Simulizi: Lisa

Kwa kuwa hapakuwa na matukio ya kupiga picha mchana huo, Eliza alirudi hotelini kwa gari. Alipofika hotelini aliingia bafuni kuoga. Baada ya kutoka bafuni, alitoka akiwa amejifunga taulo tu mwilini.
Alipotoka nje, alipigwa na butwaa baada ya kuona sura ile kwenye kochi. Chester alikuwa bado amevalia shati na suruali ile ile ya bei ghali kutoka asubuhi. Chini ya nywele zake fupi nyeusi kulikuwa na uso wa kifahari na mzuri. Nani angefikiria kwamba mtu kama huyo angeingia kwenye chumba cha mtu mwingine bila kugonga hodi?
"Chester Choka, umeingiaje?" Eliza akawa mnyonge. Chini ya hali kama hizo, hakuweza kujizuia kuacha utulivu wake.
"Kupitia mlangoni." Chester aliinua vidole viwili virefu vilivyoshikilia kadi nyembamba ya chumba kati yao.
Alimtazama mwanamke aliyekuwa mbele yake kwa shauku. Taulo hilo la waridi lilikuwa limefungwa kwenye sehemu za siri za mwanamke huyo, likifichua tu mabega na mapaja yake ambayo yalikuwa yamefunikwa na matone ya maji. Alikuwa ameosha tu nywele zake nene na likuwa hajazikausha na zilikuwa zimefungwa kwa nyuma. Uso wake na mfupa wa shingo ulikuwa wa kupendeza sana hivi kwamba mwanamume yeyote angekuwa na wazimu juu yake.
Hata hivyo, kilichomfanya Chester atpagawe zaidi ni macho yake meusi. Alionekana kama Charity enzi hizo. Hivyo ndivyo pia Charity alivyoonekana baada ya Chester kufanya naye mapenzi kwa mara ya kwanza. Alikuwa ametoka bafuni na nywele zake zimefungwa kwenye bun. Macho yake pia yalikuwa yameonekana vile vile, yakiwa yamebeba dalili ya wasiwasi na aibu huku akijaribu kujituliza.
Ghafla, Chester alihisi mwili wake ukiungua ovyo.
Watu wengi walisema kwamba alikuwa mwanamume wa kucheza wa wanawake, lakini wakati huo, hata hivyo, alikuwa tu kama kijana ambaye hakuwahi kuona dunia kabla. Ilikuwa kana kwamba Chester alikuwa amegeuka kuwa kijana ambaye ndo kwanza anabalehe na kukutana na mwanamke.
Imekuwa muda gani? Miaka saba au minane? Ilikuwa ni muda mrefu sana kwamba alikuwa karibu kusahau kuhusu hilo.
Eliza alikuwa akitetemeka kwa hasira, lakini alipata utulivu haraka sana. Harakaharaka akasogea pembeni ya kitanda na kuzishika zile nguo kitandani.
Chester alikazia macho yake kwenye mapaja yake manene chini ya taulo bila kuangalia pembeni. Eliza aliweza kumfumbia macho na kuelekea bafuni na nguo zake. Akiwa amefunga taulo, hakuweza kupiga hatua kubwa kuingia bafuni. Kwa hivyo, alitembea kwa tahadhari sana. Alikuwa na woga sana hivi kwamba hakuthubutu kupumua kwa nguvu kwa kuhofia kwamba Chester angemlazimisha busu la mapenzi kama alivyokuwa akifanya hapo awali.
Bado alikuwa hajavaa nguo zake. Ikiwa Chester angefanya hivyo sasa, asingeweza kupambana naye. Kwa bahati nzuri, Chester alibaki amekaa pale bila kuinuka. Baada tu ya Eliza kuingia bafuni na kufunga mlango ndipo aliposhusha pumzi.
Chester alivuta sigara, na moshi huo ukafunika kilindi cha macho yake. Akashusha pumzi nyingine ndefu. Katikati ya usumbufu wake, alilaani kimoyomoyo. Hakuwahi kufikiria kwamba siku moja angemfuata mwanamke kwa unyonge vile. Ni lazima kutokana na ukweli kwamba hakuwa na uhusiano kwa muda mrefu.

Punde, mlango wa bafuni ulifunguliwa kwa mara nyingine. Eliza alitoka akiwa amevalia fulana ya kawaida ya mistari ya pinki na suruali ya jeans. Alionekana kama msichana ambaye bado yuko chuo kikuu.
“Sikutarajia ungevaa shati la waridi,” Chester alisema bila kujijua.
 
"Kwanini siwezi kuvaa pink?" Eliza aliuliza.
Ilikuwa ni kweli kwamba mara chache alivaa pink, lakini shati hii
ilifadhiliwa na brand ya kifahari. Kwa kuwa alikuwa amepokea pesa kuwa balozi wa brand hiyo, ilimbidi kuivaa.
Chester aliyekuwa ameshika sigara alipigwa na butwaa. Kope zake ndefu ziliweka vivuli chini ya macho yake.
Kweli, nani alisema Eliza hawezi kuivaa? Tangu alipokutana naye, macho yake yaliyofanana sana na Charity yalimfanya ahisi kana kwamba roho ya Charity ilikuwa ndani ya mwili wa Eliza. Baada ya yote, alikumbuka kwamba Charity hakupenda mavazi ya rangi ya pink. Daima alikuwa baridi na mtulivu. Hata rangi ya nguo zake ilisema yote.
“Chester Choka, sijali unachofanya na wasanii wengine wa kike chini ya Felix Media, lakini nikukumbushe kuwa unahitaji kubisha hodi kabla ya kuingia chumbani kwangu wakati mwingine. Usiingie bila ruhusa yangu.”
Eliza hakuweza tena kumvumilia mtu huyu. “Ingawa nimesainishwa kwa Felix Media, sikuuza mwili wangu wote kwa kampuni. Tafadhali nipe faragha.”
"Je, hauelewi nia yangu ya kuingia ndani?"

Chester aliinua miguu yake yote juu ya meza ya kahawa, macho yake yakiwa meusi na yasiyo na mwisho. “Eliza wewe ni mwanamke mjanja sana. Ulicheza dau na Director Kalulu kuhusu uigizaji wako mbele ya wafanyakazi. Ulimzidi kiongozi wa kiume, ambaye ni mwigizaji bora zaidi, sembuse Cindy. Ulitaka kumjulisha Director Kalulu kuwa wewe ni mwigizaji kamili ili akupandishe kuwa kinara wa kike. Kwa hivyo, Director Kalulu hakuwa na chaguo ila kumwondoa Cindy.”
“Sawa, hakuna ninachoweza kufanya kuhusu hilo. Hapo awali, nilikubaliana na nafasi ya kuigiza kama msaidizi wa kinara wa kike, lakini mchumba wako alihonga wafanyakazi ili kunisumbua siku ya kwanza.”
Eliza akaanza kupaki vitu vyake kwa utulivu. “Kusema kweli mchumba wako Cindy hanipendi kwa sababu aliniona nikitoka ofisini kwako nikiwa nimechanganyikiwa juzi. Amekuwa akinifikiria kama mwiba kwake tangu wakati huo. Ikiwa kila mtu angekuwa tayari kumaliza kushoot filamu hii kwa amani, ningefurahi kucheza kando yake kama mwigizaji msaidizi wa kwanza. Lakini ni wazi, hakuwa na nia ya kufanya hivyo.”
Eliza aliinua kichwa na kumtazama Chester kwa upole. “Samahani, siwezi kuvumilia na kumwepuka kila wakati. Kadiri ninavyoepuka ndivyo anavyofurahi kunidhulumu. Zaidi ya hayo, kwanini nilaumiwe kwa uigizaji wake mbaya?”
“Unawezaje kumsema vibaya mchumba wangu mbele yangu na kumfanya aonekane hana thamani?” Chester kwa huzuni alifungua kitufe kwenye kola yake.
“Ninasema ukweli tu. Ikiwa ungependa kusikia maneno ya uwongo na ya kumpambapamba, unaweza kutafuta mtu mwingine.” Eliza aliendelea bila huruma, “Yeye si mtu wa thamani. Labda yupo vizuri tu kitandani. Vinginevyo, kwanini ungemchagua kati ya wanawake wengine wengi warembo?”
"Eliza… " Chester alisimama na kumsogelea. Alimkandamiza kidevu, akitabasamu bila huruma.
Ni wakati huo tu aligundua kuwa ngozi yake ilikuwa laini sana. Ilijisikia ajabu kwa kugusa. Huku kidevu chake kikiwa kimebanwa, midomo yake ya waridi iliyopinda juu kidogo ilionekana kuwa ya mvuto sana hivi kwamba alikuwa na msukumo wa ghafla wa kuibusu.
Eliza alishusha pumzi. Aliweza kuhisi waziwazi mabadiliko katika macho ya mwanamume huyo na harufu yake yenye kutisha akiwa umbali wa karibu sana. Kwa kuhofia matokeo yake, hakuthubutu kufanya uzembe.
 
“Eliza! Unanielewa vizuri sana.” Chester akamsogelea huku akitabasamu vibaya. Eliza alirudi nyuma taratibu mpaka alipotua kitandani.
Chester akainama na kuweka mikono yake yote miwili kitandani. Wote wawili walibaki katika hali ya kutazamana. “Eliza usisahau kuwa mwisho wa siku Cindy ni mchumba wangu. Ulipomlazimisha Director Kalulu kumfukuza, ilikuwa ni kofi la uso kwangu. Watu ambao hapo awali walithubutu kunifanyia hivi hawako tena Kena.”
“Kwa hiyo?” Eliza alimtazama mwanaume huyo kwa macho yake ya mawe.
Chester alijihisi mnyonge. Kwa uso wake mzuri na utambulisho wake wa pekee, mwanamke yeyote ambaye alimwona wakati huo angeona haya na kuyeyuka. Eliza pekee aliishi kama mwanamke mwenye damu baridi. "Naweza kukuangamiza."
Baada ya muda, aliendelea, "Baada ya kusema hivyo, ikiwa utafikiria kulala nami usiku, ninaweza kukuacha."
Eliza alitazama chini huku maneno ya kejeli yakipita kwenye kilindi cha macho yake. Huyu ndiye mwanaume ambaye alikuwa akimpenda sana. Alikuwa kweli... chukizo.
"Kama ningekubali, nisingepigana na wewe ofisini mara ya mwisho." Eliza akatikisa kichwa. “Bwana Choka, kweli... Ulikuwa ukifanya hivyo na Charity, huh?”
Mwili wa Chester ukawa mgumu. kutajwa kwa Charity kuligusa ujasiri wake mbichi. "Lakini nilisikia wakati Charity alikamatwa wakati huo, wewe ndiye uliyemwekea wakili wa kumpeleka jela."
Eliza alijitenga na mkono wake na kusema kwa macho ya baridi, "Ingawa sijazungumza na Charity kwa muda mrefu, nitakumbuka uso wake milele. Yeye ni rafiki yangu wa utotoni. Samahani lakini siwezi kulala na yule mwanaume aliyekuwa akilala na rafiki yangu. Mimi sioni raha tu. Afadhali nipoteze kila kitu. Pamoja na hayo, sitaki kufanywa kama kipozeo na wanaume."

Sura ya: 733

Eliza aliinua mkono wake na kuitoa saa yake. Kulikuwa na kovu kubwa kwenye mkono wake. “Unaweza kuona hili? Hii ilitokea katika uhusiano wangu wa awali. Kila mtu alisema kwamba nilimwendea Monte Kalanja kwa sababu ya hali yake. Kiukweli nilikuwa nampenda sana lakini aliniacha. Nilichagua kujiua, lakini sikufa. Hah. Mwishowe, alidhihaki jaribio langu la kujiua na kusema ilikuwa njia ya kupata huruma yake.”
Chester alikaza macho yake kwa mshangao kwenye kovu maarufu kwenye mkono wake. Hakuweza kujua ni kwanini mtu jeuri kama yeye angejiua. Je! alikuwa akimpenda sana Monte Kalanja, yule fisadi?
"Mimi sio Monte," Chester alisema kwa sauti ya kishindo, "Monte huwafuata wanawake ili kushinda mioyo na miili yao, lakini nataka mwili wako tu."
Eliza alipigwa na butwaa. Ghafla, alicheka. "Kweli, wewe ni fisadi waziwazi. Je, unajaribu kusema kwamba sivutii hata kidogo isipokuwa mwili wangu?”
Macho ya kina Chester yalikuwa ya kuzua utata. " Labda..."
“Sawa. Tangu niingie kwenye tasnia hii, nimeona ufuska wa kila aina. Lakini nikivua nguo zangu mbele yako leo, naweza kufanya hivyo mbele ya mwanamume mwingine kesho pia.” Eliza akatikisa kichwa. "Ikiwa ningeishi maisha kama hayo, kipaji changu kisingekuwa na maana tena. Ningekuwa nategemea utelezi badala ya akili na kipaji changu."
"Wakati mtu mashuhuri akianguka chini kabisa, unajua ni watu wangapi watamchukulia kama kicheko?" Chester alitania.
“Najua. Baadhi ya watu mashuhuri wamebadili taaluma zao na kuwa walimu na hata watu wa mauzo. Bila kujali, hizo bado ni kazi. Kutengeneza dola 3,000 hadi 4,000 kwa mwezi bado kunatosha kujikimu,” Eliza alijibu bila kujali.
Akiwa amemtazama kwa makini, Chester hakuweza kujizuia kushawishika na maneno yake.
Kulikuwa na wanawake wengi sana karibu naye ambao walijaribu sana kupanda ngazi. Miongoni mwao, Cindy alikuwa mkali zaidi. Llakini, Eliza alikuwa tofauti. Alikuwa baridi na safi kama dimbwi la maji.
Eliza aliingiza vitu vyake kwenye begi lake na kulifunga zipu bila kumwangalia. “Bwana Choka, kama ungependa kubaki hapa, unaweza kuendelea kubaki hapa. Nitarudi mjini.”
Alipomaliza kuongea, alitaka kuchukua sanduku lingine. Mkono mrefu ulinyooka haraka na kuchukua sanduku hilo kabla ya kufanya hivyo.
"Kwa bahati nzuri, ninarudi mjini pia. Turudi pamoja.” Chester alimtazama.
 
"Nadhani umekosea, unapaswa kumchukua Cindy." Eliza alijaribu kurudisha sanduku lake, lakini hakuweza kulisogeza hata baada ya muda fulani. "Bwana Choka, nitakuwa katika shida ikiwa watu wataniona nikiwa nawe."
"Je, bado unaogopa kupata matatizo wakati tayari uko tayari kuacha tasnia ya burudani na kutafuta kazi nyingine?" Chester alikunja midomo yake kwa kujieleza.
Eliza alikosa la kusema. "Ikiwa Cindy atajua kuhusu hilo, hataniruhusu niende hata nikiamua kuacha tasnia ya burudani."
“Hilo ni tatizo lako, basi. Siyo langu.” Chester akavuta begi lake.
Eliza alimfuata kwa haraka. Wawili hao walianza kuvutana.
"Unataka wengine waone hii, huh?" Chester aliinua uso wake.
Eliza hakuwa na jinsi zaidi ya kuteremka chini bila kupenda. Kisha akaingia kwenye gari lake. Dereva alipomwona Eliza, uso wake haukuonekana kufurahi. Muda mfupi baadaye, akawasha gari kwa utulivu.
Eliza ambaye alikuwa mwisho wa akili yake, alimtumia ujumbe Loida kumjulisha kuwa ameondoka.
Safari ya kurudi mjini ilichukua muda wa nusu saa.
Baada ya kuitazama simu yake kwa muda, Eliza alijisikia vibaya, akafumba macho. Kwa kuwa alikuwa amesoma script hadi usiku wa manane jana, upesi alilala.
Chester akageuka nyuma na kumtazama yule mwanamke aliyekuwa ameegemea dirisha huku akiwa amefumba macho. Kope zake zilikuwa nene kama manyoya, wakati pua yake ilikuwa ndogo lakini ndefu. Alikuwa mrembo sana. Alituliza macho yake kwake kwa muda fulani.
Alipoona tabia yake, dereva aliyekuwa mbele aligeuza macho kimakusudi. Kichwa cha Eliza mara moja kikaelekea kwake na kutokea kumwangukia begani.
Chester alimtazama dereva ambaye alitabasamu kwa aibu. Baada ya yote, dereva alimuelewa zaidi, kwa kuzingatia kwamba alikuwa amemfanyia kazi kwa miaka mingi.
Kwa jinsi Chester alivyomtazama mwanamke huyo, dereva alikuwa na hakika kwamba alikuwa na hisia naye. Kwa kweli, Chester hakuwa na nia ya kumfanya chochote. Tangu Eliza aseme kuwa hataki kuchangia mwanaume mmoja na Charity, aliachana na wazo la kulala naye. Wanawake wengine wangeweza kufanya hivyo isipokuwa yeye kwa sababu alikuwa rafiki wa Charity.
Wakati huo, hata hivyo, mwanamke huyo alikuwa ameegemea bega lake. Harufu iliyokuwa ikitoka kwenye nywele zake ilikuwa sawa kabisa na harufu ya Charity. Ajabu ni kwamba kila mara alikuwa akikumbuka harufu ya Charity.
Chester akakaza mkono kwenye simu yake. Kila mara mwanamke huyo alipoibuka akilini mwake, alihisi kana kwamba kuna mtu anayeuponda moyo wake. Hisia hiyo ilikuwa na nguvu tangu alipomwona Eliza.
Baada ya safari ya nusu saa, Eliza aliamka gari liliposimama. Aliyafumbua macho yake kwa kupigwa na butwaa, akajikuta ametulia begani mwa mwanaume huyo. Aliinua kichwa chake na kukutana na macho meusi ya Chester yaliyobeba tabasamu la busara. "Je, bega langu lilikuufaa?"
Eliza alikunja uso kwa hasira. Alikuwa amepanga kujiweka mbali naye, lakini aliishia kulala begani mwake.
“Samahani. Nilikuwa na usingizi mzito sana.”
"Kwa sababu yako, bega langu linauma." Chester aliinamisha uso wake. "Je, huoni haja ya kunisaidia?"
"Nitatengeneza pesa zaidi kwa kampuni yako." Eliza alipomaliza tu sentensi yake, alichungulia dirishani na kugundua kuwa alikuwa amefika jirani yake. Hata hivyo, alijuaje mahali alipoishi? Ghafla alikumbuka kwamba kampuni yake ilikuwa na anwani yake. Alikuwa ni mtu muweza wa yote.
“Pesa?” Chester akatabasamu. "Samahani, pesa si kitu ambacho nahitaji sana."

“Hilo ni tatizo lako.” Eliza alifungua mlango ili ashuke kwenye gari.

Mkono ghafla ukamshika mkono na kuuvuta. Eliza ambaye alishikwa na butwaa alianguka kifuani mwake. "Chester Choka, niachie." Eliza alihangaika chini ya fahamu. Kisha akamsikia mwanaume akitweta.
 
“Eliza, mikono yako imeshika wapi? ” Chester aliuliza kwa sauti nzito.
Eliza alitazama chini na kuona mikono yake ilidongokea sehemu ambayo haikutakiwa kushika. Hata hivyo... aliitikia kwa nguvu japo mikono yake ilikuwa inakandamiza mapaja yake tu. Akiwa ameduwaa kidogo, aliuliza, “Chester Choka, umekata tamaa kiasi gani? Hata Cindy hawezi kukidhi matamanio yako, huh?”
“Eliza niambie leo umenitongoza mara ngapi? Siku zote nimekuwa nikivumilia.” Tabasamu baya na la kukasirika lilienea kwenye uso mzuri wa Chester.
Eliza alifungua mdomo wake. Alipokuwa karibu kuzungumza, Chester alimkatiza, “Usielezee. Nilikuja chumbani kwako ili kukukanya kuhusu Cindy, lakini ulikuwa unaoga. Mbaya zaidi ulitoka bafuni bila kuvaa nguo zako.
Pia, uliegemeza kichwa chako kwenye bega langu kwenye gari. Kwa taarifa yako, nina nguvu sana katika kipengele hiki.” Alimsogelea na kumtamkia maneno machache ya mwisho kwa sikio lake kwa kumtania.

Sura ya: 734
Eliza alichukizwa sana alipomwona Chester alishindwa kujizuia.
Baada ya kimya cha muda, alisema, “Kama ungekuwa single, ningeweza kuwa na hamu kidogo na wewe. Lakini sasa kwa kuwa tayari una mchumba unayetarajia kumuoa, naona kama unanizingua. Kama mwanamke mzuri, ninahisi kuwa wewe ni- ”
“Unahisi nini kuhusu mimi?” Alipomwona akijizuia, Chester alimkatisha bila subira.

Eliza alisema, “wewe ni mchafu sana, tabia yako ni ya kuchukiza, lakini unaifurahia, ukifikiri kwamba wewe ni mtu mzuri sana katika kucheza na wanawake.”

Uso mzuri wa Chester ulitiwa giza na kumfanya aonekane mbaya.
“Sawa Eliza.” Alitabasamu kwa huzuni kabla ya kumsukuma nje ya gari ghafla. “Ondoka nje.”
Eliza alitoka nje haraka na kuchukua mizigo yake na kuondoka. Baada ya kuona kuwa hatazami nyuma hata kidogo, Chester akatoa sigara. Akaikata sigara hiyo vipande viwili badala ya kuiwasha. Muda mfupi baadaye, alicheka kicheko cha baridi, jambo ambalo lilipelekea uti wa mgongo wa dereva kuwa baridi.

Chester alirudi kwenye ghorofa ya juu ya makazi yake ambayo ilikuwa zaidi ya mita 300 za mraba. Mara akatoka nje ya lifti, akamwona Cindy pale mlangoni.
Mara tu alipomwona Chester, Cindy alimsogelea kwa macho mekundu. “Bwana Choka, Shedrick aliniomba niache filamu ya Director Kalulu. Alisema Eliza atachukua nafasi kama mwanamke kinara... "
“Najua.” Chester alifungua mlango kwa alama ya vidole.
Cindy akavuta shati lake. “Chester, kila mtu huko nje anajua kuwa mimi ni mchumba wako. Zaidi ya hayo, tayari nimejiunga na filamu ya Mke Mwenza na kuanza shooting. Nikiacha baada ya siku moja, watu watanionaje? Kwa hakika watadhani kwamba Director Kalulu hakubaliani na uigizaji wangu. Kila mtu atanidhihaki. Utanioa hivi karibuni. Sio tu kwamba jambo hili litaniletea aibu mimi bali pia wewe na familia ya Choka.”
Chester akageuka na kutazama macho yake meusi na yenye kuvutia.
Hakuweza kujizuia kumfikiria Eliza, ambaye alikuwa mtulivu na mwenye busara. Ingawa alizungumza kwa ukali, angalau alikuwa mkweli na muwazi.
“Chester... Mbona unanitazama hivi?” Kumtazama kwake kulimfanya Cindy akose raha. "Ninasema ukweli tu."
"Cindy, kwa hivyo unagundua kuwa umeniletea aibu, huh?" Chester alikoroma. “Nilikusaidia kupata nafasi katika filamu ya Mke Mwenza, lakini ulitakiwa kuondoka baada ya siku moja. Hakika wewe ni aibu kwangu.”
Uso wa Cindy ulijawa na aibu. “Yote yalikuwa ni kwa sababu ya Eliza—”
 
“Je, ni kwa sababu aliigiza vizuri na kukufanya usiwe mtu wa maana?” Chester alimkatisha, "Nilikuwa kwenye seti. Kama mtu wa nje, niliona jinsi alivyokupiga kumbo kwa uwezo wake. Unadhani Director Kalulu atakuruhusu kuendelea na shooting na kukuacha upoteze ubora wa filamu yake? Vyovyote vile, wewe ni aibu."
Akiwa ameudhishwa na lawama zake, Cindy alihisi hisia inayowaka usoni mwake. "Kampuni haikupaswa kumruhusu Eliza kujiunga na filamu mara ya kwanza."
“Nilifikiri utaweza kumpiku Eliza, ukizingatia jinsi unavyofanya vizuri mbele yangu. Nani alijua kuwa uigizaji wako ni mzuri katika maisha halisi lakini ni mbaya sana mbele ya kamera?” Sura ya dhihaka iliosha uso wa Chester.“ Zaidi ya hayo, je, unafikiri kwamba Director Kalulu ni mpumbavu? Kwa kuzingatia uigizaji wako mbaya siku ya kwanza, kwa nini atake kuendelea na wewe?"
Cindy alipofungua kinywa chake, Chester alisema bila subira, “Imetosha. Acha kuigiza mbele yangu. Huwezi kufanya lolote vizuri. Pia nikukumbushe kuwa nilikubali kukuoa lakini haimaanishi kwamba unaweza kutumia utambulisho wangu kuwadhulumu wengine huko nje.”
Uso wa Cindy uligeuka kuwa wa kutisha. “Ni kwa sababu ya Eliza? Kama nilivyosema, Monte Kalanja– “
Kabla ya kumaliza sentensi yake, Chester alimkandamiza shingoni. “Cindy Tambwe, nini kinakupa haki ya kumkosoa Eliza? Kama ningejua, nisingemruhusu mtu asiyefaa kitu kama wewe kuwa machoni pangu. Potelea mbali.” Chester akamuachia. “Kama bado hujajirekebisha, ninaweza kuchagua kutokuoa wakati wowote. Unajua hilo?"
Midomo ya Cindy ilitetemeka. Kuonekana kwa macho yake ya kutojali lakini mazuri kulimjaza hofu na woga. "Sawa, Chester. Usiwe na wazimu. nitaondoka sasa hivi.”
Baada ya lifti kushuka, Cindy alikuwa akitetemeka kwa hasira. Alitamani kumuua Eliza ikiwezekana. Hata hivyo, alichohofia zaidi ni kwamba Chester angeamua kutomuoa. Alimpenda mwanaume huyo. Ingawa alikuwa hamjali na mkatili, bado alikuwa akimpenda.
Kwa upande wa Eliza... Asingechelewa
kushughulika na Eliza baada ya kuolewa na Chester. Cindy akasaga meno. Wakati huo huo simu yake iliita na kuonyesha nambari ngeni.
Akiwa ameshtuka, akapokea simu bila kufikiria sana. Kicheko cha kupendeza kilisikika baadaye. "Hi, Cindy. Ni muda mrefu umepita tangu tukutane. Una akili kiasi gani sasa. Utafunga ndoa na Bwana Choka hivi karibuni.”
Cindy alipigwa na butwaa kwa muda na kuona ni vigumu kuamini. “Wewe ni Lina?”
 
Wakati huo, familia ya Jones ilikuwa imesambaratika na John Jones alikamatwa. Hakuwahi kumuona Lina tangu wakati huo basi, Lina aliwezaje kupata nambari yake ya simu?
“Cindy, sikutarajia ungeweza kuitambua sauti yangu. Nilidhani umenisahau zamani,” Lina alijibu huku akicheka.
Cindy alikunja uso wake asijue la kusema. Alikuwa akijikombakomba kwa Lina wakati huo kwa sababu alikuwa na manufaa kwake. Baada ya Lina kutoweka kwa miaka kadhaa, Cindy hakuthubutu kumsogelea kwani hakujua hali yake ya wakati huo. Lina anaweza kuwa chini na nje wakati huo.
“Umekuwaje miaka hii? Nilisikia kuwa una rafiki mkubwa anayeitwa Sarah Njau, lakini inaonekana hayuko sawa baada ya Alvin kumwacha.” Lina alisikika akiwa ametulia.
Cindy alifungua mdomo wake kidogo. “Umejuaje yote hayo?”
Lina alifoka. "Tangu Lisa akufichue kwa kuiga kazi yake, uhusiano wako na Chester haujakuwa mzuri, sivyo?"
Moyo wa Cindy ukapiga kelele, akanyamaza.
“Sawa. Tusiongelee matukio hayo yasiyofurahisha,” Lina alisema kwa tabasamu, “Narudi Kenya siku iliyofuata kesho. Tukutane nikirudi Nairobi.”
Cindy alihisi kukosa raha. “Unapanga kuja Nairobi? Lakini hili ni eneo la Alvin na Lisa!”
"Ninarudi wakati huu kwa madhumuni ya kushughulika nao," Lina alisema kwa njia nyepesi, "Usijali. Nisingepanga kurudi ikiwa sijawa na ujasiri. Alvin ni kipaji, lakini ikilinganishwa na ulimwengu, yeye si kitu. Kuna watu wengine wanaoweza kumwangamiza kwa urahisi kama kuponda chungu.”
"Lina, wewe ni ..."
“Kumbuka kutomwambia mtu yeyote kuhusu mambo yangu. Sisi ni marafiki, sawa? Bado nakumbuka kwamba unataka kuolewa katika familia ya Choka na kupata nafasi kama Bibi Choka. Ninaweza kukusaidia,” Lina alisema kwa huzuni.
Cindy akashtuka. Alielewa tabia ya Lina vizuri. Lina alikuwa mkatili kuliko mtu mwingine yeyote.
“Lina, karibu tena.” Cindy alitabasamu bila kufafanua.

Sura ya: 735


Katika clubhouse usiku.

Chester alipiga mpira wa pool table kwa nguvu kwa kutumia stick, huku akili yake ikiwa haipo.
Sauti za mipira mingine iliyogongwa kwenye meza zilisikika mara moja. Mpira mmoja hata ukaanguka nje ya meza na kugonga uso wa Rodney.
Rodney aliruka upesi. "Damn, Chester. Hujagusa mwanamke kwa muda mrefu, huh? Kwanini unatutolea mpira nje?” Rodney alidhihaki.
Chester alivuta uso mrefu bila kutamka neno lolote. Rodney na Alvin walitazamana.
“Bro, Cindy si yupo, au hakufurahishi?”
"Ni lini amenifurahisha?" Chester aliuliza kwa sauti ya chini isiyojali.
Rodney na Alvin wote wakanyamaza kwa wakati mmoja. Baada ya muda, Rodney alisema, "Chukua tu mwanamke mwingine. Sio kana kwamba wewe ni mtu wa uadilifu wa hali ya juu. Unacheza na wanawake sana. Hehe. Zaidi ya hayo, huku familia yako ikichukua nusu ya tasnia ya burudani, unaweza kumfanya mwanamke yeyote mrembo alale nawe. Hakuna kinachoweza kukuzuia.”
Alvin alikubali kwa kichwa.
Tofauti na wao, huenda Chester ndiye aliyekuwa mwaminifu kwa mwenzi wake hata kabla ya kufunga ndoa. Kwa kweli, ndoa haikuwa kitu kwake.
“Hah... ” Kicheko kikali kilimponyoka kooni Chester, kikasikika kuwa cha kutisha.
Rodney alitetemeka na kusema bila fahamu, “Vipi kuhusu yule uliyekula naye... Anaitwa nani, mwigizaji huyo...”
"Eliza Robbins," Alvin alikumbusha.
“Ndio. Eliza ni mrembo sana. Pamela amekuwa akizungumzia jinsi alivyo mrembo.” Baada ya Rodney kumaliza kuzungumza, kwa namna fulani aligundua kuwa sura ya Chester imekuwa mbaya. Hata mazingira yalikuwa ya baridi sasa. "Uh ... nilisema kitu kibaya?"
"Chester ana maoni yasiyofaa juu yake. Yeye si kikombe chake cha chai,” Alvin alisema. “Oh, sawa. Angalia jinsi kumbukumbu yangu ilivyo mbaya." Rodney aligonga kichwa chake.
Kichwa cha Chester kilitikisika. Kama angelijua hilo, angechagua kubaki nyumbani. Kuzungumza na Rodney na Alvin kulifanya damu yake ichemke.
"Kwa hiyo, kwanini ulienda hadi kwenye seti leo?" Alvin aliuliza ghafla, "Unaonekana kuwa kuna kitu kinakuvutia, huh?"
Chester alifungua kinywa chake. "Niambie ... Je! nyinyi watu mmewahi kukutana na mwanamke ambaye alikufanya uhisi msisimko licha ya wewe mwenyewe?"
Alvin na Rodney walimtolea macho ya ajabu kwa wakati mmoja.
 
Baada ya muda kidogo, Alvin alitabasamu. “Si ni kawaida yako kusisimka mbele ya kila mwanamke? Kuna ajabu gani? Unapanga kumdanganya mwanamke gani wakati huu?”
“Hahahaaa” Chester akacheka. Ilibainika kuwa machoni pa wengine, alikuwa fisadi kamili.
"Unampenda Eliza, sivyo?" Rodney alisema.
"Labda. Lakini mwanamke huyu hanipi nafasi yoyote.” Chester ghafla akatabasamu na kutabasamu. "Kusema ukweli na nyinyi, ni muda mrefu tangu nilipokutana na mwanamke wa kupendeza."
"Hapana, tayari umeanguka ndani yake, Chester?" Rodney alicheka.
“Huyu jamaa?” Alvin akanyanyua nyusi zake. "Hiyo haiwezekani. Hawezi kuanguka kwa mwanamke. Pengine ni kwa sababu hajashinda penzi la mwanamke huyo.”
“Labda.” Rodney aliitikia kwa kichwa. "Lakini ukweli, baadhi ya wanawake wako tayari kukuacha ucheze nao. Hata hivyo, wanawake wanaojitambua hawatajihusisha na wanaume wanaoenda kuoa. Mwanamke akikukaribia ingawa anajua kuwa utaoa hivi karibuni, kimsingi yeye ni b*tch. Kama ningekuwa mwanamke, nisingefanya hivi.”
Alvin akaitikia kwa kichwa. "Hiyo ni sawa. Chester, ikiwa mwanamke anakukataa, basi mwache. Usim’force”
Rodney alisema huku akitabasamu, “Usijali. Chester sio mtu anayependa kulazimisha watu.
Chester alishindwa cha kusema. Hakika, asingelazimisha watu. Hata hivyo, Eliza, yule b*tch, aliufanya moyo wake kusisimka.

•••
Siku iliyofuata.
Ilikuwa ni siku adimu ya mapumziko. Eliza alilala ndani. Baada ya kuamka, alianza kuandaa kifungua kinywa. Ghafla, alipokea simu.
“Bi Robbins, nilipata taarifa kutoka kituo cha polisi. Baada ya Mason kukamatwa, alikiri kwamba alimchoma Maurine hadi kufa na kuelekeza lawama kwa Charity. Charity hakuwa na hatia. Polisi tayari wamefuta mashtaka ya jinai ya Charity.”
Eliza alikuwa anakaanga yai. Aliposikia habari hizo, hakusogea kwa muda mrefu hadi sauti ya upande wa pili wa simu ikasikika tena. "Bi Robbins, ... Je! bado unasikiliza?"
“Nimekusikia.” Eliza akageuza yai tena. Alisema, "Charity tayari amekufa. Wazazi wake pia wamekufa. Kuna manufaa gani katika kufuta mashtaka yake ya uhalifu?”
Mtu huyo alinyamaza baada ya kusikia hivyo.
"Asante. nakata simu.” Eliza akaweka simu yake chini. Alizima moto na kufunga macho yake. Hakuwahi kuhisi kukasirika tangu kuzaliwa tena.
Mwili wake ungekuwa tayari umeliwa na samaki. Lakini, walisema tu kwamba hakuwa na hatia. Hahah, walichekesha!
Eliza aliweka mikono yake juu ya meza ya jikoni. Alianza kucheka mpaka macho yakawa mekundu. Ilibainika kuwa Mason ndiye aliyemfanyia njama hizo mwaka huo. Lakini, alikuwa na chuki gani na Mason? Familia yake yenye furaha iliharibiwa kabisa kwa sababu yake. Hakuwa na hamu ya kupata kifungua kinywa tena.
Ilipofika saa sita mchana, alifungua mlango na kushuka chini ili kutupa taka. Alipofika chini, kivuli cha mtu kilitokea kwenye mlango wa ngazi. "Ellie..."
Eliza alipoona sura hiyo alihisi karaha moyoni mwake. Mara akageuka na hakutaka hata kutupa takataka nje tena. Hata hivyo, mkono ulimshika kwa nyuma.
"Ellie, mimi ni baba yako." Jacob Robbins alimshika mkono. “Acha tuende.” Eliza aligeuza kichwa nyuma kwa ubaridi.
Kuangalia macho yale ya baridi, Jacob alitetemeka. Hata hivyo, bado aliuma meno yake. “Ellie, mimi ni mgonjwa. Wewe ni nyota sasa, na unapata pesa nyingi. Nipe pesa za kutibu ugonjwa wangu.”
“Utibu ugonjwa wako?” Eliza alicheka. “Una ugonjwa gani? Rekodi yako ya matibabu iko wapi?"
“Ni... Ni nyumbani. Nilisahau kuichukua,” Jacob alisema, “Sihitaji mengi. Nipe tu milioni mia."
"Ugonjwa wako lazima uwe mkali sana. Milioni mia zinatosha kununua figo. Labda una saratani ya figo?" Eliza alisema huku akitabasamu.
"Hiyo ni sawa. Eliza ukitaka nibaki hai basi nipe pesa. Nakuhakikishia sitakuomba pesa tena,” Jacob alisema.
"Sahau. Ulisema vivyo hivyo ulipokuja kuniazima milioni hamsini mara ya mwisho.” Eliza alitoa mkono wake. “Nakumbuka nilisema kwamba itakuwa mara ya mwisho kukupa pesa. Hatuna tena uhusiano wowote kati yetu. Pia, usinichukulie kama mjinga. Unafikiria kuchukua pesa na kumtumia mwanao tena, sivyo?”
 
Jacob, ambaye nia yake ya kweli ilikuwa imefichuliwa, hakuona haya ya kuficha hata kidogo. Alisema kwa sauti tu, “Wewe ni mtoto wangu. Kuna ubaya gani nikikuomba pesa za kujikimu? Unapata bilioni kadhaa kwa mwaka, lakini unataka kuninyima milioni mia tu? Katika ndoto zako. Ninakuambia, lazima unipe pesa leo. Usipofanya hivyo, nitafanya suala hili kuwa kubwa. Nitawaambia watu wengine kuwa wewe, staa maarufu, unakataa kumtunza baba yako. ”
“Utajua mwenyewe.” Eliza akageuka na kuondoka. Hakutaka kumpa Jacob hata senti.
Zamani akiwa bado hajawa Eliza, pesa zote alizimwa na baba yake huyo alipoingia tu kwenye tasnia ya burudani. Miaka yote hiyo, familia nyingine ya Jacob ilitegemea pesa za Eliza kuishi.
Jacob alikuwa amewatelekeza Eliza na mama yake alipokuwa mdogo. Kila Eliza alipokuwa akimfikiria Jacob, alihisi hasira.
“Usiende.” Jacob alimshika na kuanza kupiga kelele, “Jamanii, njooni hapa mtazame! Huyu ni supastaa Eliza Robbins. Mimi ni baba yake.…”
“Inatosha. Acha kupiga kelele. Nitakupa pesa,” Eliza alimkatisha Jacob.

“Haraka basi.” Jacob alitabasamu kwa hasira. Alitumia mbinu hiyo kila mara, na haikushindikana kamwe.
“Nifuate huko juu." Eliza akageuka na kwenda juu. Jacob alimfuata mara moja.
 
Sura ya: 736


Wote wawili hawakujua kwamba wakati wanapanda juu, Chester alikuwa anafika huku akiwa ameweka mkono mfukoni, na kumuona mtu wa makamo akimfuata Eliza huko juu. Akakodoa macho. Aliwafuata, lakini alikuwa amechelewa kwa hatua. Eliza alikuwa tayari ameingia ndani na Jacob.
Baada ya kuingia nyumbani kwake, Eliza alifunga mlango. Alichukua kisu na kumpa Jacob. “Menya hili apple. Nitaenda kuchukua kadi yangu."
“Sawa.” Jacob hakusita hata kidogo. Cha msingi ilikuwani kupata pesa, alikuwa tayari kumenya chochote, achilia mbali apple.
Eliza baada ya kupanda ghorofani kwa haraka akatoa kadi kwenye pochi na kumrushia Jacob. "Kuna milioni moja ndani."
Macho ya Jacob yakaangaza. Haraka akaweka apple na kisu pembeni. Akaiweka kadi mfukoni. "Nilijua kuwa sikukuzaa wewe, binti yangu bure–"
Kabla hajamaliza kuongea alijikuta akianguka chini huku akiufagia mguu wa Eliza.
“Unathubutuje kunipiga?” Jacob alinyanyuka huku akiwa amekasirika. Alipotaka kuinua mkono, ghafla Eliza aliivunja chupa ya mvinyo mahali karibu na kichwa chake.
Vipande vya vioo vilitawanyika usoni mwa Jacob. Macho yake yalibanwa papo hapo kutokana na hofu. Hakuweza kufikiria nini kingetokea ikiwa chupa hiyo ingepigwa usoni mwake ...
Jacob alimeza mate. Alipoona uso wa Eliza maridadi na mzuri, alishtuka tena. "Unathubutuje kunipiga ..."
Kabla hajamalizia sentensi yake Eliza alichukua kipande kimoja cha chupa nyuma yake na kumchoma nacho mkononi. Jacob alipiga kelele kwa maumivu na kujaribu kupinga kwa nguvu zake zote, lakini Eliza alitengua mkono wake mmoja mara moja. Alipopigana zaidi, mkono wake mwingine pia uliteguka.
“Eliza una kichaa. Niue ukiweza! Ilimradi usiniue, hakika nitafichua kilichotokea leo.” Sifa za Jacob zilipinda kutokana na maumivu.
“Unanilazimisha nikuue?” Eliza aliinua uso wake. Macho yake yalijaa ukatili wa baridi.
"Wewe ... utafanya nini?" Jacob alifadhaika. “Usifanye hivyo. Shangazi yako Rachel na Nicholas wanajua kwamba nimekuja kwako leo.”
“Jacob, unadhani mimi ni rahisi kudhulumiwa? Bahati mbaya sana mimi si Eliza wa zamani. Eliza aliyetangulia alikuacha tu umdhulumu kwa sababu ulimpiga kila mara alipokuwa mdogo. Alikuogopa, lakini mimi sikuogopi.” Eliza akasimama. Alikanyaga kidole cha Jacob kwa nguvu.
Jacob alipiga kelele kwa uchungu. Eliza akachukua kitambaa na kumchomeka mdomoni.
"Unapaswa kuridhika na kile ulicho nacho." Eliza alidhihaki, “Nilipokuwa mdogo, hukuwa tayari kulipa hata senti moja kwa ajili ya karo yangu ya shule. Si hivyo tu, hukutaka hata kuniona. Usijali kwamba ulimsaliti mama yangu na kuoa mtu mwingine. Uliendelea kunitusi kwa ajili ya mwanao mwingine ingawa nilipitia magumu mengi kufikia hali niliyo nayo leo. Kumnunulia nyumba, gari, na kumwanzishia kampuni hakukutoshi. Wewe na mkeo ni familia iliyojaa vampires. Mbaya sana..."
Bahati mbaya sana Eliza Robbins alikuwa tayari amekufa. Eliza wakati huo alikuwa Charity.
Hapo awali Eliza alikuwa msichana mwenye moyo mwororo na asiyejua mambo. Japokuwa Charity alikuwa ameukalia mwili wa Eliza, lakini Charity bado alikuwa na kumbukumbu zote za Eliza.
Charity alikuwa mtu ambaye alikufa hapo awali. Maisha yake gerezani yalikuwa magumu. Baada ya hapo, alifanya kazi kwa bidii kwenye mgodi pia.
 
Alikuwa mwanamke mwenye umri wa miaka 22, lakini moyo wake tayari ulikuwa mgumu kama jiwe. Eliza akainama na kupapasa mfukoni mwa Jacob. Alipata simu, na kipengele cha kurekodi sauti cha simu kimewashwa.
Uso wa Jacob ulibadilika.
“Wewe ni baba mzuri sana. Inabidi hata uweke rekodi ya sauti unapokutana nami. Ulikuwa unafikiria kunichafulia na kuiweka kwenye mtandao ikiwa sitakusikiliza, sivyo?” Eliza alicheka kwa baridi na kumfukuza. “Nitakunyang’anya simu. Hata hivyo, ngoja nikutahadharishe kwamba leo nakufundisha somo dogo. Sitakupa hata senti siku zijazo. Hili likitokea wakati mwingine, hakika nitafanya mwanao mpendwa apoteze mkono au mguu. Afadhali niamini. Sasa potea! ”
Jacob alificha macho yake meusi. Akainamisha kichwa na kutikisa kichwa kwa makini. Kisha akauendea mlango huku akichechemea.
Wakati alifungua mlango, kivuli cha mtukilimfunika kama sanda. Mwanaume huyo alikuwa na uso mzuri na wa kiungwana. Mwili wake wote ulitoa ubadhirifu. Macho ya Jacob yaliangaza alipomwona. Mara moja akasema, “Bwana mdogo, lazima uwe mtu wa Eliza. Hebu niambie, kwanini huyu mwanamke ni mbaya sana? Mimi ni baba yake lakini alitengua mikono yangu na hata kunipiga.”
Chester aliinamisha kichwa huku macho yake yasiyo na mwisho yakimtazama Jacob.
Alikuwa amemuona Jacob akiingia huku mwili mzima ukiwa bado upo sawa. Baada ya muda mfupi tu, Jacob sasa alikuwa na majeraha machache usoni na mikono yake yote miwili ililala kiunyonge kando yake kutokana na kulegea. Mwangaza wa ajabu uliangaza kwenye macho meusi ya Chester.
“Inaonekana hukutilia maanani maneno yangu sasa hivi.” Eliza akasogea. Uso wake maridadi ulikuwa na tabasamu juu yake, lakini ulitoa hisia za giza na hatari.
Ilikuwa ni mara ya kwanza Chester kuona upande huo wa Eliza. “Ulimfanya hivi?”
"Ndio, yeye ndiye aliyenifanya hivi." Jacob aliitikia kwa kichwa huku akitetemeka. “Huyu mwanamke ni mkatili sana. Mimi ni baba yake mzazi. Nilikuwa naomba tu pesa kutoka kwake kwa sababu naumwa.”
"Kwa hivyo ... hata baada ya kuzungumza nawe kwa muda mrefu, unafikiri nilikuwa natania?" Eliza alicheka na kupiga hatua mbele.
Jacob aliogopa sana hata hakuthubutu kubaki pale kwa sekunde nyingine. Hakuchukua hata lifti na kukimbia kwa kasi kwa kutumia ngazi.
Eliza akageuka na kurudi nyumbani kwake. Alifunga mlango kwa nguvu, lakini haukujifunga. Ulizuiwa na mkono wa Chester.
"Eliza, wewe ni kidume sana, huh?" Chester alimtazama mwanamke aliyekuwa mbele yake. Alivaa fulana nyeupe na suruali ya kawaida ya kijivu. Nywele zake zilikuwa zimefungwa kwenye mkia wa farasi. Akiwa mkatili, angeweza hata kumpiga baba yake mzazi. Mwanamke wa aina hii alikuwa nadra.
"Siyo biashara yako ya kujua." Eliza aliinua kichwa chake huku macho yake yakiwa yamejawa na dharau.
Alikuwa katika hali mbaya sana, hasa sasa alipokuwa akikabiliana na mtu aliyempeleka jela.
Uso wa Chester ulibadilika. Akakodoa macho. “Pole sana Eliza. Hakuna mtu aliyethubutu kuzungumza nami hivi hapo awali.”
“Nina hali mbaya sana hivi sasa,naomba uniache tu.” Eliza alisema kwa upole.
 
Chester aliposikia hivyo alipigwa na butwaa. Alionekana kana kwamba alikuwa amesikia mzaha. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mwanamke kuthubutu kuongea naye hivyo.
“Basi kaa mbali nami,” Eliza aliendelea.
"Eliza, unatamani kifo?" Chester alikasirika. "Wewe ni msanii wa kampuni yangu, lakini ulimpiga baba yako kwa mikono yako mwenyewe hadi hali hiyo. Unadhani hataripoti polisi? Au unafikiri atakuwa mjinga sana kutishiwa na wewe?”
"Bila shaka, najua hatahisi kutishwa nami."
Eliza aliingia ndani na kuchukua kisu mezani.
"Unafanya nini?" Chester alifikiri Eliza alitaka tu kumenya tunda au kitu, lakini alikuwa amevaa glavu wakati anachukua kisu. Aliupeleka mkono wake nyuma yake na kujichoma kisu kwa nguvu. Damu ilichuruzika mgongo mzima mara moja.
"Eliza, una wazimu?!" Macho ya Chester yalimtoka huku akipiga kelele kwa hasira.
Eliza alimpuuza. Baada ya kutoa kisu, alivua glavu na kuwaita polisi. Alisema kwa unyonge, “Halo, hiki ni kituo cha polisi? Mtu alinichoma kisu. Natoa taarifa polisi.”
Chester alitazama tukio hilo kwa mshtuko.
Mpaka Eliza akaweka simu chini, ndipo Chester akaelewa kila kitu. "Eliza, wewe ni mwanamke mwendawazimu."
“Uko sahihi. Mimi ni mwanamke mwendawazimu.”

Sura ya: 737


Eliza aligeuza kichwa chake nyuma, na uso wake ulikuwa ukibadilika rangi. “Kwa kweli, ni pesa tu, lakini sitaki kumpa hata senti. Kwanini mimi? Zaidi ya kunizaa, hakunitumia hata senti moja. Nilipokuwa mdogo, mimi na mama yangu tulikuwa tu mifuko yake ya kupiga ngumi. Alitupiga kila alipotaka. Baada ya kukua na kuwa supastaa, alikuwa akija kunitafuta ili kuniomba pesa. Sio tu kwamba sina budi kumkimu, bali pia nalazimika kumhudumia mwanawe na mke wake wa sasa pia. Ha, hakika ninamfanya afe leo. ”
Chester alifungua mdomo wake kidogo. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuona mwanga wa baridi na wa kichaa kama huo kwenye macho ya mwanamke. "Huogopi kwamba ... nitasema ukweli?"
“Bwana Choka, kama hutaki kunipoteza mimi mtengeneza pesa wa kampuni yako, ukae kimya. ” Eliza alitabasamu kabla ya kuzimia.
Lakini, hakuanguka chini. Chester alimbeba kwa haraka. Mwanamke katika kumbatio lake alikuwa mwembamba, na uso wake ulikuwa umepauka kana kwamba angekufa sekunde yoyote. Chester alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa umejipinda kama nyuki. Hapo hapo akatoa huduma ya kwanza kwa Eliza, kisha akambeba na kushuka chini kwa haraka.
Harakaharaka akampeleka kwenye chumba cha dharura cha hospitali yao. Alivaa koti jeupe kisha akatumia mkasi kukata nguo zake wazi kutibu jeraha lake. Makadirio ya Eliza yalikuwa sahihi sana. Jeraha lilikuwa kubwa, lakini halikuwa hatari kwa maisha.
Baada ya habari kutoka kuwa supastaa Eliza Robbins alidungwa kisu nyumbani kwake na kulazwa hospitalini, ilivutia vyombo vya habari. Haikupita hata nusu saa tayari kulikuwa na mapaparazi wengi kwenye lango la hospitali hiyo. Wakati huohuo, kundi jingine la wanahabari lilikuwa likikimbilia kituo cha polisi.
Baada ya kuangalia kamera za usalama, polisi walimkamata mshukiwa mkuu, Jacob Robbins.
Wakati Jacob anapelekwa katika kituo cha polisi, bado alikuwa akibweka, “Mimi sio mhalifu. Sikujaribu kumuua Eliza. Ilikuwa ni yeye. Alinipiga! Alimpiga baba yake mwenyewe. Majeraha yote niliyopata yalitokana na Eliza.”
“Inatosha. Nyamaza. Silaha aliyochomwa Eliza ni kisu. Alama zako za vidole ziko juu yake, na kadi yake ya benki iko mfukoni mwako pia." Polisi walipiga meza.
Jacob alipigwa na butwaa. Alielewa kila kitu mara moja. “Yeye ndiye aliyenipa kadi. Alinipa kisu hicho na kuniambia nimenya apple. Kwa makusudi alinifanya niache alama za vidole kwenye kisu.”
“Ushahidi uko wapi?” polisi waliuliza, "Unasema maneno matupu bila uthibitisho."
“Ushahidi?” Jacob alisema kwa haraka, “Niligongana na mtu nilipokuwa naondoka. Yeye ni shahidi. Hakuna kilichotokea kwa Eliza wakati huo.
“Unamzungumzia mtu huyu?” Polisi walipiga picha nje. Jacob aliitazama. Akaitikia kwa kichwa. “Ndiyo, ni yeye.”
“Samahani, tayari tumemhoji. Alisema alipoingia ndani aliona Eliza amepoteza fahamu na unatoroka kwa hofu. Yeye ndiye aliyempeleka Eliza hospitalini,” polisi walifoka.
 
Jacob alipigwa na butwaa. Baada ya muda, ilionekana kana kwamba alikuwa ameenda wazimu. “Eliza, wewe b*tch. Unathubutuje kunitupangia njama kama hii?!" Hata hivyo, hakuna aliyemwamini.
Muda si mrefu, wanamtandao walichimbua historia ya Jacob. Alikuwa baba mzazi wa Eliza, lakini alipenda kucheza kamari na kunywa pombe tangu Eliza alipokuwa mdogo. Mtu fulani alijitokeza na kusema kwamba alikuwa jirani ya Jacob kwa zaidi ya miaka 20 hapo awali. Sio tu kwamba Jacob hakuwa na kazi wakati huo, lakini mara nyingi aliwapiga Eliza na mama yake pia.
Baadaye, mama Eliza alishindwa kuvumilia na akaachana na Jacob. Alimchukua Eliza na kuondoka.
Jacob alioa tena mwanamke mwingine na kupata mtoto naye. Lakini, familia nzima ilikuwa ya walafi na wavivu. Kabla ya Eliza kuwa maarufu, Jacob, mke wake mpya, na mtoto wake waliishi maisha dunii. Baada ya Eliza kuwa maarufu, Jacob alinunua nyumba chache ghafla. Mwanawe hata aliendesha gari aina ya Porsche ambalo lilikuwa na thamani ya zaidi ya mamilioni mengi na kuanzisha kampuni. Hata hivyo kwa mujibu wa wafanyakazi wa kampuni hiyo walisema mtoto wa Jacob hana uwezo hata kidogo. Kampuni ilikuwa ikipoteza pesa wakati wote. Familia nzima ilikuwa inanyonya pesa za Eliza.
Wanamtandao walianza kuwakemea kwa hasira.
[Eliza ana bahati mbaya sana kuwa na baba kama huyo. Yeye ni mnyonge sana.]
[Hah, nilisikia mke wa Jacob alikuwa akicheza poker siku nzima. Wote watatu katika familia wamekuwa wakitumia pesa za Eliza. Walipokosa pesa, wangeomba zaidi kutoka kwa Eliza.]
[Nadhani Eliza hakuweza kuvumilia tena. Hakutaka kumpa Jacob pesa zaidi wakaanza kugombana. Kwa hiyo, Jacob alichukua kisu na kumchoma Eliza. Jacob ana rekodi ya uhalifu. Nilisikia alitumia kisu na kumchoma mke wake wa zamani pia. Yeye ni mbaya sana.]
[Mwana wa Jacob ni mtu asiyefaa kitu. Anajua tu kuendesha gari lake la michezo na kutongoza wanawake kila siku. Nyumba na gari lake vyote vililipwa na Eliza. Eliza hakuwa tayari, hivyo Jacob alisema anakwenda kufichua kwa vyombo vya habari kwamba Eliza hataki kumjali na kumnyanyasa. Hakuwa na chaguo.]
[Ninajisikia vibaya kwa Eliza. Nashangaa hali yake ikoje sasa?]
[Jacob lazima aadhibiwe vikali. Mtu wa aina hii hastahili kuwa baba hata kidogo.]
Katika ukumbi wa hospitali, Chester aliwasha sigara kimya kimya akiwa bado amevalia koti lake jeupe.
Meneja wa Eliza, Hamid Kipchoge, alikimbia. Alipomuona Chester, alishtuka. “Dokta Choka... Wewe...”
Kwa kweli, alikuwa na mambo mengi ya kuuliza. Kwa mfano, kwanini Chester alikuwa nyumbani kwa Eliza? Kwanini Chester ndiye aliyempeleka Eliza hospitali?
Kwa bahati nzuri, yeye tu, Shedrick, na polisi walijua kuhusu hilo. Itakuwa shida ikiwa mtu angepiga picha.
"Kuna nini kati ya Eliza na Jacob?" Chester aliuliza huku akionyesha kutojali.
Hamad alipumua. "Ni karibu sawa na kile kinachosemwa kwenye mtandao. Jacob hajawahi kumhudumia Eliza. Wakati Eliza alikuwa na umri wa miaka minne, wazazi wake waliachana. Baada ya hapo, aliishi na mama yake. Mama yake alikuwa na maisha magumu alipokuwa akimlea. Alienda kazini mchana na hata ikamlazimu kufanya kazi za muda usiku. Hatimaye, Eliza aliweza kupata umaarufu fulani.
“Hapo ndipo babake Eliza alianza kumtafuta. Alimtaka ampe pesa za matumizi kila mwezi. Hapo awali, Eliza alikuwa mtoto mwaminifu. Aliogopa kwamba Jacob angemkashifu. Pesa zote alizopata zilichukuliwa na Jacob. Zingine alimpa mama yake mzazi. Kwa kweli, hakuwa na pesa nyingi. Ni kwa sababu tu amesikia kuwa sasa ana pesa nyingi baada ya kupata umaarufu kwa kasi katika miaka hii miwili.
"Naelewa.” Chester akaitikia kwa kichwa. "Unaweza kuingia." Mara moja Hamid aliingia wodini.
Chester alisimama mbele ya dirisha. Hangeweza kujizuia kuwaza, 'Je, hiyo ndiyo sababu alichagua kujihatarisha? Ndiyo sababu iliyomfanya achukue kisu na kujichoma?’ Kwa kweli, ilikuwa mara ya kwanza kuona mwanamke ambaye angejitendea kwa ukatili sana. Eliza, Eliza… Alikuwa mtu wa aina gani? Alimfanya aseme uongo kwa polisi na kusema ni Jacob ndiye aliyemchoma kisu. Hah!
Sura ya: 738
 
Katika wodi.
Hatimaye Eliza alirejewa na fahamu. Aliwaona kwanza Hamid na Loida. Hata hivyo, Hamid alikuwa na shughuli nyingi. Aliendelea kupiga simu huku mgongo wake ukitazamana na Eliza.
"Samahani. Samahani sana. Labda italazimika kuahirishwa hadi mwezi ujao kwa sababu ya jeraha la Eliza... Ikiwa uko katika haraka, unaweza kubadilisha hadi kwa msanii mwingine. Au unaweza kumsubiri Eliza...”
“Hatimaye umeamka. Niliogopa hata kufa.” Loida alimuona Eliza kwanza. Macho yake yakaangaza.
Hamid aligeuza kichwa chake pia. Alikata simu baada ya kuongea sentensi kadhaa na kumtazama Eliza.
"Jeraha lako linaniumiza sana kichwa." Hamid alisema.
“Samahani, Hamid,” Eliza aliomba msamaha kwa unyonge. "Labda siwezi kujiunga tena na filamu ya Mke Mwenza. Na bado kuna matangazo mawili na hafla tatu ambazo nilipangwa kuhudhuria mwezi huu.”
"Watu kutoka kwa matangazo na hafla walipiga simu. Mmoja wapo lilikuwa ni la dharura zaidi, kwa hivyo nilikataa. Tunapaswa kulipa fidia kwa uvunjaji wa mkataba pia. Wengine walisema wako tayari kukusubiri.” Hamid alisugua nywele zake. "Mtu ambaye tumemuangusha kwa kweli ni Director Kalulu. Alidhamiria kukufanya uwe maarufu na kukuweka kama kinara wa kike."
Eliza akafumba macho. Kutoweza kushiriki katika filamu ya ‘Mke Mwenza’ ilikuwa ni huruma sana, lakini hakujuta. Alikuwa katika hali mbaya sana jana yake wakati Jacob alikuja na kumkosea. Alikuwa akitaka kumuondoa kwa muda mrefu tayari.
“Hata hivyo, tayari nimeshamuuliza daktari. Alisema majeraha yako sio makubwa na unaweza kusimamia kujiunga na uzalishaji baada ya mwezi.
“Director Cheever alisema anaweza kurekodi matukio mengine kwanza. Hata hivyo, baada ya kurudi kwenye utayarishaji, hata ikibidi ufanye kazi kwa muda wa ziada na kukesha usiku kucha, itabidi umalize kurekodi matukio yako mengine ndani ya miezi miwili. Katika kipindi hicho, kutakuwa na matukio mengi ya kushughulikia nayo pia. Mwili wako…”
"Naweza kufanya." Eliza aliitikia kwa kichwa.
Hamid hakuwa na furaha. Badala yake, alikunja uso. “Ingawa unaweza kujiunga na utayarishaji wa filamu pamoja na na jeraha lako bado halijapona kabisa. Ukiingia kwenye seti, itaathiri jeraha...”
"Ni sawa," Eliza alisema, "Director Kalulu tayari ananikubali kwa kuwa yupo tayari kunisubiri. Ni heshima yangu pia. Ikiwa siwezi hata kuvumilia usumbufu mdogo kama huu, ninawezaje kuishi kulingana na matarajio ya Director Kalulu?"
Hamid alipumua. Mtazamo wa mawazo mazito ukaangaza machoni pake. "By the way, Eliza, kuwa mkweli kwangu. Nini kinaendelea... kati yako na Bwana Choka? Kwanini alikuwa mahali pako? Pia, nilisikia kuwa ndiye aliyekuleta hapa.”
"Sijui kwanini alikuja kwangu pia." Eliza alikunja uso. Alisema kwa kejeli, "Lakini wanaume daima hujazwa na mawazo machafu wanapoona wanawake wazuri."
Loida alipigwa na butwaa. "Oh Mungu wangu, si ajabu Bwana Choka alikuja kwenye seti ya utengenezaji wa filamu jana. Hata alikuja kwenye chumba chako cha kuvaa. Nilidhani alikuja kumtembelea Cindy, lakini ... Tsk, Bwana Choka ni mwingi sana. Mpenzi wake alikuwa karibu, lakini bado alikuwa wazi ... "
“Kuwa makini.” Hamid alimkodolea macho Loida. Hakujisikia furaha. Badala yake, alikuwa na maumivu ya kichwa kidogo. Eliza ndiye msanii bora zaidi kati ya aliokuwa nao. Alitumaini tu kwamba Eliza angefanya kazi kwa bidii ili kupata pesa. Hakuwa na matumaini kwamba Eliza angehusika katika mahusiano yoyote, hasa kwa vile Bwana Choka hakuwa mtu yeyote wa kawaida ambaye angeweza kumuudhi.
“Kusema kweli, ikiwa Bwana Choka asingekuwa anafunga ndoa na asingekuwa na rafiki wa kike rasmi, ningefurahi sana ikiwa angetaka kukufuata. Baada ya yote, Bwana Choka ana mamlaka makubwa. Anaweza kukuwezesha kufikia urefu mkubwa zaidi. Lakini... umma tayari unajua kwamba anakaribia kuoana na Cindy. Itakuwa shida ikiwa utahusika naye. Habari zikitoka, sifa yako itaharibika.”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…