Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 86
Kwa upande wa Neema aliamini kuwa mwanae angeenda nyumbani kwa siku hiyo na angechukua ushauri aliopewa na mama Pendo wa kumpeleka Salome kwenye maombi,
“Ila mwanangu atachukia akijua nimewaambia watu kuhusu yaliyomkuta, ila sikuwa na jinsi maana Yule mtu alituona”
Akawaza ila uhakika wa Salome kufika siku hiyo hakuwa nao, wanae wale wadogo nao walikuwa wamerudi na wametulia sebleni kwao wakimuangalia mama yao akiwa na mawazo sana, mmoja akamuuliza
“Mama mbona una mawazo hivyo?”
“Nawaza kuhusu dada yenu Salome sijui leo atakuja”
“Si umpigie simu mama”
“Salome hana simu”
“Mbona anayo, huwa tunamuona nayo akiongea na watu na akiitumia”
Neema akashangaa kusikia kuwa mtoto wake ana simu maana yeye aliamini kuwa mwanae hana simu, aliwauliza wanae kwa mshangao.
“Hebu achene maneno yenu, lini mmemuona dada yenu na simu?”
“Kila siku tunamuona nayo mama, tena muda mwingine anakuwaga anaitumia sana. Toka tumehamia huku anayo”
“Mmh sijui alinunuliwa na nani? Au Ashura?”
“Sijui ila mamdogo Ashura toka siku ameanguka wakati tunakula ndio hatujamuona tena”
Neema akazidi kushangaa na kuwauliza vizuri watoto wake,
“Mbona siwaelewi?”
“Dada alituambia tukacheze eti yeye na mamdogo wanacheza michezo ya kutaniana, na tulipoondoka badae akatuita na kutupakiza kwenye gari halafu tukahamia hapa”
“Inamaana hapa hamkuja na Ashura?”
“Hatukuja nae, dada Salome alisema mamdogo kaondokea kule kule. Ila mimi nilifurahi maana ona huku tunaishi kwa amani sana”
Wakatoka nje na kucheza huku wakimuacha Neema kwenye maswali mengi sana, akajiuliza na kama Ashura aliondokea kule kule ni kwanini Salome alimdanganya kuwa aliondokea kwenye nyumba mpya waliyohamia? Na michezo gani hiyo ya kuanguka wakati wa kula? Alijiuliza maswali mengi sana bila ya majibu, na kubwa zaidi ni kuhusu kumiliki simu kwa Salome. Alijiuliza sana na mwishowe akaamua kuchukua simu yake na kumpigia Ashura ila namba haikupatikana, alipiga na kupiga lakini aliambiwa haipatikani.
Kwa upande wa Neema aliamini kuwa mwanae angeenda nyumbani kwa siku hiyo na angechukua ushauri aliopewa na mama Pendo wa kumpeleka Salome kwenye maombi,
“Ila mwanangu atachukia akijua nimewaambia watu kuhusu yaliyomkuta, ila sikuwa na jinsi maana Yule mtu alituona”
Akawaza ila uhakika wa Salome kufika siku hiyo hakuwa nao, wanae wale wadogo nao walikuwa wamerudi na wametulia sebleni kwao wakimuangalia mama yao akiwa na mawazo sana, mmoja akamuuliza
“Mama mbona una mawazo hivyo?”
“Nawaza kuhusu dada yenu Salome sijui leo atakuja”
“Si umpigie simu mama”
“Salome hana simu”
“Mbona anayo, huwa tunamuona nayo akiongea na watu na akiitumia”
Neema akashangaa kusikia kuwa mtoto wake ana simu maana yeye aliamini kuwa mwanae hana simu, aliwauliza wanae kwa mshangao.
“Hebu achene maneno yenu, lini mmemuona dada yenu na simu?”
“Kila siku tunamuona nayo mama, tena muda mwingine anakuwaga anaitumia sana. Toka tumehamia huku anayo”
“Mmh sijui alinunuliwa na nani? Au Ashura?”
“Sijui ila mamdogo Ashura toka siku ameanguka wakati tunakula ndio hatujamuona tena”
Neema akazidi kushangaa na kuwauliza vizuri watoto wake,
“Mbona siwaelewi?”
“Dada alituambia tukacheze eti yeye na mamdogo wanacheza michezo ya kutaniana, na tulipoondoka badae akatuita na kutupakiza kwenye gari halafu tukahamia hapa”
“Inamaana hapa hamkuja na Ashura?”
“Hatukuja nae, dada Salome alisema mamdogo kaondokea kule kule. Ila mimi nilifurahi maana ona huku tunaishi kwa amani sana”
Wakatoka nje na kucheza huku wakimuacha Neema kwenye maswali mengi sana, akajiuliza na kama Ashura aliondokea kule kule ni kwanini Salome alimdanganya kuwa aliondokea kwenye nyumba mpya waliyohamia? Na michezo gani hiyo ya kuanguka wakati wa kula? Alijiuliza maswali mengi sana bila ya majibu, na kubwa zaidi ni kuhusu kumiliki simu kwa Salome. Alijiuliza sana na mwishowe akaamua kuchukua simu yake na kumpigia Ashura ila namba haikupatikana, alipiga na kupiga lakini aliambiwa haipatikani.