mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 529
- 589
- Thread starter
- #61
SIMULIZI.............LISA
KURASA........131-235
Sura ya: 231
“Tatu bora? Hilo haliwezekani.” Mzee Kimaro alishikwa na butwaa.
"Unaweza kuangalia taarifa ya kifedha ya familia ya Campos kwa mwaka huu. Familia ya Campos kwa kawaida hawana biashara, wao huwekeza hisa kwenye makampuni makubwa. Baada ya Jack kuanza kusimamia kampuni, alisaini makubaliano na familia ya Campos ambayo hutoa faida ya asilimia tano kwao. Kana kwamba familia ya Campos haina nguvu za kutosha.” Taarifa hizo zilikuja kuwa pigo kwa Mzee Kimaro.
"Mara tu familia ya Kimaro itakapozama, familia ya Campos ina uhakika wa kuwa ya kwanza ambapo hawawezi kusubiri kuchukua usimamizi wa kampuni hiyo. Ikiwa nitamiliki KIM International, hadhi ya familia ya Kimaro haitabadilika kamwe. Hata hivyo, ni juu yako. Hata kama huna mpango wa kuniruhusu kuchukua kampuni, bado ninaweza kulinda hadhi yangu nchini Kenya kwa njia zangu mwenyewe. Katika hali hiyo, hali ya familia ya Kimaro haitakuwa na uhusiano wowote na mimi…”
“Lakini ugonjwa wako…” Mzee Kimaro alikuwa na wasiwasi.
“Kama huniamini, ni sawa. Niko bize, na ni lazima nikate simu sasa…”
Kwa hayo, Alvin alikuwa karibu kukata simu.
Hapo hapo, Mzee Kimaro akajibu mara moja, “Sawa, mimi tayari ni mzee. Siwezi kushindana na vijana. Nitakuruhusu uchukue KIM International, lakini ninatumai kuwa utaisimamia vyema. Mam’mdogo wako… Amekukosea, na sitarajii umlipishie kisasi. Baada ya kusema hivyo, usiende mbali sana. Baada ya yote, sisi ni familia."
"Babu, mimi hufuata kanuni ya jicho kwa jicho na jino kwa jino." Alvin alisisitiza.
“Wewe…” Mzee Kimaro alikosa la kusema.
“Huna uwezo wa kujadiliana nami tena.” Baada ya Alvin kukata simu, macho yake yalidhihirisha kupuuzia aliyoyaongea.
Lisa hakupenda maneno yake yaliyoashiria visasi. Alianguka mikononi mwake na kumkumbatia kwa nguvu. Kisha, alibadilisha mada. Je! ni kweli familia ya Campos ilifanikiwa kuwa kati ha familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya na mali zao?"
"Nini unadhani, huniamini?" Macho ya Alvin yalififia polepole.
“Hilo haliaminiki kabisa. Familia ya Campos daima imekuwa na hadhi ya chini. Nilikuwa na fikra kwamba itakuwa familia ya Choka na familia ya Shangwe ndizo ambazo zinaweza kuingia kwenye tatu bora.”
“Ndio. Familia ya Campos imekuwa ikijificha vizuri sana. Kama isingekuwa kwa ajili ya harusi ya Jerome wakati huu, nisingechunguza historia ya familia yake,” Alvin alisema “Familia ya Campos ni tata. Ninaogopa kwamba baba yangu wa kambo si rahisi kama anavyoonekana.”
Lisa alipigwa na butwaa. “Nimemwona Mason mara mbili. Ananipa hisia kwamba yeye ni mpole na mwenye urafiki. Uvumi unadai kwamba amekuwa akijishughulisha na sanaa na muziki na havutiwi kabisa na mali na mamlaka ya familia yake.”
"Nilikuwa nikifikiria hivyo pia, lakini Mason Campos ni mtu wa chinichini sana. Nadhani anajaribu kutumia njia hizo kugeuza mawazo yetu mbali naye.” Alvin alijaribu kufikiria.
Lisa aliuliza. "Kwa kuwa ni familia ya Campos iliyopanga njama ya picha dhidi yako, jambo hili linaweza kuhusishwa na Mason?"
“Labda…” Moyoni, Alvin alifadhaika kidogo. Aliinamisha kichwa chake na kumbusu kwenye midomo mara moja. "Nitaweka dhiki zote nyuma yangu kwa sasa. Hebu tufanye jambo la kufurahisha…”
“Aa…”
•••
Katika makazi ya familia ya Kimaro, Mzee Kimaro alishika simu huku akiwa amekaa kwenye kiti cha mbao, macho yake yakionyesha hisia tata.
“Kwa hiyo mazungumzo yako na Alvin yalikwendaje?” Bibi Kimaro akammiminia kikombe cha kahawa.
“Kwa kweli, hakuna maana kubishana kuhusu hilo. Yeye ni mjukuu wa familia ya Kimaro, hata hivyo. Nilipotazama video ya kuhojiwa yaya wake, nilihuzunika. Tuna deni kubwa kwake. Zaidi ya hayo, ni familia yetu wenyewe iliyofichua picha hizo…”
“Unafikiri ni nani alifanya hivyo?” Bibi Kimaro aliuliza.
"Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Lisa alidai kwamba ilikuwa familia ya Campos, kwa hivyo nadhani atakuwa ... Jack." Mzee Kimaro alihema kwa kukata tamaa. "Alvin aliniambia kuwa familia ya Campos imefanikiwa kuingia katika familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya."
Bibi Kimaro alishikwa na butwaa. “Inawezekanaje?”
“Bado unakumbuka familia ya Campos ilivyokuwa miaka 20 iliyopita? Nilimdharau Mason enzi hizo. Ingawa ana talanta ya muziki, hawakuwa na kitu kabisa enzi hizo. Baadaye, Lea alisisitiza kuisaidia familia ya Campos, na mimi nilifumbia macho. Ikiwa hii ni kweli, hufikirii kwamba familia ya Campos imekuwa ikituhujumu kwa kujificha vizuri?” Mzee Kimaro alieleza wasiwasi wake.
“Ndio. Wakati wa harusi ya Lea nakumbuka Mama Campos alivyokuwa akinung'unika jinsi biashara yao ilivyokuwa mbaya. Alitumaini kwamba tungeweza kusaidia familia yake.” Bibi Kimaro alijawa na huzuni.
“Nilikuwa namchukia Alvin kwa kuniharibia heshima ndiyo maana nilimuachia Jack kusimamia KIM International. Lakini nikiendelea kumwacha aisaidie familia ya Campos, familia ya Kimaro itapoteza sifa ya kuwa familia bora zaidi hivi karibuni.” Mzee Kimaro alimpigia simu moja kwa moja wakili wake. "Njoo hapa."
Katika muda usiozidi saa 12, habari kwamba Mzee Kimaro alihamisha hisa na mamlaka yake yote kwa Alvin zilikuwa zimesambaa Nairobi nzima. Wazao wa familia ya Kimaro ndio walikuwa wa kwanza kumtafuta Mzee Kimaro.
Valerie alikuwa wa kwanza kupinga kati yao. “Baba, una akili? Unawezaje kumruhusu Alvin kuchukua nafasi ya mwenyekiti wa KIM International? Hukumbuki jinsi alivyotufanyia hapo awali?”
"Umesemaje, sina akili?" Mzee Kimaro alikasirika sana hadi akahisi kutaka kumpiga makofi hadi kufa.
“Baba naogopa Alvin atanilenga baada ya kuchukua kampuni kwani ananichukia.” Valerie alizungusha mikono yake kwenye mguu wa Mzee Kimaro kwa mshtuko. “Kaka, Dada, ongeeni na baba, Alvin ataniua!”
Mdomo wa Spencer ulitetemeka. “Sina mgogoro na Alvin hata hivyo. KIM International itakuwa imekufa majini ikiwa hatutamruhusu kusimamia kampuni. Kila mtu huko nje anaichukulia familia yetu kama kituko kwa sasa. Wanasubiri tu kutuona tukianguka.”
“Vipi wewe?! Wewe ni mtoto wa pekee wa kiume kwa baba na mama. ulitakiwa uwe na nguvu kuliko wajukuu, lakini huna uwezo sana,” Valerie alimtukana.
"Nyamaza!" Mzee Kimaro alielekeza macho yake kwa Jack bila subira. “Unafikiri nini Jack?”
Jack alikunja ngumi. Alikuwa amejitahidi sana kabla ya kupata nafasi yake ya uenyekiti katika kampuni. Lakini, ikawa kwamba Alvin angechukua tena nafasi hiyo muhimu katika siku chache. Ilikuwa haiwezekani kwa Jack kuwa sawa na hilo. “Babu ni sawa na wewe kutishiwa na Alvin namna hii? Amekuwa akikukosea heshima waziwazi. Mara tu atakapopata nafasi ya kuongoza, ninaogopa atakudharau zaidi. Zaidi ya hayo, karibu amuue mama yake mzazi siku chache zilizopita. Ugonjwa wake umerejea.”
“Hasa. Mtu mwenye ugonjwa wa akili anawezaje kuchukua jukumu la KIM International?" Valerie akaongeza haraka.
"Kabla sijafikia uamuzi huu, mna suluhisho gani?" Mzee Kimaro alimkazia macho Jack. "Nilikupa nafasi, lakini ulichagua kufichua ugonjwa wa akili wa Alvin kwa umma badala ya kushughulikia mambo ya kampuni."
Jack ghafla alitazama juu kwa macho mekundu. “Sikufanya hivyo babu. Kuna mtu ananifanyia njama.”
“Unafikiria nini, Mason?” Mzee Kimaro alielekeza macho yake makali kwa mkwewe ghafla.
Mason alipigwa na butwaa kwa muda. Kisha akanung’unika, “Sina uhakika sana kuhusu hilo…”
Lea hakuweza kujizuia kusema, “Baba, Mason kwa kawaida hutumia wakati wake kutunga muziki. Hata hajali kinachoendelea kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos. Je, angewezaje kujua lolote kuhusu hili? Pia, Jack ni mwanangu na ninaelewa tabia yake. Nina hakika ni mtu mwingine aliyevujisha picha."
“Kwa hali hii…” Mzee Kimaro alichukua kikombe cha kahawa na kunywa kidogo kabla hajaendelea. “nilivyoamua imetosha. Hakuna haja ya kujaribu kunishauri tena. Machoni mwangu, hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kulinda nafasi ya familia ya Kimaro kama familia bora zaidi nchini Kenya.” Mzee Kimaro alisimamia msimamo wake. Hakuna mtu aliyekuwa na ujasiri wa kuzungumza upuuzi tena.
Mishipa iliyovimba ilionekana kwenye ngumi za Jack. Baada ya Jack kutoka nyumbani, alipiga mlango wa gari kwa nguvu. Akatoa simu yake na kumpigia Jerome. "Kuanzia sasa na kuendelea, Alvin ndiye mtoa maamuzi mkuu katika kampuni. Atakaporejea kwenye kampuni, ninahofia anaweza kufuta makubaliano kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos, na kufanya aslimia tano za faida kuwa batili.”
Sura ya: 232
“Nini?” Jerome alipiga kelele kwa hasira, "Nimewekeza sana katika uzalishaji wake na sasa unataka nipate hasara kubwa?"
“Hasara gani kubwa? Hamjavuna faida ya kutosha kabla ya hili?” Jack alisugua kichwa chake. "Isitoshe, niambie ukweli, je, familia ya Campos ilivujisha picha za maisha ya Alvin?"
“Una wazimu kumuamini Lisa? Mtu wa nje kama mimi angewezaje kupata picha hizo?" Jerome alishangaa.
Jack alikaa kimya huku taswira ya baba yake ikiingia kichwani mwake. Lakini kwa mawazo ya pili, ilionekana kuwa haiwezekani kwamba Mason Campos ambaye siku zote alikuwa hajali mambo hayo angefanya kitu kama hicho. “Hata hivyo, kila mtu katika familia ya Kimaro anashuku kuwa mimi ndiye niliyesababisha haya. Alvin ataniangamiza mara tu atakapopata tena ushindi wa juu.”
“Usijali. Utapata hisa za mama yako mwishoni kwa njia fulani. Jerome alikata simu hii na kupiga nyingine baada ya hapo. "Mpango haukufaulu." “Hmm, nilidharau ujasiri wa Alvin na Mzee Kimaro. Sembuse huyo mwanamke Lisa.”
Jerome alikaza macho yake. Alikuwa ameangalia historia ya Lisa hapo awali. Mwanamke huyu aliibuka hivi karibuni tu kuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investments. Alikuwa binti mdogo tu kutoka Tanzania. Hata hivyo, wakati wa kipindi cha moja kwa moja cha jana yake, mwanamke huyo alidumisha utulivu wakati akizungumza na taifa zima la Kenya—bila kusahau mawazo yake makali na ya kufikirisha huku akiipa changamoto familia yenye nguvu zaidi ya Kimaro.
Haikuwa makosa kusema kwamba Lisa alikuwa ameongoza kampuni ya Alvinarah kupitia shida hii wakati Alvin akiwa mgonjwa. Kwa sababu fulani, ilimkumbusha kuhusu mchumba wake, Melanie. Walikuwa dada wa kambo kutoka kwa baba mmoja lakini Melanie alikuwa kama mjinga.
“Kwa hiyo, nini kinachofuata?” Jerome aliuliza.
"Kwa bahati nzuri, nina mpango mbadala. Ni wakati wa kumpeleka kwenye uwanja wa vita." Mtu yule kwenye simu alijibu.
“Sawa. Nina imani na wewe kabisa.” Jerome alijibu kwa unyenyekevu. Alisikiliza mawazo ya kimkakati ya huyo mtu mwingine kwenye simu. Bila shaka, familia ya Campos ingekuwa familia yenye nguvu zaidi nchini Kenya kwa muda mfupi. Enzi ya familia ya Kimaro… ilikuwa inakaribia mwisho.
•••
Siku iliyofuata, Bibi Kimaro alimpelekea Alvin fomu ya uhamisho wa umiliki wa hisa kwenye jumba lake la kifahari ufukweni mwa bahari huko mombasa. Alipoingia ndani ya nyumba hiyo, aliona hakuna mtu mwingine ndani ya nyumba hiyo isipokuwa Aunty Yasmine ambaye alikuwa akisafisha sakafu.
“Alvin yuko wapi? Ametoka?”
"Bwana Mkubwa na Mkewe wameenda kununua mboga kwenye duka kubwa lililo jirani." Shangazi Yasmine alipiga goti ili kumsalimia yule kikongwe.
"Kununua mboga?" Maneno yale yalimponyoka kinywani Bibi Kimaro bila kujijua. Asingeweza kuamini kuwa mjukuu wake alikuwa ameenda kununua mboga ikiwa asingesikia kwa masikio yake mwenyewe.
"Alikuwa na matatizo ya ugonjwa siku mbili tu zilizopita. Anapaswa kupumzika nyumbani. Kwanini hukumzuia kutoka nje?”
“Usijali Bi Mkubwa. Bwana Kimaro hana tatizo kabisa na huchangamka sana anapokuwa na mkewe.” Kabla sauti yake haijakatika, vicheko vya furaha vilisikika kutoka nje.
Bibi Kimaro alitazama kupitia dirishani. Wanandoa wachanga walioshikana mikono walikuwa wakitembea kuelekea nyumbani. Nywele ndefu za Lisa zilining'inia mabegani mwake. Umbo lake zuri liliweza kuonekana licha ya suruali ya jeans ya mguu mpana na fulana nyeusi aliyokuwa amevaa. Pia alikuwa amevalia jozi ya viatu vyeupe vya turubai. Alionekana nadhifu na mchangamfu.
Karibu naye, Alvin alionekana mtanashati na mwenye furaha akiwa amevalia mavazi meupe ya kawaida. Alikuwa ameshika mifuko miwili ya shopping huku uso wake ukiwa na tabasamu la kupendeza. Wenzi hao walionekana kama watu waliooana hivi karibuni. Hasa, hakuonekana kama mtu ambaye alikuwa na tatizo lolote la akili.
Yule kikongwe alipigwa na butwaa kabisa kumuona. Ilikuwa ni muda mrefu sana kwamba hakuweza kukumbuka mara ya mwisho alipomwona akiwa na furaha hivi.
Bibi Kimaro alikuwa amejitayarisha hata kwa ukichaa wa Alvin akiwa njiani kwenda kwake. Hakika ilikuwa ni kutokana na matarajio yake kumuona katika hali hii ya utulivu na uchangamfu.
Wenzi hao wachanga walipomwona yule mwanamke mzee walipoingia ndani ya nyumba, mara tabasamu usoni mwa Alvin likatoweka. Macho yake yalionyesha uhasama na kujihami. Bibi Kimaro alihisi kana kwamba sindano imeuchoma moyo wake.
“Habari, Bibi,” Lisa alimsalimia mwanamke huyo mzee kwa upole kana kwamba hakuna jambo lolote baya lililokuwa limetokea kati yao hapo awali.
Bibi Kimaro alimpa tu mtazamo wa kijeuri, akikataa kujibu salamu yake.
Hasira ikawaka usoni mwa Alvin. “Kama umekuja kumkosea heshima mke wangu, tafadhali ondoka.”
“Wewe...” Bibi Kimaro aligugumia kwa hasira. “Mimi ni bibi yako. Utafurahi tu baada ya mimi kufa?"
“Ninachojua ni familia ya Kimaro ndiyo iliyonimwagia chumvi kwenye kidonda changu. Ningekuwa nimenaswa kwa nguvu katika hospitali ya magonjwa ya akili kama si Lisa.” Alvin alitabasamu kwa uchungu. "Ikiwa nyote bado mnaniona kama familia, basi kitu kidogo kabisa mnachoweza kufanya ni kumwonyesha heshima."
Bibi Kimaro alionekana kuchanganyikiwa. Lisa alisema kwa upole alipoona hivyo, “Bibi, mimi ndiye ninayepaswa kuwa na hasira kwa sababu uso wangu umeharibika kutokana na familia yako. Je, ninastahili mambo yote mabaya kwa sababu sitoki katika malezi yenye nguvu kama familia ya Kimaro?”
Bibi Kimaro alipasua midomo yake kutaka kusema kitu lakini Alvin alimkatisha kabla hajapata nafasi. “Mimi ndiye nimekuwa nikimsumbua tangu mwanzo hivyo acha kudhani kuwa ni mwanamke mlaghai. Hakuwa anajua mimi ni nani alipokutana nami mara ya kwanza. Pia nilichumbiana na Melanie baadaye ili tu kumfanya aone wivu.”
“Unawezaje kumfanyia hivyo Melanie?” Sauti ya kikongwe ilidhihirisha kutofurahishwa kwake.
"Ikiwa unampenda sana, basi mchukue kama mjukuu wako." Macho ya Alvin yalionekana kuwa makali kama moto. “Nilifanya mambo hayo kwa kukuridhisha tu. Melanie ni msichana mzuri—”
“Na Lisa je?” Bibi Kimaro alimkatiza bila subira kwa sauti ya ukali, “Wote wawili ni mabinti wa Joel Ngosha.”
“Lisa alikosea nini?” Alvin alidakia. “Je, alichagua familia aliyozaliwa? Hakuwahi kukumbana na mapenzi ya baba yake tangu akiwa mdogo lakini sasa kwa vile hatimaye ameungana na baba yake, kila mtu anamdharau. Kwa kweli, yeye ni mkubwa kuliko Melanie na mama yake ndiye aliyeachwa na Joel. Yeye ndiye mwathirika wa kweli hapa."
Bibi Kimaro hakuwa na maneno ya kubishana naye.
Alipohisi hali ya mvutano ikizidi kushamiri, Lisa alipendekeza, “Inakaribia saa sita mchana. Nyie wawili mnapaswa kuelewana nami nitaelekea jikoni kuandaa chakula cha mchana. Bibi, tafadhali kaa kwa chakula cha mchana.”
"Ikiwa unabaki tu ili uendelee kumshambulia mke wangu, basi ni bora ungeondoka tu," Alvin alisema kwa upole.
Bibi Kimaro aliona aibu sana kwa sauti ile. “Unadhani L-”
“Alvin, si rahisi kwa Bibi kufanya safari ndefu hivyo kuja hapa katika umri wake. Afadhali ukae kimya,” Lisa alifoka, na kufanya mambo yasiwe magumu kwa yule mzee. Alvin alikoroma, na Bibi Kimaro naye akakaa kimya.
Baada ya Lisa kutokomea jikoni, Bibi Kimaro alimuagiza mwanasheria atoe fomu ya kuhamisha umiliki wa hisa. “Hii imetoka kwa babu yako. Utakuwa na udhibiti kamili wa KIM International baada ya kusaini hii. Mimi na babu yako hatutaingilia mambo ya kampuni kuanzia hapo.”
Alvin akasaini karatasi bila kusita. “Siyo tu kwamba mam’dogo Valerie hajaboresha biashara ya KIM Insurance tangu achukue kitengo hicho, lakini mauzo yameshuka kiwango cha chini zaidi. Anapaswa kustaafu mapema, kuketi, na kufurahia bonasi za kila mwaka nyumbani.”
Bibi Kimaro alionekana kushtuka kabla ya kupiga kelele, “Unafanya hivi kumlipishia kisasi kwa sababu alisababisha Lisa kuharibika usoni…”
“Kwa hivyo itakuwaje kama hiyo ni kweli? Unamvumilia hata baada ya kusababisha madhara kwa mtu mwingine kwa sababu tu ni binti yako? Lakini yeye si binti yangu,” Alvin alijibu bila kujali.
“Lakini yeye ni mam’dogo wako, hata hivyo…” Bibi Kimaro akashusha pumzi ndefu. "Mbali na hilo, mauzo yake yaliimarika mwezi uliopita…”
Sura ya: 233
'Hiyo ni kwa sababu Nina Mahewa aliwekeza shilingi bilioni kadhaa." Macho ya Alvin yalidhihirisha dhamira ya hatari. “Ikiwa nilikisia kwa usahihi, alifanya hivyo baada ya mam’dogo Valerie kukubali kuharibu uso wa Lisa. Anadanganya takwimu za mauzo." Akiwa amepigwa na butwaa, Bibi Kimaro akakosa cha kusema.
“Bibi, unapaswa kushukuru. Nisingemuacha hai kama si wewe na babu.”
Alvin akainuka. “Angalia mwanao Spencer na binti zako. Mmoja wao anajali tu kusaidia familia ya mumewe, mwingine anadanganya mauzo. Mwanao pekee wa kiume ni dhaifu na hana uwezo. Unafikiri wewe na babu mngeweza kufurahia uzee wenu kwa mali mlizonazo sasa kama si mimi?” Bibi Kimaro alionekana kuwa mzee kwa miaka michache zaidi baada ya kusikia hivyo.
Saa sita kamili mchana, Lisa alitokea tena jikoni baada ya kuandaa chakula cha mchana lakini mvutano kati ya Alvin na bibi yake ulionekana kuongezeka. Alitenga chakula na kumkaribisha Bibi Kimaro mezani.
Mwisho bibi yule alionekana kushangazwa na vyakula vilivyowekwa mbele yake. Kila mlo haukuwa mzuri tu bali ulikuwa na ladha ya kupikwa nyumbani kuliko vile vya wapishi wa familia ya Kimaro. Aligundua kwamba Alvin, ambaye hakuwahi kufurahia chakula, alikuwa akila kila chakula—hasa nyama ya nguruwe.
Bibi alijaribu kipande kidogo cha nyama ya nguruwe. Walahi alitamani aachiwe sahani zote peke yake. Bakuli la nyama lilikuwa karibu kuisha alipofikia kipande cha pili.
“Usimalize yote. Bibi bado hajala vya kutosha.” Lisa akasogeza bakuli la nyama ya nguruwe kuelekea kwa Bibi Kimaro.
Alvin alikunja uso. “Kwanini hukujitayarisha nyingi?”
"Ulikula jana usiku na unataka tena mchana huu? Si afya kula nyama ya nguruwe kupita kiasi.” Aliweka mbogamboga badala yake kwenye sahani yake. “Ni muhimu kuwa na lishe bora na sio kuchagua. Ukiendeleza tabia hiyo mbaya, basi sitakupikia tena.” Lisa alimuonya.
“Sawa, nimekusikia.”
Chini ya macho ya Bibi Kimaro, mjukuu wake alianza kula mbogamboga. Mtu ambaye alikula vijiko vichache vya chakula kwa siku alikuwa akila sahani nzima wakati huu. Hata yule kikongwe alikuwa na hamu ya kula alipomwona mjukuu wake akila kwa hamu vile. Mwishowe, chakula cha mchana kilichotosha watu sita kilimalizwa na wale watatu.
Baada ya chakula cha mchana, Lisa alitenga majagi mawili ya mtindi kwenye meza. Aunty Yasmine alisema huku akitabasamu. “Hii pia imetengenezwa kwa mikono na Bi. Jones. Ni mtindi na asali na jamu safi ya strawberry ambayo aliiandaa polepole kwa masaa mawili. Alisema kunywa glasi ya mtindi baada ya mlo ni vizuri kwa usagaji chakula na kusafisha matumbo.”
Bibi Kimaro alionja kidogo kisha akanongewa tena. Mtindi ulikuwa mtamu sana. Alijisikia kuongeza glasi nyingine! lakini alikuwa na aibu sana kuomba kuongezewa.
Hata hivyo, Alvin hakuona aibu hata kidogo kuomba huduma nyingine mara baada ya hapo. Ombi lake lilikataliwa na Lisa. "Huwezi kunywa mtindi mwingi au unaweza kuvimbiwa."
"Una shida gani?" Alikunja uso lakini hakuzungumza zaidi.
Ingawa hakumpenda sana Lisa, Bibi Kimaro ilibidi akubali kwamba binti huyo alikuwa amembadilisha Alvin kuwa bora. Labda ugonjwa wa Alvin ungeimarika, kama hapo awali…
Baada ya chakula, Bibi Kimaro alisimama na kuaga ili kuondoka. “Asante kwa chakula wajukuu zangu, nimekula, nimefurahia na nimeshiba. Ni wakati wa mimi kuondoka.”
"Unaweza kukaa kwa siku chache zaidi. Kutembea na kupunga upepo baharini kunastarehesha kweli,” Lisa alisema kwa tabasamu hafifu.
Bibi Kimaro alijisikia vibaya kuona jinsi mwanamke huyo alivyoharibika usoni. “Ni sawa. Babu yako hajazoea kuwa mbali na mimi.” Baada ya kutulia kwa sekunde chache, aliendelea kusema, “Asante kwa ukarimu wako leo.”
Lisa alishangaa kusikia hivyo. Bado alikuwa akitabasamu hata baada ya yule kikongwe kuondoka zake.
Alvin alimkumbatia kwa upendo. “Bibi yangu alikutendea vibaya lakini bado ulijaribu sana kumfurahisha kwa chakula cha mchana na mtindi. Anafikiri kukushukuru mara moja ni fidia ya kutosha?"
“Ni kwa sababu yeye ni bibi yako.” Aligeuka na kuifunga mikono yake shingoni. “Ulimwambia maneno makali lakini bado najua unawajali sana babu na babi yako. Vinginevyo, usingeichukua KIM International tena. Una wasiwasi kwamba wanandoa hawa ambao wameishi maisha ya kitajiri wakati wote wangedhihakiwa na wengine katika uzee wao ikiwa KIM itaanguka?"
Alvin aliinua nmacho yake kinyonge. Hakuna mtu aliyemjua vizuri kuliko yeye.
“Alvlisa, nilikuwa na bibi pia. Ni pale tu alipotangulia mbele ya haki ndipo nilijuta kutotumia muda mwingi kuwa naye. Familia ni damu halisi na ni ngumu sana kuiondoa. Kwa sababu yako, ninaweza kujaribu kuwavumilia na kuwasamehe. Ilimradi utafurahi.” Kwa macho makali, Lisa alimtazama Alvin usoni.
Alvin alimsukuma ukutani. Hisia ambazo zilikuwa zimelala ndani ya moyo wake zililipuka kama volkano. Aliinamisha kichwa chake ili kumbusu kwa mahaba kwenye midomo. "Samahani, Lisa. Kwa ajili ya familia yangu kukuumiza.”
Uso wake uliharibiwa na familia ya Kimaro lakini bado aliwavumilia kwa ajili yake. Hata hivyo haikuwa imepita hivihivi tu. Aliahidi kuwalipa kwa yale waliyomfanyia.
"Siku moja, tutatapa mtu wa kutibu uso wako. Nitakupenda maisha yangu yote.”
Lisa alifunga macho yake karibu. Wakati huo huo, alihisi nguvu na utulivu. Haijalishi uso wake ulikuwa umeharibika vipi, kilichokuwa muhimu ni kwamba hakujali.
Siku iliyofuata, Lisa akaenda kufanya kazi katika kampuni yake. Alikuwa akitoka Mombasa hadi Nairobi na kurudi kwa ndege kila alipotaka kwenda ofisini kwake.
Alipotoka tu, Hans alijitokeza nyumbani kwa Alvin akiwa na wauguzi wachache. Kulikuwa na sura ya wasiwasi usoni mwake aliposema, "Bwana Kimaro, hawa ni wauguzi waliochaguliwa na mkurugenzi wa hospitali."
Alvin aliyekuwa anasoma kitabu cha hadithi za Jomba Wajo aliinua kichwa chake. Ugonjwa wake wa akili haukuwa kitu ambacho kingeweza kuponywa kwa siku kadhaa. Lisa alikuwa na kazi yake mwenyewe ya kufanya, kwa hivyo asingeweza kumtunza kila wakati. Ili kumzuia asipatwe tena na ugonjwa huo, ilikuwa vizuri kuwa na muuguzi aliyezoezwa ifaavyo nyumbani ili kumtazama.
Hata hivyo, alionekana kuchanganyikiwa wakati macho yake yalipotua kwenye uso mzuri sana. "Jina lako nani?"
Mwanamke huyo alionekana kushtuka chini ya macho yake kabla ya kujibu kwa sauti nyororo, "Jina langu ni Maurine Langa."
“Langa?” Alvin akashtuka kusikia jina hilo. "Una uhusiano gani na Sarah Njau Langa?"
"Yeye ni binamu yangu." Maurine alipepesa macho na kumtazama Alvin. “Unamfahamu binamu yangu?”
“Ni zaidi ya kumjua.” Alvin alihema ndani kwa ndani. "Wewe bado ni Langa, angalau. Kwanini uliishia kuwa nesi? Hii si kazi rahisi.”
"Langa sio kama tulivyokuwa hapo awali. Lakini ni sawa, angalau tuna cha kupeleka matumboni mwetu na paa juu ya vichwa vyetu.” Aliinua macho yake na kutabasamu kwa shukrani. "Pengine kuchukua kwangu taaluma hii kuna uhusiano na binamu yangu. Sisi wawili tulizoea kuwa karibu sana tulipokuwa wadogo lakini alipelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Nilijisikia vibaya sana kwake. Mpango wangu wa awali ulikuwa kuwa mwanasaikolojia aliyeidhinishwa lakini sikufanikiwa. Kwa kweli niko katika maandalizi ya kufanya mtihani tena.”
Alvin alichanganyikiwa tena aliposikia hivyo. Swali la Hans lilimrudisha kwenye ukweli. "Bwana Mkubwa, ungependa kumwajiri nani?"
"Maurine Langa, ndiyo." Alvin akachukua kitabu chake tena na kuendelea kusoma.
Tabasamu kubwa lilienea usoni mwake. “Asante, Bwana Kimaro. Nitafanya kila niwezalo kukusaidia kupona.”
Hans alionekana kushangaa. Mara tu Maurine alipoondoka kwenda nyumbani kuchukua vitu vyake, Alvin alimtazama Hans na kuagiza, “Mchunguze mwanamke huyu.”
"Bwana Mkubwa, unashuku kwamba-"
"Fanya nilichokuagiza!"
Katika muda usiozidi nusu siku, Hans alirudi na baadhi ya matokeo. “Maurine Langa hakika ni binamu wa Sarah Langa. Alikuwa akisoma nje ya nchi na hivi karibuni alirudi nyumbani. Tangu kifo cha mama yake, familia ya Langa imekuwa ikinyanyaswa sana na familia ya Njau. Maurine anabaguliwa nyumbani na hospitalini pia na kila mara hupewa jukumu la kuwaangalia wagonjwa wenye jeuri na fujo. Lakini, utendaji wake hospitalini umekuwa mzuri sana. Sio tu kwamba yeye ni mvumilivu bali pia ana mawazo yenye nguvu ya kuvumilia magumu.”
Sura ya: 234
Nuru ilizimika machoni mwa Alvin kwa sauti hiyo. "Inaweza kuwa ni bahati tu kwamba yuko hapa leo?"
"Inaonekana. Mabinti waliopendekezwa na wasimamizi wa hospitali hiyo ndio wauguzi wanaofanya vizuri zaidi kwa sasa.”
Aliitikia kwa kichwa baada ya kusikia hivyo, kigugumizi kwenye moyo wake kikatoweka. "Nani mkuu wa familia ya Njau sasa?"
"Charity Njau." Hans alijibu.
“Hakikisha KIM International na Alvinarah Media Network zinavunja mikataba yote ya ushirikiano na kampuni ya New Era Advertisings. Tutaona watapeleka wapi matangazo ya wateja wao. Nataka kumfunza somo Charity Njau kwa kuinyanyasa familia ya Langa.
Hans alikubali kwa utii na hakuongeza neno lolote.
Saa kumi na moja jioni Lisa aliondoka kazini mapema kuliko siku nyingine yoyote. Alisikia kelele kutoka kwa uwanja wa mpira wa vikapu mara tu aliposhuka kutoka kwenye gari.
Alitembea kwa wakati na kumuona Alvin akiinua mikono yake kutumbukiza mpira kwenye pete kufunga goli. Hakujua ni muda gani alikuwa akicheza mpira huo wa kikapu. Nyuma ya fulana yake nyeupe kulikuwa na unyevunyevu kidogo lakini uso wake ulionyesha hali ya jua.
Kumwona katika hali hiyo kulichukua pumzi yake. Alipokuwa bado shuleni, Ethan alikuwa mchezaji pekee wa mpira wa kikapu ambaye alisifiwa sana, lakini, akimtazama Alvin kwa wakati huo, aliona haiba ya kweli ya mwanamichezo.
“Naam!” Mfululizo wa makofi ya pongezi ulisikika kutoka upande wa pili wa uwanja. Hapo ndipo alipomwona yule mwanamke aliyelingana naye kiumri akiwa amevalia suruali ya jeans na top nyeupe. Nywele zake nyeusi zilizometa zilikuwa juu kwenye mkia wa farasi.
“Inavutia, Bwana Kimaro." Mwanamke huyo alitembea na chupa ya maji na kipande cha taulo. "Umecheza kwa dakika 40. Ni wakati wa kupumzika.”
“Sawa.” Alvin aliipokea ile chupa na kuanza kumeza vilivyomo ndani yake.
Miale ya jua la machweo iliwamulika wote wawili. Tukio hilo la aina fulani lilimchoma macho Lisa.
“Alvlisa…” Lisa aliita kabla ya kwenda haraka.
Alvin alitazama mwelekeo wa sauti hiyo na tabasamu likaenea katika uso wake wa kupendeza. "Baby, umefika nyumbani mapema leo."
"Nilirudi nyumbani mapema kwa kuhofia kuwa ungekuwa mpweke nyumbani peke yako." Alimtazama kwa karibu yule mwanamke mwingine. Alikuwa mrembo lakini hakuwa na kitu cha ajabu ikilinganishwa na yeye alivyokuwa zamani. Hata Melanie alikuwa mrembo zaidi ukilinganisha naye. Lisa alijisikia ahueni.
“Halo, Bi. Jones Mimi ndiye nesi niliyetumwa na hospitali kumuangalia Bwana Kimaro,” Maurine alijitambulisha huku akitabasamu.
“Oh, habari.” Lisa alishikwa na butwaa. Kwa sababu fulani, alihisi kana kwamba aliyaona macho hayo hapo awali lakini hakuweza kukumbuka ni wapi na lini.
“Ni heshima yangu kumwangalia Bwana Kimaro. Natumai atapona haraka iwezekanavyo.” Maurine alijieleza kitaaluma.
“Twende, naelekea ghorofani kuoga.” Alvin aliweka mkono begani kwa Lisa.
"Bwana Kimaro, unapaswa kupumzika kwa nusu saa baada ya kufanya mazoezi kabla ya kuoga," Maurine alimkumbusha.
“Sawa…” Alisita kabla ya kukubali.
Lisa alishangaa sana. Aliondoa fulana yake baada ya kupanda ghorofani. Alichukua taulo na kumpigapiga mgongoni. "Vipi mbona umeanza kucheza mpira wa kikapu ghafla?"
"Maurine Langa alisema kiasi kinachofaa cha mazoezi kinaweza kusaidia kupona kwa haraka na pia kuboresha ubora wa usingizi usiku."
“Maurine Langa?” Kitetemeshi kilipita kwenye uti wa mgongo wake.
Ni sadfa iliyoje! Aliwahi kuwa na mpenzi wa zamani mwenye jina la kati Langa pia. Sarah Langa!
“Ndio, kuna nini?” Akageuka kumtazama.
Lisa alichanganyikiwa sana. Hakuweza kusema kwamba alishituka kwa sababu jina la mwisho la nesi lilikuwa Langa. Hata hivyo, haikuwa sawa kujifanya kuwa mkarimu. “Sikutarajia ungemsikiliza msichana huyo kwa utiifu,” alisema huku akihema.
Alvin aliinua macho yake kabla ya kuinama ili kunusa midomo yake. "Hmm, nasikia harufu ya wivu."
“Nipo serious.” Akampiga kofi la mgongoni kwa utani.
Aliushika mkono wake mara moja na kuutoa kidogo. "Nisiingekuwa mtiifu hapo zamani na hata nisingekubali wazo la kuajiri muuguzi kutoka hospitali ya magonjwa ya akili. Hata hivyo, ninapenda nipone mapema kwa ajili yako, kwa hivyo ninahitaji kufanya kazi na mpango wa matibabu. Sitaki kufanya jambo lolote litakalokuumiza tena. Unaelewa?"
Aliuma midomo yake, ghafla akajisikia vibaya kwa kuwa na wivu sana. “Nimeelewa, lakini kwa nini usiajiri mtu ambaye ni mkubwa kidogo au labda nesi wa kiume? Nitakuwa nikifanya kazi ofisini na kukuacha peke yako nyumbani na msichana kweli?!”
Alvin alitabasamu kabla ya kuinua kichwa chake na macho yao yakagongana. “Una wivu kweli?”
“Alvin Kimaro!” Alimtazama kwa macho makavu.
“Usiwe na wivu bwana.” Alvin alimshusha wasiwasi. “Sekretari au mfanyakazi yeyote katika kampuni yangu ni mrembo kuliko yeye. Usingekuwa na nafasi ya kuwa Bi. Kimaro kama ningekuwa zoazoa fagio la chuma.” Alvin alijibu huku akitabasamu. “Sikuona ukiwa na wivu hivyo nilipokuwa na Melanie. Ulikuwa umekaa kimya kuhusu hilo.”
Aibu ilitanda usoni mwake alipofichua ukweli. “Siwezi kuwa na wasiwasi na hili. Naelekea chini kuandaa chakula cha jioni.” Akamtupia taulo na kuelekea kwenye ngazi.
Mara tu alipoingia jikoni, Maurine alimwendea na mpango wa lishe. "Bi. Mdogo, huu ni mpango wa lishe iliyoundwa mahsusi kwa ajili ya Bwana Kimaro. Kwa kuzingatia ugonjwa wake, ninapendekeza milo yake mikuu izingatie maelekezo haya.”
“Sawa, asante.” Lisa alipokea mpango wa chakula kabla hajauliza, "Je, tumewahi kukutana hapo awali?"
Maurine alionekana kushtuka lakini haraka akabadilisha mshangao huo na kutabasamu. "Sidhani. Hata hivyo ni mara yangu ya kwanza kukutana nawe, Bi. Kimaro. Lakini watu wengi wamesema kwamba wanaonekana kunifahamu.”
“Labda.” Lisa aliitikia kwa kichwa.
Lisa alitokea tena jikoni baada ya kupika chakula cha jioni, alimuona Alvin akiwa amekaa kwenye kochi huku Maurine akiwa amejiinamia kiunoni akijadiliana naye jambo kwa upole.
"Wakati wa chakula cha jioni," Lisa alimkumbusha.
Alvin akanyanyuka na kabla hajajonge mezani akatangaza, “Maurine na Shangazi Yasmine, kwa nini msijiunge nasi kwa mlo wa jioni wa leo?”
Hilo lilimshangaza Maurine. “Asante…” Alijibu huku akisitasita.
“Ni sawa. Usione haya wala woga. Kila mtu ni sawa katika zama za leo, na zaidi ya hayo, imekuwa ndefu kwako pia,” Lisa alisema kabla ya kugeuka kumwangalia Alvin.
Kwa kweli chakula cha jioni kilichangamka zaidi huku watu wale wanne wakiwa mezani. Hata hivyo, Lisa alikosa amani Maurine alipoendelea kumkumbusha Alvin ale nyama kidogo bali mboga na dagaa zaidi. Baada ya yote, yeye ndiye alikuwa na wajibu wa kusema maneno hayo. Kwa hivyo, ilikuwa ni ajabu sasa kwamba mtu mwingine alikuwa amechukua majukumu yake. Kwa kweli alijiona anazidi kuwa na wivu mkali.
Baada ya chakula cha jioni, yeye na Alvin walitembea ufukweni ili chakula kishuke vizuri tumboni. Waliporudi nyumbani, wote wawili walifanya kazi zao za ziada katika maktaba yao. Kwa kuwa Lisa alimaliza kazi yake mapema, alienda kuoga.
Alipotoka bafuni, aligundua kwamba Alvin alikuwa akinywa kitu kwenye glasi. Maurine alikuwa akimwangalia kwa makini pembeni. Mwanga wa taa ya manjano ulimulika juu yao kutoka darini kwa juu. Kuona jambo hilo kulimuumiza macho.
"Unakunywa nini?" Akasogea kuchungulia kwenye glasi yake. Kioevu cheupe kilionekana ndani yake, labda kilikuwa ni maziwa.
Maurine alieleza kwa upole, “Kunywa glasi ya maziwa kabla ya kulala huboresha ubora wa usingizi.”
“Asante, lakini hili ni jukumu langu,” Lisa alijibu kwa tabasamu hafifu.
Maurine alishikwa na butwaa kiasi kwamba uso wake ulipauka ghafla. Akiwa amechanganyikiwa, alitikisa kichwa kwa aibu. "Ndio, nitawaacha nyie wawili sasa."
Sura ya: 235
Maurine alimtazama Lisa kwa tahadhari kabla ya kufunga mlango nyuma yake.
Alvin alisema kwa kucheka, “Umemuogopesha binti huyo.”
Lisa alishindwa cha kusema. “Nilifanya nini cha kumuogopesha? Nilisema maneno hayo kwa uso wa kirafiki.”
"Hmm, lakini pia kwa sauti ya wivu sana." Alvin aliitikia kwa kichwa huku uso wake ukionekana kutojiweza. “Ni glasi tu ya maziwa. Hutakiwi kuwa na wivu juu yake.”
Maneno ya Alvin yalimfanya ajione kuwa ni mwanamke mwenye fikra finyu. Lisa alishusha pumzi ndefu huku akihisi mshangao mwingi ukimuandama.
“Acha kuwaza kupita kiasi. Ngoja nikukaushe nywele zako.” Alvin akachukua mashine ya kukaushia nywele.
Mara tu nywele zake zilipokauka, alipanda kitandani na uso wenye haya. Tangu wapatane, alikuwa na shauku kubwa ya kufanya mapenzi kitandani, lakini bado aliona aibu kila alipojiwazia. Hata hivyo, alijilaza tu kitandani kwa utulivu baada ya kuzima taa usiku huo. Hamu yake iliyofichika haikuwa ya kawaida. Lisa akaanza uchokozi wa makusudi. Akageuka juu juu juu na kumkandamiza Alvin na makalio yake.
"Tulia basi tulale." Alvin aliyekuwa amegeuziwa makalio na kumkandamiza ipasavyo kwenye ikulu yake akampigapiga tu mgongoni na kumpoza kwa sauti yake ya upole.
Lisa hakuamini masikio yake. Aliuma midomo yake na kuizungushia mikono yake shingoni mwake. “Alvlisa…” Lisa aliita taratibu. Ukiacha sauti yake iliyotetema kwa huba, uso wake wote ulikuwa ukizungumza mapenzi tu. Kwa bahati nzuri, Alvin hakuweza kuuona kwa sababu taa zilikuwa zimezimwa.
Hili lilimshangaza sana Alvin. Mshawasha ukatekenya kunako makao makuu yake, lakini alizuia shauku yake mara moja. “Maurine alinikumbusha kwamba dawa ninazotumia haziniruhusu nifanye hivyo kwa sasa. Ni bora tusitishe jambo hili kwa sasa.” Unyonge ulionekana katika sauti yake.
Lisa alionekana kushtuka. “Lakini kabla… Sote tulikuwa wazuri. Sio lazima, sivyo?"
“Unanitaka sana hivyo?” ghafla alisema kwa mahaba mazito.
Lisa aligeuka tu bila kujibu. Alitaka ndiyo lakini hakutaka kujirahisha sana, alihitaji kudumisha kiburi chake pia. Alitaka abembelezwe kwanza ndipo atoe!
Alvin akamkumbatia kwa nyuma. “Kuwa mvumilivu. Siwezi kufanya chochote ambacho kinaweza kunisisimua kupita kiasi kwa sasa. Ninaogopa nitafanya kitu nje ya udhibiti wangu ambacho kinaweza kukuumiza. Kama mara ya mwisho."
Lisa aliuma midomo yake, alikasirika, na mwishowe akanung'unika "sawa" baada ya muda mrefu. Usiku ule hakupata usingizi huku Alvin akipitiwa na usingizi mzito. Mawazo yake yalikuwa yakimshawishi kwamba labda nadharia ya Maurine ilikuwa sahihi. Baada ya yote, alikuwa akisumbuliwa na usingizi tangu aanze kupandisha wazimu. Muda ulikuwa umepita tangu amwone amelala vizuri sana.
Siku iliyofuata, Lisa alipokea simu kutoka hospitalini. Inavyoonekana, daktari bingwa wa mfumo wa neva, Daktari Angelo kutoka nje ya nchi alikuwa amefika kumtibu Joel. Bila kupoteza muda, alieelekea hospitali mara moja. Bibi na Babu Ngosha walikuwa tayari wameshafika.
Dk. Angelo alikuwa amemaliza uchunguzi wa Joel. "Ninahitaji kumtibu kwa kudhibiti mishipa yake kwa muda mrefu. Bado kuna matumaini kwamba Bw. Ngosha atatoka katika hali ya kukosa fahamu, lakini huenda ikawa ni safari ndefu. Muda mfupi zaidi labda utakuwa nusu mwaka hadi mwaka mzima.
"Asante sana." Lisa alishukuru.
“Usijali. Wewe ni rafiki wa Chester, kwa hiyo nitafanya kila niwezalo kukusaidia.” Dk. Angelo alisema.
Baada ya kutafakari kwa ufupi, Lisa aliomba, “Dokta Angelo, ikiwa mtu atakuja kuuliza kuhusu hali yake, tafadhali mwambie kwamba Bw. Ngosha atarudiwa na fahamu ndani ya mwezi mmoja.”
Daktari alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kutikisa kichwa. “Hakika.”
Baada ya daktari kuondoka, Mzee Ngosha hakuweza kupinga kuuliza, “Unajaribu kuchunguza kama kuna mtu alipanga kumuua baba yako?”
"Babu, unadhani ni nani anayeweza kuwa mhusika?" Aliuliza.
Mzee alikaa kimya kwa muda. Uchunguzi wa maiti ya dereva wa lori ulionyesha kwamba alikuwa alisinzia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya. Hata hivyo, mwanamume huyo hakuwa mraibu na alikuwa ametumia tu dawa hiyo kimakosa. Kwa wazi, hili lilikuwa tendo la makusudi.
“Nina uhakika ni Nina.” Mzee Ngosha alifoka kwa hasira. "Baada tu ya ajali amemwingiza Melanie kufanya kazi katika Kampuni ya Ngosha."
Lisa alikubali kwa kichwa. “Ikiwa ni hivyo, atahakikisha kwamba baba yangu hataamka kamwe. Kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee itakayomwezesha kurithi kila kitu alichoacha nyuma. Kando na hilo, ikiwa mtu mwingine yuko nyuma ya hili, mtu huyo bila shaka atajaribu kuchukua udhibiti wa Ngosha Corporation ndani ya mwezi huu. Nina hakika mhalifu atafichua asili yake hivi karibuni.”
Mzee Ngosha na Bibi Ngosha walishangaa kusikia hivyo. Kwa mara ya kwanza, walimtazama mjukuu huyo wa kike mwenye mawazo ya kuvutia kwa umakini.
"Kitu kimoja zaidi. Usimwambie mtu yeyote nilichokuambia leo, pamoja na Bam’dogo Damien.” Lisa alitoa angalizo.
Mzee alishtuka. "Unamaanisha nini? Kwamba tunapaswa kumshuku Damien pia?”
"Hawezi kuwa Damien." Bibi Ngosha akatikisa kichwa mara moja. "Hali ya miguu yake imemfanya kuwa dhaifu na mgonjwa tangu utoto.”
“Umenielewa vibaya. Ninaogopa kwamba Bam’dogo Damien anaweza kudanganywa kwa urahisi kwa sababu ya madhaifu yake ya kuzaliwa. Kadiri watu wachache wanavyojua kuhusu hili, ndivyo itakavyokuwa bora zaidi,” Lisa alisema huku akitabasamu.
Kielelezo cha wasiwasi kwenye uso wa wanandoa hao wazee hatimaye kilipungua. Waliitikia kwa kichwa kuafiki kabla ya kuondoka hospitalini.
Shani, ambaye alikuwa akimlinda Lisa pembeni, hakuweza kujizuia kuuliza, “Kwanini hukuwaambia kwamba unamshuku pia Damien Ngosha?”
“Hawataniamini. Isitoshe, mimi ni mjukuu wao tu, na Damien ni mwana wao. Ninahitaji kuwaonyesha ukweli badala ya kuwashawishi kwa maneno matupu.” Kisha, akaingia kwenye gari.
Shani alishtuka alipotazama umakini wa mwanamke huyo. Ikamjia akilini kwamba Lisa alizidi kufana na Alvin kitabia.
Punde Nina akasikia habari za Joel akitibiwa na Dk. Angelo. Alikaribia kupoteza akili aliposikia hilo. Mara moja, alipiga namba ambayo haikuseviwa kwenye simu yake. "Joel atapata fahamu ndani ya mwezi mmoja."
"Tulia. Huenda huu ukawa mtego wa Lisa.”
“Lakini Daktari Angelo ana uwezo kwelikweli. Amesaidia wagonjwa kadhaa kutoka katika hali ya kukosa fahamu,” alisema huku akifadhaika. "Joel hakika atanishuku mara tu atakapoamka, na atanitaliki. Huenda nisipate hata senti kama hilo likitokea.”
“Usijali. Nitajitahidi niwezavyo kuchukua kampuni ya Ngosha ndani ya mwezi huu.”
"Kwa hivyo utafanya nini? Sitapewa senti hata moja ya kampuni.” Nina aliuma meno. “Kwanini hukumuua?”
"Usijali ... atakufa."
“Naweza tu kuweka imani yangu kwako. Yote haya ni kwa ajili ya msichana wetu kipenzi, Mel.” Nina ghafla akasitisha maneno yake..
Alipokata simu tu, mlango ukafunguliwa. Melanie alikuwa amesimama kando ya mlango, uso wake ukiwa umepauka kama mzimu. “Mama, nani alikuwa kwenye simu? Unajaribu kumuua nani? Baba?”
Uso wa Nina ulibadilika ghafla. “Usiingize pua yako katika hili. Sasa ni saa ngapi? Mbona haupo ofisini?”
“Mama acha kujaribu kubadilisha mada. Nilisikia yote.” Melanie alimtazama mama yake kwa hofu. “Ni kweli wewe ulikodi mtu kusababisha ajali ya baba? Mama, ungewezaje kufanya hivyo? Yeye ni mume wako. Pia, unamaanisha nini unaposema 'msichana wetu kipenzi Mel'? Mimi si binti wa baba?”
“Nyamaza. Yeye si mume wangu.” Nina alijua hakuna haja ya kuweka siri hii tena. "Hiyo ni sawa. Yeye si baba yako.”
Melanie alishtuka sana. "Hiyo haiwezekani. Hapana. Joel Ngosha ni baba yangu!
“Melanie, sikiliza. Baba yako alitaka kunitaliki muda si mrefu uliopita. Alikuwa anaenda kukupa 5% tu ya hisa za Ngosha Corporation, lakini 35% kwa Lisa. Nimefanya haya yote kwa ajili yako,” Nina alifoka huku machozi yakimtoka na kumshika bintiye mabegani.
Macho ya Melanie yalijaa chuki. “Baba yangu… Kwanini? Kwanini anifanyie hivyo?”
"Kweli," Nina alisema kwa huzuni. "Sote wawili hatungekuwa na nafasi katika jumuiya ya matajir ya Nairobi ukiwa na 5% tu ya hisa. Hata Jerome angebadili mawazo yake kuhusu kuwa na wewe.”
Melanie aliuma midomo yake. Hakutaka kupata uchungu wa kuachwa tena. "Mama, kwa nini kila mtu ana upendeleo kwa Lisa? Je, mimi si binti wa baba kweli? Kwa hiyo baba yangu ni nani?"
“Acha kulia. Baba yako anakupigania upate kampuni ya Ngosha." Nina alimkumbatia bintiye karibu. "Utajua ukweli hivi karibuni."
TUKUTANE KURASA 236-240
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
KURASA........131-235
Sura ya: 231
“Tatu bora? Hilo haliwezekani.” Mzee Kimaro alishikwa na butwaa.
"Unaweza kuangalia taarifa ya kifedha ya familia ya Campos kwa mwaka huu. Familia ya Campos kwa kawaida hawana biashara, wao huwekeza hisa kwenye makampuni makubwa. Baada ya Jack kuanza kusimamia kampuni, alisaini makubaliano na familia ya Campos ambayo hutoa faida ya asilimia tano kwao. Kana kwamba familia ya Campos haina nguvu za kutosha.” Taarifa hizo zilikuja kuwa pigo kwa Mzee Kimaro.
"Mara tu familia ya Kimaro itakapozama, familia ya Campos ina uhakika wa kuwa ya kwanza ambapo hawawezi kusubiri kuchukua usimamizi wa kampuni hiyo. Ikiwa nitamiliki KIM International, hadhi ya familia ya Kimaro haitabadilika kamwe. Hata hivyo, ni juu yako. Hata kama huna mpango wa kuniruhusu kuchukua kampuni, bado ninaweza kulinda hadhi yangu nchini Kenya kwa njia zangu mwenyewe. Katika hali hiyo, hali ya familia ya Kimaro haitakuwa na uhusiano wowote na mimi…”
“Lakini ugonjwa wako…” Mzee Kimaro alikuwa na wasiwasi.
“Kama huniamini, ni sawa. Niko bize, na ni lazima nikate simu sasa…”
Kwa hayo, Alvin alikuwa karibu kukata simu.
Hapo hapo, Mzee Kimaro akajibu mara moja, “Sawa, mimi tayari ni mzee. Siwezi kushindana na vijana. Nitakuruhusu uchukue KIM International, lakini ninatumai kuwa utaisimamia vyema. Mam’mdogo wako… Amekukosea, na sitarajii umlipishie kisasi. Baada ya kusema hivyo, usiende mbali sana. Baada ya yote, sisi ni familia."
"Babu, mimi hufuata kanuni ya jicho kwa jicho na jino kwa jino." Alvin alisisitiza.
“Wewe…” Mzee Kimaro alikosa la kusema.
“Huna uwezo wa kujadiliana nami tena.” Baada ya Alvin kukata simu, macho yake yalidhihirisha kupuuzia aliyoyaongea.
Lisa hakupenda maneno yake yaliyoashiria visasi. Alianguka mikononi mwake na kumkumbatia kwa nguvu. Kisha, alibadilisha mada. Je! ni kweli familia ya Campos ilifanikiwa kuwa kati ha familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya na mali zao?"
"Nini unadhani, huniamini?" Macho ya Alvin yalififia polepole.
“Hilo haliaminiki kabisa. Familia ya Campos daima imekuwa na hadhi ya chini. Nilikuwa na fikra kwamba itakuwa familia ya Choka na familia ya Shangwe ndizo ambazo zinaweza kuingia kwenye tatu bora.”
“Ndio. Familia ya Campos imekuwa ikijificha vizuri sana. Kama isingekuwa kwa ajili ya harusi ya Jerome wakati huu, nisingechunguza historia ya familia yake,” Alvin alisema “Familia ya Campos ni tata. Ninaogopa kwamba baba yangu wa kambo si rahisi kama anavyoonekana.”
Lisa alipigwa na butwaa. “Nimemwona Mason mara mbili. Ananipa hisia kwamba yeye ni mpole na mwenye urafiki. Uvumi unadai kwamba amekuwa akijishughulisha na sanaa na muziki na havutiwi kabisa na mali na mamlaka ya familia yake.”
"Nilikuwa nikifikiria hivyo pia, lakini Mason Campos ni mtu wa chinichini sana. Nadhani anajaribu kutumia njia hizo kugeuza mawazo yetu mbali naye.” Alvin alijaribu kufikiria.
Lisa aliuliza. "Kwa kuwa ni familia ya Campos iliyopanga njama ya picha dhidi yako, jambo hili linaweza kuhusishwa na Mason?"
“Labda…” Moyoni, Alvin alifadhaika kidogo. Aliinamisha kichwa chake na kumbusu kwenye midomo mara moja. "Nitaweka dhiki zote nyuma yangu kwa sasa. Hebu tufanye jambo la kufurahisha…”
“Aa…”
•••
Katika makazi ya familia ya Kimaro, Mzee Kimaro alishika simu huku akiwa amekaa kwenye kiti cha mbao, macho yake yakionyesha hisia tata.
“Kwa hiyo mazungumzo yako na Alvin yalikwendaje?” Bibi Kimaro akammiminia kikombe cha kahawa.
“Kwa kweli, hakuna maana kubishana kuhusu hilo. Yeye ni mjukuu wa familia ya Kimaro, hata hivyo. Nilipotazama video ya kuhojiwa yaya wake, nilihuzunika. Tuna deni kubwa kwake. Zaidi ya hayo, ni familia yetu wenyewe iliyofichua picha hizo…”
“Unafikiri ni nani alifanya hivyo?” Bibi Kimaro aliuliza.
"Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Lisa alidai kwamba ilikuwa familia ya Campos, kwa hivyo nadhani atakuwa ... Jack." Mzee Kimaro alihema kwa kukata tamaa. "Alvin aliniambia kuwa familia ya Campos imefanikiwa kuingia katika familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya."
Bibi Kimaro alishikwa na butwaa. “Inawezekanaje?”
“Bado unakumbuka familia ya Campos ilivyokuwa miaka 20 iliyopita? Nilimdharau Mason enzi hizo. Ingawa ana talanta ya muziki, hawakuwa na kitu kabisa enzi hizo. Baadaye, Lea alisisitiza kuisaidia familia ya Campos, na mimi nilifumbia macho. Ikiwa hii ni kweli, hufikirii kwamba familia ya Campos imekuwa ikituhujumu kwa kujificha vizuri?” Mzee Kimaro alieleza wasiwasi wake.
“Ndio. Wakati wa harusi ya Lea nakumbuka Mama Campos alivyokuwa akinung'unika jinsi biashara yao ilivyokuwa mbaya. Alitumaini kwamba tungeweza kusaidia familia yake.” Bibi Kimaro alijawa na huzuni.
“Nilikuwa namchukia Alvin kwa kuniharibia heshima ndiyo maana nilimuachia Jack kusimamia KIM International. Lakini nikiendelea kumwacha aisaidie familia ya Campos, familia ya Kimaro itapoteza sifa ya kuwa familia bora zaidi hivi karibuni.” Mzee Kimaro alimpigia simu moja kwa moja wakili wake. "Njoo hapa."
Katika muda usiozidi saa 12, habari kwamba Mzee Kimaro alihamisha hisa na mamlaka yake yote kwa Alvin zilikuwa zimesambaa Nairobi nzima. Wazao wa familia ya Kimaro ndio walikuwa wa kwanza kumtafuta Mzee Kimaro.
Valerie alikuwa wa kwanza kupinga kati yao. “Baba, una akili? Unawezaje kumruhusu Alvin kuchukua nafasi ya mwenyekiti wa KIM International? Hukumbuki jinsi alivyotufanyia hapo awali?”
"Umesemaje, sina akili?" Mzee Kimaro alikasirika sana hadi akahisi kutaka kumpiga makofi hadi kufa.
“Baba naogopa Alvin atanilenga baada ya kuchukua kampuni kwani ananichukia.” Valerie alizungusha mikono yake kwenye mguu wa Mzee Kimaro kwa mshtuko. “Kaka, Dada, ongeeni na baba, Alvin ataniua!”
Mdomo wa Spencer ulitetemeka. “Sina mgogoro na Alvin hata hivyo. KIM International itakuwa imekufa majini ikiwa hatutamruhusu kusimamia kampuni. Kila mtu huko nje anaichukulia familia yetu kama kituko kwa sasa. Wanasubiri tu kutuona tukianguka.”
“Vipi wewe?! Wewe ni mtoto wa pekee wa kiume kwa baba na mama. ulitakiwa uwe na nguvu kuliko wajukuu, lakini huna uwezo sana,” Valerie alimtukana.
"Nyamaza!" Mzee Kimaro alielekeza macho yake kwa Jack bila subira. “Unafikiri nini Jack?”
Jack alikunja ngumi. Alikuwa amejitahidi sana kabla ya kupata nafasi yake ya uenyekiti katika kampuni. Lakini, ikawa kwamba Alvin angechukua tena nafasi hiyo muhimu katika siku chache. Ilikuwa haiwezekani kwa Jack kuwa sawa na hilo. “Babu ni sawa na wewe kutishiwa na Alvin namna hii? Amekuwa akikukosea heshima waziwazi. Mara tu atakapopata nafasi ya kuongoza, ninaogopa atakudharau zaidi. Zaidi ya hayo, karibu amuue mama yake mzazi siku chache zilizopita. Ugonjwa wake umerejea.”
“Hasa. Mtu mwenye ugonjwa wa akili anawezaje kuchukua jukumu la KIM International?" Valerie akaongeza haraka.
"Kabla sijafikia uamuzi huu, mna suluhisho gani?" Mzee Kimaro alimkazia macho Jack. "Nilikupa nafasi, lakini ulichagua kufichua ugonjwa wa akili wa Alvin kwa umma badala ya kushughulikia mambo ya kampuni."
Jack ghafla alitazama juu kwa macho mekundu. “Sikufanya hivyo babu. Kuna mtu ananifanyia njama.”
“Unafikiria nini, Mason?” Mzee Kimaro alielekeza macho yake makali kwa mkwewe ghafla.
Mason alipigwa na butwaa kwa muda. Kisha akanung’unika, “Sina uhakika sana kuhusu hilo…”
Lea hakuweza kujizuia kusema, “Baba, Mason kwa kawaida hutumia wakati wake kutunga muziki. Hata hajali kinachoendelea kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos. Je, angewezaje kujua lolote kuhusu hili? Pia, Jack ni mwanangu na ninaelewa tabia yake. Nina hakika ni mtu mwingine aliyevujisha picha."
“Kwa hali hii…” Mzee Kimaro alichukua kikombe cha kahawa na kunywa kidogo kabla hajaendelea. “nilivyoamua imetosha. Hakuna haja ya kujaribu kunishauri tena. Machoni mwangu, hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kulinda nafasi ya familia ya Kimaro kama familia bora zaidi nchini Kenya.” Mzee Kimaro alisimamia msimamo wake. Hakuna mtu aliyekuwa na ujasiri wa kuzungumza upuuzi tena.
Mishipa iliyovimba ilionekana kwenye ngumi za Jack. Baada ya Jack kutoka nyumbani, alipiga mlango wa gari kwa nguvu. Akatoa simu yake na kumpigia Jerome. "Kuanzia sasa na kuendelea, Alvin ndiye mtoa maamuzi mkuu katika kampuni. Atakaporejea kwenye kampuni, ninahofia anaweza kufuta makubaliano kati ya familia ya Kimaro na familia ya Campos, na kufanya aslimia tano za faida kuwa batili.”
Sura ya: 232
“Nini?” Jerome alipiga kelele kwa hasira, "Nimewekeza sana katika uzalishaji wake na sasa unataka nipate hasara kubwa?"
“Hasara gani kubwa? Hamjavuna faida ya kutosha kabla ya hili?” Jack alisugua kichwa chake. "Isitoshe, niambie ukweli, je, familia ya Campos ilivujisha picha za maisha ya Alvin?"
“Una wazimu kumuamini Lisa? Mtu wa nje kama mimi angewezaje kupata picha hizo?" Jerome alishangaa.
Jack alikaa kimya huku taswira ya baba yake ikiingia kichwani mwake. Lakini kwa mawazo ya pili, ilionekana kuwa haiwezekani kwamba Mason Campos ambaye siku zote alikuwa hajali mambo hayo angefanya kitu kama hicho. “Hata hivyo, kila mtu katika familia ya Kimaro anashuku kuwa mimi ndiye niliyesababisha haya. Alvin ataniangamiza mara tu atakapopata tena ushindi wa juu.”
“Usijali. Utapata hisa za mama yako mwishoni kwa njia fulani. Jerome alikata simu hii na kupiga nyingine baada ya hapo. "Mpango haukufaulu." “Hmm, nilidharau ujasiri wa Alvin na Mzee Kimaro. Sembuse huyo mwanamke Lisa.”
Jerome alikaza macho yake. Alikuwa ameangalia historia ya Lisa hapo awali. Mwanamke huyu aliibuka hivi karibuni tu kuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investments. Alikuwa binti mdogo tu kutoka Tanzania. Hata hivyo, wakati wa kipindi cha moja kwa moja cha jana yake, mwanamke huyo alidumisha utulivu wakati akizungumza na taifa zima la Kenya—bila kusahau mawazo yake makali na ya kufikirisha huku akiipa changamoto familia yenye nguvu zaidi ya Kimaro.
Haikuwa makosa kusema kwamba Lisa alikuwa ameongoza kampuni ya Alvinarah kupitia shida hii wakati Alvin akiwa mgonjwa. Kwa sababu fulani, ilimkumbusha kuhusu mchumba wake, Melanie. Walikuwa dada wa kambo kutoka kwa baba mmoja lakini Melanie alikuwa kama mjinga.
“Kwa hiyo, nini kinachofuata?” Jerome aliuliza.
"Kwa bahati nzuri, nina mpango mbadala. Ni wakati wa kumpeleka kwenye uwanja wa vita." Mtu yule kwenye simu alijibu.
“Sawa. Nina imani na wewe kabisa.” Jerome alijibu kwa unyenyekevu. Alisikiliza mawazo ya kimkakati ya huyo mtu mwingine kwenye simu. Bila shaka, familia ya Campos ingekuwa familia yenye nguvu zaidi nchini Kenya kwa muda mfupi. Enzi ya familia ya Kimaro… ilikuwa inakaribia mwisho.
•••
Siku iliyofuata, Bibi Kimaro alimpelekea Alvin fomu ya uhamisho wa umiliki wa hisa kwenye jumba lake la kifahari ufukweni mwa bahari huko mombasa. Alipoingia ndani ya nyumba hiyo, aliona hakuna mtu mwingine ndani ya nyumba hiyo isipokuwa Aunty Yasmine ambaye alikuwa akisafisha sakafu.
“Alvin yuko wapi? Ametoka?”
"Bwana Mkubwa na Mkewe wameenda kununua mboga kwenye duka kubwa lililo jirani." Shangazi Yasmine alipiga goti ili kumsalimia yule kikongwe.
"Kununua mboga?" Maneno yale yalimponyoka kinywani Bibi Kimaro bila kujijua. Asingeweza kuamini kuwa mjukuu wake alikuwa ameenda kununua mboga ikiwa asingesikia kwa masikio yake mwenyewe.
"Alikuwa na matatizo ya ugonjwa siku mbili tu zilizopita. Anapaswa kupumzika nyumbani. Kwanini hukumzuia kutoka nje?”
“Usijali Bi Mkubwa. Bwana Kimaro hana tatizo kabisa na huchangamka sana anapokuwa na mkewe.” Kabla sauti yake haijakatika, vicheko vya furaha vilisikika kutoka nje.
Bibi Kimaro alitazama kupitia dirishani. Wanandoa wachanga walioshikana mikono walikuwa wakitembea kuelekea nyumbani. Nywele ndefu za Lisa zilining'inia mabegani mwake. Umbo lake zuri liliweza kuonekana licha ya suruali ya jeans ya mguu mpana na fulana nyeusi aliyokuwa amevaa. Pia alikuwa amevalia jozi ya viatu vyeupe vya turubai. Alionekana nadhifu na mchangamfu.
Karibu naye, Alvin alionekana mtanashati na mwenye furaha akiwa amevalia mavazi meupe ya kawaida. Alikuwa ameshika mifuko miwili ya shopping huku uso wake ukiwa na tabasamu la kupendeza. Wenzi hao walionekana kama watu waliooana hivi karibuni. Hasa, hakuonekana kama mtu ambaye alikuwa na tatizo lolote la akili.
Yule kikongwe alipigwa na butwaa kabisa kumuona. Ilikuwa ni muda mrefu sana kwamba hakuweza kukumbuka mara ya mwisho alipomwona akiwa na furaha hivi.
Bibi Kimaro alikuwa amejitayarisha hata kwa ukichaa wa Alvin akiwa njiani kwenda kwake. Hakika ilikuwa ni kutokana na matarajio yake kumuona katika hali hii ya utulivu na uchangamfu.
Wenzi hao wachanga walipomwona yule mwanamke mzee walipoingia ndani ya nyumba, mara tabasamu usoni mwa Alvin likatoweka. Macho yake yalionyesha uhasama na kujihami. Bibi Kimaro alihisi kana kwamba sindano imeuchoma moyo wake.
“Habari, Bibi,” Lisa alimsalimia mwanamke huyo mzee kwa upole kana kwamba hakuna jambo lolote baya lililokuwa limetokea kati yao hapo awali.
Bibi Kimaro alimpa tu mtazamo wa kijeuri, akikataa kujibu salamu yake.
Hasira ikawaka usoni mwa Alvin. “Kama umekuja kumkosea heshima mke wangu, tafadhali ondoka.”
“Wewe...” Bibi Kimaro aligugumia kwa hasira. “Mimi ni bibi yako. Utafurahi tu baada ya mimi kufa?"
“Ninachojua ni familia ya Kimaro ndiyo iliyonimwagia chumvi kwenye kidonda changu. Ningekuwa nimenaswa kwa nguvu katika hospitali ya magonjwa ya akili kama si Lisa.” Alvin alitabasamu kwa uchungu. "Ikiwa nyote bado mnaniona kama familia, basi kitu kidogo kabisa mnachoweza kufanya ni kumwonyesha heshima."
Bibi Kimaro alionekana kuchanganyikiwa. Lisa alisema kwa upole alipoona hivyo, “Bibi, mimi ndiye ninayepaswa kuwa na hasira kwa sababu uso wangu umeharibika kutokana na familia yako. Je, ninastahili mambo yote mabaya kwa sababu sitoki katika malezi yenye nguvu kama familia ya Kimaro?”
Bibi Kimaro alipasua midomo yake kutaka kusema kitu lakini Alvin alimkatisha kabla hajapata nafasi. “Mimi ndiye nimekuwa nikimsumbua tangu mwanzo hivyo acha kudhani kuwa ni mwanamke mlaghai. Hakuwa anajua mimi ni nani alipokutana nami mara ya kwanza. Pia nilichumbiana na Melanie baadaye ili tu kumfanya aone wivu.”
“Unawezaje kumfanyia hivyo Melanie?” Sauti ya kikongwe ilidhihirisha kutofurahishwa kwake.
"Ikiwa unampenda sana, basi mchukue kama mjukuu wako." Macho ya Alvin yalionekana kuwa makali kama moto. “Nilifanya mambo hayo kwa kukuridhisha tu. Melanie ni msichana mzuri—”
“Na Lisa je?” Bibi Kimaro alimkatiza bila subira kwa sauti ya ukali, “Wote wawili ni mabinti wa Joel Ngosha.”
“Lisa alikosea nini?” Alvin alidakia. “Je, alichagua familia aliyozaliwa? Hakuwahi kukumbana na mapenzi ya baba yake tangu akiwa mdogo lakini sasa kwa vile hatimaye ameungana na baba yake, kila mtu anamdharau. Kwa kweli, yeye ni mkubwa kuliko Melanie na mama yake ndiye aliyeachwa na Joel. Yeye ndiye mwathirika wa kweli hapa."
Bibi Kimaro hakuwa na maneno ya kubishana naye.
Alipohisi hali ya mvutano ikizidi kushamiri, Lisa alipendekeza, “Inakaribia saa sita mchana. Nyie wawili mnapaswa kuelewana nami nitaelekea jikoni kuandaa chakula cha mchana. Bibi, tafadhali kaa kwa chakula cha mchana.”
"Ikiwa unabaki tu ili uendelee kumshambulia mke wangu, basi ni bora ungeondoka tu," Alvin alisema kwa upole.
Bibi Kimaro aliona aibu sana kwa sauti ile. “Unadhani L-”
“Alvin, si rahisi kwa Bibi kufanya safari ndefu hivyo kuja hapa katika umri wake. Afadhali ukae kimya,” Lisa alifoka, na kufanya mambo yasiwe magumu kwa yule mzee. Alvin alikoroma, na Bibi Kimaro naye akakaa kimya.
Baada ya Lisa kutokomea jikoni, Bibi Kimaro alimuagiza mwanasheria atoe fomu ya kuhamisha umiliki wa hisa. “Hii imetoka kwa babu yako. Utakuwa na udhibiti kamili wa KIM International baada ya kusaini hii. Mimi na babu yako hatutaingilia mambo ya kampuni kuanzia hapo.”
Alvin akasaini karatasi bila kusita. “Siyo tu kwamba mam’dogo Valerie hajaboresha biashara ya KIM Insurance tangu achukue kitengo hicho, lakini mauzo yameshuka kiwango cha chini zaidi. Anapaswa kustaafu mapema, kuketi, na kufurahia bonasi za kila mwaka nyumbani.”
Bibi Kimaro alionekana kushtuka kabla ya kupiga kelele, “Unafanya hivi kumlipishia kisasi kwa sababu alisababisha Lisa kuharibika usoni…”
“Kwa hivyo itakuwaje kama hiyo ni kweli? Unamvumilia hata baada ya kusababisha madhara kwa mtu mwingine kwa sababu tu ni binti yako? Lakini yeye si binti yangu,” Alvin alijibu bila kujali.
“Lakini yeye ni mam’dogo wako, hata hivyo…” Bibi Kimaro akashusha pumzi ndefu. "Mbali na hilo, mauzo yake yaliimarika mwezi uliopita…”
Sura ya: 233
'Hiyo ni kwa sababu Nina Mahewa aliwekeza shilingi bilioni kadhaa." Macho ya Alvin yalidhihirisha dhamira ya hatari. “Ikiwa nilikisia kwa usahihi, alifanya hivyo baada ya mam’dogo Valerie kukubali kuharibu uso wa Lisa. Anadanganya takwimu za mauzo." Akiwa amepigwa na butwaa, Bibi Kimaro akakosa cha kusema.
“Bibi, unapaswa kushukuru. Nisingemuacha hai kama si wewe na babu.”
Alvin akainuka. “Angalia mwanao Spencer na binti zako. Mmoja wao anajali tu kusaidia familia ya mumewe, mwingine anadanganya mauzo. Mwanao pekee wa kiume ni dhaifu na hana uwezo. Unafikiri wewe na babu mngeweza kufurahia uzee wenu kwa mali mlizonazo sasa kama si mimi?” Bibi Kimaro alionekana kuwa mzee kwa miaka michache zaidi baada ya kusikia hivyo.
Saa sita kamili mchana, Lisa alitokea tena jikoni baada ya kuandaa chakula cha mchana lakini mvutano kati ya Alvin na bibi yake ulionekana kuongezeka. Alitenga chakula na kumkaribisha Bibi Kimaro mezani.
Mwisho bibi yule alionekana kushangazwa na vyakula vilivyowekwa mbele yake. Kila mlo haukuwa mzuri tu bali ulikuwa na ladha ya kupikwa nyumbani kuliko vile vya wapishi wa familia ya Kimaro. Aligundua kwamba Alvin, ambaye hakuwahi kufurahia chakula, alikuwa akila kila chakula—hasa nyama ya nguruwe.
Bibi alijaribu kipande kidogo cha nyama ya nguruwe. Walahi alitamani aachiwe sahani zote peke yake. Bakuli la nyama lilikuwa karibu kuisha alipofikia kipande cha pili.
“Usimalize yote. Bibi bado hajala vya kutosha.” Lisa akasogeza bakuli la nyama ya nguruwe kuelekea kwa Bibi Kimaro.
Alvin alikunja uso. “Kwanini hukujitayarisha nyingi?”
"Ulikula jana usiku na unataka tena mchana huu? Si afya kula nyama ya nguruwe kupita kiasi.” Aliweka mbogamboga badala yake kwenye sahani yake. “Ni muhimu kuwa na lishe bora na sio kuchagua. Ukiendeleza tabia hiyo mbaya, basi sitakupikia tena.” Lisa alimuonya.
“Sawa, nimekusikia.”
Chini ya macho ya Bibi Kimaro, mjukuu wake alianza kula mbogamboga. Mtu ambaye alikula vijiko vichache vya chakula kwa siku alikuwa akila sahani nzima wakati huu. Hata yule kikongwe alikuwa na hamu ya kula alipomwona mjukuu wake akila kwa hamu vile. Mwishowe, chakula cha mchana kilichotosha watu sita kilimalizwa na wale watatu.
Baada ya chakula cha mchana, Lisa alitenga majagi mawili ya mtindi kwenye meza. Aunty Yasmine alisema huku akitabasamu. “Hii pia imetengenezwa kwa mikono na Bi. Jones. Ni mtindi na asali na jamu safi ya strawberry ambayo aliiandaa polepole kwa masaa mawili. Alisema kunywa glasi ya mtindi baada ya mlo ni vizuri kwa usagaji chakula na kusafisha matumbo.”
Bibi Kimaro alionja kidogo kisha akanongewa tena. Mtindi ulikuwa mtamu sana. Alijisikia kuongeza glasi nyingine! lakini alikuwa na aibu sana kuomba kuongezewa.
Hata hivyo, Alvin hakuona aibu hata kidogo kuomba huduma nyingine mara baada ya hapo. Ombi lake lilikataliwa na Lisa. "Huwezi kunywa mtindi mwingi au unaweza kuvimbiwa."
"Una shida gani?" Alikunja uso lakini hakuzungumza zaidi.
Ingawa hakumpenda sana Lisa, Bibi Kimaro ilibidi akubali kwamba binti huyo alikuwa amembadilisha Alvin kuwa bora. Labda ugonjwa wa Alvin ungeimarika, kama hapo awali…
Baada ya chakula, Bibi Kimaro alisimama na kuaga ili kuondoka. “Asante kwa chakula wajukuu zangu, nimekula, nimefurahia na nimeshiba. Ni wakati wa mimi kuondoka.”
"Unaweza kukaa kwa siku chache zaidi. Kutembea na kupunga upepo baharini kunastarehesha kweli,” Lisa alisema kwa tabasamu hafifu.
Bibi Kimaro alijisikia vibaya kuona jinsi mwanamke huyo alivyoharibika usoni. “Ni sawa. Babu yako hajazoea kuwa mbali na mimi.” Baada ya kutulia kwa sekunde chache, aliendelea kusema, “Asante kwa ukarimu wako leo.”
Lisa alishangaa kusikia hivyo. Bado alikuwa akitabasamu hata baada ya yule kikongwe kuondoka zake.
Alvin alimkumbatia kwa upendo. “Bibi yangu alikutendea vibaya lakini bado ulijaribu sana kumfurahisha kwa chakula cha mchana na mtindi. Anafikiri kukushukuru mara moja ni fidia ya kutosha?"
“Ni kwa sababu yeye ni bibi yako.” Aligeuka na kuifunga mikono yake shingoni. “Ulimwambia maneno makali lakini bado najua unawajali sana babu na babi yako. Vinginevyo, usingeichukua KIM International tena. Una wasiwasi kwamba wanandoa hawa ambao wameishi maisha ya kitajiri wakati wote wangedhihakiwa na wengine katika uzee wao ikiwa KIM itaanguka?"
Alvin aliinua nmacho yake kinyonge. Hakuna mtu aliyemjua vizuri kuliko yeye.
“Alvlisa, nilikuwa na bibi pia. Ni pale tu alipotangulia mbele ya haki ndipo nilijuta kutotumia muda mwingi kuwa naye. Familia ni damu halisi na ni ngumu sana kuiondoa. Kwa sababu yako, ninaweza kujaribu kuwavumilia na kuwasamehe. Ilimradi utafurahi.” Kwa macho makali, Lisa alimtazama Alvin usoni.
Alvin alimsukuma ukutani. Hisia ambazo zilikuwa zimelala ndani ya moyo wake zililipuka kama volkano. Aliinamisha kichwa chake ili kumbusu kwa mahaba kwenye midomo. "Samahani, Lisa. Kwa ajili ya familia yangu kukuumiza.”
Uso wake uliharibiwa na familia ya Kimaro lakini bado aliwavumilia kwa ajili yake. Hata hivyo haikuwa imepita hivihivi tu. Aliahidi kuwalipa kwa yale waliyomfanyia.
"Siku moja, tutatapa mtu wa kutibu uso wako. Nitakupenda maisha yangu yote.”
Lisa alifunga macho yake karibu. Wakati huo huo, alihisi nguvu na utulivu. Haijalishi uso wake ulikuwa umeharibika vipi, kilichokuwa muhimu ni kwamba hakujali.
Siku iliyofuata, Lisa akaenda kufanya kazi katika kampuni yake. Alikuwa akitoka Mombasa hadi Nairobi na kurudi kwa ndege kila alipotaka kwenda ofisini kwake.
Alipotoka tu, Hans alijitokeza nyumbani kwa Alvin akiwa na wauguzi wachache. Kulikuwa na sura ya wasiwasi usoni mwake aliposema, "Bwana Kimaro, hawa ni wauguzi waliochaguliwa na mkurugenzi wa hospitali."
Alvin aliyekuwa anasoma kitabu cha hadithi za Jomba Wajo aliinua kichwa chake. Ugonjwa wake wa akili haukuwa kitu ambacho kingeweza kuponywa kwa siku kadhaa. Lisa alikuwa na kazi yake mwenyewe ya kufanya, kwa hivyo asingeweza kumtunza kila wakati. Ili kumzuia asipatwe tena na ugonjwa huo, ilikuwa vizuri kuwa na muuguzi aliyezoezwa ifaavyo nyumbani ili kumtazama.
Hata hivyo, alionekana kuchanganyikiwa wakati macho yake yalipotua kwenye uso mzuri sana. "Jina lako nani?"
Mwanamke huyo alionekana kushtuka chini ya macho yake kabla ya kujibu kwa sauti nyororo, "Jina langu ni Maurine Langa."
“Langa?” Alvin akashtuka kusikia jina hilo. "Una uhusiano gani na Sarah Njau Langa?"
"Yeye ni binamu yangu." Maurine alipepesa macho na kumtazama Alvin. “Unamfahamu binamu yangu?”
“Ni zaidi ya kumjua.” Alvin alihema ndani kwa ndani. "Wewe bado ni Langa, angalau. Kwanini uliishia kuwa nesi? Hii si kazi rahisi.”
"Langa sio kama tulivyokuwa hapo awali. Lakini ni sawa, angalau tuna cha kupeleka matumboni mwetu na paa juu ya vichwa vyetu.” Aliinua macho yake na kutabasamu kwa shukrani. "Pengine kuchukua kwangu taaluma hii kuna uhusiano na binamu yangu. Sisi wawili tulizoea kuwa karibu sana tulipokuwa wadogo lakini alipelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Nilijisikia vibaya sana kwake. Mpango wangu wa awali ulikuwa kuwa mwanasaikolojia aliyeidhinishwa lakini sikufanikiwa. Kwa kweli niko katika maandalizi ya kufanya mtihani tena.”
Alvin alichanganyikiwa tena aliposikia hivyo. Swali la Hans lilimrudisha kwenye ukweli. "Bwana Mkubwa, ungependa kumwajiri nani?"
"Maurine Langa, ndiyo." Alvin akachukua kitabu chake tena na kuendelea kusoma.
Tabasamu kubwa lilienea usoni mwake. “Asante, Bwana Kimaro. Nitafanya kila niwezalo kukusaidia kupona.”
Hans alionekana kushangaa. Mara tu Maurine alipoondoka kwenda nyumbani kuchukua vitu vyake, Alvin alimtazama Hans na kuagiza, “Mchunguze mwanamke huyu.”
"Bwana Mkubwa, unashuku kwamba-"
"Fanya nilichokuagiza!"
Katika muda usiozidi nusu siku, Hans alirudi na baadhi ya matokeo. “Maurine Langa hakika ni binamu wa Sarah Langa. Alikuwa akisoma nje ya nchi na hivi karibuni alirudi nyumbani. Tangu kifo cha mama yake, familia ya Langa imekuwa ikinyanyaswa sana na familia ya Njau. Maurine anabaguliwa nyumbani na hospitalini pia na kila mara hupewa jukumu la kuwaangalia wagonjwa wenye jeuri na fujo. Lakini, utendaji wake hospitalini umekuwa mzuri sana. Sio tu kwamba yeye ni mvumilivu bali pia ana mawazo yenye nguvu ya kuvumilia magumu.”
Sura ya: 234
Nuru ilizimika machoni mwa Alvin kwa sauti hiyo. "Inaweza kuwa ni bahati tu kwamba yuko hapa leo?"
"Inaonekana. Mabinti waliopendekezwa na wasimamizi wa hospitali hiyo ndio wauguzi wanaofanya vizuri zaidi kwa sasa.”
Aliitikia kwa kichwa baada ya kusikia hivyo, kigugumizi kwenye moyo wake kikatoweka. "Nani mkuu wa familia ya Njau sasa?"
"Charity Njau." Hans alijibu.
“Hakikisha KIM International na Alvinarah Media Network zinavunja mikataba yote ya ushirikiano na kampuni ya New Era Advertisings. Tutaona watapeleka wapi matangazo ya wateja wao. Nataka kumfunza somo Charity Njau kwa kuinyanyasa familia ya Langa.
Hans alikubali kwa utii na hakuongeza neno lolote.
Saa kumi na moja jioni Lisa aliondoka kazini mapema kuliko siku nyingine yoyote. Alisikia kelele kutoka kwa uwanja wa mpira wa vikapu mara tu aliposhuka kutoka kwenye gari.
Alitembea kwa wakati na kumuona Alvin akiinua mikono yake kutumbukiza mpira kwenye pete kufunga goli. Hakujua ni muda gani alikuwa akicheza mpira huo wa kikapu. Nyuma ya fulana yake nyeupe kulikuwa na unyevunyevu kidogo lakini uso wake ulionyesha hali ya jua.
Kumwona katika hali hiyo kulichukua pumzi yake. Alipokuwa bado shuleni, Ethan alikuwa mchezaji pekee wa mpira wa kikapu ambaye alisifiwa sana, lakini, akimtazama Alvin kwa wakati huo, aliona haiba ya kweli ya mwanamichezo.
“Naam!” Mfululizo wa makofi ya pongezi ulisikika kutoka upande wa pili wa uwanja. Hapo ndipo alipomwona yule mwanamke aliyelingana naye kiumri akiwa amevalia suruali ya jeans na top nyeupe. Nywele zake nyeusi zilizometa zilikuwa juu kwenye mkia wa farasi.
“Inavutia, Bwana Kimaro." Mwanamke huyo alitembea na chupa ya maji na kipande cha taulo. "Umecheza kwa dakika 40. Ni wakati wa kupumzika.”
“Sawa.” Alvin aliipokea ile chupa na kuanza kumeza vilivyomo ndani yake.
Miale ya jua la machweo iliwamulika wote wawili. Tukio hilo la aina fulani lilimchoma macho Lisa.
“Alvlisa…” Lisa aliita kabla ya kwenda haraka.
Alvin alitazama mwelekeo wa sauti hiyo na tabasamu likaenea katika uso wake wa kupendeza. "Baby, umefika nyumbani mapema leo."
"Nilirudi nyumbani mapema kwa kuhofia kuwa ungekuwa mpweke nyumbani peke yako." Alimtazama kwa karibu yule mwanamke mwingine. Alikuwa mrembo lakini hakuwa na kitu cha ajabu ikilinganishwa na yeye alivyokuwa zamani. Hata Melanie alikuwa mrembo zaidi ukilinganisha naye. Lisa alijisikia ahueni.
“Halo, Bi. Jones Mimi ndiye nesi niliyetumwa na hospitali kumuangalia Bwana Kimaro,” Maurine alijitambulisha huku akitabasamu.
“Oh, habari.” Lisa alishikwa na butwaa. Kwa sababu fulani, alihisi kana kwamba aliyaona macho hayo hapo awali lakini hakuweza kukumbuka ni wapi na lini.
“Ni heshima yangu kumwangalia Bwana Kimaro. Natumai atapona haraka iwezekanavyo.” Maurine alijieleza kitaaluma.
“Twende, naelekea ghorofani kuoga.” Alvin aliweka mkono begani kwa Lisa.
"Bwana Kimaro, unapaswa kupumzika kwa nusu saa baada ya kufanya mazoezi kabla ya kuoga," Maurine alimkumbusha.
“Sawa…” Alisita kabla ya kukubali.
Lisa alishangaa sana. Aliondoa fulana yake baada ya kupanda ghorofani. Alichukua taulo na kumpigapiga mgongoni. "Vipi mbona umeanza kucheza mpira wa kikapu ghafla?"
"Maurine Langa alisema kiasi kinachofaa cha mazoezi kinaweza kusaidia kupona kwa haraka na pia kuboresha ubora wa usingizi usiku."
“Maurine Langa?” Kitetemeshi kilipita kwenye uti wa mgongo wake.
Ni sadfa iliyoje! Aliwahi kuwa na mpenzi wa zamani mwenye jina la kati Langa pia. Sarah Langa!
“Ndio, kuna nini?” Akageuka kumtazama.
Lisa alichanganyikiwa sana. Hakuweza kusema kwamba alishituka kwa sababu jina la mwisho la nesi lilikuwa Langa. Hata hivyo, haikuwa sawa kujifanya kuwa mkarimu. “Sikutarajia ungemsikiliza msichana huyo kwa utiifu,” alisema huku akihema.
Alvin aliinua macho yake kabla ya kuinama ili kunusa midomo yake. "Hmm, nasikia harufu ya wivu."
“Nipo serious.” Akampiga kofi la mgongoni kwa utani.
Aliushika mkono wake mara moja na kuutoa kidogo. "Nisiingekuwa mtiifu hapo zamani na hata nisingekubali wazo la kuajiri muuguzi kutoka hospitali ya magonjwa ya akili. Hata hivyo, ninapenda nipone mapema kwa ajili yako, kwa hivyo ninahitaji kufanya kazi na mpango wa matibabu. Sitaki kufanya jambo lolote litakalokuumiza tena. Unaelewa?"
Aliuma midomo yake, ghafla akajisikia vibaya kwa kuwa na wivu sana. “Nimeelewa, lakini kwa nini usiajiri mtu ambaye ni mkubwa kidogo au labda nesi wa kiume? Nitakuwa nikifanya kazi ofisini na kukuacha peke yako nyumbani na msichana kweli?!”
Alvin alitabasamu kabla ya kuinua kichwa chake na macho yao yakagongana. “Una wivu kweli?”
“Alvin Kimaro!” Alimtazama kwa macho makavu.
“Usiwe na wivu bwana.” Alvin alimshusha wasiwasi. “Sekretari au mfanyakazi yeyote katika kampuni yangu ni mrembo kuliko yeye. Usingekuwa na nafasi ya kuwa Bi. Kimaro kama ningekuwa zoazoa fagio la chuma.” Alvin alijibu huku akitabasamu. “Sikuona ukiwa na wivu hivyo nilipokuwa na Melanie. Ulikuwa umekaa kimya kuhusu hilo.”
Aibu ilitanda usoni mwake alipofichua ukweli. “Siwezi kuwa na wasiwasi na hili. Naelekea chini kuandaa chakula cha jioni.” Akamtupia taulo na kuelekea kwenye ngazi.
Mara tu alipoingia jikoni, Maurine alimwendea na mpango wa lishe. "Bi. Mdogo, huu ni mpango wa lishe iliyoundwa mahsusi kwa ajili ya Bwana Kimaro. Kwa kuzingatia ugonjwa wake, ninapendekeza milo yake mikuu izingatie maelekezo haya.”
“Sawa, asante.” Lisa alipokea mpango wa chakula kabla hajauliza, "Je, tumewahi kukutana hapo awali?"
Maurine alionekana kushtuka lakini haraka akabadilisha mshangao huo na kutabasamu. "Sidhani. Hata hivyo ni mara yangu ya kwanza kukutana nawe, Bi. Kimaro. Lakini watu wengi wamesema kwamba wanaonekana kunifahamu.”
“Labda.” Lisa aliitikia kwa kichwa.
Lisa alitokea tena jikoni baada ya kupika chakula cha jioni, alimuona Alvin akiwa amekaa kwenye kochi huku Maurine akiwa amejiinamia kiunoni akijadiliana naye jambo kwa upole.
"Wakati wa chakula cha jioni," Lisa alimkumbusha.
Alvin akanyanyuka na kabla hajajonge mezani akatangaza, “Maurine na Shangazi Yasmine, kwa nini msijiunge nasi kwa mlo wa jioni wa leo?”
Hilo lilimshangaza Maurine. “Asante…” Alijibu huku akisitasita.
“Ni sawa. Usione haya wala woga. Kila mtu ni sawa katika zama za leo, na zaidi ya hayo, imekuwa ndefu kwako pia,” Lisa alisema kabla ya kugeuka kumwangalia Alvin.
Kwa kweli chakula cha jioni kilichangamka zaidi huku watu wale wanne wakiwa mezani. Hata hivyo, Lisa alikosa amani Maurine alipoendelea kumkumbusha Alvin ale nyama kidogo bali mboga na dagaa zaidi. Baada ya yote, yeye ndiye alikuwa na wajibu wa kusema maneno hayo. Kwa hivyo, ilikuwa ni ajabu sasa kwamba mtu mwingine alikuwa amechukua majukumu yake. Kwa kweli alijiona anazidi kuwa na wivu mkali.
Baada ya chakula cha jioni, yeye na Alvin walitembea ufukweni ili chakula kishuke vizuri tumboni. Waliporudi nyumbani, wote wawili walifanya kazi zao za ziada katika maktaba yao. Kwa kuwa Lisa alimaliza kazi yake mapema, alienda kuoga.
Alipotoka bafuni, aligundua kwamba Alvin alikuwa akinywa kitu kwenye glasi. Maurine alikuwa akimwangalia kwa makini pembeni. Mwanga wa taa ya manjano ulimulika juu yao kutoka darini kwa juu. Kuona jambo hilo kulimuumiza macho.
"Unakunywa nini?" Akasogea kuchungulia kwenye glasi yake. Kioevu cheupe kilionekana ndani yake, labda kilikuwa ni maziwa.
Maurine alieleza kwa upole, “Kunywa glasi ya maziwa kabla ya kulala huboresha ubora wa usingizi.”
“Asante, lakini hili ni jukumu langu,” Lisa alijibu kwa tabasamu hafifu.
Maurine alishikwa na butwaa kiasi kwamba uso wake ulipauka ghafla. Akiwa amechanganyikiwa, alitikisa kichwa kwa aibu. "Ndio, nitawaacha nyie wawili sasa."
Sura ya: 235
Maurine alimtazama Lisa kwa tahadhari kabla ya kufunga mlango nyuma yake.
Alvin alisema kwa kucheka, “Umemuogopesha binti huyo.”
Lisa alishindwa cha kusema. “Nilifanya nini cha kumuogopesha? Nilisema maneno hayo kwa uso wa kirafiki.”
"Hmm, lakini pia kwa sauti ya wivu sana." Alvin aliitikia kwa kichwa huku uso wake ukionekana kutojiweza. “Ni glasi tu ya maziwa. Hutakiwi kuwa na wivu juu yake.”
Maneno ya Alvin yalimfanya ajione kuwa ni mwanamke mwenye fikra finyu. Lisa alishusha pumzi ndefu huku akihisi mshangao mwingi ukimuandama.
“Acha kuwaza kupita kiasi. Ngoja nikukaushe nywele zako.” Alvin akachukua mashine ya kukaushia nywele.
Mara tu nywele zake zilipokauka, alipanda kitandani na uso wenye haya. Tangu wapatane, alikuwa na shauku kubwa ya kufanya mapenzi kitandani, lakini bado aliona aibu kila alipojiwazia. Hata hivyo, alijilaza tu kitandani kwa utulivu baada ya kuzima taa usiku huo. Hamu yake iliyofichika haikuwa ya kawaida. Lisa akaanza uchokozi wa makusudi. Akageuka juu juu juu na kumkandamiza Alvin na makalio yake.
"Tulia basi tulale." Alvin aliyekuwa amegeuziwa makalio na kumkandamiza ipasavyo kwenye ikulu yake akampigapiga tu mgongoni na kumpoza kwa sauti yake ya upole.
Lisa hakuamini masikio yake. Aliuma midomo yake na kuizungushia mikono yake shingoni mwake. “Alvlisa…” Lisa aliita taratibu. Ukiacha sauti yake iliyotetema kwa huba, uso wake wote ulikuwa ukizungumza mapenzi tu. Kwa bahati nzuri, Alvin hakuweza kuuona kwa sababu taa zilikuwa zimezimwa.
Hili lilimshangaza sana Alvin. Mshawasha ukatekenya kunako makao makuu yake, lakini alizuia shauku yake mara moja. “Maurine alinikumbusha kwamba dawa ninazotumia haziniruhusu nifanye hivyo kwa sasa. Ni bora tusitishe jambo hili kwa sasa.” Unyonge ulionekana katika sauti yake.
Lisa alionekana kushtuka. “Lakini kabla… Sote tulikuwa wazuri. Sio lazima, sivyo?"
“Unanitaka sana hivyo?” ghafla alisema kwa mahaba mazito.
Lisa aligeuka tu bila kujibu. Alitaka ndiyo lakini hakutaka kujirahisha sana, alihitaji kudumisha kiburi chake pia. Alitaka abembelezwe kwanza ndipo atoe!
Alvin akamkumbatia kwa nyuma. “Kuwa mvumilivu. Siwezi kufanya chochote ambacho kinaweza kunisisimua kupita kiasi kwa sasa. Ninaogopa nitafanya kitu nje ya udhibiti wangu ambacho kinaweza kukuumiza. Kama mara ya mwisho."
Lisa aliuma midomo yake, alikasirika, na mwishowe akanung'unika "sawa" baada ya muda mrefu. Usiku ule hakupata usingizi huku Alvin akipitiwa na usingizi mzito. Mawazo yake yalikuwa yakimshawishi kwamba labda nadharia ya Maurine ilikuwa sahihi. Baada ya yote, alikuwa akisumbuliwa na usingizi tangu aanze kupandisha wazimu. Muda ulikuwa umepita tangu amwone amelala vizuri sana.
Siku iliyofuata, Lisa alipokea simu kutoka hospitalini. Inavyoonekana, daktari bingwa wa mfumo wa neva, Daktari Angelo kutoka nje ya nchi alikuwa amefika kumtibu Joel. Bila kupoteza muda, alieelekea hospitali mara moja. Bibi na Babu Ngosha walikuwa tayari wameshafika.
Dk. Angelo alikuwa amemaliza uchunguzi wa Joel. "Ninahitaji kumtibu kwa kudhibiti mishipa yake kwa muda mrefu. Bado kuna matumaini kwamba Bw. Ngosha atatoka katika hali ya kukosa fahamu, lakini huenda ikawa ni safari ndefu. Muda mfupi zaidi labda utakuwa nusu mwaka hadi mwaka mzima.
"Asante sana." Lisa alishukuru.
“Usijali. Wewe ni rafiki wa Chester, kwa hiyo nitafanya kila niwezalo kukusaidia.” Dk. Angelo alisema.
Baada ya kutafakari kwa ufupi, Lisa aliomba, “Dokta Angelo, ikiwa mtu atakuja kuuliza kuhusu hali yake, tafadhali mwambie kwamba Bw. Ngosha atarudiwa na fahamu ndani ya mwezi mmoja.”
Daktari alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kutikisa kichwa. “Hakika.”
Baada ya daktari kuondoka, Mzee Ngosha hakuweza kupinga kuuliza, “Unajaribu kuchunguza kama kuna mtu alipanga kumuua baba yako?”
"Babu, unadhani ni nani anayeweza kuwa mhusika?" Aliuliza.
Mzee alikaa kimya kwa muda. Uchunguzi wa maiti ya dereva wa lori ulionyesha kwamba alikuwa alisinzia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya. Hata hivyo, mwanamume huyo hakuwa mraibu na alikuwa ametumia tu dawa hiyo kimakosa. Kwa wazi, hili lilikuwa tendo la makusudi.
“Nina uhakika ni Nina.” Mzee Ngosha alifoka kwa hasira. "Baada tu ya ajali amemwingiza Melanie kufanya kazi katika Kampuni ya Ngosha."
Lisa alikubali kwa kichwa. “Ikiwa ni hivyo, atahakikisha kwamba baba yangu hataamka kamwe. Kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee itakayomwezesha kurithi kila kitu alichoacha nyuma. Kando na hilo, ikiwa mtu mwingine yuko nyuma ya hili, mtu huyo bila shaka atajaribu kuchukua udhibiti wa Ngosha Corporation ndani ya mwezi huu. Nina hakika mhalifu atafichua asili yake hivi karibuni.”
Mzee Ngosha na Bibi Ngosha walishangaa kusikia hivyo. Kwa mara ya kwanza, walimtazama mjukuu huyo wa kike mwenye mawazo ya kuvutia kwa umakini.
"Kitu kimoja zaidi. Usimwambie mtu yeyote nilichokuambia leo, pamoja na Bam’dogo Damien.” Lisa alitoa angalizo.
Mzee alishtuka. "Unamaanisha nini? Kwamba tunapaswa kumshuku Damien pia?”
"Hawezi kuwa Damien." Bibi Ngosha akatikisa kichwa mara moja. "Hali ya miguu yake imemfanya kuwa dhaifu na mgonjwa tangu utoto.”
“Umenielewa vibaya. Ninaogopa kwamba Bam’dogo Damien anaweza kudanganywa kwa urahisi kwa sababu ya madhaifu yake ya kuzaliwa. Kadiri watu wachache wanavyojua kuhusu hili, ndivyo itakavyokuwa bora zaidi,” Lisa alisema huku akitabasamu.
Kielelezo cha wasiwasi kwenye uso wa wanandoa hao wazee hatimaye kilipungua. Waliitikia kwa kichwa kuafiki kabla ya kuondoka hospitalini.
Shani, ambaye alikuwa akimlinda Lisa pembeni, hakuweza kujizuia kuuliza, “Kwanini hukuwaambia kwamba unamshuku pia Damien Ngosha?”
“Hawataniamini. Isitoshe, mimi ni mjukuu wao tu, na Damien ni mwana wao. Ninahitaji kuwaonyesha ukweli badala ya kuwashawishi kwa maneno matupu.” Kisha, akaingia kwenye gari.
Shani alishtuka alipotazama umakini wa mwanamke huyo. Ikamjia akilini kwamba Lisa alizidi kufana na Alvin kitabia.
Punde Nina akasikia habari za Joel akitibiwa na Dk. Angelo. Alikaribia kupoteza akili aliposikia hilo. Mara moja, alipiga namba ambayo haikuseviwa kwenye simu yake. "Joel atapata fahamu ndani ya mwezi mmoja."
"Tulia. Huenda huu ukawa mtego wa Lisa.”
“Lakini Daktari Angelo ana uwezo kwelikweli. Amesaidia wagonjwa kadhaa kutoka katika hali ya kukosa fahamu,” alisema huku akifadhaika. "Joel hakika atanishuku mara tu atakapoamka, na atanitaliki. Huenda nisipate hata senti kama hilo likitokea.”
“Usijali. Nitajitahidi niwezavyo kuchukua kampuni ya Ngosha ndani ya mwezi huu.”
"Kwa hivyo utafanya nini? Sitapewa senti hata moja ya kampuni.” Nina aliuma meno. “Kwanini hukumuua?”
"Usijali ... atakufa."
“Naweza tu kuweka imani yangu kwako. Yote haya ni kwa ajili ya msichana wetu kipenzi, Mel.” Nina ghafla akasitisha maneno yake..
Alipokata simu tu, mlango ukafunguliwa. Melanie alikuwa amesimama kando ya mlango, uso wake ukiwa umepauka kama mzimu. “Mama, nani alikuwa kwenye simu? Unajaribu kumuua nani? Baba?”
Uso wa Nina ulibadilika ghafla. “Usiingize pua yako katika hili. Sasa ni saa ngapi? Mbona haupo ofisini?”
“Mama acha kujaribu kubadilisha mada. Nilisikia yote.” Melanie alimtazama mama yake kwa hofu. “Ni kweli wewe ulikodi mtu kusababisha ajali ya baba? Mama, ungewezaje kufanya hivyo? Yeye ni mume wako. Pia, unamaanisha nini unaposema 'msichana wetu kipenzi Mel'? Mimi si binti wa baba?”
“Nyamaza. Yeye si mume wangu.” Nina alijua hakuna haja ya kuweka siri hii tena. "Hiyo ni sawa. Yeye si baba yako.”
Melanie alishtuka sana. "Hiyo haiwezekani. Hapana. Joel Ngosha ni baba yangu!
“Melanie, sikiliza. Baba yako alitaka kunitaliki muda si mrefu uliopita. Alikuwa anaenda kukupa 5% tu ya hisa za Ngosha Corporation, lakini 35% kwa Lisa. Nimefanya haya yote kwa ajili yako,” Nina alifoka huku machozi yakimtoka na kumshika bintiye mabegani.
Macho ya Melanie yalijaa chuki. “Baba yangu… Kwanini? Kwanini anifanyie hivyo?”
"Kweli," Nina alisema kwa huzuni. "Sote wawili hatungekuwa na nafasi katika jumuiya ya matajir ya Nairobi ukiwa na 5% tu ya hisa. Hata Jerome angebadili mawazo yake kuhusu kuwa na wewe.”
Melanie aliuma midomo yake. Hakutaka kupata uchungu wa kuachwa tena. "Mama, kwa nini kila mtu ana upendeleo kwa Lisa? Je, mimi si binti wa baba kweli? Kwa hiyo baba yangu ni nani?"
“Acha kulia. Baba yako anakupigania upate kampuni ya Ngosha." Nina alimkumbatia bintiye karibu. "Utajua ukweli hivi karibuni."
TUKUTANE KURASA 236-240
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app