Simulizi: Hiliki Ya Chumbageni

Simulizi: Hiliki Ya Chumbageni

HILIKI YA CHUMBAGENI – 20
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
“Najua siwezi kukulipa kwa wema wako, lakini kwa sababu umekiri mwenyewe kuwa unafurahishwa na mapenzi yangu, basi leo itakuwa mara kumi zaidi ya awali,” Tunu alisema kwa sauti ya chini, akionekana kuhema kwa tabu.
“Nimekwisha mimi... hivi nitaweza kurudi nyumbani kwangu kweli?” akawaza Bravo kichwani mwake.
Semina ilikuwa imeshaisha jijini Tanga, siku hiyo baadhi ya wafanyakazi walikuwa wameshaanza kuondoka kurejea kwenye vituo vyao vya kazi. Wengine walitarajiwa kuondoka siku iliyofuata!
Lakini siyo Bravo!
Bravo hakujua wala hakupanga siku ya kuondoka Tanga!
SASA ENDELEA...
ULIKUWA mperampera wa aina yake. Alivyokuwa akifikiria Bravo awali, ilikuwa tofauti kabisa. Tunu alikuwa mtaalamu kuliko kawaida.
Aliyoonyeshwa kwenye mechi ya utangulizi, kumbe ilikuwa rasharasha tu. Sasa Tunu akamwonyesha kwa undani ufundi wote aliofundwa unyagoni! Bravo alikiri kwamba, alikutana na kisima cha mahaba, ambacho hakikukauka mahaba ya kila namna.
Baada ya kazi nzito iliyofanyika ndani ya kuta nne za bafu lile ambalo lilifanyiwa usafi wa kina, kiasi kwamba mtu angeweza kula mle bafuni, walioga kwa pamoja.
Bravo aliogeshwa kama mtoto mdogo. Alisuguliwa mwili mzima na dodoki laini, kisha akamwagiwa maji yaliyosuuza mapovu yote, hadi akawa safi kabisa. Akakaushwa kwa taulo laini, kisha akafunguliwa mlango arudi chumbani.
Bravo akatoka chumbani, Tunu akaendelea kuoga, dakika chache baadaye akatoka na kumfuata Bravo. Akaanza kumpaka mafuta mwilini. Ni hapo aligundua kuwa, mpenzi wake alikuwa na kucha ndefu kwenye vidole vya miguuni na mikononi.
Akachukua mashine ya kukatia kucha, akaanza kumkata kwanza kucha za vidole vya miguuni, alipomaliza akahamia kwenye vidole vya mikononi. Baada ya zoezi lile, akachukua chupa ndogo iliyokuwa na spiriti, akaweka kwenye kitambaa, akampata kwenye vidole vyote.
Baada ya hapo, akachukua chupa ya mafuta ya maji ya nazi, akampaka kwenye vidole vile, akarudisha mahali pake. Bravo alikuwa mgeni wa kila kitu.
“Baby hayo ni mafuta gani?”
“Mafuta ya nazi.”
“Yanasaidia nini?”
“Haya ni mafuta halisi, siyo ya kiwandani. Yanalainisha ngozi na kuondoa sugu, ndiyo maana nimekupaka baada ya kukupaka spirit. Sitaki uwe na ngozi iliyokomaa mpenzi wangu,” akasema Tunu akiachia tabasamu pana usoni mwake, lililosababisha vishimo mashavuni mwake vionekane.
“Tunu nimefanya uteuzi leo hii,” hatimaye Bravo akasema alilalama kwa mahaba.
“Uteuzi wa nini tena mpenzi?”
“Nimekuteua wewe kuwa nahodha wa penzi langu kuanzia leo hii. Kwa mambo unayonifanyia, mama nimekubali wewe ndiye uwe mwamuzi wa mwisho wa kila kitu kwenye idara ya mapenzi, maishani mwangu. Sema lolote, nitafuata,” akasema Bravo akitweta.
Tunu alitabasamu.
Moyoni akajisemea: “Na bado... hapa ni Tanga Bravo.”
Lakini hata hivyo, moyoni Tunu alianza kumpenda Bravo zaidi ya ilivyokuwa awali. Mwanzo alichukulia kawaida, lakini kwa namna siku zinavyozidi kwenda na namna Bravo anavyompa umuhimu, ndivyo naye mapenzi yalivyozidi kuongezeka moyoni mwake.
“Bravo naomba nikuambie ukweli baba.”
“Ukweli gani tena malkia?”
“Kadiri siku zinavyosonga ndivyo ninavyozidi kukupenda mpenzi. Naomba usiniache baba. Najua una mke, lakini naomba unipe nafasi yangu mpenzi,” akasema Tunu kwa sauti ya kudeka.
“Unapozungumza mambo ya maana, acha kabisa kumtaja mke wangu. Achana naye, ana mapungufu mengi, lakini nimemvumilia kwa muda mrefu. Nimekuwa na wewe kwa muda mfupi tu, lakini najiona kabisa nimekuwa mwanaume kamili, nimekuwa mpya kabisa mimi,” akasema Bravo.
“Nafurahi kusikia hivyo mpenzi.”
Walimaliza siku nzima wakiwa ndani, wakifurahia ulimwengu wa mapenzi. Mchana Tunu alitoka na kwenda kununua chakula hotelini, wakala pamoja chumbani. Bravo hakusita kumweleza ukweli kuwa, chakula kile hakina ladha kama mapishi yake.
“Kama utakuwepo usiku, nitakupikia mpenzi wangu,” akasema Tunu.
“Siyo kuwepo tu mpenzi, mimi leo nalala hapa hapa kwako,” akasema Bravo akitabasamu.
“Kweli?”
“Ndiyo.”
“Haya sema mwenyewe, unataka kula nini?”
“Kiukweli nina hamu sana na ubwabwa wa nazi,” akasema Bravo akijiramba.
“Hilo limepita, mboga?”
“Nataka mchicha wa kuchanganywa na nyama.”
“Usijali baba, hayo yote utayapata, andaa njaa yako mpenzi.”
Bravo akacheka!
Jioni, mishale ya saa 10, Tunu alitoka na kwenda sokoni. Akamwacha Bravo akiwa peke yake mle chumbani. Alikagua chumba cha Tunu, akajiridhisha kuwa, mwanamke yule alikuwa mwenye kupanga utaratibu wa mambo yake sawasawa!
Tunu aliporudi, alibadili nguo, akavaa dera na kwenda kukaa jikoni kukaangiza chakula. Saa 2: 00 usiku walikuwa chini kwenye mkeka uliotandikwa juu ya zulia, wakipata chakula.
Bravo alitaka wali nyama kwa mchicha, lakini mezani kulikuwa na zaidi ya mboga nne. Dagaa uono wa kukaanga, majani ya maboga yaliyoungwa kwa nazi, matembele na bamia na nyanya chungu (ngogwe) zilizopikwa kwa pamoja.
Bravo alizidi kujionea maajabu. Walipomaliza kula, Tunu aliweka bilauri la juisi ya ubuyu iliyochanganywa na hiliki na amdalasini. Bravo akazidi kuchanganyikiwa!
“Hivi ni kwa nini sikukuona mapema, nikakuoa wewe? Ulikuwa wapi siku zote wewe mwanamke?” Bravo akasema akirudisha glasi ya juisi mkekani.
ITANDELEA....
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 21
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
Bravo alitaka wali nyama kwa mchicha, lakini mezani kulikuwa na zaidi ya mboga nne. Dagaa uono wa kukaanga, majani ya maboga yaliyoungwa kwa nazi, matembele na bamia na nyanya chungu (ngogwe) zilizopikwa kwa pamoja.
Bravo alizidi kujionea maajabu. Walipomaliza kula, Tunu aliweka bilauri la juisi ya ubuyu iliyochanganywa na hiliki na amdalasini. Bravo akazidi kuchanganyikiwa!
“Hivi ni kwa nini sikukuona mapema, nikakuoa wewe? Ulikuwa wapi siku zote wewe mwanamke?” Bravo akasema akirudisha glasi ya juisi mkekani.
SASA ENDELEA...
“KILA kitu kina muda na sababu yake. Kwa sasa usijilaumu sana mpenzi, muhimu ni kutumia kila nukta moja iliyo mbele yako kwa faida. Huu ni wakati wetu wa kufurahi, siyo kuwaza kwa nini hatukuwahi kufurahia kabla ya leo,” akasema Tunu, akipeleka glasi yake ya juisi mdomoni.
“Una maneno matamu sana, yaani matamu kama wewe mwenyewe! Nakiri Tunu mbele yako, sina ujanja. Kama kupenda ni ubwege, mimi nimekubali kuwa bwege kwako. Na nitakuwa bwege kwelikweli mpaka watu waseme nimerogwa!”
Tunu akatabasamu!
Lakini alijijua alivyo. Ni kweli alikuwa mtaalamu hasa katika eneo lile, lakini kwa watu wa Bara huwa wanapagawa zaidi kwa sababu huwa wamekutana na mambo mapya kwao.
“Na kweli utarogeka kweli... wala hutarogwa kwa uchawi.... mapenzi tu,” akajisemea moyoni mwake Tunu akitabasamu.
Bravo alikuwa amefika Kigoma, mwisho wa reli! Hakuwa na ujanja tena. Kwa Tunu alikubali kuitwa majina yote.
“Halafu baby si umesema semina imeshaisha?” Tunu akauliza.
“Ndiyo imeisha tangu jana.”
“Kweli?”
“Ndiyo... tena wengine wameshaanza kuondoka kuanzia leo. Wengi wataondoka kesho.”
“Wewe utaondoka lini?”
“Nani?” Bravo akauliza kama vile swali lile halikuwa likimuhusu.
“Naongea na wewe Bravo, kumbe unadhani naongea na nani sasa?”
“Kwa kweli sijajua, ila ninachojua kesho asubuhi nitafuata mizigo yangu hotelini nihamishie hapa kwako!” akasema Bravo bila kupindisha maneno.
“Kweli kanasa, kanasa...” akawaza Tunu akimwangalia Bravo kwa macho ya mahaba.
“Yamekuwa hayo tena baba?” akasema Tunu akimtulizia macho Bravo.
“Ndiyo kwani hutaki?”
“Siyo kama sitaki ila namuwaza dada yangu Dar, atakuwa kwenye hali gani? Utasabisha agundue kuwa umepata mwanamke mpya na hapo ndio utakuwa umeharibu kila kitu,” akasema Tunu.
“Nimeshakuambia mara ngapi, unapozungumza na mimi usimtaje sana huyo mwanamke? Wewe achana naye... ni kweli ni mke wangu, lakini kwa sasa moyoni mwangu mke wangu ni wewe, ila kwa walimwengu mke wangu ni yeye. Wewe tulia, ufurahie maisha mpenzi wangu!” akasema Bravo akimwangalia Tunu kwa macho yaliyoonyesha ubembe wa mahaba.
Tunu hakujibu kitu!
Juisi ikaendelea kunyweka!
***
Viola alifunga mlango wake wa gari kwa nguvu, kisha akaingiza ufunguo kwenye mlango, akaweka loku. Akachomoa ufunguo, kisha akaanza kutembea kivivu kuelekea mlango mkubwa wa kuingia ndani kwake.
Aliingia akiwa mwenye mawazo mengi sana. Hapakuwa na dalili ya mume wake, Bravo kuwa amerudi. Alimpita msichana wake wa kazi pale sebuleni kama hakumuona. Hata alipomsalimia, hakuitika. Mawazo yake yalikuwa kwa mumewe, Bravo.
Alijifungia chumbani kwake, moyoni alihisi kama kuna kitu kinambana kwa nguvu kifuani. Hasira zilimpanda sana. Fikra juu ya mume wake zilimwandama. Ghafla bila hiyari yake, akashangaa machozi yakianza kutiririka machoni mwake.
Maumivu ya mapenzi yalimtesa. Kitu pekee alichohisi ni kwamba tayari mume wake alikuwa ameshatekwa na mwanamke mwingine. Bravo alikuwa ameanza tabia mpya ambazo hakuzizoea kabisa.
Bravo alikuwa mpya!
“Lazima ananichiti, lazima... siyo bure,” akasema kwa sauti ya chini, akiendelea kulia kwa kwikwi huku akipiga ngumi kwa nguvu kitandani.
Akachukua simu yake, akitaka kumpigia Bravo. Alikwenda kwenye jina la mumewe aliloliandika, ‘My Ice’, akataka kubonyeza kitufe cha kupiga, lakini akasita.
Akaamua aende WhatsApp. Akaangalia namba ya Bravo kama ipo hewani, akagundua haikuwa hewani. Akazidi kuchanganyikiwa!
Lakini akataka aandike ujumbe ili akutane nao baadaye atakapokuwa hewani, ila roho yake ikasita. Akakumbuka maelekezo ya shoga yake, Mariam. Kwamba asimsumbue kwa chochote!
“Sasa nawezaje kufanya hivyo jamani? Mume wangu mwenyewe, kwa nini anitese hivi lakini? Kweli wezi wanaweza kuwa na nafasi kuliko mimi mwenye mume?” akawaza Mariam akizidi kumwaga machozi machoni mwake.
Mwisho akaona isiwe tabu, bila kuoga, bila kula. Akaamua kulala!
“Bravo kama kweli umeamua kuvunja ahadi ya ndoa yetu sawa, endelea hivyo hivyo lakini moyo wangu unaumizwa sana na haya yanayoendelea... najua lazima mume wangu atakuwa amekamatwa na nyang’au!” akawaza akizidi kulia, akiwa kitandani mwake, akisaka usingizi.
Ataupata wapi?
***
Ni kweli Bravo alikuwa ameshikwa, akashikika. Asubuhi hii, ameamkia Chuda kwa mtoto wa Kitanga, Tunu. Tayari ameshaoga, ameshakunywa chai na ameshavaa tayari kwa kwenda hotelini kuchukua begi lake ili ahamie kwa Tunu!
Siku ya kurudi Dar haijulikani!
Haya mapenzi haya!
Jamaniiiii!
ITANDELEA....
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 22

NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
Ni kweli Bravo alikuwa ameshikwa, akashikika. Asubuhi hii, ameamkia Chuda kwa mtoto wa Kitanga, Tunu. Tayari ameshaoga, ameshakunywa chai na ameshavaa tayari kwa kwenda hotelini kuchukua begi lake ili ahamie kwa Tunu!
Siku ya kurudi Dar haijulikani!
Haya mapenzi haya!
Jamaniiiii!
SASA ENDELEA...

“UMEAMKAJE mpenzi wangu?” Bravo akamsalimia Tunu asubuhi hii baada ya kuamka.
“Salama baby, shikamoo...” Tunu akamsalimia kwa adabu, akipiga goti kidogo.
“Marahaba mtoto mzuri.”
“Vipi uchovu baby, najua umechoka sana!”
“Kiasi mama, wala usijali. Vipi wewe?”
“Nipo sawa. Ratiba yako inasomekaje?”
“Hapa natakiwa kwenda hotelini nikachukue mizigo yangu, ni hivyo tu. Wewe je?”

“Mimi ilikuwa niende kazini, lakini siendi tena. Acha nikusindikize hotelini,” akasema Tunu.
Bravo akaishia kutabasamu!
Kilichofuata ilikuwa ni Tunu kuandaa kifungua kinywa haraka haraka, kisha wakakaa mezani na kufurahia pamoja chakula hicho. Wakajiandaa na kuongozana kwenda hotelini.
Mle hotelini, hapakuwa na mgeni yeyote kati ya wale waliokuwa wamekwenda kwenye semina Tanga. Bravo alielezwa hayo na dada wa Mapokezi aitwaye Eliza.
“Walibaki watatu tu, ambao wameondoka asubuhi hii na Ratco.”
“Mh mpaka basi walilopanda umejua... umejuaje sasa?”
“Walituomba tuwafanyie booking, ndiyo maana nikajua.”

“Basi poa, mimi naondoka leo mchana. Nimefuata mizigo yangu!”
“Sawa,” akasema Eliza, kisha akamuita mwenzake, Queen ambaye alimpa ufunguo wa Bravo, wakaongozana hadi chumbani.
Bravo akakukusanya kila kilicho chake na kutoka navyo. Akaagana na Eliza, kisha akarudi kwenye gari alipokuwa amemuacha Tunu, safari ya kurudi Chuda, nyumbani kwa Tunu ikaanza.
Hakujali ubora wa chumba cha Tunu, alichojua yeye ni mapenzi tu. Siku nzima walijifungia ndani. Ilipofika jioni, Bravo alitoa wazo la kutoka out.

“Ni sawa mpenzi, nitafurahi sana,” akasema Ttunu akionyesha kufurahi.
Walijiandaa vizuri, kisha usiku wa saa nne, gari la kuwapeleka kiwanja lilikuwa nje ya nyumba anayoishi Tunu.
“Upo tayari mama?”
“Nipo tayari baba.”
Bravo alipigilia suruali ya jeans ya rangi nyeusi na fulana ya kubana nyeupe. Tunu alivaa sketi fupi ya njano na kitopu cheusi. Walikuwa wamependeza sana! Kwa kuwatazama tu, hapakuwa na haja ya kuuliza kama walikuwa wapenzi.
Wakaingia kwenye gari na kuondoka Chuda. Kwao ilikuwa ni furaha tupu. Hawakujali wala kufikiria kuhusu Viola.
***

“Haya nipe habari ya nyumbani?” alikuwa ni Mariam akimuuliza Viola walipokutana asubuhi hiyo kazini.
“Shoga yangu mambo mabaya.”
“Vipi tena?”
“Jamaa hajarudi.”
“Weee hajarudi kweli?” akauliza Mariam kwa mshangao wa hali ya juu.
“Ndiyo hajarudi, jana nimesubiri sana. Nimejiandaa kumpokea mume wangu lakini hakutokea. Kiukweli nimelia sana. Nimelala bila kula wala kuoga. Moyo wangu unaniuma sana kwa hiki kinachotokea kwenye ndoa yangu,” akasema Tunu.

“Unakumbuka nilichokuambia lakini?”
“Nakumbuka vizuri sana.”
“Basi tulia mtoto wa kike, ukiona giza nene sana ujue asubuhi imekaribia. Tuliza moyo wangu. Cha muhimu kwa leo, naona nenda kaangalie hii CD ya Anti Zuh,” akasema Mariam akimkabidhi Viola CD.

“Asante sana shoga yangu.”
“Kila kitu kipo humo, nenda kaangalie kwa makini, kwa lengo la kujifunza, kuna mambo muhimu sana utayavuna kupitia hii CD,” akasema Mariam.
“Sawa, nashukuru sana.”
Siku ilikuwa ngumu sana kwa Viola. Haikuwa rahisi kuimaliza akiwa kazini. Akaomba ruhusa mchana na kurudi zake nyumbani. Alikuwa na matumaini ya kumpokea mumewe siku hiyo.

Alifikia kwenye runinga yake, akaweka CD ya Anti Zuh na kuanza kuangalia. Ni kama alivyosema Mariam, ilikuwa CD nzuri sana yenye mafundisho makubwa sana kwa wanandoa.
Alijifunza kuhusu kauli njema za mahaba, kumpetipeti mwanaume na mambo mengine mengi ya mapenzi. Mwishowe alichanganyikiwa zaidi na mafundisho ya staili 30 za mapenzi zinazopagawisha faragha!
Kwanza hakutegemea kama kulikuwa na staili thelathini za mapenzi. Yeye alijua staili tano tu, lakini Anti Zuh alionyesha staili thelathini na ladha zake. Yalikuwa mafundisho ya kipekee sana.

Kwamba, kumbe kuna staili maalumu za watu wanene, wafupi, wenye vitambi, wembamba, waliojaliwa mambo, na wenye vidubwana vidogo!
“Haaa! Mbona pambe?” akajisemea moyoni mwake Viola wakati akikodoa macho kwenye runinga.
Somo lilimuingia barabara, kuna wakati alisahau kama alikuwa na shauku na mumewe na alikuwa akimsubiri kwa hamu. Zilikuwa hisia za muda tu. Mara baada ya somo lile kufika mwisho, alijikuta akipandwa na hasira ya wivu wa mapenzi.

Alimtaka Bravo wake!
Alikuwa na dawa yake!
“Kwa darasa hili, Bravo akiwa na mimi mara moja tu, kamwe hawezi tena kutoka nje ya ndoa, hawezi. Dawa yake ninayo. Namtaka Bravo wangu,” akajisemea moyoni mwake, machozi ya huba yakimtoka machoni.

Kama ni kuvumilia; alivumilia sana, sasa uzalendo ulimshinda. Ilikuwa lazima awasiliane na Bravo wake. Akaingia kwenye ukurasa wa Bravo kwenye mtandao wa WhatsApp, akataka kuandika kitu kumuuliza kilichompata mumewe.

Wakati anaanza kuandika neno, ‘mume wangu Bravo...’ akaona maandishi yakipita juu ya ukurasa ule yakisomeka, ‘Sweet hubby is typing...’.
Akashtuka sana!
Hakutegemea kama Bravo angeweza kumwandikia ujumbe wakati ule. Akabaki anasubiri kwa hamu ujumbe wa Bravo.
Angejua!
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 23
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
Wakati anaanza kuandika neno, ‘mume wangu Bravo...’ akaona maandishi yakipita juu ya ukurasa ule yakisomeka, ‘Sweet hubby is typing...’.
Akashtuka sana!
Hakutegemea kama Bravo angeweza kumwandikia ujumbe wakati ule. Akabaki anasubiri kwa hamu ujumbe wa Bravo.
Angejua!
SASA ENDELEA...
‘SWEET hubby is typing...’ maneno hayo yalibaki kwa muda mrefu juu ya kioo cha simu yake. Kuna wakati yaliacha, kisha yakarudi tena, kuonesha kuwa alikuwa akiandika ujumbe mrefu sana.
Moyo ulimuenda mbio Viola, akiwa na shauku ya kujua kilichokuwa kikiandikwa na mume wake. Aliyatoa macho yake kwenye kioo cha simu yake bila kuyabandua hata kwa sekunde moja.
Mara ujumbe ukaingia...
Ujumbe wenyewe ulisomeka: “Viola samahani kwa kutokukujulisha mapema. Ukweli ni kwamba semina iliisha tangu juzi, lakini nilishindwa kuja jana na leo kwa sababu kuna mambo nayashughulikia huku Tanga.
“Nitakuwa huku kwa siku moja zaidi. Keshokutwa nitarudi nyumbani. Asante pia kwa utulivu wako. Angalau sasa nimekuwa na amani.”
Viola alitulia kwa muda akitafakari. Mume wake anamwambia anamshukuru kwa kutulia kwa sababu amekuwa ana amani!
Jambo hilo lilimuumiza sana moyo wake, aligundua kuna kitu hakipo sawa. Alitakiwa kumjibu mumewe, lakini alitakiwa kutumia akili ya ziada.
Maneno ya kuudhi kwa wakati ule hayakutakiwa kabisa. Alitakiwa kutumia busara na kumjibu mumewe kwa kauli njema.
“Mume wangu Bravo, mimi huwa nakunyima amani baba?” akauliza Viola kwenye ujumbe wake wa WhatsApp.
“Ndiyo, lakini sasa nimefurahi umerekebika.”
“Nisamehe mume wangu kwa hilo, lakini huwa si lengo langu kukuharibia furaha yako.”
“Kama umegundua hilo ni vema, maana umebadilika na nimekuwa na amani sasa.”
“Uko wapi lakini mume wangu kwa sasa?” akauliza Viola.
“Umeshaanza sasa mambo yako.”
“Basi mume wangu, lakini ni makosa kukuuliza ulipo baba, eeeh Bravo?”
“Siyo makosa.”
“Bali?”
“Makosa yanasababishwa na uulizaji wako. Lazima ujue kuwa wewe ni mke wangu na unapaswa kuwa chini ya himaya yangu. Lazima mwanamke awe chini ya mamlaka ya mwanaume wake na siyo kama unavyofanya wewe.”
“Samahani mume wangu. Nina ombi moja.”
“Ombi gani tena?”
“Naomba kusikia sauti yako hubby. Niruhusu nikupigie tafadhali.”
“Hatuwezi kuongea maana nipo kwenye kelele muda huu.”
“Kelele? Usiku huu mpenzi? Nilijua labda uko hotelini!”
“Hapana, sipo hotelini. Nimetoka kidogo.”
“Sasa uko wapi Bravo?”
“Huwezi kupajua, lakini nipo baa.”
“Baa?”
“Ndiyo Viola, nipo baa.”
“Mh! Bravo mume wangu ndio majibu gani sasa hayo baba?”
“Mabaya?”
“Unaona ni majibu mazuri ya kumjibu mke wako?”
“Mimi sioni tatizo, lakini inawezekana kuwa ni tatizo ila mimi nakujibu kulingana na namna wewe unavyouliza.”
“Basi nakuomba mume wangu rudi hotelini!”
“Umesema?”
“Rudi hotelini nakuomba.”
Bravo akamtumia emoji za kuonyesha anacheka kisha akaunganisha na maneno: “Kumbe nimefanya vibaya kukutafuta siyo?”
“Samahani mume wangu.”
Baada ya ujumbe huo, Bravo hakujibu kitu tena. Hata kwenye ukurasa wake hakuonekana akiandika. Baada ya dakika mbili, Bravo akaondoka hewani!
“Mume wangu amepatwa na nini? Mbona amekuwa na tabia mpya siku hizi? Anawezaje kuwa baa muda huu akawa peke yake bila mwanamke? Lazima mume wangu atakuwa ameshikwa na mwanamke, lazima kuna kitu kinaendelea kwenye maisha ya mume wangu kwa sasa,” akawaza Viola akiwa amejilaza kimya, mawazo tele kichwani mwake yakimzonga.
Ni kweli alikuwa mwenye maumivu makali, lakini hakuwa na namna ya kukabiliana nayo kwa wakati huo. Alitakiwa kutuliza kichwa chake na kupumzika. Ni kweli kuna kitu kilikuwa kinaendelea...
Hilo alikuwa na uhakika nalo kwa asilimia mia moja. Akajibembeleza kupata usingizi... japo kwa tabu, lakini alifanikiwa kulala.
Tayari ilikuwa ni saa saba na nusu usiku!
***
“Utapenda kuku wa kuchemsha au kukaanga?” Bravo alimwuliza Tunu, akiwa ameshika glasi yake ya bia ya baridi.
“Wewe utakula nini?”
“Kwa hizi bia, lazima nipate kitu cha mchemsho ndiyo nitakuwa sawa, wewe kula unachopenda.”
“Ni kweli baby natakiwa kula ninachopenda, lakini nilivyofundishwa, anachopenda mumeo lazima na wewe ukipende. Hivyo basi na miye pia nitakula kama wewe,” akasema Viola akimwangalia Bravo usoni.
“Mh! Kweli mpenzi?”
“Ndiyo.”
“Haya bwana kama ndivyo.”
“Halafu mbona umekuwa busy sana na simu, ulikuwa unachati na nani?”
“Dada yako!”
“Kama ni yeye sawa, ana nafasi yake na ninatakiwa kumheshimu kwa sababu nimemkuta,” akasema Viola kwa sauti laini, akiitoa kwa nguvu ili kushindana na sauti ya muziki iliyokuwa ikitumbuiza.
Bravo hakujibu kitu, zaidi alimuita mhudumu wa jikoni. Alipofika tu mezani kwao, bila kupoteza muda, akatoa oda zao...
“Tunahitaji mchemsho wa kuku.”
“Ngapi?”
“Mbili.”
“Poapoa bosi.”
“Iwe kienyeji, usije kuleta kuku wa Kizungu hapa, nitakurudisha nao. Usije kuniharibia uzuri wa mke wangu mpenzi. Hivi unavyomuoa, ametunzwa na vitu vya kienyeji, siyo vya madawa,” akasema Bravo akionyesha mizaha.
“Mzee hapa kwetu tunauza kitu cha kienyeji tu.”
Bravo hakuwa na muda wa kujibu kitu!
ITANDELEA....
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 24
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
“Iwe kienyeji, usije kuleta kuku wa Kizungu hapa, nitakurudisha nao. Usije kuniharibia uzuri wa mke wangu mpenzi. Hivi unavyomuoa, ametunzwa na vitu vya kienyeji, siyo vya madawa,” akasema Bravo akionyesha mizaha.
“Mzee hapa kwetu tunauza kitu cha kienyeji tu.”
Bravo hakuwa na muda wa kujibu kitu!
SASA ENDELEA...
KAMA ni bata, Bravo na Tunu walikula bata la maana. Walikula na kunywa huku wakifurahia burudani nzuri ya muziki hadi saa tisa usiku walipokodisha taksi na kurejea nyumbani kwa Tunu, Chuda.
“Sijawahi kupata raha kama leo, kweli umeniwezea mpenzi wangu!” akasema Tunu wakati wakiwa kwenye taksi wanarudi nyumbani.
“Kawaida mpenzi wangu...” akajibu Bravo.
“Kiukweli kutoka moyoni mwangu, nakuambia Bravo mimi na ujanja wangu nilikuwa sijawahi kutoka usiku. Ni mara yangu ya kwanza, lakini yenye maana sana kwangu. Umeacha kumbukumbu nzuri sana kwangu mpenzi. Umenifanya nijihisi mwanamke kamili. Asante sana baba,” akasema Tunu akiwa amelala kifuani mwa Bravo.
“Tunu wangu,” Bravo akaita.
“Yes baby,” akaitikia Tunu kwa sauti ya kudeka.
“Hiyo ni rasharasha mama, mvua inakuja mpenzi. Wewe subiri tu utakula bata si la nchi hii. Maadamu nimekupenda, nakuhakikishia nitayafanya maisha yako yenye thamani kama mwenyewe ulivyo,” akasema Bravo.
“Kweli mpenzi?”
“Nakuambia Tunu, umekutana na pesa uso kwa uso. Ni kazi yako kujilia vyako utakavyo,” akasema Bravo.
Walipofika nyumbani, Bravo alimlipa dereva kisha wakashuka na kuingia ndani. Hawakuwa na muda wa kuoga. Walivua nguo zao, kisha wakajitupa kitandani. Ilifanyika faulo moja ya aina yake!
Bila kuandaa mazingira ya mechi, wala kupasha viungo, wakaingia uwanjani. Hapakuwa na refa, mechi ikachezwa kwa uangalizi maalum wa wachezaji wenyewe. Ilikuwa fair play!
Awali ilitegemewa ingekuwa mechi ya dakika 90 kama ilivyo kawaida kwenye mechi zote za mchezo wa soka, lakini kwao ilikuwa tofauti. Hawakumaliza hata dakika kumi, mchezo ulikuwa umekwisha!
Kwenye ubao wa matangazo kulisoma sare ya 1-1. Wakakubaliana kuwa kweli wote walikuwa wakali kwenye game.
“Hivi nitawezaje kukuacha wewe mtoto?” Bravo akasema kwa sauti tulivu akionekana kupagawa.
“Kwani una mpango wa kuniacha?”
“Nikuache nimelogwa?”
“Basi huna sababu ya kujiuliza swali hilo.”
“Kweli kwako nimefika na unanijulia kwa kila hali mpenzi, ila ninachojilaumu ni kutokukujua wewe mtoto muda mrefu kabla. Ulikuwa wapi mpenzi?” akasema Bravo.
“Kila kitu kina muda na sababu zake mpenzi. Nadhani huu ndiyo muda mwafaka wa sisi kufurahia penzi letu,” akasema Tunu.
Walikumbatiana kwa nguvu, wakiwa ndani ya shuka laini, feni ikiwapuliza taratibu. Sauti zao za maongezi zikaanza kubadilika mmoja baada ya mwingine.
Walianza kuzungumza kwa sauti ya kukatakata, kisha wote wakapitiwa na usingizi wakiwa wamekumbatiana!
***
Tunu alikuwa wa kwanza kuamka. Muda ulikuwa umeshakwenda sana. Saa ya ukutani ilionyesha kuwa tayari ilikuwa ni saa nne na dakika zake za asubuhi. Mwili haukuwa na nguvu kabisa.
Akamuamsha Bravo, ambaye alionekana kuwa na mning’inio mkubwa wa pombe za jana yake. Bravo alishtuka kuona amechelewa kuamka.
“Shikamoo baby,” Tunu akamsalimia.
“Marahaba kipenzi changu. Vipi ni saa ngapi sasa?” akauliza Bravo.
“Muda umekwenda sana baba. Ni saa nne inaelekea tano!”
“Duh! Mbona hukuniamsha sasa jamani?”
“Hata mimi ndiyo nimeamka muda huu.”
“Basi tena, itabidi safari iwe kesho. Leo nitafanya maandalizi tu!” akasema Bravo.
“Haitakuletea shida kwa mkeo?” akauliza Tunu.
“Nilishakukataza kumtaja huyo mtu tunapozungumzia mambo yetu ya maana!”
“Basi samahani mpenzi wangu.”
“Hilo limeshapita.”
“Enhee sasa kinachofuata?” Tunu akamwuliza Bravo.
“Nadhani tuoge tutoke kidogo, kuna mahali nataka unisindikize.”
“Sasa si niandae chai kwanza?”
“Hapana, tutakupata kifungua kinywa hotelini, usijichoshe mpenzi wakati jana usiku tulirudi muda mbaya!” akasema Bravo kwa sauti ya kubembeleza.
“Sawa mpenzi, asante pia kwa kujali.”
Ndivyo ilivyokuwa, maandalizi yalifanyika haraka, walipokuwa tayari walitoka. Safari yao ikaishia mjini ambapo waliingia kwenye duka la mavazi.
“Chagua kitu chochote unachotaka ndani ya duka hili mpenzi,” Bravo akamwambia Tunu.
Tunu hakujivunga, alichagua nguo kama pea tano, Bravo akamwambia haitoshi. Naye akamchangulia pea nyingine tano; hiyo ilikuwa kuanzia nguo, viatu na pochi.
Bravo akalipa, wakachukua mizigo yao na kuondoka. Safari hii waliekea katika soko la Ngamiani. Bravo akamnunulia mahitaji mbalimbali ya vyakula vya nyumbani.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, wakaingia kwenye gari na kurudi zao Chuda. Walipofika, walishusha vitu na kuviingiza ndani. Baada ya kuingiza mizigo yote, Tunu alifunga mlango na kitasa.
Akamfuata Bravo kwenye kochi alilokuwa amekaa, akamwonyesha ishara kuwa asimame. Bravo akasimama. Akamwongoza hadi kitandani, akamkalisha.
“Bravo mpenzi,” Tunu akaita kwa sauti iliyojaa mahaba, akiwa ameyalegeza macho yake.
“Naam mpenzi wangu.”
“Kwa nini unanifanyia yote haya?” Tunu akauliza.
“Ni kwa sababu mbili; kwanza nakupenda kwa dhati, halafu pia unanipa mapenzi ambayo sijawahi kuyapata tangu kuzaliwa!”
“Sasa sikiliza Bravo, kama ni mapenzi, nadhani nimekuonyesha robo tu ya ujuzi wangu. Sasa nakuahidi nitakachokufanyia sasa hivi, ndiyo nitakuwa nimeonyesha angalau nusu ya ujuzi nilionao. Naomba ufuate maelekezo yangu yote nitakayokupa!” akasema Tunu akihema taratibu, macho yake yakianza kutiririsha machozi.
Bravo alipagawa!
ITANDELEA....
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 17
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
“Utashindwa wewe kaka. Viwanja vipo, ni wewe tu uamue unataka mjini, nje kidogo ya mji au nje kabisa ya mji. Chaguo ni lako!” akasema Nyumbanyingi.
Unashangaa nini?
Ni kiwanja cha Tunu kinatafutwa!
SASA ENDELEA...
“WAPI naweza kupata kiwanja kizuri katika eneo ambalo tayari limepangwa?” Bravo akamwambia Nyumbanyingi.
“Kange ni pazuri sana, kule kumekucha!”
“Siyo nje sana ya mji?”
“Hapana, ndipo stendi kubwa ya mabasi ya mikoani ilipohamishiwa. Ni eneo la washua, linakufaa sana!” akasema Nyumbanyingi.
“Tunaweza kwenda kupaona?”
“Hakuna shida, muhimu utoe mguu tu, tutakwenda.”
“Mguu ndiyo nini?” akauliza Bravo akitabasamu.
“Ni tozo ya kunitoa kijiweni kaka. Ishirini inatosha.”
“Hiyo haina shida.”
“Halafu ukilipia kiwanja unanipa asilimia kumi.”
“Haina shida, muhimu nikipende tu.”
“Basi twende zetu!”
Bravo akakodi Bajaj iliyowapeleka mpaka Kange ambapo alionyeshwa viwanja tofauti zaidi ya vitatu, akaridhika na kimoja kilichokuwa pembeni kabisa, eneo lenye miti mingi.
“Napenda sana hewa nzuri, hapa pananifaa,” akasema Bravo.
“Sasa tunafanyaje? Uko tayari tayari nimuite mhusika?” akauliza Dalali Nyumbanyingi.
“Mimi nipo tayari,” akasema Bravo.
“Subiri.”
Kweli Dalali Nyumbanyingi akainua simu na kuzungumza na mtu aliyesema ni mmiliki wa kiwanja hicho. Mwisho wa mazungumzo yao kwenye simu, ilionekana walikubaliana kuwa angefika eneo hilo baada ya muda mfupi.
“Amesema atafika hapa baada ya nusu saa!” akasema Dalali Nyumbanyingi.
“Amesema hayupo mbali sana?”
“Hapana, yupo mjini.”
“Poa, basi tutafute mahali tumsubiri, akifika atakupigia,” akasema Bravo.
“Poa.”
Jirani na eneo lile kulikuwa na mgahawa, wakaingia hapo kumsubiri mmiliki wa kiwanja kile. Wakati haya yanafanyika, Tunu hakuwa na habari kabisa!
***
Vipimo vya maabara vilitoka, Viola hakuwa akiugua chochote. Alikuwa mzima wa afya. Daktari alimwambia hapakuwa na sababu ya kupewa dawa kwa sababu hawakugundua chochote kwenye damu yake.
“Lakini sijisikii vizuri daktari,” akasema Viola.
“Unalala vya kutosha kweli?”
“Hapana, nina siku ya tatu sasa sijalala vizuri.”
“Unakula vizuri?”
“Kwa kweli kwa siku mbili hizi sizingatii sana.”
“Unaonekana una tatizo jingine nje ya maradhi ya kawaida. Nahisi una mawazo sana, nini kinakusumbua?” daktari akamwuliza akimwangalia usoni.
“Ni kweli daktari, nina matatizo ya kifamilia, yaninyima amani, nashindwa kulala!” akasema Viola.
“Pole sana, lakini hupaswi kuwa hivyo. Jitahidi kulala kadiri uwezavyo kupumzisha kichwa chako. Lala mapema, kula kwa mpangilio, utakuwa sawa kabisa, lakini usinywe dawa yoyote, huna tatizo.”
Viola alirudi nyumbani akiwa amepata ushauri wa daktari. Kweli aliamua kutulia, alijiamuru kuacha kumfuatilia zaidi mumewe. Aliamua kumpa muda. Lakini ili kutafuta faraja ya moyo wake, aliona ni bora ampigie shosti wake, Mariam ili amuombe ushauri.
Mariam ni msichana ambaye alikuwa akifanya naye kazi ofisi moja. Mara moja akampigia na kumweleza kuhusu mkasa mzima wa mume wake. Hakutaka kumficha chochote, aliamua kuwa huru kwake ili aweze kumpa ushauri utakaofaa.
“Kwani hiyo tabia alikuwa nayo siku nyingi?” akauliza Mariam.
“Hapana, ana kama siku tatu sasa. Kifupi ni tabia mpya, ambayo ameanza baada ya kwenda Tanga kikazi!” akasema Viola.
“Basi kwa vyovyote vile, kuna kitu kipya anafanya Tanga. Kipo kitu kilichombadilisha, ndiyo maana amekubadilikia,” akasema Mariam.
“Kweli?”
“Naamini hivyo. Unadhani kwa nini abadilike ghafla? Na ninavyoijua Tanga, kama ni kweli amenasa mahali, kunahitajika nguvu kubwa sana kumrudisha!”
“Sasa unanishauri nifanye nini shosti wangu?” Viola akauliza kwa shauku.
“Tuliza moyo wako shoga yangu, kwa sasa tulia, ukija kesho kazini tutayajenga vizuri mama. Wewe pumzika tu!” akasema Mariam.
“Haya asante sana shoga yangu, maana haya mambo ni mazito kwangu wala si madogo!”
“Usijali, nipo kukusaidia best.”
Wakakata simu zao.
Viola alishusha pumzi.
Alipata ahueni kubwa baada ya kuzungumza na Mariam, ambaye alimpa mwanga wa mahali pa kuanzia. Aliamua kujiongeza mwenyewe, akaamua kutomtafuta kabisa mume wake, Bravo hadi atakapoamua mwenyewe kumpigia...
“Nitafanya hivyo kama sehemu ya kumpima alivyo kwa sasa,” akajisemea moyoni mwake.
Viola alishikilia msimamo huo.
***
Mzee Shekoloa, mmiliki wa kiwanja kile alifika eneo lile na kuwasiliana na Dalali Nyumbanyingi. Bila kupoteza muda, wakakubaliana bei. Bahati nzuri, bei haikuwa kubwa, hivyo hawakuvutana sana.
“Sasa unalipia leoleo au?” akauliza Mzee Shekoloa.
“Hapana baba, ni kesho. Ningeweza kulipa leo, lakini mtu ninayemchukulia sijampanga. Nitakuja naye kesho!” akasema Bravo.
“Kwa hiyo hiyo kesho unakuja na hela kabisa?”
“Hapana.... nitakuja tuandikishiane hapa, kisha ama nitakupa cheki au tuongozane benki nikakuhamishie kwenye akaunti yako au hata ukitaka keshi, lakini benki,” akasema Bravo.
“Sawa, hakuna shida! Kesho saa ngapi sasa?”
“Saa nne asubuhi tukutane hapa. Mzee lakini nitapenda tuandikishiane ofisini kwa mtendaji au serikali ya mtaa!” akasema Bravo.
“Huo ndiyo utaratibu kijana wangu, naujua wala usiwe na shaka na hilo kabisa,” akasema Mzee Shekoloa.
***
“Hivi baby unajua sababu za kutaka majina yako yote matatu?” Bravo alikuwa anaongea na Tunu kwenye simu, muda mfupi baada ya kuachana na Dalali Nyumbanyingi, Barabara ya 12.
“Hapana mpenzi wangu.”
“Utajua kesho... naomba kesho uombe ruhusa, kuna mahali tunakwenda saa 3 asubuhi!”
“Kuna nini?”
“Utajua kesho hiyohiyo! Wewe jiandae tu.”
“Mh!” Tunu akaguna.
ITANDELEA....
Asee ndio maana wake wanatakiwa kuwa watu wa maombi sana kutuombea sisi
 
HILIKI YA CHUMBAGENI – 24
NA JOSEPH SHALUWA
ILIPOISHIA...
“Iwe kienyeji, usije kuleta kuku wa Kizungu hapa, nitakurudisha nao. Usije kuniharibia uzuri wa mke wangu mpenzi. Hivi unavyomuoa, ametunzwa na vitu vya kienyeji, siyo vya madawa,” akasema Bravo akionyesha mizaha.
“Mzee hapa kwetu tunauza kitu cha kienyeji tu.”
Bravo hakuwa na muda wa kujibu kitu!
SASA ENDELEA...
KAMA ni bata, Bravo na Tunu walikula bata la maana. Walikula na kunywa huku wakifurahia burudani nzuri ya muziki hadi saa tisa usiku walipokodisha taksi na kurejea nyumbani kwa Tunu, Chuda.
“Sijawahi kupata raha kama leo, kweli umeniwezea mpenzi wangu!” akasema Tunu wakati wakiwa kwenye taksi wanarudi nyumbani.
“Kawaida mpenzi wangu...” akajibu Bravo.
“Kiukweli kutoka moyoni mwangu, nakuambia Bravo mimi na ujanja wangu nilikuwa sijawahi kutoka usiku. Ni mara yangu ya kwanza, lakini yenye maana sana kwangu. Umeacha kumbukumbu nzuri sana kwangu mpenzi. Umenifanya nijihisi mwanamke kamili. Asante sana baba,” akasema Tunu akiwa amelala kifuani mwa Bravo.
“Tunu wangu,” Bravo akaita.
“Yes baby,” akaitikia Tunu kwa sauti ya kudeka.
“Hiyo ni rasharasha mama, mvua inakuja mpenzi. Wewe subiri tu utakula bata si la nchi hii. Maadamu nimekupenda, nakuhakikishia nitayafanya maisha yako yenye thamani kama mwenyewe ulivyo,” akasema Bravo.
“Kweli mpenzi?”
“Nakuambia Tunu, umekutana na pesa uso kwa uso. Ni kazi yako kujilia vyako utakavyo,” akasema Bravo.
Walipofika nyumbani, Bravo alimlipa dereva kisha wakashuka na kuingia ndani. Hawakuwa na muda wa kuoga. Walivua nguo zao, kisha wakajitupa kitandani. Ilifanyika faulo moja ya aina yake!
Bila kuandaa mazingira ya mechi, wala kupasha viungo, wakaingia uwanjani. Hapakuwa na refa, mechi ikachezwa kwa uangalizi maalum wa wachezaji wenyewe. Ilikuwa fair play!
Awali ilitegemewa ingekuwa mechi ya dakika 90 kama ilivyo kawaida kwenye mechi zote za mchezo wa soka, lakini kwao ilikuwa tofauti. Hawakumaliza hata dakika kumi, mchezo ulikuwa umekwisha!
Kwenye ubao wa matangazo kulisoma sare ya 1-1. Wakakubaliana kuwa kweli wote walikuwa wakali kwenye game.
“Hivi nitawezaje kukuacha wewe mtoto?” Bravo akasema kwa sauti tulivu akionekana kupagawa.
“Kwani una mpango wa kuniacha?”
“Nikuache nimelogwa?”
“Basi huna sababu ya kujiuliza swali hilo.”
“Kweli kwako nimefika na unanijulia kwa kila hali mpenzi, ila ninachojilaumu ni kutokukujua wewe mtoto muda mrefu kabla. Ulikuwa wapi mpenzi?” akasema Bravo.
“Kila kitu kina muda na sababu zake mpenzi. Nadhani huu ndiyo muda mwafaka wa sisi kufurahia penzi letu,” akasema Tunu.
Walikumbatiana kwa nguvu, wakiwa ndani ya shuka laini, feni ikiwapuliza taratibu. Sauti zao za maongezi zikaanza kubadilika mmoja baada ya mwingine.
Walianza kuzungumza kwa sauti ya kukatakata, kisha wote wakapitiwa na usingizi wakiwa wamekumbatiana!
***
Tunu alikuwa wa kwanza kuamka. Muda ulikuwa umeshakwenda sana. Saa ya ukutani ilionyesha kuwa tayari ilikuwa ni saa nne na dakika zake za asubuhi. Mwili haukuwa na nguvu kabisa.
Akamuamsha Bravo, ambaye alionekana kuwa na mning’inio mkubwa wa pombe za jana yake. Bravo alishtuka kuona amechelewa kuamka.
“Shikamoo baby,” Tunu akamsalimia.
“Marahaba kipenzi changu. Vipi ni saa ngapi sasa?” akauliza Bravo.
“Muda umekwenda sana baba. Ni saa nne inaelekea tano!”
“Duh! Mbona hukuniamsha sasa jamani?”
“Hata mimi ndiyo nimeamka muda huu.”
“Basi tena, itabidi safari iwe kesho. Leo nitafanya maandalizi tu!” akasema Bravo.
“Haitakuletea shida kwa mkeo?” akauliza Tunu.
“Nilishakukataza kumtaja huyo mtu tunapozungumzia mambo yetu ya maana!”
“Basi samahani mpenzi wangu.”
“Hilo limeshapita.”
“Enhee sasa kinachofuata?” Tunu akamwuliza Bravo.
“Nadhani tuoge tutoke kidogo, kuna mahali nataka unisindikize.”
“Sasa si niandae chai kwanza?”
“Hapana, tutakupata kifungua kinywa hotelini, usijichoshe mpenzi wakati jana usiku tulirudi muda mbaya!” akasema Bravo kwa sauti ya kubembeleza.
“Sawa mpenzi, asante pia kwa kujali.”
Ndivyo ilivyokuwa, maandalizi yalifanyika haraka, walipokuwa tayari walitoka. Safari yao ikaishia mjini ambapo waliingia kwenye duka la mavazi.
“Chagua kitu chochote unachotaka ndani ya duka hili mpenzi,” Bravo akamwambia Tunu.
Tunu hakujivunga, alichagua nguo kama pea tano, Bravo akamwambia haitoshi. Naye akamchangulia pea nyingine tano; hiyo ilikuwa kuanzia nguo, viatu na pochi.
Bravo akalipa, wakachukua mizigo yao na kuondoka. Safari hii waliekea katika soko la Ngamiani. Bravo akamnunulia mahitaji mbalimbali ya vyakula vya nyumbani.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, wakaingia kwenye gari na kurudi zao Chuda. Walipofika, walishusha vitu na kuviingiza ndani. Baada ya kuingiza mizigo yote, Tunu alifunga mlango na kitasa.
Akamfuata Bravo kwenye kochi alilokuwa amekaa, akamwonyesha ishara kuwa asimame. Bravo akasimama. Akamwongoza hadi kitandani, akamkalisha.
“Bravo mpenzi,” Tunu akaita kwa sauti iliyojaa mahaba, akiwa ameyalegeza macho yake.
“Naam mpenzi wangu.”
“Kwa nini unanifanyia yote haya?” Tunu akauliza.
“Ni kwa sababu mbili; kwanza nakupenda kwa dhati, halafu pia unanipa mapenzi ambayo sijawahi kuyapata tangu kuzaliwa!”
“Sasa sikiliza Bravo, kama ni mapenzi, nadhani nimekuonyesha robo tu ya ujuzi wangu. Sasa nakuahidi nitakachokufanyia sasa hivi, ndiyo nitakuwa nimeonyesha angalau nusu ya ujuzi nilionao. Naomba ufuate maelekezo yangu yote nitakayokupa!” akasema Tunu akihema taratibu, macho yake yakianza kutiririsha machozi.
Bravo alipagawa!
ITANDELEA....
[emoji16][emoji16][emoji16]hila wanawake sisi aya tunu endelea kushikilia kombe
 
Mtunzi wa umu nae ametukimbia au[emoji26]
 
Back
Top Bottom