Simulizi: Harakati za maisha

SEHEMU YA AROBAINI NA NNE

Ilikuwa siku nzuri sana kwangu ,kwanza nilikuwa na pesa fulani ya kutanulia angalau kwa siku moja.pia nilikuwa nimetoka kwa mtaalamu ili kujiweka sawa.huku kwa asilimia nyingi mambo yakienda kama nilivyopanga.

Ila tatizo lilikuwa moja tu,ni Jastini.
Huyu kidogo alinivuruga kichwa huku nikijiuliza.maswali mengi,au kakata rufaa? Lakini ni rufaa gani ingemuacha uraiani ?
Lakini pia inaonekana alikiri mbele ya mahakama kwa kinywa chake ni nani angemkubalia hiyo rufaa?
Kwa sheria ipi?
Any way mimi si mtaalamu wa sheria,huenda kuna namna imefanyika awe uraiani.nilijiwazia

Niliamua kumpigia simu Shabani nimwambie chombo nishasukuma,

Hey bro ,imekuwa kama bahati nimefanikiwa kufanya ile biashara na pesa yako ninayo hapa cash,vipi kesho nikuone wapi? Niliuliza kwa kujiamini.

Dah kwasasa nipo mbali kidogo nimefuata mzigo wangu lakini nadhani kesho kutwa
Tutakutana.alijibu kwa mkato huku nikiona dizaini kama atanichelewesha hivi na mimi huwa sipendi kukaa na pesa za watu muda mrefu maana akili yangu naijua.

Siku inayofuata nikiwa nimetulia ndani kifua wazi,niligundua mke wangu ananitazama kwa makini licha ya mimi kuzuga kwa kugeukia upande mwingine lakini alishaona chale kifuani.

Mmmmmh,maisha haya acha tu ina maana mume wangu bado unaamini tu habari za waganga wa jadi?
Huoni kama unaishi kwenye karne ya kizamani sana,unadhani hayo mambo yatakusaidia nini.
akilalamika mke wangu.

Kwani nimefanyaje wife mbona sikuelewi, fafanua basi nijue.nilijifanya kama sijui anazungumzia nini.

Una chale mbichi kabisa kifuani,
Kumbe hii safari yako ya siku mbili hizi ulienda hukooooooo,ndiyo maana nikashangaa tangu lini ukatumia usafiri binafsi kwa safari za kiofisi! Hata muonekano wako tu ulidhijihirisha kabisa ni safari yako binafsi.

Lakini kumbuka hii nyumba haiwezi pata baraka hata maramoja, kwasababu tunamkaribisha shetani,
Hebu fikiria leo mimi naita watumishi na mapadre kuja kusoma misa hapa huku tukimwaga maji ya baraka,
Halafu wewe nawe unaenda unakokujua unapewa vitu na kuja kuvifukia kwenye hii nyumba,lazima ikose baraka.kwasababu tunapingana! Tunakinzana,tunavutana .

Wewe ni msomi baba,naamini sehemu ulipo haupo kwa kutegemea waganga wa kienyeji bali ni elimu na ujuzi uliokuwa nao,sasa mahangaiko mengine ni ya nini?
Heshima na nidhamu kazini ni silaha tosha ya kukufanya uaminike ,sitaki kuamini kama ni mazindiko yanakufanya uwe mahali ulipo.omba Mungu atakusaidia.aliongea mke wangu kisha akatoka huku akiwa kakasirika kwa muda ule.

(Kwanza nilicheka)
Huyu anadhani ni rahisi sana kuwa kwenye nafasi fulani bila kujiwekea ulinzi na kugangamala,ila siyo kosa lake kwasababu hajawahi kuajiriwa popote akaonja joto la kufukuzwa kazi bila kosa,au kuteremshwa daraja,cheo bila hata kosa.

Au kujikuta unaahidiwa mambo fulani mazuri lakini kabla hayajatimia mpango unafeli, maofisini ndiko kwenye watu wa kila aina
Mahasidi,wazandiki, wafitini, na watu wasiopenda maendeleo ya watu wengine. Ni kweli Dunia nzima hakuna yeyote asiyemuomba MUNGU, lakini lazima ujishikilie kwa namna yeyote ile.

Hapa tumepewa siku tano eti tujitafakari, Kisha tukapewe kazi ambayo hata siijui, unaweza Kuta ni mtego huu , ili tu ufeli Kisha uwekwe pembeni au ushuke,
Ni dhahiri suti na tai zinawakera watu unaweza kuta wenye vijicho wameshafanya yao, na namuomba MUNGU isitokee hii, sitaki Tena kushika spana Mimi , kugombana na HR na kutumana vitu vya kipuuzi sitaki, ila kwa uwezo wa Mungu nitayashinda majaribu
Nilijiwazia.

Mawazo yale yalinikumbusha kitu , nikaona siku ile niitumie kuingia kwenye websites kadhaa ili nione wapi huwa nafeli, sehemu ya kwanza niliwasaka wajapan,

Mainjinia wa kijapani huwa nawaelewa sana kwanza vitu vyao vingi huwa navielewa haraka , ni taifa lipo mbele ya muda kwenye technology haswa mechanical engineering, tofauti na nchi za Zingine ambao huwa Kuna ugumu fulani kwenye Theoretical Wapo njema ukija kwenye vitendo unajikuta unaanza upya, kwangu lakini maana uwezo na uelewa tunatofautiana baina ya mtu na mtu.

Nilizurula kwenye mtandao siku hiyo huku nikibaini makosa mawili makubwa huwa nafanya, ni siku ambayo nilikuwa kama nimezaliwa upya, nakumbuka nilishawahi kupata kazi ya kwenda nchi fulani kurekebisha vifaa , Kisha nikachemka huku nikibuni visingizio ambavyo maboss walikubali, lakini kama wangefuatilia kwa umakini wangegundua kitu, lakini tayari nimeshajua kitu.

Yaani today hata bia zitashuka vizuri na Kwa kugundua hii leo lazima nikajipongeze, ashukuriwe aliyebuni hii technology siku hizi vitu vinapatikana mtandaoni tu hakika hii ni Dunia ya kisasa.

Wakati nipo kule chumbani huku nikifuatilia mambo yangu, mke wangu aliniita na kuniambia kuna wageni.

Nilivaa vizuri Kisha nikatoka nikashituka kumuona dada yake Jastini aitwaye Lydia akiwa na mke wa Jastini. Tukasalimiana huku nikiwa makini nikiwachunguza Kila hatua .

Samahani ndugu ,
Ni kwamba Jastini yupo uraiani, tumefanya mpango ameweza kutoka ila hataki tena kukaa hapa mjini anataka kwenda mkoani na kilichotuleta hapa tunaomba msaada , tumepita sehemu nyingi tumepata ila mwanangu Lewis akasema na wewe uliahidi kutoa ushirikiano hivyo tunaomba Chochote ulichonacho umuokoe ndugu yako ili kule atakapofika ajue anaanzia wapi . aliweka kituo yule Lydia.

Ok naweza kujua ni taratibu zipi zimefuatwa mpaka akatoka maana nashindwa kuelewa. niliuliza.

( Yule Lydia na mke wa Jastini waliangaliana kwa muda)

Kwani hujapenda kutoka kwa Jastini? sisi tulidhani ungefurahi ndugu yako yupo huru. aliongea Lydia huku akijifanya kunishangaa

Samahani dada, Jastini alishafungwa , zipo sababu nyingi ambazo humfanya mfungwa kuachiliwa , lakini kwa Jastini naomba mnifafanulie vizuri zaidi , mtu kahukumiwa juzijuzi tu iweje leo yupo huru. Niliuliza.

Hawakuwa na jibu lolote la maana la kunipa huku kengele ya hatari ikilia akilini mwangu nikihisi Jastini ametoka kimagumashi labda ndiyo maana hataki kuonekana mchana na pia anahitaji kuhama kabisa .

Mimi nitawasaidia kwa kiasi kidogo kwakuwa hali yenyewe ni ngumu na pia sihitaji tena muwe mnakuja hapa, nimepata taarifa kuwa Jastini alikuja hapa usiku, niseme tu kuwa mumkatalie kuwa sitaki aje tena kwasababu hata nyie hamtaki kunipa maelezo katokaje Jastini.
niliongea kwa kumaanisha.

Waliangaliana Kisha wakapokea pesa kishingo upande huku ikionesha maneno yangu yamewagusa mno na walijisikia vibaya , yaani kama si shida waliyokuwa nayo I think hata pesa wasingechukua , lakini hawakuwa na jeuri hiyo.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Loading..........................
 
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO

Mbona kama hujawafanyia jambo zuri, usingewaambia hivyo huoni kama watajisikia unyonge?
Yaani umewafukuza kabisa, kusema wasije na wasikanyage hapa.
wale ni wanawake wenzangu usingewaambia hivyo.
alilaumu kidogo mke wangu.

Kwa mfano kama Jastini katoroka jela? tufanye ni kweli katoroka na anatafutwa halafu ionekane mimi na wewe tuna ukaribu nao na tunashirikiana , huoni kama tunaweza kusaidia upelelezi?
Na watu wanaweza sema tumeratibu mpango wa yeye kutoroka, just imagine?
Vitu vingine vinawezekana, kumbuka Jastini huyuhuyu kidogo aniingize kwenye mtego mbaya huenda hata Mimi leo hii ningekuwa...................
Kabla sijamalizia

Mume wangu hebu acha hayo utaniumiza ila kifupi nimekuelewa, ila pesa uliyowapa si haba pia, ni msaada mkubwa umefanya.
Mke wangu alinikatisha huku tukiachana na zile habari kwa siku ile.

Naam, ile siku ya kwenda kazini ilifika , ilikuwa ni jumatatu (blue Monday)
Ni siku huwa ngumu kidogo kwa akina sisi wenye vipato vidogo halafu starehe nyingi kwa fujo yaani ,tena hii Jumatatu huwa
Inafanana na mwezi January hivi.

Nikiwa na begi langu nilingia ofisini kwangu Kisha nikaseti vitu vyangu huku nikijua muda wowote boss akifika atatuhitaji.
Nilikuwa kwenye PC ya ofisi nikiiangalia kumbukumbu ya kazi nilizofanya mara ya mwisho.

Hizi, mmmh , hii mbili za mwisho huenda ndiyo zilimkosesha imani boss, lakini nishazipatia ufumbuzi naamini akisema nirudie ni very easy mapema nakabidhi kazi makini na iliyotimia. Nilijipa Imani huku mapigo ya moyo yakiongezeka halafu sikujua Nini kinasababisha yale.
huenda nililazimisha kujiamini huku uoga ukichukua nafasi kubwa.

Masaa yalisogea na nikishangaa mbona siitwi wakati huo watatu sisi tulikuwa tukitumiana sms Kila mtu akiulizia kunani mbona boss hatuiti, na alisema atatuita mwenyewe.

Baada ya muda wa lunch kupita wote tuliitwa huku tukisalimiana , tukiwa wakakamavu na wasikivu huku boss akiwa anachezea simu akiwa kwenye kiti kingine kabisa cha kawaida tofauti na pale kwenye computer zake.

Vipi mmejisikiaje kukaa nyumbani siku tano , yaani wiki nzima bila kufanya kazi. yaani haki zenu mtapata kama kawaida halafu kazi haziendi,nyie si hampo.aliuliza.

Tumejisikia vibaya boss.
Wote tulijibu.

Ok ok, sawa.
Kazi mbili za Mkoa X nani alifanya?
aliuliza.

Nikaitikia kuwa ni Mimi. Kisha akaniangalia huku akitabasamu kwa kunihurumia nadhani.

Ok, wewe wa mwisho huna tatizo, tatizo lako ni Moja huwa unapenda kufanya matanuzi na magari ya serikali, Sasa kuanzia leo tabia hiyo ife , huwezi kupakia wanawake zako na mambo yasiyotakiwa , kikazi upo vizuri hutoenda sehemu yeyote na nenda kaendelee na kazi. alimruhusu mwenzetu mmoja.

Halafu wewe wa katikati, naona unapenda sana uboss , kwa taarifa tulizopata ni kwamba unapenda kunukia muda wote na ukifika site kazi huifanyi wewe mwisho wa siku Kuna vitu kwenye mashine havifanyi kazi ipasavyo, mfano engine X uliyofunga inagonga sana na Ina muungurumo usiotakiwa na hii ni kwasababu hauhakikishi , unatuma vijana huku wewe Ukiwa pembeni, hebu punguza ufaza na uboss ndugu, hujafikia hata robo ya kujiweka kwenye hiyo hali.

Tulikubaliana kabisa vifaa vikisumbua tuvue suti zetu, tai tupa huko ingia kazini shirikiana na mafundi wenzio, mbona ni rahisi sana, lakini mnapenda kuzurura na magari unaamrisha dereva akupeleke hata sehemu zisizotakiwa.nakuonya kwa mara ya mwisho hiyo tabia uongozi haujapenda na hatuajaamua kukaa kikao maana wenzangu wamesafiri. Kisha akamruhusu aendelee na kazi

Kisha nikabaki Mimi huku licha ya kuwa ndani ni full AC lakini jasho lilinitoka.

Wewe Daniel ndiyo hata sitaki niseme mengi, halafu nasikia unakunywa sana pombe, sisemi ni kosa kunywa hiyo pombe, ila inaonesha dhahiri unsitumia hata Ukiwa kazini haswa Ukiwa site.
Mimi sinywi pombe ila kamwe huwa siwadharau wanaokunywa pombe kwa ni starehe yao na pia nyie wenzetu mnachangia Pato la taifa.
alitania kidogo.

Ila Sasa imekuwa too much Kwa taarifa nilizopokea ni kwamba zikifika kwa watu wengine, wanaweza kufanya maamuzi ya kushangaza. Nataka nikupe mfano mmoja.

Hebu inyanyue hiyo photocopy mashine hiyo ndogo mpya , iinue juu kabisa nyoosha mikono mpaka juu. alisema huku nikishangaa ana maana gani huku nimeganda vilevile.

Vipi unajisikiaje Daniel.
aliuliza.

Mikono inauma boss mashine nzito hii. Nilimjibu.

Ok ok, hiyo mashine ina thamani humu ndani ndiyo maana licha ya kukuumiza mikono lakini umeitua taratibu sana huku akicheka.

Halafu chukua hii karatasi.
akanipa karatasi fulani yenye maandishi haya inyanyue juu kama mwanzo tena ishike kwa mikono miwili.

Nikafanya vile huku nikishangaa zaidi karatasi niinue juu ili iweje lakini nilivyokaa muda fulani mikono iliuma huku nikipata picha fulani.

Vipi Daniel unajisikiaje, na hiyo karatasi ni nzito kama ile mashine ya mwanzo? au hayo maandishi yamesababisha ikaongezeka uzito?aliuliza

Hapana boss nadhani mikono kukaa hewani muda mrefu ndiyo sababu wala siyo hii karatasi. nilijibu kisha akacheka sana.

Hebu Kaa hapo Dani, mfano niliokupa nadhani umeuelewa wakati mwingine nakuvumilia kama hiyo karatasi, nakubeba ili tusiimbane kulaumiana pindi ukiwa mtaani.lakini ipo siku nitachoka kukubeba, siyo utakuwa unanichosha bali nitakuwa nachoka mimi mwenyewe.

Hebu hiyo karatasi itoe copy tupate nyingine moja, aliamrisha kisha nikafanya vile.

Hayo maandishi yaliyo kwenye hiyo karatasi pengine ni mazuri yamebeba kumbukumbu nzuri hapa ofisini kwangu ,lakini ipo siku itafubaa,au kuchakaa ,unajua nitafanyaje,nitaitoa copy kama ulivyofanya.
kisha nitaachana nayo na
Siyo kuachana nayo tu itatupwa kwenye dustbin kisha itapelekwa njeeee ni uchafu tayari,huku zile kumbukumbu zikibaki tu kwani copy zake si tunazo?

Mpaka kufikia pale nilimuelewa zaidi ya kumwelewa huku nikiwa kimya nisijue la kufanya.

Daniel mimi sikutumi popote kama ambavyo niliwaambia nyinyi wote isipokuwa nakupa tahadhari,hii kazi uliiomba mwenyewe hukulazimishwa,na pia wewe siyo muhimu saaaaana hapa utaondoka na kazi zitaendelea zaidi ni wewe utahangaika tu.hebu nenda kaendelee na kazi zako.aliniruhusu huku siku hiyo nikiwa mnyoonge.

Nilirudi ofisini kisha nikatulia huku nikiwa naona kama ofisi inazunguka tu maana nilipigwa spana za kutosha japo boss aliongea kirafiki kwa mifano mingi niliyoielewa vizuri.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Itaendelea..........................
 
Kwahio dawa za Mganga Bado mbichi hazikufanya kazi
 
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA

Nilikuwa mnyonge si kidogo hata hivyo nililazimika kutimiza majukumu yangu kama kawaida kwani sikuwa na namna nyingine.

Tuliendelea kutumiana meseji huku wenzangu wakiwa angalau wana furaha lakini kwangu ilikuwa tofauti ,nilipanga kutofanya makosa yeyote kazini,japo mimi ni binadamu mambo ya hapa na pale hayaepukiki.

Dani eeh usijali mwanangu mbona boss kaongea vitu vya kawaida tu,
Huwezi amini nilivyokuwa nawaza na alivyosema tofauti ,nilikuwa nawaza habari za kwenda saiti,Dah kuishi nje ya Dar kwa kipindi hiki siwezi kabisa .

Ilikuwa ni sms ya mmoja wetu ambao tulitoka kikaangoni.
Huku akionesha kufurahi kubaki mjini.

Siku hiyo hata sikutaka kugusa pombe ,licha ya kuwa nilikuwa na extra money ya udalali ,lakini bado akili haikuwa sawa kabisa ,kumbuka niliweza fikisha siku kibao bila kugusa pombe ya aina yeyote.

Nilitoka job nikanyoosha home tu sikutaka kuchepukia popote,
Ni kipindi ambacho nilikuwa nawahi kiasi cha wife kujisikia vizuri,huku mambo yakiwa shwari.

Siku inayofuata angalau nilikuwa na amani baada ya kusikia boss anasafiri na huenda ikakatika miezi miwili, hakika ilikuwa ni shangwe haswa kwenye kundi letu .
Nilikuwa huru sana kwani hata anayekaimu nafasi yake alikuwa ni mwanetu yaani tulikuwa tunammudu vizuri tu na alikuwa humble sana.
Hakuna unoko Wala kufuatiliana.

Baada mida fulani simu ya Shabani ilingia, ikabidi nimsikilize.

Ee bro nambie, naona simu zako Ukiwa huko zipo bize sana yaani hupatikani kabisa. Niliongea kwa uchangamfu.

Ndiyo hivyo , si unajua mazao hupatikana ndani ndani kidogo ambako sometimes network ni shida?
Ila nipo mjini na vipi tunaonana wapi.
aliuliza.

Hapa bro ni baada ya kazi kuisha nadhani jiandae saa kumi na moja hivi njoo maeneo ya kazini kwangu . Nilimjibu kisha nikaendelea na mishe zangu.

Baada ya muda kufika nilimkuta Shabani akiwa sehemu tuliyopanga kukutana , akiwa mnyonge kidogo licha ya mimi kumchangamkia lakini niligundua Kuna kitu kinamsumbua, akavunja ukimya.

Dani Kuna jambo silielewi Kati ya wewe na mke wangu, hili jambo linaninyima raha kabisa na ...........

Jambo gani bro hebu funguka.
Niliuliza kwa pupa.

Imekuwaje tena ukamuuzia gari yule mwanamke, namuita mwanamke kwasababu alishapoteza sifa za kuwa mke wangu siku nyingi sana.
Yaani baada ya Mimi kukudokeza kidogo matatizo yangu ukaona umtafute muongee vizuri si ndiyo?

Tena napata mashaka kidogo Dani nakufahamu vyema sana kwa kupenda wanawake
Pengine umeamua kumnunulia gari yule mke wangu kwasababu ni juzi tu ulisema tuongozane unipe gari baada ya wewe kusema umeshindwa kupata wateja na una mambo mengi.
Halafu siku hiyohiyo ukaniambia mteja kapatikana na umeuza,
Daniel mdogo wangu kuna kitu nimegundua,nishapata picha,kumbe mke wangu siku zote ananisumbua
Kila nikifanya upelelezi nashindwa kumpata muhusika.

Pesa zangu zimevurugika,mtaji wangu umekatika na sikujua ni nani alimshawishi mke wangu kufanya yale,nasikia amejenga kwa siri, anamiliki biashara nyingine tofauti na ya mazao tuliyozoea ,nikaja kugundua baadaye tena kwa kuchelewa ni baada ya yeye......
Kabla hajamaliza maneno yake nilimkatisha.

Ujue Shabani heshima ni kitu cha bure,yaani ukijiheshimu
Utaheshimiwa.
Najua wazi unampenda mkeo , hivyo jitahidi kubalance mambo yako ili tu usijikute unagombana na Kila mtu, matatizo yako yanaumiza lakini usitafute matatizo kwa wengine acha ujinga bro.

Ni kweli Daniel napenda wanawake lakini sijawahi kumtamani mke wa rafiki yangu hata siku moja , ulinikabidhi chombo niuze, mteja aliyekuwa anahitaji nilishangaa kuona kaja na mkeo, huku mkeo akiwa ndiye mteja mwenyewe.

Unasahau nilikwambia kuwa Kuna dada anaitwa Grace alishindwa kununua baada ya kugundua ni gari ya mkeo? Atakuwa ni yeye kamshawishi mkeo achukue tu.na nilimshangaa magari yote mjini kwanini ang'ang'anie gari ile sijui kuna hirizi yake.na mimi sikufanya ajizi niliuza kutimiza kazi uliyonipa ,sasa hayo unayotaka kuyaleta nakushangaa ni zaidi ya miaka mitano mkeo sijawahi kumuona hata wewe mwenyewe unasahau tumepoteana kwa muda gani?
Niliongea kwa ukali maana tayari Shabani alitaka kunitafutia kesi na mabalaa mengine.

Ok sawa ,nipe huo mzigo basi.
aliongea kwa sauti ya chini na yenye upole.nilimkabidhi akahakikisha na kujiridhisha kisha akawa ananiangalia bila kusema chochote.

Vipi bro si mzigo umetimia au?
Maana nataka kusepa mimi.
Niliongea huku nikitaka kuinuka maana niligundua tusingeelewana.

Hebu kaa kwanza Danieli mdogo wangu,mimi nimebakiza miaka miwili tu kustaafu kwa mujibu wa sheria kwenye utumishi
Na ndiyo maana unaona najikita zaidi kwenye mambo yangu binafsi.
Lakini naumia kuona mke wangu amebadilika ukubwani.
Yaani miaka yote tumeishi na watoto wetu watatu huku wapo ambao wana kazi zao na maisha yao , kingine tayari tuna wajukuu wawili,lakini mke wangu hakui wala sijui anawaza nini nashindwa kuelewa kifupi hata kitendo cha kumnyang'anya gari nilijua atajisahihisha,lakini ndiyo kwanza kaonesha jeuri ya kununua gari lile lile na hapa ninapoongea nyumbani kwangu kunawaka moto, na hatuelewani hata chakula Sili tena maana sina imani naye, ila nilichomfanya hatokaa asahau
aliongea kwa uchungu Shabani.

Sawa bro mimi naona mnaweza kuyamaliza kwa kuwashirikisha ndugu ,jamaa na marafiki inawezekana kabisa,inabidi ujishushe bro vinginevyo mkiachana mtaanza kugawana mali na kujikuta unazidi kushuka.nilishauri

( Kwanza alicheka)
Dani hujui tu suala lilipofikia wala hahitaji chochote kutoka kwangu na anadai anaweza kuishi bila mimi.
Na haya ndiyo madhara ya utamaduni wa kimagharibi,
Mababu zetu hawakuyaishi haya,
Yaani walizifaidi ndoa vilivyo.na najuta kuoa hawa mahousegirl ,huwezi amini alikuwa mshamba tu huyu,maisha ,biashara kila kitu nilimfunza mimi lakini malipo yake ni haya huwezi amini hata watoto wetu wanamshangaa sana tu
aliongea kwa sauti kiasi cha baadhi ya watu kutuangalia.

Mbona unawatuhumu mahousegirl bro wanakosa gani unajua kilichotokea ni mapungufu ya kibinadamu tu kulingana na kila mtu hisia zinavyomtuma hata angekuwa na masters ngapi sijui angefanya haya kwani ameshaamua kaka.
Niliongea kwa uelewa wangu.

Weweeee kuna muda najuta sana bora ni ningeoa mwanamke msomi unajua hawa wasiokuwa na elimu ndiyo huja kubadilika kama hivi kutokana na ulimbukeni wa maisha?
Wewe Daniel chunguza utaniambia tu hawa waliotoka vijijini hawafai.
Jamaa aliongea kwa Jazba sana.

Kitu ambacho sitaweza,na nisingeweza ni kuoa mwanamke msomi,au mwenye kipato kunizidi, nisingeweza maana ningewezaje kumuongoza,
Woman akishakuwa na uwezo wa kumiliki kila kitu sawa na wewe au more than basi tegemea kuishi na mwanamke siyo mke.hawezi kukuheshimu na hata akifanya hivyo ni kuigiza tu,tambua huna uwezo hata wa kumkoromea au kumtishia chochote.niliongeza.

Daniiii mimi naona cha msingi ni kumuomba Mungu tu ndoa yako iwe imara basi ila kwa upande wangu nimeshaanguka.mwanaume aliongea huku macho yakibadilika.

nilimuonea huruma halafu nikawaza na mimi wife yupo kwenye biashara ,leo kwa Shabani unaweza kuta kesho kwangu eti,
Haaaaaa wewe mimi nitakata mtu kichwa kwanza anawezaje kumiliki kitu kikubwa bila ruhusa yangu.nitazika mtu akiwa hai.
Halafu ngoja lazima nianze kutembelea biashara yake nione inaendaje na nilivyo na machozi ya karibu mbona nitakufa kihoro.
Nilijiwazia.

Lakini kabla hatujaagana mke wa Shabani alikuja pale akiwa na maaskari wawili waliovaa sare,
Sura ya mwanamke yule haikuwa na huruma hata kidogo.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Itaendelea.............
 
Mweeee! Mzee wa misala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…