Simulizi: Lisa

SIMULIZI.............LISA
KURASA........131-235

Sura ya: 231

“Tatu bora? Hilo haliwezekani.” Mzee Kimaro alishikwa na butwaa.

"Unaweza kuangalia taarifa ya kifedha ya familia ya Campos kwa mwaka huu. Familia ya Campos kwa kawaida hawana biashara, wao huwekeza hisa kwenye makampuni makubwa. Baada ya Jack kuanza kusimamia kampuni, alisaini makubaliano na familia ya Campos ambayo hutoa faida ya asilimia tano kwao. Kana kwamba familia ya Campos haina nguvu za kutosha.” Taarifa hizo zilikuja kuwa pigo kwa Mzee Kimaro.

"Mara tu familia ya Kimaro itakapozama, familia ya Campos ina uhakika wa kuwa ya kwanza ambapo hawawezi kusubiri kuchukua usimamizi wa kampuni hiyo. Ikiwa nitamiliki KIM International, hadhi ya familia ya Kimaro haitabadilika kamwe. Hata hivyo, ni juu yako. Hata kama huna mpango wa kuniruhusu kuchukua kampuni, bado ninaweza kulinda hadhi yangu nchini Kenya kwa njia zangu mwenyewe. Katika hali hiyo, hali ya familia ya Kimaro haitakuwa na uhusiano wowote na mimi…”

“Lakini ugonjwa wako…” Mzee Kimaro alikuwa na wasiwasi.

“Kama huniamini, ni sawa. Niko bize, na ni lazima nikate simu sasa…”
Kwa hayo, Alvin alikuwa karibu kukata simu.

Hapo hapo, Mzee Kimaro akajibu mara moja, “Sawa, mimi tayari ni mzee. Siwezi kushindana na vijana. Nitakuruhusu uchukue KIM International, lakini ninatumai kuwa utaisimamia vyema. Mam’mdogo wako… Amekukosea, na sitarajii umlipishie kisasi. Baada ya kusema hivyo, usiende mbali sana. Baada ya yote, sisi ni familia."

"Babu, mimi hufuata kanuni ya jicho kwa jicho na jino kwa jino." Alvin alisisitiza.

“Wewe…” Mzee Kimaro alikosa la kusema.

“Huna uwezo wa kujadiliana nami tena.” Baada ya Alvin kukata simu, macho yake yalidhihirisha kupuuzia aliyoyaongea.

Lisa hakupenda maneno yake yaliyoashiria visasi. Alianguka mikononi mwake na kumkumbatia kwa nguvu. Kisha, alibadilisha mada. Je! ni kweli familia ya Campos ilifanikiwa kuwa kati ha familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya na mali zao?"

"Nini unadhani, huniamini?" Macho ya Alvin yalififia polepole.

“Hilo haliaminiki kabisa. Familia ya Campos daima imekuwa na hadhi ya chini. Nilikuwa na fikra kwamba itakuwa familia ya Choka na familia ya Shangwe ndizo ambazo zinaweza kuingia kwenye tatu bora.”

“Ndio. Familia ya Campos imekuwa ikijificha vizuri sana. Kama isingekuwa kwa ajili ya harusi ya Jerome wakati huu, nisingechunguza historia ya familia yake,” Alvin alisema “Familia ya Campos ni tata. Ninaogopa kwamba baba yangu wa kambo si rahisi kama anavyoonekana.”

Lisa alipigwa na butwaa. “Nimemwona Mason mara mbili. Ananipa hisia kwamba yeye ni mpole na mwenye urafiki. Uvumi unadai kwamba amekuwa akijishughulisha na sanaa na muziki na havutiwi kabisa na mali na mamlaka ya familia yake.”

"Nilikuwa nikifikiria hivyo pia, lakini Mason Campos ni mtu wa chinichini sana. Nadhani anajaribu kutumia njia hizo kugeuza mawazo yetu mbali naye.” Alvin alijaribu kufikiria.

Lisa aliuliza. "Kwa kuwa ni familia ya Campos iliyopanga njama ya picha dhidi yako, jambo hili linaweza kuhusishwa na Mason?"

“Labda…” Moyoni, Alvin alifadhaika kidogo. Aliinamisha kichwa chake na kumbusu kwenye midomo mara moja. "Nitaweka dhiki zote nyuma yangu kwa sasa. Hebu tufanye jambo la kufurahisha…”

“Aa…”
•••
Katika makazi ya familia ya Kimaro, Mzee Kimaro alishika simu huku akiwa amekaa kwenye kiti cha mbao, macho yake yakionyesha hisia tata.

“Kwa hiyo mazungumzo yako na Alvin yalikwendaje?” Bibi Kimaro akammiminia kikombe cha kahawa.

“Kwa kweli, hakuna maana kubishana kuhusu hilo. Yeye ni mjukuu wa familia ya Kimaro, hata hivyo. Nilipotazama video ya kuhojiwa yaya wake, nilihuzunika. Tuna deni kubwa kwake. Zaidi ya hayo, ni familia yetu wenyewe iliyofichua picha hizo…”

“Unafikiri ni nani alifanya hivyo?” Bibi Kimaro aliuliza.

"Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Lisa alidai kwamba ilikuwa familia ya Campos, kwa hivyo nadhani atakuwa ... Jack." Mzee Kimaro alihema kwa kukata tamaa. "Alvin aliniambia kuwa familia ya Campos imefanikiwa kuingia katika familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya."

Bibi Kimaro alishikwa na butwaa. “Inawezekanaje?”

“Bado unakumbuka familia ya Campos ilivyokuwa miaka 20 iliyopita? Nilimdharau Mason enzi hizo. Ingawa ana talanta ya muziki, hawakuwa na kitu kabisa enzi hizo. Baadaye, Lea alisisitiza kuisaidia familia ya Campos, na mimi nilifumbia macho. Ikiwa hii ni kweli, hufikirii kwamba familia ya Campos imekuwa ikituhujumu kwa kujificha vizuri?” Mzee Kimaro alieleza wasiwasi wake.

“Ndio. Wakati wa harusi ya Lea nakumbuka Mama Campos alivyokuwa akinung'unika jinsi biashara yao ilivyokuwa mbaya. Alitumaini kwamba tungeweza kusaidia familia yake.” Bibi Kimaro alijawa na huzuni.

“Nilikuwa namchukia Alvin kwa kuniharibia heshima ndiyo maana nilimuachia Jack kusimamia KIM International. Lakini nikiendelea kumwacha aisaidie familia ya Campos, familia ya Kimaro itapoteza sifa ya kuwa familia bora zaidi hivi karibuni.” Mzee Kimaro alimpigia simu moja kwa moja wakili wake. "Njoo hapa."

Katika muda usiozidi saa 12, habari kwamba Mzee Kimaro alihamisha hisa na mamlaka yake yote kwa Alvin zilikuwa zimesambaa Nairobi nzima. Wazao wa familia ya Kimaro ndio walikuwa wa kwanza kumtafuta Mzee Kimaro.

Valerie alikuwa wa kwanza kupinga kati yao. “Baba, una akili? Unawezaje kumruhusu Alvin kuchukua nafasi ya mwenyekiti wa KIM International? Hukumbuki jinsi alivyotufanyia hapo awali?”

"Umesemaje, sina akili?" Mzee Kimaro alikasirika sana hadi akahisi kutaka kumpiga makofi hadi kufa.

“Baba naogopa Alvin atanilenga baada ya kuchukua kampuni kwani ananichukia.” Valerie alizungusha mikono yake kwenye mguu wa Mzee Kimaro kwa mshtuko. “Kaka, Dada, ongeeni na baba, Alvin ataniua!”

Mdomo wa Spencer ulitetemeka. “Sina mgogoro na Alvin hata hivyo. KIM International itakuwa imekufa majini ikiwa hatutamruhusu kusimamia kampuni. Kila mtu huko nje anaichukulia familia yetu kama kituko kwa sasa. Wanasubiri tu kutuona tukianguka.”

“Vipi wewe?! Wewe ni mtoto wa pekee wa kiume kwa baba na mama. ulitakiwa uwe na nguvu kuliko wajukuu, lakini huna uwezo sana,” Valerie alimtukana.

"Nyamaza!" Mzee Kimaro alielekeza macho yake kwa Jack bila subira. “Unafikiri nini Jack?”

Jack alikunja ngumi. Alikuwa amejitahidi sana kabla ya kupata nafasi yake ya uenyekiti katika kampuni. Lakini, ikawa kwamba Alvin angechukua tena nafasi hiyo muhimu katika siku chache. Ilikuwa haiwezekani kwa Jack kuwa sawa na hilo. “Babu ni sawa na wewe kutishiwa na Alvin namna hii? Amekuwa akikukosea heshima waziwazi. Mara tu atakapopata nafasi ya kuongoza, ninaogopa atakudharau zaidi. Zaidi ya hayo, karibu amuue mama yake mzazi siku chache zilizopita. Ugonjwa wake umerejea.”

“Hasa. Mtu mwenye ugonjwa wa akili anawezaje kuchukua jukumu la KIM International?" Valerie akaongeza haraka.

"Kabla sijafikia uamuzi huu, mna suluhisho gani?" Mzee Kimaro alimkazia macho Jack. "Nilikupa nafasi, lakini ulichagua kufichua ugonjwa wa akili wa Alvin kwa umma badala ya kushughulikia mambo ya kampuni."

Jack ghafla alitazama juu kwa macho mekundu. “Sikufanya hivyo babu. Kuna mtu ananifanyia njama.”

“Unafikiria nini, Mason?” Mzee Kimaro alielekeza macho yake makali kwa mkwewe ghafla.

Mason alipigwa na butwaa kwa muda. Kisha akanung’unika, “Sina uhakika sana kuhusu hilo…”

Lea hakuweza kujizuia kusema, “Baba, Mason kwa kawaida hutumia wakati wake kutunga muziki. Hata hajali kinachoendelea kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos. Je, angewezaje kujua lolote kuhusu hili? Pia, Jack ni mwanangu na ninaelewa tabia yake. Nina hakika ni mtu mwingine aliyevujisha picha."

“Kwa hali hii…” Mzee Kimaro alichukua kikombe cha kahawa na kunywa kidogo kabla hajaendelea. “nilivyoamua imetosha. Hakuna haja ya kujaribu kunishauri tena. Machoni mwangu, hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kulinda nafasi ya familia ya Kimaro kama familia bora zaidi nchini Kenya.” Mzee Kimaro alisimamia msimamo wake. Hakuna mtu aliyekuwa na ujasiri wa kuzungumza upuuzi tena.

Mishipa iliyovimba ilionekana kwenye ngumi za Jack. Baada ya Jack kutoka nyumbani, alipiga mlango wa gari kwa nguvu. Akatoa simu yake na kumpigia Jerome. "Kuanzia sasa na kuendelea, Alvin ndiye mtoa maamuzi mkuu katika kampuni. Atakaporejea kwenye kampuni, ninahofia anaweza kufuta makubaliano kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos, na kufanya aslimia tano za faida kuwa batili.”

Sura ya: 232

“Nini?” Jerome alipiga kelele kwa hasira, "Nimewekeza sana katika uzalishaji wake na sasa unataka nipate hasara kubwa?"

“Hasara gani kubwa? Hamjavuna faida ya kutosha kabla ya hili?” Jack alisugua kichwa chake. "Isitoshe, niambie ukweli, je, familia ya Campos ilivujisha picha za maisha ya Alvin?"

“Una wazimu kumuamini Lisa? Mtu wa nje kama mimi angewezaje kupata picha hizo?" Jerome alishangaa.

Jack alikaa kimya huku taswira ya baba yake ikiingia kichwani mwake. Lakini kwa mawazo ya pili, ilionekana kuwa haiwezekani kwamba Mason Campos ambaye siku zote alikuwa hajali mambo hayo angefanya kitu kama hicho. “Hata hivyo, kila mtu katika familia ya Kimaro anashuku kuwa mimi ndiye niliyesababisha haya. Alvin ataniangamiza mara tu atakapopata tena ushindi wa juu.”

“Usijali. Utapata hisa za mama yako mwishoni kwa njia fulani. Jerome alikata simu hii na kupiga nyingine baada ya hapo. "Mpango haukufaulu." “Hmm, nilidharau ujasiri wa Alvin na Mzee Kimaro. Sembuse huyo mwanamke Lisa.”

Jerome alikaza macho yake. Alikuwa ameangalia historia ya Lisa hapo awali. Mwanamke huyu aliibuka hivi karibuni tu kuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investments. Alikuwa binti mdogo tu kutoka Tanzania. Hata hivyo, wakati wa kipindi cha moja kwa moja cha jana yake, mwanamke huyo alidumisha utulivu wakati akizungumza na taifa zima la Kenya—bila kusahau mawazo yake makali na ya kufikirisha huku akiipa changamoto familia yenye nguvu zaidi ya Kimaro.

Haikuwa makosa kusema kwamba Lisa alikuwa ameongoza kampuni ya Alvinarah kupitia shida hii wakati Alvin akiwa mgonjwa. Kwa sababu fulani, ilimkumbusha kuhusu mchumba wake, Melanie. Walikuwa dada wa kambo kutoka kwa baba mmoja lakini Melanie alikuwa kama mjinga.

“Kwa hiyo, nini kinachofuata?” Jerome aliuliza.

"Kwa bahati nzuri, nina mpango mbadala. Ni wakati wa kumpeleka kwenye uwanja wa vita." Mtu yule kwenye simu alijibu.

“Sawa. Nina imani na wewe kabisa.” Jerome alijibu kwa unyenyekevu. Alisikiliza mawazo ya kimkakati ya huyo mtu mwingine kwenye simu. Bila shaka, familia ya Campos ingekuwa familia yenye nguvu zaidi nchini Kenya kwa muda mfupi. Enzi ya familia ya Kimaro… ilikuwa inakaribia mwisho.
•••
Siku iliyofuata, Bibi Kimaro alimpelekea Alvin fomu ya uhamisho wa umiliki wa hisa kwenye jumba lake la kifahari ufukweni mwa bahari huko mombasa. Alipoingia ndani ya nyumba hiyo, aliona hakuna mtu mwingine ndani ya nyumba hiyo isipokuwa Aunty Yasmine ambaye alikuwa akisafisha sakafu.

“Alvin yuko wapi? Ametoka?”

"Bwana Mkubwa na Mkewe wameenda kununua mboga kwenye duka kubwa lililo jirani." Shangazi Yasmine alipiga goti ili kumsalimia yule kikongwe.

"Kununua mboga?" Maneno yale yalimponyoka kinywani Bibi Kimaro bila kujijua. Asingeweza kuamini kuwa mjukuu wake alikuwa ameenda kununua mboga ikiwa asingesikia kwa masikio yake mwenyewe.

"Alikuwa na matatizo ya ugonjwa siku mbili tu zilizopita. Anapaswa kupumzika nyumbani. Kwanini hukumzuia kutoka nje?”

“Usijali Bi Mkubwa. Bwana Kimaro hana tatizo kabisa na huchangamka sana anapokuwa na mkewe.” Kabla sauti yake haijakatika, vicheko vya furaha vilisikika kutoka nje.

Bibi Kimaro alitazama kupitia dirishani. Wanandoa wachanga walioshikana mikono walikuwa wakitembea kuelekea nyumbani. Nywele ndefu za Lisa zilining'inia mabegani mwake. Umbo lake zuri liliweza kuonekana licha ya suruali ya jeans ya mguu mpana na fulana nyeusi aliyokuwa amevaa. Pia alikuwa amevalia jozi ya viatu vyeupe vya turubai. Alionekana nadhifu na mchangamfu.

Karibu naye, Alvin alionekana mtanashati na mwenye furaha akiwa amevalia mavazi meupe ya kawaida. Alikuwa ameshika mifuko miwili ya shopping huku uso wake ukiwa na tabasamu la kupendeza. Wenzi hao walionekana kama watu waliooana hivi karibuni. Hasa, hakuonekana kama mtu ambaye alikuwa na tatizo lolote la akili.

Yule kikongwe alipigwa na butwaa kabisa kumuona. Ilikuwa ni muda mrefu sana kwamba hakuweza kukumbuka mara ya mwisho alipomwona akiwa na furaha hivi.

Bibi Kimaro alikuwa amejitayarisha hata kwa ukichaa wa Alvin akiwa njiani kwenda kwake. Hakika ilikuwa ni kutokana na matarajio yake kumuona katika hali hii ya utulivu na uchangamfu.

Wenzi hao wachanga walipomwona yule mwanamke mzee walipoingia ndani ya nyumba, mara tabasamu usoni mwa Alvin likatoweka. Macho yake yalionyesha uhasama na kujihami. Bibi Kimaro alihisi kana kwamba sindano imeuchoma moyo wake.

“Habari, Bibi,” Lisa alimsalimia mwanamke huyo mzee kwa upole kana kwamba hakuna jambo lolote baya lililokuwa limetokea kati yao hapo awali.

Bibi Kimaro alimpa tu mtazamo wa kijeuri, akikataa kujibu salamu yake.
Hasira ikawaka usoni mwa Alvin. “Kama umekuja kumkosea heshima mke wangu, tafadhali ondoka.”

“Wewe...” Bibi Kimaro aligugumia kwa hasira. “Mimi ni bibi yako. Utafurahi tu baada ya mimi kufa?"

“Ninachojua ni familia ya Kimaro ndiyo iliyonimwagia chumvi kwenye kidonda changu. Ningekuwa nimenaswa kwa nguvu katika hospitali ya magonjwa ya akili kama si Lisa.” Alvin alitabasamu kwa uchungu. "Ikiwa nyote bado mnaniona kama familia, basi kitu kidogo kabisa mnachoweza kufanya ni kumwonyesha heshima."

Bibi Kimaro alionekana kuchanganyikiwa. Lisa alisema kwa upole alipoona hivyo, “Bibi, mimi ndiye ninayepaswa kuwa na hasira kwa sababu uso wangu umeharibika kutokana na familia yako. Je, ninastahili mambo yote mabaya kwa sababu sitoki katika malezi yenye nguvu kama familia ya Kimaro?”

Bibi Kimaro alipasua midomo yake kutaka kusema kitu lakini Alvin alimkatisha kabla hajapata nafasi. “Mimi ndiye nimekuwa nikimsumbua tangu mwanzo hivyo acha kudhani kuwa ni mwanamke mlaghai. Hakuwa anajua mimi ni nani alipokutana nami mara ya kwanza. Pia nilichumbiana na Melanie baadaye ili tu kumfanya aone wivu.”

“Unawezaje kumfanyia hivyo Melanie?” Sauti ya kikongwe ilidhihirisha kutofurahishwa kwake.

"Ikiwa unampenda sana, basi mchukue kama mjukuu wako." Macho ya Alvin yalionekana kuwa makali kama moto. “Nilifanya mambo hayo kwa kukuridhisha tu. Melanie ni msichana mzuri—”

“Na Lisa je?” Bibi Kimaro alimkatiza bila subira kwa sauti ya ukali, “Wote wawili ni mabinti wa Joel Ngosha.”

“Lisa alikosea nini?” Alvin alidakia. “Je, alichagua familia aliyozaliwa? Hakuwahi kukumbana na mapenzi ya baba yake tangu akiwa mdogo lakini sasa kwa vile hatimaye ameungana na baba yake, kila mtu anamdharau. Kwa kweli, yeye ni mkubwa kuliko Melanie na mama yake ndiye aliyeachwa na Joel. Yeye ndiye mwathirika wa kweli hapa."

Bibi Kimaro hakuwa na maneno ya kubishana naye.

Alipohisi hali ya mvutano ikizidi kushamiri, Lisa alipendekeza, “Inakaribia saa sita mchana. Nyie wawili mnapaswa kuelewana nami nitaelekea jikoni kuandaa chakula cha mchana. Bibi, tafadhali kaa kwa chakula cha mchana.”

"Ikiwa unabaki tu ili uendelee kumshambulia mke wangu, basi ni bora ungeondoka tu," Alvin alisema kwa upole.

Bibi Kimaro aliona aibu sana kwa sauti ile. “Unadhani L-”

“Alvin, si rahisi kwa Bibi kufanya safari ndefu hivyo kuja hapa katika umri wake. Afadhali ukae kimya,” Lisa alifoka, na kufanya mambo yasiwe magumu kwa yule mzee. Alvin alikoroma, na Bibi Kimaro naye akakaa kimya.

Baada ya Lisa kutokomea jikoni, Bibi Kimaro alimuagiza mwanasheria atoe fomu ya kuhamisha umiliki wa hisa. “Hii imetoka kwa babu yako. Utakuwa na udhibiti kamili wa KIM International baada ya kusaini hii. Mimi na babu yako hatutaingilia mambo ya kampuni kuanzia hapo.”

Alvin akasaini karatasi bila kusita. “Siyo tu kwamba mam’dogo Valerie hajaboresha biashara ya KIM Insurance tangu achukue kitengo hicho, lakini mauzo yameshuka kiwango cha chini zaidi. Anapaswa kustaafu mapema, kuketi, na kufurahia bonasi za kila mwaka nyumbani.”

Bibi Kimaro alionekana kushtuka kabla ya kupiga kelele, “Unafanya hivi kumlipishia kisasi kwa sababu alisababisha Lisa kuharibika usoni…”

“Kwa hivyo itakuwaje kama hiyo ni kweli? Unamvumilia hata baada ya kusababisha madhara kwa mtu mwingine kwa sababu tu ni binti yako? Lakini yeye si binti yangu,” Alvin alijibu bila kujali.

“Lakini yeye ni mam’dogo wako, hata hivyo…” Bibi Kimaro akashusha pumzi ndefu. "Mbali na hilo, mauzo yake yaliimarika mwezi uliopita…”

Sura ya: 233

'Hiyo ni kwa sababu Nina Mahewa aliwekeza shilingi bilioni kadhaa." Macho ya Alvin yalidhihirisha dhamira ya hatari. “Ikiwa nilikisia kwa usahihi, alifanya hivyo baada ya mam’dogo Valerie kukubali kuharibu uso wa Lisa. Anadanganya takwimu za mauzo." Akiwa amepigwa na butwaa, Bibi Kimaro akakosa cha kusema.

“Bibi, unapaswa kushukuru. Nisingemuacha hai kama si wewe na babu.”
Alvin akainuka. “Angalia mwanao Spencer na binti zako. Mmoja wao anajali tu kusaidia familia ya mumewe, mwingine anadanganya mauzo. Mwanao pekee wa kiume ni dhaifu na hana uwezo. Unafikiri wewe na babu mngeweza kufurahia uzee wenu kwa mali mlizonazo sasa kama si mimi?” Bibi Kimaro alionekana kuwa mzee kwa miaka michache zaidi baada ya kusikia hivyo.

Saa sita kamili mchana, Lisa alitokea tena jikoni baada ya kuandaa chakula cha mchana lakini mvutano kati ya Alvin na bibi yake ulionekana kuongezeka. Alitenga chakula na kumkaribisha Bibi Kimaro mezani.

Mwisho bibi yule alionekana kushangazwa na vyakula vilivyowekwa mbele yake. Kila mlo haukuwa mzuri tu bali ulikuwa na ladha ya kupikwa nyumbani kuliko vile vya wapishi wa familia ya Kimaro. Aligundua kwamba Alvin, ambaye hakuwahi kufurahia chakula, alikuwa akila kila chakula—hasa nyama ya nguruwe.

Bibi alijaribu kipande kidogo cha nyama ya nguruwe. Walahi alitamani aachiwe sahani zote peke yake. Bakuli la nyama lilikuwa karibu kuisha alipofikia kipande cha pili.

“Usimalize yote. Bibi bado hajala vya kutosha.” Lisa akasogeza bakuli la nyama ya nguruwe kuelekea kwa Bibi Kimaro.

Alvin alikunja uso. “Kwanini hukujitayarisha nyingi?”

"Ulikula jana usiku na unataka tena mchana huu? Si afya kula nyama ya nguruwe kupita kiasi.” Aliweka mbogamboga badala yake kwenye sahani yake. “Ni muhimu kuwa na lishe bora na sio kuchagua. Ukiendeleza tabia hiyo mbaya, basi sitakupikia tena.” Lisa alimuonya.

“Sawa, nimekusikia.”

Chini ya macho ya Bibi Kimaro, mjukuu wake alianza kula mbogamboga. Mtu ambaye alikula vijiko vichache vya chakula kwa siku alikuwa akila sahani nzima wakati huu. Hata yule kikongwe alikuwa na hamu ya kula alipomwona mjukuu wake akila kwa hamu vile. Mwishowe, chakula cha mchana kilichotosha watu sita kilimalizwa na wale watatu.

Baada ya chakula cha mchana, Lisa alitenga majagi mawili ya mtindi kwenye meza. Aunty Yasmine alisema huku akitabasamu. “Hii pia imetengenezwa kwa mikono na Bi. Jones. Ni mtindi na asali na jamu safi ya strawberry ambayo aliiandaa polepole kwa masaa mawili. Alisema kunywa glasi ya mtindi baada ya mlo ni vizuri kwa usagaji chakula na kusafisha matumbo.”

Bibi Kimaro alionja kidogo kisha akanongewa tena. Mtindi ulikuwa mtamu sana. Alijisikia kuongeza glasi nyingine! lakini alikuwa na aibu sana kuomba kuongezewa.

Hata hivyo, Alvin hakuona aibu hata kidogo kuomba huduma nyingine mara baada ya hapo. Ombi lake lilikataliwa na Lisa. "Huwezi kunywa mtindi mwingi au unaweza kuvimbiwa."

"Una shida gani?" Alikunja uso lakini hakuzungumza zaidi.

Ingawa hakumpenda sana Lisa, Bibi Kimaro ilibidi akubali kwamba binti huyo alikuwa amembadilisha Alvin kuwa bora. Labda ugonjwa wa Alvin ungeimarika, kama hapo awali…

Baada ya chakula, Bibi Kimaro alisimama na kuaga ili kuondoka. “Asante kwa chakula wajukuu zangu, nimekula, nimefurahia na nimeshiba. Ni wakati wa mimi kuondoka.”

"Unaweza kukaa kwa siku chache zaidi. Kutembea na kupunga upepo baharini kunastarehesha kweli,” Lisa alisema kwa tabasamu hafifu.

Bibi Kimaro alijisikia vibaya kuona jinsi mwanamke huyo alivyoharibika usoni. “Ni sawa. Babu yako hajazoea kuwa mbali na mimi.” Baada ya kutulia kwa sekunde chache, aliendelea kusema, “Asante kwa ukarimu wako leo.”

Lisa alishangaa kusikia hivyo. Bado alikuwa akitabasamu hata baada ya yule kikongwe kuondoka zake.

Alvin alimkumbatia kwa upendo. “Bibi yangu alikutendea vibaya lakini bado ulijaribu sana kumfurahisha kwa chakula cha mchana na mtindi. Anafikiri kukushukuru mara moja ni fidia ya kutosha?"

“Ni kwa sababu yeye ni bibi yako.” Aligeuka na kuifunga mikono yake shingoni. “Ulimwambia maneno makali lakini bado najua unawajali sana babu na babi yako. Vinginevyo, usingeichukua KIM International tena. Una wasiwasi kwamba wanandoa hawa ambao wameishi maisha ya kitajiri wakati wote wangedhihakiwa na wengine katika uzee wao ikiwa KIM itaanguka?"

Alvin aliinua nmacho yake kinyonge. Hakuna mtu aliyemjua vizuri kuliko yeye.

“Alvlisa, nilikuwa na bibi pia. Ni pale tu alipotangulia mbele ya haki ndipo nilijuta kutotumia muda mwingi kuwa naye. Familia ni damu halisi na ni ngumu sana kuiondoa. Kwa sababu yako, ninaweza kujaribu kuwavumilia na kuwasamehe. Ilimradi utafurahi.” Kwa macho makali, Lisa alimtazama Alvin usoni.

Alvin alimsukuma ukutani. Hisia ambazo zilikuwa zimelala ndani ya moyo wake zililipuka kama volkano. Aliinamisha kichwa chake ili kumbusu kwa mahaba kwenye midomo. "Samahani, Lisa. Kwa ajili ya familia yangu kukuumiza.”

Uso wake uliharibiwa na familia ya Kimaro lakini bado aliwavumilia kwa ajili yake. Hata hivyo haikuwa imepita hivihivi tu. Aliahidi kuwalipa kwa yale waliyomfanyia.

"Siku moja, tutatapa mtu wa kutibu uso wako. Nitakupenda maisha yangu yote.”

Lisa alifunga macho yake karibu. Wakati huo huo, alihisi nguvu na utulivu. Haijalishi uso wake ulikuwa umeharibika vipi, kilichokuwa muhimu ni kwamba hakujali.

Siku iliyofuata, Lisa akaenda kufanya kazi katika kampuni yake. Alikuwa akitoka Mombasa hadi Nairobi na kurudi kwa ndege kila alipotaka kwenda ofisini kwake.

Alipotoka tu, Hans alijitokeza nyumbani kwa Alvin akiwa na wauguzi wachache. Kulikuwa na sura ya wasiwasi usoni mwake aliposema, "Bwana Kimaro, hawa ni wauguzi waliochaguliwa na mkurugenzi wa hospitali."

Alvin aliyekuwa anasoma kitabu cha hadithi za Jomba Wajo aliinua kichwa chake. Ugonjwa wake wa akili haukuwa kitu ambacho kingeweza kuponywa kwa siku kadhaa. Lisa alikuwa na kazi yake mwenyewe ya kufanya, kwa hivyo asingeweza kumtunza kila wakati. Ili kumzuia asipatwe tena na ugonjwa huo, ilikuwa vizuri kuwa na muuguzi aliyezoezwa ifaavyo nyumbani ili kumtazama.

Hata hivyo, alionekana kuchanganyikiwa wakati macho yake yalipotua kwenye uso mzuri sana. "Jina lako nani?"

Mwanamke huyo alionekana kushtuka chini ya macho yake kabla ya kujibu kwa sauti nyororo, "Jina langu ni Maurine Langa."

“Langa?” Alvin akashtuka kusikia jina hilo. "Una uhusiano gani na Sarah Njau Langa?"

"Yeye ni binamu yangu." Maurine alipepesa macho na kumtazama Alvin. “Unamfahamu binamu yangu?”

“Ni zaidi ya kumjua.” Alvin alihema ndani kwa ndani. "Wewe bado ni Langa, angalau. Kwanini uliishia kuwa nesi? Hii si kazi rahisi.”

"Langa sio kama tulivyokuwa hapo awali. Lakini ni sawa, angalau tuna cha kupeleka matumboni mwetu na paa juu ya vichwa vyetu.” Aliinua macho yake na kutabasamu kwa shukrani. "Pengine kuchukua kwangu taaluma hii kuna uhusiano na binamu yangu. Sisi wawili tulizoea kuwa karibu sana tulipokuwa wadogo lakini alipelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Nilijisikia vibaya sana kwake. Mpango wangu wa awali ulikuwa kuwa mwanasaikolojia aliyeidhinishwa lakini sikufanikiwa. Kwa kweli niko katika maandalizi ya kufanya mtihani tena.”

Alvin alichanganyikiwa tena aliposikia hivyo. Swali la Hans lilimrudisha kwenye ukweli. "Bwana Mkubwa, ungependa kumwajiri nani?"

"Maurine Langa, ndiyo." Alvin akachukua kitabu chake tena na kuendelea kusoma.

Tabasamu kubwa lilienea usoni mwake. “Asante, Bwana Kimaro. Nitafanya kila niwezalo kukusaidia kupona.”

Hans alionekana kushangaa. Mara tu Maurine alipoondoka kwenda nyumbani kuchukua vitu vyake, Alvin alimtazama Hans na kuagiza, “Mchunguze mwanamke huyu.”

"Bwana Mkubwa, unashuku kwamba-"

"Fanya nilichokuagiza!"

Katika muda usiozidi nusu siku, Hans alirudi na baadhi ya matokeo. “Maurine Langa hakika ni binamu wa Sarah Langa. Alikuwa akisoma nje ya nchi na hivi karibuni alirudi nyumbani. Tangu kifo cha mama yake, familia ya Langa imekuwa ikinyanyaswa sana na familia ya Njau. Maurine anabaguliwa nyumbani na hospitalini pia na kila mara hupewa jukumu la kuwaangalia wagonjwa wenye jeuri na fujo. Lakini, utendaji wake hospitalini umekuwa mzuri sana. Sio tu kwamba yeye ni mvumilivu bali pia ana mawazo yenye nguvu ya kuvumilia magumu.”

Sura ya: 234

Nuru ilizimika machoni mwa Alvin kwa sauti hiyo. "Inaweza kuwa ni bahati tu kwamba yuko hapa leo?"

"Inaonekana. Mabinti waliopendekezwa na wasimamizi wa hospitali hiyo ndio wauguzi wanaofanya vizuri zaidi kwa sasa.”

Aliitikia kwa kichwa baada ya kusikia hivyo, kigugumizi kwenye moyo wake kikatoweka. "Nani mkuu wa familia ya Njau sasa?"

"Charity Njau." Hans alijibu.

“Hakikisha KIM International na Alvinarah Media Network zinavunja mikataba yote ya ushirikiano na kampuni ya New Era Advertisings. Tutaona watapeleka wapi matangazo ya wateja wao. Nataka kumfunza somo Charity Njau kwa kuinyanyasa familia ya Langa.

Hans alikubali kwa utii na hakuongeza neno lolote.

Saa kumi na moja jioni Lisa aliondoka kazini mapema kuliko siku nyingine yoyote. Alisikia kelele kutoka kwa uwanja wa mpira wa vikapu mara tu aliposhuka kutoka kwenye gari.

Alitembea kwa wakati na kumuona Alvin akiinua mikono yake kutumbukiza mpira kwenye pete kufunga goli. Hakujua ni muda gani alikuwa akicheza mpira huo wa kikapu. Nyuma ya fulana yake nyeupe kulikuwa na unyevunyevu kidogo lakini uso wake ulionyesha hali ya jua.

Kumwona katika hali hiyo kulichukua pumzi yake. Alipokuwa bado shuleni, Ethan alikuwa mchezaji pekee wa mpira wa kikapu ambaye alisifiwa sana, lakini, akimtazama Alvin kwa wakati huo, aliona haiba ya kweli ya mwanamichezo.

“Naam!” Mfululizo wa makofi ya pongezi ulisikika kutoka upande wa pili wa uwanja. Hapo ndipo alipomwona yule mwanamke aliyelingana naye kiumri akiwa amevalia suruali ya jeans na top nyeupe. Nywele zake nyeusi zilizometa zilikuwa juu kwenye mkia wa farasi.

“Inavutia, Bwana Kimaro." Mwanamke huyo alitembea na chupa ya maji na kipande cha taulo. "Umecheza kwa dakika 40. Ni wakati wa kupumzika.”

“Sawa.” Alvin aliipokea ile chupa na kuanza kumeza vilivyomo ndani yake.
Miale ya jua la machweo iliwamulika wote wawili. Tukio hilo la aina fulani lilimchoma macho Lisa.

“Alvlisa…” Lisa aliita kabla ya kwenda haraka.

Alvin alitazama mwelekeo wa sauti hiyo na tabasamu likaenea katika uso wake wa kupendeza. "Baby, umefika nyumbani mapema leo."

"Nilirudi nyumbani mapema kwa kuhofia kuwa ungekuwa mpweke nyumbani peke yako." Alimtazama kwa karibu yule mwanamke mwingine. Alikuwa mrembo lakini hakuwa na kitu cha ajabu ikilinganishwa na yeye alivyokuwa zamani. Hata Melanie alikuwa mrembo zaidi ukilinganisha naye. Lisa alijisikia ahueni.


“Halo, Bi. Jones Mimi ndiye nesi niliyetumwa na hospitali kumuangalia Bwana Kimaro,” Maurine alijitambulisha huku akitabasamu.

“Oh, habari.” Lisa alishikwa na butwaa. Kwa sababu fulani, alihisi kana kwamba aliyaona macho hayo hapo awali lakini hakuweza kukumbuka ni wapi na lini.

“Ni heshima yangu kumwangalia Bwana Kimaro. Natumai atapona haraka iwezekanavyo.” Maurine alijieleza kitaaluma.

“Twende, naelekea ghorofani kuoga.” Alvin aliweka mkono begani kwa Lisa.

"Bwana Kimaro, unapaswa kupumzika kwa nusu saa baada ya kufanya mazoezi kabla ya kuoga," Maurine alimkumbusha.

“Sawa…” Alisita kabla ya kukubali.

Lisa alishangaa sana. Aliondoa fulana yake baada ya kupanda ghorofani. Alichukua taulo na kumpigapiga mgongoni. "Vipi mbona umeanza kucheza mpira wa kikapu ghafla?"

"Maurine Langa alisema kiasi kinachofaa cha mazoezi kinaweza kusaidia kupona kwa haraka na pia kuboresha ubora wa usingizi usiku."

“Maurine Langa?” Kitetemeshi kilipita kwenye uti wa mgongo wake.
Ni sadfa iliyoje! Aliwahi kuwa na mpenzi wa zamani mwenye jina la kati Langa pia. Sarah Langa!

“Ndio, kuna nini?” Akageuka kumtazama.

Lisa alichanganyikiwa sana. Hakuweza kusema kwamba alishituka kwa sababu jina la mwisho la nesi lilikuwa Langa. Hata hivyo, haikuwa sawa kujifanya kuwa mkarimu. “Sikutarajia ungemsikiliza msichana huyo kwa utiifu,” alisema huku akihema.

Alvin aliinua macho yake kabla ya kuinama ili kunusa midomo yake. "Hmm, nasikia harufu ya wivu."

“Nipo serious.” Akampiga kofi la mgongoni kwa utani.

Aliushika mkono wake mara moja na kuutoa kidogo. "Nisiingekuwa mtiifu hapo zamani na hata nisingekubali wazo la kuajiri muuguzi kutoka hospitali ya magonjwa ya akili. Hata hivyo, ninapenda nipone mapema kwa ajili yako, kwa hivyo ninahitaji kufanya kazi na mpango wa matibabu. Sitaki kufanya jambo lolote litakalokuumiza tena. Unaelewa?"

Aliuma midomo yake, ghafla akajisikia vibaya kwa kuwa na wivu sana. “Nimeelewa, lakini kwa nini usiajiri mtu ambaye ni mkubwa kidogo au labda nesi wa kiume? Nitakuwa nikifanya kazi ofisini na kukuacha peke yako nyumbani na msichana kweli?!”

Alvin alitabasamu kabla ya kuinua kichwa chake na macho yao yakagongana. “Una wivu kweli?”

“Alvin Kimaro!” Alimtazama kwa macho makavu.

“Usiwe na wivu bwana.” Alvin alimshusha wasiwasi. “Sekretari au mfanyakazi yeyote katika kampuni yangu ni mrembo kuliko yeye. Usingekuwa na nafasi ya kuwa Bi. Kimaro kama ningekuwa zoazoa fagio la chuma.” Alvin alijibu huku akitabasamu. “Sikuona ukiwa na wivu hivyo nilipokuwa na Melanie. Ulikuwa umekaa kimya kuhusu hilo.”

Aibu ilitanda usoni mwake alipofichua ukweli. “Siwezi kuwa na wasiwasi na hili. Naelekea chini kuandaa chakula cha jioni.” Akamtupia taulo na kuelekea kwenye ngazi.

Mara tu alipoingia jikoni, Maurine alimwendea na mpango wa lishe. "Bi. Mdogo, huu ni mpango wa lishe iliyoundwa mahsusi kwa ajili ya Bwana Kimaro. Kwa kuzingatia ugonjwa wake, ninapendekeza milo yake mikuu izingatie maelekezo haya.”

“Sawa, asante.” Lisa alipokea mpango wa chakula kabla hajauliza, "Je, tumewahi kukutana hapo awali?"

Maurine alionekana kushtuka lakini haraka akabadilisha mshangao huo na kutabasamu. "Sidhani. Hata hivyo ni mara yangu ya kwanza kukutana nawe, Bi. Kimaro. Lakini watu wengi wamesema kwamba wanaonekana kunifahamu.”

“Labda.” Lisa aliitikia kwa kichwa.

Lisa alitokea tena jikoni baada ya kupika chakula cha jioni, alimuona Alvin akiwa amekaa kwenye kochi huku Maurine akiwa amejiinamia kiunoni akijadiliana naye jambo kwa upole.

"Wakati wa chakula cha jioni," Lisa alimkumbusha.

Alvin akanyanyuka na kabla hajajonge mezani akatangaza, “Maurine na Shangazi Yasmine, kwa nini msijiunge nasi kwa mlo wa jioni wa leo?”

Hilo lilimshangaza Maurine. “Asante…” Alijibu huku akisitasita.

“Ni sawa. Usione haya wala woga. Kila mtu ni sawa katika zama za leo, na zaidi ya hayo, imekuwa ndefu kwako pia,” Lisa alisema kabla ya kugeuka kumwangalia Alvin.

Kwa kweli chakula cha jioni kilichangamka zaidi huku watu wale wanne wakiwa mezani. Hata hivyo, Lisa alikosa amani Maurine alipoendelea kumkumbusha Alvin ale nyama kidogo bali mboga na dagaa zaidi. Baada ya yote, yeye ndiye alikuwa na wajibu wa kusema maneno hayo. Kwa hivyo, ilikuwa ni ajabu sasa kwamba mtu mwingine alikuwa amechukua majukumu yake. Kwa kweli alijiona anazidi kuwa na wivu mkali.

Baada ya chakula cha jioni, yeye na Alvin walitembea ufukweni ili chakula kishuke vizuri tumboni. Waliporudi nyumbani, wote wawili walifanya kazi zao za ziada katika maktaba yao. Kwa kuwa Lisa alimaliza kazi yake mapema, alienda kuoga.

Alipotoka bafuni, aligundua kwamba Alvin alikuwa akinywa kitu kwenye glasi. Maurine alikuwa akimwangalia kwa makini pembeni. Mwanga wa taa ya manjano ulimulika juu yao kutoka darini kwa juu. Kuona jambo hilo kulimuumiza macho.

"Unakunywa nini?" Akasogea kuchungulia kwenye glasi yake. Kioevu cheupe kilionekana ndani yake, labda kilikuwa ni maziwa.

Maurine alieleza kwa upole, “Kunywa glasi ya maziwa kabla ya kulala huboresha ubora wa usingizi.”

“Asante, lakini hili ni jukumu langu,” Lisa alijibu kwa tabasamu hafifu.
Maurine alishikwa na butwaa kiasi kwamba uso wake ulipauka ghafla. Akiwa amechanganyikiwa, alitikisa kichwa kwa aibu. "Ndio, nitawaacha nyie wawili sasa."

Sura ya: 235

Maurine alimtazama Lisa kwa tahadhari kabla ya kufunga mlango nyuma yake.

Alvin alisema kwa kucheka, “Umemuogopesha binti huyo.”

Lisa alishindwa cha kusema. “Nilifanya nini cha kumuogopesha? Nilisema maneno hayo kwa uso wa kirafiki.”

"Hmm, lakini pia kwa sauti ya wivu sana." Alvin aliitikia kwa kichwa huku uso wake ukionekana kutojiweza. “Ni glasi tu ya maziwa. Hutakiwi kuwa na wivu juu yake.”

Maneno ya Alvin yalimfanya ajione kuwa ni mwanamke mwenye fikra finyu. Lisa alishusha pumzi ndefu huku akihisi mshangao mwingi ukimuandama.

“Acha kuwaza kupita kiasi. Ngoja nikukaushe nywele zako.” Alvin akachukua mashine ya kukaushia nywele.

Mara tu nywele zake zilipokauka, alipanda kitandani na uso wenye haya. Tangu wapatane, alikuwa na shauku kubwa ya kufanya mapenzi kitandani, lakini bado aliona aibu kila alipojiwazia. Hata hivyo, alijilaza tu kitandani kwa utulivu baada ya kuzima taa usiku huo. Hamu yake iliyofichika haikuwa ya kawaida. Lisa akaanza uchokozi wa makusudi. Akageuka juu juu juu na kumkandamiza Alvin na makalio yake.

"Tulia basi tulale." Alvin aliyekuwa amegeuziwa makalio na kumkandamiza ipasavyo kwenye ikulu yake akampigapiga tu mgongoni na kumpoza kwa sauti yake ya upole.

Lisa hakuamini masikio yake. Aliuma midomo yake na kuizungushia mikono yake shingoni mwake. “Alvlisa…” Lisa aliita taratibu. Ukiacha sauti yake iliyotetema kwa huba, uso wake wote ulikuwa ukizungumza mapenzi tu. Kwa bahati nzuri, Alvin hakuweza kuuona kwa sababu taa zilikuwa zimezimwa.

Hili lilimshangaza sana Alvin. Mshawasha ukatekenya kunako makao makuu yake, lakini alizuia shauku yake mara moja. “Maurine alinikumbusha kwamba dawa ninazotumia haziniruhusu nifanye hivyo kwa sasa. Ni bora tusitishe jambo hili kwa sasa.” Unyonge ulionekana katika sauti yake.

Lisa alionekana kushtuka. “Lakini kabla… Sote tulikuwa wazuri. Sio lazima, sivyo?"

“Unanitaka sana hivyo?” ghafla alisema kwa mahaba mazito.

Lisa aligeuka tu bila kujibu. Alitaka ndiyo lakini hakutaka kujirahisha sana, alihitaji kudumisha kiburi chake pia. Alitaka abembelezwe kwanza ndipo atoe!

Alvin akamkumbatia kwa nyuma. “Kuwa mvumilivu. Siwezi kufanya chochote ambacho kinaweza kunisisimua kupita kiasi kwa sasa. Ninaogopa nitafanya kitu nje ya udhibiti wangu ambacho kinaweza kukuumiza. Kama mara ya mwisho."

Lisa aliuma midomo yake, alikasirika, na mwishowe akanung'unika "sawa" baada ya muda mrefu. Usiku ule hakupata usingizi huku Alvin akipitiwa na usingizi mzito. Mawazo yake yalikuwa yakimshawishi kwamba labda nadharia ya Maurine ilikuwa sahihi. Baada ya yote, alikuwa akisumbuliwa na usingizi tangu aanze kupandisha wazimu. Muda ulikuwa umepita tangu amwone amelala vizuri sana.

Siku iliyofuata, Lisa alipokea simu kutoka hospitalini. Inavyoonekana, daktari bingwa wa mfumo wa neva, Daktari Angelo kutoka nje ya nchi alikuwa amefika kumtibu Joel. Bila kupoteza muda, alieelekea hospitali mara moja. Bibi na Babu Ngosha walikuwa tayari wameshafika.

Dk. Angelo alikuwa amemaliza uchunguzi wa Joel. "Ninahitaji kumtibu kwa kudhibiti mishipa yake kwa muda mrefu. Bado kuna matumaini kwamba Bw. Ngosha atatoka katika hali ya kukosa fahamu, lakini huenda ikawa ni safari ndefu. Muda mfupi zaidi labda utakuwa nusu mwaka hadi mwaka mzima.

"Asante sana." Lisa alishukuru.

“Usijali. Wewe ni rafiki wa Chester, kwa hiyo nitafanya kila niwezalo kukusaidia.” Dk. Angelo alisema.

Baada ya kutafakari kwa ufupi, Lisa aliomba, “Dokta Angelo, ikiwa mtu atakuja kuuliza kuhusu hali yake, tafadhali mwambie kwamba Bw. Ngosha atarudiwa na fahamu ndani ya mwezi mmoja.”

Daktari alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kutikisa kichwa. “Hakika.”

Baada ya daktari kuondoka, Mzee Ngosha hakuweza kupinga kuuliza, “Unajaribu kuchunguza kama kuna mtu alipanga kumuua baba yako?”

"Babu, unadhani ni nani anayeweza kuwa mhusika?" Aliuliza.

Mzee alikaa kimya kwa muda. Uchunguzi wa maiti ya dereva wa lori ulionyesha kwamba alikuwa alisinzia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya. Hata hivyo, mwanamume huyo hakuwa mraibu na alikuwa ametumia tu dawa hiyo kimakosa. Kwa wazi, hili lilikuwa tendo la makusudi.

“Nina uhakika ni Nina.” Mzee Ngosha alifoka kwa hasira. "Baada tu ya ajali amemwingiza Melanie kufanya kazi katika Kampuni ya Ngosha."

Lisa alikubali kwa kichwa. “Ikiwa ni hivyo, atahakikisha kwamba baba yangu hataamka kamwe. Kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee itakayomwezesha kurithi kila kitu alichoacha nyuma. Kando na hilo, ikiwa mtu mwingine yuko nyuma ya hili, mtu huyo bila shaka atajaribu kuchukua udhibiti wa Ngosha Corporation ndani ya mwezi huu. Nina hakika mhalifu atafichua asili yake hivi karibuni.”

Mzee Ngosha na Bibi Ngosha walishangaa kusikia hivyo. Kwa mara ya kwanza, walimtazama mjukuu huyo wa kike mwenye mawazo ya kuvutia kwa umakini.

"Kitu kimoja zaidi. Usimwambie mtu yeyote nilichokuambia leo, pamoja na Bam’dogo Damien.” Lisa alitoa angalizo.

Mzee alishtuka. "Unamaanisha nini? Kwamba tunapaswa kumshuku Damien pia?”

"Hawezi kuwa Damien." Bibi Ngosha akatikisa kichwa mara moja. "Hali ya miguu yake imemfanya kuwa dhaifu na mgonjwa tangu utoto.”

“Umenielewa vibaya. Ninaogopa kwamba Bam’dogo Damien anaweza kudanganywa kwa urahisi kwa sababu ya madhaifu yake ya kuzaliwa. Kadiri watu wachache wanavyojua kuhusu hili, ndivyo itakavyokuwa bora zaidi,” Lisa alisema huku akitabasamu.

Kielelezo cha wasiwasi kwenye uso wa wanandoa hao wazee hatimaye kilipungua. Waliitikia kwa kichwa kuafiki kabla ya kuondoka hospitalini.

Shani, ambaye alikuwa akimlinda Lisa pembeni, hakuweza kujizuia kuuliza, “Kwanini hukuwaambia kwamba unamshuku pia Damien Ngosha?”

“Hawataniamini. Isitoshe, mimi ni mjukuu wao tu, na Damien ni mwana wao. Ninahitaji kuwaonyesha ukweli badala ya kuwashawishi kwa maneno matupu.” Kisha, akaingia kwenye gari.

Shani alishtuka alipotazama umakini wa mwanamke huyo. Ikamjia akilini kwamba Lisa alizidi kufana na Alvin kitabia.

Punde Nina akasikia habari za Joel akitibiwa na Dk. Angelo. Alikaribia kupoteza akili aliposikia hilo. Mara moja, alipiga namba ambayo haikuseviwa kwenye simu yake. "Joel atapata fahamu ndani ya mwezi mmoja."

"Tulia. Huenda huu ukawa mtego wa Lisa.”

“Lakini Daktari Angelo ana uwezo kwelikweli. Amesaidia wagonjwa kadhaa kutoka katika hali ya kukosa fahamu,” alisema huku akifadhaika. "Joel hakika atanishuku mara tu atakapoamka, na atanitaliki. Huenda nisipate hata senti kama hilo likitokea.”

“Usijali. Nitajitahidi niwezavyo kuchukua kampuni ya Ngosha ndani ya mwezi huu.”

"Kwa hivyo utafanya nini? Sitapewa senti hata moja ya kampuni.” Nina aliuma meno. “Kwanini hukumuua?”

"Usijali ... atakufa."

“Naweza tu kuweka imani yangu kwako. Yote haya ni kwa ajili ya msichana wetu kipenzi, Mel.” Nina ghafla akasitisha maneno yake..

Alipokata simu tu, mlango ukafunguliwa. Melanie alikuwa amesimama kando ya mlango, uso wake ukiwa umepauka kama mzimu. “Mama, nani alikuwa kwenye simu? Unajaribu kumuua nani? Baba?”

Uso wa Nina ulibadilika ghafla. “Usiingize pua yako katika hili. Sasa ni saa ngapi? Mbona haupo ofisini?”

“Mama acha kujaribu kubadilisha mada. Nilisikia yote.” Melanie alimtazama mama yake kwa hofu. “Ni kweli wewe ulikodi mtu kusababisha ajali ya baba? Mama, ungewezaje kufanya hivyo? Yeye ni mume wako. Pia, unamaanisha nini unaposema 'msichana wetu kipenzi Mel'? Mimi si binti wa baba?”

“Nyamaza. Yeye si mume wangu.” Nina alijua hakuna haja ya kuweka siri hii tena. "Hiyo ni sawa. Yeye si baba yako.”

Melanie alishtuka sana. "Hiyo haiwezekani. Hapana. Joel Ngosha ni baba yangu!

“Melanie, sikiliza. Baba yako alitaka kunitaliki muda si mrefu uliopita. Alikuwa anaenda kukupa 5% tu ya hisa za Ngosha Corporation, lakini 35% kwa Lisa. Nimefanya haya yote kwa ajili yako,” Nina alifoka huku machozi yakimtoka na kumshika bintiye mabegani.

Macho ya Melanie yalijaa chuki. “Baba yangu… Kwanini? Kwanini anifanyie hivyo?”

"Kweli," Nina alisema kwa huzuni. "Sote wawili hatungekuwa na nafasi katika jumuiya ya matajir ya Nairobi ukiwa na 5% tu ya hisa. Hata Jerome angebadili mawazo yake kuhusu kuwa na wewe.”

Melanie aliuma midomo yake. Hakutaka kupata uchungu wa kuachwa tena. "Mama, kwa nini kila mtu ana upendeleo kwa Lisa? Je, mimi si binti wa baba kweli? Kwa hiyo baba yangu ni nani?"


“Acha kulia. Baba yako anakupigania upate kampuni ya Ngosha." Nina alimkumbatia bintiye karibu. "Utajua ukweli hivi karibuni."

TUKUTANE KURASA 236-240

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA......236-240

Sura ya: 236

Hans akamkabidhi Lisa taarifa alizozikusanya kwenye kampuni ya Ngosha Corporation. “Kwa siku za karibuni, Damien amekuwa akitumia muda mwingi kushawishi wanahisa kumpa nafasi na Joel. Hata alimfukuza msaidizi aliyemwamini Joel kwa kisingizio cha uongo. Ndani ya kipindi cha nusu mwezi, alikuwa amechukua udhibiti kamili wa kampuni ya Ngosha Corporation.”

Lisa alizama katika mawazo ghafla baada ya kumsikiliza kwa makini.

“Bi Jones, hivi ndivyo ulivyotabiri. Wafanyabiashara wote wameshtushwa na Damien, yule mtu mlemavu, kwa kuanza kupigania madaraka ya kampuni wakati kaka yake akiwa hajitambui hospitalini.” Hans alivutiwa sana na Lisa. Machale ya mwanamke yanaweza kuwa ya kutisha sana wakati mwingine.

“Vipi kuhusu Melanie?” Lisa aliuliza ghafla.

“Kwa sasa yeye ni Makamu Mkurugenzi. Damien alimpa nafasi hiyo mara baada ya kuchukua udhibiti wa kampuni siku chache zilizopita. Inavyoonekana, wakati wa mikutano michache iliyopita ya wanahisa, Damien alitumia muda mwingi kuwashawishi wanahisa kumpatia nafasi hiyo Melanie.”

Lisa alianguka katika mawazo mazito. “Damien ana uhusiano gani hasa na Melani, kwanini amchukulie kwa uzito hivyo? Hata alimpa jukumu la kusimamia kampuni kubwa kama Ngosha Corporation! Kando na hilo, familia ya Ngosha na familia ya Campos wanapanga ushirikiano kwa njia ya ndoa, kuna nini ndani yake?”

Aliinua kichwa chake. “Hans, nifanyie umafia kidogo. Unaweza kupata nywele za Damien na Melanie kwa kipimo cha DNA?”

Hili lilimshangaza kidogo Hans. "Unashuku kwamba ... haiwezi kuwa hivyo. Nasikia jogoo wa Damien hapandi mtungi."

“Huoni ajabu? Kwanini Damien amuumize kaka yake wa damu ili kumpigania Nina na Melanie? Kwanini amjali sana binti wa kaka yake?”

Maneno yake yalimshawishi Hans. "Hakika, nitafuatilia hili mara moja."

Ilikuwa tayari saa sita mchana wakati Hans alipoondoka na kumwacha Lisa ofisini. Aliongea na Alvin kwa furaha kwenye simu. "Hubby, umekula chakula cha mchana?"

"Bado. Nilikuwa karibu kukupigia simu nikwambie kitu. Rodney alinialika tukale kwenye jumba lake jipya la kifahari,” alisema kwa upole. "Ninaweza kulala huko pia."

"Nina wasiwasi kuhusu wewe kukaa usiku kucha mbali na nyumbani peke yako." Lisa alikuwa na wasiwasi kweli.

“Usihofu, sitakuwa peke yangu. Rodney, Chester, na Maurine watakuwapo kunitunza.” Alvin akacheka. "Mwambie Shani akulete hapa mchana ikiwa utani’miss."

“Hakika,” Lisa alikubali bila kusita. Alionekana kushtuka lakini haraka akabadilisha mshangao na mawazo ya kutaniana. "Kwa kweli siwezi kuvumilia kuwa mbali nawe hata sekunde moja."

Maneno yake yalimfanya akose la kusema. “Sawa, siwezi kuvumilia kuwa mbali na wewe pia. Njoo baada ya kazi, sawa?"

Lisa alihisi kuchanganyikiwa sana baada ya kukata simu. Kwa kweli, haikuwa kwamba hakuweza kuvumilia kuwa mbali naye, bali alikuwa na wivu. Kila siku baada ya kuondoka kwenda kazini, Maurine alikuwa akiandamana naye siku nzima. Sasa, alikuwa akimtoa out mwanamke huyo ili kujumuika na marafiki zake. Ingawa lilikuwa jambo la kawaida, Lisa hakuweza kujizuia kuhisi wasiwasi kuhusu hilo.
•••
Saa 12:30 jioni, gari moja la kifahari lilipita kwenye lango na kuingia kwenye nyumba kubwa ya kifahari. Rodney na Chester walikuwa wamengoja mlangoni kwa muda mrefu. Hata hivyo, Maurine alipotoka kwenye kiti cha nyuma cha gari, wote wawili walishangaa. Rodney hasa alikodoa macho kumtazama mwanamke huyo.

“Anaitwa Maurine Langa.” Alvin alimtambulisha haraka haraka bila kufafanua zaidi.

“Maurine Langa, Sarah… Sarah Langa unamfahamu?” Rodney aliuliza kwa msisimko baada ya kusikia jina hilo.

“Unamfahamu pia Sarah? Mimi ni binamu ya Sarah.” Maurine alitabasamu na kufunua vishimo kwenye mashavu yake.

Machozi yalianza kumtoka Rodney, lakini aliyazuia kwa haraka. "Binamu ya Sarah ni binamu yangu pia."

“Ni nini kinaendelea?” Chester akamgeukia Alvin. “Kwanini unaambatana na binamu wa Sarah?”

“Yeye ndiye muuguzi aliyependekezwa na hospitali ya wagonjwa wa akili kwa jukumu la kunitunza,” Alvin alieleza kwa uthabiti.

“Sikujua.” Chester akaitikia kwa kichwa. "Anakuhudumiaje, Umekuwa ukijisikia vizuri?”

Hapo, Maurine aliyarudisha macho yake kumtazama Alvin kwa woga.

“Usijali,” Rodney alisema huku akimpigapiga kichwani. "Sitamruhusu akubadilishe."

Maurine alinyanyua kichwa na kutabasamu kinyonge na kumtazama Rodney. "Kama nikionekana sifai lazima nibadilishwe. Hakuna kisingizio cha kuvuruga matibabu ya Bwana Kimaro."

"Yupo vizuri." Alvin alimjibu kwa haraka kabla hajatangulia kuingia ndani.

Chester alimuuliza kwa sauti ya chini, “Haya, ulimchagua yeye kwa sababu hujamsahau Sarah?”

“Usiwaze kupita kiasi.” Alvin akatabasamu. “Unakumbuka jinsi nilivyopona maradhi yangu mara ya mwisho? Daktari alisema ugonjwa wangu ulitokana na kiwewe cha mfadhaiko wa utotoni, na Sarah ndiye pekee aliyekuwa chanzo cha furaha yangu katika kipindi hicho. Labda hisia za kwamba nipo karibu na Sarah zitanisaidia kupona mapema. Kwa kweli, tangu aje nimekuwa nikijisikia vizuri sana.”

"Lakini huna wasiwasi kwamba Lisa akiju ..."

"Hawezi kujua ikiwa nyinyi wawili hamtasema." Alimkodolea macho rafiki yake kama onyo. "Mkumbushe Rodney kukaa kimya kuhusu hili."

Chester alikunja uso lakini hakuzungumza zaidi kwani Sarah alikuwa ameshaaga dunia. Akaamua kubadili mada. “Alvin, nimesikia umeamua kufanya mambo kuwa magumu sana kwa Charity Njau, kwanini?”

“Si mbaya sana, nataka tu niifundishe familia ya Njau somo rahisi. Vipi kwani, bado unampenda?” Alvin alimuuliza kwa utani.

“Aaahaah!” Chester akaruka maili sita. “Ninachojutia zaidi ni kushea mapenzi na mwanamke msaliti kama yule. Mfunze kabisa adabu yake mbwa yule.”

“Basi mwache aisome namba safari hii.” Alvin alisema na kupotezea mada.

•••
Saa kumi na nusu jioni, Lisa alikuwa njiani kuelekea kwenye jumba hilo la kifahari la Rodney. Katikati ya safari, aliona Range Rover nyeupe ikiwa imekwama kwenye matope. Binti mmoja wa makamo kama yake alikuwa amesimama kando ya barabara. Alikuwa amevalia gauni refu jekundu chini ya koti jeusi, ambalo lilimpongeza umbo lake refu na lililopinda.

"Paki pembeni," Lisa alimwambia Shani.

Shani alikunja uso baada ya kumtupia jicho huyo binti. "Bi Jones, hatupaswi kuingilia mambo ya watu."

'Jua linazama na giza litaingia sasa hivi. Si salama kumwacha mwanamke mwenzetu amekwama barabarani peke yake.” Lisa akausukuma mlango na kutoka nje ya gari. “Unahitaji msaada?”

Binti huyo aligeuka, na alishangaa macho yao yalipokutana. Lisa naye alishtuka. Binti aliyekuwa mbele yake alikuwa amefunga nywele zake ndefu kwenye fundo, akionyesha shingo yake nyembamba na ngozi yake nzuri. Sio tu kwamba alikuwa na sura nzuri, lakini umbo lake maridadi pia lilikuwa nzuri. Alionekana kuvutia hata kwa wanawake wenzake.

“Wewe ni mrembo sana,” Lisa alimpongeza kwa dhati.

"Ni heshima kusifiwa na Bi. Kimaro." Tabasamu hafifu lilienea usoni mwa binti huyo.

“Unanifahamu?” Lisa alishangaa. "Kweli, watu wengi wameniona kupitia mkutano wa waandishi wa habari. Ni ngumu kusahau sura hii."

Yule binti alikunja uso kwa huzuni. "Nadhani uzuri wa ndani hushinda mwonekano wa mwili."

“Haha, nimekubali.” Lisa alicheka. “Ilikuweje ukazama hapa?”

"Gari langu lilikuwa karibu na ukingo nilipokuwa nikipita gari lingine sasa hivi na kwa bahati mbaya likazama kwenye matope. Nimejaribu mara kadhaa kuliondoa lakini bado nimeshindwa.” Alilazimisha tabasamu la uchungu.

Lisa akasogea ili aangalie kwa karibu. “Nadhani naweza kusaidia. Nipe funguo zako.” Yule binti alipitisha funguo zake kwa mashaka.

Lisa akaweka jiwe kubwa chini ya tairi kabla hajaingia ndani ya gari. Aliwasha gari, akaweka ‘four wheel drive’ na kukanyaga moto, na gari likatoka kwenye matope ndani ya sekunde chache.

“Sikujua Bi Kimaro kuwa ni mtaalamu wa magari. Asante." Dokezo la shukrani lilipita mbele ya macho ya binti huyo.

“Usijali, sisi ni wanawake lazima tusaidiane.” Lisa aligeuka kurudi kwenye gari lake. Shani haraka aliwasha gari na kuondoka.

Hata hivyo, wazo la ajabu likamjia kichwani Lisa. Shani alikuwa kando yake akimlinda tangu siku ya kwanza, lakini siku hiyo alibaki ndani ya gari bila wasiwasi. “Shani, unamfahamu huyo binti?”

“Ndiyo,” Shani alijibu baada ya kusitasita kwa muda mfupi. “Bi Mdogo, huyo binti si kama unavyofikiria. Ana sifa mbaya sana huko Nairobi. Ni bora ukijiweka mbali naye kabisa kuepusha matatizo.”

“Kweli?” Lisa hakukubali. Maneno ya watu si ya kukubali wakati mwingine. Mbali na hilo, tofauti na wanawake wengine matajiri huko Nairobi, binti huyo hakujitambulisha au kujaribu kujipendekeza kwa Lisa hata kama alijua kuhusu utambulisho wake kama mke wa Alvin. Huenda alikuwa na kiburi kidogo, lakini alikuwa na adabu. Watu kama yeye labda walipakaziwa sifa mbaya kwa sababu ya tabia zao za kipekee za kujitegemea.

Sura ya: 237

Ilikuwa yapata saa kumi na mbili jioni wakati Lisa alipofika kwenye jumba la kifahari la Rodney. Alitoka kwenye gari na kuelekea kwenye banda lililo karibu na bwawa la kuogelea. Akiwa njiani, alisikia wahudumu aliopishana nao wakinong'ona.

"Kile ambacho kilipaswa kuwa karamu ya vyakula vya Kizungu kimebadilishwa ghafla kuwa karamu ya nyama choma. Ni uharibifu ulioje wa vyakula ambavyo vilisafirishwa kutoka Ulaya?”

"Hasa, na karibu nusu ya chakula cha jioni kilikuwa tayari kimepikwa pia. Kwa kweli siwaelewi hawa matajiri.”

“Sawa, hatuna chaguo. Yote ni kwa sababu mgeni wa Alvin Kimaro, Bi Langa, anataka karamu ya nyama choma.”

“Anamdekeza kweli. Lakini nilifikiri Bwana Kimaro anampenda sana mke wake.”

“Pengine ni kwa ajili ya kujifurahisha tu na msichana mrembo. Hukuona mkewe alivyoharibika usoni?”

“Uko sahihi. Baada ya kuwatumikia matajiri hawa kwa muda mrefu, tumeona michepuko yao mingi sana.”

Upepo wa majira ya joto ulimpiga Lisa. Hata hivyo, alihisi baridi kali kuanzia kichwani hadi miguuni baada ya kusikia maneno yale ya wahudumu. Kama asingejua kuwa kuwa Alvin alikuwa pale, labda angefikiria wahudumu wale walikuwa wanajadili mtu mwingine.

Hata hivyo, kwanini mambo yalikuwa hivyo? Ingawa Alvin alikuwa ameweka nafasi moyoni mwake kwa ajili ya Sarah, bado alimpenda Lisa. Ukweli kwamba Sarah aliwahi kuwa mpenzi wake hakikuwa kitu ambacho kinaweza kubadilishwa. Lakini kwanini avutiwe na Maurine hata watu wahisi kuwa ni mchepuko wake? Au ni kwa sababu yeye aliharibika sura?

Simu ya mkononi ya Lisa ililia kwa sauti ya juu na kumtoa kwenyemawazo yakeake. Jina la Alvin lilikuwa likiangaza kwenye skrini. Lisa alilitazama jina la Alvin, moyo wake ukamwenda mbio sana. Alipoitikia simu hiyo, sauti ya kupendeza ya Alvin ilisikika. “Mbona bado haujafika?”

“Nitakuwa hapo baada ya dakika moja.” Lisa akajibu kifupi.

“Sawa.”

Mara baada ya Alvin kukata simu, Lisa alitulia na kujitahidi sana kupotezea mawazo yaliyokuwa yakimsumbua kichwani kuhusu Maurine. Labda ni wahudumu ambao hawakuelewa hali hiyo. Kwa kuzingatia kuwa alipitia mengi na Alvin, alipaswa kumwamini zaidi.

Dakika tatu baadaye, alimuona Alvin akiwa anamsubiri uwanjani. Kulikuwa na watu wanne kwa jumla - wanaume watatu na mwanamke mmoja.

Maurine, ambaye hakujitokeza katika umati hapo awali, sasa alikuwa amevaa nguo zilizompendeza sana, kana kwamba alikuwa amebadilika kutoka kuwa mtumwa hadi kuwa malkia.

Maurine na Alvin walikuwa wamesimama mbele ya jiko la nyama choma sambamba na Rodney aliyekuwa akiongea kwa furaha karibu nao. Kwa upande mwingine, Chester alikuwa ameshika glasi ya mvinyo huku akitabasamu upande wa pili wa jiko hilo, akigeuzageuza nyama kwenye moto.

Ghafla, Lisa alishikwa na mshangao. Ingawa Alvin alikuwa mume wake, na ukiachana na Sam, Lisa hakuwahi kuwa karibu sana na marafiki zake wengine. Akiwa mke aliyempenda mume wake sana, alitamani angechanganyika na marafiki wa mume wake.

Hata hivyo, Maurine alionekana kuzoeana na marafiki zake mapema kuliko yeye. Maurine alikuwa nani? Alikuwa tu muuguzi ambaye alikuwa akimhudumia Alvin kwa muda au kuna zaidi ya hilo? Lisa alishindwa kujua. Lisa alihisi kana kwamba kuna kitu alikuwa hakijui, na jambo hilo lilimfanya akose raha sana.

“Lisa…” Akiwa wa kwanza kati yao kumwona, Chester alimpungia mkono. Alvin akageuza kichwa chake na kumpungia mkono pia.

Kwa kulazimisha tabasamu, Lisa alimsogelea Alvin na kumshika mkono. "Kwa nini mlifikiria kuwa na karamu ya nyama choma usiku wa leo?"

"Unaipenda?" Alvin aliuliza bila mpangilio huku akitabasamu.

"Utabadilisha ikiwa nitakataa?" Lisa alikodoa macho na kumtazama. Alionekana kutania, lakini moyoni mwake alikuwa serious. Ni kwa sababu tu alisikia kutoka kwa wahudumu kuwa Maurine ndiye aliyependekeza karamu hiyo.

Alvin hapo awali alikuwa amebadilisha karamu ya vyakula vya kizungu kuwa ya choma nyama. Ikiwa angebadilisha tena. ..

Alvin alipapasa kichwa chake kwa kukosa maamuzi. Kabla hajajibu, Rodney alisema, “Tayari tumetayarisha kila kitu. Utakuwa ni usumbufu sana tukiibadilisha tena."

"Ikiwa unataka kitu tofauti, mjulishe tu mpishi. Atakuandalia” Alvin alibana kidole chake na kusema kwa sauti ya kuhimiza, “Rodney ameajiri wapishi bora kabisa nchini Kenya. Wanaweza kupika chochote.”

"Nilikuwa natania." Lisa alicheka. “Nitakula nyama choma ya mbuzi. Wewe unataka kula nini? Samaki ni sawa? Lakini nguruwe ndiyo favorite yako."

Alvin alisita kwa muda, lakini alipokuwa karibu kujibu, Rodney alisema,
“Ni sawa. Maurine tayari ametayarisha nyama ya nguruwe kwa ajili ya Alvin.”

Lisa alielekeza macho yake kwa Maurine, ambaye alikuwa ameshikilia vipande vya nyama ya nguruwe, nyama iliyokuwa ni kipenzi cha Alvin.

Lisa alihisi kuishiwa pozi. Mtazamo wa woga ukajidhihirisha juu ya uso wa Maurine. Alikuwa mwishoni mwa akili zake. “Pole, Bi. Kimaro. Sikujua ungefika mapema. Nitakuacha uendelee kumwandalia mumeo.”

Rodney hakuridhika na pendekezo la Maurine. “Siyo ishu kubwa Lisa, usichukie. Ni nyama tu ya nguruwe, sivyo? Maurine ndiye anayesimamia kumtunza Alvin. Hakuna haja ya kuchukia kuhusu hilo.”

"Kwani mimi nimechukia?" Lisa alimkazia macho Rodney kwa hasira. Siku zote alikuwa akimchukia, lakini alimchukia zaidi siku hiyo.

Mtazamo wake ulimfanya Rodney kuudhika. "Umekuwa ukimwangalia Maurine kwa hasira, na ikasababisha aingiwe na hofu."

"Hapana, Rodney," Maurine alisema mara moja kwa upole. "Bi. Kimaro hata hajanikasirikia. Mbona huwa tunaelewana vizuri tu."

Rodney alikoroma, “Kwanini unamuogopa sana?”

"Mimi simuogopi bwana!" Maurine aliongeza kwa tahadhari. "Ninaonyesha heshima yangu kwake."

"Heshima? Wewe ni muuguzi, na unalipwa kutekeleza majukumu yako.” Rodney aliendelea kumtetea Maurine.

Lisa alipandwa na hasira. "Bwana Shangwe, maneno yako yananifanya nionekane kama sijakaribishwa mahali hapa. Sijawahi kumtendea vibaya Maurine, tafadhali.”

“Bi. Mdogo, Bwana Shangwe, nyinyi…” Maurine alijibu kwa haraka, lakini Lisa akamkatisha kabla hajamaliza kuzungumza, “Kwa vile tunamlipa kufanya kazi, si ni jambo la busara kwake kuwa na heshima? Unawalipa wasaidizi wako wa nyumbani na walinzi pia kutunza nyumba yako, kwa hiyo ina maana wanaweza kukukosea heshima?”

Rodney alishindwa kujizuia pia. “Lisa, umemaliza? Nimekukosea? Kwanini unaendelea kunirushia maneno? Acha nikuambie kwamba Maurine ni tofauti na watu wengine…”

“Rodney.” Alvin akakatisha sentensi yake kwa sauti nzito. “Lisa ni mke wangu. Uwe na adabu kwa shemeji yako."

Lisa alikunja uso huku akiwaza Rodney alikuwa anapanga kusema nini tena. Tofauti na watu wengine? Maurine alikuwa tofauti vipi?

Rodney akajibu kwa uchungu, “Unapaswa kumdhibiti, basi. Ikiwa ana jambo la kusema, aseme tu badala ya kuwa mbishi sana.”

"Nilifikiri nimezungumza moja kwa moja na wala sikutia mafumbo hata kidogo," Lisa alibishana bila kujali.

“Wewe…” Rodney akakomea njiani baada ya kukosa cha kusema.

“Lisa, nichomee nyama.” Alvin alimvuta ghafla Lisa. “Twende huku.”

".. Sawa." Baada ya yote, Lisa alifikiria kuwa Rodney alikuwa rafiki wa Alvin. Ikiwa angeanzisha ugomvi kuhusu jambo hilo, isingemsaidia kitu. Kwa hivyo, alitikisa kichwa na kuelekea kwenye jiko la nyama choma upande mwingine.

Lakini, bado alikuwa katika hali mbaya. Hakusema lolote tangu alipofika, lakini Rodney alionekana kama amempania kwa namna fulani. Ghafla ilimwingia kichwani Lisa kwamba tabia ya Maurine ilijaa unafiki, ambao ulimkumbusha Lina.

"Nyama itaungua usipo igeuza," Alvin alimkumbusha. “Bado umekasirika?”

"Hapana. Nilikuwa nikifikiria jambo lingine.”

“Ulikuwa unafikiria nini? Unawezaje kutengwa wakati uko pamoja nami?" Alvin aliinua uso wake na kumtazama machoni.

“Nilikuwa najiuliza… Je, wauguzi siku hizi ni matajiri sana?” Lisa aliuliza ghafla. “Ameeweza kumudu mavazi ya gharama hivi kuanzia unyayoni hadi utosini, kwa hesabu ya haraka haraka hapo anaweza kuwa ametupia milioni na ushee, ukijumlisha na nywele.”

Alvin akamjibu bila kuwaza. "Tulipoenda kuvua samaki alasiri hii, Maurine alianguka majini kwa bahati mbaya. Rodney ndiye aliyemnunulia nguo hizo za kubadilisha.”

Lisa akiwa ameduwaa, midomo yake ikatengana kidogo.

“Angalia…” Alvin alicheka bila kujizuia. “Huniamini tu, huh? Una wivu kwa sababu ya Maurine. Angalia jinsi ulivyomtisha.”

Lisa alishindwa cha kusema. Ni saa ngapi alimtisha Maurine? Maurine alionekana kutojiamini ingawa Lisa hakusema neno. Je! lilikuwa kosa lake?

“Hata wewe unafikiri nilimtisha?” Lisa aliuliza baada ya kimya cha muda.”Labda anaogopa sura yangu mbaya.”

"Lisa, sahau kuhusu hilo." Alvin alimshika tena mikono. "Ninajua kuwa hujiamini, lakini hujui hisia zangu kwako?"

Baada ya kuelewa ujumbe wake, Lisa alirudia swali lake. “Unadhani hata mimi ninamuogopa?”

"Tunaweza kuacha mada hii?" Alvin alifungua chupa ya mvinyo na kumkabidhi. "Yeye ni muuguzi, hana maana yoyote kwenye moyo wangu."

Lisa alichukua mvinyo kimya kimya. "Rodney anavutiwa na Maurine?"

"Labda. Sina uhakika.” Alvin alibadilisha mada. "Ninahisi kula ndizi."

“Sawa.” Lisa alichukua ndizi akazimenya na kuziweka kwenye grill.

Muda mfupi baadaye, Chester alikuja na sahani ya nyama ya ngurwe iliyochomwa. Alisema kwa namna ya kutania, “Shemeji naomba nipate kibali chako. Alvin anaweza kula nyama ambayo mwanamke mwingine alichoma?”

"Hapana. Anaweza kula tu nyama nitakayomchomea,” Lisa alijibu kwa ukali.

Sura ya: 238

“Kwanini umzuie…”

Kabla hata Chester hajamalizia sentensi yake, zogo kubwa lilisikika kati ya walinzi waliokuwa wakimzuia binti mmoja aliyekuwa akilazimisha kuingia ndani.

“Samahani, Bibiye. Huwezi kuingia.” Sauti ya mlinzi ilisikika. “Hujakaribishwa mahali hapa, kuwa mstaarabu sivyo utaumizwa bure.”

“Hao wanaume wote wananifahamu, kama hamuniamini hebu niachieni muone kama watanifukuza?” Yule binti alijitetea huku akifurukuta katikati ya mikono ya walinzi.

Lisa alipogeuza kichwa chake na kutazama upande ule, mara moja akamkumbuka kuwa ni yule binti ambaye alimkuta barabarani gari lake likiwa limezama kwenye matope.

"Charity, ni nani aliyekuruhusu kuja hapa?" Rodney alisimama ghafla. Uso wake ulijawa na karaha na chuki. “Potea sasa hivi kabla mashetani yangu hayajapanda.”

"Nimekuja kumtafuta Alvin Kimaro." Macho ya Charity yalilegea, lakini aliendelea kumtazama Alvin kwa nguvu. “Bwana Kimaro, ningependa kuzungumza na wewe kuhusu New Era Advertisings…”

“Unafikiri Alvin atakusikiliza?” Rodney alidhihaki, “Familia ya Njau imemkosea sana Alvin. Hulifahamu hilo? Hebu walinzi mburuteni mumtoe nje, haraka.”

Kundi la walinzi wa nyumba hiyo walimzunguka Charity mara moja na kumshika mabega yake pande zote mbili.

"Subirini." Lisa aliinuka ghafla. "Yeye ni mwanamke tu. Msimnyanyase kiasi hicho!”

"Hujui chochote kuhusu huyu mwanamke, wewe ni wakuja tu hapa Kenya, bora ungeacha kuingilia mambo yasiyo kuhusu!" Rodney alifoka. "Lisa, tafadhari usinipe wakati mgumu sana usiku wa leo, unasikia?"

"Rodney, kwa kweli tabia yako si nzuri." Uso wa Lisa ulionesha chuki waziwazi. "Tangu nilipoingia hapa unaniandama tu, kwanini?"

Rodney hakutaka kumsikiliza Lisa, akamgeukia Alvin. " Alvin, mdhibiti mkeo!"

“Lisa! Njoo huku.” Kwa mshangao, Alvin alizungumza kwa sauti ya kina wakati huu, "Usijisumbue juu ya jambo hili."

“Jambo gani? Ina maana huoni jinsi Rodney alivyokuwa mkali kwangu tangu niingie mahali hapa?” Lisa aliuliza kwa hasira.

“Simzungumzii Rodney, namaanisha Charity. Achana naye…” Alvin alionya.

Lisa aliitazama sura ya binti huyo huku akiwa amekata tamaa. "Nimeonana naye njiani wakati nakuja hapa, yeye ni rafiki yangu, bila shaka mtamruhusu aingie."

Lisa aliona kwamba wanaume wote watatu walikuwa wakimtazama kwa sura zisizo za kawaida. Aliweza kuhisi kwamba macho yao hayakuwa ya kirafiki, lakini hakujali. Alichojali tu ni kumsaidia yule binti.

Macho ya Alvin yalitoa ishara ya onyo kali alipomtazama Lisa. Ilikuwa ni muda tangu alipomtazama kwa jicho kama hilo kwa mara mwisho. “Lisa, ni afadhali usifike mbali sana. Charity hastahili kuwa rafiki yako. Kaa mbali naye.”

“Nisipofanya hivyo?” Lisa alishupaza uso wake na kumwangalia Alvin machoni.

Alvin aliinua midomo yake kwa hasira, lakini Rodney hakuweza tena kuvumilia tabia yake. "Lisa, umeshamaliza? Acha ujinga. Kuna kikomo cha uvumilivu. Alvin anaweza kukuvumilia ikiwa utathubutu kumsogelea mwanamke huyu, lakini hakika mimi sitaweza.” Lisa alibaki kimya huku macho yakimtazama Alvin.

Hata hivyo, Alvin aliweka uso mkavu bila kusema neno lolote. Hali ilikuwa ya wasiwasi kwa muda. Wakati huo, Charity alitabasamu ghafla. "Ni sawa, Bi Jones. Ukisisitiza kuwa rafiki yangu, Bwana Kimaro anaweza kukupa talaka.”

Lisa alimtazama binti huyo kwa mshangao. Mwanzo alimwita kama Bi. Kimaro walipokutana kwa mara ya kwanza, lakini kwa wakati huo akamwita Miss Jones tena, ilimshangaza sana. Ilionekana alikuwa anamfahamu, japo kwa kiasi.

Ilimshangaza pia kwanini Alvin na marafiki zake walimchukia sana Charity. Hakuona kama Charity kama ni mtu mbaya. Badala yake, alihisi kwamba Charity alikuwa wazi na mwaminifu.

“Sawa Bi. Jones, naona hapa ni wewe peke yako ndiye mwenye moyo wenye kujali angalau. Niache tu nipambane na hali yangu nisije nikakuingiza matatizoni.” Charity alisema kwa sauti ya kugusa moyo.

“Achana na Lisa, Charity,” Alvin alionya kwa sauti ya huzuni.

“Nimekosea? Kwa kuwa ni mke wako, unatakiwa kumlinda wakati wote, hasa marafiki zako wanapokuwa karibu.” Charity alikoroma kwa kejeli. "Unawaacha tu marafiki zako wamfokee wanavyoisikia, hivi, umewahi kufikiria hisia za mke wako, Bwana Kimaro?”

Koo kavu la Lisa lilijisikia vizuri kidogo. Kinyume na matarajio yake, mtu wa kwanza kuzifikiria hisia zake hakuwa Alvin bali ni mgeni ambaye alikutana naye mara mbili tu.

“Inatosha, Charity. Acha kuwachonganisha Alvin na mkewe.” Chester, ambaye alisimama kando ya jiko la kuchomea nyama, hatimaye alizungumza. Alikuwa amevaa nguo zilizompendeza sana. Hata hivyo, sura yake ilionyesha chuki kali. "Bado una ulimi mkali kama zamani. Unaudhi kama nini!”

Maneno yake yalimchoma moyo Charity. Chester alionekana kuwa mzuri zaidi, lakini chuki yake kwake ilikuwa bado ile ile. Charity alitabasamu kwa uchungu na kusema. “Nimekuwa nikijaribu kuwakwepa kwa miaka hii yote. Kwa kadiri ninavyokumbuka, sidhani kama nimefanya jambo lolote lile lililowakera. Lakini kwanini mnaifanyia hivi kampuni ya New Era Advertisings? Bwana Kimaro, Alvinarah Media Network Group ni muhimu sana kwetu. Bila mtandao wa vyombo vya habari, matangazo yetu tutauzia wapi? Alvin nakuomba pleasee…”

“Ina uhusiano gani na mimi?” Alvin alidhihirisha kiburi chake.

Uso mzuri wa Charity ulizidi kufifia. “Bwana Kimaro, kama kuna tofauti zozote kati yetu, tunaweza kuziweka kando ya biashara na kuzungumza kibinafsi? Ukinikatia mtandao wako wa vyombo vya habari bila shaka utakuwa umekata nusu ya mapato ya kampuni yangu kwa mwaka. Sawa, pengine utakuwa umenipa somo mimi, lakini vipi kuhusu mamia ya wafanyakazi wanaotegemea kuendesha maisha yao kutokana na ajira zao kwenye kampuni ya New Era Advertisings?”

Kuona jinsi Charity alivyokuwa hoi ilimkumbusha Lisa hali yake ya zamani.

"Bwana Kimaro, labda utazingatia ombi langu nikikuomba nikiwa nimepiga magoti?" Charity alimkazia macho Alvin usoni kwa kufadhaika.

Rodney alisema kikatili, “Kuomba radhi hakusaidii, Charity. Hili ni somo kwako. Rudi nyuma na ujitafakari. Kuwa binadamu mwenye heshima. Nani anajua, tunaweza kufikiria kuipa familia ya Njau nafasi ya kuishi wakati ujao.”

“Nyie watu hamjabadilika hata kidogo. Hata sijajua nimefanya nini kilichowaudhi,” Charity alitabasamu kwa kujidharau. Alipogeuka tu na kuwa tayari kuondoka, alipigwa na butwaa baada ya kuuona uso wa Maurine.

Maurine aliingia katika hofu na kujificha nyuma ya Alvin. Alvin alipoona hivyo alizidi kuchukia. "Charity, potea mara moja."

Charity akakoroma kwa mara nyingine. Macho yake yaliwakodolea wanaume wale watatu kwa zamu kabla hajamtazama Lisa kwa huruma. "Wanaume watatu wanamdanganya na kumlaghai mwanamke mkarimu asiye na hatia. Je, hiyo ni haki?”

Kichwa cha Lisa kiligonga. Alikuwa amechanganyikiwa na maumivu. Hakuweza kuelewa ni nini Charity alikuwa akimaanisha, wala hakuelewa ni kwanini watu hao watatu walibadilika sana baada ya kusikia maneno yake.

“Toka nje.” Chester alipiga hatua kuelekea kwa Charity. Akamshika mikono na kumtoa nje. Alimkokota hadi kwenye geti na kumtupa nje.

Charity, ambaye alikuwa amevaa viatu virefu, aliangukia magoti. Nywele zake pia zilichafuka. Hata hivyo, alijikakamua na punde si punde akasimama. Hakuwa jeuri wala mnyenyekevu tena. Macho yake yalikuwa makavu na makali.

"Charity, ikiwa bado una matumaini kwa kampuni yako kupata nafasi Alivinarah, bora ufunge mdomo wako," Chester alimwonya kwa kumkodolea macho makali.

"Kwa kuwa mlikuwa na ujasiri wa kumleta Maurine hapa, kwa nini mnaogopa kumjulisha binti wa watu ukweli?" Uso uliopoa wa Charity ulizidiwa na ukaidi. “Nyinyi watu hamwezi hata kumsahau mwanamke ambaye amekufa kwa miaka mingi. Ni nini kizuri kuhusu Sarah? Yeye…”

Maneno yake yalimfanya aambulie makofi. Chester alishusha makofi kadhaa usoni kwa Charity. "Nyamaza."

Charity alijaribu kupepesa machozi. “Usijali. Sitamwambia Lisa kuhusu hilo. Ni mwanamke mzuri ambaye hastahili kuumizwa. Mtu mwenye matatizo kama Alvin hafanani naye.”

"Inaonekana kama hujajifunza somo lako." Chester akamshika tena na kumkaba koo. Hata baada ya kumuacha kwa miaka mingi, mwanamke huyo aliifanya damu yake kuchemsha.

“Nimekosea kusema hivyo?” Charity alijibu huku akinyong’onyea, “Licha ya kuwa ameoa, Alvin ameamua kumweka ndugu wa mpenzi wake wa zamani kama muuguzi wake. Anajaribu kumlaghai Lisa ambaye hajawahi kumuona Sarah kwa sababu yeye sio mwenyeji wa hapa, huh? Anahisi Lisa hatoshi? Kwa vile hawezi kumshinda Sarah, kwanini aliamua kumuoa Lisa? Ili kumdanganya? Nyinyi nyote ni wababaishaji.”

"Funga mdomo wako. Hujui lolote.” Chester alimvuta moja kwa moja na kumtupa kwenye dimbwi liliyokuwa kando yake. Maji ya baridi yalipofunika mwili wake mzima, karibu ashindwe kupumia.

"Tena ushukuru kwamba mimi ndiye niliyekutoa nje. Angekuwa Rodney au Alvin, matokeo ambayo ungekutana nayo sasa yangekuwa mabaya zaidi.” Chester alimtazama Charity ambaye alikuwa katika hali mbaya. Kisha, akageuka na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Sura ya: 239

Kimya cha kutisha kilitawala baada ya Charity kuondoka. Ni sauti ya mkaa unaowaka tu ndio ilisikika katikati ya ukimya. Muda kidogo Alvin akachukua koti lake kisha akaweka mkono wake kiunoni mwa Lisa. “Sijisikii kula tena. Twende chumbani kwangu.”

“Nataka kurudi nyumbani,” Lisa alisema ghafla.

Rodney alikasirika sana. “Alvin, si uliahidi tutaenda kuvua samaki baharini kesho asubuhi? Unaweza kumwomba Hans ampeleke Lisa nyumbani. Ni mara chache sana sisi huwa huru kujumuika pamoja na kujiburudisha.”

“We baki na marafiki zako, Shani atanirudisha nyumbani.” Lisa alimsukuma Alvin na kuanza kuondoka.

"Sitabaki." Alvin alimfuata Lisa kwa hatua kubwa. Maurine naye alikusanya vitu vyake kwa haraka na kuwafuata pia.

Rodney alikasirika mpaka akapiga teke jiko la kuchomea nyama likaanguka chini.
•••
Wakiwa njiani kuelekea nyumbani, Hans aliwaendesha Lisa na Alvin waliokuwa wamekaa kwenye viti vya nyuma, pamoja na Maurine aliyekuwa ameketi kwenye siti ya abiria. Shani akaendsha peke yake gari la Lisa.

Baada ya muda, Maurine kwa uangalifu aliwapa Lisa na Alvin kipande cha keki. "Bwana Kimaro, Bibi Mdogo, chukueni kipande hiki cha keki ili kutuliza matumbo yenu kwani nyie hamkula chochote jioni hii."

Lisa alibaki kimya na kumtazama Maurine hadi uso wake ukahisi kupauka.

Akiwa amekunja uso, Alvin akanyoosha mkono wake kuchukua keki. Kisha, akaiweka mbele ya Lisa. “Itatuchukua angalau saa nyingine kufika nyumbani. Kula tu kidogo.”

"Hakuna haja. Sijisikii kula.” Lisa aliinamisha kichwa chini na kuchezea simu yake.

Safari nzima ilikuwa katika hali ya wasiwasi. Maurine aliposhuka kwenye gari baada ya kufika nyumbani, macho yake yalikuwa mekundu, alimwamngalia Lisa kwa huzuni na wasiwasi.

Lisa alimkazia macho na kumtazama. "Nini tatizo? Kwanini unainagalia kwa wasiwasi hivyo?”

“Bibi Mdogo…Samahani.”” Maurine alikuwa mwisho wa akili yake. Ilionekana kana kwamba machozi katika macho yake yangetiririka wakati wowote.

“Samahani kwa lipi?” Lisa alijitahidi kusafisha hisia za hasira usoni mwake. “Acha kuigiza kama umeudhika na kutishwa. Ndiyo maana unawafanya watu wengine wafikiri kwamba nakunyanyasa.”

Alvin akakunja sura na kujaribu kusema. “Lisa…”

“Ninasema tu kile kilicho moyoni mwangu.” Baada ya kuongea, Lisa aliingia ndani ya jumba mara moja.

Maurine aliuma mdomo. “Bwana Kimaro, mkeo haonekani kunipenda sana. Kwa kweli sijui la kufanya.”

"Nenda ukapumzike kwa sasa." Alvin alimwambia. Akageuka na kumfuata Lisa chumbani.

"Sasa kwa kuwa umeonyesha hasira yako, unajisikia vizuri?"

"Hapana.” Lisa aliinua kichwa chake na kuutazama uso mzuri wa Alvin ukiwa umekakamaa kwa hasira. “Nikisisitiza kuwa rafiki wa Charity, utanitaliki?”

"Acha upuuzi. Umechukulia kwa uzito maneno ya Charity.” Alvin aliuliza kwa kuchukizwa.

“Unaweza kujibu swali langu?” Lisa alimtazama kwa nguvu.

Alama ya kukosa subira ilitanda kwenye paji la uso la Alvin. “Sitakutaliki, lakini pia sitakuruhusu kuwa rafiki yake. Humjui Charity. Ni mwanamke mmbaya sana, hafai.”

“Ni mambo gani mabaya yasiyosameheka ambayo amefanya? Unaweza kunipa mfano?” Lisa aliuliza kwa shauku ya kutaka kujua.

Macho ya Alvin yalizidi kukolea hasira, akatazama pembeni asije kumkwaza Lisa. “Amefanya mambo mengi sana mabaya siku za nyuma. Ninakuonya kwa manufaa yako mwenyewe.”

“Ni mabaya gani hayo ambayo huwezi kuyataja? Alimuumiza mpenzi wako wa zamani?" Lisa alishindwa kujizuia kumtania Alvin.

Mwili wa Alvin ulisisimka. Aligeuka na kumtazama Lisa. “Acha kuwaza upuuzi, unasikia? Unataka tu uanze kubishana nami juu ya mwanamke ambaye hata humjui, huh? Kuna faida gani?”

“Ninabishana na wewe?” Lisa alivaa tabasamu licha ya kuwa na hali ya huzuni kali. "Ninakuuliza tu maswali ya kawaida, lakini wewe ndiye hutaki kujibu maswali yangu."

“Sipendi kubishana na wewe Lisa. Nina njaa. Nataka kula kitu.” Alvin alielekea mlangoni.

“Unaweza kujibu swali langu la mwisho? Ni kitu gani wewe na marafiki zako mnajaribu kunihadaa na kunidanganya?” Lisa alimtamkia kila neno kama alivyosikia kutoka kwa Charity, huku akimkazia macho.

Alvin alitazama nyuma tena na kuyakazia macho yake ambayo sasa yalikuwa yamejawa na hasira. “Ni lazima nirudie mara ngapi? Maneno ya Charity si ya kweli. Ni wazi kwamba anajaribu kututenganisha. Acha kuuliza maswali ya kipuuzi, la sivyo nitapoteza imani na wewe.”

Lisa alijihisi mnyonge mbele ya shutuma za Alvin. Hakuwa na maana ya kutilia shaka. Hata hivyo, hakusahau sura ya huruma aliyopewa na Charity baada ya kumwona Maurine. “Sawa. Tuache mabishano kuhusu Charity. Mwambie Maurine aondoke na utafute muuguzi mwingine, basi. Simpendi.”

Alvin alikunja uso wake kwa hasira na mshangao. “Umekuwa ukisema mengi na kuvuta uso mrefu usiku kucha kwa sababu tu humpendi Maurine na huna imani na mimi? Ulitakiwa kusema hivyo moja kwa moja kuliko kuanzisha madrama mengi. Kwanini uzungukezunguke?”

Lisa alishtuka. Ilikuwa ni muda tangu aliposikia maneno ya kijeuri kutoka kwake. Maneno hayo yalionekana kama kofi usoni mwake. “Ukiendelea kunifikiria hivi, hakuna ninachoweza kufanya. Hata hivyo, siwezi kukaa pamoja na Maurine hapa nyumbani.” Lisa alisema kwa uwazi, “Maurine sio muuguzi pekee hospitalini. Kuna wauguzi wengine pia."

“Smash!” Mlio wa glasi ikivunjika sakafuni ulisikika ghafla mlangoni.
Wote wawili waligeuza macho yao kuelekea upande huo, wakishangaa ni saa ngapi Maurine alikuwa amefika kwenye mlango wa chumba chao. Uso wake ulikuwa na wasiwasi, macho yake yalikuwa mekundu, aliyatumbulia macho maziwa yaliyomwagika pale chini na vipande vya glasi vilivyotawanyika sakafuni.

Muda mfupi baadaye, Maurine alitabasamu kwa uchungu huku machozi yakimtoka. "Bwana kimaro, kwa kuwa mke wako hanipendi, itabidi kutafuta muuguzi mwingine."

Alvin akakunja uso wake kwa hasira na hakusema chochote.

Maurine alishusha pumzi na kulazimisha tabasamu. “Huwezi kuharibu uhusiano wako na mke wako kwa sababu yangu. Naweza kuelewa hilo. Nimekuwa nikijaribu kuepuka hali ya aina hii, lakini Bi. Kimaro nahisi ananifikiria vibaya.”

Alvin aliinua kichwa chake. Sura ya kutisha ikatanda usoni mwake.

"Nitapakia na kuondoka sasa hivi." Akiwa ameduwaa, Maurine akainama ili kuokota vipande vya glasi, lakini kwa bahati mbaya alijikata kidole chake. Damu zilianza kuchuruzika sakafuni. Aliifuta damu kwa nguvu. Hata hivyo, kadri alivyozidi kuipangusa ndivyo damu inavyozidi kumwagika. Wakati huo huo machozi zaidi yalikuwa yakimwagika usoni mwake.

“Ni sawa. Viache tu, Shangazi Yasmine atasafisha baadaye.” Alvin alimvuta Maurine na kushuka naye kwenye ngazi.

Lisa alishuka pia kwenye ngazi, ambapo alimuona Alvin akipiga kelele sebuleni, “Anti Yasmine, kifaa cha huduma ya kwanza kiko wapi? Unaweza kumsaidia Maurine kufunga kidole chake?”

Shangazi Yasmine alifika kwa haraka na kumsaidia Maurine kufunga kidole chake kwa bandeji akisaidiwa na Alvin. Kulitazama tukio hilo mubashara, wasiwasi ulizidi kumjaa Lisa. Mtu kiburi kama Alvin angewezaje kuwa na wasiwasi na mgeni kama Maurine hata akamshika mkono? Je, Maurine alikuwa muuguzi tu?

Kwa bahati nzuri, maneno ya Charity yalimkumbusha. Kulikuwa na jambo linaloendela ambalo yeye hakulifahamu. Ikiwa Maurine angeendelea kukaa pale, Alvin angeweza kuishia kumjali zaidi. Lisa akahisi wivu ukimzidia kiasi cha kushindwa kuvumilia.

Sura ya: 240

Alijiuliza mambo mengi sana. Alvin alikuwa ameanza kumtenga kwa ajili ya marafiki zake na Maurine ndani ya muda mfupi tu. Je, mwaka mmoja au miwili baadaye ingekuweje? Lisa aligusa uso wake ulioharibika na akakosa matumaini. Je, Alvin bado angempenda kwa moyo wake wote? Aligeuka na kuelekea kwenye maktaba ili kujisahaulisha na mawazo hayo kwa kufanya kazi zake za ziada.

Muda mfupi baadaye, alisikia sauti ya gari ikiondoka. Alihisi pengine ni Maurine ambaye alikuwa akiondoka. Lakini, Lisa hakutoka nje ya maktaba.

Saa tano usiku, mlango wa maktaba ulisukumwa kwa nguvu. Alvin aliingia huku akiwa amekunja uso. “Lisa, unafanya nini? Angalia muda sasa, ni saa ngapi na bado haujalala, bado una hasira na Maurine, sivyo? Tayari ameondoka.”

“Unaweza kwenda kulala kwanza? Bado nina jambo la kushughulikia.” Lisa aligeuza macho yake baada ya kumtazama. Hakuweza kukubali ukweli kwamba alikuwa amebadilika kwa sababu ya mwanamke mwingine.

“Inatosha. Uvumilivu wangu una mipaka yake.” Alvin alimvuta kutoka kwenye kiti na kusema kwa jeuri, "Usiniangalie kwa sura ya kuchukiza, amka twende!"

"Usinishike kwa mkono uliotoka kumshika mwanamke mwingine." Lisa alimsukuma kwa hasira.

Alvin akapandisha hasira. "Unawaza nini Lisa? Mkono wake ulikuwa umekatwa na chupa, kwa hiyo nikamwomba Aunty Yasmine aufunge bandeji. Hilo nalo ni la kuonea wivu? Ina maana siwezi kumsaidia mwanamke yoyote kwa sababu nipo na wewe?”

Lisa alijaribu kuzuia uchungu moyoni mwake kisha akasema kwa sauti ya kwikwi, “Hujawahi kumjali hivi Hans wala Shani, lakini Maurine? Unambembeleza na kuongea naye kwa upole kuliko hata mimi, unafikiri nitajisikiaje?”

“Huna akili!” Alvin akauachia mkono wake. "Maurine ni muuguzi wangu, lazima ni mtii ili anihudumie vizuri. Suala la afya halihitaji mzaha.”

“Sijakukataza kuwa naye, ila ni lazima uchague moja, mimi au yeye” Lisa alimpa mtihani.

“Kwa kuwa unafurahia kukaa hapa, endelea kukaa na uchukue fursa hii kujitafakari. Unaweza kuwa na wivu, lakini kuna kikomo kwa hilo.” Alvin akaufunga mlango kwa nguvu na kuondoka huku akiwa amekunja uso.

Lisa alikaa kwenye kiti kimya bila kujua kuwa machozi yalikuwa yakimtoka. Usiku huo hakuingia chumbani hata kidogo.

Alvin alijirusha huku na kule kitandani peke yake kwani usingizi ulikuwa wa shida. Tangu Maurine aanze kumhudumia, hakuwa amepatwa na tatizo la kukosa usingizi. Usiku huo, alilala kwa saa moja tu. Alipoamka asubuhi iliyofuata, uso wake ulikuwa umekunjamana kwa kukosa usingizi wa kutosha. Hakutaka hata kuiona sura ya Lisa. Kwa hiyo, aliondoka nyumbani bila kupata kifungua kinywa.
•••
Baada ya kufika ofisini, Lisa alimpigia simu Hans. "Nenda kapeleleze kinachoendelea katika kampuni ya ‘New Era Advertisings’. Kisha uniletee taarifa."

Lisa alimpigia simu Pamela baadaye. "Nisaidie kitu kimoja shosti, najua kuwa una marafiki wengi zaidi hapa Nairobi kuliko mimi. Umewahi kusikia kuhusu Charity Njau anaye milikikampuni ya New Era Advertisings ?"

“Oooh! Charity Njau? Kweli,” Pamela alijibu kwa mzaha. "Nilisikia kwamba alikuwa mpenzi wa zamani wa Chester. Kuna nini kwani?"

“Sawa, nahitaji kujua zaidi ya hilo!”

Pamela aliongeza, “Nilivyosikia ni kwamba, Charity ana sifa mbaya. Uvumi umeenea kwamba yeye ni mkatili sana. Anaweza kufanya lolote bila kujali utu kwa ajili ya pesa na madaraka. Amefikia hata hatua ya kuwadhulumu ndugu zake ili kuwa mtendaji mkuu wa New Era Advertisings. Mama yake alikuwa ni sekretari tu wa Bwana Langa Njau, mwanzilishi wa kampuni hiyo ya New Era Advertisings na ndipo Charity akazaliwa. Ni baada tu ya mke halali wa Langa Njau kufariki ndipo mama yake Charity aliiteka familia ya Njau . Nilisikia mama yake pia ni katili.”

Lisa aliuliza kwa udadisi baada yakusikiliza maelezo marefu ya Pamela, "Mke wa zamani wa Langa ana waoto?"

“Swali lako linanitia wasiwasi,” Pamela alisema kwa kufadhaika. “Namfahamu mwanamume mmoja anaitwa Thomas Langa Njau. Nilihudhuria hafla moja siku chache zilizopita ambapo Thomas Njau alionyesha kuvutiwa nami, na tangu wakati huo, amekuwa akinisumbua sana.”

“Thomas Njau ?” Lisa alikunja uso. "Jina hili siyo geni kwangu."

Akiwa na mawazo, Lisa aliinuka na kusimama ghafla. “Nimekumbuka sasa. Unaikumbuka ile ishu ya Kelvin kuchomwa kisu na kupoteza figo hospitali? Enhee, basi mtu mmoja anayeitwa Zigi Kabwe alitaka kuniua. Lakini kwa bahati, Kelvin alikuja kuniokoa. Baadaye, nilisikia kutoka kwa polisi kwamba chanzo cha Zigi kutaka kuniua ni kulipiza kisasi kifo cha dada yake.”

Lisa akaweka kumbukumbu zake sawa na kuendelea.

“Thomas kutoka familia ya Njau ya hapa Nairobi alitaka kumbaka dada yake Zigi, Lily Kabwe. Lily alijiua kutokana na mfadhaiko. Familia ya Kabwe ilimshtaki Thomas, na alitakiwa kutumikia kifungo chake. Hata hivyo, Alvin alimtetea kwenye kesi na akashinda.”

“Ndiyo, nimekumbuka uliwahi kunisimulia kipindi Kelvin kalazwa hospitali.” Pamela alipigwa na butwaa. “Kwanini ameamua kunisumbua? Hataweza kunibaka kweli?”

"Kwani anajua unapoishi?" Lisa alikuwa na wasiwasi juu yake.

“Eeh! Anajua. Sijui hata alipajuaje. Nimewahi kumkuta mara mbili akinisubiri nje ya nyumba yangu ninapotoka kazini jioni.” Kadiri Pamela alivyozidi kufikiria juu yake, ndivyo alivyokuwa akiogopa zaidi. “Sidhani kama ana nia njema na mimi. Ana husiana vipi na Alvin? Kwanini alimsaidia kesi yake?”

“Bado sijajua.” Lisa alijibu. “Sidhani kama inafaa kuendelea kukaa hapo. Kaa hotelini kwa muda huu,” Lisa alimshauri kwa wasiwasi. "Nipigie simu mara moja ikiwa chochote kitatokea."

“Sawa. Nakubaliana na ushauri wako.”

Baada ya kumaliza kuongea na Pamela, Hans aliingia akiwa na habari za uchunguzi wa kampuni ya New Era advertisings.

“Bi. Jones, New Era Advertisings hujihusisha na matangazo ya redio, televisheni, magazetini, mtandaoni, mabango ya barabarani na promosheni ya bidhaa mbalimbali. Kwa muda mrefu imefanya kazi pamoja na mtandao wa vyombo vya habari vinavyomilikiwa na kampuni ya Alvin, Alvinarah Media Network Group, au AMEN Group kwa kifupi, ambayo ni kampuni iliyo ndani ya Alvinarah Group of Compannies. Pia inashirikiana na KIM Outdoors iliyo chini ya KIM International kwa ajili ya mabango ya barabarani. Lakini, Charity Njau, bosi wa New Era Advertisings kwa namna fulani alimkasirisha Alvin Kimaro, na kusababisha Alvinarah na KIM International kughairi ushirikiano wao. Kwa hivyo sasa makampuni yanayojitangaza kupitia New Era Advertisings yanajitoa kwa sababu kampuni hiyo haina uwezo wa kuwafikia wateja wao tena.”

"Charity Njau kamchukiza Alvin Kimaro, kwa lipi?” Lisa aliuliza kwa kutilia mkazo neno la mwisho.

Hans akajibu. "Kwa kweli, Charity amekuwa akisimamia New Era Advertisings vizuri kabisa kwa miaka michache iliyopita, lakini kwa bahati mbaya..." Hans akashindwa kumalizia.

"Usijali." Lisa aliitikia kwa kichwa. “Unaweza kunipatia namba ya Charity? Ningependa kukutana naye.”

Kulikuwa na mashaka mengi akilini mwake ambayo alitaka kufafanuliwa.
Thomas Njau, Charity Njau, Alvin Kimaro, Rodney Shangwe, Chester Choka, Zigi Kabwe, Maurine Langa…Je, watu hawa walikuwa na uhusiano gani?

Ilimchukua Hans muda kupata namba ya simu ya Charity. Kisha, Lisa akampigia Charity simu.

"Huyu ni Charity Njau kutoka New Era Advertisings. Nikusaidie nini?” Mwanamke huyo alikohoa katikati ya maneno yake.

"Lisa Jones. Je, una homa, Bi. Njau ?” Lisa alipigwa na butwaa.

"Ndio, nina homa kidogo."

"Una muda tukutane kwa chakula cha jioni leo?" Lisa alikuwa na hakika kwamba Charity asingekataa ombi lake kwani alikuwa akihitaji msaada. Lakini kinyume na matarajio yake yote, Charity alimkataa. "Sidhani kama naweza, Bi Jones. Najua una mashaka mengi akilini mwako, lakini New Era Advertisings sasa iko kwenye changamoto kubwa. Nikikutana nawe, kampuni yangu itaishia katika hali mbaya zaidi. Huwezi kunisaidia.”

TUKUTANE KURASA 241-245

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI...........LISA
KURASA.......241-245

Sura ya: 241

“Ni sawa, kama unafikiria hivyo. Lakini unaweza kunasidia kitu kimoja, unaweza kuniambia Maurine Langa ni nani?”

“Bi. Jones, usitake kujua kuhusu hilo.” Charity alijibu kwa mkato.

"Inaonekana una wasiwasi na mimi." Lisa aliishika simu yake kwa nguvu. “Jana ulisema Alvin na marafiki zake wanadanganya na kunilaghai, unakumbuka? Nadhani ulikuwa unanionea huruma.”

“Haina maana tena. Maadamu wewe ni jasiri, huhitaji kujali wengine wanafikiri nini juu yako,” Charity alijibu kwa sauti ya chini.

Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Sawa, sitakulazimisha. Hata hivyo, kuna jambo moja zaidi. Una kaka anayeitwa Thomas Njau? Unaweza kumwomba aache kumsumbua rafiki yangu Pamela? Mwambie kwamba yatampata makubwa kama ataendelea kumfuatilia.”

“Thomas Njau …” Sauti ya Charity ilijawa na papara. “Sawa, nitamwambia. Lakini ngoja nikukumbushe jambo pia, Bi Jones. Mwambie Maurine akae mbali na Alvin haraka iwezekanavyo.”

Moyo wa Lisa ulirukaruka. “Tayari nimemfukuza jana usiku.”

“Nina wasiwasi kwamba baadhi ya watu hawatakubali aondoke…”

Kabla Charity hajamalizia maneno yake, zogo likasikika nje ya ofisi ya Lisa. Rodney aliingia ndani ya ofisi huku akimburuta Shani nyuma yake.

"Samahani kidogo, kuna dharura imejitokeza nitakupigia baadaye." Lisa alimwambia Charity na kukata simu.

Baada ya kukata simu, Lisa alielekeza macho yake kwa Rodney ambaye alionekana kuhamaki. Ghafla, kitu kiliingia akilini mwake. Je, hiki ndicho Charity alichomaanisha kwamba baadhi ya watu hawatokubali Maurine kuondoka? Lisa alizidi kuchanganyikiwa.

"Bwana Shangwe, ni nini kimekuleta hapa ofisini kwangu?" Lisa aliinua kichwa chake na kuuliza kwa hasira.

“Acha kujifanya, Lisa. Ulimlazimisha Alvin kumfukuza Maurine?” Rodney aliweka mikono yake juu ya meza huku akiwa na hasira machoni pake. "Unawezaje kuwa na akili ndogo kiasi hicho? Nilikuwa nimeanza kukuheshimu lakini sasa unanifanya nikudharau.”

Lisa alimtazama bila kupepesa macho hata kidogo. "Sina uhusiano na wewe, kwa hivyo sijali jinsi unavyoniona."

“Mimi ni rafiki mkubwa wa Alvin na ninamuelewa. Unafikiri Alvin atakupenda mtu mwenye kuchukiza kama wewe?" Rodney alidhihaki, “Maurine alikuwa anakuheshimu, lakini unajifanya kana kwamba wewe ni wa matawi ya juu. Unafikiri unaweza kuwadharau watu wengine kwa sababu ya hadhi yako kama Bi. Kimaro? Kweli, kwa jinsi ulivyo, hakuna mwanaume ambaye atakupenda kama Alvin atakuacha.”

Maneno yake yalipenya moyoni mwa Lisa. “Tangu jana unamtetea Maurine. Wewe ni nani yake hasa, huh? Mshenga, au kuwadi wa Alvin? Unategemea kwamba atachukua nafasi yangu na kuwa shemeji yako mpya?”

Rodney alishindwa kujizuia. “Umerukwa na akili. Ninamchukulia Maurine kama dada yangu, na siwezi kuvumilia jinsi ulivyomnyanyasa.”

“Nilimnyanyasa?” Lisa alijihisi kukosewa adabu sana. "Maurine ndo kakuambia hivyo?"

“Maurine hakusema. Yeye ni mkarimu sana, lakini mimi si mpumbavu.” Rodney alimwonya vikali, “Lisa, ukithubutu kumnyanyasa tena, nitakufanya kitu kibaya hata Alvin hatakutetea.”

Rodney alipofika mlangoni wakati akiondoka, alitazama nyuma. “Nimemfahamu Alvin kwa zaidi ya miaka 20. Wewe umemjua kwa muda gani? Fikiri juu ya hilo.” Lisa alibaki ameduwaa.

Mpaka inafika usiku, Alvin hakumpigia simu kabisa. Kwa kuwa Shani alikuwa naye na alishuhudia yote, Lisa aliamini kwamba Alvin alikuwa anajua kilichotokea siku hiyo. Alijiuliza labda ni Alvin ndiye aliyemtuma Rodney kufanya aliyoyafanya. Kwa hasira, Lisa hakurudi Mombasa baada ya kazi siku hiyo. Alikula chakula cha jioni na kuanza kutembea kwenye mitaa ya katikati ya jiji la Nairobi peke yake.

Aliingia kwenye duka la Stears na kuagiza aiskrimu. Ghafla, sauti ya upole ya mwanaume, iliyozoeleka masikioni mwake ilisikika nyuma yake.
"Ice cream ni tamu eeh? Ninunulie moja basi.”

Lisa aligeuza kichwa chake nyuma na kumuona Kelvin akiwa amesimama nyuma yake akiwa amevalia suti ya kijivu. Alipendeza kiasi chake, na wanawake kadhaa walikuwa wakimtolea macho ya wivu.

Kelvin aliinamisha kichwa chake na kumtazama Lisa machoni. Macho yake yalijawa na hisia za mapenzi.

"Ni muda umepita tangu tukutane." Lisa alisema bila kujiamini.

"Ndio. Nilikuona wakati natoka kazini sasa hivi, kwa hiyo sikuweza kujizuia kukufuata hapa,” Kelvin alijibu kwa huzuni. "Umekuwaje? Huonekani kuwa na furaha sana sasa hivi…”

“Hapana. Nilikuwa nafikiria tu mambo ya kazini,” Lisa alikanusha kabisa.

"Nilidhani kwa kuwa uko na mwanaume unayempenda, ungekuwa unafurahi muda wote.” Kelvin alicheka kwa namna ya kujidharau.

“Pole, Kelvin…” Lisa alilemewa na hatia. “Sikukusudia kukuumiza.”

"Pole haijawahi kumponya mtu." Tabasamu la uchungu lilienea kwenye uso wa Kelvin. Alichukua ice cream kutoka kwa mhudumu kisha akamkabidhi moja Lisa.

"Kuna dharura imetokea. Kwaheri.” Lisa alitbofyabofya simu yake kwa uongo na kweli kisha akatoa kisingizio cha aibu kwani hakuthubutu kumkabili Kelvin.

“Hutaki hata kukaa nami kwa muda? Lisa, usinifanyie ukatili sana.” Kelvin aliongea kwa maneno ya kusihi. Lisa akawa mpole.

Baada ya wote wawili kuketi, alimsikiliza Kelvin akiongea kuhusu maisha yake na mambo yanayohusiana na kampuni yake. Hawakutambua kuwa kuna paparazi aliwapiga picha kwa siri. Nusu saa baadaye, Lisa alitoa tena udhuru wa kuondoka.

“Subiri…” Kelvin alimshika mkono ghafla. Lisa hakupenda kushikwa na Kelvin hivyo akajinasua haraka haraka.

"Hutaki hata nikikugusa tu?" Macho ya Kelvin yalijawa simanzi. Alihisi kama pigo kwake. "Tangu zamani hupendi nikuguse."

“Kelvin, lazima nikiri kwamba nina deni kubwa kwako. Nilifikiria kutumia maisha yangu yote na wewe ili kufidia hilo, lakini niligundua kuwa mahusiano hayawezi kulazimishwa. Ninaweza kutoa figo yangu na kukulipa kama hutajali,” Lisa alisema kwa uthabiti.

Kelvin alipigwa na butwaa. Muda mfupi baadaye, uso wake wa kupendeza ukaonekana wenye huzuni. “Lisa, unadhani mimi ni mtu wa aina gani? Ni kweli umenitupa, umechagua kuwa na Alvin, lakini nakupenda. Sihitaji unijibu hivi.”

Kelvin alinyanyuka taratibu na kutoa simu yake mfukoni. Alibofya na kufungua picha na kumwonyesha Lisa. Lisa aliipokea simu bila kujijua.

Picha hiyo ilikuwa ya msichana mwenye umri wa kati ya miaka 17 na 18. Alikuwa na uso mdogo, wenye umbo la mviringo na ngozi nzuri. Tabasamu lake lilikuwa tamu, na kulikuwa na vishimo viwili ‘dimpos’ mashavuni mwake. Alionekana mrembo, mzuri na mwenye kuvutia sana machoni. Lisa alishtuka kuona msichana huyo anafanana sana na Maurine. Lakini, macho ya Maurine hayakuwa mazuri na ya kupendeza kama ya msichana huyo.

“Huyu ni…”

“Mpenzi wa zamani wa Alvin, ambaye pia alikuwa mpenzi wake wa kwanza.” Kelvin alijibu kabla Lisa hajamaliza hata swali lake.

Lisa akajikuta anakosa la kusema. Ingawa alikuwa amebashiri jibu kwa kiasi fulani, alikataa kuamini. Hata hivyo, maneno ya Kelvin yalikuwa yamefichua ukweli, na yaliufanya moyo wake kubana sana kiasi cha kukosa hewa. Haishangazi Charity alisema kwamba Alvin na rafiki zake walikuwa wakimdanganya na kumlaghai. Si ajabu Charity alimtazama kwa huruma.

Aligundua ni kwanini Alvin alimuajiri Maurine kama muuguzi wake, ni kwa sababu alianana na mpenzi wake wa zamani. Ha! Alijisikiaje kumuona Maurine kila siku? Je, alimkumbuka mpenzi wake wa zamani?
Maurine alikuwa nani kwake, basi? Kwa hiyo yeye hakuwa moyoni mwa Alvin? Hivi ndivyo Alvin alimaanisha kwa upendo usiobadilika?

“Mbona unanionyesha picha hii?” Lisa alimwangalia Kelvin kwa hasira.

"Haijalishi utanichukuliaje, lakini nilihangaika sana kupata picha hii."
Kelvin aliongeza kwa uwazi, “Familia nyingi tajiri hapa Nairobi zinajua kuhusu ex-girlfriend wa Alvin. Huko nyuma, alimdekeza kama binti wa kifalme na kuambatana naye popote alipoenda. Hata alisisitiza kumuoa licha ya pingamizi la familia ya Kimaro. Kwa kuwa alikuwa binti mkubwa katika familia ya Njau , Alvin aliisaidia sana familia ya Njau kwa gharama yoyote, hata akamfungulia baba yake kampuni kubwa ya matangazo, New Era Advertisings kwa mtaji kutoka familia ya Kimaro. Sarah alipenda sana viwanja vya burudani, kwa hivyo Alvin alitumia pesa nyingi kujenga Sarah Wonderland Park kwa ajili yake.”

Sura ya: 242

Lisa alimtazama Kelvin kwa butwaa. Sarah Wonderland Park? Bila shaka, alikuwa amesikia kuhusu bustani hiyo kubwa zaidi ya burudani ya Nairobi ambayo ilitoa burudani zenye kusisimua zaidi kutoka duniani kote. Moja ya jumba hilo liligharimu dola milioni 30 kulijenga. Hata hivyo, hakujua kuwa ni Alvin ndiye aliyemjengea mpenzi wake wa zamani uwanja huo wa burudani.

Kelvin aliongea kwa sura ya huzuni. "Na kumkumbuka, jina la Alvinarah ni mchezo wa maneno wa majina yao. Lisa, watu wengi mtandaoni wanakuonea wivu, lakini unajua kuna watu wengi katika jamii ya matajiri ambao wanakudhihaki?”

"Basi, inatosha!" Lisa alitikisa kichwa, akikataa kusikia zaidi.

"Kuna jambo moja zaidi ambalo hujui." Kelvin ghafla, akamshika mkono. “Unajua kwanini Zigi Kabwe alitaka kukuua?”

Midomo ya Lisa ilitetemeka. Hakumruhusu kukwepa swali hilo. "Familia ya Zigi ilikasirika kwa sababu Alvin alimwakilisha Thomas Njau kwa kesi ya ubakaji. Alifanya hivyo kwa sababu tu mwanamume huyo ni kaka wa Sara. Hakujali chochote kwamba Thomas Njau ni mtu mbaya ambaye alikuwa amefanya mambo mengi haramu maishani, alichojali ni kumsaidia tu kaka wa mpenzi wake. Alisaliti kanuni za kazi yake mwenyewe kwa sababu ya Sarah!”

Lisa aliduwaa na kukaa kimya. Hata kama alikuwa ameshaujua ukweli huo, kusikia hivyo kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine kuliufanya moyo wake udunde haraka sana kiasi kwamba alihisi kukosa hewa.

Hapo awali, alidhani Alvin alimtetea Thomas Njau kwa sababu ya pesa.
Kisha, alipojua kwamba alikuwa mtu tajiri zaidi nchini, alifikiri kwamba alikuwa amefanya hivyo kwa sababu ya kiburi cha uwezo wake na utukufu wa kuwa juu. Kumbe, ilikuwa tu kwa sababu ya mpenzi wake wa zamani.
Sara alikuwa muhimu kiasi gani kwake, kweli?

Kelvin alisema kwa sauti ya huzuni, “Ulikuwa karibu kufa wakati huo. Kwanini mimi na wewe tuingie matatizoni kwa sababu ya matendo mabaya aliyoyafanya Alvin kwa ajili ya mpenzi wake wa zamani?”

"Kelvi, nimesema inatosha!" Lisa alitamani kulia. Alihisi kwamba angepoteza akili ikiwa angeendelea kusikiliza zaidi.

“Lisa, nakuambia haya tu kwa matumaini kwamba utabaki kuwa na akili timamu. Usiache kila kitu kwa ajili yake, ikiwa ni pamoja na moyo wako. Hana afya, na hawezi kujitolea kwako isipokuwa wewe tu ndiye mtu unayempenda. Lakini nakuapia, hutaweza kuchukua nafasi ya mtu aliyekufa."

“Nitaweza. Asante.” Lisa alisema kwa hasira kabla ya kuutoa mkono wa Kelvin uliokuwa umemshika. "Nataka nibaki peke yangu kwa muda."

“Hakika…” Kelvin aliweka nywele za Lisa nyuma ya sikio lake.

Hatimaye, Lisa alipotoka kwenye mgahawa huo wa Stears alionekana kukata tamaa. Mapenzi machoni pake yalibadilishwa mara moja na dhamira hatari.
•••
Wakati huo huo, huko Mombasa katika jumba la Alvin la ufukweni mwa bahari, Alvin alipokea picha kadhaa kutoka kwa paparazi aliyemfahamu vyema.

Kulikuwa na picha chache za Lisa na Kelvin wakila aiskrimu pamoja kwenye mgahawa wa Stears, pamoja na ile aliyomshika mkono. Ingawa ilichukuliwa kutoka upande, mapenzi machoni pa mwanaume huyo na sura yake ya huzuni ilijidhihirisha wazi kwenye picha. Ni mkutano mzuri ulioje wa wapenzi wa zamani.

Hasira ambayo alikuwa ameivumilia hapo awali hatimaye ililipuka kama volkano. Alvin aliinuka na kufagia kila kitu kwenye meza ya chakula hadi sakafuni.



Shangazi Yasmine aliruka kwa hofu kumuona Alvin akivunja kila kitu kwenye chumba cha kulia chakula mithili ya mwendawazimu huku damu zikimtoka mikononi mwake. Hapo hapo akapiga simu kwa Lisa, lakini hakupata jibu.

Alipoona Alvin akizidi kupagawa zaidi kila sekunde iliyokuwa ikipita, hakuwa na jinsi zaidi ya kumpigia Maurine. Alikumbuka Maurine alikuwa akimhudumia vyema siku za karibuni.
•••
Baada ya kutoka Stears, Lisa aliendelea kutembea kando ya barabara akiwa kachanganyikiwa. Alisahau hata gari lake. Alitembea kwa muda mrefu akiwa hajui hata anapokwenda. Kufikia wakati anajikumbuka, aligundua kuwa alikuwa kwenye mlango wa Sarah Wonderland Park.

Fataki za kupendeza zililipuka juu ya ngome. Alikuwa akiitazama bila kujielewa wakati wanandoa fulani walipompita.

"Fataki ni nzuri."

"Ndio. Je, unajua ni kwa nini inafyatuliwa kwa wakati huu kila wiki?”

“Saa ngapi sasa? Ngoja nione. Saa mbili na nusu siku ya Ijumaa…”

“Ndiyo, ilikuwa ni siku kama hii na muda kama huu ambapo tajiri aliyejenga bustani hii ya burudani kwa ajili mpenzi wake alimvisha pete ya uchumba. Fataki hii ni kumbukumbu ya uchumba wao. Fataki hazikusimama usiku mzima. Fataki zililipuka angani na kuunda neno UPENDO. Tangu wakati huo, bila kujali hali ya hewa, huwa kuna maonyesho ya fataki hapa kila Ijumaa usiku. Kuna hata imani kwamba wanandoa ambao watatazama mlipuko huo wa fataki pamoja watakuwa na furaha milele.”

“Namhusudu sana huyo tajiri na mpenzi wake. Lazima wawe na furaha pamoja sasa.”

“Nafikiri hivyo pia.” Sauti ya mazungumzo yao ilififia kwa mbali.
Lisa alikuwa akipatwa na huzuni wakati aliporudi kwenye fahamu zake.

Ilikuwa nii hadithi nzuri kama nini. Akilinganisha na Mkufu wa Malkia aliomnunulia kwenye kwa pesa chafu huko Dar es Salaam, haukuwa chocote mbele ya bustani hiyo.

Ilikuwa ni aibu kwamba tajiri huyo aliishia kuoa mwanamke wa kutisha baada ya penzi lake la kweli kufa. Kwa wakati huu, alijiona kama mjinga.
Alijutia yote. Labda hakutakiwa kumwona kabisa maishani mwake Alvin na asingeishia kupata maumivu hayo ya kuvunja moyo.

Lisa alipanda ndege ya saa nne kurudi Mombasa, Shangazi Yasmine, ambaye alikuwa amesinzia kwenye kochi, aliruka kwa furaha alipomwona akirudi.

“Bibi mdogo, umerudi nyumbani?”

“Hmm.” Lisa aliburuta miguu yake mzito kwa uchovu kupanda ngazi.

"Bibi mdogo, mbona umechelewa sana kurudi?" Aunty Yasmine alimsogelea ghafla na kumuuliza huku akitabasamu. "Umekula? Una njaa? Ngoja nikuandalie chakula.”

"Sina njaa." Alizunguka kwa mkato na kumpita Aunty Yasmine.

“Unataka maziwa? Ninaweza kukutengenezea glasi sasa hivi.” Aunty Yasmini aliharakisha kwenda kumzuia kwenye ngazi.

Lisa alimtazama mwanamke huyo kwa sekunde chache kabla ya kuangaza kwenye ghorofa ya pili. “Anti Yasmine, kunanini huko juu? Kwanini unanizuia?”

Shangazi Yasmine alikuna kichwa kwa kusitasita. “Sikuwa…”

Bila kusikiliza maelezo yake, Lisa alimsukuma na ghafla nguvu zikamjia za kukimbilia ghorofani. Harufu ya kike ambayo haikuwa yake ilisikika hadi puani alipofungua mlango wa chumba cha kulala.


Lisa aligundua Alvin alikuwa amelala fofofo kwenye kitanda kikubwa. Hata hivyo, Maurine alikuwa amelala karibu naye huku mikono yao ikiwa imeshikana kwa pamoja.

Maurine alinyanyuka kutoka kitandani baada ya kusikia mlango ukifunguliwa. Sura ya wasiwasi ikamtoka alipomwona Lisa.

“Bibi mdogo, tafadhali usinielewe vibaya…”

Lisa alimkimbilia na kumpiga kofi usoni. “Nilikuwa na hisia mbaya na wewe tangu siku ya kwanza. Umeajiriwa kama nesi, na kazi hiyo haijumuishi kulala naye kwenye kitanda chetu.”

“Sikufanya hivyo,” Maurine alisema bila msaada.

“Hukufanya hivyo?” Lisa alikasirika sana hivi kwamba alishindwa kujizuia. “Nilikufukuza jana, lakini umerudi. Unajifanya wewe ndiye mama wa nyumba hii? Wazazi wako hawakukufunza adabu? Hivi una hata chembe ya aibu kweli?"

“Punguza kelele!” Alvin aliamka ghafla na kuketi kitandani huku akionekana kuishiwa nguvu. Aliuona uso wa Maurine ukiwa na michirizi ya machozi, na kulikuwa na alama ya kofi kwenye shavu lake. Kwa upande mwingine, uso wa Lisa ulikuwa ukipiga kelele za hasira. Ilikuwa dhahiri kwamba alikuwa amempiga Maurine.

"Lisa, unafanya nini?" Alvin alimtazama kwa hasira. "Unawezaje kumalizia hasira zako kwa mtu asiye na hatia mara tu unapofika nyumbani, nimekuwa nikikudekeza sana, si ndiyo?"

Lisa alishtuka. Kwa mantiki hiyo ilibidi afumbie macho kumuona mwanamke mwingine amelala kitanda kimoja na mumewe wakiwa wameshikana mikono?

“Kwanini amerudi?” Lisa alimnyooshea kidole Maurine na kumhoji kwa huzuni. "Si ulisema umemfukuza jana?"

"Naweza kumfukuza kazi na kumwajiri tena wakati wowote ninaotaka." Macho ya Alvin yalikuwa mekundu kwa hasira. Alikuwa amemfukuza Maurine kwa matakwa yake, lakini vipi kuhusu yeye? Alikwenda kwenye kulishana aiskrimu na Kelvin badala ya kuwahi nyumbani kumtunza mumewe. Alifikiri kuhusu hisia zake alipokuwa na akishikana na mwanamume mwingine hadharani?

“Sawa, nimeelewa.” Moyo wa Lisa ulivunjika vipande milioni. Kisha akatembea kuelekea chumba cha kubadilishia nguo na kuanza kubeba vitu vyake.

Kwa kweli, hakuwa na vitu vingi vya kusema. Hata kama angeondoka bila kitu chochote haikuwa na shida. Alifungasha tu vitu vyake kama kutoa ujumbe kwa njia ya vitendo kuwa alikuwa anaondoka. Aliingiza nguo zake chache kwenye sanduku na kutoka nje.

"Unafanya nini?" Alvin akamkazia macho kwa kutoamini.

Lisa aliinua kichwa kuzuia machozi yasimtiririke. “Hakuna sababu ya mimi kukaa hapa. Nawatakia maisha mema. Nitaondoka sasa hivi.” Baada ya hapo akageuka na kuelekea mlangoni.

Alvin alishika koti lake na kulitupa chini huku akimfokea kwa hasira, “Unaniacha kwa sababu ya Kelvin? Alikuambia nini? Lisa Jones, umesahau ahadi yako? Kwamba utakaa na mimi hadi nitakapopona? Kwamba utakaa nami milele hata kama ugonjwa wangu hautaisha?” Hatimaye, machozi yalitiririka kutoka kwa macho yake ya mviringo kama mto uliofurika.

Lisa allikuwa karibu kulegeza msimamo wake lakini alichefukwa ghafla aliposikia Maurine akisema kwa unyonge, “Ni kweli, Bibi Mdogo. Bwana Kimaro anakuhitaji sana. Tafadhali acha kumuumiza.”

“Kumuumiza?” Lisa alicheka. “Nani anamuumiza nani? Yuko na mimi, lakini bado anafikiria kupata mwingine zaidi. Sina muda na ujinga kama huu. Acha Maurine atibu ugonjwa wako. Hata hivyo mimi si daktari.” Lisa alitoka nje ya chumba cha kulala, akiburuta sanduku lake nyuma.

“Sitakuruhusu kuondoka.” Alvin alikimbilia mbele yake na kumshika mkono. Macho yake yalionekana kama mnyama wa porini. “Lisa, unaniacha kwa sababu mimi ni mgonjwa? Nakuambia hutakaa uondoke kwenye nyumba hii labda uwe marehemu."

"Unataka nini toka kwangu?" Lisa aliogopa hata kumwona.

"Utaelewa tu." Alvin alimtupa begani na kwenda kumfungia kwenye chumba cha upweke.

"Alvin, huwezi kufanya hivi." Mara moja Lisa alitambua nia yake na haraka akakimbia nje, akipanga kutoroka. Hata hivyo, Alvin hakumpa nafasi hiyo. Badala yake, alifunga mlango kwa nguvu na kuufunga kwa nje.

“Alvin, nakuchukia. Nimekukosea nini? Familia yako ya Kimaro ilinitenga kwenye jela yao, na sasa unafanya vivyo hivyo. Wewe ni shetani!” Lisa alipiga ngumi kwenye mlango.

“Wewe ni Ibilisi… Ibilisi…”

Sura ya: 243

Maneno hayo ya chuki yalijirudia katika ubongo wa Alvin. Mara akaziba masikio yake kwa mikono ili asisikie. Hakutaka kusikia mwanamke aliyempenda akimwita majina hayo. Alijijua ni mgonjwa, na hakutaka kumwumiza Lisa.

Akiwa amechanganyikiwa na hali hiyo, Aunty Yasmine alinyanyuka na kushika mikono yake. “Bwana Mkubwa, huwezi kumtendea hivi Bi. Mdogo. Hakusema maneno hayo kwa makusudi. Ni kwa sababu tu ana wivu kukuona ukiwa karibu na Maurine…”

Hata hivyo, Alvin alikuwa kama mwendawazimu kwa wakati huo. Sio tu kwamba hakumsikiliza, lakini hata alimsukuma Aunty Yasmine kwa nguvu. Mwanamke yule aligonga kichwa chake chini na kuzimia.

Maurine haraka akaanza kumpepea. Aunty Yasmine alilala kimya akiwa amepoteza fahamu. Sebule ilikuwa kimya ghafla. Kelele pekee zilikuwa za Lisa akiomba msaada kutoka kwenye chumba cha upweke.

Maurine alitabasamu kwa kejeli huku macho yake yakidhihirisha chuki kali, akajiwazia. ‘Lisa Jones, bila shaka hukutegemea hili kutokea’

Ndani ya chumba cha upweke, Lisa alipiga kelele hadi sauti yake ikakauka, lakini hakuna mtu aliyekuja kumsaidia. Kwa bahati nzuri, ingawa chumba hakikuwa na madirisha, kilikuwa na taa, kitanda na hali ya usafi.
Alikuwa amechoka baada ya siku ndefu. Hakutarajia kujikuta akiwa hana umuhimu kwa Alvin. Alijisikia vibaya kuona kuwa mtu aliyekufa alikuwa na nguvu sana moyoni mwake kuliko yeye aliye hai.

Hakika alipoteza ujasiri wake wote wa kumpigania mwanaume huyo. Labda hakuna kitu kizuri alichothamini ndani yake hata baada ya mateso yote aliyopata kwa ajili yake. Alilala na kupitiwa na usingizi mzito.

Kulipokucha, Lisa hakuwa tayari kuendelea kufungiwa kwenye chumba hicho cha upweke. Kwa wakati huo, alichotaka ni kutoroka humo ndani. Alipoenda kujaribu kufungua mlango muda fulani baadaye, alishangaa kuona ukifunguka bila tatizo.

Hilo lilimshangaza. Alitoka sebuleni kwa tahadhari na kugundua kuwa tayari ilikuwa ni saa tatu asubuhi. Sebule ilikuwa kimya sana. Mwanzoni, alitaka kuondoka mara moja. Hata hivyo, alikuwa na wasiwasi kwamba huenda kuna kitu kilimtokea Alvin baada ya kukumbuka hali yake ya hasira jana yake usiku. Mwishowe, aliamua kunyata kuelekea chumbani.

Alisukuma mlango uliokuwa umefunguka kidogo na kumuona Alvin akiwa amejilaza kitandani bila nguo yoyote. Maurine, ambaye alikuwa amevaa nguo nyepesi ya kulalia, alikuwa ameketi juu yake, akimpa massage ya upole mgongoni.

"Bwana Kimaro, unajisikiaje?" Sauti ya Maurine ya kubembeleza ilijaa chumbani.

Lisa alihisi kuumwa kwa kuona hivyo. Aliondoka mahali hapo bila kuangalia nyuma. Alikuwa mjinga kiasi gani kuhangaikia hali yake baada ya kumfungia kwenye chumba cha upweke usiku kucha wakati yeye alikuwa kazama katika faraja ya Maurine?

Alipowawazia wawili hao wakifanya jambo la faragha kama lile kitandani mwake, Lisa alihisi kichefuchefu. Aliamua kuachana na mtu huyo kwa muda usiojulikana.

Pamoja na hayo, kuna kitu hakujua. Baada ya kuondoka, Maurine alitoka kwenye mwili wa Alvin na kumtazama mwanaume huyo. Bado alikuwa amepoteza fahamu. Alivaa na kumpigia Rodney simu.

Takriban nusu saa baadaye, Rodney na Chester walifika wakiwa na wasiwasi mwingi. Maurine aliwaambia marafiki hao wa Alvin waliokuwa na wasiwasi mwingi. “Nilirudi jana usiku baada ya kupigiwa simu na Aunty Yasmine. Nilimpatia dawa na hatimaye akatulia. Lisa aliporudi nyumbani alinipiga bila hata ya kunisikiliza. Alvin aliamka katikati ya ghasia na kuanza kufokeana naye.”

“Alvin alipoteza udhibiti wa hasira zake baada ya hapo, na Lisa akasema angeondoka. Alimfungia ndani ya chumba peke yake na kumjeruhi kwa bahati mbaya Aunty Yasmine. Niliita gari la wagonjwa usiku huohuo ili kumpeleka Aunty Yasmine hospitali. Sasa, sijui nini kingine cha kufanya,” Maurine alisema kwa maelezo marefu.

Alama ya kofi la Lisa kwenye shavu lake bado ilikuwa ikionekana na alikuwa amevimba. Rodney alipiga ukuta kwa ngumi aliposikia hivyo. “Lisa anaumwa kabisa. Nitamfundisha somo…”

“Tulia.” Chester alimshika rafiki yake mkono.

“Angalia alichomfanyia Alvin. Anajua kwamba akili yake haijatulia, lakini bado anamkasirisha kimakusudi. Nadhani anajaribu kumfanya apoteze akili ili aweze kurithi utajiri wake.”

Maurine alisema kwa unyonge, “Nilifungua mlango wa chumba alichofungiwa kwa siri asubuhi ya leo ili kumruhusu atoke. Nafikiri… Si wazo zuri kumfungia mtu hivyo. Unafikiri nini kitatokea ikiwa Alvin ataamka na kumkuta hayupo?”

Chester alimpongeza, “Umefanya jambo sahihi. Alvin amekosea sana kumfungia.”

“Lakini ninahofia atakasirika akimkuta Lisa ameondoka…” Mwonekano wa wasiwasi ukauwasha uso wake.

“Tutamwambia kwamba sisi ndio tuliomwacha aende zake,” Chester alimtoa wasiwasi.

"Asante."

Muda si mrefu Alvin alizinduka. Alishika kichwa chake kwa mikono yote miwili ili kupunguza maumivu ya kichwa.

“Unajisikia vizuri?” Rodney aliuliza kwa umakini.

Alvin aliinua kichwa chake kuwatazama kwa kukunja uso. “Mbona wote mko hapa? Lisa yuko wapi? Alirudi nyumbani jana usiku?"

Wote wakamtazama kwa mshangao. Rodney na Chester wakatazamana. Sekunde chache baadaye, Chester aliuliza, “Alvin, hukumbuki kilichotokea jana usiku?”

"Nini kimetokea? Si nimelala usiku kucha?” Alisikika kama kachanganyikiwa. “Niligombana naye juzi na jana nikasubiri hadi usiku sana bila kumuona. Niliingia kitandani nikiwa nimechanganyikiwa na kwa namna fulani nililala tu.”

Rodney alishtuka kweli. Chester alimpiga bega rafiki yake. “Kusema ukweli, uligombana na Lisa tena usiku wa juzi na akaondoka kwenye nyumba hii. Kwa bahati nzuri, Shangazi Yasmine alimpigia simu Maurine jana usiku. Jana tena Lisa alirudi usiku mkagombana tena. Ulimuumiza Aunty Yasmine katika harakati hizo, akapelekwa hospitali…”

Uso wa Alvin ukabadilika mara moja. "Hiyo haiwezekani. Sikumbuki lolote kati ya hayo.”

"Inaonekana hali yako imekuwa mbaya zaidi kuliko tulivyotarajia. Unaonyesha hata dalili za kuweweseka na kupata maluweluwe. Hali yako ni tata sana.” Chester akakunja uso ake.

Alvin alikunja ngumi kwenye blanketi. "Hapana. Nimekuwa nikijisikia vizuri zaidi hivi karibuni.”

“Lazima ni kwa sababu Maurine anakuhudumia vizuri.” Rodney alisema kisha akaongeza kwa hasira, “lakini Lisa anaendelea kukuchokoza. Nadhani ni bora ukiacha kuonana naye kwa wakati huu. Acha Maurine aendelee kukutunza. Ni kwa manufaa yako mwenyewe.”

“Nakubaliana na Rodney wakati huu. Ni bora ukijiweka mbali na Lisa. Nina hakika hutaki kumdhuru, sivyo?” Chester alisita. “Hivi majuzi nilisikia kuhusu huyu mtaalamu wa saikolojia, Nyasia kutoka nje ya nchi. Inavyoonekana, anaweza kuponya mgonjwa yeyote. Lakini yeye ni mtu mwenye kazi nyingi, kwa hivyo inachukua muda mwingi na bidii kuwasiliana naye.”

"Wasiliana na mtu huyu kwa njia yoyote ile." Alvin alihimiza.

Ingawa Lisa alikuwa amemwacha kwa usiku mmoja tu, hakuweza kuzuia msukumo wa kwenda kumtafuta. Hata hivyo, alihitaji kujizuia ili asimdhuru tena.
•••
Lisa alikaa hotelini baada ya kuondoka kwa Alvin. Siku iliyofuata, alishirikiana na Pamela kutafuta nyumba. Wakati huo, alikuwa ameamua kununua nyumba ili awe na mahali pake mwenyewe huko Nairobi.

“Hivi kweli haurudi nyuma? Usibadili mawazo yako tena Alvin atakapokuja kukutafuta siku chache zijazo.” Pamela hakuweza kujizuia kumtania rafiki yake.

“Wawili hao walikuwa wamelala kwenye kitanda changu. Unafikiri bado ninaweza kurudi huko?" Lisa alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa umechomwa kisu alipokumbuka tukio lile. "Akili na mwili wangu havitaki kabisa kumsikia Maurine. Uhusiano wetu ulikuwa umeanza kuimarika lakini baada ya kuja Maurine kila kitu kimesambaratika tena.”

“Uko sahihi. Inachukiza sana. Kwa kuwa hawezi kumsahau Sarah Njau, kaamua kukaa na binamu yake ili ajisikie vizuri. Kwanini bado anataka kukuweka karibu?” Pamela akamshika mkono. “Twende tukanunue nyumba. Ninajua mahali pazuri."

Sura ya: 244

Nairobi Square Garden, ni eneo linalojumuisha mabangalow na majengo ya kifahari, ni eneo lililo nje kidogo ya jiji la Nairobi. Pia kuna na malls, viituo vya michezo, na maeneo mengine muhimu.

Muuzaji aliwazungusha Lisa na Pamela kwenye ziara mchana mzima. Waliporudi kwenye kitengo cha mauzo, meneja alishtuka baada ya kumtambua Lisa, na mara moja akamjulisha bosi wake. Bosi akampigia simu Hans haraka na kumfikishia Alvin ujumbe ule. "Bwana Kimaro, Bi Jones anatazamia kununua nyumba."

Alvin aliyekuwa akisoma nyaraka za kazi ofisini kwake alikunja uso. “Anajaribu kumaanisha nini? Kwamba hana mpango wa kurudi nyumbani tena?”

Hans alijua anapaswa kumfariji Alvin badala ya kumpanikisha zaidi.
“Labda… Anataka kufanya uwekezaji? Wanawake wengi matajiri wanafanya vivyo hivyo siku hizi.”

Alvin akalegeza uso wake uliokuwa umekakamaa kwa hasira. Baada ya kufikiria kwa ufupi, alisema, “Kwa vile mke wangu anapanga kununua nyumba, waambie wampe punguzo bora zaidi. Hmm, punguzo la 90%.”

Hans alitetemeka hadi moyoni. "Lakini Bwana Kimaro, Bibi mdogo bila shaka atakuwa na shaka ikiwa utafanya hivyo. Anaweza hata kubadili mawazo yake kuhusu kuinunua.”

Alvin alimtupia jicho la kuudhi. "Basi 70%. Hawawezi kwenda chini zaidi ya hii."

“Um… sawa.” Hans alikosa la kusema. Hii ilikuwa mara yake ya kwanza kuona bosi wake akijaribu kumpa mteja punguzo zaidi ya inavyopaswa.

Lisa na Pamela waliridhika sana baada ya ziara hiyo. Kitu pekee kilichomchelewesha ni bei kwa sababu ilikuwa nje kidogo ya bajeti yake. Jumba la bei rahisi zaidi pale lingegharimu angalau mamia ya mamilioni ya shilingi.

“Tafadhali nifanyie bei nzuri zaidi. Nitahitaji siku chache kufikiria hili,” Lisa alisema mwishoni.

"Hakika, ngoja nicheki na bosi wangu." Muuzaji huyo alipotea kwa dakika tano kabla ya kutokea tena kwa furaha. "Bi Jones, habari njema! Utakuwa mteja wetu wa 1000 ukiweka amana leo. Bosi wetu amesema nyumba yoyote utakayochagua utapewa punguzo la 50%, na unaweza hata kupata nafasi ya kujiunga na droo yetu maalum ya bahati nasibu. Baadhi ya zawadi hizo ni pamoja na punguzo zaidi la bei, jokofu na vifaa vya nyumbani bila malipo, zawadi za kifahari zenye thamani ya dola laki moja, na kadhalika.”

Lisa alizidiwa na taarifa hizo za ghafla. Pamela alipiga kelele kutokana na msisimko. “Umeshinda bahati nasibu! Haraka na ulipienyumba sasa. Hakuna haja ya kuchelewa zaidi."

"Hiyo ni sawa. Ni mteja wetu wa 1000 pekee ndiye anayeweza kupata bahati kama hii. Inastahili pesa hizo hata ukinunua nyumba na kuisahau
baadaye,” muuzaji alikariri kwa kutia chumvi.

Mwishowe, Lisa alilipa pesa na kujaribu bahati yake kwenye droo. Muuzaji aliitazama na kuziba mdomo huku akipiga kelele kwa sauti. “Mungu wangu, wewe ndiye mtu mwenye bahati zaidi duniani! Umejishindia zawadi ya punguzo zaidi. Unapata punguzo zaidi la 20% juu ya 50% ya hapo awali. Kwa maneno mengine, utapata punguzo la 70%! Unaweza kuwa na nyumba ya kifahari iliyokarabatiwa kikamilifu ambayo kwa kawaida inagharimu dola milioni mbili kwa bei ya dola laki moja na nusu tu! Inashangaza!”

Lisa hakuwa na neno. Alihisi kana kwamba uchawi wa bahati ulikuwa umetupwa juu yake. Je, hatma yake ingebadilika na kuwa bora baada ya kuachana na Alvin? Alitoka nje ya kitengo cha mauzo akiwa ameduwaa.

Pamela alikuwa na mawazo tofauti na yeye. "Sidhani kama hii ni bahati tu. Haudhani inawezekana kwamba mkono wa Alvin unafanya kazi kwa siri?”

“Hapana, kwanini aniwazie mimi? Pengine anafurahia wakati wake na Maurine muda huu. Kitu pekee anachofikiria juu yangu labda ni kunifungia tena." Lisa alipuuzia kabisa mawazo ya Pamela.

“Uko sahihi. Labda hata Mungu alikuhurumia. Hebu turudi hotelini na tupakie vitu vyetu. Tunatakiwa kwenda kwenye baa usiku wa leo kusherehekea bahati yako!”

Pamela alizungusha mkono wake mabegani mwa Lisa.

Lisa hakukataa. Baada ya yote, ilikuwa imepita muda mrefu tangu aende baa pamoja na Pamela.

Saa tatu usiku wawili hao waliingia ndani ya baa pamoja. Lisa hakuwa katika mazingira kama hayo kwa muda mrefu sana. Kuwa baa kulimkumbusha maisha rahisi na ya kujiachia kabla ya kuolewa.

Hata hivyo, muda si mrefu baada ya kuanza kunywa pombe, walifikiwa na jamaa mmoja aliyevalia shati la maua. "Pamela, ni bahati njema kama nini tunakutana tena." Mwanaume huyo aliubembeleza uso wa Pamela kwa tabasamu la kejeli.

Uso wa Pamela ulizama mara moja na kuusukuma mkono wake mbali. “Thomas Njau, nimekwambia wazi kuwa sina shida na wewe. Peleka sura yako mbali na mimi.”

Lisa alishtuka kusikia mtu huyo alikuwa kaka mkubwa wa Sarah Langa.

“Usiseme hivyo. Nipe nafasi hata mara moja. Huenda usiweze kujizuia mara tu utakapoona jinsi nilivyo mtamu kitandani.” Aliendelea kumsumbua huku akiwa na tabasamu baya usoni mwake. "Ni heshima kwako kuwa mwanamke wangu. Mimi ni handsome, kwa kawaida wanawake huwa wananipapatikia..."

"Thomas, nitampigia dada yako au polisi ikiwa utaendelea na kutusumbua." Lisa alijiweka mbele ya Pamela.

“Kaa kushoto na sura yako mbaya wewe. Unafikiri wewe ni nani?” Alimtazama kwa sekunde kadhaa kabla ya kucheka ghafla. “Oh, wewe ni mke wa Alvin. Si ajabu unakuwa na kiburi sana.”

Lisa alikunja uso, lakini Pamela aliinua kichwa chake mbele kutoka nyuma. "Hiyo ni sawa. Lisa ni mke wa Bwana Kimaro, na mimi ni rafiki yake mkubwa. Kuninyanyasa ni sawa na kumnyanyasa.”

Thomas alicheka kwa sauti baada ya kusikia hivyo. “Ningeogopa ikiwa Alvin angekuwa hapa, lakini huyu ni mke wake tu. Kusema kweli, hata kama ningelala na mke wake usiku wa leo, kikubwa atakachonifanyia ni kunipiga ngumi za usoni tu. Unaniamini?"

Lisa alihisi moyo wake kuzama kwa kuona sura yake ya kiburi, lakini, ilimbidi akubali kwamba labda alikuwa sahihi. Mtu huyu alikuwa kaka wa damu wa Sarah Langa. Alvin asingemfanya lolote hata angeangamiza dunia nzima.

Thomas alimpandisha juu na chini kama anamfanyia tathmini fulani. “Tsk, wewe ni mbaya sana na hakuna kitu ukilinganisha na dada yangu. Usingeolewa na Alvin kama si kwa bahati ya kifo.”

“Ondoka!” Pamela hakuweza kuvumilia kwa muda mrefu zaidi, mikono yake iligonga meza kwa hasira. “Sijali mdogo wako ni nani, lakini kwa kaka kama wewe, nahisi atakuwa ni takataka tu kulinganisha na Lisa wangu.”

“Wewe mwanamke mjinga. Nisipokupelekea moto usiku wa leo, labda mimi siyo Tom!” Kwa uso uliopinda, Thomas alinyoosha mikono yake kushika mabega ya Pamela.

Mara mkono mzuri uliibuka ghafla kana kwamba umetoka hewani na kumshika mkono Thomas.

“Nani tena…” Alitazama juu ya mabega yake na kuganda mara moja alipoona sura ya Charity iliyofura kwa hasira.

"Nakumbuka nilikuambia uache kumsumbua Pamela." Charity alimtazama bila kujali.

Donge la chuki likaangaza ghafla machoni pake lakini likatoweka haraka kama lilivyoibuka. "Charity, unadhani wewe ni nani wa kuingilia mambo yangu?"

"Kwa hivyo nikuruhusu uendelee kufanya fujo na kuleta aibu kwa familia?" Charity alimminya zaidi kwenye kifundo cha mkono wake.

“Lo… Inauma!” Thomas aliinama na kukunja uso kwa uchungu lakini hakuweza kujinasua kutoka kwenye mkono wa Charity hata baada ya kufurukuta sana. “Niache niende, Charity. Wewe si lolotei. Familia ya Njau inasambaratika kwa sababu umemkosea Bwana Kimaro. Yote ni makosa yako!”

Charity akakunja uso. Thomas alitabasamu kwa hasira baada ya kuona hivyo. “Ngoja nikupe neno la ushauri. Alvin atakusamehe tu mara tu utakapoikabidhi New Era Advertisings kwangu. Au ungependa kuona kampuni hiyo ikikufia mikononi mwako?

Sura ya: 245

“Nyamaza. New Era Advertisings ingekufa siku moja tu chini ya uongozi wako.” Charity alimshika Thomas bega na kumpindua juu. Thomas alianguka chini bila huruma machoni pa watu.

Wote Lisa na Pamela walipigwa na butwaa. Hata hivyo, Pamela alikuwa wa kwanza kuvunja ukimya kwa kupiga makofi kwa sauti kubwa. "Wewe ni mzuri sana, Charity!"

Thomas alikasirika kwa kukosewa heshima na kuaibishwa mbele ya umati. "Charity, sitaacha hili lipite hivihivi, nakuapia." Kisha, akasimama na kutoka nje ya baa.

"Asante." Lisa alimimina glasi mbili za wine nyekundu na kumkabidhi Charity moja. Alikuwa na hisia nzuri tangu mwanzo na mwanamke huyo. Usiku huo, alimvutia sana.

“Usijali. Nilikuwa napita tu. Mmiliki wa baa aliniambia Thomas alikuwa akiwanyanyasa wanawake tena, kwa hivyo nilikuja kutazama." Charity akanywa mvinyo.

"Asante, dada!" Pamela akampa dole gumba. "Hakika ningekupa wewe kama ungekuwa mwanaume."

“Si vyema kwa wanawake kuwa dhaifu kiasi hicho," Charity alitania na kucheka. "Mimi ndiye ninayepaswa kuwaombeni msamaha ..."

"Yeye sio ndugu yako wa tumbo moja, kwa hivyo usijisumbue sana." Lisa alikokota kiti kutoka kwenye meza iliyofuata. “Unataka kujiunga nasi?”

Charity alikunja uso na kusita kwa muda. "Ningependa, lakini sisi si wa ulimwengu mmoja. Ikiwa Alvin atajua kuhusu hili…”

“Nimetengana naye,” Lisa alimkatiza. "Nimehama kutoka kwake. Sitaki kuwa mjinga tena.”

Uamuzi wa Lisa ulimshangaza Charity. “Unaweza kumwacha Alvin kweli?”

"Hasara kidogo ni bora kuliko majuto ya milele." Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Kwa kweli, nimejua kuhusu Sarah zamani sana. Nilidhani haina tatizo kwa sababu Sarah ni marehemu kwa sasa. Lakini, Alvin ameamua kutafuta mbadala wake kwa kumleta Maurine, ni kama vile anaishi na mzimu wa Sarah. Mimi sioni umuhimu wa kushindana na mbadala wake.”

“Hiyo ni sawa. Kuna samaki wengi baharini,” Pamela alikubali. “Alvin ni tajiri, lakini ili iweje? Wewe mwenyewe una pesa zako pia."

“Inatosha.” Macho ya Charity yalimetameta kwa uzuri. "Ikiwa ni hivyo, tunapaswa kuwa na furaha usiku wa leo."

Wanawake hao watatu walikuwa na umri sawa, na juu ya ushawishi wa pombe, maongezi yalienda vizuri sana. Baada ya kunywa kwa muda, watatu hao walianza kucheza kwenye jukwaa. Lisa hakuwahi kujisikia huru zaidi ya alivyokuwa muda huo. Maisha yake yalikuwa yakimzunguka Alvin kwa muda mrefu. Kwa kweli, aliishi siku zake kwa mafadhaiko na bila uhuru. Sasa, hata akapata rafiki mpya. Labda huu ulikuwa mwanzo wa kitu kizuri.

Baa hiyo ilitembelewa tu na watu matajiri na mashuhuri zaidi. Mmoja wao kati ya umati wa watu alikuwa mwimbaji mwenye wafuasi wengi sana. Alitupia klipu ya video kwenye chaneli yake ya Youtube akichezana kila Lisa.

Maoni mengi kutoka kwa wafuasi wake yalitiririka.

[Nikicheza kwenye baa baada ya kugongana na malaika watatu kutoka mbinguni. Tonight's really worth it.]

[Wasichana ni warembo sana. Mmoja anaonekana kama mtoto mchanga wa rangi mchanganyiko, na mwingine ana sifa za urembo wa kawaida. Ni aibu kwamba aliyesimama katikati ana kovu usoni, lakini umbo lake ni la kushangaza.]

[Wow, ni mimi tu, au aliye katikati anafanana na mke wa Alvin Kimaro?]


[Lazima awe yeye.]


Baadaye, hashtag #Kimaro’sWifelnPub ilisambaa kwa kasi mtandaoni. Video hiyo hata ilipata kutazamwa mara nyingi chini ya nusu saa.

Alvin alikuwa ametoka kuoga wakati Maurine alipomwendea akiwa na glasi ya maziwa. "Bwana Kimaro, ngoja nikuchane nywele zako."

Alijaribu kunyoosha mkono lakini Alvin alikwepa haraka. "Hakuna haja ya hilo." Alikunywa glasi ya maziwa na kusema kwa upole, “Shuka chini. nitakuita nikikuhitaji.”

“Lakini…” Hakuweza kuficha wasiwasi machoni mwake. “Hupaswi kuachwa peke yako katika hali hii. Ninaweza kuweka kitanda changu pembeni…”

“Hapana.” Alikunja uso kabla ya kusema, “Hiki ndicho chumba ninacholala na mke wangu. Sipendi wanawake wengine kukaa hapa.”

“Samahani. Sikuwa nimefikiria kuhusu hilo.” Maurine akatingisha kichwa. Baada ya kutoka chumbani, aliuma midomo kwa kuudhika.

Alvin hakuvutiwa naye licha ya sura yake kuwa sawa na ya Sarah Langa Njau. Ni vile tu alitaka kutumia taswira ya Sarah ili aweze kupona ugonjwa wake. Hata hivyo, haikujalisha. Alikuwa katikati ya lengo lake hata hivyo.

Alvin alitabasamu huku akitazama glasi ya maziwa. Baada ya Maurine kuondoka, Alvin alirudi kitandani kuangalia WhatsApp. Hakukuwa na ujumbe wala taarifa mpya kutoka kwa Lisa au mitandao yake ya kijamii.

Mwanamke msumbufu huyu. Je, kweli alilamua kuondoka nyumbani na kumpuuza kwa sababu tu ya ugomvi mdogo? Alikuwa ameahidi kutumia maisha yake yote pamoja naye, lakini sasa, alimwacha peke yake nyumbani. Angewezaje? Alihisi uzito wa ghafla katika kifua chake.

Ili kujizuia kuangazia hilo, alifungua kurasa zake za mitandao ya kijamii. Uso wake mzuri ulianguka baada ya kuona hashtag hiyo maarufu, #Kimaro’sMastersWifelnPub. Kisha akabofya play kwenye klipu iliyokuwa ikivuma sana.

Ndani ya baa hiyo ya kupendeza, Lisa aliwekwa kati ya Pamela na Charity huku wakisakata dansi la kufa mtu jukwaani. Alikuwa amefunga shati lake kiunoni, akifunua kiuno chake kidogo na kitufe cha tumbo. Alionekana kama video-vixen mdogo.

Alvin alikuwa amekasirika sana hata akakaribia kumwaga damu. Lisa angeacha lini kufanya mambo kama hayo? Ilikuwa imepita siku moja tu tangu aondoke, kisha akaibuka akiwa anacheza dansi kwenye baa.
Ndo maana aliamua kumfungia ndani ya chumba cha upweke ili asitoke nje na kufanya mambo ya ajabu. Mapigo ya moyo wake yaliongezeka ndani ya sekunde chache.

Ghafla, simu yake iliita na kuiona namba ilitoka kwa Thomas Langa Njau. “Bwana Kimaro, lazima unisaidie. Dharau zake zimevuka mipaka safari hii. Alinipiga hadharani na kuniaibisha sana.”

Alvin alihisi kukereka, lakini alizuia hisia zake haraka. “Hilo lilitokea wapi?”

"Kwenye baa," Thomas alifoka. “Hata sikumfanya chochote, nilimkuta na mkeo wakimsengenya Sarah kuwa ni tapeli. Sikuweza kuvumilia zaidi kuhusu hilo, kwa hiyo nikaanza kubishana naye. Hapo ndipo aliponipiga.”

Alvin alikodoa macho. Charity kwa hakika alikuwa akitamani kifo chake. Kisha, Thomas akasema kwa sauti ya chini, “Kuna jambo lingine… sina uhakika kama niseme hivi, lakini Charity anamharibu mke wako. Yuko pamoja naye wanakunywa pombe usiku wa leo. Kweli, kwa kile ninachoweza kusema, Charity alikuwa akijaribu…”

“Inatosha. Niaifahamu vyema hiyo baa. Nitakuwepo hapo mara moja.”
Alvin akacheka kwa kujidharau. Hakutarajia kwamba Charity angejaribu kujenga urafiki na Lisa baada ya kushindwa kumsamehe. Hata hivyo, asingemsamehe kwa kumtumia mke wake kufikia malengo yake.

Alvin aliagiza helkopta imfuate haraka. Mara baada ya kubadilisha nguo, alishuka ngazi.

“Bwana Mkubwa, unaenda wapi?” Maurine alimuuliza.

“Nje.” Alitoka nje na kusubiri kwa dakika kadhaa kabla ya kusikia muunguro mzito wa helkopta angani. Helkopta ikatua kwenye uwanja mkubwa.

Alipoingia kwenye helkopta, aligundua kuwa Maurine alikuwa amejwahi kupanda kabla yake. Akaamuru kwa kukunja uso, “Teremka!”

“Hapana. Ni lazima niende nawe kutokana na hali yako kutokuwa shwari.” Maurine alitabasamu kwa uchungu. "Nina hakika unaweza kushindwa kujidhibiti."

TUKUTANE KURASA 246-250

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.........LISA
KIRASA......246-250

Sura ya: 246

Alvin alinyamaza na kuamuru chopa kuondoka. Walifika kwenye baa upesi sana. Thomas ambaye alikuwa amekaa nje ya baa hiyo kwa muda mrefu, mara moja akasogea huku akiwa ameshika kiuno chake kilichojeruhiwa.

Kutokana na muziki mnene ulioziba masikio, Lisa hata hakuweza kusikia muungurumo wa helkopta. Hazikupita sekunde yeye na wenzake walijikongoja kutoka kwenye baa huku wakiwa wamekumbatiana mabega Kwa kuangalia midomo yao iliyokuwa ikipepesuka, ilidhihirisha walikuwa wamekunywa pombe nyingi.

“Bado sijatosheka, tuendeleeni kunywa, naweza kumaliza kreti zima peke yangu.” Pamela aliinua mikono yake juu hewani. "Sitarudi nyumbani hadi nilewe."

"Wacha tule nyama kwanza." Charity alikuwa amefurahi sana.

Lisa alishauri, "Tunaweza kwenda kuendelea kunywa katika nyumba yangu ya kifahari hadi alfajiri."

"Kweli! Sisi ni utatu mtakatifu, wote ni ma-single dadaz. Wanaume ni sh*t! Waache waende zao!" Charity akakubali kwa furaha.

"Sh*t! Wanaume ni nyoko!" Pamela akakandamizia kwa hasira.

Uso wa Alvin ulijawa na mawingu, Lisa hata alimdhihaki mbele ya marafiki zake? Akasogea kumvuta Lisa mikononi mwake. "Twende nyumbani haraka."

Hapo awali alikuwa ameridhika akae nje kwa muda kwa kuhofia kwamba angemdhuru, lakini ilionekana wazi kuwa asingeweza kufanya hivyo.

“Wewe ni nani na unafikiri unafanya nini?” Lisa aliinua kichwa chake akiwa ameduwaa. Baada ya kuutazama vizuri uso wake, lile tukio la Maurine akiwa amemlalia akimfanyia masaji lilimjia kichwani. Ghafla alihisi kichefuchefu na kumtapikia Alvin nguo zake zote na chini.

"Lisa Jones!" Alvin aliita jina lake herufi kwa herufi. Alitamani angemchuna ngozi akiwa hai hapohapo.

"Bwana Kimaro." Maurine alikimbia kwenda kumfuta uchafu ule mwilini
Mwake.

Baada ya kuona hivyo Pamela alikimbia mbele mara moja na kumpiga Maurine kichwani na mkoba wake. “Wewe b*tch, kwanini usitafute mwanaume wako? Umepanga kuharibu ndoa ya Lisa?”

Maurine aliugulia maumivu, Lisa alifurahi sana kuona hivyo, akasogea mbele akijifanya kumsaidia. “Pamela, usifanye hivi…”

Licha ya maneno yake hayo ya upole, Lisa alinyoosha mguu na kumpakaza Maurine kwenye matapishi yaliyokuwa chini, akasogea mbele kumkanyaga mara kadhaa. Maurine alilia kwa maumivu makali huku akishika pindo la suruali ya Alvin. “Bwana Mkubwa, nisaidie…”

“Inatosha.” Alvin alimsaidia Maurine kusimama kabla hajawatizama wale wanawake wawili, “Pamela kweli hujaelimika, Lisa, jiangalie vizuri ulevi wako, nilikuambia ujiepushe na Charity, umekaidi na kuamua kunywa pamoja naye. Kwanini husikii?”

Lisa alipapasa masikio yake na kujibu kwa dharau, “Unasema upuuzi gani, sikuelewi.”

Pamela alicheka. "Lisa, si unajua? Sisi hatujaelimika kuliko wao, kwa hivyo hatuwezi kuwa sawa nao."

“Uko sawa.” Lisa alikubali, “Twende.”

Alvin alikasirishwa kwa kupuuzwa na yule mwanamke, “Simama hapo hapo wewe ni mke wangu, nakuagiza twende nyumbani sasa hivi. Alvin alishika mkono wake tena, lakini wakati huu, nia ya hatari iliangaza macho yake yenye huzuni. “Usinifanye nipitilize kikomo cha uvumilivu wangu.”

“Kikomo? Una kikomo gani?" Lisa alicheka baada ya kumuona Thomas akiwa amesimama nyuma ya Alvin. “Kwa nini umemleta hapa? Ili kumtetea tena?”

Mara Thomas aliugulia maumivu. “Bi. Kimaro, kwa kweli unapaswa kukaa mbali na Charity. Ana kusudi la kufanya urafiki na wewe kwa nia mbaya."

“Thomas, ninajuta sana kwamba sikukupiga vya kutosha muda ule.” Charity akayafumba macho yake mazuri.

Thomas aliogopa sana na mara moja akajificha nyuma ya Alvin. “Bwana Mkubwa, tazama jinsi anavyo nitisha mbele yako.”

"Charity, inaonekana nimekuwa mkarimu sana kwako." Uso wa Alvin ulikuwa umekunjamana kwa hasira. “Nakuonya sasa ukae mbali na mke wangu. Vinginevyo, utasahau kama uliwahi kuwa mkurugenzi wa New Era Advertisings.”

Uso mzuri wa Charity ulibadilika na kupoa ghafla kama maji mtungini. Hata hivyo, Lisa alimshika mkono na kumtazama Alvin akiwa ameinamisha kichwa. “Hahitaji kufanya urafiki nami. Kuanzia sasa na kuendelea, mimi ndiye nitakayefanya urafiki naye. Yeye ndiye rafiki wa kwanza mzuri ambaye nimempata hapa Nairobi.”

Alvin alikasirika sana. “Lisa, ngoja nikukumbushe tena kuwa huyu mwanamke ni mjanja mjanja na mlaghai, lakini bado unataka kuwa rafiki yake. Wewe ni mjinga sana kutokuona hivyo?"

"Ndio, mimi ni mjinga sana ndo maana nilikupenda." Lisa alicheka kwa kebehi. “Huwezi kujua ni nani mjanja na nani mjinga? Charity hakunidanganya. Kinyume chake wewe na marafiki zako ndiyo mnanidanganya. Najua kwamba mume wangu ameweka mwanamke ambaye anaonekana kama mpenzi wake wa zamani karibu naye ili ajisikie vizuri. Je, huu ndio upendo unaoendelea kuuzungumzia? Unachukiza.”

Akiwa amepigwa na butwaa, mchanganyiko wa mshangao na aibu ukatanda usoni mwa Alvin. Hata hivyo, ilipita kwa sekunde chache tu kabla hajamkodolea macho Charity. “Ulimwambia kuhusu hili?”

Charity alikosa la kusema, mara Lisa akajiweka mbele yake kumtetea. “Angethubutu vipi kuniambia wakati unamtishia kuiangusha New Era Advertings? Uhusiano wako na Sarah ulikuwa maarufu sana hivi kwamba kila mtu hapa Nairobi anajua. Isitoshe, huenda sikuwahi kukuambia, lakini huwa unaliita jina la Sara usingizini. Hata jina la Alvinarah mchanganyiko wa maneno ya jina lako na lake. Nilijua hilo zamani. Oh, nini kingine? Ulijenga bustani ya kushangaza ili kumchumbia. Fataki bado hulipuka kila saa 8:3o usiku kama tamko la upendo wako. Mpaka hapo, mimi ninani ukilinganisha na Sarah?”

"Ni kweli. Lakini yote hayo yamepita…” Alvin hakujua la kufanya.”Huwezi kumwonea wivu mtu aliyekufa.”

Hakujua kamwe kuwa aliita jina la Sarah katika ndoto zake. Kwanini hakuweza kukumbuka lolote kati ya hayo? Alinyoosha mkono kuushika mkono wa Lisa, lakini aliutupa kwa ukali. Lisa alimtazama kwa mchanganyiko wa chuki, kukatishwa tamaa, na hasira.

"Hata mimi nilijua yamepita pia, lakini uamuzi wako wa kumweka Maurine karibu nawe unaniambia kuwa sitakuwa bora zaidi ya kumbukumbu ya mzimu, au hata kumkaribia tu." Lisa alimnyooshea Maurine kidole kinachotetemeka. “Ni mambo mangapi ya kuchukiza umefanya naye kitandani kwangu nikiwa sipo kila siku? Je, hakuna chumba kingine ndani ya nyumba? Toka Maurine aingine ndani kwetu hata hisia zangu huzijali tena. Kila anachokuambia unafuata tu.”

"Bi. Kimaro, unazungumza nini?" Akiwa na huzuni, Maurine alisema, “Wewe pekee ndiye Alvin anakujali.”

"Nyamaza! Hakuna mtu anayeweza kujifanya zaidi yako. Uliwadanganya wanaume wote na kufanya kila kitu kionekane kama ni kosa langu.” Lisa akashusha pumzi ndefu. “Lakini haijalishi. Unaweza kuwa na Alvin ukitaka kwa sababu mimi sijali tena.”

"Ikiwa hunijali, basi unamjali nani?" Alvin alimkandamiza mabega. Mwili wake ulimuuma kana kwamba anakosa hewa. “Sijafanya chochote na Maurine. Ninamweka karibu tu… kwa sababu… kwa sababu yeye ni binamu ya Sarah, na nilifikiri ni lazima nimtunze. Sivutiwi naye hata kidogo.”

"Sawa, kumtunza vipi huko mpaka kwenye kitanda chetu pia?" Lisa alicheka.

'Sikufanya hivyo.” Alvin alifoka kwa ukali, “Mbona huniamini?”

“Kwa sababu hustahili kuaminika.” Lisa akatikisa kichwa. Alihisi amani zaidi baada ya kutoa hisia zake alizozivumilia kwa muda mrefu. “Kwa sababu ya Sarah umeamua kulala chumbani kwetu na binamu yake. Kwa sababu ya Sarah umeamua kumtetea na kumlinda kaka yake. Kwa sababu ya Sarah umeamua kumchukia Charity na kuikandamiza kampuni yake. Ni nini kingine kitafuata katika siku zijazo?"

Sura ya: 247

“Lisa, acha. Twende nyumbani.” Alvin akazidi kufadhaika jinsi Lisa alivyokuwa mkali.
Hata hivyo, Lisa alibakia kusimama kama ameota mizizi chini. Alimwangalia na kummwagia tabasamu la kejeli. “Kwa sababu ya mpenzi wako wa zamani, siwezi kuwa rafiki na Charity. Oa tu Maurine ikiwa huwezi kuacha kumfikiria mwanamke huyo. Nipo radhi tupeane talaka.”
“Umemaliza? Wewe ndiye mtu ninayekupenda sasa." Kichwa chake kilikuwa kinamuuma sana. Kwa kweli hakujua ni nini kingine angeweza kusema ili kumshawishi.
"Ndio, unanipenda, lakini sio kama unavyompenda Sarah." Lisa alihema kwa uchungu. “Ikiwa Maurine, ambaye anafanana na Sarah, anaweza kuchukua nafasi yangu leo, basi inakuwaje mtu mwingine anayefanana naye zaidi atakapotokea siku moja? Mimi ni mtu ambaye anaweza kubadilishwa wakati wowote, na sitaki kuendelea na uhusiano wa aina hii tena. Samahani. Labda nisiseme hivi kwa sababu ya hali yako, lakini siwezi kukaa kando yako. Jitunze.”
“Hapana, Lisa, wewe ni wa kipekee na hakuna anayeweza kuchukua nafasi yako. Usiniache.” Alvin alimkumbatia kwa nguvu huku akiingiwa na hofu mithili ya mtoto anayekaribia kupoteza mali yake aipendayo.
Alikuwa amepitia upweke na uchangamfu wa upendo, lakini Lisa ni mwanamke pekee aliyebaki kando yake. Angewezaje kuishi ikiwa angeondoka?
"Acha. Mimi sio muhimu sana kwako. Baada ya yote, marafiki zako wanaweza kunifokea na wewe unawaangalia tu, na unaweza kunifungia wakati wowote upendao. Na nikihitaji marafiki mpaka nipate idhini yako… Sahau.” Lisa alijaribu kuunyoosha mkono wake kutoka kwake, lakini Alvin alikataa kuuachia.
“Usiende. Siwezi kuishi bila wewe. Nitamruhusu Maurine aondoke, sawa? Kisha tunaweza kurejea jinsi tulivyokuwa tunaishi hapo awali.” Alvin aliogopa sana. Hakuwahi kufikiria kuwa hivyo ndivyo itakavyoisha kwa Lisa.Kwanini watengane kwa sababu ya mabishano madogo?
"Bwana mkubwa naomba umwachie aende." Charity akasogea mbele kumsaidia Lisa.
"Charity, yote ni kwa sababu yako, sawa?" Akamtazama kwa chuki. "Unanichukia kwa kuibania kampuni yako nafasi ya ushirikiano na Alvinarah, kwa hivyo unalipiza kisasi kwa njia hii, sivyo?"
“Bwana Mkubwa, unawaza mambo kupita kiasi. Lisa sasa ni rafiki yangu. Kama marafiki yake, naweza kusema kwamba wewe na marafiki zako mmekuwa mkimtendea isivyo haki.” Charity alijibu kabla ya kumuongoza Lisa.
Pamela alifuata mara moja. Kisha wote watatu wakaingia kwenye gari na kuondoka.
Moyo wa Alvin ulipasuka sana huku akilitazama gari lile likipotea kwa mbali. Alitamani sana kuikimbia lakini ghafla, kichwa chake kilikuwa na maumivu makali, akaaanguka chini na kuzimia!
•••
Katika klabu ya usiku, Pamela aliagiza vinywaji vingine kumi na mbili, na wote watatu wakaagiza chakula.
Ingawa walikuwa wamezungumza mambo mengi, Lisa hakuweza kuacha kunywa pombe akijaribu kusahau kuhusu mateso ya Alvin. “Charity, naweza kukuuliza swali? Kwanini Alvin na marafiki zake wanakuchukia sana? Nimekufahamu kwa muda mfupi tu, lakini naweza kusema kwamba wewe ni mtu mzuri.”
"Ndio, umechukua maneno mdomoni mwangu Hata mimi nilitaka kumuuliza hivyohivyo." Pamela alitikisa kichwa.
Charity alionekana mwenye huzuni. "Labda ina uhusiano fulani na Sarah. Mama yangu alipoanza uhusiano na Langa Njau wakati huo, walimwona mama yangu kama mvurugaji tu wa familia ya Langa na hata kuwafanya wengine wanichukie pia nilipozaliwa. Nilipokuwa binti nilikutana na Chester nikiwa shule ya sekondari tukawa wapenzi, lakini haikuchukua muda tukaachana. Wote watatu walifikiri kwamba mimi nilikuwa sababu ya Sarah kukosa raha. Waliamini kwamba niliondoa ushirika na upendo wa baba ambao ulikuwa haki yake na kaka yake. Lakini siku zote nimekuwa nikitegemea juhudi zangu na uwezo wangu kufikia hapa nilipo leo.”
Lisa alipata picha halisi. “Nimegundua kitu, Alvin anawachukia sana watoto wa nje ya familia. Anaamini ni chanzo cha kuvuruga furaha ya familia. Kwa hiyo na wewe anakuchukia mpaka kwenye damu yake kwa sababu anaamini uliharibu furaha ya Sarah.” Kwa namna fulani, hii ilimkumbusha Lisa kuhusu Alvin na Jack na ndiyo maana hawakupatana maisha yao yote.

Baada ya sekunde chache, Charity alisema, "Hiyo ndiyo sababu kubwa. Alvin alimpenda sana Sarah na aliwachukia wote waliomuudhi. Kama Sarah atafufuka leo, hakika Alvin atachagua kurudi kwake na kukuacha wewe." Lisa alisikiliza maneno hayo huku akinywa bia kimya kimya.
•••
Katika hospitali. Alvin akarejewa na fahamu.
Mkono wake ulikuwa umeunganishwa na dripu. Akapepesa macho mara kadhaa. Aliweza kusikia sauti ya Rodney kutoka chumba kingine.
“Nimesema tangu mwanzo kwamba Lisa si mtu mzuri. Alvin tayari ni mgonjwa sana, lakini bado anasisitiza kutaka talaka. Hamjali hata kidogo.”
“Punguza sauti yako. Je, akiamka na kukusikia?” Chester alimtahadharisha.
“Nimekosea? Hana shukrani kwa kila kitu ambacho amempa, na bado anajaribu kushindana na mtu aliyekufa?” Rodney alizidi kulalamika.
“Bwana mkubwa, umeamka." Maurine, ambaye alikuwa ameketi kando yake, alipiga kelele alipomwona Alvin anafungua macho yake.
Mazungumzo ya koridoni yalisimama. Dakika kadhaa baadaye, Rodney na Chester waliingia chumbani kwa fujo.
"Nionyeshe hizo hati za talaka." Alvin alinyoosha mkono wake.
Rodney almkabidhi baada ya kusitasita. Alvin aliichunguza hati hiyo, ambayo ilisema kwamba Lisa hataki chochote. Alikuwa tayari kuacha ndoa bila chochote ilimradi tu akubali kusaini karatasi hizo. Vidole vyake vilishika karatasi hizo na kuzichanachana mara moja.
Kila mtu alichukulia jambo hilo kwa njia tofauti, lakini Maurine alijaribu kumfariji. “Bwana Mkubwa, usijali. Bi. Mdogo anafanya hivi kwa hasira tu. Atajuta baada ya kutulia.”
“Unatakiwa kuondoka.” Sauti ya Maurine ilimpa maumivu makali ya kichwa.
Rodney alisimama kumtetea kwa hasira. “Alvin, unasemaje? Lisa hata hajaja kukuangalia baada ya kuzimia. Ni Maurine ndiye aliyekuleta hapa.”
"Kwa hiyo? Unataka nimuoe yeye badala yake?” Alvin akanyanyua macho yake kwa jeuri. “Kwanini usimuoe wewe kwa kuwa unapenda kumtetea sana?” Rodney alishindwa cha kusema.
Machozi yalitiririka mashavuni mwa Maurine aliposema katikati ya kwikwi, “Bwana Shangwe, tafadhali acha kubishana naye. Najisikia vibaya sana. Bwana Mkubwa asingeingia kwenye vita hivi na mke wake kama si mimi. Ni bora niondoke tu." Maurine akatoka nje.
Alvin alishika midomo yake bila kutoa neno zaidi.
"Maurine, nisubiri." Rodney alipumua, kisha akamkimbilia Maurine.
Chester alisugua kichwa chake kama ishara ya kukosa cha kusema. "Utafanya nini?"
“Sitamruhusu Lisa aondoke upande wangu. Nina hakika kwamba yeye ndiye mtu ninayempenda.” Alvin aliweka msimamo.
Matukio ya kabla ya kuzimia yalimjaa akilini, na kumfanya kuchanganyikiwa. "Ni kosa langu. Labda… Sikupaswa kumruhusu Maurine abaki. Lakini sikufikiria kwamba Lisa angeniwazia mabaya zaidi. Anadai alinikuta kitandani na Maurine, lakini si kweli.”
"Labda Charity alikuwa akimpotosha." Chester alikunja uso.
“Charity Njau…” Alvin alikunja ngumi. “Sitakuwa mwema kwake tena. Nitahakikisha familia ya Njau inafilisika ndani ya mwezi mmoja.”
“Sikubaliani. Lisa atakuchukia zaidi akijua,” Chester alisema. "Familia ya Njau tayari iko mwisho wa wakati wao, itajifia yenyewe tu. We achana nayo."
“Sawa.” Alvin alihisi kichwa chake kuanza kumuuma tena. “Wewe ni mzoefu zaidi katika hili. Niambie jinsi ninavyopaswa kumrudisha.”
"Subiri, nitakutumia vidokezo vichache vya siri." Chester alimtumia mafaili machache kwenye simu. Alvin aliyapitia siku nzima.

Sura ya: 248

Usiku, Shangazi Yasine alikuja na chakula cha jioni. Hisia tata ilijidhihirisha katika moyo wa Alvin alipoona bendeji kuzunguka kichwa cha Aunty Yasmine. “Unapaswa kupumzika nyumbani. Nitamwambia Hans atafute mlezi mwingine…”
“Si sawa, Bwana Mkubwa. Kukuona ukiwa katika hali hii inanitia wasiwasi.”
Alvin akatenganisha midomo yake kutaka kusema kitu lakini akabadilisha mawazo yake. Akifikiri kwamba Aunty Yasmini angeogopa. Aliishia tu kusema kwa upole, “Pole…”
“Sijambo, lakini Bibi Mdogo hajakuelewa,” alisema. “Nyinyi mligombana kimakosa usiku huo, na sikupata nafasi ya kukueleza. Kweli, Bi. Kimaro hakumpiga Maurine bila sababu. Alikuja nyumbani akakuona wewe na Maurine mmelala kwenye kitanda kimoja. Kama ningekuwa mimi, nisingeelewa pia.”
"Nini?" Alvin alimtazama mwanamke huyo kwa macho yake meusi. "Kwanini Maurine alikuwa kitandani kwangu?"
Alijibu kwa unyonge, “Ulirudia usiku siku hiyo. Ulimshika mkono wake mara tu alipojitokeza, hata baada ya kukupeleka kitandani, ulisisitiza abaki na wewe. Bwana Mkubwa … Jnaogopa kusema lakini ulimkosea Bibi Mdogo!”
Alvin alichanganyikiwa. Ina maana alimshika mkono Maurine na kwenda naye chumbani kwake? Hakuwa na kumbukumbu yake hata kidogo.
Kisha akaendelea. “Nilitaka kumzuia Bi. Kimaro usiku ule baada ya kurudi, lakini aliwahi kukimbilia ghorofani na kuwakuta katika hali hiyo. Alilalamika na kuanza kugombana na MAurine lakini ukamuona kama mkorofi. Ulimfungia hata kwenye chumba cha upweke baada ya hapo. Naamini alishtuka sana.”
“Mimi… nilimfungia ndani ya chumba?” Hilo nalo lilimshangaza. Hakukumbuka hata kama waligombana.
"Hiyo ni kweli. Bi. Kimaro alipiga kelele za kuomba msaada usiku mzima. Alivunjika moyo sana. Alishangaa kwamba ulimfungia ndani ya chumba cha upweke baada ya kile wanafamilia wako walimfanyia mara ya mwisho.”
Hisia nzito katika kifua chake ilimsababishia maumivu makali. Alikuwa amefanya nini? Kichwa chake kilianza kumuuma tena.
Akiwa amechanganyikiwa, Aunty Yasmine haraka akachukua mto na kuuweka nyuma ya shingo yake. Hata hivyo, maumivu ya kutoboa moyo yalimzuia asilale usiku wote huo.
•••
Asubuhi. Lisa aliingia ofisini kwake. Hans alikuwa akimngoja nje ya ofisi yake kwa muda mrefu. "Bibi mdogo, haya ni majibu ya vipimo vya DNA kati ya Melanie na Bw. Joel Ngosha ambayo ulitaka nishughulikie hapo awali."
Hilo lilimshangaza Lisa. Alikuwa amekosana na Alvin, na hivyo hakutarajia msaidizi wake angeendelea kumsaidia.
"Asante." Alipokea hati kabla ya kusema, “Hii itakuwa mara ya mwisho kuomba msaada wako. Tafadhali acha kuniita Bibi Mdogo baada ya hapa. Huyo si mimi tena.”
"Wewe ni bosi wangu mradi tu umeolewa na Bwana Mkubwa." Akakunja uso kwa wasiwasi. “Kwa kweli, Bwana Kimaro anajali sana kuhusu wewe. Juzi usiku baada ya nyie kutoka kwenye baa, alizimia na hakurudiwa na fahamu hadi jana. Hayupo vizuri kwa sasa. Jana usiku, yeye…”
“Unapaswa kumtafuta Maurine. Au tembelea kaburi la mpenzi wake wa zamani.” Kuzungumza juu ya Alvin kuliharibu hisia zake. Watu wengi waliokuwa karibu na Alvin waliendelea kumwambia kwamba anamjali, kwamba hali yake ingezidi kuwa mbaya bila yeye. Aliwaamini. Hata alijishusha chini ili kuwafurahisha watu wa familia ya Kimaro. Lakini, alipata nini mwishowe? Unyonge na uongo.
“Bwana Mkubwa hampendi Maurine…”
“Hans, acha. Mimi si shirika la kutoa misaada.” Alimkatiza bila kusita, na chuki machoni mwake ilielezea kila kitu.
Hans alishindwa cha kusema. Alishusha pumzi baada ya kuingia kwenye lifti. Laiti angejua hivyo ndivyo mambo yatakavyokuwa, angemshawishi Alvin asimuajiri Maurine hapo mwanzo.

Lisa alivumilia hisia ya kichefuchefu hadi akakimbilia kwenye chumba cha kunawia ili kutapika. Alikuwa amekunywa sana jana yake hadi tumbo likaanza kumsumbua. Baada ya hapo, aliendelea kusoma hati iliyokuwa mkononi mwake.
'Haihusiani' ilionekana mbele ya macho yake kwa maneno mekundu na ya ujasiri. Hiyo ilimshangaza sana Lisa. Melanie hakuwa binti wa Joel. Hata hivyo, Joel alimtelekeza mama yake ili amuoe Nina zamani kwa sababu Nina alikuwa na ujauzito wa Melanie.

Kwa maneno mengine, Nina alikuwa amemdanganya Joel zaidi ya miaka ishirini iliyopita. Lisa akaweka hati hiyo kwa uangalifu. Hizi zilikuwa habari za kushtua lakini wakati wa kuziweka hadharani ulikuwa bado.
Akiwa anawaza hayo tu, Daktari Angelo akampigia simu. “Bi Jones, sehemu niliyokuwa nakaa jana usiku iliteketea kwa moto ghafla. Kwa bahati nzuri, ulinikumbusha kuwa ninaweza kuwa katika hatari muda wote, kwa hivyo nimekuwa nikitoka kwa siri kupitia mlango wa nyuma baada ya kufika nyumbani. Utabiri wako ulikuwa sahihi sana."
“Hilo ni la kushukuru Mungu. Tafadhali mwagize msaidizi wako atangaze kwamba ulikufa kwa moto. Kwa sasa, tafadhali endelea kumhudumia baba yangu kwa siri.”
Lisa alitabiri kuwa Damien angeweza kumdhuru daktari huyo maarufu. Kwa bahati nzuri, Daktari alizingatia ushauri wake na akaokoka. Damien na wengine lazima wangeamini kuwa Daktari Angelo alikuwa amekufa kwa muda huo.
•••
Katika makazi ya familia ya Ngosha, Nina alitabasamu kwa furaha baada ya taarifa za kifo cha daktari. “Kwa kweli ni habari njema. Joel hawezi kurejewa na fahamu hivi karibuni baada ya kifo cha Dokta Angelo. Lisa ni mjinga sana kuendelea kuhangaika na baba yake. Lazima atakuwa akilia na moyo wake sasa hivi.”
Melanie alichanganyikiwa. “Mama unamaanisha nani? Baba yangu?"
"Ndio, baba yako yuko njiani kuja hapa ili nyinyi wawili mkutane rasmi. Tutalazimika kumtegemea katika siku zijazo." Nina alimpigapiga bintiye kichwani. Ijapokuwa alimdharau mwanaume huyo miaka yote, ilimbidi akubali kwamba aliweza kumpa kile anachotaka, tofauti na Joel ambaye hakuacha kumfikiria Sheryl.
Melanie alimtazama kwa macho ya kutarajia. Dakika chache baadaye, mwanamume mmoja aliingia akisukumwa kwa kiti cha magurudumu. Melanie alipigwa na butwaa kumwona, lakini hatimaye, alifikiri kwamba yote yalikuwa ya maana. Si ajabu alifanana na Joel ingawa hakuwa baba yake halisi. Isitoshe, Damien alikuwa amemdekeza tangu alipokuwa mtoto. Haijalishi angefanya nini, angemsaidia kila wakati.
“Melanie, njoo huku. Mimi ni baba yako.” Damien alimwashiria.
“Bam’dogo Damien… ni wewe?” Alitembea kuelekea kwake kwa kusitasita.
Alikunja uso, na Nina akaeleza hali hiyo haraka. “Kwa kweli, baba yako amekuwa akinipenda tangu miaka ishirini au zaidi iliyopita. Lakini sikujua vizuri zaidi na kuweka matumaini yangu yote kwa Joel. Kabla Joel hajanioa, mimi na baba yako tulikuwa tayari tumekuweka tumboni mwangu. Baada ya hapo, niliwaambia kuwa mtoto wangu ni wa Joel ili anioe. Miaka yote, Damien amekuwa akitutunza. Bila yeye, Lisa angekuwa na udhibiti kamili wa Ngosha Corporation kwa sasa.”
“Ni kweli bam’dogo?” Melanie alikuwa katikati ya mshangao.
“Acha kuniita bam’dogo Melanie. Niite baba badala yake.” Alishika mikono ya Melanie. "Nitakupa kilicho bora zaidi."
“Asante, Baba.” Alimzungushia mikono yake shingoni. Damien alimjali sana kuliko Joel. “Baba, namchukia Lisa. Nataka afe.”
Nitamfanya yeyote anayemdhulumu binti yangu alipe kwa matendo yake. Lakini kipaumbele kwa sasa ni kuharakisha harusi yako na familia ya Campos,” alisema. "Familia ya Kimaro haitakuwa na nafasi katika jiji hili mara tu familia za Ngosha na Campos zitakapoungana tena."

Sura ya: 249

Melanie alikuwa ameduwaa. “Baba, unapanga…”
“Nataka uwe mwanamke mashuhuri wa Nairobi. Utatafutwa na kuonewa wivu na kila mtu.” Macho ya Damien yalijaa kujiamini. "Siku hiyo itakuja hivi karibuni."
Melanie aliwazia tukio hilo, na mwili wake ukatetemeka kwa msisimko.
•••
Saa tano usiku, Lisa alirudi nyumbani baada ya kutoka kutazama sinema. Alipofungua mlango, alihisi kuwa kuna kitu hakiko sawa. Harufu ya waridi sebuleni ilikuwa kali sana. Kulikuwa pia na jozi ya viatu vya kiume kwenye mlango.
Moyo wake uliruka mapigo. Akawasha taa. Maua mengi mekundu yalikuwa yamepangwa katika umbo la moyo katikati ya sebule. Alvin alikaa kwenye sofa la kitambaa huku akiwa amevalia fulana nyeusi iliyomechishwa na suruali nyeusi ya jeans. Hata nywele zake zilikatwa katika mtindo wa kiduku, ambao kwa kipindi hicho ulikuwa ukivuma katika tasnia ya burudani. Mavazi yake pamoja na sura yake, vilimfanya aonekane tofauti kabisa na alivyozoeleka.
Lisa karibu hakuweza kumtambua. Huyo alikuwa Alvin? Kwanini alionekana hivyo siku hiyo? Alionekana kama mvulana aliyetoka tu shuleni, ambaye alikuwa akimtongoza mpenzi wake kwa mara ya kwanza.
“Ninaonekana vizuri?” Alvin alimuona Lisa akimshangaa, akafunua midomo yake kuachia tabasamu zito. Ilionekana kama kidokezo cha siri cha Chester kilikuwa kimefanya kazi.
Wanawake huwapenda wanaume ambao hujua namna ya kubadilisha hisia zao muda wowote. Mwanamume ambaye anaweza kumchukiza na kumwonyesha mapenzi. Mwanamume anayeweza kumliza na kumfanya acheke. Mwanamume anayeweza kumhudhunisha na kumfurahisha. mwanaume anayeweza kucheza vizuri na hisia za mwanamke, hatakosa penzi la mwanamke ampendaye.
Ingawa hakuwahi kufanya hivi hapo awali, alikuwa tayari kubadilisha mtazamo wake mara moja moja kwa ajili ya Lisa tu.
Lisa alimsoma kwa umakini na kukunja uso. "Maurine anakutunza au anakuharibu ubongo?"
“Una wasiwasi na mimi?” Alvin alizidi kutabasamu. "Ninajisikia vizuri zaidi baada ya kukuona."
"Hapana, umekata nywele zako kwa mtindo huu wa kitoto na hata ukaingia kwenye nyumba ya mtu mwingine na kujaza rundo la takataka. Hii haimaanishi kwamba umekuwa mgonjwa zaidi?” Lisa akacheka kwa kejeli. “Nadhani vitu hivi hujavileta mahali sahihi. Ungepeleka mbele ya kaburi la Sara.”
Alvin alijikaza. Alikuwa ameishi kwa miaka 30, lakini ilikuwa ni mara ya kwanza kuhisi kana kwamba alikuwa anapigwa kofi usoni la mwanamke.
“Lazima uwe mwendawazimu. Unawezaje kujaza takataka zote hizi kwenye nyumba yangu?" Lisa aliumwa na kichwa kwa kuangalia maua yale. Alitumia siku nzima kusafisha nyumba hii mpya, lakini alikuta uchafu mwingine umetapakaa nyumba nzima.
Alvin alijisikia vibaya ghafla kutokana na kejeli za maneno ya Lisa. Alihisi moyo wake unakuwa mweusi kama umepakwa masinzi. Alikuwa ametumia muda mwingi kupanga maua yale, na mikono yake ilichomwa na miiba kila mahali. Lakini juhudi yake ilionekana kama utopolo tu kwa Lisa.
“Kwanini upo hapa?” Lisa alimtazama bila furaha. “Umeingiaje? Tafadhali ondoka mara moja, la sivyo nitakuripoti kwa polisi kwa kosa la kuvamia kwenye nyumba ya mtu bila kukaribishwa.”
“Sawa, unaweza kuendelea na kuniripoti. Nitawaonyesha polisi hiki kitu.” Alvin akatoa cheti chao cha ndoa. “Sisi bado ni mume na mke, kwa hivyo nina haki za kisheria kukaa hapa."
Lisa alikosa la kusema. Alikaribia kusahau kwamba Alvin alikuwa wakili bora zaidi nchini Kenya.
“Kwa hiyo unataka kumleta Maurine na kuwa na wanawake wawili wakimtumikia mume mmoja?” Lisa alidhihaki, "Naona huu ni utaratibu wa kawaida wa matajiri wakubwa wa hapa Nairobi ambapo mke halali na mchepuko huishi pamoja katika nyumba moja."
Alvin alisimama mara baada ya kusikia maneno yake ya kejeli. Umbo lake jembamba lilikuwa kama la mwanamitindo, lakini macho yake yalikuwa ya damu. "Nilimtaka Maurine aondoke tayari. Shangazi Yasmine aliniambia kuwa ulimpiga usiku ule kwa sababu nilikuwa nimelala kitandani na kumshika mkono Maurine. Samahani kwa kuwa sikukuelewa. Nimekuja kukuomba msamaha.”
Alvin akaanza kufafanua jambo moja baada ya jingine.

"Kuhusu Sarah Wonderland Park, ni suala lililotokea muda mrefu uliopita. Sikujua tukio la fataki la saa mbili usiku kila Ijumaa kama bado linaendelea. Siku zote ni msimamizi mkuu wa bustani hiyo ndiye ambaye alisimamia tukio hilo. Alisema fataki hizo zimekuwa kivutio cha watalii, lakini nimemwambia asitishe.”
“Kuhusu kampuni, nilikuwa bado sijakutana na wewe nilipoipa jina la Alvinarah. Hata hivyo, nitaifanya KIM International na Alvinarah ziunganishwe haraka iwezekanavyo. Baada ya hapo, hakutakuwa tena na kampuni ya Alvinarah.”
Alvin akamsogelea Lisa hatua kwa hatua, huku macho yake yakiwa yamejaa mahaba. “Lisa, rudi mpenzi. Siwezi kuwa bila wewe." Aliinamisha kichwa chake na kumbusu midomo yake kwa upendo.
Lisa alikuwa kama ameyeyukia hewani wakati huo. Hakukuwa na shaka kwamba sura, hadhi, na sauti ya Alvin ingeweza kumvutia kwa urahisi mwanamke yoyote. Hata hivyo, pumzi yake ilipokaribia kukata, Lisa alirudi kwenye fahamu zake na kupiga hatua chache nyuma. Alimtazama Alvin kwa tahadhari.
"Nimesikia hadithi zako nyingi sana. Umewahi kuniambia maneno mengi mazuri pia, lakini ulinichukuliaje? Maurine alipojitokeza kwako akili yako ikahama kabisa, ulifikiri ninamnyanyasa. Marafiki zako wote wananifikiria kama mtu mbaya ambaye ana wivu hadi kwa mtu marehemu, na ndiyo unaowasikiliza na kuwaamini. Rodney alinihakikishia kuwa Maurine hawezi kuondoka, mimi nimechoka kabisa!”
Ukimya mfupi ulipita kisha Lisa akaendelea.
"Kulikuwa na tukio na Thomas pia. Ulijua kuwa alikuwa ameoza kabisa, lakini ulimsaidia tena na tena. Mwishowe, Zigi alikuja kuniumiza kwa kisu. Hilo lilisababisha Kelvin kupoteza figo na ilinibidi kubeba hatia…”
Alvin alikodoa macho. “Kwa hiyo unafikiri kwamba Kelvin aliumia kwa sababu yangu?”
“Kumbe!” Lisa alicheka. “Kama si Kelvin, ningekuwa nimekufa. Ningekufa kwa sababu ya kaka wa mpenzi wako wa zamani." Alisema kwa kejeli na kupanda juu. Akiwa amekasirika sana, alifunga mlango na kuingia bafuni kuoga.
Baada ya kutoka kuoga, alimuona Alvin aliyetakiwa kuwa nje akiwa amejilaza kitandani kwake. Alikuwa amelala fofofo huku akikumbatia mto wake na kujifunika blanketi lake.
Lisa alikuwa karibu kupandwa wazimu. Mtu huyo aliwezaje kuingia chumbani kwake? "Alvin, ondoa wazimu wako hapa." Lisa akainua blanketi.
Alipoona Alvin hajavaa chochote chini ya blanketi, uso wake ulibadilika kwa hasira na aibu. “Mbona umevua nguo?”
Akiutazama uso wa Lisa wenye haya, midomo ya Alvin ilijipinda na kutabasamu. "Nililazimika kuvua ili kulala, bila shaka. Hukuniandalia nguo zozote za usiku pia.”
Lisa alizidi kupandwa na hasira za mshangao. Hakuwa na aibu kiasi cha kujipenyeza ndani ya nyumba yake, akaingia chumbani kwake na kulala kitandani kwake na kumlaumu kwa kutomwandalia nguo za kulalia?
“Kuwa mstaarabu na usinisumbue. Ninaweza kulala usingizi tu kwa kuvuta harufu yako. Sijalala kabisa kwa siku mbili.” Alvin alichukua blanketi na kujifunika.
Lisa alikasirika kiasi kwamba alitamani apasuke. Alijiona hana nguvu. “Alvin, unataka nini? Maurine hakutoshi sasa? Mbona bado unaning’ang’ania?”
“Tayari nimemuamuru aondoke.” Alvin akabinya midomo yake pamoja na kusema, “Ikiwa unanichukia kwa kukufungia kwenye chumbani peke yako kwa usiku mmoja, unaweza kunifungia chumbani pia.”
Lisa alifoka, “Kwanini nikufungie? mimi si mgonjwa kama wewe.”
Mgonjwa? Neno hilo lilijirudia chumbani. Uso wa Alvin ulipauka papo hapo. Alionekana kana kwamba ni mtoto. Lisa aliuma mdomo. Hakutaka kuwa na moyo dhaifu na kumuonea huruma hata kidogo.
Alvin hakusema chochote. Alinyanyuka na kutembea kwa huzuni hadi chumba kingine kabla ya kufunga milango. Lisa hakumjali na kumwacha aendelee na maigizo yake.

Sura ya: 250

Lisa aliposhuka chini ili kuchota maji, ghafla alikumbuka tukio la yaya wa Alvin kumfungia chumbani alipokuwa mdogo…
Glasi mkononi mwake ilidondoka chini na kuvunjika sakafu. Alikimbia ghorofani na kufungua chumba alichoingia Alvin.
Mwili wa Alvin ulikuwa umejikunja ndani ya kabati na kuwa kama mpira, na kichwa chake kilizikwa kwenye magoti yake. Alikuwa akitetemeka kama mbwa aliyenyeshewa mvua.
"Alvin, toka nje." Lisa alijaribu kumtoa lakini akashindwa.
“Nasikia baridi sana… Usinipige…” Alvin alikuwa akiziba masikio yake kwa nguvu zake zote.
Lisa hakutaka kumuonea huruma, lakini moyo wake ulimshinda na kujikunja kwa maumivu wakati huo.“Sitakupiga. Usilale humu twende kitandani. Kila kitu kitakuwa sawa.” Lisa alimkumbatia na kumpigapiga mara kwa mara.
Mwili wake ulipoacha kutetemeka, alimsaidia kumkokota hadi kitandani, akamlaza na kumfunika blanketi. Hata hivyo, Alvin alimshika mkono kwa nguvu. Hakuweza kumwacha aondoke hata kidogo.
Lisa alijaribu kuutoa mkono wake mara kadhaa lakini akashindwa. Hatimaye, hakuwa na chaguo ila kulala upande mwingine. Awali alipanga kwenda kulala chumba cha wageni baada ya yeye kulala, lakini yeye mwenyewe alipitiwa na usingizi kwa sababu alikuwa amechoka sana.
Hakujua alikuwa amelala kwa muda gani. Katika hali ya ukungu, alihisi mtu akibusu midomo yake kwa hamu. Wimbi la msisimko lilitanda kwenye ngozi yake.
Alifumbua macho yake ghafla. Alipomuona Alvin akiwa juu yake, alimsukuma kwa hasira. “Nani amekuruhusu kunibusu?”
“Lisa, hakika una wasiwasi na mimi. Ulilala kando yangu jana usiku. Unanijali.” Alvin alitabasamu na kumtazama kwa furaha. "Hebu tufanye kidogo."
"Si Maurine alikukataza mpaka umalize dozi?" Lisa akakumbuka tukio la Maurine akiwa ameketi juu yake chumbani. Alihisi kichefuchefu na kukimbilia chooni kutapika.
Alvin alimfuata chooni akiwa na wasiwasi. Lisa alimtazama baada ya kutapika na kutaka kuendelea kumbusu. “Usinibusu, nahisi kichefuchefu sana nikiguswa tu na wewe.”
Macho ya Alvin yaligeuka kuwa mabaya mara moja. Kwanini alimchukia kiasi hicho? Ndiyo, alikuwa na nafasi kwa Sarah moyoni mwake, lakini hakuwahi kufanya jambo lolote lililomsaliti Lisa. Akakunja uso kisha akageuka kuelekea chini.
Lisa alishuka baada ya kufanya usafi. Harufu ya mayai ya kukaanga ilikuwa ikitoka jikoni.
“Sandwichi, maziwa, na mayai ya kukaanga. Karibu tule.” Alvin alikuwa amevaa aproni na kwa kushangaza alitengeneza seti mbili za kifungua kinywa. Kutokana na mwonekano wake, alikuwa akijaribu kumfurahisha Lisa.
Lisa karibu alitaka kufungua madirisha na kuchungulia nje ili kuona kama jua lilikuwa limechomoza kutoka magharibi badala ya mashariki siku hiyo. Walikuwa pamoja kwa muda mrefu sana, lakini aliwahi kumtengenezea chakula mara moja tu—na kilikuwa na ladha mbaya sana.
Ingawa kifungua kinywa hakikuonekana kutosha kumvutia kula, alikuwa na njaa kwani alikuwa ametoka kutapika. Hata hivyo, hakutaka kula.
"Samahani, lakini mimi siwezi kula aina hii ya kifungua kinywa." Alikataa kwa kiburi na kuelekea mlangoni.
Alvin alijisikia kama sehemu ya moyo wake imeondolewa kwa kuambiwa jibu kama hilo. Lakini akakumbuka hakuwa na haki ya kukasirika kwani alikuwa amemwambia hivyhivyo wakati alipomwandalia kifungua kinywa kwa mara ya kwanza huko nyuma. Mwanamke huyo alijua jinsi ya kuweka kinyongo.
Kuona kiamsha kinywa ambacho Alvin alimtayarishia hapo awali kulimfanya awe na njaa. Aliendesha gari hadi kwenye mgahawa wa kifungua kinywa. Alisikia kutoka kwa Pamela kwamba chakula kwenye mgahawa huo hakikuwa kibaya. Alvin alimpigia simu Hans na kumwambia amfuatilie Lisa kimyakimya, na endapo ataona amekutana na Charity ampigie simu.
Lisa alipoanza tu kula baada ya kuagiza kifungua kinywa chake, Melanie na Jerome waliingia kwenye mgahawa huo wakiwa wameshikana mikono.
Meneja wa mgahawa aliwafuata wote wawili kwa makini. “Bwana Campos, Bi Ngosha, mngependa kuketi wapi?”
Melanie alitazama huku na kule na kugonganisha macho na Lisa. Macho yake yakaangaza. Alimvuta Jerome na kwenda mara moja kuelekea kwa Lisa.

“Oh, huyu si mke wa Bwana Kimaro? Kwanini unakula kifungua kinywa hapa peke yako? Yuko wapi Bwana Mkubwa Kimaro ambaye anakupenda sana?" Melanie alitazama pande zote kuangaza.
Lisa alikunja uso. Alikuwa na kifungua kinywa kizuri, lakini walipotokea tu hao watu alihisi kama inzi wameingia kwenye bakuli la supu yake ya mbuzi.
Msimamizi wa cafe aliogopa. "Bi Kimaro, samahani…"
“Huna haja ya kumwomba msamaha Bw. Cameron.” Jerome alitoa tabasamu zito. "Nadhani hatakuwa Bi Kimaro tena hivi karibuni. Nijuavyo, Bi. Jones amefukuzwa nyumbani kwa Bwana Kimaro. Nilisikia kwamba hata alitafuta nyumba ya kununua na kuhamia kwa haraka siku chache zilizopita.”
Bwana Cameron alielewa maneno yake na hapohapo heshima aliyokuwa nayo hapo awali kwa Lisa ikatoweka. Mtazamo alioutoa kwa Lisa haukuwa wa heshima tena, hata ulijawa na dharau.
"Bwana Campos, una taarifa sahihi kabisa." Lisa alijifuta mdomo na kumtupia macho makali Jerome. "Unajua zaidi kuliko vyombo vya habari. Inawezekana kwamba ulikuwa na jasusi uliyemwajiri ili kunipeleleza?"
Jerome alifoka. “Nani asiyejua kuwa Alvin alileta binamu wa mpenzi wake wa zamani nyumbani siku chache zilizopita ili amtunze? Ni kwa sababu ameona wewe hufai na unazidi kumpandisha wazimu wake.”
“Umekuwa mjinga sana.” Sauti ya Melanie ilijaa kejeli. “Alvinarah, Alvinarah, haimaanishi Alvin na Sarah? Angalia uso wako wa kutisha. Ulijidanganya kwamba unaweza kukalia nafasi ya Sarah kwa Alvin Kimaro. Lakini sina budi kukushukuru pia. Kama usingempokonya Alvin, nisingeweza kukutana na Jerome wangu ambaye ananithamini sana.”
Jerome alizipapasa nywele za Melanie. Ingawa hakuwa amempenda Melanie hapo awali, alijifanya kumpenda sana kwa sababu fulani. Joel asingekuwepo tena, kwa hivyo Melanie alikuwa mrithi wa Ngosha Corporation. Hakutaka kupiga teke kapu la bahati iliyokuwa ikimdondokea mapajani mwake. Familia ya Ngosha na familia ya Campos zingeungana. Alvin angekuwa si kitu kwa wakati huo.
"Bwana. Cameron, nadhani meza yake karibu na dirisha si kibaya,” Melanie alisema huku akinyoosha kidole kwenye meza ya Lisa. “Tutakaa hapa.”
"Basi mtoe haraka na umpeleke kwenye meza nyingine," Jerome aliamuru kwa kiburi.
Bila kukawia zaidi, Bwana Cameron alimmwambia mhudumu kusogeza vitu vya Lisa kwenye meza iliyokuwa karibu na ukuta kwenye kona ya mgahawa huo. “Bi. Jones, tafadhali kula kifungua chako huko.”
“Nyie ni…” Lisa akatikisa kichwa na kusimama.
Melanie alitabasamu. "Lisa Jones, unaona hii? Hutanishinda kamwe. Mimi ni makamu wa mwenyekiti wa Ngosha Corporation sasa. Wiki ijayo, nitaolewa na Jerome. Kufikia wakati huo, familia za Campos na Ngosha zitakuwa timu yenye nguvu. Hakuna mtu nchini Kenya atakayethubutu kusema chochote hata nifanye nini.”
“Oh, hongera basi.” Lisa akasimama taratibu. "Baba bado amelazwa kwenye kitanda cha hospitali na haijulikani ikiwa ataishi au atakufa, lakini wewe? Unapata wapi hata hiyo hamu ya kuolewa?”
"Melanie anamjali sasa baba yake, anataka amletee zawadi ya wajukuu wenye akili." Jerome alijibu mbele ya Melanie.
“Eti anamjali sana Baba! Mbona sijawahi kuwaona mkimtembelea hata mara moja baada ya kuzimia?” Lisa alitoa tabasamu la uwongo.
"Niende au nisiende sio kazi yako." Melanie alidhihaki, “Vipi kuhusu wewe? Ulipata haki za kumtunza Baba, lakini kwa faida ipi? Ngosha Corporation ni yangu, na kila kitu ambacho Baba anamiliki ni mali yangu. Huna chochote cha kurithi. Nilisikia kwamba Daktari Angelo amekufa. Hakuna mtu anayeweza kumwokoa Baba sasa. Unaweza kuukumbatia mwili wake maisha yako yote, ndicho kilichobakia.”
"Angalia sauti yako. Inaonekana huna huzuni hata kidogo kwamba Daktari Angelo amekufa na Baba hawezi kuamka.” Lisa alishtuka na kuinua kichwa chake.
Koo la Melanie lilikwama kwa muda. Alisema kwa hasira, “Je, unaweza kupotea haraka? Usitusumbue tukiwa tunapata kifungua kinywa chetu.”
"Endelea kuwa jeuri kwa sasa, lakini siku zako zinahesabika." Lisa akatoa noti kadhaa na kuzitupa mezani. “Nitawaachia meza, lakini siku nyingine… msitarajie kama itatokea tena.” Alichukua mkoba wake na kuondoka baada ya kumaliza kuzungumza.

Hans, aliyekuwa amejificha kwenye kona moja, aliripoti kwa Alvin kila kitu alichokiona akifanyiwa Lisa.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.........LISA
KIRASA......246-250

Sura ya: 246

Alvin alinyamaza na kuamuru chopa kuondoka. Walifika kwenye baa upesi sana. Thomas ambaye alikuwa amekaa nje ya baa hiyo kwa muda mrefu, mara moja akasogea huku akiwa ameshika kiuno chake kilichojeruhiwa.

Kutokana na muziki mnene ulioziba masikio, Lisa hata hakuweza kusikia muungurumo wa helkopta. Hazikupita sekunde yeye na wenzake walijikongoja kutoka kwenye baa huku wakiwa wamekumbatiana mabega Kwa kuangalia midomo yao iliyokuwa ikipepesuka, ilidhihirisha walikuwa wamekunywa pombe nyingi.

“Bado sijatosheka, tuendeleeni kunywa, naweza kumaliza kreti zima peke yangu.” Pamela aliinua mikono yake juu hewani. "Sitarudi nyumbani hadi nilewe."

"Wacha tule nyama kwanza." Charity alikuwa amefurahi sana.

Lisa alishauri, "Tunaweza kwenda kuendelea kunywa katika nyumba yangu ya kifahari hadi alfajiri."

"Kweli! Sisi ni utatu mtakatifu, wote ni ma-single dadaz. Wanaume ni sh*t! Waache waende zao!" Charity akakubali kwa furaha.

"Sh*t! Wanaume ni nyoko!" Pamela akakandamizia kwa hasira.

Uso wa Alvin ulijawa na mawingu, Lisa hata alimdhihaki mbele ya marafiki zake? Akasogea kumvuta Lisa mikononi mwake. "Twende nyumbani haraka."

Hapo awali alikuwa ameridhika akae nje kwa muda kwa kuhofia kwamba angemdhuru, lakini ilionekana wazi kuwa asingeweza kufanya hivyo.

“Wewe ni nani na unafikiri unafanya nini?” Lisa aliinua kichwa chake akiwa ameduwaa. Baada ya kuutazama vizuri uso wake, lile tukio la Maurine akiwa amemlalia akimfanyia masaji lilimjia kichwani. Ghafla alihisi kichefuchefu na kumtapikia Alvin nguo zake zote na chini.

"Lisa Jones!" Alvin aliita jina lake herufi kwa herufi. Alitamani angemchuna ngozi akiwa hai hapohapo.

"Bwana Kimaro." Maurine alikimbia kwenda kumfuta uchafu ule mwilini
Mwake.

Baada ya kuona hivyo Pamela alikimbia mbele mara moja na kumpiga Maurine kichwani na mkoba wake. “Wewe b*tch, kwanini usitafute mwanaume wako? Umepanga kuharibu ndoa ya Lisa?”

Maurine aliugulia maumivu, Lisa alifurahi sana kuona hivyo, akasogea mbele akijifanya kumsaidia. “Pamela, usifanye hivi…”

Licha ya maneno yake hayo ya upole, Lisa alinyoosha mguu na kumpakaza Maurine kwenye matapishi yaliyokuwa chini, akasogea mbele kumkanyaga mara kadhaa. Maurine alilia kwa maumivu makali huku akishika pindo la suruali ya Alvin. “Bwana Mkubwa, nisaidie…”

“Inatosha.” Alvin alimsaidia Maurine kusimama kabla hajawatizama wale wanawake wawili, “Pamela kweli hujaelimika, Lisa, jiangalie vizuri ulevi wako, nilikuambia ujiepushe na Charity, umekaidi na kuamua kunywa pamoja naye. Kwanini husikii?”

Lisa alipapasa masikio yake na kujibu kwa dharau, “Unasema upuuzi gani, sikuelewi.”

Pamela alicheka. "Lisa, si unajua? Sisi hatujaelimika kuliko wao, kwa hivyo hatuwezi kuwa sawa nao."

“Uko sawa.” Lisa alikubali, “Twende.”

Alvin alikasirishwa kwa kupuuzwa na yule mwanamke, “Simama hapo hapo wewe ni mke wangu, nakuagiza twende nyumbani sasa hivi. Alvin alishika mkono wake tena, lakini wakati huu, nia ya hatari iliangaza macho yake yenye huzuni. “Usinifanye nipitilize kikomo cha uvumilivu wangu.”

“Kikomo? Una kikomo gani?" Lisa alicheka baada ya kumuona Thomas akiwa amesimama nyuma ya Alvin. “Kwa nini umemleta hapa? Ili kumtetea tena?”

Mara Thomas aliugulia maumivu. “Bi. Kimaro, kwa kweli unapaswa kukaa mbali na Charity. Ana kusudi la kufanya urafiki na wewe kwa nia mbaya."

“Thomas, ninajuta sana kwamba sikukupiga vya kutosha muda ule.” Charity akayafumba macho yake mazuri.

Thomas aliogopa sana na mara moja akajificha nyuma ya Alvin. “Bwana Mkubwa, tazama jinsi anavyo nitisha mbele yako.”

"Charity, inaonekana nimekuwa mkarimu sana kwako." Uso wa Alvin ulikuwa umekunjamana kwa hasira. “Nakuonya sasa ukae mbali na mke wangu. Vinginevyo, utasahau kama uliwahi kuwa mkurugenzi wa New Era Advertisings.”

Uso mzuri wa Charity ulibadilika na kupoa ghafla kama maji mtungini. Hata hivyo, Lisa alimshika mkono na kumtazama Alvin akiwa ameinamisha kichwa. “Hahitaji kufanya urafiki nami. Kuanzia sasa na kuendelea, mimi ndiye nitakayefanya urafiki naye. Yeye ndiye rafiki wa kwanza mzuri ambaye nimempata hapa Nairobi.”

Alvin alikasirika sana. “Lisa, ngoja nikukumbushe tena kuwa huyu mwanamke ni mjanja mjanja na mlaghai, lakini bado unataka kuwa rafiki yake. Wewe ni mjinga sana kutokuona hivyo?"

"Ndio, mimi ni mjinga sana ndo maana nilikupenda." Lisa alicheka kwa kebehi. “Huwezi kujua ni nani mjanja na nani mjinga? Charity hakunidanganya. Kinyume chake wewe na marafiki zako ndiyo mnanidanganya. Najua kwamba mume wangu ameweka mwanamke ambaye anaonekana kama mpenzi wake wa zamani karibu naye ili ajisikie vizuri. Je, huu ndio upendo unaoendelea kuuzungumzia? Unachukiza.”

Akiwa amepigwa na butwaa, mchanganyiko wa mshangao na aibu ukatanda usoni mwa Alvin. Hata hivyo, ilipita kwa sekunde chache tu kabla hajamkodolea macho Charity. “Ulimwambia kuhusu hili?”

Charity alikosa la kusema, mara Lisa akajiweka mbele yake kumtetea. “Angethubutu vipi kuniambia wakati unamtishia kuiangusha New Era Advertings? Uhusiano wako na Sarah ulikuwa maarufu sana hivi kwamba kila mtu hapa Nairobi anajua. Isitoshe, huenda sikuwahi kukuambia, lakini huwa unaliita jina la Sara usingizini. Hata jina la Alvinarah mchanganyiko wa maneno ya jina lako na lake. Nilijua hilo zamani. Oh, nini kingine? Ulijenga bustani ya kushangaza ili kumchumbia. Fataki bado hulipuka kila saa 8:3o usiku kama tamko la upendo wako. Mpaka hapo, mimi ninani ukilinganisha na Sarah?”

"Ni kweli. Lakini yote hayo yamepita…” Alvin hakujua la kufanya.”Huwezi kumwonea wivu mtu aliyekufa.”

Hakujua kamwe kuwa aliita jina la Sarah katika ndoto zake. Kwanini hakuweza kukumbuka lolote kati ya hayo? Alinyoosha mkono kuushika mkono wa Lisa, lakini aliutupa kwa ukali. Lisa alimtazama kwa mchanganyiko wa chuki, kukatishwa tamaa, na hasira.

"Hata mimi nilijua yamepita pia, lakini uamuzi wako wa kumweka Maurine karibu nawe unaniambia kuwa sitakuwa bora zaidi ya kumbukumbu ya mzimu, au hata kumkaribia tu." Lisa alimnyooshea Maurine kidole kinachotetemeka. “Ni mambo mangapi ya kuchukiza umefanya naye kitandani kwangu nikiwa sipo kila siku? Je, hakuna chumba kingine ndani ya nyumba? Toka Maurine aingine ndani kwetu hata hisia zangu huzijali tena. Kila anachokuambia unafuata tu.”

"Bi. Kimaro, unazungumza nini?" Akiwa na huzuni, Maurine alisema, “Wewe pekee ndiye Alvin anakujali.”

"Nyamaza! Hakuna mtu anayeweza kujifanya zaidi yako. Uliwadanganya wanaume wote na kufanya kila kitu kionekane kama ni kosa langu.” Lisa akashusha pumzi ndefu. “Lakini haijalishi. Unaweza kuwa na Alvin ukitaka kwa sababu mimi sijali tena.”

"Ikiwa hunijali, basi unamjali nani?" Alvin alimkandamiza mabega. Mwili wake ulimuuma kana kwamba anakosa hewa. “Sijafanya chochote na Maurine. Ninamweka karibu tu… kwa sababu… kwa sababu yeye ni binamu ya Sarah, na nilifikiri ni lazima nimtunze. Sivutiwi naye hata kidogo.”

"Sawa, kumtunza vipi huko mpaka kwenye kitanda chetu pia?" Lisa alicheka.

'Sikufanya hivyo.” Alvin alifoka kwa ukali, “Mbona huniamini?”

“Kwa sababu hustahili kuaminika.” Lisa akatikisa kichwa. Alihisi amani zaidi baada ya kutoa hisia zake alizozivumilia kwa muda mrefu. “Kwa sababu ya Sarah umeamua kulala chumbani kwetu na binamu yake. Kwa sababu ya Sarah umeamua kumtetea na kumlinda kaka yake. Kwa sababu ya Sarah umeamua kumchukia Charity na kuikandamiza kampuni yake. Ni nini kingine kitafuata katika siku zijazo?"

Sura ya: 247

“Lisa, acha. Twende nyumbani.” Alvin akazidi kufadhaika jinsi Lisa alivyokuwa mkali.
Hata hivyo, Lisa alibakia kusimama kama ameota mizizi chini. Alimwangalia na kummwagia tabasamu la kejeli. “Kwa sababu ya mpenzi wako wa zamani, siwezi kuwa rafiki na Charity. Oa tu Maurine ikiwa huwezi kuacha kumfikiria mwanamke huyo. Nipo radhi tupeane talaka.”
“Umemaliza? Wewe ndiye mtu ninayekupenda sasa." Kichwa chake kilikuwa kinamuuma sana. Kwa kweli hakujua ni nini kingine angeweza kusema ili kumshawishi.
"Ndio, unanipenda, lakini sio kama unavyompenda Sarah." Lisa alihema kwa uchungu. “Ikiwa Maurine, ambaye anafanana na Sarah, anaweza kuchukua nafasi yangu leo, basi inakuwaje mtu mwingine anayefanana naye zaidi atakapotokea siku moja? Mimi ni mtu ambaye anaweza kubadilishwa wakati wowote, na sitaki kuendelea na uhusiano wa aina hii tena. Samahani. Labda nisiseme hivi kwa sababu ya hali yako, lakini siwezi kukaa kando yako. Jitunze.”
“Hapana, Lisa, wewe ni wa kipekee na hakuna anayeweza kuchukua nafasi yako. Usiniache.” Alvin alimkumbatia kwa nguvu huku akiingiwa na hofu mithili ya mtoto anayekaribia kupoteza mali yake aipendayo.
Alikuwa amepitia upweke na uchangamfu wa upendo, lakini Lisa ni mwanamke pekee aliyebaki kando yake. Angewezaje kuishi ikiwa angeondoka?
"Acha. Mimi sio muhimu sana kwako. Baada ya yote, marafiki zako wanaweza kunifokea na wewe unawaangalia tu, na unaweza kunifungia wakati wowote upendao. Na nikihitaji marafiki mpaka nipate idhini yako… Sahau.” Lisa alijaribu kuunyoosha mkono wake kutoka kwake, lakini Alvin alikataa kuuachia.
“Usiende. Siwezi kuishi bila wewe. Nitamruhusu Maurine aondoke, sawa? Kisha tunaweza kurejea jinsi tulivyokuwa tunaishi hapo awali.” Alvin aliogopa sana. Hakuwahi kufikiria kuwa hivyo ndivyo itakavyoisha kwa Lisa.Kwanini watengane kwa sababu ya mabishano madogo?
"Bwana mkubwa naomba umwachie aende." Charity akasogea mbele kumsaidia Lisa.
"Charity, yote ni kwa sababu yako, sawa?" Akamtazama kwa chuki. "Unanichukia kwa kuibania kampuni yako nafasi ya ushirikiano na Alvinarah, kwa hivyo unalipiza kisasi kwa njia hii, sivyo?"
“Bwana Mkubwa, unawaza mambo kupita kiasi. Lisa sasa ni rafiki yangu. Kama marafiki yake, naweza kusema kwamba wewe na marafiki zako mmekuwa mkimtendea isivyo haki.” Charity alijibu kabla ya kumuongoza Lisa.
Pamela alifuata mara moja. Kisha wote watatu wakaingia kwenye gari na kuondoka.
Moyo wa Alvin ulipasuka sana huku akilitazama gari lile likipotea kwa mbali. Alitamani sana kuikimbia lakini ghafla, kichwa chake kilikuwa na maumivu makali, akaaanguka chini na kuzimia!
•••
Katika klabu ya usiku, Pamela aliagiza vinywaji vingine kumi na mbili, na wote watatu wakaagiza chakula.
Ingawa walikuwa wamezungumza mambo mengi, Lisa hakuweza kuacha kunywa pombe akijaribu kusahau kuhusu mateso ya Alvin. “Charity, naweza kukuuliza swali? Kwanini Alvin na marafiki zake wanakuchukia sana? Nimekufahamu kwa muda mfupi tu, lakini naweza kusema kwamba wewe ni mtu mzuri.”
"Ndio, umechukua maneno mdomoni mwangu Hata mimi nilitaka kumuuliza hivyohivyo." Pamela alitikisa kichwa.
Charity alionekana mwenye huzuni. "Labda ina uhusiano fulani na Sarah. Mama yangu alipoanza uhusiano na Langa Njau wakati huo, walimwona mama yangu kama mvurugaji tu wa familia ya Langa na hata kuwafanya wengine wanichukie pia nilipozaliwa. Nilipokuwa binti nilikutana na Chester nikiwa shule ya sekondari tukawa wapenzi, lakini haikuchukua muda tukaachana. Wote watatu walifikiri kwamba mimi nilikuwa sababu ya Sarah kukosa raha. Waliamini kwamba niliondoa ushirika na upendo wa baba ambao ulikuwa haki yake na kaka yake. Lakini siku zote nimekuwa nikitegemea juhudi zangu na uwezo wangu kufikia hapa nilipo leo.”
Lisa alipata picha halisi. “Nimegundua kitu, Alvin anawachukia sana watoto wa nje ya familia. Anaamini ni chanzo cha kuvuruga furaha ya familia. Kwa hiyo na wewe anakuchukia mpaka kwenye damu yake kwa sababu anaamini uliharibu furaha ya Sarah.” Kwa namna fulani, hii ilimkumbusha Lisa kuhusu Alvin na Jack na ndiyo maana hawakupatana maisha yao yote.

Baada ya sekunde chache, Charity alisema, "Hiyo ndiyo sababu kubwa. Alvin alimpenda sana Sarah na aliwachukia wote waliomuudhi. Kama Sarah atafufuka leo, hakika Alvin atachagua kurudi kwake na kukuacha wewe." Lisa alisikiliza maneno hayo huku akinywa bia kimya kimya.
•••
Katika hospitali. Alvin akarejewa na fahamu.
Mkono wake ulikuwa umeunganishwa na dripu. Akapepesa macho mara kadhaa. Aliweza kusikia sauti ya Rodney kutoka chumba kingine.
“Nimesema tangu mwanzo kwamba Lisa si mtu mzuri. Alvin tayari ni mgonjwa sana, lakini bado anasisitiza kutaka talaka. Hamjali hata kidogo.”
“Punguza sauti yako. Je, akiamka na kukusikia?” Chester alimtahadharisha.
“Nimekosea? Hana shukrani kwa kila kitu ambacho amempa, na bado anajaribu kushindana na mtu aliyekufa?” Rodney alizidi kulalamika.
“Bwana mkubwa, umeamka." Maurine, ambaye alikuwa ameketi kando yake, alipiga kelele alipomwona Alvin anafungua macho yake.
Mazungumzo ya koridoni yalisimama. Dakika kadhaa baadaye, Rodney na Chester waliingia chumbani kwa fujo.
"Nionyeshe hizo hati za talaka." Alvin alinyoosha mkono wake.
Rodney almkabidhi baada ya kusitasita. Alvin aliichunguza hati hiyo, ambayo ilisema kwamba Lisa hataki chochote. Alikuwa tayari kuacha ndoa bila chochote ilimradi tu akubali kusaini karatasi hizo. Vidole vyake vilishika karatasi hizo na kuzichanachana mara moja.
Kila mtu alichukulia jambo hilo kwa njia tofauti, lakini Maurine alijaribu kumfariji. “Bwana Mkubwa, usijali. Bi. Mdogo anafanya hivi kwa hasira tu. Atajuta baada ya kutulia.”
“Unatakiwa kuondoka.” Sauti ya Maurine ilimpa maumivu makali ya kichwa.
Rodney alisimama kumtetea kwa hasira. “Alvin, unasemaje? Lisa hata hajaja kukuangalia baada ya kuzimia. Ni Maurine ndiye aliyekuleta hapa.”
"Kwa hiyo? Unataka nimuoe yeye badala yake?” Alvin akanyanyua macho yake kwa jeuri. “Kwanini usimuoe wewe kwa kuwa unapenda kumtetea sana?” Rodney alishindwa cha kusema.
Machozi yalitiririka mashavuni mwa Maurine aliposema katikati ya kwikwi, “Bwana Shangwe, tafadhali acha kubishana naye. Najisikia vibaya sana. Bwana Mkubwa asingeingia kwenye vita hivi na mke wake kama si mimi. Ni bora niondoke tu." Maurine akatoka nje.
Alvin alishika midomo yake bila kutoa neno zaidi.
"Maurine, nisubiri." Rodney alipumua, kisha akamkimbilia Maurine.
Chester alisugua kichwa chake kama ishara ya kukosa cha kusema. "Utafanya nini?"
“Sitamruhusu Lisa aondoke upande wangu. Nina hakika kwamba yeye ndiye mtu ninayempenda.” Alvin aliweka msimamo.
Matukio ya kabla ya kuzimia yalimjaa akilini, na kumfanya kuchanganyikiwa. "Ni kosa langu. Labda… Sikupaswa kumruhusu Maurine abaki. Lakini sikufikiria kwamba Lisa angeniwazia mabaya zaidi. Anadai alinikuta kitandani na Maurine, lakini si kweli.”
"Labda Charity alikuwa akimpotosha." Chester alikunja uso.
“Charity Njau…” Alvin alikunja ngumi. “Sitakuwa mwema kwake tena. Nitahakikisha familia ya Njau inafilisika ndani ya mwezi mmoja.”
“Sikubaliani. Lisa atakuchukia zaidi akijua,” Chester alisema. "Familia ya Njau tayari iko mwisho wa wakati wao, itajifia yenyewe tu. We achana nayo."
“Sawa.” Alvin alihisi kichwa chake kuanza kumuuma tena. “Wewe ni mzoefu zaidi katika hili. Niambie jinsi ninavyopaswa kumrudisha.”
"Subiri, nitakutumia vidokezo vichache vya siri." Chester alimtumia mafaili machache kwenye simu. Alvin aliyapitia siku nzima.

Sura ya: 248

Usiku, Shangazi Yasine alikuja na chakula cha jioni. Hisia tata ilijidhihirisha katika moyo wa Alvin alipoona bendeji kuzunguka kichwa cha Aunty Yasmine. “Unapaswa kupumzika nyumbani. Nitamwambia Hans atafute mlezi mwingine…”
“Si sawa, Bwana Mkubwa. Kukuona ukiwa katika hali hii inanitia wasiwasi.”
Alvin akatenganisha midomo yake kutaka kusema kitu lakini akabadilisha mawazo yake. Akifikiri kwamba Aunty Yasmini angeogopa. Aliishia tu kusema kwa upole, “Pole…”
“Sijambo, lakini Bibi Mdogo hajakuelewa,” alisema. “Nyinyi mligombana kimakosa usiku huo, na sikupata nafasi ya kukueleza. Kweli, Bi. Kimaro hakumpiga Maurine bila sababu. Alikuja nyumbani akakuona wewe na Maurine mmelala kwenye kitanda kimoja. Kama ningekuwa mimi, nisingeelewa pia.”
"Nini?" Alvin alimtazama mwanamke huyo kwa macho yake meusi. "Kwanini Maurine alikuwa kitandani kwangu?"
Alijibu kwa unyonge, “Ulirudia usiku siku hiyo. Ulimshika mkono wake mara tu alipojitokeza, hata baada ya kukupeleka kitandani, ulisisitiza abaki na wewe. Bwana Mkubwa … Jnaogopa kusema lakini ulimkosea Bibi Mdogo!”
Alvin alichanganyikiwa. Ina maana alimshika mkono Maurine na kwenda naye chumbani kwake? Hakuwa na kumbukumbu yake hata kidogo.
Kisha akaendelea. “Nilitaka kumzuia Bi. Kimaro usiku ule baada ya kurudi, lakini aliwahi kukimbilia ghorofani na kuwakuta katika hali hiyo. Alilalamika na kuanza kugombana na MAurine lakini ukamuona kama mkorofi. Ulimfungia hata kwenye chumba cha upweke baada ya hapo. Naamini alishtuka sana.”
“Mimi… nilimfungia ndani ya chumba?” Hilo nalo lilimshangaza. Hakukumbuka hata kama waligombana.
"Hiyo ni kweli. Bi. Kimaro alipiga kelele za kuomba msaada usiku mzima. Alivunjika moyo sana. Alishangaa kwamba ulimfungia ndani ya chumba cha upweke baada ya kile wanafamilia wako walimfanyia mara ya mwisho.”
Hisia nzito katika kifua chake ilimsababishia maumivu makali. Alikuwa amefanya nini? Kichwa chake kilianza kumuuma tena.
Akiwa amechanganyikiwa, Aunty Yasmine haraka akachukua mto na kuuweka nyuma ya shingo yake. Hata hivyo, maumivu ya kutoboa moyo yalimzuia asilale usiku wote huo.
•••
Asubuhi. Lisa aliingia ofisini kwake. Hans alikuwa akimngoja nje ya ofisi yake kwa muda mrefu. "Bibi mdogo, haya ni majibu ya vipimo vya DNA kati ya Melanie na Bw. Joel Ngosha ambayo ulitaka nishughulikie hapo awali."
Hilo lilimshangaza Lisa. Alikuwa amekosana na Alvin, na hivyo hakutarajia msaidizi wake angeendelea kumsaidia.
"Asante." Alipokea hati kabla ya kusema, “Hii itakuwa mara ya mwisho kuomba msaada wako. Tafadhali acha kuniita Bibi Mdogo baada ya hapa. Huyo si mimi tena.”
"Wewe ni bosi wangu mradi tu umeolewa na Bwana Mkubwa." Akakunja uso kwa wasiwasi. “Kwa kweli, Bwana Kimaro anajali sana kuhusu wewe. Juzi usiku baada ya nyie kutoka kwenye baa, alizimia na hakurudiwa na fahamu hadi jana. Hayupo vizuri kwa sasa. Jana usiku, yeye…”
“Unapaswa kumtafuta Maurine. Au tembelea kaburi la mpenzi wake wa zamani.” Kuzungumza juu ya Alvin kuliharibu hisia zake. Watu wengi waliokuwa karibu na Alvin waliendelea kumwambia kwamba anamjali, kwamba hali yake ingezidi kuwa mbaya bila yeye. Aliwaamini. Hata alijishusha chini ili kuwafurahisha watu wa familia ya Kimaro. Lakini, alipata nini mwishowe? Unyonge na uongo.
“Bwana Mkubwa hampendi Maurine…”
“Hans, acha. Mimi si shirika la kutoa misaada.” Alimkatiza bila kusita, na chuki machoni mwake ilielezea kila kitu.
Hans alishindwa cha kusema. Alishusha pumzi baada ya kuingia kwenye lifti. Laiti angejua hivyo ndivyo mambo yatakavyokuwa, angemshawishi Alvin asimuajiri Maurine hapo mwanzo.

Lisa alivumilia hisia ya kichefuchefu hadi akakimbilia kwenye chumba cha kunawia ili kutapika. Alikuwa amekunywa sana jana yake hadi tumbo likaanza kumsumbua. Baada ya hapo, aliendelea kusoma hati iliyokuwa mkononi mwake.
'Haihusiani' ilionekana mbele ya macho yake kwa maneno mekundu na ya ujasiri. Hiyo ilimshangaza sana Lisa. Melanie hakuwa binti wa Joel. Hata hivyo, Joel alimtelekeza mama yake ili amuoe Nina zamani kwa sababu Nina alikuwa na ujauzito wa Melanie.

Kwa maneno mengine, Nina alikuwa amemdanganya Joel zaidi ya miaka ishirini iliyopita. Lisa akaweka hati hiyo kwa uangalifu. Hizi zilikuwa habari za kushtua lakini wakati wa kuziweka hadharani ulikuwa bado.
Akiwa anawaza hayo tu, Daktari Angelo akampigia simu. “Bi Jones, sehemu niliyokuwa nakaa jana usiku iliteketea kwa moto ghafla. Kwa bahati nzuri, ulinikumbusha kuwa ninaweza kuwa katika hatari muda wote, kwa hivyo nimekuwa nikitoka kwa siri kupitia mlango wa nyuma baada ya kufika nyumbani. Utabiri wako ulikuwa sahihi sana."
“Hilo ni la kushukuru Mungu. Tafadhali mwagize msaidizi wako atangaze kwamba ulikufa kwa moto. Kwa sasa, tafadhali endelea kumhudumia baba yangu kwa siri.”
Lisa alitabiri kuwa Damien angeweza kumdhuru daktari huyo maarufu. Kwa bahati nzuri, Daktari alizingatia ushauri wake na akaokoka. Damien na wengine lazima wangeamini kuwa Daktari Angelo alikuwa amekufa kwa muda huo.
•••
Katika makazi ya familia ya Ngosha, Nina alitabasamu kwa furaha baada ya taarifa za kifo cha daktari. “Kwa kweli ni habari njema. Joel hawezi kurejewa na fahamu hivi karibuni baada ya kifo cha Dokta Angelo. Lisa ni mjinga sana kuendelea kuhangaika na baba yake. Lazima atakuwa akilia na moyo wake sasa hivi.”
Melanie alichanganyikiwa. “Mama unamaanisha nani? Baba yangu?"
"Ndio, baba yako yuko njiani kuja hapa ili nyinyi wawili mkutane rasmi. Tutalazimika kumtegemea katika siku zijazo." Nina alimpigapiga bintiye kichwani. Ijapokuwa alimdharau mwanaume huyo miaka yote, ilimbidi akubali kwamba aliweza kumpa kile anachotaka, tofauti na Joel ambaye hakuacha kumfikiria Sheryl.
Melanie alimtazama kwa macho ya kutarajia. Dakika chache baadaye, mwanamume mmoja aliingia akisukumwa kwa kiti cha magurudumu. Melanie alipigwa na butwaa kumwona, lakini hatimaye, alifikiri kwamba yote yalikuwa ya maana. Si ajabu alifanana na Joel ingawa hakuwa baba yake halisi. Isitoshe, Damien alikuwa amemdekeza tangu alipokuwa mtoto. Haijalishi angefanya nini, angemsaidia kila wakati.
“Melanie, njoo huku. Mimi ni baba yako.” Damien alimwashiria.
“Bam’dogo Damien… ni wewe?” Alitembea kuelekea kwake kwa kusitasita.
Alikunja uso, na Nina akaeleza hali hiyo haraka. “Kwa kweli, baba yako amekuwa akinipenda tangu miaka ishirini au zaidi iliyopita. Lakini sikujua vizuri zaidi na kuweka matumaini yangu yote kwa Joel. Kabla Joel hajanioa, mimi na baba yako tulikuwa tayari tumekuweka tumboni mwangu. Baada ya hapo, niliwaambia kuwa mtoto wangu ni wa Joel ili anioe. Miaka yote, Damien amekuwa akitutunza. Bila yeye, Lisa angekuwa na udhibiti kamili wa Ngosha Corporation kwa sasa.”
“Ni kweli bam’dogo?” Melanie alikuwa katikati ya mshangao.
“Acha kuniita bam’dogo Melanie. Niite baba badala yake.” Alishika mikono ya Melanie. "Nitakupa kilicho bora zaidi."
“Asante, Baba.” Alimzungushia mikono yake shingoni. Damien alimjali sana kuliko Joel. “Baba, namchukia Lisa. Nataka afe.”
Nitamfanya yeyote anayemdhulumu binti yangu alipe kwa matendo yake. Lakini kipaumbele kwa sasa ni kuharakisha harusi yako na familia ya Campos,” alisema. "Familia ya Kimaro haitakuwa na nafasi katika jiji hili mara tu familia za Ngosha na Campos zitakapoungana tena."

Sura ya: 249

Melanie alikuwa ameduwaa. “Baba, unapanga…”
“Nataka uwe mwanamke mashuhuri wa Nairobi. Utatafutwa na kuonewa wivu na kila mtu.” Macho ya Damien yalijaa kujiamini. "Siku hiyo itakuja hivi karibuni."
Melanie aliwazia tukio hilo, na mwili wake ukatetemeka kwa msisimko.
•••
Saa tano usiku, Lisa alirudi nyumbani baada ya kutoka kutazama sinema. Alipofungua mlango, alihisi kuwa kuna kitu hakiko sawa. Harufu ya waridi sebuleni ilikuwa kali sana. Kulikuwa pia na jozi ya viatu vya kiume kwenye mlango.
Moyo wake uliruka mapigo. Akawasha taa. Maua mengi mekundu yalikuwa yamepangwa katika umbo la moyo katikati ya sebule. Alvin alikaa kwenye sofa la kitambaa huku akiwa amevalia fulana nyeusi iliyomechishwa na suruali nyeusi ya jeans. Hata nywele zake zilikatwa katika mtindo wa kiduku, ambao kwa kipindi hicho ulikuwa ukivuma katika tasnia ya burudani. Mavazi yake pamoja na sura yake, vilimfanya aonekane tofauti kabisa na alivyozoeleka.
Lisa karibu hakuweza kumtambua. Huyo alikuwa Alvin? Kwanini alionekana hivyo siku hiyo? Alionekana kama mvulana aliyetoka tu shuleni, ambaye alikuwa akimtongoza mpenzi wake kwa mara ya kwanza.
“Ninaonekana vizuri?” Alvin alimuona Lisa akimshangaa, akafunua midomo yake kuachia tabasamu zito. Ilionekana kama kidokezo cha siri cha Chester kilikuwa kimefanya kazi.
Wanawake huwapenda wanaume ambao hujua namna ya kubadilisha hisia zao muda wowote. Mwanamume ambaye anaweza kumchukiza na kumwonyesha mapenzi. Mwanamume anayeweza kumliza na kumfanya acheke. Mwanamume anayeweza kumhudhunisha na kumfurahisha. mwanaume anayeweza kucheza vizuri na hisia za mwanamke, hatakosa penzi la mwanamke ampendaye.
Ingawa hakuwahi kufanya hivi hapo awali, alikuwa tayari kubadilisha mtazamo wake mara moja moja kwa ajili ya Lisa tu.
Lisa alimsoma kwa umakini na kukunja uso. "Maurine anakutunza au anakuharibu ubongo?"
“Una wasiwasi na mimi?” Alvin alizidi kutabasamu. "Ninajisikia vizuri zaidi baada ya kukuona."
"Hapana, umekata nywele zako kwa mtindo huu wa kitoto na hata ukaingia kwenye nyumba ya mtu mwingine na kujaza rundo la takataka. Hii haimaanishi kwamba umekuwa mgonjwa zaidi?” Lisa akacheka kwa kejeli. “Nadhani vitu hivi hujavileta mahali sahihi. Ungepeleka mbele ya kaburi la Sara.”
Alvin alijikaza. Alikuwa ameishi kwa miaka 30, lakini ilikuwa ni mara ya kwanza kuhisi kana kwamba alikuwa anapigwa kofi usoni la mwanamke.
“Lazima uwe mwendawazimu. Unawezaje kujaza takataka zote hizi kwenye nyumba yangu?" Lisa aliumwa na kichwa kwa kuangalia maua yale. Alitumia siku nzima kusafisha nyumba hii mpya, lakini alikuta uchafu mwingine umetapakaa nyumba nzima.
Alvin alijisikia vibaya ghafla kutokana na kejeli za maneno ya Lisa. Alihisi moyo wake unakuwa mweusi kama umepakwa masinzi. Alikuwa ametumia muda mwingi kupanga maua yale, na mikono yake ilichomwa na miiba kila mahali. Lakini juhudi yake ilionekana kama utopolo tu kwa Lisa.
“Kwanini upo hapa?” Lisa alimtazama bila furaha. “Umeingiaje? Tafadhali ondoka mara moja, la sivyo nitakuripoti kwa polisi kwa kosa la kuvamia kwenye nyumba ya mtu bila kukaribishwa.”
“Sawa, unaweza kuendelea na kuniripoti. Nitawaonyesha polisi hiki kitu.” Alvin akatoa cheti chao cha ndoa. “Sisi bado ni mume na mke, kwa hivyo nina haki za kisheria kukaa hapa."
Lisa alikosa la kusema. Alikaribia kusahau kwamba Alvin alikuwa wakili bora zaidi nchini Kenya.
“Kwa hiyo unataka kumleta Maurine na kuwa na wanawake wawili wakimtumikia mume mmoja?” Lisa alidhihaki, "Naona huu ni utaratibu wa kawaida wa matajiri wakubwa wa hapa Nairobi ambapo mke halali na mchepuko huishi pamoja katika nyumba moja."
Alvin alisimama mara baada ya kusikia maneno yake ya kejeli. Umbo lake jembamba lilikuwa kama la mwanamitindo, lakini macho yake yalikuwa ya damu. "Nilimtaka Maurine aondoke tayari. Shangazi Yasmine aliniambia kuwa ulimpiga usiku ule kwa sababu nilikuwa nimelala kitandani na kumshika mkono Maurine. Samahani kwa kuwa sikukuelewa. Nimekuja kukuomba msamaha.”
Alvin akaanza kufafanua jambo moja baada ya jingine.

"Kuhusu Sarah Wonderland Park, ni suala lililotokea muda mrefu uliopita. Sikujua tukio la fataki la saa mbili usiku kila Ijumaa kama bado linaendelea. Siku zote ni msimamizi mkuu wa bustani hiyo ndiye ambaye alisimamia tukio hilo. Alisema fataki hizo zimekuwa kivutio cha watalii, lakini nimemwambia asitishe.”
“Kuhusu kampuni, nilikuwa bado sijakutana na wewe nilipoipa jina la Alvinarah. Hata hivyo, nitaifanya KIM International na Alvinarah ziunganishwe haraka iwezekanavyo. Baada ya hapo, hakutakuwa tena na kampuni ya Alvinarah.”
Alvin akamsogelea Lisa hatua kwa hatua, huku macho yake yakiwa yamejaa mahaba. “Lisa, rudi mpenzi. Siwezi kuwa bila wewe." Aliinamisha kichwa chake na kumbusu midomo yake kwa upendo.
Lisa alikuwa kama ameyeyukia hewani wakati huo. Hakukuwa na shaka kwamba sura, hadhi, na sauti ya Alvin ingeweza kumvutia kwa urahisi mwanamke yoyote. Hata hivyo, pumzi yake ilipokaribia kukata, Lisa alirudi kwenye fahamu zake na kupiga hatua chache nyuma. Alimtazama Alvin kwa tahadhari.
"Nimesikia hadithi zako nyingi sana. Umewahi kuniambia maneno mengi mazuri pia, lakini ulinichukuliaje? Maurine alipojitokeza kwako akili yako ikahama kabisa, ulifikiri ninamnyanyasa. Marafiki zako wote wananifikiria kama mtu mbaya ambaye ana wivu hadi kwa mtu marehemu, na ndiyo unaowasikiliza na kuwaamini. Rodney alinihakikishia kuwa Maurine hawezi kuondoka, mimi nimechoka kabisa!”
Ukimya mfupi ulipita kisha Lisa akaendelea.
"Kulikuwa na tukio na Thomas pia. Ulijua kuwa alikuwa ameoza kabisa, lakini ulimsaidia tena na tena. Mwishowe, Zigi alikuja kuniumiza kwa kisu. Hilo lilisababisha Kelvin kupoteza figo na ilinibidi kubeba hatia…”
Alvin alikodoa macho. “Kwa hiyo unafikiri kwamba Kelvin aliumia kwa sababu yangu?”
“Kumbe!” Lisa alicheka. “Kama si Kelvin, ningekuwa nimekufa. Ningekufa kwa sababu ya kaka wa mpenzi wako wa zamani." Alisema kwa kejeli na kupanda juu. Akiwa amekasirika sana, alifunga mlango na kuingia bafuni kuoga.
Baada ya kutoka kuoga, alimuona Alvin aliyetakiwa kuwa nje akiwa amejilaza kitandani kwake. Alikuwa amelala fofofo huku akikumbatia mto wake na kujifunika blanketi lake.
Lisa alikuwa karibu kupandwa wazimu. Mtu huyo aliwezaje kuingia chumbani kwake? "Alvin, ondoa wazimu wako hapa." Lisa akainua blanketi.
Alipoona Alvin hajavaa chochote chini ya blanketi, uso wake ulibadilika kwa hasira na aibu. “Mbona umevua nguo?”
Akiutazama uso wa Lisa wenye haya, midomo ya Alvin ilijipinda na kutabasamu. "Nililazimika kuvua ili kulala, bila shaka. Hukuniandalia nguo zozote za usiku pia.”
Lisa alizidi kupandwa na hasira za mshangao. Hakuwa na aibu kiasi cha kujipenyeza ndani ya nyumba yake, akaingia chumbani kwake na kulala kitandani kwake na kumlaumu kwa kutomwandalia nguo za kulalia?
“Kuwa mstaarabu na usinisumbue. Ninaweza kulala usingizi tu kwa kuvuta harufu yako. Sijalala kabisa kwa siku mbili.” Alvin alichukua blanketi na kujifunika.
Lisa alikasirika kiasi kwamba alitamani apasuke. Alijiona hana nguvu. “Alvin, unataka nini? Maurine hakutoshi sasa? Mbona bado unaning’ang’ania?”
“Tayari nimemuamuru aondoke.” Alvin akabinya midomo yake pamoja na kusema, “Ikiwa unanichukia kwa kukufungia kwenye chumbani peke yako kwa usiku mmoja, unaweza kunifungia chumbani pia.”
Lisa alifoka, “Kwanini nikufungie? mimi si mgonjwa kama wewe.”
Mgonjwa? Neno hilo lilijirudia chumbani. Uso wa Alvin ulipauka papo hapo. Alionekana kana kwamba ni mtoto. Lisa aliuma mdomo. Hakutaka kuwa na moyo dhaifu na kumuonea huruma hata kidogo.
Alvin hakusema chochote. Alinyanyuka na kutembea kwa huzuni hadi chumba kingine kabla ya kufunga milango. Lisa hakumjali na kumwacha aendelee na maigizo yake.

Sura ya: 250

Lisa aliposhuka chini ili kuchota maji, ghafla alikumbuka tukio la yaya wa Alvin kumfungia chumbani alipokuwa mdogo…
Glasi mkononi mwake ilidondoka chini na kuvunjika sakafu. Alikimbia ghorofani na kufungua chumba alichoingia Alvin.
Mwili wa Alvin ulikuwa umejikunja ndani ya kabati na kuwa kama mpira, na kichwa chake kilizikwa kwenye magoti yake. Alikuwa akitetemeka kama mbwa aliyenyeshewa mvua.
"Alvin, toka nje." Lisa alijaribu kumtoa lakini akashindwa.
“Nasikia baridi sana… Usinipige…” Alvin alikuwa akiziba masikio yake kwa nguvu zake zote.
Lisa hakutaka kumuonea huruma, lakini moyo wake ulimshinda na kujikunja kwa maumivu wakati huo.“Sitakupiga. Usilale humu twende kitandani. Kila kitu kitakuwa sawa.” Lisa alimkumbatia na kumpigapiga mara kwa mara.
Mwili wake ulipoacha kutetemeka, alimsaidia kumkokota hadi kitandani, akamlaza na kumfunika blanketi. Hata hivyo, Alvin alimshika mkono kwa nguvu. Hakuweza kumwacha aondoke hata kidogo.
Lisa alijaribu kuutoa mkono wake mara kadhaa lakini akashindwa. Hatimaye, hakuwa na chaguo ila kulala upande mwingine. Awali alipanga kwenda kulala chumba cha wageni baada ya yeye kulala, lakini yeye mwenyewe alipitiwa na usingizi kwa sababu alikuwa amechoka sana.
Hakujua alikuwa amelala kwa muda gani. Katika hali ya ukungu, alihisi mtu akibusu midomo yake kwa hamu. Wimbi la msisimko lilitanda kwenye ngozi yake.
Alifumbua macho yake ghafla. Alipomuona Alvin akiwa juu yake, alimsukuma kwa hasira. “Nani amekuruhusu kunibusu?”
“Lisa, hakika una wasiwasi na mimi. Ulilala kando yangu jana usiku. Unanijali.” Alvin alitabasamu na kumtazama kwa furaha. "Hebu tufanye kidogo."
"Si Maurine alikukataza mpaka umalize dozi?" Lisa akakumbuka tukio la Maurine akiwa ameketi juu yake chumbani. Alihisi kichefuchefu na kukimbilia chooni kutapika.
Alvin alimfuata chooni akiwa na wasiwasi. Lisa alimtazama baada ya kutapika na kutaka kuendelea kumbusu. “Usinibusu, nahisi kichefuchefu sana nikiguswa tu na wewe.”
Macho ya Alvin yaligeuka kuwa mabaya mara moja. Kwanini alimchukia kiasi hicho? Ndiyo, alikuwa na nafasi kwa Sarah moyoni mwake, lakini hakuwahi kufanya jambo lolote lililomsaliti Lisa. Akakunja uso kisha akageuka kuelekea chini.
Lisa alishuka baada ya kufanya usafi. Harufu ya mayai ya kukaanga ilikuwa ikitoka jikoni.
“Sandwichi, maziwa, na mayai ya kukaanga. Karibu tule.” Alvin alikuwa amevaa aproni na kwa kushangaza alitengeneza seti mbili za kifungua kinywa. Kutokana na mwonekano wake, alikuwa akijaribu kumfurahisha Lisa.
Lisa karibu alitaka kufungua madirisha na kuchungulia nje ili kuona kama jua lilikuwa limechomoza kutoka magharibi badala ya mashariki siku hiyo. Walikuwa pamoja kwa muda mrefu sana, lakini aliwahi kumtengenezea chakula mara moja tu—na kilikuwa na ladha mbaya sana.
Ingawa kifungua kinywa hakikuonekana kutosha kumvutia kula, alikuwa na njaa kwani alikuwa ametoka kutapika. Hata hivyo, hakutaka kula.
"Samahani, lakini mimi siwezi kula aina hii ya kifungua kinywa." Alikataa kwa kiburi na kuelekea mlangoni.
Alvin alijisikia kama sehemu ya moyo wake imeondolewa kwa kuambiwa jibu kama hilo. Lakini akakumbuka hakuwa na haki ya kukasirika kwani alikuwa amemwambia hivyhivyo wakati alipomwandalia kifungua kinywa kwa mara ya kwanza huko nyuma. Mwanamke huyo alijua jinsi ya kuweka kinyongo.
Kuona kiamsha kinywa ambacho Alvin alimtayarishia hapo awali kulimfanya awe na njaa. Aliendesha gari hadi kwenye mgahawa wa kifungua kinywa. Alisikia kutoka kwa Pamela kwamba chakula kwenye mgahawa huo hakikuwa kibaya. Alvin alimpigia simu Hans na kumwambia amfuatilie Lisa kimyakimya, na endapo ataona amekutana na Charity ampigie simu.
Lisa alipoanza tu kula baada ya kuagiza kifungua kinywa chake, Melanie na Jerome waliingia kwenye mgahawa huo wakiwa wameshikana mikono.
Meneja wa mgahawa aliwafuata wote wawili kwa makini. “Bwana Campos, Bi Ngosha, mngependa kuketi wapi?”
Melanie alitazama huku na kule na kugonganisha macho na Lisa. Macho yake yakaangaza. Alimvuta Jerome na kwenda mara moja kuelekea kwa Lisa.

“Oh, huyu si mke wa Bwana Kimaro? Kwanini unakula kifungua kinywa hapa peke yako? Yuko wapi Bwana Mkubwa Kimaro ambaye anakupenda sana?" Melanie alitazama pande zote kuangaza.
Lisa alikunja uso. Alikuwa na kifungua kinywa kizuri, lakini walipotokea tu hao watu alihisi kama inzi wameingia kwenye bakuli la supu yake ya mbuzi.
Msimamizi wa cafe aliogopa. "Bi Kimaro, samahani…"
“Huna haja ya kumwomba msamaha Bw. Cameron.” Jerome alitoa tabasamu zito. "Nadhani hatakuwa Bi Kimaro tena hivi karibuni. Nijuavyo, Bi. Jones amefukuzwa nyumbani kwa Bwana Kimaro. Nilisikia kwamba hata alitafuta nyumba ya kununua na kuhamia kwa haraka siku chache zilizopita.”
Bwana Cameron alielewa maneno yake na hapohapo heshima aliyokuwa nayo hapo awali kwa Lisa ikatoweka. Mtazamo alioutoa kwa Lisa haukuwa wa heshima tena, hata ulijawa na dharau.
"Bwana Campos, una taarifa sahihi kabisa." Lisa alijifuta mdomo na kumtupia macho makali Jerome. "Unajua zaidi kuliko vyombo vya habari. Inawezekana kwamba ulikuwa na jasusi uliyemwajiri ili kunipeleleza?"
Jerome alifoka. “Nani asiyejua kuwa Alvin alileta binamu wa mpenzi wake wa zamani nyumbani siku chache zilizopita ili amtunze? Ni kwa sababu ameona wewe hufai na unazidi kumpandisha wazimu wake.”
“Umekuwa mjinga sana.” Sauti ya Melanie ilijaa kejeli. “Alvinarah, Alvinarah, haimaanishi Alvin na Sarah? Angalia uso wako wa kutisha. Ulijidanganya kwamba unaweza kukalia nafasi ya Sarah kwa Alvin Kimaro. Lakini sina budi kukushukuru pia. Kama usingempokonya Alvin, nisingeweza kukutana na Jerome wangu ambaye ananithamini sana.”
Jerome alizipapasa nywele za Melanie. Ingawa hakuwa amempenda Melanie hapo awali, alijifanya kumpenda sana kwa sababu fulani. Joel asingekuwepo tena, kwa hivyo Melanie alikuwa mrithi wa Ngosha Corporation. Hakutaka kupiga teke kapu la bahati iliyokuwa ikimdondokea mapajani mwake. Familia ya Ngosha na familia ya Campos zingeungana. Alvin angekuwa si kitu kwa wakati huo.
"Bwana. Cameron, nadhani meza yake karibu na dirisha si kibaya,” Melanie alisema huku akinyoosha kidole kwenye meza ya Lisa. “Tutakaa hapa.”
"Basi mtoe haraka na umpeleke kwenye meza nyingine," Jerome aliamuru kwa kiburi.
Bila kukawia zaidi, Bwana Cameron alimmwambia mhudumu kusogeza vitu vya Lisa kwenye meza iliyokuwa karibu na ukuta kwenye kona ya mgahawa huo. “Bi. Jones, tafadhali kula kifungua chako huko.”
“Nyie ni…” Lisa akatikisa kichwa na kusimama.
Melanie alitabasamu. "Lisa Jones, unaona hii? Hutanishinda kamwe. Mimi ni makamu wa mwenyekiti wa Ngosha Corporation sasa. Wiki ijayo, nitaolewa na Jerome. Kufikia wakati huo, familia za Campos na Ngosha zitakuwa timu yenye nguvu. Hakuna mtu nchini Kenya atakayethubutu kusema chochote hata nifanye nini.”
“Oh, hongera basi.” Lisa akasimama taratibu. "Baba bado amelazwa kwenye kitanda cha hospitali na haijulikani ikiwa ataishi au atakufa, lakini wewe? Unapata wapi hata hiyo hamu ya kuolewa?”
"Melanie anamjali sasa baba yake, anataka amletee zawadi ya wajukuu wenye akili." Jerome alijibu mbele ya Melanie.
“Eti anamjali sana Baba! Mbona sijawahi kuwaona mkimtembelea hata mara moja baada ya kuzimia?” Lisa alitoa tabasamu la uwongo.
"Niende au nisiende sio kazi yako." Melanie alidhihaki, “Vipi kuhusu wewe? Ulipata haki za kumtunza Baba, lakini kwa faida ipi? Ngosha Corporation ni yangu, na kila kitu ambacho Baba anamiliki ni mali yangu. Huna chochote cha kurithi. Nilisikia kwamba Daktari Angelo amekufa. Hakuna mtu anayeweza kumwokoa Baba sasa. Unaweza kuukumbatia mwili wake maisha yako yote, ndicho kilichobakia.”
"Angalia sauti yako. Inaonekana huna huzuni hata kidogo kwamba Daktari Angelo amekufa na Baba hawezi kuamka.” Lisa alishtuka na kuinua kichwa chake.
Koo la Melanie lilikwama kwa muda. Alisema kwa hasira, “Je, unaweza kupotea haraka? Usitusumbue tukiwa tunapata kifungua kinywa chetu.”
"Endelea kuwa jeuri kwa sasa, lakini siku zako zinahesabika." Lisa akatoa noti kadhaa na kuzitupa mezani. “Nitawaachia meza, lakini siku nyingine… msitarajie kama itatokea tena.” Alichukua mkoba wake na kuondoka baada ya kumaliza kuzungumza.

Hans, aliyekuwa amejificha kwenye kona moja, aliripoti kwa Alvin kila kitu alichokiona akifanyiwa Lisa.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
LISA KITABU CHA SITA

SIMULIZI............LISA
KURASA.......251-255

Sura ya: 251

Baada ya Lisa kuondoka, Melanie alinyamaza kwa muda na kugeuka kumwangalia Jerome. “Ulisema Alvin kamleta binamu wa Sarah ili kumuuguza. Ni kweli?
“Una wasiwasi kuhusu Alvin?” Jerome alimshika mkono na kuuchezea. "Bado huwezi kumsahau tu, huh?"
"Hapana. Ni wewe tu moyoni mwangu sasa." Melanie alishusha macho na kutabasamu. “Nina hamu tu ya kutaka kujua.”
Jerome alijibu kwa kujiamini. “Si hivyo tu, ugonjwa wa Alvin umezidi kuongezeka. Hata alizimia siku chache zilizopita na kupelekwa hospitali kwa dharura.”
Hans aliyekuwa kajificha kwenye kona fulani, alishuhudia kila kitu kilichotokea. Papo hapo alichukua simu kisha akampigia Alvin na kumpa ubuyu wote.
“Bwana Mkubwa, Bibi mdogo alikutana na Jerome Campos na Melanie Ngosha. Wawili hao walishirikiana pamoja na meneja Cameron kumfedhehesha Lisa hata kumfukuza kwenye meza aliyokuwa amekaa."
Mbele ya kibaraza akiwa anaota jua la asubuhi, Alvin alisikiliza simu hiyo na kupandwa na ghadhabu. “Ni wakati wa kuwaadhibu watu hao wawili. Wape zawadi kubwa. Kuhusu mgahawa huo, hakuna sababu ya kuendelea kufanya kazi tena.”
Katika mgahawa, Jerome na Melanie walikuwa ndo kwanza wameanza tu kula kifungua kinywa chao wakati kundi la maafisa wa Afya kutoka jiji walipovamia mgahawa huo na kumkamata meneja wa mgahawa huo. "Kuna mtu aliripoti kwamba aliumwa na tumbo baada ya kula kifungua kinywa hapa. Kwa hiyo, mgahawa huu lazima ufungwe kwa uchunguzi. Watu wote wasio watumishi wanapaswa kuondoka."
Maafisa waliwafukuza watu wote nje ya mgahawa huo. “Ondoka haraka.”
Melanie alikasirika. “Bado sijamaliza kula kifungua kinywa changu. Unajua mimi ni nani?"
"Sina haja ya kujua wewe ni nani, lakini najua unatuzuia kufanya kazi yetu." Maafisa waliwafukuza na hata kutupa vitu vyao nje.
Melanie aliendelea kusema kwa hasira, “Nitawaripoti!”
Jerome pia hakuwa katika hali nzuri. “Usijali mpenzi, najuana na watu wa juu zaidi. Ninaweza kuwafanya watu hao wapoteze kazi kwa simu moja tu.”
"Jerome, kweli? Wewe ni ‘so amazing!’ Wafunze adabu mbwa hawa!" Uso wa Melanie ulijaa jeuri.
Jerome alitabasamu na kutoa simu yake. Alikuwa karibu kupiga simu sehemu wakati alipoona simu ya sekretari wake ikiingia ghafla. “Bwana Campos, tuko taabani. Idara ya sheria ya KIM International ilimtuma mwanasheria wao. Walisema katika kipindi cha miaka 20 familia ya Campos imevuna faida ya bilioni 80 kutoka KIM International isivyo halali, wakati familia za Campos na Kimaro zikishirikiana katika miradi ya pamoja. Wametuma notisi kutaka warudishiwe fedha zao.”
"Nini?" Uso wa Jerome ulibadilika ghafla. “Alvin ana wazimu?”
“Wameleta nyaraka zote. Kila kitu kiimewekwa wazi." Katibu akatabasamu kwa uchungu.
"Damn!" Jerome alikasirika. Hatimaye alielewa, kuanzia tukio la Lisa hadi tatizo la akaunti za kampuni, hayakuwa ni bahati mbaya tu. Lazima kulikuwa na mkono wa Alvin. Huyu Alvin alikuwa anakaribia kuwa kichaa, na kichaa chake sasa kilimgeukia yeye. Kwa bahati mbaya, yote yalikuwa kweli.
Miaka hiyo yote Lea alipokuwa akiongoza kampuni ya KIM, alikuwa ameisaidia sana familia ya Campos. Hata alishirikiana na familia ya Campos kwenye miradi mingi ya pamoja. Kwa kawaida, KIM International haikushiriki katika miradi hiyo, hivyo kimsingi walifumba macho na kuwaachia familia ya Campos kupitia kampuni yao ya Campos Ltd. kupata faida. Ni siku chache zilizopita ndipo walipokaza sera zao baada ya Alvin kushika nafasi ya uongozi.
Sio kwamba familia ya Campos haikuwa na bilioni 80, lakini, kutoa kiasi kikubwa cha pesa kama hicho kwa ghafla kungeathiri mradi mkubwa ambao familia ya Campos ilikuwa karibu kuanza. Mradi huo ungeweza kubadilisha mustakabali wa familia ya Campos. Kwa hiyo, wasingeweza kutoa pesa hizo.
•••
Lisa alifika kwenye ofisi za kampuni yake asubuhi na mapema. Meneja Mkuu alipokuja kuchukua saini yake, alisema kwa wasiwasi, “Nimesikia kwamba… umetengana na Bw. Kimaro na unajitayarisha… kwa talaka?”
Kalamu iliyokuwa ikisaini karatasi ilisimama. Lisa aliinua kichwa chake kwa utulivu. “Inazungumzwa hivyo nje?”

"Ndio, kampuni zingine ambazo zilikuwa na makubaliano ya mdomo na sisi hapo awali zilighairi ushirikiano wao tena na sisi. Hawapokei hata simu za kampuni yetu sasa hivi.” Meneja alieleza kwa wasiwasi.
"Usijali. Kipaumbele chetu kwa sasa ni kuzingatia tu kuendeleza ujenzi wa jengo letu la ofisi kwenye uwanja wetu mpya.” Lisa hakuwa na wasiwasi hata kidogo. "Pia, uwaonye wafanyakazi kufuatilia mambo yasiyowahusu. Ni vyema kila mtu azingatie tu kufanya kazi zake kwa bidii.”
“Sawa.” Meneja Mkuu aliinamisha kichwa kwa simanzi baada ya kutoka ofisini. Alidhani nafasi ya Mawenzi Investments ingepanda kwa kasi baada ya kuungwa mkono na Alvin Kimaro.
Hali katika kampuni ilikuwa tulivu asubuhi nzima. Ilipofika karibu saa sita mchana, Alvin aliingia ghafla kwenye lango la ofisini za Mawenzi. Wafanyakazi kwenye ofisi ya mapokezi walihisi kutetemeka kwa kila hatua ambayo Alvin alikuwa akipiga kuwasogelea.
Kama kawaida, minong’ono ya mishangao ikasikika miongoni mwa wafanyakazi hao;
“Ni Alvin Kimaro…”
“Ooh! Jmani huyu kaka ni mzuri! Nilikuwa sijawahi kumuona kwa karibu hivi. Kwa kweli ni mzuri, bosi atakuwa anafaidi sana....”
“Thubutu! Nasikia ndoa yao ina migogoro kama nini, hivi tunavyoongea wanataka kuachana…”
“Mbona sasa yuko hapa? Au ndo atakuwa kamletea talaka bosi wetu?
“Oh Mungu wangu, hapana.”
“Bwana Kimaro, karibu…” Mhudumu wa mapokezi wa kike alimpokea kwa tahadhari. “Tukusaidie nini?”
“Huoni hii?” Alitikisa kontena la chakula alilokuwa amebeba. “Nimekuja hapa kumletea chakula mke wangu.”
Mhudumu yule aliingiwa na hofu. Si alisikia walipeana talaka? Kwanini Bwana Kimaro alimpelekea chakula yeye binafsi basi?
"Yuko wapi?" Alvin aliinua macho yake na kupepesa.
Yule mhudumu wa mapokezi alikaribia kupofushwa kwa hofu ya kumkaribia tu Alvin, na alikuwa kwenye hatihati ya kuzimia. "Saa hii ... ameenda kwenye mgahawa kula."
Alvin alielekea kwenye mgahawa bila wasiwasi. Hii ilikuwa mara yake ya pili kutembelea ofisi za Mawenzi. Aliiona sura ya Lisa kwenye mgahawa haraka sana. Alikuwa anavutia macho kweli. Alivaa suti ya rangi ya khaki siku hiyo, na nywele zake ndefu zilikusanyika upande mmoja. Kutokana na mwonekano wake wa kipekee, alikuwa anaonekana kama ametoka ulimwengu mwingine kabisa.
Watendaji wachache wa kampuni walikusanyika karibu naye. Hakujua wanazungumza nini, lakini hali ilikuwa wazi walikuwa na mazungumzo ya kupendeza. Alvin akakunjua uso wake kwa tabasamu. Alitembea kwa hatua ndefu kuwasogelea.
Lisa alikuwa akijadiliana na watendaji hao kuhusu maendeleo ya ujenzi wa ofisi za kampuni ya Mawenzi kwenye uwanja wake aliopewa na Joel. Kisha, alihisi mazingira yakitulia ghafla na kila mtu alikuwa akitazama nyuma yake.
Wanawake walikuwa hoi huku wanaume wakiwa na sura za woga na zenye heshima. Lisa aligeuka kuangalia kulikoni, na ghafla macho yake yakakutana na uso mzuri wa Alvin. Mapigo ya moyo wake yalianza kwenda kasi.
"Babe, nimekuandalia chakula cha mchana." Sauti ya Alvin ilikuwa ya upole, tamu na ya kuvutia utadhani asali ilikuwa ikichuruzika kutoka kwenye maneno yake.
Lisa alikunja uso. Alikuwa karibu kusema kitu wakati Meneja Mkuu alisimama mara moja na kusema. "Katika hali hiyo, Mwenyekiti Jones, unapaswa haraka kwenda ofisini na kula chakula chako na Bwana Kimaro."
Meneja wa Idara ya Masoko alitabasamu kutoka sikio hadi sikio. "Bwana Kimaro, una mapenzi mazito sana kwa mkeo."
Meneja wa Idara ya Mahusiano ya Umma ambaye alikuwa ni mdada, alisema, “Wanaume wazuri kama Bwana Kimaro wanakaribia kutoweka duniani. Mume wangu hajawahi kuniandalia chakula maishani mwangu.”
Mambo yalitiwa chumvi zaidi wakati msimamizi wa mgahawa alipoishiwa nguvu na kusema, “Chakula katika mgahawa wetu hakika hakiwezi kuwa kitamu kama kile ambacho Bwana Kimaro amekuandalia. Bi. Jones, hupaswi kuruhusu juhudi zake zipotee.”
Hao walikuwa wafanyakazi wake au wa Alvin? Lisa alikosa jibu.
"Twende," Alvin alizungusha mkono kiunoni mwake na kumnong'oneza sikioni, "Hutaweza kugombana nami ambapo kila mtu anatutazama, sivyo?"
Lisa alikosa la kusema. Hakuwa na budi ila kuelekea naye ofisini kwake.

Sura ya: 252

Lisa alikaa kimya kwa muda. Kisha, akasema, “Uliajiri mpishi akutengenezee haya yote, sivyo?”
“Hapana, nilitumia asubuhi nzima kukutengenezea chakula cha mchana nyumbani,” Alvin alisema, “Wewe ulikuwa ukinipikia huko Dar es Salaam. Sasa, ni zamu yangu kukukirimu.”
Lisa alidhihaki, “Alvin Kimaro, wewe ni stadi kwa kuigiza. Ulikuwa pia ukifanya hivi ulipokuwa ukiishi na Sarah zamani?”
"Iwe unaamini au la, nimekupikia tu kwa sababu nakupenda." Alvin akamtengea chakula. "Kula."
"Sili." Lisa alikataa kijeuri
“Lisa, huna akili timamu. Je, wewe pia hukuwa na mpenzi wa zamani?”
“Sawa, nitatafuta mvulana anayefanana na Ethan anihudumie nyumbani kwangu. Hiyo ni sawa?" Lisa alimtazama. Hakika, aliona kutoridhika machoni pake na akacheka. "Unaona, umewahi kujiweka katika viatu vyangu kufikiria juu ya hali hiyo?"
“Samahani,” Alvin aliomba msamaha kwa dhati. Kwa kweli alijihisi kukosea kuhusiana na suala la Maurine. "Sitarudia tena."
"Alvin, hakuna nafasi nyingine tena," Lisa alisema kwa msisitizo.
“Usiseme hivyo mpenzi.” Alvin akajiweka sawa kwenye kiti. "Ikiwa hutakula, basi sitaondoka."
Lisa alimkazia macho. Hakujua amfanyeje mtu yule ili amwelewe.
“Kuwa mstaarabu.” Alvin alikuwa akigonga juu ya uso wa meza na ghafla akasema, "Mbona unakuwa kama mtu asiye na macho? Kwanini huoni kwamba ninakupenda?” Alvin alitabasamu kwa umaridadi.
"Inawezekana sina macho ya kuona mapenzi ya kinafiki." Japo Lisa alitia kichwa ngumu, bado maneno ya kupendeza ya Alvin yalikuwa yakimwingia kidogokidogo.
Midomo yake ikafunguka tena ili kusema kitu, lakini Alvin akaiminya haraka kwa mkono wake. “Usiongee.” Alvin alihema kwa nguvu na kusema. “Unajua moyo wangu wote umejaa mapenzi yako. Unataka nifanye nini unielewe?"
“Unataka ufanye nini? Kufa tu!” Lisa alichukua glasi ya maji na kunywa ili kuondoa hasira iliyomkaba kooni mwake. “Sitaki uongee tena.”
“Sawa, sitasema lolote usiponiruhusu, nitakusikiliza.” Alvin aliweka sura ya utii.
Lisa alikuwa karibu kumfukuza Alvin, lakini alikosa sababu ya kumtimua. Hakuwa tena Alvin yule mwenye kiburi na jeuri kama alivyokuwa zamani. Hakutaka kula chakula chake, lakini alikuwa na njaa sana, hivyo ilimbidi kushika uma na kijiko na kuanza kula chakula. Hakikuwa kitamu sana, lakini ladha yake ilikuwa inaruhusu kupitika mdomoni.
Alvin akaegemeza kidevu chake kwenye mikono yake. “Hatimaye ninaelewa kwanini ulifurahia kunipikia hapo awali. Kuona mtu ninayempenda anakula chakula nilichotengeneza inanifurahisha sana.”
Lisa alinyamaza. Alifurahia kumpikia lini? Hapo mwanzo, alimpikia ili kujipendekeza kwa nia ya kuwa shangazi wa Ethan. Baada ya hapo, ni yeye ndiye aliyemlazimisha.
“Nipe simu yako. Nataka nitoe namba yangu kwenye blacklist.” Alvin alinyoosha mkono wake.
"Hapana." Lisaaligoma.
'Basi nitaichukua kwa nguvu." Alvin alisimama, umbo lake refu likionekana kutawala. Lisa akakosa ujanja na kumtupia simu yake.
Alvin aligonga skrini mara chache na kujiondoa kwenye blacklist ya simu yake na Whatsapp. Baada ya kumrudishia simu, alichukua simu yake na kuigonga mara kadhaa pia.
Muda si mrefu simu ya Lisa ikaita kwa mtetemo. Aliitazama na kulikuwa na taarifa: [Ni Wako Pekee alikutumia ujumbe.]
Ni Wako Pekee?… Lisa alibubujikwa na mshtuko.
“Umeupokea ujumbe wangu? Hilo ndilo jina langu jipya la Whatsapp.” Alvin akamtazama.
"Unajaribu kumaanisha nini hapa?" Lisa alikuwa katika ukungu.
"Nakupenda."
Lisa alikumbuka kwamba alipokuwa akijaribu kumvutia siku za nyuma, aliweka jina lake la Whatsapp kama 'Alvlisa'. Hapo awali alikuwa ametulia lakini kukumbuka hilo kulimfanya uso wake kuwa na aibu.
"Angalia status yangu." Alvin alimkumbusha.
Lisa akaifungua huku akitetemeka. Ilikuwa imeandikwa hvi: [Kama kukupenda ni kifungo cha maisha, basi nakubali adhabu hiyo kwa hiari]
Akiwa kama wakili, hilo ndilo lilikuwa tamko la kimahaba ambalo angeweza kulifikiria. Alvin aliinamisha kichwa na kukohoa. "Umeipenda?".
Lisa aliinamisha kichwa chake na kutabasamu kwa aibu. Alipoinua kichwa chake moja kwa moja aliweka kiganja chake kwenye shavu la Alvin.
"Unafanya nini?" Alvin aliuliza kwa mshangao.

"Nakuangalia kama una homa." Lisa alijibu. Hakuamini kama Alvin alitamka maneno yale akiwa mzima,.
Uso wa Alvin ulisinyaa ghafla. "Inatosha, nilitumia usiku kucha kujaribu kufikiria hii. Kwa mtu kama mimi, dakika moja inatosha kuniingizia kipato cha dola 10,000. Jiulize nimepoteza kiasi gani kwa ajili ya hilo.”
Lisa alikoroma moyoni. Je! alikuwa akimaanisha kwamba alipoteza mamilioni ya dola kwa ajili yake?
"Usijali. Wewe huwezi kulinganishwa na pesa, wewe ni mke wangu wa thamani sana." Alvin akafunga kontena la chakula. “Njoo nyumbani mapema leo usiku. Nitakupikia chakula cha jioni.”
“Asante, lakini hakuna haja. Nimefanya miadi ya kwenda kwenye spa na Charity.”
Alvin alikunja uso na kumtazama tena. Alipotaka kuongea tu, Lisa alimkatisha, “Najua unataka kunizuia nisiende nae tena na kumsema vibaya. Samahani, lakini yeye ni rafiki yangu sasa. Kwangu mimi ni mwadilifu, mkarimu, mpole, mwema, na ana mambo mengine mengi mazuri.”
Alvin alitaka kupasua kichwa chake na kukitikisa. “Nadhani amekuvuruga ubongo. Mwanamke huyo si mzuri kama unavyofikiaria.”
“Nilimruhusu kwa hiari yangu mwenyewe anivuruge ubongo. Una shida gani na hilo?" Lisa alitabasamu bila kufafanua. “Utawaambia rafiki zako wazuri kunifedhehesha tena?”
“Unamaanisha nini kusema hivyo?” Alvin alikunja uso.
“Mara ya mwisho, sikufanya chochote zaidi ya kumwomba Maurine aondoke, lakini rafiki yako mzuri, Rodney, alikuja kwenye kampuni yangu na kunifokea kama mtoto mdogo.” Lisa aliongea kwa huzni, lakini uso wake ulikuwa umejaa kejeli. “Sasa nikiambatana na Charity labda watakushauri unitaliki.”
Macho ya Alvin yaliingia giza. Hakujua kuhusu hilo.
“Alvin, nataka uondoke. Usinisumbue tena. Sitaki kuandamwa kama kichaa na rafiki zako. Wanaweza hata kufikiria kuwa mimi nilikufuata wewe kwa sababu ya maslahi yangu binafsi. Mimi nimeridhika na maisha yangu.” Lisa alikuwa akipitia nyaraka zake huku akiongea.
Ndita zilikunjamana kwenye uso wa Alvin kiasi kwamba zingeweza kumminya inzi hadi akafa. Hakujua mawazo ya Chester, lakini Rodney alikuwa kama vile Lisa alivyomdhania kuwa.
Alvin akasogea mbele na kumshika Lisa mkono. Lisa aliinua kichwa chake. Alimuona akiitoa simu yake na kupiga namba ya Rodney. Hata akaweka simu kwenye kipaza sauti.
Simu ilipounganishwa, sauti ya Rodney ilisikika kwa uzito na uwazi. “Alvin, nilikuwa karibu kukupigia simu. Je, Lisa alihack akaunti yako? Jina lako 'Ni Wako Pekee' lilinichukiza sana hivi kwamba nilitapika chakula changu chote cha jana usiku."
“Sikudukuliwa. Niliibadilisha mimi mwenyewe.” Alvin alitamani Rodney angekuwa karibu ili ampige ngumi hadi afe. “Acha porojo zako. Hebu nikuulize, ulienda Mawenzi Investments na kumkoromea Lisa?"
“Huyo mwanamke amekuambia nini? Anaweza kuacha—”
Alvin akamkatisha. Macho yake yalizidi kuwa makali sana. “Ulimwambia nini?”
“Sikusema lolote. Sikumbuki, lakini nilimuonya aache kumnyanyasa Maurine na kwamba asifikirie kuwa yuko juu kwa sababu tu amekuwa Bi. Kimaro—”
“Rodney Shangwe…” Alvin alikunja vibaya uso wake na kusema neno baada ya neno, “Lisa na mimi kugombana ni mambo yetu wenyewe. Huna haki ya kusema lolote kuhusu hilo. Isitoshe, ikiwa una wasiwasi sana kuhusu Maurine, unaweza kumchukua na kumtunza jinsi unavyotaka.”

"KIM International haihitaji faida kama hizo. Familia za Campos na Kimaro ni jamaa tuliounganishwa kwa ndoa. Miradi hii ndiyo maamuzi niliyofanya wakati huo nilipotaka kuisaidia familia ya Campos. Babu yako anajua hili pia—”
“Basi unaweza kumtafuta babu yangu. Kwanini ujisumbue kunitafuta mimi?” Alvin alitabasamu kwa kejeli.
Uso wa Lea ukabadilika. “Babu yako amestaafu. Ninakukumbusha usifanye mambo bila huruma. Vinginevyo, msinilaumu kwa kukosa huruma kwako.”
“Sijui unamaanisha nini kwa maneno hayo, lakini…” Alvin ghafla alichukua rimoti na kuwasha skrini kubwa ukutani. Nyuso za wanahisa wachache wa KIM International zilionekana wazi kwenye skrini. “Samahani mama. Nilikuwa nikifanya mkutano kwa njia ya video na wanahisa. Wamesikia kila kitu ulichosema hivi punde.”
Mkurugenzi Kennedy, ambaye alikuwa mkubwa kati ya wanahisa, alisema, "Makamu Mkurugenzi Lea Kimaro, ikiwa tutachukua hizo bilioni 80, tunaweza kuzigawanya kati yetu na kila mmoja angekuwa na milioni mia chache. Bila shaka, tunajua kwamba wewe ni tajiri na hujali. Lakini sisi tunahitaji pesa."
Mkurugenzi Martin alisema kwa kejeli, “Tunaelewa kwamba familia ya Campos ni familia ya mume wako, kwa hivyo tuliwafumbia macho watoto walioongoza KIM International wakati huo. Lakini hatukujua kamwe familia ya Campos ilikuwa imechukua bilioni 80. Huu ni ujinga sana.”
Mkurugenzi Morris aliguna. “Hii siyo haki, huwezi kuipa familia ya Campos shilingi bilioni 80 bila sababu. Siku zote umekuwa upande wa familia ya Campos, hatukubali hata kidogo.”
Mkurugenzi Kennedy akaongezea, “Mwanao, Willie, alitia saini mradi mwingine na familia ya Campos tena muda si mrefu na akatoa asilimia tano ya faida kwao. Kwa bahati nzuri, Bwana Alvin Kimaro alikatisha ushirikiano nuo. Vinginevyo, familia ya Campos ingepata zaidi ya maelfu ya mabilioni.”
Mkurugenzi Morris alisema, "Tunahitaji esa zetu zirudi, ama tutachukua maamuzi mgumu."
Uso wa Lea ulibadilika ghafla nakuwa mpole, na mwili wake ulikuwa ukitetemeka. Alikuwa amesimamia KIM International kwa miaka makumi kadhaa, na hii ilikuwa mara ya kwanza kwa wanahisa kumkosoa. "Mabwana, ninakubali kwamba niliisaidia Campos Ltd. hapo awali, lakini haiwezekani kwamba walichukua kiasi cha bilioni 80. Haya yote yamezushwa tu na Alvin.”
Mkurugenzi Kennedy alitabasamu. “Sidhani kama madai haya yalitungwa na mtu yoyote yule. Familia ya Campos wanajulikana kwa tamaai, kwa hivyo labda hata wewe ulikuwa gizani.”
"Hapana!" Lea hakuamini hata kidogo.
Alvin aliinua kichwa chake kuelekea kwenye skrini na kusema, “Sawa, wanahisa. Nitamwelewesha mama yangu vizuri.”
"Asante, Bwana Mkubwa Kimaro." Hangout ya Video iliisha.
Mason alikunja uso na kusema, “Alvin, unawezaje kumtendea mama yako hivi? Atakabiliana vipi na watu wengine kuanzia sasa?”
Alvin akatabasamu. "Uncle, kama ningekuwa wewe, ningesema hivi ili kumsitiri mke wangu, 'Mpenzi wangu, ili usijisikie vibaya, tutarudisha tu shilingi bilioni 80 kwa KIM International'.
Mason alikuwa mdogo kama pilitoni kutokana na aibu. Shilingi bilioni 80 hazikuwa pesa ndogo. Haikuwa rahisi kiasi hicho kuzitoa kirahisirahisi tu.
“Mpenzi wangu…” Mason alitaka kumbembeleza Lea lakini akamkatisha.
“Sawa, Alvin anajaribu kukuweka kwenye hali ngumu. Naelewa." Lea alimvuta Mason. “Twende zetu.”
Alipofika mlangoni, Lea aligeuka nyuma. Sauti yake ilikuwa ya huzuni aliposema, “Alvin, nitakumbuka kofi hili la uso ulilonipa leo. Kuanzia sasa, usiniite 'Mama'. Hatuna uhusiano tena.”
Katika maegesho ya magari, Mason Campos aliegemeza kichwa chake mikononi mwake kwa shida na hakusema neno. Lea aliuma mdomo na kusita. Akatoa kadi kwenye pochi yake na kumpa. "Nina shilingi bilioni 60 hapa. Unaweza kuingiza kwenye Kampuni ya Campos ili kuimarisha mzunguko wa pesa.”
"Mpenzi wangu ..." Mason alimtazama kwa hatia na huzuni. "Siwezi kuchukua hii."

Sura ya: 253

"Alvin, hii ni mara ya pili unanikoromea kwa sababu ya mwanamke huyo." Rodney alikasirika pia. “Maurine ni binamu wa Sarah. Sarah hayupo hapa tena. Ninafanya hivi ili kulinda familia yake.”
"Ndio, siku zote nilifikiria hivyo pia. Ndiyo maana niliachana na kanuni zangu kwa ajili ya Sarah tena na tena. Miaka yote hii Thomas amefanya maovu mangapi?!” Alvin alikiri kwa masikitko. "Miaka minne iliyopita, alisababisha kifo cha binti asiye na hatia. Ushahidi wote ulielekeza kwake, hata hivyo nilivumilia Kenya nzima kunikosoa na kupigania kesi kwa ajili yake. Baada ya kesi hiyo, nilichukia kazi yangu na kujiondoa kutoka kwa jumuiya ya wanasheria. Miaka yote hii, Zigi amekuwa na kisasi na mimi, na wewe unajua hilo.” Rodney alikuwa kimya.
Alvin alimshika mkono Lisa kwa nguvu. “Nilimtetea Thomas kwa miaka minne, na hata niliwatetea Sarah na kaka yake na mama yao walipokuwa wakinyanyaswa na mama yao wa kambo. Hata hivyo, hilo limesababisha matatizo katika ndoa yangu. Lisa hanielewi vizuri hatimaye. Siwezi kuwa na uhusiano na Sarah maisha yangu yote. Si haki kwa Lisa.”
Rodney alikunya sura yake bila kuridhika. “Kwa hiyo, haya ndiyo mapenzi uliyomwahidi Sarah? Inaonekana kama Sarah si chochote tena kwako.”
“Sarah tayari amekufa. Pengine… ulimpenda zaidi kuliko mimi?” Mwili wa Rodney ulisisimka. Alvin aliendelea. “Kama bado unapenda kuwa rafiki na ndugu yangu mzuri, natumaini utamheshimu mke wangu.”
Alvin alikata simu na kumtazama moja kwa moja Lisa ambaye alikuwa ameduwaa. Ubongo wake ulikuwa umechanganyikiwa.
Hapo awali alikuwa amesikia kwamba Alvin alikuwa wakili mkubwa nchini Kenya, lakini ghafla alitoweka kwenye tasnia hiyo kwa muda. Ilibainika kuwa ni kwa sababu ya Thomas. Si hivyo tu, ina maana pia Rodney alimpenda Sarah? Lisa aliona mapichapicha tu kwenye akili yake.
“Lisa, nakuomba tuache yaliyopita na tugange yajayo, sawa?” Alvin alisema kwa umakini huku akimshika Lisa.
Akili ya Lisa ilipotea kwa muda, lakini haraka akautoa mkono wake. Hakuweza kujua ni sentensi gani kati yake ilikuwa ya kweli au ya uwongo.
'Ni sawa. Bado tuna wakati." Alvin akasimama. “Unaweza kuendelea na kazi yako. Sitakusumbua tena.” Baada ya kuongea alifunga mlango na kuondoka.
Lisa alikaa hapo kwa muda mrefu, lakini hakuweza kusoma hata neno moja kwenye nyaraka zilizokuwa mbele yake.
Baada ya kutoka Mawenzi Investments, Alvin aliendesha gari hadi hospitali kwa ajili ya kutiwa dripu. Hali ya ugonjwa wake haikuwa shwari, hivyo angeweza tu kudungwa dawa kwa ajili ya kutuliza.
Sindano ilipodungwa tu, Lea aliingia kwa hasira. “Alvin, ni kweli uliagiza idara ya sheria kudai shilingi bilioni 80 kutoka kwa Kampuni ya Campos?! Unataka kuwamaliza? Nadhani unaanza kuwa na kichaa cha pesa sasa."
Mason alisimama nyuma ya Lea, akitabasamu. “Najua unanilaumu kwa kuwa pamoja na mama yako. Ni sawa kwa kuwa hunipendi, lakini familia ya Campos haina hatia. Alvin, nakuomba, achana na kampuni ya Campos.”
"Mason, usimbembeleze." Kuona mwanaume aliyempenda anambembeleza mwanaye, moyo wa Lea ulimuuma sana.
Alvin alitabasamu kwa huzuni. "Uncle Mason, unataka niseme zaidi? Nimeona matapeli wengi kama wewe wanaojifanya wakarimu kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu. Ni ajabu sana mama yangu hajagundua njama zako kwa miaka yote aliyoishi na wewe.”
Uso wa Mason ulikauka. Lea alikuwa anakaribia kupandwa wazimu kutokana na hasira. “Chunga mdomo wako! Mason hajawahi kukufanyia chochote kibaya. Nilikuwa najua una akili kumbe nilikuwa na najidanganya. Si tu kwamba huna akili, huna adabu, huna heshima na huna utu.”
Alvin aliongea kwa msisitizo. “Kivipi mimi sina utu? Kwa kudai haki ya familia ya Kimaro? Shilingi bilioni 80 kwa hakika ni faida ambayo ni haki ya KIM International kutokana na miradi yetu ya pamoja na Campos Ltd kwa miaka yote hii. Taarifa ya akaunti yangu imeandikwa kwa uwazi. Wao ndio hawakutupa hizo pesa. Ninadai pesa za KIM International zirudishwe, na bado unanikaripia. Mama, ninafanya hivi kwa manufaa ya KIM International.”

"KIM International haihitaji faida kama hizo. Familia za Campos na Kimaro ni jamaa tuliounganishwa kwa ndoa. Miradi hii ndiyo maamuzi niliyofanya wakati huo nilipotaka kuisaidia familia ya Campos. Babu yako anajua hili pia—”
“Basi unaweza kumtafuta babu yangu. Kwanini ujisumbue kunitafuta mimi?” Alvin alitabasamu kwa kejeli.
Uso wa Lea ukabadilika. “Babu yako amestaafu. Ninakukumbusha usifanye mambo bila huruma. Vinginevyo, msinilaumu kwa kukosa huruma kwako.”
“Sijui unamaanisha nini kwa maneno hayo, lakini…” Alvin ghafla alichukua rimoti na kuwasha skrini kubwa ukutani. Nyuso za wanahisa wachache wa KIM International zilionekana wazi kwenye skrini. “Samahani mama. Nilikuwa nikifanya mkutano kwa njia ya video na wanahisa. Wamesikia kila kitu ulichosema hivi punde.”
Mkurugenzi Kennedy, ambaye alikuwa mkubwa kati ya wanahisa, alisema, "Makamu Mkurugenzi Lea Kimaro, ikiwa tutachukua hizo bilioni 80, tunaweza kuzigawanya kati yetu na kila mmoja angekuwa na milioni mia chache. Bila shaka, tunajua kwamba wewe ni tajiri na hujali. Lakini sisi tunahitaji pesa."
Mkurugenzi Martin alisema kwa kejeli, “Tunaelewa kwamba familia ya Campos ni familia ya mume wako, kwa hivyo tuliwafumbia macho watoto walioongoza KIM International wakati huo. Lakini hatukujua kamwe familia ya Campos ilikuwa imechukua bilioni 80. Huu ni ujinga sana.”
Mkurugenzi Morris aliguna. “Hii siyo haki, huwezi kuipa familia ya Campos shilingi bilioni 80 bila sababu. Siku zote umekuwa upande wa familia ya Campos, hatukubali hata kidogo.”
Mkurugenzi Kennedy akaongezea, “Mwanao, Willie, alitia saini mradi mwingine na familia ya Campos tena muda si mrefu na akatoa asilimia tano ya faida kwao. Kwa bahati nzuri, Bwana Alvin Kimaro alikatisha ushirikiano nuo. Vinginevyo, familia ya Campos ingepata zaidi ya maelfu ya mabilioni.”
Mkurugenzi Morris alisema, "Tunahitaji esa zetu zirudi, ama tutachukua maamuzi mgumu."
Uso wa Lea ulibadilika ghafla nakuwa mpole, na mwili wake ulikuwa ukitetemeka. Alikuwa amesimamia KIM International kwa miaka makumi kadhaa, na hii ilikuwa mara ya kwanza kwa wanahisa kumkosoa. "Mabwana, ninakubali kwamba niliisaidia Campos Ltd. hapo awali, lakini haiwezekani kwamba walichukua kiasi cha bilioni 80. Haya yote yamezushwa tu na Alvin.”
Mkurugenzi Kennedy alitabasamu. “Sidhani kama madai haya yalitungwa na mtu yoyote yule. Familia ya Campos wanajulikana kwa tamaai, kwa hivyo labda hata wewe ulikuwa gizani.”
"Hapana!" Lea hakuamini hata kidogo.
Alvin aliinua kichwa chake kuelekea kwenye skrini na kusema, “Sawa, wanahisa. Nitamwelewesha mama yangu vizuri.”
"Asante, Bwana Mkubwa Kimaro." Hangout ya Video iliisha.
Mason alikunja uso na kusema, “Alvin, unawezaje kumtendea mama yako hivi? Atakabiliana vipi na watu wengine kuanzia sasa?”
Alvin akatabasamu. "Uncle, kama ningekuwa wewe, ningesema hivi ili kumsitiri mke wangu, 'Mpenzi wangu, ili usijisikie vibaya, tutarudisha tu shilingi bilioni 80 kwa KIM International'.
Mason alikuwa mdogo kama pilitoni kutokana na aibu. Shilingi bilioni 80 hazikuwa pesa ndogo. Haikuwa rahisi kiasi hicho kuzitoa kirahisirahisi tu.
“Mpenzi wangu…” Mason alitaka kumbembeleza Lea lakini akamkatisha.
“Sawa, Alvin anajaribu kukuweka kwenye hali ngumu. Naelewa." Lea alimvuta Mason. “Twende zetu.”
Alipofika mlangoni, Lea aligeuka nyuma. Sauti yake ilikuwa ya huzuni aliposema, “Alvin, nitakumbuka kofi hili la uso ulilonipa leo. Kuanzia sasa, usiniite 'Mama'. Hatuna uhusiano tena.”
Katika maegesho ya magari, Mason Campos aliegemeza kichwa chake mikononi mwake kwa shida na hakusema neno. Lea aliuma mdomo na kusita. Akatoa kadi kwenye pochi yake na kumpa. "Nina shilingi bilioni 60 hapa. Unaweza kuingiza kwenye Kampuni ya Campos ili kuimarisha mzunguko wa pesa.”
"Mpenzi wangu ..." Mason alimtazama kwa hatia na huzuni. "Siwezi kuchukua hii."

Sura ya: 254

“Usiwe mjinga. Ikiwa familia ya Campos inapanga kwenda mahakamani na Alvin, hakuna nafasi kabisa ya kushinda. Alvin ni mtaalamu wa sheria. Hakuna mtu anayeweza kumshinda.” Lea akakabidhi kadi mkononi mwake. "Ninaendesha kampuni pia. Ninajua jinsi mzunguko wa pesa wa kampuni ya Campos Ltd. ulivyo mkubwa. Unaweza kunirudishia pesa hii pale tu kampuni itakapokuwa na mtaji wa kutosha.”
"Asante." Mason alimkumbatia. Lea akatabasamu.
Wakati huo huo, Mzee Kimaro alimpigia ghafla. “Uko wapi? Nina jambo la kujadili na wewe. Rudi nyumbani kwangu mara moja."
“Sawa…”
“Uje peke yako.” Mzee Kimaro alisisitiza. Lea alipigwa na butwaa.
Saa moja baadaye, Lea aliingia sebuleni. “Baba, kwanini umeniita hapa?”
"Hebu nikuulize, una pesa ngapi benki?" Mzee Kimaro alimtazama kwa ukali.
Lea alibana midomo yake pamoja bila kuelezeka. “Sina salio kubwa. Niliwekeza sehemu.”
Mzee Kimaro alisimama taratibu. “Niweke wazi kuhusu kiasi gani ulicho nacho na uliwekeza kiasi gani. Usiniambie kwamba ulimkopesha Mason pesa hizo?”
Lea aliuma meno yake na kusema, “Baba, Alvin alidai shilingi bilioni 80 kutoka kwa Campos Ltd kwa ghafla. Familia ya Campos inaweza kupata wapi pesa nyingi hivyo—”
“Kwa hiyo umempa kweli?” Bibi Kimaro aliuliza kwa kutetemeka.
“Ndiyo.” Lea akaitikia kwa kichwa.
Alipomaliza, Mzee Kimaro alimpiga kofi usoni. “Mjinga wewe!”
“Baba…” Lea alikuwa ameduwaa kutokana na kupigwa. Tangu alipokuwa mchanga, hakupokea chochote ila sifa kutoka kwa Mzee Kimaro- isipokuwa kwa wakati aliposisitiza kuolewa na Mason.
"Nilidhani ulikuwa na akili hapo awali, lakini kwanini shimo kwenye ubongo wako linakua kubwa unapoanza kuzeeka?" Mzee Kimaro alitupa hati usoni mwake. “Tazama mwenyewe. Huu ni uchunguzi wangu wa hivi karibuni kuhusu familia ya Campos. Campos Ltd ina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 900. Kwa kweli, nyingi zilitumika kwa uwekezaji, lakini bado kuna angalau dola bilioni 100 kwenye akaunti ya kampuni.”
Lea alishtuka baada ya kuziona zile nyaraka. Wakwe zake walikuwa wakimwambia kila mara kwamba familia ya Campos ilikuwa na matatizo ya ya pesa hivyo alijitutumua kuwasaidia. “Hii… Sikujua kwamba wakwe zangu walikuwa wajanja sana, lakini hii hakika haina uhusiano wowote na Mason. Mawazo yake yote ni kutunga muziki na mara nyingi husafiri. Hausiki kabisa kusimamia kampuni. Hasimamii Kampuni ya Campos hata kidogo…”
Mzee Kimaro akatikisa kichwa kwa kukatishwa tamaa. “Kama wakwe zako wangekuwa werevu kiasi hicho, hawangekuwa masikini na waliofeli kwenye maisha. Kampuni ya Campos imekuwa ikijiendesha kwa ujanja ujanja sana miaka hii yote. Kuna mtu anafanya hila nyuma ya pazia.”
"Baba, usitake kusema kwamba mtu huyu ni Mason, sawa?" Lea hakuamini hata kidogo. “Nimelala naye kitanda kimoja kwa miaka makumi kadhaa. Hakuna anayemuelewa kuliko mimi.”
Bibi Kimaro alisema kwa unyonge, “Babu yako tayari amechunguza. Jack na Valerie siyo walioeneza picha kuhusu ugonjwa wa akili wa Alvin. Kuna watu wengi tu katika familia ya Kimaro, unadhani angekuwa nani kama si yeye?”
Lea alishtuka. Hakutaka kuwa na mashaka, lakini kama hilo lilifanywa na Mason…
“Na…” Mzee Kimaro alisema, “Unajua kuhusu ndoa kati ya familia ya Campos na familia ya Ngosha sivyo? Ilipaswa kuwa tukio la furaha, lakini tangu Joel alipoingia kwenye ajali, familia za Campos na Ngosha sasa zinaunganisha nguvu na pesa kuingia katika sekta ya fedha, vifaa, na biashara ya mtandaoni. Tayari wana kampuni tanzu. KIM International imezingirwa na iko katika hali ngumu.”
Bibi Kimaro alisema, "Ndiyo maana Alvin anataka Campos Ltd kufidia shilingi bilioni 80 ili kupunguza mzunguko wao wa mtaji na kufanya mipango yao kuwa bure. Lakini wewe…”
Lea alijilaza kwenye kiti. Alihisi baridi pande zote.
"Imekuwa bahati tuna Alvin, tungeendelea kukuachia kampuni mikononi wako, muda si mrefu tungeisahau KIM International." Mzee Kimaro alitaka kumpiga kofi. “Potelea mbali, sitaki kukuona.”

Lea hakujua alitokaje kutoka kwa nyumba ya familia ya Kimaro. Alikuwa ametumia pesa zake alizochuma kwa bidii kusaidia familia ya Campos, kumbe alikuwa anaisaidia kuiba biashara ya familia ya Kimaro? Hapana, ilibidi arudishiwe pesa yake hata iweje!
Aliporudi kwenye fahamu zake, akamwpigia simu Mason kwa haraka. "Mason, unaweza kunirudishia zile bilioni 60? Usijali, tayari nimezungumza kuhusu hilo na baba yangu. Alisema atamzuia Alvin—”
“Oooh! Pole, mpenzi wangu. Tayari nimempa Jerome pesa hizo,” Mason alisema kwa unyonge, “Jerome tayari amehamisha pesa hizo kwenye akaunti ya KIM International.”
Uso wa Lea ulikuwa mweupe kama karatasi. Alihisi kana kwamba kuna kitu kinamzuia kooni.
“Ni sawa, mpenzi. Unaweza kumwomba Alvin akupe pesa,” Mason alisema kwa furaha, “Asante kwa kuwa msaada mkubwa kwa familia ya Campos. Nakupenda."
Kama ingekuwa zamani, Lea angeguswa, lakini kwa muda huo, mwili wake wote ulihisi baridi. "Mason, nijuavyo, biashara ya familia ya Campos imekuwa ikifanya vizuri miaka hii michache. Je, akaunti yake haina shilingi bilioni 80?”
"Mpenzi, wazazi wangu walisema hakuna pesa. Nadhani hawawezi kunidanganya.”
Lea alifarijika kidogo. Familia ya Campos lazima ilimdanganya Mason pia. Haikuwezekana kwamba Mason angemdanganya.
•••
Katika ofisi kwenye ghorofa ya juu. Baada ya Mason kukata simu, uso wake wa kiungwana ulibadilishwa na sura kejeli na dharau, akaitupa simu yake pembeni.
Jerome alitabasamu kwa furaha. “Uncle, Lea ni mjinga sana. Nilikuwa nasita kumpa Alvin pesa hizo, lakini mama yake katoa bilioni 60 kirahisi kabisa. Hahah, Alvin labda atakufa kwa kufadhaika ikiwa angejua tulichukua pesa za mama yake na kumlipa yeye.”
"Mwanamke huyu anaanza kuwa na shaka," Mason alisema kwa utulivu.
“Haijalishi, lakini, hakuna mtu anayeweza kuzuia kunyanyuka kwa familia ya Campos sasa.” Jerome alitabasamu. “Uncle, unashangaza. Umeinyanyua familia ya Campos peke yako hadi kufikia kiwango hiki?”.
“Ndiyo maana nataka umuoe Melanie haraka iwezekanavyo. Ndoa pekee ndiyo inaweza kufunga familia mbili kwa nguvu kwenye mashua moja.”
“Nitafanya. Baada ya hapo, nitaimeza Ngosha Corporation hatua kwa hatua. Kufikia wakati huo, familia ya Campos ndiyo itakuwa juu ya utukufu wa Kenya.” Jerome alizidi kufurahi huku akiwaza juu yake.
"Sawa, Alvin hapaswi kututawala kwa muda mrefu pia." Mason alikodoa macho.
•••
Usiku huohuo. Katika spa.
Nusu ya mwili wa Lisa ulikuwa umezama kwenye sinki la maziwa. “Mahali hapa ni pazuri sana. Ni mara yangu ya kwanza kuja hapa.” Baada ya kuongea alikodoa macho na kumtazama Charity aliyekuwa anaingia kuoga. "Wow, unaonekana mwembamba lakini una mwili mzuri."
Aibu hafifu ilionekana kwenye uso wa Charity, ambaye ilikuwa nadra kwake kutokeea akiwa uchi kwa wanawake wenzake. Lisa alimtazama kwa husuda. Wakati huo, sauti ya mwanamke ilisikika kutoka upande wa pili wa ukuta.
“Maurine, nilisikia kwamba bei za hapa ni za juu sana. Una pesa gani ya kutuleta hapa?"
"Najua, lazima ni Alvin Kimaro ambaye alikupa pesa, sivyo?"
Maurine alisema kwa aibu, “Bwana Kimaro ni mkarimu sana. Ingawa simhudumii tena, alinipa kadi hii ya benki. Alisema naweza kuitumia nipendavyo.”
“Wow, nina wivu sana. Bwana Kimaro lazima awe amekupenda."
“Mh! Kwa mhudumu kama wewe, hata mtawaanaweza kuvunja nadhiri yake. Inaonekana kama Alvin kakupenda. Ukiniuliza, ningesema unaonekana mrembo zaidi kuliko huyo Lisa. Nani anajua? Unaweza kuwa Bi. Kimaro katika siku zijazo.”

Sura ya: 255

Masikio ya Charity yalihisi kuziba baada ya kusikia maneno hayo. Alikuwa karibu kusimama na kuwafuata, lakini Lisa alikandamiza mabega yake chini.
"Utamwacha aende hivihivi tu?" Charity akamtazama.
“Usiwe na haraka. Hebu tumalize kuoga kwanza.” Lisa akatikisa kichwa na kufumba macho.
Dakika 20 baadaye, Maurine na wanawake wengine watatu walitoka kwenye chumba cha kubadilishia nguo wakiwa wamevaa nguo za kuogea. Mara wakawaona Lisa na Charity wakiwazuia njia.
"Bi Kimaro, unataka kufanya nini? Bila shaka hutanipiga tena, sivyo?” Maurine alikuwa na hofu kwenye uso wake.
Mwanamke mrefu, aliyekonda nyuma yake alikuja mbele na kusema, "Madam Kimaro, hakuna haja ya wewe kumalizia hasira yako kwa mwanamke asiye na hatia. Wakati mwingine wanaume wanapokusaliti, lazima ujitafakari. Baada ya yote, inachukua vidole viwili ili kuvunja chawa.”
Macho ya Charity yakageuka kuwa ya kutisha. “Si ajabu nyie mnapatana. Inaonekana kama ndege wafananao huruka pamoja.”
Lisa alicheka. “Maurine, nataka tu unipatie kadi ya benki uliyo nayo sasa hivi. Alvin na mimi ni mume na mke, mali yake ni mali yetu ya pamoja. Nina haki ya kurudisha pesa alizokupa.”
“Bibi mdogo sijui unaongea nini. Pesa zangu natafuta kwa jasho langu mwenyewe,” Maurine alisema kwa huzuni.
"Kwa kazi ya kuuza mwili wako kwa Alvin?" Charity alimdhihaki, “Maurine, umekuwaje hivi? Nakumbuka ulikuwa mwaminifu sana enzi hizo. Katika siku yako ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 18, ulikataa mkufu wa almasi ambao Sarah alikupa kwa sababu ulikuwa wa bei ghali, mbona umekuwa tofauti sana sasa hivi?”
"Charity, sijawahi kubadilika." Macho ya Maurine yalikuwa yakilengwa machozi.
Macho ya Charity yakaangaza kwa kutoamini.
"Sawa, ikiwa hautaitoa, nitaita polisi." Lisa akatoa simu yake kwa hasira. “Kama bado utaikatalia kadi yenye jina la mume wangu mpaka polisi watakapokuja, nitasema wewe ni mwizi na utasema uliipata wapi. Kwa kweli, ikiwa una uwezo, unaweza kumpigia simu Alvin aje."
Alipoona karibu mambo yanakuwa mazito, Maurine aliuma mdomo wake na kutoa kadi mfukoni mwake. “Unaweza kupiga simu polisi, lzkini kadi hii nilipewa na Rodney. Ninaweza kumwita aje na kuhakikisha jambo hili.”
Marafiki zake walipigwa na butwaa. "Maurine, si ulisema sasa hivi kwamba ni Alvin aliyekupa?"
Uso wa Maurine ulikuwa mdogo kwa aibu. Aliongea kwa kigugumizi, “Kadi ambayo Alvin niliisahau nyumbani…”
Charity alimdhihaki, “Kwanini wote wawili Alvin na Rodney walikupa kadi ya benki? Nilisikia kwamba matajiri wanapenda kushea wanawake wao na marafiki zao. Kumbe ni kweli?"
Jinsi marafiki wa Maurine walivyomchukuia ilikuwa tofauti ghafla. Macho yao sasa yalikuwa yamejaa dharau na kebehi.
"Charity, twende." Lisa alimshika Charity mkono na kuondoka zao. Kwa kuwa kadi ambayo Maurine alikuwa nayo ilikuwa ya Rodney, hakuwa na haki ya kuendeleza jambo hilo zaidi.
Charity alimtazama tena Maurine na kunong'ona, "Maurine huyu ni wa ajabu."
“Ndiyo, ni mtu anayejua kujirahisisha…”
“Hapana, Maurine binamu wa Sarah ninayemfahamu mimi ni tofauti na huyu. Mara nyingi alikuja nyumbani kwetu kucheza. Nilikutana naye mara nyingi wakati huo. Kutokana na kile ninachokumbuka, Maurine alikuwa mtu mwaminifu na mwenye tabia njema. Nilimjaribu sana kipindi hicho lakini hakuwa na tamaa hata kidogo. Katika siku yake ya kuzaliwa ya 18, Sarah alimpa zawadi ya mkufu wa almasi, lakini aliukataa kabisa…”
Moyo wa Lisa ulidunda kwa nguvu. "Unataka kusema kwamba Maurine huyu ni feki?"
Charity akaitikia kwa kichwa. "Si hivyo tu, Maurine aligonga lori kwa bahati mbaya siku za nyuma alipokuwa akiendesha baiskeli kurudi nyumbani akitoka shule. Vipande vya chuma kwenye lori viliacha jeraha kubwa kwenye shingo yake, na kovu likabaki milele. Hata hivyo, shingo ya Maurine huyu haina kovu lolote sasa hivi….”
Hatua za Lisa zilisimama. Kichwa chake kilikuwa karibu kulipuka. Ikiwa Maurine huyo alikuwa feki, ni nani aliyekuwa anajifanya Maurine na nia yake ilikuwa nini?

Kweli, alipokutana na Maurine kwa mara ya kwanza, alifikiri kwamba macho na sauti yake ilikuwa ya kawaida sana. Tabia yake ilimfanya amfikirie… Lina. Ubaridi uliuvaa ghafla mwili wake.
“Charity, sitaendelea kukaa hapa kwenye spa tena. Nilikumbuka tu kwamba nina kikao cha kuhudhuria. Nitaondoka kwanza.” Lisa alibadili nguo haraka haraka na kurudi nyumbani kwa kasi.
Aliposukuma mlango wa nyumba yake ya kifahari, alimwona Alvin akiwa amekaa kwenye sofa mle ndani akifanya kazi zake.
“Lisa si ulisema unaenda spa? Mbona umerudi mapema." Alvin akaweka laptop yake chini na kusimama. “Umekula—”
“Alvin, hebu nikuulize, ulikutana na Lina ulipokuwa bado Dar es Salaam baada ya kila kitu kutokea?” Lisa alimkatisha.
"Kwanini unauliza kuhusu Lina?" Macho ya Alvin yakawa ya kutisha.
“Baada ya Jones na mkewe kwenda jela, Lina alitoweka ghafla. Ulikuwa na uhusiano wowote na kutoweka kwake?" Lisa alimkazia macho.
Alvin alikunja uso. "Ni kweli. Nilimpa somo dogo. Yeye…” Ghafla alisikia maumivu makali kichwani mwake. “Nilimfanya nini? Kwanini sikumbuki?”
Moyo wa Lisa ulifadhaika. Alidhani kumbukumbu ya Alvin ilikuwa nzuri wakati wote. “Mpigie Hans umuulize. Hakika anajua.” Alvin alisema na kumshangaza sana Lisa.
Lisa alimpigia simu Hans. "Unakumbuka Alvin almfanya nini na Lina Jones? Usiwe na wasiwasi, ni yeye aliyesema nikuulize."
“Bwana Mkubwa, si uliniambia nimpeleke Lina kwenye kijiji cha ukiwa na kumuozesha kwa yule mzee?” Hans alishangaa.
Lisa akamwuliza harakaharaka. “Kijiji hicho kiko wapi?”
“Usijali Bi Mdogo. Lina lazima atakuwa anateseka sana kwa sasa. Hawezi kamwe kutoroka kutoka hapo kwa maisha yake yote,” Hans alisema kwa uhakika.
"Fuatilia kujua kama bado yupo huko au la…" Alvin aliamuru.
“Bibi mdogo…”
“Fanya kama nalivyosema,” Lisa aliongea kwa sauti thabiti.
“Sawa.” Hans alikubali tu.
Baada ya simu kukatika, Alvin aliuliza kwa sauti ya kutoridhishwa, “Kwanini umerudi ghafla na kuuliza kuhusu Lina?”
“Mimi ndiye ninayepaswa kukuuliza. Kwanini hukumbuki mambo uliyofanya hapo awali?” Lisa alimkazia macho. "Na maumivu ya kichwa chako yanatokana na nini?"
“Una wasiwasi na mimi?” Macho ya Alvin yakaangaza. Alinyoosha mikono yake na kumkumbatia. "Nilijua. Bado unanijali.”
“Alvin, acha kuekti ujinga. Nani anakujali wewe…” Wakati Lisa akihangaika kumsukuma, alishangaa kuona alama za sindano nyuma ya mkono wake. Alikumbuka Hans akisema kwamba Alvin alikuwa amezimia siku chache zilizopita.
“Mbona umeacha kuongea?” Alvin alizika uso wake kwenye shingo yake, na akasikia harufu ya kushangaza. “Lisa, una harufu ya maziwa mwilini mwako. Una harufu nzuri…” Lisa aliona haya. Alinukia vizuri kwa sababu alikuwa ameoga maziwa.
Hata hivyo, bado walikuwa katika ugomvi. Angewezaje kutaka kustarehe naye? Alikuwa anaota! Alimsukuma na kupiga hatua chache nyuma.
“Maurine wako ana harufu hii ya maziwa pia. Nilikutana naye na marafiki zake ambao kwa bahati walikuwa wakioga jirani kwenye spa. Alijitapa kuwa ulimpa kadi ya benki ya kutumia atakavyo.”
Alvin alikunja uso akiwa hafahamu chochote kuhusu hilo. "Sijawahi kumpa kadi ya benki. Maurine anawezaje kusema mambo kama hayo?”
"Unamaanisha nini? Unafikiri ninamsingizia?” Lisa karibu kufa kutokana na kuchanganyikiwa.
Alvin alijikaza. Kwa kawaida, kwa hadhi yake, alikuwa akiongea tu bila kuficha. Hata hivyo, alijionea kwamba kuzungumza ovyo kungeleta shida tu. “Sawa, hukumsingizia. Yote ni makosa yangu.”
“Kwa hiyo ulimpa kweli?” Lisa alimpiga teke kwa hasira na kwenda juu kwa hasira.

TUKUTANE KURASA 256-260

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......256-260

Sura ya: 256

Alvin aliibana miguu yake na kuguna kabla ya kumfuata ghorofani. Alipofika ghorofani, alimkuta Lisa akijiandaa kwenda kuoga. Alifungua kabati na kugundua nguo nyingi za kiume na hata chupi za kiume ndani.
Kichwa chake kilikuwa na maumivu kutokana na hasira. "Alvin, ni nani aliyekuruhusu kuweka nguo zako hapa?!"
''Sikuwa na nguo za kubadili tangu nimehamia hapa. Kwa hiyo niliamua kuleta chache." Alvin alisimama nyuma yake na kusema kama jambo la kweli.
Lisa alichukua nguo zake akitaka kuzitupa chini. Hapo hapo, Alvin alisema bila kujali, “Unaweza kuzitupa nje kabisa. Nitamwomba Hans alete nguo mpya kesho.”
Lisa ilibidi kujisalimisha kwa tabia yake isiyo na aibu. "Sawa, ninakubali kukuruhusu ukae hapa. Lakini utakaa kwenye chumba cha wageni."
"Hapana." Alvin akapepesa macho yake meusi. “Sababu ya mimi kuhamia hapa ni kulala chumba kimoja na wewe. Kwanini unataka nihamie kwenye chumba kingine? Mimi si mjinga.”
Lisa alizidi kuchanganyikiwa. Yeye ndiye aliyevamia nyumba yake, lakini alikuwa akijifanya kana kwamba ndiye mmiliki wa nyumba hiyo. Lisa aliogopa kwamba angekufa kwa hasira ikiwa angendelea kuzungumza naye, kwa hiyo akaenda kuoga.
Alipotoka kuoga alimuona Alvin akiwa ameshika mop. Alikuwa anasafisha sebule ya kulia chakula. Mwendo wake ulikuwa wa kusuasua kiasi kwamba ilionekana kana kwamba alikuwa ameshika mop kwa mara ya kwanza.
Lisa alificha mkanganyiko aliokuwa nao moyoni. Aligeuka na kuweka nguo kwenye mashine ya kufulia kwenye chumba cha kufulia. Alipomaliza, alimuona Alvin akiwa anadeki sebuleni sasa.
Dakika kumi baadaye, Lisa alishuka kwenda kuchukua mtindi kutoka kwenye friji. Aliporudi alimwona Alvin akisafisha tena sebule ya kulia chakula.
Lisa alikunja uso. "Inatosha. Unataka kubandua sakafu? Sio lazima uendelee kudeki sehemu ya kulia chakula mara zote hizo.”
"Ni saa ngapi nilideki sebule ya kulia?" Alvin alizuia huzuni yake na kusema, "Bado sijasafisha chumba cha kulia chakula."
"Alvin, acha kujifanya hujui unachokifanya!" Lisa alikosa la kusema.
“Nimesema nini kibaya?” Alvin alionekana kuwa na huzuni.
Lisa hakumwelewa kabisa Alvin, alikuwa anajaribu kumuigizia makusudi au alikuwa na tatizo? Lisa alitulia na kujaribu sana kumchunguza kwa makini. Ilionekana kana kwamba hakuwa anajifanya. Wakati huo, alikumbuka alipomuuliza kuhusu Lina hapo awali. Hakuweza hata kukumbuka alichomfanya hapo awali. Pia alishangazwa na kuumwa kwake na kichwa na kuzimia, mbona hakuwa na dalili hizo hapo awali? Moyo wake uliruka mapigo.
"Sawa, chukulia sijasema chochote." Lisa aligeuka na kwenda juu. Hata alifunga mlango kwa makusudi.
Haikupita hata nusu saa, Alvin alifungua mlango kwa urahisi na kuingia ndani. Lisa ambaye alikuwa amevua nguo zake zote alikuwa anajipaka mafuta. Aliposikia kelele za mlango kufunguliwa, alipiga kelele na kuvuta nguo zake mara moja. Hata hivyo, hakuweza kuchukua nguo kwa wakati kwa kuwa alikuwa amechanganyikiwa sana. Maeneo makubwa ya mwili wake bado yalikuwa wazi.
Alvin mwanzoni hakuwa na mawazo yoyote, lakini kuona Lisa alivyokuwa amenona maeneo fulani ilimfanya ahisi joto.
"Kwanini umefunika huko?" Alvin alienda mbele na kumshika bega lake lililokuwa wazi kwa mkono mmoja huku akiitoa mikono yake iliyofumika chini ya kitovu kwa mkono mwingine.
Lisa, ambaye hatimaye alifanikiwa kujizungushia shuka maeneo yake nyeti, aliona macho ya Alvin yakianza kuwaka kwa uchu wa kingono. Alikuwa na aibu na hasira. "Alvin, umeingiaje chumbani kwangu wakati niliufunga kwa funguo?"
“Hii…” Alvin akamuonyesha ufunguo mkononi mwake. "Huu ni ufunguo ambao unaweza kufungua kila kitu."
Lisa alikuwa karibu kuzimia. Kitu cha aina hiyo kweli kilikuwepo! Lisa alitaka kumpokonya, lakini Alvin alikuwa na kasi zaidi na haraka akawahi kuuweka mbali. Hakuweza kuwahi kasi yake na akaanguka kifuani mwake.
"Njoo tulale." Alvin akamkumbatia.


Lisa alijitahidi kutoka kwenye kumbatio lake lakini alishindwa. Bila kufikiria, alimuuma sana begani.

Alvin hakuhisi maumivu yoyote na akamtazama tu kama kawaida. “Endelea kuuma. Hukuwahi kunaimbia kuwa kumng’ata mtu ni ishara ya upendo? Uking’ata sana ndivyo unavyonipenda sana.”
Lisa karibu azibe mdomo kwa mshangao. Hiyo ilikuwa zamani sana, lakini bado aliikumbuka. Sasa kwanini muda mfupi uliopita alikuwa akipoteza kumbukumbu?
“Mbona hauumi tena? Unaogopa kuniumiza?” Alvin aligusa masikio yake kama mtoto wa paka, sauti yake ilikuwa nyororo yenye nguvu ya sumaku. "Ni sawa, we ng’ata tu, siogopi maumivu."
Lisa alikuwa ameshuka moyo kabisa sasa. Ikiwa angemng'ata, ilikuwa ishara ya mapenzi, lakini ikiwa asingemng’ata, basi ilimaanisha kuwa aliogopa kumuumiza. Alikuwa mwathirika wa ule usemi wa ‘ukinipiga umenionea, ukiniacha umeniogopa!’ Hakukuwa na jinsi angeweza kushinda dhidi yake.
"Twende tukalale." Alvin alimkumbatia na kuzima taa kabla ya kulala. Muda si mrefu alilala baada ya kupumbazwa na harufu yake nzuri.
Lakini, Lisa hakuweza kulala. Alikuwa anapata njaa kutokana na mawazo. Alikula sana wakati wa chakula cha jioni na Charity, lakini alikuwa na njaa tena kabla haijafika hata saa tano usiku. Ni lini hamu yake ya kula iliongezeka kiasi hicho?
Siku inayofuata, Lisa alipozinduka, tayari ilikuwa saa tatu asubuhi. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuamka akiwa amechelewa sana. Alishuka haraka haraka, Alvin aliyekuwa amekaa kwenye sofa akisoma gazeti, mara akainuka. "Nimekuandalia kiamsha kinywa, kwa hivyo-"
"Alvin Kimaro, ulizima kengele yangu?" Lisa alimkatisha kwa hasira.
"Kengele yako ililia kwa muda mrefu lakini ulikuwa bado umelala kama nguruwe mdogo, kwa hivyo niliizima."
"Hiyo haiwezekani. Kawaida mimi huamka kwa sauti ndogo tu.” Lisa alishtuka, akakataa kukubali kwamba alikuwa amelala sana.
Macho yake yalikuwa yamemtoka pande zote, na nywele zake zilikuwa zimechanganyikana alipoamka tu.
Alvin alicheka tu. “Nilijua kwamba ungenilaumu Kwa bahati nzuri, nilirekodi video kama uthibitisho.”
Alicheza video hiyo. Kwenye skrini, Lisa alikuwa amelala fofofo juu ya mkono wake huku kengele ikilia kwa nguvu. Alikunja uso tu na kuvuta blanketi kabla ya kuendelea kulala.
Kama asingeona hiyo kwa macho yake mwenyewe, asingejua kuwa alilala hivyo. Hata alitumia mkono wake kama mto. Ilikuwaje, mbona hakuwa na mazoea ya kulala sana?
“Kuwa mvumilivu. Kifungua kinywa kiko kwenye jiko. Kitakuwa tayari muda si mrefu.” Alvin aliutazama uso wake uliopooza na kutabasamu. Kisha, akaenda jikoni kupika.
Hapo awali Lisa alitaka kusema 'Sitaki kula', lakini tumbo lake liliguna ghafla, hivyo hakuweza kusema maneno hayo. Hata hivyo, yeye ndiye aliyempikia kabla. Ilikuwa wakati wake wa kumlipa.
Dakika tatu baadaye, bakuli la tambi lilitolewa. Lisa alionja na kupata ladha isiyo ya kawaida. “Hukuweka chumvi?”
"Hiyo haiwezekani. Nakumbuka niliweka.” Alvin alionja na kugundua kuwa kweli hakuweka chumvi.
"Leta chumvi.” Lisa akaamuru.
Alvin alinyanyuka kufuata chumvi. Lisa alimtazama akitembea kuelekea sehemu tofauti kabisa. “Subiri, chumvi iko jikoni. Kwanini unaenda chooni?”
Alvin aliduwaa kana kwamba ameamka kutoka kwenye ndoto na kubadili njia kuelekea jikoni.
Nyuma yake, uso wa Lisa uliongezeka kuwa na mshangao zaidi. Alikuwa akiigiza kama bibi yake ambaye alipata shida ya akili, lakini Alvin alikuwa bado mdogo sana…
Ghafla, kengele ya mlango ililia. Alifungua geti na Hans akaingia kwa haraka huku akiwa amekunja sura nzito. “Bibi mdogo, nilipata mtu wa kuchunguza jambo hilo jana usiku. Lina Jones alitoroka miezi michache iliyopita.”

Sura ya: 257

Kama ilivyotarajiwa… Lisa alikuwa na uhakika zaidi wa jibu moyoni mwake sasa.
Hata hivyo, uso wa Alvin ukabadilika kwa hasira. “Mjinga wewe! Ungewezaje kumruhusu atoroke hata baada ya kumpeleka kwenye kijiji hicho cha mbali kabisa?”
Hans alikasirika lakini akajizuia. "Mzee huyo alisema kuwa kuna gari lilimchukua alipokuwa akimkimbiza."
“Ni vigumu kuamini kwamba Lina Jones bado ana marafiki wowote. Nenda ukafuatilie gari hilo,” Alvin aliamuru kwa ukali.
“Sawa.” Hans alinyamaza na hakuweza kujizuia kuuliza, “Bibi mdogo, uliniuliza ghafla nimchunguze Lina Jones jana. Je! unafahamu kitu chochote?"
Alvin naye alimtazama Lisa kwa kuchanganyikiwa.
“Siwezi kukuambia sasa hivi.” Lisa alitazama pembeni. Alvin pengine asingemwamini kama angesema kwamba Maurine Langa anaweza kuwa Lina Jones. Angeweza hata kumlaumu kwa kutumia mbinu chafu kumpakazia Maurine.
"Niambie. Sipendi unaponificha mambo.” Alvin alimvuta begani kwa ubabe.
Lisa alikosa la kusema. “Basi kwanini hukufikiria jinsi nilivyohisi ulipoweka Maurine Langa kama muuguzi wako huku ukinificha ukweli?”
Alvin akafunga breki ya mdomo kuhusu hilo, akageuza mada. "Kula. Tambi kabla hazijapoa.” Hakuthubutu kuuliza chochote zaidi kwani aliogopa kumchukiza.
Lisa aliinama tena kuendelea kula kifungua kinywa chake. Lakini alipoonja tu tena akahisi kukasirika. "Alvin, chumvi yangu iko wapi?"
“Hii hapa.” Alvin akamkabidhi ile chumvi huku akionyesha mbwembwe.
Hans alikosa la kusema kabisa baada ya kutazama tukio hilo. Hakutarajia kamwe kama Alvin alikuwa ni mtu wa utani kiasi hicho.
Jina lake la WhatsApp pia lilikuwa limebadilishwa na kuwa jina la utani kama 'Ni Wako Pekee', na kufanya kila mtu afikiri kwamba akaunti yake ilikuwa imedukuliwa.
“Enhee! Hans, si ulisema kuna mkataba wa ugavi nilipaswa kusaini jana? Umekuja nayo leo?" Alvin aliuliza ghafla.
Hans alishangaa. “Bwana Mkubwa, tayari ulitia saini jana, hukumbuki?”
Alvin alikunja uso na kutaka kukumbuka zaidi, lakini kichwa kilimuuma tena na uso ukawa umekunjamana kwa maumivu.
“Bwana Kimaro, twende hospitali. Unahitaji dripu ya IV." Hans alimtazama Lisa kwa kumsihi. “Bibi mdogo, unaweza kumpeleka? Gari langu liliharibika na nilichukua teksi kuja hapa. Bibi Mdogo, Bwana Mkubwa anahitaji kupata dripu ya IV kila siku. Lazima aende.”
Lisa alikosa la kusema. Hakuwa tayari kabisa kuamini hilo. Ilikuwaje Alvin akawa mgonjwa sana?
"Ngoja nimalize mlo wangu." Alichukua tena uma wake. Alvin alimpiga Hans kwa siri sura ya kufurahisha kwa kazi nzuri ya kumshawishi Lisa ampeleke hospitali.
Dakika 15 baadaye, Lisa alitoa BMW mpya kutoka karakana. Kabla ya Alvin kuingia ndani, aligeuka na kumwambia Hans, “kalete gari mpya nililomnunulia majuzi.”
Lisa ghafla akakumbuka kuwa gari alilompa lilikuwa na plate namba ya '4EVA. Lilikuwa gari pekee la aina yake nchini, hivyo alifurahi sana alipolipokea. Hata hivyo, hakuwa na haja malo tena.
"Hakuna haja, silipendi tena." Baada ya kumaliza kuzungumza, aliongeza, “Alvin, unapaswa kuacha tabia yako ya kutumia namba kutangaza mapenzi yako kwa wengine. Ninaogopa nitachukizwa ikiwa nitaingia ndani ya gari hilo.” 4EVA? Upuuzi gani. Kufikiria tu kulimfanya atamani kutapika.
Uso wa Alvin uliingia simanzi mara moja. "Sikufikiria kulipua fataki saa mbili usiku kila siku ya Ijumaa. Ilikuwa wazo la Rodney—”
“Ndiyo, Bi Kimaro. Ninaweza kuthibitisha hilo,” Hans alisema kwa umakini.

Lisa alitabasamu na kutikisa kichwa. “Oh, najua. Jina la Alvinarah pia halikupendekezwa na wewe, lakini lilikuwa wazo la Chester. Pia haukuwa na wazo la kuita jina la Sarah katika ndoto yako. Alikuwa ni Sarah ambaye alikukumbuka kutoka kwenye ulimwengu mwingine."
Alvin akaishia kuguna tu tena. Kama wakili, ilikuwa mara ya kwanza kupata hisia za kushindwa kujitetea.
Baada ya gari kufika hospitali, Lisa alisema bila kujali, “Nimekufikisha hospitali. Lazima niende ofisini kwa ajili ya mkutano.". Lisa akawasha gari na kuondoka. Hakutaka kuwa na moyo wa huruma kwa sababu tu Alvin alikuwa akionyesha huruma. Ni nani ambaye alimhurumia alipokuwa na huzuni na kuteseka?

Wakati anaondoka, ghafla akamwona Maurine Langa akiwa amevalia nguo ndefu ya maua ya bluu. Nywele zake ndefu zilipepea huku akiwa ameshikilia rundo la maua mkononi mwake.
Lisa ghafla akaahirisha kuondoka na kumpigia simu Hans. “Upo wodi gani?”
"Bibi mdogo, unakuja?" Hans alishangaa sana.
“Ndiyo.”
"Ghorofa ya 5, wodi ya VIP6."
Baada ya Hans kumalizia simu pale juu, aligeuka na kuona macho ya Alvin yakiwa yanawaka moto wa furaha. “Anakuja?”
“Ndiyo.” Hans alicheka. "Inaonekana anakupenda. Ingawa maneno yake ni makali, bado hawezi kukuacha utoke moyoni mwake."
Alvin alitabasamu na papo hapo akamgeukia muuguzi, “Fanya hivi baadaye…” Alvin akautoa mkono wake ghafla. “Nidunge sindano ukisikia mlango unagongwa, lakini uchome vibaya ili damu itoke zaidi. Kadiri itakavyoonekana kutisha zaidi, ndivyo nitakavyokupa pesa nyingi zaidi.”
Nesi alipigwa na butwaa. Hakuwahi kufikiria kwamba Alvin angetumia mbinu ya kitoto ya kujidhuru ili kupata huruma ya mwanamke. Ilibadilisha kabisa mtazamo wake kwake.
Dakika tano baadaye, hodi ikasikika. Nesi akashtuka na kumchoma sindano vibaya Alvin na kusababisha damu kutoka. Alvin aliuma mdomo wake uliopauka kidogo. Mwonekano dhaifu ulifunuliwa kwenye uso wake mzuri na maridadi. Ingawa alikuwa na maumivu, bado alionekana kuvutia.
Moyo wa nesi ulikaribia kuyeyuka. Alvin alikuwa mwigizaji mzuri sana. Angeweza kuiba mioyo ya wasichana wadogo na hata wanawake wazee. Angeweza kuwafanya wasitake chochote zaidi ya kumlinda mikononi mwao.
Wakati huo, Hans alifungua mlango na Maurine, ambaye aliingia na maua safi, mara moja akageuka sura. "Bwana Kimaro, kwanini unavuja damu nyingi?"
Uso wa Alvin haukuweza kujizuia kuwa mkali. Maurine alikimbia na kumsukuma nesi, akimshutumu kwa maneno makali, “Unajua hata kufanya kazi yako? Unawezaje kumuumiza mgonjwa namna hii?”
Nesi akagugumia, “Mimi...” “Bwana Kimaro, alisema...” Maurine haraka alichukua usufi wa pamba kutoka kwenye trei ili kukandamiza jeraha lake linalovuja damu.
Alvin alitaka kumzuia, lakini Maurine alimng'ang'ania. “ Bwana Kimaro, usiogope. Tukiacha hivi itavimba. Inauma? Nitakupuliza…”
Lisa aliingia ndani wakati huo. Hapo awali hakutaka kukasirika, lakini mara baada ya kuingia, alimuona nesi akiwa amesimama pembeni huku Maurine akiwa amemshika mkono Alvin. Midomo yake ilikuwa karibu kugusana na mkono wa Alvin.
Alipofikiria jinsi alivyokaribia kuamini kuwa hakukuwa na kitu kati yake na Maurine, Lisa hakutaka kitu zaidi ya kujipiga makofi mawili.
Sura ya: 258

"Lisa, usielewe vibaya." Alvin alimsukuma Maurine bila fahamu. “Aliuona mkono wangu ukivuja damu, kwa hiyo—”
“Sawa, lakini muuguzi si yuko hapa? Ina uhusiano gani naye?" Lisa alimkatisha kwa hasira. “Kwa kuwa huwezi kuvumilia kumuacha kiasi hiki, mbona bado unanisumbua? Unaona raha nikishuhudia mahaba yenu?”
Uso mzuri wa Alvin mara moja ukageuka kuwa mbaya kama mzimu. Haikujulikana ikiwa ni kwa sababu alikuwa amepoteza damu nyingi au kwa sababu alichomwa na maneno ya Lisa.
Maurine alieleza kwa haraka, “Bibi Mdogo, Maneno ya Bwana Kimaro yote ni ya kweli. Angalia mkono wake, bado unavuja damu…”
“Funga mdomo wako.” Lisa alimfokea. “Maurine Langa, nimekuvumilia kwa muda mrefu sana. Unafikiri mimi ni boya siyo?” Ghafla alikimbia na kushika nywele ndefu za Maurine na kuzivuta kwa nguvu, kisha akamchapa makofi kwenye mashavu yote mawili.
“Ahhhh! Bibi mdogo, usinipige! Bwana Kimaro, nisaidie!” Maurine alilia na kuhangaika huku akiburutwa pembeni na Lisa.
“Lisa, tulia. Mwache aende zake." Alvin alikimbia kumvuta Lisa.
Hata hivyo, Lisa alikataa kuachia nywele za Maurine, na kumfanya mwanamke huyo apige kelele kubwa kwa maumivu.
"Lisa Jones, unapibu kifo?" Rodney, aliyeingia ghafla aliona tukio hili na mara moja akamwangusha Lisa chini. Alikuwa na nguvu nyingi, hivyo Lisa alijibamiza chini na kuumia vibaya.
Maumivu yale yalisababisha mwili wake kuhisi kusambaratika. Hata hivyo, suala kubwa zaidi ni kwamba alihisi kitu kikimtoka sehemu za siri. Ghafla, muuguzi alimnyooshea kidole na kupiga kelele, “Unavuja damu!”
Lisa alitazama chini na kuona damu ikichuruzika kutoka chini alipokuwa amekaa. Aliigusa kwa mkono wake. Bado kulikuwa na mchuruziko mwingi. Akili yake ilimtoka.
Alvin alimnyanyua kwa woga. “Muite daktari haraka!” Alipiga kelele na kukimbilia chumba cha dharura huku akiwa amembeba Lisa. Kwa haraka daktari akampeleka Lisa kwa uchunguzi wa mwili.
Mlango ulipofungwa, Alvin alikuwa akisubiri nje kwa hamu. Maurine alikuja huku akilia. “Bwana Kimaro, samahani. Yote ni makosa yangu. Bibi Mdogo kanielewa vibaya tena.”
Alvin alimtazama kwa macho yaliyojaa hasira. Mwanzoni, aliamua tu kumwacha Maurine lakini hakuridhika naye. Wakati huo, hata hivyo, hisia kali za chuki zilimpanda alipokumbuka kuona Lisa akivuja damu.
“Si nilikuambia uondoke? Nani alikuambia uje?”
Rodney alisimama mbele ya Maurine. “Maurine alikuja tu kukutembelea kwa nia njema. Lisa Jones ndiye aliyempiga bila sababu yoyote.”
“Ni mke wangu. Hukupaswa kumsukuma.” Kifua cha Alvin kilijawa na hasira kali.
Rodney alikasirika. “Nilimsukuma tu, kwani nilijua kama angeanguka? Labda ni kipindi chake cha kuingia mwezini. Usifadhaike kwa hilo.”
"Afadhali uombe jambo baya lisimfike." Alvin hakuweza kuhangaika kuzungumza naye upuuzi kwa kuhofia kukasirishwa. Hata hivyo, pia alitumaini kwamba Lisa alikuwa tu kwenye kipindi chake.
Nusu saa baadaye, daktari alitoka na Alvin akamfuata. "Daktari, vipi hali yake?"
“Bwana Kimaro, ujauzito aliobeba mke wako umetikisika na mwili wa mkeo unaonyesha dalili za kuharibika kwa mimba. Inabidi abaki hospitalini ili kuzuia hali hiyo.”
“Ana mimba?” Alvin aliganda mwili mzima.
“Ndiyo, ni zaidi ya mwezi mmoja. Ni mapacha wa kufanana.”
“Mapacha wa kufanana?” Mwili wa Alvin ukazidi kutetemeka kwa mshtuko.
“Ndiyo, mapacha, lakini ni kwa sababu ni mapacha ndiyo maana hata ameweza kuathirika kwa urahisi,” daktari alisema kwa hasira, “Ninyi ni watu wazima mnahitaji kuwa makini zaidi. Ikiwa ajali hii ingetokea nje ya hospitalini leo na asingepata matibabu kwa wakati, basi vitoto vingekuwa vimepotea. Ikiwa kuharibika kwa mimba kwake kunaweza kuzuiwa au la itategemea jinsi mambo yanavyoendelea baadaye.”
“Asante daktari.” Alvin ghafla alihisi kupasuka kwa hofu.

Yeye na Lisa walikuwa tayari kupata mtoto pamoja, lakini hakuna kitu kilichotokea kati yao tangu Maurine atokee. Zaidi ya hayo, daktari huko Dar es Salaam pia alikuwa amesema kwamba ingekuwa vigumu kwake kupata mimba kutokana na hali ya mwili wake, kwa hiyo hakuwahi kufikiria sana jambo hilo. Lakini, alikuwa amebeba watoto wake sasa. Walikuwa mapacha. Jambo la kusikitisha ni kwamba watoto wangeweza kupotea. Alihisi kama ameanguka kutoka mbinguni hadi duniani.
"Rodney Shangwe!" Alvin alimpiga Rodney ngumi ya uso kwa hasira.
“Ningejuaje kuwa ana mimba?” Rodney pia alikasirika kidogo lakini alikataa kukiri kosa lake. "Lilikuwa kosa lake kutogundua kuwa ana mimba na kuzunguka na kuwapiga watu wengine kama mwanamke mwendawazimu. Ni kosa lake mwenyewe!”
“Ondoka nje!” Alvin alimpiga teke kali. "Chukua Maurine wako mpotee! Nakuonya usije tena hospitali kuniona, sawa?”
Baada ya yote, walikuwa marafiki kwa miaka mingi. Hakutaka wafukuzwe hospitalini.
“Sawa, hatutakuja tena. Maurine wende zetu.” Rodney alimvuta Maurine na kuondoka.
Maurine aliinamisha kichwa chake huku sura ya kero ikimulika machoni mwake. Hakutarajia Lisa kuwa mjamzito, na mapacha pia. Kwanini alikuwa na bahati sana? Watoto hao hawakupaswa kuruhusiwa kuwepo!
Lisa aliposukumwa nje ya chumba cha dharura, bado alikuwa amechanganyikiwa. Alipataje mimba? Alikuwa hata amebeba mapacha. Kama ingekuwa zamani, angekuwa na furaha, lakini sasa… alikuwa na hisia tofauti moyoni mwake. Baada ya yote, walikuwa mwili na damu yake mwenyewe—watoto wake. Alipenda na kutaka, lakini hii ingemfanya ashikwe zaidi na Alvin.
“Lisa, usijali. Watoto wetu wataokolewa.” Uso wa Alvin uliokuwa umefadhaika mara moja ukatokea mbele yake. Wakati huo, uso wake ulikuwa umejaa furaha. “Unashangaza sana. Ni mara ya kwanza na unanipa mapacha. Mtoto, wewe nikupendeje8?"
“Unaweza kuondoka? Naudhika kwa kukutazama tu.” Lisa alijisikia vibaya na alikuwa mwepesi wa kukasirika.
“Siwezi. Wewe ni mama wa watoto wangu, kwa hiyo ni lazima nikutunze vizuri.” Alvin hakuwa na hasira hata kidogo. “Nesi, tafadhali mlete kwenye wodi yangu. Nitamtunza mwenyewe.”
“Sitaki.” Lisa alimkazia macho. "Isipokuwa unataka kunikasirisha hadi kuharibika kwa mimba."
Daktari hakuweza kujizuia kumkumbusha, “Bwana Kimaro, hupaswi kuwasumbua wanawake wajawazito. Jambo muhimu kwa sasa ni kumwacha awe mtulivu. Kuwa mwenye busara na makini na na zingatia lishe yake. Mwache alee vijitoto kwa amani ya akili.”
“Sawa, basi muweke kwenye wodi iliyo karibu na yangu. Siwezi kuvumilia kuwa mbali na yeye.” Alvin aliwaza na kuongea.
Lisa hakutaka chochote zaidi ya kukaa mbali naye kadiri awezavyo, lakini kila mtu hospitalini alimsikiliza kwa utiifu Alvin, hivyo upesi akapangiwa wodi namba 6 VIP.
Aunty Yasmine naye alipangwa kumhudumia. "Bibi mdogo, hongera! Mimi ni mzuri katika kupika vyakula vyenye lishe. Nitahakikisha unajifungua watoto wawili wenye afya njema, Bi.Kimaro.”
"Lo, ni bora ikiwa ni mvulana na msichana, lakini hata wasichana wawili itakuwa poa tu." Alvin alitabasamu kwa furaha. "Napenda mabinti zaidi. Lakini wote ni sawa, watoto ni watoto tu!"
"Hahah, pamoja na sura zenu zilivyo za kuvutia, haijalishi kama ni wavulana au wasichana, wataonekana wazuri sana," Aunty Yasmine aliunga mkono.
"Ndio, nafikiri hivyo pia." Akiwasikiliza wakizungumza, Lisa alishindwa kuvumilia na kusema, “Alvin Kimaro, unaweza kutoka? Si unatakiwa kuwekewa dripu ya IV?”

Sura ya: 259

Alvin alikwenda kitandani na kumtazama kwa macho ya upole. “Lisa, kwa kweli hakuna kinachoendelea kati yangu na Maurine. Yule nesi aliyenichoma sindano hiyo alisababisha mkono wangu utokwe na damu, na Maurine akamsukuma nesi alipoona damu ikivuja kwa wingi. Ndio maana ulikiona ulichokiona hapo awali. Usikasirike. Wewe ni mama sasa."
Lisa alicheka. Alikuwa akimlaumu kwa kuwa na akili ndogo hata baada ya kuwa mama. Alikuwa akimtwika lawama sasa. “Shangazi Yasmine, unaweza kuniletea simu yangu?” Hakutaka kuzungumza naye.
Aunty Yasmine akamkabidhi simu. Lisa alituma ujumbe kwa Pamela na kuanza kucheza mchezo bila kumwangalia Alvin hata kidogo. Alvin alikaa kwa muda hadi alipotolewa na daktari kwenda chumba cha pili kuwekewa dripu ya IV.
Hans aliingia na rundo la nyaraka, lakini Alvin akazifyagilia mbali. “Siko katika hali ya kusoma hizi sasa. Nenda uninunulie vitabu vya mwongozo wa kulea wanawake wajawazito.”
Hans alikuwa anaumwa na kichwa sasa. "Hapana, hati hizi ni za muhimu sana -"
"Ni za muhimu zaidi kuliko watoto wangu?" Macho ya Alvin yalikuwa makali.
Hans hakuwa na lakusema tena.
Mchana, Pamela aliingia na kumuona Lisa akinywa uji wa lishe akiwa amelala kwenye kitanda cha hospitali. Alipumua, akisema, "Inaonekana hautaweza kutoroka kamwe kwenye mikono ya Alvin Kimaro maishani mwako."
Lisa alihisi kuchanganyikiwa. Pia alikuwa amelifikiria tatizo hili. Hakuweza kufikiria kuwatoa watoto hao, lakini ikiwa angewazaz, bila shaka angenaswa na Alvin. Familia ya Kimaro isingeruhusu damu yao ipotee nje, na ilikuwa vigumu zaidi kwake kuwaacha watoto baada ya kuwazaa.
“Tusilizungumzie hilo. Njoo hapa nikuambie kitu." Lisa alimpungia mkono. Pamela akaenda, na Lisa akaweka mkono mfukoni mwa Pamela.
Pamela akaingiza mkono mfukoni kwa kuchanganyikiwa. "Unanipa bahasha ya nini?"
Lisa akamvuta karibu na kusema kwa sauti ya chini, “Nywele za Maurine Langa zimo ndani ya bahasha hiyo. Nenda omba likizo na urudi Dar es Salaam na nywele hizi. Chukua nywele za Jones Masawe na Salome Masawe kutoka gerezani ili kufanya kipimo cha DNA. Kumbuka kuiweka siri. Hakuna anayetakiwa kujua kuhusu jambo hili. Unatakiwa kuwa makini.”
Kila mtu alifikiri kwamba alikuwa ameshika nywele za Maurine kwa sababu alikuwa na wivu na hasira, lakini sababu yake halisi ilikuwa kupata nywele za Maurine. Ilibidi awe na kisingizio halali. Vinginevyo, Maurine angekuwa na shaka.
Macho ya Pamela yalimtoka. “Hilo haliwezekani…”
“Inawezekana sana. Lina hajulikani alipo, na Maurine huyu ananipa hisia ninazozifahamu sana,” Lisa alisema, “Ikiwa Maurine Langa ni Lina Jones, lazima kuwe na nguvu zinazomuunga mkono. Mtu aliye nyuma yake lazima awe anamlenga Alvin. Hili si jambo ambalo tunaweza kulishughulikia kwa nguvu za kikatili.”
“Si ungemwambia Alvin?” Pamela akabanwa na mate.
“Ataniamini? Halafu Alvin si mtulivu, hata kama tanaiamin anaweza kulishughulikia kwa papara”
Pamela akanyamaza kimya. Alvin kweli angeweza asimwamini. "Kwa hali hiyo, nitarudi Dar es Salaam kesho saa sita mchana."
Muda si mrefu baada ya kuondoka, Hans aliingia na baadhi ya nyaraka huku akiwa na tabasamu usoni mwake. Baada ya yote, Lisa alikuwa na ujauzito wa watoto wa Alvin, hivyo nafasi yake ingeimarika zaidi na Mawenzi ingekuwa na maisha mazuri ya baadaye. Alijua alikuwa akimtumikia mtu sahihi.
"Bi. Jones, Meneja Mkuu alinipa hizi nyaraka na kusema kwamba itabidi uzichunguze wewe binafsi."
Lisa alichukua nyaraka hizo wakati Alvin alipoingia ghafla. Uso wake ulisinyaa alipoziona zile nyaraka. “Daktari alisema kwamba hawezi kufanya kazi sasa. Ni nani aliyekuruhusu kuleta vitu hivi ili kumsumbua wakati amebeba watoto wangu?”
Hans alikasirika kidogo na Lisa hakufurahishwa. “Unasemaje? Kwa hiyo nisisimamie kampuni kwa sababu tu nimelbeba watoto wako? Siwezi kukaa na kumtegemea mwanamume ambaye anaweza kuanzisha uhusiano usio na utata na mwanamke mwingine wakati wowote. Ninaweza hata kutupwa ghafla siku moja na kuachwa bila chochote.”
Kichwa cha Alvin kilikufa ganzi. “Sitaweza—”

“Hutaweza? Tulipooana mara ya kwanza uliniambia wazi kwamba sitapata hata senti moja tukiachana.” Lisa alicheka.
Hans alishtuka na kumtazama kwa siri Alvin. Alifikiri kwamba Alvin alikuwa mpenzi wa ajabu tu, lakini kumbe ni mjinga mtakatifu pia! Aligundua kuwa alikuwa mbaya zaidi kuliko alivyomfikiria. Alikuwa mtu tajiri zaidi nchini lakini hivyo ndivyo alivyosema kwa mke wake wa ndoa?
Alvin alihisi dharau ya Lisa kwake na sura yake ikaingia simanzi mara moja. Akatoa pochi yake kwenye mfuko wake wa nyuma na kumrushia. “Sawa, nitakupa pesa zangu zote kuanzia sasa, sawa?”
"Hapana Asante. Kuna wanaume wachache tu ambao huweka pesa zao kwenye pochi siku hizi. Wengi wao huhifadhi pesa zao kwenye miradi” Lisa hata hakumtazama.
Alvin hakuweza kushindana naye, ikabidi tu kumwambia Hans, "Nipe hati hizo, nitazishughulikia.”
Hans alijikongoja aliposikia maneno hayo. Ilimshangaza na kumchekesha. Alvin alisema hakuwa na muda wa kushughulika na masuala ya kampuni yake, hata hivyo alikuwa na muda wote wa kuingilia masuala ya kampuni nyingine. Alvin alichukua zile nyaraka na kutafuta sehemu kwenye sofa ili kuzisoma kwa makini.
Shangazi Yasmine aliingia akiwa na matunda na kushangaa. “Bwana Kimaro, umemaliza kuchukua dripu ya IV? Kwa kawaida huchukua angalau saa nne.”
Hans alisema kwa unyonge, "Bwana Kimaro alitumia sindano kubwa zaidi na kuimaliza kwa saa mbili tu ili aje kukaa na Bi. Mdogo."
Shangazi Yasmine alipigwa na butwaa.
Lisa kimya kimya alitazama kasi ya dripu yake ya IV. Sindano yake ilikuwa ndogo tu, lakini maumivu yake yalikuwa hayawezi kuvumilika. Ikiwa angetumia sindano kubwa zaidi, maumivu yake yangekuweje? Hakupata picha!
Kutokana na hali ya kutisha ya Alvin, kila mtu alitoka wodini kimyakimya kumkwepa.
Dakika kumi baadaye, Lisa aliusogeza mwili wake na kujiandaa kutoka kitandani. Mara Alvin akanyanyuka. “Usinyanyuke. Daktari alisema unapaswa kukaa kitandani."
"Naenda kujisaidia." Lisa alifoka. "Daktari hakunizuia kwenda chooni."
“Usijali. Nitakubeba kama unataka kwenda.” Alvin hakuzungumza zaidi na kumnyanyua. Alimuweka chini kwenye choo na kumvua gauni lake kwa nguvu.
Uso mzima wa Lisa ulikakamaa kwa hasira. “Ondoka, nataka nibaki peke yangu.”
“Daktari alisema tunapaswa kukuhudumia kwa uangalifu…”
“Samahani, lakini siwezi kujisaidia ukiwa karibu.”
“Kuwa mpole. Wataalamu wanasema kwamba mwanamke anapokuwa mjamzito, baba mtarajiwa anapaswa kumtunza mke wake na kumfariji. Nikikuacha peke yako, hakika utakuwa na mawazo yasiyofaa.” Alvin alimbembeleza kwa upole na subira.
"Inatosha. Sitafanya kitu kama hicho.”
"Wataalamu wanasema kwamba wanawake hawamaanishi wanachosema."
Lisa alikuwa karibu kufa kutokana na maneno yake ya ajabu. Ni aina gani ya wataalamu wa kijinga walikuwa wakimshauri? "Simama nje au sitaweza kujisaidia." Alvin alitoka nje na kusubiri mlangoni.
Lisa alipoinuka, aligundua kuwa pedi ilikuwa imechafuka sana na alihitaji kubadilisha, lakini pedi mpya zote zilikuwa nje. Aliuma mdomo na kumwambia Alvin aliyekuwa nje kwa sauti ya chini, “Alvin, nisaidie pedi. Au unaweza kumwambia Aunty Yasmine aniletee.”
"Hakuna haja."Alvin akafungua droo na kuchukua pedi. Alifungua moja na kuisoma kwa muda. Haraka akagundua njia sahihi ya kuitumia.
Baada ya kufungua mlango, Lisa alitoa mkono wake nje.
"Simama. Nitakuwekea,” Alvin alisema, “Hutakiwi kuinama. Watoto walioko tumboni wataumia."
“Jamani, ina maana nisiiname kisa ujauzito?” Lisa alihisi mateso sasa.

Sura ya: 260

“Kuwa mpole. Huu ni wakati muhimu katika maisha yetu. Ni kwa ajili ya watoto wetu waliomo tumboni.” Alvin alimnyanyua na kumsaidia kuweka pedi.
Wakati wa mchakato mzima, Lisa alitaka kuvunja kichwa chake na kujiua kwa aibu. Aliporudi kitandani, uso wake wote ulikuwa umetapakaa aibu.
Alichukukua kisu na kutaka kula tunda moja, lakini Alvin aliinuka tena palepale aliposhika kisu ili kukata tunda. "Kaa chini, nitakumenyea.”
Kwa kifupi, Alvin alikaa wodini mchana na usiku, siku nzima. Lisa hakuruhusiwa kugusa chochote. Alichowezaa kufanya ni kukaa na kulala tu. Vingine vyote alifanyiwa na Alvin
Kwa sababu ya kulala sana, Lisa aliamka saa kumi na mbili asubuhi siku iliyofuata. Alipofumbua macho alimkuta Alvin amelala kwenye mto wake. Hakujua ni saa ngapi alibanana naye jana usiku. Hasira yake iliwaka alipokumbuka taswira ya jinsi Maurine alivyomshika mkono jana yake. Hata hivyo, sura safi ya Alvin alipokuwa amelala ilipendeza zaidi machoni kuliko alipokuwa macho.
Kope zake zilikuwa nene kama mbawa za kipepeo, ngozi yake haikuwa na vinyweleo, na macho yake, pua na midomo vyote vilipendeza sana. Vipengele vyake vilionekana kama kazi ya sanaa iliyoundwa kwa uangalifu na Mungu…
Alipokuwa akitafakari, macho meusi ya Alvin yakafunguka ghafla. Lisa aliogopa na kumpiga teke bila fahamu. "Ni nani aliyekuruhusu kupanda hapa jana usiku?"
Alvin alikaa kwa uchungu na kutazama huku na kule. Kulikuwa na mwanga wa kuchanganyikiwa katika macho yake. “Hii si hospitali? Mbona unavaa scrubs?"
Moyo wa Lisa ulizama mara moja. Ndani ya siku mbili walizokaa pamoja, alihisi kumbukumbu ya Alvin inazidi kuwa mbaya. Hata hivyo, hakutarajia kwamba angesahau kwamba alikuwa mjamzito baada ya kuamka. Hata kumbukumbu ya mzee wa miaka 80 isingekuwa mbaya kiasi hicho.
"Ni sawa ikiwa hukumbuki." Alishuka kutoka kwenye kitanda cha hospitali ili kuosha uso wake na kupiga mswaki.
'Niambie. Ni nini kilikupata? Una tatizo lolote?" Alvin alimkimbilia na kumshika mkono.
Shangazi Yasmine aliyekuwa amelala chumba jirani alisikia makelele hayo hiyo na mara moja akaamka kwenda kuwaangalia.
“Bibi mdogo, unataka kula nini kwa kifungua kinywa?”
"Sijisikii chochote."
“Haiwezekani. Unabeba watoto wawili wadogo tumboni mwako sasa hivi. Huwezi kuwa mzembe.” Shangazi Yasmine alitafakari huku akitabasamu. “Nitakupikia uji wa mtama—”
“Ulisema nini? Ana mimba?” Alvin alifoka kwa furaha.
Aunty Yasmine akanyamaza na kumwangalia Alvin kiajabu. “Bwana Kimaro, umesahau? Ulifurahi sana jana na hata siku nzima ulisoma vitabu vya kulea ujauzito."
Alvin aliganda kabisa. Kwanini hakuweza kukumbuka hata kidogo? Alitaka kufikiria zaidi, lakini ubongo wake ulianza kumuuma. Alifunika kichwa chake kwa mikono miwili. Alikuwa na maumivu makali sana hata akashindwa kusimama.
Lisa alimtazama Aunty Yasmine. "Mwambie daktari anayemhudumia aje."
Punde, Daktari Melisa na Dokta Chester walikusanyika kufanya uchunguzi wa kina juu ya Alvin. Dakika kumi baadaye, Daktari Melisa alisema kwa maneno mazito, “Hii ni dalili ya kupoteza kumbukumbu. Sikutarajia hali yake kuwa mbaya haraka hivyo, Bwana Kimaro.”
Alvin hakuweza kukubali. "Lakini nimekuwa nikinywa dawa na kwenda kwa dripu ya IV kila siku. Kwanini haifanyi kazi hata kidogo? Je, unafanya kazi yako ipasavyo? Haufai.”
Daktari Melisa alishtuka kwa aibu kutokana na karipio hilo. "Sielewi kwa nini hii inatokea pia. Nilijaribu niwezavyo…”
“Sawa, Alvin, tulia. Daktari Melisa ndiye mtaalam bora katika uwanja huu nchini,” Chester alizungumza.
“Ninapaswa kutulia vipi? Sikuweza hata kukumbuka kuwa mke wangu ni mjamzito. Je, inawezekana kesho sitamtambua mke wangu?” Uso wa Alvin ulionyesha kukereka. Midomo ya daktari Melisa ikasogea lakini hakusema chochote kwa muda mrefu.
Hata hivyo, Alvin angeweza kukisia kwamba alikuwa sahihi. Alikaa kwa hasira na kuvivunja vitu vilivyokuwa kwenye meza ya kitanda.
"Alvin, tulia." Chester na Daktari Melisa walikuja mbele kujaribu kumzuia, lakini Alvin akawasukuma mbali.
Lisa aliuma mdomo na kwenda mbele. "Alvin Kimaro, unajaribu kuwatisha watoto wako tumboni mwangu?"

Alvin aliganda na kulitazama tumbo lake huku akikunja ngumi kwa maumivu. "Mimi ni mgonjwa. Labda hata nisingewatambua kama wangesimama mbele yangu katika siku zijazo.”
“Hilo halitatokea. Tayari nimepata habari kuhusu Nyasia, mtaalamu wa saikolojia. Maadamu tutampata, tuna njia ya kukuponya.” Chester akampiga bega. "Nijuavyo, hakuna ugonjwa ambao Nyasia hawezi kutibu."
Macho ya Alvin yalififia. Hilo lingeweza kuwa tumaini lake pekee. “Lisa, usijali kuhusu mimi. Nenda kitandani ukapumzike.”
Lisa aliitikia kwa kichwa na kurudi wodini kwake. Chester alimfuata muda si mrefu. “Lisa, najua kwa sasa haujaridhika na Alvin, lakini pia unaifahamu hali yake ya sasa. Natumai utaacha kugombana na Alvin kwa muda huu. Ni kwa ajili yake na kwa ajili ya watoto.”
"Utasema kwamba ninaweza kuathiri hisia zake na kwamba hali yake inayozidi kuzorota inahusiana nami, sivyo?" Lisa bila fahamu alihisi kuchanganyikiwa na jinsi mtu huyu alivyokuwa akiuweka ugonjwa wa Alvin juu yake. Ni kana kwamba alikuwa akimwomba avumilie ingawa alionewa.
Chester aliifuta miwani yake kwa hasira. "Ugonjwa wa Alvin kwa kweli ulidhoofika sana wakati wa kukupa talaka."
"Lakini kwanini ninahisi kwamba afya yake ilianza kuzorota baada ya Maurine Langa kutokea?" Lisa alisema kwa unyonge.
Chester alikunja uso. "Sio lazima umtupie hili Maurine kwa wakati huu."
“Kwa kweli sielewi kwanini nyie wote mnamtetea. Ni kwa sababu tu yeye ni binamu ya Sarah Langa? Uliweza hata kuachana na Charity Njau kwa sababu ya Sarah?”
Uso mpole wa Chester ulipoa ghafla. “Charity alikuambia nini? Kuachana naye hakuhusiani na mtu yeyote. Nilimchukia tu…”
Lisa alitazama mlango nyuma yake na kujisikia vibaya. “Charity…”
Chester aligeuka na kumuona Charity akiwa amevalia suti nyeusi ya kikazi. Suti iliukumbatia vyema mwili wake na kukifafanua kiuno chake chembamba. Alikuwa amebeba matunda na juisi mikononi mwake. Nywele zake nyeusi zilikuwa zimefungwa, na uso wake ulikuwa umepoa.
Macho yao yalipogongana, Charity akadhihaki. "Ni bahati mbaya. Mimi pia nilichukizwa na wewe. Kwa bahati nzuri, tuliachana mapema. Vinginevyo, ningekuwa na wasiwasi kuhusu kupata STD.”
Uso wa Chester ukafifia ghafla, akageuka nyuma na kumuonya Lisa, “Kumbuka nilichokuambia. Usimchokoze Alvin. Vinginevyo, ninaweza kumfanya Daktari Angelo amwache baba yako.”
Macho ya Lisa yalimtoka, akainamisha kichwa chini huku akikunja blanketi kwa nguvu. Chester akageuka na kuelekea mlangoni, akampiga kwa nguvu Charity begani.
Charity alijikwaa na kumlaani, "Chester Choka, huna aibu kiasi gani kumtishia mwanamke?!"
"Fuatilia mambo yako mwenyewe, au usinilaumu kwa kukutupa tena kwenye maji." Chester aliondoka na uso ulionyooka.
Charity akauma meno na kusema. "Achana nao. Ni kundi la wahuni wasio na akili!"
Lisa alikuwa tayari amekasirika na ghafla alicheka aliposikia laana ya Charity. "Hawana akili. Wanacheza tu kwenye kiganja cha Maurine Langa.”

TUKUTANE KURASA 261-265

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI...........LISA
KURASA.......261-265

Sura ya: 261

Lisa alikaa hospitalini kwa siku sita. Siku moja kabla ya kuwa tayari kuruhusiwa, Bibi Kimaro alimpigia simu Alvin.
“Utakuwepo nyumbani kwako leo? Zabibu zimeiva, kwa hivyo nitakuletea na kuja kukusalimia pia. Hutaki hata kuja kumuona bibi mzee kama mimi mpaka nianze kuja kwako kwanza?”
“Zabibu ni nzuri. Ikiwa mwanamke mjamzito atakula zabibu nyingi zaidi, labda watoto watazaliwa na macho yenye nguvu zaidi,” Alvin alisema baada ya kufikiria.
“Nini… ulisema nini?” Bibi Kimaro alishikwa na kigugumizi.
'Ni nini hasa ambacho hujaelewa? Nitakuwa baba.” Alvin alitabasamu. Sauti yake ilifurahisha alipotamka kwa mbwembwe, "Baba wa mapacha."
"Alvin, kwanini hukutuambia habari muhimu kama hii?" Sauti ya Bibi Kimaro ilikaribia kumtia uziwi. “Mapacha! Mungu wangu! Familia ya Kimaro haijawahi kupata mapacha.”
Mzee Kimaro, ambaye alikuwa akisoma gazeti na miwani yake ya macho, pia aliketi na kutega masikio yake.
“Kwanini nikuambie? Najua humpendi Lisa.” Alvin akasimama kwa mbwembwe. “Ningekuambia huenda ungemtesa tena.”
Bibi kizee yule alihisi moyo ukimuuma kwa kuambiwa vile. “Mimi… Hiyo ilikuwa zamani. Ikiwa ana mimba ya mapacha, bila shaka, nitamhudumia ipasavyo. Mko nyumbani sasa, sivyo? Nitakuja mara moja…”
“Hayupo.” Alvin alishtuka ghafla. “Yupo hospitalini. Alianguka na karibu vitoto vitoke."
"Nini? Hiyo ilitokeaje? Wajukuu zangu wa thamani wako sawa? Angewezaje kuwa mzembe hivi wakati tayari ni mama…”
“Hapana, si kosa lake. Ilisababishwa na uzembe wangu,” Alvin alijibu bila kufafanua.
“Usie na maana wewe… Huna hata haya.” Bibi Kimaro akakata simu. Chini ya dakika 40 baadaye, yeye na Mzee Kimaro walionekana hospitalini kwa wakati mmoja.
Kuonekana kwa wazee hao wawili kulimtia hofu Lisa. Baada ya yote, alikutana na Bibi Kimaro mara tatu tu na Mzee Kimaro mara mbili. Kila wakati, hawakuwa wameonekana kuwa na furaha kumuona. Sasa, mara tu walipoingia ndani, nyuso zao zilijaa tabasamu za kupendeza. Ilimfanya ajisikie wa ajabu sana.
“Babu, Bibi…” Lisa alinyanyuka, lakini Mzee Kimaro mara moja akasema kwa sauti ya kusikitisha, “Usinyanyuke. Watoto walio tumboni mwako ni muhimu zaidi.” Lisa alishangaa. Kweli, tayari alikuwa ametarajia hii.
"Babu, Lisa ni muhimu vile vile," Alvin alimkatiza, akiwa na kinyongo.
Bibi Kimaro mara moja alimkazia macho. "Ikiwa unajua yeye ni muhimu, kwanini ulisababisha vitoto vyake vikajeruhiwa?"
Alvin alikunja uso lakini alikuwa mtiifu na hakukanusha. Wazee wale wawili walipoona hivyo, Mzee Kimaro aligonga miwani yake na kusema. “Mjinga sana wewe. Kwanini huna akili ya kujizuia. Unawezaje kuwa na tamaa wakati mkeo tayari ni mjamzito?"
Alvin na Lisa waliganda kwa wakati mmoja. Sentensi hiyo iliwatia aibu kwa kiasi fulani. Kisha, Bibi Kimaro alisema kwa dhati, “Ninaelewa kwamba nyinyi ni wachumba wapya na hamwezi kujizuia, lakini bado mnapaswa kuzingatia watoto walio tumboni. Hamuwezi kulala pamoja kwa muda huu, au mwishowe mtawadhuru watoto.”
Uso wa Lisa uliganda na kusinyaa kwa aibu. Je, walifikiri kwamba vitoto vyake viliathirika kwa sababu alikuwa amelala na Alvin? Mungu wangu!
Uso wa Alvin nao ukawa mtupu. Hakuweza kuelewa jinsi gani wazee hao wawili walifikia hitimisho hilo hata kidogo.
“Hapana, Bibi. Sisi—”
“Inatosha, msitake kusema zaidi.” Bibi Kimaro aliwakatisha, “Ukiruhusiwa kesho, uje nyumbani uishi kwenye makazi ya familia ya Kimaro. Nitaajiri mpishi bora wa kuhudumia lishe yako urudi kwenye afya. Pia, hali ya hewa kwenye makazi yetu ni nzuri na inafaa kwa wewe kulea watoto wako. Nitabaki na uhakika ikiwa nitawaona mkilala katika vyumba tofauti."
“Siendi.” Alvin alikataa kabisa. Alikataa kulala katika vyumba tofauti. Hakuweza kuvumilia hata ikiwa ni kwa siku moja tu.
Hapo awali Lisa alitaka kupinga, lakini moyo wake uliguswa kidogo na maneno ya Bibi Kimaro. Alikubali kwa kichwa. "Niko tayari kuhamia katika nyumba yako. Bibi, wewe ni mtu mwenye uzoefu na umezaa watoto kadhaa, kwa hiyo nadhani uko sahihi.”
"Hiyo ni sawa." Bibi Kimaro alimpa sura ya kuidhinisha. Kwa mara ya kwanza, aliridhika kidogo na Lisa.

Macho mazito ya Alvin yakatua kwenye uso wake mdogo. Alijua anachofikiria. Alitaka kumkwepa na hakutaka kulala naye. “Sikubaliani."
“Ni bure kwako kukataa,” Mzee Kimaro aliamuru, "Kwa vyovyote vile, mapacha wa kwanza wa familia ya Kimaro lazima wazaliwe wakiwa na afya njema."
Alvin akajilaumu mwenyewe. Hakupaswa kuwaambia wawili hao kuhusu ujauzito. Kiherehere chake kilimponza.
Wazee hao wawili walipoondoka, alimwangalia Lisa bila furaha. "Ulifanya hivyo kwa makusudi."
“Ndiyo.” Lisa alitazama juu na kusema, "Alvin Kimaro, kumbukumbu yako sio nzuri, lakini sitasahau jinsi mimba yangu ilivyotaka kutoka. Labda ni salama zaidi kwangu kuishi na hawa wazee kwa sasa. Angalau sitalazimika kuvumilia vitisho vya rafiki zako, ugonjwa wako usije ukadhoofika na kuwa kosa langu.”
Mwale wa mwanga baridi uliangaza machoni mwa Alvin. Mara moja alielewa kwamba lazima Chester na Rodney walimwambia kitu. Alvin alikuwa amezungumza nao hapo awali, lakini walikuwa marafiki kwa zaidi ya muongo mmoja, wasingeweza kugombana kirahisi.
“Samahani…”
“Hakuna haja ya samahani. Sidhani tu kwamba nina thamani kuzidi Sarah. Ikiwa moyo wako ungejazwa na mimi, ningebeba jukumu lote.Lakini unanificha mambo yako mengi, na uhusiano wako na Maurine Langa haueleweki. Kwanini niwajibike kwa hali ya ugonjwa wako? Nalazimika kuvumilia hata kama sina furaha.”
Lisa alijiachia na kujilaza kitandani, hakutaka tena kumtilia maanani. Alikuwa amekasirika sana Chester alipomtumia Joel kumtishia.
Asubuhi iliyofuata. Bibi Kimaro alimtuma dereva kwenda kumchukua Lisa. Mlinzi wa nyumba alimpangia kukaa kwenye chumba cha zamani cha Alvin.
Alikuwa ameingia kwenye chumba hiki hapo awali, lakini kilikuwa kimeachwa wakati huo. Hata hivyo, sakafu ilikuwa imefunikwa na kapeti ya manyoya kwa muda huo, na pia kulikuwa na TV na viti viwili vya mapumziko. Chumba hicho pia kilipambwa kwa maua yenye harufu nzuri.
"Kwanini hii inaonekana tofauti na nilipokuwa nalala mimi?" Alvin alionyesha mashaka yake.
"Bibi Kimaro alisema kuwa chumba cha hapo awali kilikuwa baridi sana na hakifai kwa wanawake wajawazito, kwa hivyo mbunifu aliongeza vitu vichache mara moja." Mlinzi wa nyumba alisema, "Bwana Kimaro, chumba chako kiko kwenye jengo linalofuata."
Alvin aliuma meno na kusema. “Kwanini mniweke kwenye nyumba tofauti? Nataka chumba cha jirani.”
"Hapana, Bibi Kimaro alisema kwamba anaogopa utaingia katikati ya usiku."
Alvin alikasirika kiasi cha kutaka kutapika damu. “Inatosha. Nitalala chumba cha jirani. Huo ndio uamuzi wangu wa mwisho. Vinginevyo, nitaondoka naye moja kwa moja.”
"Sawa Bwana Mkubwa." Mhudumu wa nyumba alinyamaza kwa muda kabla ya kukubaliana kinyonge.
Mchana, Lisa alilala hadi saa kumi jioni Aunty Yasmine akampelekea glasi ya mtindi. Baada ya kumaliza kunywa, alienda kwenye matembezi uani.
Ilibidi akubali kwamba makazi ya familia ya Kimaro yalikuwa yakifahari sana. Yalichukua eneo kubwa, na hewa ya pale ilikuwa safi sana. Hakuwa ametembea kwa muda mrefu alipowaona Valerie na Queenie wakiingia kwenye makazi yale ya kifahari.
"Lisa Jones, unawezaje kuthubutu kuonyesha uso wako hapa?" Valerie alilipuka ghafla baada ya kumuona.

Sura ya: 262

Valerie alimchukia Lisa. Aliamini yote ni sababu yake kwamba Alvin alimuondoa kwenye wadhifa wa mkurugenzi wa kitengo cha Bima cha kampuni ya KIM International baada ya kushika wadhifa wa kuongoza kampuni tena, na kumfanya adharaulike na kuwa mtu asiye na maana. Moyo ulimuuma kwa chuki kila alipokuwa akimfikiria Lisa Jones.
“Aunty, kwanini nisiwe hapa? Mimi ni mke wa Alvin.” Lisa aliinua uso na kutabasamu.
“Koma, usiniite ‘Aunty’! Hufai. Unanitia kichefuchefu tu.” Valerie alifadhaika.
“Ndio hivyo, wewe ni binti wa haramu. Hatukutambui hata kidogo.” Queen naye alimdharau.
“Usiniudhi,” Lisa alisema kwa sauti ya chini, bila ya kutishika hata kidogo.
Valerie alicheka kwa hilo. “Kwa hiyo nikikuudhi itakuwaje? Vipi ikiwa nitakupiga kabisa?" Aliinua mkono wake wakati akisema, lakini Queen haraka akamshika. “Mama, Bibi…”
Valerie alisimama na kugeuka kutazama, na kumwona Bibi Kimaro akitembea kuelekea kwao. Alikuwa mbali sana, kwa hiyo Valerie hakujali hata kidogo. "Kwa hivyo ikiwa bibi yako anakuja? Hata yeye pia hampendi b*tch huyu asiye na haya.” Alitupa mkono wake chini alipomaliza kuzungumza, lakini Lisa aliushika. Valerie alimtikisa kwa nguvu, na Lisa akarudi nyuma hatua chache.
Bibi Kimaro, ambaye hakuwa mbali sasa, alipatwa na hofu. "Mtoto wangu mpendwa, uko sawa?" Bibi Kimaro alikuwa na wasiwasi na haraka akakimbia.
Valerie alitabasamu. “Mama, sijambo…”
Kabla hajamaliza, Bibi Kimaro alimshika mkono Lisa kwa wasiwasi huku akiwa anahofia kwamba Lisa angedhurika kwa kuguswa na Varelia.
“Bibi, wewe...” Queenie alifungua mdomo kwa kutoamini kile kilichokuwa kikitokea mbele ya macho yake. Bibi Kimaro kweli alimuita Lisa 'mtoto wake kipenzi'. Ni kweli au alikuwa anaota?
“Bibi, sijambo.” Uso wa Lisa ulionekana kukunjamana vibaya huku akigusa tumbo lake. "Lakini nina wasiwasi kwamba sitaweza kujifungua salama ikiwa nitaendelea kuishi hapa."
“Una mimba?” Valerie alipigwa na butwaa.
"Nyamaza!" Bibi Kimaro alimkazia macho kwa hasira. “Unaltaka kuleta shida tena hata nyumbani8? Nimezaaje binti asiyefaa kama wewe? Jambo lolote likitokea kwa vitukuu wangu wa thamani, sitakusamehe kamwe.”
Valerie alikanyaga miguu yake kwa hasira. "Mama, mimba yake inaweza kuwa feki. Nani amedhibitisha kuwa ni kweli ana mimba? Pia alikuwa na mpenzi hapo awali. Huenda mtoto hata asiwe wa Alvin.”
Lisa ghafla alimtazama kwa macho ya hasira. “Aunty, samahani, si wewe unayelala na mimi. Alvin si mjinga kiasi cha kutojua kama ujauzito ni wake ama si wake. Lakini sikuelewi kabisa. Mimi ni mgeni tu niliyekuja Nairobi na hakuna baya nililokufanyia, lakini wewe una chuki ngumu dhidi yangu sijui kwanini. Mara ya kwanza, kwa makusudi ulitafuta mtu wa kunipeleka kwenye chemchemi ya maji moto ambayo Willie Kimaro alikuwa akizama ndani yake kwa lengo la kunitengenezea kashfa ili sifa yangu iharibike. Mara ya pili, hata umeniharibu sura yangu. Tayari nimekusamehe, lakini wewe bado unanichukia tu. Nimewahi kukufanyia nini?”
Bibi Kimaro alishtuka. Haishangazi Lisa alipotea mara ya kwanza alipoenda kwenye makazi hayo. Wakati huo, hata alikuwa amemlaumu Lisa kwa kukimbia, lakini hakujua kwamba yote yalikuwa njama ya Valerie.
"Valerie, umekuwa mbaya sana na hutaki kukubali makosa yako." Bibi Kimaro alikatishwa sana tamaa na yeye.
“Mama usisahau kuwa ni kosa lake Alvin kuniondoa kwenye nafasi yangu ya ukurugenzi na kunifanya nidharaulike. Hapo awali, nilikuwa nikiheshimiwa, lakini sasa, kila mtu ananiona lofa, hata Nina hanijali tena,” Valerie alilalamika.
"Alvin alikufukuza katika nafasi yako kwa sababu huna sifa." Bibi Kimaro alikatishwa tamaa kabisa na watoto wake baada ya Alvin kumfunulia ukweli mara ya mwisho. "Hata unamruhusu Nina Mahewa kukusaidia kughushi kazi zako. Ikiwa angekuacha uendelee kufanya kazi, ungeharibu tu kampuni.”
"Mama, unamtetea tu kwa sababu ni mjamzito." Macho ya Valerie yalikuwa mekundu kwa hasira.

Bibi Kimaro akatikisa kichwa. “Inatosha, huna hata aibu. Unachojua ni kukosea tu lakini si kujutia makosa yako. Sio tu kwamba haukubali makosa yako, lakini bado una nia ya kumdhuru Lisa. Ninaweza kusema kuwa moyo wako ni mbaya. Kosa langu ni kukudekeza tangu utoto. Sasa kwa kuwa Lisa atakuwa analea ujauzito wake hapa, huruhusiwi kuja hapa bila idhini yangu kuanzia leo.”
Valerie alipigwa na butwaa. "Mama, hapa ni nyumbani kwetu..."
Queenie pia aliingiwa na wasiwasi. “Bibi, msamehe mama. Hakukusudia—”
“Babu yako na mimi tumezeeka. Tunataka tu kuishi maisha ya amani, si vurugu kila siku. Hatuwezi kuvumilia tena tabia zenu mbaya. Queenie, kama na wewe una tabia za mama yako, basi si utaondoka naye.”
Bibi Kimaro alikuwa amechoka sana. Alipunga mkono na kuwaambia walinzi kuwatoa nje.
“Bibi, samahani...” Lisa alionekana kuomba msamaha.
“Usiombe msamaha. Niliona wazi kuwa yeye ndiye alikuwa anakuchokoza. Ni kweli kwamba sikupendi kiasi hicho, lakini bado ninaweza kutofautisha kati ya mema na mabaya.” Bibi Kimaro alinyooka sana.
Lisa hakuhisi kukasirika. Kinyume chake, tabia ya bibi huyo ilimfanya ahisi raha zaidi.
“Ikiwa mtu yeyote atakunyanyasa, niambie tu. Wewe pia ni mke wa Alvin. Katika siku zijazo, utakuwa msimamizi wa familia hii kwa hiyo unastahili kuishi kama kwako.”
Lisa aliganda. Kwa hiyo Bibi Kimaro alikuwa amekubali? Hata hivyo, bado haikujulikana ikiwa Alvin na yeye wangeweza kutembea hadi mwisho kutokana na jinsi walivyokuwa wakati huo.
Bibi Kimaro alipomuona amenyamaza, alimtazama usoni na kupata utulivu moyoni. Kisha akageuka na kuondoka na mfanyakazi wa nyumbani.
•••
Jioni, Lisa alimpigia simu Pamela. "Iliendaje?"
"Usijali, Dar es Salaam ni jiji la familia ya Masanja. Ni mchezo wa kitoto kupata nywele za Jones kutoka jela,” Pamela alisema, “Tayari nimewaambia watu wangu wafanye haraka. Tutapata matokeo baada ya siku mbili.”
“Basi nitakuachia jambo hili.”
“Haya, sisi kimsingi ni ndugu, usiwe na wasiwasi . Afadhali uwatunze mapacha wangu. Nataka kuwa godmother wao.”
"Ndio, hakika utakuwa godmother wao. Hutaweza kuepuka hili.” Lisa alikata simu na kuiweka pembeni wakati mlango wa chumba ulipofunguliwa ghafla. Alvin akiwa amevalia vazi la bluu bahari aliingia huku akiwa ameshikilia vitabu vichache. "Nani anataka kuwa godmother wa mapacha wangu? Pamela au Charity?"
Sauti ya ghafla na mwonekano wa Alvin uliufanya mwili wa Lisa kuruka kwa hofu. “Alvin, umeingiaje humu? Si bibi alikuambia ulale jirani? Kwanini unakuja kwenye chumba changu?"
"Nimezoea kulala na wewe." Alvin kama kawaida alinyanyua blanketi na kuketi kitandani.
Lisa alichukia sana. Hata hivyo, ilionekana kwamba popote alipokaa, hakuna kitu kingeweza kumzuia asije kumtafuta. “Ondoka mara moja, au nitamwambia Bibi…”

Sura ya: 263

“Jaribu. Bibi ameshazima simu yake saa hii ili alale." Alvin kwa nguvu alimnyanyua, na mkono wake wa kushoto ukapapasa tumbo lake. "Acha nione ikiwa watoto wetu wawili wamekua kidogo leo."
"Wana mwezi mmoja tu sasa. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote." Lisa aliusukumia mkono wake mbali bila kujali. “Ondoka. Nataka kulala."
“Hujajibu swali langu.” Alvin alimkazia macho. "Nani anataka kuwa godmother wa watoto wangu? Ikiwa ni Pamela Masanja, sikubaliani kwa sababu IQ yake inatia wasiwasi. Ikiwa ni Charity Njau, sikubaliani zaidi…”
“Alvin, daktari alisema natakiwa kupumzika kwa muda mrefu, mbona unakuja katikati ya usiku ili kunisumbua, huwapendi watoto wako?” Lisa alikasirika na kumpiga na mto. “Watoto ni wangu. Ni uamuzi wangu juu ya nani atakuwa godmother wao. Usipoacha kunisumbua, sitawazaa.”
"Umesema nini?" Uso wa Alvin ukakunjamana ghafla. "Lisa Jones, fikiria kabla ya kuzungumza. Usifikiri kwamba watoto hawataelewa unachosema kwa sababu tu wamo tumboni sasa. Umefikiria juu ya hisia zao?"
Lisa alikuwa mjamzito, kwa hiyo hisia zake zilifadhaika kwa urahisi. Kwa maudhi machache tu, macho yake yakawa mekundu kwa manung'uniko. “Wewe ndio umenitia hasira. Nakwambia ukitaka turudiane lazima ukubali marafiki zangu pia.”
Alvin aliingiwa na hofu alipoanza kulia. “Sawa, usilie basi.”
Lisa hakulia tu, bali machozi pia yalimtoka kwa wingi na kupiga kelele zaidi. “Zaidi ya hayo, unathubutuje kuwadharau marafiki zangu?! Je, Rodney Shangwe ni bora kiasi hicho? Nadhani yeye ni mjinga kuliko nguruwe. Kuhusu Chester Choka, yeye ni mchafu kuliko mbwa. Wote ni bure.”
Alvin ghafla alipigwa na butwaa kwa lawama zake. Kimantiki, alipaswa kukasirika kwasababu alikuwa akiwadhihaki marafiki zake. Hata hivyo, alipoona machozi yake, moyo wake ulimuuma kana kwamba unayeyuka kutokana na maumivu. “Usilie. Kulia si vizuri kwa watoto walio tumboni.”
“Wacha nilie tu kwa sababu unanikera sana. Nataka nipumzike lakini unanisumbua tu.” Lisa alishindwa kabisa kujizuia. Maumivu aliyokuwa akiyavumilia moyoni yalimtoka ghafla.
Hata Shangazi Zara, ambaye alikuwa akimilinda Alvin katika mlango wa chumba kidogo cha jirani, alishtushwa na kelele hizo na akaingia ndani mara moja.
"Bwana Kimaro, umeingiaje?" Zara mara moja alimkaripia Alvin. “Bibi Kimaro aliniambia nikuchunge mlangoni kwako. Mke wako sasa anapitia kipindi muhimu, kwa hiyo hamwezi kulala pamoja. Kwanini umeingilia dirishani na kuja kumsumbua? Fanya haraka utoke nje.”
Ilikuwa sawa kama angekuwa mtumishi wa kawaida tu, lakini Shangazi Zara alikuwa na bibi huyo mzee kwa makumi ya miaka. Ingawa Alvin hakuthubutu kumbishia chochote, lakini bado alijisikia huzuni sana.
"Nilikuja tu kuwasimulia watoto hadithi." Alvin alijitetea kijinga.
Lisa aliyapapasa macho yake na kubanwa na hasira. “Ulikuja…? Usitake kunikasirisha zaidi. Ondoka!”
"Bwana Kimaro, tafadhali ondoka haraka." Shangazi Zara akamtoa nje kwa haraka.
Mpaka kila mtu alipoondoka ndipo Lisa aliachia machozi yake taratibu, lakini moyo wake ulikuwa bado umekasirika. Alipoamka siku iliyofuata, alikuwa na uvimbe mwepesi chini ya macho yake.
Wakati wa kifungua kinywa, wazee wale wawili waligundua kuhusu tukio la jana yake usiku na Mzee Kimaro alishindwa kujizuia papo hapo. “Unawapenda kweli watoto wako? Una umri gani sasa? Huna akili hata kidogo!”
Bibi Kimaro naye alikasirika. "Kibaraza kitafungwa kuanzia leo. Usimruhusu apate nafasi ya kuingia chumbani kwa mjamzito tena mpuuzi huyu asiye na nidhamu!”
Alvin, ambaye uso wake uliangukia kwenye karipio lao, aliupapasa kwa mguu wake mguu wa Lisa kwa upole. “Mpenzi…”
Lisa alitazama pembeni na kumpuuza kabisa.

•••
Siku mbili baadaye huko Dar es Salaam, Pamela alipokea simu kutoka hospitali alikopeleka nywele za Maurine na Jones kwa uchunguzi, na mara moja akakimbia kuelekea huko. Pamela akaipata ripoti hiyo haraka na kuona maneno makubwa 'positive match' juu yake. Mara moja alimlaani Lina Jones na mababu zake wote.
Alipiga namba ya Lisa, akisema, "Ulikuwa sahihi! Maurine Langa kweli ni binti wa damu wa Jones. Yeye ni Lina Jones."
Lisa alipapasa paji la uso wake. Kwa kweli hakutaka matokeo yawe ya kweli. Hata hivyo, katika hali ya ugonjwa wa Alvin ulivyozidi kuwa mbaya na dawa na maziwa ambayo Maurine alikuwa akimpa Alvin kila siku… Je, hiyo ilikuwa dawa ya kawaida? Ghafla alishtuka.
“Nitachukua picha na kukutumia. Fanya haraka ukamwambie Alvin.” Pamela alimwambia na kukata simu.
“Pamela Masanja, ni wewe!” Mara Pamela akashtuliwa ghafla baada ya kukata simu, uso wa Linda Sheba uliyajaza macho yake. Alionekana mwenye furaha sana kumuona Pamela.
Linda alienda pale hospitali kumpeleka Patrick Jackson, ambaye tangu apigwe kibuti na Pamela huko Nairobi aligeuka kuwa mlevi wa kupindukia hivyo alikuwa akisumbuliwa na afya mbovu.
Hata hivyo, Pamela alitaka kutapika damu mara tu alipomuona Patrick. Alirudi tu Dar es Salaam kwa siku chache lakini akaishia kukutana na mtu aliyemchukia zaidi.
Linda alikunja uso ghafla na kuuliza. "Pamela, kwanini umerudi Dar es Salaam? Nilisikia kwamba umepata mpenzi mpya huko Nairobi. Ungewezaje kumfanyia hivi Patrick?”
“Hilo halikuhusu. Hebu nipishe niondoke zangu.” Sauti ya Pamela ilikuwa imejaa papara.
Macho ya Linda yalikuwa mekundu kwa kuzidiwa huzuni. “Samahani! Naomba msamaha kwa niaba yake, anateseka sana Patrick, hana hata hamu ya kula siku hizi, kutwa anakunywa pombe tu ili kujisahaulisha mawazo yako. Hata ufanisi wake wa kazi umepungua sana. Nashukuru sana kukuona hapa vinginevyo nilipanga kukufuata Nairobi ili kumuombea msamaha!”
Patrick alionekana mnyonge sana. Umbo lake refu sasa lilikuwa limeinama kidogo, na uso wake wa kupendeza sasa ulionekana kupauka kama kipande cha muhogo. Macho yake yalikuwa yamepoa kama mtu aliyekosa matumaini ya kuishi. Alionekana kujichokea kabisa.
Pamela aliweza kuhisi mara moja kuwa Patrick hakuwa vizuri. Moyo wake ulijikaza, lakini alishusha haraka wasiwasi moyoni mwake. Tayari walikuwa wameachana. Haikuwa ikimhusu tena hata kama alikuwa hajisikii vizuri. Zaidi ya hayo, ilikuwa bado ni kama zamani. Iwe alikuwa anaumwa au la, ishu ni kwamba, Linda alikuwa kando yake.
Patrick alimtazama moja kwa moja. Pamela alikuwa amejipodoa kidogo tu lakini uso wake ulikuwa bado mzuri. Patrick hakuwahi kuacha kumfikiria tangu walipoachana. Mara nyingi hakuweza kudhibiti hisia zake zilizomuumiza moyo. Hapo awali alikuwa hapendi kunywa pombe, lakini sasa marafiki zake walipomtaka aende kujumuika nao, hakuweza kuwakatalia.Mara alianza kuumwa kwa sababu alikunywa pombe kupita kiasi na hakuzingatia kula, na hatimaye aliishia kuumiza tumbo lake.
Linda alimuona Patrick akimkazia macho Pamela naye akauzuia wivu moyoni mwake kabla ya kulazimisha tabasamu. “Pamela kwanini usirudishe moyowakokwa Patrick? Ulikuwa karibu mara ya mwisho ku…
Alikuwa karibu mara ya mwisho kufanya nini? Pamela alikunja uso. Maneno hayo yalionekana kuwa na maana iliyofichwa. Alikuwa karibu mara ya mwisho kuolewa naye, ama?
Hata hivyo, tayari alishakata tamaa na Patrick Jackson na hakuwa na mpango wa kwenda sambamba na mawazo ya Linda.
"Una fikra mbaya. Hatuna tena chochote cha kufanya kati yetu. Niko bize, kwa hiyo nitaondoka sasa hivi.” Pamela akawaacha na kuondoka.
Patrick alihisi maumivu ya moyo wake yakizidi kuwa makali, karibu kuufanya mwili wake utetemeke kwa uchungu. Hapo awali, Pamela alikuwa na wasiwasi mwingi juu yake. Kila alipohisi kuumwa hata kidogo, Pamela angemhudumia hadiapone. Angekaa naye usiku kucha ili tu kumhudumia. Sasa, hakutoa hata neno la kufariji.
"Patrick, twende." Linda alimshika Patrick na kumuongoza kwenye idara ya vipimo.

Baada ya Patrick kuingia kwenye chumba cha daktari, Linda alibaki akimsubiri nje kwenye mabenchi ya kupumzikia. Aliyakumbuka vizuri maongezi aliyomfumania Pamela akiongea na Lisa. Alichukua simu yake na kupiga namba za Lina. “Lina, otea nimemwona nani hospitali sasa hivi?”
“Nani?”
“Pamela Masanja, alikuwa kwenye ofisi za uchunguzi wa vinasaba. Kama sikumsikia vibaya alimtajia Lisa jina lako huku akisema kwamba matokea yameonyesha kufafana kwako na Jones Masawe. Ina maana Lisa alikuwa haamini kama wewe ni mtoto wa Jones?”

Sura ya: 264

“Uchunguzi wa vinasaba?” Sauti ya Lina upande wa pili wa simu ilionyesha mshangao. “Ina maana Pamela amerudi Dar es Salaam?”
“Hata mimi nimeshangaa kwanini karudi Dar ghafla,” Linda aliongea kwa wasiwasi. “Isije kuwa anataka kurudiana na Patrick! Sitamwacha afanikiwe kwa hilo—”
“Linda, tutaongea zaidi baadaye,” Lina alimkatisha ghafla. “Kuna dharura imejitokeza ghafla.” Lina alikata simu na ghafla akahisi kuwa kichwa chake kinamuuma. Alikuwa amepoteza sehemu kubwa ya nywele wakati Lisa alipomvuta nywele hapo awali.
Moyo wa Lina ukadunda kwa hofu. Hapo hapo akapiga namba ya siri na kusema, “Rafiki wa Lisa Pamela alionekana kwenye idara ya uchunguzi wa DNA kwenye hospitali ya Golden Life huko Dar es Salaa. Nahisi Lisa ameshanishtukia.Atakuwa alinyofoa nywele zangu na kumpa rafiki yake akafanye uchunguzi wa ili kuhakikisha kama ni Lina.”
“Nitalishughulikia hilo kikamilifu.” Sauti ya ajabu kutoka kwenye simu ilisikika.
Lina aliingiwa na wasiwasi. “Sasa nifanyeje bosi? Ikiwa Alvin na genge lake watagundua kuwa mimi ni Maurine Langa feki, bila shaka wataniua."
“Usijali. Maadamu unatufanyia kazi, sitakuacha ufe.” Sauti hiyo ilimtoa wasiwasi.
•••
Lisa alizipokea zile nyaraka kutoka kwa Pamela kwa njia ya whatsapp na moja kwa moja akaenda maktaba kumtafuta Alvin. Alvin mara chache alienda ofisini kwa siku hizo na kwa kawaida alifanyia kazi zake katika chumba cha maktaba. Aliusukuma mlango na kuingia ndani.
Macho ya Alvin yalimtoka alipomuona. Aliona nia ajabu sana. Kwa siku kadhaa, Lisa hakuwa amejisumbua hata kumtafuta. “Umenimiss?
Lisa alikwenda moja kwa moja kwenye pointi. Aliwasha simu yake, na kumuonyesha kile cheti cha matokeo ya uchunguzi wa DNA.
Wakati Alvin alipoona ripoti ya uchunguzi wa DNA kati ya Jones Masawe na Maurine Langa, uso wake wote ukaganda. “Hiyo ina maana gani? Wao ni baba na binti?” Alipigwa na butwaa kidogo. Maurine alikuwa binamu wa Sarah Langa. Kwanini ghafla akawa binamu wa Lisa? "Hapana, Maurine Langa halisi hawezi kuwa binti wa Jones Msawe.” Alvin alibisha.
“Ni kwa sababu Maurine Langa wa sasa ni feki. Yeye ni Lina Jones baada ya kufanyiwa upasuaji wa plastiki.” Lisa alimwambia.
Alvin aliganda kabisa. Baada ya muda mrefu, alimtazama Lisa kwa macho tata. “Lisa, najua humpendi Maurine. lakini si vyema kumzushia jambo kubwa kama hili—”
“Hapana, siwezi kumzushia, huu ni ushahidi tosha.” Lisa alimshawishi Alvin. “Sikuwahi kufikiri hivyo hapo kabla. Nilishangaa Maurine alikuwa amenifahamu vipi mara ya kwanza nilipokutana naye, lakini sikufikiria sana jambo hilo wakati huo. Kisha, nilikwenda kwenye spa na Charity nikamwona Maurine pale. Charity alisema kuwa Maurine halisi alipata ajali alipokuwa mdogo ambayo ilimpa kovu kubwa chini ya shingo yake lakini hakuona kovu hilo kwenye shingo la Maurine huyu. Isitoshe, tabia yake ni tofauti kabisa na Maurine anayemjua yeye. Ndiyo maana nilivuta nywele zake pale hospitalini na kuzifanyia uchunguzi kwa kulinganisha na nywele za Jones Masawe. Imetokea kwamba wao ni baba na binti wa damu.”
Lisa alimtazama Alvin kwa umakini. “Je, hukumbuki kwamba Lina Jones alichukuliwa na watu wasiojulikana huko kijijini mlikompeleka?”
"Lakini nilimwomba Hans achunguze maisha ya zamani ya Maurine na hakupata chochote cha kutilia shaka..."
"Alichopata kinaweza kuwa cha juu juu tu. Je! unamfahamu Maurine Langa halisi? Unajua tabia yake? Unajua aliko?" Lisa aliendelea, “Fikiria kwa makini. Marafiki zako wanaendelea kusema kwamba kumbukumbu yako inazidi kuwa mbaya kwa sababu nilikukasirisha, lakini lazima ulihuzunika sana pia Sarah Langa alipokufa. Je, hili lilikutokea wakati ule? Tangu Maurine Langa alipoanza kukuhudumia, kwanini umekuwa ukisahau kumbukumbu zako?”
Uso wa Alvin ukawa mweupe kama karatasi. Kwa hakika, ilikuwa tangu Maurine aanze kumhudumia tu ndipo alianza kupata maumivu ya kichwa mara kwa mara na alipata shida ya kumbukumbu.

"Nina uhakika 100% kuwa yeye ni Lina Jones. Kusudi lake ni nini kwa kutokea ghafla karibu nawe? Je, alikuongezea chochote kwenye maziwa na dawa ambazo huwa anakuandalia? Umewahi kufikiria kuhusu hilo?” Macho ya Lisa yalikuwa na huzuni. "Unadungwa dripu na kunywa dawa kila siku, na ulikuwa na uwezo wa kupata nafuu hapo awali. Mbona zimekuwa bure sasa?”
Alvin alikosa la kusema. Pia alianza kuamini maneno yake.
"Unaweza kumwambia mtu kumshika Maurine mara moja na kumpeleka kwa uchunguzi wa uzazi? Nina uhakika kwamba yeye ni Lina Jones.” Lisa alikumbusha kwa dhati, “Chukua hatua sasa kabla hawajashtukia. Pia, aliyemtorosha Lina ndiye aliyepanga haya yote. Mtu aliye nyuma ya Lina lazima awe na nia mbaya na wewe!”
“Ndiyo.” Mara Alvin akampigia simu Hans. "Mteke Maurine Langa mara moja. Ninataka kupata ripoti ya uchunguzi wa uzazi kuhusu Maurine na Alex Langa Njau ndani ya saa 24."
Lisa alihisi kufarijika kidogo. Mwishowe, bado hakuamini kwamba ripoti hiyo haikuwa ya kweli, lakini ilimbidi aithibitishe yeye binafsi kabla ya kuwa na uhakika. Hata hivyo, haikujalisha. Alichosema aliamini kuwa ni kweli.
•••
Saa nane za usiku, Alvin ghafla alipokea simu kutoka kwa Hans. “Bwana Mkubwa, kuna habari mbaya. Maurine Langa amekufa.”
"Nini kimetokea?" Alvin alikaa ghafla.
"Nilimfungia ndani ya nyumba moja nje kidogo ya jiji. Usiku wa manane, walinzi walimfumania mtu akijaribu kumwokoa Maurine na kuanza kumkimbiza, lakini waliporudi, walikuta walinzi wengine wawili wakiwa wamepoteza fahamu na nyumba inawaka moto. Maurine aliteketea na moto hadi kufa.” Hans alisema kwa huzuni, “Nadhani hawakuwa watu waliojaribu kumwokoa Maurine. Walikuwa wakitaka kumteketeza.”
“Nakuja sasa hivi.” Alvin akakata simu na kuliendesha kwa haraka hadi eneo lilipotokea tukio hilo.
Aliposhuka kwenye gari, alimuona Rodney akiwa amesimama mbele ya begi lenye mabaki ya mwili wa Maurine. Macho yake yalikuwa mekundu, alipomuona Alvin, alimkimbilia ili kumpiga ngumi.
"Tulia." Alvin akaishika ngumi yake.
“Nitawezaje kuwa mtulivu? Kwanini umemfungia Maurine? Amekufa. Umemuua!” Rodney alimlalamikia. “Najua hawezi kufananishwa na Lisa Jones, lakini bado ni binamu wa Sarah. Yeye ni msichana asiye na hatia."
"Huenda asiwe Maurine Langa," Alvin alisema kwa upole.
Rodney alicheka kwa hasira. “Mimi si kipofu. Ni nusu tu ya uso wake ulichomwa moto. Bado niliweza kumtambua.”
"Lisa alimfanyia uchunguzi wa uzazi. Yeye ni Lina Jones, lakini alifanyiwa upasuaji wa plastiki ili kufanana na Maurine.” Alvin alikunja uso. "Nilimteka ili kujua aliyepanga haya yote ni nani."
“Unasema nini?” Rodney alionyesha kuwa na mashaka.
“Kwanini nikudanganye?” Alvin alipomaliza kuzungumza, ghafla Hans aliingia na kuzungumza, “Bwana Mkubwa, idara ya uchunguzi imetoka na matokeo. Ripoti inaonyesha kuwa Maurine na Alex Langa wana uhusiano wa damu.”
"Alvin Kimaro, wewe b*stard!" Rodney alimpiga kweli ngumi ya uso safari hii.
Alvin alirudi hatua chache nyuma na kushindwa kurejesha usawa wake. Uso wake wote ulikuwa na huzuni. "Una uhakika hakuna kosa lolote?" Alvin alipigwa na butwaa.

Sura ya: 265

“Ni hospitali ya Dokta Choka, kwa hivyo hawezi kuwa amekosea. Baadaye, daktari wa uchunguzi atachukua mwili kwa ajili ya uchunguzi . Itafahamika kama alikuwa amefanyiwa upasuaji wa plastiki au la.”
“Sawa.” Alvin akasugua kichwa chake. "Tafuta ni nani aliyetuma watu hapa jana usiku."
“Kuna nini cha kuchunguza tena? Ni wazi Lisa Jones ndiye aliyefanya haya. Bado unamsikiliza yule mwanamke?!” Rodney alipiga kelele kwa huzuni, “Yule mwanamke ni mkatili sana! Maurine hakuwahi kamwe kufikiria kukutongoza, lakini Lisa bado alijaribu kumuua Maurine kwa kila njia na hatimaye amefaulu.”
"Lisa sio mtu wa aina hiyo." Alvin alikanusha. "Lazima alidanganywa."
"Hata kama alidanganywa, ni kwa sababu ya mawazo yake finyu. Ni mjinga sana huyo mwanamke”
"Rodney Shangwe, umemaliza?" Alvin alishindwa kuvumilia tena.
“Hapana, sijamaliza. Nimemvumilia muda wote huu kwa sababu ni mkeo, sasa sitaweza kumvumilia tena.” Rodney alifoka.
“Acheni kugombana!” Chester alishuka kwenye gari na kusikia sauti zao za ugomvi.
“Sijali. Sitaacha jambo hili lipite hivi hivi. Hata kama Alvin atachagua kumlinda mke wake, sitamsamehe kamwe.” Rodney aligeuka na kuondoka baada ya onyo hilo.
"Nini mwazo yako, ?" Chester alienda kwa Alvin.
"Lisa anamwonea wivu Maurine, lakini sidhani kama angekuwa mkatili kiasi hiki." Alvin akasugua kichwa chake. “Kama Charity Njau asingesema kwamba Maurine huyu ni feki, Lisa asingemshuku…”
“Charity Njau.” Chester alikunja uso. "Ni yeye tena." Baada ya kutulia, alisema kwa upole, “Afadhali awe hana uhusiano na hili. La sivyo, nitahakikisha kwamba ameozea jela.”
Mchana, matokeo ya uchunguzi wa maiti yalitumwa kwa Alvin.
"Bwana Kimaro, mtu aliyeteketea kwenye eneo la tukio imebainishwa kuwa ni Maurine Langa. Wazazi wake pia wamefanyiwa ulinganisho kamili wa vinasaba na kuthibitisha hilo.”
Hans alipomaliza kuongea, alimuona Alvin akiwa ameshika kichwa chake kwa mikono yote miwili huku mwili ukimtetemeka kwa maumivu.
“Bwana Kimaro…”
“Wazazi wa Maurine wanasemaje?” Alvin alivumilia maumivu na kuuliza kwa sauti ya kuchoka.
“Walikuwa wakilia bila kukoma. Unafikiri wangewezaje kupokea taarifa kama hizo? Wanataka haki itendeke.” Hans alipumua.
"Lifanyie kazi hilo."
“Kuna jambo moja zaidi.” Hans aliongeza. “Aliyewahadaa walinzi jana usiku na aliyewasha moto wamenaswa. Wana…wanahusiana na Charity Njau. Ni watu ambao wamekuwa wakifanya kazi na Charity nyuma ya pazia.”
“Charity Njau, kwa hivyo alikuwa ni yeye…” Alvin aligonga meza kwa ukali na kusimama, uso wake mzuri ukiwa umejawa na hasira ya kutisha.
"Rodney aliwapigia polisi na wamepeleka maafisa wao kwa familia ya Njau kumkamata." Hans alisema.
“Waambie polisi wampe mwanamke huyo adhabu nzito zaidi. Sitaki aachiliwe maisha yake yote.” Alvin aliuma meno yake na kuamuru neno baada ya neno
“Imeeleweka.”

•••
Katika makazi ya familia ya Njau, hakuna aliyekuwa anajua kilichokuwa kikiendelea. Boris Langa Njau, Baba wa Charity alikuwa akifanya kazi zake sebuleni kwa utulivu wote huku mkewe, Jennifer Musyoka, akiketi kimya jikoni akimtengenezea chai.
Charity akatoka akiwa amevalia mavazi ya ofisini, alikutanisha macho yake na baba yake aliyekuwa ametulia sebuleni.
"Charity, unaenda ofisini?" Bwana Langa alimwona na kumpungia mkono binti yake kipenzi.
“Baba.” Charity akatembea kuelekea kwake. “Hali ya kampuni si nzuri kwa sasa—”
“Usijali. Usiwaze sana kuhusu hilo. Ikiwa familia ya Kimaro inataka kweli kutufilisi, basi hatuwezi kuwazuia.” Boris alimtazama na kusema kwa utulivu, "Ikiwa kampuni itanyanyuka, basi itanyanyuka tu. Ikibidi tutaiuza tu na kuanzisha kampuni ya mambo mengine. Haijalishi hata kama tutalazimika kuhama jiji la Nairobi, mradi tu familia yetu ya watu watatu iwe na furaha. Wakati fulani, ninapomwona msichana kama wewe akifanya kazi kwa bidii sana kiasi kwamba hapati hata wakati wa kupumzika, mimi na mama yako huumia moyo sana.”
Jennifer aliitikia kwa kichwa na kusema kwa sauti ya upole, “Baba yako na mimi tumezeeka. Hatujali ni pesa ngapi unapata. Cha muhimu ni kuwa uko salama na mwenye furaha.”

"Asanteni." Moyo wa Charity ukapata faraja. “Nitajaribu kwa mara nyingine kumbembeleza Alvin. Ikiwa nitashindwa kupata nafasi kwenye mtandao wake, basi nitaiuza kampuni. Baada ya hapo, familia yetu inaweza kuondoka Nairobi…”
Alipomaliza tu kuzungumza, kundi kubwa la polisi liliingia ghafla. “Bi. Njau, polisi wamepata ushahidi wa kuhusika kwako katika kesi ya mauaji. Uko chini ya ulinzi.” Afisa mmoja akamfunga pingu mara moja.
Charity alipigwa na butwaa. “Kesi gani ya mauaji? Sijui unazungumzia nini.”
“Maurine Langa amekufa. Uliwaambia Shaka na Solo wamchome moto. Tayari wamekiri hilo kwenye maelezo yao polisi.”
Akili ya Charity ikaganda ghafla. "Hiyo haiwezekani. Shaka na Solo ni watu wangu sawa, lakini sikuwahi kuwaambia wafanye hivyo.”
"Hakuna mhalifu anayekubaligi kosa lake, lakini tayari tuna uthibitisho wa uhakika." Bila kusema neno jingine, afisa huyo alimsukuma Charity nje ya mlango.
"Hiyo haiwezekani. Binti yangu hajawahi kuua mtu kamwe!” Boris Njau alikimbia na kumvuta polisi huyo.
Mwanaume huyo alimsukumiwa mbali. "Sio tu kwamba binti yako aliua mtu, lakini pia ana rekodi mbaya za kihalifu. Ataozea jela maisha yake yote.”
Boris alianguka chini. Mwili wake wote ukakamaa na kuzimia kwa mshtuko mara moja.
“Mpenzi amka!” Jennifer alichanganyikiwa na kupiga simu kwa haraka kuita ambulance kwa hofu.
Familia ya Njau ilikuwa ikiporomoka. Watumishi walitazama kwa macho yao wenyewe wakati familia ya Njau, ambayo ilikuwa juu kwa miaka kadhaa, ikitoweka kama moshi.
Moyo wa Lisa haukutulia. Ulikuwa ukitetemeka kwa siku mbili mfululizo. Alikuwa amepata ushahidi kwamba Maurine Langa alikuwa ni Lina, kwa hiyo lazima Alvin angekuwa anachunguza jambo hilo. Lakini tangu alipozipata taarifa hizo, hakuwa amerudi nyumbani na hakuweza kumpata kwenye simu pia. Zaidi ya hayo, hakuweza kuipata hata simu ya Charity pia. Hisia ya hofu na wasiwasi ilizidi kuwa na nguvu moyoni mwake.
Wakati huo, Pamela alimpigia simu. “Jamani, nitakufa kwa hasira! Kwa kweli Rodney Shangwe alimwambia meneja mkuu wa Osher anifukuze kazi. Yeye ni mwendawazimu kabisa. Kichwa chake lazima kimejaa mavi tu!"
"Nini kimetokea? Si ulitia saini mkataba?”
Ndio, nilitia saini mkataba wa miaka mitano lakini wamenifukuza bila maelezo yoyote wala kunilipa fidia yoyote, na hata wameniweka kwenye orodha ya blacklist, sitaweza kuajiriwa na kampuni yoyote nchini Kenya… sijui nilifanya kosa gani.” Pamela aliongea kwa masikitiko.
Lisa alishtuka. Halikuwa tatizo kubwa kwa Pamela kufukuzwa kazi, lakini kumworodhesha kwenye blacklist hakika ilikuwa ni kumwangamiza. Rodney Shangwe alikuwa na chuki gani kubwa na Pamela hadia kaamua kumfanyia hivyo?
“Usijali. Nitamuuliza Alvin kuhusu hali hiyo,” Lisa alisema kwa wasiwasi.”Si wazo zuri kukuajiri kwenye kampuni yangu, lakini ikibidi nitafanya hivyo, usiwaze sana.”
“Sawa. Je, umeweza kuwasiliana na Charity hivi karibunii? Nilitaka kumpigia nipate kinywaji naye lakini sikuweza kumpata.” Pamela alisema kwa sauti ya huzuni.
“Hujaweza kumpata pia? Hata mimi nimejaribu kumtafuta sijampata”
"Ndio, kunaweza kuwa na kitu kimemtokea?" Pamela aliuliza kwa jazba.
"Nenda kwa familia ya Njau na ujaribu kuulizia." Lisa alizidi kuwa na wasiwasi
Pamela alifukuzwa kazi na kuwekwa kwenye blacklist, na simu ya Charity haikuweza kupatikana. Nini kilikuwa kinaendelea?

TUKUTANE KURASA 266-270

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......266-270

Sura ya: 266

Baada ya kukata simu, Lisa aliendelea kumtafuta Alvin bila mafanikio, hatimaye akampigia simu Hans. Hans alipokea baada ya kuita kwa muda mrefu. "Bibi mdogo, kuna nini, mbona una wasiwasi sana?"
“Mbona Alvin hapokei simu zangu?”
"Bwana Kimaro yuko ... kwenye mkutano."
“Tangu jana, na juzi hapokei simu zangu,” Lisa alisema kwa hasira, “Mwambie arudi nyumbani jioni, au… Au nitaenda kwake badala yake.”
“Bibi mdogo usiwe na wasiwasi, Kimaro ana shughuli nyingi…”
“Ana shughuli gani zinazomfanya asifike nyumbani kwa siku kadhaa na hapokei simu zangu? Au labda amepata mwanamke mwingine tena?" Lisa alicheka kwa kejeli.
“Hapana, Bwana Kimaro amebanana tu na shughuli nyingi” Hans, akihisi maumivu ya kichwa yakimjia.
Saa nane usiku, Lisa alipokea tena simu kutoka kwa Pamela. "Charity alikamatwa na polisi. Walisema alikodi watu wa kumuua Maurine Langa. Baba yake alipatwa na mshtuko wa moyo na kupelekwa hospitalini. Mama yake anatafuta msaada kila mahali lakini hakuna aliye tayari kumsaidia. Uvumi umeenea kwamba familia za Kimaro, Choka, na Shangwe zilitoa agizo. Yeyote atakayethubutu kumwokoa Charity Njau watashughulika naye.”
“Inawezaje kuwa hivyo?” Lisa alihisi kama ubongo wake unaweza kulipuka. "Maurine Langa amekufa?"
“Ndio. Maurine Langa ameteketea kwa moto" Pamela alisema, “Niko hospitalini na wazazi wake sasa. Wanatia huruma sana. Ndugu zao wote wanawakwepa sasa, na watumishi wao wote pia wamekimbia. kampuni yao pia ina hatihati ya kufilisiwa.”
"Naenda kumtafuta Alvin." Kichwa cha Lisa kilikuwa kimekufa ganzi.
Hakuweza kusubiri hadi kupambazuke. Aliendesha gari moja kwa moja hadi getini, lakini mlinda mlango alikataa kumfungulia geti.
"Bibi mdogo, huwezi kutoka peke yako bila ruhusa ya Bibi au Mzee Kimaro." Mlinda mlango akatazama pembeni.
“Fungua. Lazima nitoke nje leo. Naenda kutamtafuta Alvin.” Lisa hakuwa na subira tena. "Usipofungua milango, nitagonga."
“Usifanye hivyo! Tulia." Mlinda mlango huyo alikuwa amefikia mwisho wa akili yake wakati gari nyeusi aina ya BMW lilipoingia ghafla na Alvin akatoka ndani yake.
“Bwana Kimaro, afadhali umefika kwa wakati. Bibi mdogo alikuwa anataka kwenda kukutafuta." Mlinda mlango akafanya kama amemwona mwokozi wake.
Lisa alikaa kwenye gari akiwa ameegemea usukani. Alvin aliposogea kwenye dirisha la gari, alimuona akiwa bado amevaa nguo za kulalia za pinki. Katika kipindi hicho, watumishi walikuwa wakimhudumia chakula na vinywaji vyenye lishe kwa wingi, kwa hiyo ngozi yake ilikuwa ikipendeza zaidi kuliko hapo awali.
"Nimerudi. Hebu tuingie ndani.” Alvin alifungua mlango na kumshusha kutoka kwenye gari.
“Alvin, niache!” Lisa alilalamika. “Nataka kukuuliza hivi ni kweli Charity alimuua Maurine Langa? Siamini kama anaweza kufanya hivyo, hizi ni njama tu mnamfanyia. Kwanini mnakuwa makatili hivi kwa kumuonea mwanamke asiye na hatia?”
Alvin alikaa kimya na kumbeba hadi ndani na kumuweka taratibu kwenye sofa.
“Alvin, umesikia nilichosema? Kwanini mnampakazia Charity kesi ya mauaji kisha Rodney anamfukuza kazi Pamela na kumweka kwenye blacklist? Wote ni marafiki zangu. Walifanya kosa gani?" Lisa alishindwa kujizuia na kusimama. “Vipi kuhusu Maurine Langa? Nilikuambia kuwa yeye ni Lina Jones. Nini kingine unahitaji kufanya ili uamini?"
"Lisa nyamaza." Uso mzuri wa Alvin ulionyesha jeuri fulani. "Umedanganywa na Charity tangu mwanzo."
“Sikudanganywa, Lina ndiye Maurine…”
“Jionee mwenyewe.” Alvin alitoa ripoti mbili mikononi mwake. "Moja wapo ni ripoti ya uchunguzi wa nywele, ambapo nyingine ni ripoti ya uchunguzi wa maiti ya Maurine. “Haya yote yanathibitisha kuwa yeye ni mtoto wa familia ya Alex Langa Njau. Daktari amemchunguza uso wake na kugundua kuwa hajawahi kufanyiwa upasuaji wa plastiki. Yeye ndiye Maurine halisi. Charity amekuwa akikudanganya.”
Lisa mara moja akapitia taarifa hizo. Mara tu alipoona maneno yaliyoandikwa juu ya ripoti hiyo, kichwa chake kilikaribia kulipuka.
“Hii haiwezekani. Charity asingeweza kunidanganya.” Alitikisa kichwa akiwa haamini.

“Nadhani utakuwa umepumbazwa naye. Umemjua kwa muda gani? Kwa nini unataka kumwamini Charity kuliko mimi? Nimekuambia kwa muda mrefu kuwa huyo mwanamke hafai, si mtu mzuri.”
Tabia yake ya ukaidi ilianza kumfanya Alvin kupandwa na hasira. “Nilikusikiliza na kumfungia Maurine, lakini Charity baadaye aliagiza watu wachome moto nyumba na kumteketeza Maurine hadi kufa. Aliyewasha moto huo amejulikana, na ni mtu ambaye alitekeleza maagizo ya Charity.”
Lisa alirudi nyuma na kukaribia kujikwaa kwenye kochi bila kujijua. Alvin alishika kiuno chake kwa haraka na kumwonya kwa upole, “Jihadhari Lisa. Una mimba sasa…”
Kabla hajamaliza kusema, Lisa alimsukuma. “Nina uhakika Maurine ni Lina. Nilipokutana naye mara ya kwanza, nilimfahamu vizuri…”
“Acha kung’ang’ana Lisa. Unamuonea wivu Maurine tu, ndiyo maana unatoa visingizio vya kila aina kuunga mkono madai yako kuwa yeye ni Lina.” Macho yenye huzuni ya Alvin yalidhihirisha hali ya kukata tamaa. “Mbona huniamini? Kwanini unaelemewa kirahisi hivi na wivu na kulaghaiwa na Charity? Sasa kwa kuwa Maurine amekufa, wazazi wake wamepoteza binti. Je, huoni hatia hata kidogo?”
“Hivi ndivyo unavyoniona?” Lisa alianguka katika hali ya kukata tamaa kabisa. “Kwanini na wewe huniamini, basi? Jambo hili sio rahisi kama inavyoonekana. Pia, Pamela amefanya nini?"
“Hakufanya lolote. Ulimwomba akusaidie kupima DNA paternity, na kitendo hicho kilimkasirisha Rodney,” Alvin alijibu bila kujali, “Unapaswa kujisikia mwenye bahati kwa kuwa upo na mimi. Vinginevyo, Rodney angekufanya kitu kibaya sana. Angeiharibu kabisa Mawenzi Investments.”
Sura ya Lisa ilipwaya kabisa. Je, hii ilimaanisha kwamba Pamela alifukuzwa kazi na kuwekwa kwenye blacklist kwa sababu tu alikuwa amemkosea Rodney? Charity alipakaziwa kesi kwa kuwa alimshtukia Maurine Langa feki? Na Lisa alipona tu kwa sababu ya Alvin? Alitazama huku macho yake yakiwa yametua kwenye uso wa Alvin, hakutaka kuamini kabisa alichokisema. Ni lini watu hao kama Alvin na Rodney walianza kufikiria kuwa wanaweza kumwangamiza mtu yoyote bila kujali hadhi yake?
"Ni kosa langu," Lisa alinong'ona kwa macho mekundu ghafla. "Sikupaswa kukutongoza nilipokuona pale baa kwa mara ya kwanza."
Ikiwa asingemtongoza, asingeolewa naye, na asingeingia kwenye matatizo yote yale.
"Lisa, unajua unachosema?" Alvin alikasirishwa na tabia yake ya dharau. Anawezaje kujuta kuolewa naye kwa sababu watu hao?!
Je, Charity na Pamela walikuwa muhimu kuliko yeye? Alikuwa mume wake, wakati wao walikuwa ni marafiki zake tu.
“Utawasaidiaje Charity na Pamela? Ni marafiki zangu.” Lisa alimsihi huku machozi yakimtoka bila kujizuia. Alifahamiana na Pamela tangu wakiwa shule ya sekondari. Pamela alikuwa kando yake licha ya magumu aliyopitia miaka yote hiyo.
“Siwezi kuwasaidia.” Alvin hakujisikia tena kubishana na Lisa. Akageuka na kuondoka.

Sura ya: 267

"Nakuchukia, Alvin." Lisa alitokwa na machozi.
“Pumzika vizuri. Usirudi ofisini kwa sasa. Nitashughulikia kila kitu kinachohusiana na Mawenzi Investments kwa niaba yako hadi utakapojifungua watoto hao wawili.” Alvin hakuwa na la kufanya zaidi ya kusema hivyo bila kupenda kwani alishindwa kuvumilia kumuona akilia. Kwa hayo, akapiga kisigino na kutembea kuelekea getini.
“Simama…” Lisa alitaka kumfuata, lakini Hans alimzuia. “Bi Kimaro, bora uache kubishana na Bwana Kimaro. Kwa sababu yako, uhusiano wake na Rodney Shangwe umegeuka kuwa mbaya hivi karibuni. Wazazi wa Maurine pia walikuja kumlaumu Alvin kwa kifo cha binti yao, ana huzuni sana kwa sasa na huenda hali ya ugonjwa wake ikawa mbaya tena.”
Lisa alisimama na kuuliza kwa mshangao, "Hans, ni kweli maiti ni ya Maurine?"
“Ndio. Madaktari waliofanya uchunguzi wa kitaalamu na kipimo cha DNA ni waaminifu sana kwa Alvin, kwa hivyo matokeo hayawezi kuwa na makosa. Hakika ulikosea, Bi Kimaro.”
Inawezekana kweli alikosea? Alvin alidai kuwa Charity amekuwa akimdanganya, lakini Lisa mwenyewe alihisi kwamba Maurine alionekana kufanana na Lina, hasa macho yake na tabia zake fulanifulani.
Kwanini taarifa alizozipata Alvin zilipingana na za Pamela? Kwanini za Pamela zilionyesha kuwa ni Lina na za Alvin zilionyesha kuwa yeye ndiye Maurine halisi?
Je, inawezekana kwamba Lina, ambaye alikuwa akijifanya kuwa Maurine, alimrudisha Maurine halisi baada ya kujua kwamba Lisa alikuwa ameujua ukweli? Baada ya yote, ikiwa Lina angejifanya kuwa ni Maurine, basi walipaswa kumteka kwanza Maurine halisi ili mchongo wao usishtukiwe. Moyo wa Lisa ulishtuka sana.
Kadiri Lisa alivyozidi kuwaza kuhusu jambo hilo, ndivyo alivyoona kuwa inawezekana. Alimpigia simu Pamela mara moja. “Ulipofanya kipimo cha DNA, uligongana na mtu yeyote? Inawezekana kwamba suala hilo lilistukiwa?”
“Ulinisisitiza niwe makini. Kwa kawaida, sikumwambia mtu yeyote, isipokuwa wakati wa kupata nywele za Jones. Nilimwomba kaka yangu msaada kwa hilo. Hata hivyo, unajua tabia ya kaka yangu, sivyo? Hatuwezi kumtilia shaka.”
Lisa alikunja uso kwa kuchanganyikiwa. Kwa kweli, alimwamini sana Forrest. "Hakuna mtu yeyote aliyekuona kwenye idara ya uchunguzi, kama mtu yeyote ambaye alikuwa karibu na Lina?"
'Sidhani hivyo… Nilipoenda kuchukua ripoti hospitalini, nilikutana na wapenzi wasio na haya, Patrick na Linda. Siku hiyo Patrick hakujisikia vizuri, hivyo Linda akampeleka hospitali.”
“Linda?” Lisa alinong'ona baada ya kusikia hilo, "Inawezekana yeye ndiye aliyeunguza picha. Lina alikuwa na marafiki wengi matajiri wa kike huko Dar es Salaam alipokuwa bado kwenye chati, na pia Linda alihudhuria hata sherehe ya uchumba ya Lina na Ethan akiwa na Patrick. Ni rafiki mkubwa wa Lina.”
“Unashuku anaweza kuwa Linda?” Pamela alipigwa na butwaa.
“Mwambiye kaka yako afanye uchunguzi ili kujua ikiwa Linda alipiga au kupokea simu yoyote siku hiyo mlipokutana naye hospitali.”
Lisa alimweleza Pamela kilichotokea baada ya yeye kumtumia ripoti yake, jambo ambalo lilimfanya ashangae. "Unashuku kuwa Lina aligundua kuhusu hilo, ndiyo sababu wakabadilisha haraka na kumrudisha Maurine halisi?"
"Ndio. Mtu aliye nyuma ya tukio hili ametufanya sote tuanguke kwenye mtego wake. Kwa sababu yake, uhusiano wangu na Alvin unaanza kuvunjika. Pia amesababisha uhusiano wa Alvin na Rodney kuwa mbaya. Hata familia ya Njau sasa iko kwenye kona kali huku Charity akiwa jela.”
“Charity ndiye anayeteseka zaidi. Huenda akakaa gerezani milele licha ya kuwa hajafanya kosa lolote,” Pamela alinung’unika, “Ingekuwa bora nisimjue aliyefanya hivyo, au nitamuua bila shaka.”
"Kwa maana hiyo, Lina atakuwa ametoroka. Sijui ameenda wapi,” Lisa alisema huku akitabasamu kwa uchungu.
"Ni nyota ya ajabu." Pamela alikasirika. Baada ya kukata simu, alipanga kurudi Dar es Salaam kwa ndege ya mapema zaidi.
Ndege ilipotua tu, alipokea rekodi za simu ya Linda kutoka kwa Forrest, kaka yake. Baada ya kuzichambua, alipata rekodi ya simu ambayo Linda alipiga kwenda kwa Lina siku hiyo walipokutana hospitalini.

Hata hivyo, kila kitu kilikuwa sawa na matarajio ya Lisa. Linda ndiye aliyebumbulua mchongo mzima. Alikuwa ni Linda ambaye alisababisha Lina amfanyie njama ya kesi ya mauaji Charity.
Akiwa amesimama kwenye uwanja wa ndege, Pamela alihisi kizunguzungu. Moja kwa moja akaelekea kwenye kampuni ya Patrick bila hata kujua aliisimamishaje teksi.
Linda alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya Patrick wakati huo. Pamela mara moja alipanda ghorofani baada ya kufika. Linda, ambaye alikuwa amevalia maridadi, alipigwa na butwaa mara tu alipomwona. “Pamela, nini kinakuleta hapa? Unamtafuta Pat—”
“Ninakutafuta wewe.” Pamela alipiga pande zote mbili za uso wa Linda mara moja. Kwa muda mrefu Pamela alikuwa akitaka kufanya hivyo, lakini alikuwa akiungojea tu muda muafaka.
Hata hivyo, sasa…
Kwa sababu ya Linda, Charity alienda jela.
Kwa sababu ya Linda, Alvin hakumwelewa Lisa.
Kwa sababu ya Linda, Rodney alimfukuza kazi na kumweka kwenye blacklist.
“Linda, ningeweza kukuvumilia kama ungefanya kitu kingine chochote, lakini hukupaswa kuwasiliana na Lina. Ulimwambia nini? Umetuweka kwenye kona kali!”
Kwa kuzingatia sura yake ndogo, Linda ni wazi hakuweza kurudisha mapigo ya Pamela. Muda si muda, uso wake ukavimba.
Kwa bahati nzuri, baadhi ya watu katika kampuni walikuja kumtoa Pamela nje. Kila mtu alijua kuwa Pamela hapo awali alikuwa mpenzi wa Patrick, kwa hivyo hawakuthubutu kumvuta kwa nguvu. Mwishowe, ikawa kwamba Linda aliumizwa kabisa.
"Niache, Pamela! Sijui hata kidogo unachokiongelea.” Linda alihisi kana kwamba ngozi yake ya kichwa itnachunika kwa nguvu.
“Acha kujifanya mbele yangu. Nionyeshe simu yako na tutaweka kila kitu wazi. Nina uhakika huwa uliwasiliana na Lina kupitia WhatsApp.”
Pamela alipounyanyua mguu wake ili ampige teke Linda, sauti ya Patrick ilisikika nyuma yake ghafla. "Unafanya nini Pamela?" Alimsukuma Pamela akaanguka chini.
Patrick alimvuta Linda mara moja. Akiwa na nywele chafu na uso uliovimba, Linda alianguka mikononi mwake mara moja. "Patrick, nimeumiaaa!"
"Samahani kwa kuchelewa." Baada ya kuona mikwaruzo kwenye ngozi ya Linda, Patrick alizidi kung'aka kwa Pamela. “Pamela, angalia jinsi ulivyo mkorofi sasa. Nilipokuja kukutafuta huko Nairobi, ulinionyeshea jeuri mbele ya mwanamume mwingine. Sasa, umekuja ofisini kwangu kumpiga Linda bila sababu. Unafikiri sina ujasiri wa kukufanyia chochote?”
"Mambo yangu hayakuhusu." Pamela akauma meno na kusimama. “Najuta kabisa kukufahamu Patrick. Kama nisingewafahamu, msingenipeleleza pale hospitali juzi .”
“Sijui unasema nini. Hata hivyo, lazima uombe msamaha kwa Linda sasa hivi, au nitapiga simu polisi.” Maneno yake yalimkasirisha sana Patrick.
“Niombe msamaha? Haha. Ninajilaumu kwa kutokuwa mkatili vya kutosha. Nitampiga makofi kila nitakapomuona Linda!” Pamela alishindwa kujizuia na kupiga kelele.
Huku akitetemeka kwa hasira, Patrick akatoa simu yake kuwapigia polisi, lakini Linda akamzuia mara moja. “Usiwaite polisi. Pamela labda ana wivu tu—”
'Kuna kikomo cha wivu. Angalia, haonyeshi hata kujutia makosa yake. Nani anajua kama atakupiga tena?” Patrick aliongea kwa unyonge huku akiwa ameweka uso wa wasiwasi.
"Bwana Jackson, unamtetea sana mfanyakazi wako, huh?" Forrest, ambaye alikuwa mrefu na mwenye umbo lenye nguvu, ghafla alimsogelea. Macho yake meusi yalikuwa mazito kwa huzuni. “Upo radhi mpenzi wako wa zamani, ambaye ulikuwa na uhusiano naye kwa miaka minane, apelekwe kituo cha polisi kwa ajili ya mwanamke huyu. Si ajabu kwamba Pamela alichagua kutokuwa nawe.”
Wafanyakazi waliokuwa karibu nao walianza kunong’onezana wao kwa wao.
"Si ajabu kwamba Pamela alikasirika. Inawezekana kwamba Bwana Jackson alimsaliti kwa Linda?”
"Ina maana kwamba Pamela amesalitiwa?"
“Hilo linawezekana. Ninawaona wakiwa pamoja mara nyingi sana.”

Sura ya: 268

Mara baada ya Patrick kusikia maneno hayo, uso wake mzuri ulianza kuonyesha hasira. “Hili lieleweke vizuri, yeye ndiye aliyemvamia na kumpiga Linda bila sababu. Nimeachana naye kwa muda mrefu.”
“Unajua nini kilimfanya ampige Linda?”
Baada ya kusikia swali kali la Forrest, Patrick alipigwa na butwaa. "Haijalishi ni sababu gani, si sawa alivyofanya."
Pamela alitoa tabasamu, ambalo lilionekana kuficha huzuni kwenye uso wake wa machozi. Kwa kweli alijilaumu kwa kuangukia kwa mtu kama huyo wakati huo. Alikuwa kipofu?
Forrest alimpigapiga Pamela begani kwa huzuni. “Si sawa kumpiga mtu, lakini kwa kuwa ni mpenzi wako wa zamani, huelewi tabia yake? Kweli, labda usingeweza kujisumbua kumwelewa. Kwako, hata nywele tu za mwanamke huyu ni muhimu zaidi kuliko moyo wa Pamela. Labda, machoni pako, Pamela ni takataka tu.”
Patrick aliganda kwa muda. "Forrest, tunazungumzia tukio la kupigwa makofi, sio thamani ya Pamela ama Linda. Siwezi kujadili kile kilichotokea huko nyuma pia. Tumeachana kwa muda mrefu.”
“Uko sahihi. Nimesikitika tu kwa sababu dada yangu alipoteza muda wa ujana wake kwa mwanaume kama wewe.” Macho ya Forrest yalionyesha kutojali. "Kweli, kwa kuwa Pamela alimpiga Linda, inamaanisha kwamba anastahili kupigwa. Unaweza kuwaita polisi waje kwenye nyumba ya familia ya Masanja na kumkamata Pamela. Ngoja tuone kama utafanikiwa kumkamata.” Baada ya hayo, Forrest alimchukua Pamela na kuondoka naye.
"Forrest, kimsingi unampoteza Pamela kwa tabia hiyo." Akiwa ameumizwa na maneno yake, Patrick alihisi kuwa amepoteza heshima yake.
"Ndio, kwa sababu yeye ni dada yangu mpendwa, ninamjali, kwa nini nisimtetee?” Forrest alikoroma kisha akaondoka bila kuangalia nyuma.
Pamela, ambaye alilindwa mikononi mwa Forrest, hakugeuka na kumtazama Patrick tena.
Kwa upande mwingine, Patrick alihisi mzigo mkubwa wa hasira kifuani mwake ghafla. Alikumbuka Pamela akisema kwamba alijuta kuwahi kumpenda. Je, alisema tu kwa hasira au alimaanisha?
“Lo. Inauma…” Akiwa amejiegemeza kwenye mikono ya Patrick, Linda alifunika uso wake na kuugulia maumivu. "Inauma sana, Patrick."
"Ngoja nikupeleke hospitali." Patrick akamshika mkono.
“Siwezi hata kunyanyua mguu. Nadhani miguu yangu yote imejeruhiwa." Tabasamu la uchungu likaonekana usoni mwa Linda. Patrick hakuwa na la kufanya zaidi ya kumbeba na kuteremka kwenye ngazi.
"Unajua kwanini Pamela alishindwa kujizuia na kukupiga kofi, Linda?"
Sasa kwa vile Patrick alikuwa amerejesha utulivu wake, ilimgusa kwamba Pamela, ingawa alikuwa na kiburi, mara nyingi asingemshambulia mtu bila sababu hata awe na hasira kiasi gani. Zaidi ya hayo, ilikuwa imepita nusu mwaka tangu waachane. Ikiwa angekusudia kumsababishia Linda matatizo, angefanya hivyo kipindi hawajaachana.
“Ningejuaje? Nilikutana naye hospitalini mara ya mwisho. Sijakutana naye tangu wakati huo.” Linda aliongea kwa hasira.
Patrick akakaa kimya. Kuanzia siku hiyo na kuendelea, angejawa na majuto na kinyongo kwa Pamela kila alipokumbuka yaliyotokea siku hiyo, Kwa bahati mbaya, hakuna kitu ulimwenguni kinachoweza kuponya majuto.
Katika maegesho ya gari, muda mfupi baada ya Pamela kuingia ndani ya gari, alimuona Patrick akiwa amembeba Linda na kumwingiza ndani ya gari lake. Wakati huo, alihisi kukata tamaa sana. Angalau hakujuta kumpenda wakati huo, ingawa penzi lake lilikuwa la upande mmoja. Hata hivyo, sasa alijuta sana kwa kupoteza muda wake kwa mwanamume kama huyo. Hakuweza kujua jinsi alivyopofushwa na kumwangukia Patrick. Matone makubwa ya machozi yalitiririka mashavuni mwake.
Forrest akamkabidhi kipande cha tishu. “Usilie. Patrick hastahili thamani ya machozi yako. Mungu anakuonyesha haya kwa sababu anataka kukuepusha na unafiki wa mwanamume huyu"

“Kaka.” Pamela alilia kwa uchungu. “Mjinga kiasi gani mimi! Ni kwa sababu ya Patrick na mwanamke wake ndiyo maana nimeishia kuwatia marafiki zangu matatizoni.”
“Usifikirie kupita kiasi. Ulikuwa unamsaidia rafiki yako tu. Hukutegemea kama haya yangetokea.” Forrest alimtuliza na kusema. "Unatakiwa tu uwe makini, Patrick ni mhuni sana. Ni wazi mwanawake mzuri kama wewe hamstahili kabisa."

“Nifanye nini basi?” Pamela alikasirika sana. “Nimefukuzwa kazi sababu ya Linda na kuwekwa kwenye blacklist. Hakuna kiwanda chochote kitakubali kuniajiri iwe ni Kenya au Tanzania.”
"Unaweza kurudi Dar es Salaam na kusimamia kampuni ya familia yetu au uende tena kusoma nje ya nchi." Forrest alimtazama machoni. “Unapokuwa mwanakemia bingwa unayejulikana sehemu nyingi duniani, Rodney hataweza kukufanya chochote wakati huo. Zaidi ya hayo, ataweza hata kukubembeleza urudi ufanye naye kazi.”
Pamela alipokuwa akipata picha ya mawazo hayo ya kaka yake, wimbi la hisia lilimtawala. Muda mfupi baadaye, hata hivyo, alivaa uso wa ujasiri. "Hapana. Ninawezaje kumuacha Lisa akiwa juu na kuti kavu? Zaidi ya hayo, Charity yuko jela. Dhamiri yangu itanisuta nikiondoka na kuwatelekeza.”
"Huna chochote unachoweza kuwasaidia hata ukibaki kuwa nao, kuna faida gani ya wewe kuendelea kuwafikiria?" Maneno ya Forrest yalimuacha hoi kabisa.
•••
Baada ya Pamela kumjua aliyevujisha siri, alimtaarifu Lisa. Lisa alipopokea ujumbe kutoka kwa Pamela, akaenda jengo la jirani kumtafuta Alvin. Alisukuma mlango na kuingia ndani ya chumba hicho, na kumkuta mtumishi akisafisha sakafu ya chumba kilichokuwa tupu. “Alvin yuko wapi?”
“Bwana Kimaro amehamia kwenye nyumba nyingine pembeni ya hii. Hujui hilo, Bibi Mdogo?” mtumishi aliuliza kwa mshangao.
Lisa alitetemeka, akihisi baridi. Hapo awali, Alvin alisisitiza sana kulala karibu naye. Wakati mwingine, hata aliingia chumbani kwake kupitia dirishani usiku. Kwanini alibadirika ghafla? Je! ni baada ya Maurine kufariki? Je, ni kwa sababu alikuwa na matatizo naye?
Lisa alihisi Alvin amemchukia ghafla. Alichangia kifo cha Maurine na hivyo kuharibu uhusiano wa Alvin na Rodney. Alitoa kicheko cha uchungu alipogundua kuwa alikuwa akijipinga mwenyewe. Alvin alipokuwa akimsumbua, alijikuta akiudhika na kumtaka apotee. Sasa kwa kuwa alikuwa ameondoka, alikuwa akiumia kutokuwepo kwake.
Lisa alienda kwenye jengo la jirani kwa huzuni. Alipofika tu getini, akasikia kitu kikivunjika ndani. Harakaharaka akaingia ndani na kumkuta Alvin akiwa amekaa kwenye kochi huku akionyesha huzuni. Hans na Chester walikuwa wakimkandamiza pande zote mbili. Chester alikuwa anajiandaa kumchoma sindano ya kichwa.
“Kuna nini… Ana tatizo gani?” Kwa kuona macho ya Alvin ambaye alikuwa akitokwa na jasho baridi na maumivu, Lisa alikuwa mwisho wa akili yake.
“Kichwa kinamuuma, kwa hiyo ninamdunga sindano ili kumpunguzia maumivu,” Chester alijibu bila kujali.
“Kwanini uko hapa? Ondoka." Alvin alimkazia macho.
Lisa alikunja ngumi kwa hofu na hasira. Hakutarajia kwamba Alvin sasa alilazimika kutegemea sindano ili kukabiliana na maumivu ya kichwa. Kwa maana hiyo hali yake ilikuwa mbaya zaidi? Hofu ilizidi kutanda ndani yake.
"Siondoki." Lisa akamsogelea. Alipoona kiganja chake kikitetemeka, alisita kwa muda kabla ya kukishika.
Kope za Alvin zilitetemeka. Akainamisha kichwa kumtazama. Mwanamke huyo ambaye alikuwa amevalia pajama nyeupe, alikuwa akichuchumaa kando yake. Muda ulikuwa umepita tangu awe mpole na mwenye upendo kwake namna ile. Akaurudisha mkono wake nyuma na kufumba macho.

Sura ya: 269

Dakika 20 baadaye, zoezi la sindano lilikamilika. Chester akamtahadharisha. "Jitahidi kupata muda wa kupumzika zaidi na pia usikasirike hovyohovyo. Nimewasiliana na Dokta Nyasia amesema atakuja wiki ijayo. Ni yeye pekee anayeweza kutibu ugonjwa wako.”
“Ok!” Alvin alijibu kwa unyonge.
Chester alimtupia jicho Lisa na kumuuliza Alvin, “Unahudhuria mazishi ya Maurine Jumapili hii?”
Alvin alishindwa cha kusema.
"Afadhali uhudhurie, au Rodney ataendelea kukulaumu." Kwa hayo, Chester alisimama na kujiandaa kuondoka. “Naondoka sasa hivi.”
"Subiri." Lisa alisimama. "Nina kitu cha kuwaonyesha nyie."
Akabofya rekodi ya simu ya Linda na kuwasikilizisha. "Hii ilitokea wakati Pamela alipoenda hospitalini huko Dar es Salaam kupata ripoti ya uchunguzi wa DNA ya Maurine na Jones. Mwanamke anayeitwa Linda alikutana na Pamela akiwa idara ya uchunguzi wa vinasaba. Linda alisikia mazungumzo yetu wakati Pamela aliponipigia kunipa matokeo, kisha akampigia Lina. Inawezekana kuwa Lina alipofahamu ishu hiyo, haraka akamrudisha Maurine Langa halisi na yeye akatoweka—'”
“Unamaanisha nini?” Chester alikatiza sentensi yake kwa sura ya huzuni.
“Lina ndiye aliyejifanya Maurine Langa, na kuna mtu aliyemtengeneza kwa makusudi. Inawezekana alitoroka baada ya kupokea simu ya Linda, akamrejesha Maurine halisi. Alishuku kuwa nilitumia nywele zake kufanya kipimo cha DNA na Jones. Alijua kuwa tayari nimeanza kushuku kuwa yeye sio Maurine wa kweli, kwa hivyo Alvin alipoenda kumshika, tayari alikuwa ametoka kwa ujanja na kumrudisha Maurine halisi. Ikiwa huniamini, unaweza kusikiliza hii simu kutoka kwa Linda…”
“Sikukuambia sitaki kusikia tena jambo hili?” Alvin akauachia mkono wake, huku macho yake yaliyokuwa na huzuni yakionyesha ukali kwa namna fulani.
Lisa alitamani Alvin amwelewe, lakini alishindwa amwelewesheje. “Lakini inatia shaka. Hebu nyie angalieni—”
“Inatosha. Usiongelee tena kuhusu hilo.” Chester alikatiza hotuba yake kwa mshtuko. “Wewe ndiye uliyemtaka Alvin achunguze hivyo akamfungia Maurine. Kwa sababu hiyo, Maurine alipoteza maisha.”
Chester alikuwa na fikra nzuri kwa Lisa kabla ya hii. Hata hivyo, kwa vile alikuwa amechangia kifo cha Maurine, Alvin, Chester, na Rodney sasa walikuwa na maelewano mabaya kati yao. Hii ilikuwa imemweka Chester katika hali mbaya.
"Mkipuuza mambo haya ya kutiliwa shaka, muuaji aliye nyuma ya pazia atapata upenyo wa kuponyoka. Charity pia ni binadamu. Ikiwa kweli alifanyiwa njama na mtu, maisha yake yataharibiwa vile vile. Baada ya yote, yeye ni ex wako, Chester…”
“Ninachojutia na kuchukizwa zaidi ni kuwa pamoja na mwanamke huyo asiyefaa,” Chester alisema kwa uwazi, “Amekuwa hafai tangu nilipokutana naye.”
Lisa alihisi kana kwamba ametumbukizwa kwenye dimbwi la maji baridi. Kwanini watu hawa walikuwa wakaidi sana?
“Ulikuja kunitafuta kwa sababu tu ya jambo hili, sivyo?” Alvin alimtazama kwa hasira.
"Alvin, nakuomba..." Lisa alimtazama kwa kumsihi. “Kuchunguza rekodi ya simu ni jambo dogo tu..."
“Toka nje.” Alvin alielekeza nje. "Sina muda wa kupoteza na upuuzi wako." Alvin alikasirishwa na maneno yake alipomuelekeza nje. Kichwa chake kilianza kumuuma tena.
“Lisa, wewe ni mke wake. Kuwa mstaarabu kwa sasa! Usimkasirishe kwa ajili ya watu hao wasio na maana.” Chester alikasirika. "Hans, mwondoe."
“Samahani, Bibi Mdogo.” Hans akamkokota kuelekea mlangoni.
Wakati Lisa alitaka kurudi tena ndani ya jengo hilo, tayari Hans alikuwa ameshafunga lango. Hakuweza hata kumuona Alvin sasa. Ni lini Alvin na uhusiano wake walifikia hatua hii?
Sebuleni, Chester alimkumbusha Alvin, “Afadhali usikutane na Lisa kwa muda kuanzia sasa kwa faida yako, mpaka Dokta Nyasia atakapokuja. Siku zote nyie wawili mnashindwa kuelewana mkionana macho kwa macho na hatimaye mnaishia kugombana. Hali yako inazidi kuwa mbaya kila unapokutana naye.”
“Mm. Alvin akalipapasa paji la uso wake. Pengine ndiye angehisi kuumia zaidi ikiwa asingemwona. Baada ya yote, ni Lisa ndiye alitaka kumuona kwanza.
•••
Jumapili. Mbele ya chumba cha mazishi.

Wakiwa wamevalia suti nyeusi, Alvin na Chester walitoka kwenye gari na kuingia kwenye chumba cha maombolezo. Hawakugundua kuwa kuna mtu alikuwa akiwatazama kwa sura ya ushindi ndani ya gari jeusi lililokuwa mbali kidogo. Alikuwa Lina Jones, ambaye aliweza kukimbia.
‘Hehe. Kwa bahati nzuri, nilimrudisha Maurine kwa siri mapema. Nyinyi watu hamkuweza kamwe kufikiria kwamba nimekuwa nikimwiga Maurine Langa, sivyo?' Lina alijiwazia kwa furaha. Alitabasamu kutoka sikio hadi sikio. 'Alvin, Lisa, fikirieni juu ya madhara yote ambayo nyie mmenisababishia. ‘Season two’ bado itaendelea hadi nihakikishe nawapeleka kuzimu!'
“Umefanya kazi nzuri,” mwanamume aliyeketi kwenye kiti cha abiria alisema bila huruma, “Maurine amekufa, lakini Charity yuko jela. Zaidi ya hayo, Alvin, Lisa, na Rodney wako katika mzozo. Kila kitu kimekwenda vizuri zaidi kuliko vile nilivyofikiria."
Lina akajigusa usoni. “Baada ya kusema hivyo, uso huu hauwezi kutumika kwa sasa…”
“Nenda nje ya nchi ukampumzike kwa sasa. Bado utakuwa na kazi fulani.” Mwanaume huyo alipiga vidole vyake na kumtaka dereva awashe gari.
Alvin alipofika mlangoni ghafla aligeuka nyuma na kuliona lile gari jeusi likiondoka.
"Nini tatizo?" Chester aliuliza.
Alvin alikunja uso. "Ilionekana kama kuna mtu alikuwa akitutazama sasa hivi."
"Kipi cha ajabu, si kawaida kwa watu kukuangalia?"
"... Twende." Alvin akageuka.
Alipoingia tu ndani ya chumba kile, alikutana na Rodney ambaye alikuwa akitoa heshima zake. Rodney alitazama kando baada ya kumpiga Alvin jicho kali la kuchoma.
Chester alienda mbele kutoa heshima zake, huku Alvin akienda mbele na kuomboleza kifo cha Maurine kimya kimya.
Bi. Langa alisema kwa uwazi, “Bwana Kimaro, fanya haraka na uondoke mara baada ya kutoa heshima kwa Maurine. Kwa kuzingatia hali halisi, hapa si mahali unapopaswa kuwepo.”
Alex Langa Njau, baba mzazi wa Maurine, alipandwa na hasira pia. Lakini alipotaka kuongea tu, aliona sura ya mwanamke akiingia ndani. Alex akaganda, akabaki kutetemeka. Alitamani kukimbia lakini alihisi kama miguu yake imeota mizizi pale alipokanyaga. Haja kubwa na ndogo vyote viligonga hodi kwa wakati mmoja. Macho yake yalimtoka hadi mwisho kama yanayotaka kuchomoka kwenye soketi zake…
“Kuna nini? Mbona ume...” Bi. Langa alipogeuka na kutazama upande ule, alishtuka sana hadi akaanguka chali, akatua chini na kuzimia papo hapo.
Rodney, Chester, na Alvin walipigwa na butwaa kabisa. Wakageuza vichwa vyao na kutazama upande ule kwa wakati mmoja. Kila mmoja alichukua njia yake na kukimbia baada ya kumwona mwanamke aliyekuwa nyuma yao.
Walimwona mwanadada aliyevalia gauni jeusi lenye umbo dogo lililoangazia mwili wake mdogo. Nywele zake zilikuwa zimefungwa kwa upole, huku uso wake mzuri na wenye kung'aa ukipakwa vumbi la unga fulani. Huku taa nyeupe zikimulika usoni mwake safi, alionekana kustaajabisha kama mzimu.
Sigara aliyokuwa ameishika Rodney ilidondoka chini. Chester alipepesa macho yake pande zote kwa mshangao.
Alvin ambaye alikimbia na kusimama kwenye kona ya chumba, alijikaza na kumtazama yule mwanamke aliyemfahamu vyema na kumsogelea taratibu.
“Sa-Sarah… Sarah ni wewee…” Maneno hayo hatimaye yalimtoka kwa shida bila kujifahamu. “Sa-Sarah, wewe ni mzimu?”
“Umetumwa leo kuja kumchukua Maurine?” Rodney aligugumia kwa macho yasiyoamini.
Sarah alitoa tabasamu hafifu huku akimwangalia. "Rodney, bado una utani wako kama zamani?"
Chester hakuweza kujizuia kuuliza kwa fadhaa, “Sarah, si tayari umekufa? Mbona…”
“Samahani, niliwahadaa. Kwa kweli, bado niko hai, lakini…sikuweza kurudi kwa sababu ambazo siwezi kuzisema kwa sasa.” Mwonekano wa kukata tamaa na kutojiweza kihisia ulivuka uso wake mzuri.
“Ni nini kilikuzuia kurudi?” Rodney aliuliza kwa wasiwasi, “Unajua kwamba kila mtu anajua umekufa? Kwa miaka hii, tulivunjika moyo kabisa, hasa Alvin. Karibu avunjike…”
Alvin aliendelea kukaa kimya kama bubu huku akipigwa butwaa.
Sarah alimtupia jicho huku machozi yakimtoka. "Samahani, nilikuwa na sababu zangu za kutorudi."
"Ni kwanini ulilazimika kudanganya kifo chako huko nje ya nchi kwa miaka yote hii na usitake kutujulisha?" Rodney aliuliza kwa hasira.

Sura ya: 270

Sarah alikunja midomo yake kwa uchungu bila kutamka neno lolote.
“Ni sawa, Rodney. Sarah lazima awe na sababu zake,” Chester aliingilia kati. Rodney alimtazama Sarah kwa huzuni na hatimaye akahema.
“Mbona umerudi ghafla?” Alvin aliyekuwa kimya ghafla aliongea.
Moyo wa Sarah uliumia macho yake yalipotua kwenye uso alioufahamu mzuri. Aligeuza macho yake polepole kwenye picha ya Maurine nyuma yake. “Ni kwa sababu sikutarajia kifo cha Maurine. Kwa kuzingatia kwamba yeye ni binamu yangu mpendwa, bado ninapaswa kutoa heshima zangu za mwisho kwake.” Kila mtu alinyamaza.
Alex Langa alitembea ghafla kuelekea kwa Sarah. Akamkumbatia na kububujikwa na machozi. “Sarah mbona umerudi sasa hivi? Kifo cha Maurine kilikuwa cha kuhuzunisha na kisichokuwa cha haki.”
"Mjomba, Maurine alikufa vipi?" Sarah aliuliza huku akibubujikwa na machozi.
Hapo hapo Alex alimkazia macho Alvin. "Ilikuwa haswa ni sababu ya mke wake akishirikiana na Charity."
Sura ya Sarah ikawa ngumu kidogo, na uso wake ukabadilika polepole. Alipepesa macho na kuelekeza kwa Alvin. “Alvinic…”
Alvin alikwepa macho yake. “Ni Charity…”
“Alvin, acha kuwa upande wa Lisa,” Rodney alisema kwa hasira, “nimetamani sana kusema kwamba Lisa hastahili kuwa nawe kwa vile amejaa nia mbaya. Sasa kwa vile Sarah amerudi, unaweza kuachana na Lisa na kurudi kwa Sarah?”
Alvin akakunja uso wake. Alipokaribia kujibu, Sarah alisema kwa haraka, “Rodney, acha kuzungumza upuuzi. Alvinic tayari ana mke. Unawezaje kumshawishi aachane naye? Zaidi ya hayo, siwezi kuwa na Alvinic tena…”
“Kwanini? Daima hajawahi kukusahau. Au nii kwa sababu hupendi—”
“Inatosha,” Alvin alikatiza sentensi yake kwa sura ya kufoka, “Rodney, ninafurahi kwamba Sarah amerudi, lakini tayari nina mke”
“Acheni ubishi. Kurudi kwa Sarah ni tukio la furaha. Tunapaswa kusherehekea usiku wa leo,” Chester alisema.
Sarah aliinua kichwa na kusema. "Asante. Mnaweza kuondoka kwanza. Ninataka nipate muda wa utulivu pamoja na mjomba na shangazi yangu.” Wanaume watatu walitoka nje ya chumba.
Rodney alihisi kuongezeka kwa furaha kutoka ndani ya moyo wake. Ni Alvin na Chester pekee ndio walikuwa wamekunja uso kwa undani. Haikuwa wazi ni nini kilikuwa akilini mwao.
"Sikutarajia kamwe kuwa Sarah angekuwa bado yuko hai."
Baada ya muda, Chester akahema. "Kwa bahati mbaya, hakurudi kwa wakati. Inawezekana akamkosa Alvin."
“Shukrani kwa mtu huyu mwenye mawazo kigeugeu. Ikiwa ungesubiri nusu mwaka zaidi, ungekutana na Sarah tena.” Rodney alifoka.
Alvin aliwasha sigara yake huku akimpuuza Rodney.
•••
Saa mbili na nusu usiku, Sarah alifika kwa kuchelewa kwenye chumba cha faragha cha hoteli kilichoandaliwa kwa ajili ya mapokezi yake na kina Rodney. “Samahani kwa kuchelewa. Baada ya Maurine kuzikwa, mjomba na shangazi yangu walilia sana, hivyo ilibidi nikae nao muda mrefu nikiwaliwadha.”
'Ni sawa. Tunaelewa." Chester aliinua mkono wake. "Keti chini."
Wanaume watatu walikuwa wameketi mbalimbali na kila mmoja kwenye kochi refu. Chester alikaa katikati, ambapo Alvin na Rodney walikaa pande tofauti. Baada ya kusitasita kwa muda, Sarah alikaa karibu na Rodney.
"Sarah, kwa kuwa sisi watatu tuko hapa, unaweza kutuambia ilikuweje hadi leo tukuone ukiwa hai wakati tunajua ulikuwa umekufa?" Chester alimkazia macho. “Sisi ni marafiki zako. Tuliumia sana moyoni tulipojua kuwa umekufa. Je, huoni kwamba unapaswa kutupa maelezo?”
"Sarah aliinamisha macho yake. Akiwa katika hali ya hofu, alichukua glasi ya mvinyo mwekundu uliokuwa juu ya meza. Kisha, akalazimisha tabasamu lililojaa uchungu na woga. "Pengine mnafahamu kwamba tulitekwa nyara na Al-Shabaab nilipokuwa na rafiki yangu katika utafiti huko kwenye msitu wa Garisa baada ya kumaliza masomo yangu ya chuo kikuu nje ya nchi."
“Ndio. Alvin alitumia nusu mwaka kukutafuta huko. Baadaye, maiti iliyooza ilipatikana karibu na hifadhi ya msitu huo. Ilikuwa ni mwanamke, na sote tulidhani ni wewe,” Rodney alisema kwa huzuni.
Sarah alichezea glasi ya divai mkononi mwake. “Hapana, haikuwa mimi!”

Alvin, Chester, na Rodney walishangaa sana. Mkono wa Alvin ulitetemeka huku akishika glasi ya mvinyo. Akainua macho na kumtazama Sarah kwa mshtuko.
"Sitaeleza ilivyokuwa. Nimevumilia mateso mengi sana. Ilikuwa inauma sana kuishi kwenye kambi ya magaidi huko Somalia baada ya kutekwa.” Sarah alikunja midomo yake na kuinywa mvinyo. “Niliteswa tena na tena. Baada ya muda, nilifanikiwa kutoroka na kuzamia meli hadi ulaya. Nilifanikiwa kwenda Ujerumani ambako nilipata kazi ya kulea wazee kwenye kituo cha kukulelea wazee. Sikuwa na visa, kwa hivyo sikuweza kurudi. Nilijaribu kuwasiliana na familia ya Njau, lakini hawakunijali kabisa. Waliniambia moja kwa moja kwamba huku kila mtu anajua kuwa mimi ni marehemu hivyo nisijisumbue hata kurudi."
“Walienda mbali sana. Hawa watu ni binadamu kweli?” Rodney alitupa glasi ya mvinyo na kusimama kwa hasira.
"Nilifikiria kuhusu kuwasiliana na Alvinic, lakini ... sikustahili hata kuwa naye." Sarah akapepesa macho, machozi yakimtoka. “Yeye ni mwanamume mwenye mustakabali mzuri mbele yake, ilhali mimi tayari nilikuwa na mwili mchafu zaidi. Wale magaidi wa Al-Shabaab walikuwa wakitubaka kwa zamu kila siku. Hata usichana wangu niliokuwa nimemtunzia Alvinic ulitolewa kinyama na wale magaidi wasio na huruma. Nilitumaini angeweza kupata mwanamke bora baada ya mimi kuondoka kwenye maisha yake.”
Alvin alifumba macho. Moyo wake ulikuwa ukiwaka kwa maumivu. Hakuwazia mateso ambayo Sara alikuwa amepitia huku akihisi kwamba amekufa. Ikiwa angewahi kurudi kabla hajakutana na Lisa, angemuoa Sarah bila kusita. Sasa kwa kuwa Lisa alikuwa na ujauzito wa watoto wake, hisia zake kwake zilikuwa zimebadilika.
“Sawa, usilie.” Chester akamkabidhi Sarah kipande cha tishu.
Rodney alihisi kana kwamba kisu kilikuwa kikimpasua moyoni. “Usijali Sarah. Haijalishi umepitia unyanyasaji kiasi gani, hatutawahi kukudharau. Wewe ndiye mwanamke safi kila wakati mioyoni mwetu."
“Asante.” Sarah alitabasamu huku machozi yakimtoka. "Kwa kweli, kuna sababu nyingine iliyonifanya nirudi tena kwa wakati huu." Pamoja na hayo, aliwakabidhi kadi tatu za biashara.
Alvin alipigwa na butwaa baada ya kuona kadi ya biashara mkononi mwake. "Wewe ndiye mwanasaikolojia maarufu kimataifa, Dokta Nyasia?"
“Ni jambo la kustaajabisha kusema kwamba ninajulikana kimataifa. Baada ya kusema hivyo, mimi nina ujuzi kabisa katika kutibu aina hizi za kesi. Kituo cha wazee huko Munich Ujerumani ambacho nilikifanyia kazi kwa muda mrefu kilinigharamia masomo yangu ya ‘psychiatrist’ hadi ngazi ya PhD. Nilisomea Saikolojia ili kuwasaidia zaidi wazee wenye matatizo hayo.” Tabasamu tamu lilienea kwenye uso wa Sarah. Alinyoosha mkono wake kwake. "Bwana Kimaro, nimekuja kukusaidia."
Kwa hisia tofauti, Alvin alipeana naye mikono.
Rodney alisema, “Sarah, wewe ni mzuri. Ni kama Mungu alikuwa anakuandaa ili uje kumsaidia Alvin.”
“Sikutarajia angerudia tena hali yake,” Sarah alisema huku akitabasamu.
'Yote ni kwa sababu--"
"Kunywa pombe yako." Alvin alitumia glasi ya mvinyo kusimamisha mdomo wa Rodney.
Sarah alicheka kuona hali ile. “By the way, nataka kumtembelea Charity…”
“Kwanini unataka kumtembelea? Alikunyanyasa sana wakati huo.” Chester alikunja uso.
“Hasa. Hata alikuzuia usirudi. Utasema yeye ni ndugu yako kweli?”
"Pamoja na hayo, yeye ni dada yangu wa kambo. Zaidi ya hayo, sijui hukumu yake itakuwa ya muda gani wakati huu. Labda sitamwona tena. Natumai atajifunza kutokana na makosa yake.” Sarah alitoa kicheko cha uchungu.
•••
Siku inayofuata. Katika kituo cha Polisi, Charity alikaa kimya kwenye kona. Kulikuwa na michubuko mwili mzima na usoni. Hakuna sehemu hata moja ya mwili wake iliyoachwa bila kujeruhiwa.
Kundi la wahalifu wakatili walikuwa wakimtazama. Kama asingekuwa na ujuzi wa msingi wa karate, angekuwa tayari ameteswa hadi kufa.
"Charity, kuna mtu alikuja kukutembelea." Kelele ilisikika kutoka nje.
Charity alijitahidi kuinuka na kusimama. Hakuna mtu aliyekuja kumtembelea katika kipindi chote alichoswekwa ndani, hata wazazi wake. Ni wazi, mtu fulani alikuwa amezuia asitembelewe na watu. Kwa wakati huo ni nani angeweza kumtembelea?.

TUKUTANE KURASA 271-275

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI...........LISA
KURASA......271-275
Sura ya: 271

Charity akatoka. Alipomtazama vizuri yule mwanamke, macho yalimtoka ghafla. "Sarah, bado uko hai?"
“Naam, niko hai. Nimerudi, Charity.” Macho ya Sarah yalimtiririka. “Hata hivyo, sikutarajia kwamba ungeishia hivi. Tsk, una harufu mbaya."
“Kwanini umerudi?” Charity alimtazama kwa hasira. Kila mara mwanamke huyu alipokuwa karibu, watu wa karibu na Charity walikuwa wakiishia kuumizwa tu. Charity alikuwa na hisia kwamba Mungu alikuwa ameondoa maisha ya Sara. Hakutarajia kwamba Sara alikuwa amerudi.
“Niko hapa ili kurudisha kila kitu changu kilichopotea,” Sarah alikunja midomo yake na kusema kwa furaha, “Kwa kuzingatia kwamba mama yako aliharibu familia yangu, unafikiri nifanye nini ili kumlipisha kisasi?”
“Unapanga kufanya nini?” Charity akamtazama. “Sarah, mama yangu hajawahi kukutesa. Alikutendea mema kuliko mimi.”
“Hiyo ni kwa sababu alikuwa anajaribu kumbembeleza baba yangu. Vinginevyo, ungewezaje kuchukua kampuni ya New Era Advertisings? Wewe na mama yako mmekuwa mkipanga na kula njama. Haha, kwa kuwa sasa baba amepoteza fahamu hospitalini baada ya kupata mshtuko wa moyo, Jennifer hana mtu wa kumtegemea. Nitamlipa pole pole kwa mateso yote ambayo mama yangu amevumilia. Nitayafanya maisha yake kuwa mabaya zaidi ya kuzimu.”
“Baba hakumtaliki mama yako. Alikuwa na tabia mbaya ya kuwatongoza wanaume wengine huko nje…”
“Nyamaza!” Sarah alikatiza sentensi yake ghafula kwa maneno makali, “Unawezaje kuthubutu kunijibu katika hali kama hii?”
"Sarah, ikiwa chochote kitatokea kwa mama yangu, utajuta kwanini uliamua kufufuka." Kwa macho mekundu ya damu, Charity alimtazama huku akiwa ameshika vyuma vya dirisha vilivyokuwa mbele yake.
“Haha, usijali. Nimefufuka ili nije kukushughulikia.” Akiwa amefunika mdomo wake, Sarah alicheka kwa dharau. “Kumbe nimesikia unaelewana na mke wa Alvin.” Wimbi la kufadhaika lilimkumba Charity. “Sasa nimerudi, ni wakati wake wa kupotea,” Sarah alisema kwa msisitizo na kukunja midomo yake.
"Endelea kuota. Alvin anampenda Lisa,” Charity alisema bila huruma, “Tayari wameoana. Huwezi kufananishwa naye.”
“Kweli? Lakini Alvin amekuwa akitumia muda na mimi kila siku. Hataki hata kurudi kwa anayeitwa mke wake. Unapaswa kujua kuwa uhusiano wangu na Alvin hauna mpinzani.”
Kwa hayo Sarah akageuka taratibu. “Kwaheri. Huenda hatutaweza kukutana tena katika siku zijazo kwa sababu utafia jela." Macho ya Charity yalifichua dokezo la kuchanganyikiwa.
Alipoona hali ya kutoamini usoni mwa Charity, Sarah alitabasamu na kusema, “Pengine hujui kwamba wakili anayewakilisha familia ya Langa wakati huu ni Bw. Shea. Chester Choka ndiye aliyechonga naye na kumwomba ahakikishe unafungwa milele.”
"Chester Choka?" Aliposikia jina hilo, Charity alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa unawaka moto. Hakukuwa na mtu katili zaidi kuliko mpenzi wake huyo wa kwanza.
“Kwa kuzingatia kwamba utafia jela, nitakuambia jambo fulani kwa hisani. Hapo awali, Chester alikubali kuwa na uhusiano na wewe sio kwa sababu alikuwa akikupenda. Alikuwa akinipenda mimi, na ilimbidi kuwa na wewe kwa sababu alitaka kuniumiza mimi kwa kumkatalia. Kwa hivyo ulipompanulia tu mapaja yako ukiwa na miaka 17, akaishia kukutolea usichana wako na kukuacha.”
Sarah aligundua kuwa macho meusi ya Charity yalikuwa yamelegea ghafla. Huku akijisikia fahari, aliondoa miguu yake iliyovalia viatu vya visigino virefu.
Mwili wa Charity ukateleza chini taratibu. Kisha akachuchumaa na kukaa chini. Ilimchukua muda mrefu kujinyanyua pale. Alichukia jinsi alivyokuwa mjinga wakati huo. Kwanini alimwangukia mtu ambaye alionekana kuwa mpole kwa nje lakini kwa kweli alikuwa mkatili sana?
Njia pekee ambayo angeweza kujilinda ilikuwa ni kuyapotezea maneno ya Sarah na kuvumilia. Matone makubwa ya machozi yalianguka sakafuni.
Chester Choka, Sarah Langa, Rodney Shangwe, Alvin Kimaro: Charity aliapa kwamba asingewasamehe hadi siku atakapokufa.
•••
Akiwa katika makazi ya familia ya Kimaro, Lisa alijihisi kama ndege wa kufugwa. Angeweza tu kuzunguka ndani ya uzio na hakuwa na mahali pengine pa kwenda. Ilikuwa imepita wiki moja tangu alipomuona mara ya mwisho Alvin.

Alijihesabu kuwa mwanaume huyo tayari amesahau kuhusu ujauzito wake. Alikuwa ameshuka moyo kabisa na kupoteza hata hamu ya kula. Jambo hili liliwatia wasiwasi sana Mzee Kimaro na Bibi Kimaro.
"Mpigie Alvin," Bibi Kimaro alimwagiza mfanyakazi wa nyumba wakati wa chakula cha jioni. “Hawezi kumpuuza mke wake na watoto hata awe na shughuli nyingi kiasi gani. Nilitaka walale vyumba tofauti lakini sikumuamuru amtupe mke wake kando.”
Mlinzi wa nyumba akapiga simu mara moja. "Bwana Kimaro alisema anafanya kazi za ziada ofisini kwake."
“Kwa hiyo hana hata muda wa kupumzika! Anafikiria nini?!" Mzee Kimaro alipiga ngumi kwenye meza.
"Tusimlaumu sana labda kweli amezidiwa na kazi, ukizingatia kwa sasa anashughulika pia na kampuni ya Lisa." Bibi Kimaro akamtupia jicho mzee huyo na kuonesha ishara kuelekea upande wa Lisa kwa kutumia kidevu chake.
Mzee Kimaro alikuwa na wasiwasi. Alvin alimfanya Lisa kuwa mke wake lakini sasa alikuwa amemtelekeza. Je, inawezekana kwamba alikuwa na mabadiliko yoyote kwenye moyo wake? Mzee huyo hakumpenda Lisa sana lakini hakuweza kujizuia kumuonea huruma mwanadada huyo ambaye sasa alionekana kuwa dhaifu na amechoka.
“Babu, Bibi, hakuna haja ya kumpigia simu. Tuligombana sisi wawili, kwa hiyo huenda hataki kuniona kwa sasa.” Lisa aliinua kichwa chake kwa utulivu. "Nimechoka sana kukaa ndani ya nyumba kila siku. Naweza kwenda nje kesho kumuona rafiki yangu?”
“Mh, sawa basi. Lakini unapaswa kuwa waangalifu. Aunty Yasmine atakwenda nawe,” Bibi Kimaro alisema bila kusita.
Hata hivyo, siku iliyofuata Lisa alipopanga kuondoka nyumbani, Shani alijaribu kumzuia. "Bibi mdogo, samahani lakini Bwana Kimaro ametoa amri kwamba hairuhusiwi kuondoka kwenye nyumba hii."
“Anapanga kunifungia milele?” Lisa alimtazama mlinzi wake kwa masikitiko. Mwanamume huyo angewezaje kumtendea unyama hivyo?
Maneno ya kinyonge yalienea kwenye uso wa Shani. “Najua unataka kwenda kortini kwa ajili ya kesi ya Charity Njau lakini hili litamkasirisha Bwana Kimaro…”
“Kwa hiyo siruhusiwi hata kumuona rafiki yangu kwa mara ya mwisho?” Lisa alipiga hatua chache kuelekea kwa Shani. "Mwambie kwamba ikiwa sitaondoka kwenye nyumba hii leo, nita ...." Kisha, akaonyesha ishara mbaya kwenye tumbo lake.
Shani alishtuka. "Bibi mdogo, tafadhali tulia."
“Siwezi kutulia. Mimi ni mwanamke mjamzito lakini ninaishi kama mfungwa. Nini kinampa haki ya kunifungia? Mimi ni binadamu! Ni afadhali nikate tamaa ya watoto ikiwa haya ndiyo maisha ninayopaswa kuvumilia milele.” Macho yake yalikuwa yakimtoka machozi, hata mikono yake ilikuwa inatetemeka muda huo.
Shani aliogopa sana kwamba Lisa alitishia kuwadhuru watoto, kwa hivyo alikubali upesi na kutabasamu kwa uchungu. “Hakika, tafadhali nenda. Nitampigia simu Bwana Kimaro baadaye.
Mara Lisa akapiga hatua kubwa kuelekea lango kuu. Alikuwa tayari anachelewa. Labda kupoteza sekunde nyingine kungemfanya akose kesi.

Sura ya: 272

Katika chumba cha kifahari kwenye hoteli ya nyota tano, Sarah alikuwa akisoma rekodi ya ugonjwa wa Alvin kwenye kochi. Alvin akaweka kikombe cha kahawa mbele yake.
Alikunywa haraka kabla ya kutabasamu. "Bado unakumbuka kuwa napenda Americo Coffee?”
"Ndiyo, sio wanawake wengi wanaopenda kahawa chungu." Alvin alikaa kwenye kochi lililo mkabala na Sarah. Ghafla alikumbushwa juu ya mwanamke nyumbani, Lisa, ambaye alipenda kahawa tamu. Kila mara alikunywa kahawa yake yenye sukari nyingi na cream.
Sarah aliona namna alivyokuwa amepotea kwenye mawazo. Mwanaume huyu alikuwa amekaa mbele yake lakini alikuwa amesafiri maili mia kadhaa kimawazo. Ni wazi kwamba alikuwa akimfikiria mwanamke mwingine. Asingefanya hivyo zamani. Moyo wake ukafadhaika, na kabla hajalifunga lile faili, alitabasamu. "Nina uhakika 80% kwamba ninaweza kutibu hali yako kabisa na kuzuia kujirudi tena kwa ugonjwa wako kwa siku zijazo."
Mwale wa mwanga ulionekana machoni mwa Alvin. Alipasua midomo yake kusema kitu wakati Shani alipompigia ghafla. "Bwana Kimaro, Bibi Mdogo ameondoka kuelekea mahakamani."
Uso wake ulianguka papo hapo. "Sikukuambia kwamba haruhusiwi kuondoka kwenye nyumba hiyo kwa sasa?"
"Samahani, lakini Bibi Mdogo alitishia maisha ya watoto ..." alielezea bila kusita.
"Vizuri sana." Kwa hasira, karibu aitupe simu yake. Mwanamke huyo alikuwa akitumia hata maisha yake na ya watoto kumtishia sasa. Hivi kweli aliwajali hata hao watoto kweli? Ina maana mapacha hao hawakuwa muhimu kwake kuliko Charity? Alihisi hasira na kukata tamaa kwa wakati mmoja.
Alvin akanyanyuka ghafla. “Tutaendelea siku nyingine. Ninahitaji kuwa mahali pengine sasa."
"Kweli, lakini ni bora kutoiahirisha au uwezekano wa kupona utakuwa mdogo." Sarah akaingiza simu yake kwenye mkoba wake. Wawili hao wakaelekea chini pamoja.
Melanie, ambaye alikuwa akitoka kwenye korido iliyokuwa karibu, aliwaona na harakaharaka akajongea kwenye kona ili kupiga picha.
"Melanie, kwanini umejificha hapa?" Jerome alimfuata na kuweka mkono juu ya kiuno chake.
"Tazama hii." Alimuonyesha picha. “Ni Sarah Njau! Hajafa!” Akafinya macho. "Huyu ndiye Sarah, tofauti na yule Maurine ambaye anafanana naye tu. Tsk, unafikiri wenzi hao walikuwa wakifanya nini pamoja kwenye chumba cha hoteli?” Melanie alifurahishwa na kitendo hicho. “Unadhani Lisa atazipokeaje picha hizi?”
Jerome alishtuka. “Nilisikia anakaa kwa Mzee Kimaro kutokana na ujauzito wake. Nina hakika kwamba atapoteza watoto wake ikiwa atagundua kuwa mume wake anachafuana na mpenzi wake wa zamani.”
“Uko sawa.” Alitabasamu kwa ndani. “Lisa alidhani alishinda kwa sababu aliolewa na Alvin, lakini inavyoonekana ataachwa hivi karibuni.”
•••
Mahakama ya Nairobi.
Kesi ilikuwa inaishilizia wakati Lisa na Pamela walipoingia eneo la tukio. Charity alikuwa amesimama kizimbani. Ilikuwa ni muda tangu walipokutana mara ya mwisho. Mwanamke huyo aliyekuwa mrembo na mzuri alikuwa akionekana dhaifu na amechoka, nywele zake zikiwa kavu na zilizotimkatimka.
“Sikufanya hivyo. sikuua mtu yeyote.” Alikanusha vikali licha ya ushahidi wote ulioelekezwa kwake. "Nimetengenezewa njama tu."
Bw. Shea alisema kwa uthabiti, “Si lazima ukubali lakini inasalia kuwa kweli kwamba uliwakodisha watu kumuua Maurine Langa katika moto wa kikatili. Kinachochukiza zaidi ni kwamba hata hujutii matendo yako!”
Jaji kiongozi alikunja uso kabla ya kutangaza hukumu ya mwisho, “Mshtakiwa Charity Njau amepatikana na hatia ya mauaji. Kutokana na ukaidi wake na kutoonyesha dalili za kujutia kitendo chake, mshtakiwa anahukumiwa kifungo cha maisha jela na kunyimwa haki za rufaa mara moja.”
"Hapana, binti yangu hakuua mtu yeyote!" Jennifer alisimama kwa nguvu, uso wake ukiwa na machozi. Askari wa usalama walijaribu kumzuia kuondoka eneo lililotengwa.
Macho ya Charity yalimtoka machozi. Ingawa alitazamia hili kutokea, hakuweza kujizuia kuhisi kukata tamaa wakati hatimaye ulipofika.
“Charity…” Lisa alimtazama kwa huzuni. “Samahani…” Lisa alihisi hatia. Charity asingeingia kwenye matatizo hayo kama Lisa asingefanya kipimo cha DNA.

"Sikutarajia nyinyi wawili mngekuja." Midomo ya Charity ilitetemeka. Ilikuwa ni ukweli kwamba walikuwa hawajafahamiana kwa muda mrefu.
"Tunaamini kuwa huna hatia." Mashavu ya Pamela tayari yalikuwa yamelowa kwa machozi. “Bila shaka tutakata rufaa dhidi ya kesi hiyo na kuwatunza wazazi wako.”
"Asanteni. Lakini ikiwezekana, tafadhali wasaidieni wazazi wangu waondoke Nairobi haraka iwezekanavyo...” Kabla hajamaliza maneno yake, maafisa wa kutekeleza sheria walikuja kumburuta. Alitazama nyuma kwa mara ya mwisho na kusema. “Jihadhari na Sarah Njau…”
Kwa sababu ya umbali huo na sauti yake iliyochoka, Lisa aliona tu midomo yake ikicheza lakini hakuweza kusikia alichosema. “Anasema nini? Anasema tujihadhari na nini?"
“Hata mimi sijasikia vizuri.” Pamela alijaribu kufikiria jinsi Charity alivyotamka. “Jihadharini na nani sijui…”
Lisa alichanganyikiwa. Hakuweza kutafakari sana kwa sababu Jennifer Musyoka nusura azimie kwa kulia sana. Wawili hao walimshika mkono haraka mwanamke huyo aliyekuwa amehuzunika. “Anti Jennifer, usijali. Bado kuna matumaini maadamu Charity yuko hai. Tutamtoa hata ikichukua mwaka, miaka miwili au mitatu.”
“Asanteni.” Jennifer alithamini msaada huo.
"Lakini wewe na mumeo mnapaswa kuondoka Nairobi hivi karibuni," Lisa alisema kwa sauti ya wasiwasi. “Charity alipendekeza kwamba ninyi wawili muondoke hapa mara moja. Nadhani amegundua kuwa kuna kitu kibaya, kwa hivyo anadhani ninyi wawili mnaweza kuwa hatarini.”
Sura ya kuchanganyikiwa iliosha uso wa Jennifer. "Mimi na Boris hatukumchukiza mtu yeyote."
"Lakini nadhani Charity yuko makini kuhusu hili, hata mimi nahisi wasiwasi sana," Pamela alisema, "Naweza kuwapeleka Dar es Salaam. Familia yangu itawapokea huko. Ninaweza kumwomba kaka yangu mkubwa awatunze.”
“Asante, kwa kweli.” Sauti ya Jennifer ilidhihirisha shukrani ya kweli.
“Unapaswa kuondoka sasa hivi kwenda kufungasha. Charity atakuwa na utulivu zaidi ikiwa mtaondoka hivi karibuni," Lisa alihimiza.
Baada ya Jennifer kuondoka, Pamela alishusha pumzi ndefu. "Familia ya Njau ilikuwa moja ya familia tajiri hapa Nairobi hapo awali. Sikutarajia wangeangukia katika hali hii katika siku chache.”
“Hakika,” Lisa alijibu.
"Angalia matatizo uliyonayo kwa sasa. Nitaondokaje na kukuacha ukiwa hivi?" Pamela alisikitika.
"Unaondoka?" Lisa alishangaa.
"Ndio. Ninafuatiliwa na Rodney kwa sasa, kwa hivyo kaka yangu alipendekeza kwamba niondoke nchini kwa muda.” Alishusha macho yake chini kwa huzuni. "Siwezi kukusaidia wewe au Charity kwa kukaa hapa. Nataka kuwa na nguvu zaidi. Siku moja, ninataka kutengua uamuzi wa kesi yake.”
Lisa alishtuka. “Uko sahihi. Hatuna uwezo sana.”
Hakuwa na nguvu hata ya kuweza kuondoka kwenye nyumba ya Kimaro siku hiyo ikiwa asingetumia maisha ya watoto kama tishio. Alitaka kuwa na nguvu zaidi, lakini kwa wakati huo, hakuwa na uhuru wa kibinafsi.
"Pamela, unapaswa kwenda." Alimtazama sana rafiki yake. “Nimeelewa matumaini yako. Nitajitahidi kuwa na nguvu pia baada ya kujifungua watoto. Sisi bado ni marafiki hata kama tuko katika nchi tofauti. Unapanga kuondoka lini?"
“Bado sijafikiria juu yake. Labda mwezi ujao.”
"Sawa, nijulishe mapema na nitakufanyia party ya kukuaga." Lisa alimkumbatia rafiki yake kwa nguvu. Pamela ndiye rafiki pekee ambaye angeweza kumtegemea katika jiji hilo lakini naye alikuwa anaondoka tena. Angekuwa peke yake tena kwa muda usiojulikana. Pamela alianza kulia kwa mara nyingine.
Wakati huo huo, gari jeusi la kifahari likasimama pembeni yao na Alvin akatoka ndani yake kwa hatua kubwa. Alionekana kuogofya, na kwa ujasiri, Pamela alimkinga Lisa nyuma yake.
“Sogea!” Macho yake yalidhihirisha dhamira ya hatari. "Pamela Masanja, nasema pisha njia! Nimekuwa nikikuvumilia kwa muda mrefu sasa."
Sura ya: 273

“Alvin, nimekuwa nikikuvumilia kwa muda mrefu pia. Lisa ana mimba ya watoto wako. Kwanini bado una mnyanyasa? Kwanini umtelekeze tu kwa bibi yako kisha upotee? Anahitaji mtu ambaye anaweza kumjali na kumtegemea,” Pamela alifoka kwa hasira, “Lini utaacha kuwa na hali ya kubadilika-badilika na kukasirisha? Yeye pia ni mtu mwenye mipaka.”
"Nyamaza! Huna haki ya kuingilia mambo yetu.” Alvin alimsukuma na kumsukumia Lisa kwenye gari.
Lisa alifumba macho. Kusema kweli, alikasirishwa sana na jinsi Alvin alivyokuwa mkorofi kwa Pamela.
"Kuna nini hutaki hata kuhangaika kunitazama sasa?” Alvin alikibana kidevu chake. "Fungua macho yako."
Lisa alihisi uchovu umeenea mwilini mwake. Uso wake wa kifahari ulionekana mara tu alipofungua macho yake tena. Bado ulikuwa uso ule ule, lakini moyo wake ulimuuma kwa kutokujua. "Alvin, Pamela yuko sahihi. Lini utaacha kuwa na tabia mbaya na dharau? Unakuwa mtu asiyeeleweka muda wote. Unaweza kunipa nyota wakati uko katika hali nzuri lakini utanifungia kwenye friji wakati una hasira mbaya. Nimechoka kuishi hivi.”
“Unadhani mimi napenda kufanya hivyo? Kwanini hutaki kuwa mke mwema? Unajua kuwa namchukia Charity lakini ulinitishia watoto ili tu kukutana naye.” Macho yake yalikuwa yamejaa hasira. "Ina maana watoto wetu sio muhimu kwako kuliko Charity kwamba uko tayari kuwatumia ili kunitishia?"
Lisa akadhihaki. “Unadhani nilikuwa na chaguo jingine? Mimi pia ni binadamu lakini unanifungia kwenye banda kama ndege. Nimepoteza uhuru wangu wote. Nisingebeba watoto wako kama ningejua haya yangekuwa maisha yangu baada ya kunioa.” Mwili wake ulitetemeka.
Muda mrefu baadaye, macho yake ya chuki yalikata tamaa. "Lisa, hustahili kuwa mama." Alidhihaki.
Lisa alihisi kana kwamba kuna kitu kimeingia ndani yake na akamfokea kwa mbwembwe, “Nitaliki ikiwa hufikirii kuwa ninastahili kuwa mama! Nenda katafute mtu ambaye anaweza kufanana nawe!”
Alikunja ngumi kuwa mipira huku akihisi moyo wake ukizidiwa na mapigo. "Hans, mrudishe kwa bibi."
"Hapana, sitarudi kwenye nyumba hiyo."
“Huna chaguo,” alisema huku akimkazia macho.
Lisa alipasua midomo yake lakini hakuna neno lililotoka. Badala yake, machozi yalianza kutiririka mashavuni mwake huku akimpiga ngumi za mgongoni. “Alvin kwanini unanifanyia hivi? Niambie nilikosa nini! Nimepoteza kila kitu, uso wangu, uhuru wangu…”
Hata wale marafiki wawili ambao walimjali sana. Mmoja alifungwa na mwingine alikuwa anaondoka hivi karibuni. Mwanaume pekee aliyempenda alikuwa hamjali pia.
“Umerukwa na akili…” Alvin alifoka na muda huohuoi Lisa alianguka chini kwa mfadhaiko. Alimnyanyua mara moja lakini tayari alikuwa ameshazimia.
“Hospitali,” Alvin aliagiza kwa hasira. Hans akatekeleza haraka.
•••
Katika hospitali.
Baada ya uchunguzi mfululizo, daktari alisema bila kujali, "Bwana Kimaro, nilikuambia hapo awali kwamba ujauzito wa mke wako bado haujatulia kwa hivyo hupaswi kumfadhaisha."
“Ni nini hasa kilimtokea?” Alvin aliuliza kwa wasiwasi.
“Nadhani amekuwa akivumilia hasira na huzuni nyingi hivi karibuni, bila kusahau kwamba mabadiliko ya homoni katika mwili wake yanamfanya apate hisia tofauti. Unapaswa kuwa mwangalifu na kumjali zaidi ili awe katika hali nzuri kila wakati. Kama mume wake, unapaswa kujaribu kutomkasirisha mara kwa mara.” Daktari akashusha pumzi. “Nimeona wanawake wengi wajawazito wakianguka katika mfadhaiko. Wao ndio walio hatarini zaidi kihisia katika hatua hii. Tumia wakati mwingi pamoja naye.”
Akakunja uso. "Haitaji kampani yangu."
Daktari akatabasamu. “Bila shaka anafanya hivyo. Mimi mwenyewe ni mwanamke na nimejifungua pia. Licha ya kile anachosema, kila mwanamke bado anatamani sana urafiki wa mume wake wakati na baada ya ujauzito.”
Alvin alionekana kushtuka. Baada ya daktari kuondoka, Alvin aliburuta kiti karibu na kitanda, akihisi uchovu. Ni lini mara ya mwisho alimtazama Lisa kwa ukaribu hivyo? Kwa muda sasa, wangeishia kwenye mabishano kila mara walipokutana. Ghafla aligundua kuwa alikuwa amepungua uzito na alionekana dhaifu kuliko hapo awali. Alipaswa kuongeza uzito wakati wa ujauzito.

Baada ya kusitasita kwa muda mfupi, Shani, ambaye alikuwa amesimama karibu, hakuweza kupinga kusema, “Bwana Kimaro, kwa kweli, nadhani umekuwa mkali sana kwa Bibi Mdogo hivi karibuni—”
Alvin alimtupia jicho baridi kabla hajamaliza sentensi yake.
“Um… Ninaelewa sababu yako ya kutotaka Bibi Mdogo kukutana na marafiki zake ili kumzuia kuwaza kupita kiasi. Lakini amekuwa akichoshwa na upweke kukaa ndani muda wote. Hurudi nyumbani wala hauulizi habari zake. Anaonekana mwenye huzuni sana akisimama karibu na dirisha kila siku kutazama ulimwengu wa nje…”
Alvin alijisikia vibaya kusikia hivyo. Watu walidhani kuwa mke wake anatia huruma? "Sikujibu simu zake kwa sababu kila mara anataka kubishana nami kuhusu Charity."
“Lakini Bibi Mdogo hajui hilo. Anafikiria tu kwamba umemchoka,” Shani alinong'ona.
Alvin alikaa kwenye ukimya mzito baada ya kusikia hivyo. Dakika 20 hivi baadaye, Lisa alifungua macho yake taratibu. Mara tu alipogundua mahali alipokuwa, mikono yake ilirukia tumboni haraka. “Watoto wangu…”
“Usijali, watoto wako salama.” Alvin alisema kwa upole huku akimshika mikono.
Sura ya mshangao ilienea usoni mwa Lisa. Kwa sekunde moja, alifikiria kuwa bado anaota.
“Mbona unanitazama?” Alipiga kichwa chake kwa upole na kuweka mikono yake karibu na midomo yake. “Lisa, nakiri nilikuwa na makosa. Badala ya kukaa na wewe na kukubaliana na wewe ukiwa mjamzito, niliendelea kugombana na wewe. Sikukusudia lakini mambo mengi sana yametokea hivi karibuni. Nipe muda. Upo tayari tusafiri nje ya nchi hali yangu itakapoimarika? Hatujasafiri pamoja hapo awali.”
Baada ya kimya kifupi, hakuweza kujizuia kusema, “Utanijali tena kwa siku chache kabla ya kunibadilikia tena? Naona huo ndiyo utaratibu wako siku hizi.”
Alvin alitabasamu kwa uchungu. "Ni lazima tuingie katika hali hii kwa sababu ya Charity? Fikiria kuhusu watoto. Unataka wakue bila wazazi?"
Machozi yakaanza kumtoka Lisa. Alikua bila wazazi, kwa hivyo hakutamani watoto wake wawe hivyo.
“Nimekuwa nikipuuza simu zako kwa sababu sikutaka kukuumiza. Upendo wangu kwako haujabadilika.” Alimshika mkono kwa nguvu kabla ya kumpa busu nyuma yake. "Nitajaribu niwezavyo kumaliza kazi mapema na kurudi nyumbani haraka, sawa?"
“Sitaki kuongea na wewe.” Lisa aligeuza na uso wake nyuma yake.
Kwa kweli, alikuwa amechanika kwa ndani. Hakuweza kukubali kutojali kwake lakini pia hakuweza kusamehe ukweli kwamba walikuwa wamempeleka Charity gerezani.
Baada ya Lisa kumaliza kuingizwa dripu, Alvin alimpeleka nyumbani kwa bibi yake.
Bibi Kimaro hakujua kwamba alikuwa amezimia bali alifurahi kuwaona wanandoa hao wakirudi pamoja. Aliwaamuru wasaidizi wa jikoni kupika chakula kizuri sana.

Sura ya: 274

Usiku huo, Mzee Kimaro ghafla alimuuliza Alvin, “Mama yako anaendeleaje kwenye kampuni siku hizi?
“Nina muda sijamuona” Alvin alijibu.
Mzee Kimaro alikoroma kwa sauti nzito. “Bado anamsaidia Mason? Ananichukiza sana.”
Alvin alikataa kutoa maoni yake. Alimjua Lea, alimpenda na kumwamini Mason kupita kiasi.
“Wow, mnakula chakula cha jioni.” Willie na Jack ghafla wakaingia “Babu, Bibi, mnadhani nilikutana na nani kwenye baa usiku huu? Niligongana na Sa—’”
Ghafla aliganda baada ya kuwaona Lisa na Alvin kwenye meza ya kulia chakula. Rangi zote zilimtoka usoni papo hapo. Hawakutegemea kuwakuta kwenye makazi ya familia Kimaro.
Jack, kwa upande mwingine, alimtazama Alvin kwa utulivu kabla ya kujiweka karibu na Mzee Kimaro.
“Uligongana na nani, mbona umekatisha ghafla?” Mzee Kimaro aliuliza.
Willie alivuta pumzi kwa kina kabla ya kujibu, “Um… hakuna mtu. Nahisi njaa. Shangazi Yasmine, tafadhali unaweza kunipitishia sahani?”
Mzee Kimaro alimkazia macho na kutoa mkoromo wa dharau. "Unajua tu jinsi ya kubarizi kwenye baa, lakini kwenye majukumu ya kazi,walaa! Kwanini nyinyi wawili hamwezi kujifunza kitu kutoka kwa Alvin? Angalia jinsi anavyosimamia vyema KIM International.”
Uso wa Jack ulianguka na akakunja ndita ghafla. Babu yake asingeweza kamwe kutambua kazi nzuri aliyoifanya hata iweje.
Kwa upande mwingine, Willie hakuonekana kuwa na wasiwasi hata kidogo. "Babu, sio kila mtu ana talanta kama yeye. Kenya inaweza kuwa na mtu mmoja tu tajiri zaidi."
“Uko sawa.” Bibi Kimaro alisema. Aligeuka ghafla na kulitazama tumbo la Lisa na kutabasamu. “Lakini watoto walio tumboni mwa Lisa hakika watarithi akili za baba yao.”
Alvin akakipapasa kichwa cha Lisa taratibu. "Sijali kitu kingine chochote mradi tu wawe na afya."
"Hiyo ni sawa." Hisia ngumu ilijidhihirisha katika moyo wa Jack alipoona hivyo.
“Sawa, Jack, Alvin atakuja kuwa baba hivi karibuni. Wewe ni lini utatafuta mchumba uoe?” Bibi Kimaro ghafla alibadilisha mtazamo wake kwa mjukuu wake mwingine. “Nimefikiria juu yako na kuona binti kutoka kwa familia ya—”
“Bibi, tafadhali acha kunitambulisha kwa wasichana wa ajabu.” Jack aliziba masikio yake. "Familia ya Campos ilinipendekeza kwa hafla ya kuchagua mchumba siku chache zijazo na ninakaribia kupoteza akili."
Bibi Kimaro alikunja uso. “Wanakutambulisha kwa nani?”
"Binti kutoka kwa familia ya Ngugi, binti wa mwanahisa mwingine katika Kampuni ya Campos."
"kwa hiyo wewe unafikiria nini?" bibi mzee aliuliza.
Jack alihisi kutetemeka hadi kwenye uti wa mgongo wake. "Bado sifikirii kuoa."
"Hmm, kumbuka kuwa wewe ni Kimaro. Hatukukulea ili uwe chombo cha familia ya Campos,” Mzee Kimaro alimkumbusha kwa upole, “Familia ya Campos pia haitamruhusu mtu wa nje kujipenyeza ndani ya biashara zao.”
Jack aliinamisha kichwa chake kula chakula chake taratibu. Kwa kweli, alikuwa amefikiria kujaribu bahati yake katika Kampuni ya Campos kwani hakuthaminiwa kwenye kampuni ya KIM International. Lakini, Jerome Campos alikuwa tayari akifirikiwa kukabidhiwa mikoba ya Campos Ltd. Labda nafasi yake ingekuwa ya chini zaidi katika familia ya Campos kuliko akiwa na familia ya Kimaro. Kwa kweli alihisi kama hafai popote.
Baada ya chakula cha jioni, Mzee Kimaro alisimama na kusema. “Alvin, twende maktaba pamoja nami, nina jambo la kuzngumza na wewe.”
Alvin alikunja uso kabla ya kumgeukia Lisa. “Unaweza kwenda kupumzika kwanza. Nitaungana nawe baadaye.”
"Sio lazima." Lisa alitembea kuelekea mlangoni bila kujali.
Ndani ya maktaba, Mzee Kimaro alipumua kwa muda mrefu kabla hajaanza kuongea. "Familia ya Campos haijaribu hata kuficha tamaa zao mbaya sasa. Wanataka kumtumia Jack kama zana ya kujipenyeza kwa familia za matajiri kupitia ndoa. Umemsikia Jack sasa hivi, nini maoni yako kuhusu hilo?”
"Sijali mradi tu watu wa familia ya Kimaro hawaniangusha." Mzee Kimaro alikosa la kusema.

Baada ya chakula, Lisa alienda kupumzika kwenye bustani. Shangazi Yasmine alikuwa ameondoka kwenda kumtafutia blanketi. Mahali alipokuwa ameketi kulimpa mtazamo mzuri wa Mlima wa Sherman wakati wa usiku huo wa mbaramwezi. Harufu hafifu ya majira ya kiangazi ilimkumba huku upepo wa usiku ukivuma.
"Hongera kwa ujauzito wako." Jack akamsogelea taratibu. Lisa hakumtazama hata kidogo.
“Haya, bado unanikasirikia? Wewe ni mke wa mtu tajiri zaidi Kenya.” Akaketi karibu yake. “Unapaswa kunishukuru. Bado ungekuwa mpenzi wa kisirisiri kama nisingekuwa mimi."
Lisa akamkazia macho, akakosa la kusema. Hakuwahi kukutana na mtu asiye na aibu zaidi yake. Kwa kweli, hakumkasirikia tena kwa kumfanyia njama chafu mara ya mwisho. Mambo mengi sana yalikuwa yametokea baada ya hapo na kulikuwa na watu wengi sana ambao alikuwa amekasirishwa nao.
Jack alimwambia baada ya kuona utulivu wake. “Um… nimekuja kukuambia ujihadhari...”
“Huh? Nijihadhari na nini?”
"Juu ya Alvin. Nilisikia wanaume wanavutiwa kirahisi na wanawake wengine pindi wake zao wakiwa wajamzito, hivyo inabidi umuangalie, haha,” alisema kwa nusu-utani. “Um… Inabidi niondoke hapa, kuna baridi sana. Hupaswi pia kukaa hapa kwa muda mrefu utapata nimonia.” Jack alipunga mkono na kugeuka ili kuondoka na kumwacha Lisa akiwa amekunja uso.
Lisa alijiwazia kwanini Jack alimfuata kumwambia hivyo? Alikuwa mtu wa pili siku hiyo aliyempa onyo kama hilo. Charity alikuwa amesema vivyo hivyo, lakini alipaswa kuwa makini na nani?
“Jack amekuambia nini?” Alvin alimwona Jack akiwa anaishilizia wakati yeye alipofika kwa Lisa akitokea ndani. uso wake ulikunjamana kwa hasira.
“Hakuna kitu.” Lisa aliangalia upande mwingine.
“Usiamini neno lolote analosema. Bado hafurahii kupoteza nafasi ya kuongoza kampuni. Anajua wewe ni udhaifu wangu hivyo atajaribu kuzua mafarakano kati yetu.” Kisha kumwambia hayo, akamchukua mikononi mwake. “Umekaa hapa kwa muda wa kutosha. Turudi ndani kutazama sinema.”
"Hapana." Lisa aliinamisha kichwa chini, akihisi kupasuka. Hakutaka kukaa chumbani peke yake lakini pia hakuweza kumsamehe kwa kumtelekeza kwa muda wa siku kadhaa.
"Wanawake huwa wanasema kinyume na kile wanachotaka." Alipokumbuka maneno hayo ya Daktari, Alvin alimbeba hadi kwenye chumba cha sinema.
Alikuwa amekaa kwenye nyumba hiyo kwa muda sasa lakini hii ilikuwa mara ya kwanza walikuwa wakitazama sinema kwa pamoja. Kufikiria jambo hilo kulimhuzunisha. "Alvin, lazima uwe umetazama sinema nyingi hapa na marafiki au wapenzi wako."
“Si…” Alikuwa karibu kukataa lakini akakumbuka kwamba alikuwa ametazama sinema na Melanie mara ya kwanza Lisa alipotembelea jumba hilo. Mwanamke huyo kweli alikuwa na wivu. Lisa alichaia tabasamu la kichefuchefu kabla hajageuzia uso wake pembeni.
Alvin aliurejesha uso wake ili kumpa busu kwenye midomo. “Usiwe na wivu, sikutazama sinema na Melanie mara ya mwisho. Nilikuwa kwenye simu yangu na sikujua sinema yake hata inahusu nini.”
“Sikuwa na wivu. Niache.” Ghafla aliona aibu baada ya kuona tabasamu lake la uvivu.
"Siendi popote. Chagua filamu unayopenda tutazame. Nimekuandalia korosho za kutafuna. Ni nzuri kwa ukuaji wa ubongo wa watoto."
Alimtazama na kisha akachukua korosho kabla ya kutikisa kichwa kukubali. “Nafikiri hivyo pia. Itakuwa balaa ikiwa watoto wangu watakuwa na akili ya polepole kama baba yao.” Mwishowe, alichagua filamu ya James Bond, ambayo iligeuka kuwa nzuri sana.
Alvin alimlisha korosho kimahaba mara kwa mara wakati filamu inaendelea. Lisa hakuwa na hamu ya kula korosho hizo lakini akajikuta zinamnogea. Aliishia kula takriban pakiti tano peke yake.

Sura ya: 275

Wakati filamu ikiwa imekolea, simu ya Alvin iliita ghafla. Akaitoa mfukoni. Lisa aliiba kwa kuitazama na kugundua mtu anayeitwa Nyasia alikuwa akimpigia simu.
“Nitaenda nje kupokea." Alitoka chumbani na kuitikia simu kwa sauti ya chini. “Kuna nini?”
“Siwezi kukupigia simu mpaka niwe na sababu?” Sauti ya Sarah ya kukata tamaa ilisikika kutoka upande wa pili.
'Siyo kwamba…mimi…” Alvin akajikanyagakanyaga.
Mwanamke kwa upande mwingine alicheka. “Pole kwa kukusumbua. Nilifanya utafiti kuhusu hali yako wakati wa mchana na nikaja na mpango wa matibabu. Hebu tuanze matibabu usiku wa leo.”
“Leo usiku?” Alvin alishangaa.
“Uh-ha. Nimeandaa mipango 30 ya matibabu kwa sasa na itafanywa kwa nyakati tofauti za siku. Muda mzuri zaidi ni usiku na nadhani mwili wa mwanadamu ndio huwa umetulia zaidi kwa wakati huu, kwa hivyo itakuwa rahisi kwako kuungana na hisia zako za kweli. Kando na hilo, ni vigumu kutibu hali yako kadiri tunavyoahirisha kwa muda mrefu. Usiku wa leo ni wakati mzuri zaidi.”
Alvin alikunja uso na kusema baada ya kusitasita kwa muda mfupi, “Samahani lakini nina shughuli nyingi kwa sasa…”
“Naona. Najua utakuwa umebanwa na mkeo! Samahani kwa hilo…” Sarah alisikika akifadhaika. "Karibu nilisahau kuwa wewe ni mume wa mtu sasa."
“Ni sawa. Vipi kesho usiku?” Alvin aliuliza.
“Hakika.” Alitabasamu kwa uchungu. "Nina wivu sana na mke wako."
Hili lilimshangaza. Hisia ngumu ikatokea moyoni mwake. Ikiwa mambo yangeenda kulingana na mipango, Sara angekuwa mke wake sasa.
Wakati akiwaza ni kitu gani cha kumwambia, tayari mtu wa upande wa pili wa simu aliaga na kukata simu. Alisimama pale kwa sekunde chache kabla ya kuingia tena kwenye chumba cha sinema.
Lisa aliinua macho yake kumtazama. “Mmempata mwanasaikolojia Nyasia?”
"Ndio. Inaonekana kuna nafasi naweza kupona kabisa.” Akamkumbatia Lisa kwa furaha.
"Ni mwanaume au mwanamke?" Lisa alihoji baada ya kusitasita kwa muda mfupi.
“Una wivu tena?” Alvin aliinua macho yake. "Babe, lazima uamini kuwa ninakujali wewe na watoto tu kwa sasa." Bila kumpa nafasi ya kujibu, alibana midomo yake juu ya lips zake.
Lisa alitaka kukataa lakini ilikuwa imepita muda mrefu sana tangu wapeane busu kwa mahaba. Kwa sekunde kadhaa, akili yake ilipotea kabisa. Hatimaye, alimvuta mikononi mwake alipokuwa karibu kukosa pumzi.
Filamu ilipoisha, alimbeba juu hadi chumbani. Alvin alikaa kitandani huku akiwasomea vitabu vya hadithi watoto waliokuwa tumboni mwa mama yao. Sauti yake ya sumaku ilituliza masikio ya Lisa. Hatimaye, alilala kwa kubembelezwa na sauti hiyo. Alikuwa akisumbuliwa na kukosa usingizi kwa siku kadhaa. Muda mrefu ulikuwa umepita tangu apate usingizi mzuri.
Asubuhi iliyofuata. Alvin alipokea simu kutoka kwa Rodney baada ya kuzinduka. "Alvin, Sarah alilewa jana usiku na nikamrudisha nyumbani."
“Sawa…” Alvin aliitikia kwa mkato.
“Nafikiri alitoka kunywa pombe kwa sababu yako,” Rodney alilalamika kwa kufadhaika, “aliendelea kunung’unika kuhusu kukosa nafasi kwako na hata kulia.”
Alvin alisugua kichwa chake. Alikuwa amehisi sauti yake isiyo ya kawaida wakati wa mazungumzo yao jana yake usiku. “Rodney, nimeoa. Kweli…Ikiwa unampenda, unapaswa kuwa naye badala ya kumpa mtu mwingine.”
Hilo lilimshangaza Rodney. Aliweza kuonja uchungu mdomoni mwake. "Siku zote amekuwa akinichukulia kama rafiki na shemeji yake."
“Utajuaje kama hutajaribu? Nitakuwa baba hivi karibuni. Hii sio haki kwake pia,” Alvin alishauri. Kulikuwa na ukimya wa muda mrefu upande wa pili wa simu.
Alvin alivaa kabla ya kwenda kumtazama Lisa. Aliandamana naye wakati wote wa kifungua kinywa kabla ya kuondoka kwenda kazini.
Aunty Yasmine alimtania Lisa baada ya kuona mwanga wa furaha usoni mwake. "Inaonekana kama Bwana Kimaro ndiye tiba yako."
Lisa aliona haya na kuuma mdomo. Alichukia kwamba ujinga wao umepelekea madhara kwa Charity na Pamela. Hata hivyo, hakuweza kujizuia kutamani penzi la Alvin sasa akiwa mjamzito.

Alvin alimpigia simu ilipofika usiku. "Ninafanya kazi ya ziada usiku wa leo, kwa hivyo sitakuwa nyumbani kwa chakula cha jioni. Pia nina mkutano wa kijamii baadaye na sijui huo utaisha lini. Nitalala katika nyumba ya New Metropolis Park.”
“Sawa.” Ghafla Lisa akakumbuka ukumbusho wa Jack baada ya simu. Akiwa amechanganyikiwa, alishika kichwa chake kwa mikono yake yote miwili. Alitamani angemuuliza Jack vizuri alimaanisha nini alipomwambia awe makini na Alvin. Maurine alikuwa amekufa. Pengine ni Nyasia ndiye alikuwa changamoto nyingine muda huo?
Saa mbili usiku ujumbe uliingia kwenye simu yake wakati anakaribia kuoga. Alipokea picha iliyotumwa na nambari isiyojulikana kwenye whatsapp.
Alibofya kwenye picha. Alvin alikuwa akitembea kwenye korido ya hoteli ya nyota tano na mwanamke aliyevalia nguo ndefu. Mwanamke huyo alikuwa amevaa mtandio na mikunjo yake mirefu ilikuwa imening'inia kwenye pande za mabega yake kiasili. Wawili hao walionekana wakamilifu kana kwamba mwanamke katokea kwenye ubavu wa mwanamume.
Lisa alishtushwa na ukweli kwamba mwanamke huyo alifanana sana na yule kwenye picha ambayo Kelvin aliwahi kumuonyesha.
Alikuwa akifikiri kwamba Maurine anafanana sana na mwanamke huyo lakini sifa zake hazikuwa zikiendana sawia kama yule aliyekuwa kwenye picha. Mwanamke huyu alikuwa hata zaidi ya kufanana. Hapana, alifanana kabisa na Sara. Hata Alvin alikuwa akimwangalia kwa upole.
Lisa aliangalia tarehe chini ya picha. Ilichukuliwa jana saa tatu asubuhi. Ilikuwa wakati alipokuwa akikimbilia mahakamani. Alvin alikuwa akifanya nini hotelini na mwanamke huyu? Alikuwa nani?
Alihisi baridi kali ikipenya hadi kwenye uti wa mgongo wake. Alihisi presha zaidi kuliko alipopata habari kuhusu Maurine. Maurine hakuwa amemtisha kiasi hiki hapo awali.
Mara simu yake ikaita. Ilitoka kwa nambari ile ile iliyotuma picha hizo. Mara moja akaipokea. Kicheko cha furaha cha Melanie kilisikika. “Dada yangu kipenzi, umeiona picha? Umezipenda?"
“Zinakuhusu nini wewe?…” Lisa alisema kwa utulivu huku akijaribu kila awezalo kuzuia hisia zake.
Melanie alicheka. "Sawa, labda bado hujui kuhusu hili lakini mwanamke kwenye picha ni Sarah Njau. Hajafa.”
“Ni ujinga gani huo?” Lisa alikunja uso. Hilo lingewezekanaje? Sara alikuwa amekufa kwa muda mrefu.
“Ninasema ukweli. Nimemwona Sarah ana kwa ana hapo awali na hakika huyo ni yeye. Mbali na hilo, nimefuatilia. Sarah hakufa nje ya nchi wakati huo. Alirudi nyumbani siku chache zilizopita kwa ajili ya mazishi ya Maurine. Alvin, Rodney, na Chester wanakula bata pamoja naye kila siku, wakimchukulia kama binti wa kifalme. Kweli, niliona kwa macho yangu kwamba alikuwa akitoka naye kwenye chumba cha hoteli jana asubuhi. Unafikiri wapenzi wa zamani wangefanya nini katika chumba cha hoteli?”
Kweli, binadamu anaweza kukunyima neno la hekima litakalokusaidia, lakini umbea? Atakupa bila gharama yoyote. Mkono wa Lisa uliokuwa umeshika simu ulianza kutetemeka. Miguu yake ilikuwa ikizidiwa na udhaifu. Taswira ya Alvin kuwa kitandani na mwanamke mwingine ilipeleka maumivu makali kwenye moyo wake.
"Nina hakika kwamba lazima utaumia sana na kuogopa sasa." Melanie alicheka kwa furaha. “Najisikia vibaya sana kwako. Ingawa wewe ni mjamzito, mume wako anakutana kwa siri na mpenzi wake wa zamani. Naona hukuwa na wazo kuhusu hili. Habari hii nitakupa bure maana mimi ni dada mzuri sana.” Alikata simu baada ya hapo.
Lisa akaketi kitandani. Sarah alikuwa hai? Hilo liliwezekanaje?
Hakutaka kuamini, lakini picha ilikuwa uthibitisho.

TUKUTANE KURASA 276-280

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......276-280

Sura ya: 276

Huyo ndiye mwanamke ambaye Alvin alimfikiria hata katika ndoto zake.
Charity alikuwa amemuonya hapo awali kwamba Sarah alikuwa ni mwanamke mwenye nguvu sana kwa Alvin. Lisa asingekuwa na nafasi ikiwa Sarah angalikuwa hai.
Sawa, Charity pia alisema ‘ajihadhari’ jana yake. Alikuwa anamaanisha ajihadhari na Sarah Njau? Lisa alitetemeka. Alikuwa katika mshtuko mkubwa. Charity alikuwa akimwonya kujihadhari na Sarah Njau. Kwa hiyo, tayari alijua kwamba Sara alikuwa angali hai. Nini kingine alijua?
Mbali na hilo, Jack pia alikuwa amemkumbusha Lisa jana yake usiku. Kila mtu alijua juu ya hilo isipokuwa yeye mwenyewe. Je, Alvin angerudiana na Sarah?
Moyo ulimdunda huku akiligusa tumbo lake bila kujua. Hapana! Hakujali jinsi alivyokuwa zamani, lakini alikuwa baba wa watoto sasa. Walihitaji familia kamili. Hakutaka watoto wake walelewe na single mother. Hapo hapo akashika simu yake kumpigia Alvin.
"Samahani, nambari unayopiga haipatikani." Alikuwa anafanya nini hata akashindwa kupokea simu yake? Inawezekana kwamba alikuwa pamoja na Sara?
Hakuweza kuizuia akili yake kuendelea na mawazo hayo na haraka akampigia simu Hans. “Mbona Alvin hapokei simu zangu?”
Hans, ambaye alikuwa akifanya kazi kwa muda wa ziada ofisini, alishikwa na mshangao. “Bwana Kimaro anapatiwa matibabu ya kisaikolojia hivi sasa. Daktari anasema hatakiwi kusumbuliwa.”
“Matibabu? Unamaanisha Dk. Nyasia?”
"Ndiyo, daktari alisema ni muhimu kuanza kumtibu haraka iwezekanavyo.” Hans alikuwa na wasiwasi. Alitumai Alvin angeweza kupona haraka. Ingekuwa balaa endapo Lisa angegundua kuwa Nyasia ni Sarah Njau aliyefariki dunia.
Lisa aliuliza baada ya ukimya wa muda mrefu, "Analala huko New Metropolis Park?"
“Ndiyo.”
Lisa alitamani angeweza kwenda kumngoja kwenye nyumba hiyo ya New Metropolis Park, lakini, alijua asingeweza kuruhusiwa kuondoka katika familia ya Kimaro. Alizidiwa na majuto kwa kukubali kuhamia katika nyumba ya familia ya Kimaro hapo mwanzo.
•••
Saa mbili na nusu usiku, Alvin aliingia kwenye baa ya hoteli ya Peninsula iliyokuwa ikicheza wimbo wa jazz. Alimwona Sarah ambaye alikuwa amekaa baa mara ya kwanza. Usiku huo alikuwa amevalia gauni refu jeupe. Alionekana kama ua la thamani ambalo lilichanua tu usiku.
“Si ulisema tuna ratiba ya kutibu ugonjwa wangu usiku huu? Kwanini tunakutana hapa?" Akamsogelea na kuketi karibu yake.
"Ungependa kwenda hospitali ya kuchosha au kliniki ya wagonjwa wa akili?" Sarah alitabasamu.
Alvin akaminya midomo yake. Hakika, hakutaka kukutana katika mojawapo ya sehemu hizo.
“Hapa ndio mahali pazuri zaidi. Hakuna kelele wala ghasia nyingi.” Saraha alimwambia kwa utulivu.
Kwa mshangao wake, mhudumu wa baa alikuja na vinywaji viwili. Akampa kila mmoja cha kwake.
“Tunakunywa pia?” Alvin akakunja uso.
"Unataka kutibiwa katika hali hii ya wasiwasi?" Sarah alielekeza mkono kwenye moyo wake na kisha kichwa chake. "Mwanasaikolojia hufanya nini? Tunashughulikia maeneo haya mawili. Kunywa tembe hakusaidii ugonjwa wa moyo wala akili.” Alvin alichukua pombe hiyo kimya kimya.
Sarah alimtazama Alvin. Ingawa alikuwa ameketi katika eneo lenye giza, sifa zake za kupendeza zilibaki za kuvutia. Alihisi haja ya kuushinda moyo wake. “Alvinic unaweza kunifanyia upendeleo? Unaweza kuiacha New Era Advertisings?”
“Unataka kuichukua, huh?”
"Hapana. Nina shughuli nyingi za kutosha kwa hiyo sina muda wa kusimamia kampuni.” Sarah alitoa kicheko cha uchungu. “Baba yangu ameanguka tena huku Charity akiwa gerezani. Baba yangu anachojali zaidi ni kampuni yake. Ninahofia hataweza kuendelea bila kampuni yake.”
Chembe ya upole ikaangaza machoni mwa Alvin. “Wewe bado ni yule yule. Hata hivyo, usisahau jinsi baba yako alivyokutendea ulipokuwa ukitangatanga huko ulaya kwa miaka hii.”
“Hiyo ni hadithi nyingine. Ninafanya tu kile ninachopaswa kuwa kama binti. Angalau nina dhamiri safi.” Sarah akahema. “Zaidi ya hayo, kaka yangu hana kazi licha ya kwamba tayari ni mtu mzima. Ninapaswa kumsaidia kugeuza ukurasa mpya ili asiwe mtu mbaya kama hapo awali.”
Kwa kutajwa kwa Thomas, Alvin alifunua sura ya kuchukiza. "Ni wakati wa kubadilika."

Sarah alimcheka ghafla. “Nilifikiri ningehitaji kuweka jitihada fulani ili kukushawishi. Sikutarajia kwamba ungekubali kwa urahisi.”
"Nina deni kwako," Alvin alisema.
"Hapana. Huna deni kwangu,” Sarah alijibu huku akiinamisha kichwa chini na kutazama mvinyo iliyokuwa mezani.
Nusu saa baadaye, wote wawili walipanda ghorofani pamoja.
Kelvin alitokezea kwenye kona yenye giza na kuchukua picha za wawili wale. Alitabasamu baada ya kuona picha iliyokuwa mkononi mwake. Alipokuwa akifanya kazi ofisini kwake mchana huo, ghafla alipokea ujumbe wa ajabu kutoka kwa Melanie ambao ulimwambia atembelee hoteli hiyo kuchukua udaku wa Alvin.
[Lisa, inaonekana uko hatarini.] Kelvin alimtumia Lisa picha hiyo kupitia WhatsApp. [Niliona haya nilipokuwa na rafiki yangu kwenye Hotel ya Peninsula usiku huu. Wote wawili waliingia katika chumba cha faragha ghorofani. Nilisikia una mimba. Afadhali uendelee kulea mimba yako peke yako. Unaweza kuja kwangu muda wowote ikiwa unahitaji msaada.]
•••
Wakati Lisa alipopokea picha hiyo, moyo wake ulibadilika kuwa wa baridi. Ilionekana kana kwamba shimo lilikuwa limetobolewa moyoni mwake.
Jana yake, Melanie aliwanasa wakitoka kwenye chumba cha hoteli hiyo. Siku hiyo, walionekana tena pamoja. Alimaanisha nini kwenda kutibiwa? Alimaanisha nini kwa kujishughulisha na kazi? Haya yote yalikuwa ni uongo. Alitaka tu kumweka Sarah karibu yake. Vipi kuhusu yeye na watoto wachanga tumboni mwake?
Lisa alilipuka kwa hasira kwani alishindwa kuvumilia tena. Ilibidi aondoke kwenye nyumba ya Kimaro na kwenda kumtafuta Alvin, lakini alidhani kwamba hakuna mtu ambaye angekubali kumruhusu. Baada ya kuwaza, akatafuta namba ya simu ya Jack na kumpigia.
“Ni nadra kwamba unanipigia simu kwa hiari yako mwenyewe," Jack alisema kwa mshangao.
“Jack, tafadhali nitoe kwenye nyumba hii. Nina jambo la dharura la kushughulikia.” Baada ya kufikiria kidogo, aligundua kwamba Jack alikuwa mtu pekee katika familia ya Kimaro ambaye angeweza kumwomba msaada.
Jack alipasuka kwa mshangao. “Ni usiku sana sasa. Ni nini muhimu sana ambacho unahitaji kushughulikia? Ikiwa bibi na babu yangu watajua kuhusu hilo, hakika watanizika nikiwa hai. Pia, Alvin…”
“Sifanyi chochote cha hatari. Ninahitaji tu kushughulikia mambo kadhaa ya haraka. Nitakuwa na uhakika wa kujitunza mimi na watoto wangu.” Lisa alimhimiza kwa utulivu. “Jack, usisahau uliahidi kunisidia baada ya kunikasirisha. Kama bado una hatia kuhusu hilo…”
“Sawa, sawa. Umeshinda. Nitakutoa. Njoo chini kwa siri. Usiruhusu mtu yeyote ajue.” Jack akashusha pumzi.
Dakika kumi baadaye, Lisa aliingia kisiri kwenye gari la Jack. Mlinzi alipogundua kuwa ni gari la Jack, hakulizuia gari hilo na kuliruhusu litoke nje ya nyumba ile.
"Unaenda wapi?" Jack alipomkazia macho, akajikuta bado amevaa nguo za kulalia. Alishangaa ni jambo gani la dharura lililomkurupua kiasi hicho.
"Peninsula Hotel."
"Mbona unaelekea hotel saa hizi?" Wasiwasi ulikzidi kuongezeka kwa Jack. Alijua kabisa kwamba familia ya Kimaro ilikuwa na wasiwasi sana juu ya watoto wa tumbo la Lisa.
"Ili kuangalia ikiwa Alvin yuko kitandani na mtu mwingine." Jack alifunga breki. Lisa aliongeza bila kujali, “Jack, tayari unajua kwamba Sarah bado yuko hai na Alvin amekutana naye hivi karibuni? Ulinikumbusha kuwa wanaume wanavutiwa kirahisi na wanawake wakati wake zao wakiwa wajawazito. Ulikuwa unamaanisha niwe makini na Sarah, sivyo?"

Sura ya: 278

Jack alipapasa paji la uso wake. Wakati mwingine, wanawake walikuwa na machale sana hivi kwamba ilionekana kana kwamba walikuwa na antena. “Kwa kweli, nilisikia tu kwamba Alvin, Rodney, na genge lake wamekutana pamoja na Sarah hivi majuzi. Sina uhakika na mambo mengine.”
"Badala ya kujitenga na mpenzi wake wa zamani, anafuatana naye na kuzurura naye badala yake. Je, hii haimaanishi kwamba atanisaliti mapema au baadaye?” Lisa aliuma mdomo, akihisi uvimbe kwenye koo lake. "Sitaki watoto wangu wakue bila baba."
“Sawa.” Jack aliendelea kuendesha.
Dakika 40 baadaye, gari lilikuwa limeegeshwa mbele ya Peninsula Hotel. Lisa aliufungua mlango wa gari na kutoka nje.
"Nisubiri." Akiwa na wasiwasi kwamba kuna kitu kingetokea kwa watoto wachanga tumboni mwake, Jack alimfuata haraka.
Lisa alipanda ngazi na kuusukuma mlango wa kila chumba cha faragha. Aliposukuma mlango wa chumba cha nne, aliona mwanamume na mwanamke wakiwa wamekumbatiana kwenye kochi. Mwanaume mrefu na mzuri alikuwa Alvin. Wakati huo huo, Sarah alikuwa akigusa kichwa chake kwa upole, kilichokuwa kimeegemea kifua chake.
Mlango uliposukumwa kwa nguvu, Sarah alishikwa na butwaa. Lisa alitazama eneo la tukio huku akiwa amejikita mahali hapo. Hisia nyingi zilimtawala sana. Alihisi kutapika. Kweli alijisikia kutapika.
Huyu ndiye mwanaume ambaye alikuwa akimpenda sana, lakini alikuwa ameegemea kifua cha mwanamke mwingine, tena alionekana kuzama kabisa kwenye hisia nzito kiasi cha kutojitambua. Kwa mtazamo huu mbele yake, alikiri kwamba hakuwahi kumshinda Sara. Angeweza kuchagua kutompenda Lisa, lakini angalau alipaswa kuzingatia watoto wake. Akilipuka kwa hasira, akaongeza mwendo wake kuelekea kwao.
Sarah alimsukuma Alvin kwa haraka. “Wewe ni mke wa Alvinic? Sio jinsi inavyoonekana…”
Lisa alichukua glasi ya mvinyo kutoka mezani na kummwagia Sarah usoni.
“Ah!” Sarah alipiga kelele.
Bado kichwa cha Alvin kilikuwa kinamuuma sana akiwa amejiinamia kwenye kochi. Sarah alipokuwa akimpatia matibabu muda ule, alitumia mbinu za kisaikolojia zinazojulikana kama Hypnosis, kumfanya akumbuke kumbukumbu zake mbaya za utotoni ili aweze kuzibadilisha kwa kumbukumbu nzuri badala yake. Katikati ya kukata tamaa na kutokuwa na uwezo, aliamshwa na kelele.
Mara tu maono yake yalipoonekana wazi, aligundua kuwa Sarah alikuwa amelowa na katika hali ya kusikitisha huku Lisa akiwa ameshikilia glasi ya divai kwa hasira.
"Unafanya nini?" Alvin akaruka na kusimama ghafla na kumtazama Lisa.
Sarah akamshika mkono mara moja. “Usikasirike, Alvinic. Yeye hakuwa na maana mbaya juu yangu. Nadhani alituelewa vibaya.” Macho ya Lisa yakatua kwenye mkono wa Sarah ulioshika kwenye mkono wa Alvin. Alipoona tukio hilo lisilopendeza, machozi yalianza kumtoka. Ni kutokuelewana? 'Alvinic' lilikuwa jina la utani la kupendeza.
"Wewe ni Sarah, sivyo?" Lisa alimtazama bila kujali, macho yake yalionyesha ukali. “Nilihisi kwamba upendo wa kwanza wa mume wangu ulikuwa safi na wa kipekee. Inatokea kwamba wewe huna tofauti na wale wanawake ambao wanafeki kuwa na huruma na kupanga njama za siri dhidi ya watu wengine.”
Uso mzuri wa Sarah ulipauka ghafla. “Kwa kweli ni kutokuelewana. Nilikuwa nikimtibu Alvin tu.”
“Kutibu?” Lisa alitoa kicheko. “Ni tiba gani hii? Chumba cha hoteli kimegeuka kuwa wodi ya wagonjwa, na pombe ndiyo dawa, na tiba ni mahaba?”
“Inatosha.” Alvin alikemea huku akionekana kulegea. Huku akiumwa na kichwa, aliendelea kumsikia Lisa akipiga kelele sana. Kichwa chake kilizidi kuwa na hali mbaya na akaruka kwa hasira. “Lisa nilikuambia utunze ujauzito wako nyumbani, lakini ulikuja hapa kumshambulia Sarah kwa maneno makali saa hizi. Unatafuta nini?”
Hali ya kutoamini ikapita usoni mwa Lisa. Yeye ndiye aliyekuwa akifanya mambo yasiyostahili na mwanamke mwingine. Hata hivyo, hakuwa na aibu wala wasiwasi hata kidogo. Badala yake, alikuwa akimlaumu.
“Kwa hivyo unanilaumu kwa kukukatisha starehe zako na mpenzi wako wa zamani?” Lisa alimkejeli Alvin katikati ya kwikwi zake.

"Nilisema sijafanya chochote, kwa hivyo inamaanisha hakuna kitu kinaendelea kati yetu. Kwanini huwa unawadhalilisha watu kabla ya kujua ukweli? Omba msamaha kwa Sarah sasa hivi,” Alvin alimuamuru kwa huzuni.
“Kuomba msamaha?” Lisa aliuliza kana kwamba alikuwa ametoka tu kusikia mzaha wa kuchekesha zaidi duniani.
“Ni sawa, Alvinic," Sarah alizungumza naye mara moja. “Bora uondoke na mkeo sasa. Ah-choo.” Sarah alipiga chafya na kujikunyata kitandani.

Hisia za kuchanganyikiwa zilimtawala Lisa ghafla. Wakati Maurine, ambaye alikuwa amefanana tu na Sarah alipotokea hapo awali, Lisa na Alvin walikuwa na mzozo mkali na walikuwa kwenye hatihati ya talaka. Sasa Sarah mwenyewe alikuwepo, je Lisa bado angekuwa na matumaini ya kumshinda? Macho ya Lisa yalitoa hali ya kuchanganyikiwa.
Aliyesimama mlangoni alikuwa Jack ambaye alikuwa akijizuia kuingilia suala hilo. Hata hivyo, alipoitazama sura ya Lisa inayotetemeka na upweke, alishindwa kuvumilia hali hiyo tena. Alisema licha ya nafsi yake, “Umeenda mbali sana, Alvin. Baada ya yote, yeye ni mke wako. Tayari umeoa, lakini unafanya mambo ya faragha na mwanamke mwingine kwenye chumba cha faragha usiku namna hii. Umewahi kufikiria hisia za Lisa?”
"Kwani nimefanya nini na Sarah?" Alvin alimtazama Lisa kwa hasira na kusema, “Jack ndiye aliyekuleta hapa? Umesha sahau alichokufanyia mara ya mwisho? Anajaribu tu kutusambaratisha. Kwanini kila mara huwa na watu wenye nia potovu?”
“Nani ana shida ya kuwatenganisha nyie? Lazima utakuwa umerukwa na akili.” Jack alishindwa kujizuia.
“Sawa. Twende zetu.” Lisa alimkokota Jack. Alikuwa amechoka. Hakupaswa kwenda.
"Ni nani aliyekuruhusu kumshika mkono?" Alvin alimsogelea Lisa na kumvuta kwake. "Jack, bora ukae mbali naye."
Baada ya kuona tukio hilo, sura ya Sarah iliganda. Alikunja ngumi kwa siri, na macho yake yalikuwa mazito kwa wivu.
"Unataka Jack akae mbali nami, lakini wewe kwanini hutaki kukaa mbali na Sarah?" Lisa alijitenga na Alvin na kumdhihaki. "Unaweza kufanya kitu kama hicho, lakini huruhusu watu wengine kufanya vivyo hivyo, sivyo? Alvin, kama unataka kurudiana pamoja na Sarah, unaweza kuniambia moja kwa moja. Sikuomba uwe nami. Ulidai kuwa unahitaji kufanya kazi ya ziada na kwenda kutibiwa, lakini kumbe unanidanganya. Unajua jinsi nilivyojihisi nilipokuona umeegemea kifua chake sasa hivi?”
Alvin alipigwa na butwaa, na uso wake ulikuwa umekunjamana. Hakujua kama alikuwa amemwegemea Sarah kifuani.
Wakati huo, Sarah alimsogelea Lisa. "Alvinic, ngoja nimuelezee." Kwa hayo, Sarah akamkabidhi kadi ya biashara. "Bi. Kimaro, mimi ni Nyasia, mwanasaikolojia ambaye anahusika na matibabu ya ugonjwa wa Alvin. Nilikuwa namtibu kweli sasa hivi. Nilijaribu kumfanya akumbuke kumbukumbu zake za utoto ili kumsaidia kushinda kiwewe chake, lakini alishindwa kujizuia. Basi nikamkumbatia ili kumtuliza, ndipo nyie mkaingia.”
Baada ya kupokea kadi, Lisa alipigwa na butwaa. Kamwe hangeweza kutarajia kwamba Sarah alikuwa yule Daktari anayeitwa mwanasaikolojia, Nyasia, ambaye Chester alikuwa amemtaja kuwa mwenye kipaji na asiyeeleweka.
Kwa wazi, mwanamke huyu hakuwa rahisi. Ikiwa angemtibu ugonjwa wa Alvin kila siku, angeweza kumnasa kwa mbinu za hila.
“Kweli, alikuwa akinitibu sasa hivi. Sababu iliyonifanya nisikuambie ni kwamba niliogopa utatuelewa vibaya na kufikiria mambo kupita kiasi kama sasa,” Alvin alisema.
Lisa aliinua kichwa chake bila huruma na kudhihaki, "Kwa hiyo mnataka niwaombe msamaha kwa hilo?"
Ikiwa Alvin angekuwa na ujasiri wa kumfanya aombe msamaha kwa Sarah, uhusiano wao bila shaka ungeharibika. Alvin alikosa la kusema.
Jack alisema kwa namna ya mzaha, “Kwanini aombe msamaha? Huu ni uonevu. Sarah ni ex wako, na kwa kweli mko peke yenu katika chumba cha faragha. Ulimfokea mkeo mjamzito dakika tu ulipomwona. Ni kawaida kwa mwanamke kuingiwa na wivu kwa kumkuta mumewe akiwa katika hali kama hiyo, hata kama ingekuwa ni wewe.”

Sura ya: 279

Lisa alimtazama Jack kwa hisia tofauti. Ilikuwa ni muda tangu alipokuwa na fikra tofauti kuhusu yeye. Jack alimkazia macho huku akionyesha safu ya meno meupe.
Baada ya kuona vitendo vyao vya kuteteana, uso wa Alvin ukaingia simanzi.
Sarah kisha akasema kwa upole, “Matibabu yako yamekamilika kwa leo, Alvinic. Unaweza kumpeleka mkeo nyumbani kwanza.”
“Sawa.” Alvin akaitikia kwa kichwa. Ilimtia wasiwasi kuwaona Lisa na Jack wakirudi pamoja. Kwa upande wa Sara, alikuwa na hakika kwamba alikuwa na uwezo wa kuendesha gari peke yake kwenda nyumbani.
Lisa alipofika mlangoni aligeuka nyuma na kumtazama Sarah. “Dokta Nyasia, natumai unaweza kumfuata Alvin nyumbani ikiwa unataka kuendelea kumtibu. Samahani kwa kuwa na wivu, kwani wewe ni mrembo na pia ni ex wa Alvin huku mimi ni mjamzito tu. Kwa kuzingatia kuwa wewe ni mwanamke pia, nina uhakika unaelewa hisia zangu.”
“Naelewa." Sarah akaitikia kwa tabasamu hafifu.
Sarah alipogundua kuwa Alvin ameondoka bila kuangalia nyuma, uso wake mzuri ulibadilika ghafla. Kweli Alvin alimuacha peke yake pale? Ingekuwa zamani, asingefanya hivyo kabisa. Kwa mwonekano wa mambo, alionekana kujali umuhimu wa mwanamke huyo mbaya usoni mwake. Ilibidi alishughulikie suala hilo kwa mbinu nyingine.
Jack alitoka nje ya hoteli na alikuwa karibu kuondoka. Ghafla, Lisa akamwita, “Asante kwa leo Jack. Nitakununulia chakula cha jioni kukushukuru.” Ilikuwa ni muda mrefu tangu atoke nje. Harufu ya nyama choma kando yake ikaingia puani na kumfanya atamani kula nyama choma ghafla.
"Wewe ni mjamzito na unataka kula nyama choma?" Alvin alikunja uso kwa nguvu sana mpaka uso wake mzuri ukawa unachukiaza. “Twende nyumbani.”
“Najua hutakubali ndiyo maana sikuomba hata ruhusa yako. Ikiwa unataka kwenda nyumbani, unaweza kutangulia peke yako." Lisa alimpa Jack ishara kwa macho. Baada ya hapo, wote wawili walitembea hadi upande mwingine. Kulikuwa na baa ya kawaida pale na ilikuwa imechangamka sana.
Alipomwona Alvin aliyechanganyikiwa nyuma yake, Jack ghafla aliinua uso wake kwa majivuno. ‘Afadhali! Ingawa sina uwezo wa kutosha kushindana nawe kazini, angalau naweza kukutesa kidogo kupitia mke wako' Jack alijiwazia.
Alvin alipandwa na hasira. “Lisa, nisingekuwa na shida na wewe kula nyama za mitaani kabla ya kuwa mimba. Lakini kwa kuwa sasa una mimba, huwezi kuwahatarisha watoto wetu!”
“Haya, kaka, umekosea kusema hivyo. Nani amesema wajawazito hawawezi kula nyama choma? Ni sawa ilimradi atumie kidogo,” Jack alicheka na kusema huku akikonyeza macho.
Lisa alikubali kabisa kwa kichwa. Ikiwa asingekuwa na mimba wakati huo, alitamani hata kupata chupa chache za divai. “Nimekuwa nikila chakula cha wapishi wa Kimaro kila siku. Hakina ladha. Wewe mwenyewe hukujali hata kunitoa nje, lakini unathubutu vipi kunizuia sasa? sijali. Lazima nipate nyama choma leo." Harufu ya nyama ilimfanya Lisa adondoshe udenda.
"Kaka, unaweza kutangulia nyumbani ikiwa hutaki kula." Jack alimfuata Lisa huku akitabasamu.
Alvin alihisi hamu kubwa ya kumkanyaga Jack usoni. Hatimaye, alivuta uso mrefu na kuwafuata. Baada ya kupata viti vyao kwenye klabu ile ya usiku, kelele za jirani na mazingira mabaya yalimfanya Alvin kukunja uso.
Kila mtu aligiza nyama choma za kutosha, isipokuwa Alvin.
Alvin alishindwa cha kusema. Kwa fikra zake aliona hata bia tu zinazouzwa hapo hazina kiwango cha yeye kutumia, sembuse chakula? Thubutu! Mara ya mwisho alilazimishwa na Lisa kula nyama za kuku huko Coco Beach katika mazingira kama hayo, na alisumbuliwa na kinyaa cha mdomoni kwa wiki nzima.
Hata hivyo, hakuweza kuruhusu watoto wake wateseke. Aliinuka na kuelekea kwenye jiko la nyama choma. "Bwana, umeosha vyombo vyako?"
“Mke wangu ameosha vyombo hivi mara kadhaa. Vipo safi bosi wangu,” mchoma nyama alijibu huku akitabasamu.
Alvin hakuamini hata kidogo. "Hiyo haiwezekani. Nilisikia kwenye mitandao kuwa huwa mnafutafuta sahani zenu, na hata nyama wakati mwingine mnachoma zilizoharibika."
Mchoma nyama alikosa la kusema. “Bosi, kama unaona nyama zetu hazifai, kanunue sehemu nyingine.”

'Sawa, mimi binafsi nitaosha vyombo ambavyo mke wangu atatumia." Alvin alichukua sahani kadhaa na kuelekea bombani.Mchoma nyama alishindwa hata kusema, kwa miaka kumi ya uzoefu wake wa kuchoma nyama kwenye baa hiyo, hakuwahi kuona mtu wa dizaini kama hiyo.
Lisa alitingisha mdomo bila kusema, kisha akagusa tumbo lake, "Watoto wangu wana bahati iliyoje."
Jack alicheka. "Jack unachekea nini? Funga domo lako!" Alvin alionya kwa mshtuko.
"Nimekosea? Bdo unaendelea kunishangaza sana broo. Kwanza, badala ya kutibiwa hospitalini, unatibiwa kwenye chumba cha hoteli na ex wako. Haha, sijawahi kusikia kuhusu mtaalamu yeyote anayetibu hivi. Jiangalie, broo,” Jack alijibu bila kujali.
“Kwanini unaendelea kukazia fikira jambo hili? Kila mwanasaikolojia ana njia yake mwenyewe ya kuwatibu wagonjwa.” Sura ya papara ilivuka uso wa Alvin,
"Sawa, unaweza kuwa huna nia mbaya, lakini una uhakika gani kwamba Sarah hana hisia na wewe?" Jack alishtuka, “Kama haya yangetokea nyuma, nisingepata tabu kukukumbusha, hakika mimi ni mhuni, mimi pia si mtu mzuri. Lakini kama ningekuwa kwenye viatu vyako na mke wangu ni mjamzito, bila shaka ningejiweka mbali na wanawake wengine, sembuse ex wangu. Sababu inayonifanya niseme hivyo ni kwamba sitaki kuona wapwa zangu wakikua katika familia isiyokamilika. Ninaweza kuelewa aina hii ya maumivu, sawa?"
Sura ya Alvin ikabadilika, Lisa alimtazama Jack kwa kumshangaa, alikiri kuwa alikuwa na kinyongo dhidi yake, lakini kilitoweka wakati huo,
Jack na Alvin waliendelea kubishana wao kwa wao kwa muda mrefu. Baada ya kuona tukio hilo, tabasamu mwanana lilienea usoni mwa Lisa,
“Unatabasamu nini?” Jack aliuliza.
“Ni nadra sana kuwaona nyinyi wawili mkiongea kama hivi” Lisa akasema kwa ghafula, “Kwa kweli, nyinyi watu mnaweza kukubaliana, kusaidiana, na kusikilizana.”
Jack alisema, “Ni nani anaweza kuelewana na kichaa huyu?"
Alvin pia alisema, "Siwezi kuvumilia hata kusikia sauti yake."
Lisa alikosa la kusema. Baada ya yote walikuwa ni ndugu. Baada ya kumaliza kula nyama choma zaoi, wale watatu walirudi kwenye nyumba ya ya Mzee Kimaro.
Punde tu baada ya kuingia chumbani, ghafla Alvin alipokea simu kutoka kwa Rodney. "Alvin, ungewezaje kumuacha Sarah peke yake? Ungemrudisha nyumbani angalau. Wakati anaelekea nyumbani peke yake sasa hivi, mwendesha bodaboda alimpora na kumjeruhi."
Alvin alipigwa na butwaa, na uso wake ukakunjamana. “Sarah si ana gari?”
"Angekuwa na wakati gani wa kupata gari wakati ndo kwanza amerudi Nairobi?" Rodney aliongea kwa hasira, “Pia alikuwa amelowa nguo zote, nilipomuuliza kilichotokea alikataa kuniambia. Broo, umeenda mbali sana.”

Sura ya: 280

Alvin alikunja midomo yake kwa kuudhika. "Mtunze."
Baada ya simu kukatika, Lisa aligeuza kichwa na kumtazama Alvin. "Nini tatizo? Kuna kitu kilimpata Sarah?"
“Umesikia kila kitu?” Macho ya Alvin yaliangaza. Alikuwa amerekebisha sauti hadi kiwango cha chini kabisa, hivyo alishangaa kwamba kweli Lisa alisikia.
Hakusikia chochote, kwa kweli. Ilikuwa tu kwamba angeweza kufahamu mbinu za Sarah. Hakika, mwanamke huyo hakuwa rahisi.
Lisa alikoroma. “Siyo tu kwamba nilikisia kwa usahihi kwamba kuna jambo limemtokea, lakini pia nina uhakika kwamba Rodney ndiye aliyepiga simu hiyo. Rodney alikulaumu kwa kutompeleka Sarah nyumbani na alishangaa kwanini alikuwa amelowa, lakini Sarah hakumwambia ukweli.”
Alvin alipigwa na bumbuwazi hata akakaribia kutilia shaka kama masikio ya Lisa yalikuwa na kinasa sauti. Alikuwa amepunguza sauti hadi yeye mwenyewe akawa anasikia kwa shida, Lisa alisikiaje?
“Umejuaje?”
Lisa alikunja midomo yake. Kama ilivyotarajiwa, hisia zake zilikuwa sahihi. "Hata Lina alitumia mbinu kama hizo hapo awali. Sioni tofauti kati ya wasichana hawa wawili."
Alvin aliposikia hivyo alikunja uso.
Lisa alishtuka. “Kwanza kabisa, utaingiwa na huruma kwa vile kuna jambo limemtokea. Pili, hakumwambia Rodney kuwa ni mimi niliyemwagia mvinyo hivyo utamuona ni mwanamke muelewa. Kwa kawaida wanawake hujifanya wavumilivu ili kumvutia umakini wa mwanamume.”
Alvin akalipapasa paji la uso wake na kusema. “Lisa, najua humpendi Sarah, lakini humjui vya kutosha—”
“Sawa. Najua yeye ni mkarimu. Huenda umemfahamu kwa zaidi ya miaka kumi, wakati mimi ndiyo nimemuona kwa mara ya kwanza usiku wa leo. Hutajisikia vizuri kwamba ninamkashifu mpenzi wako wa kwanza ambaye hukuweza kumsahau milele.” Lisa aliitikisa kichwa. “Lakini samahani. Kwa macho yangu, yeye ni mwanamke ambaye anaweza kumpokonya mume wangu na kuharibu familia ya watoto wangu.”
“Kwanini huniamini?” Alvin alikuwa akichemka kwa hasira. "Kwa maana hiyo mimi ni mtu asiyewajibika kwako?"
"Uaminifu unapatikana kwa kujengwa tu. Umefanya nini ili kuujenga? Ilikuwa Maurine hapo awali na Sarah sasa.” Lisa hakuweza kujizuia kuongeza, “Ulienda naye hotelini jana, na nimekukuta naye pia hotelini leo. Ninyi wawili mmekuwa mkitumia muda mwingi pamoja na huwa hurudi nyumbani. Nitajisikiaje?”
Alvin alipigwa na butwaa. “Umejuaje…”
“Watu wengi waliwaona mkijachia tu. Walituma hata picha zenu kwenye simu yangu. Niambie jinsi ninavyopaswa kujisikia ikiwa kila mtu huko mtaani anajua mpenzi wako amerudi na kisha wanakuona ukibadilisha naye tu viwanja kula bata.” Lisa alijifuta machozi usoni mwake. “Mimi ni mwanamke mjamzito. Kwanini huwezi kunifanya nijisikie salama zaidi? Unajua nilivyofadhaika nilipoziona hizo picha? Mbaya zaidi sikuweza kukupata hata kwenye simu.”
“Nilikuwa tu nikijadiliana naye kuhusu hali ya ugonjwa wangu pale hotelini asubuhi hiyo. Hatukufanya lolote lingine.” Alvin alinyoosha mikono kumkumbatia huku akiwa na hofu kubwa.
Hata hivyo, Lisa alimsukuma mbali. “Usinishike. Nasikia harufu ya mwanamke mwingine juu yako. Inanichukiza.”
"Nilianza lini kunuka harufu ya mwanamke mwingine?" Alvin aliinamisha kichwa chini na kunusa mwili wake. Papo hapo aligundua harufu yake hafifu, sura yake ilibadilika kidogo. “Nitaenda kuoga.”
Lisa aligeuza uso wake mbali naye, hakujisumbua kumtazama tena. Haikuwa nia yake kumwaga machozi. Hata hivyo, Alvin alihisi kana kwamba Lisa alikuwa amebadilika na kuwa mtu tofauti tangu alipopata mimba. Alianza kuwa na wasiwasi juu ya kila kitu hata kama ni kidogo tu.
Alvin akahema. Moja kwa moja akavua nguo zake mbele yake.
"Unafanya nini?" Lisa alipigwa na butwaa. Uso wake ulijawa na hasira na aibu. Ingawa walikuwa wanandoa, hakuweza kuvumilia kumwona uchi chini ya mwanga mkali.
“Unaweza kuangalia mwili wangu ili kuona kama kuna dalili zozote za kulala na mwanamke. Mimi sina hatia.” Alvin akanyoosha mikono yake na kugeuka mbele ya Lisa.
Lisa hakuweza kuendelea kumtazama. Alisimama kwa haraka na kumsukuma mbali.

“Acha kulia mpenzi wangu. Ukilia utaniliza na mimi.” Alvin alichukua nafasi hiyo kumvuta mikononi mwake na kumkanda busu usoni mwake. Baada ya hapo, alisema bila aibu, "Kila mara unanituhumu bila kupata ukweli wako. Sarah alikuwa ni mpenzi wangu, lakini kwa sasa anajua nina mke. Ana wajibu wa kunitibu tu kwa sasa.”
"Alvin, nachukia tabia yako hii." Lisa aliinua mikono yake na kumpiga. Hakujisikia vizuri. Badala yake, alihisi huzuni zaidi na kulia kwa uchungu zaidi. “Sikubali kukutana na Sarah."
"Hilo haliwezekani, mpenzi." Tabasamu la uchungu likaangaza usoni mwa Alvin. "Ninahofia ni yeye pekee anayeweza kutibu ugonjwa wangu. Unataka niugue ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu nikiwa na umri mdogo na kukusahau wewe na watoto wetu?”
Lisa aliuma mdomo kwa uchungu. “Siwezi kuvumilia nyinyi mkitumia muda mwingi pamoja kila wakati. La sivyo… bora umuoe tu nijue moja, nami nitaangalia ustaarabu mwingine.”
Alvin alibana mashavu yake kwa nguvu. “Wewe ni mke king’ang’anizi kiasi gani? Sikutambua hilo mapema.”
Lisa alimkazia macho. "Alvin, unahitaji kuelewa kuwa nisingekujali kama sio watoto."
"Unamaanisha nini?" Macho ya Alvin yalimkazia. "Kwa hiyo umekaa nami kwa sababu ya watoto tu?"
“Fikiria ulichofanya. Mwanzoni, ulimweka Maurine kando yako, na sasa una Sarah pamoja nawe. Ninahisi kuchoka. Sijui mapenzi yangu kwako yatadumu kwa muda gani,” Lisa alisema ukweli wake kwa uchungu.
Alvin alisikitika sana. Hakutarajia kwamba Sarah angegeuka kuwa mwanasaikolojia wake pia.
Baada ya kusema hivyo, kwa kweli hakuwa na nia ya kurudiana na Sarah. “Nimekuelewa, babe.” Kisha akaelekea bafuni.
Wakati Alvin anatoka bafuni, Lisa alikuwa tayari amejilaza kitandani. Aliendelea kujirusha huku na kule huku akipata shida kupata usingizi.
Alvin akajilaza kitandani na kumzungushia mikono yake. “Sitalala nje ya chumba hiki leo. Nataka kulala na wewe.” Lisa aligeuza mwili wake na kumpuuza. "Ninashuku kuwa tumekuwa tukigombana siku hizi hasa kwa sababu tunalala tofauti sasa. Kama wanandoa, tunahitaji kuwa karibu ili kuboresha uhusiano wetu.” Kwa hayo, Alvin akambusu usoni.
Hapo awali, alipanga tu kumpa busu. Hata hivyo, aliishia kumbusu kwa muda mrefu kuliko alivyopanga, labda kwa sababu hakuwa na uhusiano wa karibu sana naye kwa muda mrefu sana.
Lisa aliduwaa huku akimbusu. Nusu ya moyo wake ilimkataa huku nusu nyingine ikienda pamoja naye. Kwa hayo, Alvin akanogewa. Kweli, walikuwa wamegombana lakini walikuwa wakibiringishana kwa mahaba mazito pale kitandani kama wapenzi waliokamiana kwa muda mrefu.
Siku iliyofuata, hatimaye Lisa alikuwa akijisikia vizuri baada ya kulala vizuri. Hakika, Sarah alikuwa amekuja, na alionekana kumhitaji Alvin. Ilipokuja suala la kushughulika na mwanamke wa aina hii, Lisa alipaswa kuwa jeurikuliko yeye.
Ikiwa hilo lingetokea mapema, Lisa angeweza kuachana na uhusiano huo usio na utulivu. Sasa kwa kuwa alikuwa mjamzito, ilimbidi ailinde familia yake. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kumpambania Alvin wake.
Baada ya kutafakari kwa muda, aligeuza mwili wake na kumwambia Alvin, “Kuanzia leo na kuendelea, nitatembelea ofisi kwako mara kwa mara. Kila siku nafungiwa humu ndani, sina pa kwenda na huwa nafikiria kupita kiasi, jambo ambalo linanisababishia mfadhaiko. Naweza kuwaathiri watoto waliomo tumboni.”
Alvin alikunja uso na alikuwa na wasiwasi juu yake. “Lakini—”
“Nimechoshwa na kufikiria juu yako kila wakati. Ulipokosa kurudi siku zile, nilijiuliza labda umeangukia kwamwanamke mwingine, au labda hunipendi kwa kuwa mimi ni mjamzito, na hunipendi kwa kuwa na wivu. Itaendelea kuishi katika mazingira kama hayo tena.” Lisa alikatisha sentensi yake. Sauti yake ilijaa dhiki.
Alvin akashusha pumzi. Baada ya kufikiria migogoro waliyokuwa nayo kwa siku kadhaa, hakutaka kupingana naye. “Sawa.”
TUKUTANE KURASA 281-285

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.............LISA
KURASA........281-285

Sura ya: 281

“Pia, huruhusiwi kutumia muda mwingi na Sarah peke yako isipokuwa unapoenda kutibiwa. Najua Rodney na Chester wako kwenye uhusiano wa kirafiki, kwa hivyo watakutana mara nyingi. Mkikutana nyinyi wanne wakati ujao, lazima na mimi niwepo.”
Lisa aliuzika uso wake kwenye kifua cha Alvin kwa sura ya kupendeza.
Ilikuwa ni muda mrefu tangu aongee kwa upole hivyo mbele ya Alvin. Akawa na moyo mpole na kuchanganyikiwa mara moja. “Lakini Rodney na Chester—”
“Najua hawanipendi, lakini ni sawa. Ninaweza kuvumilia maadamu nitaweza kuzuia mume wangu asinyang’anywe na mwanamke mwingine.” Lisa aliinua kichwa chake na kupepesa macho yake makubwa ya kupendeza. “Ni kwa sababu wewe ni mzuri sana. Nakupenda."
“Babe, nitakusikiliza.” Macho ya Alvin yakaangaza. Akainamisha kichwa chake na kumbusu kwenye midomo.
Akashusha pumzi huku akiwa ametawaliwa kabisa na mahaba ya yule mwanamke. Katika hali hiyo, jambo gani lingeweza kutokea kati ya Sara na yeye? Lakini, haikujalisha. Maadam alitaka kuwa naye anapokuwa pamoja na marafiki zake, ilibidi amkubalie mradi tu alikuwa na furaha.
Alvin aliamka na kuelekea sebuleni huku mkono wake ukiwa umeshika kiuno cha Lisa. Mdomo wa Lisa ulikuwa umevimba kidogo, na mashavu yake yalikuwa yamepauka.
Akiwa na uzoefu wa miaka mingi wa mambo kama hayo yeye mwenyewe, Bibi Kimaro hakuwa mgeni juu ya kile kilichotokea kwao baada ya kuwaona asubuhi wakiwa vile. Alifarijika na kuwa na wasiwasikwa wakati mmoja. “Hivi ndivyo nyinyi wawili mnapaswa kuishi kama wanandoa. Lakini mnapaswa kuwa waangalifu. Daktari alisema hivyo hospitalini—”
“Hatukufanya chochote, Bibi. Sio lazima uendelee kunikumbusha. Mimi si mtoto.” Uso wa Alvin ulisinyaa baada ya kusikia maneno hayo, huku Lisa akitamani ardhi immeze.
Moyoni mwake, Jack alikuwa akionyesha kutoridhika kwake wakati anapata kifungua kinywa chake. Alvin na Lisa walikuwa na mzozo mkali jana yake, lakini walionekana kuwa na uhusiano mzuri asubuhi hiyo kama mbaazi mbili kwenye ganda moja. Kweli mambo ya wapendanao usipende kuyafungia kibwewbwe.
Jack hakuwa na uhakika kama ni Alvin ndiye alikuwa mtaalam wa kutuliza wanawake, au Lisa alikuwa mtaalam wa kushughulika na wanaume. Lakini, wanandoa hao kweli walikuwa wataalam.
"Halafu, nilisikia kuwa ninyi watatu mmerudi pamoja jana usiku," Mzee Kimaro ghafla aliuliza. “Mlikuwa wapi usiku huo?”
"Khooh, khohooh!" Jack karibu apaliwe sandwich yake.
Alvin alimtazama kwa hasira. "Lisa alinikuwa ameni’miss, kwa hivyo Jack alimleta kunitembelea nyumbani kwangu jana. Tulikula chakula cha jioni pamoja kabla ya kurudi nyumbani.”
Kwa hayo, Lisa alikanyaga mguu wake. Alimm’miss? Ha! Hakuwa na aibu kama nini kusema uwongo kama huo. Kwa kweli, alikuwa ameenda kumfumania kama alikuwa kitandani na Sarah.
Alvin alimtazama kwa jicho la huzuni. Hata hivyo, Lisa alitazama pembeni na kumpuuza.
Mzee Kimaro hakuona mkanganyiko wao na hivyo alitikisa kichwa kwa hali ya utulivu. "Sikutarajia kwamba ungeenda kula chakula cha jioni na Jack."
Jack alikoroma. "Ni Shemeji ndiye aliyeomba, vinginevyo nisingekula naye chakula cha jioni."
Bibi Kimaro alikodoa macho. Alifurahi kwamba Lisa alikuwa amefaulu kuwapatanisha ndugu wale mahasimu. “Hiyo ni nzuri. Kama ndugu, mnapaswa kuungana katika hatua hii. Hatima imewafunga nyinyi kwa damu, kwa hivyo mnapaswa kuthamini udugu wenu milele.”
Alvin na Jack wote walivuta nyuso ndefu. Hawakuthamini kifungo chao cha damu hata kidogo.
Baada ya kiamsha kinywa, Lisa alisema, “Bibi, mwanasaikolojia wa Alvin atakuja nyumbani kumtibu. Unafikiri matibabu yanapaswa kufanyika wapi? Na pia, nadhani unamjua mwanasaikolojia mwenyewe. Yeye ni Sarah Langa Njau.
Mshindo ukasikika! Kijiko katika mkono wa Bibi Kimaro kilianguka kwenye meza. Aliuliza kwa msisimko, “Si amekufa?”
“Hapana, amerudi. Hakuwa amekufa, ila tu kuna mkanyiko ulitokea.” Alvin alieleza.
Mzee Kimaro alikunja zaidi uso wake. Alikuwa amekutana na Sarah enzi hizo na hakumpenda zaidi kuliko Lisa. “Je, hakuna wanasaikolojia wengine duniani? Kwanini ni lazima umwambie Sarah atibu ugonjwa wako? Tafuta mtu mwingine."

Bii Kimaro aliitikia kwa kichwa. “Hasa. Unawezaje kumwomba mpenzi wako wa zamani akutibu? Umewahi kufikiria hisia za mkeo?”
Lisa akashusha pumzi. Kwa mwonekano wake, Bibi Kimaro na Mzee Kimaro hawakuwa wakimpenda Sarah.
Tabasamu la uchungu likatokea usoni mwa Alvin. "Chester alisema kuwa yeye ndiye mwanasaikolojia mahiri zaidi nchini Ujerumani. Nilipomwomba aje hapo awali, sikutarajia angekuwa Sarah pia.”
Mzee Kimaro alikaa kimya kwa muda kabla hajakubali kwa kichwa. "Sawa, lakini lazima uwe mwangalifu na tabia yako. Usipotee. Natumai hutafuata nyayo za mama yako.”
'Bila shaka sitaweza, babu." Alvin akaitikia kwa kichwa.
Akiwa njiani kuelekea ofisini, alimpigia simu Sarah ili wazungumze kuhusu eneo la matibabu yake.
“Kwa kweli nilitarajia hii. Nitakutibia kwa Mzee Kimaro, basi. Lakini babu na bibi yako hawakunipenda kabisa kipindi kile. Ninaogopa—”
“Nimewajulisha kuhusu hilo. Wanaelewa.”
“Sawa basi.” Sarah alinyamaza kwa muda kabla ya kuendelea, “Kusema kweli, nilikuja na mpango wa kutibu ugonjwa wako katika mazingira ya awali. Sasa kwa kuwa eneo limebadilishwa, lazima nipange upya kila kitu. Katika hali hii, huenda usiweze kupona haraka kama tulivyopanga. Natumai umeelewa.”
Alvin alikunja uso. Bila shaka, alitarajia kupona haraka iwezekanavyo. Hata hivyo, kwa kuwa ilimsumbua Lisa kwamba alikuwa peke yake na Sarah, hakuweza kufanya chochote kuhusu hilo. “Sawa basi. By the way, ulikuwa sawa jana usiku? Mbona hukuniambia kuwa hukuwa na gari? Ningemwomba dereva wangu akupeleke nyumbani.”
“Siyo ishu kubwa. Ungeendelea kunijali zaidi jana usiku, ndivyo mke wako angetuelewa vibaya zaidi,” Sarah alisema kwa sauti ya chini, “Sitaki kuharibu uhusiano mzuri ambao uko nao na mkeo hatimaye.”
Alvin alijikandamiza kwenye paji la uso wake. “Sarah, unaweza kuwa na furaha pia. Cha kusikitisha ni kwamba hatujapangiwa kuwa pamoja, lakini kuna mtu ambaye amekuwa akikujali sana tangu zamani…”
“Unamaanisha… Rodney?” Sarah alifungua kinywa chake na kusema kwa hisia mseto.
“Mm. Kwa kweli, amekuangukia kwa muda mrefu.”
"Hapana. Rodney anastahili mtu bora zaidi. Wanawake waliochafuliwa kama mimi hawastahili kuwa naye. Hebu tuishie hapa. Unaweza kuendelea na mambo yako. Nitakutana na wewe kkwa babu yako usiku wa leo."
Alvin alishusha pumzi baada ya kukata simu. Alitumaini kwamba Sarah hatimaye angempata mpenzi wa kumweka busy. Kwa njia hii, Lisa asingeweza kuwa na wasiwasi juu yake baada ya kujua kwamba Sarah ana mpenzi.
•••
Akiwa katika ofisi yake ndani ya kampuni ya Mawenzi, baada ya kuangalia utendaji wa kampuni ofisini, Lisa aligundua kuwa kampuni hiyo imefanya vizuri zaidi licha ya kutokuwepo kwake kwa siku kadhaa.
Meneja Mkuu alisema kwa tabasamu, "Bwana Kimaro kwa hakika anastahili kutambulika kama mtu tajiri zaidi nchini Kenya na talanta yake ya ajabu katika mambo ya biashara. Licha ya kutumia muda mfupi kushughulika na mambo ya Mawenzi, aliiingizia kampuni hiyo mapato makubwa kwa kutoa maagizo machache tu. Mauzo ya bidhaa yameongezeka kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea.
Lisa alijikuta anaingiwa na wivu. Sio tu kwamba Alvin alikuwa mzuri, lakini pia alikuwa na kipaji cha biashara zaidi kuliko wengine. Jinsi gani alipendelewa! Jambo hilo lilimfanya Lisa, ambaye alikuwa mkurugenzi wa kampuni hiyo, ahisi kana kwamba hahitajiki.
"Pamoja na hayo, kampuni yetu imekuwa hapa Nairobi kwa karibu nusu mwaka. Kando na ujenzi wa ofisi zetu mpya hapa Nairobi, kwanini hakuna miradi ya ujenzi kwenye mikoa mingine?” Lisa aliuliza kwa kutoridhika.
Meneja Mkuu alilazimisha tabasamu. “Mwenyekiti Jones, Baada ya kampuni ya Ngosha kuungana na Campos Ltd. Wamekuwa na kiburi sana. Melanie sasa ni naibu Mkurugenzi mkuu na amekuwa akitufuatilia sana. Amekuwa akipandilia bei kila eneo tunalotaka kununua huko mikoani na hivyo kuharibu biashara.”
Lisa aliinua uso wake na kugonga meza kwa upole. "Sawa. Hakuna haraka."
Angesubiri tu aone Melanie bado angeweza kuwa na jeuri baada ya taarifa za Melanie kutokuwa binti Joel kufichuka.

Sura ya: 282

“Halafu, Mkurugenzi mpaya wa kampuni ya New Era Advertisings amechaguliwa leo tu. Amekuletea mwaliko wa kushiriki party ya kumpongeza.” Meneja Mkuu alimkumbusha Lisa.
Lisa alipigwa na butwaa. "Nani huyo?"
"Thomas Njau, mtoto mkubwa wa Boris Langa Njau na mke wake wa zamani.” Meneja Mkuu alieleza. “Hapo awali, nilisikia kwamba New Era Advertisings ilinyimwa nafasi ya kuuza matangazo yao kwenye mtandao wa Alvinarah Media Network Group na KIM Outdoor hivyo kukaribia kufilisika baada ya kupoteza wateja wao wote. Lakini cha kushangaza, AMEN Group na KIM Outdoor wamekubali kuwapa nafasi ya kuendelea kufanya nao biashara hivi punde mara tu Thomas alipochukua kampuni hiyo.
Hali ya Lisa ikabadilika kidogo. Aligundua kila kitu ndani ya muda mfupi. Thomas Njau, yule mwanaharamu, alichukua nafasi hiyo mara tu baada ya Charity Njau kuhukumiwa kifungo cha maisha. Bila kupepesa macho Alvin na Sarah walikuwa na mkono katika uamuzi huo.
Haijalishi ni kiasi gani Lisa na Charity walikuwa wamemsihi Alvin wakati huo, alikataa katakata kuiruhusu New Era Advertisings kuchomoka kwenye ndoano. Hata hivyo, sasa Sarah alikuwa amerudi, Thomas akawa Mkurugenzi wa kampuni na kupewa nafasi ya kuendelea na biashara.
'Alvin, oh Alvin, unaweza usiwe na wazo la kurudiana na Sarah, lakini bado ana nafasi ya pekee moyoni mwako.’ Lisa alijiwazia. Kama si Lisa ambaye alikuwa mjamzito, pengine Alvin angempa umuhimu zaidi Sarah kuliko yeye. Lisa akashusha pumzi ndefu. Alilazimika kudhibiti hisia zake kwa ajili ya watoto wake.
Akiwa katika mawazo yake, alipokea ujumbe wa WhatsApp kutoka kwa 'Ni Wako Pekee'. [Babe, uko sawa katika siku yako ya kwanza ya kazi? Una njaa? Unataka kula nini? Nitamwomba Hans akuletee chakula.]
'Jamani wewe, mpuuzi. Nenda kafie mbele huko!' Lisa alitamani kumwambia maneno hayo lakini bila kupenda akayazuia kwenye mawazo yake. Aliitupa simu yake na hakutamani hata kujibu ujumbe huo.
Dakika kumi baadaye, Alvin alimpigia simu. “Babe, kwa nini hukujibu ujumbe wangu?”
"Sikutaka kujibu." Lisa alitamani sana kuficha kinyongo chake dhidi ya Alvin, lakini alikasirika sana hivi kwamba alishindwa kufanya hivyo.
"Nini tatizo?" Alvin alichanganyikiwa. "Kuna mtu katika kampuni amekukosea?"
“Umeniudhi.” Kwa hasira, Lisa aliongeza, “Kwanini ulimruhusu Thomas kuchukua nafasi ya Mkurugenzi wa New Era Advertisings? Unajua kwamba alinidhalilisha katika baa wakati huo na kufanya yale matendo maovu ambayo yalikaribia kumfanya Zigi aniue? Lakini umeamua kumsikiliza Sarah na kumsaidia Thomas haijalishi ni mwovu kiasi gani, sivyo? Hapo awali, uliahidi kwamba hautamjali tena. Umesahau kuhusu hilo tayari?"
Alvin kichwa kilianza kumuuma. "Nilikuwa nalipa somo New Era Advertisings hasa kwa sababu ya Charity-"
"Sawa. Kabla ya hili, ulikuwa ukitaka kuharibu New Era Advertisings. Sasa Sarah amerudi, umesitisha mipango yako yote. Nina hakika alikubembelezai. Alipokusihi, ulikubaliana naye. Lakini nilipokusihi, ulikataa. Mke wako ni nani hapa?"
"Lisa, tutabishana tena juu ya hili? Mbona siku zote unataka kunichokoza tu? Kwani utakuwaje ikiwa utaachana na mambo ya familia ya Njau?” Alvin aliongea kwa ukali kidogo.
Lisa akakata simu. Alijiona si muhimu kama Sarah katika moyo wa Alvin. Aliumia sana moyoni hata akakaribia kutokwa na machozi. Hata hivyo, hakutaka kulia kwa sababu yake tena. Hakustahili machozi yake.
Alasiri, Lisa alienda hospitali kumtembelea Joel. Daktari Angelo alimweleza kipande cha habari njema. "Baba yako anaweza kupata fahamu baada ya miezi miwili."
“Kweli?” Lisa alifurahi sana. Ilikuwa habari nzuri zaidi ambayo alikuwa amesikia kwa kipindi hicho.
Lisa hakuwahi kutamani uwepo wa Joel zaidi ya wakati huu. Alitamani sana apate fahamu ili angalau awe na mwanafamilia wa kumtegemea.
“Baba naomba uamke upesi. Ninateseka, na ninakukumbuka sana.”
Matone yake ya machozi yalitua nyuma ya mkono wa Joel. Hakuona kwamba vidole vyake vinatetemeka.
Baadaye, alienda kumwangalia Boris Langa katika wadi nyingine ya hospitali. Aligundua alipokuwa akiingia ndani kwamba mtu huyo alikuwa akihangaika kufikia beseni chini ya kitanda.

"Mjomba Boris, niruhusu nikusaidie." Haraka akasogea kumshika mkono. "Mimi ni rafiki wa Charity."
“Asante.” Akalipokea lile beseni huku akionekana kuwa na aibu kidogo. Lisa akatoka kidogo kumuachia faragha.
Dakika kadhaa baadaye, Lisa alirudi na kwenda kumimina yaliyokuwamo kwenye beseni ndani ya sinki la choo.
"Mjomba Boris, mbona uko peke yako? Aunty Jennifer na mlezi wako wapi?
“Mlezi hakuwa na nafasi asubuhi ya leo, na Jennifer aliondoka nyumbani kwenda kufungasha mizigo yetu. Alisema anataka kunihamisha hadi hospitali nyingine huko Dar es Salaam. Lakinitangu aondoke hajafika na siwezi kumpata kwa simu pia.” Alisikika akiwa na wasiwasi. “Natamani kwenda kumtafuta lakini siwezi katika hali hii. Kwa bahati nzuri, Pamela alifika hapo awali kwa hivyo nilimwomba amchunguze Jennifer.”
Lisa alikuwa na hisia mbaya na ghafla akakumbuka ombi la Charity la kuwatoa wazazi wake kutoka Nairobi haraka iwezekanavyo. “Vipi kuhusu mwanao? Au Sarah? Alirudi si muda mrefu uliopita. Si alikuja kukuchunga?”
“Sarah?” Boris alionekana kushtuka. “Si amekufa?”
“Nadhani bado hujui kwamba hajafa. Hata nilikutana naye ana kwa ana.”
Hakuwa na la kusema. Sarah alikuwa na muda wa kuhudhuria mazishi ya Maurine na wala hata hakumtembelea baba yake mzazi ambaye alikuwa amelazwa hospitalini kwa siku chache. Hakupaswa kuwa hivi hata kama baba yake alikuwa ameoa mwanamke mwingine.
'Kwa kweli sikuwa na wazo.” Alitikisa kichwa kwa unyonge huku tabasamu la uchungu likitanda usoni mwake. "Hata hivyo, sitarajii chochote kutoka kwa hao watoto wangu wawili. Tangu mwanzo nimekuwa nikiwategemea Charity na Jennifer, lakini sasa Charity yuko ndani…” Machozi yalimtoka. "Kabla polisi hawajaja kumkata, niilikuwa tnikimwambia Charity mchana huo kwamba tunapaswa kuuza kampuni na kuondoka Nairobi kabla hatujafilisika kabisa ..."
Lisa aliuliza baada ya kusita kidogo, "Unajua kwamba Thomas amechukua New Era Advertisings?"
“Thomas?” Mshangao ulimwagika usoni mwake kabla ya kutikisa kichwa. “Huyo mpuuzi hana uwezo wa kuendesha kampuni. Majuto yangu makubwa katika maisha haya ni kumzaa mtoto huyu. Amefanya mambo mengi ya kutisha katika maisha yake lakini kwanini hajafungwa gerezani? Atakuwa mbaya zaidi baada ya kuwa Mkurugenzi."
Hilo lilimshangaza Lisa. Hakujua kuwa Boris hakuridhika na mtoto wake, ingawa kwa mawazo ya pili, alikuwa akisema ukweli tu. Sekunde chache baadaye, Boris alishusha pumzi ndefu na kutikisa mkono wake hewani. “Sawa, mimi sijali kuhusu biashara tena. Ninachotaka sasa ni kuondoka Nairobi na Jennifer. Tunaweza kujaribu tuwezavyo kumtoa Charity gerezani. Ninajua kwa hakika kwamba hana hatia. Hakuwa na sababu ya kumuumiza Maurine. Walikuwa marafiki na walicheza pamoja tangu walipokuwa wadogo…”
Lisa aliuliza kwa kusitasita, “Kwa hiyo, wewe pia huna uhusiano mzuri na Sarah? Vinginevyo, kwa nini hajaja kukuona…”
Kimya kirefu kilipita hadi Lisa akajishtukia kwa kumuuliza swali hilo. "Samahani. Huna budi kujibu hili…”
“Ni sawa. Labda ananilaumu kwa kuoa tena.” Alitabasamu kwa uchungu. “Sikuwa na namna nyingine. Wakati huo nilikuwa busy sana na kazi na mama yake Sarah alikuwa akinisaliti na wanaume wengine nyuma yangu. Sikuweza kuvumilia tena na mwishowe nikampa talaka. Lakini ili kuhakikisha watoto hao wawili wangekua katika mazingira yenye afya, sikuwahi kumsema vibaya mke wangu wa zamani hata mara moja. Labda walidhani mimi ndiye niliyemsaliti mama yao na polepole wakajitenga nami kwa sababu hiyo. Kwa kweli, Jennifer aliwajali kama watoto wake lakini wao hawakuthamini upendo wake—kama vile mama yao.”
Lisa alishangaa kujua hivyo. Ilionekana kuwa Boris pia alikuwa na hali ngumu. Ni wazi kwamba Sarah na kaka yake hawakuwa watu wazuri lakini Alvin na marafiki zake hawakuliona hilo. Jambo hili lilimvunja moyo sana Lisa.
Muda si mrefu, Pamela alimpigia simu. “Lisa, kuna kitu kibaya kimetokea. Mama yake Charity amekufa.”
Lisa alipigwa na butwaa na kukaa kimya. Alijilazimisha kuitikia kwa utulivu kabla ya kutoka nje ya wodi.

Sura ya: 283

“Ooh! Mungu wangu, ni kosa letu. Hatukuwa makini,” Lisa alinong’ona kwa masikitiko.
'Ni kweli." Pamela alikasirika. “Mjomba Boris alisema kuwa hakuweza kuwasiliana na Aunty Jennifer tangu alipoondoka nyumbani asubuhi ya leo kwenda kufungasha, kwa hiyo nilikuja kumtafuta nyumbani kwao. Watumishi wao wote walikuwa wameondoka na ilinibidi kupanda juu ya ukuta ili niingie. Alikuwa amelala kwenye dimbwi la damu kwenye sakafu ya bafuni na alikuwa ameacha kupumua nilipomkuta. Polisi walikuja hapo awali na kusema lazima alianguka na kugonga kichwa chake chini. Wanafikiri alikufa baada ya kupoteza damu nyingi.”
“Inawezekanaje?” Lisa alisisimka hadi kwenye uti wa mgongo wake. "Alionekana kuwa mzima kabisa, angewezaje kuanguka bila sabau. Uliangalia kamera za uchunguzi?"
"Kamera zote zimezimwa tangu juzi," Pamela alijibu, "Lakini niliangalia kamera za cctv za nyumba ya jirani. Sarah alionekana akiingia asubuhi ya leo lakini aliondoka baada ya nusu saa.”
Lisa alikuwa anatetemeka kwa hofu na hasira. “Hakika anahusika katika hili. Anamchukia Aunty Jennifer.”
"Najua, lakini daktari wa magonjwa alisema haina uhusiano wowote na mauaji ya kupangwa. Hawakuweza kupata alama za vidole vya mtu mwingine wala dalili inayoonyesha kuwa ameuawa. Mbali na hilo, Aunty Jennifer inakadiriwa kuwa alifariki majira ya saa 9:00 asubuhi lakini Sarah alitoka nyumbani saa 8:30 asubuhi”
Baada ya kimya kifupi cha pande zote, Pamela alisema huku midomo ikimtetemeka, “Lisa, nilisoma hapo awali kwamba baadhi ya wanasaikolojia wanatisha kwani wanaweza kutumia njia ya hypnosis kumpumbaza mtu ili…”
“Unamaanisha… Sarah alimpumbaza kisaikolojia Aunty Jennifer?” Lisa alikuwa akitetemeka mwili mzima.
“Hilo linawezekana. Angeweza kumpambuza Aunty Jennifer katika hali ya nusu fahamu ili aanguke kwa bahati mbaya. Kwa njia hii, hakutakuwa na ushahidi wowote unaoelekeza kwa Sarah kama muuaji.”
Lisa alisugua paji la uso wake. Kifo cha Jennifer kilitia shaka sana. Charity angejisikia vibaya kiasi gani ikiwa angejua kuhusu jambo hilo akiwa gerezani? Boris pia. Angeachwa peke yake bila mtu kando yake. “Wacha tujaribu tuwezavyo kumficha mjomba Boris hili kwa sasa. Ninaogopa hataweza kuchukua habari hii kwa sasa. Tunapaswa kuingilia kati na kushughulikia mazishi ya Aunty Jennifer.”
•••
Saa mbili usiku Lisa alirudi kwa Mzee Kimaro akiwa amechoka. Alipoingia tu mlangoni, akawaona Alvin na Sarah wakiteremka kwenye ngazi wakiwa wamekaribiana. Mwanamume alikuwa amevalia nguo za mapumziko zenye mistari myeusi na myeupe. Nywele zilizostawi kwenye kichwa chake zilifanya macho yake ya ukali yaonekane laini na tulivu. Mwanamke, kwa upande mwingine, alikuwa amevalia suruali ya jeans ya kubana na kitop kilichofichua kiuno chake chembamba na ngozi nyororo. Ilionekana kana kwamba walikuwa wamiliki wa nyumba hiyo. Lisa alikosa raha kuona jambo hili. Alikuwa mrembo sana kuliko Sarah lakini ngozi yake haikuwa katika hali yake nzuri tangu kuharibika.
“Bi. Kimaro, umerudi. Tumemaliza matibabu ya leo kwa Alvinic,” Sarah aliongea kwanza kwa sauti ya upole.
“Unajua ni saa ngapi sasa hivi? Tayari saa usiku ndiyo unarudi. Baada ya kukuruhusu urudi kazin tayari ushaanza kuruka ratiba ya chakula cha jioni nyumbani.” Alvin alikunja uso, akionekana kuchukizwa. Yeye ndiye alitaka Sarah amtibu pale nyumbani lakini alifika tu nyumbani baada ya matibabu yake kuisha.
“Alvinic, usiseme hivyo. Wanawake wanahitaji kuwa na uhuru wao pia,” Sarah alisema huku akitabasamu.
Lisa alihisi kukasirishwa na sauti zao. "Bi Njau, umesikia kwamba mama yako wa kambo amefariki bafuni leo?"
“Nilisikia…” Macho ya Sarah yalimtoka. "Nilienda kumsalimia tu asubuhi ya leo na muda mfupi baadaye, nikasikia taarifa za kifo chake.”

“Kweli?” Kengere ya tahadhari iligonga kichwani mwa Lisa huku akikumbushwa ghafla dhana ya Pamela. Mwanamke huyu alitisha. "Nilienda kumtembelea baba yako hospitalini leo. Anatia huruma sana. Alikuwa anamtegemea tu mkewe llakini naye amekufa na hakuna mtu wa kumtunza. Hata alikuwa akihangaika kuchukua beseni la kujisaidia peke yake. Wewe na kaka yako mmefanikiwa na ni matajiri sasa. Angalau mnapaswa kumwajiri mlezi hata kama humpendi baba yako.”
“Uko sahihi. Mimi si binti bora.” Sarah alionekana kujuta.
"Kweli, hajui kuwa umejitahidi kwa kadri anavyoweza?" Alvin alimtazama Lisa kwa sura ya kuchukizwa kidogo baada ya kusema vile. “Lisa, hayo ni mambo yao ya kifamilia. Hujui mengi kuhusu hilo, na hupaswi kuingiza pua yako ndani yake pia. Sarah alikuwa amejaribu kuajiri mlezi lakini baba yake alimkataa. Nilimsikia akizungumza kuhusu hili mapema mchana wa leo. Anapanga kuandaa mazishi ya kifahari kwa mama yake wa kambo, unataka afanye nini zaidi ya hapo?”
Lisa alijisikia kumpiga Alvin kichwani alipoona jinsi alivyokuwa amechukua upande wa Sarah kabisa. Ina maana hakuona kwamba Sarah alikuwa ni mwanamke mjanja?
“Ni sawa, Alvinic. Inaonyesha kwamba Lisa ni mkarimu kwa vile anamjali rafiki yake. Niondoke sasa. Nahitaji kwenda kushughulikia mazishi ya kesho,” Sarah alisema huku akitabasamu kwa uchungu.
Lisa alikosa la kusema. Huenda Jennifer asingepumzika kwa amani ikiwa Sarah ndiye aliyekuwa akiandaa mazishi yake. "Hapana, mimi na Pamela tutashughulikia mazishi ya Aunty Jennifer."
“Usilete matatizo. Unaweza kufanya nini na tumbo lako kubwa la ujauzito?" Alvin alisema kwa hasira, "Wewe si binti ya Jennifer, kwa hivyo huwezi hata kushika maiti yake."
“Lisa, usijali. Nitalishughulikia hili.” Sarah alitabasamu.
Lisa aliuma mdomo. Angewezaje kutokuwa na wasiwasi? Sarah aliweza hata kuwa sababu ya kifo cha Jennifer. Mtu matata kama yeye hakika angemfanya Jennifer ashindwe kupumzika kwa amani.
Baada ya Sarah kuondoka, Lisa moja kwa moja alikataa kukubaliana na Alvin.
“Lisa, bado una hasira na mimi kuhusu kilichotokea asubuhi? Kwanini kila mara tunagombana kuhusu familia ya Njau? Nakuahidi nitakaa mbali na Sarah baada ya ugonjwa wangu kupona.” Alvin alimshika mkono.
Lisa aligeuka ghafla na kumtazama kwa hasira. “Alvin, unatambua kwamba huwa unamtetea sana Sarah anapokuwa karibu? Inafanya nionekane kama mimi ni mtu asiye na akili.”
Alijisikia huzuni. “Lisa, unaweza kuacha kunikera kila unapokutana na Sarah? Kwanini unajali sana mambo ya familia ya Njau?”
"Sawa, kwanini na wewe unamjali sana Sarah?" Akashusha pumzi ndefu kwani hakutaka kubishana naye. Baada ya yote, umbali kati yao uliongezeka zaidi baada ya kila mabishano. Hata hivyo, hakuweza kujizuia kulipiza kisasi baada ya kusikia maneno ya kijinga yaliyotoka kinywani mwake.
Lisa aliufunga mlango kwa nguvu huku akihisi kuishiwa nguvu. Hakuweza kufikiria jinsi Charity angehuzunika baada ya kujua kwamba mama yake alikuwa amefariki.
•••
Siku iliyofuata. Pamela alimpigia tena wakati Lisa anakula kifungua kinywa. "Lisa, mjomba Boris amekufa kwa mshtuko wa moyo asubuhi ya leo."
“Clang!” Kijiko alichokuwa ameshika kilianguka kwenye sahani.
Pamela akaendelea. “Nilipotoka kwenda kununua kifungua kinywa cha Mjomba Boris asubuhi ya leo, Thomas alifika na kumwambia kuhusu kifo cha Aunty Jennifer. Mjomba Boris alipata mshtuko wa moyo papo hapo na alikimbizwa kwa huduma ya dharura. Daktari alisema mjomba Boris amekufa baada ya kupoteza matumaini ya kuishi.” Pamela alianza kulia.
“Nakuja mara moja.” Lisa alisimama haraka na kuacha kula.
Alvin akamshika mkono. "Unaenda wapi? Keti na upate kifungua kinywa.”
Lisa aliusukuma mkono wake kwa nguvu na kumfokea kwa macho ya machozi, "Mjomba Boris amekufa! Thomas alienda hospitali na kumweleza kuhusu kifo cha Aunty Jennifer. Wenzi hao walipendana kwa mioyo yao yote. Huyo mjinga Thomas ndiye wa kulaumiwa kwa hili. Yote ni kwa sababu yako. Kwanini ulimsaidia mtu kama huyo? Hakuna jambo baya lingetokea kama angefungwa muda mrefu uliopita.”

Uso mzuri wa Alvin uliganda na Lisa akaendeleakumsomea. “Una furaha sasa? Charity amefungwa maisha na wazazi wake wote wamekufa. Hatimaye, Sarah na Thomas wako mpendwa ndio pekee waliosalia katika familia ya Njau.” Lisa alimtazama kwa masikitiko na kunyata bila kuangalia nyuma.

Sura ya: 284

Pamela alikuwa akibishana na ndugu wa Njau wodini wakati Lisa alipofika hospitalini baada ya muda mfupi sana.
"Ondoka mbele yangu, Pamela. Sina neno kama unataka kuchukua maiti ya baba yetu. Lakini kama kweli unataka…” Thomas alitania na kutabasamu kwa hasira. "Kubali kwanza kuwa mwanamke wangu na ninakuhakikishia kwamba unaweza kupanga mazishi ya baba yangu."
“Una akili kweli wewe, au laana inakusumbua? Baba yako amekufa tu lakini unacheka huku unawaza mapenzi?” Pamela alikasirika. "Asingekufa kama si wewe kumletea habari za kushtukiza."
“Kosa langu ni vipi?” Thomas akacheka tena kifedhuli. “Kujua ni lazima angejua tu hatakama nisingemwambia. Kama ni kufa angekufa mapema au baadaye,” alijibu, bila kujali. "Kwa kweli sioni hata maana ya kuwa na huzuni juu ya mzee huyo. Hakika alistahili hilo.”
“Thomas Njau, wewe ni shetani kabisa.” Pamela alishangaa kabisa. “Ni sawa kweli kumwambia maneno hayo mtu aliyekuleta katika ulimwengu huu na kukulea?”
“Ni kosa lake kwa kututelekeza na kuwa karibu na Jennifer na binti yake. Kwanza nimemfanyia upendeleo sana hata kuja kuchukua mwili wake leo.”
“Utapigwa na radi!” Kwa hasira, Pamela alimpiga ngumi ya kifua.
“Unathubutu vipi kunipiga ngumi? Mwanamke mjinga, nitakuchuna ukiwa hai!” Thomas akainua mkono kumpiga Pamela.
Lisa haraka alimkinga Pamela nyuma yake na kumtazama kwa jeuri. “Jaribu kunipiga. Nimebeba vitukuu vya familia ya Kimaro. Ukithubutu kutuumiza, basi huenda ukalazimika kujiondoa kwenye nafasi ya ukurugenzi ambayo ndiyo umetoka kuichukua tu.”
Thomas aliganda kwa sekunde moja kabla ya kumdhihaki. “Vitukuu wa familia ya Kimaro? Kwa hiyo? Dada yangu atakuwa na Alvin muda si mrefu.”
“Kaka...” Sarah alikunja uso kabla ya kumtikisa kichwa.
“Kwani uongo? Ninasema ukweli tu. Nafasi hii ni yako hata hivyo na yeye ndiye aliyeiba nafasi yako. Nadhani anapaswa kujiongeza kwa kuwa umerudi. Hupaswi kuingilia furaha ya dada yangu na Alvin,” Thomas alisema na kutoa mkoromo wa dharau.
Lisa akajibu kwa kejeli, “hakuna maana ya kuniambia mimi hivi. Kama una ubavu ongea maneno hayo mbele ya Alvin uone.”
Thomas alimuangalia sana mwanamke yule. “Nimekosea? Hebu tazama jinsi Alvin anavyomjali dada yangu! Alinisaidia kurejesha New Era Advertisings mara tu aliporejea na hata kuwezesha biashara kubwa yenye thamani ya shilingi bilioni kumi kwa kampuni yetu jana. Angalia vizuri uso wako mbaya kwenye kioo. Unawezaje kujilinganisha na dada yangu na sura yako ya kutisha?"
Pamela akaruka kama risasi iliyofyatuliwa ghafla. "Kama Lisa asingeharibika sura, angeonekana mrembo mara elfu zaidi ya yule mjinga."
“Unamwita nani mjinga? Omba msamaha kwa Sarah sasa hivi!” Rodney, ambaye alikuwa ameingia tu chumbani na kusikia sentensi ya mwisho, alionya kwa uso wa mawingu.
Tabasamu baridi lilienea kwenye uso wa Pamela. “Nimesema kitu gani kibaya? Kwanini niombe msamaha? Ulisikia kile Thomas alichotuambia kabla?"
“Bwana Shangwe, umekuja kwa muda muafaka. Wanawake hawa wamekuwa wakimfokea dada yangu,” Thomas alisema mara moja, “Lisa hata alitutishia kwa sababu ana ujauzito wa Alvin. Pamela hata alinipiga ngumi. Angalia, alama ya uvimbe bado inaonekana."
Rodney alimtazama kabla ya kuelekeza macho yake ya chuki kwa wanawake hao wawili. “Ombeni msamaha.”
Jambo hili lilimkasirisha sana Pamela. "Rodney Shangwe, unaumwa kichwani? Je, unaamini ujinga wowote wanaosema…”
Rodney akamjibu kwa kofi. Pamela aliganda kabisa, huku Lisa akiwa amekasirishwa na hilo. “Unawezaje kumpiga rafiki yangu…”
Kabla hajamalizia sentensi yake, Pamela tayari alikuwa amejitupa kwa Rodney kama mnyama wa porini, akimng’ata na kumpiga kwa fujo.
“Unathubutuje kunipiga makofi wewe mbwa?! Wewe usiye na akili, tena nimekupania kwa muda mrefu sana.” Alivuta na kuvuta nywele zake. Kumbe mtu mwenyewe alikuwa na mikwara tu hakuwa hata na nguvu. Mwishowe, alimng'ata usoni.
“Unapaswa kula korosho zaidi ili kuimarisha ubongo wako wenye akili za matope. Lakini nadhani umechelewa sana na hali yako. Sina cha kupoteza na sikuogopi kwa lolote. Tayari umenifukuza kazi yangu na kuniweka kwenye blacklist, kwa hiyo sikuogopi tena.” Pamela alifoka.

Pamela alikasirika sana. Alimpiga ngumi na teke Rodney, na kuchana shati lake na karibu amnyofoe nywele kwa kuzivutavuta. Hata uso wake ulikuwa umejaa alama za meno na alama za vidole. Wengine walitazama tu, wakiwa wamepigwa na butwaa.
Rodney, ambaye hakuwahi kupigwa ngumi na teke namna hiyo na mwanamke, alitumia juhudi nyingi kuhangaika kujinasua kutoka kwa Pamela aliyekuwa mkali kama paka aliyekanyagwa mkia.
“Unabipu kifo!” Rodney alikakamua na kumsogelea kwa hasira huku akionekana kudhamiria kumwangamiza mwanamke huyo. Lisa haraka akakimbia kwenda kumkumbatia rafiki yake kwa nguvu.
“Rodney!” Sauti ya Alvin ya onyo ilisikika pale chumbani ghafla. Alijivuta na kumkinga mkewe ndani ya sekunde chache.
Alvin alikuwa amekimbilia eneo la tukio baada ya kujua kwamba Rodney alikuwa ameenda hospitali pia. Lisa na Rodney hawakuwa wakipatana vizuri tangu ishu ya Maurine itokee, hivyo Alvin alihisi wangeonana macho kwa macho ingeleta shida kubwa na pengine wangembana kabisa. Hakuwa amekosea.
“Alvin mbona bado unawasaidia? Angalia hali niliyo nayo! Yote ni kwa sababu ya Pamela Masanja!” Rodney alipiga kelele.
"Ni wewe uliyempiga Pamela kwanza." Lisa alimtazama kwa hasira.
“Kwa sababu alimwita Sarah mjinga. Isitoshe, ninyi wawili mmekuwa mkimdharau Sarah na kaka yake tangu mwanzo. Naapa nitakufundisha somo leo hata iweje!” Rodney alikasirika kadri alivyozidi kuwaza.
Pamela pia hakurudi nyuma. "Nilifanya hivyo kwa sababu Thomas alisema Lisa ana sura mbaya."
"Ulisema mke wangu ana sura mbaya?" Alvin alimtupia macho ya kutisha sana Thomas.
Thomas alitetemeka kabla ya kusema kwa sauti ya kigugumizi, "Sikusema."
Pamela alikoroma. "Sio tu kwamba alisema Lisa ana sura mbaya, alisema pia ajipange kuachana na wewe kwa sababu dada yake mdogo amerudi. Hata alijisifu kuwa hivi karibuni Sarah atakuwa na ujauzito wa mtoto wako pia.”
"Pamela Masanja, acha uongo!" Thomas alipiga kelele. “Sarah, uwe shahidi yangu. Sikusema lolote kati ya hayo. Kinyume chake, hao wawili walikuita mjinga.”
"Nilisikia hivyo pia," Rodney alisema kwa upole.
"Sarah, nataka kusikia kutoka kwako." Alvin akahamishia macho yake kwa Sarah.
Sarah alitabasamu kinyonge. “Achana nayo tu, Rodney. Wacha yaliyopita yawe yamepita. Kipaumbele sasa ni kumpeleka baba yangu kwenye nyumba yake ya milele. Bi Masanja, Bi Kimaro, kwa kweli siko katika hali ya kubishana hivi sasa.”
Lisa alikunja uso kwa jibu lake la kijanja. Sio tu kwamba aliweza kuonyesha kuwa alikuwa anasamehe, lakini alidokeza kwa hila kwamba ni Lisa na Pamela ambao ndio walikuwa wakorofi.
"Alvin, umesikia hivyo?" Rodney alitabasamu kwa kejeli. “Mpeleke mkeo nyumbani na umuonye. Sarah kasamehe, lakini sitawaacha tena wakati mwingine nitakapowaona wanamnyanyasa tena. Hata na wewe ukiwepo.” Rodney alimaliza. Alvin alikunja uso lakini hakuzungumza kitu.
Ghafla, Lisa alicheka. “Nilijua haya yangetokea. Nilijua hakuna ambaye angetuamini mimi na Pamela hata tujitetee kiasi gani. Ndiyo maana… nilikuwa ninarekodi.”
Akatoa simu yake. Rekodi ya sauti ilichezwa. Maluweluwe yalionekana kwenye sura ya kila mtu. Thomas aliogopa na kufadhaika huku uso wa Sarah ukiwa umepauka kama mzimu. Uso wa Rodney pia ulikunjamana. Kwa kweli hawakutarajia Thomas angesema maneno yale ya kutisha.

Sura ya: 285

Thomas hakupaswa kushikilia kinyongo hicho hata kama alimdharau baba yake. Mtu huyo alikuwa amekufa sasa, baada ya yote.
Uso mzuri wa Alvin taratibu ukajaa mawingu. Alimtazama Sarah bila kujali. Hakuwa na wasiwasi kuhusu Thomas kwani mtu huyo alikuwa na sifa mbaya, lakini bila shaka hakutarajia Sarah angesema uwongo ili kuficha habari za kaka yake. Alikuwa karibu kutoelewa hali hiyo.
"Alvinic, naweza kuwaomba msamaha kwa niaba ya kaka yangu?" Sarah alifadhaika lakini akapata utulivu haraka, na kulazimisha tabasamu. “Thomas amekuwa hivi siku zote. Nimemwambia mara nyingi kwamba hakuna kitakachotokea kati yetu wawili lakini hakutaka kusikiliza. Hakuna mengi ninayoweza kufanya kuhusu hilo. Isitoshe, sikushiriki katika mabishano hayo tangu mwanzo lakini mwishowe nilidhalilishwa.”
“Sarah, hutakiwi kuomba msamaha kwani si wewe uliyewalaani wengine. Yote yalikuwa Thomas.” Rodney hakuweza kupinga kumfariji. "Zaidi ya hayo, Pamela ana makosa kwa kukuita mjinga pia."
Pamela alicheka kwa kejeli. “Ni msamaha ulioje, Bi Njau. Ikiwa Lisa asingerekodi mazungumzo, labda maneno uliyosema hapo awali yangefanya wengine wafikiri kwamba ni mimi na Lisa tulioanzisha mabishano hayo. Kinyume chake, Thomas angekuwa ameondolewa lawama zote. Haya yote yangesababisha Lisa na Alvin Kimaro kugombana tena.”
Sarah aliinua kichwa chake, akijionyesha kuwa hana hatia. “Samahani, sikufikiria hilo. Nitakuwa makini zaidi wakati ujao.”
"Hakuna haja ya wakati ujao! Pamela Masanja, utaacha lini kumuandama Sarah?" Rodney hakuweza kuvumilia kumuona Sarah akisikitika.
“Imetosha,” Alvin alionya kabla ya kumwangalia Thomas. "Inaonekana umekuwa ukinizoea kupita kiasi kwa sababu nilikusaidia. Sikujua kuhusu mradi mkubwa ulioupata jana. Labda watendaji wangu walifikiri mimi na wewe tupo karibu kivile hivyo wakajaribu kujipendekeza kwangu kwa kukufurahisha. Nitatoa neno baadaye kusitisha kolabo.”
Kwa mshtuko, Thomas alijaribu haraka kuokoa hali hiyo. “Bwana Mkubwa Kimaro, samahani. Ilikuwa ni kosa langu kusema mambo yasiyofaa. Tafadhali usighairi ushirikiano wetu. Nakuomba."
Pamela alidhihaki. “Kweli, umesema mambo mengi yasiyo sahihi. Mara ya mwisho kwenye baa, hata ulisema kwamba Bwana Kimaro hatakufanya lolote hata kama ungelala na Lisa kwa lazima.”
Miguu ya Thomas ilikuwa inatetemeka wakati huo. Alikaribia kuanguka na kupiga magoti chini.
“Alisema hivyo kwako?” Alvin alikodoa macho na kumgeukia Lisa.
Lisa akafungua midomo yake. “Utaniamini nikisema ndiyo?”
Alvin alimtazama kwa hatari yule mtu. Huenda asingeshawishika ikiwa asingesikia maneno ya dharau ambayo Thomas alimwambia Lisa mapema kwenye rekodi. Ghafla, aliweza kuelewa kwa nini walikuwa wakirumbana kila mara kuhusu mtu huyo. Kumbe, mke wake alikuwa amefedheheshwa sana na mtu huyo. Alihisi damu yake ikichemka chini ya ngozi yake. Alvin alimpiga Thomas kifuani kwa nguvu.
“Thomas!” Sarah alionekana kufadhaika. "Omba msamaha haraka kwa Bi. Kimaro na uahidi kwamba hutamtamkia maneno ya dharau tena. Sitaendelea kukusaidia ikiwa utafanya hivi tena.”
“Samahani, Bwana Mkubwa Kimaro. Nilikosea." Mara Thomas alipiga magoti chini na kumsujudia Lisa. "Bibi mdogo, sitakukosea tena."
"Alvin, nadhani hiyo inatosha," Rodney alisema. Hakuwa na wasiwasi kuhusu Thomas bali alijisikia vibaya baada ya kuona sura ya Sarah ya wasiwasi.
"Kumbuka, nitakukata ulimi ikiwa hii itatokea tena. Zaidi ya hilo, sitaingilia tena maswala ya familia ya Njau. Sitakutetea hata ukiua mtu au kuchoma moto mahali.”
Baada ya kusema hivyo bila kujali, Alvin aligeuka na kuzungumza kwa upole na Lisa, “Twende. Sarah na kaka yake wanaweza kushughulikia mazishi ya baba yao.” Kisha akamgeukia Rodney, “Boris ndiye baba mzazi wa Sarah hata iweje, basi wape mkono wa fadhili, sawa? Chukua mwili wa Jennifer Musyoka na uzike karibu na kaburi la mumewe.”
“Ndiyo, nitafanya hivyo.” Rodney aliitikia kwa kichwa.
Lisa alijisikia faraja baada ya kusikia hivyo na kuondoka na Pamela.
Ingawa Rodney aliweza kuwa mkorofi wakati fulani, hakuwa mtu mbaya au mkatili. Boris na mkewe wangeweza kuzikwa pamoja kwa amani ikiwa alikubali akishughulikia mazishi.

Giza lilitanda kwenye macho ya Sarah. Kwa kweli, hakuwa amepanga kumzika Jennifer ipasavyo. Ilikuwa ni nje na matarajio yake kwamba Alvin angemuagiza Rodney kwa makusudi kushughulikia suala hili. Je, alikuwa amepoteza imani naye?
Muhimu zaidi, alishtuka kwamba Lisa alirekodi mazungumzo yao kwa siri. Ilimfanya ahisi kana kwamba alikuwa amejipiga risasi mguuni.
Lisa mjinga! Alimchukia kama alivyomchukia Charity.
•••
Katika maegesho ya magari, Pamela alimnong’oneza Lisa kwa sauti ya chini, “Nimegundua kuwa Rodney ana hisia na Sarah. Huyo mwanaume asiye na akili anatumiwa na huyo mwanamke mjanja bila kujijua. Oh sh*t, unafikiri atakuwa amewahi kumbusu Sarah? Mawazo yake yananifanya niwe mgonjwa. Jamani! Niliwahi kumbusu Rodney kwa nguvu. Je, hiyo inamaanisha kwamba mimi pia nimembusu Sarah?”
Lisa alishangaa sana. “Kwanini ukambusu kwa nguvu Rodney? Hukuona wanaume wengine wowote wa kuchagua? Kumbusu ombaomba ovyo ovyo mitaani ni bora kuliko kumbusu Rodney.”
“Unakumbuka Patrick alipokuja kunitafuta hapo awali? Rodney alikuwa karibu kwa bahati hivyo nilimbusu ili kulipiza kisasi kwa Patrick. Ninajuta sana sasa nahisi kutapika.”
Sura ya kuchanganyikiwa ilienea kwenye uso wa Lisa. “Usithubutu kusema maneno ya hivyo mbele yangu. Mpenzi wa zamani wa Sarah ni mume wangu. Nadhani wamebusuana mara nyingi zaidi kuliko ninavyoweza kuhesabu.”
'Hiyo ni sawa. Umembusu pia Sarah kwa njia isiyo ya moja kwa moja mara nyingi. Labda unapaswa kuosha kinywa chako vizuri ukifika nyumbani.”
Alvin aliyekuwa akitembea mbele yao alikosa la kusema. Je, wawili hao hawakujua kwamba mwangwi wa sauti ulikuwa mkubwa kwenye maegesho? Aliweza kusikia kila neno walilosema. Walikuwa wakimkosoa yeye na Rodney kana kwamba walikuwa mafungu ya takataka. Kweli?
Ghafla Alvin akasimama. Pamela mara moja aliona sura tata usoni mwake. “Gari langu limeegeshwa pale. Tutaonana baadaye.”
“Hata mimi nimepaki hukoo…” Lisa aligeuka, akitaka kuondoka.
Alvin akamshika mkono mara moja. “Shani ataendesha gari lako kurudi nyumbani. Utapanda gari langu.”
"Sitaki kupanda gari lako." Bado alikuwa na hasira naye.
“Lisa, samahani. Lakini nimemuadhibu Thomas na wewe pia umeona.” Aliinamisha kichwa chake chini, akionekana kuomba msamaha. "Mazishi ya Boris na Jennifer yatashughulikiwa na Rodney. Hakuna tatizo.”
"Kwa hiyo?" Aliinua kichwa chake kudhihirisha kukata tamaa katika macho yake. “Ungeniamini kama sikuwa na rekodi? Ninyi nyote bado mngefikiri kwamba mimi na Pamela tuliwanyanyasa Sarah na kaka yake.”
Aibu ilimwangazia usoni mwake. “Sikutarajia—”
“Kuna mambo mengine mengi ambayo hukutarajia.” Lisa alidhihaki. “Msamaha wako una faida gani? Wafu hawatarudi wakiwa hai hata hivyo. Tafadhali, kumbuka mtu unayemsaidia ni takataka ya aina gani.”
“Uko sahihi kabisa kwamba Thomas ni takataka. Kwa hiyo unataka kuendelea kubishana kuhusu takataka hiyo?” Alisema kwa upole, “Kwanini nisikupeleke shopping baada ya kazi leo?”
TUKUTANE KURASA 286-290

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......286-290

Sura ya: 286

“Siko katika moodya kufanya shopping. Zaidi ya hilo, ninatumai kuwa utaacha kuegemea upande wa Sarah kila wakati. Sijali jinsi unavyofikiri alikuwa mkarimu na asiye na hatia hapo awali lakini alikuwa amepotea kwa miaka michache. Unajua nini kimempata kwa kipindi chote hicho? Bado unamchukulia kuwa mtu yule yule wa zamani?" Lisa alinyakua mkono wake kutoka kwa Alvin na kunyata bila kuangalia nyuma.
Alvin alikuna kichwa chake kwa upole huku uso wake ukiwa umekunjamana. Kusema kweli, alikatishwa sana tamaa na Sara siku hiyo. Ni kana kwamba alikuwa mtu tofauti. Kwa kweli angemuelewa vibaya Lisa ikiwa si kwa kurekodi aliyoisikia.
Wakati huo, alijaribu kuchambua tabia yake kwa kichwa cha tafakuri. Ilionekana kana kwamba siku zote alikuwa akiegemea upande wa Sarah kila kulipokuwa na mgogoro kati yake na Lisa. Kwa nini? Lisa alikuwa mke wake. Alipaswa kumwamini mke wake. Ilionekana kana kwamba alitakiwa kujiweka mbali na Sara.
•••
Asubuhi iliyofuata baada ya kifungua kinywa, Lisa alitoka kwenye kabati la nguo la kutembea akiwa amevaa nguo ndefu nyeusi.
Alvin, ambaye pia alikuwa amevalia suti nyeusi, alikuwa akingoja mlangoni kwa muda. “Unahudhuria mazishi ya Boris Njau? Ngoja nikupe lifti.” Lisa akamtupia jicho kali. Alihisi huzuni lakini akatabasamu hata hivyo. “Siendi huko kwa ajili ya Sarah. Nataka tu kuhakikisha kwamba hakuna mtu wa kukuonea tena.”
“Hatimaye umesema jambo la heshima,” Lisa alitania.
Alvin hakuwa na la kusema. Ni lini hakuwa na heshima katika maneno yake? Alvin akapotezea.Hakuwa na tatizo kwa kudhihakiwa ikiwa ilimfanya mke wake ajisikie vizuri.
“Twende. Nadhani unapaswa kuomba msamaha kwa Mjomba Boris.” Lisa alisema kwa upole. Hakutaka kubishana naye na wala hakumlaumu kwa kushindwa kuuona ukweli. Baada ya yote, Sarah hakuwa rafiki yake wa utotoni tu bali pia mpenzi wake wa zamani. Kwa upande mwingine, yeye na Alvin walikuwa wamefahamiana kwa muda usiozidi mwaka mmoja. Isitoshe, Sara alikuwa mwanamke mjanja. Hakuwa na la kufanya ila kudhihirisha taratibu rangi halisi za mwanamke huyo mjanja.
“Mimi? Nikaombe msamaha?” Alvin alionekana kushangaa.
“Thomas asingekuwa gerezani muda mrefu uliopita kama si wewe hivyo asingepata nafasi ya kumfanya mjomba Boris afe."
Hakika. ilibidi aende kuomba msamaha.
•••
Katika chumba cha mazishi. Lisa aliingia kutoa heshima zake. Thomas na Sarah walikuwa wamesimama kando ya jeneza, wote wakiwa wamevalia mavazi meusi.
Macho ya Sarah yalikuwa yamevimba kwa machozi. Aliinua kichwa kuwasalimia. "Alvinic, Madam, asanteni kwa kuja."
Alvin aliitikia kwa kichwa kabla ya kumgeukia Lisa. "Hebu tuketi mahali fulani ikiwa umechoka."
Uso wa Sarah uliganda. Alvin hakumuuliza hata anaendeleaje. Licha ya uchovu wa dhahiri usoni mwake, bado alikuwa na wasiwasi juu ya Lisa kuwa amechoka.
Lisa aliuliza baada ya kuona mle ndani kulikuwa na jeneza moja tu badala ya mawili. “
“Mama alizikwa na kampuni ya mazishi,” Sarah alisema kwa nia ya kuomba msamaha, “nilikuwa na shughuli nyingi za kupanga vitu vya baba yangu hospitalini jana hivyo niliajiri kampuni ya mazishi kushughulikia maiti ya mama. Tayari walikuwa wameshahifadhi maiti ya mama kaburini niliporudi nyumbani kuandaa mazishi ya baba.”
Lisa nusura aripuke kwa hasira. Sio tu kwamba Aunty Jennifer alikufa ghafla, lakini pia alizikwa bila hata salamu za kwaheri.
'Sio kosa la Sarah," Rodney aliibuka kumtetea Sarah. "Alijaribu kadri awezavyo. Mbali na hilo, tayari alipanga makaburi. Mjomba Boris atazikwa pembeni ya kaburi la Aunty Jennifer.”
Lisa alishusha pumzi ndefu. Kusikia hivyo akaridhika kidogo. Kweli, angalau, Aunty Jennifer na Mjomba Boris wangezikwa karibu na kila mmoja ili wasiwe peke yao.

Lisa akasogea mbele kutoa heshima zake. Sarah, akiwa mshiriki wa familia, alijiunga nao kutoa shukrani zake. Sarah alijitahidi kadri awezavyo kuwa karibu zaidi na Lisa. Walipokuwa wameinamisha vichwa vyao chini, Sarah alinong'ona kwa sauti ndogo kiasi cha kuweza kusikia wao wawili tu. “Unafikiri huyo mwanamke anaweza kuzikwa karibu na kaburi la baba yangu? Hah, mwili wa Jennifer tuliutelekeza mochwari, bila shaka atakuwa alizikwa na City kwenye makaburi yasiyo na ndugu. Kilicho ndani ya kaburi la pembeni ya baba yangu ni jeneza tupu!”
Mwili wa Lisa ulikuwa ukitetemeka kwa wakati huu. Aliinua kichwa chake, na kuona sura ya huzuni ya Sarah. Ilikuwa ni kama kwamba hakuwa amesema kitu chochote cha kinyama kwa Lisa.
Mwanamke huyo angewezaje kuwa mkatili namna hiyo? Lisa alihisi huenda Sarah alikuwa anajaribu kumuingiza kwenye mtego. Hata hivyo, hakuweza kujizuia kumsukuma kwa hasira hadi chini.
Sarah alianguka na kugonga kichwa chake kwenye jeneza, akaanza kulia kwa nguvu na machozi yakimtoka. "Bibi mdogo, nimekukosea nini tena?"
"Lisa, unafanya nini?" Rodney alikimbia mbele kumsaidia Sarah kusimama.
"Lisa, ni ujinga gani tena huu unafanya?" Chester naye alienda kumsaidia Sarah.
Alvin alichanganyikiwa lakini alijua Lisa si mtu asiye na akili. “Lisa, kuna nini?”
“Nini tena? Amepandwa wazimu. Alvin, mtoe hapa sasa hivi au jiandae kuandaa msiba mwingine kwa Mzee Kimaro,” Rodney alifoka.
“Sarah Njau, sijawahi kuona mwanamke mkatili kama wewe. Utakufa kifo kibaya sana wewe mwanamke." Lisa alikunja ngumi kwa hasira na kuondoka. Asingeweza kusema lolote akaeleweka wakati watu wote walikuwa wakimlinda mwanamke huyo mjanja.
Hata hivyo, siku moja, Sara angelazimika kulipa kwa ajili ya mambo yote mabaya ambayo alikuwa amefanya.
“Mwanamke kichaa kweli huyu! Alvin, usimlete tena karibu yangu siku nyingine. Sitaki kumuona tena huyo mwanamke.” Rodney alichukizwa sana na Lisa wakati huo.
“Rodney, usiseme hivyo. Hakufanya hivyo makusudi,” Sarah alisema huku akimshika mkono mwanaume huyo. "Kulingana na uzoefu wangu wa kitaaluma, labda ujauzito wake utakuwa unampelekesha."
"Ujauzito?" Alvin alishikwa na butwaa.
"Ndio, mwanamke mjamzito hupitia mabadiliko ya homoni yanayobadilika-badilika, kama vile kuwa na wasiwasi hata kwa vitu vidogovidogo, kutilia shaka, kuwa na hasira mbaya, kuwa na wivu sana na uhusiano wao, na wakati mwingine kuwachukia tu watu bila sababu.”
Rodney alisema kwa mshangao, "Wow, nadhani Lisa ana dalili hizi zote."
Alvin alihisi kichwa kinamuuma. Alikuwa bado hajapona ugonjwa wake mwenyewe. Ingekuwa mbaya sana ikiwa Lisa naye angepata shida kama yake. “Nitamfuata.”
Wakati Alvin anakimbilia mlangoni, Lisa alikuwa ameshaingia ndani ya gari. Saa moja baadaye, Lisa alitembea taratibu mbele ya lango la gereza. Dakika kadhaa baadaye, Charity, ambaye alikuwa amevalia sare ya rangi ya machungwa, alitokea huku miguu yake ikiwa imefungwa pingu. Nywele zake zilikuwa zimekatwa. Alionekana amekonda na kuchoka sana. Hata ule uzuri wake wa asili sasa ulianza kufifia.
“Lisa, ni wewe. Nilidhani ni wazazi wangu.” Charity alitabasamu baada ya kumuona.
Ngumi za Lisa zilizokunjwa zilitetemeka juu ya magoti yake. Alijitahidi sana kujizuia asimweke wazi. “Wazazi wako… Pamela na mimi tumewasafirisha hadi Dar es Salaam. Afya ya baba yako si nzuri kwa sasa na mama yako anahitaji kumtunza. Labda hawatarudi kukutembelea mara kwa mara.”
"Asante, Lisa." Charity alitoa shukrani za kweli. “Hatujafahamiana kwa muda mrefu, lakini! sikufikiria kama ungenisaidia sana.”
“Hapana, ni kosa langu kukuingiza humu ndani. Ikiwa nisingechunguza utambulisho wa Maurine, asingefungiwa na Alvin na kuchomwa moto akiwa hai na muuaji.”
"Sielewi kwanini mtu anaamua kunifanyia hivi." Macho ya Charity yalidhihirisha hasira kali.
“Ni Sarah!" Lisa alimtazama mwanamke huyo. "Najua yuko hai."

Sura ya: 287

“Nilifikiria kuhusu hilo pia. Lakini hakujitapa kuhusu hilo mara ya mwisho alipokuja kwa hivyo sifikirii hivyo.” Charity akatingisha kichwa huku sura ngumu ikitawala uso wake. "Alisema alitaka kumchukua Alvin wake na kurudisha wadhifa wa Bi Kimaro. Unapaswa kuwa mwangalifu dhidi yake.”
Lisa alishtuka. Ilionekana kuwa mawazo yake yalikuwa sawa. “Kweli? Lakini hasemi hivyo mbele ya Alvin na marafiki zake.”
"Siku zote amekuwa kama kinyonga." Midomo ya Charity ilitetemeka. "Amewateka wote Alvin na genge lake, wanamchukulia kama binti wa kifalme."
Lisa alicheka. “Najua. Hivi ulijua kabla ya hii kwamba Sara hakuwa amekufa? Hata akawa mwanasaikolojia maarufu, Nyasia. Yeye ndiye anayemtibu Alvin kwa sasa.”
Charity alionekana kushtuka kweli. “Nilifikiri kweli amekufa. Miaka kadhaa iliyopita, alikuwa anafanya utafiti wake kwenye msitu wa Garisa baada ya kuhitimu masomo yake nje ya nchi. Alitekwa nyara na magaidi wa Al-Shabaab alipoenda msituni na marafiki zake. Magaidi hao waliwageuza kuwa wako zao wakawa wanawabaka kila siku. Lakini alifanikiwa kutoroka kwenye kambi ya magaidi huko Somalia na kuzamia Ulaya.”
“Kwanini hakuwasiliana na familia yake au hata Alvin? Badala yake, aliishi kwa siri na kuwa mwanasaikolojia maarufu.” Lisa aliuliza.
“Kuna kitu hakiko sawa kuhusu hili.” Charity naye hakuweza kuelewa.
Lisa alijiuliza mambo mengi sana baada ya kusikia kisa cha kutoweka kwa Sarah. Ghafla, Charity akasema, “Lisa, achana naye kama unaweza. Uko peke yako bila msaada. Nina wasiwasi huwezi kushindana na Sarah na mwishowe utapoteza kila kitu.”
Lisa alizama katika mawazo. Bila shaka, alikuwa amefikiria kuacha naye pia. Hata hivyo, moyo wake ulipata maumivu makali kila alipokuwa akifikiria kumtoa Alvin kwa mtu mwingine, au alipowaza taswira ya yeye na Sarah kuwa mke na mume. Kwanini amwache aende? Alikuwa mume wake. Baba wa watoto wake.
Charity alishusha pumzi akimtazama. “Vinginevyo, hutakiwi kumruhusu amtibu Alvin. Ni mchakato mrefu na itambidi kutumia muda mwingi akiwa na mpenzi wake huyo wa zamani. Sara hakika ataleta matatizo katika kila nafasi anayopata. Huenda usiweze kumshughulikia hasa kwa kuwa wewe ni mjamzito.”
Lisa alitabasamu kwa uchungu. Hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa yakienda. Kabla ya kuondoka, aligeuka na kumwambia Charity kwa huruma, “Hata iweje, siku zote, nitakuwa rafiki yako na hutawahi kuwa peke yako.”
Charity alishtuka na kufadhaika. Haikuelewa chochote mpaka Sarah alipoenda kumwona muda si mrefu baadaye ndipo hatimaye alielewa ukweli.
Alasiri, Lisa alishangaa kumkuta Alvin nyumbani baada ya kurudi kwa Mzee Kimaro. Alikuwa amekaa kwenye kochi sebuleni. Alitembea moja kwa moja hadi kwenye ngazi bila kumtazama.
"Lisa, subiri." Alvin alimkimbilia kumshika mkono. “Njoo tupumzike sebuleni, nimeleta mpishi maarufu atupikie chakula kizuri sana leo.”
Lisa alimtazama mwanaume huyo juu na chini kwa mashaka. "Huna hasira kwamba nilimsukuma Sarah asubuhi hii?"
Alvin alishtuka, akakuna pua. "Nilikuwa karibu kukasirika lakini nilipojifikiria mara mbili, nikajua mke wangu asingemsukuma mtu bila sababu."
Wakati huo huo, uvimbe ulijitengeneza kooni mwa Lisa na machozi yakaanza kumtoka papo hapo. Mungu pekee ndiye aliyejua jinsi alivyokasirika siku hiyo. Alikuwa amejipanga kugombana tena na Alvin lakini hakutarajia kwamba angemwamini safari hii.
Moyo wake uliokuwa umechoka ghafla ukapata nguvu ya kujiamini kuendelea na safari hii ya maisha pamoja naye.
“Haya, mbona unalia tena?” Alvin alishikwa na mshangao. "Machozi yako yamekuwa kama mvua tangu upate mimba na yanakuja bila kualikwa, kwanini?" Alipapasa huku na kule kutafuta kitambaa.
"Alvlisa." Lisa alimkumbatia na kuuzika uso wake kifuani mwake.
“Ndiyo, niko hapa.” Alvin akampigapiga Lisa kidogo mgongoni. Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu alipomwita jina hilo. Kulikuwa na hisia mchanganyiko katika moyo wake. Labda hakuwa akimjali vya kutosha jambo ambalo lilimfanya awe na huzuni. “Lakini nilikuwa na hasira kidogo leo. Hukupaswa kuendesha gari kwa kasi hivyo leo. Je, wewe na watoto mkijeruhiwa?”

“Sitafanya hivyo tena.” Alitikisa kichwa. Baada ya kufikiria kwa ufupi, aliinua macho yake na kusema, “Kwa kweli, sikumsukuma kimakusudi leo. Sarah aliniambia kwenye kaburi la Aunty Jennifer limezikwa jeneza tupu. Maiti yake waliitelekeza mochwari na imezikwa na city kwenye makaburi yasiyojulikana. Sikuweza kuvumilia…”
Mshtuko mkubwa uliandikwa usoni mwa Alvin. Lisa hakushangaa kuona mwitikio wake huo. “Najua hutaniamini na pengine hata kufikiria kuwa nampakazia. Lakini haijalishi.”
“Ni vigumu sana kuamini hivyo,” Alvin alisema kwa uaminifu huku akiendelea kumbembeleza mgongoni. Asingemsamehe Sarah hata kidogo ikiwa angejua ni kweli alifanya hivyo. Hata kama Jennifer alikuwa mvunja nyumba ya mama yake, alikuwa tayari amekufa. Isingekuwa sawa kuitupa maiti yake kusikojulikana.
“Hmm, hata mimi sitaki kuamini hivyo pia. Natumai alikuwa anadanganya tu,” Lisa alijibu kwa uchovu.
“Sawa, acha kuwaza kupita kiasi. Nitamwambia Aunty Yasmine alete chakula." Akambeba mpaka bustanini.
Jua lilikuwa linawaka na kulikuwa na joto kiasi ndani ya bustani. Lisa aliegemeza kichwa chake kifuani mwa Alvin huku akimlisha chakula. Alichangamka baada ya hapo na kwa namna fulani akalala huku akiwa amejiegemeza kwenye mikono yake.
Baada ya kumbeba na kumrudisha chumbani, alitoka chumbani na kumuita Hans. "Nenda uchunguze indani ya kaburi la Jennifer kuna jeneza tupu."
“Itakuwa imeenda wapi tena maiti yake, imefufuka?" Hans alishangaa.

“Fanya hivyo mara moja!” Alvin alimfokea msaidizi wake.
Siku iliyofuata. Sarah alifika mapema nyumbani kwa Mzee Kimaro kumtibu Alvin. Lisa na Alvin walikuwa wakimsubiri pale sebuleni. Lisa alikuwa ameghairi makusudi kwenda ofisini siku hiyo.
Sarah alionekana mrembo akiwa amevalia vazi jepesi la majira ya joto la waridi na mikono iliyochanika. Macho yake bado yalionekana kuwa na kichefuchefu kidogo kutokana na kilio cha msibani, ambacho kilimfanya aonekane mwenye huzuni kiasi fulani.
Hata hivyo, Lisa alikuwa tayari ameona unyama uliojificha nyuma ya sura hiyo nzuri. Mwanamke huyo alikuwa muovu mara elfu zaidi ya Lina.
"Bibi mdogo." Dokezo la vitisho likaangaza machoni pa Sarah. Baada ya kupeana salamu za kawaida, alimgeukia Alvin.
"Wacha tuanze kipindi chetu cha pili cha matibabu."
Lisa alisimama na kuhoji. “Bibi Njau, unaweza kunieleza undani wa kipindi hiki cha pili? Ni aina gani ya njia ya matibabu inahitajika?"
"Tiba ya huzuni. Kwa maneno rahisi, inamfanya mgonjwa kudhibiti kwa makusudi msisimko, furaha, na kusahau wasiwasi wake katika mtazamo hasi, na hivyo kubadilisha hisia zake kuwa mtazamo chanya.”
Lisa alikunja uso kwa sauti hiyo. "Inaonekana kuwa hatari sana."
Tabasamu likatanda usoni mwa Sarah. “Uko sahihi. Lakini Alvin amekuwa mgonjwa kwa miaka 20 na hali yake haiwezi kuponywa ikiwa tutakwepa hatari. Isitoshe, kusema ukweli, akikataa matibabu, hali yake inaweza kuwa mbaya na kuwa sawa na ugonjwa wa Alzheimer katika muda wa chini ya mwaka mmoja.”
Uso wa Alvin ulianguka. “Kwanini hukusema hivi kabla?”
"Sikutaka kukuhangaisha au kukufanya uhisi kulemewa kupitia vipindi vya matibabu." Sarah alicheka kwa uchungu. “Sina jinsi zaidi ya kukuambia kwa sasa maana nahisi kama huniamini sana. Lazima nikueleze kwa uaminifu uzito wa hali hiyo.”

Sura ya: 288

“Twende ghorofani kwa matibabu,” Alvin alisema kabla ya kuelekea kwenye ngazi.
Lisa aliuma midomo yake alipoona watu wale wawili wakitoweka juu ya ngazi. Sarah bila shaka alikuwa mwanamke mjanja. Kwa maneno machache tu, alimfanya Lisa kuonekana hajali hali ya Alvin kwa sababu tu ya wivu wake.
Lisa alisubiri sebuleni muda wote tangu kipindi cha matibabu kianze. Dakika 40 hivi baadaye, sauti ya vitu vikivunjwa na sauti ya mwanamke akipiga kelele ghafla ikasikika kutoka juu. Alikimbilia kwenye chanzo cha mzozo huo mara moja, na kukuta chumba kilikuwa kimefungwa kwa ndani.
“Shangazi Yasmine, leta funguo haraka,” Lisa aliamuru.
Mlinzi wa nyumba alipanda ngazi kwa wasiwasi akiwa na funguo ya ziada. Wakati anakaribia kufungua mlango, mara ulifunguka wenyewe kutoka ndani. Alvin ambaye alikuwa amevalia suruali ndefu alionekana kufadhaika huku akitoka nje ya chumba kile kwa kasi akiwa amembeba Sarah mikononi mwake. Kichwa cha mwanamke huyo kilikuwa kinavuja damu na kulikuwa na kamba iliyozungushwa shingoni mwake.
"Nini kimetokea?" Lisa aliuliza kwa mshtuko.
Alvin alikuwa anataka kueleza kitu pale Sarah alipougulia maumivu ghafla.
“Usilie. Nitakupeleka hospitali sasa hivi.” Alvin alimfariji kwa upole. Bila hata kumwangalia Lisa, alitoka nje ya nyumba haraka huku Sarah akiwa bado amemkumbatia.
Jumba kubwa la kifahari liligeuka ghafla kuwa kimya. Lisa alihisi kutetemeka hadi kwenye uti wa mgongo wake.
Alitazama ndani ya chumba kilichovurugika. Meza na viti vilikuwa vimesambaratika huku na kule. Alikuwa amemwona Alvin hapo awali alipokuwa amerudiwa na ugonjwa wake. Huenda mbinu za matibabu ya Sarah zilimfanya arudiwe na hali yake tena na baada ya kupata fahamu zake aljikuta amemdhuru Sarah. Lisa alikuwa amemtahadharisha hapo awali kuwa mbinu hizo za kusisimua ugonjwa wake ni hatari lakini Sarah akasisitiza tu kuzitumia.
“Bibi Mdogo…” Shangazi Yasmine alimtazama kwa wasiwasi.
“Sijambo. Fuatilia kujua anapelekwa hospitali gani. Nitakwenda kumtembelea,” Lisa alisema.
Dakika 20 baadaye, aliambiwa kwamba walikuwa katika hospitali ya Chester. Shani alimkimbiza huko mara moja.
Lisa alisikia sauti nyororo ya Alvin ikimbembeleza Sarah mara baada ya kuukaribia mlango. "Unajisikiaje sasa?"
“Niko sawa. Ni mkwaruzo mdogo tu...”
“Mkwaruzo mdogo? Ninajua jinsi ninavyoweza kuwa mkali wakati wa kurudi ugonjwa tena. Kwanini hukuniambia mapema kwamba matibabu yanaweza kuwa hatari?”
“Haijalishi. Sijali kuumia kwangu hata kidogo ikiwa inamaanisha kuponya hali yako." Sarah alisema kwasauti nyororo.
“Sarah…”
“Sawa, huna haja ya kusema lolote. Sikustahili lakini natumai unaweza kuwa na maisha ya kawaida. Kusoma saikolojia halikuwa lengo langu lakini wewe ndiye uliyenipa motisha iliyonifanya niendelee mbele. Tafadhali niruhusu nitibu ugonjwa wako. Nataka uwe na maisha ya kawaida yenye furaha.”
“Samahani… Sarah…” Sauti nzito ya mwanamume huyo ilijawa na majuto na kufadhaika.
Lisa hakuweza kusikia neno lingine. Alikuwa karibu kuusukuma mlango ili aingie ndani wakati mkono ulipomvuta ghafla. Alitazama begani na kukutana na sura isiyojali ya Rodney ikimtazama. “Hebu tuzungumze.”
Rodney akampeleka kwenye korido tulivu na kuwasha sigara kabla ya kukaa kwenye ngazi. Moshi uliotoka kwenye midomo yake ulionyesha upweke machoni pake.
“Ikiwa lengo lako nikuniambia nimwachie nafasi yangu Sarah, basi samahani, lakini sitakubali hilo," Lisa alisema kwa upole.
"Lazima utakuwa umefikiria na kugundua hilo pia. Sarah hajaacha kumpenda Alvin na bado anamjali,” Rodney alijibu huku akionekana kuudhika. "Lakini mambo yamefikia hivi kwa sababu yako."
Lisa alicheka kwa kejeli. “Kwanini Sarah hakurudi nyumbani mapema ikiwa hakuwa amekufa? Kwani kosa langu ni lipi hapo? Yeye alikuwa amekufa na Alvin akaamua kunioa. Angekuwa anataka kuolewa naye si angemfahamisha mapema kuwa bado yupo hai amsubiri? Kwanini alimua kukaa kimya, alifikiri Alvin angemngoja milele?”
"Siyo kwamba hakutaka kurudi nyumbani lakini alihisi kuwa hastahili kuwa Alvin tena. Ni kwa sababu yeye…” Macho ya Rodney yakamtoka. "Hujui amepitia nini."
"Sijui na sina mpango." Midomo yake ilitetemeka.

"Lisa, unawezaje kuwa na moyo mgumu kiasi hiki?" Rodney alichukia. “Sarah alianza kabla yako. Kimsingi wewe huna haki ya kuwa na Alvin baada ya Sarah kurudi.”
Lisa alihisi kama hana la kusema. “Najua unampenda Sarah lakini tafadhali usitumie hilo kuwaumiza wengine. Unataka nimuonee huruma? Kweli, lakini vipi kuhusu ndoa yangu na watoto wangu? Nani atanihurumia?”
"Unajua jinsi walivyokutana?" Akavuta pumzi ndefu ya sigara. “Alvin alikutana na Sarah alipopelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Sarah hakuwa mgonjwa lakini alipelekwa huko na familia ya Njau. Sarah alimjali sana Alvin kama rafiki yake, hatua kwa hatua hali yake ilibadilika kuwa bora na chanya. Alikuwa kama mwanga wa jua wakati wa siku za giza. Pia ni kwa sababu yake nilimfahamu Sarah. Yeye ni mtu mzuri sana. Ingawa walikuwa hawasomi katika shule moja, alimwandikia barua za kumtia moyo kila siku kuanzia shule ya msingi hadi walipokua na kufaulu maishani. Amefahamiana naye kwa miaka 20. Sawa, umeolewa na Alvin lakini ni baada ya kufikiria kuwa Sarah amekufa. Alvin ni mwanamume anayewajibika, lakini sasa umemweka njia panda. Wewe ni mjamzito, lakini bado anamuona Sarah kama mke wa maisha yake. Unafikiri ni vizuri kuwa katikati yao?”
Kila neno lililotoka kinywani mwa Rodney lilipenya moyoni mwa Lisa kama kisu kikali. Hakujua kuwa wawili hao walikuwa wamekutana katika hospitali ya magonjwa ya akili.
“Sarah alisomea saikolojia kwa sababu ya Alvin. Anajitolea maisha yake yote kwake, "Rodney alisema kwa upole. "Kwa nini huwezi kuwapa baraka zako?"
Lisa alicheka kwa kejeli. "Ni nani atakayenipa mimi na watoto wangu baraka basi?" Aligeuka kuusukuma mlango mzito wa mbao. “Rodney, huwezi kunifanya nionekane sina haki kwa sababu tu unampenda Sarah. Kwanini wewe ndiye unajitia kimbelembele sana kumpigania Sarah? Sijamwona Chester akifanya hivyo, hata Alvin mwenyewe hapambani kama wewe. Wewe una nini hasa na Sarah? Amekupa nini?”
Badala ya kurudi kwenye wodi ya hospitali, aliamua kuondoka kabisa hospitalini. Alitembea kando ya barabara kwa muda mrefu bila mpango wowote.
Alvin alimpigia akiwa ametembea hadi miguu imeanza kumuuma. "Shani alisema ulikuja hospitalini. Uko wapi? Mbona sikuoni?”
“Niliondoka,” Lisa alijibu kwa upole, "Utarudi lini nyumbani?"
“Lisa, samahani. Sarah amejeruhiwa kwa sababu yangu na Thomas hayupo. Ninaweza kukaa kwa muda mrefu zaidi…”
“Ndiyo, ni sawa.” Lisa alikata simu na kuelekea nyumbani kwa Pamela.
Alimkuta Pamela akiwa anapakia vitu vyake. “Unaondoka lini?”
"Aamh! Mwezi ujao. Naenda Marekani lakini bado sijapata visa. Ninapanga kurudisha vitu hivi vyote Dar es Salaam.” Pamela aliutazama uso wa rafiki yake uliopauka kwa wasiwasi. "Kuna nini?"
“Hakuna kitu, nimechoka tu.” Lisa alimkumbatia rafiki yake huku machozi yakimtiririka bila kujizuia. “Hatimaye unaondoka! Ninaogopa siwezi kuvumilia kwa muda mrefu zaidi. Inaonekana kama kila mtu katika jiji hili ananiona kama adui. ”
“Ikiwa…nitakaa?” Pamela aliuliza na kuuma mdomo.
“Hapana, sahau. Huwezi kunisaidia hata ukikaa.” Lisa alifuta machozi yake kwa nyuma ya mikono yake. “Ni kwamba mengi yametokea hivi karibuni. Sarah ameanza kufanya harakati zake. Alvin anasema hatarudiana naye lakini najua bado anamjali.”
Pamela alishusha pumzi baada ya kumwona yule mwanamke aliyekuwa akihangaika. “Lisa, najua unajaribu kuokoa ndoa yako kwa sababu ya watoto lakini inaonekana juhudi ni za upande mmoja. Itakuchosha. Kwa nini usipumzike tu?”
“Pamela…”

Sura ya: 289

Pamela alikunja uso. “Miaka yote hii ya kuwa na Patrick imenifunza kitu. Mwanaume mzuri hatakuacha hata wanawake wengine wawe na hila kiasi gani. Ikiwa wewe tu ndiye unayefanya kazi kwa bidii ili kudumisha ndoa wakati wote, basi bado itavunjika hivi karibuni au baadaye.”
Lisa alionekana kushtuka.
Pamela akampiga begani. "Kuna wanawake wengi sana katika ulimwengu huu ambao wako tayari kuwa waharibifu wa ndoa za watu, bila kusahau Alvin ndiye mwanaume tajiri zaidi nchini Kenya. Wanawake wengi wangependa kujirusha juu yake na ni juu yake kujua wakati wa kujiweka mbali nao. Acha tu mambo yatokee kwa kawaida. Baada ya yote, haifai kumthamini mtu ambaye anaweza kuondoka kwa urahisi kutoka kwako.”
"Hapo umenena kiutu uzima."
'Ni sawa. Acha nikuandalie chakula cha jioni leo.”
“Sawa.”
Lisa alirudi kwa Mzee Kimaro baada ya chakula cha jioni lakini Alvin bado alikuwa hajarudi. Chumba alikihisi ni kitupu haswa akiwa peke yake.
Usiku wa siku hiyo, kumbukumbu za Alvin kuondoka kwenye nyumba hiyo huku Sarah akiwa amemkumbatia ziliendelea kumjaa akilini akiwa amejilaza kitandani. Pia alikumbuka mazungumzo ya Alvin na Sarah hospitalini mapema siku hiyo. Nani alijua ni muda gani Sarah angeendelea kuwa katika maisha yao? Lisa alikuwa mjamzito, lakini bado ilimbidi aendelee kumlinda Sarah huku akimwangalia mumewe kana kwamba yuko vitani. Ilikuwa inachosha sana.
Labda, kama Pamela alivyosema, haikufaa kumthamini mtu ambaye angeweza kuondoka kwa urahisi. Iliwezekana kweli kuwa hivyo. Aliamua kutojali tena.
Mikono yake ilienda kwenye tumbo lake. Kuanzia siku hiyo aliamua kutumia muda mwingi kuwapenda watoto wake ili kuhakikisha wangeingia katika ulimwengu huu wakiwa na afya njema.
Upande wa pili wa kitanda ulikuwa bado mtupu alipoamka asubuhi iliyofuata. Shangazi Yasmine alikuwa tayari ametayarisha kifungua kinywa aliposhuka ngazi baada ya kunawa. Alvin alikuwa akimngoja kando ya meza ya chakula huku akionekana kuwa na huruma. "Samahani jana usiku ... nilichelewa sana kurudi nyumbani."
“Ni sawa.” Alichukua bakuli la mtori na kuanza kunywa.
Mwitikio wake usio na wasiwasi ulimshangaza Alvin. “Nilitaka kufika nyumbani mapema ili kukaa nawe jana usiku lakini jeraha la Sarah ghafla—”
“Acha kumzungumzia mambo ya Sarah hapa. Unaweza kufanya chochote unachotaka,” Lisa alimkatiza kwani hakutaka hisia zake ziharibike kwa kusikia jina hilo.
Alvin alikunja uso, akidhani kwamba Lisa alikuwa na wivu tena. “Lisa, natumai unaelewa kuwa mimi ndiye niliyemjeruhi Sarah jana usiku. Siwezi tu—”
“Ninaelewa. Ndiyo maana sisemi mengi.” Lisa aliendelea kunywa mtori wake kwa amani.
Alvin aligawanya midomo yake laini na kusema kwa uchungu, "Lakini huonekani kama unaelewa."
Kwa sekunde moja, ghafla alikumbushwa maneno ya Rodney aliyomwambia jana yake. Je! wanaume hao walikuwa na shida gani? Kwao, ilionekana kana kwamba Lisa ndiye aliyekuwa na makosa kwa sababu tu alikuwa amejitokeza katika maisha yao baadaye kuliko Sarah.
“Kwahiyo unataka nini kutoka kwangu?” Lisa aliinua kichwa chake. “Utafikiri mimi ni mtu mwenye wivu nikikuzuia kumtembelea. Baada ya yote, wewe ndiye uliyemjeruhi. Lakini unasema sielewi ninaposema unaweza kufanya unavyotaka. Niambie, ni aina gani ya jibu litakalokuridhisha?”
"Hicho sio nilichomaanisha." Alvin hakuwa na neno la kujitetea.
"Sijali kitakachotokea kati yako na Sarah kuanzia sasa." Lisa akanywa funda la mtori. "Sitajisumbua tena kuhusu hilo."
Kutojali kwake kulimfanya Alvin ajisikie vibaya. “Niamini ninaposema wewe pekee ndiye ninayekupenda. Baada ya kupona kabisa, nitahakikisha najiweka mbali naye.”
"Vyovyote." Lisa alichoka kusikia maneno yale yale tena na tena lakini Alvin hakuchoka kuyasema.
Lisa alipomaliza kupata kifungua kinywa alivaa na kuondoka nyumbani.
"Unaenda wapi?" Alvin aliuliza.
"Kazini."
Kuanzia siku hiyo na kuendelea, alijikita kazini kabisa. Wakati mwingine, angetembelea nyumba ya sanaa au kwenda kufanya shopping na Pamela baada ya kazi. Siku za wikendi, angefanya kazi ya hisani, kusoma vitabu, kuandika miradi, kufanya mazoezi au kutembea na Bibi Kimaro. Kila siku ilikuwa ya kutajirisha na yenye tija.

Kwa upande mwingine, Alvin hakuona tena simu au ujumbe kutoka kwa Lisa. Siku za nyuma, kila mara alikuwa akipiga simu kuuliza kuhusu aliko na ratiba kwa sababu ya Sarah. Hata hivyo, alikuwa ameacha kuuliza. Hakutaka kumpigia simu na kila mara ni yeye ndiya alikuwa akimpigia simu kwanza. Meseji zake kila mara zilijibiwa kwa maneno machache tu. Hata alikuwa ameacha kujitokeza wakati Sarah alipokuja kwa ajili ya matibabu yake.
Alipojumuika na marafiki zake Rodney na Chester kwenye jumba la klabu usiku, Lisa hakuonyesha nia ya kuandamana naye na hata hakumhoji. Kwa mara ya kwanza, alielewa kweli alichomaanisha kwa kusema 'kutomsumbua' tena. Hisia hii ilimtia wasiwasi. Hata kazini, mara nyingi alikuwa akikengeushwa na kujitenga bila kujua.
Hans alishangazwa na tabia yake ya ajabu. "Bwana Kimaro, kuna kitu kinakusumbua akilini mwako?"
Alvin alikunywa kahawa yake kabla ya kuuliza kwa kawaida, “Sikurudi nyumbani jana kwa sababu tulikuwa tukistarehe na kina Rodney klabu hadi usiku sana. Je, Madam aliwasiliana nawe?"
Hapo awali, Hans angepokea simu nyingi kutoka kwa Lisa ikiwa Alvin angechelewa kurudi nyumbani usiku. Alvin kwa makusudi hakumjulisha jana yake usiku kwa sababu alikuwa ameamua kumchunia.
Hans alijibu kwa mshangao. “Hapana.”
Alvin alishindwa cha kusema. Alilegeza tai yake kwa kuchanganyikiwa. “Vipi kuhusu bibi? Shani? Shangazi Yasmine?” Lazima angewaomba wengine wamchunguze.
"Hakuna chochote kutoka kwao pia." Hans alipepesa macho. "Bwana Mkubwa, una wasiwasi na Bibi Mdogo?"
"Hapana." Alvin alimkazia macho msaidizi wake. "Sitaki tu afikirie kupita kiasi tena na kuathiri watoto."
'Najua unamuwazia sana ila unajifanya kupotezea tu' Hans alijiwazia.
“Bwana Mkubwa, usijali. Bibi Mdogo anakuwaga na Bibi Kimaro muda mwingi na mara kwa mara wanaendaga kucheza karata kwenye makazi ya Mzee Ngugi.”
"Karata?" Midomo ya Alvin ilitetemeka. "Bado anaweza kucheza katika hali yake?"
"Kwanini isiwe hivyo?" Hans aliuliza. “Bibi Kimaro anasema Bibi Mdogo ana bahati ya kushinda kwa sababu ya ujauzito wake. Hata alimwezesha Bibi Kimaro kushinda dau la mamilioni ya shilingi walilowekeana na Bibi Ngugi kwenye mchezo wao mara ya mwisho.”
“Bibi mpumbavu. Nitakwenda kumtoa mke wangu nyumbani.” Alvin akanyanyuka na kusimama wakati simu yake ilipoita. Ilikuwa kutoka kwa Rodney.
"Alvin, njoo tena usiku wa leo.”
"Hamchoki tu kutoka kila usiku?" Alvin hakuonekana kuvutiwa kabisa.
Rodney alionekana kuchangamka sana. "Sam yupo hapa pia leo."
“Nitakujulisha baadaye.” Alvin akakata simu.
Dereva akaambiwa ampeleke kwenye makazi ya Mzee Ngugi.
Familia ya Ngugi iliishi jirani na Familia ya Kimaro. Kundi la vikongwe lilikusanyika kucheza karata. Kulikuwa na vikundi viwili tofauti vikicheza kwenye bustani. Kati yao, Bibi Kimaro ndiye alikuwa mzee zaidi, lakini hii haikumzuia kucheza kwa mapenzi.
Lisa alikuwa mdogo kati ya wanawake. Alikuwa akifahamiana na wanawake hao matajiri baada ya kucheza nao mara kadhaa. Lakini, mmoja wa wanawake waliocheza kwenye kundi lake siku hiy alikuwa Madam Campos, mama wa Jerome Campos.
Baada ya kushindwa mara mbili mfululizo, Madam Campos alisema kwa sauti ya kipekee, “Lisa, hapa kuna neno la ushauri. Mwanamke mjamzito anapaswa kutumia muda mfupi kucheza karata na muda mwingi kuongea na mume wake.”
Lisa alitabasamu bila kutoa maoni zaidi.
Madam Campos alijifanya kana kwamba anajali kweli. "Nilisikia kutoka kwa mwanangu Jerome kwamba kila mara humwona Bwana Kimaro akiingia na kutoka kwenye baa na vilabu na mwanamke kutoka kwa familia ya Njau."
Mmoja wa wanawake waliokuwa karibu alisema, “Natumaini hauzungumzi kuhusu Sarah Njau.”

Sura ya: 290

“Ndiyo, ni yeye.” Madam Campos alicheza kadi. "Wanaume, wanahitaji kudhibitiwa. La sivyo, wataungana na mtu mwingine.”
"Una hoja hapo." Lisa alicheza karata yake ya mwisho. "Nimeshinda."
Madam Campos aliandika cheki huku akisema kwa kejeli. “Huelewi ninachosema?”
“Ninaelewa,” Lisa alisema kwa utulivu, “Lakini siku hizi si jambo la kawaida sana kwa wanaume kuchepuka? Nilisikia kwamba Bw. Campos alikuwa na uhusiano usioeleweka na sekretari wake hapo awali…”
Madam Campos alihisi kufedheheshwa. “Hizo ni tetesi tu. Ninazungumzia kinachoendelea kwako sasa hivi.”
“Nimekuuliza, ni wanaume wangapi ambao huwasaliti wake zao? Zaidi ya hayo, Alvin ndiye mtu tajiri zaidi nchini Kenya. Kuna wanawake wengi ambao wanataka kufanya naye ngono. Siwezi kuwajali wote. Ninapaswa kuzingatia mambo yangu mwenyewe. Wakati mapacha niliowabeba wanapozaliwa, sitakuwa na wasiwasi hata kuhusu milo yangu katika siku zijazo.” Lisa alianza kuzichanga tena zile kadi bila kujali.
Baada ya kuzichanga zile kadi, aligundua kuwa wanawake waliokuwa kwenye meza yake walikuwa wakimtazama kwa sura isiyo ya kawaida.
Aligeuka nyuma kutazama. Alvin alikuwa amesimama nyuma yake akiwa na sura ngumu. Hakujua ni kiasi gani cha mazungumzo aliyoyasikia.
Madam Campos aliangua kicheko. “Bwana Kimaro, umesikia? Mke wako hajali hata kidogo.”
"Madam Campos, unapaswa kuzingatia mambo yako mwenyewe. Nadhani ulimshika mumeo akidanga mara nyingi tangu familia ya Campos iwe tajiri.” Alvin alimtupia Madam Campos jicho kali. Tabasamu lake likawa ngumu, na alihisi kana kwamba alikuwa ameanguka kwenye ziwa lenye maji ya barafu.
“Acha kucheza. Twende zetu.” Alvin alimvuta Lisa kwenye kiti.
"Halo, Alvin, unafanya nini?" Bibi Kimaro, aliyekuwa kwenye meza nyingine, alisimama kwa kutoridhika. "Tumekuwa tukicheza kwa saa moja."
“Bibi, saa moja haitoshi? Unataka acheze kwa muda gani? Unataka watoto wangu wajifunze karata wakiwa bado tumboni kabla ya kuwazaa?”
Baada ya kunyanyuka pale, Alvin alimshika mkono Lisa na kuliendea gari. Lisa alikaa siti ya nyuma. Wakati huo uso wa Alvin ulikuwa umejaa kejeli. “Siku hizi unajali mambo yako mwenyewe tu?”
“Unataka nini tena? Nikikufuatilia shida, nikkuacha uendelee na mambo yako napo shida!” Lisa alipiga miayo kivivu. Tabia yake ya kutojali ilimfanya Alvin kujawa na chuki.
“Mimi ni mume wako. Unapaswa kuniweka kwanza.”
“Oh.” Lisa aliitikia kwa kichwa.
“Unamaanisha nini unaposema ‘oh’? Umeyapuuza maneno yangu?” Alvin alihisi kuwa matendo na maneno yake hayakuwa na athari hata kidogo.
"Unataka nifanye nini Alvin?" Lisa alisema kwa hasira, "Kila kitu ninachokifanya nakosea. Ni kweli naumia na mambo yako mengi tu lakini inanisaidia nini hata kama nitasema? Mara zote tunaishia kugombana tu. Sasa nimeona nikae kimya ili kuwalinda watoto waliomo tumboni, hilo nalo limekukera? Niambie unataka nifanyeje, nitafanya tu usijali."
Alvin hakuweza kupata neno la kumjibu Lisa. Alijawa na mfadhaiko. Ikawa kimya ndani ya gari, Lisa alisoma riwaya za Jomba Wajo kwenye simu yake kimyakimya.
"Kuna mionzi mikali kutoka kwenye simu. Usiendelee kuitazama itaathiri watoto.” Alvin alichukua simu yake.
Lisa alitazama tu dirishani. Hakuwa na hata nguvu ya kubishana naye.
“Babe, usiwe hivi. Ikiwa kuna jambo lolote ambalo linakuchukiza, niambie tu. Hakuna haja ya kuliweka ndani ya moyo wako." Alvin alipunguza sauti yake na kujaribu kumbembeleza.
"Sina jambo lolote. Ninaishi maisha ya kuridhisha kabisa,” Lisa alimjibu kivivu.
Alvin, ambaye alihisi kupuuzwa kabisa, alihuzunika. “Si uliniambia tutakuwa tunaenda wote ninapokuwa natoka na kina Rodney na wengine? Ninabarizi nao usiku wa leo kwenye jumba la klabu. Tunaweza kwenda wote.”
“Siendi.” Lisa alihisi angeharibu hisia zake kwa kukutana na Sarah.
"Huna wasiwasi kwamba Sarah atakuwepo huko pia?"
"Sina wasiwasi." Lisa alimtazama Alvin huku akitabasamu. "Mbali na hilo, kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine hakukufanyi usiwe mume wangu."
Kwa hiyo alimaanisha kwamba asingejali hata kama angelala na Sara? Hapana, haiwezi kuwa. Alipomkumbatia Sarah kwa bahati mbaya hapo awali, alikuwa na wivu kwa muda mrefu.

“Mtoko wa usiku wa leo ni wa kumkaribisha Sam. Yuko hapa Nairobi,” Alvin alisema ili kumfurahisha, “Unapaswa kwenda.”
Lisa alipigwa na butwaa. Sam na yeye walitokea katika nchi moja na jiji moja, na uhusiano wake na Sam ulikuwa mzuri sana. “Sawa. Hata hivyo sijamuona kwa muda mrefu.”
Hatimaye Alvin akachangamka kidogo. Hakutarajia kuwa kuna siku angelazimika kumtegemea Sam kumfurahisha Lisa.
Sam, ambaye alikuwa akivua samaki ziwa Naivasha muda huo, alipiga chafya. Kwa mujibuwa imani, chafya ni ishara ya kukumbukwa na mtu. “Nani ananikumbuka tena hapa Nairobi? Inaweza kuwa Lisa?"
Sam alitoa simu yake na kutuma ujumbe wa Whatsapp kwa Lisa mara moja: [Lisa, tunaweza kuonana? Nitamwambia Alvin tukutane usiku wa leo.]
Alvin aliyekuwa ameshika simu ya Lisa, nusura ateme damu kutokana na hasira alipoona ujumbe huo ukionekana kwenye skrini yake. Kwanini Sam aliwasiliana na Lisa kwenye simu yake bila kumtaarifu yeye?
•••
Saa mbili za usiku, katika jumba la klabu ya usiku huko Nairobi.
Alvin alitokezea akiwa amezungusha mkono wake kwenye kiuno cha Lisa na kuingia. Sam, Rodney, na Sarah walikuwa tayari wameketi kwenye sofa la ngozi, wakinywa na kuzungumza.
Walipoingia wote wawili, Sam mara moja akawapungia mkono huku akitabasamu. "Hi, Lisa. Nimekumiss sana!”
Alvin alimpiga jicho kali. Sam alihisi baridi mara moja kana kwamba alikuwa kwenye ncha ya Kusini ya dunia.
"Bwana Harrison, nimekumiss pia!” Lisa alitabasamu huku akiitikia kwa kichwa. “Ni nini kimekuleta Nairobi?"
"Kuna mkutano wa biashara." Sam akakipapasa kiti kilichokuwa kando yake. "Keti hapa, Lisa."
Sam alipomaliza kuongea, tayari Alvin alikuwa amekaa kwenye siti ambayo Sama alimwelekeza Lisa. Lisa alivutwa na Alvin kukaa upande mwingine.
Kuona kwamba kulikuwa na mtu mkubwa kati ya Lisa na yeye, uso wa Sam ukapooza ghafla.
"Hujaridhika na mimi kukaa hapa?" Alvin alikodoa macho.
"… Hapana kabisa." Sam alitabasamu kwa unyonge.
Sarah, ambaye alikuwa ameketi upande mwingine, alificha macho yake yenye giza. Alitabasamu na kusema, “Alvinic, hatimaye umemtoa mke wako ‘out’ leo. Nimefurahi sana kwa sababu mimi ndiye mwanamke pekee ninayefuatana nanyi kila wakati.”
Lisa alitabasamu bila kufafanua na kumtazama Alvin. "Si ajabu ulikuwa na shughuli nyingi za kijamii usiku. Kwa hiyo ulikuwa na Sara kila wakati ulipotoka.”
Alvin alihisi kuwashwa kichwani. Alipokuwa akitaka kuzungumza, Rodney alisema bila kuridhika, “Usiwe na wivu. Chester na mimi tupo nao kila wakati. Sio Alvin na Sarah pekee.”
“Tsk tsk, Bi Njau, kweli unawafanya watu wakuonee wivu. Umezungukwa na vijana mashuhuri watatu wa Kenya, kama binti wa kifalme.” Lisa alitabasamu zaidi.
Rodney alikunja uso. "Lisa, umemkuta kila mtu akifurahia wakati wake hapa. Kwanini unataka kuharibu hali ya hewa mara tu unapoingia?”
“Rodney…” Alvin alikodoa macho yake kumuonya.
“Nimesema kitu kibaya?” Rodney alilalamika. “Sarah na sisi watatu tumefahamiana tangu tulipokuwa wadogo. Ana marafiki wachache tu kama sisi waliosalia hapa Nairobi. Kuna ubaya gani kwa yeye kufuatana na sisi?”
“Hakuna kitu kibaya. Sikusema kitu kama hicho.” Lisa alishtuka kwa sura isiyo na hatia. “Bwana Shangwe, unakuwa hunitendei haki. Ulisema kuwa ninawashambulia wengine kwa maneno yangu, lakini nakumbuka ni Bi Njau ndiye aliyeanzisha mada hii. Yeye ndiye aliyesema kuwa yeye ndiye mwanamke pekee hapa kila wakati. La sivyo, ningejuaje kuwa ninyi watu huwa mnamwalika kwenye ‘hangout’ zetu?.”
Kila mtu alipigwa na butwaa. Alvin alionekana kuwa na mawazo tele.

TUKUTANE KURASA 291-195

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI...........LISA
KURASA......291-295

Sura ya: 291

Sarah alishika glasi yake kwa nguvu. Kisha ghafla aliinamisha kichwa chake na kukohoa.
"Uko salama? Koo lako bado halijatulia?" Rodney aliuliza mara moja kwa wasiwasi.
Lisa akasema, “Kidonda chako bado hakijapona? Ni bora kupumzika nyumbani ikiwa hujisikii vizuri.”
"Lisa, umesema vya kutosha?" Rodney hakuweza kumvumilia tena. Alionya, "Unapaswa kuelewa hili vizuri. Sarah alinyongwa na Alvin kwa sababu alikuwa anatibu ugonjwa wake. Kama mke wake, sio tu kwamba huna shukrani, lakini hata unakosa huruma.”
Lisa alihisi uchungu na kupiga kelele. "Bwana Shangwe, unawezaje kusema hivyo? Siku ile si wewe uliyeniambia kwamba Alvin na Sarah bado wana hisia kwa kila mmoja na kuniambia niachane nao. Katika hali hiyo, nimshukuru kwa lipi wakati aliumia akiwa anamtibu mpenzi wake?”
Lisa aliposema hivyo hofu ilitanda machoni mwa Rodney. Kwa jinsi alivyokuwa akimtizama ni kana kwamba alitaka kumla akiwa hai.
Sura za Sam na Alvin zilibadilika kwa kusikia maneno hayo, hasa hasa Alvin. Kifua chake kilikuwa kikitokota kwa hasira. "Rodney, ulimtafuta lini na kumwambia maneno hayo?"
"Rodney, haukupaswa kufanya hivyo." Sarah alipumua kwa wasiwasi. “Nilishawahi kukuambia, mimi na Alvinic tayari tumesonga mbele.”
“Sawa, yote ni makosa yangu.” Rodney akapiga teke kiti kusafisha njia Alisimama na kuelekea uani.
“Naenda kuzungumza naye.” Sarah alimfuata kwa haraka.
Uso wa Alvin ulijawa na mfadhaiko. Alijuta kumleta Lisa. “Jamani mbona hukuniambia kuwa Rodney kakuambia maneno hayo? Kama ningelijua hilo, ningekusaidia kumpa somo kali.”
“Lisa. Rodney huwa ni mropokaji tu. Usiweke maneno yake moyoni.” Sam alisema kisha akabadilisha mada. "Unaonaje tukienda kucheza pool?"
Lisa aliitikia kwa kichwa. “Sawa.”
Alitembea kuelekea kwenye pool table akiwa na Sam. Alvin alisema kwa wasiwasi, “Una mimba. Haifai kwako kucheza pool. Kwanini nisicheze huku wewe unatazama pembeni?”
Lisa alikunja uso, na Sam akasema kwa haraka, "Alvin, jaribu kuzuia hisia zako mbaya. Hata hatuchezi soka. Ulimwita Lisa ili tu aketi hapo na kufanya drama na Sarah?”
“Drama?” Lisa nusura aanguke kicheko. “Sawa, nitakuwa makini. Unaweza kukaa pembeni, usitusumbue.” Sauti ya Lisa ilikuwa shwari.
Alvin alichanganyikiwa kupita kiasi. Mtazamo wake kwake ulikuwa mbaya zaidi kuliko mtazamo wake kwa Sam.
“Mpenzi wangu, unataka kula nini? nitakuagizia.”
“Chochote.”
Baada ya Alvin kuondoka hatimaye, Sam alimwangalia Lisa na kusema kwa upole, “Pole, lazima ulikuwa na wakati mgumu siku za karibuni, sivyo?”
Machozi yalimtoka Lisa na nusura kulia, lakini, aliyazuia na hakuonyesha hisia zake. “Hunilaumu mimi? Nilidhani ungekuwa upande wa Sarah pia.”
“Sina ukaribu kiasi hicho na Sarah. Wewe ndiye unatoka jiji mmoja na mimi, hata hivyo, "Sam alisema kwa furaha, "Watazamaji ndiyo wanaaona mchezo vizuri. Niliona sasa hivi kwamba Sarah si mtu wa kawaida hivyo.”
Lisa alimtazama kwa mshangao.
“Rodney anampenda Sarah kupita kiasi. Imekuwa hivi kila wakati. Machoni mwake, Sarah ni binti wa kifalme mzuri huku Chester akimchukulia kama dada. Kuhusu Alvin, moyo wake umebeba hatia kwa Sarah, lakini nina hakika kwamba hampendi Sarah kivile,” Sam alisema kwa umakini.
“Haijalishi.” Lisa alitabasamu kwa unyonge. “Ataamua mwenyewe.”
Sam alikunja uso. “Wewe…”
“Nimechoka. Nataka tu kujipenda mimi na watoto wangu zaidi,” Lisa alijibu. Chembe ya wasiwasi iliangaza machoni pa Sam.
"Mpenzi wangu, kula matunda." Alvin alimpelekea sinia la matunda.
Mlango wa chumba cha faragha ulifunguliwa tena. Chester aliingia huku mkono wake ukiwa umemzunguka mwanamke mmoja mwenye umbo refu. Mwanamke huyo alikuwa na nywele nyeusi ndefu na zilizotambaa kuanzia kichwani na kuangukia mabegani mwake. Alikuwa amevaa shati la maua na mikono ya mikunjo, lililomechishwa na sketi fupi ya denim nyeupe.
Hata hivyo, Lisa alipoutazama vizuri uso wa mwanamke huyo, alikosa la kusema. F*ck! Ilikuwa siku mbaya kama nini! Mwanamke huyo alikuwa Cindy Tambwe, mwanamuziki maarufu, ambaye alikuwa hajakutana naye kwa muda mrefu.

Tangu alipojitenga na familia ya Jones, Lisa hakukutana na Cindy kwa muda mrefu, lakini mara nyingi aliona habari za burudani zinazohusiana naye kwenye mitandano. Ilionekana kana kwamba Cindy alikuwa anakuwa maarufu zaidi. Lakini, Lisa hakuwa na uhusiano na Cindy, kwa hivyo hakumjali. Jambo la kushangaza ni kwamba Cindy sasa alikuwa akishirikiana na Chester. Lisa alikumbuka Pamela alishawahi kumdokeza kwamba Cindy alipata bwana tajiri jijini Nairobi, akili yake sasa ikafunguka baada ya kumwona akiwa na Chester.
Hivi Alvin na marafiki zake walikuwa na matatizo gani? Chester hakutaka mwanamke mzuri kama Charity bali alimchagua Cindy ambaye alikuwa na sura ya kuchongesha.
Kumbukumbu ya Alvin sasa haikuwa nzuri, hivyo hakumkumbuka Cindy, lakini, Sam alimtambua mara moja.
“Lisa, nilisikia kilichotokea kwenye uso wako, hatujaonana kwa muda mrefu. Nimekukumbuka sana." Macho ya Cindy yalimtoka alipomuona Lisa. Alikwenda kwa Lisa kwa furaha.
"Samahani, lakini sijisikii kuwa karibu na wewe." Lisa aliinua mkono kuashiria asisogee karibu.
Chester alikunja uso na kumuuliza Cindy, “Nyie mnajuana?”
“Hatufahamiani tu. Lisa na mimi tulisoma shule moja ya msingi na sekondari. Uhusiano wetu ulikuwa mzuri wakati wote, lakini aliwasiliana nami mara chache baada ya kuja Nairobi.” Cindy akatabasamu vibaya.
Chester aliinua macho yake. Uso wake ulionekana wenye mawazo ghafla. Alikumbuka kuwa Lisa alikuja tu Nairobi baada ya Joel kumrudisha. Baada ya kumsikiliza Cindy, inawezekana Lisa alikatisha mawasiliano na Cindy baada ya kupata mafanikio?
Lisa hakujali Chester alifikiria nini juu yake na alisema moja kwa moja, “Hujui kwanini niliacha kuwasiliana nawe?”
“Hiyo ni sawa." Sauti ya Sam ilisikika. “Nakukumbuka huko Dar es Salaam, mara nyingi alijichanganya na kundi la wanawake wa kawaida kama Janet Kileo. Ndio, hata tuliwahi kuwakuta wakiwafanyia fujo Lisa na Pamela kwenye mgahawa. Alvin, unakumbuka?"
Alvin akauchuna tu. Angewezaje kusema kwa sauti kwamba alikuwa amesahau mambo mengi? Lakini, kulingana na kile Sam alichosema, alikumbuka mwanamke huyo hakika hakuwa mzuri.
"Chester, kwanini una’date na mwanamke kama huyu?" Alvin alikunja uso. Hakuficha chukizo machoni pake.
Uso wa Cindy ulipauka kidogo, na macho yake yakaangaza machozi kutokana na aibu. "Bwana Harrison, nilikuwa mwimbaji mdogo wakati huo. Janet na wengine walikuwa wakijaribu kuniunga mkono. Lisa, najua unanidharau, lakini mimi sina nguvu kama wewe. Lazima nijitegemee mara nyingi na kuwa mwangalifu sana. Nitaharibikiwa nikimkosa mtu kama Chester.” Alimshika mkono Chester huku akitetemeka. "Chester, unapaswa kujua kuhusu maisha yangu ya zamani."
"Wacha yaliyopita yawe ya zamani." Chester aliinua tabasamu la kustaajabisha huku akipigapiga nyuma ya mkono wake. "Nenda ukaketi."
“Chester, huyu ndiye mpenzi wako mpya? Yeye ni mrembo sana.” Wakati huo, Sarah na Rodney walirudi.
Sarah alimsogelea Cindy huku akitabasamu na kumshika mkono. "Inapendeza usiku wa leo kwani nimepata kampani ya wanawake wenzangu pia. Hey, kwa nini unalia?"
“Hakuna kitu…” Cindy aliinamisha kichwa chake na kufuta machozi yake kwa haraka.

Sura ya: 292

Sarah mara moja akahisi damu yake ikiendana na Cindy. Alijihisi faraja kuwa naye utadhani alikuwa rafiki yake wa siku nyingi. "Twende tukaimbe nyimbo kadhaa."
Lisa aliwatazama wale wanawake wawili bila la kusema. Walionekana kuendana kabisa kitabia. Walikuwa ni pea iliyotengenezwa mbinguni. Laiti angejua, bora asingeenda.
Muda si muda, muziki ulianza kuchezwa katika chumba cha faragha. Lisa aliutambua wimbo huo mara moja. Ulikuwa wa Bruno Mars' 'Count On Me'.

“Oh-oh
Ukijikuta umekwama katikati ya bahari
nitasafiri duniani kukutafuta
Ukijikuta umepotea gizani na huoni
nitakuwa nuru ya kukuongoza…”

Pamela Lisa na Cindy mara nyingi waliimba wimbo huo pamoja hapo awali kwa hivyo ulimgusa sana Lisa.
Wakati huo, Cindy alichukua kipaza sauti na kusema, “Lisa, nyanyuka tuimbe pamoja. Tuliwahi kuimba wimbo huu zamani tulipokuwa marafiki. Najua nilifanya makosa kadhaa hapo awali na sijui niseme nini zaidi ya samahani. Lakini nimeu’miss urafiki wetu. Isingekuwa kwa kunitia moyo, nisingefika hapa nilipo katika tasnia ya burudani. Nimekukumbuka sana. Ni kweli..”
Aliposema maneno matatu ya mwisho, alisisitiza kidogo. Lisa alikuwa ameduwaa kwa muda, lakini haraka akaona ni jambo la kuchekesha.
Cindy hakuwa hata na aibu? Alikuwa amefanya mambo mengi sana ambayo yalimzidishia uchungu kwenye jeraha lake wakati huo.
“Cindy, unataka kuigiza, lakini sina hamu na drama zako,” Lisa alimdhihaki.
Chester akaweka glasi yake chini. Kidokezo cha chuki kiliangaza machoni pake. Rodney hakuweza kumvumilia tena na akasema, “Lisa, Cindy anakuomba msamaha kwa dhati. Kwanini unakuwa hivi? Unadhani wewe ni mzuri sana kwa sababu tu wewe ni mke wa Alvin?”
Sarah akasema. “Kwa kweli, ninaelewa hisia za kutoelewana na rafiki yako. Lakini baada ya kuwa na urafiki mzuri wa miaka mingi, ni vyema kusahau maudhi machache aliyokufanyia na kurejesha furaha yenu ya zamani. Ninauonea wivu sana urafiki ambao ulianzisha wakati wa shule ya msingi hadi sekondari. Msiruhusu urafiki huo upotee kwa sababu ya changamoto chache tu za maisha.”
Lisa alikosa la kusema. Maneno ya Sarah yalikuwa na maana nzito ndani yake. wengine wasingeelewa kwa urahisi alichokuwa akimaanisha. Alimaanisha kuwa urafiki wake na Alvin ambao ulianza miaka ishirini huko nyuma na baadaye kuzaa mapenzi kati yao haukutakiwa uachwe upotee hivihivi kwa sababu ya changamoto ya Lisa.
Kila mmoja wa watu waliokuwepo hapo alikuwa akimtazama Lisa kwa sura ya kuchukiza kana kwamba ni mtu mwenye fikra finyu na mbaya.
Baada ya muda mfupi, Lisa alicheka. “Hii ni mara yangu ya kwanza kujua kuwa mtu aliyetendewa ubaya ataonekana na makosa kwa kutosamehe wengine hata kama walimuumiza vibaya hapo awali. Cindy sasa ananiomba msamaha wa kinafiki kwa sababu anajua nipo juu zaidi yake. Nilipokuwa naporomoka miezi kadhaa nyuma alimuunga mkono Lina kuninyanyasa kwa kila nafasi waliyoyapata. Msamaha wake utakuwa na maana gani kwangu?" Lisa akaweka chini fimbo ya kuchezea pool. “Sichezi tena. Naona sistahili kuendelea kuwepo hapa nisije nikaharibu hisia za watu wengine.” Aligeuka na kuondoka baada ya kusema hayo.
Alvin akamshika mkono kwa haraka. “Lisa…”
“Alvin, mwache aondoke. Tumeshoshwa kabisana mke wako. Amekuwa msumbufu sana tangu alipotokea. Kila mtu alikuwa ametulia hapa kabla hajaja.” Rodney alisema kwa sauti ya ukali.
Lisa alitazama nyuma na kumpiga jicho la chuki. "Kusema kweli, kukaa na watu wasio na akili kama nyinyi pia inanichosha sana.”
Wakati huo, uso wa Chester ulibadilika pia. Alisema kwa ukali kuliko alivyowahi hapo kabla, “Alvin, mwondoe na usije naye tena siku nyingine.”
“Vizuri tu. Sina mpango wa kujiunga na nyie tena pia.” Lisa alitupa mkono wa Alvin na kuondoka. Alvin aliwatazama Chester na Rodney kwa hasira kabla ya kumfuata.
Baada ya wawili hao kuondoka, Cindy alionekana kuwa na sura ya wasiwasi na majuto. "Ni kosa langu. Kama nisingemwomba Lisa msamaha, hili lisingetokea.”
“Sio kosa lako. Lisa ndiye mwenye kiburi na jeuri.” Rodney alisema.
“Clank!” Sam ghafla akatupa imbo ya pool table kwenye meza. “Nyie endeleeni kufurahi, mimi naondoka.”

“Unaondoka kwanini?” Rodney aliuliza kwa mshangao, "si tumekuja hapa kukukaribisha wewe usiku wa leo?"
"Hakuna maana." Sam aliweka mikono mfukoni na kuuendea mlango. Aligeuka nyuma ghafla na kumtazama Cindy. “Alichosema Lisa kilikuwa sahihi. Hii ni mara yangu ya kwanza kuona kwamba msamaha wa kinafiki unaweza kufanywa kwa njia hii. Rodney na Chester hawakuwa Dar es Salaam wakati huo. Hawaelewi tabia yako hata kidogo. Ingekuwa mimi, nisingekusamehe kwa mambo uliyofanya pia. Chester, umefanya uamuzi mbaya wakati huu.” Aliondoka mara baada ya kuongea.
Chester aliachwa akiwa kama haelewi kinachoendelea. Cindy naye alianza kuhisi msisimko wa aibu.
Baada ya kutoka nje ya jumba hilo, Lisa alishusha pumzi ndefu. Kama ilivyotarajiwa, kila alipokuwa akikabiliana na marafiki wa Alvin, aliishia kugombana nao tu.
Lisa aligusa tumbo lake na kusema. “Samahani watoto wangu. Niliahidi sitakasirika lakini sikuweza kujizuia tena.”
"Lisa, nitakurudisha nyumbani." Alvin alimshika mkono. "Nitamwambia dereva aendeshe gari." Lisa alikaa kimya.
Akiwa njiani kurudi nyumbani, hakuzungumza neno lolote pia.
Alvin aliusoma uso wake kwa wiziwizi. Macho yake yalionekana kuchoka. "Samahani. Sikutakiwa kukupeleka huko leo. Alichosema Rodney kilikuwa kibaya mno.”
“Uko sahihi. Sitaki tena unipeleke kwa marafiki zako wakati mwingine,” Lisa alijibu kwa utulivu.
Kwa kweli, bado alihisi kukata tamaa moyoni mwake. Kila alipokuwa akikabiliana na kundi la marafiki wa Alvin, kila mara alijihisi kuwa anapambana nao peke yake. Alvin hakuwahi hata siku moja kuchukua upande wake kwa msimamo thabiti. Hakuweza hata kukumbuka ni mara ngapi hali kama hiyo ilikuwa imetokea.
Gari iliposimama, Lisa alishuka kwenye gari mara moja, kimyakimya.
“Mpenzi wangu, babe…”Alvin alimwita kwa nyuma, lakini Lisa hakutazama nyuma. Hatua kwa hatua, Alvin alianza kuwa na hasira pia. “Unataka nini? Utanionyesha tabia hii hadi lini?”
Lisa alisimama na kugeuza kichwa chake. "Labda nitaacha utakapoacha kujumuika na Rodney na wengine."
Alvin akachoka ghafla. Ingawa hakufurahishwa na Rodney na Chester, alikuwa amewajua kwa miaka 20. Walikuwa wameongozana naye kwa njia panda na nyembamba. Haikuwa kutia chumvi kusema kwamba walikuwa ni ndugu walioapishwa.
"Nilijua hautakuwa tayari." Lisa alitoa tabasamu la kujidharau kisha akageuka nyuma kuondoka.
Kwa kusema ukweli, alielewa kuwa ndege wafananao huruka pamoja. Rodney na Chester walikuwa wamekwisha kabisa kwa wale wanawake wawili hata waliwachukulia kama mabinti wa kifalme. Mapema au baadaye, Alvin angekuwa hivyo pia. Hakutaka kuwa kama Sarah na Cindy.
Kuanzia siku hiyo, Lisa hakumtafuta tena Alvin. Si hivyo tu, Makazi ya familia ya Kimaro yalichukua eneo kubwa sana hivi kwamba wangeweza kukaa hata wiki bila kuonana. Alvin alikuwa na hasira nyingi sana ndani yake, lakini hakuwa na pa kuzitolea.
Ilikuwa siku ya jumapili. Sarah alifika nyumbani kwa Mzee Kimaro kama kawaida kwa matibabu ya Alvin. Alipoingia ndani alimsikia Alvin akishindwa kujizuia. "Lisa yuko wapi? Yeye ndiye alitaka nipatiwe matibabu kyangu hapa nyumbani. Dr Nyasia anakuja lakini bado sioni hata kivuli chake.”
"Bibi Mdogo anatembea mara nyingi na Bibi Kimaro," Shangazi Yasmine alisema kwa uso wa uchungu, "Alisema yeye si daktari na hatakuwa na msaada mkubwa, kwa hivyo hataki kuwasumbua ninyi wawili."
Kichwa cha Alvin kilikuwa katika maumivu ya hasira. Maneno ya aina gani hayo? Yeye ndiye aliyekuwa akimhofia kuwa na uhusiano wa kimapenzi kana kwamba anajihadhari na mwizi, lakini ghafla akaacha kabisa kumfuatilia. Alimaanisha nini?
Sarah aliumia ndani kwa ndani kisiri. Hakutarajia hisia za Alvin kwa Lisa zingekuwa za ndani sana. Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu arudi lakini bado uhusiano wake na Alvin haukua karibu zaidi, badala yake ulikua ukizidi kuwa wa mbali zaidi. Hiyo ina maana, asingekutana naye tena baada ya ugonjwa wake kupona kabisa? Ilionekana kana kwamba angelazimika kutumia nafasi ya ugonjwa wake kuendelea kumsogeza karibu.
"Alvinic." Sarah alitembea na kuuliza kwa wasiwasi, "Lisa bado ana hasira kuhusu kile kilichotokea mara ya mwisho?"

Alvin alikosa jibu. Hakuweza kuelewa Lisa alichokuwa anawaza hata kidogo. Wakati fulani, alishuku kwamba alikuwa na unyogovu kabla ya kuzaa, lakini kulingana na Shani, aliishi vizuri na washiriki wengine wa familia ya Kimaro. Ilikuwa tu wakati alipokuwa akikabiliana naye. Lisa alianza lini hata kukataa kuzungumza naye?

Sura ya: 293

Alvin alihisi wasiwasi na hofu moyoni mwake.
“Si ajabu hukuungana na Rodney na wengine hata walipokualika. Samahani, labda sikupaswa kwenda. Mwishowe, urafiki wako na Rodney na wengine umekuwa mbaya,” Sarah alisema kwa hatia.
“Sio kosa lako. Cindy ndiye wa kulaumiwa,” Alvin alisema kwa huzuni, “Hivi dunia nzima hakuna wanawake wengine wazuri? Kwanini Chester ameamua kuwa na mwanamke huyu mwenye sifa mbaya kwenye tasnia ya muziki?”
"Kwani humjui Chester? Daima amekuwa na tabia ya kuchezea wanawake, hasa wenye umaarufu fulani. Labda anatoka naye tu kwa kujifurahisha. Anaweza kuachana naye baada ya muda mfupi.” Sarah alitazama wakati. "Wacha tuanze matibabu."
“Sawa.” Alvin akasimama.
Katika chumba cha matibabu, Sarah alicheza wimbo wa ajabu kwenye simu yake. Wimbo huo haukuwa wa Kiswahili na ulisikika kuwa wa zamani sana. Alvin alikuwa hajawahi kusikia kabla. "Kwanini unacheza wimbo leo?"
"Ndiyo, tunabadilisha hisia zako kwa njia nyingine leo. Huu sio wimbo in such, wahindi wanaitaga ‘mantra’." Sarah akatoa sarafu ya zamani. "Baadaye, utaangalia sarafu hii kwa umakini."
Dakika tatu baadaye. Alvin alisikia sauti kubwa ya kutetemeka masikioni mwake. Ni kana kwamba alikuwa amepoteza fahamu mara moja, na macho yake meusi yalionekana kuwa matupu.
Baada ya Sarah kuendelea kuuliza maswali machache na kuthibitisha kuwa kweli amepoteza fahamu, aliinama chini na kumnong’oneza sikioni, “Alvin, mtu unayempenda ni Sarah. Mtu unayempenda ni Sarah. Unamchukia Lisa zaidi na zaidi …”
Jioni mida ya saa kumi, Lisa alikuwa amepumzika kwenye bustani ya Bibi Kimaro.
Hapo hapo, Shangazi Yasmine alikuja na kumshauri kwa msisitizo, “Bibi mdogo, unapaswa kurudi kwenye chumba sasa. Bwana Kimaro alikuwa akipiga kelele alipokuja kukutazama na kukukosa.”
“Nirudi ili akanikasirikie?” Lisa aliinamisha kichwa chini ili kunusa harufu ya maua aliyokuwa ameshikiria. “Sirudi nyuma. Tutaishia kwenye vita kila ninapomwona Sarah. Sitaki kuathiri hisia zangu.”
"Lakini ikiwa hujali, huogopi kwamba Bwana Mkubwa atanyakuliwa na Sarah?" Aunty Yasmine akahema. “Bibi mdogo, nitakuwa mkali kwa maneno yangu. Ikiwa nyinyi wawili mnataka kuachana, hakuna mtu katika familia ya Kimaro ambaye atakuruhusu uchukue watoto. Wewe ndio unapata tabu sana kuwa mjamzito wa watoto sasa. Unaweza kuvumilia kuwaona wakimwita Sarah mama yao katika siku zijazo?”
"Hiyo ni kweli." Shani akaitikia kwa kichwa. “Hata kama Sara atawalea watoto vizuri, lakini utajisikiaje wewe kama mama yao kuwa mbali nao? Bwana Kimaro alikua akinyanyaswa alipokuwa mdogo pia. Bibi Kimaro ni mzee. Hataweza kushugulika na watoto."
Utulivu machoni mwa Lisa ukatanda taratibu. Asingeweza kamwe kuruhusu Sarah kuwa mama wa kambo wa watoto wake. Mwanamke mwovu kama Sarah angewanyanyasa.
Alikuwa amechoka sana kwa siku za karibuni, hivyo aliendelea kuepuka tatizo hilo. Shangazi Yasmine na Shani walikuwa wamempa ukumbusho wakati huo wa muhimu.
“Sawa, nitarudi.” Kujificha na kutokabiliana na tatizo isingemsaidia hata hivyo. Alishikilia maua yake na kurudi chumbani kwake.
Alipofika mlangoni mwa jengo lililokuwa na vyumba vyao, alimuona Alvin na Sarah wakitoka ndani. "Sarah, ngoja nikurudishe." Alvin ghafla akamshika mkono Sarah.
“Alvinic…” Sarah alipigwa na butwaa. Aliutoa mkono wake mara baada ya kumuona Lisa pembeni. Alisema kwa wasiwasi, "Bibi mdogo, usielewe vibaya."
Lisa alijisikia vibaya sana alipomuona Alvin akiushika mkono wa Sarah kwa macho yake. “Alvin, wewe—”
“Kwanini umekuja?” Alvin alimkatisha na kumpa jicho la kuudhi.
Kulikuwa na jua kali la kiangazi Nairobi siku hiyo, lakini Lisa alihisi ubaridi hewani ghafla.
Hata kama alikuwa amemkamata kwa bahati mbaya, sio tu kwamba hakujielezea, lakini pia hakuficha karaha aliyokuwa nayo baada tu kumuona Lisa akitokea. Angewezaje kufanya hivyo?
"Alvinic, usiwe hivyo," Sarah alisema kwa haraka, "Yeye ni mke wako, hata hivyo."
Alvin alishtuka. “Kama sikuamini kuwa umekufa hapo awali, asingekuwa mke wangu. Twende, Sarah. nitakurudisha.” Baada ya kuongea alimshika Sarah mkono na kuondoka zake.

Lisa alihisi kana kwamba damu mwilini mwake ilikuwa imepoa. Machozi yalimtoka huku akisema, “Alvin, unathubutu kuondoka? Ukiondoka, sitakusamehe tena.”
Alvin alitazama nyuma. Mwanamke nyuma yake alikuwa amevaa mavazi mapana ya ujauzito. Alikuwa na ujauzito wa miezi miwili, lakini umbo lake lilikuwa dhaifu kana kwamba upepo ungeweza kumpeperusha wakati wowote.
Wakati huo, moyo wake ulipiga kwa uchungu. Alitaka kurudi, lakini akakumbuka sauti kichwani mwake iliyosema, “Mtu unayempenda ni Sarah…Lisa si mwanamke unayempenda.”
“Sihitaji msamaha wako hata kidogo.” Alvin akaripuka kwa ukali. “Najisikia vibaya sana kukaa mahali pamoja na wewe.” Alimshika Sarah mkono na kuondoka bila kuangalia nyuma.
Hakuona uso wa Lisa ukibadilika na kuwa kama mfu kwa muda ule. Angewezaje kuwa hivyo… bila huruma? Yule Alvin aliyeapa kumpenda milele alikuwa wapi? Yule Alvin aliyesema hampendi Sarah alikuwa wapi? Ghafla, Lisa aliona tu mbele yake!
Shangazi Yasmine alimshikilia mara moja. Shani alimwita daktari wa familia kwa haraka.
Bibi Kimaro na Mzee Kimaro walisikia habari hiyo na mara moja wakakimbia. Waliposikia kuwa Alvin amemshika mkono Sarah na kuondoka naye, Bibi Kimaro alipandwa na hasira. “Huu ni ujinga. Mkewe ni mjamzito lakini bado anashikana na mwanamke mwingine kutoka nje. Mwambieni arudi mara moja."
“Tayari nimejaribu kupiga simu lakini Bwana Mkubwa hapokei simu zangu," Aunty Yasmine alisema bila msaada.
“Mjinga huyo! Nipe simu." Mzee Kimaro alichukua simu na kupiga namba ya Alvin.
"Ni nini, babu?"
“Alvin mkeo amezimia. Rudi hapa sasa hivi!” Mzee Kimaro alifoka, “Sijali kilichotokea kati yako na Sarah siku za nyuma, lakini wewe ni mwanamume uliyeoa sasa. Wewe ndiye uliyemuoa kwa hiari. Unapaswa kuchukua jukumu sasa kwa kuwa yeye ni mjamzito. Mwanaume anapaswa kuwajibika kwa matendo yake mwenyewe.”
Alvin alinyamaza upande wa pili wa simu. Alipotaka kuongea tu, sauti ya mwanamke aliyekuwa akipiga kelele kwa maumivu ilisikika.
“Babu, nina jambo la kufanya hapa. Siwezi kuzungumza nawe sasa hivi. Hata mimi si daktari. Unaweza kumpeleka kwa daktari ikiwa amezimia. Nitawalea watoto. Kuhusu Lisa, ninaweza tu kumtaliki na kumpa kiasi cha pesa.” Alvin alikata simu baada ya kumaliza kuongea.
Mzee Kimaro karibu ateme damu. Je, hayo ndiyo maneno ambayo mtu kama Alvin angesema? Kwanini alikuwa na mjukuu asiye na moyo na asiye na shukrani?
Aligeuka nyuma na kumuona Lisa ambaye alikuwa amezinduka. Hakuna aliyejua alipoamka. Alimtazama kwa macho yaliyojaa na tabasamu la huzuni.
"Babu, Alvin anataka kunitaliki na kunilipa pesa?" Lisa alikuwa na sura ya huzuni.
Mzee Kimaro alijikaza. Alikumbuka kuwa kila mara ilibidi aweke loud speaker kwa sababu alikuwa mzee na hasikii vizuri. Lisa alikuwa amesikia kila kitu.
Bibi Kimaro naye aliingiwa na hofu. Aliogopa kwamba Lisa atakuwa katika mshtuko. Zaidi ya hayo, alikuwa na mimba ya mapacha sasa. "Tulia. Maadamu mimi na babu yako tuko hapa, hatutamruhusu akutaliki. Kuhusu Sarah, hatutakubali Alvin kuwa naye pamoja.”
"Hukukubali Alvin kuwa pamoja nami hapo awali, lakini bado alinioa mwishowe, utawezaje kumzuia asimuoe Sarah?" Lisa alisema.

Sura ya: 294

Alvin alikuwa akitawala familia ya Kimaro. Ikiwa alitaka kufanya jambo lolote kwa njia yake, hakuhitaji hata kuwasikiliza wale wazee wawili.
Sura ya Bibi Kimaro ikabadilika. “Ni nini kinaendelea kati yenu nyie wawili? Tuligundua kuwa hamkuwa mkizungumza hapo awali. Lakini tulifikiri kwamba ni mambo ya kawaida ya wapenzi hivyo tukajua mtarekebisha tofauti zenu.”
Lisa alihisi baridi kali kwenye kifua chake. Yeye pia hakujua. Je, Alvin alikuwa amechoshwa na yeye kwa kutozungumza naye kwa muda, hivyo alitaka kurudiana na Sarah? Kwa kweli hakutarajia Alvin kuwa mkatili kiasi kile.
“Usijali. Tutakaa naye na kuongea naye. Unapaswa tu kuzingatia kuwatunza watoto kwa sasa." Huu ulikuwa wakati adimu wakati Mzee Kimaro alipokuwa akimfariji mtu kwa upole sana. Lisa alifumba macho na hakusema neno lolote.
Chumba kilipotulia tena, Aunty Yasmine alileta bakuli la mtori na kumsihi anywe. “Bibi mdogo, lazima uwe na chochote. Hata kama huna njaa, watoto walio tumboni mwako wanahitaji pia kula.”
“Shangazi Yasmine, siwezi kumuacha Sarah awe mama yao wa kambo. Ninahisi kukosa raha,” Lisa alinong’ona.
“Usilie Bibi Mdogo. Kusema kweli, nadhani Bwana Kimaro bado ana wewe moyoni mwake. Jioni hii tu kabla ya Sarah kuja, alikuwa akikutafuta kila mahali. Maneno yake yanatofautiana na hisia zake, lakini ninaona kwamba anataka kupatana na wewe. Si hivyo tu, amekuwa akirudi nyumbani kila siku sasa hivi. Jana usiku alikuwa hata akirandaranda kwenye mlango wako.” Aunty Yasmine alisema kwa kusitasita, “Au ni kwa sababu umempuuza kwa muda mrefu sana hivyo sasa anajaribu kukuchokoza?”
"Asingetumia njia hiyo ya kikatili kunichokoza, itakuwa moyo wake umebadilika sana." Lisa alitabasamu kwa uchungu na kutikisa kichwa. “Hapana, moyo wake haujawahi kubadilika. Amekuwa akimpenda Sara muda wote.”
“Sio hivyo. Bwana Kimaro anakupenda kweli." Shangazi Yasmine aliona ni vigumu kueleza kwa maneno. "Kwanini ghafla akawa hivi? Ni ajabu sana.”
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. “Anti Yasmine, una uhakika kwamba Alvin alikuwa akinitafuta kabla Sarah hajafika?”
"Hakika. Alisema hata wewe ndiye uliyependekeza kuwa Dokta Nyasia aje kwa Kimaro kwa ajili ya matibabu yake, lakini ukatoweka muda ulipofika. Alikuwa anakulaumu kwa kutokuwa naye.”
Lisa alishangaa. Hakika, ilionekana kwamba Alvin alikuwa amegeuka kuwa mnyonge ghafla. Alikumbuka kwamba baada ya Sarah kukutana na Jennifer mara ya mwisho, Jennifer alifariki muda mfupi baadaye. Je, inawezekana kwamba Sarah alikuwa amemchanganya Alvin na kitu cha ajabu? Lisa aliingiwa na wasiwasi mkubwa kuhusu hilo.
Alilala kitandani akiutafuta usingizi usiku mzima, lakini hakuweza kulala hata kidogo. Siku iliyofuata, mwili wake haukujisikia vizurii. Aliamka na kuuliza kwenye chumba alichokuwa analala Alvin. Alipogundua kuwa hakuwa amerudi kwa usiku mzima, moyo wake ulipata simanzi sana.
Alikuwa ameondoka na Sarah jana yake. Je, walitumia usiku pamoja? Je! kuna kitu kilitokea? Kichefuchefu kilimjia.
Alijitupa kwenye kochi kwa uchovu wa mwili na akili.
"Bibi mdogo, nikupe maji?" Shangazi Yasmine alimpigapiga mgongoni, akiwa na wasiwasi mwingi.
“Niko sawa. Tayarisha gari. Naenda kumtafuta kwenye kampuni yake,” Lisa alisema kwa unyonge.
Shangazi Yasmine alikuwa na wasiwasi. “Lakini uko katika hali hii…”
“Nataka kurekebisha mambo fulani,” Lisa alisema kwa msisitizo.
"Basi, tayarisha gari," Shani alisema, "Hatuwezi kuruhusu Bwana Kimaro aendelee kuwa hivi."
Aunty Yasmine akahema kwa nguvu. Alienda kuandaa gari la kumpeleka Lisa KIM International.
Lisa alipofika, mhudumu wa mapokezi alimtambua mara moja. Alama ya huruma iliangaza machoni pake. "Bibi mdogo, Bosi... Hayuko huru kwa sasa.”
Lisa alimtazama mhudumu yule machoni na kumuona ana wasiwasi mwingi. Alisema kwa kusisitiza, "Bado nitaapanda hata kama ana shughuli nyingi." Alielekea moja kwa moja juu.
Alipousukuma mlango wa ofisi kufunguka, sauti ya Alvin ya kukasirika ilisikika kutoka ndani. "Ni nani aliyekuruhusu kuingia bila kubisha hodi"
Kabla hajamaliza sentensi yake, alisimama ghafla alipomuona Lisa.

Lisa aliona kilichokuwa kikiendelea ofisini. Sarah alikuwa amekaa kwenye mapaja ya Alvin. Tukio lile lilikuwa la kuchukiza sana hata akatamani kujirusha kutoka juu ya ghorofa ile hadi chini.
“Bibi mdogo…” Sarah alisimama mbali na mapaja ya Alvin kwa hamaki. "Samahani…"
“Acha kujifanya Sarah. Huoni hata aibu kujirahisisha kwa mwanaume aliyeoa?” Lisa hakuweza kuvumilia tena. Alikimbia na kuinua mkono wake na kumpiga Sarah kofi la usoni. Hata hivyo, Alvin alishika kifundo cha mkono wake kabla hajarudisha kofi jingine.
Alvin akamtazama kwa ukali. “Lisa, unafikiri wewe ni nani? Unathubutu vipi kumpiga Sarah? Potelea mbali.” Kisha akautupa mkono wake kwa nguvu. Kama Shani asingemshikilia Lisa, angeanguka chini moja kwa moja.
“Bwana Kimaro, huwezi kufanya hivi. Bibi Mdogo ni mjamzito,” Shani alimkumbusha.
"Kama unalijua hilo kwanini umemruhusu kutoka nyumbani wakati nilikuambia umchunge?" Alvin alisema kwa hasira.
Lisa alionyesha tabasamu la huzuni. “Unafikiri angeweza kunizuia? Nitakubali vi[i mume wangu afuatane na mwanamke mwingine na kumkumbatia? Ningewezaje kulala ikiwa hukurudi nyumbani na bila shaka ulilala naye pia?"

Alvin aligeuza macho yake na hakumjibu. Hata hivyo, kukaa kimya kulimaanisha kwamba alikuwa akikubali kimyakimya. Wakati huo, Lisa aligubikwa na kukata tamaa na huzuni. Uso wake ulikuwa mweupe kama karatasi.
Alvin akakaa kimya. Kwa sababu fulani, alihisi maumivu moyoni mwake.

Wakati huo, Sarah alisema ghafla, “Samahani, Lisa. Jana nilikuwa sijisikii vizuri…”
“Kwahiyo ukaamua kuondoka na mume wangu na kwenda kulala naye kwa vile tu ulikuwa haujisikii vizuri? Ha, Sarah Langa Njau, bila shaka huna haya. Unaweza kuacha kujifanya kuwa huna hatia?”
Lisa alishindwa kuvumilia kusikiliza neno lingine. Alishusha pumzi ndefu huku akihofia kwamba angeweza kushindwa kujizuia. “Unaweza kuniruhusu niongee na mume wangu faraghani? Ikiwa una ujasiri wa kutosha kubaki hapa, basi ninaweza tu kuwaita waandishi wa habari. Tunaweza kufanya mazungumzo pamoja.”
Hasira ilitanda machoni mwa Alvin. “Hili ni suala langu binafsi. Watamfikiriaje Sarah ukiwaita waandishi hapa?”
Lisa alicheka kwa kejeli. Wasiwasi wake pekee ulikuwa sura ya Sarah. Vipi kuhusu yeye? Ina maana yeye alikuwa mtu wa kumfanyia tu dharau jinsi anavyopenda?
"Kwanini unacheka?" Alvin alihisi kukosa raha na kukerwa na tabasamu lake.
“Alvinic, acha kurumbana naye. Ninapaswa kuondoka.” Sarah akachukua mkoba wake pembeni yake kisha akasema, "Mtandao umeendelea siku hizi. Waandishi wa habari wakijua kuhusu hili, bila shaka watu watakukosoa kwa maneno makali.”

“Sarah…” Alvin aliyumba kidogo. Kama ilivyotazamiwa, ni Sarah aliyekuwa akimjali sana. "Nitamwambia dereva akurudishe."

“Sawa, nitakusubiri.” Baada ya kusema hivyo kwa upendo, Sarah aligeuka na kumtupia jicho Lisa huku mgongo wake ukiwa umemtazama Alvin. Aliondoka kwa fujo.
Lisa alikunja ngumi. Aliogopa kwamba asingeweza kujizuia na kumnyonga Sara hadi kufa.
"Lisa, ikiwa utathubutu kumuumiza Sarah, sitakuacha kamwe." Alvin alipomwona na kumuonya huku akikunja uso.
Lisa akayasogeza macho yake pembeni na kumtazama mwanamume huyo mwenye sura nzuri na ya kupendeza lakini asiye na moyo. Ni wazi bado alikuwa mwanaume aliyempenda, lakini macho yake hayakuwa ya kawaida kiasi kwamba yalimfanya aogope. Alikuwa tayari kuamini kwamba Alvin alikuwa amebadilishwa moyo na Sarah na kuwa mkatili.
"Alvin, mbona umebadilika ghafla?" Alitazama moja kwa moja machoni mwa mwanaume huyo. Macho yake yalikuwa mekundu na yamevimba. “Ulisema wazi kwamba una mimi tu moyoni mwako hivi sasa na hujawahi kufikiria kurudiana na Sarah. Ulikuwa ukinidanganya muda wote?”
Alvin alishikwa na butwaa. Alionekana kusahau kila kitu. Ni lini alimtakia maneno hayo?

Sura ya: 295

Ilikuwa haiwezekani.
Alvin alikunja uso. “Lisa, mwanamke ninayempenda amekuwa Sarah muda wote. Haijawahi kubadilika.” Mwili wa Lisa ulitetemeka.
Alitumia sentensi moja fupi tu kukana maisha yao yote ya nyuma. Alimaanisha nini kwake?
"Kwa hiyo yote uliyoniambia kwenye jumba la baharini yalikuwa ni uongo? Ulisema utanipenda katika maisha yako yote." Lisa alikuwa karibu kuangua kilio. “Unawezaje kunifanyia hivi? Umebadilika tu ghafla. Je, huoni kwamba wewe ni mtu wa ajabu sana?”
“Usiseme neno lingine. Naujua moyo wangu mwenyewe.” Alvin alikasirishwa na macho yake. “Nimechoshwa na wewe tangu zamani sana. Isingekuwa watoto, tungekuwa tushaachana zamani.”
Lisa alishusha pumzi. Wakati huo, alihisi moyo wake ukizidi kuwa baridi na baridi zaidi. Ilikuwa hivyo? Je, alikuwa amemvumilia muda wote huu? Je, asingeweza kusimama naye tena?
Hata hivyo, Alvin hakujali. Aliendelea kusema kikatili, “Baada ya wewe kuzaa watoto, nitakupa talaka. Usijali, nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka. Kitatosha kwako kutumia maisha yako yote. Kuanzia leo na kuendelea, acha kumsumbua Sara. Ikiwa sivyo, utabeba matokeo yake."
Alipokuwa akisema maneno hayo, macho yake yalijawa na hasira kali iliyopenya mwilini mwa Lisa. Damu yake ikaingia baridi.
“Alvin, mpumbavu wewe! Wewe ni mpumbavu kweli!” Hakuweza kuvumilia tena. Alilia na kuchukua kikombe mezani na kumrushia.
Alvin alikwepa kwa kutikisa kichwa. Alipoona anapandisha hasira kiasi cha kukaribia kupoteza akili yake, alijidhibiti ili asiweze kumuumiza. Akabonyeza intercom. "Waite walinzi ndani na kumtoa mtu huyu."
“Bwana Kimaro…” Shangazi Yasmine alisema huku akiwa na hofu, “Bwana Mkubwa, huwezi kufanya hivi.”
“Anti Yasmine, unahitaji kukumbuka ni nani anayekulipa mshahara,” Alvin alionya kwa ukari.
“Usiseme tena, Alvin. Ikiwa unataka kunipa talaka, unaweza kunipa wakati wowote unaotaka. Lakini sitawahi kutoa watoto wangu kwa mtu yeyote. Si hivyo tu, sitawahi kumwacha Sarah awe mama yao wa kambo.” Baada ya Lisa kumfokea kana kwamba amerukwa na akili, aligeuka na kuondoka huku akiwa amechanganyikiwa.
Alvin alipata maumivu ya kichwa kutokana na kelele hizo. Haukupita muda mrefu, Hans aligonga mlango na kuingia. "Bwana Mkubwa, nilipata matokeo baada ya kuchunguza kaburi..."
"Kaburi gani?" Alvin aliinua kichwa na kuuliza.
Hans alipigwa na butwaa. Je, Sarah hakuwa anatibu ugonjwa wa Alvin? Kwanini kumbukumbu yake haikuwa bora lakini badala yake ilizidi kuzorota? Hata hivyo, alipofikiria kuhusu matokeo ya uchunguzi, alihisi baridi moyoni mwake. Alisema kwa haraka, “Wakati fulani uliopita, ulinitaka nichunguze kaburi la Jennifer. Nilishirikiana na mlinzi wa makaburi hayo kufanya uchunguzi. Kwa kweli kilichomo kwenye jeneza si mwili wa binadamu, ni mwili wa mbwa!”
“Unataka kusema nini?” Alvin alizidi kuchanganyikiwa huku akimsikiliza, hivyo akamkatisha kwa kuudhika.
“Bi. Njau alisema angemzika Boris karibu na kaburi la Jennifer, lakini mwili kwenye uliomo kwenye jeneza la Jennifer si wa binadamu…”
“Unashuku kwamba Sarah hakuuzika mwili wa Jennifer kulipiza kisasi kwake?”
“Hilo linawezekana,” Hans aligugumia kujibu. Baada ya yote, Alvin ghafla alikuwa akimthamini sana Sarah wakati huo.
Alvin akatazama juu. Hasira usoni mwake ilikuwa imefurika. “Inatosha. Sarah hayuko hivyo.”
Ilikuwa haiwezekani kwa yeye kuamini.
“Lakini…”
“Hans, naona kwamba umekuwa ukielewana vizuri na Lisa hivi karibuni. Una nia ya kumsaidia. Ngoja nikuambie, hakuna anayemuelewa Sarah zaidi yangu. Yeye ndiye mwanamke ninayempenda. Sitamruhusu mtu yeyote kumhoji,” Alvin alisema kwa hasira, “Jambo hili linaishia hapa.”
Hans alishangaa. "Bwana Mkubwa, sijawahi-"
"Toka nje." Alvin alifungua laptop yake na kutoa amri ya kuondoka.
Hans alihisi kuchanganyikiwa na akaona ni ajabu. Ushahidi ulikuwa mbele yake, lakini Bwana Mkubwa alionekana kana kwamba hakuweza kutofautisha kati ya mema na mabaya hata kidogo. Alvin aligeuka kuwa kuwa wa ajabu sana. Ni kana kwamba alikuwa amegeuka kuwa mtu mwingine.

Ndiyo, Hans alikiri kwamba Alvin alimpenda Sarah hapo awali, lakini aliweza kuona kwamba alikuwa na Lisa moyoni mwake pia. Hans alihisi kuwa kuna kitu hakikuwa sawa kadiri alivyofikiria zaidi juu yake.
Hans alienda kwa Mzee Kimaro baada ya kutoka kazini siku hiyo. Tangu Lisa aliporudi kutoka ofisini kwake asubuhi, aliendelea kukaa kwenye kibaraza chake na kutazama nje bila kusema neno.
Hans alipofika, alimtazama kwa huzuni. “Alvin anataka uniambie nini? Au hana uwezo tena wa kuvumilia hivyo kakuambia ulete hati za talaka?”
“Bibi mdogo, umeelewa vibaya. Bwana Mkubwa hajui kwamba nimekuja kukutafuta.” Hans alisema kwa kusitasita, “Ninajua kwamba Bwana Mkubwa amekuwa akichukulia mambo tofauti sana siku hizi. Nadhani hii sio dhamira yake. Amekuwa wa ajabu…”
“Unashuku kwamba Sarah alimfanyia kitu wakati wa matibabu?” Lisa aliuliza kwa sauti ya chini.
Hans alifungua kinywa chake. Muda mfupi baadaye, alisema kwa hali ya kuchanganyikiwa, “Siwezi kueleza kwa kweli, lakini ninahisi kama Bwana Mkubwa amevurugwa akili. Kweli, hapo awali aliniomba nichunguze kaburi la Jennifer. Kuzungumza kimantiki, alipaswa kuwa na shaka kidogo na Sarah. Lakini matokeo yalipotoka, hakujali kabisa. Hii si kawaida yake ya kufanya mambo. Hata alipokuwa akimpenda Sarah siku za nyuma, hakuwahi kuwa mtu wa namna hii. Kando na hilo… Kabla ya hili, Bwana Mkubwa alikuwa akimkwepa Sarah kadri iwezekanavyo isipokuwa wakati wa vipindi vya matibabu. Hivi majuzi, alikwepa hata tafrija zilizofanywa na Rodney na wengine. Sasa, cha kushangaza, ghala akawa karibu sana na Sarah. Hii ni ajabu sana.”
Uso wa Lisa ulikuwa umepauka na kujawa huzuni. "Nilihisi pia. Aunty Yasmine aliniambia kuwa ni kana kwamba Alvin amegeuka kuwa mtu tofauti baada ya kipindi chake cha juzi cha matibabu na Sarah. Ndiyo maana nilijikaza na kwenda kumtafuta kwenye kampuni.”
Moyo wa Hans uliruka. Ilionekana kana kwamba alikuwa amekisia kwa usahihi. “Bibi Mdogo, Bwana Mkubwa lazima awe amechezewa kisaikolojia. Usimchukulie maneno yake ya kuumiza kwa uzito. Hakika ana wewe moyoni mwake. Mimi ni msaidizi wake binafsi, naweza kuhisi kitu.”
“Niambie, ninaweza kufanya nini? Ananidharau sasa.” Lisa alitabasamu kwa huzuni. "Nilienda ofisini kwake lakini nikafedheheshwa. Sasa ananichukia.”
Hans alisema kwa wasiwasi, “Bibi mdogo, ingawa sielewi ni kwa nini Bwana Mkubwa amekuwa hivi ghafla, wewe ni mke wake na yeye ni baba wa watoto. Hakika hutaki aendelee kuwa hivi, sivyo?”
Lisa akatikisa kichwa. Alikuwa katika kuchanganyikiwa. “Ni kweli sitaki hilo, lakini uelewe kuwa Alvin ndiye anatawala familia ya Kimaro sasa. Hata kama wanafamilia wa Kimaro wananiamini, hakuna tunachoweza kubadilisha ikiwa Alvin mwenyewe hataniamini. Ana nguvu zote na ushawishi. Mzee Kimaro na Bibi Kimaro ni wazee, huku Rodney na Chester wanamwamini Sarah sana. Hawatanisaidia chochote.”
Moyo wa Hans ulizama. Ilibidi akubali kwamba alichosema Lisa kilikuwa ukweli. "Bibi mdogo, kusema kweli, sikuwahi kufikiria kuwa Bi Njau angetisha vile vile. Ikiwa tutamwacha mtu kama huyo abaki kando ya Bwana Mkubwa, fikiria jinsi atakavyowatendea watoto wawili ulio na ujauzito wao sasa katika siku zijazo.”
Lisa aliumia sana. Hilo ndilo alilokuwa na wasiwasi nalo. Aliinamisha kichwa chini na kugusa tumbo lake. Macho yake yalishika alama ya uchungu mwingi. 'Watoto, nifanye nini ili kuwalinda?'
"Hans, unaweza kutafuta mwanasaikolojia mzuri? Usiruhusu Chester ajue. Nataka kujifunza kuhusu hali ya jumla ya Alvin.”
TUKUTANE KURASA 296-300

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.............LISA
KURASA........296-300

Sura ya: 296

"Sawa." Hans akashusha pumzi ya furaha. Kwa bahati nzuri, Lisa alikuwa hajakata tamaa.
Kama msaidizi wa mtu tajiri zaidi wa Kenya, Hans alikuwa na uhusiano mzuri pia na watu mashuhuri. Harakaharaka akampata daktari anayeitwa Dr Mauki. Ingawa Dk. Mauki alikuwa amestaafu kwa miaka mingi, alikuwa na uzoefu mkubwa katika utafiti wa kisaikolojia.
Jioni hiyo, Hans aliongozana na Lisa kukutana na Dk Mauki.
Baada ya Dk. Mauki kusikia kuhusu mabadiliko ya Alvin, alirekebisha miwani yake ya kusomea. Alisema, “Nilipokuwa na majadiliano ya kitaalamu na wanasaikolojia wakuu kutoka Ulaya na Marekani, niliwasikia wakitaja ujuzi wa kale wa kisaikolojia ujulikanao kama ‘Hypnotic Mind Control’ ambao ungeweza kuharibu hisia na kumbukumbu za mtu na kumtengenezea hisia tofauti. Dalili za rafiki yako zinafanana kabisa na hizo.”
Lisa alishtuka. Aliuliza kwa hamaki, “Je, inaweza kuponywa?”
Dk Mauki alicheka kwa uchungu. "Tayari nimesema kwamba ujuzi huu wa hypnotic ni wa kale sana. Marafiki zangu wanasaikolojia kutoka sehemu mbalimbali duniani walisema hivyo tu kwa msingi wa uvumi. Hakuna hata anayejua jinsi ya kufanya. Ustadi huu mbaya umepigwa marufuku katika taaluma ya kisaikolojia. Inavyoonekana, hakuna hata mmoja atakayethubutu kujaribu katika hali ya kawaida kwa sababu kudhibiti ubongo na hisia za binadamu ni jambo lisiloweza kutabirika. Mara nyingi hufanyika bila idhini ya mhusika ili matokeo yawe bora. Kwa sababu ni kinyume cha maadali ya taaluma yetu kubadili akili ya mtu bila idhini yake, ujuzi huu hutumiwa na watu wenye nia mbaya tu hivyo ulianza kusahaulika polepole.”
Lisa na Hans waliogopa sana. Hawakutarajia kwamba Sarah angekuwa mkatili kiasi kwamba angetumia ustadi wa hypnotic ambao umepigwa marufuku, kubadili akili ya Alvin. Alikuwa mtu aliyempenda, kwa ajili ya wema.
Ilikuwa ni bahati kwamba Alvin alikuwa sehemu ya asilimia ambayo haikua nyuma ya kurekebishwa.
"Kwa hiyo hakuna nafasi kabisa?" Lisa aliuliza huku akikataa kukata tamaa.
“Hiyo ni kweli, Bw. Mauki. Tafadhali fikiri juu yake,” Hans alisema kwa haraka, “Ingawa umestaafu, najua kwamba una ujuzi zaidi kuhusu hili kati ya wanasaikolojia wote nchini Kenya.”
Dk Mauki alipumua. "Kwa hakika siwezi kumponya, na kuna madaktari wachache sana wanaoweza kutibu ugonjwa huu. Hata ukipata daktari anayeweza kufanya hivyo, nitakushauri usifanye hivyo kwa sababu mchakato wa matibabu ni hatari zaidi. Nafasi za kupona ni asilimia moja tu, kwa hivyo sijawahi kusikia kesi zilizofaulu. Nadhani waliopata matibabu bado ni walemavu."
Akili ya Lisa ilikuwa tupu, na ni kana kwamba moyo wake pia ulikuwa umeacha kupiga.
Sebule ilikuwa kimya kwa dakika nzima. Kisha, Lisa akauliza. "Kwa hivyo njia bora ni kumwacha aendelee kuwa hivi?"
“Ndiyo, ndivyo ninavyomaanisha.” Dk. Mauki akanywa kahawa.
Hans aliuliza kwa wasiwasi, “Vipi kuhusu baadaye? Je, kutakuwa na madhara yoyote?"
"Mbali na hisia zake kudhibitiwa na mtu mwingine, hakuna kitu kikubwa. Itakuwa kama anaishi ndotoni.” Dr Mauki alimtazama Lisa kwa huruma. "Ni wale tu aliowapenda hapo awali ndiyo watakuwa hawana bahati."
Midomo ya Lisa ilitetemeka. Yeye hakuwa na bahati mbaya tu. Alikuwa katika kuzimu pia.
"Asante, Dk. Mauki." Alisimama na kutoka nje ya nyumba ya Dokta Mauki akiwa kama hana roho.
Hans alimfuata kwa wasiwasi. “Bibi mdogo. ..”
“Acha kuniita ‘Bibi Mdogo’. Labda sitakuwapo tena hivi karibuni.” Lisa aliyatazama yale magari yaliyokuwa yakitembea barabarani huku akijisikia mnyonge.
Ilikuwa ni ndoa kamilifu. Hakujua kwanini alikuwa akipitia mambo hayo sasa. Lisa pia hakuelewa ni kosa gani alilofanya.
“Sikuwahi kufikiria kwamba Sarah angetisha sana. Bwana Mkubwa hawatarajii kama haya yanafanyaika pia," Hans alisema kwa wasiwasi.
“Hans, hatuwezi kufanya lolote. Ikiwa tutammshughulikia Alvin kwa nguvu, tutaweza hata kumuumiza. Mwache tu, Mungu atasaidia.”
Hata kama hakumpenda tena, bado angekuwa wa kawaida kwa sehemu kubwa. Ilikuwa tu kwamba hisia zake zilikuwa chini ya udhibiti wa mtu mwingine. Bado alikuwa mtu tajiri zaidi nchini Kenya ambaye kila mtu alimheshimu.
"Na wewe je?" Hans alimuhurumia kweli.

"Mimi?" Lisa alitazama chini na kugusa tumbo lake. “Hans, kama kweli unamjali Alvin, lazima unisaidie. Sarah yuko tayari kumuumiza hata Alvin. Ikiwa watoto wangu wote wawili wataangukia mikononi mwake wakati ujao, bila shaka watateseka sana.”
“Usijali Bibi Mdogo. Ilimradi ni kwa manufaa ya watoto wa Bwana Mkubwa, nitakuunga mkono kwa nguvu zangu zote bila kujali utakachochagua kufanya—”
Hans hakuwa amemaliza kuzungumza Alvin alipompigia. "Ulienda wapi? Leo ni siku ya kuzaliwa ya Sarah. Nenda kClub yoyote maarufu na ukodi ukumbi na kuupamba. Nataka kumfanyia suprise! Umesikia nilichosema?” Sauti ya Alvin ilikuwa kali.
"... Sawa, nitaenda mara moja." Hans alimtazama Lisa kwa huruma. “Bibi Kijana—”
“Kuwa upande wa Alvin na ufanye chochote anachokuomba ufanye.” Lisa akamkumbusha, “Kama unatakakunisaidia, mfanye Alvin na wanafamilia wa Kimaro wafikiri kwamba mimba yangu imeharibika. Ni hapo tu ndipo ninaweza kuondoka.”
“Unataka kuondoka?” Hans alishangaa.
"Ndiyo, hiyo ndiyo njia pekee kwa watoto wangu wawili kuweza kuishi." Macho ya Lisa yalijawa na uchovu.
Hans alitikisa kichwa bila kusita. Alikuwa na deni kubwa kwa Alvin. Maadamu angeweza kuwasaidia watoto wake, alikuwa tayari kusaidia kwa njia yoyote aliyoweza.
Baada ya Hans kuondoka, familia ya Kimaro ilituma gari kumrudisha Lisa kwenye nyumba ya kifahari. Usiku akiwa amelala kwenye kitanda kikubwa tupu, alipokea simu kutoka kwa Kelvin. “Lisa kuna nini kati yako na Alvin? Nilisikia kuwa wewe ni mjamzito. Anawezaje kukufanyia hivi?”
Lisa alikaa kimya kwa muda na kukunja blanketi. Kisha, alijifanya kama hakuna kitu kibaya na akacheka. “Umesikia nini?”
'Sikusikia chochote. Niliona kwa macho yangu mwenyewe." Sauti ya Kelvin ilijaa hasira. "Alvin amekodiukumbi mzima kusherehekea siku ya kuzaliwa ya Sarah usiku wa leo. Aliajiri na mtu kwenda kununua mauwaridi safi kutoka nje na kuajiri mpishi mkuu wa vyakula vya Kizungu kutoka Dubai. Hata alilipua fataki kando ya bahari kwa saa mbili mfululizo na kumzawadia jumba la kifahari la dola milioni 5. Kila mtu katika Nairobi anajua kuhusu hilo sasa…”
"Kwa hiyo?" Lisa alitamka maneno hayo mawili kwa sauti kali.
Alijkuwa amejitahidi sana kupotezea mambo fulani, lakini aliposikia kwamba Alvin alikuwa akimthamini sana Sarah, alihisi maumivu makali kana kwamba kuna kisu kinampasua kipande kwa kipande. Alikuwa karibu kupandwa kichaa kutokana na wivu, lakini angeweza kufanya nini? Alvin alikuwa amelazwa akili.
“Lisa, nilikuzuia sana wakati ule. Alisema anakupenda. Lakini muda haujapita na tayari ameshakutupa wewe na mimba yako!” Kelvin alikasirika.
“Kelvin, usiseme tena. Nimechoka. Nataka kupumzika.”
“Lisa, usiogope. Haijalishi nini kitatokea, nitakuwa… daima kuwa rafiki yako. Unaweza kunitafuta kwa msaada. Ninaendelea vizuri sasa. Mimi si yule mnyonge tena ambaye ninaweza kukanyagwa tu na Alvin,” Kelvin alisema kwa upole.
“Sawa, asante.” Baada ya Lisa kukata simu, hakulala kwa usiku mzima.
Siku iliyofuata, alitazama simu yake. Habari ya mjini kwenye mitandao ilikuwa inamhusu Alvin. [Alvin Kimaro ls Having An Affair],
[Alvin Kimaro Amkabidhi Mpenzi Wake Mpya Jumba la kifahari la Dola Milioni 5]
[Alvin Kimaro sasa Ambwaga Rasmi Mke Wake Aliyeharibika Sura: Aibuka Na Chombo Safi!]
[Alvin Kimaro Alitumia Usiku Huo Pamoja Na Mpenzi Wake Mpya Hotelini]
[Utambulisho wa Mpenzi Mpya wa Kimaro Wavunja Rekodi!].
Lisa alichukua tu picha chache na kuzitazama. Picha ya Alvin akiwa amemshika Sarah mkono huku wakiingia kwenye jumba hilo la klabu ilizunguka mtandaoni. Pia kulikuwa na picha walipoingia ndani ya hoteli hiyo wakiwa wamekumbatiana na video za fataki hizo za kupindukia.

Sura ya: 297

Alvin na Sarah walionekana kukaribiana sana katika kila picha kana kwamba walikuwa mapacha walioungana.
Katika ukurasa wake wa facebook, Sarah aliweka picha ya keki ya ngazi tatu. Juu ya keki hiyo kulikuwa na wanasesere wawili, binti wa kifalme na mwana mfalme. Alikuwa ameandika nukuu pia: [Sikuwahi kufikiria kuwa ungesherehekea siku yangu ya kuzaliwa pamoja nami tena. Nakupenda. Yote yalianza na wewe, na yataishia na wewe!]
Picha na ujumbe wa Sarah vilizua ghasia mtandaoni!
[F*ck, nilifikiri Alvin Kimaro alikuwa mtu muungwana sana. Juzijuzi hapa aliufahamisha ulimwengu juu ya msimamo wake kwa mke wake. Muda haujapita, anatutambulisha uhusiano wake mpya wa kimapenzi sasa. Ni upuuzi gani huu?]
[Me too. I even envied the otherworldly love between The Great Kimaro and his wife.] Hii ilikuwa ni komenti kutoka Naijeria.
[Lisa is so pitiful.] Mchangiaji kutoka Afrika Kusini.
[Mwanamke huyu anaonekana kama kikongwe. What a shameless person.] Mchangiaji kutoka Kenya
[Die, you b*tch!] Mchangiaji kutoka Uganda akimkashifu Sarah.
[Kujitongozesha kwa mume wa mtu mwingine, huoni aibu?] Mchangiaji kutoka Tanzania.
Sarah hakuambulia hata komenti moja ya kumsifia, zote zilikuwa zikimponda tu!
Lisa alizima simu yake. Aliinuka na kupiga mswaki akijitahidi kupotezea kila kitu alichojionea. Alifikiri asingelia tena, lakini akiwa katikati ya kupiga mswaki, alibubujikwa na machozi. Ni kwa sababu aliuona mswaki wa Alvin kwenye sinki la kuogea.
Alipotoka nje ya chumba chake saa 8:30 asubuhi, wajakazi waliopita mara kwa mara walimtazama kwa huruma.
Alijua kwamba kila mtu alikuwa ameona habari hiyo.
Alipokaribia sebule ya chakula, sauti ya Iveta, ambaye alikuwa mkwe wa Kimaro aliyeolewa na Spencer, mtoto pekee wa kiume wa Mzee Kimaro, ilisikika kutoka ndani. “Nilidhani Alvin anampenda sana Lisa lakini alibadili moyo wake ndani ya siku chache tu. Hata alitoa Jumba la kifahari na maonyesho ya fataki kwa mwanamke mwingine. Nadhani hamjali tena Lisa.”
Spencer alisema, “Siwezi hata kushangaa. Tulijua ni kiasi gani Alvin alimpenda Sarah hapo awali, na Lisa… Uso wake umeharibika. Haonekani mrembo tena.”
“Uko sahihi. Hata kama ningekuwa mimi, nisingevumilia sura ya kutisha kama ile. Alvin naye ni mtu jamani, tusimlaumu sana!” Iveta alikandamizia.
Bibi Kimaro alisema. "Wanaosikitisha ni wale watoto wawili ambao bado hawajatoka tumboni."
Iveta alisema, “Alvin bila shaka atataka watoto, sivyo? Mimi ni mama pia. Naamini Lisa hakika hataweza kuvumilia kuwaacha watoto wake wawili kwa familia ya Kimaro.”
Mzee Kimaro alisema kwa sauti nzito, “Hata hivyo, watoto wa familia ya Kimaro lazima wakae katika familia ya Kimaro. Hakuna anayeweza kuwachukua.”
Lisa alisimamisha hatua zake bila kupenda. Aligeuka na kuondoka bila mtu yoyote kumwona.
•••
Katika ofisi za KIM International, Alvin aliona habari mbaya kwenye kompyuta yake. Uso wake ulibadilika ghafla. "Umegundua ni nani aliyesambaza habari hiyo?"
“Ni kampuni ya vyombo vya habari iliyofadhiliwa kwa siri na familia ya Campos," Hans alisema ukweli.
"Familia ya Campos?"
Alvin alikodoa macho. Alitokea hisia mbaya na hatari wakati huu. "Vema, familia ya Campos inaenda kinyume na mimi sasa."
Hans alitetemeka kidogo, lakini alijipa ujasiri na kusema, “Bwana Mkubwa, kwanini usiujulishe umma kwamba wewe hauna uhusiano wa kimapenzi na Sarah bali ni marafiki? Umeoa sasa, kwa hivyo si vizuri kwa sifa ya Kampuni ikiwa hii itaenea.”
Alvin alikaa kimya kwa muda. Kabla hajamjibu, Thomas akampigia simu. “Bwana Kimaro, kuna kitu kimetokea. Sarah aliumia baada ya kugongwa na mtu alipotoka asubuhi ya leo.”
Nusu saa baadaye, Alvin alifika hospitalini. Thomas alikuwa amesubiri kwa muda mrefu mlangoni. “Bwana Kimaro, hatimaye umefika. Sarah bado amelala kitandani. Daktari alisema ana mshtuko wa ubongo.”
Alvin alikunja uso. Akausukuma mlango wa wodi ile kwa nguvu. Paji la uso la Sarah lilikuwa limefungwa bandeji. Uso wake mzuri, mdogo, ulikuwa na hali dhaifu.
“Mbona hukuniambia?” Alvin aligusa jeraha kwenye paji la uso wake.
Sarah aligugumia kwa maumivu na kulazimisha tabasamu. "Hakuna shida, ni mkwaruzo mdogo tu."

Thomas, ambaye alikuwa pembeni, mara moja alisema, “dada, kwanini usiseme ukweli?” Alimgeukia Alvin kwa sauti ya huzuni, “Dada yangu alivuja damu nyingi sana Bwana Kimaro. Nakusihi ufuatilie hili kwa ajili ya Sarah. Sijui ni mtu gani aliyefichua picha zenu mkisherehekea siku yake ya kuzaliwa, lakini sasa kila mtu kwenye mitandao anamkaripia dada yangu na kumwita majina ya ajabu. Hata wengine wanamwita malaya. Kwa vyovyote vile, wanatumia kila aina ya maneno machafu kumzungumzia. Wengine hata wanadiriki kumfuatilia mpaka nyumbani kwake. Ni hatari sana kwake.”
Alvin alitafakari kwa muda na kusema, “Kwa hali hiyo, itabidi ahamie kwenye nyumba yangu sasa.”
“Ndiyo.” Macho ya Thomas yakaangaza. "Nilisikia kwamba ulinunua nyumba ya kifahari karibu na bahari miaka michache iliyopita. Sarah anapenda kuishi kando ya bahari. Twende huko.”
Alvin aliganda. Kweli alikuwa na jumba la kifahari kando ya bahari huko Mombasa, lakini… aliwahi kuishi huko na Lisa. Alikuwa chini ya maamuzi tata. Akubali ama akatae!
“Kaka…” Sarah alimkazia macho Thomas lakini kwa haraka akamgeukia Alvin. Kwa sura nzuri, alisema, "Alvin, ulinunua jumba la kifahari ufukweni mwa bahari kwa sababu ulikumbuka niliwahi kusema napenda kuishi kando ya bahari?"
Akiwa amekabiliana na macho ya mwanamke huyo yanayometameta, Alvin alitazama pembeni na kutabasamu. “Ni kweli mpenzi!”
'Basi nitahamia huko,” Sarah aliuma mdomo wake uliopauka na kusema kwa tabasamu tamu.
Alvin alikuwa hoi na aliishia tu kutikisa kichwa.
Thomas aliongeza, “Lakini hiyo siyo solution. Huwezi kujificha milele katika jumba la Alvin Kimaro. Huwezi hata kwenda kazini kwa sasa kwa sababu ya maneno ya watu. Kila mtu anakuita wewe ni mchepuko tu. Hii si haki kwako dada yangu. Ni wazi nyinyi wawili mlipendana kabla ya Lisa. Kwanini wakuseme vibaya?”
“Kaka achana nao. Tayari nimeridhika kwamba nimerudiana na Alvin.” Macho ya Sarah yakarembua kwa deko. "Niko tayari kuitwa mchepuko milele ikiwa ni kwa ajili yake."
Alvin alikipapasa kichwa chake na kuhisi hisia za hatia nyingi moyoni mwake. "Usijali, sitakuacha uwe mchepuko milele." Dokezo la chuki likaangaza machoni pake. "Naenda kwa Mzee Kimaro sasa hivi kushughulikia suala lako."
Baada ya kutoka hospitali, Alvin aliingia kwenye gari. Saa moja baadaye, alifunga breki mbele ya makazi ya familia ya Kimaro
Jua lilikuwa linaangaza sana, na Lisa alikuwa ameketi kwenye bustani ya Bibi Kimaro akila zabibu huku akisoma kitabu cha riwaya za Jomba Wajo. Sekunde kadhaa baadaye, hisia za ajabu zikamjia ndani ya moyo wake. Alihisi kama Alvin alikuwa karibu yake, lakini zilitoweka ghafla baada ya kugeuza kichwa chake na kuona mimea tu na upepo.
Aliporudisha tena mawazo yake kwenye kitabu, alisikia tambo za mtu zikitembea kwa hatua kubwa. Aliinua kichwa chake baada ya kusikia sauti ya nyayo hizo. Alvin alijitokeza akiwa amevalia suruali ya kawaida ya rangi ya kijivu iliyokoza na shati la bluu juu yake. Mikono yake ilikuwa imekunjwa. Mwonekano wake mzuri uliweza kuufanya moyo wa mwanamke yeyote kupepesuka, lakini ilisikitisha kwamba macho yake yalikuwa yamejawa na mapenzi sifuri.
Macho yake yalitisha zaidi kuliko walipokutana mara ya kwanza. Lisa alijipa moyo kwamba alikuwa amezoea ujeuri wa mwanamume huyo, lakini kwa wakati huo hakuweza kuwa na ujasiri wa kukabilana naye hata kidogo. Mwanaume aliyempenda sana alionekana kuwa hatari zaidi ya mtu yoyote aliyemfahamu kwa wakati huo.
“Unataka nini?” Lisa aliuliza huku akiinamisha macho yake kana kwamba anaficha huzuni ndani yake.
“Wewe ni mke wangu. Chochote ninachokitaka kwako nitachukua muda wowote ninapohitaji.” Alvin alifoka na kumfanya Lisa kupigwa na butwaa kwa jinsi alivyosema maneno hayo.
“Kwa hiyo bado unajua kuwa mimi ni mkeo? Nilidhani umesahau zamani,” Lisa alisema kwa dhihaka.
Alvin alikasirika. “Usinisumbue. Nahitaji ufanye kitu kimoja tu kwa sasa. Nitaitisha mkutano wa vyombo vya habari. Unatakiwa kutoa taarifa kwa umma kwamba mimi na wewe tuliachana mwezi uliopita. Kuhusu ndoa yetu, ilikuwa ni ndoa ya mkataba tangu mwanzo na mktaba wetu umekwisha rasmi.”

Lisa alimtazama kwa mshtuko. Macho yake yalionyesha kutokuamini.

Sura ya: 298

Alvin hakufurahishwa na macho yake na hakuweza kujizuia kuwasha sigara. Baada ya kuvuta pumzi, kadhaa aliufanya moyo wake kuwa mgumu. “Umenisikia? Nilikuoa tu kwa sababu nilikuwa nakerwa na familia ya Kimaro kuwa wananilazimisha kuoa. Na wewe ulitaka nikuoe tu kwa sababu ulinidhania kuwa mimi ni mjomba wa Ethan Zakaria Lowe.”
Lisa alishindwa kuvumilia tena. "Ndio, sikatai, tulifunga ndoa mwanzoni tu kwa sababu ya mkataba, lakini baadaye, sote wawili tulikubali kukaa kwenye uhusiano. sikukulazimisha.”
"Nyamaza." Alvin alijikuta maneno yake yakimchoma. “Ni kwa sababu wewe ndiye ulianza kunitongoza. Unafikiri mwanamke mwenye ujasiri wa kumtongoza mwanamume huyo ni mwanamke wa muoa kweli?”
Ingawa moyo wake ulikuwa tayari umejawa na matundu, macho ya Lisa bado yalikuwa mekundu kwa kukata tamaa. "Alvlisa, ni wewe kweli? Au Sarah ameshakufanya kuwa msukule? Ili tu Sarah asionekane mbaya kwa wengine, unataka niseme uongo na kutangaza kuwa tayari tumeachana. Ulimwengu wa nje utafikiri kwamba nilikuja kwako kwa sababu ya pesa za familia ya Kimaro. Ndiyo, jina la Sarah litatakaswa, lakini vipi kuhusu jina langu? Nitalaaniwa mpaka kwenye kaburi langu. Umewahi kufikiria hisia zangu kweli?"
“Kwanini nizingatie hisia zako? Sikupendi na sikuhitaji.” Alvin alikunja uso bila kujali, maneno yake yalizidi kuwa makali na ya kuchoma moyo.
Hatimaye Lisa aliachia kicheko cha uchungu, machozi yote yakimtoka. Hakujua ilikuwa ni kwa sababu njama za Sarah zilikuwa na nguvu sana, au ni kwa sababu Alvin hakuwahi kumsahau Sarah tangu mwanzo.
Alvin alijikuta akicheka bila raha. “Umesikia nilichosema?”
“Kwanza, hujali kuwa umemsaliti mke wako, lakini unataka nijishushe ili kulinda heshima ya Sarah na sifa zako! Endelea kuota. Watu kwenye mtandao hawana makosa. Sarah atabaki kuwa mchepuko tu." Lisa alishindwa kujizuia na kumfokea.
"Nyamaza!" Alvin alimpiga kofi usoni bila huruma. Lisa aliganda na kufunika uso wake, machozi makubwa yakitiririka mashavuni mwake.
"Lisa Jones, nakuonya, nisikusikie tena ukimtukana Sarah." Alvin alikodoa macho na kuonya neno kwa neno. "Ninakushauri ufanye kama ninavyosema, au nitamwambia Chester amwambie Daktari Angelo aache kutibu ugonjwa wa baba yako."
"Alvin, nyoko wewe." Lisa alilazimishwa kulia na kulia kwa kukata tamaa.
“Namaanisha.” Kwa sababu fulani, Alvin hakutaka kuona sura yake ya kulia na akageuka kuondoka.
“Alvin Kimaro, nitadili na wewe hatua kwa hatua” Lisa akasema kwa ghafula, “sijali hata kama utanitaliki, sitakuachia watoto wangu na nitafuta uhusiano wote na wewe.”
"Endelea kuota. Watoto ni wangu.” Alvin alimtishia. “Lisa Jones, kama unataka Mawenzi ikufilie mbali, endelea kucheza na mimi. Najua pia Joel ndiye ndugu yako pekee aliyebaki duniani. Jitafakari!” Alvin alimaliza na kuondoka bila kuangalia nyuma. Lisa aliitazama sura yake isiyo na huruma iliyoonekana kugubikwa na giza.
Katika muda usiozidi dakika 20, Lisa alipokea simu kutoka kwa Daktari Angelo akisema kuwa asingeweza kuendelea kumtibu tena Joel.
Lisa alichanganyikiwa. Ikiwa angekosa mtu wa kumtibu Joel, Nina Mahewa na binti yake wasingemjali pia. Familia ya Ngosha iliongozwa na Damien sasa. Joel angekufa muda si mrefu.
Hakuwa na chaguo tena, na suluhisho pekee ilikuwa ni kukubali mkutano wa vyombo vya habari ili kukiri kwa dhati kuwa yeye na Alvin hawakuwa mke na mume tangu kitambo.
[Natamka kwa dhati kwamba Alvin Kimaro si mume wangu tangu mwezi jana. Natamani apate mpenzi wake wa kuendelea kumtunza kwenye hali yake. Sasa kwa kuwa mambo yamefikia hatua hii, sina budi kusema ukweli. Mimi na Alvin Kimaro tuliachana mwezi uliopita. Tulioana tu kwa sababu Alvin alilazimishwa na familia yake, na kila mmoja wetu alichukua kile alichohitaji katika ndoa yetu. Hakukuwa na hisia za kimapenzi kati yetu.]
[Sarah Boris Langa Njau ni mpenzi wa Alvin wa utotoni ambaye alitengana naye kwa sababu ya zisizozuilika. Yeye si mchepuko. Kwa dhati ninawatakia wawili hao kila la heri.]
Baada ya chapisho hilo kupakiwa…Wanamtandao wengi walimkaripia Lisa kwenye profile yake.

[Unamaanisha nini kusema kila mmoja alichukua kile alichohitaji? Alvin Kimaro lazima awe amekupa pesa nyingi basi!]
[What the f*ck, kwa kweli niliamini katika uhusiano wako hapo awali. I feel like a fool now.]
[How much money did you receive?]
[Nafikiri unapaswa kuacha kuwa Mkurugenzi wa Kampuni na kuingia katika uigizaji. Uigizaji unakufaa.]
Mara tu baada ya hapo, Sarah alianza kuchapisha picha mbalimbali za Alvin na yeye wakati wa miaka yao ya shule. Wanamtandao wengi walianza kusifia upendo wao wa muda mrefu.
Lisa hakuzingatia hilo. Ali’delete kabisa app ya Facebook kwenye simu yake na hakusoma tena habari hizo.
Pamela akampigia simu kwa hasira. "Lisa Jones, umekuwa kichaa? Unamaanisha nini kusema uliachana na Alvin Kimaro mwezi uliopita? Hujaachika hata kidogo! Ana uhusiano wa kimapenzi na yule malaya Sarah Njau. Wanawezaje kukufanyia uhuni kama huu? mbona unafosi kuwa mpole kiasi hicho? Ningekuwa mimi, heeeh! Sijui tu. Umesikia watu hao wanavyokuita? Hapana, sikubali. Nataka kuwafunza adabu mbwa hao wawili, hawanijui eeh?!”
“Pamela, sikuwa na chaguo. Alvin alinitishia baba yangu. Nisingetoa kauli hiyo, angesimamisha matibabu ya baba yangu,” Lisa alisema akiwa hoi.
“Bado unasema Alvin ni binadamu? Kweli ni!@#$%^&. Fanya haraka uachane naye! Mbwa huyo!” Pamela alikasirika.
"Nadhani atanitaliki tu baada ya kuzaa watoto."
"Anataka kuiba watoto wako pia?" Pamela karibu kutapika damu. “Si ana Sarah? Mwache azae na Sarah. Beba watoto wako mama!”
"Familia ya Kimaro inawezaje kuruhusu watoto wao kulelewa nje?" Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Usijali, nitafikiria njia.”
“Kweli sikubali. Huwezi kumruhusu Sarah awe mama wa kambo wa watoto wako.” Pamela alionya.
“Bila shaka.” Lisa alikata simu huku akiwa na uso wa huzuni.
•••
Sarah alihamia kwenye jumba la kifahari la ufukweni mwa bahari huko Mombasa.
Thomas alitazama huku na huko na kusema, “Sarah, mahali hapa ni pa anasa sana. Haishangazi ulikuwa unasumbua ubongo wako kujaribu kupata njia ya kuingia humu. Nilisikia kwamba huu ndio ufukwe wa bei ghali zaidi huku Mombasa.”
"Sikutaka kuhamia hapa kwa sababu ni ghali." Sarah alitabasamu na kuketi kwenye sofa.
“Najua. Ni kwa sababu hapa ndipo Lisa Jones na Alvin walikuwa wakikaa. Hehe, Lisa akigundua, labda atatapika damu kwa hasira." Thomas alimtazama dada yake kwa mshangao. “Alikuwa akijifanya kana kwamba ni Bibi Kimaro, lakini sidhani kama anaweza kulinganishwa hata na thamani ya kinyesi cha Bibi Kimaro kwa sasa. Hujui ni familia ngapi za kitajiri huko Nairobi zinajikombakomba kwangu sasa. Kila mtu anajua kuwa wewe ndiye Bibi Kimaro wa siku zijazo.”
"Hakuna haraka. Nitakapoolewa na Alvin, kutakuwa na watu wengi zaidi ambao watakusujudia,” Sarah alisema kwa kiburi. "Kwa jinsi mambo yanavyoenda, utakuwa mfalme hivi karibuni."
Simu ya Thomas iliita ghafla na akaenda pembeni kuipokea. Ghafla alianza kucheka. Kisha, akarudi na kusema, “Natoka.”
"Wapi?" Sarah akamtazama kwa wasiwasi. “Usiende kufanya ujinga wako tena. Japo Alvin ananipenda, hatakubaliana na ujinga wako, usiniharibir.”.”
"Usijali, naenda kumpa Pamela Masanja somo dogo tu la namna ya kuishi jijini Nairobi." Thomas alifoka.
Sarah akacheka kidogo. "Rafiki ya Lisa Jones?"
“Ndiyo. Anaonekana mrembo sana, lakini ana kiburi sana. Nilipomfuata hapo awali, alinikataa na kunitukana. inaniuma sana kukataliwa na msichana mimi.”
“Hah, bado nakumbuka aliponitukana hospitalini." Sarah aliongea kwa sauti ya kisasi.
Thomas alikoroma. “Nilimwekea mtu wa kumfuatilia kwa siku kadhaa sasa. Niliapa, nisipomf*** labda mimi si Thomas Njau.”
Sarah aliikunjua uso wake kwa tabasamu. Ingekuwa ni mtu mwingine yeyote, asingemkubalia. Lakini kwa Pamela Masanja, hakuwa na pingamizi. Hakumpenda kwa kuwa ni rafiki wa Lisa.
"Sawa broo. Nenda kafurahie, ila usimwue tu. Kula kabisa huo mk***”
“Usijali. Najua ninachofanya.” Thomas alivimba kichwa.

Sura ya: 299

Baada ya Lisa kuoga, Pamela alimtumia ujumbe akimkaribisha waende baa kufanya party ya kumfariji kwa matatizo yake. Lisa alijua kwamba Pamela alihofia yeye kuwa peke yake na mawazo yake, kwa hiyo alikubali kwa furaha.
Lisa alipokuwa tayari, alimpigia simu Pamela ili kumwambia kuwa angempitia nyumbani kwake. Lakini badala ya kujibu, Pamela alipiga kelele, "Fanya haraka unisaidie. Nimevamiwa! Siwezi kutoka.”
“Umevamiwa na nani…” Lisa alichanganyikiwa na ghafla akamsikia Pamela akisema, “Kuna watu wanagonga mlango kwa fujo ... hawasemi hata wao ni kina nani…”
“Bam!”Ghafla, kulikuwa na sauti kubwa za harakati kwenye upande wa pili wa simu. Kisha, ikawa kimya!
Lisa kwa haraka akarudia kupiga namba ya simu ya Pamela lakini simu haikuweza kupokelewa. Hisia mbaya ilimtawala. Umbali kutoka nyumbani kwa Mzee Kimaro mpaka nyumbani kwa Pamela ulikuwa angalau saa moja kwa gari. Kwa vyovyote vile asingeweza kufika kwa wakati na kumuokoa Pamela.
Baada ya kutafakari, alimpigia simu Kelvin kwa haraka. Kelvin aliishi karibu sana na Pamela. "Kelvin, kuna mtu alivamia nyumba ya Pamela. Unaweza kuharakisha huko na kunisaidia kuangalia? Ninaogopa kuna kitu kibaya kimemtokea. Piga namba hii kujua anuani yake."
“Sawa, nitaenda huko sasa hivi.”
Baada ya kukata simu, Lisa alipiga simu polisi na mara moja akaendesha gari hadi getini.
Mlinzi wa getini hakumruhusu atoke, lakini, kwa kuwa alikuwa na wasiwasi sana, aligonga geti kwa gari. Geti bado lilikuwa limefungwa na halikuweza kuachia njia, lakini mlinzi aliogopa na kumfungulia geti haraka. Baada ya kumruhusu atoke, mlinzi alimpigia mfanyakazi wa nyumbani.
Lisa aliendesha gari kwa kasi kama siku ile alipopata ajali. Speed meter ilisoma 150kph. Umbali wa saa moja kwa mwendo wa kawaida ulipunguzwa hadi dakika 20 tu. Hatimaye alifika kwenye nyumba ya Pamela.
Alipoingia, mlango wa ghorofa ulikuwa tayari umefunguliwa. Sebuleni kulikuwa vululuvululu na sauti za mapambano zilisikika kutokea chumbani.
Aliingia ndani kwa haraka. Pamela alikuwa amelala kitandani, macho yake yakiwa yameduwaa. Nguo za sehemu ya juu ya mwili wake zilikuwa zimechanika na matiti yakiwa wazi huku uso na mwili ukiwa na michubuko.
Kelvin alikuwa akipambana na wanaume watatu peke yake, wawili ambao walikuwa warefu na wenye misuli, na waziwazi walionekana kuwa majambazi. Kelvin alikuwa tayari amejeruhiwa katika sehemu nyingi. Mtu wa tatu hakuwa mwingine bali Thomas Njau. Alichukua fursa hiyo kushughulika na Pamela, akimalizia kumvua suruali yake.
“Wewe mjinga!” Lisa alimkemea kwa hasira. Tukio hili lilimtoboa macho Lisa bila huruma. Bila kujali alishika pipa la taka lililokuwa pembeni na kumponda Thomas.
Thomas alipandwa na hasira na kumfuata, akamshika na kumtupia mbali.
“Lisaa…” Kelvin alimkimbilia na kumdaka kbal hajaanguka chini. vinginevyo angefikia tumbo, na sijui ingekuweje kwa mapacha wake.
Hata hivyo, wale majambazi wawili waliokuwa nyuma yake waliona hivyo na mara moja wakamchoma Kelvin kisu begani.
“Kelvin...” Lisa alishtuka na kumshika kwa hofu.
"Usijali, ni ... jeraha dogo." Kelvin alikunja uso wake kwa maumivu, lakini bado alijilazimisha kumtoa wasiwasi Lisa.
Moyo wa Lisa ulitetemeka huku macho yake yakimtoka machozi. Hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Kelvin kuchomwa kisu ili kumuokoa. Lakini, Lisa aliishia kuhisi hatia tu juu yake na hakuweza kumlipa chochote kingine.
"Huyu ni mpenzi wako au wa Pamela?" Thomas hakuelewa somo hapo. "Lisa Jones, inaonekana umekuwa ukimsaliti mume wa dada yangu."
“Thomas Njau, mnyama wewe! Tayari nimewaita polisi. Utajuta kuzaliwa safari hii. Tuone kama Alvin atakutetea tena.” Lisa hakuwahi kumchukia mtu kama alivyokuwa akimchukia Thomas wakati huo.
“Hehe, endelea kuota. Alvin ni mume wa dada yangu, wakili maarufu. Hakika atanisaidia.” Thomas alionyesha kujigamba kwa jazba na dharau. "Baada ya yote, nimefanya mambo kama haya mara nyingi hapo awali. Sikuzote amenisaidia.”
Aliendelea kusema 'mume wa dada yangu', lakini Alvin alikuwa mume wa Lisa. Maneno hayo yalimkera sana Lisa hadi mwili ukamtetemeka.

Kwa bahati nzuri, polisi waliingia ndani wakati huo na kuwakamata haraka Thomas na wenzake.
Kelvin na Pamela walipelekwa hospitalini haraka. Akiwa amekaa kwenye gari la wagonjwa akielekea hospitali, simu ya Lisa iliita bila kukoma. Zote zilikuwa simu kutoka kwa familia ya Kimaro, akiwemo Alvin.
Aliitikia wito wake na mara akasikia kishindo cha Alvin chenye hasira. "Lisa Jones, uliendesha gari usiku tena kwa kasi ya kuhatarisha maisha. Ulithubutu hata kugonga geti la uzio. Ninakwambia, ikiwa chochote kitatokea kwa watoto wangu, nitaondoa maisha yako.”
"Alvin, kwa hivyo bado unakumbuka kuwa una watoto, huh?" Lisa alishindwa kujizuia na kumfokea mtu huyo, “unajuwa kwanini nilitoka nje? Ni kwa sababu Thomas Njau alivamia katika nyumba ya rafiki yangu mkubwa na kutaka kumbaka. Yote ni makosa yako. Ni kwa sababu yako huyo fisadi amekuwa na kiburi na ukosefu wa maadili. Alvin Kimaro, nakuchukia. Ninakuchukia sana!” Baada ya kutoa hisia zake, machozi yake yalidondoka kama mkufu wa lulu uliovunjika. Alifunika uso wake na kuruhusu kububujikwa na machozi.
Kelvin ambaye alikuwa amelala kiunyonge kwenye machela, aliushika mkono wake kwa macho yaliyojaa wasiwasi. Lisa akakata simu na kuruhusu kilio chake kirindime ndani ya gari la wagonjwa. Hakuwahi kuwa na majuto zaidi ya siku hiyo. Hakupaswa kamwe kuwa na moyo mpole na mwanaume huyo. Hakupaswa kamwe kumruhusu amtawale.
•••
Usiku sana hospitalini. Baada ya dakika 40 katika Emergency Room, daktari alitoka. "Mgonjwa wa kike hakushambuliwa kabisa lakini bado alipata majeraha katika maeneo mengi. Ana mshtuko wa moyo, na kwa vile alikuwa amelewa dawa, huenda ikamchukua zaidi ya saa kumi kupata fahamu.”
Hatimaye Lisa alishusha pumzi. Asante Mungu… Asante Mungu Thomas hakufanikiwa kumwingilia Pamela. Vinginevyo, hakujua jinsi Pamela angeikabili habari ya kubwakwa na Thomas.
"Vipi kuhusu mgonjwa wa kiume?" Lisa aliuliza kwa haraka.
“Kisu kilichomwa kwenye mkono wake, na tatizo ni kwamba kilijeruhi mishipa karibu na jeraha la awali. Anahitaji kufanyiwa upasuaji. Baada ya operesheni,Itachukua angalau miezi sita kupona kabisa."
"Tafadhali umfanyie upasuaji mara moja." Lisa alilipa pesa kabisa. na kulala pamoja na Pamela wodini. Pamela alikuwa bado amepoteza fahamu. Uso wakewote ulikuwa umevimba.
Baadaye, polisi pia walifika kukusanya ushahidi wa tukio lile kwenye jeraha la mwathirika. Lisa alipomaliza kutoa maelezo yake, tayari ilikuwa saa nane usiku. Alikuwa na shughuli nyingi na uchovu hata kichwa kilikuwa kikimdunda. Hakuweza kuvumilia tena hivyo akajilaza pembeni ya Pamela ili apumzike.
Ghafla Alvin akaingia. Uso wake ulikuwa umeumuka kwa hasira. Macho yake yalikuwa meusi sana kama anga la usiku.
Alimtazama Lisa chini-uu kwa dharau. Katika akili yake, maneno, 'Ninakuchukia. I really hate you' yalitawala.

Sura ya: 300

Alvin hakuelewa ni kwa nini, lakini moyo wake ulikosa raha aliposikia maneno hayo.
“Twende nyumbani.” Alvin akamtazama, sauti yake ikiwa chini kana kwamba ana amrisha mtu asiye na thamani kwake.
Lisa hakutetereka na hakuweza kuwa na wasiwasi hata kumtazama. Kusikia sauti yake tu kulifanya damu yake ichemke kwa hasira.
“Umesikia nilichosema? Una mimba sasa. Huwezi kukaa hapa namna hii.” Alvin akamvuta juu.
Hata hivyo, Lisa alimsukuma na kutabasamu kwa huzuni. “Unadhani nimependa kukaa hapa saa hizi? Marafiki zangu wawili bado hawana fahamu. Unafikiri nitakuwa na hamu ya kwenda kulala nyumbani? Bila shaka, mtu kama wewe ambaye hana moyo kwa mtu yoyote isipokuwa kwa Sarah Njau anaweza kufanya hivyo.”
Alvin aliutazama uso wake uliopauka na kusitasita kabla ya kuvua koti lake na kumvisha, kisha akasema, “Usiwaue watoto wangu kwa baridi.” Nuru ya macho yake ikafifia tena. Lisa alitabasamu kwa dhihaka yake.
Muda si mrefu akakaa, Lakini ghafla simu yake ikaita. Aliitazama na kuona jina la 'Sarah' likiangaza kwenye skrini alipotoa simu yake. Alvin akainuka na kwenda pembeni kuipokea.
Akiwa kwenye korido ile tulivu, Sauti ya Sarah iliweza kusikika kutoka kwenye simu hadi kwa Lisa aliyekuwa kitandani ndani ya wodi..
Wakati huo taa za chumba cha upasuaji zilizimika. Kisha daktari akamsukuma Kelvin nje. Kelvin alikuwa macho, na mara tu alipomwona Lisa, alitabasamu kwa unyonge. “Lazima utakuwa umechoka. Rudi ukapumzike. Sijambo…”
Alvin ambaye alitoka kupokea simu yake, akageuka na kuliona tukio la Kelvin na Lisa wakitazamana. macho yake yakamtoka kwa hasira. “Umetoka wodini kuja kumpokea Kelvin akitoka kwenye upasuaji?”.
"Kama asingewahi mapema ili kumuokoa Pamela, Pamela angekuwa amebakwa na shemeji yako mpendwa." Lisa alimtazama Alvin kwa hasira. “Alichomwa kisu mkononi na watu wa Thomas, palepale alipochomwa na Zigi kipindi kile alipomsababisha apoteze figo. Wakati huu, nitahakikisha anapelekwa jela na kuozea huko milele, hata kama utamtetea.”
Alvin akakuna kichwa chake. Hakutarajia Thomas angefanya jambo kama hilo tena. Kusema kweli naye alikasirika sana, lakini alipomuona Lisa anakasirika kwa niaba ya Kelvin, aliona inakera. "Lisa Jones, unamuonea huruma?"
"Ninachojua ni kwamba kama si yeye, Pamela angebakwa leo. Kama si yeye, ningekuwa tayari nimepoteza watoto wangu.” Lisa alimtazama kwa chuki machoni mwake. “Ukithubutu kwenda mahakamani kwa ajili ya Thomas tena wakati huu, tutapambana mahakamani.”
Alvin alijikuta katika hali mbaya zaidi, na akamtazama tena kwa ukali. “Jipange.” Kisha akageuka na kumwambia Hans, "Kaa hapa na kumwangalia." Baada ya hapo, aliondoka bila kuangalia nyuma.
Lisa alimtazama hadi kivuli chake kilipopotea. Alichanganyikiwa. Alimaanisha nini aliposema ajipange? Je, ni kweli angemtetea Thomas hata iweje? Lisa aliogopa. Alikuwa akimtishia tu Alvin. Ikiwa angeenda kinyume na Alvin, asingeweza kushinda hata kama angeajiri wakili bora.
“Lisa.” Sauti ya upole ya Kelvin ilisikika kando yake ghafla.
Aligeuka, na Kelvin akatabasamu kwa unyonge. “Mfuate.”
"Hakuna haja." Lisa akatikisa kichwa. Ingekuwa na faida gani? Kwa wakati huo, Alvin lazima angekuwa anaenda kituo cha polisi kumtoa Thomas au Mombasa kumfuata Sarah.
Kwa kweli, alikisia kwa usahihi. Dakika ishirini baadaye, alisikia mungurumo wa helkopta. Sarah alifika kituo cha polisi na muda mfupi baadaye Alvin alifika pia. Sarah alionekana mwenye huzuni na macho yake yakiwa yamevimba.
“Alvinic…” Sarah alijitupa mikononi mwake mara moja alipomwona na kuanza kulia. “Samahani kwa matatizo yaliyotokea tena kwa kaka yangu. Sikutarajia angekukatisha tamaa hivyo.”
“Ni kwa sababu nimekuwa nikimsaidia kila wakati ndiyo maana anazidi kuwa jeuri, sivyo?” Uso wa Alvin ulikuwa umejaa hasira. “Hata alidiriki kuingia katika nyumba ya mtu na kumchoma kisu na kumtia dawa za kulevya. Anafikiri yeye ndiye bosi wa Nairobi? Kwanini asichukue bunduki na kwenda kuiba benki, basi?”
Sarah alieleza kwa haraka, “Anampenda sana Pamela Masanja. Ni sawa ikiwa Pamela hampendi, lakini alimtukana tena na tena. Kwa hiyo, broo akakasirika babe..”

“Kwa hiyo? Hana makosa?" Alvin aliuliza kwa hasira.
“Siyo hivyo…” Sarah hakutarajia Alvin angekuwa mkali. Akijua kwamba angezidi kumchukiza, machozi yake yalizidi kumdondoka aliposema kwa huzuni, “Hilo silo ninalomaanisha. Amekosea, na pia nimekatishwa tamaa sana. Yote ni makosa yangu…”
“Sawa, haina uhusiano wowote na wewe. Thomas ndiye mjinga.” Alvin akampigapiga mgongoni mwake taratibu.
“Alvinic, niliwauliza polisi. Walisema tayari wamefungua kesi. Ikiwa upande wa walalamikaji watakaza zaidi, anaweza kwenda jela kwa miaka kumi." Sarah alisihi huku machozi yakimlenga lenga. “Nina kaka mmoja tu. Wazazi wangu wamekwenda. Akienda jela, basi nitapoteza familia yangu yote.”
"Lakini bado una mimi," Alvin alisema kwa upole. Kwa kweli hakutaka kumuokoa Thomas wakati huo.
'Hiyo ni tofauti. Ni yeye pekee ambaye bado nina uhusiano wa damu naye.” Sarah alilia kwa uchungu kifuani mwake.
Alvin akampapasa mgongoni, macho yake yakiwa yanamulika kwa mng'ao usioeleweka. Sarah alipoona anasitasita kujibu kwa muda, akauma mdomo na kutabasamu kwa uchungu. “Basi sawa, kama unaona ni ngumu kumsaidia kaka yangu. Nitafikiria njia mwenyewe."
“Unafikiria nini?” Alvin aliuliza kinyonge.
'Nitamwomba Pamela msamaha. Kusudi amsamehe kaka yangu, nitakubali chochote atakachosema. Ninaweza hata kupiga magoti mbele yake.” Sarah akatoka kwenye kumbatio lake. “Naenda hospitali sasa hivi.”
Hata hivyo, Alvin alimzuia. “Pamela bado hajaamka. Hakuna maana kwenda."
“Basi… basi nitasubiri hadi atakapoamka. Nitamwomba msamaha kuonyesha uaminfu wangu kwake. Pia nitamlipia gharama zake zote za matibabu.” Sarah alimsukuma Alvin mbali kwa ukaidi. “Alvinic, lazima niende. Ndugu yangu yuko kwenye matatizo."
Bila kungoja jibu lake, aliondoka kuelekea hospitali. Alvin alijikuta akimfuata bila kujijua.
•••
Lisa alirudi kwenye wodi ya Pamela baada ya kuachana na Kelvin. Pamela alikuwa akiota ndoto mbaya. Alitingisha kichwa chake kwa hofu na kusema, “Hapana, usinipige. Inauma."
“Pamela, Pamela, nyamaza. Niko hapa!" Lisa alimshika mkono haraka huku machozi yakimdondoka.
Kwa kuwa Pamela alikuwa mtoto pekee wa kike na pia mtoto wa mwsiho, familia ya Masanja ilimlea kama binti wa kifalme, na hakuwahi kupigwa hata na chelewa tu. Lakini sasa, hata ndoto iliweza kumfanya aogope sana. Ilikuwa wazi kuwa aliteswa sana kabla ya kuzimia.
“Lisa…” Kwa kupigwa na butwaa, Pamela alifumbua macho yake ya woga na kumkazia macho. “Ninaota?”
“Hapana, huoti ndoto. Uko sawa sasa. Thomas hakufanikiwa. Bado wewe ni bikra.” Lisa alimkumbatia. "Kwa bahati nzuri, Kelvin alifika kwa wakati na kukuokoa."
Pamela alinung'unika, "Lisa, hunidanganyi? Kweli haku…”
“Hakufanya hivyo. Kama nasema uwongo, basi nikatwe radi." Lisa aliapa.
Macho ya Pamela yalikuwa mepesi kwa muda. Kisha, kana kwamba anakumbuka jambo fulani, machozi yalimtoka. “Lisa, niliogopa sana, niliogopa sana. Huyo kichaa Thomas alileta watu wake na kuingia ndani ya nyumba yangu kwa nguvu. Nilikataa, lakini walinipiga, na wakasema wangenibaka kwa zamu. Walininywesha dawa kwa nguvu. Asante Kelvin kwa kuniokoa.”
“Namchukia sana Thomas. Mnyama huyo, anathubutu vipi…” Hasira moyoni mwa Lisa iliwaka alipokuwa akimsikiliza Pamela. Hakuwahi kutarajia kuwa genge la Thomas lingekuwa la kikatili kiasi hicho.
Kama asingemjulisha Kelvin, Pamela angekuwa amebakwa au kufa kabisa.
“Usijali shosti, yamepita. Shukuru Mungu upo salama.” Lisa alizuia hasira yake ili kumfariji Pamela.
Pamela aliendelea kulia mikononi mwake. Hata hivyo, kwa kuwa alilemewa na dawa za kulevya, haikuchukua muda kabla ya kuhisi kizunguzungu tena na kuzimia.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…