Naweka kituo hapa hadi iisheSEHEMU YA TATU
Asubuhi na mapema kukiwa na baridi fulani kali kiasi nilioga , nikavaa nguo za kawaida kwani nilitahadharishwa na wenyeji kuhusu aina ya barabara ile wakinitaka nifike kwanza Nangurukuru ndipo naweza vaa nitakavyo. nilisogea stendi ya pale Liwale huku nikiiangalia aina ya siti nitakayokaa kwenye ile tiketi.
Watu walikuwa wengi huku magari mawili ya kwanza ya abiria yakiwa yanaondoka, sisi gari letu lilikuwa bado linapakia mizigo, sikutaka kuingia mapema kwani watu waliosongamana pale mlangoni walileta kero kiasi.
Baada ya watu kupungua pale mlangoni, niliingia nikipenyapenya katikati ya watu waliosimama, lakini nilikuta kwenye siti yangu amekaa mama mmoja aliyekuwa anaongea lafudhi ya kisukuma.
Samahani mama, nadhani hii sehemu nakaa Mimi angalia tiketi yangu, nikampa ajionee ili tuondoe utata.
Akasema hapana, ile ni sehemu yake, akanionesha tiketi yake, ikiwa imeandikwa sehemu ile ile, hivyo alikuwa sahihi, nililaumu sana kitendo cha watu kuuza siti mara mbili, nikaamua kuja huku mbele nikasimama Kisha nikampigia dereva wangu kuwa kama hajatoka Lindi mjini basi aje Liwale anichukue lakini simu haikupatikana.
Nikaamua moja kusimama huku gari likiondoka kwa mbwembwe, watu tumebanana kama tupo kwenye daladala za Gongo la mboto, tulitembea kwa muda fulani huku nikiwa sioni nje , yaani sijui tupo wapi Kuna muda gari inalala kama inaanguka huku mabonde nayo nikiyasikia vizuri . Baadaye gari lilisimama dereva akashuka, nusu saa nzima dereva haondoki gari linaunguruma tu, watu tukaanza kushuka mmoja mmoja huku tukamuona dereva kwenye uvungu wa gari akiwa na spana zake.
Nikaona kazi ipo, nikawauliza wenyeji kwani tupo wapi wakajibu tupo sehemu inayoitwa kaburi la mzungu, huku wakidai safari bado kabisa. nilitoka nikaenda kwenye mti fulani nikiwa peke yangu huku nikishangaa kundi kubwa la watu yaani wote Hawa tumetoka kwenye gari hii, kumbe hizi Marco polo Zina nguvu sana eeh. nilijisemea moyoni.
Nilimpigia dereva akapokea nikamweleza hali halisi akadai yeye iwe isiwe atanisubiri hivyo nisiwe na shaka. Lakini wakati nikiwa pale alikuja jamaa mmoja mwenye mwili uliokosa mazoezi huku akiwa hazingatii diet. akanisalimia kwa kunipa tano.
Loh kaka kumbe huku usafiri ni wa tabu hivi, hakika leo tumepatikana , yaani hiyo gari sijui hawakuikaguaaaa? Naona Springs zimecheza ndiyo wanahangaika kufunga hapo, tuombe MUNGU tuondoke salama dah. aliongea kwa masikitiko yule jamaa huku nikitambua kuwa naye ni mgeni kama mimi.
Yaani ndiyo hivyo huku usafiri shida,.......... Kabla sijamalizia sentensi yangu , alikuja mwanamke huku akimvuta jamaa mkono kwa nguvu.
Hivi Mume wangu unanitaka nini lakini, kwanini unaniharibia? mtaalamu ulimsikia vizuri sana, alitwambia msipeane mikono na mtu yeyote, hadi mtakapo fika na kuoga hii dawa , Sasa kwanini unakuwa hivyo? Mwanamke aling'aka huku akinitolea macho mimi kana kwamba ndiye niliyesababisha.
halafu na wewe mwenye midevu kwanini unapenda kusalimia salimia watu ovyo ovyo ili iweje. Kila mtu ana Harakati zake kwenye maisha,jitahidi kudili na mambo yako.mwanamke yule alianza kuniletea shombo.
Kwanza nilishangaa lakini nilishindwa nimfanyaje.
Mke wangu hebu kuwa na adabu basi, huyu jamaa nimemkuta Mimi na Mimi ndiye nimeanza kumsalimia hivyo makosa ni yangu , hebu achana na watu wengine mke wanguuu.
aliongea jamaa kwa kujikaza huku Kwa dakika kadhaa nilivyowaona ni dhahiri mwanamke alikuwa na sauti kuliko jamaa.
Haya ushaharibu tayari, inatakiwa turudi kwa mtaalamu , na Mimi duka langu sitafungua hadi tutakapo kamilisha vigezo na masharti yote, japo sharti moja umeshavunja , na turudi tu kwa mtaalamu Mimi siendi mjini tena . alilalamika yule mwanamke.
Lakini mke wangu mbona unakosa aibu vitu gani unaongea ? jamaa alimlaumu mkewe.
Mimi kuona vile nikatoka nikaenda kukaa kwenye mti mwingine nikiwaacha wanalumbana, huku nikiwaza mbali namna watu walivyo washirikina, au haya mambo yapo kweli, isije kuwa huwa nadharau tu kumbe waganga wanasaidia, maana hizi kazi za kutumwa hiziiiii, tutatumwa Hadi lini? Basi kama nimeandikiwa kutumwa, nipande hata cheo basi, si bado nitaendelea kuwa mtumishi. niliwaza sana huku majibu yakiwa mengi.
Watu walikaa vikundi vikundi wakipiga stori zinazofanana, wapo walizungumza namna ya uchomaji mkaa, wapi walizungumza kuhusu kilimo, wapo vijana waliongelea kuhusu uchimbaji wa madini sijui wapi huko. lakini baada ya Mimi kuona dereva na mafundi bado wapi uvunguni mwa gari nilirudi kwenye mti nilipokuwa mwanzo.
Nikaona yule jamaa na mkewe wanakuja nilipo, Hawa wanataka nini tena? Naamua kukaa peke yangu bado wananifuata fuata?
Wakizingua tena nawachana wasinione mnyonge, nilijisemea moyoni.
Dah aisee shemu noma sana yaani, gari sijui litapona saa ngapi,aliongea yule mwanamke huku jamaa akiwa mita kadhaa akiongea na simu.
Ila shemu naomba nisamehe bwana nimejikuta naropoka , nisamehe bure si unajua wanawake sisi. aliongea kwa sauti ya kubana huku nikibaini sauti nzuri lakini pia na yeye alikuwa Mashallah, sura nzuri na shepu ya kwenda. Wakati huo mumewe anaongea na simu na anazidi kwenda mbali zaidi.
Yaani wanawake bwana, wanakimbilia kwenye jinsia yao wakikosea, mwanzo walikuwa wanasema wakiwezeshwa wanaweza, si hawa?
Tena Sasa hivi wamebadilika wanadai , mwanamke anaweza bila kuwezeshwa. niliwaza sana.
Vipi shemu usinung'unike, naona nisamehe sana, alizidisha maneno.
Usijali shemu najua jamaa alikukwaza ikapelekea kuwa kwenye ile hali, nashukuru kama umetambua ulipoteleza, na MUNGU akubariki . Baadaye tukaitwa nikijua gari limepona.tukawa kwenye eneo la tukio.
Jamani tuwe wa kweli tumejitahidi kwa kadri ya uwezo wetu, lakini tumeshindwa hivyo Kuna gari linakuja kutufaulisha naomba tuwe wavumilivu kiasi ni bahati mbaya imetokea hakuna anayependa hii hali .Dereva aliweka kituo huku abiria wengi wakikata tamaa, Mimi nikarudi kwenye ule mti ili nimpigie dereva wangu anifuate lakini simu haikupokelewa.
Yule jamaa na mkewe walikuja tena,aisee kaka Kuna sehemu zingine sijui watu wanawezaje kuishi yaani tangu muda ule hakuna hata gari la mizigo kupita? jamaa aliongea huku akicheka sana. Lakini kumbe taarifa zilishafika Liwale mjini kuwa chombo kimeharibika hivyo pikipiki (bodaboda) zikaanza kuja ili kama Kuna wanaoahirisha safari basi warudi Liwale.
Wakati tukiwa pale chini ya mtu lilikuja gari lililopakia chupa za soda tupu , huku wakidai wanaenda Kilwa Masoko kwahiyo anayetaka kufika walau Nangurukuru ambako ndiko kwenye usafiri wa uhakika basi achangie elfu kumi, Mimi sikuuliza nilikuwa nishachomoa kumi yangu ipo mkononi huku baadhi wakidai hela ile ni nyingi sana na pia hawazi kuacha nauli zao walizolipa kwenye bus, umasikini mbaya sana.
Sisi watatu tulipanda kwenye ile Eicher, wanaume wawili tukiwa nyuma yule mwanamke akapanda kwa dereva.
Je, tutafika salama? usikose sehemu inayofuata.
Itaendelea.........................
Pomoja sanaSEHEMU YA HAMSINI NA MBILI
Alishuka kwenye gari akiniacha nikiwa tuli mle ndani huku nikichora mazingira ya mtu mmoja mmoja.
Heka heka zilikuwa nyingi na magari yaliyoingia na kutoka yalikuwa si haba,nikaona wenye harusi yao huenda siyo wanyonge mavumba yapo.
Medi alipotea kwenye macho yangu huku dakika zikienda nikajua ,na tabia yake ilivyo basi huko ndani alikoingia sijui kama atatoka mapema,kweli nusu saa ilipita huku nikianza kujiona mjinga kwa kubebwabebwa tu ,yaani mimi nilivyo ni wa kuzurulishwa mitaani? Khaah Medi kaniweza leo.
Baada ya muda fulani alikuja akiwa na watu wawili hivyo mwanamke na mwanaume walioonekana kama timu ya mapambo.
Dada eeeh huyu ni rafiki yangu ni mmoja wa watu muhimu hapa wilayani na amekuja kwa shughuli maalumu.si unajua kaka yangu ni aliyeshika tenda ya kutengeneza kile kipande cha barabara kutoka barabara kuu kuja zilipo ofisi ya DC,
Basi huyu ni mmoja wa watu wetu.
Naomba aheshimiwe na atakaa meza kuu kama ilivyo kwa wengine japo mimi nitakuwa kwenye timu ya vinywaji hivyo sitatulia.alinitambulisha kwa yule mwanamke wa makamo.
Karibu sana,karibu ndugu ,anaitwa nani vile? aliuliza yule dada.
Naitwa Daniel (nikitaja majina mawili)nilisaidia kujibu.
Sawa karibu,na jisikie huru sana naitwa Mama mapambo,ndiyo jina langu maarufu hapa kwa shughuli ya upambaji lakini pia anayeoa ni mdogo wangu wa tumbo moja hivyo kwa leo nipo kwenye nafasi nyingi.aliongea yule mama mwenye tabasamu rafiki.
Yaani dada leo ni Two in one,unacheza huku na huku ila maharusi wakifika lazima utatulia tu.
aliongea Medi ambaye pengine waya wa aibu ulikuwa ..........
Sasa Dani wewe nenda kajiandae,mimi nipo hapa na hata kwangu si mbali hivyo chukua gari nenda nalo kajiandae maana maharusi nadhani wako njiani ,huoni hizo Coaster zilizotangulia.na watu ndiyo wenyewe hao.alishauri Medi.
Nilirudi kisha nikajiandaa huku nikijipongeza kwa kuikumbuka na kuibeba Kaunda suit yangu nyeusi ambayo niliivaa siku moja tu,kifupi ilikuwa ni mpya, nilijicheki kwa mirror ili nione ndevu na nywele zisiwe rough sana maana nipo ugenini kuhudhuria kwenye sherehe za watu ukiwa hueleweki ni noma , heshima huwa inashuka.kila kitu kilikuwa poa . nikachukua perfume fulani niliwahi kununua mkoani Mtwara,huku wife akadai haipendi,alidai eti nikiitumia sinukii vizuri. Licha ya kuwa ilikuwa haina harufu kabisa yaani ni inakufanya tu uwe Smart man lakini siyo kila mtu anajua umepakaa perfume.si mpenzi wa Cheni wala pete ,kwanza huwa siwezi kutembea na kitu kinanitekenya shingoni ,hata saa huwa navaa basi tu.
Nilihakiki code yangu nikaona sijazingua nikatoka huku muhudumu wa pale akishindwa kujizuia hisia zake.
Aisee kiukweli kaka tangu ufike hapa sijawahi kukuona ukiwa hivyo jamani , hongera sana,yaani hadi raha .aliongea kwa sauti fulani tamu ya kike.
Sikumjibu ila nilitabasamu tu kuashiria nimependa pongezi zake.
Saa kumi na moja nilishuka kwenye gari nje ya ukumbi ule nikiambiwa watu wameshakula na kinachoendelea ni taratibu zingine tu.nilimpigia rafiki yangu na mwenyeji wangu Medi simu haikupokelewa lengo niongozane naye ,siyo naingia halafu naanza kupepesa macho nisijue nakaa wapi .
Cha ajabu Medi hakupokea simu nikaamua kuingia ndani ya ule ukumbi ,huku muziki fulani ukiendelea kuwaburudisha watu nikasimama mwisho kabisa kwa majamaa fulani ambao huenda hawakualikwa pale
Sina hili wala lile MC alianza kuongea kwa mbwembwe huku akionesha kazi anaijua
Aaaaaah kabla ya yote niwapongeze wale wote tuliomuunga mkono ndugu yetu na huu ni mfano wa kuigwa ,kwa wale ambao tulikuwa kanisani natumai mmesikia vizuri Padre aliyebariki ndoa hii,na kwa wasiokuwepo nitaongea hakika na mimi najuta kuoa kienyejienyeji.aliongea yule
MC huku akiwavunja mbavu watu.
Nikiwa busy na simu haswa baada ya kuona mtaalamu niliyempigia asubuhi akashindwa kupokea anapiga,huku nikitaka nitoke nje nikamsikilize maana nilikuwa near by exist door mara nikasikia kama natajwa jina.
Kuna ndugu yetu hapa bila shaka ni mgeni lakini ningependa aje akae huku mbele jamani,halafu wanakamati mmesahau majukumu yenu? Hebu ndugu yangu uliyesimama hapo nyuma naomba uje mbele hapa basi usijisikie unyonge Mr.aliweka kituo MC
Moyo ulilipuka kwa uoga huku nikijikaza nikisogea kwenda safu ya mbele,watu wakishangilia huku wakiimba baba, baba ,babaaaa, baba
Huyoooo,amependeza na suti yake.
Duh ile siku sitaisahau ,yaani mtu hujajiandaa halafu unaitwa mbele huku maelfu ya macho yakikutazama.
Hebu kabla hujakaa tusalimiane baaaasi,eeeeh hebu jitambulishe.aliongea MC huku nikijikaza na kujitambulisha vizuri,ukumbi wote ukalipuka kwa shangwe na vigelegele,yule aitwaye mama mapambo akaja na kunikumbatia mbele za watu .
Duh ilikuwa ni aibu kwangu .maana mtu anakukumbatia hujui kitu , pengine ana mume hujui,na huyo mume kama akikumaindi maana wanaume tunajijua wenyewe,wenzetu wanawake (baadhi) wanaweza kufanya jambo hata la hatari lakini wasilione kwa muda huo kutokana na furaha kupitiliza.
Nilikaribishwa nikae,huku mtu wa pembeni nisiye mfahamu akiniita , Mr Dani,mr Dani ,kugeuka hamadi!
alikuwa ni Fatma yule askari.
Yaani niliduwaa ila sikushangaa yeye kuwa pale maana yeye ni mwenyeji zaidi kule.
Akahama alipo na kuja kukaa karibu yangu,ikawa hatuongei ila tukikutanisha macho yetu kila mmoja anatabasamu.
Kweli ukitaka kuanguka ,au kuangusha ufalme wa kidume yeyote basi watumie wanawake warembo.
Nasisitiza wawe warembo.
Utafanikisha zoezi lako.
Sasa endelea............
Wakati wa kuwasilisha zawadi uliwadia kama mtiririko wa ratiba ulivyokuwa huku Dj akiweka wimbo fulani wa vijembe yaani kila aliyekuwepo kama hakutoa basi ndo utafanyaje.
Watu walianza kuinuka huku kila mtu akipigiwa makofi kulingana na alichotoa au alichoahidi,huku Mc akisisitiza kuwa wanaoruhusiwa kuahidi ni wale wanaofahamika tu ila kama ni mgeni na huna kwa wakati huo usiahidi chochote labda kama unajiamini utatoa kweli. Wakati huo mahali nilipokaa mimi nadhani walikaa wenye nafasi nzuri kipesa ,yaani wajuba hawakuwa na wasiwasi hata ,pia mijimama iliyokuwa pale ( malkia wa nguvu) walikuwa na tabasamu za pesa tu , mmmh ubaridi ukaanza kuniingia kila nikikumbuka kilichomo kwenye wallet miguu iliishiwa nguvu hata lile tabasamu kwa Fatma lilipungua.nilikuwa nawaza au nimpigie wife aniongezee pesa?
Lakini mbona sijawahi fanya hivi.
Na nilivyotambulishwa kwa mbwembwe ndiyo nilichoka kabisa
Huku Fatma akiwa kama kagundua kitu toka kwangu,akanisogelea na kuninong'oneza kitu huku nikizidi kuwa muoga.
Jifunze,
Elimika,
Burudika.
Weekend njema wadau wangu.
Itaendelea..................
[emoji23][emoji23][emoji28]duh!We jamaa una kimavi walahi, ngoja tusubiri misara tu ili tuanze kukupa pole, kwamaana huchelewagi
Kwahio mie ndo Delilah πhaya usijali ngoja nimuite SamsonNourhan ongea na Samson wewe unammudu
we nae unapenda sana kimokoSamson njoo bwana utupe japo kimoko π usituache sana,tunajua una majukumu yako nje ya JF ila tunashindwa kujizuia π
Eeeh bora ya kimoko chenye ujazo kuliko viwili vya kuparasa πwe nae unapenda sana kimoko
Eeeeh yamekua ayoEeeh bora ya kimoko chenye ujazo kuliko viwili vya kuparasa π
Ngoja nipambanie kwanza ugali wa watoto kwanza saa kumi na mbili jioni usikose kuchunguliaJack Daniel njoo Mhandisi