Elton Tonny
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 396
- 2,976
- Thread starter
-
- #181
FOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Siku hiyo ikakucha, na sasa ikiwa ni asubuhi na mapema, Nora akaamka kutoka usingizini akijihisi uchovu mwingi wa kiakili. Alitulia tu kitandani hapo akiwaza mambo mengi sana kuhusu vitu ambavyo Lexi alimwambia kuhusu baba yake. Aliwaza pia kuhusu mambo ambayo yeye mwenyewe alikuwa amefanya, ikiwa alikuwa akipita kwenye njia sahihi au la, na kama upande ambao alichagua kujiweka ulikuwa ni upande mzuri au mbaya.
Hakujua mambo mengi sana, lakini kama ni jambo moja alilotaka kujua ilikuwa ni habari kumhusu Lexi. Akajinyanyua kutoka kitandani na kuivuta simu yake, kisha akatafuta namba ya Luteni Michael kumuuliza ikiwa Lexi alifikishwa kule alikopelekwa. Lakini akasita kwanza. Akafikiria jambo fulani, kisha akaona aache tu kufanya hivyo. Moyoni mwake alibeba hisia nzito za hatia kutokana na kitendo fulani alichokifanya, na ijapokuwa hakuwa na uhakika kama kilifanikiwa au la, hakutaka kuanza kujichoresha haraka sana kwa sababu ingemletea shida mapema. Na yeye alikuwa na siri pia.
Akaamua tu kuianza siku yake kwa kujisafisha na kupata kiamsha kinywa, kisha ndiyo angetoka na kuelekea kwenye ofisi yake. Akampigia mdogo wake simu kumsalimu huku akinywa chai, na kabla hajamaliza maongezi yao, mlango wa chumba chake ukagongwa. Akatoka kwenda kuangalia ni nani, na hapo mlangoni akamkuta Luteni Michael pamoja na Mario na Hussein. Hakushtuka. Akatoa tabasamu la kirafiki, huku wenyewe wakimwangalia kwa umakini sana.
"Karibuni," Nora akawakaribisha.
"Nora... tunahitaji kuzungumza," Luteni Michael akamwambia.
"Ndiyo, haina shida. Karibuni ndani," Nora akasema.
Mario na Hussein wakatazamana. Luteni Michael akaendelea tu kusimama hapo.
"Kuna tatizo lolote?" Nora akauliza.
"Yule mwanamke ametoroka," Mario akamwambia.
Nora akatazama chini kwa njia ya kawaida tu.
"Hujasikia kuhusu hilo?" Hussein akamuuliza pia.
Nora akatikisa kichwa kukanusha.
"Ametoroka vipi?" akauliza.
"Ameua wanajeshi wanne waliokuwa wanamlinda na kukimbia. Inashangaza sana kwamba ameweza kufanya jambo hilo kwa wepesi wa hali ya juu. Unafikiri aliwezaje kufanya hivyo?" Luteni Michael akauliza.
"Sijui Michael. Lexi... hamkutakiwa kumwekea watu wanne kumlinda. Ana... ana ustadi mkubwa kwenye mambo mengi," Nora akasema.
Wanajeshi wakaangaliana kwa njia yenye utata.
"Kwa hiyo... hawajamkamata bado?" Nora akauliza.
"Nora... sitaki kuku-accuse kwa lolote. Lakini ni muhimu sana ikiwa utasema ukweli. Ni wewe ndiyo ulimsaidia atoroke?" Luteni Michael akamuuliza.
"Mimi? What... ningemsaidia vipi..."
"Kapteni anafikiri ni wewe ndiye uliyefanya huyo mwanamke akaweza kuwatoroka wanajeshi wale. Anataka tukupeleke kwake ili... akuhoji," akasema Luteni Michael.
Nora akashusha pumzi, kisha akasema, "Haina tatizo. Nitaenda pamoja nanyi."
Luteni Michael alimtazama Nora kwa hisia sana.
Mwanamke huyo akarudi ndani na kuchukua vifaa vyake vichache, kisha akaongozana na wanaume hawa watatu mpaka kule alikokuwa Kapteni Erasto. Ilikuwa ni kwenye jengo lile lile, na baada ya kufikishwa kwenye ofisi yake, Nora akaketi na kutazamana na Kapteni Erasto. Mario na Hussein walimsubiria Luteni Michael nje, hivyo ofisini humo kukawa na watu watatu; Kapteni Erasto, Luteni Michael na ACP Nora.
"Nora... nafurahi kwamba umekuja bila kulazimishwa. Step ya kwanza inayoonyesha kwamba unajaribu kuthibitisha hauna hatia. Bila shaka umesikia kuhusu kilichotokea, siyo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Ndiyo. Nimesikia," Nora akajibu.
"Haijakushangaza hata kidogo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Kuna mambo mengi sana ambayo yule mwanamke amefanya huwa yananishangaza. Nimemzoea kwa njia hiyo tayari kwa hiyo... wakati huu sijashangaa sana kuhusu hilo," Nora akasema.
"Mambo kama yapi mengine ambayo amefanya yaliyokushangaza?"
"Ni mengi. Sikudhani angeweza kumkalisha chini Luteni, lakini aliweza," Nora akasema.
"Alibahatisha tu kwa sababu niliangukia kichwa," Luteni Michael akajitetea.
Kapteni Erasto akatabasamu.
"Unajaribu kuwa mcheshi wakati unajua tuko chini ya hali gani?" Kapteni Erasto akamuuliza Nora.
"Sielewi Kapteni unamaanisha nini..."
"Unajua ninachomaanisha. Unajua ulichokifanya. Umemsaidia kutoroka kwa sababu zako za kibinafsi, lakini kwa faida gani? Ili awaue wanaume wenye familia zao kwa ajili yako, au?"
"Mimi sijui unacho..."
"Kaa kimya!" Kapteni Erasto akafoka kwa hasira.
Nora akatulia tu. Luteni Michael akaangalia pembeni.
"Najua ni jinsi gani ulivyo na akili. Umeigeuzia hii kwangu kwa sababu mimi ndiyo nilikagua kile chakula na kuruhusu kipite, kwa hiyo hata kama ikichunguzwa huwezi kukutwa na shida, si ndiyo? Ulifanyaje vile? Ulificha vipi kitu kilichomsaidia atoroke mule?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Kapteni... bado sielewi, na sijui unachomaanisha. Sijafanya lolote unalosema," Nora akaendelea kukataa.
Kapteni Erasto akatoka upande wa kiti chake na kumfata Nora alipoketi.
"Najua una kiburi kwa sababu unajiona kuwa immune cause baba yako ni General. Kwamba... hautaguswa, mtoto wa mfalme. Lakini kwa kitendo ulichofanya, unafikiri tukimwambia baba yako atakuacha salama? Au hujui kwamba yeye ndiye aliyekuwa anamhitaji zaidi mwanamke huyo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
Luteni Michael akamtazama kimaswali. Nora akaendelea kukaa kwa utulivu tu.
"Huenda hiyo ndiyo sababu ukaona umsaidie mpenzi wako malaya mkubwa wewe! Kwa sababu unajua baba yako anataka kummaliza yeye mwenyewe. Unaweza ukajiona ni kama umeshinda, lakini huo ushindi hautafika mbali. Tutamkamata huyo mshenzi mwenzako na kumnyonyoa kila sehemu ya ngozi yake mbele ya macho yako. Na yote hiyo kwa ajili ya General... how do you like your father princess, huh?" Kapteni Erasto akasema kwa dharau.
Luteni Michael alikuwa anamtazama Kapteni Erasto kwa umakini sana. Mambo mengi aliyosema yalimshangaza mno.
"Umemaliza?" Nora akauliza kiutulivu.
"Hapana darling. Muziki ndiyo umeanza tu. Vifo vya ma-comrade wetu lazima vitalipwa, hata kwa damu zisizo na hatia. Na hiyo itakuwa ni juu yako," Kapteni Erasto akamwambia kwa ukaribu.
Nora akamwangalia kwa hisia kali, kisha akasimama na kutoka ndani ya ofisi hiyo.
"Kapteni... ni nini kinaendelea? Umeniagiza nimfate, nimlete, na sasa anaondoka... kihivyo tu?" Luteni Michael akauliza.
"Unafikiri nitamfanyaje? Nitamfunga? Unajua baba yake hataruhusu hilo... na ndiyo kinachompa kiburi hata kama akifanya nini," Kapteni Erasto akasema kwa kuudhika.
"Kwa hiyo kumbe Lexi alikuwa anapelekwa kwa General. Naweza kuuliza ni kwa nini? Nilifikiri anapelekwa kambi ya mateso ili aseme ukweli," Luteni Michael akauliza.
"Haina haja ya kujiingiza sana kwenye mambo ya General. Wewe na team yako pigeni utafiti wenu mmnase huyo mshenzi. Na... hakikisha macho yenu hamyaondoi kwa huyo mwanamke, Nora. Anajua mambo mengi kuliko anavyojionyesha," Kapteni Erasto akasema.
"Una uhakika ni yeye ndiye ambaye alimsaidia Lexi?"
"Damn! Ndiyo! Ni yeye ndiye amemsaidia Lexi. Aagh, silipendi hilo jina Luteni naomba usilitaje tena ukiwa mbele yangu! Nenda upige kazi mwanaume, acha maswali mengi," Kapteni Erasto akamwamuru.
Luteni Michael kweli bado alikuwa na maswali mengi sana kichwani kwake, lakini akatii na kuondoka hapo upesi sana. Alikuwa anataka kumwahi Nora ili aweze kuongea naye, na kwa tukio zuri akamkuta akiwa pamoja na Mario na Hussein, pamoja na mwanamke mwingine mwanajeshi aliyeitwa Samia wakiwa wanaongea. Akawafuata hapo walipokuwa wamesimama.
"Yaani hata hatulali dada, huyu Lexi atatukondesha sana mwaka huu," Mario akawa anamwambia Nora.
"Kwa hiyo... kweli aliwaua wanajeshi wale wote?" Nora akauliza.
"Ndiyo... ndiyo wanavyosema. Demu yuko vizuri eeh?" akasema Hussein.
"We mjinga kweli yaani watu wamekufa halafu unamsifia muuaji?" Samia akasema.
"Sijamsifia. Ila wewe kweli fikiria. Yaani wanajeshi sita... wenye silaha na mafunzo hao... wametorokwa na mwanamke aliyefungwa pingu. We ungeweza?" Hussein akamuuliza Samia.
"Ndiyo ninge...."
"Vijana, nahitaji kuongea na ACP," Luteni Michael akayakatisha maongezi yao.
Wanajeshi hao watatu wakaondoka hapo na kuwaacha wawili hawa.
"Nora... nini kinaendelea?" Luteni Michael akauliza.
"Nilifikiri Erasto amemaliza kukupigia mstari juu ya hilo," Nora akasema.
"No monkey business. Niambie ukweli. Umefanya kama vile anavyodai?"
"Unataka nikwambie nini Michael? Kile ambacho unataka kusikia siwezi kukisema, na kile ambacho hautaamini ndiyo nitakachokisema. Mimi ninaacha... mwamini mnachotaka kuamini. I don't care anymore," Nora akasema.
"Ni sababu gani inayomfanya baba yako amhitaji sana Lexi? Ni nini kimefichika?"
"Sijui Michael. Sijui. Lakini naweza tu kusema kwamba... lolote ambalo anafikiria juu yake si zuri... lakini niko mbali sana kiuwezo kuweza kufanya lolote..."
"Ungefanya nini Nora? Yule mwanamke ni... mwovu. Ni msaliti, ni mwongo, ni mtu mbaya sana ambaye amesababisha uharibiwe sifa yako. Unawezaje hata kuwaza kufanya lolote kwa ajili yake?"
Nora akatulia kidogo na kuangalia pembeni.
"Nora... ninajua una moyo mzuri. Lakini kuna watu wanatumia hilo kama udhaifu ili kukufanyia ubaya. Usijiruhusu... usijiruhusu uchezewe namna hiyo. Unastahili mambo mengi mazuri kwa kazi zako zote kwa ajili ya masilahi ya nchi hii... siyo hivi. Kashifa zote, kuvunjiwa heshima, kuhukumiwa... kwa ajili ya nini? Kwa nini? Eh? Kwa nini unapitia haya yote kwa ajili ya huyo mwanamke Nora?" Luteni Michael akauliza kwa hisia.
Nora akaangalia tu chini bila kutoa neno lolote. Luteni Michael akashusha pumzi kwa kufadhaika.
"Unajua haya yote hayataishia pazuri. Hawataacha kukusumbua. Wata... watafanya kila kitu..."
"Najua. Najua Michael," Nora akamkatisha.
"Kwa hiyo... uko radhi kupoteza kila kitu... kwa ajili yake?" Luteni Michael akauliza.
"Ningeweza kufikia hatua hiyo... lakini sasa... sijui. Mambo mengi yamebadilika. Nitakuwa tayari tu kwa lolote litakalokuja mbele yangu. Niko tayari," Nora akasema.
Luteni Michael akatikisa kichwa chake kwa huzuni.
"Okay. Kanali ameitwa na General hii asubuhi, nafikiri kuhusiana na hii ishu. Mambo upande wetu yanakwenda kwa kasi sana, Lexi atapatikana muda siyo mrefu. Natumaini utakuwa tayari kwa kitakachotokea baada ya hapo," Luteni Michael akamwambia.
Nora akamtazama machoni kwa hisia, kisha akatikisa kichwa chake kuonyesha amemwelewa. Akamwacha hapo na kuondoka zake akiwa na mambo mengi sana kichwani. Mario na Hussein walimchukua na kumrudisha mpaka hotelini kwake tena. Alikuwa anajihisi vibaya sana, na baada ya kuingia ndani ya chumba chake, akaanza kulia kwa uchungu mwingi. Alijihisi kuwa kwenye njia panda na hakukuwa na wa kumsaidia kujua pa kwenda.
Simu yake iliita sana, akipigiwa na watu wa kazini, lakini hakujisumbua kuigusa tena na kujilaza tu kitandani kwa muda mrefu akihisi hatia na
upweke mwingi.
★★★★
Upande wa Kanali Oswald Deule. Alikuwa amefika kwenye jumba la kifahari la Jenerali Jacob, ambapo aliitwa ili kukutana naye. Kwenye jumba hilo kubwa ndipo biashara na mikutano ya muhimu baina ya Jenerali na watu wake ilifanywa, na mara kwa mara wote walioshiriki kwenye mipango haramu ya Jenerali na Raisi walialikwa hapo ili kufanya mazungumzo au mambo yao ya kisiri, na Kanali Oswald alikuwa ni kati ya watu wachache waliokwenda hapo nyakati ambazo Jenerali angewaita.
Lakini wakati huu Kanali Oswald alijua dhumuni la kuitwa kwake halikuwa zuri, kwa sababu alichomwahidi Jenerali hakikuwa kimetimia. Alijua fika kuwa Jenerali Jacob alikuwa mwanaume makini asiyependa mchezo hata kidogo, hivyo kuwa kwake hapo angehitaji kujinyenyekeza sana ili mambo yasimharibikie. Alikaribishwa na mabaunsa walinzi wa jengo lile waliomwongoza mpaka sehemu ya ndani, kisha wakamwomba awape silaha yake yoyote aliyokuwa nayo kwa kuwa Jenerali hakupenda silaha ndani ya jengo lake. Lilikuwa jengo jeupe, safi na pana sana. Kulikuwa na wanawake wengi waliofanya kazi hapo, waliovalia chupi na sidiria kama wanamitindo, wakitumiwa pia kama watoaji wa burudani; kutia ndani na mapenzi.
Alipofika usawa wa ngazi zilizoelekea juu ya ghorofa la pili, Kanali Oswald akamwona Luteni Jenerali Weisiko pamoja na Jenerali Jacob mwenyewe, wakiwa wamesimama huku wakionekana kuongelea mambo fulani kwa umakini. Walikuwa wamezungukwa na wanawake watano ambao walikuwa nusu uchi kabisa, wakiwashika-shika mwilini na kuchezesha miili yao mbele yao kama kuwapa burudani. Bila hata kumwangalia, Jenerali Jacob akamtolea ishara Kanali Oswald kuwa apande mpaka hapo juu. Wasiwasi ulimjaa mwanaume huyu, lakini akasogea mpaka huko na kuwasalimu wakubwa wake hao.
"Za safari Oswald? Umeona mnyama gani anayekula nyama njiani?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aa... safari ilikuwa tulivu. General... najua kwamba nimekosea, na haikuwa kwa... nia mbaya... yaani... tulizungukwa na...."
"Nimekuuliza umeona mnyama gani wakati unakuja?" Jenerali Jacob akamkatisha.
Kanali Oswald akabaki kimya tu.
"Nilitakiwa kufurahia usingizi wangu ili nikiamka asubuhi niifurahie zawadi ambayo uliahidi kuniletea. Nimeufurahia usingizi, lakini mbona zawadi siioni?" akauliza Jenerali Jacob.
"General... kumradhi sana kwa kuwa..."
Jenerali Jacob akanyanyua vidole vyake juu kumkatisha. Weisiko akawaambia wanawake wale waondoke hapo, nao wakatii. Jenerali Jacob akamsogelea karibu Kanali Oswald, ambaye alikuwa anahisi kama anataka kufa vile kwa presha.
"Kwa nini ulinidanganya?" Jenerali Jacob akauliza.
"Siku... sikukudanganya General. Kuna mambo tu yalitokea bila..."
Kanali Oswald akashindwa kuendelea. Aliona jinsi wawili hao walivyomwangalia kwa njia fulani iliyoonyesha walikuwa na lengo fulani baya sana kumwelekea. Lakini mara ghafla Jenerali Jacob akaanza kucheka kwa njia iliyoonyesha hakuwa na ubaya wowote kumwelekea. Kanali Oswald akachanganywa na hili, lakini naye akajifanya kutabasamu.
"Hahahah.... usiniambie hapo ulipo mikojo tayari ilikuwa imeanza kukushuka! Ulikuwa unaogopa sana eeh?" Jacob akamuuliza.
"General..."
"Kanali... usihofu. Mimi tayari nilikuwa najua huyo msichana alitoroka wakati naongea nawe kwenye simu. Najua unafikiri labda nimekasirika sana na nitakufanya jambo fulani baya, lakini hiyo siyo sababu niliyokuitia hapa. Nimekuita hapa ili kukuonyesha jambo lingine. Uko tayari?" Jenerali Jacob akamwambia.
Kanali Oswald akatikisa kichwa kukubali.
Kisha Jenerali Jacob akatabasamu na kuanza kuondoka kuelekea chini ya ngazi zile. Kanali alipomwangalia Weisiko, aliona bado mwanaume huyo alikuwa anamtazama kwa njia isiyo ya kirafiki kabisa, hivyo akajua bado kulikuwa na nuksi. Hawa hawakuwa watu wa kusamehe na kusahau, lakini kama ni kuwaomba msamaha basi angepiga hata magoti ili aupate.
"Unafanya nini Oswald? Nifate," Jenerali Jacob akasema.
"Sawa mkuu," Kanali Oswald akajibu na kuanza kumfata haraka.
Walishuka ngazi pamoja mpaka sehemu ya chini na kuanza kuelekea upande mwingine ndani ya jengo hili. Kanali Oswald hakujua ni wapi au ni nini angeenda kuonyeshwa, hivyo akajikaza tu kiume na kujifariji kwamba mambo yote yangekuwa sawa. Wakafika kwenye mlango mmoja wa chumba ambacho kilikuwa kimejitenga, kisha Jenerali Jacob akaufungua na kuingia ndani. Kanali Oswald akamfuata, na baada ya kuingia aliweza kuona kilikuwa chumba chenye vifaa vingi vilivyotunzwa, kama stoo vile, nacho kilikuwa na giza kiasi.
Jenerali Jacob akasimama usawa wa pazia kubwa jeupe lililokuwa limetundikwa katikati ya chumba na kumgeukia Kanali Oswald.
"Unajua point ya mambo yote tunayofanya ni nini?" Jenerali Jacob akauliza.
"Ni kwa ajili ya taifa General," Kanali Oswald akajibu.
"Oh good. Kwa hiyo kama unajua hilo, inamaanisha unajua pia kwamba hatutakiwi kuruhusu makosa ya aina yoyote kwenye kazi..."
"General..."
"Sijasema kwamba mambo yote yaliyotokea ni makosa yako. Ila unabidi tu uelewe kwamba hawa... Mess Makers wamekuwa... mwiba mkali sana kwangu... na nilipoku-assign uwashughulikie niliamini kabisa kwamba wasingesikika tena..."
"General..."
"...na uliniahidi, uliniahidi... kwamba wasingesikika tena. Huwa sipendi ahadi fake Oswald unajua hilo. Na pia huwa sipendi kuchafua mikono yangu mwenyewe, ndiyo maana nikakuweka unitolee huo uchafu. Nataka tu kujua ni kwa nini umeshindwa kutimiza hiyo ahadi," Jenerali Jacob akasema kwa sauti tulivu.
"General... sijashindwa. Nakuhakikishia Jabari na huyo mwanamke nitawaleta kwako. Hivi tunavyozungumza wanafatiliwa sehemu zote za jiji hili, na hawawezi kufika mbali kwa sababu hawataweza kutoka nje ya mkoa huu. Na hata kama waki...."
"Kanali... haujaona mnyama yoyote anayekula nyama wakati unakuja huku?" Jenerali Jacob akamkatisha na kumuuliza hivyo kwa mara nyingine tena.
Kanali Oswald hakuweza kumwelewa kabisa, lakini alijua bila shaka swali lake lilikuwa na maana fulani. Ikiwa angetoa jibu lisilo sahihi, basi lazima kuna jambo lingetokea. Lakini hakujua ajibu nini, kwa hiyo akaona tu aseme ukweli.
"Hapana General. Sijaona mnyama yoyote anayekula nyama wakati nakuja," Kanali Oswald akajibu.
Jenerali Jacob akacheka sana, kisha akasema, "Basi... wacha nikuonyeshe jambo fulani."
Akalishika pazia lile na kulivuta lote, naye Kanali Oswald akatoa macho kwa mshangao mkubwa. Hapo aliweza kuona ndoo mbili chini, zikidondokewa na damu kutoka kwenye kiwiliwili cha mtu kilichotundikwa juu kama nyama za buchani. Yaani, hakikuwa na kichwa, wala mikono na miguu. Kuanzia shingoni mpaka usawa wa mapaja ndiyo mwili uliokuwepo, na sehemu zake za siri zilikuwa zimekatwa. Hakujua ulikuwa ni mwili wa nani, lakini ilionekana kuwa ni mwanaume kutokana na kutokuwa na matiti makubwa, na uimara wake tumboni.
Lilikuwa ni jambo moja la kikatili sana, naye Kanali Oswald akamtazama Jenerali akiwa anajikaza. Kuona jinsi ambavyo damu bado zilitiririka ilimaanisha jambo hilo lilikuwa limefanyika siku hiyo hiyo na muda mfupi tu uliopita.
"Hivi ndivyo nilivyopigia picha kuuona mwili wa Jabari na binti yake leo. Ingenipa furaha sana kama ningeweza kuikatakata miili yao namna hii... kwa mikono yangu mwenyewe," Jenerali Jacob akasema.
Kanali Oswald akabaki kimya tu.
"Unajua huyu ni nani? Oh, bila shaka huwezi kujua. Lakini kiukweli Oswald... sijaridhika. Nimejitahidi kutoa hasira yangu namna hii lakini... bado sijaridhika. Bado... nahitaji kuitoa hasira nayohisi kutoka kifuani kwangu. Utanisaidia vipi?" Jenerali Jacob akauliza huku anamwangalia Oswald kwa umakini.
"General... nakuahidi... nakuahidi kwa maisha yangu, nitakupa Jabari na Lexi. Nitawa..."
Kabla hajamaliza kuongea, wanaume wawili wenye miili mikubwa wakaingia ndani hapo pamoja na Luteni Jenerali Weisiko, na wanaume hao wakamshika kwa nguvu Kanali Oswald mikononi. Hofu kubwa ilimwingia mwanaume huyu kwa kuwa alitambua sasa kwamba huu ulikuwa ni mwisho wake.
"General, General... tafadhali nisamehe, nisamehe, nisamehe... General niamini... General nita... nitafanya lolote kwa ajili yako... nimefanya mengi sana ajili yako... General tafafhali usinitendee kwa... tafa... tafadhali General..."
Kanali Oswald akawa anamsihi sana Jenerali asimuumize. Alihisi kile ambacho ametoka kuonyeshwa ndiyo ambacho angefanyiwa. Wanaume wale wawili wakaendelea kumshikilia kwa nguvu na kumpigisha magoti chini, naye Weisiko akasimama pembeni yake Jacob akiwa ameshikilia panga lenye makali pande zote mbili.
"Bado naweza kuwa msaada mkubwa kwako General... tafadhali... niruhusu nirekebishe hili... ninakuhakikishia... General nitawaleta kwako please..."
"Acha kulia-lia kama bwege bwana. Tulia... na hii haitauma sana," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia huku akimsogelea na panga leke.
"Tafadhali General... kila kitu kilikuwa kinaenda vyema. Angefika kwako kama isingekuwa ya binti yako... General tafadhali usifanye hivi... nimekufanyia mambo mengi sana... siwezi kukuangusha..."
"Subiri," Jenerali Jacob akasema.
Luteni Jenerali Weisiko akatulia kidogo na kumwangalia usoni. Kanali Oswald alikuwa anapumua kwa hofu huku akitokwa na jasho.
"Unamaanisha nini isingekuwa ya binti yangu?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aam... ni ACP Nora ndiye aliyefanya mpaka Lexi akatoroka," Kanali Oswald akajibu kwa hofu.
"Kwa nini afanye kitu cha namna hiyo?" Jenerali Jacob akauliza.
"Binti yako alikuwa na urafiki naye... lakini inaonekana pia kwamba anampenda," Oswald akajibu.
"Nini?" Jenerali Jacob akashangaa.
"Unatutania eti?" Weisiko akamuuliza pia.
"Hapana mkuu, hapana. Ni kweli. Kabla ya kuanzisha safari ile... alituomba sana... Nora... alituomba tumruhusu amwone kwa mara ya mwisho... na mimi kwa sababu namheshimu binti yako nikamruhusu General kwa sababu alionyesha uhitaji. Ila akasaliti imani yetu kwake..."
Kabla hajamaliza kuongea, Weisiko akamshika kidevuni kwa nguvu na kumpiga usoni kwa kishikio cha panga lake. Damu zikaanza kumtoka puani Kanali Oswald, akihisi maumivu makali pia.
"General... niruhusu niukatekate ulimi wake sasa hivi huyu mpuuzi," Weisiko akasema huku anamwangalia Kanali Oswald kiukatili.
"Ngoja..."
Jenerali Jacob akasema hivyo na kusogea karibu zaidi na Kanali Oswald.
"Unajua nitakupa kifo kibaya zaidi ya kile unachofikiria nikijua unamsingizia mtoto wangu," Jenerali Jacob akasema kwa uzito.
"Hapana Jenerali... simsingizii. Lexi asingeweza kutoroka kabisa. Ninajua aliweka kitu fulani kwenye chakula alichoomba kumpatia kabla ya safari, na alikificha kwa akili sana... hatukuweza kutambua. General niamini... siwezi nikasema jambo hilo kuhusu mwanao kama... kama sina uhakika. Na najua sipaswi kumfanya lolote kwa sababu ni binti yako, ila ndiyo hivyo ameshatu-cost tayari na sasa inabidi tu tuendelee kuwatafuta wakina..."
"Kaa kimya," Luteni Jenerali Weisiko akamkatisha.
Kanali Oswald akatulia maana alikuwa anaongea haraka-haraka kama cherehani.
"Ulikuwa wapi kuniambia kuhusu hilo muda huo wote?" Jenerali Jacob akauliza.
"Hatukujua... samahani... Lexi alikuwa anamtumia binti yako ili kupata taarifa nyingi na kujua mambo yote kuhusu mipango yetu. Binti yako ni mtu mzuri, kwa hiyo yule mwanamke amemfanyia ulaghai mwingi sana. Hata hii ya kumsaidia atoroke ninajua atakuwa tu amemfanyia ulaghai..." Kanali Oswald akaongea kwa kujifanya anamtetea mtoto wa Jacob.
Jenerali Jacob akavuta pumzi ndefu na kuishusha, akitafakari mambo haya. Kanali Oswald akawa anauangalia kwa hofu mwili ule uliokatwa, kwa kupigia picha kwamba na yeye angefanywa namna hiyo.
"Hata ijapokuwa unachosema kinashangaza, bado ni makosa yako kwamba mpaka sasa haujaweza kuwaleta watu hao kwa General. Ukifikiri hicho kitakuwa ni kisingizio cha kukuacha salama, umekwama ndugu yangu," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia.
"Hapana mkubwa... mimi niko loyal kwenu, sikuzote. Sikumshuku binti yako mwanzoni kwa sababu aliaminika... imetokea tu kwamba akausaliti uaminifu huo... haikuwa lengo langu... haikuwa... tafadhali General... nionyeshe msamaha... niko tayari kufanya lolote kwa ajili yako... nitahakikisha..."
"Basi, basi, inatosha. Nyanyuka," Jenerali Jacob akamwambia.
Kanali Oswald akabaki tu kumwangalia.
"Huelewi Kiswahili? Amesema nyanyuka," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia kiukali.
Wanaume wale wawili walikuwa wamemwachia Kanali Oswald, hivyo akajinyanyua na kusimama huku bado akiwa mwenye wasiwasi mwingi.
"Sitaki makosa ya aina yoyote yajitokeze tena, unanielewa?" Jenerali Jacob akamwambia.
"Ndiyo... ndiyo General. Sitakuangusha," Kanali Oswald akasema.
"Acha kuogopa. Sikuwa na lengo la kukuua, najua uko loyal sana," Jenerali Jacob akamwambia huku amemshika bega.
Luteni Jenerali Weisiko akacheka kidogo, naye Kanali Oswald akatoa tabasamu la woga-woga.
"Ila, nataka uwe unanijulisha kila kitu kinachoendelea kuanzia sasa, na ninakupa wiki mbili tu washenzi wale uwe umewaleta kwangu, do you understand?" Jenerali Jacob akasema.
"Ondoa shaka General. Nakuahidi nitawaleta kwako mapema kabla ya muda huo," Kanali Oswald akatoa ahadi.
"Acha kujitapa kwa maneno hewa Kanali. Unatoa ahadi halafu hai..."
"Hapana Luteni Jenerali. Zamu hii hata Mungu hataweza kunizuia. Nitahakikisha siwakwazi na ninawaleta kwenu. Nitawaletea wale watu kwenu... kwako General..." Kanali Oswald akaapa.
Jenerali Jacob akatabasamu na kusema, "Vizuri."
Kanali Oswald akashusha pumzi ya utulivu. Alikuwa anahisi kama vile angejiharishia kabisa.
"General... vipi kuhusu hili suala la Nora?" Luteni Jenerali Weisiko akamuuliza.
"Nora... nitadili naye mimi mwenyewe. Kanali hakikisha hakuna mpuuzi yeyote anamgusa binti yangu, unanielewa?" Jenerali Jacob akasema.
"Ndiyo mkuu," Kanali Oswald akajibu.
"Sawa. Unahisi njaa?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aaa... ndiyo General... nahisi njaa kiasi," Kanali Oswald akajibu kiwoga-woga.
"Okay. Sahau haya yote, twende tukapate chakula..."
Jenerali Jacob akasema maneno hayo na kuwatolea ishara wanaume wale wawili kuwa walirudishie pazia lile pale juu, kisha akamshika Kanali Oswald begani kirafiki na kuanza kuondoka pamoja naye. Waliongozana mpaka kwenye meza ya chakula huku Jenerali akimwambia Kanali anapaswa kuacha kuogopa kwa kuwa hangemfanyia jambo baya.
Baada ya kuketi kwenye viti pamoja na Weisiko, Jenerali Jacob akaagiza vyakula kwa ajili yao viletwe, na kusema kwa wanawake wale kwamba wamletee chakula "special" Kanali Oswald. Yeye Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko walikuwa wameletewa vyakula vizuri vya aina mbalimbali, kisha Kanali akaletewa sinia pana lililofunikwa kwa juu na kuwekewa mbele yake. Akahisi bila shaka kulikuwa nuksi kwa ndani, naye akamtazama Jenerali kwa wasiwasi.
"Najua wewe uko loyal kwangu, lakini nataka kuona ikiwa utafanya KILA KITU nitakachokuamuru... kama ulivyotoka kusema muda ule," Jenerali Jacob akasema hivyo huku akitabasamu.
Kanali Oswald akameza mate akianza kuingiwa na hofu kwa kufikiri labda alikuwa anapewa nyoka ale. Kisha Jenerali Jacob akamwambia mwanamke aliyemletea sinia hilo alifunue, na baada ya kulifunua, Kanali Oswald akafumba macho na kugeukia pembeni.
"General... General nini hiki?" Kanali Oswald akauliza kwa kufadhaika sana.
"Ndiyo chakula special kwa ajili yako. Sikuwa na jinsi ila kukupa wewe maana ulisema hukuona mnyama yeyote anayekula nyama wakati unakuja. Nataka unithibitishie kwamba na wewe ni mnyama... hahahahah..." Jenerali Jacob akasema hivyo na kuanza kucheka pamoja na Luteni Jenerali Weisiko.
Kanali Oswald akakitazama tena "chakula" hicho. Kilikuwa ni kichwa kilichokatwa cha mwanaume, na mwanaume huyo alikuwa ndiye yule mwanajeshi ambaye aliendesha gari lile lililokuwa likimsafirisha Lexi usiku wa jana. Pembeni ya kichwa hicho kulikuwa na uume wake uliokatwa, na mipira ya uzazi ikiwa imekatwa na kusambaza damu kwenye sinia hilo. Vyote vikiwa vibichi!
"General..."
"Kula. Nataka ule chochote kati ya hivyo, then mambo mengine yatafuata," Jenerali Jacob akasema.
Kanali Oswald alihisi kuchoka. Alijua alipaswa kula la sivyo cha moto angekiona. Akajitoa akili na kujikaza kiume, kisha akachukua kisu kidogo pembeni na uma, naye akaanza kuikata sehemu ndogo ya sikio kwenye kichwa ili ale, lakini Jenerali Jacob akamzuia.
"Nimekwambia chagua kati ya hivyo ule, sijakwambia ukate. Ukichagua kichwa, ujue unakila chote," Jenerali Jacob akasema.
Aisee!
Wanawake waliokuwa pembeni walihisi vibaya sana kumwelekea Kanali Oswald. Walimwonea huruma. Kanali Oswald akabaki tu kuangalia vitu hivyo mbele yake. Alijiuliza hata walimleta mwanaume huyo huku saa ngapi. Akamtazama Weisiko kidogo, naye akamtolea ishara kwa macho yake kuwa achague na ale. Kanali Oswald akafumba macho na kukaza meno yake, kisha akaweka kisu na uma pembeni, halafu akauchukua uume ule na kuudumbukiza mdomoni!
"Usimeze... tafuna!" Jenerali Jacob akasema kiutulivu.
Kanali Oswald akawa ameweka tango hilo dogo mdomoni huku ametoa macho kimshangao. Akaanza kutafuna huku akijikaza asitapike. Kwachu, kwachu, kwachu, akaendelea kutafuna huku watu hapo ndani wakimwangalia kwa umakini. Wanawake kadhaa walikuwa wameziba macho na midomo wasiamini walichoona. Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko wakaendelea kumwangalia mpaka alipomaliza kutafuna na kumeza, kisha akawa anajitahidi asitapike hata kidogo.
Wawili hao wakaanza kumcheka sana.
"Hahahahaa... mnofu tu..." Jenerali Jacob akasema.
"Mnofu tu," Luteni Jenerali Weisiko akamalizia huku akicheka.
Jenerali Jacob akatoa ishara kwa kiganja chake, kisha chupa kubwa ya wine ikaletwa hapo na kuwekwa mezani.
"Hiyo ilikuwa tamu siyo? Shushia na Hennessey hapo kidogo," akasema Jenerali Jacob, naye Luteni Jenerali Weisiko akacheka.
Kanali Oswald akaichukua chupa hiyo na kuanza kupiga fundo nyingi sana, akijihisi vibaya sana mwilini mwake. Majenerali wakawa wanamcheka tu.
"Safi sana Kanali. Sasa nimeamini unaweza kufanya lolote kwa ajili yangu. Hey, toa hilo sinia, mletee chakula kingine kizuri," Jenerali Jacob akasema.
"No... hap.. hapana. Nahisi kushiba... niko sawa General," Kanali Oswald akasema.
Majenerali wakaangaliana na kucheka pamoja kwa sifa.
Kanali Oswald akabaki tu kupumua kiuchovu utafikiri alikuwa amelishwa tembo mzima. Luteni Jenerali Weisiko akamnyooshea dole gumba kumpongeza, naye Kanali Oswald akatabasamu kinyonge na kunyanyua kidole gumba pia. Jenerali Jacob na Weisiko wakaendelea kula huku wakicheka sana kutokana na kitendo ambacho walikuwa wamemfanyia mwanaume huyo.
★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Siku hiyo ikakucha, na sasa ikiwa ni asubuhi na mapema, Nora akaamka kutoka usingizini akijihisi uchovu mwingi wa kiakili. Alitulia tu kitandani hapo akiwaza mambo mengi sana kuhusu vitu ambavyo Lexi alimwambia kuhusu baba yake. Aliwaza pia kuhusu mambo ambayo yeye mwenyewe alikuwa amefanya, ikiwa alikuwa akipita kwenye njia sahihi au la, na kama upande ambao alichagua kujiweka ulikuwa ni upande mzuri au mbaya.
Hakujua mambo mengi sana, lakini kama ni jambo moja alilotaka kujua ilikuwa ni habari kumhusu Lexi. Akajinyanyua kutoka kitandani na kuivuta simu yake, kisha akatafuta namba ya Luteni Michael kumuuliza ikiwa Lexi alifikishwa kule alikopelekwa. Lakini akasita kwanza. Akafikiria jambo fulani, kisha akaona aache tu kufanya hivyo. Moyoni mwake alibeba hisia nzito za hatia kutokana na kitendo fulani alichokifanya, na ijapokuwa hakuwa na uhakika kama kilifanikiwa au la, hakutaka kuanza kujichoresha haraka sana kwa sababu ingemletea shida mapema. Na yeye alikuwa na siri pia.
Akaamua tu kuianza siku yake kwa kujisafisha na kupata kiamsha kinywa, kisha ndiyo angetoka na kuelekea kwenye ofisi yake. Akampigia mdogo wake simu kumsalimu huku akinywa chai, na kabla hajamaliza maongezi yao, mlango wa chumba chake ukagongwa. Akatoka kwenda kuangalia ni nani, na hapo mlangoni akamkuta Luteni Michael pamoja na Mario na Hussein. Hakushtuka. Akatoa tabasamu la kirafiki, huku wenyewe wakimwangalia kwa umakini sana.
"Karibuni," Nora akawakaribisha.
"Nora... tunahitaji kuzungumza," Luteni Michael akamwambia.
"Ndiyo, haina shida. Karibuni ndani," Nora akasema.
Mario na Hussein wakatazamana. Luteni Michael akaendelea tu kusimama hapo.
"Kuna tatizo lolote?" Nora akauliza.
"Yule mwanamke ametoroka," Mario akamwambia.
Nora akatazama chini kwa njia ya kawaida tu.
"Hujasikia kuhusu hilo?" Hussein akamuuliza pia.
Nora akatikisa kichwa kukanusha.
"Ametoroka vipi?" akauliza.
"Ameua wanajeshi wanne waliokuwa wanamlinda na kukimbia. Inashangaza sana kwamba ameweza kufanya jambo hilo kwa wepesi wa hali ya juu. Unafikiri aliwezaje kufanya hivyo?" Luteni Michael akauliza.
"Sijui Michael. Lexi... hamkutakiwa kumwekea watu wanne kumlinda. Ana... ana ustadi mkubwa kwenye mambo mengi," Nora akasema.
Wanajeshi wakaangaliana kwa njia yenye utata.
"Kwa hiyo... hawajamkamata bado?" Nora akauliza.
"Nora... sitaki kuku-accuse kwa lolote. Lakini ni muhimu sana ikiwa utasema ukweli. Ni wewe ndiyo ulimsaidia atoroke?" Luteni Michael akamuuliza.
"Mimi? What... ningemsaidia vipi..."
"Kapteni anafikiri ni wewe ndiye uliyefanya huyo mwanamke akaweza kuwatoroka wanajeshi wale. Anataka tukupeleke kwake ili... akuhoji," akasema Luteni Michael.
Nora akashusha pumzi, kisha akasema, "Haina tatizo. Nitaenda pamoja nanyi."
Luteni Michael alimtazama Nora kwa hisia sana.
Mwanamke huyo akarudi ndani na kuchukua vifaa vyake vichache, kisha akaongozana na wanaume hawa watatu mpaka kule alikokuwa Kapteni Erasto. Ilikuwa ni kwenye jengo lile lile, na baada ya kufikishwa kwenye ofisi yake, Nora akaketi na kutazamana na Kapteni Erasto. Mario na Hussein walimsubiria Luteni Michael nje, hivyo ofisini humo kukawa na watu watatu; Kapteni Erasto, Luteni Michael na ACP Nora.
"Nora... nafurahi kwamba umekuja bila kulazimishwa. Step ya kwanza inayoonyesha kwamba unajaribu kuthibitisha hauna hatia. Bila shaka umesikia kuhusu kilichotokea, siyo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Ndiyo. Nimesikia," Nora akajibu.
"Haijakushangaza hata kidogo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Kuna mambo mengi sana ambayo yule mwanamke amefanya huwa yananishangaza. Nimemzoea kwa njia hiyo tayari kwa hiyo... wakati huu sijashangaa sana kuhusu hilo," Nora akasema.
"Mambo kama yapi mengine ambayo amefanya yaliyokushangaza?"
"Ni mengi. Sikudhani angeweza kumkalisha chini Luteni, lakini aliweza," Nora akasema.
"Alibahatisha tu kwa sababu niliangukia kichwa," Luteni Michael akajitetea.
Kapteni Erasto akatabasamu.
"Unajaribu kuwa mcheshi wakati unajua tuko chini ya hali gani?" Kapteni Erasto akamuuliza Nora.
"Sielewi Kapteni unamaanisha nini..."
"Unajua ninachomaanisha. Unajua ulichokifanya. Umemsaidia kutoroka kwa sababu zako za kibinafsi, lakini kwa faida gani? Ili awaue wanaume wenye familia zao kwa ajili yako, au?"
"Mimi sijui unacho..."
"Kaa kimya!" Kapteni Erasto akafoka kwa hasira.
Nora akatulia tu. Luteni Michael akaangalia pembeni.
"Najua ni jinsi gani ulivyo na akili. Umeigeuzia hii kwangu kwa sababu mimi ndiyo nilikagua kile chakula na kuruhusu kipite, kwa hiyo hata kama ikichunguzwa huwezi kukutwa na shida, si ndiyo? Ulifanyaje vile? Ulificha vipi kitu kilichomsaidia atoroke mule?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"Kapteni... bado sielewi, na sijui unachomaanisha. Sijafanya lolote unalosema," Nora akaendelea kukataa.
Kapteni Erasto akatoka upande wa kiti chake na kumfata Nora alipoketi.
"Najua una kiburi kwa sababu unajiona kuwa immune cause baba yako ni General. Kwamba... hautaguswa, mtoto wa mfalme. Lakini kwa kitendo ulichofanya, unafikiri tukimwambia baba yako atakuacha salama? Au hujui kwamba yeye ndiye aliyekuwa anamhitaji zaidi mwanamke huyo?" Kapteni Erasto akamuuliza.
Luteni Michael akamtazama kimaswali. Nora akaendelea kukaa kwa utulivu tu.
"Huenda hiyo ndiyo sababu ukaona umsaidie mpenzi wako malaya mkubwa wewe! Kwa sababu unajua baba yako anataka kummaliza yeye mwenyewe. Unaweza ukajiona ni kama umeshinda, lakini huo ushindi hautafika mbali. Tutamkamata huyo mshenzi mwenzako na kumnyonyoa kila sehemu ya ngozi yake mbele ya macho yako. Na yote hiyo kwa ajili ya General... how do you like your father princess, huh?" Kapteni Erasto akasema kwa dharau.
Luteni Michael alikuwa anamtazama Kapteni Erasto kwa umakini sana. Mambo mengi aliyosema yalimshangaza mno.
"Umemaliza?" Nora akauliza kiutulivu.
"Hapana darling. Muziki ndiyo umeanza tu. Vifo vya ma-comrade wetu lazima vitalipwa, hata kwa damu zisizo na hatia. Na hiyo itakuwa ni juu yako," Kapteni Erasto akamwambia kwa ukaribu.
Nora akamwangalia kwa hisia kali, kisha akasimama na kutoka ndani ya ofisi hiyo.
"Kapteni... ni nini kinaendelea? Umeniagiza nimfate, nimlete, na sasa anaondoka... kihivyo tu?" Luteni Michael akauliza.
"Unafikiri nitamfanyaje? Nitamfunga? Unajua baba yake hataruhusu hilo... na ndiyo kinachompa kiburi hata kama akifanya nini," Kapteni Erasto akasema kwa kuudhika.
"Kwa hiyo kumbe Lexi alikuwa anapelekwa kwa General. Naweza kuuliza ni kwa nini? Nilifikiri anapelekwa kambi ya mateso ili aseme ukweli," Luteni Michael akauliza.
"Haina haja ya kujiingiza sana kwenye mambo ya General. Wewe na team yako pigeni utafiti wenu mmnase huyo mshenzi. Na... hakikisha macho yenu hamyaondoi kwa huyo mwanamke, Nora. Anajua mambo mengi kuliko anavyojionyesha," Kapteni Erasto akasema.
"Una uhakika ni yeye ndiye ambaye alimsaidia Lexi?"
"Damn! Ndiyo! Ni yeye ndiye amemsaidia Lexi. Aagh, silipendi hilo jina Luteni naomba usilitaje tena ukiwa mbele yangu! Nenda upige kazi mwanaume, acha maswali mengi," Kapteni Erasto akamwamuru.
Luteni Michael kweli bado alikuwa na maswali mengi sana kichwani kwake, lakini akatii na kuondoka hapo upesi sana. Alikuwa anataka kumwahi Nora ili aweze kuongea naye, na kwa tukio zuri akamkuta akiwa pamoja na Mario na Hussein, pamoja na mwanamke mwingine mwanajeshi aliyeitwa Samia wakiwa wanaongea. Akawafuata hapo walipokuwa wamesimama.
"Yaani hata hatulali dada, huyu Lexi atatukondesha sana mwaka huu," Mario akawa anamwambia Nora.
"Kwa hiyo... kweli aliwaua wanajeshi wale wote?" Nora akauliza.
"Ndiyo... ndiyo wanavyosema. Demu yuko vizuri eeh?" akasema Hussein.
"We mjinga kweli yaani watu wamekufa halafu unamsifia muuaji?" Samia akasema.
"Sijamsifia. Ila wewe kweli fikiria. Yaani wanajeshi sita... wenye silaha na mafunzo hao... wametorokwa na mwanamke aliyefungwa pingu. We ungeweza?" Hussein akamuuliza Samia.
"Ndiyo ninge...."
"Vijana, nahitaji kuongea na ACP," Luteni Michael akayakatisha maongezi yao.
Wanajeshi hao watatu wakaondoka hapo na kuwaacha wawili hawa.
"Nora... nini kinaendelea?" Luteni Michael akauliza.
"Nilifikiri Erasto amemaliza kukupigia mstari juu ya hilo," Nora akasema.
"No monkey business. Niambie ukweli. Umefanya kama vile anavyodai?"
"Unataka nikwambie nini Michael? Kile ambacho unataka kusikia siwezi kukisema, na kile ambacho hautaamini ndiyo nitakachokisema. Mimi ninaacha... mwamini mnachotaka kuamini. I don't care anymore," Nora akasema.
"Ni sababu gani inayomfanya baba yako amhitaji sana Lexi? Ni nini kimefichika?"
"Sijui Michael. Sijui. Lakini naweza tu kusema kwamba... lolote ambalo anafikiria juu yake si zuri... lakini niko mbali sana kiuwezo kuweza kufanya lolote..."
"Ungefanya nini Nora? Yule mwanamke ni... mwovu. Ni msaliti, ni mwongo, ni mtu mbaya sana ambaye amesababisha uharibiwe sifa yako. Unawezaje hata kuwaza kufanya lolote kwa ajili yake?"
Nora akatulia kidogo na kuangalia pembeni.
"Nora... ninajua una moyo mzuri. Lakini kuna watu wanatumia hilo kama udhaifu ili kukufanyia ubaya. Usijiruhusu... usijiruhusu uchezewe namna hiyo. Unastahili mambo mengi mazuri kwa kazi zako zote kwa ajili ya masilahi ya nchi hii... siyo hivi. Kashifa zote, kuvunjiwa heshima, kuhukumiwa... kwa ajili ya nini? Kwa nini? Eh? Kwa nini unapitia haya yote kwa ajili ya huyo mwanamke Nora?" Luteni Michael akauliza kwa hisia.
Nora akaangalia tu chini bila kutoa neno lolote. Luteni Michael akashusha pumzi kwa kufadhaika.
"Unajua haya yote hayataishia pazuri. Hawataacha kukusumbua. Wata... watafanya kila kitu..."
"Najua. Najua Michael," Nora akamkatisha.
"Kwa hiyo... uko radhi kupoteza kila kitu... kwa ajili yake?" Luteni Michael akauliza.
"Ningeweza kufikia hatua hiyo... lakini sasa... sijui. Mambo mengi yamebadilika. Nitakuwa tayari tu kwa lolote litakalokuja mbele yangu. Niko tayari," Nora akasema.
Luteni Michael akatikisa kichwa chake kwa huzuni.
"Okay. Kanali ameitwa na General hii asubuhi, nafikiri kuhusiana na hii ishu. Mambo upande wetu yanakwenda kwa kasi sana, Lexi atapatikana muda siyo mrefu. Natumaini utakuwa tayari kwa kitakachotokea baada ya hapo," Luteni Michael akamwambia.
Nora akamtazama machoni kwa hisia, kisha akatikisa kichwa chake kuonyesha amemwelewa. Akamwacha hapo na kuondoka zake akiwa na mambo mengi sana kichwani. Mario na Hussein walimchukua na kumrudisha mpaka hotelini kwake tena. Alikuwa anajihisi vibaya sana, na baada ya kuingia ndani ya chumba chake, akaanza kulia kwa uchungu mwingi. Alijihisi kuwa kwenye njia panda na hakukuwa na wa kumsaidia kujua pa kwenda.
Simu yake iliita sana, akipigiwa na watu wa kazini, lakini hakujisumbua kuigusa tena na kujilaza tu kitandani kwa muda mrefu akihisi hatia na
upweke mwingi.
★★★★
Upande wa Kanali Oswald Deule. Alikuwa amefika kwenye jumba la kifahari la Jenerali Jacob, ambapo aliitwa ili kukutana naye. Kwenye jumba hilo kubwa ndipo biashara na mikutano ya muhimu baina ya Jenerali na watu wake ilifanywa, na mara kwa mara wote walioshiriki kwenye mipango haramu ya Jenerali na Raisi walialikwa hapo ili kufanya mazungumzo au mambo yao ya kisiri, na Kanali Oswald alikuwa ni kati ya watu wachache waliokwenda hapo nyakati ambazo Jenerali angewaita.
Lakini wakati huu Kanali Oswald alijua dhumuni la kuitwa kwake halikuwa zuri, kwa sababu alichomwahidi Jenerali hakikuwa kimetimia. Alijua fika kuwa Jenerali Jacob alikuwa mwanaume makini asiyependa mchezo hata kidogo, hivyo kuwa kwake hapo angehitaji kujinyenyekeza sana ili mambo yasimharibikie. Alikaribishwa na mabaunsa walinzi wa jengo lile waliomwongoza mpaka sehemu ya ndani, kisha wakamwomba awape silaha yake yoyote aliyokuwa nayo kwa kuwa Jenerali hakupenda silaha ndani ya jengo lake. Lilikuwa jengo jeupe, safi na pana sana. Kulikuwa na wanawake wengi waliofanya kazi hapo, waliovalia chupi na sidiria kama wanamitindo, wakitumiwa pia kama watoaji wa burudani; kutia ndani na mapenzi.
Alipofika usawa wa ngazi zilizoelekea juu ya ghorofa la pili, Kanali Oswald akamwona Luteni Jenerali Weisiko pamoja na Jenerali Jacob mwenyewe, wakiwa wamesimama huku wakionekana kuongelea mambo fulani kwa umakini. Walikuwa wamezungukwa na wanawake watano ambao walikuwa nusu uchi kabisa, wakiwashika-shika mwilini na kuchezesha miili yao mbele yao kama kuwapa burudani. Bila hata kumwangalia, Jenerali Jacob akamtolea ishara Kanali Oswald kuwa apande mpaka hapo juu. Wasiwasi ulimjaa mwanaume huyu, lakini akasogea mpaka huko na kuwasalimu wakubwa wake hao.
"Za safari Oswald? Umeona mnyama gani anayekula nyama njiani?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aa... safari ilikuwa tulivu. General... najua kwamba nimekosea, na haikuwa kwa... nia mbaya... yaani... tulizungukwa na...."
"Nimekuuliza umeona mnyama gani wakati unakuja?" Jenerali Jacob akamkatisha.
Kanali Oswald akabaki kimya tu.
"Nilitakiwa kufurahia usingizi wangu ili nikiamka asubuhi niifurahie zawadi ambayo uliahidi kuniletea. Nimeufurahia usingizi, lakini mbona zawadi siioni?" akauliza Jenerali Jacob.
"General... kumradhi sana kwa kuwa..."
Jenerali Jacob akanyanyua vidole vyake juu kumkatisha. Weisiko akawaambia wanawake wale waondoke hapo, nao wakatii. Jenerali Jacob akamsogelea karibu Kanali Oswald, ambaye alikuwa anahisi kama anataka kufa vile kwa presha.
"Kwa nini ulinidanganya?" Jenerali Jacob akauliza.
"Siku... sikukudanganya General. Kuna mambo tu yalitokea bila..."
Kanali Oswald akashindwa kuendelea. Aliona jinsi wawili hao walivyomwangalia kwa njia fulani iliyoonyesha walikuwa na lengo fulani baya sana kumwelekea. Lakini mara ghafla Jenerali Jacob akaanza kucheka kwa njia iliyoonyesha hakuwa na ubaya wowote kumwelekea. Kanali Oswald akachanganywa na hili, lakini naye akajifanya kutabasamu.
"Hahahah.... usiniambie hapo ulipo mikojo tayari ilikuwa imeanza kukushuka! Ulikuwa unaogopa sana eeh?" Jacob akamuuliza.
"General..."
"Kanali... usihofu. Mimi tayari nilikuwa najua huyo msichana alitoroka wakati naongea nawe kwenye simu. Najua unafikiri labda nimekasirika sana na nitakufanya jambo fulani baya, lakini hiyo siyo sababu niliyokuitia hapa. Nimekuita hapa ili kukuonyesha jambo lingine. Uko tayari?" Jenerali Jacob akamwambia.
Kanali Oswald akatikisa kichwa kukubali.
Kisha Jenerali Jacob akatabasamu na kuanza kuondoka kuelekea chini ya ngazi zile. Kanali alipomwangalia Weisiko, aliona bado mwanaume huyo alikuwa anamtazama kwa njia isiyo ya kirafiki kabisa, hivyo akajua bado kulikuwa na nuksi. Hawa hawakuwa watu wa kusamehe na kusahau, lakini kama ni kuwaomba msamaha basi angepiga hata magoti ili aupate.
"Unafanya nini Oswald? Nifate," Jenerali Jacob akasema.
"Sawa mkuu," Kanali Oswald akajibu na kuanza kumfata haraka.
Walishuka ngazi pamoja mpaka sehemu ya chini na kuanza kuelekea upande mwingine ndani ya jengo hili. Kanali Oswald hakujua ni wapi au ni nini angeenda kuonyeshwa, hivyo akajikaza tu kiume na kujifariji kwamba mambo yote yangekuwa sawa. Wakafika kwenye mlango mmoja wa chumba ambacho kilikuwa kimejitenga, kisha Jenerali Jacob akaufungua na kuingia ndani. Kanali Oswald akamfuata, na baada ya kuingia aliweza kuona kilikuwa chumba chenye vifaa vingi vilivyotunzwa, kama stoo vile, nacho kilikuwa na giza kiasi.
Jenerali Jacob akasimama usawa wa pazia kubwa jeupe lililokuwa limetundikwa katikati ya chumba na kumgeukia Kanali Oswald.
"Unajua point ya mambo yote tunayofanya ni nini?" Jenerali Jacob akauliza.
"Ni kwa ajili ya taifa General," Kanali Oswald akajibu.
"Oh good. Kwa hiyo kama unajua hilo, inamaanisha unajua pia kwamba hatutakiwi kuruhusu makosa ya aina yoyote kwenye kazi..."
"General..."
"Sijasema kwamba mambo yote yaliyotokea ni makosa yako. Ila unabidi tu uelewe kwamba hawa... Mess Makers wamekuwa... mwiba mkali sana kwangu... na nilipoku-assign uwashughulikie niliamini kabisa kwamba wasingesikika tena..."
"General..."
"...na uliniahidi, uliniahidi... kwamba wasingesikika tena. Huwa sipendi ahadi fake Oswald unajua hilo. Na pia huwa sipendi kuchafua mikono yangu mwenyewe, ndiyo maana nikakuweka unitolee huo uchafu. Nataka tu kujua ni kwa nini umeshindwa kutimiza hiyo ahadi," Jenerali Jacob akasema kwa sauti tulivu.
"General... sijashindwa. Nakuhakikishia Jabari na huyo mwanamke nitawaleta kwako. Hivi tunavyozungumza wanafatiliwa sehemu zote za jiji hili, na hawawezi kufika mbali kwa sababu hawataweza kutoka nje ya mkoa huu. Na hata kama waki...."
"Kanali... haujaona mnyama yoyote anayekula nyama wakati unakuja huku?" Jenerali Jacob akamkatisha na kumuuliza hivyo kwa mara nyingine tena.
Kanali Oswald hakuweza kumwelewa kabisa, lakini alijua bila shaka swali lake lilikuwa na maana fulani. Ikiwa angetoa jibu lisilo sahihi, basi lazima kuna jambo lingetokea. Lakini hakujua ajibu nini, kwa hiyo akaona tu aseme ukweli.
"Hapana General. Sijaona mnyama yoyote anayekula nyama wakati nakuja," Kanali Oswald akajibu.
Jenerali Jacob akacheka sana, kisha akasema, "Basi... wacha nikuonyeshe jambo fulani."
Akalishika pazia lile na kulivuta lote, naye Kanali Oswald akatoa macho kwa mshangao mkubwa. Hapo aliweza kuona ndoo mbili chini, zikidondokewa na damu kutoka kwenye kiwiliwili cha mtu kilichotundikwa juu kama nyama za buchani. Yaani, hakikuwa na kichwa, wala mikono na miguu. Kuanzia shingoni mpaka usawa wa mapaja ndiyo mwili uliokuwepo, na sehemu zake za siri zilikuwa zimekatwa. Hakujua ulikuwa ni mwili wa nani, lakini ilionekana kuwa ni mwanaume kutokana na kutokuwa na matiti makubwa, na uimara wake tumboni.
Lilikuwa ni jambo moja la kikatili sana, naye Kanali Oswald akamtazama Jenerali akiwa anajikaza. Kuona jinsi ambavyo damu bado zilitiririka ilimaanisha jambo hilo lilikuwa limefanyika siku hiyo hiyo na muda mfupi tu uliopita.
"Hivi ndivyo nilivyopigia picha kuuona mwili wa Jabari na binti yake leo. Ingenipa furaha sana kama ningeweza kuikatakata miili yao namna hii... kwa mikono yangu mwenyewe," Jenerali Jacob akasema.
Kanali Oswald akabaki kimya tu.
"Unajua huyu ni nani? Oh, bila shaka huwezi kujua. Lakini kiukweli Oswald... sijaridhika. Nimejitahidi kutoa hasira yangu namna hii lakini... bado sijaridhika. Bado... nahitaji kuitoa hasira nayohisi kutoka kifuani kwangu. Utanisaidia vipi?" Jenerali Jacob akauliza huku anamwangalia Oswald kwa umakini.
"General... nakuahidi... nakuahidi kwa maisha yangu, nitakupa Jabari na Lexi. Nitawa..."
Kabla hajamaliza kuongea, wanaume wawili wenye miili mikubwa wakaingia ndani hapo pamoja na Luteni Jenerali Weisiko, na wanaume hao wakamshika kwa nguvu Kanali Oswald mikononi. Hofu kubwa ilimwingia mwanaume huyu kwa kuwa alitambua sasa kwamba huu ulikuwa ni mwisho wake.
"General, General... tafadhali nisamehe, nisamehe, nisamehe... General niamini... General nita... nitafanya lolote kwa ajili yako... nimefanya mengi sana ajili yako... General tafafhali usinitendee kwa... tafa... tafadhali General..."
Kanali Oswald akawa anamsihi sana Jenerali asimuumize. Alihisi kile ambacho ametoka kuonyeshwa ndiyo ambacho angefanyiwa. Wanaume wale wawili wakaendelea kumshikilia kwa nguvu na kumpigisha magoti chini, naye Weisiko akasimama pembeni yake Jacob akiwa ameshikilia panga lenye makali pande zote mbili.
"Bado naweza kuwa msaada mkubwa kwako General... tafadhali... niruhusu nirekebishe hili... ninakuhakikishia... General nitawaleta kwako please..."
"Acha kulia-lia kama bwege bwana. Tulia... na hii haitauma sana," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia huku akimsogelea na panga leke.
"Tafadhali General... kila kitu kilikuwa kinaenda vyema. Angefika kwako kama isingekuwa ya binti yako... General tafadhali usifanye hivi... nimekufanyia mambo mengi sana... siwezi kukuangusha..."
"Subiri," Jenerali Jacob akasema.
Luteni Jenerali Weisiko akatulia kidogo na kumwangalia usoni. Kanali Oswald alikuwa anapumua kwa hofu huku akitokwa na jasho.
"Unamaanisha nini isingekuwa ya binti yangu?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aam... ni ACP Nora ndiye aliyefanya mpaka Lexi akatoroka," Kanali Oswald akajibu kwa hofu.
"Kwa nini afanye kitu cha namna hiyo?" Jenerali Jacob akauliza.
"Binti yako alikuwa na urafiki naye... lakini inaonekana pia kwamba anampenda," Oswald akajibu.
"Nini?" Jenerali Jacob akashangaa.
"Unatutania eti?" Weisiko akamuuliza pia.
"Hapana mkuu, hapana. Ni kweli. Kabla ya kuanzisha safari ile... alituomba sana... Nora... alituomba tumruhusu amwone kwa mara ya mwisho... na mimi kwa sababu namheshimu binti yako nikamruhusu General kwa sababu alionyesha uhitaji. Ila akasaliti imani yetu kwake..."
Kabla hajamaliza kuongea, Weisiko akamshika kidevuni kwa nguvu na kumpiga usoni kwa kishikio cha panga lake. Damu zikaanza kumtoka puani Kanali Oswald, akihisi maumivu makali pia.
"General... niruhusu niukatekate ulimi wake sasa hivi huyu mpuuzi," Weisiko akasema huku anamwangalia Kanali Oswald kiukatili.
"Ngoja..."
Jenerali Jacob akasema hivyo na kusogea karibu zaidi na Kanali Oswald.
"Unajua nitakupa kifo kibaya zaidi ya kile unachofikiria nikijua unamsingizia mtoto wangu," Jenerali Jacob akasema kwa uzito.
"Hapana Jenerali... simsingizii. Lexi asingeweza kutoroka kabisa. Ninajua aliweka kitu fulani kwenye chakula alichoomba kumpatia kabla ya safari, na alikificha kwa akili sana... hatukuweza kutambua. General niamini... siwezi nikasema jambo hilo kuhusu mwanao kama... kama sina uhakika. Na najua sipaswi kumfanya lolote kwa sababu ni binti yako, ila ndiyo hivyo ameshatu-cost tayari na sasa inabidi tu tuendelee kuwatafuta wakina..."
"Kaa kimya," Luteni Jenerali Weisiko akamkatisha.
Kanali Oswald akatulia maana alikuwa anaongea haraka-haraka kama cherehani.
"Ulikuwa wapi kuniambia kuhusu hilo muda huo wote?" Jenerali Jacob akauliza.
"Hatukujua... samahani... Lexi alikuwa anamtumia binti yako ili kupata taarifa nyingi na kujua mambo yote kuhusu mipango yetu. Binti yako ni mtu mzuri, kwa hiyo yule mwanamke amemfanyia ulaghai mwingi sana. Hata hii ya kumsaidia atoroke ninajua atakuwa tu amemfanyia ulaghai..." Kanali Oswald akaongea kwa kujifanya anamtetea mtoto wa Jacob.
Jenerali Jacob akavuta pumzi ndefu na kuishusha, akitafakari mambo haya. Kanali Oswald akawa anauangalia kwa hofu mwili ule uliokatwa, kwa kupigia picha kwamba na yeye angefanywa namna hiyo.
"Hata ijapokuwa unachosema kinashangaza, bado ni makosa yako kwamba mpaka sasa haujaweza kuwaleta watu hao kwa General. Ukifikiri hicho kitakuwa ni kisingizio cha kukuacha salama, umekwama ndugu yangu," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia.
"Hapana mkubwa... mimi niko loyal kwenu, sikuzote. Sikumshuku binti yako mwanzoni kwa sababu aliaminika... imetokea tu kwamba akausaliti uaminifu huo... haikuwa lengo langu... haikuwa... tafadhali General... nionyeshe msamaha... niko tayari kufanya lolote kwa ajili yako... nitahakikisha..."
"Basi, basi, inatosha. Nyanyuka," Jenerali Jacob akamwambia.
Kanali Oswald akabaki tu kumwangalia.
"Huelewi Kiswahili? Amesema nyanyuka," Luteni Jenerali Weisiko akamwambia kiukali.
Wanaume wale wawili walikuwa wamemwachia Kanali Oswald, hivyo akajinyanyua na kusimama huku bado akiwa mwenye wasiwasi mwingi.
"Sitaki makosa ya aina yoyote yajitokeze tena, unanielewa?" Jenerali Jacob akamwambia.
"Ndiyo... ndiyo General. Sitakuangusha," Kanali Oswald akasema.
"Acha kuogopa. Sikuwa na lengo la kukuua, najua uko loyal sana," Jenerali Jacob akamwambia huku amemshika bega.
Luteni Jenerali Weisiko akacheka kidogo, naye Kanali Oswald akatoa tabasamu la woga-woga.
"Ila, nataka uwe unanijulisha kila kitu kinachoendelea kuanzia sasa, na ninakupa wiki mbili tu washenzi wale uwe umewaleta kwangu, do you understand?" Jenerali Jacob akasema.
"Ondoa shaka General. Nakuahidi nitawaleta kwako mapema kabla ya muda huo," Kanali Oswald akatoa ahadi.
"Acha kujitapa kwa maneno hewa Kanali. Unatoa ahadi halafu hai..."
"Hapana Luteni Jenerali. Zamu hii hata Mungu hataweza kunizuia. Nitahakikisha siwakwazi na ninawaleta kwenu. Nitawaletea wale watu kwenu... kwako General..." Kanali Oswald akaapa.
Jenerali Jacob akatabasamu na kusema, "Vizuri."
Kanali Oswald akashusha pumzi ya utulivu. Alikuwa anahisi kama vile angejiharishia kabisa.
"General... vipi kuhusu hili suala la Nora?" Luteni Jenerali Weisiko akamuuliza.
"Nora... nitadili naye mimi mwenyewe. Kanali hakikisha hakuna mpuuzi yeyote anamgusa binti yangu, unanielewa?" Jenerali Jacob akasema.
"Ndiyo mkuu," Kanali Oswald akajibu.
"Sawa. Unahisi njaa?" Jenerali Jacob akauliza.
"Aaa... ndiyo General... nahisi njaa kiasi," Kanali Oswald akajibu kiwoga-woga.
"Okay. Sahau haya yote, twende tukapate chakula..."
Jenerali Jacob akasema maneno hayo na kuwatolea ishara wanaume wale wawili kuwa walirudishie pazia lile pale juu, kisha akamshika Kanali Oswald begani kirafiki na kuanza kuondoka pamoja naye. Waliongozana mpaka kwenye meza ya chakula huku Jenerali akimwambia Kanali anapaswa kuacha kuogopa kwa kuwa hangemfanyia jambo baya.
Baada ya kuketi kwenye viti pamoja na Weisiko, Jenerali Jacob akaagiza vyakula kwa ajili yao viletwe, na kusema kwa wanawake wale kwamba wamletee chakula "special" Kanali Oswald. Yeye Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko walikuwa wameletewa vyakula vizuri vya aina mbalimbali, kisha Kanali akaletewa sinia pana lililofunikwa kwa juu na kuwekewa mbele yake. Akahisi bila shaka kulikuwa nuksi kwa ndani, naye akamtazama Jenerali kwa wasiwasi.
"Najua wewe uko loyal kwangu, lakini nataka kuona ikiwa utafanya KILA KITU nitakachokuamuru... kama ulivyotoka kusema muda ule," Jenerali Jacob akasema hivyo huku akitabasamu.
Kanali Oswald akameza mate akianza kuingiwa na hofu kwa kufikiri labda alikuwa anapewa nyoka ale. Kisha Jenerali Jacob akamwambia mwanamke aliyemletea sinia hilo alifunue, na baada ya kulifunua, Kanali Oswald akafumba macho na kugeukia pembeni.
"General... General nini hiki?" Kanali Oswald akauliza kwa kufadhaika sana.
"Ndiyo chakula special kwa ajili yako. Sikuwa na jinsi ila kukupa wewe maana ulisema hukuona mnyama yeyote anayekula nyama wakati unakuja. Nataka unithibitishie kwamba na wewe ni mnyama... hahahahah..." Jenerali Jacob akasema hivyo na kuanza kucheka pamoja na Luteni Jenerali Weisiko.
Kanali Oswald akakitazama tena "chakula" hicho. Kilikuwa ni kichwa kilichokatwa cha mwanaume, na mwanaume huyo alikuwa ndiye yule mwanajeshi ambaye aliendesha gari lile lililokuwa likimsafirisha Lexi usiku wa jana. Pembeni ya kichwa hicho kulikuwa na uume wake uliokatwa, na mipira ya uzazi ikiwa imekatwa na kusambaza damu kwenye sinia hilo. Vyote vikiwa vibichi!
"General..."
"Kula. Nataka ule chochote kati ya hivyo, then mambo mengine yatafuata," Jenerali Jacob akasema.
Kanali Oswald alihisi kuchoka. Alijua alipaswa kula la sivyo cha moto angekiona. Akajitoa akili na kujikaza kiume, kisha akachukua kisu kidogo pembeni na uma, naye akaanza kuikata sehemu ndogo ya sikio kwenye kichwa ili ale, lakini Jenerali Jacob akamzuia.
"Nimekwambia chagua kati ya hivyo ule, sijakwambia ukate. Ukichagua kichwa, ujue unakila chote," Jenerali Jacob akasema.
Aisee!
Wanawake waliokuwa pembeni walihisi vibaya sana kumwelekea Kanali Oswald. Walimwonea huruma. Kanali Oswald akabaki tu kuangalia vitu hivyo mbele yake. Alijiuliza hata walimleta mwanaume huyo huku saa ngapi. Akamtazama Weisiko kidogo, naye akamtolea ishara kwa macho yake kuwa achague na ale. Kanali Oswald akafumba macho na kukaza meno yake, kisha akaweka kisu na uma pembeni, halafu akauchukua uume ule na kuudumbukiza mdomoni!
"Usimeze... tafuna!" Jenerali Jacob akasema kiutulivu.
Kanali Oswald akawa ameweka tango hilo dogo mdomoni huku ametoa macho kimshangao. Akaanza kutafuna huku akijikaza asitapike. Kwachu, kwachu, kwachu, akaendelea kutafuna huku watu hapo ndani wakimwangalia kwa umakini. Wanawake kadhaa walikuwa wameziba macho na midomo wasiamini walichoona. Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko wakaendelea kumwangalia mpaka alipomaliza kutafuna na kumeza, kisha akawa anajitahidi asitapike hata kidogo.
Wawili hao wakaanza kumcheka sana.
"Hahahahaa... mnofu tu..." Jenerali Jacob akasema.
"Mnofu tu," Luteni Jenerali Weisiko akamalizia huku akicheka.
Jenerali Jacob akatoa ishara kwa kiganja chake, kisha chupa kubwa ya wine ikaletwa hapo na kuwekwa mezani.
"Hiyo ilikuwa tamu siyo? Shushia na Hennessey hapo kidogo," akasema Jenerali Jacob, naye Luteni Jenerali Weisiko akacheka.
Kanali Oswald akaichukua chupa hiyo na kuanza kupiga fundo nyingi sana, akijihisi vibaya sana mwilini mwake. Majenerali wakawa wanamcheka tu.
"Safi sana Kanali. Sasa nimeamini unaweza kufanya lolote kwa ajili yangu. Hey, toa hilo sinia, mletee chakula kingine kizuri," Jenerali Jacob akasema.
"No... hap.. hapana. Nahisi kushiba... niko sawa General," Kanali Oswald akasema.
Majenerali wakaangaliana na kucheka pamoja kwa sifa.
Kanali Oswald akabaki tu kupumua kiuchovu utafikiri alikuwa amelishwa tembo mzima. Luteni Jenerali Weisiko akamnyooshea dole gumba kumpongeza, naye Kanali Oswald akatabasamu kinyonge na kunyanyua kidole gumba pia. Jenerali Jacob na Weisiko wakaendelea kula huku wakicheka sana kutokana na kitendo ambacho walikuwa wamemfanyia mwanaume huyo.
★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893