Kitomari xxiv
JF-Expert Member
- Sep 26, 2021
- 1,283
- 12,555
Daaah nimeisoma kwa hasira na gadhabu zikimwelekea Kevin,
Yaan atajuta
Yaan atajuta
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
dah kit kinazid kuchanja mbugaFOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Hatimaye Lexi akawa amefika nje ya hoteli aliyokaa Nora. Usiku ulikuwa umekwishaingia sasa, na maghorofa ya hoteli hiyo yalionekana yakimeremeta kwa taa zake nyingi. Alikuwa amekwishamtumia Nora ujumbe kwamba angefika hapo, na kusema angemweleza pia alikokuwa na kwa nini hakupatikana kwa siku hizo chache. Akaizima tena simu yake na kushuka kutoka kwenye gari na kuelekea huko ndani mpaka alipofika nje ya mlango wa chumba cha Nora. Akashusha pumzi ya kujiweka sawa, kisha akaugonga mlango kistaarabu na kusubiri. Hazikupita sekunde nyingi, nao mlango ukafunguliwa.
Lexi alihisi mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi zaidi baada ya kumwona Nora kwa mara nyingine tena. Alivutiwa zaidi na jinsi alivyosuka wakati huu, na kufanya ajiulize ikiwa aliamua kujipendezesha kwa ajili yake. Nora alikuwa amesimama ndani hapo huku ameushikilia mlango na kumwangalia Lexi kwa hisia sana, kwa sababu kihalisi alikuwa amemkumbuka mno "mwanamke" huyu. Ijapokuwa kuna mambo mengi yaliyokuwa yakipita akilini mwake, akaachia tabasamu la mbali kuonyesha amefurahi kumwona, naye Lexi akatabasamu pia.
Nora akamkaribisha ndani, na baada ya Lexi kuingia akaufunga mlango na kushusha pumzi ndefu huku akiwa amefumba macho yake, naye akamgeukia taratibu.
"Pole, nimekufanya usubiri sana?" Lexi akamuuliza.
"Hapana. Nami ndiyo nimefika tu," Nora akajibu.
"Okay... sawa. Umekula?" Lexi akauliza.
Nora akatikisa kichwa kukubali.
"Ona... kulikuwa na mambo fulani ya kifamilia hapa katikati na... nilihitajika huko. Yalikuwa mambo mengi ndiyo maana nilikuwa sipatikani. Nisamehe kwa kukufanya uni-miss sana," Lexi akasema.
"Usijali... haina shida. Kwa hiyo... familia yako... mambo yako vizuri sasa?" Nora akauliza.
"Yeah, tumejitahidi kuyajenga. Kila kitu kiko sawa," Lexi akasema.
"Umefanyaje mkononi?" Nora akauliza.
Lexi akajitazama sehemu ya mkono wake iliyofungwa kwa bendeji, ambapo aliumizwa na yule mnyama wake, Zelda.
"Aam... niliumia tu kidogo wakati niko huko. Siyo kitu serious sana," Lexi akasema.
Nora akabaki kumtazama kwa njia ambayo ilimwambia Lexi kwamba mwanamke huyo alikuwa anawaza jambo fulani kumhusu.
"Vipi wewe? Mambo yamekwendaje huku wakati sipo?" Lexi akamuuliza.
Nora akabaki kumtazama tu.
"Uko sawa mheshimiwa?" Lexi akauliza kwa njia ya kujali.
Nora akamsogelea karibu na kuuliza, "Wewe unaonaje? Niko sawa?"
Swali hilo likamfanya Lexi atambue kuwa kweli kuna jambo hapa halikuwa sawa. Wazo la kwamba huenda Nora alikuwa amegundua yeye ni nani likamwingia, lakini akajitahidi kutoonyesha itikio lolote la kubabaika.
"Naona kama vile hauko sawa. Una hasira na mimi kwa sababu sikukujibu hizi siku mbili, eti?" Lexi akauliza.
"Sina hasira nawe. Nimeumia tu," Nora akasema.
Lexi akabaki kimya.
"Ila sijaumia kwa sababu ya wewe kutonijibu... la. Nimeumia kwa sababu... nilifikiri nimepata kitu fulani ambacho nakijua, ila sasa nimetambua kuwa sikijui kabisa," Nora akasema.
Kauli hiyo ilimtikisa sana Lexi moyoni. Nora alisema maneno hayo kwa hisia nzito sana, na Lexi tayari akawa ameshakisia mwanamke huyu alielekea wapi ingawa alitaka kuhakiki zaidi.
"Mheshimiwa... mbona unaongea hivyo? Sielewi, niambie unamaanisha nini..." Lexi akasema.
"Oh Lexi... kwa nini lakini? Kwa nini ilipaswa kuwa wewe? Why was it supposed to be like this?" Nora akauliza na kuanza kudondosha machozi.
Lexi tayari akawa ameelewa. Nora alijua. Alijua kila kitu. Lakini utata ni kwamba alijua jinsi gani, na kwa sababu hiyo Lexi akaona aendelee kulazimisha mambo.
"Mheshimiwa... sielewi... tafadhali niambie, unamaanisha nini? Unaniogopesha..." Lexi akamwambia.
"Ahah... nakuogopesha. Hivi wewe ni nani? Kwa nini umeingia kwenye maisha yangu kama mwangaza mpya wa furaha lakini kumbe ni kitovu kikuu cha maumivu Lexi? Unafurahia sana kuumiza watu, eti? Furaha yako ipo kwenye huzuni za wengine, si ndiyo? Tell me. Najua unajua nachomaanisha. Tusizungukane kama watoto, just... tell me. Hakuna mtu mwingine hapa. Niambie tu. Kwa nini unafanya mambo haya yote? Kwa nini unaumiza watu wengi sana? Pesa? Ni pesa tu? Au kuna kingine dada yangu?" Nora akaendelea kuuliza.
Lexi alikuwa anamwangalia sana asijue la kusema. Angeanzia wapi kumwelezea maana ya mambo yote yeye na wenzake waliyokuwa wamefanya? Kuona kwamba hakuwa amemwitia labda maaskari ili wamkamate kulionyesha kwamba mwanamke huyu aliumizwa sana na ukweli alioujua kiasi kwamba alitaka kusikia kutoka kwa Lexi pekee sababu yake ni nini, ili amhukumu yeye kama yeye. Hii ilionyesha bado kuna vitu aliviona ndani ya Lexi vilivyompa matumaini ya kwamba huenda alikuwa na sababu iliyompelekea kufanya mambo mabaya, ingawa hiyo haingehalalisha matendo hayo yaliyopingana na sheria.
Lexi akabaki kutazamana na Nora tu kwa hisia sana, akijiuliza aseme nini sasa. Ajaribu kumwelewesha vizuri sababu zake, au amdanganye tu?
★★
Wakati hayo yakiwa yanaendelea, Luteni Michael, akiwa pamoja na Alex, Mario, Hussein, Rachel, Tariq na Zachary, walikuwa wanarejea jijini Dar es Salaam kutokea mkoa mwingine walipokuwa wamekwenda kutafiti masuala ya Mess Makers. Ulikuwa ni uamuzi wa Kanali Oswald Deule, ambaye kwa kujifanya mtaalamu sana aliwaagiza kwenda huko lakini hawakupata matokeo yoyote chanya.
Sasa wakiwa njiani kuelekea kule ambako jengo lao la utafiti lilikuwepo, wakatumiwa taarifa na Bobby zilizowaacha wote midomo wazi. Alikuwa amewatumia vigezo kwa njia ya simu vilivyowaonyesha watu sita ambao walitambulishwa kuwa Mess Makers. Kulikuwa na picha zao, majina yao, na taarifa chache zilizothibitisha kwamba wao kweli ndiyo waliokuwa Mess Makers. Hawa walikuwa ni Lexi Sona, Oscar Amari, Victor Quawey, Mensah Dodzi, Kevin Dass, na Kendrick Jabari!
Ni wawili tu ndiyo ambao hawakuwepo kwenye orodha hiyo, yaani LaKeisha na Torres.
Luteni Michael akamuuliza Bobby taarifa hizo alizipata vipi, naye akasema zilikuwa zimerushwa tu kutoka kwenye chanzo kisichojulikana, na alipojaribu kukifatilia akashindwa kukipata. Taarifa zilizothibitisha kwamba watu hao walikuwa ni kutoka kundi la Mess Makers ni pamoja na rekodi za sauti za maongezi yao wakati ule walipoiba dhahabu kwenye treni, wakati ambao Kendrick Jabari alifanya mpango wa kumteka ACP Nora ili kumuua kupitia kwa wanaume wale saba, na wakati ambao Salim Khan alikufa.
Ingawa hakukuwa na taarifa nyingi sana, mambo hayo tu yalitosha kabisa kuthibitisha kwamba ilikuwa ni kweli hasa kwa kuona uwepo wa Oscar na Kevin kati ya watu hao. Bobby alimwambia Luteni Michael kuwa mambo hayo yalikuwa yamesambazwa mpaka kwenye vyombo vya habari, na bila shaka yangekuwa yameshafika mpaka kwa wakuu wao. Wanajeshi waliopata taarifa hizo walishangaa sana kujua kwamba Kendrick Jabari alikuwa hai, kwa sababu walimfahamu kuwa na cheo cha Kapteni miaka kadhaa nyuma kabla ya tukio lililosababisha "kifo" chake.
Ikabidi Luteni Michael amtafute Kanali Oswald, ambaye naye tayari alikuwa amezipata na kumwambia waanze kutafuta ni wapi ambapo watu hao wangekuwa kupitia kwa Manengo na Bobby. Walikuwa wakimlenga zaidi Kendrick Jabari, hasa kwa sababu ya utata wa yeye kuhusika na Mess Makers wakati ilidhaniwa alikuwa amekufa kitambo. Manengo akawa amefanikiwa kujua kwamba Kendrick Jabari alikuwa nchini humo kwa zaidi ya mwaka sasa kutokea Ghana, na alikuwa akimiliki kampuni zilizohusiana na madini. Hakuwahi kuonwa hadharani lakini aliziendesha kampuni hizo kwa muda mrefu, na ikashangaza kwamba hakuwa ametambulika kwa muda wote huo.
Baada ya kufatilia taarifa za mawasiliano ya kawaida za Kendrick na wengine, kama walivyofanya tu mara ya kwanza kwa Kevin Dass, Manengo akabaini kuwa kwa sasa mwanaume huyo alikuwa kwenye moja ya kampuni zake pamoja na wenzake wawili, na eneo hilo lilikuwa hapo hapo jijini. Upesi, taarifa hizo zikatumwa kwa Luteni Michael ili yeye na wenzake wapitilizie huko huko. Kanali Oswald akawaambia kwamba angetuma taarifa kwa vyombo vya usalama vya maeneo ya huko kwenye kampuni ya Kendrick ili waagize vijana mahiri kwenda kuwakamata watu hao wakati Luteni Michael na wengine wakiwa njiani kuelekea huko.
Safari ya timu ya Luteni Michael ikageuza mkondo haraka sana. Luteni Michael alijawa na hamu kubwa mno ya kuja kumwonyesha Nora ukweli huo kumhusu Lexi ambao tokea mwanzo aliuhisi, lakini Nora na kila mtu akamwona mjinga. Alikuwa na hasira sana pia iliyomfanya atake kuwa wa kwanza kumshika Lexi ili amwonyeshe nini maana ya dharau kama aliyomwonyesha siku ile kwenye chumba cha Nora.
★★
Kufichuliwa kwa timu ya Mess Makers kulianza kusambaa kutoka kwenye vyombo vya habari, na pia mitandao ya kijamii haikuwa nyuma kuifanya hiyo kuwa mada iliyoongoza zaidi a.k.a "number one trending." Zilifika kwa wakuu wa jeshi, yaani Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko, na hata Raisi Paul Mdeme pia, na wote walikuwa wameachwa midomo wazi kwa kutoamini kabisa ukweli huo. Waliwasiliana na kuanza kuulizana iliwezekana vipi kwa Kendrick Jabari kuwa hai muda wote huo na wenyewe wasijue, na kilichoshangaza hata zaidi ni kumwona mtoto wa Meja Casmir akiwa hai pia.
Jenerali Jacob alimkumbusha Weisiko sasa kwamba kwa sababu ya kutokufuatilia kwake mambo vizuri usiku ule, mwanaume huyu alikuwa amesababisha madhara makubwa yaliyoletwa na wawili wale na kundi lao wakati huu. Ikawa wazi sasa kwamba hii ishu yote ya "Mess Makers" ilitokana na Kendrick Jabari na mtoto wa Casmir kama njia yao ya kuwalipizia kisasi. Ingawa bado hawakuweza kuelewa wawili wale walitaka kuwalipizia kisasi kwa njia gani kikamili, bado kuwa kwao hai ilikuwa ni tatizo kwa Majenerali na Raisi kwa sababu ni watu waliojua ukweli wote kuhusiana na Demba Group miaka nane iliyopita.
Raisi Paul Mdeme alikuwa amewasiliana na Jenerali Jacob na kumwambia kuwa haya yote yalikuwa makosa yao yeye na Weisiko kwa kukosa kuwamaliza wawili wale miaka mingi iliyopita, na sasa mambo mengi hata zaidi yangevurugika. Jenerali Jacob alipandwa na hasira sana. Hivi siyo jinsi alivyotaka mambo yaende hata kidogo, kwa sababu vyombo vya habari kujua kuhusu watu hao mapema namna hiyo kungeweza kufichua siri zao nyingi sana.
Akamwamuru Weisiko afanye juu chini ili kuwakamata watu hao upesi, kwa njia zozote zile ambazo tayari zilikuwa zimewekwa, afanye lolote lile ili kuwapeleka watu hao upande wao waweze kuwashughulikia wenyewe. Weisiko akamwambia tayari hilo lilikuwa likifanyiwa kazi, na bila shaka wangehakikisha wanafanikiwa; iwe isiwe.
★★
Lexi bado alikuwa kwenye chumba cha hoteli pamoja na Nora, akiwa bado anatafuta namna ya kujieleza kwake, lakini akashindwa. Nora alikuwa anaongea maneno yenye kuonyesha hisia nyingi za kuvunjika moyo, akimwambia kwamba kwa sababu ya mambo hayo, angetakiwa kumfunga pingu na kumpeleka jela yeye mwenyewe ikiwa hangempa sababu nzuri ni kwa nini alifanya mambo mabaya kuielekea serikali hii.
Lexi aliwaza; ikiwa kweli Nora angetaka kumtia mikononi mwa sheria, basi angekuwa amemwekea mtego mapema wakati alipofika hapo. Aliona ukweli wa kwamba mwanamke huyu hakuwa na hasira wala chuki kumwelekea, bali aliumia sana kwa sababu alidhani yeye ni tofauti. Sasa akawa anapambana na hisia zake mwenyewe hata zaidi, kwa sababu ilionekana ni kama alitakiwa kujigawa mara mbili kutoka kwenye yale aliyofanya, na kile alichohisi moyoni. Hata kama angesema nini, alijua mwanamke huyu asingemwamini kirahisi.
Wakati Nora alipokuwa akiendelea kusubiri jibu kutoka kwa Lexi, simu yake ikaita. Akaitoa kutoka mfukoni mwa suruali yake na kupokea bila kuangalia ni nani, huku bado akiwa anamtazama Lexi machoni. Lakini baada ya kutambua kwamba ilikuwa ni Bobby ndiye aliyempigia, akaweka umakini wake hata zaidi. Mwanaume huyo akamjulisha mambo yote yaliyokuwa yakiendelea, akisema Mess Makers walikuwa wamefichuliwa na mtu fulani asiyejulikana.
Mwonekano wa sura ya kushangaa kiasi usoni kwa Nora ukamwambia Lexi kuwa kuna jambo lilikuwa likiendelea; jambo baya. Nora hakuongea chochote kile zaidi ya kuitikia na kuendelea tu kumsikiliza Bobby, ambaye akamwambia kwamba alikuwa amemtumia taarifa hizo zenye kushangaza kwenye mfumo wake wa siri wa kutunza mambo. Huo ulikuwa umeunganishwa kwenye "tablet" yake Nora, hivyo upesi akampita Lexi na kuifata ilipokuwa kwenye mkoba wake. Akamgeukia Lexi na kumtazama kidogo, kisha akaiwasha na kuanza kutafuta habari hizo. Alikuwa anataka kuona uthibitisho zaidi ikiwa Lexi angekuwapo pia kwenye taarifa hizo, na baada ya kumwona, akachoka sana. Akafumba macho yake na kutikisa kichwa chake kidogo, akiwa amehisi kuvunjika moyo hata zaidi.
Alipogeuka nyuma tena ili amwonyeshe vizuri zaidi sasa Lexi ukweli yeye mwenyewe, akashangaa kukuta kwamba Lexi tayari alikuwa ameondoka. Yaani ilikuwa ghafla na kwa njia ya haraka, naye hakuwa ametambua hilo. Kwa haraka akafikiria kwamba ni lazima tu Lexi angekuwa amekimbia ili labda kwenda kuwaonya wenzake, na kwa sababu Bobby alikuwa amemtumia taarifa za walikokuwa wenzake na Lexi, Nora akaamua kwamba angekwenda huko huko pia. Akarudi sehemu yenye droo upesi na kutoa bastola yake, kisha akazifunga nywele zake vizuri kwa nyuma na kutoka hapo haraka sana.
Moto sasa ungeanza kuwa mkali zaidi!
★★★★
Kendrick alikuwa bado pamoja na vijana wake kule kwenye kampuni yake, na sasa walikuwa wamemaliza kufanya yale ambayo Torres alihitaji kufanya. Hii ilikuwa ni hatua ya kwanza, na hatua ya pili ndiyo ingekamilisha mpango wao maalum waliokuwa wameuweka. Azra alipata kujionea mambo mengi hapo yaliyothibitisha kwamba watu hawa waliofahamika kama "Mess Makers" hawakuwa wabaya kama alivyodhani, na hisia mpya ya kujiona kuwa "sahihi" ikamwingia kwa sababu ya kuwa upande wao. Kendrick akamwambia kwamba kuna mambo mengi wangetimiza pamoja, mambo ambayo yangekuwa faida kwa watu wengi sana kutokana na yale waliyoyafanya.
LaKeisha pamoja na wengine walikuwa pembeni, na mwanamke huyu alikuwa ameboeka, hivyo akaamua tu kuzama kwenye mitandao ya kijamii; akitafuta udaku wa hapa na pale. Si ndiyo akazibamba sasa zile taarifa! Mwanzoni alihisi ni kama masihara, lakini alipofuatilia vizuri, akatambua kwamba kundi lao lilikuwa limevurugwa.
Upesi akawaonyesha wenzake mambo yalikuwa vipi, na wao pia wakapigwa na butwaa zito baada ya kuona mambo hayo. Wakaanza kujiuliza iliwezekana vipi wao kuweza kutambulika kirahisi namna hiyo mpaka kwenye mitandao ya kijamii, na fikira ya kwanza ilikuwa ni ACP Nora. Walidhani labda mwanamke huyo ndiye aliyefanya jambo fulani kuwafichua baadhi yao. Walianza kuzivunja laini na simu zao zote za kawaida, nao wakaanza kujiandaa kutoka jengoni hapo haraka iwezekanavyo.
Walitumia lifti ile ya kibinafsi kushuka mpaka kule chini ili waelekee kwenye magari yao, pale waliposhtushwa na magari matatu yaliyokuwa yamefika upande huo na kusimama umbali fulani kutoka kwao. Waliweza kuyatambua kwa haraka kuwa magari ya wanajeshi maalum, au majasusi, nao wakajiuliza walifikaje hapo haraka hivyo na hata walijuaje wangekuwa hapo.
Majasusi hao maalum wakashuka wakiwa wamevalia nguo nyeusi na kushikilia bunduki huku wakiwaelekea wakina Kendrick, nao walikuwa wakiwaambia wajisalimishe haraka sana. Kendrick na vijana wake wakaanza kukimbilia pande ambazo kulikuwa na nguzo nene zilizoshikilia ghorofa ili wajifiche, wakati huo Victor akawa ametoa bastola yake ndogo na kuwafyatulia risasi ili kuwachengua, na majasusi hao wakajikinga kwenye baadhi ya magari na nguzo za pembeni. Victor akawahi na kujirusha kwenye nguzo moja, kitu kilichofanya adondoshe begi lake, huku majasusi wale wakianza kusogea taratibu na kufyatulia risasi nyingi sana upande wa Mess Makers, zilizotoboa kuta, magari, na kupasua sehemu za nguzo zile walizojifichia.
LaKeisha alikuwa anatukana kwa hasira kwa sababu ya kutoelewa haya yote yaliwezekana vipi, lakini wakati huo huo tayari Torres akawa amemwelekeza Mensah cha kufanya, kwa kuwa walikuwa wamejifichia sehemu moja. Kwenye moja ya mabegi waliyokuwa nayo, kulikuwa na zile nguo zao za mapambano, naye akamwambia Mensah avae moja haraka sana ili awashughulikie majasusi wale. Alijua mwanaume huyu alikuwa na shabaha nzuri sana, na kwa hapa aliyekuwa na bastola ni Victor pekee, hivyo akamwambia Victor amrushie bastola Mensah, na baada ya Victor kufanya hivyo, Torres akamwambia Mensah awalenge majasusi wale sehemu za miguu au mikono ili kuwaangusha chini, lakini ahakikishe haui yeyote kati yao. Mensah alikuwa anataka kuwaua wote kwa sababu alihisi hasira, lakini Torres akasisitiza afuate alichomwelekeza.
Baada ya Mensah kumaliza kuvaa nguo yote, majasusi wale walikuwa karibu zaidi na nguzo waliyojifichia Kendrick na Azra, ambao walijitahidi kujibana hapo kwa uangalifu, nao wakatoa onyo la mwisho kwamba ikiwa wasingetoka basi wangewaua wote. Lakini papo hapo Mensah akatokea mbele yao, akiwa amejiviringisha kutoka alipokuwa amejibanza na Torres, naye akaanza kufyatua risasi kwa ustadi sana. Majasusi walikuwa wameanza kumfyatulia na yeye pia, lakini zikawa zinadunda, huku za kwake Mensah zikiwapata mmoja baada ya mwingine na kuwaangusha chini.
Walibaki majasusi 7 kati ya 15 waliofanikiwa kujikinga kwenye magari, huku wenzao wakiwa chini wanajivuta-vuta huku wakisikilizia maumivu ya risasi zilizowapata miguuni na sehemu za mikono. Mensah akajiviringisha mpaka kwenye gari moja na kujibanza, akihisi kama kuna vitu vingi vya moto vikiuchoma mwili wake kutokana na kumiminiwa risasi nyingi, lakini hakuwa ameumizwa sana kutokana na nguo yake kumlinda.
Kutokea kwenye nguzo nyingine, LaKeisha akamuuliza Torres kwa kikabila cha Hausa ikiwa na wao wangepaswa kuvaa nguo zao za mapambano, lakini Torres akasema muda usingetosha, na majasusi hao bila shaka walikuwa wanapanga kufanya jambo fulani kwa ukimya huo waliouweka. Mensah akasema risasi za kwenye bastola yake zingeisha haraka, hivyo labda kuvaa nguo zao kungesaidia. Lakini vipi kuhusu Kendrick na Azra, ambao hawakuwa na nguo za aina hiyo hapo? Victor pia alikuwa amedondosha begi lake mbali na alipokuwa, hivyo na yeye asingeweza kuweka kitu mwilini cha kumlinda.
Majasusi wale walikuwa wanafanya mpango wa kuwazunguka taratibu, naye Kendrick akasema kama Mensah angeweza, basi asogee mpaka pale ambapo majasusi wale walioumia walidondoshea bunduki zao na kuzichukua ili kuwapa wenzake. Mensah akachungulia kidogo, na hapo hapo risasi zikafyatuliwa upande wake na kufanya ajikinge tena, na hivyo akamwambia Kendrick haingekuwa rahisi sana kwa sababu nguo yake isingeweza kustahimili nguvu kubwa ya risasi za majasusi hao kwa muda mrefu.
Azra alipochungulia kidogo, akaona kweli majasusi hao waliobaki walikuwa wanazunguka kwa mtindo wenye ustadi, na sasa walikuwa wakikaribia sehemu aliyojikalisha Victor. Akataka sana kumwonya, lakini hiyo ingemhatarisha zaidi yeye na Kendrick kwa sababu majasusi wangeona walipokuwa wamejibanza, naye akashindwa kujua afanye nini ili kumsaidia mwanaume huyo.
Jasusi mmoja alikuwa akisema kwamba hakukuwa na haja ya kujificha tena, kwa kuwa walikuwa na mabomu, hivyo wajitokeze kabla ya wao kuwarushia. Torres alijua hiyo kuwa njia yao ya kuwalaghai tu, kwa sababu kama wangekuwa na mabomu hapo wangekuwa wameyarusha, ila wasingeweza kwa sababu na wao yangewaua.
Wakati mchezo huu mdogo wa "nasaka mke wangu" ulipokuwa ukiendelea, Kendrick na wengine wakashtushwa baada ya kusikia sauti za vishindo na mayowe ya kadiri kutoka kwa baadhi ya majasusi wale. Wakaanza kusikia na sauti za risasi, lakini hazikupigwa kuelekea upande wao, bali ule walikotokea majasusi wale. Mensah alipochungulia, akamwona mtu akiwa anawachanganya majasusi hao, na kwa haraka akatambua ilikuwa ni Lexi baada ya kuona nguo alizovaa kuwa kama zao za mapambano. Torres akauliza ni nini kinaendelea, naye Mensah akawafahamisha wote kwamba ilikuwa ni Lexi.
Kusikia hivyo, Azra akanyanyuka na upesi kujibinua sarakasi nyingi mpaka karibu kabisa na Victor, naye akamvuta na kuangukia naye pambeni, kwa sababu ni wakati huo huo tayari jasusi yule alikuwa amefika usawa wake na kuanza kufyatua risasi, hivyo akawa amesaidia Victor asipigwe. Mensah akamwona jasusi huyo na kumpiga risasi kifuani, naye akaanguka chini.
"Shit!"
Neno hilo lilimtoka Mensah baada ya kutambua kwamba alitenda kwa uharaka lakini akawa amesababisha kifo. Kendrick, LaKeisha na Torres walichungulia pia na kumwona Lexi akijitahidi kuwashughulikia majasusi wengine waliobaki, naye Mensah akajisogeza sehemu nzuri ili kuwalenga miguuni wanaume hao. Walikuwa wanammiminia Lexi risasi mwilini kila alipotoka kwa mmoja na kumfata mwingine, na nguo yake pia ikawa inapungukiwa na uwezo wa kuzizuia risasi zile.
Mensah aliwalenga vizuri majasusi hao walipokuwa wamekengeushwa na Lexi, naye akawatandika risasi miguuni na kuwafanya waanguke chini huku wakiugulia maumivu. Upesi Mess Makers wakawafata wote na kuwanyang'anya bunduki zao, maana bado kuna wengine walikuwa wakijitahidi kuonyesha uimara kwa kufyatua risasi ingawa nao walikuwa wamejeruhiwa kwa risasi. Mensah alikuwa amewatandika risasi kwa ufundi ambao ungewafanya wasinyanyuke, lakini wasingekufa.
Walipokaribiana, Torres akamuuliza Lexi ilikuwa vipi mpaka watu hawa wakajua utambulisho wao, naye Lexi akawaonya wote kuwa wangepaswa kuondoka haraka sana kwa sababu wengine walikuwa wanakuja kuwakamata. Kabla hawajafikiria kufata magari, hapo hapo tena yakaingia magari mawili ya maaskari wengine wakija upande wao kwa kasi. Lexi akawaambia wenzake waondoke haraka sana, na yeye angejaribu kuwazubaisha maaskari hao ili wenzake waponyoke. Kendrick akawa anakataa, akisema walipaswa kuondoka kwa pamoja, lakini Lexi akalazimisha na kumwambia angetoka akiwa salama, hivyo watangulie na yeye angefata. Akafanya kama kuwaamuru kabisa, nao wakaanza kuelekea kwenye gari ambalo halikuwa lao, kwa sababu ya kwao yalikuwa yameharibiwa kwa kupigwa risasi.
Lexi akawageukia maaskari wale, wakiwa 8, waliokuwa wameshafika hapo na kushukia umbali mfupi wakiwa na mabunduki yao, na wakiwa wamewaona majasusi wale waliopigwa risasi, naye akaanza kuelekea upande wao huku akiwa amenyoosha mikono yake juu. Mmoja wao alikuwa anafoka kwa sauti akisema Lexi apige magoti na wengine walioingia kwenye gari watoke, lakini Lexi akaendelea tu kuwafata bila woga.
Mmoja wa maaskari hao akafyatua risasi mguuni kwa Lexi, lakini Lexi akaanza kukimbia kuwaelekea kwa kasi sana, huku akipindisha mwili wake huku na huko. Maaskari hao wakawa wanafyatua risasi zao ambazo hazikuwa na nguvu kali sana kama za bunduki walizotumia majasusi, naye Lexi akawafikia na kuanza kuwapiga kwa mitindo ya sarakasi nyingi.
Torres akawa amefanikiwa kuliwasha gari waliloingia, naye akaligeuza na kuanza kuelekea upande wa kutokea. Alipokaribia usawa ambao Lexi alikuwa akipambana na wale maaskari, alitaka kusimama hasa kwa sababu wengine walikuwa wanamwambia afanye hivyo ili wamsaidie Lexi na yeye aingie kwenye gari, lakini Lexi akatoa ishara kwamba wasisimame na waondoke haraka sana. Torres alihuzunika mno, lakini alikuwa anajua kile ambacho Lexi anafanya, yaani kuwatanguliza wao badala yake yeye.
Akapitiliza tu na kuwafanya LaKeisha na Mensah wabaki wakilalamika kwa nini alimsikiliza Lexi wakati alikuwa kwenye shida. Torres aliliondoa gari hapo kwa kasi sana, huku akisema Lexi alifanya hivyo kwa sababu alijua wakitoroka wao, hata kama yeye angekamatwa basi wangeweza kutafuta njia ya kumsaidia. Lakini Kendrick alijua ingekuwa ngumu kufanya hivyo sasa hivi kwa sababu tayari wengi wao walijulikana, hivyo ikaonekana ni kama wamemwacha Lexi peke yake kwenye shimo lenye simba wakali. Akafumba macho yake akihisi huzuni kuu moyoni, na gari lao likafanikiwa kutoka eneo hilo.
Lexi alijitahidi kupambana na maaskari hao waliokuwa watata sana, naye akafanikiwa kuwafanya wote wapoteze fahamu. Alihisi kuchoka na maumivu kiasi kwa sababu ijapokuwa nguo yake ilisaidia kuzuia risasi, zilikuwa zimedunda kwa njia iliyofanya ahisi kama mtu aliyepondwa na kokoto ndogo ndogo mwilini. Akawa anapumua kiuchovu, naye akaamua kuivuta "mask" yake na kuitupa pembeni, halafu angeelekea kwenye gari mojawapo kati ya yale waliyokuja nayo maaskari ili aondoke hapo.
Akaanza kulielekea moja, na ile tu alipoufikia mlango wa gari hilo, sauti aliyoifahamu vizuri sana ikamsemesha kwa nguvu.
"Tulia!"
Lexi akanyanyua macho yake na kukuta ni Nora, akiwa amesimama kutokea umbali mfupi mwanzoni kabisa kwenye mwingilio wa eneo hilo la maegesho. Alikuwa ameshika bastola huku ameilekeza kwa Lexi, naye akaanza kutembea polepole kumwelekea huku akiwa amekunja sura yake kuonyesha hasira. Akasimama baada ya mwendo huo mfupi, naye Lexi akaachia mlango wa gari na kubaki anamtazama kwa umakini.
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
WhatsApp +255 787 604 893
Mkuu shukran sana mambo yanazidi kuoamba moto[emoji4][emoji4][emoji4]FOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
"Hatimaye!" Nora akasema kwa njia yenye kejeli.
Lexi akaendelea tu kumtazama.
"Caught in the act. Ahah... nakuogopesha bado? Mbona inaonekana ni kama mimi ndiyo nayepaswa kuogopa? Mm? I mean... hao watu wote walio hapo chini wananifanya natetema kwenye mabuti yangu sasa hivi," Nora akasema.
"Nora..."
"SHUT UP!" Nora akafoka kwa nguvu.
Lexi akatulia tu. Pumzi za Nora zikaanza kuongezeka kasi. Alikuwa na hasira kali sana kwa kuhisi amesalitiwa.
"Sogea hapa," Nora akasema.
Lexi akaendelea kusimama tu.
"Nimesema sogea, sitaki mchezo, nitakupasua kichwa!" Nora akasema kwa ukali.
Lexi akatii. Hakuona haja tena ya kukimbia, na kiukweli ilikuwa ni kama hisia za maumivu za Nora zilimfanya ajutie sana, na hiyo ikamtia udhaifu. Akatembea taratibu mpaka sehemu hiyo iliyokuwa na uwazi kiasi, naye akasimama hapo huku Nora akiwa bado amemwelekezea bastola.
"Kwa hiyo... familia yako... iliyokuwa na matatizo mengi sana kwa hizo siku mbili... ndiyo Mess Makers?" Nora akauliza.
"Hautaweza kuelewa.... kuna mambo mengi...."
"No, sihitaji kuelewa chochote. Kila kitu kiko wazi. Wewe ni mwizi. Wewe ni muuaji. Wewe ni mwongo. Wewe ni mshenzi Lexi!" Nora akasema.
Lexi akabaki kumtazama.
"Hivi akili yangu ilikuwa wapi? Yaani... unajua kama ni tuzo, we mwanamke unastahili tuzo ya mwaka ya kuwa mshenzi bora kuliko washenzi wote waliowahi kuwepo. Akili yako imejaa uozo, na mimi... ukaniambukiza. Nijitetee kwamba nilikuwa sijui? Unajua siyo natural kabisa, labda uliniroga. Mimi kutoka tu na mwanamke haikuwahi kuingia akilini mwangu. Ulifanyaje? Uchawi wa 'Mess Makers,' si ndiyo? Unapata faida gani Lexi kwa kuumiza hawa watu wote? Kwa kuniumiza mimi? Mbona uko tofauti kabisa na kile ambacho sura yako inaonyesha? Kwa nini unafanya mambo yote haya? Eeh?" Nora akazungumza kwa hisia.
Lexi akadondosha chozi na kusema kwa mkazo, "Ni kwa sababu ya baba yako."
Nora akakunja uso wake kimaswali.
"Baba yangu amefanya nini?" akauliza.
"Ni yeye ndiye chanzo cha maisha yangu kuwa namna hii. Aliniibia aina ya maisha ambayo nilitaka kuwa nayo nikiwa bado mdogo... na ingawa najua hutaweza kunielewa leo, ipo siku utaelewa," Lexi akasema kwa hisia.
"Ahah... ahahahah... Unapenda maigizo sana. Lakini unajua... unastahili pongezi. Hakuna mtu ambaye amewahi kufanya mambo uliyofanya kwenye hii nchi, na hapo kiukweli lazima tu nikupe respect. Ila ukitegemea kwamba baada ya kila kitu ambacho umefanya kuna mtu ataamini upuuzi wowote unaoongea... dada yangu umefeli sana. Yaani wewe haufai. Wewe ni nyoka zaidi ya nyoka. Na unajua sikuzote mwisho wa nyoka ni kupondwa tu kichwa... na hicho ndiyo kitakachokupata wewe," Nora akasema.
"Basi unasubiri nini? Niponde," Lexi akasema.
"Nini?"
"Niponde kichwa sasa hivi!" Lexi akasema kwa sauti yenye ukali.
"Usinisemeshe hivyo Lexi, nitakupasua!" Nora akamwonya.
"Go ahead. Do it!" Lexi akamwambia na kuanza kumfata.
"Usinijaribu Lexi! Tulia hapo hapo ulipo...."
"Unafikiri mimi nilipenda kuwa na maisha ya namna hii? Unafikiri sikutaka kuja kuoa, kuwa na watoto, kuishi maisha mazuri ya familia? Nilitaka kuwa na vitu hivyo, lakini baba yako akaviiba kutoka kwangu!" Lexi akaongea kwa hasira.
"Acha kuongea upuuzi! You're nothing but a psychopath!" Nora akasema kwa ukali.
Lexi akasimama mbele ya bastola ya Nora na kusema, "Maybe I am. Na kila kitu ambacho nimefanya sijafanya kwa sababu za kibinafsi tu. Ndiyo kuna watu wameumia, lakini angalau sikuwaumiza kwa kudhamiria. Baba yako aliua watu zaidi ya 200, wazazi wangu included. Ungejua, ungekuwa unajua hata chembe ndogo ya mambo niliyopitia usingenihukumu hata kidogo," Lexi akaongea kwa mkazo.
Nora akawa anatikisa kichwa kukataa mambo aliyosikia.
"Haijalishi nimefanya nini. Sijutii. Na sitajali hata mbwa yeyote akisema nini. Na kwa sababu hiyo, ninakuomba ukipasue kichwa changu," Lexi akasema.
Nora akawa anapumua kwa hasira.
Lexi akasogea nyuma kidogo na kusema, "Do it."
Mikono ya Nora iliyoshikilia bastola ikaanza kushuka taratibu na kufanya batola hiyo ielekee kifuani kwa Lexi.
"Oh reminder, unajua hii ni proof, kwa hiyo usipige kifuani, nilenge kichwa ukipasue!" Lexi akasema kwa ukali.
Nora akaendelea kumtazama kwa hisia nyingi zilizovurugika, akihisi kusalitiwa, hasira, hatia, huzuni, na kuchanganywa sana na kila jambo. Alishindwa kuelewa ikiwa hicho ndani ya Lexi kilikuwa ni kiburi, au kuna jambo lingine lililokuwa nyuma ya pazia kubwa lililoficha siri nyingi kumhusu "mwanamke" huyo. Hasira aliyokuwa nayo ilimtaka ampasue kichwa ukweli, lakini kuna kitu kikawa kinamzuia.
Lexi alikuwa anamwangalia kwa njia fulani iliyoonyesha huzuni, akitambua ni jinsi gani mwanamke huyu alivyokuwa ameumizwa sana kujua ukweli kumhusu. Lakini alijua pia kwamba kwa jinsi mambo yalivyokuwa yamejitengeneza mpaka kufikia hatua hii, isingekuwa rahisi sana kumshawishi Nora kukubali kwamba upande aliotumikia ulikuwa mbaya sana, kwa hiyo kama angeamua kumuua, basi alikuwa tayari kwa hilo.
Wakiwa bado wanaangaliana huku Nora akiwa bado ameielekeza bastola yake kwa Lexi, gari mbili ngumu sana za kijeshi zikaingia eneo hilo walilosimama kwa kuvunja kuta za pembeni zilizozunguka jengo hilo kubwa. Wote walibaki kuzitazama tu mpaka ziliposimama usawa wao, kisha kwenye gari la kwanza wakashuka wanaume wawili na mwanamke mmoja, waliovalia nguo za kijeshi huku wakiwa wameelekeza bunduki kwa Lexi na Nora na kuanza kuwafafa. Hao walikuwa ni Tariq, Rachel na Zachary. Nora akawatambua haraka wale walioanza kushuka kwenye gari la pili, nao walikuwa ni Alex, Mario, Hussein na mwanaume wa kazi, Luteni Michael mwenyewe.
Nora akashusha mikono yake iliyomwelekezea Lexi bastola, ambaye alikuwa amesimama kwa utulivu tu huku anamwangalia Nora machoni kwa hisia. Luteni Michael akawa anawaelekea huku amekaza sura yake kwa hasira.
"Nilichosema Nora, na wewe ukajifanya unajua sana kusoma mioyo. Nini hiki sasa? Rafiki yako ndiye msaliti," Luteni Michael akawa anaongea.
Nora akabaki kumtazama tu. Wanajeshi wa Luteni Michael wakawa wamewazingira Lexi na Nora huku wamewaelekezea bunduki mpaka Luteni alipofika karibu zaidi.
"Unapaswa ujue njia za mwovu sikuzote ni fupi malaya wewe. Umefanya wengine watoroke ndiyo, lakini nitahakikisha unapanua mdomo kusema wako wapi kama unavyowatanulia hiyo shombo yako!" Luteni Michael akamtolea maneno makali Lexi.
Lexi akabaki kimya tu. Hakuwa na njia nyingine ya kutoroka hili. Luteni Michael akamsogelea karibu zaidi akimwangalia kwa hasira. Baadhi ya majasusi wale waliokuwa wameumizwa kwa risasi wakawa wanawaambia wawapatie msaada, naye Alex, Rachel, pamoja na Zachary wakawafata ili kuwapa huduma na kuita magari ya hospitali ya dharura.
"Ahah... Mario, Hussein, bado mnamwona huyu kuwa rafiki mtakatifu na wa kawaida tu wa ACP? Angalieni hao jamaa wote hapo chini, mwanamke ndala ndefu kweli kweli! Tukikutoa hapa mpumbavu wewe na kukupeleka sehemu nyingine, jua kwamba utaumia sana. Kwa hiyo ni bora useme washenzi wenzio walipo malaya mkubwa wewe!"
Luteni akaendelea kutoa kashifa, lakini Lexi akabaki kimya tu.
"Mhm... nisingetarajia lolote la maana kutoka kwa mtu kama wewe. Toka mara ya kwanza nilipokuona nilijua tu wewe ni mfano halisi wa Shetani. Unatia sana kinyaa. Tundu la mama yako ni lazima liwe linajuta kukuleta kwenye hii dunia..."
Wee! Hapo Luteni Michael akawa amegusa pabaya. Lexi akamtazama kwa hisia kali sana. Maneno yake mengine yote kumhusu angeweza kuyapuuzia, lakini baada ya kumkashifu na mama yake, alishikwa na hasira kali kupita maelezo.
"Na itakuwa wazi zaidi baa...."
Kabla Luteni Michael hajamaliza kuongea, Lexi alimtandika ngumi mbili za haraka na nzito sana usoni kwake, kisha akaivuta nyingine ya nguvu sana huku akiruka na kumtandika usoni tena. Wanajeshi wake wakaanza kumfuata Lexi, lakini Luteni Michael akawazuia baada ya kurudi nyuma kidogo. Akawaambia watulie ili ashughulike naye yeye mwenyewe. Kisha akaanza kumfata na kujaribu kumshika, lakini Lexi akaipiga pembeni mikono yake kwa nguvu na kumwasha kofi usoni! Wengine wakabaki kuwaangalia kwa mshangao kiasi.
Luteni Michael akakasirika na kumrushia ngumi, lakini Lexi akakwepa na wakati huo huo kumpiga tumboni na chini ya kidevu kwa kasi sana. Muda si muda, wawili hawa wakawa wanapigana. Walipigana kama wanaume, ijapokuwa Lexi alionekana kuwa mdogo sana kwa Luteni Michael hasa kutokana na mwili wake kuwa wa mwanamke. Nora alikuwa anawaambia kwa sauti ya juu waache, lakini wakaendelea kutandikana sana. Luteni Michael alikuwa anashangaa kiasi kuona jinsi ambavyo Lexi alimsumbua sana, hata alipompiga ngumi zake nzito, "mwanamke" huyu alikuwa na kiwango cha juu sana cha kustahimili maumivu na kuendelea kupambana naye bila woga wowote.
Pamoja na Luteni Michael kuwa na mwili mkubwa na uliokomaa sana, Lexi hakuwa nyuma kujibu mapigo yake. Alitumia mtindo wa kupigana kama bondia fulani hivi, na sasa akaonekana akivuja damu puani na pembezoni mwa jicho lake, huku Michael akiwa na vimbe (nundu) kadhaa usoni kwa sababu ya ngumi za haraka za Lexi. Wakaangushana chini wakiwa wanaendelea kutandikana haswa, na kufikia hapa walikuwa wamesogea usawa ule wa kuta zilizobomolewa magari yale mawili yalipoingia hapo.
Luteni Michael akaja juu ya Lexi na kuanza kushusha ngumi nzito akilenga uso wake, lakini Lexi akawa anauziba, kisha kwa akili akamgeuza na yeye ili awe chini, naye akawa anampiga ngumi za tumbo Michael huku jamaa akimkaba kwa mkono wake mmoja usawa wa ubavu wake. Lexi hakukata tamaa. Maneno yale ya Luteni Michael yalifanya kumbukumbu za mama yake zimrudie, jinsi alivyouliwa usiku ule mbele yake. Hangeweza kuvumilia mtu yeyote ambaye angesema jambo baya kumhusu.
Nora alikuwa anapiga sana kelele kumwambia Luteni Michael aache kupigana na mwanamke, huku Mario na Hussein wakimshikilia kwa nguvu ili asijiingize pale, na wao wakitazama pambano hilo zito. Luteni Michael akafanikiwa kumsukuma Lexi pembeni, kisha akaokota jiwe la tofali moja lililobomoka chini hapo na kumrukia nalo akitaka kumpiga, lakini Lexi akakwepa kwa kujiviringisha akiwa amelala chini bado. Kwa mtindo wa sarakasi, Lexi akajinyanyua kwa kuizungusha miguu hewani na kufanikiwa kumtandika usoni kwa mguu mmoja, naye Luteni Michael alipoweweseka kidogo, Lexi akausawazisha mwili wake na kumpiga miguuni, jambo lililofanya Michael aanguke na kubamiza kichwa chake chini kwa nguvu.
Maumivu yaliyompata wakati huu yalikuwa makali, na kwa sekunde chache akashindwa kujinyanyua baada ya pigo hilo, na hapo hapo Lexi akamfuata chini na kuendelea kumtandika ngumi za usoni. Alikuwa anampiga huku analia kwa hasira nyingi, huku Luteni Michael akijaribu kuficha uso wake na kumdhibiti kwa wakati ule ule, lakini bado Lexi akaendelea tu. Jambo hili liliwashangaza hata wanajeshi wa Luteni Michael kwa sababu ilionekana ni kama Lexi amemzidi nguvu mwanaume huyo.
Kwa hasira alizokuwa nazo, Lexi akachukua jiwe zito la tofali lililokuwa pembeni kidogo na kulinyanyua juu ili amponde nalo kichwani, na ile Tariq alipotaka kuwahi ili amzuie, Lexi akafanikiwa kulishusha kwa nguvu na kuponda! Wote walishangaa sana na kubaki wametazama tu chini hapo, na Tariq akasimama akimwangalia Lexi kwa makini. Wanajeshi wote walikuwa wanaangaliana wasiamini kama kweli Luteni wao mwenye mafunzo na uwezo mkubwa alikuwa ameshindwa kwenye pambano hilo na "mwanamke."
Lexi akawa anapumua kwa nguvu na kwa kasi sana, huku jasho na damu vikimtoka usoni. Akajitoa juu ya Luteni Michael taratibu na kukaa pembeni, akipumua kwa uchovu huku anamwangalia Luteni huyo. Luteni Michael akaangalia tofali hilo taratibu, ambalo Lexi alikuwa ameponda pembeni kidogo tu na kichwa chake, na siyo yeye. Lexi akageuza shingo yake taratibu na kumtazama Nora usoni kwa hisia, akihisi maumivu mengi mwilini mwake, naye Nora akashindwa kujizuia kumwangalia kwa huruma.
Mario na Hussein wakamwachia Nora na kwenda kumsaidia Luteni Michael asimame, naye Tariq pamoja na Alex wakamnyanyua Lexi na kumfunga pingu mikononi. Luteni Michael alikuwa anamtazama Lexi kimaswali sana. "Mwanamke" huyo angeweza kumuua kama alitaka, lakini hakufanya hivyo. Hakujua lengo lake lilikuwa nini, au alijaribu kuthibitisha nini, lakini hiyo haikuwa sababu ya kumwona kuwa mtu mzuri. Bado alimchukia sana kwa sababu ya mambo mengi yeye na watu wake waliyofanya.
Luteni Michael akawaamuru wanajeshi wake wampeleke Lexi ndani ya gari, nao wakatii na kumpeleka upesi. Bado Nora alikuwa amesimama hapo tu kama mtu aliyeghafilika sana, hivyo Luteni Michael akamfata na kumwambia walipaswa kuondoka haraka. Akamwongoza mpaka kwenye gari lake (Nora) na kuingia pamoja naye, kisha akamwomba yeye ndiyo aendeshe, nao wakaondoka kutoka kwenye jengo hilo. Tariq, Alex, Mario na Hussein ndiyo ambao waliongoza gari lililombeba Lexi, wakiwaacha Rachel na Zachary pamoja na majasusi wale walioumizwa ili kuangalia mahitaji yao mpaka msaada ukifika.
Jengo hilo la kampuni ya Kendrick lilikuwa limegeuka kuwa kama uwanja mdogo wa vita kwa usiku huo. Mambo yaliharibika sana. Mtu muhimu zaidi wa kundi la Mess Makers alikuwa amekamatwa, na hii ilikuwa ni pigo kubwa kwa wale waliobaki. Lexi alikuwa akimuwaza sana Azra. Alikuwa tu ametoka kumwahidi kwamba hangeruhusu jambo lingine liwatenganishe, lakini sasa akawa mbali naye tena. Mara nyingi hisia huongoza watu kuchukua maamuzi mabaya, na kila mara alipofikiria jinsi alivyohatarisha uhai wake kwa sababu ya hisia zake, akajiona mbinafsi sana kwa kuwa ni kama alimsahau Azra. Sasa isingekuwa rahisi kutoka mikononi mwa wabaya wao, na hapa alijua kilichokuwa kikimsubiri huko mbele ni kifo tu.
Kulikuwa na ukimya sana baina ya Luteni Michael na ACP Nora kwenye safari hii ya kumpeleka Lexi akiwa mfungwa rasmi. Luteni Michael alimjulisha Kanali Oswald Deule kwamba alikuwa amemkamata mtu aliyeamini kuwa kitovu kikubwa cha kundi la Mess Makers, na sasa walikuwa njiani kumpeleka kwenye sehemu yao ili kumfunga. Lakini Kanali akamwambia wampeleke kwenye jengo lile maalumu la usalama wa taifa ili wakamhoji huko, akisema kwamba yeye alikuwa huko pamoja na viongozi wengine pia.
Luteni Michael akatii, na safari ya kuelekea huko ikaendelea.
★★★★
Baada ya kumfikisha Lexi huko, Luteni Michael na ACP Nora walikwenda pamoja naye mpaka sehemu za ndani za jengo hilo, na kadiri walivyozidi kuingia ndani ndivyo wanajeshi kadhaa walivyoongezeka ili kuwasindikiza. Walipofika sehemu fulani za ndani zenye korido kadhaa zilizoachana, Lexi akapelekwa upande mwingine, nao wakina Luteni na ACP wakaelekea ule mwingine. Lexi alikuwa akipelekwa sehemu yenye chumba maalumu cha mahojiano, na wengine wakaelekea kwenye ofisi ambayo viongozi wale wengine walikuwepo.
Walipofika kwenye ofisi hizo, Luteni Michael na ACP Nora waliwakuta viongozi wawili wa jeshi la nchi; Kanali Oswald Deule pamoja na Kapteni Erasto Shimuye, na viongozi wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP) Donald Ngassa na Kamishna wa Polisi (CP) Patrick Msuwa. Luteni Michael na ACP Nora wakawapa wote salamu za heshima, kisha wakaanza kuwaelezea yale yote yaliyotokea. Muda ulikuwa umesonga sana, ikiwa inakaribia saa 7 usiku sasa, lakini hakuna yeyote hapo aliyewaza kuhusu usingizi.
Nora alilaumiwa sana kwa sababu ya kuamini mtu ambaye alikuwa ni adui, na hivyo kusababisha siri za mipango yao mingi kuwa wazi kwa watu hao waliowaona kuwa wabaya. Mambo mengi yakasemwa kuhusu mipango yao kuharibika na ikaonekana kwamba Nora alikuwa amechangia sana kuleta matatizo hayo. Mwanamke huyu alibaki kimya tu akipokea lawama hizo, na kiukweli hakukazia sana fikira walichosema kwa kuwa akili yake ilikuwa ikitafakari yale yote yaliyotokea, na ambayo Lexi alimwambia kwenye jengo lile.
★
Lexi akawa ameketi kwenye kiti mbele ya meza fupi, akisubirishwa mahojiano kati yake na mtu ambaye angehusika. Alifahamu vizuri hatua na taratibu hizi, hivyo akawa ametulia tu huku mikono yake ikiwa juu ya meza ikifungwa kwa pingu. Nguo zake maalum za mapambano zilikuwa zimeondolewa mwilini mwake, hivyo sasa alikuwa amebaki na T-shirt nyeusi yenye mikono mirefu na suruali nyeusi pia; za mtindo wa aina moja.
Kuna mwanamke fulani akaingia ambaye alikuwa amevalia nguo za kijeshi pia, naye akaanza kuusafisha uso wa Lexi uliokuwa umechafuliwa kwa damu na uvimbe mdogo sehemu kadhaa. Lexi alitulia tu, akiliona jambo hili kama kejeli ya aina fulani ambayo watu hawa walikuwa wakimfanyia, na baada ya mwanamke huyo kumwekea plasta chache usoni, akatoka ndani hapo.
Chumba hiki kilikuwa kidogo, chenye mwanga hafifu wa taa iliyomulika kutokea juu ya ukuta katikati, nacho hakikuwa na kitu kingine chochote zaidi ya meza hiyo, viti viwili, na Lexi pekee. Kutokea juu ya ukuta mmoja kulikuwa na kitu kama kioo kipana, ambacho Lexi angeweza kujiona kila wakati alipokiangalia. Nje ya chumba hicho walikuwepo wanajeshi kadhaa waliolinda sehemu hiyo.
★
Luteni Michael, Kapteni Erasto, Kanali Oswald, IGP Donald, CP Patrick, na ACP Nora walitoka kwenye ofisi za kule walikokuwa na kuja upande wa pili wa chumba hicho ambacho Lexi alikuwa amewekwa. Walikuwa bado wakijadili kuhusiana na kukamatwa kwake baada ya kufahamika kuwa alikuwa mmoja wa kundi la Mess Makers, na ni hatua zipi zichukuliwe dhidi yake kwa sababu ya kundi hilo kusababisha hasara nyingi kitaifa.
Kanali Oswald Deule, akiwa ndiyo mwenye cheo kikubwa zaidi kwa waliokuwa hapo, alipendekeza kwamba baada ya kufanya jitihada zote za kuhakikisha Lexi anatoboa siri zote za kundi lao, walipaswa kumpa mateso makali sana ili iwe somo na fundisho kwa wengine. Ijapokuwa lilikuwa ni jambo lililokubaliwa na wengine, halikumpendeza Nora hata kidogo. Akawaambia kwamba hakukuwa na haja ya kumuumiza mwanamke huyu kwa sababu haingesaidia lolote; kwamba walikuwa wameshamkamata, hivyo kama ni kumtumia ili kuwapata wengine, na hasa Kendrick Jabari, basi ingetosha, na njia inayofaa zaidi ya kumwadhibu ni kifungo.
Lakini pendekezo lake lilipuuzwa, naye Kanali Oswald akamwambia Luteni Michael kuwa ikiwa baada ya Kapteni Erasto kumhoji Lexi na mwanamke huyo asiseme lolote, basi amfunge kwenye chumba chenye giza na kupeleka wanajeshi wampe mateso mpaka aseme kila kitu; lakini wahakikishe hafi. Alijua fika kwamba Lexi alikuwa mtu imara sana, hasa baada ya kuambiwa mambo aliyoyafanya kwa wale majasusi na maaskari muda mfupi nyuma, hivyo akamsihi sana Luteni Michael atumie njia mbadala kila wakati ili kuweza kumvunja (kiakili) na kumfanya amwage mtama.
Nora akaomba yeye ndiye awe wa kumhoji Lexi kwa kuwa kwa kipindi fulani alikuwa pamoja naye sana hivyo alijua jinsi ya kuzungumza naye kwa njia ambayo ingemfanya afunguke kwa mambo mengi, lakini Kanali Oswald akapinga hilo na kumwambia kwamba wakumhoji angekuwa ni Kapteni Erasto na si mwingine. Luteni Michael alimwangalia Nora kwa umakini, akijua kabisa kwamba mwanamke huyu alikuwa akiumia kihisia kwa sababu mtu aliyemwamini alikuwa ndiye mtu aliyemsaliti kwa muda mrefu sana. Alimwonea huruma kwa kiasi fulani, lakini alitaka pia amwonyeshe ni jinsi gani alikuwa amekosea sana kumwamini mtu kama Lexi. Na sasa alikuwa akijionea.
Baada ya hapo, Kapteni Erasto akatoka walipokuwa na kuingia kwenye chumba kile alichokuwepo Lexi. Kilikuwa kimejengwa kwa chini kutokea walipokuwa wengine, hivyo wao waliweza kuwaona kupitia kioo kile kipana, lakini ambacho kama ungekuwa kwa ndani usingeweza kuona nje. Yaani, Lexi na Kapteni Erasto wakiwa ndani ya kile chumba wasingeweza kuwaona wakina Kanali, Luteni, IGP, CP na ACP Nora kwa kule juu, lakini hawa wangeweza kuwaona. Kulikuwa na vifaa vidogo vya sauti vilivyounganishwa kutokea kwenye chumba kile, hivyo wakina Nora wangeweza kusikia maongezi yao. Jeshi lilikuwa kimaendeleo zaidi!
Kapteni Erasto akaketi kiti cha pili na kutazamana na Lexi machoni. Alimwangalia kwa njia ya kawaida tu, naye Lexi alikuwa akimtazama kwa njia ambayo haikuonyesha hisia yoyote kabisa; yaani hakuogopa hata kidogo, bali alikuwa ametulia kabisa huku uso wake ulioumia ukionekana kuwa na damu zilizokauka kwa mbali baada ya "kusafishwa." Kapteni Erasto akatabasamu kikejeli, kisha akaweka mikono yake juu ya meza na kufanya kama anasogeza uso wake kumwelekea ili amtazame vizuri zaidi.
"Mambo vipi?" akamuuliza.
Lexi akabaki kimya tu.
"Sihitaji kujitambulisha maana unafahamu mambo mengi sana, kwa hiyo nitachukulia na mimi unanifahamu. Inawezekana hadi unajua mlango wa nyumba yangu una rangi gani," Kapteni akasema.
"Nyeupe," Lexi akajibu.
"Ahahahah... wewe una... unajua kila kitu eti? Ni mfano halisi wa mfano wa Mungu au siyo?" Kapteni Erasto akauliza.
Lexi akakaa kimya.
"Tusijizungushe sana. Nafikiri unajua jinsi hii inavyokwenda. Nataka uniambie kila kitu kuhusu operesheni zenu, na baada ya hapo, labda hata tunaweza kulegeza kifungo utakachopewa. Unaonaje binti?" Kapteni akasema.
Lexi akabaki tu kimya, akimwangalia kama vile hajaelewa chochote kilichosemwa.
"Ngoja nikuulize kitu. Unampenda Raisi wetu?" Kapteni akauliza.
Lexi akabaki kimya tu.
"Mm? Unampenda? Humpendi? Kwa nini haumpendi?"
Kimya.
"Wewe na wenzako kuiba mabilioni ya pesa inaonyesha hamna upendo wowote kwa hii nchi, na kwa Raisi wetu. Lakini watu wote wanampenda Raisi. He's great! Nyie mna shida gani? Eeh? Kama usipompenda Raisi, utampenda nani sasa?"
"Masanja Mkandamizaji anatosha," Lexi akajibu.
"Ahahahah... kwa nini unampenda Masanja Mkandamizaji?"
"Kwa sababu mama yangu alimpenda, baba yangu alimpenda... na dada yangu alimpenda," Lexi akasema kwa hisia.
"Hiyo ndiyo sababu? Kwa hiyo kama mama yako angekuwa mpumbavu, baba yako angekuwa mshenzi, na dada yako angekuwa mjinga, wewe ingekuwa vipi?" Kapteni Erasto akauliza kwa dharau.
"Basi ndiyo ningempenda Raisi," Lexi akajibu kwa uhakika.
Kanali Oswald, akiwa kwenye upande wa pili wa chumba hiki, hakuweza kujizuia kutabasamu kidogo kutokana na jinsi Lexi alivyoonyesha ujasiri mwingi. Nora alikuwa akisikiliza huku wasiwasi mwingi ukimvaa kwa sababu alijua mambo haya yote yangeishia wapi.
"Okay. Siyo wote wanaompenda Raisi, lakini siyo lazima kumpenda mtu ili kuthamini mambo aliyokufanyia. Na Raisi wetu amefanya mambo mengi kwa ajili ya nchi hii. Wewe na wenzako mmeweza kuiba moja kati ya mambo ambayo yangesaidia kupanua mafanikio hata zaidi..."
"Na ufisadi pamoja na umwagaji wa damu kwa kwenda mbele..." Lexi akamkatisha.
"Una uhakika gani na hayo unayosema? Mm?"
Lexi akatazama pembeni.
"Hauvunjiki kirahisi eti? Mtu unaonekana kuwa mwenye akili timamu... eti unaenda kuiba mia mbili benki na wahuni wenzako wa majalalani! Akili yako ina akili? Naelewa kwamba baba yako alichomwa moto kama muhindi, lakini hayo siyo makosa yetu...."
Lexi akakaza ngumi kwa kuhisi hasira sana.
"Halafu nasikia eti umepigana hadi na Luteni... ahahahah... haki ya Mungu. Ngoja nikwambie kitu. Kuna kipindi fulani, watu fulani, walifikiri kwamba wanaweza kubadili mambo fulani kwa sababu tu wana vifaa fulani mikononi mwao. Matumaini ya kwamba... wangekuwa huru, au wangepata vyeo vikubwa, ama mshahara mnono zaidi, yakawafanya watumie vifaa hivyo kuanzisha uasi. Walifanikiwa kwa kiasi fulani, lakini hawakujua ni nini maana ya ushindi. Ushindi... ulikuwa ni dhidi yao. Nafikiri unajua naongelea nini, hasa kama utakuwa ulisoma historia ya nchi. Watu kama hao, ndiyo kama nyie. Mnafikiri kwamba kwa sababu mmeweza kunyakua na kukimbia umbali fulani, basi mtaweza kujificha. Uko mbele yangu sasa kuthibitisha kwamba hilo haliwezekani hata kidogo. Ahahahah... unahisije? Bado unajiona kuwa mshindi?" Kapteni Erasto akaongea kwa njia yenye dharau.
Lexi akatabasamu kidogo, kisha akasema, "Nilifikiri ulisema hautajizungusha sana... lakini una mdomo mrefu malaya tupa kule."
"Wisecracking, hilo nalifahamu kukuhusu. Nataka uniambie... Kendrick Jabari yuko wapi, na operesheni zake zote ziko maeneo yapi?"
"Unanionaje, me ni GPS?" Lexi akauliza kikejeli pia.
"Binti ni bora useme wakati ninakuomba kistaarabu, la sivyo... aagh unajua kitakachotokea. Sema tu haujui ni jinsi gani kitakavyotokea. SEMA!" Kapteni Erasto akafoka.
Lexi akawa anamtazama tu bila wasiwasi.
"Nikinyanyuka kutoka hapa, nikaenda nje, jua kwamba hiyo ndiyo tiketi yako ya mwisho ya maongezi ya kistaarabu. Kitakachofuata... ni bora uongee sasa hivi. Itaku-save maumivu mengi. Najaribu kukusaidia kwa kuwa una akili, lakini unapaswa tu kuitumia vizuri. Kwa mara ya mwisho, niambie Kendrick Jabari yuko wapi... na operesheni zake zote zilizobaki ziko wapi?" akauliza tena.
Lexi akawa ameangalia upande wa kioo kile. Ni kama alikuwa akimwangalia mtu pale, na ijapokuwa hakuweza kuona yeyote, upande wa pili Nora aliweza kumwona vizuri sana, na ilikuwa ni kama wanatazamana kwa hisia mno. Baada ya Kapteni Erasto kuona Lexi havunjiki kiurahisi, akatikisa kichwa taratibu, kisha akanyanyuka na kuondoka hapo. Alirudi upande wa pili wa chumba hicho na kusema kilichobaki tu hapo ni kumpatia mateso makali sana mpaka aseme ukweli wote; na si vinginevyo.
Kanali Oswald Deule akawaambia watatu hawa wa Jeshi la Polisi, yaani IGP Donald, CP Patrick, na ACP Nora, kwamba sasa kwa kuwa walimshika Lexi, mambo ambayo yangefuata katika kushughulika naye ingekuwa ni masuala ya kijeshi, kwa hiyo kwa kuwa kila kitu kingekuwa chini ya mikono yao basi walipaswa tu kuondoka na kumwacha hapo ili washughulike naye wenyewe. IGP Donald Ngassa na CP Patrick Msuwa hawakuwa na neno, lakini bado ACP Nora alitaka kujua ni aina gani ya mateso waliyotaka kumpa, na kwa nini walisisitizia sana jambo hilo.
Kwa njia yenye kejeli, Kanali Oswald akamwambia Nora kwamba hiyo ndiyo njia ya baba yake ya kufanya mambo kama alikuwa hajui, kwa hiyo alipaswa kuacha kuuliza-uliza maswali na kufata kile alichoambiwa. Kihalisi, Kanali Oswald alikuwa na nia nyingine, na hili ni jambo ambalo Nora aliweza kuhisi. Wakuu hawa wa jeshi wakawaambia wakuu hawa wa polisi waondoke sasa, nao wakatii na kutoka ndani ya chumba hicho, wakiwaacha wawili humo. Luteni Michael hakuwepo ndani ya chumba hicho wakati huo.
Baada ya watatu hao kuwa wametoka ndani ya chumba hicho, Nora akasema alihitaji kuelekea choo kwa ajili ya haja, hivyo wenyewe watangulie tu naye angewakuta huko nje ya jengo. IGP Donald na CP Patrick wakatangulia, huku Nora akijifanya kuelekea upande mwingine, lakini alipoona wameishia, akarudi tena usawa wa chumba kile walichotoka na kusimama karibu hapo. Akaanza kusikiliza maongezi ya Kanali Oswald na Kapteni Erasto ndani humo huku akijifanya amesimama tu hapo akisubiria mtu fulani.
"Lakini bado hawajaipata, kwa hiyo nafikiri kumuua itakuwa kazi bure tu..." Kapteni Erasto akasikika.
"Na hata sidhani kama kumtesa itasaidia maana huyu binti ni mtata sana, anaweza kuwa tayari kufa kwa ajili ya Jabari lakini siyo kum-snitch," akasema Kanali Oswald.
"Kwa nini unasema hivyo?"
"Fikiria alikuwa tayari kujitoa ili Jabari akimbie. Anajiamini sana..."
"Kanali... kuna aina za mateso ambazo ni lazima akizipitia atasema tu kila kitu..."
"Mambo siyo rahisi kama unavyofikiria. General alikuwa anamtaka sana aliposikia tu jina lake kwa mara ya kwanza na kuagiza atafutwe upesi na kupelekwa kwake; mzima au akiwa amekufa. Hiyo inakwambia nini? Siyo Jabari tu ndiyo dili kubwa hapa, ni huyu msichana. Kuna mambo mengi anayojua ambayo General anataka kuhakikisha hayafiki mbali. Huyu na kundi lao wamefanya mengi kumzingua Raisi na General. Kwa nini? Kila jambo linafanya nitake sana kuelewa mambo yote yaliyofichwa... lakini kuna vizuizi vingi sana," Kanali Oswald akasema.
"Sasa... kama ni hivyo, kwa nini umewaambia wengine kuwa atapitia mateso mpaka aseme ukweli ikiwa hiyo siyo...."
"Nimewaambia walichohitaji kusikia. Unapaswa ufikirie mbali Erasto. Fikiria kwa kina ni nini tutapata tukimpeleka huyu malaya akiwa hai kwa General. Nafikiri anamhitaji zaidi akiwa hai kuliko akiwa amekufa, ili labda afurahie zaidi kumuua yeye mwenyewe. Nataka sisi ndiyo tuwe wa kwanza kumpeleka, na ninajua tunaweza kupata faida kubwa sana," akasema Kanali Oswald.
"Oooh... okay... sasa ninaelewa. Kuna siri imejificha hapa kati, na huyu demu anaijua. Ikiwa tuta... tutampeleka kwa General akiwa hai na kusema atuingize kwenye mipango yao, basi na sisi tutafurahia mambo mengi kama Weisiko tu sivyo?" Kapteni Erasto akauliza.
"Angalau umenipata! Hahahah..." Kanali Oswald akasema.
"Kwa hiyo tunamtoa hapa muda siyo mrefu?" Kapteni Erasto akauliza.
"Ndiyo. Nimeshafanya mipango. Anapelekwa sehemu nyingine kwanza," Kanali Oswald akaongea.
Nora, bado akiwa nje mlangoni hapo, alisikia vizuri sana yale waliyosema. Sasa mambo mengi hata zaidi yaliendelea kumchanganya.
"Nora, vipi?"
Akashtushwa na sauti ya Luteni Michael akiuliza hivyo, ambaye alikuwa amefika hapo bila yeye kutarajia na kumfanya ajiulize ikiwa alitambua kwamba alikuwa anasikiliza maongezi ya viongozi wale. Kanali Oswald na Kapteni Erasto nao pia wakawa wamemsikia Michael kutokea mlangoni kule, naye Erasto akaanza kwenda kuona nini kilikuwa kinaendelea.
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893
Ndio uhalisia huo Mkuu. Oi Mkuu Elton Tonny shukrani na unajua aisee hauandiki simulizi kufuata matakwa ya msomajiHili la kukamatwa kwa Lexi siungi mkono Hoja.Asante sana
Mkuu Elton Tonny
Shukran kaka, inapendeza kuona umezama kwenye development ya storyNdio uhalisia huo Mkuu. Oi Mkuu Elton Tonny shukrani na unajua aisee hauandiki simulizi kufuata matakwa ya msomaji
Tuongezee episod mzeeKazi nzuri bro,
ila huyo Kevin hebu tukabidhi walau tumbanike yaan anakera sanaaa
Ahsante mkuuFOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA AROBAINI
★★★★★★★★★★★★★★
"S... Simi... Simi...." Lexi akawa anasema.
"Alexandra... njoo... twende... twende huku..." Isiminzile akamwambia.
Akamsaidia Lexi kusimama vizuri, kisha akaanza kuongozana naye kuelekea upande mwingine wa barabara na kuvuka majengo kadhaa mpaka walipofikia usawa wa gari lake aina ya Hilux, ambayo ilikuwa ni pickup nyeusi. Isiminzile akaenda na kufungua mlango wa nyuma wa gari hilo na kumwambia Lexi aingie na kujilaza kwenye siti za nyuma za gari hilo, naye akatii na kuingia haraka.
Isiminzile akaufunga mlango upesi na kuanza kurudi upande ule aliotokea na Lexi. Wakati wakilifuata gari lake, damu zilizodondokea chini zilikuwa zimeishia kwenye jengo la nyuma kidogo kutokea gari lake lilipokuwa, hivyo akaenda na kujisimamisha hapo mpaka wanajeshi walipofika ndani ya sekunde chache. Wakamkuta akiwa amesimama huku akionekana kushangaa, nao kwa ukali wakamshika na kumuuliza kama alimwona mwanamke fulani mweupe akikimbilia upande huo.
"Sema!" mwanajeahi mmoja akafoka huku akipumua kwa kasi.
"Nn..ndiyo nimemwona!" Isiminzile akakubali.
"Ameelekea wapi?" mwingine akamuuliza.
"Amenipita hapa... anavuja damu... si ndiyo huyo?" Isiminzile akauliza.
"Eee... yuko wapi?!"
"Ameelekea huko hivi..."
Isiminzile akadanganya kwa kuwaonyeshea upande tofauti na gari lake lilipokuwa. Bila kuchelewa wanajeshi wale wakaanza kuelekea huko kwa kasi sana. Kwa kiasi fulani, Isiminzile alikuwa akiogopa sana, lakini baada ya wanajeshi wale kuondoka, akarudi upesi kwenye gari lake na kumkuta Lexi akiwa bado amejilaza ndani yake. Akaingia kwenye usukani na kuliwasha, kisha akaanza kuligeuza haraka ili amwahishe kwenye hospitali ya mbali kidogo na eneo hili ili kumwepusha na wanajeshi wale.
Lexi alikuwa akiugulia maumivu ya risasi kwa sauti ya chini, huku akihisi mkono na sehemu kubwa ya mwili wake unakufa ganzi kutokana na kupoteza damu nyingi. Isiminzile aliendesha gari kwa kasi huku akimwangalia "mwanamke" huyu kupitia kioo, mpaka akamfikisha kwenye hospitali moja iliyowachukua kama dakika 7 hivi kuifikia. Akawahi kushuka haraka na kumfata huko nyuma, kisha akamsaidia kutoka ndani ya gari. Lexi alitaka kuweka kipingamizi kuhusu kwenda kule ndani, lakini Isiminzile akasisitiza sana waende kwa sababu alikuwa amepoteza damu nyingi sana.
Wakaelekea pamoja mpaka ndani ya jengo lile, na wauguzi kadhaa wakaja kumsaidia Lexi kuelekea chumba cha matibabu ya dharura. Ilikuwa ni hospitali kubwa ya kibinafsi iliyomilikiwa na wahindi, na baada ya Isiminzile kuulizwa ni nini kilikuwa kimesababisha mpaka mwanamke huyu akapigwa risasi, akasema kwamba alikuwa sehemu mbaya kwa wakati mbaya kwa kuwa maaskari walikuwa wanamkimbiza mwalifu fulani na kujaribu kumpiga risasi lakini kwa tukio baya ikampiga Lexi. Alipoulizwa uhusiano wake na Lexi, Isiminzile akasema alikuwa ni mchumba wake, naye angelipia gharama zake zote zilizohitajika.
Lexi akiwa kwenye chumba kile cha matibabu, alikataa kuchomwa sindano ya usingizi na kusema waitoe risasi akiwa bado macho. Akaomba watumie tu sindano ya ganzi ili kupunguza maumivu yake, lakini akakataa katakata kuchomwa ya usingizi. Daktari akafanya kama alivyoambiwa kwa kuwa aliona mwanamke huyu alikuwa anaelewa kile anachoomba. Akasaidizana na wauguzi kuitoa risasi, kisha wakaanza kufanya taratibu za kushona sehemu hiyo ya bega iliyotobolewa, halafu waifunike. Yote hayo yalichukua muda mrefu kiasi mpaka inafika saa 9.
Wakati Lexi akiwa anaendelea kupewa huduma, muuguzi mmoja alimtambua. Alikuwa amemwona kwenye mitandao ya kijamii kuwa mmoja kati ya watu wa kundi la Mess Makers, naye akammwomba daktari watoke nje ya chumba hicho mara moja ili wazungumze. Akaanza kumwambia kuhusu jambo hilo, na wakati alipokuwa akiongea vitu hivyo hapo nje, Isiminzile alikuwa amesimama pembeni akiwasikiliza bila wao kutambua uwepo wake. Daktari yule akamwambia muuguzi kuwa asiseme wala kufanya jambo lolote ambalo lingemshtua mwanamke huyo, ili yeye aende kuwataarifu mapolisi kwa njia ya simu waje kumkamata. Muuguzi akakubali na kurudi kwa Lexi, naye daktari akaelekea kwenye ofisi yake kufanya jambo hilo.
Isiminzile akaingia upesi kwenye chumba alichokuwepo Lexi na kukuta wauguzi watatu kutia ndani yule aliyemtambua Lexi, naye akamsogelea Lexi karibu zaidi. Wauguzi wale wakaanza kumfukuza kwa kusema hakutakiwa kuingia kwenye chumba hicho, naye Isiminzile akamwambia Lexi hivi, "Tunapaswa kuondoka." Lexi hakuhitaji maelezo zaidi. Akajitoa kitandani na kuanza kuvaa T-shirt yake, ingawa alihisi maumivu kupita kiasi. Wauguzi wale wakawa wanauliza ni kitu gani wanafanya, na yule mmoja akawaambia kwamba huyu mwanamke ni mmoja wa "magaidi" wanaojiita Mess Makers.
Lexi akajitahidi kupitisha T-shirt yake mwilini ingawa kidonda chake kikubwa hakikuwa kimefunikwa bado, kisha akachukua dawa za kupunguza maumivu na kuanza kuondoka huku akizibugia. Wauguzi wakawa wanajaribu kuwazuia kwa kutumia nguvu, lakini Lexi akajitahidi kuwatandika wawili kwa njia ambayo iliwaumiza kidogo, naye Isiminzile akamdhibiti mmoja wao na kusaidia watoke hapo haraka. Waliondoka upesi kabla ya wauguzi wale kuanza kuita msaada, na uzuri kwa wakati huu hakukuwa na watu wengi kwenye hospitali hiyo. Wakaelekea mpaka kwenye gari la Isiminzile, naye akaliondoa hapo upesi.
Wakiwa ndiyo wameanza mwendo, Lexi alionyesha kuwa na maumivu ya hali ya juu ingawa alijitahidi kujikaza. Kichwa kilimuuma, mwili ulimuuma, na kuna viungo vyake ambavyo bado hakuvihisi vyema kutokana na ganzi kuenea mwilini. Isiminzile akasema kwamba angempeleka kwake, lakini Lexi akakanusha na kumwambia kwa sababu amemsaidia, yeye pia alikuwa amejiweka hatarini. Akamwomba atoe simu yake kisha apige namba fulani. Isiminzile akatii. Baada ya kupiga, namba hiyo ikawa haipatikani. Lexi akatambua kwamba bila shaka wenzake walikuwa wameziharibu simu zao za kawaida, hivyo akamwambia Isiminzile apige nyingine, halafu aseme tu hivi, "Zelda hajambo? Mwambie anipitie pale pale alipopitia," kisha akate bila kusikiliza chochote.
Ingawa Isiminzile hakuelewa jambo hilo, akafanya kama alivyoambiwa, na baada ya kupiga namba hiyo akasema maneno hayo, kisha akakata upesi.
★
Ni wakati huo huo ndiyo Torres alipokuwa bado akikaza misuli ya mitambo yake pale namba fulani ilipopiga kwenye kifaa kile maalum cha mawasiliano ya Mess Makers, kama ambavyo wote walikuwa navyo. Alishangaa kiasi kuona namba hiyo ngeni, naye akaiunganisha upesi kwenye mifumo ya kompyuta zake ili akipokea, hata kama ingekuwa ni mtego, basi wanaoutega wasiweze kujua sehemu alipo. LaKeisha bado alikuwa pembeni yake muda huo, pamoja na Azra, nao wakaweka umakini kuona ni nini kingefuata.
Ndipo baada ya kupokea, Torres, Azra, na Lakeisha wote wakasikia sauti ya mwanaume ikisema "Hallo... Zelda hajambo? Mwambie anipitie pale pale alipopitia," kisha simu ya mwanaume huyo ikakata mawasiliano. Torres alikunja uso wake kimaswali. LaKeisha akamuuliza hicho kilikuwa ni nini, ni nani aliyekuwa anamuuliza ikiwa Zelda hajambo, na alimjua vipi Zelda. Azra akawa wa kwanza kutambua kwamba hiyo ni njia ya Lexi ya kuwasiliana nao kwa kificho, na baada ya kumwambia hivyo Torres, jamaa akaanza kufatilia namba hiyo ilikuwa wapi. Akapata kuona kwamba ilikuwa jijini Dar, ikitembea kutoka huko, yaani kwa usawa wa barabara ya kuelekea nje ya mji.
Torres sasa akawa ametambua kwamba Lexi alikuwa anamtumia ujumbe kumwambia alipo ili afanye jambo fulani kwenda kumsaidia, na ilionekana alikuwa akitoroka. Akamwambia hayo LaKeisha, na LaKeisha akatoka upesi kwenda kuwaita wengine. Baada ya wote kuwa wamefika na kuambiwa yaliyoendelea, Kendrick akawapa ruhusa Torres, LaKeisha na Azra kwenda huko upesi ili kumsaidia Lexi, kwa kuwa ni wao tu ndiyo ambao hawakujulikana bado, na hivyo uwezekano wa kumleta Lexi hapo bila wao kufatiliwa ulikuwa mkubwa. Alijua kwamba kutokana na wao kutoroka usiku huo, ulinzi na ufatiliaji kutoka kwa watu wa usalama ungekuwa mkubwa hata zaidi, kwa hiyo watatu hao wangetakiwa kwenda wakiwa katika hali ya kawaida lakini kwa tahadhari kubwa sana.
Bila kuchelewa, watatu hao wakaondoka hapo kwenye sehemu yao ya maficho, wakitumaini kuwahi na kukutana njiani pamoja na Lexi ili kumrudisha huku. Yaani hawa watu walikuwa hawapumziki! Habari hizi hazikumfurahisha Kevin hata kidogo, ambaye alikuwa anashangaa ni jinsi gani Lexi angekuwa ametoroka ikiwa alikamatwa kweli. Akabaki tu kuombea kwamba huko ambako Torres, LaKeisha na Azra wangekwenda na wenyewe wakamatwe pamoja na Lexi, kwa sababu hakutaka mwanamke yule arudi hapo tena.
★★★★
"NINI?!"
Hilo lilikuwa ni swali lililoulizwa kwa sauti ya juu sana na Kanali Oswald Deule baada ya kupokea taarifa kwamba Lexi ametoroka. Alishindwa kuelewa iliwezekanaje mwanamke huyo mmoja awatoroke wanajeshi sita wenye silaha kali, tena akiwa amefungwa. Taarifa hizo alizipata kupitia kwa mwanajeshi yule aliyekuwa akiendesha gari ambalo lilitumiwa kumsafirisha Lexi kuelekea kule walikodhamiria.
Kanali Oswald alikuwa pamoja na Kapteni Erasto pia wakati akiongea na mwanajeshi huyo kwa simu. Akamwamuru mwanajeshi huyo pamoja na mwenzake wafanye juu chini kuhakikisha Lexi anakamatwa kabla jua halijachomoza, yaani wamtafute kila kona ya eneo hilo na kila nyumba, la sivyo kungekuwa na adhabu mbaya sana kwa ajili yao. Akawaambia angewaongezea watu wa kuanza kumsaka, na kwa sababu mwanajeshi yule alikuwa amemwambia kwamba walimpiga risasi Lexi, Kanali Oswald akasisitiza wakague na hospitali za kuzunguka eneo hilo lote pia. Kisha akakata simu na kuirusha pembeni kwa nguvu akiwa anapumua kwa hasira kali.
"Hawa vijana ni washenzi sana!" akasema Kanali Oswald.
"Tokea mwanzoni nilihisi kabisa kwamba kuna jambo halingeenda sawa maana huyo mwanamke ni mchawi siyo kama anavyoonekana. Haiwezekani... yaani haiwezekani kabisa eti atoroke... aisee! Hivi kwa haya mambo watu tunalala saa ngapi?" akasema Kapteni Erasto kwa kuudhika.
"Zungusha magari na upige blockade kwenye njia zote za kutoka ndani ya jiji. Hakutakiwi kuondoka hata kwa mabasi ya abiria bila kukaguliwa alifajiri ya leo, umenielewa?" Kanali Oswald akatoa amri.
"Nimeshatoa agizo hilo mkuu. Najua ndani ya muda mfupi tutazipata habari zake," Kapteni Erasto akasema.
Kanali Oswald alikuwa anazunguka huku na huku ndani ya chumba hicho walichokuwa kwa kukosa amani kabisa.
"Kanali... utamjulisha General kuhusu jambo hili wakati gani?" Kapteni Erasto akamuuliza.
"No, no. Sitamwambia lolote mpaka nihakikishe huyo malaya amerudishwa mikononi mwetu. Hili suala halipaswi kumfikia kwanza, umenielewa? Liwe kama halijatokea kabisa!" Kanali Oswald akasema.
"Lakini vipi kama... je kama asipokamatwa?" Kapteni Erasto akamuuliza.
Kanali Oswald akamfata na kumtandika ngumi nzito tumboni. Kapteni Erasto alihisi maumivu na kubaki ameinama huku ameshika tumbo lake.
"Atakamatwa mpumbavu wewe! Si umetoka kuniambia ndani ya muda mfupi tutazipata habari zake? Na iwe hivyo. Kwa sababu ikiwa hatakamatwa nitahakikisha nakuua kwanza kabla Jenerali hajaniua mimi. Unaelewa matapishi yangu?" Kanali Oswald akafoka kwa hasira.
"Ndiyo mkuu," Kapteni Erasto akajibu bila kumtazama.
Kanali Oswald akasogea pembeni akiwaza mambo mengi sana. Alikuwa na wasiwasi mwingi kwa kuwa alijua kama Lexi hangekamatwa, basi Jenerali Jacob angekasirika kupita maelezo. Na ni wakati huu alipokuwa tu anamfikiria Jenerali Jacob simu yake ikaita, na mpigaji hakuwa mwingine ila Jenerali mwenyewe. Akafumba macho na kumeza mate, kisha akajituliza na kupokea.
"Habari za wakati huu Jenerali Jacob?" Kanali Oswald akatoa salamu huku anamwangalia Kapteni Erasto.
"Kanali... mmefikia wapi?" sauti tulivu ya Jenerali Jacob ikasikika.
"Aa... bado yuko barabarani analetwa huko. Usijali kuhusu lolote General, enjoy usingizi wako tu, kila kitu kitakuwa sawa kufikia asubuhi," akasema Kanali Oswald.
"Ikiwa unasema kila kitu kitakuwa sawa inamaanisha kuna kitu hakiko sawa. Kuna tatizo lolote?" Jenerali Jacob akauliza.
"No, no, no, sijamaanisha hivyo. Ni kwamba tu... sasa hivi ni usiku kwa hiyo... kila jambo kama..."
"Kanali..."
Oswald akakatishwa na mmoja wa wanajeshi waliofanyia kazi kwenye jengo hilo aliyeingia hapo ofisini ghafla. Kapteni Erasto akamzuia kwa ishara kumwambia akae kimya kwanza.
"Ndiyo General... everything is under control. Umeniamini katika hili mkuu, sitakuangusha. Nitamfikisha huko haraka na... kama tu tulivyoongea," akasema Kanali.
"Hmm... okay. Wacha nirudi kulala sasa. Nategemea mambo mazuri sana nikiamka asubuhi na kwenda kule. Kazi nzuri sana Kanali," Jenerali Jacob akasema.
Kanali Oswald akafumba macho kwa kuhisi hofu hata zaidi.
Simu ikakatwa, naye Kanali Oswald alikuwa anahisi ni kama Jenerali Jacob alikuwa anamwambia mambo kwa njia ya kebehi; yaani ni kama tayari alijua kuhusu Lexi kutoroka ila akawa anamchezea akili. Ikiwa hiyo ilikuwa ndivyo mambo yalivyo, basi Kanali Oswald akatambua kwamba alikuwa amejivuruga sana.
"Una shida gani?" Kapteni Erasto akamuuliza mwanajeshi yule aliyeingia.
"Tumepata taarifa kuhusu mwanamke mweupe aliyepigwa risasi kuingia kwenye hospitali moja... wamemtambua kuwa mmoja wa Mess Makers," mwanajeshi huyo akasema.
Kanali Oswald akamsogelea.
"Na nini kingine?" akamuuliza.
"Alikuwa na mwanaume mwingine ambaye alimpeleka hapo, lakini watu wetu walipofika wakakuta wameshaondoka. Ndiyo wako in pursuit sasa kutafuta barabara zote ambazo ni possible gari walilotumia lilipita..."
"Waambie wahakikishe hafiki mbali, tunaingia huko pia. Tutumie location hizo," Kanali Oswald akatoa amri.
Mwanajeshi huyo, ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye kitengo cha kupokea na kutuma taarifa muhimu kwa wanajeshi walio kwenye "mission," akatoka upesi na kurudi kwenye vyumba maalumu vya mawasiliano.
Kanali Oswald na Kapteni Erasto wakatoka upesi pia na kuelekea huko ambako Lexi alikuwa akifuatiliwa. Walitumia helicopter ndogo ya kijeshi ili kuwahi, nao wakaendelea kuwasiliana na wanajeshi waliokuwa wametangulia kupata kujua walifikia wapi, na baada ya mwendo wa kama dakika 15 hivi wakawa wamefika sehemu ambayo wanajeshi walilizingira gari lile la Isiminzile!
Eneo hili lilizungukwa na miti mingi kwa pande za pembeni na barabara kuu, hivyo magari ya wanajeshi yaliyokuwepo yalimulika gari hilo lililoonekana kusimama hapo kwa njia fulani ya mtego. Walihitaji kuwa makini sana kwa sababu waliwaelewa sana Mess Makers kwenye masuala ya mabomu, hivyo wakafikiria huenda kama Lexi angekuwa humo basi angekuwa amejitega na bomu kabisa.
Lakini baada ya helicopter ya Kanali na Kapteni kutua, Kanali Oswald aliwaambia wanajeshi kuwa walikuwa wanapoteza muda mwingi kukaa kuliangalia gari badala ya kufanya jambo la maana kujua kama mtu wao yuko humo au la. Kapteni Erasto na wanajeshi kadhaa wakaanza kulielekea gari hilo kwa umakini sana, na baada ya kulifikia karibu, wakalikagua pande zote na kipimo maalumu cha kuhisi mabomu na kukosa, kisha wakaanza kufungua milango na kuangalia ndani lakini na penyewe hakukuwa na mtu ndani yake.
Ikaja kwa kushangaza sana kwa sababu haingewezekana gari hilo kujiendesha lenyewe mpaka kufikia hapo. Ikabidi uchunguzi wa kina uanze kufanywa na kufanya Kapteni Erasto kutambua haraka kwamba walikuwa wanapotezewa muda tu ili Lexi aweze kutoroka. Akamwambia Kanali Oswald inaonekana labda wenzake Lexi ambao walitoroka pia siku hiyo, walikuwa wametumia njia hii kuwazubaisha ili mwanamke huyo aweze kuwatoroka. Kanali Oswald akaanza kuuliza wanajeshi wengine ambao walikuwa kwenye barabara zote za jiji kama kuna magari waliyaruhusu yapite bila kuyachunguza, lakini wakakanusha.
Hasira ilimjaa baba huyo ambaye alipiga kelele kwa nguvu kwa kutambua kwamba habari yake ilikuwa imekwisha. Aliwaza sana angemwambia nini Jenerali Jacob ambaye bila shaka angekasirishwa sana na jambo hili. Ilikuwa imefika saa 10 usiku sasa, na haikuonekana tena kama wangeweza kumpata mwanamke huyo na kundi lake lenye akili kupita maelezo.
Kapteni Erasto akamwahidi Kanali kwamba hawataacha kumtafuta Lexi hata kama wasipolala kwa siku zote zitakazofuata. Akatoa amri kwa wanajeshi wengine kuondoka eneo hilo na kuendelea kutafuta sehemu nyingine za jiji hilo.
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893