James Hadley Chase
JF-Expert Member
- Mar 25, 2020
- 1,984
- 3,695
HILIKI YA CHUMBAGENI
MWANDISHI: JOSEPH SHALUWA
“BABY umeamkaje?”
“Honey mzima?”
“Mpenzi wangu umeshatoka hotelini?”
“Laazizi wangu, jamani nakutumia text zote hizo na hujibu kitu, kuna nini?”
“Bravo unajua ulivyonizoesha mume wangu, mbona unanifanyia ukatili mkubwa namna hii?”
“Baba yangu, nini kimekupata? Nataka kuona japo text moja tu kutoka kwako nijisikie amani. Nashindwa hata kuondoka nyumbani bila kupata ujumbe wako.”
“Bravo sasa unanipa wasiwasi mpenzi wangu, maana meseji zote huku kwangu inaonekana umezisoma, lakini hujibu kitu, kuna nini?”
Alikuwa ni Viola akituma ujumbe kwa Bravo, mume wake kupitia njia ya Mtandao wa Kijamii wa WhatsApp. Usiku mzima wa siku hiyo hakuweza kulala usingizi mzuri kutokana na mawazo aliyokuwa nayo juu ya mume wake.
Ni siku ya tano sasa, mume wake yupo safarini Tanga, kikazi. Alitarajia kukaa huko kwa wiki mbili. Ni muda mrefu sana kwa wanandoa hao wabichi, wenye umri mdogo, damu zao zikichemka!
Viola na Bravo ni wanandoa wapya, ndoa yao ikiwa na miezi mitatu tu tangu walipofunga. Ilikuwa ndoa ya kidini, iliyofungwa kanisani. Wakiwa ndiyo kwanza wameoana, walikwenda mapumzikoni kwenye fungate lao, visiwani Zanzibar ambapo walifurahi huko kwa wiki moja.
Baadaye waliamua kwenda jijini Mbeya na kupumzika milimani kabisa, Tukuyu katika hoteli moja ya kifahari. Walifurahia penzi la ndoa yao mpya kwa baridi tamu, iliyowanasisha karibu muda wote waliokuwa mjini Tukuyu.
Siku za mapumziko zilipokatika, walirejea jijini Dar es Salaam na kuanzisha maisha yao mapya ya ndoa. Kabla ya kuoana, Viola alikuwa akiishi nyumbani kwa wazazi wake, Temeke.
Bravo yeye alikuwa akiishi Kijitonyama, wiki mbili kabla ya kufunga ndoa aliamua kupangisha nyumba nzima, eneo jingine kabisa. Aliamua kuhamia Mbezi Beach, katika eneo ambalo hajulikani!
Walipotoka Tukuyu walifikia Mbezi Beach. Wakaingiza zawadi zao za pande zote, maisha yakaanza rasmi. Yalikuwa maisha yenye furaha, kila mmoja akifurahia kuwa na mwenzake. Jambo moja ambalo Viola alishangazwa nalo kutoka kwa Bravo ni utundu mpya baada ya kufunga ndoa yao.
Ni kweli mara kadhaa wakiwa kwenye uchumba walikuwa wakikutana faragha, tena wakati mwingine walilala pamoja hadi asubuhi, lakini Brano hakuwa mjuzi wa kiwango kile alichokutana nacho kwenye ndoa.
“Baby mbona umekuwa tofauti sana baada ya ndoa?” Viola alimwuliza mume wake, wakiwa katikati ya kazi ya wanandoa, hotelini Tukuyu.
“Kwanini mpenzi?”
“Umekuwa mtundu zaidi, unanifanya nijisikie salama zaidi kuwa na wewe. Unanipa vitu adimu laazizi, ambavyo sikuwahi kuvipata kabla,” akasema Viola.
“Kwani kabla ya Send-off yako ulifanyiwa sherehe gani?” Brano akamwuliza.
“Kitchen Party.”
“Ilikuwa kwa ajili ya nini?”
“Kubwa zaidi ni kufundishwa namna ya kuishi na mume, kufundishwa utundu wa jikoni na chumbani!”
“Safi sana, hata mimi ni hivyohivyo, nilipata darasa kutoka kwa wazee wa Kinyiramba. Maanko zangu walinipa mautundu, ndiyo maana unaona nakula ile kitu roho inataka,” akasema Bravo akionyesha mizaha.
Wote wakaishia kucheka!
ITANDELEA....
MWANDISHI: JOSEPH SHALUWA
“BABY umeamkaje?”
“Honey mzima?”
“Mpenzi wangu umeshatoka hotelini?”
“Laazizi wangu, jamani nakutumia text zote hizo na hujibu kitu, kuna nini?”
“Bravo unajua ulivyonizoesha mume wangu, mbona unanifanyia ukatili mkubwa namna hii?”
“Baba yangu, nini kimekupata? Nataka kuona japo text moja tu kutoka kwako nijisikie amani. Nashindwa hata kuondoka nyumbani bila kupata ujumbe wako.”
“Bravo sasa unanipa wasiwasi mpenzi wangu, maana meseji zote huku kwangu inaonekana umezisoma, lakini hujibu kitu, kuna nini?”
Alikuwa ni Viola akituma ujumbe kwa Bravo, mume wake kupitia njia ya Mtandao wa Kijamii wa WhatsApp. Usiku mzima wa siku hiyo hakuweza kulala usingizi mzuri kutokana na mawazo aliyokuwa nayo juu ya mume wake.
Ni siku ya tano sasa, mume wake yupo safarini Tanga, kikazi. Alitarajia kukaa huko kwa wiki mbili. Ni muda mrefu sana kwa wanandoa hao wabichi, wenye umri mdogo, damu zao zikichemka!
Viola na Bravo ni wanandoa wapya, ndoa yao ikiwa na miezi mitatu tu tangu walipofunga. Ilikuwa ndoa ya kidini, iliyofungwa kanisani. Wakiwa ndiyo kwanza wameoana, walikwenda mapumzikoni kwenye fungate lao, visiwani Zanzibar ambapo walifurahi huko kwa wiki moja.
Baadaye waliamua kwenda jijini Mbeya na kupumzika milimani kabisa, Tukuyu katika hoteli moja ya kifahari. Walifurahia penzi la ndoa yao mpya kwa baridi tamu, iliyowanasisha karibu muda wote waliokuwa mjini Tukuyu.
Siku za mapumziko zilipokatika, walirejea jijini Dar es Salaam na kuanzisha maisha yao mapya ya ndoa. Kabla ya kuoana, Viola alikuwa akiishi nyumbani kwa wazazi wake, Temeke.
Bravo yeye alikuwa akiishi Kijitonyama, wiki mbili kabla ya kufunga ndoa aliamua kupangisha nyumba nzima, eneo jingine kabisa. Aliamua kuhamia Mbezi Beach, katika eneo ambalo hajulikani!
Walipotoka Tukuyu walifikia Mbezi Beach. Wakaingiza zawadi zao za pande zote, maisha yakaanza rasmi. Yalikuwa maisha yenye furaha, kila mmoja akifurahia kuwa na mwenzake. Jambo moja ambalo Viola alishangazwa nalo kutoka kwa Bravo ni utundu mpya baada ya kufunga ndoa yao.
Ni kweli mara kadhaa wakiwa kwenye uchumba walikuwa wakikutana faragha, tena wakati mwingine walilala pamoja hadi asubuhi, lakini Brano hakuwa mjuzi wa kiwango kile alichokutana nacho kwenye ndoa.
“Baby mbona umekuwa tofauti sana baada ya ndoa?” Viola alimwuliza mume wake, wakiwa katikati ya kazi ya wanandoa, hotelini Tukuyu.
“Kwanini mpenzi?”
“Umekuwa mtundu zaidi, unanifanya nijisikie salama zaidi kuwa na wewe. Unanipa vitu adimu laazizi, ambavyo sikuwahi kuvipata kabla,” akasema Viola.
“Kwani kabla ya Send-off yako ulifanyiwa sherehe gani?” Brano akamwuliza.
“Kitchen Party.”
“Ilikuwa kwa ajili ya nini?”
“Kubwa zaidi ni kufundishwa namna ya kuishi na mume, kufundishwa utundu wa jikoni na chumbani!”
“Safi sana, hata mimi ni hivyohivyo, nilipata darasa kutoka kwa wazee wa Kinyiramba. Maanko zangu walinipa mautundu, ndiyo maana unaona nakula ile kitu roho inataka,” akasema Bravo akionyesha mizaha.
Wote wakaishia kucheka!
ITANDELEA....