Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #281
SEHEMU YA 200 ............. MWISHO
Walifika na kushangaa watu wamejaa halafu eneo limekuwa majivu tupu, halafu Kulwa na Doto pamoja na Ana walipomuona Salome walimkimbilia na kupiga magoti mbele yake,
“Tafadhali msamehe mama yetu, najua hatorudia tena. Tunajua una uwezo wa kubadilisha huu moto na kurudisha nyumba yetu. Sisi hatuna haja na nyumba ila tunahaja na mama yetu, tusaidie Moza”
Neema na Patrick waliwashangaa sana huku wakiuliza kuwa ni kitu gani kimetokea, ila Ana alimwambia Patrick kuwa amuulize Yule binti yake anajua kila kitu,
“Huyu tumekuja nae hapa sababu tupo nyumbani haelewi chochote kile, ndiomana tumemleta hapa labda awe na kumbukumbu. Kwani kumefanyaje tena mbona nyumba imeteketea?”
Salome nae akaongea,
“Mbona umeniita Moza, Moza si alishakufa na mlivyo na roho mbaya mlinikataza hata kumuaga Moza mara ya mwisho”
Wakamshangaa, na Neema alikuwa wa kwanza kumshangaa binti yake kuwa anakumbuka vyema kitendo cha yeye kutaka kumuaga Moza na mwisho wa siku kuingia kwenye kaburi la Moza, ila hilo tukio la kuingia kaburini hakujua kama analikumbuka, ikabidi amuulize
“Walivyokukatalia kumuaga Moza ilikuwaje?”
“Sijui ila nakumbuka tulirudi nyumbani nikalala”
“Mmmh ukalala!”
“Ndio nikalala, si ni jana tu ndiyo Moza amekufa!”
Walikuwa wakimshangaa hata wale vijana waliomleta Ana na kumkuta ndugu yao Jack kwenye nyumba hiyo walishindwa kumuhoji maswali yoyote Salome kwani alionekana akiongea kama mtu asiye na mwelekeo.
Patrick alihoji kwa makini maana ile ilikuwa ni nyumba yake pia, ikabidi mlinzi wao ajaribu kumuelekeza kwa kifupi jinsi ilivyokuwa mpaka kushtukia nyumba ikiungua,
“Kwahiyo Rose ameungulia humo”
“Sijui, itakuwa hivyo maana sisi tuliamriwa tutoke nje na tulipotoka tu nyuma yake kukatokea mlipuko wa hali ya juu na gafla kila kitu kilikuwa kimeteketea kama ilivyoonekana yani hakuna tulichookoa”
“Kwahiyo huyo Moza mlimuona kabisa”
“Ndio, na mwanzoni alikuwa ni huyo Salome halafu badae ndio akageuka na kuwa Moza”
Patrick aliona kuwa hapo kutakuwa na tatizo, hivyo akamuomba Neema waondoke pamoja na Salome kurudi nyumbani maana walikuwa wakimsonga songa kumuuliza maswali Salome ambapo hakuwa na jibu ya swali hata moja.
Walimchukua Salome na kuondoka nae, huku wakiacha pale watu wakiendelea kufurika na kushangaa yale majanga ya moto, wakati wanaondoka Kulwa aliwashtua ndugu zake kuwa wawafate hao watu maana hawakuwa na pakukaa kwa kipindi hicho na wala hawakujua kuwa ni wapi waelekee.
Walipofika nyumbani, wakina Kulwa nao walikuwa wamegika,
“Tafadhalini tupokeeni, hatuna pa kwenda sisi”
Patrick aliwatazama, na kwavile hali nzima ya kilichotokea hakuielewa aliwahurumia na kuwakaribisha pale nyumbani huku akisema kuwa atatafuta utaratibu wa wao kupata sehemu ya kuishi.
Ila kwa upande wa Neema bado alikuwa na maswali kwa binti yake tu,
“Eti wewe ndio ulikuwa Moza!”
“Sikuelewi mama”
“Eti ulikuwa ukitoweka toweka?”
“Mama sikuelewi yani maswali yote unayoniuliza ni yananichanganya tu”
“Mwanangu, mimi ndio sielewi kabisa. Ulikuwa wapi kipindi chote hiki kama huna kumbukumbu ya chochote kilichotokea, inamaana kipindi chote hiki nilikuwa naishi na Moza!”
Alisisimka mwili kwa uoga, ila bado hakuelewa chochote.
Siku zilipita ila hakuonekana Rose wala Moza tena na akili ya Salome ilikuwa ikirudi kwa taratibu kwani kila kitu kilikuwa ni kipya machoni mwake kwa kipindi hiko.
***MWISHO
Asanteni sana kwa kuwa nami tangu mwanzo hadi mwisho wa Simulizi hii. Ni matumaini yangu umejifunza mambo mengi.
Pongezi nyingi kwa mwandishi wetu ATUGANILE MWAKALILE. Weka maoni yako kwa kile ulichojifunza.
Endelea kufurahia simulizi nyingine zitakazorushwa na BURE SERIES
Walifika na kushangaa watu wamejaa halafu eneo limekuwa majivu tupu, halafu Kulwa na Doto pamoja na Ana walipomuona Salome walimkimbilia na kupiga magoti mbele yake,
“Tafadhali msamehe mama yetu, najua hatorudia tena. Tunajua una uwezo wa kubadilisha huu moto na kurudisha nyumba yetu. Sisi hatuna haja na nyumba ila tunahaja na mama yetu, tusaidie Moza”
Neema na Patrick waliwashangaa sana huku wakiuliza kuwa ni kitu gani kimetokea, ila Ana alimwambia Patrick kuwa amuulize Yule binti yake anajua kila kitu,
“Huyu tumekuja nae hapa sababu tupo nyumbani haelewi chochote kile, ndiomana tumemleta hapa labda awe na kumbukumbu. Kwani kumefanyaje tena mbona nyumba imeteketea?”
Salome nae akaongea,
“Mbona umeniita Moza, Moza si alishakufa na mlivyo na roho mbaya mlinikataza hata kumuaga Moza mara ya mwisho”
Wakamshangaa, na Neema alikuwa wa kwanza kumshangaa binti yake kuwa anakumbuka vyema kitendo cha yeye kutaka kumuaga Moza na mwisho wa siku kuingia kwenye kaburi la Moza, ila hilo tukio la kuingia kaburini hakujua kama analikumbuka, ikabidi amuulize
“Walivyokukatalia kumuaga Moza ilikuwaje?”
“Sijui ila nakumbuka tulirudi nyumbani nikalala”
“Mmmh ukalala!”
“Ndio nikalala, si ni jana tu ndiyo Moza amekufa!”
Walikuwa wakimshangaa hata wale vijana waliomleta Ana na kumkuta ndugu yao Jack kwenye nyumba hiyo walishindwa kumuhoji maswali yoyote Salome kwani alionekana akiongea kama mtu asiye na mwelekeo.
Patrick alihoji kwa makini maana ile ilikuwa ni nyumba yake pia, ikabidi mlinzi wao ajaribu kumuelekeza kwa kifupi jinsi ilivyokuwa mpaka kushtukia nyumba ikiungua,
“Kwahiyo Rose ameungulia humo”
“Sijui, itakuwa hivyo maana sisi tuliamriwa tutoke nje na tulipotoka tu nyuma yake kukatokea mlipuko wa hali ya juu na gafla kila kitu kilikuwa kimeteketea kama ilivyoonekana yani hakuna tulichookoa”
“Kwahiyo huyo Moza mlimuona kabisa”
“Ndio, na mwanzoni alikuwa ni huyo Salome halafu badae ndio akageuka na kuwa Moza”
Patrick aliona kuwa hapo kutakuwa na tatizo, hivyo akamuomba Neema waondoke pamoja na Salome kurudi nyumbani maana walikuwa wakimsonga songa kumuuliza maswali Salome ambapo hakuwa na jibu ya swali hata moja.
Walimchukua Salome na kuondoka nae, huku wakiacha pale watu wakiendelea kufurika na kushangaa yale majanga ya moto, wakati wanaondoka Kulwa aliwashtua ndugu zake kuwa wawafate hao watu maana hawakuwa na pakukaa kwa kipindi hicho na wala hawakujua kuwa ni wapi waelekee.
Walipofika nyumbani, wakina Kulwa nao walikuwa wamegika,
“Tafadhalini tupokeeni, hatuna pa kwenda sisi”
Patrick aliwatazama, na kwavile hali nzima ya kilichotokea hakuielewa aliwahurumia na kuwakaribisha pale nyumbani huku akisema kuwa atatafuta utaratibu wa wao kupata sehemu ya kuishi.
Ila kwa upande wa Neema bado alikuwa na maswali kwa binti yake tu,
“Eti wewe ndio ulikuwa Moza!”
“Sikuelewi mama”
“Eti ulikuwa ukitoweka toweka?”
“Mama sikuelewi yani maswali yote unayoniuliza ni yananichanganya tu”
“Mwanangu, mimi ndio sielewi kabisa. Ulikuwa wapi kipindi chote hiki kama huna kumbukumbu ya chochote kilichotokea, inamaana kipindi chote hiki nilikuwa naishi na Moza!”
Alisisimka mwili kwa uoga, ila bado hakuelewa chochote.
Siku zilipita ila hakuonekana Rose wala Moza tena na akili ya Salome ilikuwa ikirudi kwa taratibu kwani kila kitu kilikuwa ni kipya machoni mwake kwa kipindi hiko.
***MWISHO
Asanteni sana kwa kuwa nami tangu mwanzo hadi mwisho wa Simulizi hii. Ni matumaini yangu umejifunza mambo mengi.
Pongezi nyingi kwa mwandishi wetu ATUGANILE MWAKALILE. Weka maoni yako kwa kile ulichojifunza.
Endelea kufurahia simulizi nyingine zitakazorushwa na BURE SERIES