kama kila kitu alichosema kilikuwa kweli basi kingepatana na ushahidi uliokuwepo, kwa hiyo wangepaswa kusubiri tu.

Blandina alikuwa ameelekeza zaidi fikira zake kwa Draxton. Mwanaume huyo alikuwa ameonyesha akili nzuri sana hapo, lakini kilichokuwa akilini mwake Blandina ilikuwa kwa nini, baada ya kumpa namba zake na kuahidiwa kwamba angetafutwa, hakuwa ametafutwa. Alikuwa anatamani hata amfate hapo hapo amuulize, lakini akaamua kuvunga tu kama vile hamjui. Muda mfupi baadaye, waamuzi wale wakatoka tena baada ya kufanya mazungumzo yao, kisha hakimu akapelekewa karatasi iliyokuwa na mambo waliyotoka kuandika baada ya kufikia makubaliano.

Hakimu akasema kwamba kutokana na mambo yote hapo, uamuzi uliofikiwa ulikuwa kupitia ushahidi huo kwa uhakika zaidi wakati huu, hivyo Agnes angefanyiwa vipimo tena, na video ile ingechunguzwa vyema ili kuona uhalali wa madai yake kwa asilimia zote. Akasema taratibu hizo zingeanza leo leo, kwa hiyo hakukuwa na haja ya kuweka tarehe ya mbali sana kuja kusikiliza hukumu; kesho hiyo hiyo mida ya saa saba ndiyo hukumu ya kesi hii ingesomwa. Baada ya kusema hayo, akagonga nyundo yake ya mbao pale mezani, kisha akaondoka, na watu wakaanza kunyanyuka pia huku wakiendelea kuliongelea sana jambo hilo.

Japheth akarudishwa na askari wake mlinzi kule alikopaswa kufungiwa, huku ndugu zake wakibaki kuzungumza na mwanasheria wake. Namouih akatoka nje pia pamoja na Agnes na mama yake kuzungumza naye, kwa kuwa sasa ilionekana kweli kwa upande wa dada huyu kulikuwa na jambo lenye nuksi, na hivyo akawa anataka kujua ikiwa hakupewa taarifa za kutosha. Lakini Agnes akamhakikishia na kuendelea kumhakikishia kwamba upande wake ndiyo uliokuwa umeonewa, na akazidi kumwomba Namouih ampiganie kwa nguvu zote ili haki itendeke kweli.

Blandina alikuwa anasubiri sehemu ya mwingilio wa jengo hilo la mahakama, na aliyekuwa akisubiriwa ni Draxton. Alitaka sana kuzungumza naye hasa kuhusiana na ni kwa nini hakuwa amemtafuta kama alivyokuwa amemwahidi. Haikuchukua muda mrefu sana na watu wa familia ya Japheth wakatoka na kuondoka. Blandina akawa anasubiri kwa hamu sana mwanaume yule atoke pia, lakini akawa anakawia. Hivyo akaamua kurudi ndani na kuangalia alipokuwa, naye akamwona akiwa amesimama na mmoja wa waamuzi wale, ambaye alikuwa mwanamke wa miaka kama 40 hivi, na alionekana kuzungumza naye kwa shauku sana kuonyesha ni kama walifahamiana vizuri.

Akaendelea kumsubiri tu bila kujionyesha, na sasa mwanamke huyo akaonekana akichukua simu ya Draxton na kuandika jambo fulani hapo; makisio ya Blandina ikiwa ni namba za simu. Blandina akazungusha macho yake kwa kukerwa sana na jinsi mwanamke huyo alivyoonyesha kujitongozesha waziwazi, na ni hapa ndiyo akaanza kumwona Draxton anakuja upande wake ili aondoke bila shaka, naye akaanza kumfata pia.

Blandina alipomfikia karibu akasema, "Habari yako mheshimiwa... Maximilian Draxton?"

Draxton akatabasamu kwa mbali na kubaki amemwangalia tu.

"Lipi litafaa zaidi kukuita? Maximilian au Draxton?" Blandina akauliza.

"Draxton," mwanaume akajibu.

"Ndiyo ulikuwa unapiga sound kwa jury hapo au we' ndiyo ulikuwa unapigwa sound?" Blandina akauliza.

"Alikuwa ananisalimu kwa kuwa ni siku nyingi hajaniona," Draxton akamwambia.

"Salamu hadi kupeana na manamba, au siyo? Na mimi je? Tusingekutana leo ndiyo ningesahaulika kabisa eti?"

"Ona... najua sikukutafuta, ila ni kuwa... mambo mengi yaliingiliana..."

"Kuingiliana kumaanisha tokea mwanzo ulijua sisi tuko timu pinzani kwenye hii kesi eeh? Ndiyo maana ukaona unikwepe?"

"Si hivyo. Samahani Blandina," Draxton akasema kwa upole.

Blandina akatabasamu kidogo. "Em' niite hivyo tena," akamwambia.

Draxton akaangalia chini na kusema, "Blandina," kisha akamwangalia tena.

"Nikifikiri ungekuwa umeshasahau na jina langu," Blandina akasema.

"La. Nilikuwa tu busy kutafiti vitu vingi, muda ukanimeza," Draxton akamwambia.

Blandina akacheka kidogo na kusema, "Naonekana kama kupe sana eh? Kama niko desperate mno kutafutwa nawe yaani..."

"La."

"Usijali Draxton. Mimi haitakuwa na shida sana kwangu... ukiniambia tu kwamba hauwezi kupata muda kwa ajili ya...."

"No, si hivyo, I swear," Draxton akamkatisha huku akimsogelea karibu zaidi.

Blandina aliipenda sana hali hii kwa kuwa ilimfanya atambue kwamba mwanaume huyu alikuwa na mwelekeo wa kujali hisia za wengine.

"Ona, sitaki uhisi vibaya... na sikuwa na nia ya kukuacha kwenye mataa..."

"Lakini ukafanya hivyo..."

"Am sorry. Niambie ungependa nifanye nini ili kutoa kama... apology," Draxton akamwambia.

"Ni rahisi sana kwenu kusema maneno kama hayo, ila kuyatimiza sasa..."

"No, niambie. Chochote kile ambacho kitakuwa ndani ya uwezo wangu, nitafanya."

"Kweli?"

"Usiniombe gari lakini..."

"Ahahahaa... okay. Nataka unipeleke out."

"Sawa. Ungependa twende wapi? Au... me ndiyo nichague sehemu?"

"No, mimi ndiyo nachagua..."

Draxton akatabasamu kwa mbali.

"Nina wazo zuri la sehemu ya kwenda. Utatakiwa unipitie mida ya jioni ili twende huko, nataka uwe kama..."

"Date wako?" Draxton akamalizia maneno ya Blandina.

"Nilikuwa sijafikiria huko ila, inasikika vizuri," Blandina akasema.

"Sawa. Tutachekiana baadaye," Draxton akasema.

Blandina akacheka kwa chini huku akitikisa kichwa kuonyesha haamini.

"Vipi?" Draxton akauliza.

"Nahisi ni kama nitapaswa kujiandaa kwenda mwenyewe tu," Blandina akamwambia.

"La, tutaenda pamoja. Niamini," Draxton akasema kwa umakini.

Blandina akabaki kumtazama sana machoni, kama vile anauona uthibitisho wa asilimia mia moja kwamba maneno ya mwanaume huyo yalikuwa ya kweli kabisa kupitia utizami wake.

"Umeniamini?" Draxton akaongea.

"Nitaamini zaidi ukifika kweli. Lakini, utajua vipi niko wapi?" Blandina akauliza.

"Kuna app fulani ya kujua maeneo ninayo... naangalia namba yako ya simu ilipo then nakufikia. Kwa hiyo... usizime simu," Draxton akamwambia.

Blandina akatabasamu kwa njia fulani hivi kuonyesha hisia nzuri kutokana na kupenda namna mwanaume huyo alivyoongea.

"Nitakupigia. Mida ya jioni, sawa?" Draxton akasema.

Blandina akatikisa kichwa kukubali, naye Draxton akampita na kuondoka.

Mwanamke huyu alibaki hapo akimtafakari kiasi. Kuna upande fulani kumhusu Draxton uliomvutia sana, na hali ya kiutu aliyokuwa nayo ilimfanya Blandina atamani sana kujiingiza kwenye maisha yake, kwa sababu ya hali fulani isiyoelezeka alimwona kuwa tofauti na wanaume wengine aliowafahamu. Akatoka hapo pia na kuelekea nje, na sasa Namouih alikuwa amesimama pembezoni mwa gari lake, akionekana kumsubiri. Blandina akamfata huku akitabasamu kwa shauku kubwa, na Namouih akimwangalia kwa njia ya kawaida.

"Ulikuwa unaongea na huyo mtu wako bila shaka..." Namouih akasema.

"Hahah... girl mbona umekaza sana? Kafika na bonge la style yaani. Sekunde chache tu utashtukia kakuvurugia kesi haahahah..." Blandina akasema huku akicheka.

"Hawezi kufika popote na tumaneno twake twa kuwapagawisha vichwa mbovu kama wewe... alimchanganya mtoto kidogo tu, lakini haitakuwa na tatizo," Namouih akamwambia.

Blandina akacheka sana.

"Hearing ya sentence tunamaliza hii kitu kwa ushindi, na itanipa furaha kujua haushobokei mtu aliye timu pinzani," Namouih akasema.

"Ahahahah... baby tulia. Hizi kesi ni kazi tu, zitapita. Ila me Draxton simwachi salama. Anaonekana mzuri kwa bed huyo!" Blandina akaongea kwa madoido.

"We' ndiyo unayewaza kutomwacha ila yeye ashakuacha. Utaishia kuonana naye mshakamani tu kwingine ni ndoto," Namouih akasema huku akianza kuufungua mlango wa gari lake.

"Aa wapi. Leo tunakula naye," Blandina akasema.

Namouih akakunja uso kimaswali na kuuliza, "Unamaanisha nini?"

"Nimemwalika kwa ajili ya dinner leo," Blandina akasema huku akitabasamu.

Namouih akaufunga tena mlango wa gari. "What? Yaani... unataka aje leo... nyumbani?" akauliza.

"Yeah," Blandina akasema.

"Blandina... unawezaje kumwalika tu mtu ambaye hata haumfahamu... aje nyumbani... kweli hivi..."

"Si ndiyo nataka tujuane sasa? Kaniahidi atakuja..."

"Ya kukutext hakukuahidi kwani?"

"Kwani una tatizo na hilo? Ikiwa hautaki nije naye haina kwere, nitaenda naye sehemu nyingine..."

"No Blandina, sijamaanisha hivyo. Ninataka tu uwe mwangalifu..." Namouih akasema kwa upole.

"Acha basi nawe! Guy ni attorney huyo! Unajua tokea mwanzo nilidhani labda nilipagawa bure lakini sa'hivi nimejua kweli... ni Mungu ndiye alinikutanisha naye. Hadi profession zetu zinafanana! Hii haikuwa random baby, huyu jamaa napita naye," Blandina akaongea kwa uhakika.

Namouih akatabasamu huku akitikisa kichwa. "Kwa hiyo, anakufata, au mnakutana sehemu?" akamuuliza.

"Ananifata," Blandina akajibu kwa nyodo fulani hivi.

"Wacha! Malkia," Namouih akasema.

"Hahaaa... usiulize," Blandina akanena huku akirudisha nywele zake kwa nyuma kimaringo.

Wawili hawa wakaanza kucheka kwa pamoja, naye Blandina akazungukia upande mwingine wa gari na wote kuingia huku wanapiga story zenye kufurahisha. Namouih akampeleka Blandina kule alikoishi, yaani nyumbani kwa Blandina, baada ya kupata chakula kidogo kwenye mgahawa fulani, nao wakaagana kwa muda huo mpaka wakati ambao wangeonana tena jioni kwa sababu Namouih alihitaji kwenda kwake kumwandalia rafiki yake mambo mazuri kwa ajili ya kukutanika kwao baadaye.


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.

WhatsApp no: +255 787 604 893

e-mail: eltontonny72@gmail.com
 
CHANGE

Story by Elton Tonny

Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha

R-rated 18+


ILIPOISHIA.....

Baada ya mwanasheria Draxton kupambania kesi upande wa mtuhumiwa wa ubakaji na kufichua kwamba mtoa mashtaka alikuwa amedanganya, Blandina anazungumza naye na kuuliza kwa nini hakuwa amemtafuta baada ya yeye kumwachia namba mara ya kwanza walipokutana. Draxton anasema kwamba kuna mambo mengi yalikuwa yameingiliana, naye anamwomba Blandina samahani na kuuliza afanye nini ili ikubaliwe.

Blandina anapendekeza watoke pamoja jioni hiyo, akiwa na lengo la kwenda pamoja naye nyumbani kwa Namouih ambako amepata mwaliko wa mlo wa jioni. Draxton anakubali na kumwacha Blandina akiwa ameahidi kumtafuta, na mwanadada huyo anajiunga na Namouih ili waweze kuondoka mahakamani hapo. Lakini anapomfikishia taarifa ya kwamba amemwalika mtu wa timu pinzani kwenye kesi yao, ni jambo ambalo linasikika vibaya kwa mwanamke huyu.

"Blandina... unawezaje kumwalika tu mtu ambaye hata haumfahamu... aje nyumbani... kweli hivi..." Namouih anamuuliza akiwa ameshangazwa na hilo.

"Si ndiyo nataka tujuane sasa? Kaniahidi atakuja."

"Ya kukutext hakukuahidi kwani?"

"Kwani una tatizo na hilo? Ikiwa hautaki nije naye haina kwere, nitaenda naye sehemu nyingine..."

"No Blandina, sijamaanisha hivyo. Ninataka tu uwe mwangalifu..." Namouih akasema kwa upole.

"Acha basi nawe! Guy ni attorney huyo! Unajua tokea mwanzo nilidhani labda nilipagawa bure lakini sa'hivi nimejua kweli... ni Mungu ndiye alinikutanisha naye. Hadi profession zetu zinafanana! Hii haikuwa random baby, huyu jamaa napita naye," Blandina akaongea kwa uhakika.

Namouih akatabasamu huku akitikisa kichwa. "Kwa hiyo, anakufata, au mnakutana sehemu?" akamuuliza.

"Ananifata," Blandina akajibu kwa nyodo fulani hivi.

"Wacha! Malkia," Namouih akasema.

"Hahaaa... usiulize," Blandina akanena huku akirudisha nywele zake kwa nyuma kimaringo.

Wawili hawa wakaondoka hapo hatimaye, Namouih akampeleka Blandina kule alikoishi, yaani nyumbani kwa Blandina, nao wakaagana kwa muda huo mpaka wakati ambao wangeonana tena jioni kwa sababu Namouih alihitaji kwenda kwake kumwandalia rafiki yake mambo mazuri kwa ajili ya kukutanika kwao baadaye.


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA NANE

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Basi, jioni haikukawia kufika siku hii, naye Blandina akawa amejiandaa kwa ajili ya muda ambao angeutumia na mwanasheria kijana kwa jina la Draxton usiku huo. Alikuwa na matarajio mazuri sana, hivyo alihakikisha anapendeza na ananukia vizuri sana ili jamaa asimchukulie poa hata kidogo. Alitaka kumwonyesha leo kwamba anajua.

Alijiremba vizuri sana usoni, nywele zake za kusukwa akiziachia mpaka mgongoni, mwilini akivaa nguo fulani yenye muundo kama wa shati refu lililoishia sehemu za chini za mapaja yake, likiwa kama limekatwa mipasuo midogo kwa pembeni na hivyo mapaja yake kwa upande kuonekana vyema. Lilikuwa refu lakini kutokana na hips zake nene na kalio kubwa ilifanya linyanyukie juu kidogo namna hiyo. Sehemu ya kifuani liliacha uwazi mpana kwenye mstari uliotenganisha matiti yake na hivyo kuyaonyesha kwa juu kiasi. Lilikuwa na rangi ya blue kwa ujumla mchanganyiko na rangi zingine, na ni hilo pekee ndiyo alilovaa pamoja na nguo za ndani. Miguuni alivalia viatu vyeusi virefu vyenye kamba zilizoifunga miguu yake kwa kupanda mpaka sehemu za supu. Alipendeza.

Akiwa anajiweka sawa zaidi, simu yake ikaita, na tabasamu la furaha likatoka midomoni mwake baada ya kuona ni yule yule aliyemtarajia. Akapokea, naye Draxton akaongea kutokea upande wa pili, akisema tayari alikuwa nje ya nyumba aliyoishi bibie, hivyo achukue muda wote aliohitaji kujiandaa, naye angekuwa hapo nje akimsubiri. Blandina akavutiwa na huu utendewaji wa kama vile yeye ni malkia, naye akamwambia angetoka muda si mrefu. Baada ya maongezi hayo, Blandina akajigusa hapa na pale kuhakikisha anatoka nje kuua macho ya mtu, kisha akaelekea nje ya nyumba aliyoishi.

Alipotoka nje ya geti, akaliona gari la Draxton, aina ya Frester nyeusi, likiwa limeegeshwa upande wa pili wa barabara iliyozitenganisha nyumba za maeneo hayo, na Draxton mwenyewe akiwa amesimama nje kwa kuliegamia. Akatembea taratibu mpaka alipomfikia jamaa, naye akatabasamu kwa hisia. Draxton alikuwa amevaa sweta jepesi la mikono mirefu, lililokuwa na rangi ya blue iliyolowana, na lilimbana vizuri kuonyesha jinsi kifua chake kilivyojengeka vizuri kilivyokuwa. Alivalia suruali nyeusi ya kardet na viatu vyeusi chini, naye akatabasamu pia kwa kupendezwa na mwonekano wa Blandina.

"Umependeza," Draxton akaongea kwa sauti tulivu.

"Asante," Blandina akamjibu huku akitabasamu.

"Hawajambo huko ndani?"

"Niko mwenyewe hapo na dada wa kazi..."

"Aaaa... sawa. Naona hii mitaa imetulia."

"Yeah kidogo. Hakuna fujo sana."

"Sawa. Twend'zetu," Draxton akasema.

Blandina akatikisa kichwa kukubali, kisha Draxton akamfungulia mlango wa gari sehemu ya mbele, naye Blandina akapita karibu yake na kuingia kukaa. Ndani ya gari la Draxton palinukia vizuri sana, na jamaa akazungukia mpaka upande wa usukani na kuingia pia. Akaliwasha gari lake na kulitia mwendoni huku Blandina akimwangalia tu kwa jinsi alivyokuwa kimya sana, naye akachekea kwa chini.

"Vipi?" Draxton akauliza.

"Hamna kitu. Unaonekana makini kweli," Blandina akasema.

"Ahah... ndiyo hivyo. Usinilaumu sana nikikuboa mpaka ukahisi kufa," Draxton akamwambia.

"Ahahahah... sifikirii kama utaboa sana. Jinsi ulivyokuwa unaongea mahakamani leo yaani... nilijua u-special wako ni wa hali ya juu."

"Usiwahi kufikiri hivyo maana bado hujanijua vizuri."

"Ndiyo nataka sasa kukujua. Sijakutana na wanaume wengi ambao wako tayari kuninunulia chupa nyingine baada ya kuivunja..."

"Chupa tu? Hujui kwamba wapo watakaokununulia mpaka majumba na magari?"

"Magari hayajawahi kunibabaisha..."

"Mmm... kwa hiyo kumbe ni hapo kwenye chupa ndiyo palikukamata eeh?"

"Pamoja na mambo mengine."

Draxton akatabasamu kidogo na kusema, "Well, Blandina, hii ni kama apology tu kwa kuku..."

"Wewe unaiona kama apology tu na siyo kitu kingine zaidi?" Blandina akamkatisha.

"Mambo mengine huja baada ya muda. Ndiyo tumekutana tu kwa mara nyingine," Draxton akamwambia.

"Mmmm... napenda jinsi ulivyo on point. Bila shaka umewapangisha wanawake wengi foleni," Blandina akasema.

Draxton akacheka huku akiwa amefumba mdomo.

"Angalau nimepata bahati ya kuendeshwa nawe leo," Blandina akasema.

"Kwa nini uione kama bahati?" Draxton akauliza.

"I don't know. Labda we' ndo' uniambie. Ni nini kimenifanya nisiweze kuku-resist?"

"Mmm... nimependa jinsi ulivyo on point pia. Napenda mwanamke asiyeficha hisia zake na kutarajia mwanaume tu ndiyo awe mwenye kufunguka kwake."

"Kumbe? Hujakutana na wengi walio hivyo kwani?"

"Wapo wengi. Sema, mimi siyo mtu wa kukaa kutafuta..."

"Oooh kwa hiyo mpaka wewe ndiyo utafutwe..."

"Wewe ni tofauti Blandina. Unajua unachotaka, uko care, na ukisharidhika unatulia. Ungeweza kunipotezea tu na kuamua kujitafutia mtu mwingine lakini inaonekana fikira zako zimeridhishwa na mimi. Kwa hiyo niko hapa kujaribu kutokuzivunja moyo."

"Ahahah... fikira zina moyo?"

"Ni tamathali tu..."

"Me naziona kama swagger. Unaongea kwa njia fulani tofauti... nzuri sana..."

"Wewe pia."

"Kwa hiyo umeshakuwa na wanawake wengi eeh? With that charm who could resist you?"

"Ahahahah... usinione vibaya lakini kuhusu hilo..."

"Mhm... hapana wala, mimi pia nimepita kwa wanaume kadhaa. But kila mara inakuwa ni kama sijui kuchagua, au labda mimi ndiyo mwenye tatizo kwenye...."

"La, siyo wewe," Draxton akamkatisha.

Blandina akamwangalia kwa utulivu.

"Wewe Blandina unataka kupendwa, ndiyo maana moyo wako ni rahisi kupenda. Sema, watu wengi huwa wanalipenda tu wazo la kupenda na hawafilirii nini kiendelee zaidi wakishapenda, ndiyo maana muda ukipita hilo wazo wanalichoka kumwelekea mtu waliyedhani walimpenda. Wewe unataka kutulia, ila watu unaowapata wanafikiri unataka kucheza, kwa sababu huwaonyeshi mapema kwamba unategemea watulie nawe, kwa hiyo baadaye ukija kuwaonyesha... wanazingua. Hilo si tatizo lako kwa sababu ni wenyewe ndiyo wanakuwa wanashindwa kuona jinsi mambo yalivyo kihalisi," Draxton akamwambia kwa ustaarabu.

Blandina akamwangalia sana, kisha akauliza, "Unawezaje kuongea hivyo kuhusu mimi wakati ndiyo tumekutana tu?"

"Niliwahi kusoma saikolojia kidogo," Draxton akamwambia.

Blandina akatabasamu na kuangalia mbele.

"Samahani kama nime...."

"No, no, nimependa maneno yako. Ulichosema ni kweli, maana hata me nwenyewe nilikuwa sijafikiria hivyo ila ni kweli kabisa," Blandina akamwambia.

"Usijali sana, ni kitu cha kawaida," Draxton akasema.

"Kwa hiyo... unasema kwamba nikikuonyesha nataka kutulia nawe, na wewe utatulia na mimi?" Blandina akauliza.

"Ahahah... huko bado sana kufika Blandina. Ndiyo tumekutana tu, kama nilivyosema," Draxton akaongea.

"Sawa," Blandina akajibu kiupole huku akiangalia mambo fulani kwenye simu yake.

Wakaendelea na mwendo, huku Blandina akimwelekeza pa kwenda, na sasa giza lilikuwa linavizia kwa mbali baada ya jua kutua.

"Tunaenda mahali fulani hususa? Maana huku sijawahi fika," Draxton akamuuliza, wakiwa mwendoni bado.

"Ndiyo. Rafiki yangu anaandaa mlo wa jioni pamoja na mume wake, wanataka ku-share pamoja nami kwa sababu sikuwa nimeonana na mume wake muda mrefu... ni rafiki yangu pia, yaani wananikaribisha," Blandina akasema.

Draxton akabaki kimya, lakini Blandina akatambua ni kama jambo hilo halikumfurahisha.

"Vipi? Haujapenda kwamba... tunaenda huko?" Blandina akauliza.

"La, si hivyo. Nilifikiri ingekuwa mimi na wewe tu, sikuwa... sikudhani kungekuwa na wengine."

"Haupendi mijumuiko eeh?"

"Kawaida tu. Ungeniandaa mapema."

"Usiwaze. Ni watu wazuri sana na... nitafurahi kukutambulisha kwao," Blandina akamwambia.

Aliongea hivyo utadhani tayari alikuwa kwenye uhusiano na mwanaume huyu, naye Draxton akampa tu tabasamu na kuendelea kuendesha na maongezi mengine kuendelea. Blandina alikuwa akiuliza mambo fulani kuhusu maisha ya Draxton, lakini mwanaume huyu angekwepa kujibu moja kwa moja na kugeuza mada zimwelekee Blandina, ambaye angeongea kwa uhuru kuhusu mambo yake mengi.

β˜…β˜…

Nyumbani kwa wanandoa Efraim Donald na Namouih, maandalizi kwa ajili ya kumkaribisha rafiki yao yalikuwa yamekamilika kufikia wakati huu, katika maana ya msosi. Namouih ndiye aliyetengeneza chakula kizuri kwa ajili ya rafiki yake na mume wake, lakini bado wazo la Blandina kuhusu kumleta Draxton hapo lilimkera. Lilimkera hasa kwa sababu mtu huyo alikuwa upande pinzani wa kesi waliyopigania, akiwa mtetezi wa mbakaji wa msichana mdogo, na jinsi alivyotoa kauli mbalimbali mahakamani zilizoonwa na wengine kuwa zinapatana na akili kulimfanya Namouih amchukulie Draxton kwa njia fulani kama adui. Ingawa Blandina kumleta mwanaume huyo hapo kulimkera sana Namouih, kungempatia pia nafasi ya kumsoma zaidi, kwa sababu alipanga kuona mwanaume huyo alijengekaje kiutu.

Efraim Donald tayari alikuwepo nyumbani, akiwa amekaa zake kwenye sofa huku akipitia mambo kadhaa kwenye simu, na TV kubwa ukutani ikionyesha habari za saa, ikiwa ni saa moja tayari. Namouih alipokuwa amemaliza kusaidizana na Esma katika masuala ya mapishi, akaelekea juu ili kujiweka sawa zaidi kimwili. Alijiwekea mwonekano wa kawaida tu kama mke wa nyumbani kwa kuvaa dera refu lenye urembo mwingi, naye akarejea kwa mume wake na kuketi karibu yake sofani, akipiga naye story na kujipiga picha za selfie pamoja naye. Angalau yale yaliyotokea jana baina yao walikuwa wameyaweka pembeni kwa wakati huu.

Hazikupita dakika nyingi na simu yake ikaita, ikiwa ni Blandina anayepiga, naye akapokea na kujua sasa kwamba rafiki yake alikuwa nje ya geti tayari. Namouih akamwambia sawa, kisha akanyanyuka na kwenda mpaka mlangoni, naye akamwita Alfani akimwambia kuna mtu nje hivyo akafungue geti kumruhusu aingie. Baada ya Alfani kufanya alichoambiwa, gari lisilo geni sana machoni mwa Namouih likaingia, akitambua ni la Draxton kwa sababu alimwona mapema leo akiondoka nalo kutoka mahakamani. Akawa amesimama tu hapo huku akilitazama mpaka lilipoegeshwa nyuma ya magari yao, kisha milango ikafunguka na wawili wale kutoka.

Namouih akawa amemkazia macho Draxton, ambaye alionekana kuangalia umaridadi wa eneo la nyumba hiyo mpaka Blandina alipomfata na kukishika kiganja chake, kisha wakaanza kutembea kwa ukaribu kumwelekea Namouih. Blandina alionekana kuwa mbingu ya 18 maana aliongea na jamaa huku akicheka kwa furaha, na Namouih akajiambia tu moyoni 'haya.' Efraim Donald naye akawa ametoka na kusimama pembeni ya mke wake, na baada ya Blandina na Draxton kufika karibu, Namouih akamkumbatia rafiki yake huku wakisemeshana kwa uchangamfu.

"Nakuona shemeji," Blandina akamwambia Efraim baada ya kuachiana na Namouih.

"Nakuona na wewe, yaani huachi tu kunenepa! Ni kilo, kilo, tani..." Efraim akasema, nao wakacheka na kukumbatiana pia.

Namouih akawa amempuuzia kabisa Draxton, hata kumwambia tu 'karibu' hakutaka.

"Donald, huyu ni Maximilian Draxton," Blandina akamtambulisha hatimaye.

"Vipi kaka?" Efraim akamsalimu.

"Safi," Draxton akajibu.

Wanaume wakapeana mikono kirafiki, naye Efraim Donald akatambua kwamba mikono ya Draxton ilikuwa na nguvu sana.

"Karibu sana. Naitwa Efraim. Ukipenda niite Donald," Efraim akamwambia.

"Nimefurahi kukufahamu Efraim. Niite Draxton," naye pia akajitambulisha.

Efraim akasema, "Draxton ni jina lenye nguvu. So, wewe na huyu kibibi mna...."

Blandina akacheka na kusema, "Umeanza!"

"Ahahah... gesture ya kwanza. Mnapendezeana," Efraim akamwambia.

"Well, bado siye ni marafiki tu, ila kwenye kupendezeana uko sahihi..."

Blandina ndiye aliyesema maneno hayo huku akimlalia Draxton begani, naye Efraim akatabasamu, huku Namouih akizungusha macho kikejeli.

"Karibu dear. Ulivyovaa utafikiri unataka kuua mtu," Namouih akamwambia Blandina.

"Na bado..." Blandina akajibu.

Wawili hawa wakaongoza kuingia ndani, huku wanaume wakiwafuata nyuma.

Ndani hapo palikuwa pazuri sana, Draxton aliona hilo, nao wakaelekea mpaka masofani na kukaa. Blandina aliongea kwa uchangamfu sana alipozungumza na Efraim Donald. Maongezi yalipohamia kwa Draxton, hakuongea sana kujihusu zaidi ya kusema yeye ni mwanasheria anayejitegemea tu na siyo kwamba ameajiriwa sehemu yoyote binafsi au serikalini. Akasema ni muda mrefu kiasi ulikuwa umepita tokea mara ya mwisho aliposimamia mtu kwenye kesi, kwa hiyo wakati huu alikuwa amerudi tena upande huo ili kufanyia kazi kipawa chake cha uanasheria. Namouih hakumsemesha hata kidogo ingawa wote kuwa wanasheria kungefanya wawe na mengi ya kuongelea, na kwa kiasi fulani suala la Draxton kuchuana naye kwenye kesi likazungumziwa, lakini kwa njia nzuri tu kwenye maongezi yao changanyikeni.

Basi, imefika saa mbili hivi, Namouih akawaongoza wengine kwenda kuketi kwenye meza ya chakula, naye Blandina akamshika tena Draxton kiganjani na kutembea karibu yake mpaka walipoketi vitini. Kulikuwa na vyakula vingi vilivyofunikwa ndani ya vyombo vya kutunzia, naye Blandina akatania kuhusu kutoa sala kabla ya kula, akimwambia Efraim afanye hivyo. Efraim Donald akasema kwamba chakula kilikuwa kimeshabarikiwa pindi tu mke wake alipomaliza kukipika, kwa hiyo haikuwa na haja ya kusali, na hilo likafanya wengine wacheke. Esma alikuwepo pia hapo akisaidia kupangilia mambo vyema, naye akakaa pia kwenye kiti kimoja. Ni Namouih pekee ndiye aliyekuwa amesimama sasa, akimimina juice (sharubati) ya mchanganyiko wa parachichi na ndizi kwenye glasi za wengine. Alipomaliza ya Efraim, akaifata ya Esma, kisha ya Blandina. Lakini alipoifikia ya upande wa Draxton, akamwangalia kidogo na kuona jambo fulani.

Mwanaume huyo alifumba macho taratibu na kuinamisha uso wake, akivuta, au akitoa hisia fulani hivi. Hii ilikuwa ni mara ya pili Namouih kumwona anafanya hivyo, ya kwanza ikiwa ni mapema ya leo walipokuwa mahakamani, naye akashindwa kuelewa alikuwa na tatizo gani. Wengine hawakutambua jambo hilo, naye Namouih akaghairi kumwekea jamaa juice na kwenda kuiwekea glasi ya sehemu ambayo angekaa yeye. Blandina alikuwa anaongelea vituko vya shuleni pamoja na Esma na Efraim, naye akawa ametambua kwamba Namouih hakumwekea mtu wake juice. Hii haikukaa sawa machoni pake, na kwa kuhisi Namouih alifanya hivyo kwa makusudi, akalichukua jagi lenye juice na kuanza kummiminia Draxton kwenye glasi bila kumtazama Namouih, lakini Namouih akawa anamtazama tu mwanaume huyo kwa jicho la chini.

Sasa Draxton akawa ameketi sawa baada ya Blandina kumaliza kumwekea juice, akisikiliza maongezi baina ya marafiki sehemu hiyo.

"Ahahah... basi ikifika somo la Mathe kila mtu anachoka," akasema Efraim Donald.

"We, acha! Utajaribu kuchagua combi yoyote ile ili kuiepuka, lakini ndiyo ilikuwa imeziganda zote," akasema Blandina.

"Ma-pythagoras theorem na ma-logarithm yalikuwa yananiacha hoi," Esma akaongea.

"Me yaani hata nilikuwa siyakumbuki hayo majina," Namouih akasema na kumfanya Esma acheke.

"Halafu sasa ikifika wakati wa paper, mtu anaomba ile, kuna kitabu fulani kidogo cha mahesabu..."

"Four Figure," Esma akamkumbusha Efraim.

"Ee Four Figure. Unaiomba kama show tu yaani hauifanyii kitu, unajikuta uko makini kweli kufanya ma-calculation," Efraim Donald akaongea hivyo na kufanya wengine wacheke kidogo.

Wakati huu, wanawake walikuwa wanajipakulia vyakula, kisha Namouih akaanza kumpakulia mume wake. Blandina naye akaanza kumpakulia Draxton, na ilikuwa ni kama alifanya hivyo ili kumchengua rafiki yake ingawa hilo halikuwa lengo lake kihalisi. Alitaka tu kumwonyesha Draxton kwamba alimjali sana, naye Draxton akamwonyesha tabasamu la shukrani. Blandina alipotaka kumwekea mboga za majani, mwanaume huyu akamwambia asiweke.

"Hauli majani?" Efraim Donald akamuuliza.

"Ndiyo, huwa... sili mboga za majani," Draxton akamwambia.

"Kwa nini?" Namouih akauliza.

Hii ndiyo ilikuwa mara ya kwanza anamsemesha tangu alipofika hapo, naye Draxton akamwangalia tu.

"Una allergy?" Blandina akamuuliza Draxton huku akiwa ameacha kumwekea.

"Yeah, unaweza kusema hivyo," Draxton akajibu.

Namouih akafanya ile cheko kwa pumzi wanayofanyaga wanawake ya bila kutoa sauti huku akiangalia chini, kwa njia fulani ya dharau, na Blandina akawa amemwona.

"Nafahamu jamaa fulani mhindi... alikuwa akila majani tu, hey! Asubuhi anaamka na mapele shingoni mpaka mgongoni. Unajua kuna allergy ambazo huwa zinaua," akasema Efraim.

"Yeah ni kweli. Mimi nikila huwa najihisi vibaya sana... kama kuumwa," akasema Draxton.

"Kwa hiyo we' ni nyama tu... eti?" Namouih akamuuliza.

"Pamoja na vyakula vingine," Draxton akajibu na kuanza kula.

"Watu wanaokula majani tu na siyo nyama huwa kwa kiingereza wanaitwa vegetarians, eti?" akauliza Esma.

"Ndiyo," akajibu Efraim Donald.

"Vipi wale wanaokula nyama tu?" Esma akauliza tena.

"Nyamatarians," Blandina akamjibu kiutani.

Hilo likafanya wengine wacheke.

"Unaiga ile ya took inakuwa tookunti?" Efraim Donald akamwambia Blandina, naye akacheka kidogo.

"Nakutania mwaya. Ila sijui wanaitwaje labda mpaka tutafute Google," Blandina akamwambia Esma.

"Wanaokula nyama pekee hufuata mlo unaoitwa carnivore diet. Kwa hiyo wanaitwa carnivores," Draxton akamwambia Esma.

"Ahaa... umesema cani...." Esma akauliza.

"Carnivores," Draxton akamwambia.

"Halafu kweli, hiki kitu kama tuliwahi kusoma kwenye biology," akasema Blandina.

"Nitayakumbuka sasa?" Efraim Donald akasema, nao wakacheka kidogo.

Namouih akamtazama Draxton akila taratibu, kisha akamuuliza, "Unakulaga nyama za aina zote?"

Draxton akatulia kidogo, kisha akatikisa kichwa kukubali.

"Hadi za watu?"

Blandina akashusha kijiko alichokuwa karibu kuingiza mdomoni na kumtazama Namouih kwa mkazo baada ya yeye kuuliza swali hilo.

Draxton akakiangalia tu chakula chake bila kutoa jibu kwa hilo swali.

"Hahah... honey, matani gani tena hayo?" Efraim akamuuliza mke wake huku akiendelea kula.

"Ahah... yeah, nilikuwa natania tu. Manyamatarian wengi sana siku hizi," Namouih akaongea, ikiwa ni kwa njia ya kejeli.

"Ahahahah... natamani ningeweza kuwaona mnavyochuana kwenye hiyo kesi ya Agnes, nione moto wenu. Ulisema ana miaka mingapi?" Efraim Donald akamuuliza mke wake.

"Ana 19. Mbakaji wake ana 26," Namouih akajibu huku akimtazama Draxton kama vile anamwambia yeye.

"Mechi za kombe la dunia zinaanza hivi karibuni. Unafatilia?" Draxton akamuuliza Efraim, akiwa amebadili mada upesi.

"Yah! Haloo, ninaitabiria mambo makubwa sana Senegal ingawa Mane atakosa, wana kikosi kizuri sana," Efraim Donald akasema.

"Ndiyo ni kweli. Hata Morocco pia, wanacheza vizuri sana," Draxton akamwambia.

Efraim Donald akaanza kuzungumzia mambo fulani kuhusu soka, huku Draxton akimsikiliza, naye Namouih akaendelea kula. Aliponyanyua macho yake kumwangalia Blandina, akakuta anamtazama tu, kwa njia iliyoonyesha kwamba alikasirishwa na jambo fulani. Namouih akauliza kupitia macho 'vipi,' naye Blandina akaacha kumwangalia na kuendelea tu kula huku akionekana kukosa shangwe aliyokuwa nayo mwanzoni. Esma aliona hilo pia, lakini akakausha tu na kuendelea kula.

Namouih hangehitaji kukisia kuhusu ni nini kilichomkwaza rafiki yake, alijua kabisa kwamba Blandina alikasirishwa na jinsi yeye alivyomtendea Draxton. Akaendelea tu kula pia, huku maongezi ya hapa na pale yakiwasindikiza vizuri mpaka walipomaliza mlo na kushiba. Draxton alionyesha ustaarabu mzuri sana kwenye kula, na Blandina alifurahia sana uwepo wake hapo. Wanaume wakaelekea tena kwenye masofa huku sasa Efraim akimwambia Draxton kuhusu usafirishaji wa mizigo na magari kwenda nje ya nchi, na wanawake wakasaidiana kupeleka vyombo sehemu ya jikoni.

Walipofika tu huko, Namouih akimwambia Esma awapishe yeye na Blandina kwanza, na dada huyo akatii na kuwaacha.

"Okay, najua kuna kitu kiko kifuani kwako kwa hiyo, ropoka," Namouih akasema.

"Usifikiri sijui ulichokuwa unajaribu kufanya," Blandina akasema kwa mkazo.

"Kufanya nini? Nimetukana mtu?"

"Namouih naomba tuheshimiane. Kama shida ni mimi kumleta Draxton hapa ungeniambia nikaacha, siyo kuanza kumfanyia vile..."

"Hivi kweli Blandi... yaani unanikasirikia mimi rafiki yako wa miaka mingi over a guy you just met yesterday? Na uko tayari kabisa kugombana nami kisa nini, nime...."

"Ni maisha yangu. Mimi huwa siji kutoka sehemu yoyote kukuamulia namna unavyotakiwa kuiendesha ndoa yako, kwa hiyo naomba uyaache maamuzi yangu kuwa yangu," Blandina akaongea kwa hisia kali.

Namouih akabaki kimya, kwa kutambua kwamba Blandina alikasirika sana.

"Ulivyomfanyia imekupa faida gani? Ili iweje? Tena unafanya hivyo mbele yangu bila kujali nitakavyohisi?"

"Blandi...."

"Unauliza kama anakula nyama ya mtu kumaanisha ye' ni mchawi au? Unamfanyia hivyo kwa kuwa mnapingana kwenye kesi au ni chuki tu isiyokuwa na maana yoyote ile? Namouih sijapenda. Ulivyofanya ni vibaya, na sitawahi tena kuja kukanyaga hapa," Blandina akasema.

"Blandina... sikia... mimi... sioni kama huyo kaka anakufaa... kabisa... sidhani kama yuko...."

"Naomba uniache tu Namouih. Niache nichague yeyote nayetaka. Wewe siyo mama yangu kuniamulia nitakayekuwa naye kama wa kwako alivyokuamulia wa kukuoa!" Blandina akasema kwa mkazo.

Namouih akaishia tu kumwangalia rafiki yake kwa huzuni, ambaye alitoa maneno hayo kuonyesha ni jinsi gani alikuwa amevunjwa moyo na yale aliyomtendea mtu wake. Blandina akampita Namouih na kuondoka kutoka hapo jikoni, akimwacha mwanamke huyu bila amani moyoni.

Efraim Donald na Draxton walipatana vizuri sana, na mume huyo wa Namouih hata akamwomba namba za simu kijana huyu mwenye akili iliyompendeza mno. Muda wa dakika kadhaa ambazo Blandina na Draxton waliendelea kuwa hapo, walipiga story tu na kushushia vinywaji taratibu mpaka Blandina aliposema alitaka kuondoka na "rafiki" yake, yaani Draxton. Hakuwa amedhamiria waondoke mapema sana, lakini kwa sababu ya kilichotokea, mwanamke huyu hakujihisi vizuri kuendelea kubaki hapo. Namouih alikuwa akitafuta hata nafasi ndogo tu ya kuongea na Blandina tena, lakini aliona wazi jinsi rafiki yake huyo alivyomkwepa ingawa si moja kwa moja, kuonyesha bado alikuwa amekasirika. Hivyo mwishowe wakaagana, ikiwa ni saa nne ya saa tano sasa, na wawili hao waliofika hapo kama wageni wakaondoka hatimaye.

Wakiwa wamerudi ndani baada ya wageni kuondoka, Efraim Donald akamuuliza Namouih kuhusu suala la yeye kumsemesha Draxton kwa njia mbaya, akimwambia kwamba alijifanya tu kama hakuona matendo yake, ila aliyaona. Namouih, tayari akiwa hana amani baada ya Blandina kumwonyesha ameudhika, akasema tu kwamba hakuwa na nia mbaya, lakini Efraim Donald akamrekebisha na kusema hiyo haikuwa sahihi kwa kuwa huenda kijana yule alijihisi vibaya. Lakini akamwambia tu apotezee jambo hilo kwa kuwa bila shaka lingesahaulika, nao wakaanza kufanya maandalizi ya kujipumzisha.

β˜…β˜…

Wakiwa mwendoni kuelekea kwake Blandina, Draxton alimwambia mwanamke huyu namna ambavyo alifurahia ushirika wake (company). Akaweka wazi jinsi alivyofurahia chakula na ushirika wa marafiki zake Blandina, na mwanamke huyu akawa anatafuta njia ya kumwombea Namouih samahani kwa jinsi alivyotenda kumwelekea, lakini akawa anashindwa. Alihisi jambo hilo lingeharibu maongezi yao mengine, lakini pia alitaka tu lisahaulike.

Wakiwa wamefika kwake Blandina hatimaye, Draxton akasimamisha gari usawa wa geti la nyumba hiyo, naye akamtazama machoni mwanamke huyu aliyekuwa anamwangalia kwa upendezi mwingi.

"Hii ndiyo part tunayosema 'goodnight' siyo?" Draxton akamwambia.

"Mbona bado mapema kusema 'goodnight?'" Blandina akasema hivyo huku akilaza kichwa chake kwenye siti aliyokalia, na akimtazama mwanaume kwa uvutio.

Draxton akatabasamu na kusema, "Okay. Good-before-night."

Blandina akatabasamu na kusema, "Bado haitoshi."

"Nini huwa kinatosha kwenye hii dunia?"

"Kwangu mimi... labda ni kujua tu kwamba hii haitakuwa mara ya mwisho tunafanya hivi..."

"Una matarajio mengi sana juu yangu eti?"

"Ndiyo. Niambie unataka nifanye nini ili yatimie..."

"Sitarajii chochote Blandina. Wewe ni mwanamke mzuri, lakini kwenda unakotaka nahisi itakuwa kuharakisha mno."

"Unaogopa mapenzi ya mwendokasi eeh?" Blandina akaongea hivyo huku akianza kutembeza kidole chake kwenye mkono wa Draxton taratibu.

"Nilikuwa hata sijafikiria ikiwa ungetumia hilo neno leo," Draxton akamwambia.

Blandina akamsogelea karibu na uso wake, naye Draxton akaupitisha mkono wake usawa wa ubavu wa mwanamke huyu ili aegamie hapo.

"Ulikuwa hujafikiria ningesema neno... mapenzi?" Blandina akamwambia hivyo karibu kabisa na mdomo wake.

Draxton akatulia kidogo, kisha akatikisa kichwa kukanusha huku akimwangalia mdomoni.

"Ungependa nikuonyeshe linamaanisha nini?" Blandina akasema kwa sauti ya deko.

"Tayari najua linamaanisha nini, ila...."

"Bado hujalijua kutoka kwangu," Blandina akamalizia maneno ya jamaa.

Draxton akahisi kiganja cha Blandina kikitembea taratibu kutokea pajani kwake na kuelekea mpaka sehemu ya kati ya suruali yake. Hisia murua zilikuwa zimeanza kuwavaa wawili hawa, naye Blandina akawa anafurahia sana pumzi za taratibu kutoka kwa Draxton karibu na mdomo wake, na akihisi jinsi mtambo wa jamaa ulivyoanza kuwa mgumu pole kwa pole.

"Twende ndani..." Blandina akasema kwa sauti iliyoonyesha hisia nzuri sana.

Draxton akaacha kumtazama mdomoni na kuangalia mkono wa bibie ulioshika sehemu yake ya kati, kisha akasema, "Nahisi ni kama... nitaharakisha... sijui kama niko tayari..."

"Mhmhm... basi mimi nitakuongoza..." Blandina akasema kwa maringo.

Kisha mwanamke huyu akaanza kuibusu midomo ya Draxton taratibu, naye Draxton akawa anamruhusu aendelee kufanya hivyo. Blandina alikuwa ameingiwa na hamu kubwa sana ya kutaka kulionja penzi la mwanaume huyo kijana kiasi kwamba akaendelea kumbusu kimahaba sana na kuongeza kasi, lakini Draxton akaivunja busu yao na kuketi sawa zaidi. Blandina akawa anamwangalia usoni kwa hamu sana, lakini akijiuliza kwa nini aliivunja busu ghafla.

"Draxton... kuna tatizo?" Blandina akauliza huku akitembeza kiganja chake kidevuni kwa Draxton.

Draxton akiwa amefumba macho, akatikisa kichwa kukanusha.

"Mbona hivyo?" Blandina akauliza.

Draxton akamtazama kwa ufupi, akiona jinsi mwanamke huyo alivyokuwa na hamu kweli, naye akasema, "Hamna tatizo. Nafikiri... itakuwa... itakuwa vizuri zaidi tukienda ndani."

Blandina akaachia tabasamu la furaha na kuung'ata mdomo wake wa chini kidogo, kisha akatikisa kichwa kukubali na kutoka ndani ya gari. Draxton akashika usukani kwa nguvu sana na kufumba macho yake, naye akawa anapumua kwa nguvu kiasi ili kujipa utulivu. Alipofumbua macho, akamwona Blandina akiwa amesimama getini huku akitazama upande wa gari, hivyo mwanaume akajiweka sawa na kutoka pia. Akafunga gari vyema na kumfata Blandina, nao wakaingia ndani kule baada ya msichana wa kazi kufika na kuwafungulia geti. Aliitwa Hamida.

Nyumba aliyoishi Blandina ilikuwa ya kupanga, yaani yote kwa ujumla alikuwa analipia yeye akiwa mpangaji pekee. Ilikuwa nzuri yenye rangi ya blue na madirisha yenye vioo vyeusi vikubwa, na ndani palikuwa pazuri sana pia, kukiwa na vifaa vingi vya kisasa vilivyopangiliwa vyema kwenye vyumba vyote hapo. Akawa anamwambia Draxton jinsi ambavyo hakuwahi kuwa na mpango wa kujenga nyumba, lakini ikiwa angepata pesa za kutosha kununua nyumba kabisa, angenunua. Muda wote Blandina aliozungumza, Draxton alikuwa kimya, akimfuata tu kwa ukaribu mpaka walipoingia ndani kwenye sehemu ya sebule na msaidizi wake wa kazi kusimama pembeni yao kama vile anasubiri kuambiwa kitu fulani.

Blandina alipomwangalia msichana wake wa kazi, akatambua kwamba alikuwa anamtazama Draxton kwa upendezi mwingi, na hilo likamkera.

"Ulikuwa umeshalala?" Blandina akamuuliza.

"Ndiyo nilikuwa nime..nimejilaza, ila sikusinzia," Hamida akajibu.

"Haya we' rudi ukalale. Tutaonana kesho," Blandina akamwambia na kuweka pochi yake ndogo mezani.

Draxton akamtazama Hamida na kukuta anamwangalia kwa njia fulani hivi ya uvutio, naye Blandina akaona hilo.

"Haujanisikia au?" Blandina akauliza kwa sauti ya juu kidogo.

"Sawa dada..."

Hamida akajibu hivyo haraka na kuondoka, huku kalio lake nene kiasi likitikisika kwa nyuma ndani ya dera alilovaa. Blandina akasonya kidogo, naye Draxton akatabasamu.

"Usiwe hivyo," Draxton akamwambia.

"Nini, we' hujaona alivyokuwa anafanya hapo? Sijui yukoje," Blandina akasema kwa kukereka.

"Unakasirikia hicho tu, je ukinikuta nimesimama na mwanamke mwingine?"

"Namuua, halafu wakinikamata unakuja kupiginia kesi yangu ili nitoke."

Draxton akacheka kidogo na kutazama pembeni.

Blandina akamsogelea na kupitisha mikono yake kiunoni mwake, akiigundisha miili yao huku anamwangalia usoni. "Tulikuwa wapi kweli?" akauliza kwa sauti ya chini.

Draxton akapitisha mikono yake mgongoni kwa Blandina, akifanya kama kumkumbatia, kisha akaanza kuilamba shingo ya mwanamke huyu kwa njia fulani kama vile anataka kuitafuna... taratibu. Blandina hakuwa ametarajia kabisa kwamba Draxton angeanzia hapo, lakini msisimko uliomwingia ukamfanya ahisi kulegea na kuanza kutoa miguno kwa pumzi za mdomo. Mwanamke naye hakuwa nyuma; akapeleka mkono wake wa kushoto mpaka sehemu ya kati ya suruali ya jamaa na kuanza kupavuta-vuta, na sasa Draxton akawa analiminya kalio la bibie kwa nguvu na kulizungusha-zungusha kwa njia iliyompa mhemko mwingi sana Blandina. Alikuwa amewaza kwamba labda wangefanyiana haya wakiwa chumbani, ila hata kuanzia hapa hapa haikuwa mbaya, kwa sababu tayari penzi lilikuwa mwendoni.

Draxton akaiacha shingo ya Blandina na kuifata midomo yake sasa, nao wakaanza kunyonyana ndimi kwa uzito, huku sasa Blandina akiwa anafungua kifungo cha suruali ya Draxton na kuelekea kuishusha zipu yake. Draxton alikuwa anaongeza kasi katika busu zake na tomasa, akiwa kama anamsukuma Blandina kuelekea ukutani, na kwa kukosa mhimili kidogo Blandina akaitoa mikono yake kwa chini na kumshika kiunoni na shingoni. Lakini ni baada ya kumshika shingoni ndiyo mwanamke huyu akafumbua macho na kuvunja denda yao ili amwangalie Draxton vizuri. Alipoigusa shingo ya mwanaume huyu, Blandina alihisi joto kali sana kama vile alikuwa ameshika nguo iliyopigwa pasi kwa muda huo huo. Draxton akawa anapumua kwa uzito kiasi, huku sasa akiangalia chini, na bado miili yao ikiwa karibu.

"Draxton... uko sawa?"

Blandina akamuuliza hivyo, lakini Draxton akamwachia na kurudi nyuma kidogo, akipumua vile vile, na akijishika magotini kama mtu aliyechoka baada ya kukimbizwa kwa muda mrefu. Blandina akamsogelea na kuishika shingo yake tena, lakini joto kali la hapo likamfanya aiachie upesi sana.

"Draxton... mbona unachemka hivi... shida ni nini?" Blandina akauliza hivyo akiwa haelewi kilichokuwa kinaendelea.

Draxton hakujibu lolote, bali akageuka tu na kuanza kuondoka. Tena hadi akaanza na kukimbia kabisa kuelekea nje. Ajabu!

Blandina akaanza kumfata huku akimwita sana, lakini mwanaume huyo akatoka mpaka nje kabisa na kwenda kwenye gari lake. Blandina alipofika nje, tayari Draxton alikuwa ameshaligeuza gari na kulitia mwendoni kutoka maeneo hayo. Dada wa watu akabaki kusimama hapo nje akiwa ameachwa na butwaa zito, hisia nzuri za kimahaba zilizokatizwa, na maswali mengi sana kichwani. Alijihisi vibaya sana kwa sababu ya kitendo cha Draxton, naye akawa anataka kujua ni nini kilichomsibu mwanaume huyo mpaka akaamua kukimbia namna hiyo.


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Itakuwa ikiruka hapa siku za Jumamosi na Jumapili. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.

WhatsApp no: +255 787 604 893

e-mail: eltontonny72@gmail.com
 
CHANGE

Story by Elton Tonny

Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha

R-rated 18+


MUHTASARI MFUPI....

Baada ya mwanasheria Draxton kupigania upande pinzani kwenye kesi ya msichana ambaye Namouih alimwakilisha, Blandina anamwalika mwanaume huyo kwa ajili ya mlo wa jioni nyumbani kwa Namouih na Efraim Donald. Draxton anakwenda hapo pamoja naye, lakini Namouih hapendezwi hata kidogo na mwanaume huyo, na hata anafanya na kuongea vitu vyenye kuonyesha hilo. Blandina anachukizwa na matendo ya rafiki yake, anamwambia ukweli kwamba hajapenda, na kisha anaondoka na Draxton akiwa amemkasirikia rafiki yake. Namouih anajihisi vibaya kwa kumkwaza rafiki yake hata ingawa aliona yote aliyotenda kuwa sawa mwanzoni, na Efraim Donald anamrekebisha juu ya hilo.

Draxton anamrudisha Blandina anapoishi, na mwanamke huyo anamwonyesha wazi kwamba anataka sana kushiriki naye mapenzi. Anamwalika ndani, naye anamwomba waendeleze kile walichokuwa wameanzisha ndani ya gari. Draxton akaanza kumwonyesha mahaba kwa njia iliyonsisimua sana Blandina, na mwanamke huyu hakuacha kuonyesha hamu aliyokuwa nayo kwa Draxton. Draxton alikuwa anaongeza kasi katika busu zake na tomasa, akiwa kama anamsukuma Blandina kuelekea ukutani, na kwa kukosa mhimili kidogo Blandina akaitoa mikono yake kwa chini na kumshika kiunoni na shingoni. Lakini alipoigusa shingo ya mwanaume huyu, Blandina alihisi joto kali sana kama vile alikuwa ameshika nguo iliyopigwa pasi kwa muda huo huo. Draxton akawa anapumua kwa uzito kiasi, huku sasa akiangalia chini, na bado miili yao ikiwa karibu.

"Draxton... uko sawa?"

Blandina akamuuliza hivyo, lakini Draxton akamwachia na kurudi nyuma kidogo, akipumua vile vile, na akijishika magotini kama mtu aliyechoka baada ya kukimbizwa kwa muda mrefu. Blandina akamsogelea na kuishika shingo yake tena, lakini joto kali la hapo likamfanya aiachie upesi sana.

"Draxton... mbona unachemka hivi... shida ni nini?" Blandina akauliza hivyo akiwa haelewi kilichokuwa kinaendelea.

Draxton hakujibu lolote, bali akageuka tu na kuanza kuondoka. Tena hadi akaanza na kukimbia kabisa kuelekea nje. Ajabu!

Blandina akaanza kumfata huku akimwita sana, lakini mwanaume huyo akatoka mpaka nje kabisa na kwenda kwenye gari lake. Blandina alipofika nje, tayari Draxton alikuwa ameshaligeuza gari na kulitia mwendoni kutoka maeneo hayo. Dada wa watu akabaki kusimama hapo nje akiwa ameachwa na butwaa zito, hisia nzuri za kimahaba zilizokatizwa, na maswali mengi sana kichwani. Alijihisi vibaya sana kwa sababu ya kitendo cha Draxton, naye akawa anataka kujua ni nini kilichomsibu mwanaume huyo mpaka akaamua kukimbia namna hiyo.


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA TISA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Asubuhi iliyofuata, tayari Namouih alikuwa ofisini kwake. Kupitia na kuandaa-andaa mambo kadhaa kabla muda wa hukumu ya kesi ya Agnes mahakamani ilikuwa lazima, naye alikuwa ametafutwa na mama yake Agnes kuulizwa ikiwa mambo yangekwenda safi. Tena, na hapa Namouih akamkumbusha kwamba yeye siyo mwamuzi wa mwisho wa matokeo ya kesi hiyo, na ingawa upande wao ulionekana kuwa na nguvu zaidi ya kushinda, wangepaswa tu kusubiri matokeo huko huko mahakamani, na yeye alikuwa amejiandaa vyema kumpigania Agnes mara hii ya mwisho.

Basi, imefika mida ya saa tatu asubuhi, Blandina akawa ameingia ndani ya ofisi ya Namouih na kumkuta akiwa makini kuandika mambo fulani kwenye karatasi mezani kwake. Namouih aliponyanyua uso na kuona ni rafiki yake, akasitisha kuandika na kuendelea kumtazama. Blandina alikuwa amevalia kiblauzi cheupe kilichofunikwa kwa koti jekundu la kike, sketi nyeusi iliyoishia magotini na viatu virefu vya rangi nyekundu. Alipendeza. Akasimama tu sehemu ya mlangoni huku akitazamana na Namouih kwa hisia, kisha akapiga hatua mbili mbele na kusimama tena.

"Samahani Nam... uko bize?" Blandina akauliza kwa ustaarabu.

Namouih akalifunika kablasha lenye karatasi alilokuwa akiandikia, kisha akanyanyuka na kutoka upande wake wa meza na kuanza kumfata Blandina huku amenyoosha mikono yake mbele kuonyesha alitaka kumkumbatia. Blandina akapiga hatua chache mbele pia na kukutana naye, kisha marafiki hawa wakakumbatiana kwa upendo. Walielewana sana. Namouih alikuwa amevalia gauni refu lililoubana mwili wake kiasi kufikia kwenye supu za miguu, lenye rangi ya damu ya mzee na nyeupe, viatu vyekundu vya kuchuchumia, na nywele zake akizibana kwa nyuma kama kawaida. Wakaendelea kukumbatiana kwa sekunde chache, kisha wakaachiana na kushikana mikono kwa chini wakiwa karibu bado.

Blandina akaanza kusema, "Nam, am so sorry kwa jinsi nilivyozungumza jana, yaani...."

"Worry out mpenzi. Mimi ndiyo nikuombe aamahani kwa kweli. Nilivyofanya haikuwa poa. Nilidhani labda hata ungenichukia," Namouih akamwambia.

"Hapana, siwezi. Naomba tu tuyasahau eti? Ninaomba radhi tena kwa maneno yangu."

"Usiwaze mommy. Ila, nakuomba utengue kauli moja tu kwenye yale uliyosema..."

"Ndiyo... chochote."

"Usije kuacha kurudi kwangu tena," Namouih akasema.

Blandina akatabasamu na kutikisa kichwa kukubali. Namouih akaanza kuzishika nywele za rafiki yake kwa njia ya kuzichezea kidogo.

"Umechelewa kufika leo?" Namouih akauliza.

"Ee kidogo, nilipita kule garage kulifata gari. Wameshalitengeneza," Blandina akasema.

"Ahaa... sawa. Utakuwepo baadaye kusikiliza hukumu?"

"Ndiyo nitakuja."

"Okay. Oh, ona, kuna ishu moja nimepokea. Njoo," Namouih akamwambia.

Akaelekea mezani kwake tena na kuketi, huku Blandina akikaa kwenye kiti cha upande wa mbele wa meza hiyo akimtazama kwa umakini kusikiliza atakachosema.

"Kuna hii kesi mpya nimechukua, inahusu mtoto fulani wa miaka 12. Anasoma darasa la sita. Mwalimu wa somo la Historia amempiga sana na kumuumiza vibaya mno. Yuko hospitali amelazwa, na huyo teacher amefunguliwa mashtaka na wazazi wa huyo mvulana... wanataka afungwe," Namouih akaeleza.

"Huyo mwalimu ni mwanaume?" Blandina akauliza.

"Yeah."

"Kisa cha kumuumiza mtoto ni nini?"

"Huwezi amini. Yaani nasikia eti aliuliza swali darasani 'what is history?' huyo mvulana akajibu 'Clouds FM,' ndiyo kikawaka," Namouih akasema.

Blandina akaanza kucheka na kufunika mdomo wake kwa kiganja chake, naye Namouih akatabasamu na kutikisa kichwa chake kwa njia ya kusikitika.

"Acha masihara basi!" Blandina akasema.

"Well, inawezekana dogo alikuwa tu analeta ujanja, au ni utukutu kama unavyojua watoto lakini kumpiga mpaka anaenda kulazwa siyo jambo sahihi kabisa..." Namouih akaongea.

"Ila kweli..."

"Ingewezekana hii system ya kutandika wanafunzi iondolewe lingekuwa jambo bora maana walimu wengi wanaitumia vibaya na kuvuka mipaka hadi kuwatendea watoto kama ng'ombe... na sijui wanapata faida gani kuona watoto wakikaa kulialia tu..." Namouih akasema.

"Wanazitoa hasira zao hapo pia. Ng'ombe kwa jina la mwanafunzi ndiyo itikadi ya shule nyingi, na walimu watafanyaje? Wana-enjoy," Blandina akasema.

"Well, huyu jamaa lazima apewe fundisho, hili haliwezi kufumbiwa macho, na ninahitaji kukupatia ili ulishughulikie."

"Seriously?"

"Yeah. Sidhani kama litafika mahakamani huko ukili-handle vizuri kabisa kama kawaida yako. Utaweza bila shaka, si ndiyo?"

"Yeah I mean, ndiyo, nitaweza. Asante Nam-Nam," Blandina akakubali kwa shauku.

"Ahah... usijali. Ngoja nimalize kuandika mambo fulani, yapitie, then utai-handle. Ukipenda kukutana na mama yake baadaye namba yake ya simu na detail zingine zitakuwa hapa..."

"Sawa."

Namouih akaendelea kuandika huku akisema, "Baadaye nataka kuongea na Draxton, nimwombe samahani pia kwa sababu ya jana. Mliliongelea hilo mlipoondoka?"

"Hapana, na... sidhani kama alilikazia fikira sana. Potezea tu Namouih... ishapita," Blandina akasema.

"Yeah, ila bado nakuwa na kahisia kabaya moyoni maana nilitenda kitoto sana. Nitaongea naye tu kwa njia nzuri ili kuwa peace naye zaidi. Si unajua na hii kesi ya Agnes na Japheth mambo yanaweza yakawa...."

Namouih akaishia hapo baada ya kumwangalia Blandina na kuona ametazama sehemu moja kama anatafakari jambo fulani.

"Blandina..." Namouih akaita.

Akashtuka kiasi na kuitika, "Bee?"

"You good?" Namouih akauliza.

Blandina akatikisa kichwa kukubali, lakini Namouih akaona jambo fulani usoni kwake, kama huzuni.

"Kuna tatizo lingine?" Namouih akauliza.

Blandina akabaki kumtazama tu.

Namouih akaacha kuandika kabisa na kusema, "Niambie."

Blandina akashusha pumzi na kusema, "Ni Draxton."

"Amekufanyaje?"

"Hajafanya kitu... yaani... hajanifanya kitu..."

"Unamaanisha nini?"

"Jana tulirudi home... nikamkaribisha ndani... things were going great yaani... nilipoanza tu ku-make out pamoja naye akabadilika ghafla na kuondoka," Blandina akaeleza.

"Katikati ya... in the middle yaani, akaondoka tu?"

"Tena siyo kuondoka tu, akakimbia kabisa. Sikumwelewa yaani sijui ana shida gani? Au ndiyo yale mambo ya Yusufu na mke wa Potifa?"

"Mh... hilo nalo jipya."

"Nimejaribu kumpigia, wapi. Nimejaribu kum-text, nothing... hajajibu mpaka sasa hivi..."

"Tatizo linaweza kuwa nini? Anawezaje kuikimbia keki tamu kama hii? Anaumwa?"

"Ahah... sijui tu. We were hugging, and kissing... mara akaanza kuchemka sana, tena sana yaani. Nilipomuuliza tatizo nini, akaondoka tu," Blandina akaongea hivyo na kupiga ulimi ndani ya mdomo kwa njia ya kusikitika.

Namouih akabaki kutafakari jambo hilo kwa uzito sana.

"Just when I thought I'd wake up in bliss this morning (yaani nilipodhani tu kwamba ningeamka vizuri asubuhi hii)," Blandina akasema huku ameangalia chini.

"Ongea naye baadaye tukienda court. Lazima kutakuwa na explanation, sidhani kama yeye ni mjinga," Namouih akasema.

"Ndiyo, lakini mie ndiyo nabaki kuonekana kama mjinga. Amefanya hivyo, lakini bado nam-feel sana..."

"Yaani utafikiri siyo wewe! Unamkubali mno yaani... kupita maelezo?"

"Mno. Mpaka nashindwa kuelewa ni kwa nini."

"Mwambie. Mwambie hivyo ajue uko serious naye. Anaonekana kuwa mwerevu sana, kwa hiyo subiri tu usikie atakachosema," Namouih akamwambia.

Blandina akaupokea ushauri huo wa rafiki yake vizuri, na baada ya hapo Namouih akampa kablasha lile lenye taarifa za kesi ya mwalimu aliyemjeruhi mvulana mdogo, kisha akamuaga na kurudi kule nje kwenye ofisi yake binafsi.

Namouih aliachwa kimawazo baada ya kusikia kile Blandina alichomwambia. Alikuwa tayari kuweka pembeni maoni yake mabaya kumwelewa Draxton, ila baada ya rafiki yake kumpa ubuyu huo ikawa ni kama mashaka yake kumwelekea jamaa yakaamshwa tena. Kama tu alivyomuuliza Blandina muda mfupi nyuma, aliwaza sana ni kitu gani ambacho kingemfanya mwanaume yule amkimbie mwanamke mzuri kama rafiki yake, naye akawa anahofia kwamba huenda alificha kitu fulani kama ugonjwa au chochote ambacho kingemwathiri na rafiki yake pia endapo angeendelea kuwa naye kimahusiano.

β˜…β˜…

Ilitimia mida ya saa saba kamili mchana, na watu wote muhimu waliohitajika pale mahakamani wakawa wamefika. Baraza la wazee wa mahakama lilikuwepo pia, sambamba na waamuzi, na sasa ushahidi ule uliohitaji kuhakikiwa ulikuwa tayari. Agnes tayari alikuwa amefanyiwa vipimo na daktari tofauti na yule mwingine siku iliyopita, na majibu yalikuwa tayari. Video ile pia ilikuwa imehakikiwa na kuwekwa tayari kwa ajili ya maelezo ambayo yangetolewa kufikia hukumu iliyostahili.

Upande wa mtoa mashtaka, Namouih akatoa maelezo yake kuhusiana na hukumu aliyoona ilistahili kutolewa kwa sababu ya mambo yote hayo. Aliwaasa waamuzi kuona namna ambavyo vitendo vya kikatili kwa wanawake vinavyowaharibia mfumo wa maisha na kuwafanya washindwe kusonga mbele katika nyanja mbalimbali, hivyo akaomba mahakama itende kwa jicho kuu kuelekea suala hilo kwa kumpa Agnes alichostahili; haki. Upande wa mtuhumiwa, Draxton akaomba Japheth apewe hukumu ya kuachiliwa (judgement of acquittal), akisema kwamba upande wa mtoa mashtaka haujatoa ushahidi wa kutosha na sahihi kuthibitisha kwamba mtuhumiwa amefanya kosa, kwa hiyo akaiomba mahakama iamue kesi hiyo katika upande wa mtuhumiwa (favor).

Baada ya wawili hao kumaliza kazi yao hiyo, wakatulia sasa ili hatimaye vigezo vyote kupelekea hukumu ya mwisho visomwe. Hakimu akaanza kusoma marejeo muhimu kuelekea kesi hii ya ubakaji. Msichana wa miaka 19 kwa jina la Agnes Mhina alidai kwamba kijana aliyeitwa Japheth Warioba alimbaka usiku wa siku fulani wawili hao walipokutana kwenye nyumba ya wageni ili kuzungumza. Aliripoti tukio hilo kwa askari siku 3 baadaye, na ndiyo kijana huyo akakamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa sababu ushahidi wa jambo hilo ulikuwepo. Lakini kutokana na mambo fulani kuwa na dosari ndani ya ushahidi uliotolewa, baraza la waamuzi lilifikia mkataa kwamba ungepaswa kuhakikiwa kabla ya saa hii ya hukumu, na ndicho kilichofanyika.

Wakati hakimu alipokuwa akisema hayo, Agnes alionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana kiasi kwamba ikabidi Namouih amtulize kwa kumshika viganja. Hakimu akaendelea kusema kwamba baada ya majibu ya vipimo kutoka, iligundulika kwamba msichana huyu hakuwa na vidonda sehemu zake za siri, ambavyo bado vingekuwepo endapo kama kweli angekuwa ameingiwa kimwili kwa njia iliyomuumiza sana. Akaeleza kwamba walikuwa wameshamhoji daktari yule wa maabara ndogo aliyetoa vipimo bandia na kugundua kuwa alikuwa mpenzi wake Agnes, na wawili hawa walitunga hadithi hii ya uwongo ili kumkomoa kijana yule bila kueleweka sababu ni nini ya kutaka kumfanyia hayo. Kwa jicho la haraka yeyote angeweza kusema kwamba hiyo ni kwa sababu walitaka afungwe na kuwalipa kiasi cha faini ambacho Agnes alitakiwa kupewa.

Kwa upande wa ile video, ni kweli kwamba wawili hao walifanya mapenzi siku hiyo, lakini baada ya Japheth kuwa amehojiwa pia siku iliyopita aliweka wazi kwamba usiku ule yeye na Agnes walipokutana walikunywa kileo kidogo, ila inaonekana alileweshwa kwa sababu alikuja tu kuamka asubuhi akiwa ameachwa bila nguo mwilini. Kwa hiyo, Agnes na aliokuwa anashirikiana nao wakaitengeneza vizuri na kuitia sauti kwa njia ambayo ingefanya ionekane kweli msichana huyu alibakwa, lakini Agnes akaja kujichanganya mwenyewe kwa kusema alizibwa mdomo na Japheth. Agnes alikuwa analia sana huku akimwangalia mama yake mara kwa mara kwa njia iliyoonyesha hofu, na Namouih akiwa ameshatambua hiyo ingeelekea wapi, akafumba macho yake kwa kusikitika.

Kutokana na mambo hayo, hakimu akatoa hukumu ya kumwachilia huru Japheth Warioba haraka iwezekanavyo, na kusema kwamba Agnes angetakiwa kubaki chini ya ulinzi kutokana na kutoa madai ya uwongo chini ya kiapo cha mahakama. Japheth alifurahi sana. Akapeana mikono na Draxton huku akimshukuru kutoka moyoni mwake kwa kumsaidia sana. Kwa upande wake Agnes, binti alishikwa na askari wa ulinzi hapo na kutiwa pingu, kwa kuwa alikuwa amebaki na mambo mawili ya kufanya baada ya jambo la hila yeye na wenzake walilopanga kutofanikiwa: alipie faini kubwa sana, au apewe kifungo jela.

Baada ya hakimu kuondoka, askari aliyemshikilia Agnes akaanza kuondoka pamoja naye huku binti huyo akimlilia mama yake. Mama yake mwenyewe alikuwa amekaa tu kwenye benchi huku ameifunika midomo yake kwa kiganja, akionekana kuwa na huzuni sana. Yote hayo yalikuwa kwa ajili gani? Ndugu za Japheth walimshukuru sana Draxton hapo, kisha wakaanza kuondoka kuelekea nje baada ya ushindi wao. Namouih akamfata Draxton na kumnyooshea mkono wa pongezi ya kirafiki, naye Draxton akaushika na kukubali pongezi hiyo. Kisha mwanamke akaenda kwenye meza aliyokuwa ameketi na kuanza kukusanya vilivyo vyake, ikiwa ndiyo mara ya kwanza kabisa kwake kupoteza kesi tokea alipoanza mlolongo wake wa uanasheria (career).

Blandina bado alikuwa mahakamani humo baada ya kumaliza pindi hiyo iliyokuwa na msisimuo wa hali ya juu. Wakati tu Namouih alipomaliza kupeana mikono na Draxton, wawili hawa wakatazamana kwa sekunde kadhaa. Ulikuwa utizami ulioongea mengi, na ilionekana kwamba Draxton alikuwa anajaribu kuisoma akili ya mwanamke huyu kutokana na jinsi alivyoangaliwa. Blandina akanyanyuka tu kutoka alipokuwa ameketi na kuanza kuelekea nje, naye Draxton akaanza kuelekea huko pia. Namouih aliona jambo hilo, na ingawa alitamani kujua yale ambayo yangeendelea huko nje, angepaswa tu kusubiri kuja kusikia rafiki yake angesema nini.

Yeye Namouih akatoka nje pia na kuwawahi watu wa familia yake Japheth, ambao bado walikuwa eneo hilo la nje la mahakama. Akawapa pongezi kwa kupata ushindi, na akakazia kwamba kumtetea Agnes ilikuwa ni sehemu ya kazi yake kwa sababu wanasheria hawatakiwi kuhukumu vitu kwa misingi yao binafsi tu, lakini bado akamwomba radhi Japheth kwa kilichompata. Japheth akasema Mungu amekuwa mkubwa kwake kwa kumletea mwanasheria Draxton, kwa sababu alidhani angekwenda jela na hivyo hakungekuwa na mtu wa kuitunza familia yake na mama yake ambaye alikuwa mgonjwa.

Namouih akauliza namna ambavyo kijana huyu alikutana na Draxton, akitaka kujua kama walifahamiana sana, lakini Japheth akasema hapana; hakumfahamu sana mwanasheria yule. Ni kwamba Draxton alimtafuta Japheth yeye mwenyewe na kusema angemsaidia, lakini mwanzoni hakutaka ajulikane ndiyo maana akamwambia atulie tu mpaka siku ya kusikilizwa kesi ndiyo angejitokeza, na alikuwa mtu mmoja makini aliyemwahidi kabisa ushindi. Namouih alishangazwa kiasi na jinsi ambavyo Draxton alikuja ghafla tu ndani ya kesi hii na kuonyesha kipawa kikubwa sana kilichofunua mambo kwa njia sahihi kabisa ambayo haingekuwa rahisi kwa yeyote kufanya. Yaani bila Draxton, mtu yeyote yule angeamini kabisa kwamba Japheth alimbaka Agnes, kwa hiyo mwanamke huyu akawa anataka kujua mengi zaidi kuhusu mwanaume huyo.

Wakati huo, Blandina alikuwa akielekea pale alipoegesha gari lake, bila kugeuka nyuma hata mara moja, lakini alijua wazi kwamba Draxton alikuwa anamfata. Alipoufikia mlango wa mbele wa gari lake, sauti ya Draxton ikasikika akimwita kabla hajaingia ndani ya gari. Blandina akatulia tu, lakini hakuitika wala kugeuka, naye Draxton akawa amefika nyuma yake.

"Blandina... tunaweza kuongea?" Draxton akasema kwa sauti ya chini.

"Tuongee nini? Hauna mambo mengine ya kukimbilia?" Blandina akauliza pia kwa sauti ya chini.

"Kuhusu jana. Nahitaji kuomba samahani..."

Blandina akamgeukia, kisha akasema, "Nilidhani uko tofauti na wanaume niliowapitia, na kiukweli uko tofauti. Ila ni utofauti nisiouelewa kabisa, kwa hiyo nakuomba unieleweshe nini maana ya kile ulichofanya jana."

"Sina sababu yoyote ya kujitetea kwa nilichokifanya..."

"Mmmm... kwa hiyo unataka uniacheje?"

"Utakavyoamua tu Blandina. Ona, sikufanya vile kwa nia ya... labda kukuumiza...."

"Unaumwa?" Blandina akamkatisha.

"Naam?"

"Unaumwa? Kama una ugonjwa fulani labda unaogopa kuusema, au unaogopa labda...."

"Kwamba nitakuambukiza? Nini, kama UKIMWI?"

"Me sijasema hivyo, ni wewe. Vipi, ndiyo hali halisi au?"

"La Blandina... siumwi ugonjwa wa namna hiyo."

"Sasa shida ni nini? Kwa nini uli... au labda una tatizo la kutoamsha kwa muda mrefu?"

Draxton akatabasamu na kuangalia chini.

"Niambie tu nijue. Jana Draxton, ulisema natakiwa kuonyesha kwamba nataka kutulia. Ninakwambia sasa hivi kwa uhakika kabisa. Ninataka kutulia nawe," Blandina akasema kwa uhakika.

Draxton akamwangalia tu machoni kwa hisia.

"Ahah... naonekana kama zumbu yaani... ila ndiyo ukweli. Nataka tuendelee kuwa... well, tuanzishe jambo zuri baina yetu. Na, sidhani kama tutafika mbali endapo labda una tatizo, au mwanamke mwingine, halafu hautaki kusema. Ni bora nikajua," Blandina akasema kwa hisia.

"Kama nikikwambia nina tatizo?" Draxton akauliza.

"Tatizo gani?"

"Sina tatizo Blandina ila... niseme tu nina muda mrefu sijawa na mwanamke na... jana nilikuwa overwhelmed."

"Okay, sawa haina shida, si ilikuwa mizuka tu? Kama hauna tatizo basi...."

"La. Blandina... sidhani kama mimi na wewe tutafika huko unakotarajia," Draxton akamwambia.

"Kwa nini?"

"Iko hivyo tu."

"Ahah... sikuelewi... yaani..."

"Sitaki kukupa sababu yoyote kwa nini iko hivyo, na wala sitaki uje ujute kuwa na mtu kama mimi."

"Kwani wewe ukoje? Draxton hujanipa sababu yoyote kuhisi labda utaniumiza. In fact, sijawahi kukutana na mwanaume kama wewe, ni utofauti wako ndiyo unaonifanya nitake sana kuwa nawe..."

"Blandina..."

"Draxton mimi nimekupenda. Nimekupenda," Blandina akasema kwa hisia.

"Usiharakishe kufikiri hivyo. Kumpenda mtu huchukua muda, na kumjua, na...."

"Mimi sihitaji muda Draxton, ninajua nimekupenda. Uko sahihi. Uko sahihi. Ninataka sana kupendwa kwa dhati na ndiyo maana ni rahisi kwangu kupenda. Lakini kwa wakati huu, ninataka... ninahitaji kupendwa na wewe. Sijui ikiwa unaniona kama mjinga...."

"La..."

"...lakini nimekupenda wewe Draxton. Kama kweli hauna tatizo, ninakuomba unipende pia," Blandina akamalizia maneno yake.

Draxton akainamisha uso wake.

"Kuna njia nyingi sana za kufurahishana, si lazima sex. Nisamehe kwa kuwahi kukimbilia huko ikiwa hauhitaji hilo kwa sasa, lakini bado nakuhitaji sana. Nataka... nataka tu kuwa nawe. Unanifanya najihisi tofauti sana, na ndiyo maana nakuwa nataka kuendelea kufurahia hilo," Blandina akaongea kwa hisia.

"Hata baada ya nilichokifanya jana na kukwambia mambo haya, yaani bado...."

"Najua una sababu zako, lakini hata usiponiambia kwa sasa haitakuwa na shida. Ninakuamini. Draxton... nakupenda."

"Oh Blandina..."

Draxton aliona kweli mwanamke huyu aliamini kile ambacho alikisema yeye mwenyewe, na ingawa alikuwa anajaribu kumtolea mbali, jinsi alivyomwonyesha uhitaji wa kuwa naye ni jambo lililomvutia sana kihisia kumwelekea. Blandina akakishika kiganja kimoja cha Draxton huku akimtazama kwa hisia za mapenzi ya dhati kabisa, na mwanaume huyu akakibana kiganja cha bibie kiasi.

"Nimejaribu sana kuepuka wengi, lakini wewe... huepukiki," Draxton akamwambia.

"Najua nina mvuto kwako... sema tu unajishaua," Blandina akasema.

Draxton akatabasamu kwa mbali, kisha akasema, "Sawa. Blandina... ninajipa nafasi ya kuwa nawe, maana ukweli ni kwamba... ninatamani kupendwa pia."

Blandina akatabasamu.

"Nitajitahidi kuwa mzuri kwako, ila...."

"Achana mambo ya ila bwana. Just be you. Napenda sana jinsi ulivyo. Nitakupa furaha Draxton, mimi ni wako kuanzia sasa, na sitaruhusu chochote kinichukue kutoka kwako," Blandina akasema.

"Wow. Una maneno mazuri sana. Huwa unapiga zoezi kwenye kioo?"

"Ahahahah... practice makes perfect. Ila no, haya yanatoka moyoni. Nataka ushibe ukiwa na mimi..."

Draxton akatabasamu, naye Blandina akacheka kidogo kwa haya.

"Hongera kwa ushindi wa kesi," Blandina akasema.

"Asante. Unaelekea wapi now?" Draxton akamuuliza.

"Siendi kokote. Wewe?"

"Kuna... kazi fulani nataka kufanya... naelekea nje ya jiji."

"Mh! Unaondoka kabisa?"

"Ahahah... la. Nitarudi jioni. Vipi tukikutana muda huo?"

Blandina akatabasamu na kusema, "Sawa. Ila siyo kwamba unataka kinikimbia tena?"

"Ahahahah... sitakukimbia tena, usinikariri hivyo. Nataka kuwa pamoja nawe pia. Na-enjoy company yako."

"Mimi pia Draxton."

Draxton akatikisa kichwa kuonyesha uelewa, kisha akamkumbatia kwa wororo. Blandina hakuwa ametarajia kukumbatiwa eneo hilo la mahakamani, lakini hii ikampa furaha sana na yeye kulirudisha kumbatio la mwanaume huyo kwa upendo. Draxton akamwachia na kusema angempigia baadaye, naye Blandina akakubali. Mwanaume akaondoka hapo kuelekea kwenye gari lake, naye Blandina akamtazama kwa ufupi na kisha kuishika simu yake na kuanza kupitia mambo fulani.

Alipoangalia upande mwingine wa eneo hilo la mahakama, akamwona Namouih akiwa amesimama huku anamtazama, na rafiki yake huyo akamwonyesha ishara kwa kichwa kuuliza 'vipi?' Blandina akanyanyua tu dole gumba kuonyesha mambo yako safi, na Namouih akatikisa kichwa na kuonyesha ishara ya kumwambia kwamba wangeongea baadaye, kisha marafiki hawa wakaachana na kuingia kwenye magari yao ili kuondoka hapo.

β˜…β˜…

Muda mfupi baadaye, Namouih akawa amerudi ofisini kwake baada ya kuvunjiwa rekodi ya kutopoteza kesi hata moja toka alipoianza kazi yake, akiwa amepigania kesi kubwa 34 na kushinda zote isipokuwa hii. Sikuzote alichukua kesi ambazo alikuwa na uhakika wa kupata ushindi, na hata kesi ya Agnes ilionekana kabisa kuwa ya ushindi kwake. Lakini mwanaume yule, Draxton, akawa amemfumbua macho zaidi kwa wakati huu ili asijiamini kupita kiasi wakati mwingine, hasa kwa kuwa jambo hilo lilifanya ionekane kama alikuwa anafanya kazi kwa mazoea.

Wakati huu, Blandina alikuwa ameondoka kwenda kukutana na mama wa mvulana yule aliyelazwa baada ya kupigwa vibaya sana na mwalimu wake, ili afahamiane naye na kuanza kushughulika na mashtaka aliyotoa. Hivyo Namouih akawa ofisini kwake akijaribu kutafuta taarifa za ndani kuhusiana na mwanasheria Draxton. Alisaka mambo mengi, lakini aliyoyapata yalikuwa yale ambayo tayari aliyafahamu. Hakukuwa na habari zozote juu ya familia yake, mahali alikoishi, wala sehemu aliyosomea sheria na kwa muda gani. Kwa kumtazama tu kijana yule alikuwa na umri mdogo sana kuweza kuwa amemaliza masomo ya sheria na kupata uzoefu wa kutetea kesi mahakamani, kwa hiyo alitaka kujua tu hata kitambulisho chake cha uanasheria kilitoka wapi.

Ilimshangaza kiasi kuona jinsi ambavyo habari nyingi za mwanaume yule ziliwekwa usiri wa hali ya juu, naye akafikiria kuja kuongea na Blandina kuhusu hilo na kuona angesemaje. Ikawa imefika mida ya jioni ya saa kumi, naye akapigiwa simu na kujulishwa kwamba Agnes alikuwa ameachiliwa kutoka rumande baada ya kulipiwa dhamana kubwa sana. Akauliza ni nani ambaye alikuwa amemlipia pesa hizo, naye akaambiwa kwamba haikujulikana ni nani kwa sababu zilipelekwa na mwakilishi ambaye hakusema mengi sana kujihusu, bali baada tu ya kumtoa Agnes, binti akafurahi sana na kuondoka pamoja naye wakisema wanaenda nyumbani.

Namouih akifikiri kwamba ilikuwa ni mtu wa karibu na familia ile, akaamua kumpigia mama yake Agnes na kumuuliza kuhusu hilo, lakini mama ya Agnes akashangaa na kuanza kuuliza kwa shauku ikiwa kweli Agnes aliachiliwa. Jambo lililomchanganya Namouih kiasi lilikuwa kwamba binti huyo alitakiwa kuwa amepelekwa nyumbani kwao lakini bado hata mama yake hakujua kama ameshatoka. Akamwambia tu mama yake kwamba amtafute, na yeye Namouih angemtafuta pia. Akawa anawaza labda aliyemtoa alikuwa mtu wake mwingine mwenye mipango naye ya kiulaghai-laghai, naye akatikisa kichwa chake kwa kusikitika baada ya kukumbuka namna ambavyo alidanganya sana kuhusu kubakwa.

Baadaye, Blandina akawa amerejea na kumwambia Namouih kwamba alikuwa amemaliza kuwapanga wazazi wote wa mvulana yule, na kwamba lazima mwalimu aliyetenda ukatili kwa mtoto angefungwa. Akamwambia pia kwamba ana mipango jioni hiyo ya kukutana na Draxton baada ya wao kuwa wapenzi rasmi sasa, naye Namouih akauliza vipi kuhusu kitendo kile cha jamaa kumkimbia, aliamua kukipotezea tu? Blandina akamwambia hilo waliliweka pembeni kwanza, na yeye alichoangalia zaidi kwa wakati huu ilikuwa kufurahia uhusiano wake mpya na Draxton kwa njia yoyote ile ambayo ingekuwepo, na akamwomba Namouih amuunge mkono kwa hilo.

Namouih akiwa hataki kumkwaza rafiki yake, akaona asimwambie kuhusu yeye kuyachunguza maisha ya Draxton na kusema anamuunga mkono kwa asilimia zote kabisa. Blandina akafurahi sana. Akamwambia kwa sababu hawakuwa na kazi za lazima basi watoke kwenda kupata kinywaji huku yeye Blandina akisubiri Draxton arejee. Akasema alikuwa ameshawasiliana naye, na leo wakikutana tena alitaka mambo baina yao yapambe moto. Namouih hakuwa na kipingamizi kwa hilo, naye akafunga kompyuta yake na kuanza kuondoka pamoja naye huku akimwambia kuhusiana na suala la Agnes kuachiliwa kutoka kifungoni.

Wawili hao wakaelekea katikati ya jiji na kuingia ndani ya kumbi moja kubwa sana iliyokuwa imechangamka. Ni sehemu ile ile ambayo marafiki hawa walipendelea kwenda mara nyingi. Wanaume kadhaa na wanawake waliwashobokea mno, lakini wawili hawa wakaketi kivyao sehemu ya pekee na kuletewa vinywaji walivyoagiza. Wakaendelea kufurahia maongezi ya hapa na pale wakikumbushia na kesi ya leo mpaka inafika saa mbili usiku, ndipo simu yake Namouih ikaita.

Akakuta namba ngeni kabisa, na baada ya kupokea na kuzungumza kidogo, akaweka uso ulioonyesha mshangao mkubwa sana. Blandina akaanza kumuuliza tatizo ni nini, naye Namouih akamalizia maongezi hayo kwa kusema ameielewa sehemu hiyo na kwamba anakwenda huko upesi. Alipoishusha simu, akamwangalia rafiki yake kwa njia ya mshangao sana, naye Blandina akauliza shida ni nini kwa mara nyingine tena.

"Agnes... Agnes ameuawa Blandina!"

"Ati?!!" Blandina akashangaa.

"Oh Allah..." Namouih akasema na kuinamisha uso wake kwa kusikitika.

"Nam... nini kimetokea?" Blandina akauliza.

"I don't know... wamenipigia simu... mwili wake umepatikana huko.... nahitaji kwenda ili nijue nini kimetokea..." Namouih akasema huku akisimama.

"Tunaweza kwenda pamoja. Ngoja nimwambie Draxton..."

"Hapana Blandina, usijali. Wewe msubiri Draxton... mengine yatafata baadaye. Nitakupigia," Namouih akasema.

"Sawa... kuwa mwangalifu..." Blandina akamwambia.

Marafiki hawa wakakumbatiana na kuagana, naye Namouih akamwacha rafiki yake hapo na kuelekea kwenye gari lake ili aende huko ambako kisa hiki kipya kilikuwa kimezuka.

Majanga yalikuwa hayaishi. Aliyekuwa amempigia alimwambia kwamba kule kwenye eneo la tukio bado maaskari hawakuwa wamefika, na namba yake Namouih ndiyo ya mwisho kuipigia simu ya Agnes walipoipata sehemu aliyouliwa. Eneo hilo halikuwa mbali sana kutokea pale Namouih na Blandina walipokuwa, kwa hiyo haikuwa ngumu mno kwa Namouih kufika huko. Ilikuwa ni kwenye nyumba ndogo tu isiyojulikana mmiliki wake ni nani, na baada ya Namouih kufika hapo aliweza kuona watu wakiwa wamekusanyika kwa nje kuzunguka sehemu ya kuingilia ndani kule.

Akalisimamisha gari lake umbali mfupi kutokea hapo, naye akashuka na kumpigia simu Efraim Donald ili amwambie alikokuwa kwa kuwa aliona kwamba angechelewa kwenda nyumbani kwa sababu ya dharura hii. Lakini alipogeuza shingo yake upande mwingine wa eneo hilo, akaona jambo fulani lililofanya mkono wake ulioshika simu ushuke taratibu mpaka chini. Huko aliweza kuona gari lile jeusi aina ya Frester, na mtu aliyefungua mlango wa sehemu ya kuingilia dereva hakuwa mwingine ila Draxton mwenyewe!



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.

WhatsApp no: +255 787 604 893

e-mail: eltontonny72@gmail.com
 
CHANGE

Story by Elton Tonny

Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha

R-rated 18+


ILIPOISHIA....

Baada ya Namouih kupoteza kesi kwa mara ya kwanza kabisa dhidi ya Draxton, aliyekuwa anamsimamia anatiwa chini ya ulinzi, msichana wa miaka 19 aliyeitwa Agnes. Baadaye siku hiyo, Namouih anataarifiwa kwamba Agnes ametolewa dhamana na mtu asiyejulikana, naye anajaribu kumtafuta mama yake kuuliza kama binti amesharejea nyumbani ila mzazi huyo anakanusha, huku akiwa amefurahi kujua binti yake ameachiliwa. Kwa kutaka kujiburudisha kidogo baada ya siku hiyo yenye kuvunja moyo kiasi, Namouih anakubaliana na Blandina kukutana sehemu yao waliyopendelea kwenda ili kunywa kidogo, huku Blandina akimgojea Draxton aje kumchukua kwa sababu walikuwa na mpango wa kutoka usiku.

Wakaendelea kufurahia maongezi ya hapa na pale wakikumbushia na kesi ya siku hiyo mpaka inafika saa mbili usiku, ndipo simu yake Namouih ikaita. Akakuta namba ngeni kabisa, na baada ya kupokea na kuzungumza kidogo, akaweka uso ulioonyesha mshangao mkubwa sana. Alipewa taarifa kwamba Agnes ameuawa, naye akamwambia Blandina. Kwa kuwa iliwashangaza wote kwa kutojua ni nini kilikuwa kimetokea, Namouih akamuaga Blandina ili aharakishe kwenda huko, huku rafiki yake akibaki kumsubiri mpenzi wake.

Eneo hilo la tukio halikuwa mbali sana kutokea pale Namouih na Blandina walipokuwa, kwa hiyo haikuwa ngumu mno kwa Namouih kufika huko. Ilikuwa ni kwenye nyumba ndogo tu isiyojulikana mmiliki wake ni nani, na baada ya Namouih kufika hapo aliweza kuona watu wakiwa wamekusanyika kwa nje kuzunguka sehemu ya kuingilia ndani kule. Akalisimamisha gari lake umbali mfupi kutokea hapo, naye akashuka na kumpigia simu Efraim Donald ili amwambie alikokuwa kwa kuwa aliona kwamba angechelewa kwenda nyumbani kwa sababu ya dharura hii.

Lakini alipogeuza shingo yake upande mwingine wa eneo hilo, akaona jambo fulani lililofanya mkono wake ulioshika simu ushuke taratibu mpaka chini. Huko aliweza kuona gari lile jeusi aina ya Frester, na mtu aliyefungua mlango wa sehemu ya kuingilia dereva hakuwa mwingine ila Draxton mwenyewe!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA KUMI

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Namouih akaendelea kumwangalia na kumwona anaingia ndani ya gari lake hilo, kisha likawaka na kuanza mwendo kutoka eneo hilo. Alishangaa sana. Draxton alikuwa anafanya nini huku? Si Blandina alisema kwamba mtu wake huyo alikuwa anarejea kutoka safari fupi nje ya mji wao na kwenda kumpitia ili wakajivinjari? Alikuwa anafanya nini huku karibu kabisa na nyumba ya tukio la mauaji ya binti ambaye ni yeye mwenyewe Draxton ndiye aliyemfichua leo kuwa mwongo? Kulikuwa na uhusiano wowote kati yake na jambo hilo lililokuwa limetokea?

Maswali mengi sana yakaendelea kupita kichwani kwake Namouih, na hakuwa ametambua kwamba wakati huo aliokuwa amezubaa, mume wake upande wa pili alikuwa amepokea simu wakati ule Namouih ameushusha mkono wake, na baada ya Efraim Donald kuona kimya tu, akakata na kumpigia tena. Namouih akashtushwa na mtetemo wa simu yake, ndipo akapokea na kumwambia Efraim yaliyojiri. Mume wake akatoa pole na kusema ajitahidi kuwa mwangalifu na asisogelee chochote mpaka maaskari wafike hapo, ndipo simu ikakatwa baada ya hapo.

Namouih akatulia kidogo na kutazama upande ule ambako Draxton alionekana muda mfupi nyuma. Yaani kama ni mashaka basi yalikuwa yameongezeka zaidi hata sasa, naye akatazama tena kule kwenye ile nyumba ambayo alijua binti yule angekuwemo. Hakujua hata ni jinsi gani alivyokuwa ameuawa, hivyo akatafuta namba ya mama yake Agnes na kumpigia ili ampe taarifa hizo. Lakini akasitisha kufanya hivyo baada ya gari tatu za maaskari kufika hapo, na nyingine aliyoitambua upesi sana baada ya kuzisoma namba zake za usajili. Ilikuwa ni Toyota Prado nyeupe ya yule rafiki yake mpelelezi, yaani Felix. Mwanamke akaanza kulielekea pale lilipoegeshwa, huku sasa baadhi ya waandishi wa habari wakianza kufika eneo hilo na kamera zao.

Maaskari waliofika hapo wakaanza kuwaambia watu wasogee pembeni ili waingie kule ndani, na waandishi wa habari wakielekea huko pia ili kuchukua tukio hilo. Felix akawa ameshuka kutoka kwenye gari lake akiwa pamoja na wapelelezi wengine wawili, naye akamwona Namouih akimfata. Akamuuliza alikuwa anafanya nini hapo, ndiyo Namouih akamweleza kwamba msichana aliyetaarifiwa kwamba ameuawa ni mtu aliyetoka kumsimamia kwenye kesi mapema ya siku hii, hivyo alikuwa hapo kujua ni nini kilichotokea. Felix akamwambia angoje hapo ili aende kule ndani kuona kama tukio hilo lilikuwa na uhusiano na mambo yale aliyokuwa anapeleleza, naye akaelekea huko pamoja na wenzake akimwacha Namouih anasubiri hapo nje.

Baada ya muda mrefu kupita, Namouih akaanza kuwaona maaskari wale wakiutoa mwili wa aliyeuawa ukiwa umefunikwa kwa shuka kuuzunguka wote, nao wakaupeleka kwenye moja ya magari yao ili bila shaka upelekwe mochwari. Hatimaye Felix akawa ametoka ndani huko pia, huku akijitahidi kuwakwepa waliokuwa wanawauilza maswali, naye akamfata Namouih mpaka karibu ili aanze kumweleza kilichotokea.

"Vipi Felix? Nini kimempata Agnes?" Namouih akauliza.

Felix akashusha pumzi na kusema, "Yale yale mambo niliyowaambia Namouih."

"Nini?!" Namouih akasema kwa mshangao.

"Mwili wake wa baridi sana. Sehemu ya chini ya tumbo lake imekatwa na... hana ulimi mdomoni. Ni mambo yenye kutisha sana," Felix akasema.

Namouih akawa ameuziba mdomo wake kwa kiganja, akionekana kuhuzunika sana.

"Kibaya zaidi ni kwamba hakuna mtu yeyote aliyemwona wakati anaingia hapo, na haijulikani aliingia na nani. Tumeuchunguza mwili wake lakini hauna fingerprint zozote wala clue yoyote iliyoachwa ambayo inaweza kutusaidia kumkamata anayefanya haya... inakera sana..." Felix akaongea kwa hasira.

"Ina maana... Felix jamani... haya mambo yataendelea mpaka lini?" Namouih akauliza.

"Yaani hata sielewi. Hii ndiyo mara ya kwanza kisa kama hiki kimetokea ndani ya nyumba. Namaanisha... kwa kawaida tungewakuta wakiwa wamefukiwa au sehemu za nje kama mara ya mwisho... lakini huyu... inaonekana muuaji wake alikuwa na haraka sana leo... lakini bado hatujawa na njia ya kutambua ni nani hasa," Felix akamwambia.

"Felix... chunguzeni kwa umakini zaidi. Kwa watu wengi hili litakuwa jambo jipya, lakini unajua kabisa kwamba limeendelea kwa muda mrefu sana. Hawa watoto wanakufa hivi kwa nini? Tafadhali... fatilia kwa kina ujue ni nani ambaye alimtolea dhamana huyu msichana leo, kwa sababu ndiyo huyo huyo aliyemleta huku. Yaani me hata sikupewa taarifa yoyote ile, mama yake hajui mtoto yuko wapi, halafu sasa hivi apewe tu taarifa kwamba amempoteza? Aah!" Namouih akasema hivyo kwa mkazo.

"Ondoa shaka Namouih, tutazama zaidi kwenye hili. Nikwambie tu kiukweli... naona afadhali sasa hivi kwamba jambo hili litakuwa wazi kwa wengi maana sikuona faida yoyote ya kulificha kwa muda mrefu... ni hasara kubwa tu ndiyo tuliyoendelea kupata. Kila kitu watashughulikia watu hawa kwa hiyo... wewe nenda nyumbani kapumzike..." Felix akamwambia.

"Lakini vipi kuhusu.... "

"Usijali Namouih. Wewe nenda tu. Tutawasiliana," Felix akasema.

Namouih alionekana kuwa ndani ya taharuki nzito sana, kwa sababu jambo hilo lilimfanya aumie mno. Kuna ile hali fulani ya kuhisi hatia iliyompata kwa sababu hakufatilia mambo vizuri baada ya kupewa taarifa kwamba Agnes ametolewa kifungoni na mtu asiyejulikana mpaka janga hilo kutokea. Lakini pia ni suala la Draxton kuonekana eneo hilo ndiyo lililomchanganya zaidi. Kama kwa kufikiria tu labda alipata taarifa za kifo cha Agnes na kuja huku lingekuwa wazo la haraka kuingia akilini, basi ni nani aliyempa taarifa? Hapana. Hapa alihisi kabisa kwamba mwanaume yule alikuwa akifanya mchezo mbaya sana, na kama angeendelea kuachiliwa hivi hivi tu basi huenda mambo haya mabaya yangeendelea kutokea.

Akaingia ndani ya gari lake akiwa ameghafilika sana, naye akaona ampigie Blandina simu ili amjuze kuhusu mambo yaliyokuwa yametokea. Baada ya Blandina kupokea na kuuliza kulikoni, Namouih akaeleza wazi namna Agnes alivyouawa, na rafiki yake huyo akahuzunika sana na kutoa pole. Namouih akamuuliza ikiwa wakati huu tayari alikuwa na Draxton, naye Blandina akakubali, akisema kwamba Draxton alikuwa akimpeleka yeye Blandina kumwonyesha alipokaa jijini hapo. Namouih aliingiwa na wasiwasi sana. Ni ile fikira ya kwamba huenda Blandina angejikuta ndani ya hali kama iliyomkuta Agnes kwa sababu ya kupelekwa asikokujua na mwanaume huyo mwenye njia fulani za siri mno, lakini angeweza vipi kumwambia rafiki yake huyo kwa njia ambayo isingemuudhi au kumkwaza kama ilivyotokea usiku wa jana?

Namouih akamwambia Blandina awe mwangalifu sana kwa sababu vitendo hivi vya kikatili vingeweza kutokea sehemu yoyote ile, naye Blandina akamwambia asiwaze kwa sababu alikuwa salama mikononi mwa Draxton. Namouih akakata simu na kuinamisha kichwa chake kwenye usukani kwa kusikitika sana, na akihofia mengi. Hakuwa na uhakika kuhusu kile alichokihisi kumwelekea Draxton, lakini machale yake yalimwambia kwamba yule hakuwa mtu mzuri kabisa. Na sasa huenda rafiki yake kuwa pamoja naye kungeleta matatizo hata zaidi. Akasali kwa Mungu ili ampe ulinzi Blandina, naye akawasha gari lake na kuanza kuondoka eneo hilo ili aende nyumbani.

β˜…β˜…

Upande wa wapendanao, yaani Blandina na mpenzi wake mpya kwa jina la Draxton, walikuwa mwendoni ndani ya gari la mwanaume huyu baada ya kukutana. Muda ule ambao Namouih alimwacha Blandina na kwenda kufuatilia tukio la Agnes, mwanamke huyu alimtafuta Draxton kwa simu na kuuliza kama alikuwa amesharejea jijini, naye Draxton akasema hakuwa mbali sana hivyo Blandina ajiandae tu naye angempitia kwake. Kwa hiyo Blandina alitoka hapo na kwenda nyumbani kwake ili kujiweka vizuri zaidi kimwili kwa ajili ya kukutanika kwake na mpenzi wake huyo.

Baada ya Draxton kumfikia Blandina saa kama moja baada ya hapo, mwanamke akapanda ndani ya gari lake akiwa amependeza sana na kuuliza ni wapi walipokuwa wanaenda. Ndiyo Draxton akamwambia alitaka kumpeleka akapaone pale alipoishi, na alikuwa na mpango mzuri sana kwa ajili ya mrembo huyu. Hisia nzuri sana za Blandina kumwelekea mwanaume huyo zilimfanya asahau hata ishu ya Agnes kuuawa na kufurahia tu nafasi hiyo ya kuwa pamoja na Draxton, na ndipo walipokuwa mwendoni kuelekea huko akapigiwa simu na Namouih, ambaye alimjuza kuhusu yaliyotokea na kumwambia awe mwangalifu.

Alipokata simu, Blandina akamwangalia Draxton na kusema, "Hivi umeshasikia?"

"Kusikia nini?" Draxton akauliza.

"Agnes ameuawa Draxton," Blandina akasema.

Draxton akatulia kidogo, bila hata kuonyesha mshangao wowote wa kinafiki, naye akasema, "Ndiyo. Nafahamu hilo."

"Mbona hujaniambia?"

"Nilijua tayari ungekuwa unafahamu, na sikutaka kuharibu wakati wetu huu mzuri..."

"Mm.. Draxton! Yule mtoto unajua tumetoka tu kumwona leo mahakamani halafu unasema hivyo?"

"Samahani. Ila ni kweli... sikutaka hilo jambo liingilie mambo yetu. Itakuwa mbaya sana tukifurahia usiku huu kwa sababu Agnes amekufa? Ikiwa unataka tunaweza kuahirisha...."

"No, Draxton sijamaanisha hivyo. Roho tu inaniuma. Namouih ndiyo ananiambia sasa hivi kwamba ameuliwa kikatili sana, kama tu wasichana ambao...."

Blandina akaishia hapo baada ya kukumbuka kwamba kitu alichotaka kusema hakutakiwa kukisema.

Draxton akamwangalia na kuuliza, "Kama wasichana ambao?"

Blandina akaangalia mbele ya gari na kubaki kimya.

"Kuna jambo fulani ambalo ni kuu sana hapa eti?" Draxton akauliza.

"Hapana..." Blandina akasema.

"Niambie Blandina. Unaweza kuniamini," Draxton akasema.

Blandina akamtazama, kisha akaanza kumwambia mambo yote ambayo rafiki yake mpelelezi, yaani Felix, alikuwa amewaambia yeye na Namouih siku kadhaa nyuma kuhusiana na vifo vya wasichana matineja waliouawa kwa kukatwa matumbo yao. Akamweka wazi kuwa muuaji hakuwa amepatikana mpaka sasa, na watu waliokuwa wanafanya upelelezi walificha tu mambo hayo mpaka wakati huu. Draxton alikuwa anamsikiliza kwa umakini sana, naye akasema kwa kweli mambo yote hayo hayakuwa mazuri hata kidogo, na ingehitajika nguvu ya ziada kwa waliofanya uchunguzi kuweza kumbaini msababishi wa mambo hayo ili watu wasiendelee kupoteza maisha.

Basi, baada ya mwendo wa dakika kadhaa, Draxton akalisimamisha gari lake nje ya nyumba fulani kubwa iliyozungushiwa uzio wa ukuta mrefu. Akamwambia Blandina kwamba hapo ndipo alipoishi, ikiwa ni nyumba ya kupanga, na kulikuwa na wapangaji wengine watatu na familia zao. Yaani ilikuwa ni kubwa sana kutoshea vyumba zaidi ya vinne au zaidi kwa kila mpangaji hapo, lakini yeye Draxton alikuwa amechukua vyumba vitatu tu na choo na bafu. Akamkaribisha Blandina kwenda ndani, na mpenzi wake huyo akaanza kuongozana naye mpaka ndani ya geti la nyumba hiyo.

Kweli walikuta baadhi ya watu hapo, nao wakawasalimia vizuri na kuwapita kuelekea mpaka upande wenye vyumba vyake Draxton. Wanawake watu wazima waliokuwepo hapo walimwangalia mno Blandina, tena kwa njia za husuda, na mwanamke huyu alilitambua hilo wazi lakini ndiyo kwanza hakuwa na muda nao. Wawili hawa wakaufikia mlango wa chumba cha Draxton, na jamaa akaufungua na kumwambia mrembo apite ndani. Blandina alipenda sana jinsi ambavyo ndani kwa mwanaume huyo kulipangiliwa vyema sana. Kuanzia zulia kubwa chini, vitu vya samani, TV ndogo ya bapa (flat screen) ukutani, masofa matatu yenye rangi nyekundu, yaani palikuwa pasafi sana.

Blandina akawa anapaangalia huku akitabasamu, kisha akamgeukia Draxton na kuuliza, "Unaishi na nani humu?"

"Peke yangu tu," Draxton akasema.

"Mmmm..." Blandina akaguna hivyo huku akimwangalia kwa njia iliyoonyesha hamwamini.

"Ahahahah... nini sasa?"

"Sidhani. Hao wamama walivyokuwa wananiangalia hapo nje, yaani kama siyo mmoja wao basi wote umeshawanyandulia humu ndani," Blandina akasema.

Draxton akaipitisha mikono yake kiunoni mwa mrembo na kuusogeza mwili wake karibu naye huku akitabasamu na kusema, "Mbona una wivu sana?"

"Mm... yaani me niwaonee wivu hao? Nitakuwa nimekosa kazi ya kufanya labd...."

Kabla Blandina hajamaliza maneno yake, Draxton akaifata midomo yake na kuanza kumtandika denda ya taratibu sana, naye Blandina akazungusha mikono yake nyuma ya shingo ya jamaa akijibu busu hiyo kwa upendo. Kisha Draxton akaikatisha na kumwangalia usoni.

"Nimekuchagua wewe tu. Usiwaze kabisa kuhusu mambo ya nje," Draxton akamwambia kwa ukaribu.

"Unanipenda Draxton?" Blandina akauliza kwa njia ya deko.

Draxton akatikisa kichwa kukubali.

"Basi kwa nini ulinitesa?"

"Kumaanisha?"

"Siku ile... ulipoondoka tu ghafla... nilipata shida sana... ulinlacha pabaya..."

Draxton akainamisha uso wake.

"Draxton... niambie tu shida ilikuwa nini. Sitakusumbua tena juu ya hili. Ni nini kilikupata?" Blandina akauliza kwa hisia.

Draxton akamwachia na kukishika kiganja chake, kisha akaanza kumvuta kuelekea ndani ya chumba ambacho alitumia kulala. Palikuwa pazuri sana pia, nao wakafika na kukaa kwenye kitanda chake kikubwa chenye godoro laini; lililofunikwa kwa shuka jeupe na safi sana. Blandina alikuwa anamwangalia sana kwa subira, akiwa anataka kusikia angesema nini.

"Nahitaji kukuomba samahani Blandina... kweli nilivyofanya siku ile haikuwa vizuri. Kuna... hali fulani ambayo huwa inanipata... unaweza kuchukulia ni kama jinsi allergy yangu kwa mboga za majani inavyofanya nihisi kuumwa... ni hivyo hivyo pia inapokuja kwenye suala la sex...." Draxton akamwambia.

Blandina akawa ameshindwa kuelewa. "Unamaanisha... kila mara ukitaka... au mwanamke anapotaka kufanya sex nawe, unaanza kuumwa?"

"Ni kama hivyo."

"Kwa nini? Una allergy na sex?"

Draxton akabaki kimya na kuangalia tu chini.

"Nielezee Draxton. Hiyo hali yako inakuzuia kuwa na mwanamke kwa nini? Ni nini kinakusumbua? Umeshawahi kwenda kwa daktari...."

"Blandina..."

"...ukajaribu kuona tatizo ni nini? Labda kuna tiba, Draxton... unamaanisha hauwezi ku-share nami mapenzi?" Blandina akauliza kwa hisia.

"Najua vitu hivyo havieleweki vizuri lakini... ndiyo hali halisi. Nikijaribu kukupa penzi... sitafanikiwa. Nimekuja nawe hapa kukuweka wazi juu ya hilo kwa kuwa Blandina... nimevutiwa nawe pia. Nina... nina hisia za kimapenzi kwako. Ila nahitaji kujua kama utakuwa tayari kuendelea kuwa nami nikiwa namna hii... kwa sababu nilijaribu kukukwepa ila nikashindwa kwa kuwa umeniingia sana. And this is ridiculous yaani... najua kabisa haitapatana na akili wewe kuwa nami kama hatutaweza...."

Blandina akamkatisha kwa kumkumbatia kwa upendo, naye Draxton akafumba macho taratibu.

"Hakuna kinachoshindikana Draxton. Nilikwambia mimi ni wako, na sitaruhusu chochote kinichukue kutoka kwako. Unaamini hilo?" Blandina akaongea akiwa bado amemkumbatia.

Draxton akabaki tu kimya.

Blandina akamwachia na kumwangalia usoni. "Unaamini kwamba nakupenda Draxton?" akamuuliza.

"Naamini. Sema... naogopa Blandina..." Draxton akasema.

"Ahah... unaogopa nini mpenzi wangu?" Blandina akauliza huku anaushika uso wake.

Draxton akatulia kidogo na kisha kusema, "Naogopa kukupoteza Blandina."

Blandina akaachia tabasamu la hisia, kisha akasema, "Hautanipoteza. Usijali. Sijakupenda tu kwa sababu ya jambo hilo, nimekupenda wewe kama ulivyo. Hilo tatizo lako... labda tutalipatia ufumbuzi baadaye... lakini nina imani mimi nawe tutafika mbali."

Draxton akabaki kumtazama kwa njia iliyoonyesha hisia nyingi sana kwake, naye Blandina akamsogelea mdomoni mwake na kuanza kumbusu kimahaba sana. Ingawa alitaka jambo hilo lielekee mbele zaidi, akajitoa mdomoni mwake na kuendelea kumshikilia usoni.

"Ninafahamu mtu mmoja ambaye hajawahi kupeana mapenzi na mume wake toka walipooana... na wanapendana vizuri tu. Sijui hiyo huwa inakaaje lakini... kwangu mimi haitakuwa na shida sana Draxton," Blandina akasema.

"Kweli? Hata tuseme miaka ikipita? Utaweza kuvumilia?"

"Mhmhmhm... tutapaswa kusubiri kuona mambo yatakavyokuwa. Ila ninajua upendo wangu kwako ni mkubwa kuliko hata sex..."

Kauli hiyo ikamfanya Draxton acheke kwa chini.

"Blandina... sitataka kukuumiza. Ikifika hatua ukaona kwamba hautaweza kuendelea nami wewe achana nami tu... najua kuna wanaume wengi watakaoweza kukupa vile mimi nimeshindwa...."

"Hivi Draxton kwa nini unapenda kuwa negative sana? Si nimetoka kukwambia kwamba hilo siyo tatizo? Usiongee hivyo tena, me sipendi. Kwani hao wanaume siwaoni? Mimi nimekuchagua wewe regardless... ungekuwa hauna mkono, au mguu, au jicho, jua nimekupenda wewe. Please..." Blandina akaongea kwa uhakika.

Draxton hakuwa na namna ila kumwacha mwanamke huyu aamue kwa namna ambavyo moyo wake ulimsukuma. Yeye pia alivutiwa naye, lakini hali yake isiyoeleweka ilimfanya ahisi labda angemwonea sana kama wangeendelea kuwa na uhusiano kwa njia hii, lakini kwa sababu mwanamke alionyesha kuwa na uhakika kwenye uamuzi wake, basi mwanaume akaona asimkwaze. Kwa hiyo wawili hawa wakaendelea kupata maongezi, na kuna mambo fulani ambayo Draxton alisema kujihusu yaliyomshangaza sana Blandina, lakini bado hisia zake kwake zilikuwa zenye nguvu mno na hivyo aliyachukulia mambo yote hayo kuwa kawaida. Mwanaume hata akapika kwa ajili yao wote, nao wakala na kulala pamoja usiku huo uliokuwa mzuri sana kwa Blandina kutokana na kuweza kulala ndani ya kumbatio la mwanaume wake.


β˜…β˜…β˜…


Usiku huo ulipita, na sasa ikiwa ni siku mpya ya Alhamisi, tayari vyombo vingi vya habari vilikuwa vimeshatangaza tukio lile la mauaji lililompata Agnes Mhina, na tayari mama na ndugu zake walikuwa wamezipata taarifa. Maaskari kama kawaida yao walitoa ahadi kwamba muuaji angepatikana tu, lakini bado ukweli kuhusu vifo vya namna hiyo kuwa vimetokea kwa muda mrefu ukafichwa, yaani haikuwekwa wazi kwamba tukio kama lililompata Agnes limekuwa likiendekea kwa muda mrefu sana. Maandalizi ya msiba wa Agnes yalianza upesi, kukiwa na watu wengi wa familia yake na marafiki waliokwenda kumfariji mama yake.

Namouih pia alikuwa amepanga kwenda msibani huko siku ya leo na kesho ili kutoa pole yake. Usiku uliotangulia baada ya yeye kufika nyumbani, alieleza kile alichoona kwa Efraim Donald kuhusiana na Draxton, akimwambia alimwona mwanaume yule eneo la tukio kisha akaondoka upesi sana. Aliwaza kwamba huenda alikuwa pale kwa sababu fulani, lakini ni kwa nini awe hapo wakati alikuwa amemwambia Blandina kwamba ameenda nje ya jiji? Akasema alihisi jamaa alificha jambo fulani, naye angetakiwa kumwambia Felix kuhusu ishu hiyo. Mume wake akamwambia Namouih aache kuwaza mbali sana kwa sababu hiyo ingesababisha aanze kufikia mikataa asiyokuwa na uhakika nayo. Jambo hili lingetakiwa kuachwa mikononi mwa polisi, na kama alikuwa na mashaka basi amuulize Draxton mwenyewe kabla ya kuongea na askari.

Bado moyo wa Namouih haukujihisi wepesi kuelekea pigo za yule mwanaume. Akawasiliana na Blandina kumuuliza ikiwa mambo upande wake yalikwenda vizuri, na rafiki yake huyo akasema angalau leo ameamkia pazuri ingawa ilikuwa siku ya huzuni kwa wengine. Akamwambia kwamba alilala kwa Draxton na alifurahia sana kuwa naye. Kwa hiyo Namouih akaona aache kwanza kumwambia kuhusu ishu ya jana, kisha akasema wakikutana ofisini wataongea mambo mengine kabla ya wote kwenda kumpa pole mama yake Agnes kule msibani. Blandina akakubali, kisha baada ya hapo simu zikakatwa.

β˜…β˜…

Muda wa saa tatu asubuhi hii tayari marafiki hawa wakawa ndani ya ofisi yake Namouih. Blandina alikuwa amevaa nguo nyeupe kwa juu kama sweta lililombana mpaka kufikia shingoni na sketi nyeusi iliyoishia magotini, naye Namouih alivaa blauzi nyepesi ya njano na sketi nyeusi pia kufikia magotini, wakiwa na mionekano maridadi kwenye nyuso zao. Namouih alikuwa amemuuliza Blandina kwa nini alivaa nguo ya namna hiyo wakati jiji lao lilizungukwa na joto kali, naye Blandina akasema hakuhisi joto kabisa, na sasa maongezi yakageukia kwa mpenzi wake mpya.

"Kwa hiyo akakupeleka kwake... ni pazuri?" Namouih akawa anauliza.

"Pasafi! Acha! Mwanzoni nikafikiri labda kuna demu mwingine huwa anaenda kumtengenezea hapo..." Blandina akasema.

"Inawezekana."

"Aa wapi... anajielewa tu."

"Kwa hiyo zamu hii mambo yakaenda fresh kabisa tofauti na mara ya kwanza?"

"Mmm... yeah."

"Mmm yeah inamaanisha mka... arrr?" Namouih akauliza, akimaanisha kufanya mapenzi.

Blandina akatikisa kichwa kukanusha.

Namouih akakunja sura kwa njia ya maswali.

"Draxton anasema ana shida fulani inapokuja kwenye suala hilo. Ni kama vile ana allergy na sex," Blandina akasema.

"Excuse me?!" Namouih akashangaa.

"Yeah."

Namouih akaanza kucheka, naye Blandina akamtazama kwa njia ya kukerwa.

"Ahahahah... sorry. Sijaelewa yaani..." Namouih akasema.

"Asa' mbona umecheka kama hujaelewa?"

"Am sorry... okay? Si... sijategemea ungesema kitu kama hicho..."

"Ndiyo hivyo. Inachekesha sawa lakini ndiyo hali halisi. Draxton anapatwa na shida fulani kila akijaribu tendo... inakuwa kama anaumwa. Na anasema akipitiliza anaweza kuzidiwa," Blandina akamwambia.

"Kuzidiwa? Kwamba akifanya sex anaweza hata kufa au?"

"Sijajua."

"Kwa hiyo utafanyaje sasa? Utaendelea kuwa naye?"

"Well, nimemshauri tuje kwenda kwa daktari kujua ana shida gani lakini bado anachekecha kichwa chake. So in the meantime... na mimi nitakuwa kama wewe," Blandina akasema.

"Unamaanisha nini?"

"Na wewe si haupewi haki yako? Lakini mbona bado uko na Donald na anakupenda sana? Me mwenyewe... nampenda Draxton yaani... kwa asilimia zote. Kwa hiyo nitaendelea kuwa naye regardless ana hali gani... na hiyo haitakuwa na shida kubwa kwangu."

Namouih akainamisha uso wake na kusema, "Unajua kwamba baada ya muda utachoka?"

"Kama wewe?" Blandina akauliza.

Namouih akamwangalia usoni.

"Ahah... usijali. Ndiyo tumeanza tu... you never know," Blandina akasema.

"Sawa. Fuata tu moyo wako Blandina, ila tafadhali nakuomba uwe mwangalifu sana," Namouih akasema.

"Kuwa mwangalifu na Draxton? Usijali. Ninamjua. Ana... amepitia changamoto nyingi maishani. Anastahili kuwa na mtu wa kumpenda..."

"Kila mtu ana mtu wa kumpenda, na...."

"Siyo Draxton," Blandina akamkatisha.

"Nini?"

"Draxton hana mtu yeyote Namouih. Yuko mwenyewe tu. Hana ndugu wala dada, hata watu wa kiukoo. Wote wameshakufa."

"Wote?!" Namouih akauliza kwa mshangao.

"Yeah, aliniambia jana. Kwa hiyo... unaweza kuelewa ni mtu mpweke. Hana hata marafiki yaani..."

"Huyo ni mtu wa aina gani Blandina? Hana ndugu, hana marafiki, ina maana anaishije?"

"Kama unavyomwona."

"Hata hajaajiriwa, sehemu yoyote ile, anategemea tu pesa za mtu mmoja mmoja, si ndiyo? Lakini ana gari, analipia vyumba, halafu hana wazazi wala ndugu, mara sijui hawezi ku-sex...."

"Unataka kusema nini Nam?" Blandina akamkatisha.

"Blandina, najua umempenda sawa, lakini unahitaji kuwa mwangalifu. Haya... jana alikwambia alikoenda?" Namouih akauliza.

"Ndiyo alisema. Alienda kuonana na yule jury wa siku ile mahakamani maana alihitaji msaada wake kumkutanisha na kiongozi wa masuala ya jurisprudence nje ya mkoa, walikuwa na mambo yao maana wanafahamiana... ndiyo akarudi na kunipitia," Blandina akasema.

"Alikwambia chochote kuhusiana na Agnes?"

"Ndiyo, aliniambia. Alikuwa anajua Agnes aliuawa. Namouih mbona umeanza tena kuwa judgmental namna hii?" Blandina akauliza kwa kufadhaika.

Namouih akafumba macho yake kwa kujihisi vibaya baada ya kutambua alipitiliza mno, naye akasema, "Samahani Blandina. Ninawaza tu kuhusu usalama wako. Ninakupenda sana rafiki yangu."

"Usijali Nam. Me nitakuwa sawa. Namwamini Draxton. Nakuomba tu na wewe uniamini mimi," Blandina akimwambia.

Namouih akavishika viganja vya rafiki yake na kuomba samahani kwa mara nyingine tena, naye Blandina akasema ilikuwa sawa. Baada ya hapo, wawili hawa wakaanza kupitia masuala ya kazi mpaka inafika saa saba hivi mchana, kisha ndiyo wakaondoka kwa pamoja kwenda kule msibani hatimaye.

β˜…β˜…

Baada ya Namouih na Blandina kwenda msibani, walitumia muda wa kama masaa matatu huko mpaka inafika saa kumi na moja ndiyo wakaamua kuondoka. Walikuwa wameonana na mama yake Agnes na kumpa pole kwa rambirambi kubwa, nao wakamwahidi kurudi tena kesho kwa ajili ya mazishi. Blandina alikuwa amewasiliana na Draxton mapema akimtaka aje nao pia lakini kwa sababu fulani mwanaume huyo alishindwa kuja. Alisema tu kwamba angekuja kesho, naye Blandina akaridhia hilo.

Ingawa hakusema lolote tena, Namouih bado alikuwa na mashaka kumwelekea Draxton, na kama tu mume wake alivyokuwa amemshauri, akawa ameamua kwamba angeongea naye yeye mwenyewe kuhusiana na uwepo wake jana kwenye tukio la mauaji ya Agnes. Ikiwa kile ambacho rafiki yake alikiona kwa Draxton kilikuwa kizuri kweli, basi naye angehitaji kuondoa mashaka yoyote kumwelekea ili mambo yawe shwari, na njia pekee ya kufanikisha hilo ni kuongea naye ili aache kumhukumu vibaya kama hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo.

Katika maongezi yao wakati wanapata chakula, Namouih akawa ameulizia kule ambako Draxton aliishi, naye Blandina akamwelekeza bila ya kutambua kwamba rafiki yake alikuwa na lengo la kwenda huko. Walikuwa wanakula kwenye mgahawa mmoja maeneo ya huko huko kwa kina mama yake Agnes, na baada ya kumaliza, Blandina akasema alihitaji kwenda kumtumia pesa mama yake mzazi kwanza, kisha ndiyo wangeondoka kurudi upande wao wa jiji. Lakini Namouih akamwambia atangulie tu kwa sababu yeye alipanga kwenda sehemu nyingine kwanza, hivyo aidha wangekutana baadaye au wangewasiliana tu maana hakukuwa na mpango wa kurudi ofisini tena, na Blandina alitaka kwenda nyumbani.

Hivyo, Blandina akamwacha Namouih hapo na kutangulia kuondoka, kwa kuwa wote walikuja na magari yao. Ni baada tu ya Blandina kuwa ameondoka ndiyo Namouih akanyanyuka pia na kwenda kwenye gari lake. Sehemu aliyokuwa amepanga kwenda ni moja tu; kwa Draxton. Hakuwa na uhakika kama anngemkuta, lakini kutokana na maelezo ya rafiki yake alielewa kwamba nyumba ile ilikuwa na watu wengine kama wapangaji kwa hiyo angejaribu hata kuwauliza kuhusu jinsi walivyomwona mwanaume huyo kimtazamo endapo kama asingemkuta. Yaani na yeye leo angekuwa kama mpelelezi kwa njia yake mwenyewe.

β˜…β˜…

Mwanamke huyu aliendesha gari lake mpaka maeneo sahihi kabisa kama alivyoelekezwa na Blandina, naye akawa amefika karibu kabisa na nyumba ambayo Draxton alikuwa anaishi. Ilikuwa rahisi kwake kupatambua baada ya kuliona gari la mwanaume huyo nje ya geti la nyumba, na hilo likamwambia kwamba kijana yule alikuwepo. Kwa hiyo angehitaji kwenda huko kuonana naye moja kwa moja. Akaliegesha gari lake nyuma ya gari la Draxton, naye akashuka na kulifunga. Kisha akaelekea mpaka getini na kuligonga kistaarabu, naye akasimama kwa utulivu.

Eneo hilo lilikuwa na nyumba kadhaa zilizoachana, na maduka machache ya bidhaa. Baadhi ya watu waliokuwepo walimtazama Namouih sana, hasa wakina mama, na ni jambo ambalo mwanamke huyu alikuwa ameshazoea hivyo akawapuuzia tu. Hazikupita sekunde nyingi na geti hilo likafunguliwa, akiwa amefungua mvulana mdogo, naye akamwamkia Namouih na mwanamke huyu kumwitikia vizuri. Akamuuliza kuhusu Draxton, lakini mvulana huyu alionekana kutolitambua hilo jina, hivyo Namouih akamnyooshea kidole gari la Draxton na kumuuliza kama mwenye nalo alikuwa ndani.

Baada ya mvulana huyo kukubali, Namouih akamwambia amwelekeze mlango wa chumba cha Draxton, naye akaingia ndani ya geti hilo akiongozwa na huyo mtoto. Sehemu ya ndani hapo kulikuwa na wanawake wawili watu wazima waliomzidi Namouih umri kiasi pamoja na msichana mwingine rika kama la Agnes tu, naye akawasalimu na wenyewe kuitikia. Mvulana yule akaendelea kumwongoza mpaka kufikia kona iliyoelekea upande mwingine wa nyumba hiyo, uliokuwa na njia fupi kama korido, naye akamwambia ni vyumba vya huko mwishoni ndiyo huyo "mkaka" aliishi.

Namouih akamshukuru, kisha akaanza kwenda taratibu mpaka alipofikia mwisho wa kona ile na kufika sehemu iliyokuwa na uwazi zaidi. Palikuwa na stendi zenye kamba za kuanikia nguo, zikiwa na nguo chache, naye akasimama hapo hapo alipokuwa baada ya kumwona Draxton sehemu hiyo. Alikuwa amesimama kwa njia ya kuinama, chini kukiwa na ndoo yenye nguo alizokuwa anafua. Yaani alikuwa anaonekana kwa upande wa utosi wake wa kichwa; ikiwa angesimama wima basi angetazamana na Namouih moja kwa moja, na hakuwa amevaa kitu chochote kwa juu, bali pensi nyepesi na viatu vyeupe vya kushindia.

Kwa sekunde hizo chache ambazo Namouih alibaki kumwangalia, Draxton alikuwa anaendelea tu kufua, kisha mara ghafla akaacha na kutulia. Namouih akaendelea kumwangalia kwa umakini, na jamaa akasimama wima sasa na kumtazama mwanamke huyu usoni sawia. Hapa ndiyo Namouih alipata kukiona kifua cha mwanaume huyo kwa mara ya kwanza kabisa, na kiukweli hangebisha, kilikuwa kifua cha mwanaume halisi. Draxton alikuwa na kifua kilichotuna na kujikata vyema, na tumbo lake, tumbo lake lilikuwa limetunisha mifuko yake sita ya nguvu (six packs) kwa uimara wa hali ya juu mpaka kufanya hadi ile miwili ya chini zaidi kuonekana (kitu ambacho kingefanya ziitwe eight packs); na zilichoreka vizuri mno mpaka Namouih akashindwa kujizuia kumtazama hapo.

Lakini alipomtazama mwanaume huyo usoni, akakuta akiwa anamwangalia kwa njia ya kawaida kabisa, yaani hakushangaa kumwona hapo hata kidogo ingawa hakujua amefikaje, na wala hakuonyesha nia ya kutaka kumkaribisha. Hivyo Namouih akapiga hatua chache mbele na kusimama huku anamwangalia kwa njia iliyoonyesha kujiamini.

"Habari Draxton?" Namouih akamsalimu

Draxton akabaki kimya na kuendelea kumwangalia tu.

"Hautaki salamu yangu? Nimekushtua sana kufika hapa?" Namouih akauliza.

"Habari ni nzuri, Namouih," Draxton akamwambia.

Namouih akatabasamu na kuangalia pembeni huku anatikisa kichwa chake.

"Karibu. Umetoka msibani, siyo?" Draxton akamuuliza.

"Ndiyo. Mbona wewe hukuja?" Namouih akauliza.

Draxton akaiangalia ndoo yenye nguo alizokuwa anafua, kisha akamwangalia tena Namouih.

"Aaaa... ulikuwa unafanya usafi... hongera," Namouih akasema.

Draxton akatulia kidogo, kisha akasema, "Samahani Namouih, huu siyo muda mzuri sana. Ikiwa una maongezi na mimi tunaweza kupanga wakati mwingine."

"Kwa nini huu usiwe muda mzuri? Kwa sababu uko kifua wazi? Umejikata kweli... uko vizuri," Namouih akamwambia.

Draxton akaangalia pembeni na kutabasamu kwa mbali sana.

"Mgeni ndiyo nimefika halafu unanifukuza jamani?" Namouih akasema.

"Sijakufukuza. Ninajua umekuja huku kufanya kama... uchunguzi," Draxton akamwambia

"Unajuaje hilo? Uchunguzi wa nini sasa... je kama nimepita kukusalimia tu?" Namouih akauliza.

"Mimi ni mwanasheria pia Namouih. Nakuelewa vizuri," Draxton akasema.

"Unaelewa nini? Mbona unajishtukia sana wakati me sijasema lolote...."

Namouih akaacha kuongea baada ya Draxton kuanza kupiga hatua kumwelekea mpaka akafika mbele yake kabisa. Mwanaume alikuwa anamwangalia kwa njia fulani yenye umakini, utadhani alimsogelea ili kumpiga, naye Namouih akaendelea kumtazama machoni kwa kujiamini.

"Unataka kusema nini Namouih?" Draxton akauliza kwa sauti tulivu.

Namouih akamshusha taratibu mpaka tumboni na kumpandisha mpaka machoni tena, kisha akasema, "Nilikuona jana. Jana usiku... nilikuona pale kwenye nyumba ambayo Agnes aliuawa."

"And with that... unafikiri nimefanya kitu fulani kinachohusiana na kifo chake?"

"Mbona unajiwahi hivyo?"

"Si ndiyo unachowaza?"

"Sijasema hivyo, hayo ni mawazo yako. Nataka kujua ulikuwa unafanya nini pale wakati ulimwambia Blandina umeenda wapi sijui na jury wako..."

Draxton akatabasamu kidogo.

"Nini kinakuchekesha?" Namouih akauliza kwa uthabiti.

"Hujanichekesha. Navutiwa tu na jinsi unavyopenda haki," Draxton akamwambia.

"Well, sijaja hapa kutoa burudani kwako. Nataka ukweli," Namouih akasema.

"Ukweli ni kuwa, nilikwenda na huyo jury wangu nje ya jiji kumsaidia na mambo fulani, kwa sababu aliniomba. Wakati narudi, Japheth akanipigia simu na kuniambia kwamba Agnes alimtafuta muda si mrefu kabla ya kifo chake, na alionekana kuwa kwenye shida fulani... ila hakujua ni shida gani maana mawasiliano yalikata. Ndiyo ikabidi nimwombe Japheth namba za Agnes... nilipojaribu kumtafuta sikumpata, kwa hiyo nikaamua kuifuatilia namba yake kwa kutumia app fulani ya simu yangu. Nilipofika eneo lile ndiyo nikakuta ameshauawa..." Draxton akaeleza.

Namouih akamtazama sana usoni, kisha akaanza kutikisa kichwa kwa kukataa yale aliyosikia.

"Ndiyo ukweli huo Namouih."

"Hapana, unadanganya. Yaani umeibuni hiyo story vizuri sana mpaka...."

"Kwa nini nibuni chochote?"

"...umejichanganya kwa kusema ooh sijui Japheth akanipigia, wakati namba yangu ndiyo iliyokuwa ya mwisho kufanya mawasiliano na simu ya Agnes! Unaongea nini?" Namouih akasema kwa mkazo.

"Namba yako ndiyo ya mwisho kumpigia yeye, siyo yeye kukupigia wewe. Aliyempigia simu Japheth alikuwa ni Agnes mwenyewe... inaonekana wewe ulikuja kumpigia baadaye..." Draxton akamwambia.

"Hapana... umeitunga hii story Draxton...."


"Chukua mambo yote niliyosema uende kuyafanyia utafiti wewe mwenyewe... ndiyo utajua kama nasema ukweli au la... lakini siyo kuja tu hapa na kuanza kunirushia madai yasiyo ya kweli. Tafadhali Namouih. Wewe kama mwanasheria unatakiwa kujua kwamba hupaswi kufikia conclusion bila kuwa na uthibitisho kamili... so please use some sense," Draxton akamwambia kwa ustaarabu lakini kwa uthabiti pia.

Namouih alikuwa amekuja kujua ukweli wa kile kilichompa mashaka kumwelekea mwanaume huyo kutokana na kifo cha Agnes, lakini kwa jinsi Draxton alivyojieleza ilimfanya aanze kuona kwamba huenda alimhukumu vibaya mno, tena kupita kiasi. Akaangalia tu chini akiwa anafikiria maneno ya mwanaume huyu, naye Draxton akaamua tu kurudi pale alipokuwa ameweka ndoo yenye nguo ili amalizie kuzifua, kwa kuwa jioni ya giza ilikuwa imeshaanza kuingia. Ni pale tu mwanaume huyu alipogeuka nyuma na kumpa mgongo Namouih ndiyo mwanamke akamtazama na kuona jambo lililomfanya atoe macho kwa mshangao.

Nyuma ya mgongo wa Draxton, usawa ule ule kabisa, Namouih aliweza kuyaona maneno yale ya mchoro wa tattoo aliyoyaona usiku ule ambao yeye na Blandina waligonga kiumbe fulani cha ajabu, ambacho kilikuwa na mwonekano kama wa mtu kabisa. "LIVING IN MY HEART YOU ARE, SO YOU AREN'T DEAD."



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Itakuwa ikiruka hapa siku za Jumamosi na Jumapili. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.

WhatsApp no: +255 787 604 893

e-mail: eltontonny72@gmail.com
 
CHANGE

Story by Elton Tonny

Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha

R-rated 18+


MUHTASARI MFUPI....

Baada ya Namouih na Blandina kwenda msibani kwa mama yake Agnes, walitumia muda wa kama masaa matatu huko mpaka inafika saa kumi na moja ndiyo wakaamua kuondoka. Ingawa hakusema lolote tena kwa Blandina, Namouih bado alikuwa na mashaka kumwelekea Draxton, na kama tu mume wake alivyokuwa amemshauri, akawa ameamua kwamba angeongea naye yeye mwenyewe kuhusiana na uwepo wake jana kwenye tukio la mauaji ya Agnes. Ikiwa kile ambacho rafiki yake alikiona kwa Draxton kilikuwa kizuri kweli, basi naye angehitaji kuondoa mashaka yoyote kumwelekea ili mambo yawe shwari, na njia pekee ya kufanikisha hilo ni kuongea naye ili aache kumhukumu vibaya kama hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo.

Katika maongezi yao wakati wanapata chakula, Namouih akawa ameulizia kule ambako Draxton aliishi, naye Blandina akamwelekeza bila ya kutambua kwamba rafiki yake alikuwa na lengo la kwenda huko. Mwanamke huyu aliendesha gari lake mpaka maeneo sahihi kabisa kama alivyoelekezwa na Blandina, naye akawa amefika pale Draxton alipokuwa anaishi. Alimkuta mwanaume huyo akiwa kifua wazi, akifanya usafi wa nguo, naye akamfata na kumuuliza kuhusu mashaka yake. Draxton alipinga madai ya Namouih, akigusia pia kwamba kama alihitaji kuthibitisha mambo basi afanye uchunguzi zaidi na siyo kufikia mikataa isiyokuwa sahihi.

Namouih alikuwa amekuja kujua ukweli wa kile kilichompa mashaka kumwelekea mwanaume huyo kutokana na kifo cha Agnes, lakini kwa jinsi Draxton alivyojieleza ilimfanya aanze kuona kwamba huenda alimhukumu vibaya mno, tena kupita kiasi. Akaangalia tu chini akiwa anafikiria maneno ya mwanaume huyu, naye Draxton akaamua tu kurudi pale alipokuwa ameweka ndoo yenye nguo ili amalizie kuzifua, kwa kuwa jioni ya giza ilikuwa imeshaanza kuingia. Ni pale tu mwanaume huyu alipogeuka nyuma na kumpa mgongo Namouih ndiyo mwanamke akamtazama na kuona jambo lililomfanya atoe macho kwa mshangao.

Nyuma ya mgongo wa Draxton, usawa ule ule kabisa, Namouih aliweza kuyaona maneno yale ya mchoro wa tattoo aliyoyaona usiku ule ambao yeye na Blandina waligonga kiumbe fulani cha ajabu, ambacho kilikuwa na mwonekano kama wa mtu kabisa. "LIVING IN MY HEART YOU ARE, SO YOU AREN'T DEAD."


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Namouih alianza kupumua kwa kasi kiasi, huku mapigo yake ya moyo yakiongeza midundo ndani ya kifua chake. Draxton yeye akaifikia ndoo yake na kuendelea kufua, asitake kumtazama tena Namouih ili aondoke tu yeye mwenyewe, lakini mwanamke huyu ndiyo akawa kama amegundishwa hapo hapo aliposimama baada ya kuona alichokiona. Akawa anamwangalia Draxton kimaswali mno, asielewe ni nini kilichokuwa kinaendelea. Alipotoka tu kufikiri kwamba labda alimhukumu vibaya, jambo hilo lingine likazuka.

Draxton alikuwa ametambua kwamba bado Namouih aliendelea kusimama hapo, hivyo akaamua tu asimame vizuri ili amwambie aondoke kwa ustaarabu. Lakini alipomwangalia usoni, akakuta Namouih anamtazama kwa njia fulani mpya, siyo udadisi tena, bali kama hofu. Akabaki tu kumtazama na yeye, hivyo Namouih akaangalia chini kidogo na kugeuka ili aanze kuondoka. Akafikia mwisho wa ukuta wa nyumba kutokea hapo na kugeuka tena kumwangalia Draxton, naye akakuta mwanaume huyo anamwangalia kwa yale macho yake makali fulani hivi, kama tu siku ya juzi walipokutana mahakamani kwa mara ya kwanza. Namouih akaacha kumwangalia na kuondoka hapo upesi sana, mpaka akalifikia gari lake na kukaa ndani; akitulia kwanza ili kurudia jambo lile vizuri kwenye akili yake.

Haingewezekana kufikiri labda macho yake yaliona mambo vibaya. Alichokiona kilikuwa sahihi kabisa kupatana na kile alichokiona usiku ule. Ile tattoo, jinsi maneno yale yalivyokuwa yamechorwa kwenye mwili wa yule "mtu" waliyemgonga, ndiyo namna hiyo hiyo yalivyokuwa yamechorwa mgongoni kwa Draxton. Lakini alikumbuka mambo ya usiku ule vizuri sana ambayo yalimchanganya. Yule mtu waliyemwona, alikuwa na ngozi nyeupe kama mzungu, lakini Draxton hakuwa mweupe namna hiyo, yaani hata chembe ya weupe aliokuwa nao Namouih, Draxton hakuwa ameifikia. Pia yule mtu alikuwa na nywele nyingi na nyeupe sana kichwani ilhali Draxton alikuwa na nywele fupi sana zilizonyolewa kwa ukawaida kichwa chake chote, na nyeusi.

Ikiwa hakuwa yule waliyemgonga siku ile, basi inawezekana walikuwa wawili, au walikuwa na kundi la watu wa namna hiyo. Alihofia sana kuhusu usalama wa Blandina hata zaidi wakati huu, lakini angemwambia kwa njia gani suala hili bila kumkwaza, hasa baada ya yeye kuwa amemwahidi kwamba angeacha kumhukumu vibaya Draxton? Alichokuwa amekosa tu ni ushahidi wa uhakika, lakini alijua isingekuwa ngumu kwa Blandina kumwamini endapo kama angeupata, kwa sababu rafiki yake huyo alikuwepo pia usiku ule. Namouih alichanganyikiwa sana. Akabaki hapo hapo kwenye gari lake kwa dakika zaidi ya 20 akiwaza vitu vingi, kisha hatimaye akaondoka tu ili kuelekea nyumbani.


β˜…β˜…β˜…


"Aaaaaah!"

Hiyo ilikuwa ni sauti ya juu sana ya kelele kutoka kwa Namouih. Alikuwa ameamka kutoka usingizini, naye akawa ameketi kitandani huku akipumua kwa presha sana. Mwili wake ukashtuka kiasi baada ya kuhisi mguso begani, naye akageuka na kukuta ni mume wake ndiye aliyemshika hivyo.

"Namouih... nini?"

Efraim Donald akauliza hivyo huku akionyesha uso wenye kujali sana. Namouih akaanza kuangalia mazingira waliyokuwepo. Ndiyo, walikuwa kwenye chumba chao. Ilikuwa asubuhi sasa. Siku hii ilikuwa mpya, jana ilipita. Akafumba macho na kuinamisha uso wake kwa mfadhaiko kiasi, naye Efraim akamshika mabega yake yote.

"Ni nini Namouih? Ndoto mbaya?* akamuuliza.

Namouih akatikisa kichwa kukubali.

"Umeota nini?" Efraim Donald akauliza.

"Hhh... ni ndoto mbaya sana, inatisha, sitaki hata kuizungumzia," Namouih akasema.

Efraim Donald akamwambia pole, kisha akachukua simu yake iliyokuwa pembeni.

"Saa ngapi?" Namouih akauliza.

"Saa moja," Efraim akasema.

"Nisamehe kwa kukuamsha," Namouih akamwambia.

"Usiwaze. Rudi tu kulala..."

"Sidhani kama nitaweza. We' ndiyo urudi kulala, me ngoja nkajimwagie tu..."

"Unaelekea ofisini baada ya hapo?"

"Hamna... nitatulia tu kwanza... nicheze na Angelo kidogo ndiyo... niende na msibani..."

"Ni lazima sana uende huko msibani? Si umeshawapa salamu za rambirambi jana?"

"Ndiyo, ila nitaenda tu kwa muda mfupi... nilikuwa namsimamia yule msichana unajua hilo..."

"Haya, sawa. Pole ya ndoto tena," Efraim Donald akamwambia huku akijilaza upande mwingine.

Namouih akamwangalia kwa kitambo kifupi, kisha akanyanyuka na kuelekea bafuni. Ndoto mbaya aliyokuwa ameona usingizini ilikuwa imemkosesha amani kabisa, na fikira ya kwanza kwake ikawa kwamba huenda jambo hilo lilihusiana moja kwa moja na mambo aliyotoka kuona jana. Kwa nini? Alikumbuka kabisa namna ambavyo aliota ndoto mbaya sana usiku ule alipomwona yule kiumbe mwenye tattoo aliyokuja kuiona tena jana kwa Draxton, halafu na leo akawa ameota ndoto mbaya. Hapo kulikuwa na uhusiano kabisa, naye akawa ameingia bafuni na kujimwagia maji huku akitafakari nini afanye ili kufichua kilichofichika juu ya Draxton.

β˜…β˜…

Muda mfupi baadaye, Namouih akawa ameondoka nyumbani na kuelekea ofisini kwake, akiwa na mwonekano nadhifu wa kiofisi uliompendezea sana. Alimkuta Blandina huko tayari, nao wakaanza kushughulika na mambo fulani ya kikazi. Namouih alikuwa amemuuliza Blandina kama jana alikutana tena na Draxton baada ya wawili hawa kuachana, akiwa anataka kujua kama mwanaume yule alimwambia kuhusu yeye kwenda pale alipoishi. Lakini Blandina akasema tu kwamba ndiyo, Draxton alikutana naye mida ya saa moja, nao wakaenda sehemu nzuri sana kupata chakula, kisha wakaenda na kwake kutulia kidogo kabla ya jamaa kuondoka kurudi kule alikoishi.

Kwa hiyo Blandina kutosema lolote kuhusiana na ishu hiyo kukamfanya Namouih atambue kuwa mwanaume yule hakumwambia lolote, hivyo naye akaona akae kimya tu. Rafiki yake huyo akasema kwamba baadaye wakienda msibani, yeye alikuwa anatoka pamoja na Draxton kuelekea huko kisha ndiyo mambo yao mengine yangefuata. Blandina alionekana kufurahia sana uhusiano wake na mwanaume huyo mpaka Namouih akashindwa kujua aanzie wapi kumwambia kuhusu mambo aliyofikiria. Akaona tu aache kwanza, naye akaamua kumtafuta yule kijana kwa jina la Japheth Warioba ili amuulize mambo machache kuhusiana na kile ambacho Draxton alimwambia jana.

Baada ya kuongea naye, kweli Japheth alimweleza kwamba Agnes alimtafuta muda fulani kabla ya kuja kusikia kuhusu taarifa ya kifo chake. Akamwambia kuwa mwanzoni hakutaka kumjibu baada ya binti huyo kutoka kudanganya kuhusu yeye kumbaka, lakini akapokea simu yake tu ili asikie alitaka kusema nini, na ndipo akaanza kumsikia akiongea kwa hofu sana na kuomba msaada wake. Namouih akamuuliza ni nini ambacho Agnes alikuwa anaombea msaada, lakini Japheth akasema hakujua kwa sababu simu ilikata ghafla, na ndiyo yeye akampigia mwanasheria Draxton ili kumwambia hayo kabla ya maafa yale kumkuta binti.

Namouih akamshukuru na kumwambia yeye pia ajitahidi kuwa mwangalifu, na kama kuna jambo lolote ambalo lingezuka basi amtaarifu endapo kama msaada wake ungehitajika, naye Japheth akakubali na kuagana naye. Ingawa hii ilikuwa nija moja ya kuthibitisha kwamba Draxton hakuhusika na kifo cha Agnes, bado haikuelezea uajabu wa hali alizokuwa nazo kabisa. Mambo kama ile tattoo, mara yeye kutoweza kufanya mapenzi, jinsi alivyokuwa akimtazama kwa macho fulani makali, na namna alivyoongea kwa upole ambao Namouih aliuona kuwa wa kinafiki ni vitu ambavyo viliisumbua sana akili yake.

Ni wakati alipokuwa akiendelea kuwaza na kuwazua ofisini kwake pale Blandina alipoingia tena na kusema ndiyo alitaka kuondoka kwa sababu Draxton alikuwa anamsubiri nje. Namouih alibaki kumtazama tu rafiki yake kama vile hajasikia kilichosemwa, naye Blandina akamshtua kidogo na kurudia maneno yake. Namouih alikuwa amemsikia, ila tu kuna wazo lililokuwa limemwingia wakati huo baada ya kujua Draxton yupo huko nje, naye akamkubalia Blandina na kumwambia kwamba wenyewe watangulie, naye angeenda muda si mrefu. Kwa hiyo Blandina akamuaga na kuondoka hapo.

β˜…β˜…

Hazikupita dakika nyingi, Namouih akachukua mkoba wake pia na kuondoka kutoka kwenye kampuni yao. Lengo lake lilikuwa Blandina na Draxton wakishaondoka tu, na yeye pia atoke, kwa sababu alitaka kwenda pale mwanaume huyo alipoishi. Kwa nini? Kama msemo mmoja wa waswahili unavyokwenda, ikiwa haujui mambo mengi kumhusu mtu, ongea na majirani zake, watakwambia. Mwanamke alikuwa ameamua kwenda huko ili aweze kupata chochote kile chenye nuksi ambacho bila shaka hata majirani wa mwanaume huyo pale alipoishi wangekuwa wamejionea.

Akafika na kugonga geti la nyumba hiyo, nalo likafunguliwa, zamu hii ikiwa ni mwanamke mwingine ambaye bila shaka aliishi hapo. Namouih akamsalimu na kujitambulisha, kisha akaomba kuingia ndani na kumwambia kwamba alihitaji kuzungumza pamoja naye na wakubwa wengine waliokuwepo. Mwanamke huyu akamkaribisha mpaka ndani ya chumba ambacho yeye na wengine walikaa, kisha akaja mwanamke mwingine pia pamoja na yule msichana wa rika kama la Agnes. Ni hawa tu ndiyo waliokuwepo kwa wakati huu, nao wakajitambulisha kwa majina ya Salhat, Rehema, na Kuluthum.

"Asanteni sana, mimi naitwa Namouih. Najua hamjatarajia ujio wangu hapa, na sitachukua muda wenu mwingi sana," Namouih akasema.

Wote wakamwambia haikuwa na shida, nao wakaweka umakini wao ili kumsikiliza.

"Sawa. Mimi ni mwanasheria, na ninafanya kazi sambamba na huyu kijana anayeishi hapa... Draxton. Hatujajuana kwa muda mrefu hivyo nilikuwa nahitaji kujua mambo machache tu kumhusu ili kufanya naye kazi vizuri zaidi. Sijui ameishi hapa kwa muda gani?" Namouih akauliza.

"Mh... yaani me ndo' leo nalisikia jina lake kwako. Huwa sijui hata anaitwa nani... ila ana muda sana hapa, sisi tumehamia tumemkuta..." Rehema akasema.

"Kumbe?" Namouih akauliza.

"Ndiyo. Huwa hata hatusemeshi, yuko kivyake mno yaani zaidi ya salamu hakuna kingine," akasema Rehema.

"Kumbe ni mwanasheria?" Kuluthum akauliza.

"Ndiyo..." Namouih akajibu.

"Hmm... yaani dada, me mpaka nikafikiriaga labda ana matatizo ya akili, ila kuona mpaka ana gari sisi tukajua lazima awe anafanya kazi nzuri, au labda tapeli," Salhat akasema na kufanya wenzake wacheke kidogo.

"Kwa hiyo hajihusishi na nyie hata kidogo? Hata kwenye maongezi na waume zenu, au labda mwenye nyumba..." Namouih akauliza.

"Mwenye nyumba anampendaga kweli, anasema huyu kijana ni mpole, mstaarabu, na amekaa hapa kwake kwa muda mrefu bila kuleta zengwe kabisa..." akasema Rehema.

"Haletagi hata marafiki hapa..." Kuluthum akaongea.

"Sijawahi hata kuona analeta demu au mshakji yeyote," akasema Rehema.

"Ila kuna kale kadada nimeona ameanza kukaleta hapa ile juzi..." Salhat akasema.

"Kakoje?" Rehema akauliza.

"Kapo tu hivi... Kuluthum si ulikaona?" Salhat akasema.

"Ee nilikaona. Kana shepu-shepu hivi na tako kubwa, alikaleta juzi juzi tu hapo... yaani ndiyo mara ya kwanza kumwona analeta mtu hapa..." akasema Kuluthum.

Namouih akawa amebaki kimya, akielewa kwamba waliyemzungumzia ni Blandina.

"Mambo ya sijui kuongea na waume zetu hanaga. Akiambiwa kuna jambo linahitajika, huwa anatenda tu upesi bila shida yoyote. Sema hana urafiki yaani. Huko kazini kwenu huwa ana marafiki hata?" Salhat akamuuliza Namouih.

"Hapana. Ni mtu fulani ambaye... amejichimbia sana kama anaficha kitu fulani hivi..." Namouih akasema.

Wanawake hao wakaanza kukubaliana na kauli hiyo, wakisema ni kweli kabisa.

"Eee... si mliniona ile juzi nipolikuja hapa?" Namouih akauliza.

"Ndiyo..." Salhat akajibu.

"Yeah, yaani nilikuja kumuuliza jambo fulani muhimu sana lakini akawa ananipa majibu kwa njia kama vile yeye mtakatifu hivi... halafu anavyoangalia machoni yaani mpaka unaogopa..." Namouih akasema na kuwafanya wacheke.

"Sasa huwa anafanyaje hizo kazi? Watu huwa wanamwelewa?" akauliza Kuluthum.

"Kikazi yuko vizuri sana, ila ndiyo kama hivyo yaani... haeleweki. Kwa hiyo ni kawaida yake kuja hapa kila siku, kazini, anatoka, kazini, anarudi, hivyo yaani?" Namouih akauliza.

Salhat akasema, "Kama hivyo dada, kabisa. Sema wakati mwingine huwa harudi kulala kwake. Anaweza kupitisha usiku mmoja au siku chache hajaja... inakuwa labda yuko safarini sijui...."

Wanawake hao wakaendelea kuzungumza mambo mengi, na Namouih akawa amepata mwanga kiasi kuhusiana na tabia za Draxton. Ikawa wazi kwake kuwa mwanaume yule aliishi maisha ya maigizo, yaani alijifanya mtu mwema, wa kivyake, na asiye na makuu ili kuficha maovu aliyokuwa anafanya. Alikuwa anaamini kabisa moyoni mwake kwamba mwanaume yule alikuwa mwovu, na kwa njia moja ama nyingine angemfunua mbele ya Blandina.

Baada ya kuwa amemaliza maongezi hayo na mashoga zake wapya, akawaaga na kuondoka hapo hatimaye. Safari yake ilikuwa kuelekea kule msibani ambako mwanaume huyo angekuwepo pia, naye akajiweka sawa kiakili zaidi ili aje kufanya jambo ambalo lingemlazimu tu Draxton afichuke kutoka kwenye kichaka cha maovu aliyokuwa akitenda.


β˜…β˜…β˜…β˜…


Ilipita wiki nzima kabisa baada ya matukio hayo yote bila ya Namouih kuwa amepata uthibitisho mzuri wa matendo ya Draxton yaliyofichika. Alijitahidi sana kwa kila nafasi aliyopata kuchunguza mienendo ya yule kaka, lakini ikawa kama kazi bure. Upande wa Felix wa upelelezi haukuwa umepata matokeo yoyote mazuri katika uchunguzi wa kifo cha Agnes, na ikawa kama vile suala hilo limeacha kukaziwa sana fikira ingawa lilikuwa jambo zito mno. Ni kutokana tu na matukio kuwa mengi sehemu mbalimbali za maisha ya watu, lakini la Agnes angalau lilizunguka sana mpaka kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa hiyo wakati huu Namouih alikuwa akiendelea na masuala ya kazi, lakini bado hakuwa amesahau kuhusu utata wa tattoo ile mgongoni kwa Draxton, ikiwa ndiyo moja kati ya manbo makuu yaliyomshawishi kuamini kuwa mwanaume yule si mtu mzuri. Na tokea siku ile alipoota ndoto mbaya sana baada ya kuiona tattoo ile, hakuwa amesumbuliwa na ndoto nyingine mbaya tena. Ikiwa ni siku ya ijumaa sasa, alikuwa ofisini kwake tu ametulia, naye akawa anajibu simu za "wateja" wao ambao walikuwa wanampigia simu kumjulisha mambo kadha wa kadha au kutoa shukrani kwake kwa msaada wake katika kesi zao. Ndipo Blandina akaingia ofisini hapo na kukaa kwenye sehemu iliyokuwa na sofa, akimwangalia Namouih kwa njia fulani ya kuudhika-kudeka.

Namouih akatabasamu na kumalizia maongezi yake kwenye simu, kisha akanyanyuka kutoka kwenye kiti chake na kwenda kukaa na rafiki yake. "Vipi na wewe, mbona umeweka sura utadhani mtoto aliyenyimwa ubwabwa?" akamuuliza kiutani.

"Si napendezea lakini?" Blandina akauliza kiutani.

"Yeah, ni mashavu yako tu ndiyo yanakuwa yanaonekana kama umeyajazia vyura," Namouih akasema.

Blandina akacheka kidogo, kisha akashusha pumzi na kusema, "Vitu vingi."

"Nini, wimbo wa Young Lunya au?"

"Ahahahaa... acha zako bwana..."

"Kama sikosei shida iliyopo inaanziwa na herufi D..."

Blandina akamwangalia na kutikisa kichwa kukubali.

"Mhmhm... nini kimetokea sa'hivi?"

"Siyo jambo kubwa wala...."

"We' niambie tu. Sita-judge," Namouih akasema kwa ustaarabu.

"Okay. Mambo yamekuwa yanaenda fresh sana, Drax ananitendea vizuri mno, every time tukiwa pamoja... ni raha," akasema Blandina.

"Naona hadi sa'hivi ameshakuwa 'Drax,'" Namouih akasema kiutani.

"Ahah... yeah. Ila hiyo jana tena, mambo yamevurugika kidogo..."

Namouih akamshika kiganjani na kuuliza, "What happened?"

"Mara kwa mara nilikuwa namkumbusha kwenda kumwona daktari kuhusu lile suala, lakini kila mara ambayo nililigusia angekwepa au kusema tungetafuta wakati mwingine. Sasa jana usiku nilikuwa kwake, na tulikuwa tumepanga nilale pale. Katika michezo yetu na utani na nini, hamu ikawa imenizidia, nikaanza kumbusu... na kumshika. Mwanzoni alijaribu kunikumbusha kwamba hangeweza kuendelea na jambo hilo, lakini nikaona nijaribu kulazimisha, kistaarabu tu... ila Draxton akaanza tena kuchemka na kunisukuma kwa nguvu..." Blandina akaeleza.

"Wewe! Haukuumia?" Namouih akauliza kwa mshangao kiasi.

"Hapana tulikuwa kitandani... alinisukumia tu pembeni. Nilishtuka sana yaani," Blandina akasema.

"Nini kikaendelea?"

"Akaanza kuniomba samahani akidhani nimeumia sana... na bado alikuwa anaonekana kuumwa. Ikanibidi nimwambie kwa ukali kabisa ni lazima twende kuonana na daktari kwa sababu hiyo haikuonekana kuwa shida ndogo... lakini ndiyo akasema hangeweza kwenda. Nilipomuuliza kwa nini, hakunijibu, ila akasema tu kuwa jambo hilo halikuwa ndani ya uwezo wake... na eti kama Blandina nahisi kutoweza kuendelea naye, basi tungepaswa tu kukomesha mapenzi yetu...."

"Ah-ah!" Namouih akashangaa.

"Yaani Nam, sijui nakosea wapi. Atakuwa anatafuta kigezo tu cha kutaka tuachane... yaani... ah..." Blandina akaongea kwa mfadhaiko.

Namouih akatikisa kichwa kwa kumwonea huruma rafiki yake. Hilo lilikuwa jambo zito, kwa sababu alielewa namna ambavyo Blandina alimpenda yule kijana. Hakutaka kumwona rafiki yake akiendelea kuugua moyoni namna hii juu ya mtu aliyeonekana kutojali hisia zake kwa asilimia zote, na ingawa ilikuwa inaonekana ni kama upuuzi wa Blandina kuendelea kulazimisha mapenzi kwa jamaa, bado Namouih alimwona Draxton kuwa ndiyo mbaya.

Akamuuliza hivi, "Blandina... baada ya kitendo hicho... wewe unataka kuachana na huyo mwanaume?"

Blandina akatikisa kichwa kukanusha na kusema, "Bado nampenda mno kuwaza masuala ya kuachana Namouih. Hajanifanya chochote lakini nampenda sana, hajui tu. Ni kwamba... nakuwa nataka kumwelewa, lakini yeye... ni kama ananisukuma mbali inapokuja kwenye suala hilo, ila bado hisia zangu kwake zina nguvu nyingi sana..."

"Kwa hiyo una mpango gani?" Namouih akauliza kwa upole.

"Nimeamua kumwacha tu mpaka akinitafuta yeye mwenyewe. Leo niliamkia kwake nikakuta ameshaondoka, na hatujatumiana hata jumbe za salamu...." Blandina akasema.

"Oh, kwa hiyo ulilala kwake, ukaamka asubuhi ukakuta hayupo, halafu hajasema lolote mpaka sasa hivi?" Namouih akauliza.

"Aina hiyo," Blandina akasema.

Namouih akatikisa kichwa kwa kusikitika, kisha akasema, "Pole Blandina."

"Mhm... asante. Hhaaa.... angalau nimelitoa jambo hilo kifuani, ndiyo maana nilikuja kuongea nawe, nashukuru kwa kunisikiliza," Blandina akamwambia.

Namouih akamwambia, "Usijali, unajua niko hapa kwa ajili yako. Ukihitaji msaada kwa lolote, we' niambie tu, sawa? Ninataka sana kukusaidia darling."

"Asante love. Asante," Blandina akasema na kukumbatiana naye kwa kuhisi faraja.

Basi, baada ya hapo Blandina akamwacha ili akashughulikie masuala mengine ya kazi, na Namouih akabaki kwenye sofa akimtafakari rafiki yake. Jitihada yoyote aliyoweka katika kumchunguza Draxton haikuwa imefanikiwa, na bado alikuwa anahofia kwamba huenda siku moja mwanaume yule angekuja kumuumiza vibaya sana rafiki yake, lakini ni kama Blandina alikuwa amepofushwa na upendo aliokuwa nao kumwelekea kuona hilo.

Kwa hiyo sasa akawa ameamua jambo moja tu; kuupata ukweli kutoka kwa Draxton kwa njia ya lazima. Yaani angemfata na kutumia njia fulani ambayo ingemlazimu mwanaume yule aseme kila kitu yeye mwenyewe. Alikuwa ameshahisi kuchoshwa sana na jinsi ambavyo kila mara jina la mwanaume yule lingetajwa ingempa hisia mbaya, na sasa alikuwa ameazimia kwenda kukomesha hilo. Akanyanyuka na kuzifunga kazi zake zote, kisha akabeba mkoba wake na kuondoka kwenye jengo hilo la ofisi yake.

β˜…β˜…

Namouih alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwake. Esma hakuwa ametarajia rejeo hilo la mapema kutoka kwa Namouih, naye akawa anamuuliza ikiwa alikuwa anaumwa. Namouih akakanusha na kusema hakuwa amerudi ili kukaa, alitaka kutoka tena, ila kuna kitu fulani alikuwa amepitia hapo nyumbani. Akaelekea mpaka chumbani kwake, naye akaenda kabatini na kuifungua. Akachuchumaa na kuingiza mkono wake chini kabisa, akiusukumia ndani zaidi upande wa nyuma ili kutoa kitu fulani alichokuwa anatafuta, naye akautoa baada ya kukipata, na sasa akawa ameishikilia bastola ndogo kwenye kiganja chake huku akiitazama kwa umakini.

Huu ndiyo uliokuwa mpango wake. Alitaka kuona mwanaume yule angetenda vipi pale ambapo angefatwa na kuulizwa kuhusu mambo yake ya siri, yaliyokuwa ya ajabu pia, na kama angeleta fujo, basi Namouih angehakikisha anamtandika hata risasi ya mguuni. Lakini siyo kwamba alikuwa anamfata bila kuhakikisha anatoka na kitu chenye kuthibitisha kuwa mwanaume yule alitenda mabaya. Alikuwa amenunua kifaa kidogo cha mfumo wa kurekodi sauti, ili kama ni maongezi au jambo lolote ambalo lingetokea akiwa pamoja naye basi kungekuwa na kitu kilichobaki cha kuthibitishia, na angekificha kifaa hiki kwa umakini sana. Akaondoka hatimaye baada ya kuificha bastola nyuma ya kiuno chake.

Bastola hii ilikuwa ya Efraim Donald, ambaye aliitumia kipindi cha nyuma sana kwenye masuala ya uwindaji, na sasa ilikuwa imekaa tu ndani hapo kwa muda mrefu bila matumizi. Namouih alikuwa amefundishwa kutumia bastola na mume wake kwenye zile shule za mafunzo ya shabaha, hivyo alielewa vizuri kile alichokuwa anakwenda kufanya. Akaingia kwenye gari lake na kuanza kuelekea kule ambako Draxton aliishi. Hakujali endapo kama angekwenda huko na kukuta hayupo; angemsubiri tu. Yaani alikuwa ameazimia kabisa kwamba leo ingekuwa leo, na angekomesha mchezo wa mwanaume yule uliokuwa unamwathiri vibaya rafiki yake ingawa mwanaume mwenyewe alionekana kutojali hilo. Kujiingiza kwake sana kwenye suala hili kulionyesha namna gani alimpenda Blandina, na angehakikisha anafanikiwa katika jambo hili ili amsaidie rafiki yake.

Baada ya mwendo wa dakika kadhaa, akawa anakaribia kuingia mitaa ya eneo aliloishi Draxton, lakini wakati akiwa barabarani bado akaona jambo fulani. Sehemu ya barabara iliyoingia upande huo kuelekea alikoishi jamaa, yaani barabara iliyoiacha lami kuu, aliweza kuliona gari aina ya Frester nyeusi likitokea huko, na kwa haraka akawa ametambua ni gari la Draxton. Ikambidi apunguze mwendo ili kuona lingeelekea wapi, nalo likaingia lami kuu na kuanza kuelekea upande mwingine wa barabara, yaani mbele ya Namouih. Mwanamke huyu akaanza kulifuatilia gari hilo taratibu, akihakikisha hajiweki sehemu za karibu ili mwanaume yule asije kutambua alikuwa na kupe kwenye mkia wake.

Kufatilia gari la Draxton kulimfikisha Namouih kwenye maeneo ambayo hayakuwa na makazi mengi ya watu, na gari la Draxton lilitumia njia mbalimbali zenye kuchanganya kiasi kulifikia eneo la huku lakini Namouih alitambua kwamba bado mwanaume huyo hakuwa amejua kama anafatiliwa. Akaendelea kulifuatilia gari hilo mpaka lilipofika eneo lenye miti mingi kama mapori vile, na gari la Draxton likaiacha barabara ya lami na kuingia barabara ya changarawe kuelekea upande wa mapori hayo. Namouih akaongeza kasi ili aliwahi, akiingia barabara hiyo pia na kuendelea kulifuatilia. Yaani alihisi kama siku hii ilikuwa ya bahati kwake kwa sababu mwanaume huyu alimleta sehemu ya mbali alikokuwa na jambo fulani la siri, na Namouih angeweza kujua ni nini hasa kilichofanya aje huku.

Akafika sehemu fulani ndani ya eneo hilo na kuona gari la Draxton likiwa limeegeshwa tu karibu na miti, na kwa sababu hakujua ikiwa tayari jamaa alishuka au la, akasimama kwa umbali aliokuwa na kuamua kusubiri kwanza. Sekunde tano kupita akaona mlango wa gari la Draxton ukifunguka, na mwanaume mwenyewe akitoka, kisha akaanza tu kutembea kuelekea upande wenye miti mingi zaidi. Namouih hangeweza kuona nyumba yoyote aehemu hiyo, na hivyo akawa anajiuliza ni nini ambacho kingempeleka mwanaume huyo sehemu hizo zilizojificha sana.

Hangekaa kukisia jibu la swali lake, lakini akiwa anakumbuka vyema kwamba jamaa alikuwa na tattoo kama ya yule kiumbe waliyemgonga usiku ule, akaikoki vizuri bastola yake na kulisogeza gari lake mpaka karibu kabisa na gari la Draxton. Akashuka. Akalisogelea na kuanza kuchungulia kwa ndani, kisha akajaribu kuufungua mlango upande wa usukani, nao ukafunguka. Akatazama kule Draxton alikoelekea lakini hakuweza kumwona, hivyo akajiingiza ndani hapo na kuanza kukagua vitu vilivyokuwepo ili kuona kama angepata jambo lolote lenye kuthibitisha masuala yenye utata kumhusu mwanaume huyo. Akaangalia makaratasi mengi yaliyotunzwa humo, akapekua upande wa nyuma wa gari, akanyanyua siti ili kuchunguza kwa chini, yaani chochote kile ili tu apate lolote, lakini hakupata jambo lenye kuridhisha haja zake.

Akajitoa hapo na kuangalia huku na kule kuona kama Draxton alikuwa anarudi lakini hakumwona. Wazo la kwamba ingefaa zaidi kama angemfatilia jamaa huko huko alikoenda alikuwa nalo, lakini isingekuwa rahisi kumpata sasa hivi maana alikoelekea hakukujulikana. Akawaza tu kuondoka hapo upesi kisha angetumia fursa nyingine kumfatilia jamaa moja kwa moja, au aje huku wakati mwingine ili atafiti eneo hili yeye mwenyewe. Akarudi usawa wa gari la Draxton na kuufunga mlango wake, na hapo akashtuka sana baada ya kumwona mwanaume huyo akiwa amesimama nyuma yake! Yaani kupitia kioo cheusi cha mlangoni aliweza kumwona kwa nyuma, na kwa haraka akageuka na kumtazama pia.



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.

WhatsApp no: +255 787 604 893

e-mail: eltontonny72@gmail.com
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…